
-
-
"Najisikia vibaya namna watu wanavyoniona na kuanza kuniita Yesu, wanafikia hata kutundika picha zangu katika nyumba zao, mimi ni mwigizaji tu, mimi ni mtu" - Jonathan Roumie(50), mwigizaji wa Marekani
Aidha, Jonathan Roumie katika mahojiano amesema maisha yake binafsi alikuwa na hali mbaya kiuchumi hakuwa na uhakika siku inayofuata atakula nini, alikuwa mwigizaji ila kiuchumi alikuwa bado hajafanikiwa. Baada ya mambo kuzidi kuwa magumu siku moja ni kama alikuwa anamuomba Mungu kuhusu hali anayopitia ili mambo yake yakae sawa
Baada ya miezi kama mitatu ndio akapata nafasi ya kuigiza kama Yesu katika series ya "The Chosen" iliyoanza kuoneshwa 2017 ambayo imejipatia umaarufu mkubwa sana hadi sasa imetazamwa na watu zaidi ya milioni 250 na misimu mipya inafuata huku ikipongezwa kwa kinachoonekana kuigizwa
Umaarufu wa uhusika wake kama Yesu umempa umaarufu mkubwa na fursa nyingi ikiwemo katika mikutano na makongamano makubwa ya kidini na app za dini ya kikiristo
Jonathan ambaye ni mkatoliki, alipoulizwa na New York Times, je ni tukio gani gumu analokumbuka ambalo alishakutana nalo baada ya kuigiza kama Yesu, amejibu kwa kusema kuna kipindi alikuwa katika mkutano kwenye uwanja wenye watu takribani 40,000 baadaye alishuka stejini akaenda kwenye chumba fulani uwanjani hapo, mmoja wa walinzi alikuja akamwambia nje kuna mwanamke ana mtoto kwenye kiti cha magurudumu anaomba kusalimiana na wewe
Jonathan alitoka akaonana na mwanamke husika na mwanae ambaye kwa ufupi alieleza jinsi Yesu alivyoponya mtu katika hiyo series ya "The Chosen" na kusema angependa mwanae pia apone yaani akimtaka Jonathan amponye mtoto wake. Ilibidi Jonathan amueleze ukweli kwamba yeye sio mponyaji wala mhubiri bali ni mwigizaji tu.
Jonathan akamueleza wafanye maombi wote ilichukua kama dakika moja, walipomaliza maombi wakafurahi na kushukuru kisha Jonathan akarudi alipokuwa huku akitokwa na machozi akihisi amewaangusha matarajio waliyokuwa nayo kwake ila amesema ni bora waujue ukweli kuwa yeye sio Yesu wala mponyaji bali ni mwigizaji tu
Ukiacha hayo ya uhusika wake wa Yesu na dini, Jonathan Roumie amegusia pia kwamba alishafika Tanzania na Rwanda sababu kuna watoto kadhaa wanaoishi katika mazingira magumu huwa anawasaidia na familia zao
Jonathan Roumie pia ameweka wazi kwamba anatamani watu pia wawe wanamuona katika nyuma ya pazia(behind the scene) anayopitia katika kujiandaa na uigizaji wake kama Yesu ili watu wengine waelewe wajue kumtofautisha katika maisha halisi na kisanaa
KUMBUKA, zipo filamu nyingine miaka ya nyuma kuhusu Yesu zilizohusisha waigizaji wengine kabla ya sasa Jonathan Roumie kupata umaarufu na uhusika wa Yesu katika series maarufu ya "The Chosen"
(Swahili Word)
"Najisikia vibaya namna watu wanavyoniona na kuanza kuniita Yesu, wanafikia hata kutundika picha zangu katika nyumba zao, mimi ni mwigizaji tu, mimi ni mtu" - Jonathan Roumie(50), mwigizaji wa Marekani Aidha, Jonathan Roumie katika mahojiano amesema maisha yake binafsi alikuwa na hali mbaya kiuchumi hakuwa na uhakika siku inayofuata atakula nini, alikuwa mwigizaji ila kiuchumi alikuwa bado hajafanikiwa. Baada ya mambo kuzidi kuwa magumu siku moja ni kama alikuwa anamuomba Mungu kuhusu hali anayopitia ili mambo yake yakae sawa Baada ya miezi kama mitatu ndio akapata nafasi ya kuigiza kama Yesu katika series ya "The Chosen" iliyoanza kuoneshwa 2017 ambayo imejipatia umaarufu mkubwa sana hadi sasa imetazamwa na watu zaidi ya milioni 250 na misimu mipya inafuata huku ikipongezwa kwa kinachoonekana kuigizwa Umaarufu wa uhusika wake kama Yesu umempa umaarufu mkubwa na fursa nyingi ikiwemo katika mikutano na makongamano makubwa ya kidini na app za dini ya kikiristo Jonathan ambaye ni mkatoliki, alipoulizwa na New York Times, je ni tukio