• Washauri wamzuia Trump kushambulia Iran, lakini Lindsey Graham amsukuma aanzishe mashambulizi.

    Mvutano wa kisiasa umeibuka ndani ya kambi ya Rais wa Marekani, kufuatia taarifa kwamba baadhi ya Washauri wake wa karibu wamemtaka asichukue hatua ya kijeshi dhidi ya Iran. Hata hivyo, sauti kinzani imejitokeza kutoka kwa Seneta wa chama cha Republican, Lindsey Graham, ambaye amemtaka Rais huyo kupuuza ushauri huo na kuidhinisha mashambulizi.

    Kwa mujibu wa ripoti ya Axios, mjadala mkali umeendelea ndani ya duru za Ikulu ya White House kuhusu hatma ya sera ya Marekani dhidi ya Iran, wakati hali ya usalama Mashariki ya Kati ikiendelea kuwa tete.

    Taarifa zinaeleza kuwa baadhi ya Washauri wa karibu wa Rais Donald Trump wana hofu kuwa shambulio lolote la kijeshi dhidi ya Iran linaweza kusababisha mzozo mpana wa kikanda, na hata kuvuta mataifa mengine kuingia vitani. Wanaonya kuwa hatua hiyo inaweza kuathiri maslahi ya Marekani kimataifa, pamoja na uchumi wa dunia.

    Kwa mtazamo wao, njia ya diplomasia na vikwazo vya kiuchumi bado zinaweza kuwa mbinu mbadala ya kushinikiza Tehran bila kuingia kwenye mapambano ya wazi ya kijeshi.

    Kinyume chake, Seneta Lindsey Graham amesisitiza kuwa Marekani inapaswa kuonyesha nguvu na uthabiti dhidi ya Iran. Amedai kuwa kusita kuchukua hatua kunaweza kutafsiriwa kama udhaifu, na kuipa Iran nafasi ya kuendelea na kile anachokiona kama vitendo vya uchokozi katika ukanda huo.

    Kauli yake inaongeza presha ya kisiasa kwa Rais Trump, hasa kutoka kwa makundi ya wahafidhina wanaotaka msimamo mkali dhidi ya Tehran.

    Huku mjadala huo ukiendelea, macho ya jumuiya ya kimataifa yameelekezwa Washington. Uamuzi wowote wa Marekani unaweza kubadilisha mwelekeo wa siasa za Mashariki ya Kati na kuathiri usalama wa kimataifa.

    Kwa sasa, haijafahamika ni msimamo gani utachukuliwa rasmi na Ikulu, lakini kinachoonekana wazi ni kwamba mgawanyiko wa kimtazamo ndani ya uongozi wa Marekani umeibuka wazi katika suala la Iran.

    Toa maoni yako
    #Habari
    Washauri wamzuia Trump kushambulia Iran, lakini Lindsey Graham amsukuma aanzishe mashambulizi. Mvutano wa kisiasa umeibuka ndani ya kambi ya Rais wa Marekani, kufuatia taarifa kwamba baadhi ya Washauri wake wa karibu wamemtaka asichukue hatua ya kijeshi dhidi ya Iran. Hata hivyo, sauti kinzani imejitokeza kutoka kwa Seneta wa chama cha Republican, Lindsey Graham, ambaye amemtaka Rais huyo kupuuza ushauri huo na kuidhinisha mashambulizi. Kwa mujibu wa ripoti ya Axios, mjadala mkali umeendelea ndani ya duru za Ikulu ya White House kuhusu hatma ya sera ya Marekani dhidi ya Iran, wakati hali ya usalama Mashariki ya Kati ikiendelea kuwa tete. Taarifa zinaeleza kuwa baadhi ya Washauri wa karibu wa Rais Donald Trump wana hofu kuwa shambulio lolote la kijeshi dhidi ya Iran linaweza kusababisha mzozo mpana wa kikanda, na hata kuvuta mataifa mengine kuingia vitani. Wanaonya kuwa hatua hiyo inaweza kuathiri maslahi ya Marekani kimataifa, pamoja na uchumi wa dunia. Kwa mtazamo wao, njia ya diplomasia na vikwazo vya kiuchumi bado zinaweza kuwa mbinu mbadala ya kushinikiza Tehran bila kuingia kwenye mapambano ya wazi ya kijeshi. Kinyume chake, Seneta Lindsey Graham amesisitiza kuwa Marekani inapaswa kuonyesha nguvu na uthabiti dhidi ya Iran. Amedai kuwa kusita kuchukua hatua kunaweza kutafsiriwa kama udhaifu, na kuipa Iran nafasi ya kuendelea na kile anachokiona kama vitendo vya uchokozi katika ukanda huo. Kauli yake inaongeza presha ya kisiasa kwa Rais Trump, hasa kutoka kwa makundi ya wahafidhina wanaotaka msimamo mkali dhidi ya Tehran. Huku mjadala huo ukiendelea, macho ya jumuiya ya kimataifa yameelekezwa Washington. Uamuzi wowote wa Marekani unaweza kubadilisha mwelekeo wa siasa za Mashariki ya Kati na kuathiri usalama wa kimataifa. Kwa sasa, haijafahamika ni msimamo gani utachukuliwa rasmi na Ikulu, lakini kinachoonekana wazi ni kwamba mgawanyiko wa kimtazamo ndani ya uongozi wa Marekani umeibuka wazi katika suala la Iran. Toa maoni yako #Habari
    0 Σχόλια 0 Μοιράστηκε 52 Views
  • Zelensky asema Putin ameanzisha vita ya tatu ya Dunia.

    Volodymyr Zelensky ametoa kauli nzito akidai kuwa Vladimir Putin tayari ameanzisha Vita ya tatu ya Dunia, akisisitiza kuwa suluhisho pekee ni kuiwekea Urusi shinikizo kali kijeshi na kiuchumi ili kuizuia isisambaze zaidi mgogoro huo.

    Katika mahojiano aliyofanya na BBC Mjini Kyiv, Kiongozi huyo wa Ukraine alieleza kuwa nchi yake haitaanguka mikononi mwa Urusi, bali itaibuka mshindi mwishoni mwa vita. Alisisitiza kuwa Ukraine haiwezi kutoa ardhi yake kama gharama ya amani, hasa ikizingatiwa kuwa majeshi ya Urusi hayajafanikiwa kuiteka kikamilifu licha ya kupeleka wanajeshi wengi vitani.

    “Nafikiri Putin tayari ameanzisha Vita ya Tatu ya Dunia. Swali si tu kwamba ameianzisha, bali ni wapi anaweza kufika na namna gani dunia inaweza kumzuia,” alisema Zelensky.

    Aliongeza kuwa Urusi inalenga kubadili mfumo wa kimataifa na kuwalazimisha watu kuishi katika mfumo ambao hawajauchagua wenyewe.

    Akizungumzia pendekezo la Urusi la kutaka Ukraine ikabidhi takribani asilimia 20 ya maeneo yake, ikiwemo sehemu za Mkoa wa Donetsk na maeneo ya kusini, Zelensky alikataa wazo hilo vikali.

    Kwa mujibu wake, suala hilo halihusu ardhi pekee, bali linahusu maisha ya Raia wa Ukraine na mustakabali wa taifa. Alisema kukubali masharti hayo kungekuwa sawa na kuwasaliti Wananchi na kuipokonya nchi hadhi yake.

    Zelensky ameitaka jumuiya ya kimataifa kuongeza vikwazo vya kiuchumi dhidi ya Moscow pamoja na kuimarisha msaada wa kijeshi kwa Ukraine. Anaamini kuwa presha ya pamoja ndiyo njia pekee ya kuzuia mzozo huo kuenea zaidi na kuathiri usalama wa dunia kwa upana wake.

    Kauli yake inakuja wakati mapigano kati ya Ukraine na Urusi yakiendelea katika maeneo kadhaa ya mashariki na kusini mwa nchi hiyo, huku hali ya kisiasa na kiusalama ikiendelea kuwa tete katika ukanda wa Ulaya Mashariki.

