• Iran yafanya mazoezi ya kijeshi katika mlango wa Hormuz, njia muhimu ya mafuta Duniani.

    Serikali ya Iran imeendesha mazoezi ya kijeshi katika eneo la kimkakati la Strait of Hormuz, mojawapo ya njia muhimu zaidi za usafirishaji wa mafuta duniani.

    Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya ndani, mazoezi hayo yalihusisha vikosi vya majini, makombora ya masafa mbalimbali pamoja na ndege zisizo na rubani (drone). Hatua hiyo imekuja wakati kukiwa na mvutano wa kisiasa na kiusalama katika eneo la Mashariki ya Kati.

    Mlango wa Hormuz unaunganisha Ghuba ya Uajemi na Bahari ya Oman, na ni njia ambayo sehemu kubwa ya mafuta ya dunia hupita kila siku. Inakadiriwa kuwa karibu theluthi moja ya mafuta yanayosafirishwa kwa njia ya bahari hupitia katika mkondo huo mwembamba lakini wenye umuhimu mkubwa kiuchumi.

    Afisa wa kijeshi wa Iran wamesema kuwa lengo la mazoezi hayo ni “kuimarisha uwezo wa kujilinda na kulinda mipaka ya majini ya taifa.” Aidha wameongeza kuwa “usalama wa eneo hili ni jukumu la mataifa ya ukanda huu, na si mataifa ya kigeni.”

    Hatua hiyo imeibua mjadala katika jumuiya ya kimataifa, hasa kwa kuzingatia umuhimu wa njia hiyo kwa uchumi wa dunia. Wataalamu wa masuala ya nishati wanaonya kuwa mvutano wowote katika eneo hilo unaweza kusababisha kupanda kwa bei ya mafuta katika soko la kimataifa.

    Hadi sasa, hakujaripotiwa tukio lolote la moja kwa moja lililoathiri meli za kibiashara, lakini macho ya dunia yanaendelea kuelekezwa katika eneo hilo nyeti.

    Toa maoni yako
    #Habari
    #Iran #Military #Exercise #Oil #Route
    Iran yafanya mazoezi ya kijeshi katika mlango wa Hormuz, njia muhimu ya mafuta Duniani. Serikali ya Iran imeendesha mazoezi ya kijeshi katika eneo la kimkakati la Strait of Hormuz, mojawapo ya njia muhimu zaidi za usafirishaji wa mafuta duniani. Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya ndani, mazoezi hayo yalihusisha vikosi vya majini, makombora ya masafa mbalimbali pamoja na ndege zisizo na rubani (drone). Hatua hiyo imekuja wakati kukiwa na mvutano wa kisiasa na kiusalama katika eneo la Mashariki ya Kati. Mlango wa Hormuz unaunganisha Ghuba ya Uajemi na Bahari ya Oman, na ni njia ambayo sehemu kubwa ya mafuta ya dunia hupita kila siku. Inakadiriwa kuwa karibu theluthi moja ya mafuta yanayosafirishwa kwa njia ya bahari hupitia katika mkondo huo mwembamba lakini wenye umuhimu mkubwa kiuchumi. Afisa wa kijeshi wa Iran wamesema kuwa lengo la mazoezi hayo ni “kuimarisha uwezo wa kujilinda na kulinda mipaka ya majini ya taifa.” Aidha wameongeza kuwa “usalama wa eneo hili ni jukumu la mataifa ya ukanda huu, na si mataifa ya kigeni.” Hatua hiyo imeibua mjadala katika jumuiya ya kimataifa, hasa kwa kuzingatia umuhimu wa njia hiyo kwa uchumi wa dunia. Wataalamu wa masuala ya nishati wanaonya kuwa mvutano wowote katika eneo hilo unaweza kusababisha kupanda kwa bei ya mafuta katika soko la kimataifa. Hadi sasa, hakujaripotiwa tukio lolote la moja kwa moja lililoathiri meli za kibiashara, lakini macho ya dunia yanaendelea kuelekezwa katika eneo hilo nyeti. Toa maoni yako #Habari #Iran #Military #Exercise #Oil #Route
    0 Commenti 0 condivisioni 10 Views
  • Military
    Military👐
    Like
    1
    1 Commenti 0 condivisioni 187 Views
  • OPERATION ENTEBBE -2

    Tayari zilikuwa zimepita siku tatu tangu ndege ya Air France Flight 139 kuondoka Tel Aviv na hatimaye kutekwa baada ya kuruka jijini Athens iliposimama kuchukua abiria. Lakini pia zilikuwa zimepita siku mbili tangu ndege hii kutua katika uwanja wa ndege wa Entebbe nchini Uganda. Katika siku zote mbili hizi tangu ndege hii itue uwanjani hapa, rais wa Uganda Idd Amin Nduli Dadaa alikuwa anafika uwanjani hapo kila siku “kuwajulia hali” mateka hao.
    Kwa muda wa siku hizi zote mbili tangu ndege itue uwanjani hapo, magaidi hawa walioiteka ndege kwa kushirikiana na jeshi la Uganda kuchunguza majina ya kila abiria kama ambavyo yalikuwa yameandikwa kwenye pasport. Lengo lao la kufanya hivi ilikuwa ni kujaribu kufahamu uraia wa kila mateka waliye naye. Baada ya kufanya uchambuzi huu wa passport zote, hatimaye siku hii ya tatu, yaani tarehe 29 June 1976 kiongozi wa magaidi hawa Wilfred Bose akiwa na karatasi mkononi aliingi ndani ya terminal ambayo walikuwa wanaitumia kuwahifadhi mateka na kisha akaanza kusoma majina ya kila abiria. Alichokuwa anakifanya ni kusoma majina ya mateka ambao passport zao zilionyesha walikuwa ni raia wa Israel. Lakini pia alisoma majina ya mateka wengine ambao licha ya passport zao kuonyesha kuwa hawakuwa raia wa Israel lakini walikuwa na majina ya kiyahudi. Pamoja na hao pia mateka wote ambao walikuwa na uraia pacha na uraia huo mmojawapo ukiwa ni Israel basi nao waliunganishwa kwenye list hii.
    Baada ya kuwatenganisha raia wote wa Israel na kuwaweka kwenye chumba kingine peke yao hapo hapo kwenye terminal, kuna mwanadada raia wa Ufaransa aliyeitwa Jocelyne Monier yeye jina lake halikuitwa kwenye ile list ya wanaotakiwa kutengwa kwenye chumba kingine (Waisrael na Wayahudi). Lakini ‘boyfriend’ wake alikuwa ni Muisrael na aliitwa jina na kutengwa na wengine katika kile chumba kingine. Mwanadada huyu ili kuonyesha kumtia moyo mpenzi wake na kupinga huu ubaguzi uliokuwa unafanywa na hawa magaidi, kwa hiari yake alijipeleka kwenye chumba cha mateka wa Kiisrael. Si mwanadada huyu pekee ambaye alifanya kitendo hiki cha ushujaa, lakini pia kulikuwa na mwanamama mwingine aliitwa Janet Almog (rai wa Marekani) na mateka mwingine aliyeitwa Jean-Jacques Mimouni (raia wa Ufaransa) nao kwenye kuonyesha hali ya kuwaunga mkono wenzao waliotengwa kwenye chumba kingine na kupinga ubaguzi uliokuwa unafanywa na maharamia hawa, nao walijipeleka kwa hiari yao kwenye chumba ambacho mateka hao walikibatiza jina “Chumba cha Waisrael”, ambacho mateka wote walijua fika kwamba kuna jambo baya maharamia hao walikuwa wamepanga kulifanya.

    Licha ya maharamia kwa kushirikiana na jeshi la Uganda kufanya uchambuzi huu wa kina kuhusu uraia wa kila mateka waliye naye, lakini walifanya kosa kubwa sana ambalo lilkuja kuwagharimu sana hapo baadae. Kwenye uchambuzi wao wote huu walioufanya walishindwa kumng’amua mateka mmoja mwanajeshi wa Israel ambaye alikuwa ana uraia pacha na siku hiyo alikuwa anatumia passport ambayo sio ya Israel. Mateka huyu alikuja kuwa muhimu sana huko mbeleni kuwapatia Mossad Intelijensia mujarabu kabisa kuhusu watekaji, jengo wanaloshikilia mateka, na namana wanavyoshirikiana na jeshi la Uganda.
    Siku iliyofuata yaani June 30, maharamia haya wakawaachia mkupuo wa kwanza wa mateka wasio raia wa Israel au wayahudi. Katika mkupuo huu wa kwanza waliachia mateka 48 ambao walikuwa ni wazee, watoto na akina mama wenye watoto wadogo.
    Baada ya mkupuo huu wa kwanza wa kuwaachia mateka hawa wachache, maharamia wakaweka wazi matakwa yao ili waweze kuachia mateka wengine. Kwanza kabisa walitaka walipwe fedha kiasi cha dola za Kimarekani milioni 5. Na pili walitakakuachiwa kwa wafungwa 53 wenye asili ya kipalestina wanaotuhumiwa kwa ugaidi, ambao kati yao 40 walikuwa kwenye jela za Israel na 13 katika nchi nyingine za Ulaya. Watekaji hawa wakatoa ‘ultimutum’ kwamba kama matakwa yao hayatatekelezwa ndani ya masaa ishirini na nne yajayo (mpaka tarehe 1 July saa 8 mchana) basi wataanza kuua raia wa Israel mmoja baada ya mwingine.
    Dunia nzima ni kama ilisimama kwa masaa kadhaa kutokana na sintofahamu iliyogubika kila mahali. Sintofahamu hii ililetwa na ukweli kwamba, ilikuwa inajulikana wazi kwa miaka yote kwamba Israel wana sera ya kutofanya mazungumzo au makubaliano na Magaidi. Kwahiyo kila mtu alikuwa nafahamu kuwa kuna uwezekano mkubwa ndani ya masaa 24 yajayo ulimwengu ukashuhidia watu zaidi ya 200 wakichinjwa kama kuku.