gani gumu analokumbuka ambalo alishakutana nalo baada ya kuigiza kama Yesu, amejibu kwa kusema kuna kipindi alikuwa katika mkutano kwenye uwanja wenye watu takribani 40,000 baadaye alishuka stejini akaenda kwenye chumba fulani uwanjani hapo, mmoja wa walinzi alikuja akamwambia nje kuna mwanamke ana mtoto kwenye kiti cha magurudumu anaomba kusalimiana na wewe Jonathan alitoka akaonana na mwanamke husika na mwanae ambaye kwa ufupi alieleza jinsi Yesu alivyoponya mtu katika hiyo series ya "The Chosen" na kusema angependa mwanae pia apone yaani akimtaka Jonathan amponye mtoto wake. Ilibidi Jonathan amueleze ukweli kwamba yeye sio mponyaji wala mhubiri bali ni mwigizaji tu. Jonathan akamueleza wafanye maombi wote ilichukua kama dakika moja, walipomaliza maombi wakafurahi na kushukuru kisha Jonathan akarudi alipokuwa huku akitokwa na machozi akihisi amewaangusha matarajio waliyokuwa nayo kwake ila amesema ni bora waujue ukweli kuwa yeye sio Yesu wala mponyaji bali ni mwigizaji tu Ukiacha hayo ya uhusika wake wa Yesu na dini, Jonathan Roumie amegusia pia kwamba alishafika Tanzania na Rwanda sababu kuna watoto kadhaa wanaoishi katika mazingira magumu huwa anawasaidia na familia zao Jonathan Roumie pia ameweka wazi kwamba anatamani watu pia wawe wanamuona katika nyuma ya pazia(behind the scene) anayopitia katika kujiandaa na uigizaji wake kama Yesu ili watu wengine waelewe wajue kumtofautisha katika maisha halisi na kisanaa KUMBUKA, zipo filamu nyingine miaka ya nyuma kuhusu Yesu zilizohusisha waigizaji wengine kabla ya sasa Jonathan Roumie kupata umaarufu na uhusika wa Yesu katika series maarufu ya "The Chosen" (Swahili Word) -
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo wa Tanzania , Profesa Palamagamba Kabudi anatarajiwa kukutana na Viongozi wa klabu za Simba SC na Yanga SC kuzungumzia sakata la uamuzi wa klabu ya Simba SC kugomea mechi ya watani wa jadi iliyokuwa ifanyike Machi 8, 2025 kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam.
Pamoja na Viongozi hao wa klabu ya Simba SC na Yanga SC, Wengine ambao wanatarajiwa kushiriki kikao hicho kilichopangwa kufanyika Machi 27 mwaka huu ni Viongozi wa Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania (TFF) pamoja na Viongozi kutoka Bodi ya Ligi Kuu ya Tanzania Bara (TPBL).
Ikumbukwe kwamba klabu ya Simba Sports SC iligomea mchezo huo kwa madai ya ukiukwaji wa Kanuni namba 17(45) ya Kanuni za Ligi Kuu Tanzania Bara kwa zuiliwa kwa Vijana (Mabausa) waliodhaniwa kuwa ni wa klabu ya Yanga SC, ambayo inaruhusu klabu ngeni kufanya mazoezi kwenye Uwanja wa mechi angalau mara moja kabla ya siku ya mechi.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo wa Tanzania 🇹🇿, Profesa Palamagamba Kabudi anatarajiwa kukutana na Viongozi wa klabu za Simba SC na Yanga SC kuzungumzia sakata la uamuzi wa klabu ya Simba SC kugomea mechi ya watani wa jadi iliyokuwa ifanyike Machi 8, 2025 kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam. Pamoja na Viongozi hao wa klabu ya Simba SC na Yanga SC, Wengine ambao wanatarajiwa kushiriki kikao hicho kilichopangwa kufanyika Machi 27 mwaka huu ni Viongozi wa Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania (TFF) pamoja na Viongozi kutoka Bodi ya Ligi Kuu ya Tanzania Bara (TPBL). Ikumbukwe kwamba klabu ya Simba Sports SC iligomea mchezo huo kwa madai ya ukiukwaji wa Kanuni namba 17(45) ya Kanuni za Ligi Kuu Tanzania Bara kwa zuiliwa kwa Vijana (Mabausa) waliodhaniwa kuwa ni wa klabu ya Yanga SC, ambayo inaruhusu klabu ngeni kufanya mazoezi kwenye Uwanja wa mechi angalau mara moja kabla ya siku ya mechi. -
Rais wa Nchi ya Burundi , Evariste Ndayishimiye anasema kuwa Nchi ya Rwanda ina mpango wa kuivamia Burundi kupitia Congo ambapo anasema Nchi hiyo itakuwa imekosea sana.