    Toa maoni yako
    #Habari
    Zelensky asema Putin ameanzisha vita ya tatu ya Dunia. Volodymyr Zelensky ametoa kauli nzito akidai kuwa Vladimir Putin tayari ameanzisha Vita ya tatu ya Dunia, akisisitiza kuwa suluhisho pekee ni kuiwekea Urusi shinikizo kali kijeshi na kiuchumi ili kuizuia isisambaze zaidi mgogoro huo. Katika mahojiano aliyofanya na BBC Mjini Kyiv, Kiongozi huyo wa Ukraine alieleza kuwa nchi yake haitaanguka mikononi mwa Urusi, bali itaibuka mshindi mwishoni mwa vita. Alisisitiza kuwa Ukraine haiwezi kutoa ardhi yake kama gharama ya amani, hasa ikizingatiwa kuwa majeshi ya Urusi hayajafanikiwa kuiteka kikamilifu licha ya kupeleka wanajeshi wengi vitani. “Nafikiri Putin tayari ameanzisha Vita ya Tatu ya Dunia. Swali si tu kwamba ameianzisha, bali ni wapi anaweza kufika na namna gani dunia inaweza kumzuia,” alisema Zelensky. Aliongeza kuwa Urusi inalenga kubadili mfumo wa kimataifa na kuwalazimisha watu kuishi katika mfumo ambao hawajauchagua wenyewe. Akizungumzia pendekezo la Urusi la kutaka Ukraine ikabidhi takribani asilimia 20 ya maeneo yake, ikiwemo sehemu za Mkoa wa Donetsk na maeneo ya kusini, Zelensky alikataa wazo hilo vikali. Kwa mujibu wake, suala hilo halihusu ardhi pekee, bali linahusu maisha ya Raia wa Ukraine na mustakabali wa taifa. Alisema kukubali masharti hayo kungekuwa sawa na kuwasaliti Wananchi na kuipokonya nchi hadhi yake. Zelensky ameitaka jumuiya ya kimataifa kuongeza vikwazo vya kiuchumi dhidi ya Moscow pamoja na kuimarisha msaada wa kijeshi kwa Ukraine. Anaamini kuwa presha ya pamoja ndiyo njia pekee ya kuzuia mzozo huo kuenea zaidi na kuathiri usalama wa dunia kwa upana wake. Kauli yake inakuja wakati mapigano kati ya Ukraine na Urusi yakiendelea katika maeneo kadhaa ya mashariki na kusini mwa nchi hiyo, huku hali ya kisiasa na kiusalama ikiendelea kuwa tete katika ukanda wa Ulaya Mashariki. Toa maoni yako #Habari
    0 Σχόλια 0 Μοιράστηκε 43 Views
  • DRC na Burundi zafungua rasmi mpaka wa Kavimvira–Gatumba.

    Leo hii Februari 23, 2026, Mpaka wa Kavimvira–Gatumba unaounganisha Nchi za Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na Burundi umefunguliwa rasmi kuanzia asubuhi hii, katika hatua inayotajwa kuwa muhimu kwa uhusiano wa kikanda na ushirikiano wa kiuchumi kati ya mataifa hayo mawili.

    Ufunguzi huo unafuatia kipindi cha kusubiri kilichosababisha kusimama kwa sehemu ya shughuli za usafirishaji na biashara mpakani. Mamlaka za pande zote mbili zimesema hatua hiyo inalenga kurejesha hali ya kawaida katika mzunguko wa watu na bidhaa.

    Kwa mujibu wa taarifa za awali, kufunguliwa kwa mpaka huo kutaruhusu:

    - Kurejea kwa shughuli za kawaida za kibiashara

    - Kuimarika kwa usafiri wa wananchi wanaovuka mpaka

    - Kuongezeka kwa ubadilishanaji wa bidhaa na huduma

    - Kuimarisha uhusiano wa kijamii na kiuchumi kati ya jamii za mpakani

    Mashuhuda katika eneo la mpakani wameripoti kuongezeka kwa idadi ya Wasafiri na Wafanyabiashara tangu saa za mapema asubuhi, huku malori ya mizigo na mabasi yakianza kuvuka kwa utaratibu wa kawaida.

    Hata hivyo, mamlaka zimehimiza wananchi kuzingatia sheria na taratibu za mipakani ili kuhakikisha usalama na uendeshaji mzuri wa shughuli zote.

    Wachambuzi wa masuala ya kikanda wanasema hatua hiyo inaweza kuchochea ukuaji wa uchumi katika ukanda wa Maziwa Makuu, hususan kwa jamii zinazotegemea biashara ya kuvuka mpaka kati ya DRC na Burundi.

    Toa maoni yako
    #Habari
    DRC na Burundi zafungua rasmi mpaka wa Kavimvira–Gatumba. Leo hii Februari 23, 2026, Mpaka wa Kavimvira–Gatumba unaounganisha Nchi za Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na Burundi umefunguliwa rasmi kuanzia asubuhi hii, katika hatua inayotajwa kuwa muhimu kwa uhusiano wa kikanda na ushirikiano wa kiuchumi kati ya mataifa hayo mawili. Ufunguzi huo unafuatia kipindi cha kusubiri kilichosababisha kusimama kwa sehemu ya shughuli za usafirishaji na biashara mpakani. Mamlaka za pande zote mbili zimesema hatua hiyo inalenga kurejesha hali ya kawaida katika mzunguko wa watu na bidhaa. Kwa mujibu wa taarifa za awali, kufunguliwa kwa mpaka huo kutaruhusu: - Kurejea kwa shughuli za kawaida za kibiashara - Kuimarika kwa usafiri wa wananchi wanaovuka mpaka - Kuongezeka kwa ubadilishanaji wa bidhaa na huduma - Kuimarisha uhusiano wa kijamii na kiuchumi kati ya jamii za mpakani Mashuhuda katika eneo la mpakani wameripoti kuongezeka kwa idadi ya Wasafiri na Wafanyabiashara tangu saa za mapema asubuhi, huku malori ya mizigo na mabasi yakianza kuvuka kwa utaratibu wa kawaida. Hata hivyo, mamlaka zimehimiza wananchi kuzingatia sheria na taratibu za mipakani ili kuhakikisha usalama na uendeshaji mzuri wa shughuli zote. Wachambuzi wa masuala ya kikanda wanasema hatua hiyo inaweza kuchochea ukuaji wa uchumi katika ukanda wa Maziwa Makuu, hususan kwa jamii zinazotegemea biashara ya kuvuka mpaka kati ya DRC na Burundi. Toa maoni yako #Habari
    0 Σχόλια 0 Μοιράστηκε 43 Views
  • Trump kutoa hotuba ya Taifa: Je, Ni kipimo cha Chama cha Republican?

    Hii Jumanne, Marekani inatarajia kusikiliza hotuba ya Rais Donald Trump, hotuba ambayo wengi wanaiona kama kipimo cha namna chama chake cha Republican kitakavyoshikilia imani ya wapiga kura kuelekea uchaguzi wa katikati ya muhula.

    Hotuba hii siyo tu ni nafasi ya kuwasilisha mpango wa serikali, bali pia ni fursa ya Trump kuonyesha mwelekeo wa sera na jinsi anavyopanga kushawishi umaarufu wa chama chake katika majimbo yote ya nchi. Ushuru wa kimataifa, ambao ameeleza unaongezwa kutoka asilimia 10 hadi 15, ni moja ya hoja ambazo zitaangaziwa na zitakuwa kipimo cha sera zake za uchumi.

    Hata hivyo, kura za maoni zinaonesha kuwa imani ya wananchi katika baadhi ya majimbo imepungua, kutokana na namna rais Trump alivyosimamia serikali katika muhula wake wa kwanza tangu kurejea madarakani. Hii inafanya hotuba yake kuwa kipimo cha umakini wa umma na nguvu ya chama chake kushikilia uongozi wa Bunge na Seneti.

    Wakati hotuba hii kwa kawaida inatarajiwa kuzungumzia zaidi masuala ya ndani ya nchi, kitisho cha Iran kutokana na mpango wake wa nyuklia kinaweza kuigubika hotuba yote. Trump ameendelea kushinikiza hoja za kuishambulia Iran, jambo linalotarajiwa kuvutia hisia na mjadala mkali nchini na kimataifa.

    Kwa hakika, hotuba ya Jumanne sio tu taarifa kwa taifa, bali ni kioo cha mustakabali wa kisiasa wa Republican na jinsi Rais Trump anavyopanga kuendeleza sera zake katika muhula huu wa pili.

