Rais wa Senegal aagiza kuondolewa kwa picha zake katika ofisi za umma.
Rais wa Senegal, Bassirou Diomaye Faye, ametoa agizo rasmi linalowataka Afisa wote wa umma nchini humo kuondoa picha zake katika ofisi zote za serikali.
Katika hotuba yake kwa taifa, Rais Faye anayehesabiwa miongoni mwa Viongozi vijana zaidi barani Afrika, alisisitiza kuwa nafasi yake ni ya kulitumikia taifa, si kuabudiwa au kupewa hadhi ya kipekee kupita kiasi.
Akizungumza kwa msisitizo, Kiongozi huyo alisema: “Sitaki picha yangu katika ofisi zenu, kwa sababu mimi si Mungu wala mimi si sanamu bali mimi ni Mtumishi wa taifa.”
Kauli hiyo imeibua mjadala mpana kuhusu mtazamo wake wa uongozi unaolenga unyenyekevu na uwajibikaji ndani ya utumishi wa umma.
Mbali na kuagiza kuondolewa kwa picha zake, Rais Faye aliwataka Watumishi wa umma kuweka picha za Watoto wao katika ofisi zao kama njia ya kujikumbusha wajibu wao kwa familia na taifa. Kwa mujibu wake, hatua hiyo itasaidia kuongeza ari ya uwajibikaji kazini.
Alisema: “Badala yake wekeni picha za Watoto wenu ili uweze kuziangalia wakati wowote unapotaka kuwa mvivu au kutowajibika.”
Wachambuzi wa masuala ya siasa wanaona hatua hiyo kama ishara ya kujaribu kubadili utamaduni wa kisiasa unaoweka kiongozi katikati ya taasisi, na badala yake kuhimiza mfumo unaotanguliza misingi ya utumishi na uwajibikaji.
Hatua ya Rais Faye inaonekana kuendana na ahadi zake za kampeni zilizolenga mageuzi, uwazi na kurejesha imani ya Wananchi kwa taasisi za umma nchini Senegal.
Toa maoni yako
#Habari
Rais wa Senegal, Bassirou Diomaye Faye, ametoa agizo rasmi linalowataka Afisa wote wa umma nchini humo kuondoa picha zake katika ofisi zote za serikali.
Katika hotuba yake kwa taifa, Rais Faye anayehesabiwa miongoni mwa Viongozi vijana zaidi barani Afrika, alisisitiza kuwa nafasi yake ni ya kulitumikia taifa, si kuabudiwa au kupewa hadhi ya kipekee kupita kiasi.
Akizungumza kwa msisitizo, Kiongozi huyo alisema: “Sitaki picha yangu katika ofisi zenu, kwa sababu mimi si Mungu wala mimi si sanamu bali mimi ni Mtumishi wa taifa.”
Kauli hiyo imeibua mjadala mpana kuhusu mtazamo wake wa uongozi unaolenga unyenyekevu na uwajibikaji ndani ya utumishi wa umma.
Mbali na kuagiza kuondolewa kwa picha zake, Rais Faye aliwataka Watumishi wa umma kuweka picha za Watoto wao katika ofisi zao kama njia ya kujikumbusha wajibu wao kwa familia na taifa. Kwa mujibu wake, hatua hiyo itasaidia kuongeza ari ya uwajibikaji kazini.
Alisema: “Badala yake wekeni picha za Watoto wenu ili uweze kuziangalia wakati wowote unapotaka kuwa mvivu au kutowajibika.”
Wachambuzi wa masuala ya siasa wanaona hatua hiyo kama ishara ya kujaribu kubadili utamaduni wa kisiasa unaoweka kiongozi katikati ya taasisi, na badala yake kuhimiza mfumo unaotanguliza misingi ya utumishi na uwajibikaji.
Hatua ya Rais Faye inaonekana kuendana na ahadi zake za kampeni zilizolenga mageuzi, uwazi na kurejesha imani ya Wananchi kwa taasisi za umma nchini Senegal.
Toa maoni yako
#Habari
0 Commentaires
0 Parts
3 Vue