Mahakama ya Kijeshi Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imetoa hati ya kukamatwa kwa Kiongozi wa umoja wa makundi ya Waasi Nchini humo ya Alliance Fleuve Congo (AFC/M23), Corneille Nangaa.
Televisheni ya Taifa ya DR Congo (RTNC) imeripoti kuwa hati ya kukamatwa kwa Nangaa imetolewa Jumanne Februari 4, 2025, baada ya kuhusika katika mauaji ya maelfu ya Raia katika mapigano yaliyoibuliwa na Wapiganaji wake katika Jimbo la Kivu Kaskazini Nchini humo. Mahakama hiyo katika hati yake imesema kutekeleza mauaji ya Raia katika mapigano hayo ni kinyume cha sheria za Nchi na sheria za kimataifa.
Mahakama imeamuru Nangaa akamatwe akiwa mahali popote atakapokutwa Duniani na kufikishwa katika Mahakama ya kijeshi Nchini DR Congo akituhumiwa kuhusika katika kile ilichokitaja kuwa ni uasi na uhalifu wa kivita dhidi ya Raia.
Ikumbukwe kwamba Mahakama hiyo hiyo ya Kijeshi iliwahi kumuhukumu Corneille Nangaa miaka kadhaa iliyopita akiwa hayupo Mahakamani (alikuwa amekimbia nje ya Nji) kunyongwa hadi kufa kwa kosa la uhaini.
Televisheni ya Taifa ya DR Congo (RTNC) imeripoti kuwa hati ya kukamatwa kwa Nangaa imetolewa Jumanne Februari 4, 2025, baada ya kuhusika katika mauaji ya maelfu ya Raia katika mapigano yaliyoibuliwa na Wapiganaji wake katika Jimbo la Kivu Kaskazini Nchini humo. Mahakama hiyo katika hati yake imesema kutekeleza mauaji ya Raia katika mapigano hayo ni kinyume cha sheria za Nchi na sheria za kimataifa.
Mahakama imeamuru Nangaa akamatwe akiwa mahali popote atakapokutwa Duniani na kufikishwa katika Mahakama ya kijeshi Nchini DR Congo akituhumiwa kuhusika katika kile ilichokitaja kuwa ni uasi na uhalifu wa kivita dhidi ya Raia.
Ikumbukwe kwamba Mahakama hiyo hiyo ya Kijeshi iliwahi kumuhukumu Corneille Nangaa miaka kadhaa iliyopita akiwa hayupo Mahakamani (alikuwa amekimbia nje ya Nji) kunyongwa hadi kufa kwa kosa la uhaini.
Mahakama ya Kijeshi Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo 🇨🇩 imetoa hati ya kukamatwa kwa Kiongozi wa umoja wa makundi ya Waasi Nchini humo ya Alliance Fleuve Congo (AFC/M23), Corneille Nangaa.
Televisheni ya Taifa ya DR Congo (RTNC) imeripoti kuwa hati ya kukamatwa kwa Nangaa imetolewa Jumanne Februari 4, 2025, baada ya kuhusika katika mauaji ya maelfu ya Raia katika mapigano yaliyoibuliwa na Wapiganaji wake katika Jimbo la Kivu Kaskazini Nchini humo. Mahakama hiyo katika hati yake imesema kutekeleza mauaji ya Raia katika mapigano hayo ni kinyume cha sheria za Nchi na sheria za kimataifa.
Mahakama imeamuru Nangaa akamatwe akiwa mahali popote atakapokutwa Duniani na kufikishwa katika Mahakama ya kijeshi Nchini DR Congo akituhumiwa kuhusika katika kile ilichokitaja kuwa ni uasi na uhalifu wa kivita dhidi ya Raia.
Ikumbukwe kwamba Mahakama hiyo hiyo ya Kijeshi iliwahi kumuhukumu Corneille Nangaa miaka kadhaa iliyopita akiwa hayupo Mahakamani (alikuwa amekimbia nje ya Nji) kunyongwa hadi kufa kwa kosa la uhaini.