    Toa maoni yako
    #Habari
    Trump kutoa hotuba ya Taifa: Je, Ni kipimo cha Chama cha Republican? Hii Jumanne, Marekani inatarajia kusikiliza hotuba ya Rais Donald Trump, hotuba ambayo wengi wanaiona kama kipimo cha namna chama chake cha Republican kitakavyoshikilia imani ya wapiga kura kuelekea uchaguzi wa katikati ya muhula. Hotuba hii siyo tu ni nafasi ya kuwasilisha mpango wa serikali, bali pia ni fursa ya Trump kuonyesha mwelekeo wa sera na jinsi anavyopanga kushawishi umaarufu wa chama chake katika majimbo yote ya nchi. Ushuru wa kimataifa, ambao ameeleza unaongezwa kutoka asilimia 10 hadi 15, ni moja ya hoja ambazo zitaangaziwa na zitakuwa kipimo cha sera zake za uchumi. Hata hivyo, kura za maoni zinaonesha kuwa imani ya wananchi katika baadhi ya majimbo imepungua, kutokana na namna rais Trump alivyosimamia serikali katika muhula wake wa kwanza tangu kurejea madarakani. Hii inafanya hotuba yake kuwa kipimo cha umakini wa umma na nguvu ya chama chake kushikilia uongozi wa Bunge na Seneti. Wakati hotuba hii kwa kawaida inatarajiwa kuzungumzia zaidi masuala ya ndani ya nchi, kitisho cha Iran kutokana na mpango wake wa nyuklia kinaweza kuigubika hotuba yote. Trump ameendelea kushinikiza hoja za kuishambulia Iran, jambo linalotarajiwa kuvutia hisia na mjadala mkali nchini na kimataifa. Kwa hakika, hotuba ya Jumanne sio tu taarifa kwa taifa, bali ni kioo cha mustakabali wa kisiasa wa Republican na jinsi Rais Trump anavyopanga kuendeleza sera zake katika muhula huu wa pili. Toa maoni yako #Habari
    0 Σχόλια 0 Μοιράστηκε 45 Views
  • Kesi ya uhaini dhidi ya Tundu Lissu yaahirishwa tena Mahakamani.

    Kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu, imeahirishwa hadi kesho baada ya Mahakama kushindwa kuendelea na usikilizwaji wake kufuatia mjadala mzito wa kisheria. Chanzo cha mvutano huo ni notisi iliyowasilishwa na upande wa Jamhuri ikieleza nia ya kuleta ushahidi mpya Mahakamani.

    Jamhuri: Notisi Iliwasilishwa kwa mujibu wa sheria.

    Upande wa Mashtaka umeeleza kuwa uliwasilisha notisi hiyo tarehe 20 Februari 2026 kwa mujibu wa kifungu cha 308 cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai. Wakili wa Serikali alidai kuwa notisi hiyo ina maudhui ya ushahidi unaokusudiwa kuongezwa kama nyongeza ya ushahidi uliowasilishwa awali na ACP Amini Mahamba.

    Kwa hoja ya Jamhuri:

    - Kifungu cha 308(1) kinatoa mwongozo wa kuwasilisha ushahidi wa ziada.

    - Kifungu cha 308(4) kinahusu ushahidi uliopo katika jalada la kesi.

    - ACP Mahamba alikuwa Mchunguzi wa matukio yaliyotokea wakati na baada ya uchaguzi wa Oktoba 29, 2025.

    Kwa mtazamo wa Jamhuri, ushahidi huo ni wa kuimarisha hoja zao na unafuata taratibu za kisheria.

    Lissu apinga: “Si shahidi mpya”

    Hata hivyo, Tundu Lissu alipinga vikali notisi hiyo akisema haikidhi matakwa ya kisheria.

    Kwa mujibu wa hoja yake:

    - Kifungu cha 308(1) kinahusu shahidi mpya ambaye ushahidi wake haukusomwa wakati wa hatua ya awali (committal proceedings).

    - Upande wa Jamhuri hauleti shahidi mpya, bali unataka kuongeza ushahidi wa shahidi ambaye tayari alishatoa ushahidi wake.

    - Notisi hiyo haimtaji shahidi mpya kama sheria inavyotaka.

    Lissu alisisitiza kuwa hatua hiyo ni kinyume cha utaratibu wa kisheria na inalenga kupanua wigo wa kesi nje ya hati ya mashtaka.

    Aidha, Lissu alieleza kuwa maelezo yanayohusu matukio ya uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025 hayamo kwenye hati ya mashtaka.

    Alidai kuwa:

    - Serikali inaonekana kutaka kubadilisha hati ya mashtaka bila kufuata utaratibu.

    - Wakati wa matukio hayo, yeye alikuwa mahabusu kwa miezi sita na nusu.

    - Kuruhusu notisi hiyo ni sawa na kufungua “sanduku la Pandora” kwa kuingiza masuala mapya yasiyo kwenye mashtaka ya awali.

    Kutokana na mvutano huo wa kisheria, Mahakama ililazimika kuahirisha kesi hiyo hadi kesho ili kutoa mwongozo au uamuzi kuhusu uhalali wa notisi ya Jamhuri.

    Uamuzi utakaotolewa unaweza kuwa na athari kubwa katika mwelekeo wa kesi hiyo, hasa kuhusu tafsiri na matumizi ya kifungu cha 308 katika mazingira ya ushahidi wa ziada.

    Toa maoni yako
    #Habari
    Kesi ya uhaini dhidi ya Tundu Lissu yaahirishwa tena Mahakamani. Kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu, imeahirishwa hadi kesho baada ya Mahakama kushindwa kuendelea na usikilizwaji wake kufuatia mjadala mzito wa kisheria. Chanzo cha mvutano huo ni notisi iliyowasilishwa na upande wa Jamhuri ikieleza nia ya kuleta ushahidi mpya Mahakamani. Jamhuri: Notisi Iliwasilishwa kwa mujibu wa sheria. Upande wa Mashtaka umeeleza kuwa uliwasilisha notisi hiyo tarehe 20 Februari 2026 kwa mujibu wa kifungu cha 308 cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai. Wakili wa Serikali alidai kuwa notisi hiyo ina maudhui ya ushahidi unaokusudiwa kuongezwa kama nyongeza ya ushahidi uliowasilishwa awali na ACP Amini Mahamba. Kwa hoja ya Jamhuri: - Kifungu cha 308(1) kinatoa mwongozo wa kuwasilisha ushahidi wa ziada. - Kifungu cha 308(4) kinahusu ushahidi uliopo katika jalada la kesi. - ACP Mahamba alikuwa Mchunguzi wa matukio yaliyotokea wakati na baada ya uchaguzi wa Oktoba 29, 2025. Kwa mtazamo wa Jamhuri, ushahidi huo ni wa kuimarisha hoja zao na unafuata taratibu za kisheria. Lissu apinga: “Si shahidi mpya” Hata hivyo, Tundu Lissu alipinga vikali notisi hiyo akisema haikidhi matakwa ya kisheria. Kwa mujibu wa hoja yake: - Kifungu cha 308(1) kinahusu shahidi mpya ambaye ushahidi wake haukusomwa wakati wa hatua ya awali (committal proceedings). - Upande wa Jamhuri hauleti shahidi mpya, bali unataka kuongeza ushahidi wa shahidi ambaye tayari alishatoa ushahidi wake. - Notisi hiyo haimtaji shahidi mpya kama sheria inavyotaka. Lissu alisisitiza kuwa hatua hiyo ni kinyume cha utaratibu wa kisheria na inalenga kupanua wigo wa kesi nje ya hati ya mashtaka. Aidha, Lissu alieleza kuwa maelezo yanayohusu matukio ya uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025 hayamo kwenye hati ya mashtaka. Alidai kuwa: - Serikali inaonekana kutaka kubadilisha hati ya mashtaka bila kufuata utaratibu. - Wakati wa matukio hayo, yeye alikuwa mahabusu kwa miezi sita na nusu. - Kuruhusu notisi hiyo ni sawa na kufungua “sanduku la Pandora” kwa kuingiza masuala mapya yasiyo kwenye mashtaka ya awali. Kutokana na mvutano huo wa kisheria, Mahakama ililazimika kuahirisha kesi hiyo hadi kesho ili kutoa mwongozo au uamuzi kuhusu uhalali wa notisi ya Jamhuri. Uamuzi utakaotolewa unaweza kuwa na athari kubwa katika mwelekeo wa kesi hiyo, hasa kuhusu tafsiri na matumizi ya kifungu cha 308 katika mazingira ya ushahidi wa ziada. Toa maoni yako #Habari
    0 Σχόλια 0 Μοιράστηκε 42 Views
  • Vita vya M23: Wiki ngumu kwa Waasi katika eneo la Masisi.

    Wiki hii imekuwa ya majaribu makubwa kwa Waasi wa M23 na washirika wao katika eneo la Masisi, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo. Kwa mujibu wa taarifa kutoka vyanzo vya ndani, makundi hayo yanadaiwa kupata hasara kubwa katika mapigano dhidi ya vikosi vya ndani vinavyopambana nao.

    Leo hii Jumatatu, 23 Februari 2026, Muungano unaojumuisha Wazalendo, CMPDN na Pareco-FF ulitangaza kuwa umefanikiwa kuwaondoa wapiganaji wa M23 katika eneo la Kaniro. Hatua hiyo inaelezwa kuwa ya kimkakati, kwani sasa inawakaribisha wapiganaji hao karibu na Katale-centre, eneo lililo jirani na Masisi-centre.

