Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres, amelikataa pendekezo la Rais wa Marekani , Donald Trump, la kudhibiti Mji wa Gaza na kuwahamisha Wapalestina katika Nchi za Misri na Jordan. Katika mkutano na Waandishi wa habari alikokuwa na Waziri Mkuu wa Israel , Benjamin Netanyahu, Trump alipendekeza Marekani kuwa na umiliki wa muda mrefu wa Gaza, jambo lililokosolewa vikali na Jumuiya ya kimataifa.

Guterres alisema katika kamati ya Umoja wa Mataifa kuhusu haki za Wapalestina kwamba haki za Wapalestina zinahusisha kuishi kwa uhuru katika Nchi yao, lakini haki hizo zimekuwa zikididimiza. Pia amesema, suluhisho la kudumu linahitajika kupatikana kwa mataifa mawili, ambapo Israel na Palestina wangeishi kwa amani.

Msemaji wa Umoja wa Mataifa, Stephane Dujarric, alisema hatua yoyote ya kuwahamisha Wapalestina ni "safisha safisha ya kikabila", akisisitiza umuhimu wa kuheshimu sheria za kimataifa. Baada ya ukosoaji mkubwa, maafisa wa Donald Trump walijitetea, wakisema kuhamisha Wapalestina kutakuwa kwa muda tu, na hakutakuwa na kupeleka Wanajeshi kutekeleza mpango huo.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres, amelikataa pendekezo la Rais wa Marekani ๐Ÿ‡บ๐Ÿ‡ธ, Donald Trump, la kudhibiti Mji wa Gaza na kuwahamisha Wapalestina katika Nchi za Misri na Jordan. Katika mkutano na Waandishi wa habari alikokuwa na Waziri Mkuu wa Israel ๐Ÿ‡ฎ๐Ÿ‡ฑ, Benjamin Netanyahu, Trump alipendekeza Marekani kuwa na umiliki wa muda mrefu wa Gaza, jambo lililokosolewa vikali na Jumuiya ya kimataifa. Guterres alisema katika kamati ya Umoja wa Mataifa kuhusu haki za Wapalestina kwamba haki za Wapalestina zinahusisha kuishi kwa uhuru katika Nchi yao, lakini haki hizo zimekuwa zikididimiza. Pia amesema, suluhisho la kudumu linahitajika kupatikana kwa mataifa mawili, ambapo Israel na Palestina ๐Ÿ‡ต๐Ÿ‡ธ wangeishi kwa amani. Msemaji wa Umoja wa Mataifa, Stephane Dujarric, alisema hatua yoyote ya kuwahamisha Wapalestina ni "safisha safisha ya kikabila", akisisitiza umuhimu wa kuheshimu sheria za kimataifa. Baada ya ukosoaji mkubwa, maafisa wa Donald Trump walijitetea, wakisema kuhamisha Wapalestina kutakuwa kwa muda tu, na hakutakuwa na kupeleka Wanajeshi kutekeleza mpango huo.
Like
1
ยท 0 Comments ยท0 Shares ยท312 Views