
-
-
-
0 Comments ·0 Shares ·157 Views
-
Ya Mange Kimambi kuhusu sakata la Mbosso na Zuchu kujitoa kwenye Lebo ya WCB Wasafi.
Mnaosema Mbosso bora angebaki wasafi hivi mnawaza nini? Hivi mnadhani hawa wasanii ni wajinga wanapoamua kutoka kwa Diamond?
Wanatoka coz wanaona hawapati matunda ya kazi zao, wanapiga kazi kubwa, wanakuwa famous nchi nzima ila hakuna pesa ya maana wanayopata, faida kubwa inaenda kwa kampuni ndo maana wanaona bora watoke wakajitafutie hata kama ni kidogo ila angalau ni chake na hatumiki tena kumtajirisha mtu.
Nawaambia hata Zuchu leo akiachwa na Dai kesho yake asubuhi na mapema anatoka Wasafi. kinachomuweka Zuchu wasafi ni kwamba yuko obsessed na kuolewa na Diamond.
Oh yeah, bado tukiwa kwenye hiyo topic ya king’ang’a ngoja niwaambie hivi, ni ngumu mnooo Diamond kumuacha king’ang’a, tena mnooooo. Hivi ndugu zangu mnajua maisha yalivyo magumu, mnataka Diamond amuache mwanamke anaemuingizia mabilioni ya pesa then aje kwenu vishanshuda wa mjini mnaosubiri kupewa? Itabidi akununulie gari, akupangie nyumba, akupe hela ya mawigi, akupe hela ya kulea ukoo wako, then uombe akujengee nyumba, why aingie kwenye matatizo hayo wakati Zuchu hayo mambo yote anajifanyia mwenyewe na on top of that anamwingizia pesa kwenye account? Yani aache mwanamke ambae hamcosti hata senti moja na bado anamwingizia mahela kwenye account aje kwenu omba omba na makalio yenu ya Uturuki? Itabidi Zuchu ashuke kimziki aache kumwingizia Diamond mahela ndo atapigwa chini. Yani Zuchu siku akishindwa kumwingizia Dai pesa kwenye account ndio ataachwa na sio kabla.Sasa acheni kujaji uzuri wako vs wa king’ang’a, jaji pesa utakayoweza kumwingizia Dai kwenye account Vs Zuchu anayomwingizia ndo utapata majibu. Na sasa hivi Zuchu kawaka moto Dai amuoe au anaingia mitini mnadhani Dai atachagua nini? Ampoteze top money maker wa Wasafi au aoe?Tumieni akili hapo, mnadhani atachagua nini?
Basi kwa hii posti kama namuona Dai atavyoniletea barua ingine ya lawyer huku Marekani . Weee mi sio kina Mwijaku uliowatishia na vibarua vya lawyer siku hizi wameufyata wooote. Weeee, mimi tutagaragazana mahakamani mpaka woote tufilisike kwa kulipa malawyer . Chezea wapare tunavyopenda kesi .Yes guys, kama mnenoti siku hizi hakuna mtu bongo anadhubutu kumchamba Dai, wooote kawanyoosha kwa kuwatishia lawyer.
Ya Mange Kimambi kuhusu sakata la Mbosso na Zuchu kujitoa kwenye Lebo ya WCB Wasafi. Mnaosema Mbosso bora angebaki wasafi hivi mnawaza nini? Hivi mnadhani hawa wasanii ni wajinga wanapoamua kutoka kwa Diamond? Wanatoka coz wanaona hawapati matunda ya kazi zao, wanapiga kazi kubwa, wanakuwa famous nchi nzima ila hakuna pesa ya maana wanayopata, faida kubwa inaenda kwa kampuni ndo maana wanaona bora watoke wakajitafutie hata kama ni kidogo ila angalau ni chake na hatumiki tena kumtajirisha mtu. Nawaambia hata Zuchu leo akiachwa na Dai kesho yake asubuhi na mapema anatoka Wasafi. kinachomuweka Zuchu wasafi ni kwamba yuko obsessed na kuolewa na Diamond. Oh yeah, bado tukiwa kwenye hiyo topic ya king’ang’a ngoja niwaambie hivi, ni ngumu mnooo Diamond kumuacha king’ang’a, tena mnooooo. Hivi ndugu zangu mnajua maisha yalivyo magumu, mnataka Diamond amuache mwanamke anaemuingizia mabilioni ya pesa then aje kwenu vishanshuda wa mjini mnaosubiri kupewa? Itabidi akununulie gari, akupangie nyumba, akupe hela ya mawigi, akupe hela ya kulea ukoo wako, then uombe akujengee nyumba, why aingie kwenye matatizo hayo wakati Zuchu hayo mambo yote anajifanyia mwenyewe na on top of that anamwingizia pesa kwenye account? Yani aache mwanamke ambae hamcosti hata senti moja na bado anamwingizia mahela kwenye account aje kwenu omba omba na makalio yenu ya Uturuki? Itabidi Zuchu ashuke kimziki aache kumwingizia Diamond mahela ndo atapigwa chini. Yani Zuchu siku akishindwa kumwingizia Dai pesa kwenye account ndio ataachwa na sio kabla.Sasa acheni kujaji uzuri wako vs wa king’ang’a, jaji pesa utakayoweza kumwingizia Dai kwenye account Vs Zuchu anayomwingizia ndo utapata majibu. Na sasa hivi Zuchu kawaka moto Dai amuoe au anaingia mitini mnadhani Dai atachagua nini? Ampoteze top money maker wa Wasafi au aoe?Tumieni akili hapo, mnadhani atachagua nini? Basi kwa hii posti kama namuona Dai atavyoniletea barua ingine ya lawyer huku Marekani 🤣. Weee mi sio kina Mwijaku uliowatishia na vibarua vya lawyer siku hizi wameufyata wooote. Weeee, mimi tutagaragazana mahakamani mpaka woote tufilisike kwa kulipa malawyer 🤣. Chezea wapare tunavyopenda kesi 🤣🤣.Yes guys, kama mnenoti siku hizi hakuna mtu bongo anadhubutu kumchamba Dai, wooote kawanyoosha kwa kuwatishia lawyer.0 Comments ·0 Shares ·727 Views -
0 Comments ·0 Shares ·355 Views
-
Kwa faida ya wengi ambao wanahoji kuhusu Kibu Denis na Uraia, ikawaje picha akacheza timu ya Taifa na FIFA wakapitisha, mkapitie kwenye website ya FIFA kuhusu “Guide to submitting a request for eligibility or change of association “
Hapo FIFA wana mambo mawili kubadili Mashirikisho ama kuomba uhalali wa kucheza timu ya taifa, mfano Pacome akitaka kucheza Tanzania anaangukia kigezo cha kubadili Mashirikisho (Change of association) ila KIBU wakati anataka kucheza Tanzania, tuliomba uhalali ambapo tukaangukia kigezo cha “Request for eligibility “ kwakuwa Kibu ni Mkimbizi na hakuwa Raia wa Congo na hata angekuwa Raia bado ni rahisi kwakuwa ana haki ya Ukimbizi FIFA wanaitambua.
Sasa FIFA kwenye eneo hilo kwa mujibu wa RGAS, kifungu cha saba (7) ambapo KIBU kukimbilia Tanzania haikuwa kwasababu za Kimpira bali kusaka Hifadhi hivyo ilihitajika cheti chake cha Ukimbizi na sababu za Kibinadamu, hiyo haina mlolongo wowote mrefu, anakidhi vigezo kwa haraka na anatwanga timu ya Taifa.
Hivyo KIBU ni kesi tofauti na hii ya Wachezaji wa Singida.
(Farhan JR)
Kwa faida ya wengi ambao wanahoji kuhusu Kibu Denis na Uraia, ikawaje picha akacheza timu ya Taifa na FIFA wakapitisha, mkapitie kwenye website ya FIFA kuhusu “Guide to submitting a request for eligibility or change of association “ Hapo FIFA wana mambo mawili kubadili Mashirikisho ama kuomba uhalali wa kucheza timu ya taifa, mfano Pacome akitaka kucheza Tanzania anaangukia kigezo cha kubadili Mashirikisho (Change of association) ila KIBU wakati anataka kucheza Tanzania, tuliomba uhalali ambapo tukaangukia kigezo cha “Request for eligibility “ kwakuwa Kibu ni Mkimbizi na hakuwa Raia wa Congo na hata angekuwa Raia bado ni rahisi kwakuwa ana haki ya Ukimbizi FIFA wanaitambua. Sasa FIFA kwenye eneo hilo kwa mujibu wa RGAS, kifungu cha saba (7) ambapo KIBU kukimbilia Tanzania haikuwa kwasababu za Kimpira bali kusaka Hifadhi hivyo ilihitajika cheti chake cha Ukimbizi na sababu za Kibinadamu, hiyo haina mlolongo wowote mrefu, anakidhi vigezo kwa haraka na anatwanga timu ya Taifa. Hivyo KIBU ni kesi tofauti na hii ya Wachezaji wa Singida. (Farhan JR) -
"The Unforgetable THROW BACK
Ilikuwa mwaka 2003 takribani Miaka 22 iliyopita nikiwa naingia kwenye ukumbi wa DIAMOND JUBILEE - UPANGA kwa kusukuma Mkokoteni 'KiZALI LA MENTALI' feat @sir_nature kwenye uzinduzi wa Album yangu ya pili ya MAPINDUZI HALISI ambayo baadae ilikuja kutangazwa na KILIMANJARO MUSIC AWARDS wakati huo (sasa TMA) kuwa album bora ya HIP HOP kwa mwaka 2003, Nilikuwa nimezungukwa na MIILI VIBANDA (Bouncers) pamoja na Producer wangu bora wa muda wote Tanzania @majani187 of BONGO RECORDS na @solothang_aka_ulamaa
NB: Ni wasanii wachache sana tuliokuwa na uwezo wa kuujaza ukumbi mkubwa wa DIAMOND JUBILEE na ukatapika kisawasawa
Je wewe ulikuwa wapi kipindi hiki???" - Professor Jay, Msanii wa muziki Hip-hop Tanzania
"The Unforgetable THROW BACK 🔥🔥🔥 Ilikuwa mwaka 2003 takribani Miaka 22 iliyopita nikiwa naingia kwenye ukumbi wa DIAMOND JUBILEE - UPANGA kwa kusukuma Mkokoteni 'KiZALI LA MENTALI' feat @sir_nature kwenye uzinduzi wa Album yangu ya pili ya MAPINDUZI HALISI ambayo baadae ilikuja kutangazwa na KILIMANJARO MUSIC AWARDS wakati huo (sasa TMA) kuwa album bora ya HIP HOP kwa mwaka 2003, Nilikuwa nimezungukwa na MIILI VIBANDA (Bouncers) pamoja na Producer wangu bora wa muda wote Tanzania @majani187 of BONGO RECORDS na @solothang_aka_ulamaa 👑 NB: Ni wasanii wachache sana tuliokuwa na uwezo wa kuujaza ukumbi mkubwa wa DIAMOND JUBILEE na ukatapika kisawasawa💪💪💪 Je wewe ulikuwa wapi kipindi hiki???" - Professor Jay, Msanii wa muziki Hip-hop Tanzania -
DUNIA NA MAAJABU YAKE
(Muundo wa Dunia na Maajabu Yaliyomo)
1. UMRI WA DUNIA
HII Dunia yetu ina historia ndefu mno tangu ilipojiunda angani, miaka takribani bilioni 4.5 iliyopita.
Tarakimu za umri huo wa miaka bilioni 4.5 ni 4,500,000,000, yaani miaka milioni elfu nne na mia tano iliyopita.
Dunia ambayo kwa lugha ya Kiingereza inafahamika vyema kwa jina la 'Earth', pia hujulikana kama 'the World', ikimaanishwa ulimwengu.
Aidha, Dunia ni sayari pekee kwenye himaya ya sayari zilizopo chini ya jua ambayo jina lake halitokani na majina ya "Miungu wa Dola" ya Kigiriki au ya Kirumi.
Asili ya jina la 'earth' ni 'erde' lenye asili ya nchini Ujerumani, na maana yake ni udongo au ardhi.
Mpaka kuweza kupata umri huo wa dunia wanasayansi walifanya kazi ya kutafiti na kisha kuwasilisha matokeo yao kwenye makongamano ya kisayansi duniani, ambapo matokeo hayo yalijadiliwa kwa kina na hatimaye kukubalika kama hivi.
Kumbuka katika majadiliano hayo huwepo mivutano mikali miongoni mwa wanasayansi waalikwa, ambapo pia jopo la wanasayansi wanaowasilisha utafiti husika hujikuta wakitakiwa kujibu hoja mbalimbali za wanasayansi wenzao.
Kuna wakati baadhi ya matokeo ya tafiti kadhaa hukataliwa, huku watafiti husika wakitakiwa kurejea upya tafiti zao.
Wanasayansi hupata umri wa sayari kwa kupima umri wa miamba ya sayari husika, ambapo mwamba wenye umri mkubwa zaidi kuliko miamba yote ndiyo huchukuliwa kuwa umri wa sayari husika.
Itakumbukwa kuwa Msahafu wa Biblia (Sura ya Mwanzo 1) husimulia jinsi Mwenyezi Mungu alivyoumba "mbingu na nchi na vyote vilivyomo kwa siku 6," lakini pia Msahafu huohuo kwenye aya zingine hueleza kuwa miaka elfu moja ya duniani yaweza kuwa sawa na siku moja kwenye ya Makazi ya Mwenyezi Mungu.
Ni dhahiri kuwa binadamu tukiwa hatuna hoja sahihi kwa maelezo ya aina hiyo, ndipo tunaona ni vyema mambo ya Mwenyezi Mungu kumwachia Yeye Mwenyewe Mwenyezi Mungu.
2. KUUMBIKA DUNIA, SAYARI, JUA, NYOTA
Kimsingi, Dunia kama zilivyo sayari zingine zote ilijiunda kutokana na mabaki ya vitu vilivyotumika kuunda Jua.
Jua ambalo ni nyota kama zilivyo nyota zote angani, lilijiunda lenyewe kwenye eneo la anga lijulikanalo kama 'Pillars of Creation' (nguzo za uumbaji) katika ukanda wa anga wenye upana ambao huonekana kutokuwa na mwisho.
Ukanda huo ujulikanao kama 'Solar Nebula,' umegubikwa na mawingu ya vumbi la huko angani pamoja na aina mbalimbali za gesi na hewa, ikiwemo haidrojeni na heliumu.
'Solar' ni jina la nishati itokanayo na joto la jua, na 'Nebula' kwa lugha ya Kilatini ni "wingu" au vumbi la gesi asilia mithili ya ukungu.
Hivyo, 'Solar Nebula' ni ukanda katika anga ya mbali wenye mawingu yaliyosheheni nishati yenye joto, sawa na nishati ya joto la jua.
Sasa basi, tunafahamu vyema kuwa jua hutoa mionzi hatari yenye joto kali mithili ya moto mkali, na ambayo ikiboreshwa kisayansi pia huweza kutoa nishati ya umeme.
Hivyo, kwa muktadha huo, hebu ngoja sasa tuleta pamoja hewa za gesi, zikiwemo haidrojeni na heliumu, mawingu yenye nishati ya umeme wa jua, vumbi la angani na tufani itokanayo na mchafuko mbaya wa hali ya hewa huko anga za mbali.
Na ili kuweza kupata matokeo yanayotakiwa, hebu pia tutambue uwepo wa nguvu kubwa ya asili katika kiwango kijulikanacho kwa jina la "Supernatural Power", ambayo ndiyo huwa kisababishi cha mambo yote.
Kisayansi, "Supernatural Power" ni nguvu kubwa ya asili ambayo huendesha mifumo mbalimbali ya asili, ambapo duniani nguvu hiyo hujulikana kama Nguvu ya Mungu.
Nguvu asili hiyo, yaani Supernatural Power, husababisha tufani ambayo huvurumisha kwa pamoja vitu vyote hivyo, (gesi, hewa, mawingu yenye nishati ya joto na vumbi la angani) ili kuunda tufani yenye umbo la duara.
Duara hiyo ni kama ile itokanayo na kimbunga kikali duniani, na ambacho sasa tutaona kikifungamanisha pamoja vitu vyote hivyo katika mchafuko mkubwa wa hali mbaya ya hewa.
Natumia maneno ya msisitizo kuelezea "ukubwa" wa mchafuko huo wa hali ya hewa katika eneo hilo la anga, kwani katika kuunda sayari au nyota nguvuasili kubwa hutumika.
Aidha, tufani hiyo ya duara itakayoanza kidogo kidogo kama kimbunga kikali, itazidi kukua hadi kuwa na kipenyo cha takribani kilomita 10 hadi 200 au zaidi na kwendelea.
Tufani hiyo ndiyo itavurumisha kwa pamoja gesi na hewa za naitrojeni na heliumu, mawingu ya nishati ya joto na vumbi la angani (kama kifanyavyo kimbunga kikali katika eneo tambarare la duniani).
Pia, wakati mchafuko huo wa hali mbaya ya hewa ukiendelea, hebu ngoja sisi watazamaji tujibanze mahali fulani kwa mbali kushuhudia duara hiyo ya tufani ikijizungusha yenyewe bila kukoma kwa kipindi cha miaka mingi.
Kitakachofuata ni kuanza kuona kiini cha moto kikianza kujiunda katikati ya duara hiyo ya tufani kali, huku pia nje ya duara hiyo vitu kibao vikivutwa kujiunga na mzunguko wa hiyo tufani ya duara.
Vitu hivyo ni pamoja na vumbi zaidi la angani, na gesi zaidi zenye joto kali.
Wakati huohuo kipenyo na mzingo wa duara hiyo vitazidi kuongezeka upana na ukubwa, mfano wa duara yenye umbo sawa na la mpira mkubwa wa miguu.
Hivyo, baada ya miaka takribani milioni moja tutashangaa kuona lile vumbi likigeuka taratibu kuwa miamba ya moto ndani ya kiini cha tufani hiyo ya duara.
Miamba hiyo ni kutokana na lile vumbi la angani ambalo hatimaye limeshikamana pamoja mithili ya zege, na hatimaye kuwa miamba ndani ya tufani ya duara.
Sanjari na kuundika huko ndani ya kitovu cha hiyo tufani ya duara, pia kwelekea nje ya duara hiyo utaundika udongo ambao ardhi, mchanga na mawe.
Kimsingi, vitu hivyo pia ni matokeo ya lile vumbi la angani ambalo lilikusanywa pamoja na kuvutwa na kasi ya mzunguko wa tufani.
Hatua hiyo mpya inatokana na kuwepo mshikamano na mgandamizo wa zile chembechembe za lile vumbivumbi ndani ya tufani.
Vurumai hiyo ya mzunguko wa hiyo tufani ya duara yenye vumbi, itazidi kukua hadi kuunda sumaku ya asili ndani ya kile kitovu cha duara ya tufani.
Kutokana na duara hiyo ya tufani kuongezeka ukubwa, hatimaye sumaku iliyopo kwenye kitovu cha duara hiyo itaishiwa nguvu ya kwendelea kunasa vumbi zaidi kuja kwenye mzingo wa hiyo duara ya tufani.
Kumbuka kuwa wakati huo hiyo duara pia itaunda kimo kutoka kwenye usawa wa ardhi yake kwenda ndani kwenye kitovu chake, na hivyo kuwa duara ya mviringo kama umbo mfano wa mpira mchezo wa miguu.
Baada ya kupita maelfu ya miaka mingi, duara hiyo ambayo hapo awali ilianza kama umbo la tufani na kuzidi kukua huko angani, sasa itakuwa na joto kali kupita kiasi na kuanza kung'aa kama jua.
Jua hilo, ndiyo nyota mojawapo ya zile ambazo huonekana usiku ziking'aa angani.
Lakini pia wakati wa kujiunda nyota hiyo, kama tulivyoona hapo awali, baadhi ya mabaki yake yaliyokuwa yakitawanyika angani wakati ile tufani ya duara ikijizungusha, huweza kujikusanya pamoja na kuunda sayari ambazo huzunguka baadhi ya hizo nyota.
Hivyo ndivyo zilivyojiunda sayari zote ambazo huelea kwa kulizunguka jua letu.
Mathalani, sayari zote ambazo hulizunguka jua, ikiwemo dunia zilijiunda kutokana na mabaki ya vitu kama gesi, michanga na mawe ambavyo vilitawanyika angani wakati jua likijiunda (kama ambavyo imeelezwa hapo awali).
3. KIINI CHA DUNIA
Dunia yetu ambayo wastani wa nusu kipenyo cha umbo lake la duara ni kilomita 6,371, mzingo wake ni kilomita takribani 40,041.
Kama zilivyo sayari zote katika himaya ya jua, dunia nayo ilijiunda wakati jua likijiunda lenyewe.
Yaani kwamba sayari ni mabaki ya vitu vilivyotumika kuliunda jua.
Kadhalika kama zilivyo sayari zingine zote, dunia nayo ina kiini chake ambacho kipo katikati ya ardhi yake.
Kiini hicho kina nguvu kubwa ya sumaku ambayo, pamoja na mambo mengineyo, 'huvuta' umbo hilo la duara kutoka juu ya ardhi kwenda katikati ya kiini hicho.
Muundo huo ndio hulifungamanisha pamoja umbo la duara la dunia, na hivyo kuzuia umbo hilo lisifumke kutoka ardhini na kusambaratika.
Hiyo ni sawa na mpira wa miguu unavyoweza kupasuka na kusambaratika, kama utajazwa upepo kupita kiasi chake.
Kiini hicho ambacho kipo katikati kabisa ya dunia, kinajulikanacho kwa jina la kisayansi la 'Inner Core.'
Kiini hicho kina joto kali la sentigredi 6,230 ambacho ndio kiasi cha joto la jua.
Kiini hicho kina umbo la duara lenye nusu kipenyo cha kilomita 1,250.
Kama ingetokea kuchimba ardhi wima kwenda kwenye kiini hicho, mchimbaji angeanza kukutana na joto la kiini hicho kuanzia kimo cha umbali wa kilomita 5,150 kutoka usawa wa juu ya ardhi tunayotembea.
Katika historia ya uchimbaji ardhi, kina kirefu kilichowahi kuchimbwa ardhini ni mita 12,345 (kilomita 12.345) huko Sakhalini, nchini Urusi, kwa ajili ya uvunaji wa mafuta ya petroli.
Kiini cha dunia kinaundwa na madini mchanganyiko wa nikeli (nickle), chuma (iron) na dhahabu.
Kwa mujibu wa utafiti, inakadiriwa kuwa kama dhahabu hiyo ingechimbwa na kuchomwa mpaka kuwa kimiminika sawa na uji na kisha kumwagwa chini, ingeweza kuifunika dunia yote kwa unene wa sentimeta 45.
Kiini hicho muhimu kwa uhai wa sayari hii ya dunia kiligunduliwa mwaka 1936 na mtaalamu wa matetemeko ya ardhi wa nchini Denmark, mwanamama Dkt. Inge Lehmann.
Dkt. Lehmann alihitimu shahada yake ya kwanza katika fani ya Hisabati mwaka 1910, ya Uzamili mwaka 1920 (zote kutoka Chuo Kikuu cha Copenhagen nchini mwake), na ile ya Uzamivu kutoka Chuo Kikuu cha Cambridge nchini Uingereza.
Alifariki kwa uzee mwaka 1993 akiwa na umri wa miaka 104.
4. MAJI DUNIANI
Kupatikana maji kwenye dunia yetu, ni mojawapo ya miundo ambayo haipo katika sayari zingine ambazo tuna taarifa za kitafiti kuzuhusu.
Maji ni muhimili muhimu kwa ajili ya uhai wa viumbe wote na mimea, ambavyo kwa pamoja havipo katika sayari zingine za himaya ya jua.
Kwa mujibu wa tafiti nyingi ambazo zimefanyika kwa miongo mingi ya miaka kujaribu kubaini nini chanzo cha kuwepo maji duniani, hakuna hata utafiti mmoja ulioonesha kwa usahihi matokeo ya kuridhisha.
Miongoni mwa tafiti hizo ni pamoja na ule wa mwaka 2005, ambapo Mkuu wa Idara ya Masomo ya Sayari na Mwezi katika Chuo Kikuu cha Arizona nchini Marekani, Profesa Michael Julian Drake, na mwenzake ambaye ni mtaalamu wa Vimondo, Dkt. Huberto Campins, wa Chuo Kikuu cha Central Florida, walitafiti nini chanzo cha kuwepo maji duniani.
Katika mawasilisho yao kwenye kongamano la kisayansi la Chama cha Wanataaluma wa Maarifa ya Anga za Juu (IAU), watafiti hao walikanusha madai ya uwezekano wa dunia hapo kale kugongwa na kimondo kikubwa na kusababisha maji kulipuka kutoka ardhini.
Wakiwasilisha matokeo ya utafiti wao kwenye mkutano wa kongamano hilo, magwiji hao wa masuala ya sayari walieleza kwenye waraka wao uitwao "Origin of water on the terrestial planets" (chanzo cha kuwepo maji kwenye sayari).
Walidai kuwa maji yaliyopo duniani yaliumbika kwenye ardhi ya dunia tangu mwanzo, wakati ikijiunda angani.
Ikumbukwe kuwa eneo la uso wa dunia likiwa ni jumla ya kilomita za mraba milioni 510, asilimia 70.8 ya eneo hilo imefunikwa na maji na asilimia 29.2 ni nchi kavu, ikiwemo milima, mabonde na ardhi tambarare.
5. HEWA YA OKSIJENI
Muundo mwingine muhimu katika sayari hii ya dunia ni hewa ambazo ni tawala, yaani Naitrojeni ambayo kwa usahihi imeenea kwa asilimia 78.08 ya hewa yote ya dunia, Oksijeni asilimia 20.95, 'Argon' asilimia 0.93, hewa ya Ukaa (Carbon dioxide) asilimia 0.039, na asilimia moja ni hewa mithili ya mvuke wa maji (water vapour).
Hewa ya Oksijeni ambayo ni nguzo muhimu kwa ajili ya uhai wa viumbe wote na pia haipatikani kwenye sayari nyingine chini ya jua, inadhaniwa ilianza kupatikana duniani miaka takribani bilioni 2.5 iliyopita kufuatia "kukomaa kwa kiini cha dunia."
Kwa mujibu wa matokeo ya tafiti mbalimbali na nadharia za kisayansi, inaoneshwa kuwa kukomaa kwa kiini hicho cha dunia hatimaye ndiko kulisababisha kuzuka duniani milipuko ya volikano ambayo pia ilisababisha kuzuka mabonde na milima.
Inaoneshwa kuwa tayari wakati huo maji yaliishakuwepo duniani, na kuwezesha kuzuka chembechembe ndogo sana za kibakteria zijulikanazo kwa jina la kisayansi la 'cyanobacteria' au 'blue-green algae'.
Kwa kutumia mwanga wa jua, maji na hewa ya ukaa, chembechembe hizo ziliweza kuzalisha hewa mbalimbali, ikiwemo 'Carbonhydrates' na Oksijeni.
Kwa kuwa hizo chembechembe ndogo za kibakteria huishi baharini, ilikuwa rahisi kwa oksijeni kutokea baharini kupepea na kuenea katika anga ya dunia na kuzuiliwa hapo na nguvu asili ya uvutano ya dunia ili pia ibaki ikienea pote duniani.
Mpaka wakati wa kuzuka duniani mimea na viumbe hai miaka takribani bilioni 3.5 iliyopita, tayari oksijeni ilikwa ni tele duniani; na hivyo kutumika kudumisha uhai wa viumbe hadi wakati huu.
6. UKANDA WA 'OZONE'
Muundo mwingie muhimu wa asili kwa dunia ni ukanda wa anga ujulikanao kwa jina la 'ozone' ambao umetanda kama 'mwavuli' kwenye anga ya dunia, na kuikinga isidhuriwe na mionzi hatari ya sumu kutoka kwenye Jua.
Ukanda huo maarufu kama 'ozone layer' umetanda kuanzia usawa wa kilometa 15 kutoka ardhini kwenda juu angani mpaka ukomo wa kilomita takribani 50, ambapo huchuja asilimia kati ya 97 na 99 ya mionzi hatari kwenye miale ya joto la jua.
Miongoni mwa matatizo yanayosababishwa na mionzi hiyo hatari kutoka kwenye jua, ni pamoja na magonjwa ya saratani ya ngozi kwa bianadamu.
Pia juu ya ukanda wa tabaka la ozone kuna ukanda mwingine uitwao "atmosphere" ambao ni madhubuti kiasi kwamba vitu vinavyotoka anga za juu na kujaribu kuupenya ili kufika duniani, hukumbana na joto kali na kusambaratishwa kwa kuunguzwa.
Si kwamba tabaka hilo lina joto, isipokuwa kasi ya "kuanguka" vitu hivyo kutoka juu angani kuja dunia husababisha msuguano na chembechembe za gesi katika eneo hilo na kuzalisha joto mithili ya ndimi za moto.
Picha za video za vyombo vya 'Apollo' vikirejea duniani kutoka mwezini vikiwa na wanaanga ndani yake na kupenya tabaka hilo kwa kasi ya kilomita 39,000 kwa saa, huonekana kughubikwa na ndimi za moto wa rangi ya njano na bluu.
Rangi hizo ni ishara ya ukali wa moto huo, lakini kutokana na waundaji wa vyombo hivyo kutumia mchanganyiko wa mabati na plastiki ngumu visivyopenywa na joto, Apollo huonekana kulichana tabaka hilo na kutokea upande wa pili ambao ni anga ya dunia.
Hivyo basi, mfano huo mdogo unaonesha uimara wa tabaka hilo la 'ozone', ambalo kama ambavyo tumeona huchuja mionzi ya sumu kutoka kwenye mwanga wa jua ili kutolete madhara kwa viumbe duniani.
Mwanga huo ukisafiri kutoka juani umbali wa kilomita milioni 150 kwa kasi ya kilomita 299,793, hutua duniani ndani ya dakika 8 na sekunde 19 ukiwa tayari umechujwa wakati ukipenya tabaka hilo.
'Ozone' iligunduliwa mwaka 1913 na wanasayansi wawili wa nchini Ufaransa, Charlest Fabry na Henri Buisson, ambapo kipimo cha kasi ya mwanga kiligunduliwa na mwanasayansia wa anga za juu wa nchini Denmark, Ole Roemer, mwaka 1676.
7. NGUVU ASILI YA UVUTANO
Muundo mwingine wa dunia ni nguvu ya asili ya uvutano ya dunia, maarufu kama 'gravitation', ambayo huvuta vitu kuvirejesha chini duniani pale vinaporushwa kwenda juu au vile vinavyoanguka kutoka juu angani.
Nguvu hiyo ina manufaa makubwa, kwani bila kuwepo duniani binadamu na viumbe wengine wangepeperuka kama karatasi kwenda juu wakati wakitembea juu ya ardhi ya hii.
Kadhalika, nguvu hiyo husaidia kuvuta hewa ya oksijeni na kuiweka karibu na ardhi kwa ajili ya matumizi mbalimbali.
Pia, nguvu hiyo husaidia kuiweka dunia, mwezi, jua na sayari zingine katika uwiano wa umbali usio na madhara kutoka kila moja.
Nguvu hiyo ya asili ndiyo huliweka joto la jua duniani na kubaki kuwa katika kiwango kinachotakiwa, na hivyo kuwezesha viumbe kupata joto la wastani na pia katika kiwango mwanana.
Nguvu hiyo huvuta mvua kuja duniani na kuwezesha maji ya bahari, maziwa na mito kutulia duniani.
Mathalani, bila nguvu asili hiyo kuwepo duniani, maji 'yangemwagika' kutoka duniani kwa kutawanyika kama upepo na kupaa kwenda juu angani na kutoweka kabisa.
Na ndio maana ukirusha maji kwenda juu, hurudi chini ardhini.
Hebu angalia mfano huu kwamba wanaanga waliokwenda mwenzini walilazimika kuvaa mavazi yenye uzito wa kilo 80 hapa duniani, lakini mavazi hayo kule mwezini yakawa na uzito wa kilo 3.
Mavazi hayo, yaani viatu, koti, suruali, na kofia nzito yenye miwani maalumu ya kukinga macho dhidi ya mionzi hatari ya jua, vyote kwa pamoja viliunganishwa na kuwa mfano wa sare za 'ovaroli' za mafundi wa magari.
Mavazi hayo pia mgongoni yakiwa yameunganishwa kwa pamoja na mtungi wa hewa ya oksijeni kwa ajili ya kupumua, yalivaaliwa mahsusi muda mfupi baada ya chombo kutua mwezini.
Hivyo, msomaji wangu tafakari nini kilisababisha mavazi kuwa mazito hapa duniani, lakini yawe mepesi kule mwezini?
Jibu ni kwamba nguvu asili ya uvutano hapa duniani ni kubwa kuliko ya kule mwezini.
Na ndipo tunaona umuhimu wa muundo huo wa nguvu asili ya uvutano, ambapo hapa duniani huvuta vitu kuja chini kwa kasi ya mita 9.81 kwa sekunde, lakini kwa kuwa nguvu ya mwezi ni hafifu, huvuta vitu kwa kasi ndogo ya mita 1.62 kwa sekunde.
Ingawa nguvu hiyo ya asili iligunduliwa kuwepo duniani miaka mingi iliyopta, mwanafizikia bingwa wa Uingereza, Sir Isaac Newton (1642-1727), ndiye anatambulika kama mgunduzi wa hesabu hizo za nguvu asili hiyo.
Anaeleza kuwa vitu vyote vyenye maumbo asili, ikiwemo jua, sayari, dunia, mwezi, na vimondo, kila kimoja kina nguvu hiyo katika viwango tofauti.
Kanuni hiyo, kwa mujibu wa matokeo ya utafiti wake, hueleza kuwa nguvu hiyo ndiyo hufanya jua kuvuta sayari zake ili kulizunguka, huku pia kila sayari ikitumia nguvu 'binafsi' (na kwa uwiano maalumu) kujihami isivutwe hadi kwenda kuligonga jua au kugongana na sayari zingine au vimondo.
Nguvuasili ya jua ni mita 274 kwa sekunde, ikiwa ni zaidi ya kiasi cha nguvuasili ya kila sayari.
Muundo huo wa kila sayari kujihami kivyake katika mstari wa njia yake hufahamika kisayansi kama "sayari kuhami mazingira ya njia yake"; yaani kwamba 'a planet has to clear the neighbourhood around its orbit.'
Newton akiwa amezaliwa 'mtoto-njiti' na baadaye kuibuka kuwa mwenye akili nyingi kiasi cha kukaribia kuwa sawa na mtu wa miujiza, hakuwahi kuoa kutokana na kinachoelezwa kuwa ni " kutokana na kutingwa na shughuli za kimasomo."
Huoneshwa kuwa muda mwingi alikuwa maabara akifanya tafiti mbalimbali za kisayansi, au akiwa maktaba akijisomea, ama akiandika kitabu, au akifundisha wanafunzi wake.
Alikuwa bingwa mwenye kipaji cha taaluma nyingi, ikiwemo Fizikia, Kemia, Hisabati, Maarifa ya Anga za Juu, Uchumi, Falsafa, na Theolojia ambayo ni taaluma ya masuala ya kiroho.
Kwa mujibu wa historia, mwanasayansi huyo gwiji wa kuigwa alihitimu shahada zake zote mbili za sayansi, yaani 'Bachelor' na 'Masters', mwaka 1665 na 1668 katika Chuo Kikuu cha Cambridge, nchini Uingereza.
Akiwa na umri wa miaka 84, mwanasayansi huyo anayedhaniwa na wengi kuwa bingwa wa hesabu za kisayansi kuliko wote duniani, alifariki mwaka 1727 akiwa usingizini.
Ripoti ya uchunguzi wa mwili wake huonesha kuwa alikuwa na tatizo la figo, lakini pia alikutwa na kiasi kingi cha zebaki.
Zebaki hiyo, yamkini, ni kutokana na kudumu mno kwenye maabara za Kemia na Fizikia, ambazo hutumia kemikali aina mbalimbali, zikiwemo hewa za gesi, katika kufanya majaribio ya kisayansi.DUNIA NA MAAJABU YAKE (Muundo wa Dunia na Maajabu Yaliyomo) 1. UMRI WA DUNIA HII Dunia yetu ina historia ndefu mno tangu ilipojiunda angani, miaka takribani bilioni 4.5 iliyopita. Tarakimu za umri huo wa miaka bilioni 4.5 ni 4,500,000,000, yaani miaka milioni elfu nne na mia tano iliyopita. Dunia ambayo kwa lugha ya Kiingereza inafahamika vyema kwa jina la 'Earth', pia hujulikana kama 'the World', ikimaanishwa ulimwengu. Aidha, Dunia ni sayari pekee kwenye himaya ya sayari zilizopo chini ya jua ambayo jina lake halitokani na majina ya "Miungu wa Dola" ya Kigiriki au ya Kirumi. Asili ya jina la 'earth' ni 'erde' lenye asili ya nchini Ujerumani, na maana yake ni udongo au ardhi. Mpaka kuweza kupata umri huo wa dunia wanasayansi walifanya kazi ya kutafiti na kisha kuwasilisha matokeo yao kwenye makongamano ya kisayansi duniani, ambapo matokeo hayo yalijadiliwa kwa kina na hatimaye kukubalika kama hivi. Kumbuka katika majadiliano hayo huwepo mivutano mikali miongoni mwa wanasayansi waalikwa, ambapo pia jopo la wanasayansi wanaowasilisha utafiti husika hujikuta wakitakiwa kujibu hoja mbalimbali za wanasayansi wenzao. Kuna wakati baadhi ya matokeo ya tafiti kadhaa hukataliwa, huku watafiti husika wakitakiwa kurejea upya tafiti zao. Wanasayansi hupata umri wa sayari kwa kupima umri wa miamba ya sayari husika, ambapo mwamba wenye umri mkubwa zaidi kuliko miamba yote ndiyo huchukuliwa kuwa umri wa sayari husika. Itakumbukwa kuwa Msahafu wa Biblia (Sura ya Mwanzo 1) husimulia jinsi Mwenyezi Mungu alivyoumba "mbingu na nchi na vyote vilivyomo kwa siku 6," lakini pia Msahafu huohuo kwenye aya zingine hueleza kuwa miaka elfu moja ya duniani yaweza kuwa sawa na siku moja kwenye ya Makazi ya Mwenyezi Mungu. Ni dhahiri kuwa binadamu tukiwa hatuna hoja sahihi kwa maelezo ya aina hiyo, ndipo tunaona ni vyema mambo ya Mwenyezi Mungu kumwachia Yeye Mwenyewe Mwenyezi Mungu. 2. KUUMBIKA DUNIA, SAYARI, JUA, NYOTA Kimsingi, Dunia kama zilivyo sayari zingine zote ilijiunda kutokana na mabaki ya vitu vilivyotumika kuunda Jua. Jua ambalo ni nyota kama zilivyo nyota zote angani, lilijiunda lenyewe kwenye eneo la anga lijulikanalo kama 'Pillars of Creation' (nguzo za uumbaji) katika ukanda wa anga wenye upana ambao huonekana kutokuwa na mwisho. Ukanda huo ujulikanao kama 'Solar Nebula,' umegubikwa na mawingu ya vumbi la huko angani pamoja na aina mbalimbali za gesi na hewa, ikiwemo haidrojeni na heliumu. 'Solar' ni jina la nishati itokanayo na joto la jua, na 'Nebula' kwa lugha ya Kilatini ni "wingu" au vumbi la gesi asilia mithili ya ukungu. Hivyo, 'Solar Nebula' ni ukanda katika anga ya mbali wenye mawingu yaliyosheheni nishati yenye joto, sawa na nishati ya joto la jua. Sasa basi, tunafahamu vyema kuwa jua hutoa mionzi hatari yenye joto kali mithili ya moto mkali, na ambayo ikiboreshwa kisayansi pia huweza kutoa nishati ya umeme. Hivyo, kwa muktadha huo, hebu ngoja sasa tuleta pamoja hewa za gesi, zikiwemo haidrojeni na heliumu, mawingu yenye nishati ya umeme wa jua, vumbi la angani na tufani itokanayo na mchafuko mbaya wa hali ya hewa huko anga za mbali. Na ili kuweza kupata matokeo yanayotakiwa, hebu pia tutambue uwepo wa nguvu kubwa ya asili katika kiwango kijulikanacho kwa jina la "Supernatural Power", ambayo ndiyo huwa kisababishi cha mambo yote. Kisayansi, "Supernatural Power" ni nguvu kubwa ya asili ambayo huendesha mifumo mbalimbali ya asili, ambapo duniani nguvu hiyo hujulikana kama Nguvu ya Mungu. Nguvu asili hiyo, yaani Supernatural Power, husababisha tufani ambayo huvurumisha kwa pamoja vitu vyote hivyo, (gesi, hewa, mawingu yenye nishati ya joto na vumbi la angani) ili kuunda tufani yenye umbo la duara. Duara hiyo ni kama ile itokanayo na kimbunga kikali duniani, na ambacho sasa tutaona kikifungamanisha pamoja vitu vyote hivyo katika mchafuko mkubwa wa hali mbaya ya hewa. Natumia maneno ya msisitizo kuelezea "ukubwa" wa mchafuko huo wa hali ya hewa katika eneo hilo la anga, kwani katika kuunda sayari au nyota nguvuasili kubwa hutumika. Aidha, tufani hiyo ya duara itakayoanza kidogo kidogo kama kimbunga kikali, itazidi kukua hadi kuwa na kipenyo cha takribani kilomita 10 hadi 200 au zaidi na kwendelea. Tufani hiyo ndiyo itavurumisha kwa pamoja gesi na hewa za naitrojeni na heliumu, mawingu ya nishati ya joto na vumbi la angani (kama kifanyavyo kimbunga kikali katika eneo tambarare la duniani). Pia, wakati mchafuko huo wa hali mbaya ya hewa ukiendelea, hebu ngoja sisi watazamaji tujibanze mahali fulani kwa mbali kushuhudia duara hiyo ya tufani ikijizungusha yenyewe bila kukoma kwa kipindi cha miaka mingi. Kitakachofuata ni kuanza kuona kiini cha moto kikianza kujiunda katikati ya duara hiyo ya tufani kali, huku pia nje ya duara hiyo vitu kibao vikivutwa kujiunga na mzunguko wa hiyo tufani ya duara. Vitu hivyo ni pamoja na vumbi zaidi la angani, na gesi zaidi zenye joto kali. Wakati huohuo kipenyo na mzingo wa duara hiyo vitazidi kuongezeka upana na ukubwa, mfano wa duara yenye umbo sawa na la mpira mkubwa wa miguu. Hivyo, baada ya miaka takribani milioni moja tutashangaa kuona lile vumbi likigeuka taratibu kuwa miamba ya moto ndani ya kiini cha tufani hiyo ya duara. Miamba hiyo ni kutokana na lile vumbi la angani ambalo hatimaye limeshikamana pamoja mithili ya zege, na hatimaye kuwa miamba ndani ya tufani ya duara. Sanjari na kuundika huko ndani ya kitovu cha hiyo tufani ya duara, pia kwelekea nje ya duara hiyo utaundika udongo ambao ardhi, mchanga na mawe. Kimsingi, vitu hivyo pia ni matokeo ya lile vumbi la angani ambalo lilikusanywa pamoja na kuvutwa na kasi ya mzunguko wa tufani. Hatua hiyo mpya inatokana na kuwepo mshikamano na mgandamizo wa zile chembechembe za lile vumbivumbi ndani ya tufani. Vurumai hiyo ya mzunguko wa hiyo tufani ya duara yenye vumbi, itazidi kukua hadi kuunda sumaku ya asili ndani ya kile kitovu cha duara ya tufani. Kutokana na duara hiyo ya tufani kuongezeka ukubwa, hatimaye sumaku iliyopo kwenye kitovu cha duara hiyo itaishiwa nguvu ya kwendelea kunasa vumbi zaidi kuja kwenye mzingo wa hiyo duara ya tufani. Kumbuka kuwa wakati huo hiyo duara pia itaunda kimo kutoka kwenye usawa wa ardhi yake kwenda ndani kwenye kitovu chake, na hivyo kuwa duara ya mviringo kama umbo mfano wa mpira mchezo wa miguu. Baada ya kupita maelfu ya miaka mingi, duara hiyo ambayo hapo awali ilianza kama umbo la tufani na kuzidi kukua huko angani, sasa itakuwa na joto kali kupita kiasi na kuanza kung'aa kama jua. Jua hilo, ndiyo nyota mojawapo ya zile ambazo huonekana usiku ziking'aa angani. Lakini pia wakati wa kujiunda nyota hiyo, kama tulivyoona hapo awali, baadhi ya mabaki yake yaliyokuwa yakitawanyika angani wakati ile tufani ya duara ikijizungusha, huweza kujikusanya pamoja na kuunda sayari ambazo huzunguka baadhi ya hizo nyota. Hivyo ndivyo zilivyojiunda sayari zote ambazo huelea kwa kulizunguka jua letu. Mathalani, sayari zote ambazo hulizunguka jua, ikiwemo dunia zilijiunda kutokana na mabaki ya vitu kama gesi, michanga na mawe ambavyo vilitawanyika angani wakati jua likijiunda (kama ambavyo imeelezwa hapo awali). 3. KIINI CHA DUNIA Dunia yetu ambayo wastani wa nusu kipenyo cha umbo lake la duara ni kilomita 6,371, mzingo wake ni kilomita takribani 40,041. Kama zilivyo sayari zote katika himaya ya jua, dunia nayo ilijiunda wakati jua likijiunda lenyewe. Yaani kwamba sayari ni mabaki ya vitu vilivyotumika kuliunda jua. Kadhalika kama zilivyo sayari zingine zote, dunia nayo ina kiini chake ambacho kipo katikati ya ardhi yake. Kiini hicho kina nguvu kubwa ya sumaku ambayo, pamoja na mambo mengineyo, 'huvuta' umbo hilo la duara kutoka juu ya ardhi kwenda katikati ya kiini hicho. Muundo huo ndio hulifungamanisha pamoja umbo la duara la dunia, na hivyo kuzuia umbo hilo lisifumke kutoka ardhini na kusambaratika. Hiyo ni sawa na mpira wa miguu unavyoweza kupasuka na kusambaratika, kama utajazwa upepo kupita kiasi chake. Kiini hicho ambacho kipo katikati kabisa ya dunia, kinajulikanacho kwa jina la kisayansi la 'Inner Core.' Kiini hicho kina joto kali la sentigredi 6,230 ambacho ndio kiasi cha joto la jua. Kiini hicho kina umbo la duara lenye nusu kipenyo cha kilomita 1,250. Kama ingetokea kuchimba ardhi wima kwenda kwenye kiini hicho, mchimbaji angeanza kukutana na joto la kiini hicho kuanzia kimo cha umbali wa kilomita 5,150 kutoka usawa wa juu ya ardhi tunayotembea. Katika historia ya uchimbaji ardhi, kina kirefu kilichowahi kuchimbwa ardhini ni mita 12,345 (kilomita 12.345) huko Sakhalini, nchini Urusi, kwa ajili ya uvunaji wa mafuta ya petroli. Kiini cha dunia kinaundwa na madini mchanganyiko wa nikeli (nickle), chuma (iron) na dhahabu. Kwa mujibu wa utafiti, inakadiriwa kuwa kama dhahabu hiyo ingechimbwa na kuchomwa mpaka kuwa kimiminika sawa na uji na kisha kumwagwa chini, ingeweza kuifunika dunia yote kwa unene wa sentimeta 45. Kiini hicho muhimu kwa uhai wa sayari hii ya dunia kiligunduliwa mwaka 1936 na mtaalamu wa matetemeko ya ardhi wa nchini Denmark, mwanamama Dkt. Inge Lehmann. Dkt. Lehmann alihitimu shahada yake ya kwanza katika fani ya Hisabati mwaka 1910, ya Uzamili mwaka 1920 (zote kutoka Chuo Kikuu cha Copenhagen nchini mwake), na ile ya Uzamivu kutoka Chuo Kikuu cha Cambridge nchini Uingereza. Alifariki kwa uzee mwaka 1993 akiwa na umri wa miaka 104. 4. MAJI DUNIANI Kupatikana maji kwenye dunia yetu, ni mojawapo ya miundo ambayo haipo katika sayari zingine ambazo tuna taarifa za kitafiti kuzuhusu. Maji ni muhimili muhimu kwa ajili ya uhai wa viumbe wote na mimea, ambavyo kwa pamoja havipo katika sayari zingine za himaya ya jua. Kwa mujibu wa tafiti nyingi ambazo zimefanyika kwa miongo mingi ya miaka kujaribu kubaini nini chanzo cha kuwepo maji duniani, hakuna hata utafiti mmoja ulioonesha kwa usahihi matokeo ya kuridhisha. Miongoni mwa tafiti hizo ni pamoja na ule wa mwaka 2005, ambapo Mkuu wa Idara ya Masomo ya Sayari na Mwezi katika Chuo Kikuu cha Arizona nchini Marekani, Profesa Michael Julian Drake, na mwenzake ambaye ni mtaalamu wa Vimondo, Dkt. Huberto Campins, wa Chuo Kikuu cha Central Florida, walitafiti nini chanzo cha kuwepo maji duniani. Katika mawasilisho yao kwenye kongamano la kisayansi la Chama cha Wanataaluma wa Maarifa ya Anga za Juu (IAU), watafiti hao walikanusha madai ya uwezekano wa dunia hapo kale kugongwa na kimondo kikubwa na kusababisha maji kulipuka kutoka ardhini. Wakiwasilisha matokeo ya utafiti wao kwenye mkutano wa kongamano hilo, magwiji hao wa masuala ya sayari walieleza kwenye waraka wao uitwao "Origin of water on the terrestial planets" (chanzo cha kuwepo maji kwenye sayari). Walidai kuwa maji yaliyopo duniani yaliumbika kwenye ardhi ya dunia tangu mwanzo, wakati ikijiunda angani. Ikumbukwe kuwa eneo la uso wa dunia likiwa ni jumla ya kilomita za mraba milioni 510, asilimia 70.8 ya eneo hilo imefunikwa na maji na asilimia 29.2 ni nchi kavu, ikiwemo milima, mabonde na ardhi tambarare. 5. HEWA YA OKSIJENI Muundo mwingine muhimu katika sayari hii ya dunia ni hewa ambazo ni tawala, yaani Naitrojeni ambayo kwa usahihi imeenea kwa asilimia 78.08 ya hewa yote ya dunia, Oksijeni asilimia 20.95, 'Argon' asilimia 0.93, hewa ya Ukaa (Carbon dioxide) asilimia 0.039, na asilimia moja ni hewa mithili ya mvuke wa maji (water vapour). Hewa ya Oksijeni ambayo ni nguzo muhimu kwa ajili ya uhai wa viumbe wote na pia haipatikani kwenye sayari nyingine chini ya jua, inadhaniwa ilianza kupatikana duniani miaka takribani bilioni 2.5 iliyopita kufuatia "kukomaa kwa kiini cha dunia." Kwa mujibu wa matokeo ya tafiti mbalimbali na nadharia za kisayansi, inaoneshwa kuwa kukomaa kwa kiini hicho cha dunia hatimaye ndiko kulisababisha kuzuka duniani milipuko ya volikano ambayo pia ilisababisha kuzuka mabonde na milima. Inaoneshwa kuwa tayari wakati huo maji yaliishakuwepo duniani, na kuwezesha kuzuka chembechembe ndogo sana za kibakteria zijulikanazo kwa jina la kisayansi la 'cyanobacteria' au 'blue-green algae'. Kwa kutumia mwanga wa jua, maji na hewa ya ukaa, chembechembe hizo ziliweza kuzalisha hewa mbalimbali, ikiwemo 'Carbonhydrates' na Oksijeni. Kwa kuwa hizo chembechembe ndogo za kibakteria huishi baharini, ilikuwa rahisi kwa oksijeni kutokea baharini kupepea na kuenea katika anga ya dunia na kuzuiliwa hapo na nguvu asili ya uvutano ya dunia ili pia ibaki ikienea pote duniani. Mpaka wakati wa kuzuka duniani mimea na viumbe hai miaka takribani bilioni 3.5 iliyopita, tayari oksijeni ilikwa ni tele duniani; na hivyo kutumika kudumisha uhai wa viumbe hadi wakati huu. 6. UKANDA WA 'OZONE' Muundo mwingie muhimu wa asili kwa dunia ni ukanda wa anga ujulikanao kwa jina la 'ozone' ambao umetanda kama 'mwavuli' kwenye anga ya dunia, na kuikinga isidhuriwe na mionzi hatari ya sumu kutoka kwenye Jua. Ukanda huo maarufu kama 'ozone layer' umetanda kuanzia usawa wa kilometa 15 kutoka ardhini kwenda juu angani mpaka ukomo wa kilomita takribani 50, ambapo huchuja asilimia kati ya 97 na 99 ya mionzi hatari kwenye miale ya joto la jua. Miongoni mwa matatizo yanayosababishwa na mionzi hiyo hatari kutoka kwenye jua, ni pamoja na magonjwa ya saratani ya ngozi kwa bianadamu. Pia juu ya ukanda wa tabaka la ozone kuna ukanda mwingine uitwao "atmosphere" ambao ni madhubuti kiasi kwamba vitu vinavyotoka anga za juu na kujaribu kuupenya ili kufika duniani, hukumbana na joto kali na kusambaratishwa kwa kuunguzwa. Si kwamba tabaka hilo lina joto, isipokuwa kasi ya "kuanguka" vitu hivyo kutoka juu angani kuja dunia husababisha msuguano na chembechembe za gesi katika eneo hilo na kuzalisha joto mithili ya ndimi za moto. Picha za video za vyombo vya 'Apollo' vikirejea duniani kutoka mwezini vikiwa na wanaanga ndani yake na kupenya tabaka hilo kwa kasi ya kilomita 39,000 kwa saa, huonekana kughubikwa na ndimi za moto wa rangi ya njano na bluu. Rangi hizo ni ishara ya ukali wa moto huo, lakini kutokana na waundaji wa vyombo hivyo kutumia mchanganyiko wa mabati na plastiki ngumu visivyopenywa na joto, Apollo huonekana kulichana tabaka hilo na kutokea upande wa pili ambao ni anga ya dunia. Hivyo basi, mfano huo mdogo unaonesha uimara wa tabaka hilo la 'ozone', ambalo kama ambavyo tumeona huchuja mionzi ya sumu kutoka kwenye mwanga wa jua ili kutolete madhara kwa viumbe duniani. Mwanga huo ukisafiri kutoka juani umbali wa kilomita milioni 150 kwa kasi ya kilomita 299,793, hutua duniani ndani ya dakika 8 na sekunde 19 ukiwa tayari umechujwa wakati ukipenya tabaka hilo. 'Ozone' iligunduliwa mwaka 1913 na wanasayansi wawili wa nchini Ufaransa, Charlest Fabry na Henri Buisson, ambapo kipimo cha kasi ya mwanga kiligunduliwa na mwanasayansia wa anga za juu wa nchini Denmark, Ole Roemer, mwaka 1676. 7. NGUVU ASILI YA UVUTANO Muundo mwingine wa dunia ni nguvu ya asili ya uvutano ya dunia, maarufu kama 'gravitation', ambayo huvuta vitu kuvirejesha chini duniani pale vinaporushwa kwenda juu au vile vinavyoanguka kutoka juu angani. Nguvu hiyo ina manufaa makubwa, kwani bila kuwepo duniani binadamu na viumbe wengine wangepeperuka kama karatasi kwenda juu wakati wakitembea juu ya ardhi ya hii. Kadhalika, nguvu hiyo husaidia kuvuta hewa ya oksijeni na kuiweka karibu na ardhi kwa ajili ya matumizi mbalimbali. Pia, nguvu hiyo husaidia kuiweka dunia, mwezi, jua na sayari zingine katika uwiano wa umbali usio na madhara kutoka kila moja. Nguvu hiyo ya asili ndiyo huliweka joto la jua duniani na kubaki kuwa katika kiwango kinachotakiwa, na hivyo kuwezesha viumbe kupata joto la wastani na pia katika kiwango mwanana. Nguvu hiyo huvuta mvua kuja duniani na kuwezesha maji ya bahari, maziwa na mito kutulia duniani. Mathalani, bila nguvu asili hiyo kuwepo duniani, maji 'yangemwagika' kutoka duniani kwa kutawanyika kama upepo na kupaa kwenda juu angani na kutoweka kabisa. Na ndio maana ukirusha maji kwenda juu, hurudi chini ardhini. Hebu angalia mfano huu kwamba wanaanga waliokwenda mwenzini walilazimika kuvaa mavazi yenye uzito wa kilo 80 hapa duniani, lakini mavazi hayo kule mwezini yakawa na uzito wa kilo 3. Mavazi hayo, yaani viatu, koti, suruali, na kofia nzito yenye miwani maalumu ya kukinga macho dhidi ya mionzi hatari ya jua, vyote kwa pamoja viliunganishwa na kuwa mfano wa sare za 'ovaroli' za mafundi wa magari. Mavazi hayo pia mgongoni yakiwa yameunganishwa kwa pamoja na mtungi wa hewa ya oksijeni kwa ajili ya kupumua, yalivaaliwa mahsusi muda mfupi baada ya chombo kutua mwezini. Hivyo, msomaji wangu tafakari nini kilisababisha mavazi kuwa mazito hapa duniani, lakini yawe mepesi kule mwezini? Jibu ni kwamba nguvu asili ya uvutano hapa duniani ni kubwa kuliko ya kule mwezini. Na ndipo tunaona umuhimu wa muundo huo wa nguvu asili ya uvutano, ambapo hapa duniani huvuta vitu kuja chini kwa kasi ya mita 9.81 kwa sekunde, lakini kwa kuwa nguvu ya mwezi ni hafifu, huvuta vitu kwa kasi ndogo ya mita 1.62 kwa sekunde. Ingawa nguvu hiyo ya asili iligunduliwa kuwepo duniani miaka mingi iliyopta, mwanafizikia bingwa wa Uingereza, Sir Isaac Newton (1642-1727), ndiye anatambulika kama mgunduzi wa hesabu hizo za nguvu asili hiyo. Anaeleza kuwa vitu vyote vyenye maumbo asili, ikiwemo jua, sayari, dunia, mwezi, na vimondo, kila kimoja kina nguvu hiyo katika viwango tofauti. Kanuni hiyo, kwa mujibu wa matokeo ya utafiti wake, hueleza kuwa nguvu hiyo ndiyo hufanya jua kuvuta sayari zake ili kulizunguka, huku pia kila sayari ikitumia nguvu 'binafsi' (na kwa uwiano maalumu) kujihami isivutwe hadi kwenda kuligonga jua au kugongana na sayari zingine au vimondo. Nguvuasili ya jua ni mita 274 kwa sekunde, ikiwa ni zaidi ya kiasi cha nguvuasili ya kila sayari. Muundo huo wa kila sayari kujihami kivyake katika mstari wa njia yake hufahamika kisayansi kama "sayari kuhami mazingira ya njia yake"; yaani kwamba 'a planet has to clear the neighbourhood around its orbit.' Newton akiwa amezaliwa 'mtoto-njiti' na baadaye kuibuka kuwa mwenye akili nyingi kiasi cha kukaribia kuwa sawa na mtu wa miujiza, hakuwahi kuoa kutokana na kinachoelezwa kuwa ni " kutokana na kutingwa na shughuli za kimasomo." Huoneshwa kuwa muda mwingi alikuwa maabara akifanya tafiti mbalimbali za kisayansi, au akiwa maktaba akijisomea, ama akiandika kitabu, au akifundisha wanafunzi wake. Alikuwa bingwa mwenye kipaji cha taaluma nyingi, ikiwemo Fizikia, Kemia, Hisabati, Maarifa ya Anga za Juu, Uchumi, Falsafa, na Theolojia ambayo ni taaluma ya masuala ya kiroho. Kwa mujibu wa historia, mwanasayansi huyo gwiji wa kuigwa alihitimu shahada zake zote mbili za sayansi, yaani 'Bachelor' na 'Masters', mwaka 1665 na 1668 katika Chuo Kikuu cha Cambridge, nchini Uingereza. Akiwa na umri wa miaka 84, mwanasayansi huyo anayedhaniwa na wengi kuwa bingwa wa hesabu za kisayansi kuliko wote duniani, alifariki mwaka 1727 akiwa usingizini. Ripoti ya uchunguzi wa mwili wake huonesha kuwa alikuwa na tatizo la figo, lakini pia alikutwa na kiasi kingi cha zebaki. Zebaki hiyo, yamkini, ni kutokana na kudumu mno kwenye maabara za Kemia na Fizikia, ambazo hutumia kemikali aina mbalimbali, zikiwemo hewa za gesi, katika kufanya majaribio ya kisayansi.0 Comments ·0 Shares ·1K Views -
*VATICAN CITY......
Nchi? Mji? Serikali au Kampuni?*
Nadhani moja kati ya maeneo ambayo yamekuwa tata zaidi kuyaelewa basi ni mji wa Vatican… tukiachilia mbali kuhusu utata/ugumu wa kuelewa mfumo wake wa uendeshaji na historia yake lakini swali jepesi zaidi ambalo kila mtu huwa anahisi analifahamu jawabu lake ni kuhusu utambulisho wa Vatican.!! Ni swali jepesi ambalo karibia kila mtu anadhani ana jawabu sahihi lakini uhalisia ni kwamba asilimia kubwa ya watu wana jawabu lisilo sahihi… kila mtu atakueleza kwamba Vatican ni nchi inayojitegemea lakini hii ni robo tu au thelethi ya jawabu…
Leo nami niandike kidogo kuhusu eneo hili… na kwenye andishi hili fupi nitaeleza utambulisho wa Vatican ukoje kwa usahihi wake kabisa!
*Muhimu:* andishi hili halilengi kukosoa au kupinga imani ya mtu yeyote. Tahadhali zote zinazingatiwa ili kulinda heshima ya imani ya kila mtu.
Tuendelee…
Vatican City, ndio makao makuu ya Kanisa Katoliki na nyumba ya maisha ya Papa, kiongozi mkuu wa kanisa Katoliki.
Vatican ndio nchi ndogo zaidi duniani kiasi kwamba unaweza kuizunguka yote kwa mzingo (circumference) kwa muda wa dakika arobaini tu kwa kutembea kwa miguu.
Ni ajabu sana kwa namna gani nchi ndogo kiasi hiki imetokea na je ni nchi kama nchi nyingine???
Jibu la swali hili ni refu sana kiaisi kwamba unaweza hata kusoma darasani kwa mwaka mzima lakini nitajaribu kuweka katika maneno machache sana ya kueleweka kwa wepesi…
Miaka ya kale sana Papa wa Kanisa Katoliki alikuwa ni mtawala wa nchi ambayo ilikuwa inajiita *Himaya ya Papa (Papal State)* ambayo inarandana kabisa na eneo la sasa la nchi nzima ya Italia. Hii ilikuwa takribani miaka ya 754 mpaka miaka ya 1870.
Ni katika kipindi hiki ambacho Papa aliteua eneo ndani ya nchi yake Papal State ambalo likajengwa *St. Peters Basilica*, kanisa kubwa zaidi duniani na lenye nakshi adhimu zaidi. Eneo hili ambalo St. Peters Basilica ilijengwa ni eneo fulani hivi la muinuko ambako hapo hapo pia yalijengwa makazi ya Papa kuishi.
Ikumbukwe kwamba katika kipindi hiki hiki cha uwepo wa himaya ya Papal State pia ilikuwa inapakana na Ufalme wa Italy (Kingdom of Italy) japo kila moja ilikuwa inajitegemea.
Japokuwa himaya hizi mbili zilikuwa jirani lakini kulikuwa na uhasama fulani kati yao. Hii ilifanya Papa kujenga ukuta mkubwa kuzunguka makazi yake ya kuishi na kanisa la St. Peters Basilica.
Kadiri miaka ilivyozidi kwenda uhasama kati ya Italy Kingdom na Papal State ulipanuka zaidi na ilifikia hatua Kingdom of Italy wakafanya uamuzi wa kuiteka Papal State na kuifanya makao makuu ya nchi yake (Rome ya sasa).
Wakati na baada ya uvamizi huu wa Kingdom of Italy kuteka Papal State, Papa mwenyewe alikuwa amejificha ndani ya makazi yake yaliyozungushiwa ukuta ambao nimeeleza awali.
Ikumbukwe kwamba hata kipindi hiki Kanisa Katoliki tayari lilikuwa na ushawishi mkubwa duniani kwa hiyo Kingdom of Italy walihofia kuingiza majeshi kwa nguvu ndani ya makazi ya Papa na kumkamata kuogopa umaarufu wao kimataifa kudondoka.
Kwa hiyo majeshi ya Kingdom of Italy yalibakia nje mwa kuta za Vatican kwa miaka mingi sana wakiamini kwamba iko siku Papa atakata tamaa na kujisalimisha.
Lakini hii haikufua dafu kwani miongo ilipita na Papa hakujisalimisha kwa kutoka nje ya kuta za Vatican. Takribani Mapapa watano kwa muda wa karibia miaka sitini waliishi ndani ya kuta za Vatican katika hali hii. Mapapa hao kwa majina yao walikuwa ni Papa Pius IX, Papa Leo XIII, Papa Pius X, Papa Benedict XV na Papa Pius XI.
Hali hii ilisababisha Mapapa kutotambua Kingdom of Italy na pia kulalamika mara kwa mara kwa jamii ya kimataifa kwamba wanaishi kama wafungwa ndani ya kuta za Vatican kutokana na ukandamizaji wa Kingdom of Italy na hofu waliyonayo kutoka nje ya kuta za Vatican.
Hii inatufikisha mpaka miaka ya 1920s wakati wa utawala wa Benito Mussolini akiwa Waziri Mkuu wa Italy.
Mussolini alichoshwa na malalamiko haya ya Papa na majibizano ya kila mara huku Papa bado akishikilia msimamo wa kutoitambua Italy
Mussolini mwanasiasa mahiri kama ajulikanavyo akaona fursa hapa ya kuandika jina lake kwenye vitabu vya historia.
Akapendekeza makubaliano maalumu kwa Papa. Kwamba atafanya yafuatayo;
1. Italy itatoa ardhi ya Vatican kwa Papa na iwe himaya/nchi iliyo chini ya utawala wa Papa.
2. Italy itatoa fedha kama fidia kwa Papa kutokana na manyanyaso ya miaka yote.
Mussolini alihitaji Papa kufanya yafuatayo;
1. Papa atambue Italy kuwa ni nchi.
2. Papa asijihusishe wala kutoa maoni yoyote kuhusu masuala ya kisiasa na vita.
Papa na Mussolini wakafikia makubaliano na mikataba ikasainiwa na hapa ndipo taifa dogo zaidi duniani likazaliwa, Vatican.
Vatican ikaanza kujiendesha kama taifa linalojitegemea kwa kuwa na sarafu yake, serikali yake, Polisi wake, jela yake (ndio kuna jela Vatican), Posta yake, Plate number zake, Passport zake na kadhalika na kadhalika.
Vatican si kama nchi nyingine duniani kwa hiyo usidhani kwamba tayari umeielewa Vatican, hicho nilichoeleza ni theluthi tu mkanganyiko wa kuielewa Vatican kama nchi… kunywa tena glass ya maji and relax!! Nitaeleza tena kidogo…
Ili kuielewa Vatican walau kiduchu kuna watu wawili tunapaswa kuwafahamu;
1. Papa
2. Mfalme wa Vatican
Na pia kuna vitu viwili vya kuvielewa;
1. The Holy See
2. Vatican City
Tuanze kimoja kimoja…
*1. Papa*
Hii sihitaji kueleza sana karibia wote tunafahamu. Lakini kwa msingi wa awali kabisa, Papa ni askofu wa Wakatoliki wote waliopo Rome/Vatican lakini kwa kuwa yeye pia ndiye kiongozi wa Wakatoliki wote duniani ndio sababu ya Uaskofu wake kuwa Papa.
*2. The Holy See*
Kabla sijaeleza chochote kuhusu Mfalme wa Vatican kwanza nieleze kuhusu The Holy See. Hili ni moja ya mambo magumu zaidi kuyaelewa kuhusu Vatican. Nitaeleza kwa lugha nyepesi na uchache ili tusipasue vichwa kwa mikanganyiko.
Kwa tafsiri nyepesi Holy See ni 'Throne' ya Papa (nakosa neno zuri la kiswahili, sipendezwi sana na tafsiri ya 'Kiti cha Enzi').
Ni kwamba, maaskofu wote ndani ya kanisa Katoliki wanakuwa na 'throne' lakini kwa kuwa 'throne' ya Papa ni maalumu (kiongozi wa Wakatoliki wote duniani) kwa hiyo throne yake inakuwa muhimu zaidi na inaitwa 'The Holy See'.
Mapapa wanabadilika lakini The Holy See iko na itaendelea kuwepo siku zote.
Yaani kwa mfano Papa anapofariki au kustaafu kama tulivyoona mwaka juzi, Makadinali wanapokusanyika Vatican kwa uhalisia wanaenda kumchagua Kadinali mwenzao ambaye atakalia 'throne' ya 'Holy See'.
Kwa 'angle' nyingine tunaweza kusema kwamba 'The Holy See' ndiyo sheria na mamlaka yote inayofanya kanisa Katoliki kuwa namna lilivyo. Pia sheria zote za kanisa Katoliki na mfumo wake unatengenezwa na The Holy See (sio Papa).
Pia tunaweza kusema kwamba Benito Mussolini alipofanya makubaliano na Vatican aliingia mkataba ule na 'The Holy See'.
Pia unaweza usiamini lakini katika nyanja za sheria za kimataifa 'The Holy See' inatambulika kama mtu/kampuni halisi ambaye amesajiliwa kisheria.
Labda nitumie lugha nyepesi zaidi ya mfano… ukitaka kuelewa The Holy See, chukulia mfano huu kwamba Holy See ni "Catholic Church Inc." alafu Papa ndiye CEO.
Nimejitahidi kueleza kwa kifupi na kwa wepesi niwezavyo, kuielewa kwa undani zaidi The Holy See labda tunapaswa kuandaa andishi maalumu mahususi kwa ajili yake tu.
*3. Mfalme wa Vatican*
Mfalme wa Vatican ni mtawala mwenye mamlaka yote juu ya nchi ya Vatican na hii inaifanya Vatican kuwa moja kati ya nchi sita pekee duniani zenye wafalme wenye mamlaka kamili (absolute monarchy). Nchi nyingine tano ni Saudi Arabia, Brunei, Oman, Qatar, Oman na Swaziland.
Hii ndio sababu kwanini Vatican hawawezi kujiunga na Umoja wa Ulaya kwa sababu EU wanakubali nchi zenye mfumo wa kidemokrasia pekee.
Japokuwa Vatican ina tawi la 'bunge' ambalo linaundwa na makadinali wa Vatican ambayo wanatunga sheria za 'nchi' lakini bado mfalme wa Vatican anauwezo wa kuveto maamuzi yoyote ambayo wamefikia.
*Swali: Kwanini hatusikii chochote kuhusu Mfalme wa Vatican??*
Ni kwa sababu Mfalme wa Vatican na Papa ni wajibu na mamlaka mbili tofauti lakini zinakaliwa na mtu mmoja, Papa wa Kanisa Katoliki.
Hii inatupa kitu kingine cha kipekee kuhusu Vatican.
Papa anachaguliwa na makadinali wenzake - Demokrasia.
Lakini Mfalme hachaguliwi.
Hii inafanya Vatican kuwa nchi pekee kwenye historia ya dunia kuwa na Mfalme mwenye mamlaka kamili ambaye si wa kurithi na anapatikana kidemokrasia (Elected non-heridetary absolute Monarchy).
Kwa hiyo Papa kulingana na muktadha na mazingira ya suala husika kuna muda anatumia mamlaka yake kama Papa na muda mwingine inampasa kutumia mamlaka yake kama Mfalme wa Vatican.
Bado kuna mkanganyiko???
Zingatia mfano huu rahisi; tuseme kwamba kuna kampuni fulani kubwa ya kimataifa inaitwa Aman Enterprises (The Holy See kwa mada yetu). Aman Enterprises wakafanikiwa kuishwishi Tanzania kuwapatia kisiwa cha Mbudya na Bold Enterprises wanakibadilisha kisiwa cha Mbudya kuwa nchi inayojitegemea, labda iitwe Aman Land (Vatican City kwa mfano wetu).
Sasa CEO wa kampuni Bwana Aman (Papa kwa mada yetu) anahamishiamanya makao makuu ya kampuni mpaka Aman Land. Kwa kuwa Aman Land sasa ni nchi, CEO wa kampuni anakuwa pia mtawala wa nchi hii, Mfalme.
.
Kwa hiyo kwa manufaa ya kampuni kutumia 'connection' zake za kimataifa kunufaisha taifa lake la Aman Land ni vyema kutumia mamlaka kama CEO wa Bold Enterprises na kuna muda akihitaji nchi yake ya Aman Land kutunga sheria na taratibu ambazo zitanufaisha kampuni izidi kushamiri ni vyema kutumia mamlaka yake kama Mfalme wa Aman Land.
Haya ndio mamlaka mawili yaliyo chini ya mtu mmoja ndani ya vatican, Papa na Mfalme wa Vatican.
Bado kuna mkanganyiko???
Kama haujaelewa sawia usihofu kwa maana bado kuna hata nchi nyingine duniani bado hawaelewi sawa sawa mfumo mzima wa Vatican.
Mfano, Umoja wa Mataifa wamekubali The Holy See (corporation) kama mwanachama wake lakini sio Vatican City nchi yenyewe.
Passports za raia wa Vatican zinatolewa na The Holy See na sio Vatican na zinakubalika kwenye nchi nyingine japokuwa The Holy See kimataifa inatambulika kisheria kama Kampuni inayojitegemea.
Na hapa tuongee kiduchu pia kuhusu raia wa Vatican. Katika nchi nyingine raia wa wanaongezeka kutokana na kuzaliana lakini hapa Vatican hakuna hilo kutokana na idadi ndogo ya wanaweka kiasi kwamba karibia ni asilimia sufuri. Namna pekee ya kuwa raia wa Vatican ni kwa kupewa uraia na Mfalme wa Vatican ili uishi Vatican kama moja wa wasaidizi wa Papa (ambaye ndiye mfalme). Kwa hiyo siku ukiacha kazi, yaani usaidizi wako kwa Papa ukifikia kikomo, Mfalme wa Vatican (ambayr ndiye Papa) anaondoa uraia wako na unarudi kwenu.
Katika muda wowote ule raia wa nchi ya Vatican wanakadiriwa kuwa jumla karibia ya 500 ambao ndio idadi ndogo zaidi ya raia kwa nchi na ndogo kushinda hata idadi ya watu wanaoishi kwenye ghorofa moja kwenye nchi nyingi.
Na raia wote hawa ni wafanyakazi wa Papa/The Holy See ambao wanapewa uraia na Mfalme (ambaye ndiye Papa) ambapo wanafanya kazi kama Makadinali, Wanadiplomasia, walinzi au kazi nyingine za kikanisa.
Kwa ufupi sana hii ndio picha halisi ya nchi ya Vatican… na hapa ndipo ambapo maisha ya kiroho ya wafuasi zaidi ya Billioni 2 yanapoendeshwa…
*VATICAN CITY...... Nchi? Mji? Serikali au Kampuni?* Nadhani moja kati ya maeneo ambayo yamekuwa tata zaidi kuyaelewa basi ni mji wa Vatican… tukiachilia mbali kuhusu utata/ugumu wa kuelewa mfumo wake wa uendeshaji na historia yake lakini swali jepesi zaidi ambalo kila mtu huwa anahisi analifahamu jawabu lake ni kuhusu utambulisho wa Vatican.!! Ni swali jepesi ambalo karibia kila mtu anadhani ana jawabu sahihi lakini uhalisia ni kwamba asilimia kubwa ya watu wana jawabu lisilo sahihi… kila mtu atakueleza kwamba Vatican ni nchi inayojitegemea lakini hii ni robo tu au thelethi ya jawabu… Leo nami niandike kidogo kuhusu eneo hili… na kwenye andishi hili fupi nitaeleza utambulisho wa Vatican ukoje kwa usahihi wake kabisa! *Muhimu:* andishi hili halilengi kukosoa au kupinga imani ya mtu yeyote. Tahadhali zote zinazingatiwa ili kulinda heshima ya imani ya kila mtu. Tuendelee… Vatican City, ndio makao makuu ya Kanisa Katoliki na nyumba ya maisha ya Papa, kiongozi mkuu wa kanisa Katoliki. Vatican ndio nchi ndogo zaidi duniani kiasi kwamba unaweza kuizunguka yote kwa mzingo (circumference) kwa muda wa dakika arobaini tu kwa kutembea kwa miguu. Ni ajabu sana kwa namna gani nchi ndogo kiasi hiki imetokea na je ni nchi kama nchi nyingine??? Jibu la swali hili ni refu sana kiaisi kwamba unaweza hata kusoma darasani kwa mwaka mzima lakini nitajaribu kuweka katika maneno machache sana ya kueleweka kwa wepesi… Miaka ya kale sana Papa wa Kanisa Katoliki alikuwa ni mtawala wa nchi ambayo ilikuwa inajiita *Himaya ya Papa (Papal State)* ambayo inarandana kabisa na eneo la sasa la nchi nzima ya Italia. Hii ilikuwa takribani miaka ya 754 mpaka miaka ya 1870. Ni katika kipindi hiki ambacho Papa aliteua eneo ndani ya nchi yake Papal State ambalo likajengwa *St. Peters Basilica*, kanisa kubwa zaidi duniani na lenye nakshi adhimu zaidi. Eneo hili ambalo St. Peters Basilica ilijengwa ni eneo fulani hivi la muinuko ambako hapo hapo pia yalijengwa makazi ya Papa kuishi. Ikumbukwe kwamba katika kipindi hiki hiki cha uwepo wa himaya ya Papal State pia ilikuwa inapakana na Ufalme wa Italy (Kingdom of Italy) japo kila moja ilikuwa inajitegemea. Japokuwa himaya hizi mbili zilikuwa jirani lakini kulikuwa na uhasama fulani kati yao. Hii ilifanya Papa kujenga ukuta mkubwa kuzunguka makazi yake ya kuishi na kanisa la St. Peters Basilica. Kadiri miaka ilivyozidi kwenda uhasama kati ya Italy Kingdom na Papal State ulipanuka zaidi na ilifikia hatua Kingdom of Italy wakafanya uamuzi wa kuiteka Papal State na kuifanya makao makuu ya nchi yake (Rome ya sasa). Wakati na baada ya uvamizi huu wa Kingdom of Italy kuteka Papal State, Papa mwenyewe alikuwa amejificha ndani ya makazi yake yaliyozungushiwa ukuta ambao nimeeleza awali. Ikumbukwe kwamba hata kipindi hiki Kanisa Katoliki tayari lilikuwa na ushawishi mkubwa duniani kwa hiyo Kingdom of Italy walihofia kuingiza majeshi kwa nguvu ndani ya makazi ya Papa na kumkamata kuogopa umaarufu wao kimataifa kudondoka. Kwa hiyo majeshi ya Kingdom of Italy yalibakia nje mwa kuta za Vatican kwa miaka mingi sana wakiamini kwamba iko siku Papa atakata tamaa na kujisalimisha. Lakini hii haikufua dafu kwani miongo ilipita na Papa hakujisalimisha kwa kutoka nje ya kuta za Vatican. Takribani Mapapa watano kwa muda wa karibia miaka sitini waliishi ndani ya kuta za Vatican katika hali hii. Mapapa hao kwa majina yao walikuwa ni Papa Pius IX, Papa Leo XIII, Papa Pius X, Papa Benedict XV na Papa Pius XI. Hali hii ilisababisha Mapapa kutotambua Kingdom of Italy na pia kulalamika mara kwa mara kwa jamii ya kimataifa kwamba wanaishi kama wafungwa ndani ya kuta za Vatican kutokana na ukandamizaji wa Kingdom of Italy na hofu waliyonayo kutoka nje ya kuta za Vatican. Hii inatufikisha mpaka miaka ya 1920s wakati wa utawala wa Benito Mussolini akiwa Waziri Mkuu wa Italy. Mussolini alichoshwa na malalamiko haya ya Papa na majibizano ya kila mara huku Papa bado akishikilia msimamo wa kutoitambua Italy Mussolini mwanasiasa mahiri kama ajulikanavyo akaona fursa hapa ya kuandika jina lake kwenye vitabu vya historia. Akapendekeza makubaliano maalumu kwa Papa. Kwamba atafanya yafuatayo; 1. Italy itatoa ardhi ya Vatican kwa Papa na iwe himaya/nchi iliyo chini ya utawala wa Papa. 2. Italy itatoa fedha kama fidia kwa Papa kutokana na manyanyaso ya miaka yote. Mussolini alihitaji Papa kufanya yafuatayo; 1. Papa atambue Italy kuwa ni nchi. 2. Papa asijihusishe wala kutoa maoni yoyote kuhusu masuala ya kisiasa na vita. Papa na Mussolini wakafikia makubaliano na mikataba ikasainiwa na hapa ndipo taifa dogo zaidi duniani likazaliwa, Vatican. Vatican ikaanza kujiendesha kama taifa linalojitegemea kwa kuwa na sarafu yake, serikali yake, Polisi wake, jela yake (ndio kuna jela Vatican), Posta yake, Plate number zake, Passport zake na kadhalika na kadhalika. Vatican si kama nchi nyingine duniani kwa hiyo usidhani kwamba tayari umeielewa Vatican, hicho nilichoeleza ni theluthi tu mkanganyiko wa kuielewa Vatican kama nchi… kunywa tena glass ya maji and relax!! Nitaeleza tena kidogo… Ili kuielewa Vatican walau kiduchu kuna watu wawili tunapaswa kuwafahamu; 1. Papa 2. Mfalme wa Vatican Na pia kuna vitu viwili vya kuvielewa; 1. The Holy See 2. Vatican City Tuanze kimoja kimoja… *1. Papa* Hii sihitaji kueleza sana karibia wote tunafahamu. Lakini kwa msingi wa awali kabisa, Papa ni askofu wa Wakatoliki wote waliopo Rome/Vatican lakini kwa kuwa yeye pia ndiye kiongozi wa Wakatoliki wote duniani ndio sababu ya Uaskofu wake kuwa Papa. *2. The Holy See* Kabla sijaeleza chochote kuhusu Mfalme wa Vatican kwanza nieleze kuhusu The Holy See. Hili ni moja ya mambo magumu zaidi kuyaelewa kuhusu Vatican. Nitaeleza kwa lugha nyepesi na uchache ili tusipasue vichwa kwa mikanganyiko. Kwa tafsiri nyepesi Holy See ni 'Throne' ya Papa (nakosa neno zuri la kiswahili, sipendezwi sana na tafsiri ya 'Kiti cha Enzi'). Ni kwamba, maaskofu wote ndani ya kanisa Katoliki wanakuwa na 'throne' lakini kwa kuwa 'throne' ya Papa ni maalumu (kiongozi wa Wakatoliki wote duniani) kwa hiyo throne yake inakuwa muhimu zaidi na inaitwa 'The Holy See'. Mapapa wanabadilika lakini The Holy See iko na itaendelea kuwepo siku zote. Yaani kwa mfano Papa anapofariki au kustaafu kama tulivyoona mwaka juzi, Makadinali wanapokusanyika Vatican kwa uhalisia wanaenda kumchagua Kadinali mwenzao ambaye atakalia 'throne' ya 'Holy See'. Kwa 'angle' nyingine tunaweza kusema kwamba 'The Holy See' ndiyo sheria na mamlaka yote inayofanya kanisa Katoliki kuwa namna lilivyo. Pia sheria zote za kanisa Katoliki na mfumo wake unatengenezwa na The Holy See (sio Papa). Pia tunaweza kusema kwamba Benito Mussolini alipofanya makubaliano na Vatican aliingia mkataba ule na 'The Holy See'. Pia unaweza usiamini lakini katika nyanja za sheria za kimataifa 'The Holy See' inatambulika kama mtu/kampuni halisi ambaye amesajiliwa kisheria. Labda nitumie lugha nyepesi zaidi ya mfano… ukitaka kuelewa The Holy See, chukulia mfano huu kwamba Holy See ni "Catholic Church Inc." alafu Papa ndiye CEO. Nimejitahidi kueleza kwa kifupi na kwa wepesi niwezavyo, kuielewa kwa undani zaidi The Holy See labda tunapaswa kuandaa andishi maalumu mahususi kwa ajili yake tu. *3. Mfalme wa Vatican* Mfalme wa Vatican ni mtawala mwenye mamlaka yote juu ya nchi ya Vatican na hii inaifanya Vatican kuwa moja kati ya nchi sita pekee duniani zenye wafalme wenye mamlaka kamili (absolute monarchy). Nchi nyingine tano ni Saudi Arabia, Brunei, Oman, Qatar, Oman na Swaziland. Hii ndio sababu kwanini Vatican hawawezi kujiunga na Umoja wa Ulaya kwa sababu EU wanakubali nchi zenye mfumo wa kidemokrasia pekee. Japokuwa Vatican ina tawi la 'bunge' ambalo linaundwa na makadinali wa Vatican ambayo wanatunga sheria za 'nchi' lakini bado mfalme wa Vatican anauwezo wa kuveto maamuzi yoyote ambayo wamefikia. *Swali: Kwanini hatusikii chochote kuhusu Mfalme wa Vatican??* Ni kwa sababu Mfalme wa Vatican na Papa ni wajibu na mamlaka mbili tofauti lakini zinakaliwa na mtu mmoja, Papa wa Kanisa Katoliki. Hii inatupa kitu kingine cha kipekee kuhusu Vatican. Papa anachaguliwa na makadinali wenzake - Demokrasia. Lakini Mfalme hachaguliwi. Hii inafanya Vatican kuwa nchi pekee kwenye historia ya dunia kuwa na Mfalme mwenye mamlaka kamili ambaye si wa kurithi na anapatikana kidemokrasia (Elected non-heridetary absolute Monarchy). Kwa hiyo Papa kulingana na muktadha na mazingira ya suala husika kuna muda anatumia mamlaka yake kama Papa na muda mwingine inampasa kutumia mamlaka yake kama Mfalme wa Vatican. Bado kuna mkanganyiko??? Zingatia mfano huu rahisi; tuseme kwamba kuna kampuni fulani kubwa ya kimataifa inaitwa Aman Enterprises (The Holy See kwa mada yetu). Aman Enterprises wakafanikiwa kuishwishi Tanzania kuwapatia kisiwa cha Mbudya na Bold Enterprises wanakibadilisha kisiwa cha Mbudya kuwa nchi inayojitegemea, labda iitwe Aman Land (Vatican City kwa mfano wetu). Sasa CEO wa kampuni Bwana Aman (Papa kwa mada yetu) anahamishiamanya makao makuu ya kampuni mpaka Aman Land. Kwa kuwa Aman Land sasa ni nchi, CEO wa kampuni anakuwa pia mtawala wa nchi hii, Mfalme. . Kwa hiyo kwa manufaa ya kampuni kutumia 'connection' zake za kimataifa kunufaisha taifa lake la Aman Land ni vyema kutumia mamlaka kama CEO wa Bold Enterprises na kuna muda akihitaji nchi yake ya Aman Land kutunga sheria na taratibu ambazo zitanufaisha kampuni izidi kushamiri ni vyema kutumia mamlaka yake kama Mfalme wa Aman Land. Haya ndio mamlaka mawili yaliyo chini ya mtu mmoja ndani ya vatican, Papa na Mfalme wa Vatican. Bado kuna mkanganyiko??? Kama haujaelewa sawia usihofu kwa maana bado kuna hata nchi nyingine duniani bado hawaelewi sawa sawa mfumo mzima wa Vatican. Mfano, Umoja wa Mataifa wamekubali The Holy See (corporation) kama mwanachama wake lakini sio Vatican City nchi yenyewe. Passports za raia wa Vatican zinatolewa na The Holy See na sio Vatican na zinakubalika kwenye nchi nyingine japokuwa The Holy See kimataifa inatambulika kisheria kama Kampuni inayojitegemea. Na hapa tuongee kiduchu pia kuhusu raia wa Vatican. Katika nchi nyingine raia wa wanaongezeka kutokana na kuzaliana lakini hapa Vatican hakuna hilo kutokana na idadi ndogo ya wanaweka kiasi kwamba karibia ni asilimia sufuri. Namna pekee ya kuwa raia wa Vatican ni kwa kupewa uraia na Mfalme wa Vatican ili uishi Vatican kama moja wa wasaidizi wa Papa (ambaye ndiye mfalme). Kwa hiyo siku ukiacha kazi, yaani usaidizi wako kwa Papa ukifikia kikomo, Mfalme wa Vatican (ambayr ndiye Papa) anaondoa uraia wako na unarudi kwenu. Katika muda wowote ule raia wa nchi ya Vatican wanakadiriwa kuwa jumla karibia ya 500 ambao ndio idadi ndogo zaidi ya raia kwa nchi na ndogo kushinda hata idadi ya watu wanaoishi kwenye ghorofa moja kwenye nchi nyingi. Na raia wote hawa ni wafanyakazi wa Papa/The Holy See ambao wanapewa uraia na Mfalme (ambaye ndiye Papa) ambapo wanafanya kazi kama Makadinali, Wanadiplomasia, walinzi au kazi nyingine za kikanisa. Kwa ufupi sana hii ndio picha halisi ya nchi ya Vatican… na hapa ndipo ambapo maisha ya kiroho ya wafuasi zaidi ya Billioni 2 yanapoendeshwa… -
Cassowary anaitwa ,Ni jamii ya Ndege wanaopatikana Australia, ni ndege hatari zaidi Duniani ,muone hapo kama mzembe mzembe tu,
Sifa za huyu ndege yeye akihisi hatari yaani akikuhisi unataka kumuua, anaruka juu anakuvamia na shambulio lake ni kama umepigwa na silaha hizi za kisasa kama AK47 na majeraha yake lazima ufe , yeye anapokuvamia huvaa mask anayo yake ya asili , Kifupi huyu ndege huitwa Muuaji wa watu.
Mbaya kuliko zote huyu nyama yake utachemsha mawe yakaiva nyama ya huyu bado haijaiva..
ShareCassowary anaitwa ,Ni jamii ya Ndege wanaopatikana Australia, ni ndege hatari zaidi Duniani ,muone hapo kama mzembe mzembe tu, Sifa za huyu ndege yeye akihisi hatari yaani akikuhisi unataka kumuua, anaruka juu anakuvamia na shambulio lake ni kama umepigwa na silaha hizi za kisasa kama AK47 na majeraha yake lazima ufe , yeye anapokuvamia huvaa mask anayo yake ya asili , Kifupi huyu ndege huitwa Muuaji wa watu. Mbaya kuliko zote huyu nyama yake utachemsha mawe yakaiva nyama ya huyu bado haijaiva.. Share -
Watu watano wameripotiwa kufariki kutokana na hali ya hewa ya baridi ambayo imesababisha theluji na baridi kali katika sehemu kubwa ya Marekani.
Polisi wanaoshika doria katika barabara kuu ya Jimbo la Missouri wamethibitisha ajali 350 za barabarani, ambapo watu wawili walifariki mjini Kansas kutokana na hali mbaya ya hewa, na mwingine huko Virginia.
#neliudcosiah
Watu watano wameripotiwa kufariki kutokana na hali ya hewa ya baridi ambayo imesababisha theluji na baridi kali katika sehemu kubwa ya Marekani. Polisi wanaoshika doria katika barabara kuu ya Jimbo la Missouri wamethibitisha ajali 350 za barabarani, ambapo watu wawili walifariki mjini Kansas kutokana na hali mbaya ya hewa, na mwingine huko Virginia. #neliudcosiah0 Comments ·0 Shares ·164 Views -
. CAF AWARDS LIVE UPDATES
[12/16, 20:39]
*YOUNG PLAYER OF THE YEAR (WOMEN)* :
Doha El Madani (Morocco / AS FAR)
[12/16, 20:40]
*YOUNG PLAYER OF THE YEAR (MEN)* :
Lamine Camara (Senegal / AS Monaco)
[12/16, 20:40] *NATIONAL TEAM OF THE YEAR (WOMEN)* :
Nigeria
*NATIONAL TEAM OF THE YEAR (MEN)* :
Ivory Coast
[12/16, 21:11]
*CLUB OF THE YEAR (MEN)* :
Al Ahly (Egypt)
[12/16, 21:12]
*CLUB OF THE YEAR (WOMEN)* :
TP Mazembe (DR Congo)
[12/16, 21:12] *INTERCLUB PLAYER OF THE YEAR (MEN)*
Ronwen Williams (South Africa / Mamelodi Sundowns)
[12/16, 21:13]
*INTERCLUB PLAYER OF THE YEAR (WOMEN)*
Sanaâ Mssoudy (Morocco / AS FAR)
[12/16, 21:15]
*GOALKEEPER OF THE YEAR (WOMEN)*
Chiamaka Nnadozie (Nigeria / Paris FC)
[12/16, 21:28]
*GOALKEEPER OF THE YEAR (MEN)*
Ronwen Williams (South Africa / Mamelodi Sundowns).🌟 CAF AWARDS LIVE UPDATES 🌟 [12/16, 20:39] *YOUNG PLAYER OF THE YEAR (WOMEN)* : Doha El Madani (Morocco / AS FAR) [12/16, 20:40] *YOUNG PLAYER OF THE YEAR (MEN)* : Lamine Camara (Senegal / AS Monaco) [12/16, 20:40] *NATIONAL TEAM OF THE YEAR (WOMEN)* : Nigeria *NATIONAL TEAM OF THE YEAR (MEN)* : Ivory Coast [12/16, 21:11] *CLUB OF THE YEAR (MEN)* : Al Ahly (Egypt) [12/16, 21:12] *CLUB OF THE YEAR (WOMEN)* : TP Mazembe (DR Congo) [12/16, 21:12] *INTERCLUB PLAYER OF THE YEAR (MEN)* Ronwen Williams (South Africa / Mamelodi Sundowns) [12/16, 21:13] *INTERCLUB PLAYER OF THE YEAR (WOMEN)* Sanaâ Mssoudy (Morocco / AS FAR) [12/16, 21:15] *GOALKEEPER OF THE YEAR (WOMEN)* Chiamaka Nnadozie (Nigeria / Paris FC) [12/16, 21:28] *GOALKEEPER OF THE YEAR (MEN)* Ronwen Williams (South Africa / Mamelodi Sundowns) -
.TRANSFER NEWS
Yanga yarudi tena DR Congo sasa ni zamu ya winga hatari JONATHAN LOMBO.
Winga wa kulia wa AS Vita Jonathan Ikangalombo Kapela yupo katika hatua za mwisho za kujiunga na yanga sc
kwenye dirisha dogo la usajili na tayari viongozi wa yanga sc wapo DR Congo na wanaendelea na
mazungumzo ambayo yanakwenda vizuri hadi sasa.
Winga huyu msumbufu na hatari mwenye umri wa miaka 22 alisajiliwa na As Vita club mwaka 2023
akitokea DC Motema Pembe na sasa akiwa chini ya Kocha wa Zaman wa Azam fc Youssouph Dabo amekuwa na
kiwango kizuri huku akishinda tuzo ya mchezaji bora wa mechi mwaka huu kwenye Derby baina ya As Vita club Vs
Dc Motema Pembe
Yanga imeamua kurudia asili yake ya kutumia mawinga kama ilivyo kuwa tamaduni yao huku kukiwa na
mahusiano mazuri na As Vita Club ambapo yanga iliwahi kuwasajili Ducapel Moloko 2021-22,Djuma shabani na winga Tuisila Kisinda
msimu wa 2020-21 hivyo kwa sasa ni dhahiri shahiri Jonathan Lombo anakwenda kuwa mchezaji wa yanga huku akiwa
na kasi na mnyumbulifu sana.
Utambulisho wake ni suala la Muda tu dirisha dogo litakapo funguliwa mapema..🚨TRANSFER NEWS Yanga yarudi tena DR Congo sasa ni zamu ya winga hatari JONATHAN LOMBO. Winga wa kulia wa AS Vita Jonathan Ikangalombo Kapela yupo katika hatua za mwisho za kujiunga na yanga sc kwenye dirisha dogo la usajili na tayari viongozi wa yanga sc wapo DR Congo na wanaendelea na mazungumzo ambayo yanakwenda vizuri hadi sasa. Winga huyu msumbufu na hatari mwenye umri wa miaka 22 alisajiliwa na As Vita club mwaka 2023 akitokea DC Motema Pembe na sasa akiwa chini ya Kocha wa Zaman wa Azam fc Youssouph Dabo amekuwa na kiwango kizuri huku akishinda tuzo ya mchezaji bora wa mechi mwaka huu kwenye Derby baina ya As Vita club Vs Dc Motema Pembe Yanga imeamua kurudia asili yake ya kutumia mawinga kama ilivyo kuwa tamaduni yao huku kukiwa na mahusiano mazuri na As Vita Club ambapo yanga iliwahi kuwasajili Ducapel Moloko 2021-22,Djuma shabani na winga Tuisila Kisinda msimu wa 2020-21 hivyo kwa sasa ni dhahiri shahiri Jonathan Lombo anakwenda kuwa mchezaji wa yanga huku akiwa na kasi na mnyumbulifu sana. Utambulisho wake ni suala la Muda tu dirisha dogo litakapo funguliwa mapema. -
Katika historia ya Muziki wa Bongo fleva, maisha ya Diamond Platinumz, Rich Mavoco na Harmonize matukio ya wasanii hawa kufanya kazi pamoja na kutengeneza moments zilizowaaminisha wananchi kwamba ushirikiano wao utadumu muda mrefu alafu wakapishana ghafla na kupelekana hadi Basata aisee ni katika mambo yaliotengeneza pressure kubwa baina yao na hata mitaani.
Maranyingi nimekua nikimtaja Harmonize kama msanii aliotoka WCB na kufanikiwa kutengeneza mianya mingi ya biashara na mafanikio nje ya WCB tofauti na ilivyokua ikizungumzwa na wengi.
Rich Mavoco nimemvulia kofia kwa sababu ni ngumu sana msanii kupitia mapito yake alafu akafanikiwa kurudi kwenye game na kua na nguvu kama ambayo anayo lakini umewahi kufikiria upande wa Diamond Platinumz ambae ali invest kuwapa thamani zaidi wasanii hawa na baadae akawapoteza katika mazingira ambayo naamini kabisa hata yeye hakua tayari.
Kuna tetesi kwamba Harmonize alikua na migogoro na Sallam SK kabla hajaondoka WCB na CEO alijikuta kaekwa kwenye kona ambayo ilimlazimu afanye maamuzi magumu la sivyo mambo yangezidi kuharibika. Nimeshuhudia wasanii wengi wakiua lebo zao kutokana na migogoro kama hio lakini pia wadau wengi wameachana na biashara ya muziki kutokana na sintofahamu nyingi zilizopo ndani ya Game.
Upande wa Diamond Platinumz ni tofauti kidogo, pamoja na drama zote anazopitia bado lebo yake ipo imara na wasanii waliobaki kama Mbosso, Zuchu, Lavalava na D Voice wanafanya vizuri kila mtu kwa nafasi yake.
Kwa kijana kutoka Tandale kuana uvumilivu, mbinu na mipango ya kukabiliana na changamoto zote alizokumbana nazo Diamond Platinumz anastahili pongezi maana inaonesha ukomavu wake na weledi mkubwa alionao kwenye field anayojihusisha nayo.
(Jr Junior)
Katika historia ya Muziki wa Bongo fleva, maisha ya Diamond Platinumz, Rich Mavoco na Harmonize matukio ya wasanii hawa kufanya kazi pamoja na kutengeneza moments zilizowaaminisha wananchi kwamba ushirikiano wao utadumu muda mrefu alafu wakapishana ghafla na kupelekana hadi Basata aisee ni katika mambo yaliotengeneza pressure kubwa baina yao na hata mitaani. Maranyingi nimekua nikimtaja Harmonize kama msanii aliotoka WCB na kufanikiwa kutengeneza mianya mingi ya biashara na mafanikio nje ya WCB tofauti na ilivyokua ikizungumzwa na wengi. Rich Mavoco nimemvulia kofia kwa sababu ni ngumu sana msanii kupitia mapito yake alafu akafanikiwa kurudi kwenye game na kua na nguvu kama ambayo anayo lakini umewahi kufikiria upande wa Diamond Platinumz ambae ali invest kuwapa thamani zaidi wasanii hawa na baadae akawapoteza katika mazingira ambayo naamini kabisa hata yeye hakua tayari. Kuna tetesi kwamba Harmonize alikua na migogoro na Sallam SK kabla hajaondoka WCB na CEO alijikuta kaekwa kwenye kona ambayo ilimlazimu afanye maamuzi magumu la sivyo mambo yangezidi kuharibika. Nimeshuhudia wasanii wengi wakiua lebo zao kutokana na migogoro kama hio lakini pia wadau wengi wameachana na biashara ya muziki kutokana na sintofahamu nyingi zilizopo ndani ya Game. Upande wa Diamond Platinumz ni tofauti kidogo, pamoja na drama zote anazopitia bado lebo yake ipo imara na wasanii waliobaki kama Mbosso, Zuchu, Lavalava na D Voice wanafanya vizuri kila mtu kwa nafasi yake. Kwa kijana kutoka Tandale kuana uvumilivu, mbinu na mipango ya kukabiliana na changamoto zote alizokumbana nazo Diamond Platinumz anastahili pongezi maana inaonesha ukomavu wake na weledi mkubwa alionao kwenye field anayojihusisha nayo. (Jr Junior) -
TUTAREJEA KATIKA UIMARA WETU, NIAMINI - PACOME
Mchezaji wa Yanga @pacom_zouzoua kupitia ukurasa wake wa Instagram ameandika
"Habari za jioni, hivi karibuni klabu yetu imekuwa katika nyakati ngumu kwa kufungwa mfululizo, lakini niwahakikishie kuwa msimu ni mrefu sana na lazima tujifunze kutokana na vipigo vyetu ili tuweze kurejea Imara , si rahisi kwa shabiki kuuona timu yake aipendayo inafungwa kwa mara kwa mara hili tunalifahamu kwa sababu hatujawazoesha wapendwa Wananchi,
lakini nawaahidi kuwa tutapambana kwelikweli, tutapambana kama msimu uliopita ili kurudisha heshima ya klabu bora nchini... sisi tutarejea katika muda uliopangwa ujao, niamini.
Tunashindwa pamoja na tunashinda pamoja.
Asanteni wapendwa Wananchi
Profesa"
Kwa lugha ya Kingereza
Good evening everyone, lately, the club has been going through difficult times with successive defeats, but I assure you that the season is very long and we must learn from our defeats to bounce back, it is not easy for a supporter to see his favorite team chain defeats after defeats, we are aware of this because we have not accustomed you to this dear Citizens, but I promise you that we will really fight, fight like last season to restore the reputation of the best club in the country ... we will bounce back in the upcoming deadlines, believe me.
We lose together and we win together.
Thank you dear Wananchi
The professorTUTAREJEA KATIKA UIMARA WETU, NIAMINI - PACOME Mchezaji wa Yanga @pacom_zouzoua kupitia ukurasa wake wa Instagram ameandika "Habari za jioni, hivi karibuni klabu yetu imekuwa katika nyakati ngumu kwa kufungwa mfululizo, lakini niwahakikishie kuwa msimu ni mrefu sana na lazima tujifunze kutokana na vipigo vyetu ili tuweze kurejea Imara , si rahisi kwa shabiki kuuona timu yake aipendayo inafungwa kwa mara kwa mara hili tunalifahamu kwa sababu hatujawazoesha wapendwa Wananchi, lakini nawaahidi kuwa tutapambana kwelikweli, tutapambana kama msimu uliopita ili kurudisha heshima ya klabu bora nchini... sisi tutarejea katika muda uliopangwa ujao, niamini. Tunashindwa pamoja na tunashinda pamoja. Asanteni wapendwa Wananchi 💚💛 Profesa✅" Kwa lugha ya Kingereza Good evening everyone, lately, the club has been going through difficult times with successive defeats, but I assure you that the season is very long and we must learn from our defeats to bounce back, it is not easy for a supporter to see his favorite team chain defeats after defeats, we are aware of this because we have not accustomed you to this dear Citizens, but I promise you that we will really fight, fight like last season to restore the reputation of the best club in the country ... we will bounce back in the upcoming deadlines, believe me. We lose together and we win together. Thank you dear Wananchi 💚💛 The professor✅ -
Uswahilini sijui usingizi unapata saa ngapi*
Ukisema ulale sa 5 usiku.. saa 6 unaamshwa na story za sungusungu dirishani.
Kausingizi kanakuja
Saa nane unaamshwa na kelele za mwizi huyoo
Saa kumi-kumi hivi alfajiri tena kausingizi kanakuja..ghafla Saa 12 unaamshwa na muuza bagia vitumbua..
Ukasema labda saa tanotano asubuhi ujipumzishe baada ya kupata chai, ghafla muuza mboga mchicha chinese spinachi majan ya kunde huyooo!!
Kwa hasira unaamka unasema utalala saa tisa alasiri..
Saa 9 tena ...Utasikia machumachuma tunanunua friji mbovu compressor mbovu tunanunua
.. Huyo kapita.
Ile usingizi unakujakuja jitu na spika lake " tunasajili laini za chuo bure kwa alama za vidole...
Kwa hasira unaenda zako kukaa nje upunge upepo, unashangaa madogo na jezi zao..kaka shkamoo kesho tuna mechi tunaomba mchango...Uswahilini sijui usingizi unapata saa ngapi🤔* Ukisema ulale sa 5 usiku.. saa 6 unaamshwa na story za sungusungu dirishani. Kausingizi kanakuja Saa nane unaamshwa na kelele za mwizi huyoo Saa kumi-kumi hivi alfajiri tena kausingizi kanakuja..ghafla Saa 12 unaamshwa na muuza bagia vitumbua..😇😇😀 Ukasema labda saa tanotano asubuhi ujipumzishe baada ya kupata chai, ghafla muuza mboga mchicha chinese spinachi majan ya kunde huyooo!!😅 Kwa hasira unaamka unasema utalala saa tisa alasiri.. Saa 9 tena ...Utasikia machumachuma tunanunua friji mbovu compressor mbovu tunanunua😆😆 .. Huyo kapita. Ile usingizi unakujakuja jitu na spika lake " tunasajili laini za chuo bure kwa alama za vidole... Kwa hasira unaenda zako kukaa nje upunge upepo, unashangaa madogo na jezi zao..kaka shkamoo kesho tuna mechi tunaomba mchango😁😁😁... -
mbosso haingia kikaangoni baada ya kutumia Neno bomboclaaat Kwenye Verse ya Wimbo tunapendana aliyo Shirikishwa na dvoice
Na BOmboclaaat Inatumiwa Sana Na Msanii Harmonize Nchini Tanzania
J kaiga ama Verse Yake Ndo Imemupeleka uko ? David Attombosso haingia kikaangoni baada ya kutumia Neno bomboclaaat Kwenye Verse ya Wimbo tunapendana aliyo Shirikishwa na dvoice Na BOmboclaaat Inatumiwa Sana Na Msanii Harmonize Nchini Tanzania J kaiga ama Verse Yake Ndo Imemupeleka uko ? [Mefa]0 Comments ·0 Shares ·275 Views -
PROFESSOR NA WASHIKAJI ZAKE
Professor wa kitaa nakwambia utofauti mkubwa kati ya Mwanamke na Mwanaume .
MWANAMKE
-Akishindwa na maisha basi atatafuta Mwanaume wa kumuingiza kwenye mtego wa Ndoa ili apate ahueni ya maisha.
-Ataingia kwenye Ndoa sio kwa ajili ya kujenga familia ijapokuwa ni akae mbali na masumbuko ya maisha . Haitokuwepo amani kwenye Ndoa yako ukioa Mwanamke wa aina hii.
MWANAUME
-Maisha yakimshinda Mwanaume yoyote ile basi kuna machaguo mawili ambayo ni
1. Ajitoe nafsi mwenyewe na kwenda kupokea adhabu kwa Mungu ya kujiondoa uhai kabla ya muda au
2 Ajifute vumbi na maumivu yote na aendelee kupambana .
Hauna sehemu ya kulia wala kutoa malalamiko sababu wewe ndiye Mjomba, Shangazi ,Mama na Baba wa kujipa mtaji .
