PSG ilitoa Ofa ya €250 milioni kwa Lamine Yamal, Barcelona wakataa - Laporta afunguka.
Rais wa klabu ya FC Barcelona, Joan Laporta, ameweka wazi kuwa klabu ya Paris Saint-Germain (PSG) iliwahi kuwasilisha ofa nono ya euro milioni 250 kwa ajili ya kinda nyota Lamine Yamal lakini Barca waliikataa bila kusita.
Akizungumza kuhusu tukio hilo, Laporta amesema ofa hiyo iliwasilishwa takribani miaka miwili iliyopita wakati Yamal akiwa na umri wa miaka 17 pekee.
“Lamine alikuwa na miaka 17, miaka miwili iliyopita… PSG walituma pendekezo la euro milioni 250 na tulisema hapana. Nakumbuka baadhi ya watu walifikiri tulikuwa tumepoteza akili,” ameeleza Laporta.
Kwa mujibu wa Kiongozi huyo wa Barcelona, uamuzi wa kuikataa ofa hiyo haukuwa wa kifedha bali wa kimkakati na kihistoria. Klabu hiyo inaamini Yamal ni sehemu ya mradi wa muda mrefu wa kurejesha enzi za mafanikio Camp Nou.
“Kwa sisi, amekuwa asiyeuzwa. Hagusiki,” alisisitiza Laporta.
Kwa kuzingatia ukubwa wa ofa hiyo, wengi walihoji kama Barcelona walipaswa kukubali kiasi hicho kikubwa cha fedha, hasa katika kipindi ambacho klabu hiyo ilikuwa inapitia changamoto za kifedha. Hata hivyo, maendeleo ya haraka ya Yamal ndani ya kikosi cha kwanza na mchango wake katika mafanikio ya timu yameanza kuhalalisha msimamo wa uongozi.
Yamal ameonekana kuwa moja ya vipaji adimu vilivyotoka "Akademi" ya La Masia, akionesha utulivu, ubunifu na ujasiri mkubwa licha ya umri wake mdogo.
Kauli ya Laporta inaashiria wazi kwamba Barcelona haioni thamani ya Yamal kwa mizani ya fedha pekee. Kwao, ni Mrithi wa kizazi kipya cha Nyota wa klabu hiyo, Mchezaji wa kujengwa kuzunguka mradi wa baadaye.
Katika soko la sasa la uhamisho, euro milioni 250 ni kiwango kinachoweza kubadilisha historia ya klabu yoyote. Lakini kwa Barcelona, Lamine Yamal si bidhaa ya kuuzwa ni alama ya mustakabali wao.
Toa maoni yako
#Sports
Rais wa klabu ya FC Barcelona, Joan Laporta, ameweka wazi kuwa klabu ya Paris Saint-Germain (PSG) iliwahi kuwasilisha ofa nono ya euro milioni 250 kwa ajili ya kinda nyota Lamine Yamal lakini Barca waliikataa bila kusita.
Akizungumza kuhusu tukio hilo, Laporta amesema ofa hiyo iliwasilishwa takribani miaka miwili iliyopita wakati Yamal akiwa na umri wa miaka 17 pekee.
“Lamine alikuwa na miaka 17, miaka miwili iliyopita… PSG walituma pendekezo la euro milioni 250 na tulisema hapana. Nakumbuka baadhi ya watu walifikiri tulikuwa tumepoteza akili,” ameeleza Laporta.
Kwa mujibu wa Kiongozi huyo wa Barcelona, uamuzi wa kuikataa ofa hiyo haukuwa wa kifedha bali wa kimkakati na kihistoria. Klabu hiyo inaamini Yamal ni sehemu ya mradi wa muda mrefu wa kurejesha enzi za mafanikio Camp Nou.
“Kwa sisi, amekuwa asiyeuzwa. Hagusiki,” alisisitiza Laporta.
