• 0 Comments 0 Shares 123 Views
  • 0 Comments 0 Shares 126 Views
  • 0 Comments 0 Shares 127 Views
  • 0 Comments 0 Shares 130 Views
  • "Hatakama Yanga wangevuka hatua ya makundi na kwenda robo fainali ya CAF Champions Ligi, huku mshabuliaji wao kinara akiwa PRINCE DUBE bado uwezekano wa kufanya vyema ungekuwa mdogo msimu huu, kwakuwa ni dhahiri sasa kwamba DUBE sio mfungaji asilia, ni aina ya mshambuliaji anaehitaji nafasi 6 za WAZI kufunga mabao 2 dhidi ya KEN GOLD walio mkiani kwenye ligi kuu" - Jemedari Said, Mchambuzi.

    "Hatakama Yanga wangevuka hatua ya makundi na kwenda robo fainali ya CAF Champions Ligi, huku mshabuliaji wao kinara akiwa PRINCE DUBE bado uwezekano wa kufanya vyema ungekuwa mdogo msimu huu, kwakuwa ni dhahiri sasa kwamba DUBE sio mfungaji asilia, ni aina ya mshambuliaji anaehitaji nafasi 6 za WAZI kufunga mabao 2 dhidi ya KEN GOLD walio mkiani kwenye ligi kuu" - Jemedari Said, Mchambuzi.
    0 Comments 0 Shares 342 Views
  • Inaripotiwa kuwa zaidi ya Wafungwa mia moja (100) wa kike walibakwa na kisha kuchomwa moto wakiwa hai wakati wa hali ya machafuko ilipotokea baada ya Wafungwa kutoroka Gerezani Jijini Goma, Nchini Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo .

    Kulingana na ripoti mpya kutoka kwa Umoja wa Mataifa, mamia ya Wafungwa walitoroka katika Gereza la Munzenze Jumatatu iliyopita, baada ya Wapiganaji wa kundi la Waasi la M23 kuuteka Mji huo wa Goma.

    Ripoti hiyo inaeleza kwamba kati ya Wanawake 165 na 167 walivamiwa na kunyanyaswa na Wafungwa wa kiume walipovunja Gereza. Wengi wa Wanawake hao waliuawa baada ya Wafungwa hao kuchoma moto jela. Jiji hilo la Goma lina ukubwa na Watu zaidi milioni moja (1), lilitekwa na kundi la Waasi la M23, linalodaiwa kuungwa mkono na Rwanda , lilipovamia mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo.

    Inaripotiwa kuwa zaidi ya Wafungwa mia moja (100) wa kike walibakwa na kisha kuchomwa moto wakiwa hai wakati wa hali ya machafuko ilipotokea baada ya Wafungwa kutoroka Gerezani Jijini Goma, Nchini Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo 馃嚚馃嚛. Kulingana na ripoti mpya kutoka kwa Umoja wa Mataifa, mamia ya Wafungwa walitoroka katika Gereza la Munzenze Jumatatu iliyopita, baada ya Wapiganaji wa kundi la Waasi la M23 kuuteka Mji huo wa Goma. Ripoti hiyo inaeleza kwamba kati ya Wanawake 165 na 167 walivamiwa na kunyanyaswa na Wafungwa wa kiume walipovunja Gereza. Wengi wa Wanawake hao waliuawa baada ya Wafungwa hao kuchoma moto jela. Jiji hilo la Goma lina ukubwa na Watu zaidi milioni moja (1), lilitekwa na kundi la Waasi la M23, linalodaiwa kuungwa mkono na Rwanda 馃嚪馃嚰, lilipovamia mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo.
    0 Comments 0 Shares 236 Views
  • Kwa sasa, hakuna klabu yoyote iliyojaribu kumchukua Paul Pogba! . Mchezaji huyo bado anamatumaini kurudi katika Timu ya Taifa ya Ufaransa na yuko tayari kusubiri hadi majira ya kiangazi akingojea ofa kutoka kwa klabu za Ulaya.

    Ikumbukwe kwamba adhabu yake ya kusimamishwa kwa sababu ya matumizi ya madawa ya kulevya itamalizika tarehe 11 Machi.

