-
-
-
-
-
Cristiano Ronaldo amkingia kifua Garnacho: “Waacheni Watoto wafurahie mpira”.
Cristiano Ronaldo ameibuka na kutetea kijana wa Manchester United, Alejandro Garnacho, kufuatia malalamiko kutoka kwa baadhi ya mashabiki wa Argentina wanaompinga kuiga mtindo wa kusherehekea mabao wa Ronaldo anapofunga mabao.
Katika mahojiano yake ya hivi karibuni, Ronaldo alionyesha mshangao wake juu ya jinsi mashabiki wa Argentina wanavyomshambulia Garnacho kwa sababu ya kusherehekea kama yeye badala ya Lionel Messi, ambaye ni Mchezaji wa taifa lao.
“Nchini Argentina, wanasema Garnacho asisherehekee kama Cristiano, kwamba si jambo jema. Ninaliona hilo kuwa la ajabu, ni Mtoto tu, waacheni acheze,” alisema Ronaldo kwa msisitizo.
Nyota huyo mwenye mafanikio makubwa pia aliongeza kuwa hajawahi kuwazuia Wachezaji wa Ureno kumpenda Messi, akisema: "Sijawahi kumwambia Mchezaji yeyote wa Ureno asimpenda Messi.”
Kauli hii ya Ronaldo imepokelewa kwa hisia tofauti mtandaoni, huku wengi wakimpongeza kwa kukubali tofauti na kuonyesha ukomavu wa hali ya juu katika soka. Ronaldo na Messi wamekuwa wakilinganishwa kwa miaka mingi, lakini kauli hii inaonesha dalili ya kuheshimiana zaidi kuliko ushindani.
Mashabiki wanaendelea kufuatilia kwa karibu uhusiano huu unaoibuka kati ya kizazi kipya kama Garnacho na Wachezaji wakongwe waliowatangulia.
Cristiano Ronaldo amkingia kifua Garnacho: “Waacheni Watoto wafurahie mpira”. Cristiano Ronaldo ameibuka na kutetea kijana wa Manchester United, Alejandro Garnacho, kufuatia malalamiko kutoka kwa baadhi ya mashabiki wa Argentina wanaompinga kuiga mtindo wa kusherehekea mabao wa Ronaldo anapofunga mabao. Katika mahojiano yake ya hivi karibuni, Ronaldo alionyesha mshangao wake juu ya jinsi mashabiki wa Argentina wanavyomshambulia Garnacho kwa sababu ya kusherehekea kama yeye badala ya Lionel Messi, ambaye ni Mchezaji wa taifa lao. “Nchini Argentina, wanasema Garnacho asisherehekee kama Cristiano, kwamba si jambo jema. Ninaliona hilo kuwa la ajabu, ni Mtoto tu, waacheni acheze,” alisema Ronaldo kwa msisitizo. Nyota huyo mwenye mafanikio makubwa pia aliongeza kuwa hajawahi kuwazuia Wachezaji wa Ureno kumpenda Messi, akisema: "Sijawahi kumwambia Mchezaji yeyote wa Ureno asimpenda Messi.” Kauli hii ya Ronaldo imepokelewa kwa hisia tofauti mtandaoni, huku wengi wakimpongeza kwa kukubali tofauti na kuonyesha ukomavu wa hali ya juu katika soka. Ronaldo na Messi wamekuwa wakilinganishwa kwa miaka mingi, lakini kauli hii inaonesha dalili ya kuheshimiana zaidi kuliko ushindani. Mashabiki wanaendelea kufuatilia kwa karibu uhusiano huu unaoibuka kati ya kizazi kipya kama Garnacho na Wachezaji wakongwe waliowatangulia.0 Comments ·0 Shares ·289 Views -
NASA yatahadharisha: uwezekano wa Dunia kukosa oksijeni Katika miaka ijayo.
Shirika la Kitaifa la Anga na Nafasi ya Juu la Marekani (NASA) limetoa taarifa ya kisayansi inayoashiria uwezekano wa kutoweka kwa hewa safi ya oksijeni duniani katika kipindi cha miaka mingi ijayo.
Kwa mujibu wa NASA, jambo hili halitasababishwa na shughuli za kibinadamu kama vile uchafuzi wa mazingira pekee, bali linahusiana zaidi na mabadiliko ya kiasili ya Dunia na Jua. Katika uchambuzi wake, NASA inabainisha kuwa:
"Katika mabilioni ya miaka iliyopita, Dunia haikuwa na oksijeni ya kutosha. Kwa hiyo, kuna uwezekano kuwa hali kama hiyo ikajirudia tena katika mamilioni ya miaka ijayo," wamesema watafiti wa NASA.
Hali hii inaweza kuathiri sio tu maisha ya binadamu bali pia viumbe hai wote wanaotegemea oksijeni kuishi. Ingawa ni tukio linalotabiriwa kutokea baada ya mamilioni ya miaka, Wanasayansi wanasema ni muhimu kwa jamii ya kimataifa kulielewa na kuendelea na utafiti zaidi kuhusu maisha ya baadaye ya Dunia.
Kwa sasa, hakuna sababu ya hofu ya moja kwa moja, lakini onyo hili linaongeza msisitizo juu ya umuhimu wa kulinda mazingira na kuelewa kwa kina mfumo wa ikolojia wa sayari yetu.