    NCHINI ISRAEL: KIKAO CHA BARAZA LA MAWAZIRI
    Nchini Israel kikao cha dharura cha baraza la mawaziri kilikuwa kimeitishwa na waziri Mkuu Yitzhak Rabin kujadili kuhusu hatua za kuchukua kuokoa raia wake ambao wameshikiliwa mateka huko uwanja wa ndege wa Entebbe, Uganda.
    Hali ya kikao ilikuwa tete sana kutokana na kila dakika waliyokuwa wanaitumia kujadili ndivyo ambavyo walikuwa wanaikaribia saa 8 mchana ya tarehe 1 July. Walipowasilana na Ujerumani na Ufaransa ambao nao walikuwa na baadhi ya wafungwa wa Kipalestina ambao watekaji walitaka waachiwe… walipowaomba ushirikiano wao kuhusu kukabali kuachia hao wafungwa, Ujerumani na Ufaransa walikataa katakata kuachia hata mfungwa mmoja wa Kipalestina ambaye alikuwa kwenye magereza zao.
    Sintofahamu ilizidi kuongezeka. Masaa yalizidi kuyoyoma. Saa 8 mchana ya tarehe 1 July ilizidi kukaribia. Harufu ya damu ilikuwa inabisha hodi mlangoni kwao. Licha ya weledi wao wote walionao lakini mbele yao waliona giza.
    Inapaswa kukumbukwa kwamba Idd Amin aliwahi kupatiwa mafunzo ya weledi wa kijeshi nchini Isarel (Special Force Training). Kwa hiyo baraza la mawaziri likamuagiza Baruch Bar-Lev, kamanda mstaafu wa IDF ambaye alihusika kumpatia mafunzo ya kijeshi Amin kipindi yuko Israel na kufanikiwa kujenga naye ukaribu. Baraza la Mawaziri likamuagiza Baruck (marafiki zake humuita “Burka”) kufanya mawasiliano na Rais huyo wa Uganda ili kujaribu kumuomba awashawishi magaidi wanaoshikilia mateka kwenye uwanja wake wa ndege wa Entebbe wawaachie mateka hao bila masharti magumu.
    Kupitia kwa Burka, Israel ilifikia mpaka hatua ya kumuahidi Idd Amin kuwa kama atafanikisha kuachiwa kwa mateka hao basi watatumia ushawishi walionao kuhakikisha kuwa Amin anatunukiwa tuzo ya amani ya Nobel.
    Lakini Amin hakulegeza msimamo, akaendelea kuwasisitiza kuwa hakuna namna nyingine yeyote ambayo mateka hao wataachiwa bila masharti yaliyotolewa na watekaji kutimizwa.
    Baada ya juhudi hii ya kumuhonga ‘tuzo’ kugonga mwamba, Waziri Mkuu wa Israel akawasiliana na serikali ya Marekani na kuwaomba wamshawishi Rais wa Misri Anwar Sadat ambaye alikuwa anaheshimiana sana na Amin ili amshawishi kuwaamuru magaidi yaliyoko uwanjani kwake Entebbe waachiemateka bila masharti magumu.
    Amin bado akashikilia msimamo kwamba hakuna mateka atakayeachiwa pasipo masharti yaliyotolewa kutimizwa.
    Juhudi hizi za kumshawishi Amin zilikula muda mwingi sana na hatimaye wakajikuta tayari kulikuwa kumekucha asubuhi. Mbele yao kulikuwa kumebakia masaa chini ya manane kabla ya damu ya zaidi ya watu 200 kumwagika.
    Baraza la mawaziri la Israel likamuomba Amin aongee na watekaji wakubali kusogeza siku mbele ili kuipa serikali ya Israel muda wakutosha kushughulikia lojistiki na kushawishi Ujerumani na Ufaransa ili waweze kutimiza sharti la kuachiwa kwa wafungwa wa kipalestina 53 wanaotuhumiwa kwa ugaidi.
    Rais Idd Amin baada ya kushawishiwa sana akakubali ombi hili na akaieleza serikali ya Israel kwamba ni siku tatu tu pekee zinaongezwa, yaani ikimaanisha kwamba siku zitaongezwa mpaka tarehe 4 July, saa 8 mchana. Serikali ya Israel ikakubliana na hili.
    Mchana wa siku hiyo, serikali ilitoa taarifa rasmi kwa vyombo vya habari wakilaani vitendo vya kigaidi na hususani matukio ya utekeji wa raia wasio na hatia, na pia ikaendelea kusisitiza kuhusu sera yake ya kutojadili na magaidi. Lakini taarifa hii ikamalizia kwa kueleza kuwa kwa kujali zaidi uhai wa zaidi ya raia 200 ambao bado wanashikiliwa na magaidi hayo, na kujali maumivu ambayo familia zao na taifa zima linapitia, wamekubali kutimiza sharti la magaidi hao la kuwalipa fedha za kimarekani dola milioni tano pamoja na kuachiwa kwa wafungwa wa kipalestina 53 wenye tuhuma za ugaidi.
    Ilikuwa ni moja ya matukio machache ambayo yaliishangaza dunia kwa Israel kukubali kushindwa hadharani. Kwa upande wa maadui wa Israel hii ilikuwa ni sherehe kubwa kwao. Na kwa upande wa Isarel na maswahiba zake hii iikuwa ni maombolezo makubwa.
    Amin na wenzake kule Uganda walikuwa wanasherehekea baada ya taarifa hii kutolewa kwa vyombo vya habari. Walihsi kabisa harufu ya ushindi inanukia kwenye pua zao.
    Kitu ambacho walikuwa hawafahamu ilikuwa ni kwamba, Israel walikuwa wanawafanyia ‘mchezo’ wa kisaikolojia ili Amin, jeshi lake na watekaji wajiamini kwa kuona kuwa ushindi umeegemea upande wao na hatimaye wajisahau kutokana na kujiamini huku.

    NYUMA YA PAZIA
    Huko Tel aviv, makamanda wa IDF na maafisa wa Mossad walikuwa wamekusanyika katika conference room ya mako makuu ya wizara ya ulinzi kuweka mkakati wa oparesheni ya uokozi (rescue mission) wa mateka wanaoshikiliwa katika uwanja wa ndege wa Entebbe, Uganda.
    Kati ya watu muhimu ambao walikuwepo kwenye kikao hiki alikuwa ni Waziri Mkuu Rabin na Ehud Barak ambaye kipindi hicho alikuwa kamanda wa ngazi za juu kwenye jeshi anayeongoza kitengo cha Intelijensia ya jeshi (Military Intelligence).
    Moja kati ya vitu muhimu ambavyo viliwasaidia ilikuwa ni taarifa ya intelijensia iliyoletwa na Mossad kwamba uwanja wa ndege wa Entebbe ulijengwa na kampuni ya Kiisrael inayoitwa Solel Boneh.
    Kwahiyo muwakilishi kutoka katika kampuni hii ya ujenzi naye akaitwa kikaoni kwa ajili ya kuwasilisha michoro kuhusu jengo lote na uwanja wa ndege wa Entebbe ulivyo.
    Lakini pia wakati huo huo kulikuwa na maafisa wa Mossad ambao walikuwa ufaransa kuwahoji wale mateka ambao walikuwa wameachiwa awali. Mtu muhimu zaidi ambaye alitoa taarifa nzuri kwa Mossad alikuwa ni yule afisa wa jeshi niliyemuelezea awali kwamba alikuwa na uraia wan chi mbili (Israel na Ufaransa) na siku hii alikuwa ametumia passport ya nchi ya ufaransa hivyo watekaji walimuachia pamoja na wenzake wa kundi la kwanza lile la watu 48.
    Bwana huyu alitoa taarifa muhimu zaidi kuhusu kilichokuwa kinaendelea katika uwanja wa ndege wa Entebbe, kwa kuwa yeye tofauti na wenzake kutokana na uzoefu wake wa jeshi alikuwa aliweza kuwaeleza Mossad kuhusu ni salaha za namna gani watekaji walikuwa nazo, kulikuwa na ndege za aina gani za kijeshi pale uwanjani (Idd Amin aliamuru Air Force ya Uganda kulinda uwanja huo masaa 24), pia aliweza kuwaeleza kuhusu ‘rotation’ ya ulinzi ya jeshi la Uganda pamoja na taarifa nyingine muhimu ambazo abiria wengine wasingeweza kuzitilia maanani au kkuzieleza kwa ufasaha.
    Baada ya kupata intelijensia ya kutosha, mkakati wa awali ambao ulipendekezwa na jeshi ulikuwa ni kutumia ndege ya kijeshi na kisha kudondosha makomando kwenye ziwa Viktoria na kutoka hapo watatumia boti za mpira kuvuka mpaka nchi kavu na hatimaye kuelekea uwanja wa ndege ambao haukuwa mbali sana na ziwa Viktoria.
    Mkakati huu ulikuwa ni mzuri lakini ulihairishwa baada ya kupewa taarifa kuwa ziwa Viktoria lilikuwa na mamba wengi na ingeweza kuhatarisha uhai wa hawa makomando kabla hata ya kufika kwenye uwanja wa ndege. Kwahiyo ilikuwa dhahiri kwamba mkakati wowote ambao utawekwa ni lazima uwe wa kuvamia kutokea nchi kavu na ikiwezekana kutoka nchi jirani.
    Changamoto kubwa zaidi ilikuwa ni usafiri. Yaani kwamba oparesheni hii ilikuwa si tu kwamba makomando wanaotumwa kutekeleza wanaenda kupambana na magaidi wanne tu walioteka ndege, bali ilikuwa ni kana kwamba wanaenda kupambana na jeshi zima la Uganda. Kwa hiyo kikosi cha makomando ambacho kitatumwa kwenda huko lazima kiwe na watu wengi wa kutosha na pia lazima wachukue silaha nzito za kutosha. Ili kufaniskisha safari yenye makomando wengi hivi na vifaa vizito ilikuwa ni lazima kutumia ndege kubwa za kijeshi zenye uwezo mkubwa pia na hakukuwa na chaguo zuri zaid ya kutumia ndege za kijeshi za LOCKHEED C-130 HERCULES. Sasa changamoto ilikuwa inakuja kwamba huwezi kurusha dege kubwa kama hii kwenda na kurudi kutoka Israel mpaka Uganda bila kujaza mafuta tena japo mara moja.
    Katika kipindi hiki bado Israel walikuwa hawajawa na uwezo wa kufanya ‘Aerial Refuel’, yaani ndege kujazwa mafuta kwa kutumia ndege nyingine ikiwa angani. Lakini pia ilikuwa ni lazima madege hayo yakikaribia Uganda yaruke chini chini ili kukwepa kudunguliwa na kuikwepa rada ya kijeshi. Kwa hiyo ilikuwa ni lazima kupata nchi ndani ya afrika Mashariki ambao watakubali madege hayo ya kijeshi ya Israel kutua kwenye uwanja wake wa ndege na kujaza mafuta lakini pia kujiandaa na kuanzisha operation kutokea hapo na pia anga lao kutumika kuanzisha shambulizi la kijeshi kuelekea Uganda.
    Sasa japokuwa nchi zote za Afrika Mashariki zilikuwa hazikubaliana na kitendo cha Rais wa Uganda kushirikiana na watekaji, lakini hakukuwa na hata nchi moja ambayo ilikuwa iko tayari kuingia kwenye mzozo na Idd Amin kwa kuruhusu viwanja vya vya ndege kutumika na ndege za jeshi la Israel au wanajeshi kujiandaa kuvamia Entebbe au pia kuruhusu anga lao kutumia na jeshi la Israel.
    Ndipo hapa ambapo kwa haraka sana siku hiyo hiyo Waziri Mkuu Rabin akamtuma Ehud Barak na maafisa wachache wa Mossad kwenda Kenya kushawishi serikali ya Mzee Jomo Kenyatta iruhusu ndege za jeshi la Isarel kutumia kiwanja chao cha ndege. Ehud barak na wenzake hawakwenda tu moja kwa moja kwa Mzee Kenyatta, bali kwanza walienda kwa Waziri wa kilimo wa kipindi hicho Bw. Bruce McKenzie ambaye huyu aliwahi kuwa afisa wa Idara ya ujasusi ya Uingereza, MI6 na pia alikuwa swahiba mkubwa wa Ehud Barak.

