• Zelensky asema Putin ameanzisha vita ya tatu ya Dunia.

    Volodymyr Zelensky ametoa kauli nzito akidai kuwa Vladimir Putin tayari ameanzisha Vita ya tatu ya Dunia, akisisitiza kuwa suluhisho pekee ni kuiwekea Urusi shinikizo kali kijeshi na kiuchumi ili kuizuia isisambaze zaidi mgogoro huo.

    Katika mahojiano aliyofanya na BBC Mjini Kyiv, Kiongozi huyo wa Ukraine alieleza kuwa nchi yake haitaanguka mikononi mwa Urusi, bali itaibuka mshindi mwishoni mwa vita. Alisisitiza kuwa Ukraine haiwezi kutoa ardhi yake kama gharama ya amani, hasa ikizingatiwa kuwa majeshi ya Urusi hayajafanikiwa kuiteka kikamilifu licha ya kupeleka wanajeshi wengi vitani.

    “Nafikiri Putin tayari ameanzisha Vita ya Tatu ya Dunia. Swali si tu kwamba ameianzisha, bali ni wapi anaweza kufika na namna gani dunia inaweza kumzuia,” alisema Zelensky.

    Aliongeza kuwa Urusi inalenga kubadili mfumo wa kimataifa na kuwalazimisha watu kuishi katika mfumo ambao hawajauchagua wenyewe.

    Akizungumzia pendekezo la Urusi la kutaka Ukraine ikabidhi takribani asilimia 20 ya maeneo yake, ikiwemo sehemu za Mkoa wa Donetsk na maeneo ya kusini, Zelensky alikataa wazo hilo vikali.

    Kwa mujibu wake, suala hilo halihusu ardhi pekee, bali linahusu maisha ya Raia wa Ukraine na mustakabali wa taifa. Alisema kukubali masharti hayo kungekuwa sawa na kuwasaliti Wananchi na kuipokonya nchi hadhi yake.

    Zelensky ameitaka jumuiya ya kimataifa kuongeza vikwazo vya kiuchumi dhidi ya Moscow pamoja na kuimarisha msaada wa kijeshi kwa Ukraine. Anaamini kuwa presha ya pamoja ndiyo njia pekee ya kuzuia mzozo huo kuenea zaidi na kuathiri usalama wa dunia kwa upana wake.

    Kauli yake inakuja wakati mapigano kati ya Ukraine na Urusi yakiendelea katika maeneo kadhaa ya mashariki na kusini mwa nchi hiyo, huku hali ya kisiasa na kiusalama ikiendelea kuwa tete katika ukanda wa Ulaya Mashariki.

    Toa maoni yako
    #Habari
    Zelensky asema Putin ameanzisha vita ya tatu ya Dunia. Volodymyr Zelensky ametoa kauli nzito akidai kuwa Vladimir Putin tayari ameanzisha Vita ya tatu ya Dunia, akisisitiza kuwa suluhisho pekee ni kuiwekea Urusi shinikizo kali kijeshi na kiuchumi ili kuizuia isisambaze zaidi mgogoro huo. Katika mahojiano aliyofanya na BBC Mjini Kyiv, Kiongozi huyo wa Ukraine alieleza kuwa nchi yake haitaanguka mikononi mwa Urusi, bali itaibuka mshindi mwishoni mwa vita. Alisisitiza kuwa Ukraine haiwezi kutoa ardhi yake kama gharama ya amani, hasa ikizingatiwa kuwa majeshi ya Urusi hayajafanikiwa kuiteka kikamilifu licha ya kupeleka wanajeshi wengi vitani. “Nafikiri Putin tayari ameanzisha Vita ya Tatu ya Dunia. Swali si tu kwamba ameianzisha, bali ni wapi anaweza kufika na namna gani dunia inaweza kumzuia,” alisema Zelensky. Aliongeza kuwa Urusi inalenga kubadili mfumo wa kimataifa na kuwalazimisha watu kuishi katika mfumo ambao hawajauchagua wenyewe. Akizungumzia pendekezo la Urusi la kutaka Ukraine ikabidhi takribani asilimia 20 ya maeneo yake, ikiwemo sehemu za Mkoa wa Donetsk na maeneo ya kusini, Zelensky alikataa wazo hilo vikali. Kwa mujibu wake, suala hilo halihusu ardhi pekee, bali linahusu maisha ya Raia wa Ukraine na mustakabali wa taifa. Alisema kukubali masharti hayo kungekuwa sawa na kuwasaliti Wananchi na kuipokonya nchi hadhi yake. Zelensky ameitaka jumuiya ya kimataifa kuongeza vikwazo vya kiuchumi dhidi ya Moscow pamoja na kuimarisha msaada wa kijeshi kwa Ukraine. Anaamini kuwa presha ya pamoja ndiyo njia pekee ya kuzuia mzozo huo kuenea zaidi na kuathiri usalama wa dunia kwa upana wake. Kauli yake inakuja wakati mapigano kati ya Ukraine na Urusi yakiendelea katika maeneo kadhaa ya mashariki na kusini mwa nchi hiyo, huku hali ya kisiasa na kiusalama ikiendelea kuwa tete katika ukanda wa Ulaya Mashariki. Toa maoni yako #Habari
    0 Commenti 0 condivisioni 227 Views
  • Iran na Urusi kufanya mazoezi ya pamoja ya kijeshi nje ya Bahari ya Oman.