Toa maoni yakoNASA yatahadharisha: uwezekano wa Dunia kukosa oksijeni Katika miaka ijayo. Shirika la Kitaifa la Anga na Nafasi ya Juu la Marekani (NASA) limetoa taarifa ya kisayansi inayoashiria uwezekano wa kutoweka kwa hewa safi ya oksijeni duniani katika kipindi cha miaka mingi ijayo. Kwa mujibu wa NASA, jambo hili halitasababishwa na shughuli za kibinadamu kama vile uchafuzi wa mazingira pekee, bali linahusiana zaidi na mabadiliko ya kiasili ya Dunia na Jua. Katika uchambuzi wake, NASA inabainisha kuwa: "Katika mabilioni ya miaka iliyopita, Dunia haikuwa na oksijeni ya kutosha. Kwa hiyo, kuna uwezekano kuwa hali kama hiyo ikajirudia tena katika mamilioni ya miaka ijayo," wamesema watafiti wa NASA. Hali hii inaweza kuathiri sio tu maisha ya binadamu bali pia viumbe hai wote wanaotegemea oksijeni kuishi. Ingawa ni tukio linalotabiriwa kutokea baada ya mamilioni ya miaka, Wanasayansi wanasema ni muhimu kwa jamii ya kimataifa kulielewa na kuendelea na utafiti zaidi kuhusu maisha ya baadaye ya Dunia. Kwa sasa, hakuna sababu ya hofu ya moja kwa moja, lakini onyo hili linaongeza msisitizo juu ya umuhimu wa kulinda mazingira na kuelewa kwa kina mfumo wa ikolojia wa sayari yetu. Toa maoni yako0 Comments ·0 Shares ·283 Views -
-
Israel yasema itaendelea kusimamia usalama Gaza, licha ya makubaliano ya usitishaji vita.
Katika taarifa mpya iliyoibua mijadala ya kisiasa na kidiplomasia, Serikali ya Israel imesisitiza kuwa haitakubali kuachia jukumu la usalama wa Ukanda wa Gaza mikononi mwa vikosi vya kimataifa, licha ya kusaini makubaliano ya usitishaji vita yaliyosimamiwa na Marekani.
Kupitia kikao na Baraza lake la Mawaziri, Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, alinukuliwa akisema:
“Israel itaamua yenyewe ni lini na wapi itaendelea kuwakabili maadui zake. Hatutakubali kabisa nchi yoyote kutuamulia kuhusu usalama wetu.”
Kauli hiyo imekuja muda mfupi baada ya makubaliano ya muda ya usitishaji mapigano kuwasilishwa, yakiruhusu kuundwa kwa kikosi cha kimataifa kitakacholinda amani na usambazaji wa misaada ya kibinadamu ndani ya Gaza.
Kulingana na taarifa zilizotolewa, kikosi hicho kitapangwa kutoka mataifa ya Kiarabu au Kiislamu, na kazi yake kuu itakuwa kuhakikisha usalama wa Raia na kusimamia utekelezaji wa masharti ya kusitisha vita.
Hata hivyo, Netanyahu ameeleza wasiwasi mkubwa juu ya mpango huo:
“Tutashirikiana pale inapobidi, lakini hatutawahi kukubali Gaza kuwa chini ya mamlaka ya nje bila ridhaa ya Israel. Usalama wa Raia wetu ndio kipaumbele cha kwanza.”
Kwa mujibu wa Afisa wa Marekani, makubaliano haya ni sehemu ya juhudi za muda mrefu kurejesha utulivu katika eneo hilo, lakini yanategemea ushirikiano wa pande zote mbili, jambo ambalo linazidi kuonekana kuwa gumu kutokana na msimamo wa Israel.
Hii ni ishara kwamba licha ya mapendekezo ya kimataifa, Israel bado inashikilia msimamo wake wa kulinda mamlaka kamili ya usalama ndani ya Gaza, hatua inayoweza kuchelewesha utekelezaji wa makubaliano haya mapya.
Je, Israel inaweza kusimamia amani Gaza bila msaada wa Jumuiya ya kimataifa? Au je, dunia inapaswa kuingilia kati kwa nguvu zaidi?
Toa maoni yakoIsrael yasema itaendelea kusimamia usalama Gaza, licha ya makubaliano ya usitishaji vita. Katika taarifa mpya iliyoibua mijadala ya kisiasa na kidiplomasia, Serikali ya Israel imesisitiza kuwa haitakubali kuachia jukumu la usalama wa Ukanda wa Gaza mikononi mwa vikosi vya kimataifa, licha ya kusaini makubaliano ya usitishaji vita yaliyosimamiwa na Marekani. Kupitia kikao na Baraza lake la Mawaziri, Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, alinukuliwa akisema: “Israel itaamua yenyewe ni lini na wapi itaendelea kuwakabili maadui zake. Hatutakubali kabisa nchi yoyote kutuamulia kuhusu usalama wetu.” Kauli hiyo imekuja muda mfupi baada ya makubaliano ya muda ya usitishaji mapigano kuwasilishwa, yakiruhusu kuundwa kwa kikosi cha kimataifa kitakacholinda amani na usambazaji wa misaada ya kibinadamu ndani ya Gaza. Kulingana na taarifa zilizotolewa, kikosi hicho kitapangwa kutoka mataifa ya Kiarabu au Kiislamu, na kazi yake kuu itakuwa kuhakikisha usalama wa Raia na kusimamia utekelezaji wa masharti ya kusitisha vita. Hata hivyo, Netanyahu ameeleza wasiwasi mkubwa juu ya mpango huo: “Tutashirikiana pale inapobidi, lakini hatutawahi kukubali Gaza kuwa chini ya mamlaka ya nje bila ridhaa ya Israel. Usalama wa Raia wetu ndio kipaumbele cha kwanza.” Kwa mujibu wa Afisa wa Marekani, makubaliano haya ni sehemu ya juhudi za muda mrefu kurejesha utulivu katika eneo hilo, lakini yanategemea ushirikiano wa pande zote mbili, jambo ambalo linazidi kuonekana kuwa gumu kutokana na msimamo wa Israel. Hii ni ishara kwamba licha ya mapendekezo ya kimataifa, Israel bado inashikilia msimamo wake wa kulinda mamlaka kamili ya usalama ndani ya Gaza, hatua inayoweza kuchelewesha utekelezaji wa makubaliano haya mapya. Je, Israel inaweza kusimamia amani Gaza bila msaada wa Jumuiya ya kimataifa? Au je, dunia inapaswa kuingilia kati kwa nguvu zaidi? Toa maoni yako0 Comments ·0 Shares ·546 Views -
Klabu zilizofuzu kuingia hatua ya Makundi klabu bingwa barani Afrika (CAF Champignons League) huku kukiwa kumesalia klabu mbili pekee.