    Kwa hiyo Israel ikamtumia Bruce McKenzie kumshawishi Mzee Jomo Kenyatta kuruhusu anga la Kenya na viwanjavya ndege kutumiwa na makomando wa Israel na ndege zao.
    Ehud Barak na maafisa wa Mossad hawakuishia hapa tu, bali pia walifanya vikao vya siri na wafanyabiashara wakubwa nchini Kenya wenye asili ya Israel na wale ambao walikuwa na ‘marafiki’ wa Israel kuwaomba watumie ushawishi wao wa kisiasa na kiuchumi wasaidie kumshawishi Kenyatta kukubali ombi la seriakli ya Israael viwanja vyao kutumika na ndege za kijeshi za Israel na makondo wake.
    Baada ya mashinikizo haya kutoka kila upande, Mzee Kenyatta hakuwa na chaguo linguine zaidi ya kukubali ombi lao.
    Bwana huyu McKenzie pia alikuwa na ndege yakebinafsi, na Ehud Barak akaona fursa. Walitumia ndege hii ya kiraia kuruka mpaka Uganda mijini Entebbe na kukatiza juu ya anga la uwanja wa ndege wa Entebbe na walipokuwa wanapita juu ya anga la uwanja wa ndege, Ehud Barak akatumia fursa hii kupiga picha kila eneo la uwanja. Kwa kuwa hii ilikuwa ni ndege ya kiraia, jeshi la Uganda hawakushughulika nayo.
    Picha hizi zilizopigwa na Ehud Barak zilikuja kuwa na umuhimumkubwa katika maandalizi ya mwisho ya oparesheni ya makomando wa Isarel Kuvamia uwanja huu.
    Mpaka kufikia hapa maandalizi yote muhimu yalikuwa yamekamilika.
    WAKATI HUO HUO
    Upande wa watekaji kule Uganda walikuwa wanasubria mifwedha yao dola milioni 5 za kimarekani.
    Rais Idd Amin naye baada ya kufikia makubaliano na Israel kuwa masharti ya fedha na wafungwa wa kipalestina kuachiwa tarehe 4 July, naye ‘akarelax’ na akaona huo ndio muda wa kutekeleza majukumu Mengine akisubiria tarehe 4 July ifike.
    Katika kipindi hiki Idd amin ndiye alikuwa mwenyekiti wa Umoja wa Afrika kwa kuzingatia utaratibu wa uenyekiti kuzunguka kwa kila nchi kwa mwaka mmoja mmoja na wiki hii alikuwa anatakiwa kwenye kikao cha Umoja wa Afrika kilichokuwa kinafanyika Mauritius. Kwa hiyo Amin akafunga safari kuelekea Mauritius kwenda kukabidhi kijiti cha Uenyekiti.
    Ehud Barak aliposikia taarifa hii, kwa kutumia akili yake kubwa ya kuzaliwa aliyojaliwa na uzoefu wake wa ujasusi, aliona fursa adhimu kabisa hapa. Akawasiliana na walioko kikaoni huko Tel Aviv na kuwaeleza taarifa ambazo awali wote hawakuielewa.
    Ehud Barak: “Idd Amin akiwa ndani ya Uganda huwa anatumia Mercedes Limousine katika msafara wake”
    Waziri Mkuu Rabin: “Ok! Limefanyaje?’
    Ehud Barak: “Nataka mtafute gari kama hiyo… Mercedes Limousine”
    Waziri Mkuu Rabin: “la kazi gani?”
    Ehud Barak: “siku ambayo kikosi cha makomando wakipanda kwenye ndege kutoka huko Israel kwenda Uganda, gari hilo nataka pia lipakiwe ndani ya ndge!”
    Kwa dakika kadhaa wote ambao walikuwa wanamsikiliza pale kikaoni kupitia simu hakuna ambaye alielewa nini hasa Ehud Barak alikuwa anapendekeza.
    Yalikuwa yamebaki masaa machache tu ambapo, weledi, ushujaa na uzalendo uliotukuka ulikuwa unaedna kudhihirika.

