Saudi Arabia thibitisha kuonekana kwa Mwezi wa Ramadhani 1447 AH, kufunga kuanza Kesho.

Mamlaka nchini Saudi Arabia yamethibitisha rasmi kwamba mwezi wa Ramadhani umeonekana, jambo linalothibitisha kuanza kwa mwezi mtukufu wa kufunga. Kwa mujibu wa tamko rasmi na kuthibitishwa kuonekana kwa Mwezi, na hivyo kesho, Jumatano, tarehe 18 Februari 2026, itakuwa siku ya kwanza ya Ramadhani 1447 Hijiria

Ramadhani, mwezi ni wa tisa katika kalenda ya Kiislamu, hufungwa na Waislamu duniani kote kwa kuswali, kufanya ibada, na kufunga (kujizuia) kuanzia alfajiri hadi machweo ya jua. Kuonekana kwa mwezi wa Ramadhani ni kiashiria cha kuanza kwa ibada hii ya kiroho.

Mamlaka za kidini katika mataifa mengine ya GCC pia zimethibitisha uamuzi huu, huku baadhi ya nchi zikitarajiwa kuanza kufunga siku moja baadae, kulingana na muda na mahali ambapo mwezi umeonekana. Hii ni kuonyesha umuhimu wa kalenda ya Kiislamu (Hijiria) katika kuamua siku za ibada na sherehe za kidini.

Waislamu wanashauriwa kujiandaa kwa siku ya kwanza ya kufunga, kuimarisha imani na kufanya matendo mema, huku wakizingatia tamko la mamlaka husika.

Toa maoni yako
#Habari
Saudi Arabia thibitisha kuonekana kwa Mwezi wa Ramadhani 1447 AH, kufunga kuanza Kesho. Mamlaka nchini Saudi Arabia yamethibitisha rasmi kwamba mwezi wa Ramadhani umeonekana, jambo linalothibitisha kuanza kwa mwezi mtukufu wa kufunga. Kwa mujibu wa tamko rasmi na kuthibitishwa kuonekana kwa Mwezi, na hivyo kesho, Jumatano, tarehe 18 Februari 2026, itakuwa siku ya kwanza ya Ramadhani 1447 Hijiria Ramadhani, mwezi ni wa tisa katika kalenda ya Kiislamu, hufungwa na Waislamu duniani kote kwa kuswali, kufanya ibada, na kufunga (kujizuia) kuanzia alfajiri hadi machweo ya jua. Kuonekana kwa mwezi wa Ramadhani ni kiashiria cha kuanza kwa ibada hii ya kiroho. Mamlaka za kidini katika mataifa mengine ya GCC pia zimethibitisha uamuzi huu, huku baadhi ya nchi zikitarajiwa kuanza kufunga siku moja baadae, kulingana na muda na mahali ambapo mwezi umeonekana. Hii ni kuonyesha umuhimu wa kalenda ya Kiislamu (Hijiria) katika kuamua siku za ibada na sherehe za kidini. Waislamu wanashauriwa kujiandaa kwa siku ya kwanza ya kufunga, kuimarisha imani na kufanya matendo mema, huku wakizingatia tamko la mamlaka husika. Toa maoni yako #Habari
0 التعليقات 0 المشاركات 26 مشاهدة