    Iran na Urusi zinatarajiwa kuanza mazoezi ya pamoja ya kijeshi kesho Alhamisi katika maeneo ya nje ya Bahari ya Oman na kaskazini mwa Bahari ya Hindi, hatua inayotafsiriwa kama ishara ya kuimarika kwa ushirikiano wa kiusalama kati ya mataifa hayo mawili.

    Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Fars, tangazo hilo limekuja siku chache baada ya Kikosi Maalum cha Walinzi wa Mapinduzi wa Iran kufanya mazoezi ya kijeshi katika mlango wa bahari wa Hormuz, eneo nyeti linalopitisha sehemu kubwa ya usafirishaji wa mafuta duniani.

    Kamanda wa Jeshi la Wanamaji la Iran, Hassan Maghsoodloo, ameeleza madhumuni ya mazoezi hayo kwa kusema: “Lengo la mazoezi haya ni kuunda nguvu za pamoja na kuimarisha uratibu wa hatua za pamoja ili kukabiliana na vitisho vinavyoathiri usalama wa majini na usalama wa nchi zetu mbili.”

    Ameongeza kuwa: "Mazoezi haya pia yanalenga kupambana na ugaidi na kuimarisha utulivu katika eneo la kimkakati la bahari.”

    Kauli hiyo inaonesha kuwa Tehran na Moscow zinaangazia zaidi usalama wa bahari na kulinda maslahi yao ya kiuchumi na kijeshi katika njia kuu za usafirishaji wa kimataifa.

    Hatua hizi zinakuja wakati wa mvutano unaoendelea kati ya Marekani na Iran. Washington imetishia hatua za kijeshi dhidi ya Tehran, ikiishutumu kwa kile ilichodai kuwa ni ukiukwaji wa haki za Waandamanaji pamoja na kushindwa kufikia makubaliano kuhusu mpango wake wa nyuklia.

    Kwa upande wake, Iran imekuwa ikisisitiza mara kwa mara uwezekano wa kuufunga mlango wa bahari wa Hormuz wakati wa mvutano mkali na Marekani. Hata hivyo, hadi sasa, haijawahi kuchukua hatua ya kulifunga rasmi lango hilo muhimu la kimataifa.

    Mazoezi haya yanaonekana kuwa na ujumbe wa wazi wa kisiasa na kijeshi kuonesha mshikamano wa Iran na Urusi katika kukabiliana na shinikizo la Magharibi, huku yakituma ishara kwa mataifa mengine kuhusu uwezo wao wa pamoja katika kulinda maslahi ya kimkakati katika Bahari ya Hindi na Ghuba ya Oman.

    Wachambuzi wa masuala ya ulinzi wanaona kuwa ushirikiano huu unaweza kuathiri mizania ya nguvu katika eneo hilo, hasa katika kipindi ambacho diplomasia ya nyuklia bado haijafikia muafaka wa kudumu.

    Toa maoni yako
    #Habari
    Iran na Urusi kufanya mazoezi ya pamoja ya kijeshi nje ya Bahari ya Oman. Iran na Urusi zinatarajiwa kuanza mazoezi ya pamoja ya kijeshi kesho Alhamisi katika maeneo ya nje ya Bahari ya Oman na kaskazini mwa Bahari ya Hindi, hatua inayotafsiriwa kama ishara ya kuimarika kwa ushirikiano wa kiusalama kati ya mataifa hayo mawili. Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Fars, tangazo hilo limekuja siku chache baada ya Kikosi Maalum cha Walinzi wa Mapinduzi wa Iran kufanya mazoezi ya kijeshi katika mlango wa bahari wa Hormuz, eneo nyeti linalopitisha sehemu kubwa ya usafirishaji wa mafuta duniani. Kamanda wa Jeshi la Wanamaji la Iran, Hassan Maghsoodloo, ameeleza madhumuni ya mazoezi hayo kwa kusema: “Lengo la mazoezi haya ni kuunda nguvu za pamoja na kuimarisha uratibu wa hatua za pamoja ili kukabiliana na vitisho vinavyoathiri usalama wa majini na usalama wa nchi zetu mbili.” Ameongeza kuwa: "Mazoezi haya pia yanalenga kupambana na ugaidi na kuimarisha utulivu katika eneo la kimkakati la bahari.” Kauli hiyo inaonesha kuwa Tehran na Moscow zinaangazia zaidi usalama wa bahari na kulinda maslahi yao ya kiuchumi na kijeshi katika njia kuu za usafirishaji wa kimataifa. Hatua hizi zinakuja wakati wa mvutano unaoendelea kati ya Marekani na Iran. Washington imetishia hatua za kijeshi dhidi ya Tehran, ikiishutumu kwa kile ilichodai kuwa ni ukiukwaji wa haki za Waandamanaji pamoja na kushindwa kufikia makubaliano kuhusu mpango wake wa nyuklia. Kwa upande wake, Iran imekuwa ikisisitiza mara kwa mara uwezekano wa kuufunga mlango wa bahari wa Hormuz wakati wa mvutano mkali na Marekani. Hata hivyo, hadi sasa, haijawahi kuchukua hatua ya kulifunga rasmi lango hilo muhimu la kimataifa. Mazoezi haya yanaonekana kuwa na ujumbe wa wazi wa kisiasa na kijeshi kuonesha mshikamano wa Iran na Urusi katika kukabiliana na shinikizo la Magharibi, huku yakituma ishara kwa mataifa mengine kuhusu uwezo wao wa pamoja katika kulinda maslahi ya kimkakati katika Bahari ya Hindi na Ghuba ya Oman. Wachambuzi wa masuala ya ulinzi wanaona kuwa ushirikiano huu unaweza kuathiri mizania ya nguvu katika eneo hilo, hasa katika kipindi ambacho diplomasia ya nyuklia bado haijafikia muafaka wa kudumu. Toa maoni yako #Habari
    0 Commenti 0 condivisioni 377 Views
  • Nchi ya Kenya yakemea vitendo vya kuwapeleka Vijana wake kwenye vita Nchini Ukraine.