    Itaendelea
    #TheBOLD_JF
    OPERATION ENTEBBE -2 Tayari zilikuwa zimepita siku tatu tangu ndege ya Air France Flight 139 kuondoka Tel Aviv na hatimaye kutekwa baada ya kuruka jijini Athens iliposimama kuchukua abiria. Lakini pia zilikuwa zimepita siku mbili tangu ndege hii kutua katika uwanja wa ndege wa Entebbe nchini Uganda. Katika siku zote mbili hizi tangu ndege hii itue uwanjani hapa, rais wa Uganda Idd Amin Nduli Dadaa alikuwa anafika uwanjani hapo kila siku “kuwajulia hali” mateka hao. Kwa muda wa siku hizi zote mbili tangu ndege itue uwanjani hapo, magaidi hawa walioiteka ndege kwa kushirikiana na jeshi la Uganda kuchunguza majina ya kila abiria kama ambavyo yalikuwa yameandikwa kwenye pasport. Lengo lao la kufanya hivi ilikuwa ni kujaribu kufahamu uraia wa kila mateka waliye naye. Baada ya kufanya uchambuzi huu wa passport zote, hatimaye siku hii ya tatu, yaani tarehe 29 June 1976 kiongozi wa magaidi hawa Wilfred Bose akiwa na karatasi mkononi aliingi ndani ya terminal ambayo walikuwa wanaitumia kuwahifadhi mateka na kisha akaanza kusoma majina ya kila abiria. Alichokuwa anakifanya ni kusoma majina ya mateka ambao passport zao zilionyesha walikuwa ni raia wa Israel. Lakini pia alisoma majina ya mateka wengine ambao licha ya passport zao kuonyesha kuwa hawakuwa raia wa Israel lakini walikuwa na majina ya kiyahudi. Pamoja na hao pia mateka wote ambao walikuwa na uraia pacha na uraia huo mmojawapo ukiwa ni Israel basi nao waliunganishwa kwenye list hii. Baada ya kuwatenganisha raia wote wa Israel na kuwaweka kwenye chumba kingine peke yao hapo hapo kwenye terminal, kuna mwanadada raia wa Ufaransa aliyeitwa Jocelyne Monier yeye jina lake halikuitwa kwenye ile list ya wanaotakiwa kutengwa kwenye chumba kingine (Waisrael na Wayahudi). Lakini ‘boyfriend’ wake alikuwa ni Muisrael na aliitwa jina na kutengwa na wengine katika kile chumba kingine. Mwanadada huyu ili kuonyesha kumtia moyo mpenzi wake na kupinga huu ubaguzi uliokuwa unafanywa na hawa magaidi, kwa hiari yake alijipeleka kwenye chumba cha mateka wa Kiisrael. Si mwanadada huyu pekee ambaye alifanya kitendo hiki cha ushujaa, lakini pia kulikuwa na mwanamama mwingine aliitwa Janet Almog (rai wa Marekani) na mateka mwingine aliyeitwa Jean-Jacques Mimouni (raia wa Ufaransa) nao kwenye kuonyesha hali ya kuwaunga mkono wenzao waliotengwa kwenye chumba kingine na kupinga ubaguzi uliokuwa unafanywa na maharamia hawa, nao walijipeleka kwa hiari yao kwenye chumba ambacho mateka hao walikibatiza jina “Chumba cha Waisrael”, ambacho mateka wote walijua fika kwamba kuna jambo baya maharamia hao walikuwa wamepanga kulifanya. Licha ya maharamia kwa kushirikiana na jeshi la Uganda kufanya uchambuzi huu wa kina kuhusu uraia wa kila mateka waliye naye, lakini walifanya kosa kubwa sana ambalo lilkuja kuwagharimu sana hapo baadae. Kwenye uchambuzi wao wote huu walioufanya walishindwa kumng’amua mateka mmoja mwanajeshi wa Israel ambaye alikuwa ana uraia pacha na siku hiyo alikuwa anatumia passport ambayo sio ya Israel. Mateka huyu alikuja kuwa muhimu sana huko mbeleni kuwapatia Mossad Intelijensia mujarabu kabisa kuhusu watekaji, jengo wanaloshikilia mateka, na namana wanavyoshirikiana na jeshi la Uganda. Siku iliyofuata yaani June 30, maharamia haya wakawaachia mkupuo wa kwanza wa mateka wasio raia wa Israel au wayahudi. Katika mkupuo huu wa kwanza waliachia mateka 48 ambao walikuwa ni wazee, watoto na akina mama wenye watoto wadogo. Baada ya mkupuo huu wa kwanza wa kuwaachia mateka hawa wachache, maharamia wakaweka wazi matakwa yao ili waweze kuachia mateka wengine. Kwanza kabisa walitaka walipwe fedha kiasi cha dola za Kimarekani milioni 5. Na pili walitakakuachiwa kwa wafungwa 53 wenye asili ya kipalestina wanaotuhumiwa kwa ugaidi, ambao kati yao 40 walikuwa kwenye jela za Israel na 13 katika nchi nyingine za Ulaya. Watekaji hawa wakatoa ‘ultimutum’ kwamba kama matakwa yao hayatatekelezwa ndani ya masaa ishirini na nne yajayo (mpaka tarehe 1 July saa 8 mchana) basi wataanza kuua raia wa Israel mmoja baada ya mwingine. Dunia nzima ni kama ilisimama kwa masaa kadhaa kutokana na sintofahamu iliyogubika kila mahali. Sintofahamu hii ililetwa na ukweli kwamba, ilikuwa inajulikana wazi kwa miaka yote kwamba Israel wana sera ya kutofanya mazungumzo au makubaliano na Magaidi. Kwahiyo kila mtu alikuwa nafahamu kuwa kuna uwezekano mkubwa ndani ya masaa 24 yajayo ulimwengu ukashuhidia watu zaidi ya 200 wakichinjwa kama kuku. NCHINI ISRAEL: KIKAO CHA BARAZA LA MAWAZIRI Nchini Israel kikao cha dharura cha baraza la mawaziri kilikuwa kimeitishwa na waziri Mkuu Yitzhak Rabin kujadili kuhusu hatua za kuchukua kuokoa raia wake ambao wameshikiliwa mateka huko uwanja wa ndege wa Entebbe, Uganda. Hali ya kikao ilikuwa tete sana kutokana na kila dakika waliyokuwa wanaitumia kujadili ndivyo ambavyo walikuwa wanaikaribia saa 8 mchana ya tarehe 1 July. Walipowasilana na Ujerumani na Ufaransa ambao nao walikuwa na baadhi ya wafungwa wa Kipalestina ambao watekaji walitaka waachiwe… walipowaomba ushirikiano wao kuhusu kukabali kuachia hao wafungwa, Ujerumani na Ufaransa walikataa katakata kuachia hata mfungwa mmoja wa Kipalestina ambaye alikuwa kwenye magereza zao. Sintofahamu ilizidi kuongezeka. Masaa yalizidi kuyoyoma. Saa 8 mchana ya tarehe 1 July ilizidi kukaribia. Harufu ya damu ilikuwa inabisha hodi mlangoni kwao. Licha ya weledi wao wote walionao lakini mbele yao waliona giza. Inapaswa kukumbukwa kwamba Idd Amin aliwahi kupatiwa mafunzo ya weledi wa kijeshi nchini Isarel (Special Force Training). Kwa hiyo baraza la mawaziri likamuagiza Baruch Bar-Lev, kamanda mstaafu wa IDF ambaye alihusika kumpatia mafunzo ya kijeshi Amin kipindi yuko Israel na kufanikiwa kujenga naye ukaribu. Baraza la Mawaziri likamuagiza Baruck (marafiki zake humuita “Burka”) kufanya mawasiliano na Rais huyo wa Uganda ili kujaribu kumuomba awashawishi magaidi wanaoshikilia mateka kwenye uwanja wake wa ndege wa Entebbe wawaachie mateka hao bila masharti magumu. Kupitia kwa Burka, Israel ilifikia mpaka hatua ya kumuahidi Idd Amin kuwa kama atafanikisha kuachiwa kwa mateka hao basi watatumia ushawishi walionao kuhakikisha kuwa Amin anatunukiwa tuzo ya amani ya Nobel. Lakini Amin hakulegeza msimamo, akaendelea kuwasisitiza kuwa hakuna namna nyingine yeyote ambayo mateka hao wataachiwa bila masharti yaliyotolewa na watekaji kutimizwa. Baada ya juhudi hii ya kumuhonga ‘tuzo’ kugonga mwamba, Waziri Mkuu wa Israel akawasiliana na serikali ya Marekani na kuwaomba wamshawishi Rais wa Misri Anwar Sadat ambaye alikuwa anaheshimiana sana na Amin ili amshawishi kuwaamuru magaidi yaliyoko uwanjani kwake Entebbe waachiemateka bila masharti magumu. Amin bado akashikilia msimamo kwamba hakuna mateka atakayeachiwa pasipo masharti yaliyotolewa kutimizwa. Juhudi hizi za kumshawishi Amin zilikula muda mwingi sana na hatimaye wakajikuta tayari kulikuwa kumekucha asubuhi. Mbele yao kulikuwa kumebakia masaa chini ya manane kabla ya damu ya zaidi ya watu 200 kumwagika. Baraza la mawaziri la Israel likamuomba Amin aongee na watekaji wakubali kusogeza siku mbele ili kuipa serikali ya Israel muda wakutosha kushughulikia lojistiki na kushawishi Ujerumani na Ufaransa ili waweze kutimiza sharti la kuachiwa kwa wafungwa wa kipalestina 53 wanaotuhumiwa kwa ugaidi. Rais Idd Amin baada ya kushawishiwa sana akakubali ombi hili na akaieleza serikali ya Israel kwamba ni siku tatu tu pekee zinaongezwa, yaani ikimaanisha kwamba siku zitaongezwa mpaka tarehe 4 July, saa 8 mchana. Serikali ya Israel ikakubliana na hili. Mchana wa siku hiyo, serikali ilitoa taarifa rasmi kwa vyombo vya habari wakilaani vitendo vya kigaidi na hususani matukio ya utekeji wa raia wasio na hatia, na pia ikaendelea kusisitiza kuhusu sera yake ya kutojadili na magaidi. Lakini taarifa hii ikamalizia kwa kueleza kuwa kwa kujali zaidi uhai wa zaidi ya raia 200 ambao bado wanashikiliwa na magaidi hayo, na kujali maumivu ambayo familia zao na taifa zima linapitia, wamekubali kutimiza sharti la magaidi hao la kuwalipa fedha za kimarekani dola milioni tano pamoja na kuachiwa kwa wafungwa wa kipalestina 53 wenye tuhuma za ugaidi. Ilikuwa ni moja ya matukio machache ambayo yaliishangaza dunia kwa Israel kukubali kushindwa hadharani. Kwa upande wa maadui wa Israel hii ilikuwa