FC St-Éloi Lupopo
Stade Malien de Bamako
Young Africans
Simba SC
Mamelodi Sundowns
Al Hilal SC
Rivers United
Power Dynamos
Atlético Petróleos de Luanda
Al Ahly
AS FAR
JS Kabylie
MC Alger
Esperance Sportive de Tunis
Al Ahly Tripoli 1-1 RS Berkane
Ethiopian Insurance 1-1 Pyramids FCKlabu zilizofuzu kuingia hatua ya Makundi klabu bingwa barani Afrika (CAF Champignons League) huku kukiwa kumesalia klabu mbili pekee. 🇨🇩 FC St-Éloi Lupopo 🇲🇱 Stade Malien de Bamako 🇹🇿 Young Africans 🇹🇿 Simba SC 🇿🇦 Mamelodi Sundowns 🇸🇩 Al Hilal SC 🇳🇬 Rivers United 🇿🇲 Power Dynamos 🇦🇴 Atlético Petróleos de Luanda 🇪🇬 Al Ahly 🇲🇦 AS FAR 🇩🇿 JS Kabylie 🇩🇿 MC Alger 🇹🇳 Esperance Sportive de Tunis 🇱🇾 Al Ahly Tripoli 1-1 🇲🇦 RS Berkane 🇪🇹 Ethiopian Insurance 1-1 🇪🇬 Pyramids FC0 Comments ·0 Shares ·338 Views -
-
-
-
-
-
-
"Nani alaumiwe? Anaweza kuwa Injinia Hersi Said mwenyewe. Yanga ilifika fainali za Shirikisho miaka ya karibuni. Yanga ilitolewa robo fainali. Yanga ilitolewa pia makundi. Hersi anajua ndoto za Wanayanga. Huwa wananyanyasika kwa mashabiki wa mtani zao kwa kutofanya vizuri katika michuano ya CAF. Ligi ya Mabingwa.
.
Wakati huu wakiwa wamesajili wachezaji wazuri huku akiendelea kumiliki wachezaji mafundi kama kina Pacome Zouzoua, Hersi akaitafutia Yanga kocha mwanafunzi.
Ukitazama wasifu wa Folz, alikuwa amepita katika klabu kadhaa akiwa kama kocha msaidizi. Hersi na wenzake walikuwa wamecheza kamari kwa kumleta Folz. Hajawahi kuwa kocha mkuu wala kutwaa taji lolote muhimu katika maisha yake ya mpira.
Unawezaje kutimiza ndoto zako ukiwa na kocha wa namna hii. Katika lugha ya mtaani ya Waingereza tunaweza kusema Hersi na wenzake walikuwa wamecheza kamari. ‘Gambling’. Haukuwa muda wa Yanga kucheza bahati nasibu.
Ulikuwa muda wa wao kuwa na kocha ambaye ana uzoefu na anaweza kuishi katika falsafa zao. Matokeo yake Yanga wamejiweka katika hatari. Wameshafungwa ugenini na wageni wao wanaweza kuja na mbinu za ajabu. Injinia Hersi na wenzake ambao wanaongoza Yanga sasa hivi hawakufikiria kama wanaweza kuwa katika nafasi hii kwa sasa. Wakati wao wanaiwaza nusu fainali au fainali, tayari wapo hatarini kutofika hata makundi.
- Edo Kumwembe, Mchambuzi."Nani alaumiwe? Anaweza kuwa Injinia Hersi Said mwenyewe. Yanga ilifika fainali za Shirikisho miaka ya karibuni. Yanga ilitolewa robo fainali. Yanga ilitolewa pia makundi. Hersi anajua ndoto za Wanayanga. Huwa wananyanyasika kwa mashabiki wa mtani zao kwa kutofanya vizuri katika michuano ya CAF. Ligi ya Mabingwa. . Wakati huu wakiwa wamesajili wachezaji wazuri huku akiendelea kumiliki wachezaji mafundi kama kina Pacome Zouzoua, Hersi akaitafutia Yanga kocha mwanafunzi. 😀 Ukitazama wasifu wa Folz, alikuwa amepita katika klabu kadhaa akiwa kama kocha msaidizi. Hersi na wenzake walikuwa wamecheza kamari kwa kumleta Folz. Hajawahi kuwa kocha mkuu wala kutwaa taji lolote muhimu katika maisha yake ya mpira. Unawezaje kutimiza ndoto zako ukiwa na kocha wa namna hii. Katika lugha ya mtaani ya Waingereza tunaweza kusema Hersi na wenzake walikuwa wamecheza kamari. ‘Gambling’. Haukuwa muda wa Yanga kucheza bahati nasibu. Ulikuwa muda wa wao kuwa na kocha ambaye ana uzoefu na anaweza kuishi katika falsafa zao. Matokeo yake Yanga wamejiweka katika hatari. Wameshafungwa ugenini na wageni wao wanaweza kuja na mbinu za ajabu. Injinia Hersi na wenzake ambao wanaongoza Yanga sasa hivi hawakufikiria kama wanaweza kuwa katika nafasi hii kwa sasa. Wakati wao wanaiwaza nusu fainali au fainali, tayari wapo hatarini kutofika hata makundi. - Edo Kumwembe, Mchambuzi.0 Comments ·0 Shares ·482 Views -
Iran yakataa mazungumzo na Trump, yakanusha madai ya uharibifu wa nyuklia.