    Serikali ya Kenya imekemea vikali vitendo vya baadhi ya Mawakala wanaodanganya Vijana kwa ahadi za ajira, kisha kuwapeleka moja kwa moja kwenye vita vinavyoendelea nchini Ukraine.

    Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya, Musalia Mudavadi, amesema: “Tunatarajia kufanya ziara rasmi mjini Moscow kwa mazungumzo na Serikali ya Urusi, lengo likiwa kusitisha kabisa matumizi ya raia wa Kenya katika mapambano haya.”

    Mudavadi alibainisha kuwa tayari Wakenya kadhaa wamefariki dunia, huku wengine wakijeruhiwa vibaya baada ya kudanganywa kuingia mikataba ya kijeshi. Amesema: “Hatukubali upotevu wa maisha ya raia wetu. Hatua za kudumu lazima zichukuliwe.”

    Serikali ya Kenya imelaumu Mawakala wa ajira wanaoshawishi vijana kwa ahadi za mishahara mikubwa, kisha kuwapeleka mstari wa mbele vitani. Ripoti ya hivi karibuni ya shirika la habari la Ufaransa, Agence France-Presse, imethibitisha kuwepo kwa mtandao wa udanganyifu unaowaingiza vijana wasiokuwa na historia ya kijeshi kusaini mikataba na Jeshi la Urusi, kisha kupelekwa haraka kwenye Uwanja wa mapambano.

    Mudavadi amesisitiza kuwa Kenya itafuatilia pia suala la kuachiliwa kwa Wakenya waliokamatwa kama wafungwa wa kivita nchini Ukraine. Amesema hatua hizi ni muhimu ili kulinda maisha ya Raia wake.

    Toa maoni yako
    #Habari
    #Russia #Ukraine #MusaliaMudavadi #Moscow #BreakingNews #WorldNews #VitaUkraine #KenyaAbroad #HumanRights #AfricaNews
    Nchi ya Kenya yakemea vitendo vya kuwapeleka Vijana wake kwenye vita Nchini Ukraine. Serikali ya Kenya imekemea vikali vitendo vya baadhi ya Mawakala wanaodanganya Vijana kwa ahadi za ajira, kisha kuwapeleka moja kwa moja kwenye vita vinavyoendelea nchini Ukraine. Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya, Musalia Mudavadi, amesema: “Tunatarajia kufanya ziara rasmi mjini Moscow kwa mazungumzo na Serikali ya Urusi, lengo likiwa kusitisha kabisa matumizi ya raia wa Kenya katika mapambano haya.” Mudavadi alibainisha kuwa tayari Wakenya kadhaa wamefariki dunia, huku wengine wakijeruhiwa vibaya baada ya kudanganywa kuingia mikataba ya kijeshi. Amesema: “Hatukubali upotevu wa maisha ya raia wetu. Hatua za kudumu lazima zichukuliwe.” Serikali ya Kenya imelaumu Mawakala wa ajira wanaoshawishi vijana kwa ahadi za mishahara mikubwa, kisha kuwapeleka mstari wa mbele vitani. Ripoti ya hivi karibuni ya shirika la habari la Ufaransa, Agence France-Presse, imethibitisha kuwepo kwa mtandao wa udanganyifu unaowaingiza vijana wasiokuwa na historia ya kijeshi kusaini mikataba na Jeshi la Urusi, kisha kupelekwa haraka kwenye Uwanja wa mapambano. Mudavadi amesisitiza kuwa Kenya itafuatilia pia suala la kuachiliwa kwa Wakenya waliokamatwa kama wafungwa wa kivita nchini Ukraine. Amesema hatua hizi ni muhimu ili kulinda maisha ya Raia wake. Toa maoni yako #Habari #Russia #Ukraine #MusaliaMudavadi #Moscow #BreakingNews #WorldNews #VitaUkraine #KenyaAbroad #HumanRights #AfricaNews
    0 Commenti 2 condivisioni 603 Views
  • URUSI YAONYA KUCHUKUA HATUA ZA KIJESHI IWAPO GREENLAND ITAWEKWA KIJESHI

    Urusi imeonya kwamba itachukua hatua za kijeshi iwapo Greenland itawekwa miundombinu ya kijeshi itakayochukuliwa kuwa tishio kwa usalama wake, katika hatua inayoongeza tahadhari ya kiusalama katika eneo la Arctic.