ni sherehe kubwa kwao. Na kwa upande wa Isarel na maswahiba zake hii iikuwa ni maombolezo makubwa. Amin na wenzake kule Uganda walikuwa wanasherehekea baada ya taarifa hii kutolewa kwa vyombo vya habari. Walihsi kabisa harufu ya ushindi inanukia kwenye pua zao. Kitu ambacho walikuwa hawafahamu ilikuwa ni kwamba, Israel walikuwa wanawafanyia ‘mchezo’ wa kisaikolojia ili Amin, jeshi lake na watekaji wajiamini kwa kuona kuwa ushindi umeegemea upande wao na hatimaye wajisahau kutokana na kujiamini huku. NYUMA YA PAZIA Huko Tel aviv, makamanda wa IDF na maafisa wa Mossad walikuwa wamekusanyika katika conference room ya mako makuu ya wizara ya ulinzi kuweka mkakati wa oparesheni ya uokozi (rescue mission) wa mateka wanaoshikiliwa katika uwanja wa ndege wa Entebbe, Uganda. Kati ya watu muhimu ambao walikuwepo kwenye kikao hiki alikuwa ni Waziri Mkuu Rabin na Ehud Barak ambaye kipindi hicho alikuwa kamanda wa ngazi za juu kwenye jeshi anayeongoza kitengo cha Intelijensia ya jeshi (Military Intelligence). Moja kati ya vitu muhimu ambavyo viliwasaidia ilikuwa ni taarifa ya intelijensia iliyoletwa na Mossad kwamba uwanja wa ndege wa Entebbe ulijengwa na kampuni ya Kiisrael inayoitwa Solel Boneh. Kwahiyo muwakilishi kutoka katika kampuni hii ya ujenzi naye akaitwa kikaoni kwa ajili ya kuwasilisha michoro kuhusu jengo lote na uwanja wa ndege wa Entebbe ulivyo. Lakini pia wakati huo huo kulikuwa na maafisa wa Mossad ambao walikuwa ufaransa kuwahoji wale mateka ambao walikuwa wameachiwa awali. Mtu muhimu zaidi ambaye alitoa taarifa nzuri kwa Mossad alikuwa ni yule afisa wa jeshi niliyemuelezea awali kwamba alikuwa na uraia wan chi mbili (Israel na Ufaransa) na siku hii alikuwa ametumia passport ya nchi ya ufaransa hivyo watekaji walimuachia pamoja na wenzake wa kundi la kwanza lile la watu 48. Bwana huyu alitoa taarifa muhimu zaidi kuhusu kilichokuwa kinaendelea katika uwanja wa ndege wa Entebbe, kwa kuwa yeye tofauti na wenzake kutokana na uzoefu wake wa jeshi alikuwa aliweza kuwaeleza Mossad kuhusu ni salaha za namna gani watekaji walikuwa nazo, kulikuwa na ndege za aina gani za kijeshi pale uwanjani (Idd Amin aliamuru Air Force ya Uganda kulinda uwanja huo masaa 24), pia aliweza kuwaeleza kuhusu ‘rotation’ ya ulinzi ya jeshi la Uganda pamoja na taarifa nyingine muhimu ambazo abiria wengine wasingeweza kuzitilia maanani au kkuzieleza kwa ufasaha. Baada ya kupata intelijensia ya kutosha, mkakati wa awali ambao ulipendekezwa na jeshi ulikuwa ni kutumia ndege ya kijeshi na kisha kudondosha makomando kwenye ziwa Viktoria na kutoka hapo watatumia boti za mpira kuvuka mpaka nchi kavu na hatimaye kuelekea uwanja wa ndege ambao haukuwa mbali sana na ziwa Viktoria. Mkakati huu ulikuwa ni mzuri lakini ulihairishwa baada ya kupewa taarifa kuwa ziwa Viktoria lilikuwa na mamba wengi na ingeweza kuhatarisha uhai wa hawa makomando kabla hata ya kufika kwenye uwanja wa ndege. Kwahiyo ilikuwa dhahiri kwamba mkakati wowote ambao utawekwa ni lazima uwe wa kuvamia kutokea nchi kavu na ikiwezekana kutoka nchi jirani. Changamoto kubwa zaidi ilikuwa ni usafiri. Yaani kwamba oparesheni hii ilikuwa si tu kwamba makomando wanaotumwa kutekeleza wanaenda kupambana na magaidi wanne tu walioteka ndege, bali ilikuwa ni kana kwamba wanaenda kupambana na jeshi zima la Uganda. Kwa hiyo kikosi cha makomando ambacho kitatumwa kwenda huko lazima kiwe na watu wengi wa kutosha na pia lazima wachukue silaha nzito za kutosha. Ili kufaniskisha safari yenye makomando wengi hivi na vifaa vizito ilikuwa ni lazima kutumia ndege kubwa za kijeshi zenye uwezo mkubwa pia na hakukuwa na chaguo zuri zaid ya kutumia ndege za kijeshi za LOCKHEED C-130 HERCULES. Sasa changamoto ilikuwa inakuja kwamba huwezi kurusha dege kubwa kama hii kwenda na kurudi kutoka Israel mpaka Uganda bila kujaza mafuta tena japo mara moja. Katika kipindi hiki bado Israel walikuwa hawajawa na uwezo wa kufanya ‘Aerial Refuel’, yaani ndege kujazwa mafuta kwa kutumia ndege nyingine ikiwa angani. Lakini pia ilikuwa ni lazima madege hayo yakikaribia Uganda yaruke chini chini ili kukwepa kudunguliwa na kuikwepa rada ya kijeshi. Kwa hiyo ilikuwa ni lazima kupata nchi ndani ya afrika Mashariki ambao watakubali madege hayo ya kijeshi ya Israel kutua kwenye uwanja wake wa ndege na kujaza mafuta lakini pia kujiandaa na kuanzisha operation kutokea hapo na pia anga lao kutumika kuanzisha shambulizi la kijeshi kuelekea Uganda. Sasa japokuwa nchi zote za Afrika Mashariki zilikuwa hazikubaliana na kitendo cha Rais wa Uganda kushirikiana na watekaji, lakini hakukuwa na hata nchi moja ambayo ilikuwa iko tayari kuingia kwenye mzozo na Idd Amin kwa kuruhusu viwanja vya vya ndege kutumika na ndege za jeshi la Israel au wanajeshi kujiandaa kuvamia Entebbe au pia kuruhusu anga lao kutumia na jeshi la Israel. Ndipo hapa ambapo kwa haraka sana siku hiyo hiyo Waziri Mkuu Rabin akamtuma Ehud Barak na maafisa wachache wa Mossad kwenda Kenya kushawishi serikali ya Mzee Jomo Kenyatta iruhusu ndege za jeshi la Isarel kutumia kiwanja chao cha ndege. Ehud barak na wenzake hawakwenda tu moja kwa moja kwa Mzee Kenyatta, bali kwanza walienda kwa Waziri wa kilimo wa kipindi hicho Bw. Bruce McKenzie ambaye huyu aliwahi kuwa afisa wa Idara ya ujasusi ya Uingereza, MI6 na pia alikuwa swahiba mkubwa wa Ehud Barak. Kwa hiyo Israel ikamtumia Bruce McKenzie kumshawishi Mzee Jomo Kenyatta kuruhusu anga la Kenya na viwanjavya ndege kutumiwa na makomando wa Israel na ndege zao. Ehud Barak na maafisa wa Mossad hawakuishia hapa tu, bali pia walifanya vikao vya siri na wafanyabiashara wakubwa nchini Kenya wenye asili ya Israel na wale ambao walikuwa na ‘marafiki’ wa Israel kuwaomba watumie ushawishi wao wa kisiasa na kiuchumi wasaidie kumshawishi Kenyatta kukubali ombi la seriakli ya Israael viwanja vyao kutumika na ndege za kijeshi za Israel na makondo wake. Baada ya mashinikizo haya kutoka kila upande, Mzee Kenyatta hakuwa na chaguo linguine zaidi ya kukubali ombi lao. Bwana huyu McKenzie pia alikuwa na ndege yakebinafsi, na Ehud Barak akaona fursa. Walitumia ndege hii ya kiraia kuruka mpaka Uganda mijini Entebbe na kukatiza juu ya anga la uwanja wa ndege wa Entebbe na walipokuwa wanapita juu ya anga la uwanja wa ndege, Ehud Barak akatumia fursa hii kupiga picha kila eneo la uwanja. Kwa kuwa hii ilikuwa ni ndege ya kiraia, jeshi la Uganda hawakushughulika nayo. Picha hizi zilizopigwa na Ehud Barak zilikuja kuwa na umuhimumkubwa katika maandalizi ya mwisho ya oparesheni ya makomando wa Isarel Kuvamia uwanja huu. Mpaka kufikia hapa maandalizi yote muhimu yalikuwa yamekamilika. WAKATI HUO HUO Upande wa watekaji kule Uganda walikuwa wanasubria mifwedha yao dola milioni 5 za kimarekani. Rais Idd Amin naye baada ya kufikia makubaliano na Israel kuwa masharti ya fedha na wafungwa wa kipalestina kuachiwa tarehe 4 July, naye ‘akarelax’ na akaona huo ndio muda wa kutekeleza majukumu Mengine akisubiria tarehe 4 July ifike. Katika kipindi hiki Idd amin ndiye alikuwa mwenyekiti wa Umoja wa Afrika kwa kuzingatia utaratibu wa uenyekiti kuzunguka kwa kila nchi kwa mwaka mmoja mmoja na wiki hii alikuwa anatakiwa kwenye kikao cha Umoja wa Afrika kilichokuwa kinafanyika Mauritius. Kwa hiyo Amin akafunga safari kuelekea Mauritius kwenda kukabidhi kijiti cha Uenyekiti. Ehud Barak aliposikia taarifa hii, kwa kutumia akili yake kubwa ya kuzaliwa aliyojaliwa na uzoefu wake wa ujasusi, aliona fursa adhimu kabisa hapa. Akawasiliana na walioko kikaoni huko Tel Aviv na kuwaeleza taarifa ambazo awali wote hawakuielewa. Ehud Barak: “Idd Amin akiwa ndani ya Uganda huwa anatumia Mercedes Limousine katika msafara wake” Waziri Mkuu Rabin: “Ok! Limefanyaje?’ Ehud Barak: “Nataka mtafute gari kama hiyo… Mercedes Limousine” Waziri Mkuu Rabin: “la kazi gani?” Ehud Barak: “siku ambayo kikosi cha makomando wakipanda kwenye ndege kutoka huko Israel kwenda Uganda, gari hilo nataka pia lipakiwe ndani ya ndge!” Kwa dakika kadhaa wote ambao walikuwa wanamsikiliza pale kikaoni kupitia simu hakuna ambaye alielewa nini hasa Ehud Barak alikuwa anapendekeza. Yalikuwa yamebaki masaa machache tu ambapo, weledi, ushujaa na uzalendo uliotukuka ulikuwa unaedna kudhihirika. Itaendelea #TheBOLD_JF
    0 Commenti 0 condivisioni 3K Views
  • VIETNAM WAR VITA AMBAYO MAREKANI ILISHINDWA VIBAYA

