Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo , Felix Tshisekedi amesema Nchi yake iko tayari kuingia mkataba wa madini na Nchi Marekani kwa mabadilishano ya kupatiwa uwezo wa kujilinda dhidi ya Makundi ya Wapiganaji mashariki mwa taifa hilo kama vile kundi la M23 na mengineyo.
Akizungumza na kituo cha Televisheni cha Fox News leo asubuhi, Rais huyo amesema makubaliano ya aina hiyo yataiwezesha Nchi ya DR Congo kuchimba madini yake kupitia Kampuni za Marekani huku yenyewe ikinufaika kwa kuimarisha mifumo yake ya ulinzi na usalama. Nchi hiyo yenye utajiri mkubwa wa madini ikiwemo kobalti na urani imekuwa inapambana na Kundi la Waasi wa M23 linadaiwa kuungwa mkono na Nchi ya Rwanda ambalo limefanikiwa tangu mwanzoni mwa mwaka huu kuchukua udhibiti wa maeneo makubwa upande wa mashariki mwa Nchi hiyo.
Hapo jana, kundi hilo la Waasi wa M23 limeendelea kufanya mashambulizi na kuingia Mji mdogo wenye utajiri wa madini wa Walikale licha ya mwito wa kusitishwa mapigano uliotolewa na Rais Tshisekedi na mwenzake wa Rwanda Paul Kagame walipokutana Nchini Qatar mapema wiki hii.
Akizungumza na kituo cha Televisheni cha Fox News leo asubuhi, Rais huyo amesema makubaliano ya aina hiyo yataiwezesha Nchi ya DR Congo kuchimba madini yake kupitia Kampuni za Marekani huku yenyewe ikinufaika kwa kuimarisha mifumo yake ya ulinzi na usalama. Nchi hiyo yenye utajiri mkubwa wa madini ikiwemo kobalti na urani imekuwa inapambana na Kundi la Waasi wa M23 linadaiwa kuungwa mkono na Nchi ya Rwanda ambalo limefanikiwa tangu mwanzoni mwa mwaka huu kuchukua udhibiti wa maeneo makubwa upande wa mashariki mwa Nchi hiyo.
Hapo jana, kundi hilo la Waasi wa M23 limeendelea kufanya mashambulizi na kuingia Mji mdogo wenye utajiri wa madini wa Walikale licha ya mwito wa kusitishwa mapigano uliotolewa na Rais Tshisekedi na mwenzake wa Rwanda Paul Kagame walipokutana Nchini Qatar mapema wiki hii.
Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo π¨π©, Felix Tshisekedi amesema Nchi yake iko tayari kuingia mkataba wa madini na Nchi Marekani πΊπΈ kwa mabadilishano ya kupatiwa uwezo wa kujilinda dhidi ya Makundi ya Wapiganaji mashariki mwa taifa hilo kama vile kundi la M23 na mengineyo.
Akizungumza na kituo cha Televisheni cha Fox News leo asubuhi, Rais huyo amesema makubaliano ya aina hiyo yataiwezesha Nchi ya DR Congo kuchimba madini yake kupitia Kampuni za Marekani huku yenyewe ikinufaika kwa kuimarisha mifumo yake ya ulinzi na usalama. Nchi hiyo yenye utajiri mkubwa wa madini ikiwemo kobalti na urani imekuwa inapambana na Kundi la Waasi wa M23 linadaiwa kuungwa mkono na Nchi ya Rwanda π·πΌ ambalo limefanikiwa tangu mwanzoni mwa mwaka huu kuchukua udhibiti wa maeneo makubwa upande wa mashariki mwa Nchi hiyo.
Hapo jana, kundi hilo la Waasi wa M23 limeendelea kufanya mashambulizi na kuingia Mji mdogo wenye utajiri wa madini wa Walikale licha ya mwito wa kusitishwa mapigano uliotolewa na Rais Tshisekedi na mwenzake wa Rwanda Paul Kagame walipokutana Nchini Qatar πΆπ¦ mapema wiki hii.
0 Comments
Β·0 Shares
Β·37 Views