Kwa kuzingatia ukubwa wa ofa hiyo, wengi walihoji kama Barcelona walipaswa kukubali kiasi hicho kikubwa cha fedha, hasa katika kipindi ambacho klabu hiyo ilikuwa inapitia changamoto za kifedha. Hata hivyo, maendeleo ya haraka ya Yamal ndani ya kikosi cha kwanza na mchango wake katika mafanikio ya timu yameanza kuhalalisha msimamo wa uongozi.
Yamal ameonekana kuwa moja ya vipaji adimu vilivyotoka "Akademi" ya La Masia, akionesha utulivu, ubunifu na ujasiri mkubwa licha ya umri wake mdogo.
Kauli ya Laporta inaashiria wazi kwamba Barcelona haioni thamani ya Yamal kwa mizani ya fedha pekee. Kwao, ni Mrithi wa kizazi kipya cha Nyota wa klabu hiyo, Mchezaji wa kujengwa kuzunguka mradi wa baadaye.
Katika soko la sasa la uhamisho, euro milioni 250 ni kiwango kinachoweza kubadilisha historia ya klabu yoyote. Lakini kwa Barcelona, Lamine Yamal si bidhaa ya kuuzwa ni alama ya mustakabali wao.
Toa maoni yako
#Sports
PSG ilitoa Ofa ya €250 milioni kwa Lamine Yamal, Barcelona wakataa - Laporta afunguka.
Rais wa klabu ya FC Barcelona, Joan Laporta, ameweka wazi kuwa klabu ya Paris Saint-Germain (PSG) iliwahi kuwasilisha ofa nono ya euro milioni 250 kwa ajili ya kinda nyota Lamine Yamal lakini Barca waliikataa bila kusita.
Akizungumza kuhusu tukio hilo, Laporta amesema ofa hiyo iliwasilishwa takribani miaka miwili iliyopita wakati Yamal akiwa na umri wa miaka 17 pekee.
“Lamine alikuwa na miaka 17, miaka miwili iliyopita… PSG walituma pendekezo la euro milioni 250 na tulisema hapana. Nakumbuka baadhi ya watu walifikiri tulikuwa tumepoteza akili,” ameeleza Laporta.
Kwa mujibu wa Kiongozi huyo wa Barcelona, uamuzi wa kuikataa ofa hiyo haukuwa wa kifedha bali wa kimkakati na kihistoria. Klabu hiyo inaamini Yamal ni sehemu ya mradi wa muda mrefu wa kurejesha enzi za mafanikio Camp Nou.
“Kwa sisi, amekuwa asiyeuzwa. Hagusiki,” alisisitiza Laporta.
Kwa kuzingatia ukubwa wa ofa hiyo, wengi walihoji kama Barcelona walipaswa kukubali kiasi hicho kikubwa cha fedha, hasa katika kipindi ambacho klabu hiyo ilikuwa inapitia changamoto za kifedha. Hata hivyo, maendeleo ya haraka ya Yamal ndani ya kikosi cha kwanza na mchango wake katika mafanikio ya timu yameanza kuhalalisha msimamo wa uongozi.
Yamal ameonekana kuwa moja ya vipaji adimu vilivyotoka "Akademi" ya La Masia, akionesha utulivu, ubunifu na ujasiri mkubwa licha ya umri wake mdogo.
Kauli ya Laporta inaashiria wazi kwamba Barcelona haioni thamani ya Yamal kwa mizani ya fedha pekee. Kwao, ni Mrithi wa kizazi kipya cha Nyota wa klabu hiyo, Mchezaji wa kujengwa kuzunguka mradi wa baadaye.
Katika soko la sasa la uhamisho, euro milioni 250 ni kiwango kinachoweza kubadilisha historia ya klabu yoyote. Lakini kwa Barcelona, Lamine Yamal si bidhaa ya kuuzwa ni alama ya mustakabali wao.
Toa maoni yako
#Sports
0 Σχόλια
0 Μοιράστηκε
42 Views