    Vita maarufu ya Vietnam ni moja ya vita katika historia ya Marekani ambazo taifa kubwa na lenye nguvu duniani lililazimika kuondoka uwanja wa mapambano baada ya kushindwa vibaya.
    Vita hii ilipiganwa kuanzia mwaka 1955 mpaka 1975, na ilipiganwa maeneo ya Vietnam kwenyewe, Laos na Cambodia.

    Kwa juu juu ilikuwa ni vita iliyopiganwa kati ya Vietnam Kaskazini na Vietnam Kusini lakini nyuma ya pazia ilikuwa ni vita ya kijasusi kati ya wababe wa dunia wa wakati huo yaani Marekani na Urusi ya Kisovieti(proxy war), huku kila mbabe akitaka kupandikiza itikadi yake kwa upande huo, Marekani akitaka Ubepari utawale na Mrusi akitaka Ukomunisti utawale.

    Vietnam ya Kaskazini ilisapotiwa na Urusi ya wakati huo(USSR), China na nchi nyingine za Kikomunisti huku Vietnam ya Kusini ikisapotiwa na Marekani, Korea Kusini, Australia, Thailand na nchi nyingine zilizokuwa zikipinga Ukomunisti.

    Wakati vuguvugu la vita limeanza kukolea mwaka 1950 Marekani ilituma kikosi cha majasusi wake nchini Vietnam wakati huo ikiwa Koloni la Mfaransa ikijulikana kama French IndoChina kwa ajili ya mafunzo, udukuzi na kukusanya taarifa za kijasusi kabla ya kuanza mashambulizi mazito, lengo likiwa kutoa mafunzo ya kijeshi na kijasusi kwa askari wa Vietnam ya Kusini na kuviandaa vikosi vyake kwa ajili ya mapigano ya kukata na shoka.

    Ilipofika mwaka 1961 wakati vita imekolea Marekani kwa kutumia taarifa za kijasusi ilizokusanya ilipeleka kikosi maalumu cha makomando wa Jeshi la Anga maarufu kama Green Berets kwa kazi kuu ya kufanya operations za kimya kimya za anga ili kulidhoofisha jeshi la Vietnam Kaskazini.
    Kikosi hiki kiliungana baadaye na kikosi cha makomando wa anga waliojulikana kama ECO 31 na US Marines.

    Hata hivyo kutokana na udhaifu wa taarifa za kijasusi vikosi hivi havikufanikiwa sana hali iliyopelekea kuvunjwa na kuundwa kikosi maalumu kingine mwaka 1962 kilichoitwa U.S. Military Assistance Command, Vietnam (MACV) kilichokuwa chini ya Idara ya Usalama ya Marekani.

    Pamoja na uwezo mkubwa wa Marekani kimafunzo na kisilaha lakini kulikuwa na udhaifu mkubwa wa idara za kijasusi hali iliyopelekea Idara nyeti za usalama za Marekani
    ikiwemo C.I.A kushindwa kutoa makadirio hasa ya kijeshi juu ya uzito wa Vita ile.

    Kutokana na nature ya nchi za Kikomunisti kuendeshwa kwa uzalendo uliotukuka, Marekani alishindwa kukusanya taarifa za msingi za kivita kwa kutumia ujasusi wa kitaaluma, badala yake alitegemea zaidi kuwahoji askari wa adui waliokamatwa na kuteswa.

    Vietnam Kaskazini kwa kusaidiwa na Majasusi wa Russia aliweza "kuwauzia taarifa feki" majasusi wa Kimarekani, na Marekani ikaingia mkenge kwa ku-underestimate uwezo wa Vietnam Kaskazini katika ulingo wa vita, kifupi taarifa za Kijasusi zilizopelekwa Washington na washirika wake zilikuwa tofauti kabisa na kilichokuwa uwanja wa mapambano.

    Kwa mfano Majasusi wa Marekani walishindwa kujua Formation ya Vita(Battle Formation) waliyokuwa wanatumia Wavietnam.
    Wavietnam wakiwa chini ya Majasusi wao wa VCSS waliweza kuunda vikosi vinne ya kimapambano vilivyopambana kwa wakati mmoja huku makamanda na wale wapiganaji mahiri wa kikosi kimoja wakibadilishana na wa Kikosi kingine huku mapambano yakiendelea.

    Kwamba unaweza kumuona leo kamanda fulani anapigana eneo A na kikosi chake akitumia mbinu fulani za msituni, mara baada ya siku tatu unashangaa imefanyika substitution kama ya kwenye mpira kaingia kamanda mpya na mbinu mpya kwa kutumia kikosi kile kile au akaleta wapiganaji wapya kabisa, huku yule wa eneo A akipelekwa eneo B na akabadili pia mbinu za kimapambano.

    Hali hii ilidumu kwa miaka 11 mfululizo mpaka mwaka 1966 Marekani ilipostukia mchezo huu wa kubadilishana makamanda na wapiganaji waliyokuwa wakitumia wa Vietnam, na ikapelekea idara za Kijasusi za Marekani husasani C.I.A na N.A.S.A kutuma upya majasusi maalumu wa kukusanya intelijensia nyingine mpya mwaka 1967.

    Lakini pia Majasusi wa Marekani walishindwa kujua uwezo wao majasusi wa Kivietnam kujipenyeza kwenye kambi ya adui(Inflitration Capabilities) waliokuwa nao Wa Vietnam.
    Inasadikika wengi wa askari wa Kivetman ya Kusini waliokula mafunzo na mbinu za Kivita kutoka Marekani na washirika wake mwanzoni kabisa mwa vuguvugu la kivita walikuwa wa Vietnam ya Kaskazini.
    Kifupi Vikosi vya Marekani viliwapa mafunzo ya kijeshi adui zao na wakauziwa Intelijensi ya uongo.

    Kubwa kuliko Yote Marekani na washirika wake hawakujua hasa Vietnam ana askari wangapi walio mstari wa mbele kwenye mapambano na wale wa akiba, iwapo wa mstari wa mbele
    wakilemewa, hali hii ilisababishwa na ukweli kuwa Vietnam Kaskazini ilikuwa inafuata itikadi za Kikomunisti, kila mtu alikuwa askari wa kuilinda nchi yake.

    Hata kama ungefanya shambulizi ukaua askari 1000 leo, kesho watakuja wengine wapya 1000 walio na morale ya kupambana mpaka kufa kama wale wa kwanza.
    Mwanzoni hili Wamarekani hawakulijua ila kadri mapigano yalivyopamba moto, askari wengi wa Marekani na Washirika wao walianza kuogopa kwenda mstari wa mbele hasa baada ya kugundua wanapambana na askari wengi wasioisha waliokuwa tayari kufa kwa ajili ya nchi yao.

    Baada ya Ripoti ya Kikosi kipya kilichoundwa na C.I.A kuja na taarifa zao za kijasusi walizokusanya uwanja wa mapambano, mwishoni mwa mwaka 1967 walikuja kupata taarifa
    za kustua sana kuwa Vietnam nao walikuwa na Shirika lao la Kijasusi lenye nguvu kubwa na lililokuwa limebobea katika tasnia ya Ujasusi lililokuwa linapewa mafunzo ya Kijasusi toka KGB Na China, Shirika hili liliojulikana kama Viet Cong Security Service (VCSS).

    Mwanzoni taarifa za Kijasusi walizozipata Wamarekani zilikuwa feki kuwa VCSS walikuwa kikosi maalum tu cha wapambanaji walio na silaha dhaifu na si majasusi.

    VCSS walikuwa wababe wa mapigano ya msituni na guilera war huku wakiwa na maajenti wengi zaidi ya 100,000.

    Walikuwa mabingwa wa vita vya kuviziana huku askari wachache wakijificha na kufanya ambush za kijeshi dhidi ya askari wa adui zao, wakati mwingine walivaa nguo za Kiraia na kuingia mtaani na kuishi maisha ya kawaiada kabisa huku wakipanga mikakati yao ya mashambulizi ya kuvizia.

    Ilikuwa ni ngumu sana kujua yupi ni raia yupi ni askari, hali hii iliwatia hofu mno askari wa Kimarekani na washirika wao waliokuwa mstari wa mbele wa mapambano, wengi wa waliokuwa wakidhani ni raia wa kawaida walikuwa ni maajenti wa VCSS.

    Kutokana na usiri mkubwa na umakini wa hali ya juu wa VCSS ilikuwa ni ngumu kwa Marekani kupata intelijensia kutoka vyanzo vya kuaminika, taarifa nyingi zilizokusanywa zilikuwa kupitia kukamata na kutesa askari wa adui waliokamatwa uwanja wa mapambano ambao wengi walikuwa ni askari wa vyeo vya chini au raia waliojitolea kupigana waliopewa mafunzo ya muda mfupi kwa ajili ya kupambana.
    Wengi wao walikuwa na taarifa za kupikwa walizopewa makusudi kwa ajili ya kupotosha iwapo wangekamatwa.