“Tunajua kwamba Rwanda inajaribu kutushambulia kupitia eneo la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, kupitia vuguvugu la Red-Tabara. Lakini tunawaambia kwamba ikiwa wanataka kushambulia Bujumbura kupitia Congo na sisi Kigali hatuko mbali kupitia Kirundo,” alisema Rais Evariste Ndayishimiye
Baada ya kauli hiyo, Msemaji wa Serikali ya Rwanda Yolande Makolo amesema kuwa, ameshangazwa na kauli ya Rais Evariste Ndayishimiye huku akihoji Rais Ndayishimiye anaeleza kuwa ana taarifa za kuaminika kuwa Rwanda ina mpango wa kushambulia Burundi ?. Msemaji huyo alisema pia endapo hali hiyo ikitokea basi migogoro inaweza kuwa na maafa kwani inaweza kusambaa katika ukanda mzima wa Afrika Mashariki na kati.
Rais Ndayishimiye amemalizia kwa kusema kuwa tayari ameshatuma Wajumbe kadhaa kwa Rais wa Rwanda Paul Kagame wa kumtaka atekeleze makubaliano ambayo yatazileta pamoja Nchi hizo mbili pamoja lakini hadi leo hii hakuna majibu yoyote yaliyotolewa na bado anayasubiri pia.
Rais wa Nchi ya Burundi 🇧🇮, Evariste Ndayishimiye anasema kuwa Nchi ya Rwanda 🇷🇼 ina mpango wa kuivamia Burundi kupitia Congo ambapo anasema Nchi hiyo itakuwa imekosea sana. “Tunajua kwamba Rwanda inajaribu kutushambulia kupitia eneo la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, kupitia vuguvugu la Red-Tabara. Lakini tunawaambia kwamba ikiwa wanataka kushambulia Bujumbura kupitia Congo na sisi Kigali hatuko mbali kupitia Kirundo,” alisema Rais Evariste Ndayishimiye Baada ya kauli hiyo, Msemaji wa Serikali ya Rwanda Yolande Makolo amesema kuwa, ameshangazwa na kauli ya Rais Evariste Ndayishimiye huku akihoji Rais Ndayishimiye anaeleza kuwa ana taarifa za kuaminika kuwa Rwanda ina mpango wa kushambulia Burundi ?. Msemaji huyo alisema pia endapo hali hiyo ikitokea basi migogoro inaweza kuwa na maafa kwani inaweza kusambaa katika ukanda mzima wa Afrika Mashariki na kati. Rais Ndayishimiye amemalizia kwa kusema kuwa tayari ameshatuma Wajumbe kadhaa kwa Rais wa Rwanda Paul Kagame wa kumtaka atekeleze makubaliano ambayo yatazileta pamoja Nchi hizo mbili pamoja lakini hadi leo hii hakuna majibu yoyote yaliyotolewa na bado anayasubiri pia. -
-
-
-
-
Mchambuzi Farhan JR.
Nimeona andiko la Waukae @zakazakazi kuhusu TFF kutengeneza Vijana ambalo lilipaswa kuwa jukumu la Klabu na akienda mbali kusema kwamba TFF ndio Shirikisho pekee duniani ambalo lina kituo ambacho kinazalisha na kulea vipaji vya vijana, kwanza kabla ya kupingana nae kuna kitu kwanza nataka kukiweka sawa kwenye eneo hilo.
Duniani kote Mashirikisho kama TFF yamejikita zaidi kwenye DEVELOPMENT PROJECTS yaani Miradi ya maendeleo kisha wakaachia Mashindano kadhaa yasimamiwe na Bodi zao za Ligi kwa 90% bila kuyaingilia, TFF anachokifanya ni sahihi lakini pia sio sahihi sana kufanya yeye alipaswa kuwa na CLINICS tu ila kuna changamoto sehemu ambayo imeletwa na TFF wenyewe.
Duniani Klabu zinaweza kuendesha miradi ya Vijana kwasababu kuna kitu kinaitwa FALSAFA ya nchi kwenye mpira, kuanzia mifumo, afya tiba, afya lishe na miundo yote ambayo portifolio hutoka Shirikisho (TFF) Klabu zinaenda kutekeleza mifumo hiyo na kuadjust baadhi ya maeneo halafu Vijana wakienda Clinics za Kitaifa wanaenda kukazia tu.