Katika kile kinachoonekana kuwa kuendelea kwa mvutano wa kidiplomasia kati ya Marekani na Iran, Kiongozi Mkuu wa Iran, Ayatollah Ali Khamenei, ameibuka hadharani na kukataa pendekezo la Rais wa Marekani, Donald Trump, la kurejea kwenye meza ya mazungumzo.
Akizungumza kupitia vyombo vya habari vya Serikali, Khamenei alisema wazi kuwa pendekezo la Trump halikuwa la kweli, bali ni jaribio la kulazimisha makubaliano kwa njia ya vitisho.
"Trump anasema yeye ni Mtaalamu wa kufanikisha makubaliano, lakini kama makubaliano hayo yanaambatana na shinikizo na matokeo yake tayari yameamuliwa, basi hiyo siyo makubaliano bali ni kulazimisha na vitisho," - Ayatollah Ali Khamenei.
Kauli hiyo ya Khamenei imekuja kufuatia hotuba ya Trump wiki iliyopita, ambapo aliwaambia Wabunge wa Israel kwamba Marekani ingependa kufanikisha makubaliano ya amani na Tehran, hasa baada ya kutangazwa kwa usitishaji mapigano kati ya Israel na Hamas huko Gaza. Katika hotuba hiyo, Trump pia alidai kuwa:
"Marekani imeharibu kabisa maeneo ya nyuklia ya Iran."
Lakini Khamenei alikanusha vikali kauli hiyo, akisema:
"Rais wa Marekani anajivunia kusema kuwa wamebomoa na kuharibu sekta ya nyuklia ya Iran. Vizuri, endeleeni kuota!"
Kauli hizi zinaashiria kuwa uhusiano kati ya Tehran na Washington bado uko katika hali ya sintofahamu, huku Iran ikionekana kuchukua msimamo mkali dhidi ya kile inachokiona kama mbinu za mabeberu.
Kwa sasa, haijafahamika kama juhudi za kidiplomasia zitaendelea, hasa ikizingatiwa kuwa Iran bado inashikilia haki yake ya kuendesha mpango wake wa nyuklia kama nchi huru.
Je, unadhani mvutano huu unaweza kuzua mgogoro mpya wa kimataifa?
Toa maoni yakoIran yakataa mazungumzo na Trump, yakanusha madai ya uharibifu wa nyuklia. Katika kile kinachoonekana kuwa kuendelea kwa mvutano wa kidiplomasia kati ya Marekani na Iran, Kiongozi Mkuu wa Iran, Ayatollah Ali Khamenei, ameibuka hadharani na kukataa pendekezo la Rais wa Marekani, Donald Trump, la kurejea kwenye meza ya mazungumzo. Akizungumza kupitia vyombo vya habari vya Serikali, Khamenei alisema wazi kuwa pendekezo la Trump halikuwa la kweli, bali ni jaribio la kulazimisha makubaliano kwa njia ya vitisho. "Trump anasema yeye ni Mtaalamu wa kufanikisha makubaliano, lakini kama makubaliano hayo yanaambatana na shinikizo na matokeo yake tayari yameamuliwa, basi hiyo siyo makubaliano bali ni kulazimisha na vitisho," - Ayatollah Ali Khamenei. Kauli hiyo ya Khamenei imekuja kufuatia hotuba ya Trump wiki iliyopita, ambapo aliwaambia Wabunge wa Israel kwamba Marekani ingependa kufanikisha makubaliano ya amani na Tehran, hasa baada ya kutangazwa kwa usitishaji mapigano kati ya Israel na Hamas huko Gaza. Katika hotuba hiyo, Trump pia alidai kuwa: "Marekani imeharibu kabisa maeneo ya nyuklia ya Iran." Lakini Khamenei alikanusha vikali kauli hiyo, akisema: "Rais wa Marekani anajivunia kusema kuwa wamebomoa na kuharibu sekta ya nyuklia ya Iran. Vizuri, endeleeni kuota!" Kauli hizi zinaashiria kuwa uhusiano kati ya Tehran na Washington bado uko katika hali ya sintofahamu, huku Iran ikionekana kuchukua msimamo mkali dhidi ya kile inachokiona kama mbinu za mabeberu. Kwa sasa, haijafahamika kama juhudi za kidiplomasia zitaendelea, hasa ikizingatiwa kuwa Iran bado inashikilia haki yake ya kuendesha mpango wake wa nyuklia kama nchi huru. Je, unadhani mvutano huu unaweza kuzua mgogoro mpya wa kimataifa? Toa maoni yako0 Comments ·0 Shares ·403 Views -
-
Burkina Faso yatangaza utaratibu mpya wa kusimamia fedha za mashirika yasiyo ya kiserikali (NGOs).