    Moja ya mbinu iliyowashusha morale askari wa kimarekani uwanja wa vita ni hit-and-run technique waliyotumia Wavietnam, Marekani alitegemea sana jeshi la anga na vikosi maalumu kupambana huku wakiwa na silaha nzito nzito za kubeba kwa magari.
    Wavietnam walichimba mahandaki njiani kuzuia magari ya silaha na mizinga kupita msituni,
    wali-block njia za kupitishia silaha za adui kwa kuangusha miti mikubwa kabla ya kufanya ambush, walitengeneza kambi za feki za kijeshi msituni na kila mbinu ya guilera war inayofahamika katika uwanja wa mapambano kubwa ikiwa kuviziana.

    Mfano askari wa ki-Vietnam walivizia kambi ya adui na kufanya ambush ndani ya saa moja na kisha kila askari kutimuka njia yake kilomita kadhaa baada ya kufanya shambulio kabla ya kukukutana tena eneo fulani kwa ajili ya kupanga shambulio jingine, na endapo wakizidiwa katika ambush zao iliwabidi askari hao kuficha silaha kwenye mahandaki na kisha kujichanganya na raia mtaani.

    Nyingi ya kambi za kupambana za Kivietnam hazikuwa zile zilizoonekana, nyingi zilikuwa chini ya mahandaki, madege ya kimarekani yaliposhambulia kambi kwa makombora yao, nyingi ya kambi hizo zilikuwa ni feki, zilizojengwa maalumu kwa ajili ya kum-distract adui, huku silaha nzito kutoka Urusi na China zikifichwa chini ya mahandaki makubwa.

    Wamarekani na Vikosi vyao walitumia teknolojia kupambana, huku wakitumia madege ya B-52, mizinga mikubwa, helkopta, kemikali za kupukutisha majani kwenye miti maarufu kama defoliants, lakini zote hazifua dafu.

    Baada ya makamanda wa vikosi vya Marekani kuona mbinu na silaha zao hazifanikiwi wakaamua kuwahamisha raia wote ambao wengi walikuwa wakulima wadogo wadogo kutoka maeneo ambayo maajenti wa VCSS walikuwa wanayamiliki kwenda sehemu salama ambazo zilikuwa chini ya ulinzi wao, hali hii ilizaa tatizo jingine pia kwani maajenti wengi wa VCSS walijifanya raia wakajipenyeza na kuingia maeneo yaliyokuwa hayana mapigano yaliyokuwa chini ya umiliki wa Vikosi vya Wamarekani na kuanza operations upya kwenye maeneo ambayo yalikuwa
    chini ya umiliki wa adui zao.

    Hili lilipelekea mashambulizi ya kuviziana kuongezeka kwenye maeneo mbayo Wamarekani walikuwa wanayashikilia, patrol zao zilivamiwa na askari kupokonywa silaha hali iliyopelekea morale ya askari kushuka sana, ikabidi Askari wa Kimarekani waandae ndege standby kwa ajili ya kutoa msaada muda wowote patrol zao zitakapostambuliwa,
    lakini bado haikusaidia kitu kwani wengi wa askari wa patrol hawakutaka kabisa kuingia maeneo ya ndani ndani walipita njia kuu na maeneo ya wazi kuogopa mashambulizi ya kushtukiza ambayo Shirika la Kijasusi la VCSS lilikuwa limesambaza maajenti zaidi ya 100,000.

    Kutokana na ripoti za Kijasusi kuvuja nchini Marekani kuwa probability ya kuuwawa kwa askari wao walio vitani nchini Vietnam kuwa ni zaidi ya 20% na kuwa askari waliokuwa mapiganoni wengi walikuwa wanaogopa gorilla war iliyokuwa ikiendeshwa na Wavietnam, ripoti za siri za kijasusi zinasema C.I.A kwa kutumia mbinu za kijasusi waliandaa exit strategy ambayo ilikuwa ni
    kuhamasisha maandamano na propaganda ya kile kilichoitwa vuguvugu la wananchi wa Marekani kupinga nchi yao kujiingiza katika vita ya Vietnam.

    Hatimaye Marekani kwa kisingizio cha maandamano ya wananchi kupinga nchi yao kujiingiza Vietnam mwaka 1973 waliondoa vikosi vyao na kuikabidhi Vietnam Kusini jukumu la kuendelea na mapambano dhidi ya Kaskazini.

    Vietnam ya Kaskazini iliendesha mapigano kwa miaka miwili mfululizo na hatimaye mwaka 1975 ikaukamata mji mashuhuri sana wa Saigon uliokuwa unamilikiwa na Vietnam Kusini na mwaka mmoja baadaye Kusini na Kaskazini zikaungana na kutengeneza nchi moja ya Jamhuri ya watu wa Vietnam.

    Inakadiriwa kuwa vita hiyo iligharimu maisha ya WaVietnam kati ya 966,000 mpaka Milioni 3.8 Wakambodia kati ya 240,000–300,000, Walaotia kati ya 20,000–62,000 na Wamarekani zaidi ya 58,220 huku Wamarekani zaidi ya 1,626 wakipotea na hawakujulikana walipo mpaka leo