    Kwa mujibu wa taarifa hizo, mafanikio hayo yanatajwa kuwa sehemu ya operesheni pana inayolenga kuisukuma M23 kutoka katika maeneo wanayodhibiti.

    Wakati huo huo, Mji wa madini wa Rubaya unaripotiwa kuwa karibu kuzingirwa na Wazalendo. Inadaiwa kuwa makundi hayo sasa yanadhibiti barabara na njia kadhaa muhimu zinazoelekea Mjini humo, zikiwemo Kinigi, Kilonge na Kaniro.

    Rubaya inachukuliwa kuwa kitovu muhimu cha uchimbaji madini katika eneo hilo. Taarifa za makadirio zinaonesha kuwa uchimbaji wake huzalisha zaidi ya dola milioni 2.5 za Marekani kwa mwezi, kwa kiwango cha uzalishaji kinachokadiriwa kufikia tani 110 hadi 120 za madini kila mwezi.

    Kwa mujibu wa vyanzo vya ndani, Kamanda wa M23, Sultani Makenga, aliripotiwa kufika Rubaya mapema leo hii Jumatatu kwa lengo la kusimamia binafsi operesheni za kijeshi. Taarifa zinaeleza kuwa kikosi cha M23 kilichokuwa kimepelekwa Kinigi kilisukumwa nyuma hadi Kibabi.

    Kutokana na presha ya mashambulizi, Makenga anadaiwa kushuka mstari wa mbele ili kujaribu kupanga upya vikosi vilivyokuwa vinayumba.

    Hata hivyo, kasi ya Wazalendo inaelezwa kupungua kutokana na uwepo wa silaha nzito za msaada, zikiwemo vipande vya mizinga na chokaa ya milimita 120, zilizowekwa Kalonge. Silaha hizo zinaripotiwa kushambulia maeneo ya Chugi, Kinigi/Bisunzu na Kilonge, jambo linalozuia kusonga mbele kwa haraka kwa wapiganaji wa Wazalendo.

    Kuimarishwa kwa vikosi vya Waasi ndani ya Rubaya kunaonekana kulenga kulinda Mji huo wa kimkakati, hasa kutokana na umuhimu wake wa kiuchumi. Hali ya usalama katika eneo la Masisi bado ni tete, huku pande zote zikijaribu kudhibiti maeneo yenye umuhimu wa kijeshi na kiuchumi.

    Kadri mapigano yanavyoendelea, macho ya wengi yanaelekezwa katika mustakabali wa Rubaya na iwapo Muungano wa Wazalendo utafanikiwa kuudhibiti Mji huo au la.

    Toa maoni yako
    #Habari
    🇨🇩Vita vya M23: Wiki ngumu kwa Waasi katika eneo la Masisi. Wiki hii imekuwa ya majaribu makubwa kwa Waasi wa M23 na washirika wao katika eneo la Masisi, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo. Kwa mujibu wa taarifa kutoka vyanzo vya ndani, makundi hayo yanadaiwa kupata hasara kubwa katika mapigano dhidi ya vikosi vya ndani vinavyopambana nao. Leo hii Jumatatu, 23 Februari 2026, Muungano unaojumuisha Wazalendo, CMPDN na Pareco-FF ulitangaza kuwa umefanikiwa kuwaondoa wapiganaji wa M23 katika eneo la Kaniro. Hatua hiyo inaelezwa kuwa ya kimkakati, kwani sasa inawakaribisha wapiganaji hao karibu na Katale-centre, eneo lililo jirani na Masisi-centre. Kwa mujibu wa taarifa hizo, mafanikio hayo yanatajwa kuwa sehemu ya operesheni pana inayolenga kuisukuma M23 kutoka katika maeneo wanayodhibiti. Wakati huo huo, Mji wa madini wa Rubaya unaripotiwa kuwa karibu kuzingirwa na Wazalendo. Inadaiwa kuwa makundi hayo sasa yanadhibiti barabara na njia kadhaa muhimu zinazoelekea Mjini humo, zikiwemo Kinigi, Kilonge na Kaniro. Rubaya inachukuliwa kuwa kitovu muhimu cha uchimbaji madini katika eneo hilo. Taarifa za makadirio zinaonesha kuwa uchimbaji wake huzalisha zaidi ya dola milioni 2.5 za Marekani kwa mwezi, kwa kiwango cha uzalishaji kinachokadiriwa kufikia tani 110 hadi 120 za madini kila mwezi. Kwa mujibu wa vyanzo vya ndani, Kamanda wa M23, Sultani Makenga, aliripotiwa kufika Rubaya mapema leo hii Jumatatu kwa lengo la kusimamia binafsi operesheni za kijeshi. Taarifa zinaeleza kuwa kikosi cha M23 kilichokuwa kimepelekwa Kinigi kilisukumwa nyuma hadi Kibabi. Kutokana na presha ya mashambulizi, Makenga anadaiwa kushuka mstari wa mbele ili kujaribu kupanga upya vikosi vilivyokuwa vinayumba. Hata hivyo, kasi ya Wazalendo inaelezwa kupungua kutokana na uwepo wa silaha nzito za msaada, zikiwemo vipande vya mizinga na chokaa ya milimita 120, zilizowekwa Kalonge. Silaha hizo zinaripotiwa kushambulia maeneo ya Chugi, Kinigi/Bisunzu na Kilonge, jambo linalozuia kusonga mbele kwa haraka kwa wapiganaji wa Wazalendo. Kuimarishwa kwa vikosi vya Waasi ndani ya Rubaya kunaonekana kulenga kulinda Mji huo wa kimkakati, hasa kutokana na umuhimu wake wa kiuchumi. Hali ya usalama katika eneo la Masisi bado ni tete, huku pande zote zikijaribu kudhibiti maeneo yenye umuhimu wa kijeshi na kiuchumi. Kadri mapigano yanavyoendelea, macho ya wengi yanaelekezwa katika mustakabali wa Rubaya na iwapo Muungano wa Wazalendo utafanikiwa kuudhibiti Mji huo au la. Toa maoni yako #Habari
    0 Σχόλια 0 Μοιράστηκε 47 Views
  • Familia ya Kiongozi wa upinzani wa Uganda Bobi Wine yafunguka kukimbia Nchi kufuatia matukio ya siasa na usalama.

    Katika taarifa iliyotolewa, Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Robert Kyagulanyi Ssentamu, maarufu kama Bobi Wine, amethibitisha mbele ya Wakaguzi wa haki za binadamu Mjini Geneva kwamba Mke wake, Barbie Itungo Kyagulanyi, na Watoto wao wametoka Uganda kwa sababu za hofu ya maisha yao kufuatia hali tete inayojitokeza nchini mwao baada ya uchaguzi wa Rais.

    Katika hotuba yake kupitia video mbele ya Geneva Summit for Human Rights and Democracy, Bobi Wine alisema wazi: “Mke wangu na Watoto walilazimika kukimbia nchi kwa hofu ya maisha yao.” - Bobi Wine.

    Alifafanua kuwa usalama wa familia yake uliathirika sana kutokana na operesheni za vikosi vya usalama zilizoendelea mara tu baada ya uchaguzi wa 15 Januari 2026, ambapo serikali ilitangaza ushindi wa Rais Yoweri Museveni ambayo Bobi Wine ameipinga kwa madai ya udanganyifu wa kura na ukandamizaji wa upinzani.

    Bobi Wine pia alidai kwamba vikosi vya usalama: “Vilivamia nyumba yangu, vikamtesa Mke wangu, kumfanya asiwe na chaguo ila kuondoka na Watoto wakiwa nje ya nchi.” amesema

    Habari kwamba familia yake imeondoka Uganda na si tu kutoroka nyumba yao ya Magere imetolewa mara tu baada ya miezi ya mvutano mkali, ikiwa ni pamoja na madai ya mashambulizi, ulinzi mkali wa nyumba yao na vitisho vilivyowekwa na baadhi ya Afisa wa usalama.

    Katika maneno yake Mjini Geneva, Bobi Wine pia alijumuisha ombi kwa Jumuiya ya kimataifa kuhusu hatua za kulinda haki za binadamu na kuzuia ukandamizaji wa upinzani nchini Uganda.

    Taarifa hii inakuja katika wakati ambapo Uganda iko chini ya uangalizi wa kimataifa kufuatia ripoti za ghasia, mashambulizi dhidi ya wapinzani wa kisiasa, na madai ya upendeleo wa vyombo vya usalama kuelekea chama tawala.