Serikali ya Burkina Faso imechukua hatua mpya ya kuhakikisha uwazi na usimamizi madhubuti wa fedha zinazotumiwa na mashirika yasiyo ya kiserikali (NGOs) Nchini humo. Kuanzia sasa, mashirika yote yatahitajika kufungua akaunti katika Benki ya Kitaifa ya Amana ya Hazina (National Bank of Deposits of the Treasury).
Uamuzi huo unalenga kufuatilia kwa karibu michakato ya kifedha ya mashirika hayo, na kuhakikisha kuwa fedha zinazotoka kwa wahisani zinatumika kwa madhumuni yaliyokusudiwa kwa uwazi na uwajibikaji wa hali ya juu.
Hatua hii imezua mijadala kwenye majukwaa ya kijamii na ndani ya mashirika husika, ambapo baadhi wanaitazama kama njia ya kuimarisha nidhamu ya kifedha, huku wengine wakihofia kuingiliwa kwa uhuru wa mashirika ya kiraia.
Serikali bado haijatoa taarifa ya kina kuhusu jinsi utekelezaji wa agizo hili utakavyofanyika, wala ikiwa kutakuwepo na muda maalum wa mpito kwa mashirika hayo kuhamia mfumo huo mpya wa kifedha.
Toa maoni yakoBurkina Faso yatangaza utaratibu mpya wa kusimamia fedha za mashirika yasiyo ya kiserikali (NGOs). Serikali ya Burkina Faso imechukua hatua mpya ya kuhakikisha uwazi na usimamizi madhubuti wa fedha zinazotumiwa na mashirika yasiyo ya kiserikali (NGOs) Nchini humo. Kuanzia sasa, mashirika yote yatahitajika kufungua akaunti katika Benki ya Kitaifa ya Amana ya Hazina (National Bank of Deposits of the Treasury). Uamuzi huo unalenga kufuatilia kwa karibu michakato ya kifedha ya mashirika hayo, na kuhakikisha kuwa fedha zinazotoka kwa wahisani zinatumika kwa madhumuni yaliyokusudiwa kwa uwazi na uwajibikaji wa hali ya juu. Hatua hii imezua mijadala kwenye majukwaa ya kijamii na ndani ya mashirika husika, ambapo baadhi wanaitazama kama njia ya kuimarisha nidhamu ya kifedha, huku wengine wakihofia kuingiliwa kwa uhuru wa mashirika ya kiraia. Serikali bado haijatoa taarifa ya kina kuhusu jinsi utekelezaji wa agizo hili utakavyofanyika, wala ikiwa kutakuwepo na muda maalum wa mpito kwa mashirika hayo kuhamia mfumo huo mpya wa kifedha. Toa maoni yako0 Comments ·0 Shares ·409 Views -
-
AYRA STARR AANDIKA HISTORIA KWENYE YOUTUBE KUPITIA WIMBO WAKE “RUSH”.
Nyota wa muziki kutoka Nigeria, Ayra Starr, ameweka rekodi ya kipekee na kuandika jina lake kwenye vitabu vya historia ya burudani barani Afrika. Kupitia wimbo wake maarufu Rush, Ayra Starr amekuwa Msanii wa kwanza wa kike barani Afrika kufikisha zaidi ya Watazamaji milioni 500 kwenye mtandao wa YouTube kwa wimbo mmoja wa solo.
Kupitia ukurasa wake rasmi wa Instagram, Ayra alishiriki furaha yake kwa mafanikio hayo na kusema:
“Sauti ya Gen-Z kutoka Afrika inasikika! Rush imefanya historia, na hii ni mwanzo tu.”
Kwa mafanikio haya, Rush imejiunga na orodha ya video tano bora za muziki za Kiafrika zilizotazamwa zaidi kila wakati kwenye YouTube.
- Calm Down : Rema
- Jerusalema : Master KG ft. Nomcebo Zikode
- Love Nwantiti : CKay
- Magic In The Air : Magic System
Kinachovutia zaidi ni kwamba, licha ya umaarufu wa Wasanii kama Burna Boy, Wizkid, Davido, pamoja na wakali wa kimataifa kama NBA YoungBoy, Polo G, Lil Tjay, NLE Choppa, na Lil Durk, hakuna hata mmoja wao ambaye amewahi kufikisha Watazamaji zaidi ya milioni 500 kwa wimbo mmoja wa solo kwenye jukwaa la YouTube tofauti na Ayra Starr.
Rekodi hii inaendelea kuimarisha nafasi ya Ayra Starr kama sauti muhimu ya kizazi kipya cha muziki barani Afrika, hasa kwa kizazi cha Gen-Z, na kuonyesha ukuaji wa ushawishi wa Wanawake kwenye tasnia ya muziki wa kimataifa.
