Baada ya kutangaza kuwa hawatashiriki mazungumzo ya amani huko Mjini Luanda Nchini Angola , Waasi wa kundi la M23 wamesema kuwa Umoja wa Ulaya (EU) ni moja ya Taasisi inayokwamisha mazungumzo hayo kufuatia kuwekewa vikwazo na Umoja huo Viongozi wake Wakuu akiwemo Bertrand Bisimwa.

Hata hivyo, Serikali ya Kinshasa kupitia Msemaji wake Tina Salama, imesema itashiriki mazungumzo hayo licha ya Kundi la Waasi wa M23 kujiweka pembeni. Pia Serikali ya Angola vile vile imetangaza kwamba mazungumzo hayo yataendelea kama ilivyokuwa imepangwa. Wakizungumzia vikwazo hivyo vya moja wa Ulaya, Waasi hao wa M23 wamesema Taasisi kadhaa za kimataifa zinakwamisha juhudi za kutafuta amani mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo .

Ikumbukwe kwamba hapo jana, Umoja wa Ulaya ulitangaza kuwawekea vikwazo Makamanda watatu (3) wa Jeshi la Rwanda na Mkuu wa Shirika lake la uchimbaji madini kwa madai ya kuwaunga mkono Wapiganaji wanaovuruga amani mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo. Pia Umoja huo ulimuwekea vikwazo Mkuu wa kundi la M23, Bertrand Bisimwa.

Baada ya kutangaza kuwa hawatashiriki mazungumzo ya amani huko Mjini Luanda Nchini Angola ๐Ÿ‡ฆ๐Ÿ‡ด, Waasi wa kundi la M23 wamesema kuwa Umoja wa Ulaya (EU) ni moja ya Taasisi inayokwamisha mazungumzo hayo kufuatia kuwekewa vikwazo na Umoja huo Viongozi wake Wakuu akiwemo Bertrand Bisimwa. Hata hivyo, Serikali ya Kinshasa kupitia Msemaji wake Tina Salama, imesema itashiriki mazungumzo hayo licha ya Kundi la Waasi wa M23 kujiweka pembeni. Pia Serikali ya Angola vile vile imetangaza kwamba mazungumzo hayo yataendelea kama ilivyokuwa imepangwa. Wakizungumzia vikwazo hivyo vya moja wa Ulaya, Waasi hao wa M23 wamesema Taasisi kadhaa za kimataifa zinakwamisha juhudi za kutafuta amani mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ๐Ÿ‡จ๐Ÿ‡ฉ. Ikumbukwe kwamba hapo jana, Umoja wa Ulaya ulitangaza kuwawekea vikwazo Makamanda watatu (3) wa Jeshi la Rwanda ๐Ÿ‡ท๐Ÿ‡ผ na Mkuu wa Shirika lake la uchimbaji madini kwa madai ya kuwaunga mkono Wapiganaji wanaovuruga amani mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo. Pia Umoja huo ulimuwekea vikwazo Mkuu wa kundi la M23, Bertrand Bisimwa.
0 Comments ยท0 Shares ยท24 Views