DRC SAGA - PART 1

(TAHADHARI: kama wwe ni mpenzi wa udaku au story fupifupi usisome. Hii ni kwa ajili ya watu wenye "solid mind" na wanaopenda kujifunza).
______
Mgogoro wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) umebeba historia ndefu inayohitaji muda mrefu kuielezea, lakini nitajaribu kuifupisha kwa kuangazia mambo machache muhimu.

Mpelelezi wa Kiingereza, John Speke, katika kitabu chake Journal of the Discovery of the Source of the Nile (1863), aliandika kuwa asili ya Watutsi ni Pembe ya Afrika (Ethiopia, Somalia, Djibouti), na kwamba walihama katika karne ya 12 wakielekea eneo la Maziwa Makuu. Walifanya makazi yao katika maeneo ya kaskazini-magharibi mwa Ziwa Tanganyika, eneo ambalo kwa sasa ni Rwanda, Burundi, na Congo. Walipowasili, walikuta wenyeji ambao Wahutu na Watwa, ambao waliishi nao kwa amani. Wahutu na Watwa walikuwa wakulima, huku Watutsi wakiwa wafugaji.

Karne ya 18, wakoloni walipofika, waligawa maeneo ya kiutawala bila kuzingatia mipaka ya kijamii iliyokuwepo. Badala yake, walizingatia maslahi yao binafsi, jambo lililosababisha baadhi ya jamii kugawanyika katika mataifa mawili tofauti. Kwa mfano, jamii ya Wamasai iligawanywa kati ya Kenya na Tanganyika. Wahutu waligawanyika kati ya Rwanda na Burundi, huku Watutsi wakigawanyika Rwanda, Burundi na Congo maeneo ya Kivu kusini.

Watutsi pamoja na kuwa wachache kwa idadi lakini walijikuta wameathirika zaidi kwa kugawanyika maeneo mengi. Waligawanyika katika mataifa matatu tofauti ingawa walikuwa watu wa jamii moja, walioongea lugha moja, wenye mila na desturi zinazofanana.

Baada ya mipaka kuwekwa Watutsi waliojikuta katika eneo la Kivu (Congo) walitengwa na jamii nyingine za watu wa eneo hilo kama Wabembe, Wavira, na Wanyindu. Kwa kuwa sehemu kubwa ya Watutsi ilikua Rwanda, wale waliojikuta Congo walionekana kama wageni (externals) maana walikua 6% tu ya watu wa Kivu.

Walishauriwa kuhamia Rwanda, lakini hawakua wanyarwanda. Ni Wakongomani waliozaliwa hapo. Babu zao walifika hapo karne ya 12 kama nilivyoeleza juu. Kabla ya ukoloni Watutsi wote walikua jamii moja. Lakini baada ya mipaka ya wakoloni wakajikuta wamegawanywa katika nchi 3 tofauti. Sasa wafanjeje?
(Malisa GJ)

DRC SAGA - PART 1 (TAHADHARI: kama wwe ni mpenzi wa udaku au story fupifupi usisome. Hii ni kwa ajili ya watu wenye "solid mind" na wanaopenda kujifunza). ______ Mgogoro wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) umebeba historia ndefu inayohitaji muda mrefu kuielezea, lakini nitajaribu kuifupisha kwa kuangazia mambo machache muhimu. Mpelelezi wa Kiingereza, John Speke, katika kitabu chake Journal of the Discovery of the Source of the Nile (1863), aliandika kuwa asili ya Watutsi ni Pembe ya Afrika (Ethiopia, Somalia, Djibouti), na kwamba walihama katika karne ya 12 wakielekea eneo la Maziwa Makuu. Walifanya makazi yao katika maeneo ya kaskazini-magharibi mwa Ziwa Tanganyika, eneo ambalo kwa sasa ni Rwanda, Burundi, na Congo. Walipowasili, walikuta wenyeji ambao Wahutu na Watwa, ambao waliishi nao kwa amani. Wahutu na Watwa walikuwa wakulima, huku Watutsi wakiwa wafugaji. Karne ya 18, wakoloni walipofika, waligawa maeneo ya kiutawala bila kuzingatia mipaka ya kijamii iliyokuwepo. Badala yake, walizingatia maslahi yao binafsi, jambo lililosababisha baadhi ya jamii kugawanyika katika mataifa mawili tofauti. Kwa mfano, jamii ya Wamasai iligawanywa kati ya Kenya na Tanganyika. Wahutu waligawanyika kati ya Rwanda na Burundi, huku Watutsi wakigawanyika Rwanda, Burundi na Congo maeneo ya Kivu kusini. Watutsi pamoja na kuwa wachache kwa idadi lakini walijikuta wameathirika zaidi kwa kugawanyika maeneo mengi. Waligawanyika katika mataifa matatu tofauti ingawa walikuwa watu wa jamii moja, walioongea lugha moja, wenye mila na desturi zinazofanana. Baada ya mipaka kuwekwa Watutsi waliojikuta katika eneo la Kivu (Congo) walitengwa na jamii nyingine za watu wa eneo hilo kama Wabembe, Wavira, na Wanyindu. Kwa kuwa sehemu kubwa ya Watutsi ilikua Rwanda, wale waliojikuta Congo walionekana kama wageni (externals) maana walikua 6% tu ya watu wa Kivu. Walishauriwa kuhamia Rwanda, lakini hawakua wanyarwanda. Ni Wakongomani waliozaliwa hapo. Babu zao walifika hapo karne ya 12 kama nilivyoeleza juu. Kabla ya ukoloni Watutsi wote walikua jamii moja. Lakini baada ya mipaka ya wakoloni wakajikuta wamegawanywa katika nchi 3 tofauti. Sasa wafanjeje? (Malisa GJ)
0 Comments ·0 Shares ·44 Views