“Rush is not just a song, it’s a movement.” - Ayra Starr
Pongezi kwa Ayra kwa kuwakilisha Afrika kwa kishindo duniani!AYRA STARR AANDIKA HISTORIA KWENYE YOUTUBE KUPITIA WIMBO WAKE “RUSH”. Nyota wa muziki kutoka Nigeria, Ayra Starr, ameweka rekodi ya kipekee na kuandika jina lake kwenye vitabu vya historia ya burudani barani Afrika. Kupitia wimbo wake maarufu Rush, Ayra Starr amekuwa Msanii wa kwanza wa kike barani Afrika kufikisha zaidi ya Watazamaji milioni 500 kwenye mtandao wa YouTube kwa wimbo mmoja wa solo. Kupitia ukurasa wake rasmi wa Instagram, Ayra alishiriki furaha yake kwa mafanikio hayo na kusema: “Sauti ya Gen-Z kutoka Afrika inasikika! Rush imefanya historia, na hii ni mwanzo tu.” Kwa mafanikio haya, Rush imejiunga na orodha ya video tano bora za muziki za Kiafrika zilizotazamwa zaidi kila wakati kwenye YouTube. - Calm Down : Rema - Jerusalema : Master KG ft. Nomcebo Zikode - Love Nwantiti : CKay - Magic In The Air : Magic System Kinachovutia zaidi ni kwamba, licha ya umaarufu wa Wasanii kama Burna Boy, Wizkid, Davido, pamoja na wakali wa kimataifa kama NBA YoungBoy, Polo G, Lil Tjay, NLE Choppa, na Lil Durk, hakuna hata mmoja wao ambaye amewahi kufikisha Watazamaji zaidi ya milioni 500 kwa wimbo mmoja wa solo kwenye jukwaa la YouTube tofauti na Ayra Starr. Rekodi hii inaendelea kuimarisha nafasi ya Ayra Starr kama sauti muhimu ya kizazi kipya cha muziki barani Afrika, hasa kwa kizazi cha Gen-Z, na kuonyesha ukuaji wa ushawishi wa Wanawake kwenye tasnia ya muziki wa kimataifa. “Rush is not just a song, it’s a movement.” - Ayra Starr Pongezi kwa Ayra kwa kuwakilisha Afrika kwa kishindo duniani!0 Comments ·0 Shares ·726 Views -
-
Arnold Schwarzenegger awasilisha mpango wa kuokoa demokrasia Marekani.
Mwigizaji Nguli wa Hollywood na Gavana wa zamani wa Jimbo la California, Arnold Schwarzenegger, ameibuka na pendekezo la kina la kuimarisha demokrasia Nchini Marekani. Katika mahojiano yake kwenye kipindi maarufu cha Real Time with Bill Maher, Schwarzenegger alifichua mpango wa hatua tatu ambao anauona kama njia ya “kupatanisha pande zote mbili” yaani Republican na Democratic. Katika maelezo yake rasmi, Schwarzenegger alisema:
“Tunapaswa kutangaza Siku ya Uchaguzi kuwa likizo ya kitaifa, kuhakikisha kuwa ramani za kisiasa zinatengenezwa na tume huru zisizoegemea upande wowote, na kuimarisha mifumo ya utambulisho wa wapiga kura.”
Mpango huu, ambao una lengo la kuhamasisha ushiriki mpana wa Wananchi na kulinda uadilifu wa chaguzi, umeungwa mkono na hoja za kisera zinazoegemea misingi ya haki, usawa na uwazi.
Schwarzenegger pia hakusita kuelezea wasiwasi wake kuhusu Pendekezo la 50 la California, akiliona kama:
“Hila kubwa ambayo inaweza kurudisha ramani za uchaguzi mikononi mwa Wanasiasa badala ya Wataalamu huru.”
Kwa mujibu wake, hatua hiyo ya kuruhusu Wanasiasa kushiriki katika uundwaji wa ramani ya majimbo inaweza kuathiri vibaya uwakilishi wa haki kwa Wananchi.
Mpango huu wa Schwarzenegger una mvuto wa kipekee kwa kuwa unachanganya ushawishi wa jina kubwa na hoja nzito za kisera. Hata hivyo, utekelezaji wake unategemea mabadiliko ya kisheria, mjadala wa kina wa kitaifa, na maridhiano kati ya vyama viwili vikuu vya siasa.
Kwa mujibu wa Wachambuzi wa siasa za Marekani, hoja za Schwarzenegger zinaibua maswali mapana kuhusu:
- Usawa katika chaguzi,
- Usalama wa mfumo wa upigaji kura,
- Na mwelekeo wa demokrasia ya Marekani kwa vizazi vijavyo.
Mpaka sasa, bado haijajulikana iwapo pendekezo hili litaungwa mkono na Wabunge, lakini bila shaka, Schwarzenegger amejipambanua tena, safari hii siyo kwenye sinema au siasa za majimbo tu, bali kwenye uwanja mpana wa mustakabali wa kidemokrasia wa taifa lake.