    Mwisho
    VIETNAM WAR VITA AMBAYO MAREKANI ILISHINDWA VIBAYA Vita maarufu ya Vietnam ni moja ya vita katika historia ya Marekani ambazo taifa kubwa na lenye nguvu duniani lililazimika kuondoka uwanja wa mapambano baada ya kushindwa vibaya. Vita hii ilipiganwa kuanzia mwaka 1955 mpaka 1975, na ilipiganwa maeneo ya Vietnam kwenyewe, Laos na Cambodia. Kwa juu juu ilikuwa ni vita iliyopiganwa kati ya Vietnam Kaskazini na Vietnam Kusini lakini nyuma ya pazia ilikuwa ni vita ya kijasusi kati ya wababe wa dunia wa wakati huo yaani Marekani na Urusi ya Kisovieti(proxy war), huku kila mbabe akitaka kupandikiza itikadi yake kwa upande huo, Marekani akitaka Ubepari utawale na Mrusi akitaka Ukomunisti utawale. Vietnam ya Kaskazini ilisapotiwa na Urusi ya wakati huo(USSR), China na nchi nyingine za Kikomunisti huku Vietnam ya Kusini ikisapotiwa na Marekani, Korea Kusini, Australia, Thailand na nchi nyingine zilizokuwa zikipinga Ukomunisti. Wakati vuguvugu la vita limeanza kukolea mwaka 1950 Marekani ilituma kikosi cha majasusi wake nchini Vietnam wakati huo ikiwa Koloni la Mfaransa ikijulikana kama French IndoChina kwa ajili ya mafunzo, udukuzi na kukusanya taarifa za kijasusi kabla ya kuanza mashambulizi mazito, lengo likiwa kutoa mafunzo ya kijeshi na kijasusi kwa askari wa Vietnam ya Kusini na kuviandaa vikosi vyake kwa ajili ya mapigano ya kukata na shoka. Ilipofika mwaka 1961 wakati vita imekolea Marekani kwa kutumia taarifa za kijasusi ilizokusanya ilipeleka kikosi maalumu cha makomando wa Jeshi la Anga maarufu kama Green Berets kwa kazi kuu ya kufanya operations za kimya kimya za anga ili kulidhoofisha jeshi la Vietnam Kaskazini. Kikosi hiki kiliungana baadaye na kikosi cha makomando wa anga waliojulikana kama ECO 31 na US Marines. Hata hivyo kutokana na udhaifu wa taarifa za kijasusi vikosi hivi havikufanikiwa sana hali iliyopelekea kuvunjwa na kuundwa kikosi maalumu kingine mwaka 1962 kilichoitwa U.S. Military Assistance Command, Vietnam (MACV) kilichokuwa chini ya Idara ya Usalama ya Marekani. Pamoja na uwezo mkubwa wa Marekani kimafunzo na kisilaha lakini kulikuwa na udhaifu mkubwa wa idara za kijasusi hali iliyopelekea Idara nyeti za usalama za Marekani ikiwemo C.I.A kushindwa kutoa makadirio hasa ya kijeshi juu ya uzito wa Vita ile. Kutokana na nature ya nchi za Kikomunisti kuendeshwa kwa uzalendo uliotukuka, Marekani alishindwa kukusanya taarifa za msingi za kivita kwa kutumia ujasusi wa kitaaluma, badala yake alitegemea zaidi kuwahoji askari wa adui waliokamatwa na kuteswa. Vietnam Kaskazini kwa kusaidiwa na Majasusi wa Russia aliweza "kuwauzia taarifa feki" majasusi wa Kimarekani, na Marekani ikaingia mkenge kwa ku-underestimate uwezo wa Vietnam Kaskazini katika ulingo wa vita, kifupi taarifa za Kijasusi zilizopelekwa Washington na washirika wake zilikuwa tofauti kabisa na kilichokuwa uwanja wa mapambano. Kwa mfano Majasusi wa Marekani walishindwa kujua Formation ya Vita(Battle Formation) waliyokuwa wanatumia Wavietnam. Wavietnam wakiwa chini ya Majasusi wao wa VCSS waliweza kuunda vikosi vinne ya kimapambano vilivyopambana kwa wakati mmoja huku makamanda na wale wapiganaji mahiri wa kikosi kimoja wakibadilishana na wa Kikosi kingine huku mapambano yakiendelea. Kwamba unaweza kumuona leo kamanda fulani anapigana eneo A na kikosi chake akitumia mbinu fulani za msituni, mara baada ya siku tatu unashangaa imefanyika substitution kama ya kwenye mpira kaingia kamanda mpya na mbinu mpya kwa kutumia kikosi kile kile au akaleta wapiganaji wapya kabisa, huku yule wa eneo A akipelekwa eneo B na akabadili pia mbinu za kimapambano. Hali hii ilidumu kwa miaka 11 mfululizo mpaka mwaka 1966 Marekani ilipostukia mchezo huu wa kubadilishana makamanda na wapiganaji waliyokuwa wakitumia wa Vietnam, na ikapelekea idara za Kijasusi za Marekani husasani C.I.A na N.A.S.A kutuma upya majasusi maalumu wa kukusanya intelijensia nyingine mpya mwaka 1967. Lakini pia Majasusi wa Marekani walishindwa kujua uwezo wao majasusi wa Kivietnam kujipenyeza kwenye kambi ya adui(Inflitration Capabilities) waliokuwa nao Wa Vietnam. Inasadikika wengi wa askari wa Kivetman ya Kusini waliokula mafunzo na mbinu za Kivita kutoka Marekani na washirika wake mwanzoni kabisa mwa vuguvugu la kivita walikuwa wa Vietnam ya Kaskazini. Kifupi Vikosi vya Marekani viliwapa mafunzo ya kijeshi adui zao na wakauziwa Intelijensi ya uongo. Kubwa kuliko Yote Marekani na washirika wake hawakujua hasa Vietnam ana askari wangapi walio mstari wa mbele kwenye mapambano na wale wa akiba, iwapo wa mstari wa mbele wakilemewa, hali hii ilisababishwa na ukweli kuwa Vietnam Kaskazini ilikuwa inafuata itikadi za Kikomunisti, kila mtu alikuwa askari wa kuilinda nchi yake. Hata kama ungefanya shambulizi ukaua askari 1000 leo, kesho watakuja wengine wapya 1000 walio na morale ya kupambana mpaka kufa kama wale wa kwanza. Mwanzoni hili Wamarekani hawakulijua ila kadri mapigano yalivyopamba moto, askari wengi wa Marekani na Washirika wao walianza kuogopa kwenda mstari wa mbele hasa baada ya kugundua wanapambana na askari wengi wasioisha waliokuwa tayari kufa kwa ajili ya nchi yao. Baada ya Ripoti ya Kikosi kipya kilichoundwa na C.I.A kuja na taarifa zao za kijasusi walizokusanya uwanja wa mapambano, mwishoni mwa mwaka 1967 walikuja kupata taarifa za kustua sana kuwa Vietnam nao walikuwa na Shirika lao la Kijasusi lenye nguvu kubwa na lililokuwa limebobea katika tasnia ya Ujasusi lililokuwa linapewa mafunzo ya Kijasusi toka KGB Na China, Shirika hili liliojulikana kama Viet Cong Security Service (VCSS). Mwanzoni taarifa za Kijasusi walizozipata Wamarekani zilikuwa feki kuwa VCSS walikuwa kikosi maalum tu cha wapambanaji walio na silaha dhaifu na si majasusi. VCSS walikuwa wababe wa mapigano ya msituni na guilera war huku wakiwa na maajenti wengi zaidi ya 100,000. Walikuwa mabingwa wa vita vya kuviziana huku askari wachache wakijificha na kufanya ambush za kijeshi dhidi ya askari wa adui zao, wakati mwingine walivaa nguo za Kiraia na kuingia mtaani na kuishi maisha ya kawaiada kabisa huku wakipanga mikakati yao ya mashambulizi ya kuvizia. Ilikuwa ni ngumu sana kujua yupi ni raia yupi ni askari, hali hii iliwatia hofu mno askari wa Kimarekani na washirika wao waliokuwa mstari wa mbele wa mapambano, wengi wa waliokuwa wakidhani ni raia wa kawaida walikuwa ni maajenti wa VCSS. Kutokana na usiri mkubwa na umakini wa hali ya juu wa VCSS ilikuwa ni ngumu kwa Marekani kupata intelijensia kutoka vyanzo vya kuaminika, taarifa nyingi zilizokusanywa zilikuwa kupitia kukamata na kutesa askari wa adui waliokamatwa uwanja wa mapambano ambao wengi walikuwa ni askari wa vyeo vya chini au raia waliojitolea kupigana waliopewa mafunzo ya muda mfupi kwa ajili ya kupambana. Wengi wao walikuwa na taarifa za kupikwa walizopewa makusudi kwa ajili ya kupotosha iwapo wangekamatwa. Moja ya mbinu iliyowashusha morale askari wa kimarekani uwanja wa vita ni hit-and-run technique waliyotumia Wavietnam, Marekani alitegemea sana jeshi la anga na vikosi maalumu kupambana huku wakiwa na silaha nzito nzito za kubeba kwa magari. Wavietnam walichimba mahandaki njiani kuzuia magari ya silaha na mizinga kupita msituni, wali-block njia za kupitishia silaha za adui kwa kuangusha miti mikubwa kabla ya kufanya ambush, walitengeneza kambi za feki za kijeshi msituni na kila mbinu ya guilera war inayofahamika katika uwanja wa mapambano kubwa ikiwa kuviziana. Mfano askari wa ki-Vietnam walivizia kambi ya adui na kufanya ambush ndani ya saa moja na kisha kila askari kutimuka njia yake kilomita kadhaa baada ya kufanya shambulio kabla ya kukukutana tena eneo fulani kwa ajili ya kupanga shambulio jingine, na endapo wakizidiwa katika ambush zao iliwabidi askari hao kuficha silaha kwenye mahandaki na kisha kujichanganya na raia mtaani. Nyingi ya kambi za kupambana za Kivietnam hazikuwa zile zilizoonekana, nyingi zilikuwa chini ya mahandaki, madege ya kimarekani yaliposhambulia kambi kwa makombora yao, nyingi ya kambi hizo zilikuwa ni feki, zilizojengwa maalumu kwa ajili ya kum-distract adui, huku silaha nzito kutoka Urusi na China zikifichwa chini ya mahandaki makubwa. Wamarekani na Vikosi vyao walitumia teknolojia kupambana, huku wakitumia madege ya B-52, mizinga mikubwa, helkopta, kemikali za kupukutisha majani kwenye miti maarufu kama defoliants, lakini zote hazifua dafu. Baada ya makamanda wa vikosi vya Marekani kuona mbinu na silaha zao hazifanikiwi wakaamua kuwahamisha raia wote ambao wengi walikuwa wakulima wadogo wadogo kutoka maeneo ambayo maajenti wa VCSS walikuwa wanayamiliki kwenda sehemu salama ambazo zilikuwa chini ya ulinzi wao, hali hii ilizaa tatizo jingine pia kwani maajenti wengi wa VCSS walijifanya raia wakajipenyeza na kuingia maeneo yaliyokuwa hayana mapigano yaliyokuwa chini ya umiliki wa Vikosi vya Wamarekani na kuanza operations upya kwenye maeneo ambayo yalikuwa chini ya umiliki wa adui zao. Hili lilipelekea mashambulizi ya kuviziana kuongezeka kwenye maeneo mbayo Wamarekani walikuwa wanayashikilia, patrol zao zilivamiwa na askari kupokonywa silaha hali iliyopelekea morale ya askari kushuka sana, ikabidi Askari wa Kimarekani waandae ndege standby kwa ajili ya kutoa msaada muda wowote patrol zao zitakapostambuliwa, lakini bado haikusaidia kitu kwani wengi wa askari wa patrol hawakutaka kabisa kuingia maeneo ya ndani ndani walipita njia kuu na maeneo ya wazi kuogopa mashambulizi ya kushtukiza ambayo Shirika la Kijasusi la VCSS lilikuwa limesambaza maajenti zaidi ya 100,000. Kutokana na ripoti za Kijasusi kuvuja nchini Marekani kuwa probability ya kuuwawa kwa askari wao walio vitani nchini Vietnam kuwa ni zaidi ya 20% na kuwa askari waliokuwa mapiganoni wengi walikuwa wanaogopa gorilla war iliyokuwa ikiendeshwa na Wavietnam, ripoti za siri za kijasusi zinasema C.I.A kwa kutumia mbinu za kijasusi waliandaa exit strategy ambayo ilikuwa ni kuhamasisha maandamano na propaganda ya kile kilichoitwa vuguvugu la wananchi wa Marekani kupinga nchi yao kujiingiza katika vita ya Vietnam. Hatimaye Marekani kwa kisingizio cha maandamano ya wananchi kupinga nchi yao kujiingiza Vietnam mwaka 1973 waliondoa vikosi vyao na kuikabidhi Vietnam Kusini jukumu la kuendelea na mapambano dhidi ya Kaskazini. Vietnam ya Kaskazini iliendesha mapigano kwa miaka miwili mfululizo na hatimaye mwaka 1975 ikaukamata mji mashuhuri sana wa Saigon uliokuwa unamilikiwa na Vietnam Kusini na mwaka mmoja baadaye Kusini na Kaskazini zikaungana na kutengeneza nchi moja ya Jamhuri ya watu wa Vietnam. Inakadiriwa kuwa vita hiyo iligharimu maisha ya WaVietnam kati ya 966,000 mpaka Milioni 3.8 Wakambodia kati ya 240,000–300,000, Walaotia kati ya 20,000–62,000 na Wamarekani zaidi ya 58,220 huku Wamarekani zaidi ya 1,626 wakipotea na hawakujulikana walipo mpaka leo Mwisho
    0 Commenti 0 condivisioni 3K Views