    Kwa sasa, bado haijafahamika kwa umma ni nchi gani hasa Barbie Itungo Kyagulanyi na Watoto hao wamekwenda, ila uamuzi wao wa kukimbia unachukuliwa kama hatua ya kulinda usalama wa familia katika mzozo wa kisiasa unaoendelea nchini Uganda.

    Toa maoni yako
    #Habari
    Familia ya Kiongozi wa upinzani wa Uganda Bobi Wine yafunguka kukimbia Nchi kufuatia matukio ya siasa na usalama. Katika taarifa iliyotolewa, Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Robert Kyagulanyi Ssentamu, maarufu kama Bobi Wine, amethibitisha mbele ya Wakaguzi wa haki za binadamu Mjini Geneva kwamba Mke wake, Barbie Itungo Kyagulanyi, na Watoto wao wametoka Uganda kwa sababu za hofu ya maisha yao kufuatia hali tete inayojitokeza nchini mwao baada ya uchaguzi wa Rais. Katika hotuba yake kupitia video mbele ya Geneva Summit for Human Rights and Democracy, Bobi Wine alisema wazi: “Mke wangu na Watoto walilazimika kukimbia nchi kwa hofu ya maisha yao.” - Bobi Wine. Alifafanua kuwa usalama wa familia yake uliathirika sana kutokana na operesheni za vikosi vya usalama zilizoendelea mara tu baada ya uchaguzi wa 15 Januari 2026, ambapo serikali ilitangaza ushindi wa Rais Yoweri Museveni ambayo Bobi Wine ameipinga kwa madai ya udanganyifu wa kura na ukandamizaji wa upinzani. Bobi Wine pia alidai kwamba vikosi vya usalama: “Vilivamia nyumba yangu, vikamtesa Mke wangu, kumfanya asiwe na chaguo ila kuondoka na Watoto wakiwa nje ya nchi.” amesema Habari kwamba familia yake imeondoka Uganda na si tu kutoroka nyumba yao ya Magere imetolewa mara tu baada ya miezi ya mvutano mkali, ikiwa ni pamoja na madai ya mashambulizi, ulinzi mkali wa nyumba yao na vitisho vilivyowekwa na baadhi ya Afisa wa usalama. Katika maneno yake Mjini Geneva, Bobi Wine pia alijumuisha ombi kwa Jumuiya ya kimataifa kuhusu hatua za kulinda haki za binadamu na kuzuia ukandamizaji wa upinzani nchini Uganda. Taarifa hii inakuja katika wakati ambapo Uganda iko chini ya uangalizi wa kimataifa kufuatia ripoti za ghasia, mashambulizi dhidi ya wapinzani wa kisiasa, na madai ya upendeleo wa vyombo vya usalama kuelekea chama tawala. Kwa sasa, bado haijafahamika kwa umma ni nchi gani hasa Barbie Itungo Kyagulanyi na Watoto hao wamekwenda, ila uamuzi wao wa kukimbia unachukuliwa kama hatua ya kulinda usalama wa familia katika mzozo wa kisiasa unaoendelea nchini Uganda. Toa maoni yako #Habari
    0 Σχόλια 0 Μοιράστηκε 222 Views
  • Ikulu ya Marekani yatangaza Nchi zitakazoshiriki mkutano wa kwanza wa “Baraza la Amani”.

    White House imetangaza rasmi orodha ya nchi zitakazotuma wawakilishi katika mkutano wa uzinduzi wa kile kinachoitwa “Baraza la Amani,” unaofanyika leo kwenye Ukumbi Donald J. Trump Institute for Peace.

    Kwa mujibu wa taarifa hiyo, mkutano huo unalenga kuwakutanisha wadau wa kimataifa kwa ajili ya kujadili ajenda za ushirikiano wa usalama, diplomasia na utatuzi wa migogoro katika maeneo mbalimbali ya dunia.

    Orodha iliyotolewa inaonesha uwakilishi mpana kutoka Mabara tofauti, ikiashiria uzito wa mkutano huo katika medani ya siasa za kimataifa.

    - Albania
    - Austria
    - Azerbaijan
    - Bulgaria
    - Croatia
    - Cyprus
    - Jamhuri ya Czech
    - Finland
    - Ujerumani
    - Ugiriki
    - Hungaria
    - Italia
    - Poland
    - Romania
    - Slovakia
    - Uswisi
    - Uingereza
    - Norway
    - Uholanzi
    - Kosovo
    - Umoja wa Ulaya (EU)

    - Armenia
    - Bahrain
    - Cambodia
    - India
    - Indonesia
    - Israel
    - Japan
    - Jordan
    - Kazakhstan
    - Kuwait
    - Mongolia
    - Oman
    - Pakistan
    - Qatar
    - Korea Kusini
    - Saudi Arabia
    - Thailand
    - Uturuki
    - Falme za Kiarabu (UAE)
    - Uzbekistan
    - Vietnam

    - Argentina
    - El Salvador
    - Mexico

    Afrika

    - Misri
    - Morocco

    Ushiriki wa nchi kutoka kanda zenye mvutano wa kisiasa na kiusalama unaashiria kwamba mkutano huo unaweza kuwa jukwaa la mazungumzo kuhusu masuala ya usalama wa kimataifa, diplomasia ya kiuchumi na ushirikiano wa kimkakati.

    Hata hivyo, Wachambuzi wa siasa za kimataifa wanasema mafanikio ya “Baraza la Amani” yatategemea uwazi wa ajenda zake, ushirikishwaji wa pande zote na utekelezaji wa maazimio yatakayopitishwa.

    Mkutano huu wa kwanza unatarajiwa kuweka msingi wa vikao vingine vijavyo, huku macho ya jumuiya ya kimataifa yakielekezwa Washington kuona iwapo utazaa matokeo yenye tija katika kudumisha amani na utulivu wa dunia.

    Toa maoni yako
    #Habari
    Ikulu ya Marekani yatangaza Nchi zitakazoshiriki mkutano wa kwanza wa “Baraza la Amani”. White House imetangaza rasmi orodha ya nchi zitakazotuma wawakilishi katika mkutano wa uzinduzi wa kile kinachoitwa “Baraza la Amani,” unaofanyika leo kwenye Ukumbi Donald J. Trump Institute for Peace. Kwa mujibu wa taarifa hiyo, mkutano huo unalenga kuwakutanisha wadau wa kimataifa kwa ajili ya kujadili ajenda za ushirikiano wa usalama, diplomasia na utatuzi wa migogoro katika maeneo mbalimbali ya dunia. Orodha iliyotolewa inaonesha uwakilishi mpana kutoka Mabara tofauti, ikiashiria uzito wa mkutano huo katika medani ya siasa za kimataifa. - Albania - Austria - Azerbaijan - Bulgaria - Croatia - Cyprus - Jamhuri ya Czech - Finland - Ujerumani - Ugiriki - Hungaria - Italia - Poland - Romania - Slovakia - Uswisi - Uingereza - Norway - Uholanzi - Kosovo - Umoja wa Ulaya (EU) - Armenia - Bahrain - Cambodia - India - Indonesia - Israel - Japan - Jordan - Kazakhstan - Kuwait - Mongolia - Oman - Pakistan - Qatar - Korea Kusini - Saudi Arabia - Thailand - Uturuki - Falme za Kiarabu (UAE) - Uzbekistan - Vietnam - Argentina - El Salvador - Mexico Afrika - Misri - Morocco Ushiriki wa nchi kutoka kanda zenye mvutano wa kisiasa na kiusalama unaashiria kwamba mkutano huo unaweza kuwa jukwaa la mazungumzo kuhusu masuala ya usalama wa kimataifa, diplomasia ya kiuchumi na ushirikiano wa kimkakati. Hata hivyo, Wachambuzi wa siasa za kimataifa wanasema mafanikio ya “Baraza la Amani” yatategemea uwazi wa ajenda zake, ushirikishwaji wa pande zote na utekelezaji wa maazimio yatakayopitishwa. Mkutano huu wa kwanza unatarajiwa kuweka msingi wa vikao vingine vijavyo, huku macho ya jumuiya ya kimataifa yakielekezwa Washington kuona iwapo utazaa matokeo yenye tija katika kudumisha amani na utulivu wa dunia. Toa maoni yako #Habari
    0 Σχόλια 0 Μοιράστηκε 193 Views
  • Uingereza yakataa ombi la Trump kutumia kambi zake za kijeshi kushambulia Iran.

    Serikali ya Uingereza imekataa rasmi ombi la Rais wa Marekani, Donald Trump, la kutaka kutumia kambi za kijeshi za Uingereza kama vituo vya kuanzishia mashambulizi yanayoweza kulenga Iran.