Arnold Schwarzenegger awasilisha mpango wa kuokoa demokrasia Marekani. Mwigizaji Nguli wa Hollywood na Gavana wa zamani wa Jimbo la California, Arnold Schwarzenegger, ameibuka na pendekezo la kina la kuimarisha demokrasia Nchini Marekani. Katika mahojiano yake kwenye kipindi maarufu cha Real Time with Bill Maher, Schwarzenegger alifichua mpango wa hatua tatu ambao anauona kama njia ya “kupatanisha pande zote mbili” yaani Republican na Democratic. Katika maelezo yake rasmi, Schwarzenegger alisema: “Tunapaswa kutangaza Siku ya Uchaguzi kuwa likizo ya kitaifa, kuhakikisha kuwa ramani za kisiasa zinatengenezwa na tume huru zisizoegemea upande wowote, na kuimarisha mifumo ya utambulisho wa wapiga kura.” Mpango huu, ambao una lengo la kuhamasisha ushiriki mpana wa Wananchi na kulinda uadilifu wa chaguzi, umeungwa mkono na hoja za kisera zinazoegemea misingi ya haki, usawa na uwazi. Schwarzenegger pia hakusita kuelezea wasiwasi wake kuhusu Pendekezo la 50 la California, akiliona kama: “Hila kubwa ambayo inaweza kurudisha ramani za uchaguzi mikononi mwa Wanasiasa badala ya Wataalamu huru.” Kwa mujibu wake, hatua hiyo ya kuruhusu Wanasiasa kushiriki katika uundwaji wa ramani ya majimbo inaweza kuathiri vibaya uwakilishi wa haki kwa Wananchi. Mpango huu wa Schwarzenegger una mvuto wa kipekee kwa kuwa unachanganya ushawishi wa jina kubwa na hoja nzito za kisera. Hata hivyo, utekelezaji wake unategemea mabadiliko ya kisheria, mjadala wa kina wa kitaifa, na maridhiano kati ya vyama viwili vikuu vya siasa. Kwa mujibu wa Wachambuzi wa siasa za Marekani, hoja za Schwarzenegger zinaibua maswali mapana kuhusu: - Usawa katika chaguzi, - Usalama wa mfumo wa upigaji kura, - Na mwelekeo wa demokrasia ya Marekani kwa vizazi vijavyo. Mpaka sasa, bado haijajulikana iwapo pendekezo hili litaungwa mkono na Wabunge, lakini bila shaka, Schwarzenegger amejipambanua tena, safari hii siyo kwenye sinema au siasa za majimbo tu, bali kwenye uwanja mpana wa mustakabali wa kidemokrasia wa taifa lake.0 Comments ·0 Shares ·567 Views -
Vurugu mitandaoni! Ned Nwoko amvaa Regina Daniels, asema "ameharibu familia yetu".
Mitandao ya kijamii imewaka moto kufuatia tuhuma nzito zilizotolewa na Bilionea na mwanasiasa mashuhuri kutoka Nigeria, Prince Ned Nwoko, dhidi ya Mke wake, Mwigizaji maarufu wa filamu za Nigeria (Nollywood) Regina Daniels. Kupitia chapisho la video kwenye ukurasa wake wa Instagram, Nwoko amemshutumu Regina kwa kile alichokiita "vurugu za kupindukia" pamoja na matumizi mabaya ya dawa za kulevya na pombe.
Katika maneno yake, Ned aliandika: “Hakuwa hivi mwanzo… kile kinachotokea sasa kimeharibu kabisa utulivu wa familia yetu.”
Nwoko alieleza kuwa ndani ya saa 48, Regina alifanya fujo kubwa nyumbani kwao akiwapiga Wafanyakazi watatu wa ndani, kuharibu mali, na kusababisha uharibifu mkubwa bila sababu ya msingi.
Kwa mujibu wa chapisho hilo la Instagram: “Nimetoa masharti ya wazi kwake. Lazima akubali kwenda kwenye tiba ya kuacha dawa, iwe ndani au nje ya Nchi. Vinginevyo, naogopa kwa usalama wake.” - Prince Ned Nwoko.
Katika tuhuma hizo, Ned alimtaja mtu aitwaye Sammy kama Muuzaji mkuu wa dawa kwa Regina, huku pia akilitaja jina la Ann, akisema anahusika katika kile alichokiita “mzunguko wa maovu.”
Tukio hili limetikisa jamii ya mtandaoni, huku baadhi ya mashabiki wakionesha mshangao, wengine wakimtetea Regina, na wengi wakitaka ukweli wa kina juu ya maisha ya kifahari ya wawili hao.
Je, hii ni drama ya ndoa ya Mastaa au kuna jambo kubwa zaidi nyuma ya pazia?
Vurugu mitandaoni! Ned Nwoko amvaa Regina Daniels, asema "ameharibu familia yetu". Mitandao ya kijamii imewaka moto kufuatia tuhuma nzito zilizotolewa na Bilionea na mwanasiasa mashuhuri kutoka Nigeria, Prince Ned Nwoko, dhidi ya Mke wake, Mwigizaji maarufu wa filamu za Nigeria (Nollywood) Regina Daniels. Kupitia chapisho la video kwenye ukurasa wake wa Instagram, Nwoko amemshutumu Regina kwa kile alichokiita "vurugu za kupindukia" pamoja na matumizi mabaya ya dawa za kulevya na pombe. Katika maneno yake, Ned aliandika: “Hakuwa hivi mwanzo… kile kinachotokea sasa kimeharibu kabisa utulivu wa familia yetu.” Nwoko alieleza kuwa ndani ya saa 48, Regina alifanya fujo kubwa nyumbani kwao akiwapiga Wafanyakazi watatu wa ndani, kuharibu mali, na kusababisha uharibifu mkubwa bila sababu ya msingi. Kwa mujibu wa chapisho hilo la Instagram: “Nimetoa masharti ya wazi kwake. Lazima akubali kwenda kwenye tiba ya kuacha dawa, iwe ndani au nje ya Nchi. Vinginevyo, naogopa kwa usalama wake.” - Prince Ned Nwoko. Katika tuhuma hizo, Ned alimtaja mtu aitwaye Sammy kama Muuzaji mkuu wa dawa kwa Regina, huku pia akilitaja jina la Ann, akisema anahusika katika kile alichokiita “mzunguko wa maovu.” Tukio hili limetikisa jamii ya mtandaoni, huku baadhi ya mashabiki wakionesha mshangao, wengine wakimtetea Regina, na wengi wakitaka ukweli wa kina juu ya maisha ya kifahari ya wawili hao. Je, hii ni drama ya ndoa ya Mastaa au kuna jambo kubwa zaidi nyuma ya pazia?0 Comments ·0 Shares ·782 Views -
Alloyce Nyanda
Mtani wangu @gersonmsigwa mbona umekanusha kwa herufi kubwa hivyo ku likes Picha ya Mange
Unajua acha nikusaidie Mtani ufahamu kuwa katika Hii Dunia Serikali zote Duniani huwa zinajaribu kuhakikisha zina “control information
Uki Control Informatio utakuwa na nguvu ya kumuita Malaika-Shetani na shetani ukamuita Malaika na dunia itatii na haitahoji.