Endelea kwenda sababu machaguo yako pindi Maisha yakikushinda ni magumu mnoo lakini usisahau na usiku huu nakukumbusha kwamba unamachaguo mawili tu.PROFESSOR NA WASHIKAJI ZAKE ✍️ Professor wa kitaa nakwambia utofauti mkubwa kati ya Mwanamke na Mwanaume . MWANAMKE -Akishindwa na maisha basi atatafuta Mwanaume wa kumuingiza kwenye mtego wa Ndoa ili apate ahueni ya maisha. -Ataingia kwenye Ndoa sio kwa ajili ya kujenga familia ijapokuwa ni akae mbali na masumbuko ya maisha . Haitokuwepo amani kwenye Ndoa yako ukioa Mwanamke wa aina hii. MWANAUME -Maisha yakimshinda Mwanaume yoyote ile basi kuna machaguo mawili ambayo ni 1. Ajitoe nafsi mwenyewe na kwenda kupokea adhabu kwa Mungu ya kujiondoa uhai kabla ya muda au 2 Ajifute vumbi na maumivu yote na aendelee kupambana . Hauna sehemu ya kulia wala kutoa malalamiko sababu wewe ndiye Mjomba, Shangazi ,Mama na Baba wa kujipa mtaji . Endelea kwenda sababu machaguo yako pindi Maisha yakikushinda ni magumu mnoo lakini usisahau na usiku huu nakukumbusha kwamba unamachaguo mawili tu. -
MSIMAMO KWENYE RANK ZA CAF
Baada ya timu za Yanga na Simba kufanikiwa kufuzu makundi ya CAF kama nchi (Tanzania) tumeongeza pointi 7.5 (Yanga pointi 5, Simba Pointi 2.5) na kufikisha pointi 60 nafasi ya sita kwenye Association Ranking na tumezidiwa na mataifa matano (Misri-135.5, Morocco-104.5, Algeria-95, Afrika Kusini-83.5, Tunisia-72.5).
Nafasi ya 7 wapo DR Congo na Angola wakiwa na pointi 45 kila mmoja huku anayeshika nafasi ya 13 ana pointi 18.5 hivyo tuna misimu 2 hadi 3 mbele ya kupeleka timu 4 kwenye mashindano ya CAF (2 klabu bingwa Afrika na 2 kombe la shirikisho) hata timu zetu hazitafanya vizuri kwa kufika makundi ya kombe la shirikisho au klabu bingwa.
Kwenye Club Ranking mpaka sasa timu ya Simba ipo nafasi ya saba ikiwa na pointi 30.5 na Yanga ipo nafasi ya 11 ikiwa na pointi 29 kama nchi tuna pointi 60 (Simba 30.5, Yanga 29, Namungo 0.5) wanaongoza ni 1-Ahly-63, 2-Esperance-47, 3-Mamelodi-42, 4-Wydad-39, 5-Zamalek-34.5, 6-Belouizadad-31, 7-Mazembe & Simba 30.5, 9-Berkane & USM Alger-29.5, 11-Yanga 29.
Kwenye hizo timu 11 za juu timu moja tu ya Wydad ndio haipo kwenye mashindano zingine zote zipo kwenye hatua ya makundi ikiwa Ahly, Esperance, Mamelodi, Belouizdad, Mazembe na Yanga zipo makundi ya klabu bingwa Afrika huku Zamalek, Simba, Berkane na USM Alger zipo makundi ya kombe la shirikisho.
Timu ambazo zipo makundi zinaweza kuongeza pointi kulingana na performance yao kwa msimu huu kulingana na nafasi ambayo wataishia. Pointi huwa zinapatikana kama ifuatavyo kila pointi unayoipata kila msimu kulingana na nafasi uliyoishia unazidisha na coefficient code ya msimu husika
Zifuatavyo ni code kwa msimu mitano inayopigiwa hesabu kutafuta pointi 2024/25=5 2023/24=4 2022/23=3 2021/22=2 2020/21=1
Pointi zinapatikana kama ifuatavyo >Kwenye klabu bingwa Afrika (CAF Champion League) Bingwa=6 Mshindi wa pili = 5 Nusu fainali =4 Robo fainali =3 Nafasi 3 kwenye kundi = 2 Nafasi ya 4 kwenye kundi =1
Kwenye kombe la shirikisho (CAF Confederation Cup) Bingwa=5 Mshindi wa pili = 4 Nusu fainali =3 Robo fainali =2 Nafasi 3 kwenye kundi = 1 Nafasi ya 4 kwenye kundi =0.5
Pointi zinapatikana kwa kuchukua pointi ya nafasi uliyoishia unazidisha na coefficient code ya msimu husika
Simba ina pointi 30.5 ikiwa 2024/25 Makundi (Shirikisho) 0.5×5 = 2.5 2023/24 Robo (Klabu Bingwa) 3×4 = 12 2022/23 Robo (Klabu Bingwa) 3×3 = 9 2021/22 Robo (Shirikisho) 2×2= 4 2020/21 Robo (Klabu Bingwa) 3×1 = 3 Chukua 3+4+9+12+2.5 = 30.5
Yanga ina pointi 29 ikiwa 2024/25 Makundi (Klabu Bingwa) 1×5 = 5 2023/24 Robo (Klabu Bingwa) 3×4 = 12 2022/23 Mshindi 2(Shirikisho) 4×3 = 12 2021/22 Haikufuzu Makundi = 0 2020/21 Haikufuzu Makundi = 0 Chukua 0+0+12+12+5 = 29
Rejea kwenye aya ya kwanza huko juu nilisema Yanga imetengeneza pointi 5 huku Simba imetengeneza pointi 2.5 msimu huu kwa kufanikiwa kufuzu makundi, ukishafuzu makundi tapewa pointi za awali za kufuzu makundi, Yanga pointi 5 zimepatikana kwa kuchukua pointi 1 ya kufuzu makundi ya klabu bingwa zidisha na code ya msimu huu 5 (1×5=5) unapata pointi 5. Simb pointi 2.5 zinapatikana kwa kuchukua pointi 0.5 ya kufuzu makundi ya shirikisho zidisha na code ya msimu huu 5 (0.5×5= 2.5) unapata 2.5
Naomba tuelewe kuwa pointi za awali za kufuzu makundi ni sawa na timu uliyoishia nafasi ya nne kwenye kundi ila ukafanikiwa kumaliza nafasi ya tatu kwenye kundi au kufuzu robo fainali pointi zinaongezeka ila huwezi kupewa pointi zote za hatua hiyo wanajumlisha pointi ambazo bado mfano kufuzu robo klabu bingwa pointi 15 hawatajumlisha 15 zote watajumlisha 10 kwa sababu 5 ulipewa baada ya kufuzu makundi.
Yanga inaweza kuidizi Simba kwenye Club Ranking kivip? Twende pamoja iwapo timu zote zitafanikiwa kufuzu robo fainali ya klabu bingwa kwa Yanga na kombe la shirikisho kwa Simba zitakuwa na pointi zifuatazo.
Yanga kwa sasa ina pointi 29 ikifanikiwa kufuzu robo fainali ya klabu bingwa itakuwa imetengeneza pointi 15 (3×5) msimu huu chukua 29 toa 5 ambazo iliwekewa mwanzoni baada ya kufuzu makundi ya klabu bingwa zinabaki 24 jumlisha na 15 iwapo itafuzu robo (24+15 = 39) jumla Yanga inakuwa na pointi 39.
Simba kwa sasa ina pointi 30.5 ikifanikiwa kufuzu robo fainali ya kombe la shirikisho itakuwa imetengeneza pointi 10 (2×5) msimu huu chukua 30.5 toa 2.5 ambazo aliwekewa mwanzoni baada ya kufuzu makundi ya kombe la shirikisho zinabaki 28 jumlisha na 10 iwapo itafuzu robo (28+10=38) jumla Simba inakuwa na pointi 38
Je 38 na 39 ipi kubwa?
Ila iwapo timu zote Yanga na Simba zitafanikiwa kufuzu nusu fainali, Yanga klabu bingwa itakuwa na pointi 44 huku Simba kombe la shirikisho utakuwaa na pointi 43 iwapo Yanga itafuzu nusu na Simba ikaishia robo Yanga itakuwa na pointi 44, Simba itakuwa na pointi 38 na Iwapo Simba itafuzu nusu na Yanga ikaishia robo, Simba itakuwa na pointi 43 na Yanga itakuwa na pointi 39.MSIMAMO KWENYE RANK ZA CAF Baada ya timu za Yanga na Simba kufanikiwa kufuzu makundi ya CAF kama nchi (Tanzania) tumeongeza pointi 7.5 (Yanga pointi 5, Simba Pointi 2.5) na kufikisha pointi 60 nafasi ya sita kwenye Association Ranking na tumezidiwa na mataifa matano (Misri-135.5, Morocco-104.5, Algeria-95, Afrika Kusini-83.5, Tunisia-72.5). Nafasi ya 7 wapo DR Congo na Angola wakiwa na pointi 45 kila mmoja huku anayeshika nafasi ya 13 ana pointi 18.5 hivyo tuna misimu 2 hadi 3 mbele ya kupeleka timu 4 kwenye mashindano ya CAF (2 klabu bingwa Afrika na 2 kombe la shirikisho) hata timu zetu hazitafanya vizuri kwa kufika makundi ya kombe la shirikisho au klabu bingwa. Kwenye Club Ranking mpaka sasa timu ya Simba ipo nafasi ya saba ikiwa na pointi 30.5 na Yanga ipo nafasi ya 11 ikiwa na pointi 29 kama nchi tuna pointi 60 (Simba 30.5, Yanga 29, Namungo 0.5) wanaongoza ni 1-Ahly-63, 2-Esperance-47, 3-Mamelodi-42, 4-Wydad-39, 5-Zamalek-34.5, 6-Belouizadad-31, 7-Mazembe & Simba 30.5, 9-Berkane & USM Alger-29.5, 11-Yanga 29. Kwenye hizo timu 11 za juu timu moja tu ya Wydad ndio haipo kwenye mashindano zingine zote zipo kwenye hatua ya makundi ikiwa Ahly, Esperance, Mamelodi, Belouizdad, Mazembe na Yanga zipo makundi ya klabu bingwa Afrika huku Zamalek, Simba, Berkane na USM Alger zipo makundi ya kombe la shirikisho. Timu ambazo zipo makundi zinaweza kuongeza pointi kulingana na performance yao kwa msimu huu kulingana na nafasi ambayo wataishia. Pointi huwa zinapatikana kama ifuatavyo kila pointi unayoipata kila msimu kulingana na nafasi uliyoishia unazidisha na coefficient code ya msimu husika Zifuatavyo ni code kwa msimu mitano inayopigiwa hesabu kutafuta pointi 2024/25=5 2023/24=4 2022/23=3 2021/22=2 2020/21=1 Pointi zinapatikana kama ifuatavyo >Kwenye klabu bingwa Afrika (CAF Champion League) Bingwa=6 Mshindi wa pili = 5 Nusu fainali =4 Robo fainali =3 Nafasi 3 kwenye kundi = 2 Nafasi ya 4 kwenye kundi =1 Kwenye kombe la shirikisho (CAF Confederation Cup) Bingwa=5 Mshindi wa pili = 4 Nusu fainali =3 Robo fainali =2 Nafasi 3 kwenye kundi = 1 Nafasi ya 4 kwenye kundi =0.5 Pointi zinapatikana kwa kuchukua pointi ya nafasi uliyoishia unazidisha na coefficient code ya msimu husika Simba ina pointi 30.5 ikiwa 2024/25 Makundi (Shirikisho) 0.5×5 = 2.5 2023/24 Robo (Klabu Bingwa) 3×4 = 12 2022/23 Robo (Klabu Bingwa) 3×3 = 9 2021/22 Robo (Shirikisho) 2×2= 4 2020/21 Robo (Klabu Bingwa) 3×1 = 3 Chukua 3+4+9+12+2.5 = 30.5 Yanga ina pointi 29 ikiwa 2024/25 Makundi (Klabu Bingwa) 1×5 = 5 2023/24 Robo (Klabu Bingwa) 3×4 = 12 2022/23 Mshindi 2(Shirikisho) 4×3 = 12 2021/22 Haikufuzu Makundi = 0 2020/21 Haikufuzu Makundi = 0 Chukua 0+0+12+12+5 = 29 Rejea kwenye aya ya kwanza huko juu nilisema Yanga imetengeneza pointi 5 huku Simba imetengeneza pointi 2.5 msimu huu kwa kufanikiwa kufuzu makundi, ukishafuzu makundi tapewa pointi za awali za kufuzu makundi, Yanga pointi 5 zimepatikana kwa kuchukua pointi 1 ya kufuzu makundi ya klabu bingwa zidisha na code ya msimu huu 5 (1×5=5) unapata pointi 5. Simb pointi 2.5 zinapatikana kwa kuchukua pointi 0.5 ya kufuzu makundi ya shirikisho zidisha na code ya msimu huu 5 (0.5×5= 2.5) unapata 2.5 Naomba tuelewe kuwa pointi za awali za kufuzu makundi ni sawa na timu uliyoishia nafasi ya nne kwenye kundi ila ukafanikiwa kumaliza nafasi ya tatu kwenye kundi au kufuzu robo fainali pointi zinaongezeka ila huwezi kupewa pointi zote za hatua hiyo wanajumlisha pointi ambazo bado mfano kufuzu robo klabu bingwa pointi 15 hawatajumlisha 15 zote watajumlisha 10 kwa sababu 5 ulipewa baada ya kufuzu makundi. Yanga inaweza kuidizi Simba kwenye Club Ranking kivip? Twende pamoja iwapo timu zote zitafanikiwa kufuzu robo fainali ya klabu bingwa kwa Yanga na kombe la shirikisho kwa Simba zitakuwa na pointi zifuatazo. Yanga kwa sasa ina pointi 29 ikifanikiwa kufuzu robo fainali ya klabu bingwa itakuwa imetengeneza pointi 15 (3×5) msimu huu chukua 29 toa 5 ambazo iliwekewa mwanzoni baada ya kufuzu makundi ya klabu bingwa zinabaki 24 jumlisha na 15 iwapo itafuzu robo (24+15 = 39) jumla Yanga inakuwa na pointi 39. Simba kwa sasa ina pointi 30.5 ikifanikiwa kufuzu robo fainali ya kombe la shirikisho itakuwa imetengeneza pointi 10 (2×5) msimu huu chukua 30.5 toa 2.5 ambazo aliwekewa mwanzoni baada ya kufuzu makundi ya kombe la shirikisho zinabaki 28 jumlisha na 10 iwapo itafuzu robo (28+10=38) jumla Simba inakuwa na pointi 38 Je 38 na 39 ipi kubwa? Ila iwapo timu zote Yanga na Simba zitafanikiwa kufuzu nusu fainali, Yanga klabu bingwa itakuwa na pointi 44 huku Simba kombe la shirikisho utakuwaa na pointi 43 iwapo Yanga itafuzu nusu na Simba ikaishia robo Yanga itakuwa na pointi 44, Simba itakuwa na pointi 38 na Iwapo Simba itafuzu nusu na Yanga ikaishia robo, Simba itakuwa na pointi 43 na Yanga itakuwa na pointi 39. -
“Najionea vituko tu! Kama Marehemu Hans Pope aliadhibiwa kwa kuongea redioni suala la Morisson liliokuwa kwenye Kamati, sembuse hawa walioenda na Mkataba hadharani? TFF isipochukua hatua sitawaelewa!!”
— Crescentius Magori.
#paulswai💬 “Najionea vituko tu! Kama Marehemu Hans Pope aliadhibiwa kwa kuongea redioni suala la Morisson liliokuwa kwenye Kamati, sembuse hawa walioenda na Mkataba hadharani? TFF isipochukua hatua sitawaelewa!!” — Crescentius Magori. #paulswai
More Results