Rais wa Marekani , Donlad Trump ametangaza kuwa Nchi yake imedhamiria kununua na kumiliki Ukanda wa Gaza na kuhamisha Wapalestina zaidi ya milioni mbili (2) wanaoishi huko, licha ya pendekezo hilo kupingwa vikali na Jumuiya ya Kimataifa. Rais huyo amewaambia Wanahabari kuwa huenda akaruhusu mataifa ya kiarabu kuhusika katika kukarabati upya sehemu mbalimbali na kuwa atahakikisha Raia wa Palestina wataishi maisha mazuri.

Mamlaka ya Palestina na kikundi kilicho na silaha cha Hamas ambao wamekuwa vitani kwa miezi (16) na Israel na kusababisha maafa Gaza, wamemjibu wakisema ardhi ya Palestina sio ya kuuzwa''. Lakini waziri Mkuu mkuu wa Israel , Benjamin Netanyahu ameipigia upatu pendekezo hilo la Trump akilitaja ni ''mwamko mpya na bunifu''.

Haya yamekuja Wiki tatu (3) baada ya makubaliano ya kusitisha mapigano huko Gaza Huku Kundi la Hamas likiachilia huru baadhi ya Mateka wa Nchi ya Israel inayowazuia ili kubadilishana na Wafungwa wa Palestina walioko katika Magerezani Nchini Israel.

Wanajeshi wa Israel walianzisha kampeni ya kuvamia na kuharibu Gaza wakijibu shambulizi la kushtukizia la mwezi Oktoba tarehe 7 2023, ambapo watu 1,200 waliuawa na 251 wakatekwa nyara. Zaidi ya Watu 48,180 wameuliwa Gaza tangu mapigano hayo yaanze , hii ni kwa mujibu wa wizara ya afya inayosimamiwa na kundi la Hamas lililokuwa likipigana na Nchi ya Israel.

Rais wa Marekani 🇺🇸, Donlad Trump ametangaza kuwa Nchi yake imedhamiria kununua na kumiliki Ukanda wa Gaza na kuhamisha Wapalestina zaidi ya milioni mbili (2) wanaoishi huko, licha ya pendekezo hilo kupingwa vikali na Jumuiya ya Kimataifa. Rais huyo amewaambia Wanahabari kuwa huenda akaruhusu mataifa ya kiarabu kuhusika katika kukarabati upya sehemu mbalimbali na kuwa atahakikisha Raia wa Palestina wataishi maisha mazuri. Mamlaka ya Palestina na kikundi kilicho na silaha cha Hamas ambao wamekuwa vitani kwa miezi (16) na Israel na kusababisha maafa Gaza, wamemjibu wakisema ardhi ya Palestina sio ya kuuzwa''. Lakini waziri Mkuu mkuu wa Israel 🇮🇱, Benjamin Netanyahu ameipigia upatu pendekezo hilo la Trump akilitaja ni ''mwamko mpya na bunifu''. Haya yamekuja Wiki tatu (3) baada ya makubaliano ya kusitisha mapigano huko Gaza Huku Kundi la Hamas likiachilia huru baadhi ya Mateka wa Nchi ya Israel inayowazuia ili kubadilishana na Wafungwa wa Palestina walioko katika Magerezani Nchini Israel. Wanajeshi wa Israel walianzisha kampeni ya kuvamia na kuharibu Gaza wakijibu shambulizi la kushtukizia la mwezi Oktoba tarehe 7 2023, ambapo watu 1,200 waliuawa na 251 wakatekwa nyara. Zaidi ya Watu 48,180 wameuliwa Gaza tangu mapigano hayo yaanze , hii ni kwa mujibu wa wizara ya afya inayosimamiwa na kundi la Hamas lililokuwa likipigana na Nchi ya Israel.
Like
Love
2
· 0 Commenti ·0 condivisioni ·152 Views