Wenye nguvu za utoaji wa taarifa za dunia waliwahi ku control Information na kuuambia ulimwengu kuwa Muammar al-Gaddafi ni gaidi na dunia ikatii amri
Waliandika kwa lugha zao nasi tukatafsiri kwa lugha yetu na tukamuita mwana wa Afrika Gadafi ni Gaidi.
“Information is power”. Sasa wewe badala ya Kupambana ku Control Information wewe unapambana Kukanusha haitakusaidia wewe wala serikali yetu.
Na Ku control Information huwa sio kuzima Internet au kufunga Mitandao kwa sababu wanaotaka taarifa wameshajua watapataje ndio wana VPN na wapo tayari Kulipia
nataka nikushauri Msemaji ukifanyie kazi kwa haraka badala ya kukanusha na kulalamika jenga uwezo wa kumiliki nguvu ya Taarifa iliyokaribu na umma.
Jitaidi Pages za serikali zenye kutoa taarifa zifanye ziwe na nguvu ili ziwe karibu na jamii yake sasa haiwezekani Mange Kimambi awe na ukaribu na jamii kiasi hicho kuliko serikali yenyewe.
Unakuta wizara ya Afya badala ya kutengeneza maudhui yenye kuisogeza jamii karibu nayo wao wanaweza hata kupost picha waziri anasalimiana na Dkt na kuigeuza kuwa jambo la maana kupeleka kwa watu .
Sasa kwa hulka hiyo utawezaje Ku control Power ya Taarifa? ukimkuta Mange amechapa Hospital X haina Vifaa wananchi wanaona huyu ndiye anatusaidia na wewe @gersonmsigwa unabakiza kazi ya kukanusha tu wakati unayo nafasi ya kueleza situation ya Hospital hata kabla ya wengine kupost
Lazima idara za serikali zigeuzwe kuwa na uwezo wa kufanya Visibility kubwa , unadhani wewe Msigwa utaweza peke yako? Utachekwa tu
Utakanusha ma ngapi na utapinga Ma ngapi? maana hata leo kuonekana umelikes page umehaha mbaya why? Wewe Pambana kuifanya Jamii kuiamini serikali zaidi ili wampuuze Mange
Unataka kweli U contol Information kwa mbinu ya Mwijaku au Mzee wangu au Mafufu? (Utaishia kuchekesha tu)
Power of InformationsAlloyce Nyanda ✍️ Mtani wangu @gersonmsigwa mbona umekanusha kwa herufi kubwa hivyo ku likes Picha ya Mange Unajua acha nikusaidie Mtani ufahamu kuwa katika Hii Dunia Serikali zote Duniani huwa zinajaribu kuhakikisha zina “control information Uki Control Informatio utakuwa na nguvu ya kumuita Malaika-Shetani na shetani ukamuita Malaika na dunia itatii na haitahoji. Wenye nguvu za utoaji wa taarifa za dunia waliwahi ku control Information na kuuambia ulimwengu kuwa Muammar al-Gaddafi ni gaidi na dunia ikatii amri Waliandika kwa lugha zao nasi tukatafsiri kwa lugha yetu na tukamuita mwana wa Afrika Gadafi ni Gaidi. “Information is power”. Sasa wewe badala ya Kupambana ku Control Information wewe unapambana Kukanusha haitakusaidia wewe wala serikali yetu. Na Ku control Information huwa sio kuzima Internet au kufunga Mitandao kwa sababu wanaotaka taarifa wameshajua watapataje ndio wana VPN na wapo tayari Kulipia nataka nikushauri Msemaji ukifanyie kazi kwa haraka badala ya kukanusha na kulalamika jenga uwezo wa kumiliki nguvu ya Taarifa iliyokaribu na umma. Jitaidi Pages za serikali zenye kutoa taarifa zifanye ziwe na nguvu ili ziwe karibu na jamii yake sasa haiwezekani Mange Kimambi awe na ukaribu na jamii kiasi hicho kuliko serikali yenyewe. Unakuta wizara ya Afya badala ya kutengeneza maudhui yenye kuisogeza jamii karibu nayo wao wanaweza hata kupost picha waziri anasalimiana na Dkt na kuigeuza kuwa jambo la maana kupeleka kwa watu . Sasa kwa hulka hiyo utawezaje Ku control Power ya Taarifa? ukimkuta Mange amechapa Hospital X haina Vifaa wananchi wanaona huyu ndiye anatusaidia na wewe @gersonmsigwa unabakiza kazi ya kukanusha tu wakati unayo nafasi ya kueleza situation ya Hospital hata kabla ya wengine kupost Lazima idara za serikali zigeuzwe kuwa na uwezo wa kufanya Visibility kubwa , unadhani wewe Msigwa utaweza peke yako? Utachekwa tu Utakanusha ma ngapi na utapinga Ma ngapi? maana hata leo kuonekana umelikes page umehaha mbaya why? Wewe Pambana kuifanya Jamii kuiamini serikali zaidi ili wampuuze Mange Unataka kweli U contol Information kwa mbinu ya Mwijaku au Mzee wangu au Mafufu? (Utaishia kuchekesha tu) Power of Informations0 Comments ·0 Shares ·670 Views
More Stories