Swali linakuja Je Waukaye @zakazakazi FALSAFA ya Tanzania kwenye mpira wa Miguu ni ipi? Iliwasilishwa lini? Anayo nani? Hilo ni Jukumu la TFF ambalo halijatekelezwa, kuna kitu kinaitwa TALENT ID FRAMEWORK ili kupata Vijana je tunayo? Ipoje, anayo nani? Inasemaje? Klabu hazina Mwongozo kutoka kwa TFF? Academy zote nchini zipite humo LAZIMA TFF wafanye wanachoweza, tupo katikati, TFF ASIMAMIE HILO KIKAMILIFU.
TFF wasiende mbali waende tu hapo Uganda ilipo FUFA, wana Talent ID Framework ambayo Mashirikisho yoote yalipigwa huo Msasa sambamba na Kamati zao tendaji, ndio maana Uganda wapo mbali mno kwenye soka la Vijana kwenye Klabu zao na National Team, kwasababu wana ramani wanaifuata, wameintergrate mfumo wao na FIFA Talent Development Schemes (TDS) je sisi lini tutaforce Klabu zipite humo?
TFF anajipa majukumu ambayo mengine sio ya kwake, kujadili mikataba ya kibiashara sio Jukumu lake bali Vilabu na Bodi yao, TFF anabaki kama Baba pekee, duniani kote TFF zao zina majukumu yao ukitoa michuano ya FA na Ngao basi Ligi Kuu sio mali yao, TFF ASIMAMIE HASWA JUKUMU LA MAENDELEO NI LAKE.
Mchambuzi Farhan JR. Nimeona andiko la Waukae @zakazakazi kuhusu TFF kutengeneza Vijana ambalo lilipaswa kuwa jukumu la Klabu na akienda mbali kusema kwamba TFF ndio Shirikisho pekee duniani ambalo lina kituo ambacho kinazalisha na kulea vipaji vya vijana, kwanza kabla ya kupingana nae kuna kitu kwanza nataka kukiweka sawa kwenye eneo hilo. Duniani kote Mashirikisho kama TFF yamejikita zaidi kwenye DEVELOPMENT PROJECTS yaani Miradi ya maendeleo kisha wakaachia Mashindano kadhaa yasimamiwe na Bodi zao za Ligi kwa 90% bila kuyaingilia, TFF anachokifanya ni sahihi lakini pia sio sahihi sana kufanya yeye alipaswa kuwa na CLINICS tu ila kuna changamoto sehemu ambayo imeletwa na TFF wenyewe. Duniani Klabu zinaweza kuendesha miradi ya Vijana kwasababu kuna kitu kinaitwa FALSAFA ya nchi kwenye mpira, kuanzia mifumo, afya tiba, afya lishe na miundo yote ambayo portifolio hutoka Shirikisho (TFF) Klabu zinaenda kutekeleza mifumo hiyo na kuadjust baadhi ya maeneo halafu Vijana wakienda Clinics za Kitaifa wanaenda kukazia tu. Swali linakuja Je Waukaye @zakazakazi FALSAFA ya Tanzania kwenye mpira wa Miguu ni ipi? Iliwasilishwa lini? Anayo nani? Hilo ni Jukumu la TFF ambalo halijatekelezwa, kuna kitu kinaitwa TALENT ID FRAMEWORK ili kupata Vijana je tunayo? Ipoje, anayo nani? Inasemaje? Klabu hazina Mwongozo kutoka kwa TFF? Academy zote nchini zipite humo LAZIMA TFF wafanye wanachoweza, tupo katikati, TFF ASIMAMIE HILO KIKAMILIFU. TFF wasiende mbali waende tu hapo Uganda ilipo FUFA, wana Talent ID Framework ambayo Mashirikisho yoote yalipigwa huo Msasa sambamba na Kamati zao tendaji, ndio maana Uganda wapo mbali mno kwenye soka la Vijana kwenye Klabu zao na National Team, kwasababu wana ramani wanaifuata, wameintergrate mfumo wao na FIFA Talent Development Schemes (TDS) je sisi lini tutaforce Klabu zipite humo? TFF anajipa majukumu ambayo mengine sio ya kwake, kujadili mikataba ya kibiashara sio Jukumu lake bali Vilabu na Bodi yao, TFF anabaki kama Baba pekee, duniani kote TFF zao zina majukumu yao ukitoa michuano ya FA na Ngao basi Ligi Kuu sio mali yao, TFF ASIMAMIE HASWA JUKUMU LA MAENDELEO NI LAKE.