    Kwa sasa, hakuna klabu yoyote iliyojaribu kumchukua Paul Pogba! 馃嚝馃嚪. Mchezaji huyo bado anamatumaini kurudi katika Timu ya Taifa ya Ufaransa na yuko tayari kusubiri hadi majira ya kiangazi akingojea ofa kutoka kwa klabu za Ulaya. Ikumbukwe kwamba adhabu yake ya kusimamishwa kwa sababu ya matumizi ya madawa ya kulevya itamalizika tarehe 11 Machi.
    0 Comments 0 Shares 456 Views
  • Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, imemhukumu Msanii wa muziki wa zamani Ferdnand Ndikuriyo (27) maarufu Chuma cha Chuma kutoka Nchini Burundi , kutumikia kifungo cha miaka mitatu (3) Jela na kulipa faini ya Shilingi 500,000 baada ya kukutwa na hatia ya kuishi Nchini Tanzania bila kibali.

    Hukumu hiyo imetolewa leo, Februari 5, 2025, na Hakimu Mkazi Mkuu, Yusto Ruboroga, baada ya upande wa mashtaka kuthibitisha shtaka dhidi ya mshtakiwa. Ikumbukwe kwamba Chuma cha Chuma alikamatwa kwa kosa hilo Septemba 18, 2024, katika eneo la Las Vegas Casino, Upanga Wilayani Ilala, Jijini Dar es Salaam.

    Hakimu Ruboroga alisema kuwa mshtakiwa ni Mkosaji wa mara ya pili (2) na kwamba anahitaji kupewa adhabu kali ili iwe fundisho kwake na kwa Watu wengine wanaojihusisha na vitendo kama hivyo vya kuingia Nchini Tanzania bila vibali (uhamiaji haramu).

    Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, imemhukumu Msanii wa muziki wa zamani Ferdnand Ndikuriyo (27) maarufu Chuma cha Chuma kutoka Nchini Burundi 馃嚙馃嚠, kutumikia kifungo cha miaka mitatu (3) Jela na kulipa faini ya Shilingi 500,000 baada ya kukutwa na hatia ya kuishi Nchini Tanzania 馃嚬馃嚳 bila kibali. Hukumu hiyo imetolewa leo, Februari 5, 2025, na Hakimu Mkazi Mkuu, Yusto Ruboroga, baada ya upande wa mashtaka kuthibitisha shtaka dhidi ya mshtakiwa. Ikumbukwe kwamba Chuma cha Chuma alikamatwa kwa kosa hilo Septemba 18, 2024, katika eneo la Las Vegas Casino, Upanga Wilayani Ilala, Jijini Dar es Salaam. Hakimu Ruboroga alisema kuwa mshtakiwa ni Mkosaji wa mara ya pili (2) na kwamba anahitaji kupewa adhabu kali ili iwe fundisho kwake na kwa Watu wengine wanaojihusisha na vitendo kama hivyo vya kuingia Nchini Tanzania bila vibali (uhamiaji haramu).
    0 Comments 0 Shares 351 Views
  • Rais wa Marekani , Donald Trump amesaini amri ya utendaji kuiondoa rasmi Nchi ya Marekani kutoka Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa (UNHRC) na Shirika la Misaada na Kazi la Umoja wa Mataifa kwa Wakimbizi wa Kipalestina (UNRWA).

    Aidha, ameagiza mapitio ya ushiriki wa Marekani katika Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO). Hatua hiyo ilifanyika Februari 4, 2025, ambapo kipande cha video fupi kilichowekwa kwenye mtandao wa X wa Rais Trump kilionyesha Katibu wa Wafanyakazi wa Ikulu ya White House, Will Scharf, akimkabidhi Rais agizo hilo kwa ajili ya kutia saini.

    "Kwa kuzingatia hatua nyingi zilizochukuliwa na mashirika kadhaa ya Umoja wa Mataifa ambazo zimeonyesha upendeleo mkubwa wa chuki dhidi ya Marekani, tuna agizo la utendaji lililotayarishwa kwa ajili yako ambalo lingeiondoa Marekani kutoka UNHRC na UNRWA, huku pia likipitia upya ushiriki wetu katika UNESCO." amesema Will Scharf kama sababu ya Donald Trump kuamua kujiondoa kwenye Mashirika hayo.

    Ameongeza kuwa agizo hilo pia linaelekeza ukaguzi wa kina wa ushiriki wa Marekani katika Umoja wa Mataifa kwa ujumla, hususan kuhusu tofaudi kubwa za ufadhili zinazotolewa na Marekani ikilinganishwa na mataifa mengine ambayo "hayatendei haki Marekani".