    Waziri wa Mambo ya Nje wa Urusi, Sergey Lavrov, amesema kuwa Moscow haitakaa kimya endapo kutakuwa na ongezeko la uwepo wa kijeshi katika kisiwa hicho kilicho chini ya utawala wa Denmark.

    “Endapo Greenland itawekwa kijeshi na uwezo huo kuelekezwa dhidi ya Urusi, tutachukua hatua stahiki za kulinganisha, ikiwemo za kijeshi na kiufundi.”

    Lavrov amesisitiza kuwa suala la mustakabali wa Greenland linapaswa kuamuliwa na wahusika wakuu wanaohusika moja kwa moja.

    “Marekani, Denmark na Greenland wanapaswa kushughulikia suala hili wenyewe.”

    Greenland, ambayo ina mamlaka ya ndani lakini iko chini ya Ufalme wa Denmark, imekuwa na umuhimu wa kimkakati kutokana na nafasi yake katika eneo la Arctic. Ukanda huo umeendelea kuwa kitovu cha ushindani wa kijiografia na kijeshi kati ya mataifa makubwa, hasa katika muktadha wa mabadiliko ya tabianchi na njia mpya za usafirishaji pamoja na rasilimali asilia.

    Urusi imekuwa ikisisitiza mara kwa mara kwamba eneo la Arctic linapaswa kubaki kuwa eneo la ushirikiano na amani.

    “Tunataka Arctic ibaki eneo la amani na ushirikiano.”

    Hadi sasa, hakujakuwa na tangazo rasmi la uwekaji mpya wa kijeshi Greenland, lakini kauli ya Moscow inaashiria kuongezeka kwa mvutano wa kimkakati katika eneo hilo.

    Toa maoni yako
    #Habari
    URUSI YAONYA KUCHUKUA HATUA ZA KIJESHI IWAPO GREENLAND ITAWEKWA KIJESHI Urusi imeonya kwamba itachukua hatua za kijeshi iwapo Greenland itawekwa miundombinu ya kijeshi itakayochukuliwa kuwa tishio kwa usalama wake, katika hatua inayoongeza tahadhari ya kiusalama katika eneo la Arctic. Waziri wa Mambo ya Nje wa Urusi, Sergey Lavrov, amesema kuwa Moscow haitakaa kimya endapo kutakuwa na ongezeko la uwepo wa kijeshi katika kisiwa hicho kilicho chini ya utawala wa Denmark. “Endapo Greenland itawekwa kijeshi na uwezo huo kuelekezwa dhidi ya Urusi, tutachukua hatua stahiki za kulinganisha, ikiwemo za kijeshi na kiufundi.” Lavrov amesisitiza kuwa suala la mustakabali wa Greenland linapaswa kuamuliwa na wahusika wakuu wanaohusika moja kwa moja. “Marekani, Denmark na Greenland wanapaswa kushughulikia suala hili wenyewe.” Greenland, ambayo ina mamlaka ya ndani lakini iko chini ya Ufalme wa Denmark, imekuwa na umuhimu wa kimkakati kutokana na nafasi yake katika eneo la Arctic. Ukanda huo umeendelea kuwa kitovu cha ushindani wa kijiografia na kijeshi kati ya mataifa makubwa, hasa katika muktadha wa mabadiliko ya tabianchi na njia mpya za usafirishaji pamoja na rasilimali asilia. Urusi imekuwa ikisisitiza mara kwa mara kwamba eneo la Arctic linapaswa kubaki kuwa eneo la ushirikiano na amani. “Tunataka Arctic ibaki eneo la amani na ushirikiano.” Hadi sasa, hakujakuwa na tangazo rasmi la uwekaji mpya wa kijeshi Greenland, lakini kauli ya Moscow inaashiria kuongezeka kwa mvutano wa kimkakati katika eneo hilo. Toa maoni yako #Habari
    0 Commenti 0 condivisioni 175 Views
  • Kikao cha mazungumzo ya kumaliza mzozo wa Nchi ya Ukraine na Nchi ya Urusi kinaendelea Nchini Saudi Arabia 🇸 ambapo Mawaziri wa Mashauri ya Kigeni wa Urusi chini ya Sergie Lavrov na Marekani chini ya Marco Rubio. Hata hivyo, Ukraine na Umoja wa Ulaya (EU) hawajashirikishwa huku Ukraine upande wake inapinga kikao hicho kuwa makubaliano yoyote haitayatambua.