    Kwa mujibu wa taarifa za kidiplomasia, ombi hilo lilihusisha matumizi ya kambi muhimu zikiwemo Diego Garcia katika Bahari ya Hindi pamoja na RAF Fairford iliyoko Gloucestershire.

    Vyanzo vya serikali Mjini London vinaeleza kuwa uamuzi huo umechukuliwa kwa kuzingatia maslahi ya kitaifa na tahadhari dhidi ya kuongezeka kwa mvutano wa kijeshi Mashariki ya Kati.

    Msimamo huo unaonyesha kuwa Uingereza haitaki kuhusishwa moja kwa moja na operesheni yoyote ya kijeshi dhidi ya Iran bila mchakato mpana wa kidiplomasia na kibali cha kimataifa.

    Ingawa Marekani na Uingereza ni washirika wakubwa wa kijeshi kupitia Muungano wa NATO, London imeonekana kuchukua tahadhari kubwa katika suala linaloweza kusababisha vita pana katika eneo la Ghuba.

    Kisiwa cha Diego Garcia ni kituo cha kimkakati kinachotumiwa kwa ushirikiano wa kijeshi kati ya Marekani na Uingereza. Kimewahi kutumika kama kitovu cha operesheni za kijeshi katika Mashariki ya Kati, hasa wakati wa vita vya Iraq na Afghanistan.

    Kwa upande mwingine, RAF Fairford imekuwa ikitumika mara kadhaa kupokea ndege za kivita za Marekani, zikiwemo mabomu mazito ya masafa marefu kama B-52.

    Hatua ya Uingereza inaweza kuathiri kwa kiwango fulani uratibu wa kijeshi kati ya Washington na London, hasa wakati ambapo mvutano kati ya Marekani na Iran unaongezeka.

    Hadi sasa, Ikulu ya White House haijatoa tamko rasmi kuhusu msimamo wa Uingereza, huku Wachambuzi wa siasa za kimataifa wakitathmini iwapo uamuzi huo utaashiria tofauti ya kimkakati kati ya washirika hao wawili wa muda mrefu.

    Mvutano kati ya Marekani na Iran umeendelea kuwa tete, hasa katika masuala yanayohusu nyuklia na ushawishi wa kikanda.

    Je, uamuzi wa London utatuliza hali au utaongeza presha za kidiplomasia? Dunia inaendelea kufuatilia kwa karibu.

    Toa maoni yako
    #Habari
    Uingereza yakataa ombi la Trump kutumia kambi zake za kijeshi kushambulia Iran. Serikali ya Uingereza imekataa rasmi ombi la Rais wa Marekani, Donald Trump, la kutaka kutumia kambi za kijeshi za Uingereza kama vituo vya kuanzishia mashambulizi yanayoweza kulenga Iran. Kwa mujibu wa taarifa za kidiplomasia, ombi hilo lilihusisha matumizi ya kambi muhimu zikiwemo Diego Garcia katika Bahari ya Hindi pamoja na RAF Fairford iliyoko Gloucestershire. Vyanzo vya serikali Mjini London vinaeleza kuwa uamuzi huo umechukuliwa kwa kuzingatia maslahi ya kitaifa na tahadhari dhidi ya kuongezeka kwa mvutano wa kijeshi Mashariki ya Kati. Msimamo huo unaonyesha kuwa Uingereza haitaki kuhusishwa moja kwa moja na operesheni yoyote ya kijeshi dhidi ya Iran bila mchakato mpana wa kidiplomasia na kibali cha kimataifa. Ingawa Marekani na Uingereza ni washirika wakubwa wa kijeshi kupitia Muungano wa NATO, London imeonekana kuchukua tahadhari kubwa katika suala linaloweza kusababisha vita pana katika eneo la Ghuba. Kisiwa cha Diego Garcia ni kituo cha kimkakati kinachotumiwa kwa ushirikiano wa kijeshi kati ya Marekani na Uingereza. Kimewahi kutumika kama kitovu cha operesheni za kijeshi katika Mashariki ya Kati, hasa wakati wa vita vya Iraq na Afghanistan. Kwa upande mwingine, RAF Fairford imekuwa ikitumika mara kadhaa kupokea ndege za kivita za Marekani, zikiwemo mabomu mazito ya masafa marefu kama B-52. Hatua ya Uingereza inaweza kuathiri kwa kiwango fulani uratibu wa kijeshi kati ya Washington na London, hasa wakati ambapo mvutano kati ya Marekani na Iran unaongezeka. Hadi sasa, Ikulu ya White House haijatoa tamko rasmi kuhusu msimamo wa Uingereza, huku Wachambuzi wa siasa za kimataifa wakitathmini iwapo uamuzi huo utaashiria tofauti ya kimkakati kati ya washirika hao wawili wa muda mrefu. Mvutano kati ya Marekani na Iran umeendelea kuwa tete, hasa katika masuala yanayohusu nyuklia na ushawishi wa kikanda. Je, uamuzi wa London utatuliza hali au utaongeza presha za kidiplomasia? Dunia inaendelea kufuatilia kwa karibu. Toa maoni yako #Habari
    0 Σχόλια 0 Μοιράστηκε 155 Views
  • Facebook yatangaza rasmi kufunga App ya Messenger kuanzia April.

    Kampuni ya teknolojia ya META imetangaza rasmi kuwa itafunga programu yake ya ujumbe, Messenger, kuanzia mwezi April mwaka huu.

    Kwa mujibu wa tangazo hilo, hatua za kwanza za mabadiliko zitaanza kwa Watumiaji wa kompyuta za Mac na Windows, ambapo toleo la desktop la Messenger litafungwa rasmi. Kampuni hiyo imeeleza pia kuwa mwakani inapanga kuiondoa kabisa Messenger kama app huru na kubaki na Facebook kama jukwaa moja lenye sehemu ya ujumbe (messages) ndani yake.

    Messenger haikuanza kwa jina hilo. Mwaka 2008, huduma hiyo ilizinduliwa kwa jina la Facebook Chat, ikiwa ni sehemu ya mawasiliano ya moja kwa moja ndani ya Facebook.

    Mwaka 2011, huduma hiyo iliboreshwa na kubadilishwa jina rasmi kuwa Messenger, ikiwa ni app inayojitegemea kwa simu na baadaye kwa kompyuta.

    Katika kipindi cha ukuaji wake, Messenger ilitumika kama silaha ya ushindani dhidi ya majukwaa mengine makubwa ya mawasiliano kama:

    - WhatsApp
    - iMessage
    - WeChat
    - Skype

    Lengo lilikuwa ni kuimarisha mawasiliano ya Watumiaji wa Facebook bila kulazimika kuondoka ndani ya mfumo wa kampuni hiyo.

    Baada ya kufutwa kwa Messenger kama app ya pekee, Facebook itabaki kama mtandao mmoja wenye sehemu ya ujumbe ndani yake. Hii ina maana kuwa Watumiaji wataendelea kutuma na kupokea meseji, lakini kupitia mfumo wa moja kwa moja ndani ya Facebook badala ya app tofauti.

    Hatua hii inaashiria mabadiliko makubwa katika mkakati wa kidijitali wa Facebook, hasa katika kipindi ambacho kampuni nyingi za teknolojia zinaelekea kurahisisha huduma zao na kupunguza gharama za uendeshaji.

    Zaidi ya muongo mmoja baada ya kuzinduliwa kwake, Messenger sasa inaingia rasmi katika historia kama app iliyowahi kuwa moja ya majukwaa makubwa ya mawasiliano duniani.

    Toa maoni yako
    #Habari
    Facebook yatangaza rasmi kufunga App ya Messenger kuanzia April. Kampuni ya teknolojia ya META imetangaza rasmi kuwa itafunga programu yake ya ujumbe, Messenger, kuanzia mwezi April mwaka huu. Kwa mujibu wa tangazo hilo, hatua za kwanza za mabadiliko zitaanza kwa Watumiaji wa kompyuta za Mac na Windows, ambapo toleo la desktop la Messenger litafungwa rasmi. Kampuni hiyo imeeleza pia kuwa mwakani inapanga kuiondoa kabisa Messenger kama app huru na kubaki na Facebook kama jukwaa moja lenye sehemu ya ujumbe (messages) ndani yake. Messenger haikuanza kwa jina hilo. Mwaka 2008, huduma hiyo ilizinduliwa kwa jina la Facebook Chat, ikiwa ni sehemu ya mawasiliano ya moja kwa moja ndani ya Facebook. Mwaka 2011, huduma hiyo iliboreshwa na kubadilishwa jina rasmi kuwa Messenger, ikiwa ni app inayojitegemea kwa simu na baadaye kwa kompyuta. Katika kipindi cha ukuaji wake, Messenger ilitumika kama silaha ya ushindani dhidi ya majukwaa mengine makubwa ya mawasiliano kama: - WhatsApp - iMessage - WeChat - Skype Lengo lilikuwa ni kuimarisha mawasiliano ya Watumiaji wa Facebook bila kulazimika kuondoka ndani ya mfumo wa kampuni hiyo. Baada ya kufutwa kwa Messenger kama app ya pekee, Facebook itabaki kama mtandao mmoja wenye sehemu ya ujumbe ndani yake. Hii ina maana kuwa Watumiaji wataendelea kutuma na kupokea meseji, lakini kupitia mfumo wa moja kwa moja ndani ya Facebook badala ya app tofauti. Hatua hii inaashiria mabadiliko makubwa katika mkakati wa kidijitali wa Facebook, hasa katika kipindi ambacho kampuni nyingi za teknolojia zinaelekea kurahisisha huduma zao na kupunguza gharama za uendeshaji. Zaidi ya muongo mmoja baada ya kuzinduliwa kwake, Messenger sasa inaingia rasmi katika historia kama app iliyowahi kuwa moja ya majukwaa makubwa ya mawasiliano duniani. Toa maoni yako #Habari
    0 Σχόλια 0 Μοιράστηκε 166 Views
  • Kuna habari gani tena hapa
    Kuna habari gani tena hapa 🤔
    0 Σχόλια 0 Μοιράστηκε 65 Views
  • Trump aahidi kufungua mafaili ya siri kuhusu “Aliens” baada ya kauli ya Obama.

    Mjadala kuhusu uwepo wa viumbe wa angani umechukua sura mpya baada ya kauli ya aliyekuwa Rais wa Marekani, Barack Obama, na kufuatiwa na ahadi ya Rais wa sasa, Donald Trump, ya kuweka wazi mafaili ya siri yanayohusiana na suala hilo.

    Katika maelezo yake ya hivi karibuni, Obama aligusia uwepo wa viumbe wa angani, akionesha kuwa suala hilo si la kubezwa. Kauli hiyo imeamsha hisia na mijadala mikubwa miongoni mwa Wananchi na Wachambuzi wa masuala ya usalama na sayansi.

    Ingawa hakutoa ushahidi wa moja kwa moja hadharani, kauli yake imechukuliwa kama ishara kwamba kuna taarifa ambazo bado hazijawekwa wazi kwa umma.

    Kupitia ujumbe wake rasmi, Trump ameahidi kuchukua hatua. Katika ujumbe huo ameandika: “Kutokana na hamasa kubwa iliyooneshwa na Wananchi juu ya kutaka kutambua ukweli kuhusu Aliens, nimezielekeza wizara na taasisi husika kuanza mchakato wa kubaini na kutoa hadharani nyaraka za serikali zinazohusiana na maisha ya viumbe wa anga (Aliens), matukio ya vitu visivyojulikana angani (UAP), vitu vinavyoruka visivyojulikana (UFO), pamoja na taarifa nyingine zote zinazohusiana na masuala haya ambayo ni magumu lakini ya kuvutia na muhimu sana.”

    Kauli hiyo imezua maswali mengi: Je, serikali ya Marekani iko tayari kufungua mafaili yote ya siri? Au kutakuwa na taarifa chache tu zitakazowekwa wazi kwa umma?

    Katika miaka ya karibuni, taasisi za ulinzi za Marekani zimekiri kuchunguza matukio ya UAP (Unidentified Aerial Phenomena) na UFO (Unidentified Flying Objects). Baadhi ya video na taarifa tayari zimewahi kutolewa, lakini bado kuna madai kwamba sehemu kubwa ya taarifa hizo imebaki kuwa siri ya serikali.

    Ahadi ya Trump inaweza kuwa hatua mpya katika historia ya uwazi wa taarifa za usalama wa taifa au inaweza kuwa mkakati wa kisiasa unaolenga kuvutia umma.

    Je, Siri zitafunguliwa Kweli?

    Kihistoria, masuala yanayohusiana na usalama wa taifa yamekuwa yakilindwa kwa uangalifu mkubwa. Hivyo, hata kama mchakato utaanza, Wachambuzi wanaamini kuwa kuna uwezekano wa kuwepo kwa uchujaji wa taarifa kabla ya kutolewa hadharani.

    Kwa sasa, macho ya dunia yanaelekezwa Washington kusubiri kama ahadi hiyo itatekelezwa kikamilifu.

    Unadhani Serikali ya Marekani itatoa kweli siri hizi zote? Na wewe binafsi, unaamini kweli kuna viumbe wa angani wanaoishi nje ya sayari yetu?

    Toa maoni yako
    #Habari
    Trump aahidi kufungua mafaili ya siri kuhusu “Aliens” baada ya kauli ya Obama. Mjadala kuhusu uwepo wa viumbe wa angani umechukua sura mpya baada ya kauli ya aliyekuwa Rais wa Marekani, Barack Obama, na kufuatiwa na ahadi ya Rais wa sasa, Donald Trump, ya kuweka wazi mafaili ya siri yanayohusiana na suala hilo. Katika maelezo yake ya hivi karibuni, Obama aligusia uwepo wa viumbe wa angani, akionesha kuwa suala hilo si la kubezwa. Kauli hiyo imeamsha hisia na mijadala mikubwa miongoni mwa Wananchi na Wachambuzi wa masuala ya usalama na sayansi. Ingawa hakutoa ushahidi wa moja kwa moja hadharani, kauli yake imechukuliwa kama ishara kwamba kuna taarifa ambazo bado hazijawekwa wazi kwa umma. Kupitia ujumbe wake rasmi, Trump ameahidi kuchukua hatua. Katika ujumbe huo ameandika: “Kutokana na hamasa kubwa iliyooneshwa na Wananchi juu ya kutaka kutambua ukweli kuhusu Aliens, nimezielekeza wizara na taasisi husika kuanza mchakato wa kubaini na kutoa hadharani nyaraka za serikali zinazohusiana na maisha ya viumbe wa anga (Aliens), matukio ya vitu visivyojulikana angani (UAP), vitu vinavyoruka visivyojulikana (UFO), pamoja na taarifa nyingine zote zinazohusiana na masuala haya ambayo ni magumu lakini ya kuvutia na muhimu sana.” Kauli hiyo imezua maswali mengi: Je, serikali ya Marekani iko tayari kufungua mafaili yote ya siri? Au kutakuwa na taarifa chache tu zitakazowekwa wazi kwa umma? Katika miaka ya karibuni, taasisi za ulinzi za Marekani zimekiri kuchunguza matukio ya UAP (Unidentified Aerial Phenomena) na UFO (Unidentified Flying Objects). Baadhi ya video na taarifa tayari zimewahi kutolewa, lakini bado kuna madai kwamba sehemu kubwa ya taarifa hizo imebaki kuwa siri ya serikali. Ahadi ya Trump inaweza kuwa hatua mpya katika historia ya uwazi wa taarifa za usalama wa taifa au inaweza kuwa mkakati wa kisiasa unaolenga kuvutia umma. Je, Siri zitafunguliwa Kweli? Kihistoria, masuala yanayohusiana na usalama wa taifa yamekuwa yakilindwa kwa uangalifu mkubwa. Hivyo, hata kama mchakato utaanza, Wachambuzi wanaamini kuwa kuna uwezekano wa kuwepo kwa uchujaji wa taarifa kabla ya kutolewa hadharani. Kwa sasa, macho ya dunia yanaelekezwa Washington kusubiri kama ahadi hiyo itatekelezwa kikamilifu. Unadhani Serikali ya Marekani itatoa kweli siri hizi zote? Na wewe binafsi, unaamini kweli kuna viumbe wa angani wanaoishi nje ya sayari yetu? Toa maoni yako #Habari
    0 Σχόλια 0 Μοιράστηκε 198 Views
  • Vatican yakataa mwaliko wa Trump kujiunga na “Bodi ya Amani”.

    Mvutano mpya wa kidiplomasia umeibuka baada ya Vatican kukataa rasmi mwaliko wa Rais wa Marekani kujiunga na kile kilichoelezwa kama “Bodi ya Amani”, mpango ambao umekuwa ukizua mjadala mkali katika duru za kimataifa.

    Kwa mujibu wa taarifa rasmi iliyotolewa na Katibu wa Jimbo la Vatican, Cardinal Pietro Parolin, Taasisi ya Kiti Kitakatifu haitashiriki katika mpango huo, ikitaja sababu za kimsingi zinazohusiana na mwelekeo na uhalali wa jukwaa hilo.

    Katika kauli yake, Kardinali Parolin alisema: “Kuna masuala nyeti na hoja ambazo zinatuacha katika mshangao mkubwa.”

    Alisisitiza kuwa masuala ya migogoro ya kimataifa, ikiwemo hali ya Gaza, yanapaswa kushughulikiwa ndani ya mfumo wa kimataifa uliopo badala ya kuanzishwa kwa chombo mbadala kinachoongozwa na taifa moja.

    Kwa mujibu wa Vatican,
    “Migogoro ya kimataifa kama wa Gaza inapaswa kushughulikiwa chini ya mwavuli wa Umoja wa Mataifa, si kupitia jukwaa mbadala linaloongozwa na Marekani.”

    Hatua hiyo inatajwa kama pigo la kidiplomasia kwa Ikulu ya White House, hasa ikizingatiwa kuwa baadhi ya washirika wa Magharibi tayari wameonesha kusita au kujiondoa katika mpango huo kabla hata ya mkutano wake wa kwanza mkubwa.

    Uamuzi huo kutoka Vatican ya Pope Leo XIV unaongeza shinikizo kwa mpango wa Rais huyo wa Marekani, ambao ulikusudiwa kuonesha dira mpya ya uongozi wa kimataifa katika kutafuta amani.

    Kwa sasa, jicho la dunia linaelekezwa kuona hatua inayofuata ya Washington, huku Vatican ikiweka msimamo wazi: haitashiriki katika bodi hiyo mpya.

    Toa maoni yako
    #Habari
    Vatican yakataa mwaliko wa Trump kujiunga na “Bodi ya Amani”. Mvutano mpya wa kidiplomasia umeibuka baada ya Vatican kukataa rasmi mwaliko wa Rais wa Marekani kujiunga na kile kilichoelezwa kama “Bodi ya Amani”, mpango ambao umekuwa ukizua mjadala mkali katika duru za kimataifa. Kwa mujibu wa taarifa rasmi iliyotolewa na Katibu wa Jimbo la Vatican, Cardinal Pietro Parolin, Taasisi ya Kiti Kitakatifu haitashiriki katika mpango huo, ikitaja sababu za kimsingi zinazohusiana na mwelekeo na uhalali wa jukwaa hilo. Katika kauli yake, Kardinali Parolin alisema: “Kuna masuala nyeti na hoja ambazo zinatuacha katika mshangao mkubwa.” Alisisitiza kuwa masuala ya migogoro ya kimataifa, ikiwemo hali ya Gaza, yanapaswa kushughulikiwa ndani ya mfumo wa kimataifa uliopo badala ya kuanzishwa kwa chombo mbadala kinachoongozwa na taifa moja. Kwa mujibu wa Vatican, “Migogoro ya kimataifa kama wa Gaza inapaswa kushughulikiwa chini ya mwavuli wa Umoja wa Mataifa, si kupitia jukwaa mbadala linaloongozwa na Marekani.” Hatua hiyo inatajwa kama pigo la kidiplomasia kwa Ikulu ya White House, hasa ikizingatiwa kuwa baadhi ya washirika wa Magharibi tayari wameonesha kusita au kujiondoa katika mpango huo kabla hata ya mkutano wake wa kwanza mkubwa. Uamuzi huo kutoka Vatican ya Pope Leo XIV unaongeza shinikizo kwa mpango wa Rais huyo wa Marekani, ambao ulikusudiwa kuonesha dira mpya ya uongozi wa kimataifa katika kutafuta amani. Kwa sasa, jicho la dunia linaelekezwa kuona hatua inayofuata ya Washington, huku Vatican ikiweka msimamo wazi: haitashiriki katika bodi hiyo mpya. Toa maoni yako #Habari
    0 Σχόλια 0 Μοιράστηκε 152 Views
  • Marekani yakaribia vita kubwa na Iran - Ripoti ya Axios.

    Axios imeripoti kuwa mvutano kati ya Marekani na Iran unaongezeka kwa kasi, hali inayoweza kuisukuma dunia kushuhudia vita kubwa kati ya mataifa hayo mawili yenye ushawishi mkubwa kisiasa na kijeshi.

    Kwa mujibu wa ripoti hiyo, hatua za kidiplomasia zimeanza kupungua huku msimamo wa pande zote ukiwa mkali zaidi, hasa kuhusu masuala ya nyuklia na usalama wa eneo la Mashariki ya Kati.

    Chanzo hicho kimeeleza kuwa hofu kubwa inahusiana na mpango wa nyuklia wa Iran, ambao kwa muda mrefu umekuwa ukipingwa vikali na Marekani pamoja na washirika wake. Marekani imekuwa ikiishutumu Iran kwa kuendeleza teknolojia inayoweza kutumika kutengeneza silaha za nyuklia, jambo ambalo Tehran imekuwa ikilikanusha mara kwa mara.

    Mchambuzi mmoja wa masuala ya kimataifa alinukuliwa akisema, "Ikiwa hakutakuwa na suluhu ya haraka ya kidiplomasia, uwezekano wa mapambano ya moja kwa moja unaongezeka kila siku."

    Ripoti hiyo pia inaeleza kuwa Marekani imeongeza uwepo wake wa kijeshi katika maeneo muhimu ya kimkakati, huku Iran nayo ikitoa onyo kali dhidi ya kile ilichokiita vitisho vya wazi.

    Afisa mmoja wa ngazi ya juu alinukuliwa akisema, "Tuko tayari kulinda maslahi yetu na washirika wetu kwa gharama yoyote."

    Kwa upande wake, Iran imeonya kuwa haitakubali kushinikizwa au kutishwa, ikisisitiza kuwa itajibu hatua yoyote ya kijeshi kwa nguvu inayostahili.

    Jamii ya kimataifa sasa inatazama kwa karibu hali hiyo, huku Wachambuzi wakionya kuwa mgogoro wa wazi kati ya Marekani na Iran unaweza kuathiri soko la mafuta, usalama wa kimataifa na uthabiti wa kisiasa katika eneo lote la Mashariki ya Kati.

    Hadi sasa, hakuna tamko rasmi la vita lililotolewa, lakini mwelekeo wa matukio unaonyesha kuwa mvutano huo unaweza kuingia katika hatua mpya yenye athari kubwa kwa dunia nzima.

    Toa maoni yako
    #Habari
    #Iran #America #Vita #Nyuklia #SiasaZaKimataifa
    Marekani yakaribia vita kubwa na Iran - Ripoti ya Axios. Axios imeripoti kuwa mvutano kati ya Marekani na Iran unaongezeka kwa kasi, hali inayoweza kuisukuma dunia kushuhudia vita kubwa kati ya mataifa hayo mawili yenye ushawishi mkubwa kisiasa na kijeshi. Kwa mujibu wa ripoti hiyo, hatua za kidiplomasia zimeanza kupungua huku msimamo wa pande zote ukiwa mkali zaidi, hasa kuhusu masuala ya nyuklia na usalama wa eneo la Mashariki ya Kati. Chanzo hicho kimeeleza kuwa hofu kubwa inahusiana na mpango wa nyuklia wa Iran, ambao kwa muda mrefu umekuwa ukipingwa vikali na Marekani pamoja na washirika wake. Marekani imekuwa ikiishutumu Iran kwa kuendeleza teknolojia inayoweza kutumika kutengeneza silaha za nyuklia, jambo ambalo Tehran imekuwa ikilikanusha mara kwa mara. Mchambuzi mmoja wa masuala ya kimataifa alinukuliwa akisema, "Ikiwa hakutakuwa na suluhu ya haraka ya kidiplomasia, uwezekano wa mapambano ya moja kwa moja unaongezeka kila siku." Ripoti hiyo pia inaeleza kuwa Marekani imeongeza uwepo wake wa kijeshi katika maeneo muhimu ya kimkakati, huku Iran nayo ikitoa onyo kali dhidi ya kile ilichokiita vitisho vya wazi. Afisa mmoja wa ngazi ya juu alinukuliwa akisema, "Tuko tayari kulinda maslahi yetu na washirika wetu kwa gharama yoyote." Kwa upande wake, Iran imeonya kuwa haitakubali kushinikizwa au kutishwa, ikisisitiza kuwa itajibu hatua yoyote ya kijeshi kwa nguvu inayostahili. Jamii ya kimataifa sasa inatazama kwa karibu hali hiyo, huku Wachambuzi wakionya kuwa mgogoro wa wazi kati ya Marekani na Iran unaweza kuathiri soko la mafuta, usalama wa kimataifa na uthabiti wa kisiasa katika eneo lote la Mashariki ya Kati. Hadi sasa, hakuna tamko rasmi la vita lililotolewa, lakini mwelekeo wa matukio unaonyesha kuwa mvutano huo unaweza kuingia katika hatua mpya yenye athari kubwa kwa dunia nzima. