• Rais wa Marekani , Donald Trump ametupilia mbali madai kwamba Nchi ya Urusi imekataa mapendekezo ya Nchi yake ya Marekani ya kusitisha mapigano Nchini Ukraine . Kiongozi huyo wa Marekani alionyesha kwa ufanisi kuwa ni mapema kujadili kuimarisha vikwazo vya Nchi ya Marekani dhidi ya Urusi.

    "Yeye (Rais wa Urusi Vladimir Putin ) hakukataa chochote. Na wana vikwazo," - Donald Trump aliwaambia Waandishi wa habari katika Ikulu ya Marekani (White House), akijibu swali ikiwa Marekani inapaswa kuimarisha vikwazo dhidi ya Urusi kwa sababu madai ya Putin kukataa usitishaji vita Nchini Ukraine.

    "Wana takriban vikwazo zaidi kuliko mtu yeyote," aliongeza

    Putin na Trump walipiga simu mnamo Machi 18, 2025 wakijadili wazo la kusitisha mapigano kwa siku thelathini katika mzozo wa Ukraine, njia za kuzuia kuongezeka zaidi kwa mvutano na masuala kadhaa ya kimataifa, Kremlin ilisema. Kulingana na maelezo yake ya wito huo, Kiongozi huyo wa Urusi aliunga mkono mpango wa Rais wa Marekani wa kusitisha mapigano ya nishati na miundombinu Nchini Ukraine.

    Ikulu ya White House ilisema katika usomaji huo kwamba Viongozi hao wawili pia walikubaliana kuanza mazungumzo ya kiufundi "juu ya utekelezaji wa usitishaji vita wa baharini katika Bahari Nyeusi, usitishaji kamili wa mapigano na amani ya kudumu."

    Rais wa Marekani 🇺🇸, Donald Trump ametupilia mbali madai kwamba Nchi ya Urusi 🇷🇺 imekataa mapendekezo ya Nchi yake ya Marekani ya kusitisha mapigano Nchini Ukraine 🇺🇦. Kiongozi huyo wa Marekani alionyesha kwa ufanisi kuwa ni mapema kujadili kuimarisha vikwazo vya Nchi ya Marekani dhidi ya Urusi. "Yeye (Rais wa Urusi Vladimir Putin ) hakukataa chochote. Na wana vikwazo," - Donald Trump aliwaambia Waandishi wa habari katika Ikulu ya Marekani (White House), akijibu swali ikiwa Marekani inapaswa kuimarisha vikwazo dhidi ya Urusi kwa sababu madai ya Putin kukataa usitishaji vita Nchini Ukraine. "Wana takriban vikwazo zaidi kuliko mtu yeyote," aliongeza Putin na Trump walipiga simu mnamo Machi 18, 2025 wakijadili wazo la kusitisha mapigano kwa siku thelathini katika mzozo wa Ukraine, njia za kuzuia kuongezeka zaidi kwa mvutano na masuala kadhaa ya kimataifa, Kremlin ilisema. Kulingana na maelezo yake ya wito huo, Kiongozi huyo wa Urusi aliunga mkono mpango wa Rais wa Marekani wa kusitisha mapigano ya nishati na miundombinu Nchini Ukraine. Ikulu ya White House ilisema katika usomaji huo kwamba Viongozi hao wawili pia walikubaliana kuanza mazungumzo ya kiufundi "juu ya utekelezaji wa usitishaji vita wa baharini katika Bahari Nyeusi, usitishaji kamili wa mapigano na amani ya kudumu."
    Love
    1
    0 التعليقات 0 المشاركات 1كيلو بايت مشاهدة
  • Rais wa Marekani , Donald Trump ameendelea na msimamo wake na kuweka mkazo kuhusu kuifanya Nchi ya Canada kuwa jimbo la (51) la Nchi ya Marekani. Kupitia ukurasa wake wa mtandao X, Rais huyo amesema kuwa Nchi yake ya Marekani inatumia mabilioni ya fedha na punguzo za ushuru kuihudumia Canada hivyo hakuna haja Nchi hiyo kuendelea kuifaidi Marekani wakati ingeweza kuwa sehemu ya Marekani na kupata unafuu bila kuinyonya Nchi ya Marekani.

    Donald Trump amesema iwapo Nchi ya Canada itakataa mpango huo basi tozo na ushuru wa bidhaa kwa Taifa hilo utapanda mara dufu na kulingana mataifa mengine. Trump amesema iwapo Canada ikijiunga na Marekani hakutakuwa na tozo wala mazuio ya maelfu ya Raia wa Canada wanaoingia Marekani kufanya kazi.

    Ikumbukwe kwamba Nchi za Canada na Mexico ni kati ya mataifa yenye Raia wengi wanaofanya kazi za kujiingizia kipato Nchini Marekani ambao hawana vibali halali vya kazi na uhamiaji (Wahamiaji haramu). Tayari Donald Trump ameshaongea na Viongozi wakuu wa mataifa hayo na kuwapa muda wa siku thelathini (30) kuchukua hatua kwa mapendekezo yake ama utozaji wa tozo na ushuru wa asilimia (25) kwa bidhaa zao uanze mara moja.

    Viongozi wa Nchi hizo wamekiri kupokea maelekezo ya Trump na kuahidi kuchukua hatua ikiwemo kuzuia mipaka yao kuwa njia za Wahamiaji haramu. Waziri Mkuu wa Canada, Justin Tradeau amesema Canada kuwa sehemu ya Marekani haitawezekana licha ya kwamba huenda wakakutana rungu la kiuchumi kisha Wananchi wakaamua wenyewe kupitia uchunguzi (kura).

    Rais wa Marekani 🇺🇸, Donald Trump ameendelea na msimamo wake na kuweka mkazo kuhusu kuifanya Nchi ya Canada 🇨🇦 kuwa jimbo la (51) la Nchi ya Marekani. Kupitia ukurasa wake wa mtandao X, Rais huyo amesema kuwa Nchi yake ya Marekani inatumia mabilioni ya fedha na punguzo za ushuru kuihudumia Canada hivyo hakuna haja Nchi hiyo kuendelea kuifaidi Marekani wakati ingeweza kuwa sehemu ya Marekani na kupata unafuu bila kuinyonya Nchi ya Marekani. Donald Trump amesema iwapo Nchi ya Canada itakataa mpango huo basi tozo na ushuru wa bidhaa kwa Taifa hilo utapanda mara dufu na kulingana mataifa mengine. Trump amesema iwapo Canada ikijiunga na Marekani hakutakuwa na tozo wala mazuio ya maelfu ya Raia wa Canada wanaoingia Marekani kufanya kazi. Ikumbukwe kwamba Nchi za Canada na Mexico 🇲🇽 ni kati ya mataifa yenye Raia wengi wanaofanya kazi za kujiingizia kipato Nchini Marekani ambao hawana vibali halali vya kazi na uhamiaji (Wahamiaji haramu). Tayari Donald Trump ameshaongea na Viongozi wakuu wa mataifa hayo na kuwapa muda wa siku thelathini (30) kuchukua hatua kwa mapendekezo yake ama utozaji wa tozo na ushuru wa asilimia (25) kwa bidhaa zao uanze mara moja. Viongozi wa Nchi hizo wamekiri kupokea maelekezo ya Trump na kuahidi kuchukua hatua ikiwemo kuzuia mipaka yao kuwa njia za Wahamiaji haramu. Waziri Mkuu wa Canada, Justin Tradeau amesema Canada kuwa sehemu ya Marekani haitawezekana licha ya kwamba huenda wakakutana rungu la kiuchumi kisha Wananchi wakaamua wenyewe kupitia uchunguzi (kura).
    Love
    1
    0 التعليقات 0 المشاركات 1كيلو بايت مشاهدة
  • Chukua hii.

    Kuna kijiji kimoja huko Nchini Japan kiitwacho Shirakawa, nyumba zake za kihistoria zilizoezekwa kwa kutumia nyasi zinalindwa kwa majanga ya Moto. Wakati moto ukitokea mabomba hayo yaliyokuwa chini ya ardhi zaidi ya sitini (60) yanaibuka juu na kutoa maji kwa "pressure" kubwa hadi kufikia mita thelathini (30).

    Mabomba hayo yamefichwa chini ya Ardhi ili kulinda Nyumba za hizo kihistoria ya kijapani dhidi ya Moto. Mfumo huu hujaribiwa mara mbili (2) kila Mwaka yaani Mwezi Mei na Disemba kupitia kikosi cha zima moto cha eneo hilo. Hata katika hali ya hewa ya mvua, wakati wa kufanya mazoezi hutengeneza upinde wa mvua wenye kuvutia juu ya paa, na kuvutia Watazamaji kutoka Ulimwenguni kote.

    Chukua hii. Kuna kijiji kimoja huko Nchini Japan kiitwacho Shirakawa, nyumba zake za kihistoria zilizoezekwa kwa kutumia nyasi zinalindwa kwa majanga ya Moto. Wakati moto ukitokea mabomba hayo yaliyokuwa chini ya ardhi zaidi ya sitini (60) yanaibuka juu na kutoa maji kwa "pressure" kubwa hadi kufikia mita thelathini (30). Mabomba hayo yamefichwa chini ya Ardhi ili kulinda Nyumba za hizo kihistoria ya kijapani dhidi ya Moto. Mfumo huu hujaribiwa mara mbili (2) kila Mwaka yaani Mwezi Mei na Disemba kupitia kikosi cha zima moto cha eneo hilo. Hata katika hali ya hewa ya mvua, wakati wa kufanya mazoezi hutengeneza upinde wa mvua wenye kuvutia juu ya paa, na kuvutia Watazamaji kutoka Ulimwenguni kote.
    0 التعليقات 0 المشاركات 446 مشاهدة