    Katika kusisitiza hilo Ukraine imeendelea kusisitiza kwamba itaendelea kupigana vita kwa kutegemea Ulaya sio Marekani kama mwanzo huku Rais wa Nchi hiyo Volodmiry Zelensky akisema Ukraine ni Taifa huru, hivyo haliwezi kuamuliwa mambo yake na Marekani, itautetea uhuru wake hadi tone la mwisho. Marekani imejibu kwa kusema inaitaka Ukraine irejeshe haraka deni lote la usaidizi wa vita lililotolewa na Marekani tangu Februari 2022 Oparesheni ya Urusi ilipoanza.

    Kikao hiki kinachoendelea ni hatua muhimu kuelekea mkutano wa Rais Putin na Rais Trump uliopangwa mwezi Mei katika sherehe za Mashujaa wa Urusi utakaofanyika Jijini Moscow, Urusi ambapo pia mkutano huo utamwalika Rais wa China Xi Ping kama Mgeni mwalikwa muhimu.

    Kikao cha mazungumzo ya kumaliza mzozo wa Nchi ya Ukraine 🇺🇦 na Nchi ya Urusi 🇷🇺 kinaendelea Nchini Saudi Arabia 🇸 ambapo Mawaziri wa Mashauri ya Kigeni wa Urusi chini ya Sergie Lavrov na Marekani 🇺🇸 chini ya Marco Rubio. Hata hivyo, Ukraine na Umoja wa Ulaya (EU) hawajashirikishwa huku Ukraine upande wake inapinga kikao hicho kuwa makubaliano yoyote haitayatambua. Katika kusisitiza hilo Ukraine imeendelea kusisitiza kwamba itaendelea kupigana vita kwa kutegemea Ulaya sio Marekani kama mwanzo huku Rais wa Nchi hiyo Volodmiry Zelensky akisema Ukraine ni Taifa huru, hivyo haliwezi kuamuliwa mambo yake na Marekani, itautetea uhuru wake hadi tone la mwisho. Marekani imejibu kwa kusema inaitaka Ukraine irejeshe haraka deni lote la usaidizi wa vita lililotolewa na Marekani tangu Februari 2022 Oparesheni ya Urusi ilipoanza. Kikao hiki kinachoendelea ni hatua muhimu kuelekea mkutano wa Rais Putin na Rais Trump uliopangwa mwezi Mei katika sherehe za Mashujaa wa Urusi utakaofanyika Jijini Moscow, Urusi ambapo pia mkutano huo utamwalika Rais wa China 🇨🇳 Xi Ping kama Mgeni mwalikwa muhimu.
    0 Commenti 0 condivisioni 1K Views
  • Rais wa Urusi , Vladimir Putin amewaalika Rais China , Xi Jinping na Rais wa Marekani , Donald Trump kuhudhuria sherehe maarufu za Ushindi wa Urusi katika vita kuu ya pili ya Dunia (Russia’s Victory Parade) zitakazofanyika tarehe 9 Mwezi May Jijini Moscow Nchini Urusi. Mwaliko huu unatokana na ombi la Rais Donald Trump la tarehe 11 Feb 2025 alipoomba kuzuru Moscow kwa lengo la kumaliza mgogoro wa Ukraine, Kikao kilichotokana na ombi hili kilifanywa kwa njia ya simu ambapo pamoja na mambo mengine, Trump alimhakikishia Putin kwamba Marekani itaacha ufadhili wa kijeshi kwa Ukraine na pia Ukraine itaachia sehemu ya ardhi yake iliyotwaliwa kama dhamana ya usalama wake dhidi ya Moscow.

    Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Washington katika taarifa yake ilikazia na kusisitiza kile alichokizungumza Trump na Moscow na kwamba Marekani inakusudia kumaliza tofauti zao kidunia. Utawala wa Trump umekuwa na juhudi kubwa kumaliza mizozo mikubwa duniani ambayo Ikulu hiyo ilikuwa ikifadhili na kuanzisha uchokozi kwa muda mrefu, Ukiachiliambali mgogoro wa Ukraine, pia Washington inashughulika kumaliza mgogoro wa Mashariki ya Kati huko Gaza ambapo mamia ya watu wameuawa kwa ufadhili wa Marekani hiyohiyo.

    Rais wa Urusi 🇷🇺, Vladimir Putin amewaalika Rais China 🇨🇳, Xi Jinping na Rais wa Marekani 🇺🇸, Donald Trump kuhudhuria sherehe maarufu za Ushindi wa Urusi katika vita kuu ya pili ya Dunia (Russia’s Victory Parade) zitakazofanyika tarehe 9 Mwezi May Jijini Moscow Nchini Urusi. Mwaliko huu unatokana na ombi la Rais Donald Trump la tarehe 11 Feb 2025 alipoomba kuzuru Moscow kwa lengo la kumaliza mgogoro wa Ukraine, Kikao kilichotokana na ombi hili kilifanywa kwa njia ya simu ambapo pamoja na mambo mengine, Trump alimhakikishia Putin kwamba Marekani itaacha ufadhili wa kijeshi kwa Ukraine na pia Ukraine itaachia sehemu ya ardhi yake iliyotwaliwa kama dhamana ya usalama wake dhidi ya Moscow. Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Washington katika taarifa yake ilikazia na kusisitiza kile alichokizungumza Trump na Moscow na kwamba Marekani inakusudia kumaliza tofauti zao kidunia. Utawala wa Trump umekuwa na juhudi kubwa kumaliza mizozo mikubwa duniani ambayo Ikulu hiyo ilikuwa ikifadhili na kuanzisha uchokozi kwa muda mrefu, Ukiachiliambali mgogoro wa Ukraine, pia Washington inashughulika kumaliza mgogoro wa Mashariki ya Kati huko Gaza ambapo mamia ya watu wameuawa kwa ufadhili wa Marekani hiyohiyo.
    Like
    1
    0 Commenti 0 condivisioni 1K Views
  • Marais wa Urusi , V. Putin na yule wa Marekani , D.Trump walizungumza leo hii kwa muda saa moja na nusu kuhusu kumaliza vita Nchini Ukraine , kuboresha uhusiano kati ya Marekani na Urusi, na uwezekano wa kubadilishana Wafungwa.

    Aidha, Putin alimwalika Trump kwenda Mjini Moscow Nchini Urusi na akasema yuko tayari kuwakaribisha Maafisa wa Marekani kwa mazungumzo. Hii ilikuwa simu ya kwanza ya Putin na Rais wa Marekani aliyeko madarakani tangu Februari 2022, alipoongea na Biden muda mfupi kabla ya kutuma Wanajeshi Nchini Ukraine.

    Toa maoni yako
    #MvanoHabari
    #MvanoMtangazaji
    #M33
    Marais wa Urusi 🇷🇺, V. Putin na yule wa Marekani 🇺🇸, D.Trump walizungumza leo hii kwa muda saa moja na nusu kuhusu kumaliza vita Nchini Ukraine 🇮🇱, kuboresha uhusiano kati ya Marekani na Urusi, na uwezekano wa kubadilishana Wafungwa. Aidha, Putin alimwalika Trump kwenda Mjini Moscow Nchini Urusi na akasema yuko tayari kuwakaribisha Maafisa wa Marekani kwa mazungumzo. Hii ilikuwa simu ya kwanza ya Putin na Rais wa Marekani aliyeko madarakani tangu Februari 2022, alipoongea na Biden muda mfupi kabla ya kutuma Wanajeshi Nchini Ukraine. Toa maoni yako #MvanoHabari #MvanoMtangazaji #M33
    0 Commenti 0 condivisioni 1K Views
  • Nahodha wa zamani wa Timu ya Taifa ya Cameroon aliyewahi kucheza klabu ya FC Barcelona ya Hispania Samuel Eto’o (43) akiwa na Klabu ya Anzhi Makhachkala ya Urusi, aliweka rekodi ya Mchezaji anayelipwa mshahara mkubwa Duniani kati ya mwaka 2011 na 2013.

    Eto’o alikuwa akilipwa pauni 365,000 kwa wiki ambazo ni takribani Shilingi Bilioni 1.1 za Kitanzania na alipewa Ndege binafsi (Private Jet) ambayo aliweza kusafiri kila siku kutoka Makhachkala kwenda Moscow ambapo ni umbali wa (1,910 KM) kwa mujibu wa Mkataba wake.

    Samuel Eto’o hadi anaachana na Klabu hiyo, alikuwa kacheza jumla ya mechi (73), kafunga mabao (36), Pasi saidizi (assist) 16. Cha kushangaza zaidi kwa sasa Klabu hiyo haipo kabisa imefilisika na Juni 2022 ilipoteza rasmi leseni ya Klabu baada ya kupitia matatizo ya kifedha na kushindwa kucheza mchezo wowote.

    Nahodha wa zamani wa Timu ya Taifa ya Cameroon aliyewahi kucheza klabu ya FC Barcelona ya Hispania Samuel Eto’o (43) akiwa na Klabu ya Anzhi Makhachkala ya Urusi, aliweka rekodi ya Mchezaji anayelipwa mshahara mkubwa Duniani kati ya mwaka 2011 na 2013. Eto’o alikuwa akilipwa pauni 365,000 kwa wiki ambazo ni takribani Shilingi Bilioni 1.1 za Kitanzania na alipewa Ndege binafsi (Private Jet) ambayo aliweza kusafiri kila siku kutoka Makhachkala kwenda Moscow ambapo ni umbali wa (1,910 KM) kwa mujibu wa Mkataba wake. Samuel Eto’o hadi anaachana na Klabu hiyo, alikuwa kacheza jumla ya mechi (73), kafunga mabao (36), Pasi saidizi (assist) 16. Cha kushangaza zaidi kwa sasa Klabu hiyo haipo kabisa imefilisika na Juni 2022 ilipoteza rasmi leseni ya Klabu baada ya kupitia matatizo ya kifedha na kushindwa kucheza mchezo wowote.
    Like
    Love
    4
    0 Commenti 0 condivisioni 796 Views
  • Nahodha wa zamani wa Timu ya Taifa ya Cameroon aliyewahi kucheza klabu ya FC Barcelona ya Hispania Samuel Eto’o (43) akiwa na Klabu ya Anzhi Makhachkala ya Urusi, aliweka rekodi ya Mchezaji anayelipwa mshahara mkubwa Duniani kati ya mwaka 2011 na 2013.

    Eto’o alikuwa akilipwa pauni 365,000 kwa wiki ambazo ni takribani Shilingi Bilioni 1.1 za Kitanzania na alipewa Ndege binafsi (Private Jet) ambayo aliweza kusafiri kila siku kutoka Makhachkala kwenda Moscow ambapo ni umbali wa (1,910 KM) kwa mujibu wa Mkataba wake.

    Samuel Eto’o hadi anaachana na Klabu hiyo, alikuwa kacheza jumla ya mechi (73), kafunga mabao (36), Pasi saidizi (assist) 16. Cha kushangaza zaidi kwa sasa Klabu hiyo haipo kabisa imefilisika na Juni 2022 ilipoteza rasmi leseni ya Klabu baada ya kupitia matatizo ya kifedha na kushindwa kucheza mchezo wowote.

    Nahodha wa zamani wa Timu ya Taifa ya Cameroon aliyewahi kucheza klabu ya FC Barcelona ya Hispania Samuel Eto’o (43) akiwa na Klabu ya Anzhi Makhachkala ya Urusi, aliweka rekodi ya Mchezaji anayelipwa mshahara mkubwa Duniani kati ya mwaka 2011 na 2013. Eto’o alikuwa akilipwa pauni 365,000 kwa wiki ambazo ni takribani Shilingi Bilioni 1.1 za Kitanzania na alipewa Ndege binafsi (Private Jet) ambayo aliweza kusafiri kila siku kutoka Makhachkala kwenda Moscow ambapo ni umbali wa (1,910 KM) kwa mujibu wa Mkataba wake. Samuel Eto’o hadi anaachana na Klabu hiyo, alikuwa kacheza jumla ya mechi (73), kafunga mabao (36), Pasi saidizi (assist) 16. Cha kushangaza zaidi kwa sasa Klabu hiyo haipo kabisa imefilisika na Juni 2022 ilipoteza rasmi leseni ya Klabu baada ya kupitia matatizo ya kifedha na kushindwa kucheza mchezo wowote.
    0 Commenti 0 condivisioni 708 Views
  • JINSI SHIRIKA LA KIJASUSI LA URUSI FSB {KGB} LILIVYO HATARI....

    Kama waswahili wasemavyo maisha ni safari ndefu na kifo ni Siri, pengine hili ni kweli kutokana na sintofahamu iliyochukua uhai wa Alexander Litvinenko, jasusi wa zamañi wa KGB na baadae FSB ya Urusi ya sasa.

    Tutarudi Sasa tuendelee mwishoni mwa wiki za mwezi wa kumi mwaka 2006 Alexander Litvinenko alipokuwa jijini London alipotorokea baada ya rabsha dhidi ya serikali mjini Moscow, siku hiyo Litvinenko alikuwa ametembelewa na marafiki zake wawili walikuwa wanausalama ndani ya FSB na iliyokuwa KGB Dmitri Kovtun na Andrei Lugovoi, asichokijua ni kwamba wale wawili walikuwa moja ya watu hatari na pia kama wasafirishaji mahiri wa msafiri kama Litvinenko kuliendelea kaburi

    Waliikutana hotelini jijini London wakinywa na kufurahi, siku hiyo Lugovoi na Kovtun wao waliagiza bia wakanywa wakifurahi, unajua nini Litvinenko ye aliagizwa chai ya rangi akanywa huku akiwachekea wasafirishaji wa ule msemo wa kiswahili " maisha ni safari"

    Maskinii Litvinenko alipojichanganya tu Lugovoi na Kovtun wakifanya kazi yao moja waliotumwa na FSB, kumnyamazisha " traitor of the mother Russia"

    Unajua walifanya Nini? Walichukua kemikali hatari sana duniani inayoua taratibu sana jina lake Polonium 210 wakatia katika chai ya Litvinenko. Inavyosemekana alivyorudi walimchekea na kufurahi zaidi kuona Litvinenko alikuwa amesahau mbinu muhimu kabisa ya wanaintelijensia kote duniani ! Kutomwamini mtu hata mama na baba yako.
    Litvinenko alikunywa chai ile

    **********
    Lugovoi na Kovtun walichukua ndege siku tatu baadae haoo Moscow, huko walifanyiwa sherehe ya uhakika wa kazi iliyofanyika isiyo na shaka, Kovtun aliamua kuwa mfanyabiashara mkubwa wakati Lugovoi alipandishwa cheo siku chache baadae.
    ******
    Maskini Litvinenko aliagana na wanyama wale wa kwenye barafu Kama wajiitavyo wao " "bear " lakini akiwapachika majina mazuri yaani marafiki, ndugu, wapenzi kutoka home Russia. Pia aliwauliza vipi watarudi lini kumuona, kimoyomoyo Kovtun na Lugovoi walikua wakicheka na kusikitika kiunafiki,wakijua huyu mtu hana mwezi duniani. Wiki tatu nyingi! atakufa kifo Cha mateso akiwa kitandani amelala.

    ***
    November 1 mwaka 2006 Litvinenko aliugua homa ya ghafla mwili ukiungua kwa namna ya kutisha sana, alipelekwa hospitali mjini London akaishi kwa wiki 3 akiwa hoi kitandani! Wakati akifa akitoa laana kwa Putin akamshutumu amemuua.

    Huo ukawa mwisho wa Litvinenko mtu aliyekuwa ameaminiwa kutunza siri za Russia yeye alizitoa hadharani kwa m16 . Pengine ni chafu sana zenye damu lakini bila shaka kulikuwa pigo kwa vitu hivyo kuwa hadharani. Putin alivuliwa nguo hata asiijifunike.

    Tuzungimzapo Leo ni miaka karibu 12 toka mnyama huyu atutoke.

    Mwaka fulani Putin aliulizwa na mwanahabari mmoja ni kitu gani asichoweza kuvumilia na kusamehe alisema hivi.. Ye ni ngumu sana kuwasamehe wasaliti wa mother Russia.

    Ohh ndo hivyo Litvinenko hakupata bahati ya kusamehewa na Putin hivyo alikwenda.

    Chanzo: na Google
    JINSI SHIRIKA LA KIJASUSI LA URUSI FSB {KGB} LILIVYO HATARI.... Kama waswahili wasemavyo maisha ni safari ndefu na kifo ni Siri, pengine hili ni kweli kutokana na sintofahamu iliyochukua uhai wa Alexander Litvinenko, jasusi wa zamañi wa KGB na baadae FSB ya Urusi ya sasa. Tutarudi Sasa tuendelee mwishoni mwa wiki za mwezi wa kumi mwaka 2006 Alexander Litvinenko alipokuwa jijini London alipotorokea baada ya rabsha dhidi ya serikali mjini Moscow, siku hiyo Litvinenko alikuwa ametembelewa na marafiki zake wawili walikuwa wanausalama ndani ya FSB na iliyokuwa KGB Dmitri Kovtun na Andrei Lugovoi, asichokijua ni kwamba wale wawili walikuwa moja ya watu hatari na pia kama wasafirishaji mahiri wa msafiri kama Litvinenko kuliendelea kaburi Waliikutana hotelini jijini London wakinywa na kufurahi, siku hiyo Lugovoi na Kovtun wao waliagiza bia wakanywa wakifurahi, unajua nini Litvinenko ye aliagizwa chai ya rangi akanywa huku akiwachekea wasafirishaji wa ule msemo wa kiswahili " maisha ni safari" Maskinii Litvinenko alipojichanganya tu Lugovoi na Kovtun wakifanya kazi yao moja waliotumwa na FSB, kumnyamazisha " traitor of the mother Russia" Unajua walifanya Nini? Walichukua kemikali hatari sana duniani inayoua taratibu sana jina lake Polonium 210 wakatia katika chai ya Litvinenko. Inavyosemekana alivyorudi walimchekea na kufurahi zaidi kuona Litvinenko alikuwa amesahau mbinu muhimu kabisa ya wanaintelijensia kote duniani ! Kutomwamini mtu hata mama na baba yako. Litvinenko alikunywa chai ile ********** Lugovoi na Kovtun walichukua ndege siku tatu baadae haoo Moscow, huko walifanyiwa sherehe ya uhakika wa kazi iliyofanyika isiyo na shaka, Kovtun aliamua kuwa mfanyabiashara mkubwa wakati Lugovoi alipandishwa cheo siku chache baadae. ****** Maskini Litvinenko aliagana na wanyama wale wa kwenye barafu Kama wajiitavyo wao " "bear " lakini akiwapachika majina mazuri yaani marafiki, ndugu, wapenzi kutoka home Russia. Pia aliwauliza vipi watarudi lini kumuona, kimoyomoyo Kovtun na Lugovoi walikua wakicheka na kusikitika kiunafiki,wakijua huyu mtu hana mwezi duniani. Wiki tatu nyingi! atakufa kifo Cha mateso akiwa kitandani amelala. *** November 1 mwaka 2006 Litvinenko aliugua homa ya ghafla mwili ukiungua kwa namna ya kutisha sana, alipelekwa hospitali mjini London akaishi kwa wiki 3 akiwa hoi kitandani! Wakati akifa akitoa laana kwa Putin akamshutumu amemuua. Huo ukawa mwisho wa Litvinenko mtu aliyekuwa ameaminiwa kutunza siri za Russia yeye alizitoa hadharani kwa m16 . Pengine ni chafu sana zenye damu lakini bila shaka kulikuwa pigo kwa vitu hivyo kuwa hadharani. Putin alivuliwa nguo hata asiijifunike. Tuzungimzapo Leo ni miaka karibu 12 toka mnyama huyu atutoke. Mwaka fulani Putin aliulizwa na mwanahabari mmoja ni kitu gani asichoweza kuvumilia na kusamehe alisema hivi.. Ye ni ngumu sana kuwasamehe wasaliti wa mother Russia. Ohh ndo hivyo Litvinenko hakupata bahati ya kusamehewa na Putin hivyo alikwenda. Chanzo: na Google
    0 Commenti 0 condivisioni 2K Views