    Rais wa Marekani 馃嚭馃嚫, Donald Trump amesaini amri ya utendaji kuiondoa rasmi Nchi ya Marekani kutoka Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa (UNHRC) na Shirika la Misaada na Kazi la Umoja wa Mataifa kwa Wakimbizi wa Kipalestina (UNRWA). Aidha, ameagiza mapitio ya ushiriki wa Marekani katika Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO). Hatua hiyo ilifanyika Februari 4, 2025, ambapo kipande cha video fupi kilichowekwa kwenye mtandao wa X wa Rais Trump kilionyesha Katibu wa Wafanyakazi wa Ikulu ya White House, Will Scharf, akimkabidhi Rais agizo hilo kwa ajili ya kutia saini. "Kwa kuzingatia hatua nyingi zilizochukuliwa na mashirika kadhaa ya Umoja wa Mataifa ambazo zimeonyesha upendeleo mkubwa wa chuki dhidi ya Marekani, tuna agizo la utendaji lililotayarishwa kwa ajili yako ambalo lingeiondoa Marekani kutoka UNHRC na UNRWA, huku pia likipitia upya ushiriki wetu katika UNESCO." amesema Will Scharf kama sababu ya Donald Trump kuamua kujiondoa kwenye Mashirika hayo. Ameongeza kuwa agizo hilo pia linaelekeza ukaguzi wa kina wa ushiriki wa Marekani katika Umoja wa Mataifa kwa ujumla, hususan kuhusu tofaudi kubwa za ufadhili zinazotolewa na Marekani ikilinganishwa na mataifa mengine ambayo "hayatendei haki Marekani".
    0 Comments 0 Shares 549 Views
  • Msanii wa Nigeria , Wizkid achangia kumpa Bob Marley tuzo yake akiwa ni Marehemu.

    Pamoja na mafanikio makubwa aliyoyapata akiwa hai, Mwanamziki nguli Duniani, Raia wa Jamaica , Bob Marley hakuwahi kushinda tuzo ya Grammy katika maisha yake, lakini miaka michache iliopita familia yake walimtafuta Msanii kutoka Nchini Nigeria, Wizkid kwa ajili ya kufanya Collabo na Bob Marley ili waweze kuifanya upya kazi ya Bob Marley "One love, Music inspired by the Film, Album.

    Baada ya albamu hiyo kutoka ambapo Wizkid ameifanya upya imeshinda albamu bora ya mwaka ya Reggae 2025 kwenye tuzo za Grammy na kuweka rekodi ya kuwa tuzo ya kwanza ya Grammy ya Bob Marley huku shukurani kubwa amepewa Wizkid.

    Aidha, Wizkid amepokea cheti kutoka kwenye Uongozi wa Grammy na barua ya shukurani kutoka kwa familia ya Marley kwa kuifanya heshima ya baba yao kuendelea kuwepo Duniani na kumsaidia Mwanamziki huyo Mkongwe wa muziki wa Reggae kushinda Grammy yake ya kwanza.

    Msanii wa Nigeria 馃嚦馃嚞, Wizkid achangia kumpa Bob Marley tuzo yake akiwa ni Marehemu. Pamoja na mafanikio makubwa aliyoyapata akiwa hai, Mwanamziki nguli Duniani, Raia wa Jamaica 馃嚡馃嚥, Bob Marley hakuwahi kushinda tuzo ya Grammy katika maisha yake, lakini miaka michache iliopita familia yake walimtafuta Msanii kutoka Nchini Nigeria, Wizkid kwa ajili ya kufanya Collabo na Bob Marley ili waweze kuifanya upya kazi ya Bob Marley "One love, Music inspired by the Film, Album. Baada ya albamu hiyo kutoka ambapo Wizkid ameifanya upya imeshinda albamu bora ya mwaka ya Reggae 2025 kwenye tuzo za Grammy na kuweka rekodi ya kuwa tuzo ya kwanza ya Grammy ya Bob Marley huku shukurani kubwa amepewa Wizkid. Aidha, Wizkid amepokea cheti kutoka kwenye Uongozi wa Grammy na barua ya shukurani kutoka kwa familia ya Marley kwa kuifanya heshima ya baba yao kuendelea kuwepo Duniani na kumsaidia Mwanamziki huyo Mkongwe wa muziki wa Reggae kushinda Grammy yake ya kwanza.
    0 Comments 0 Shares 774 Views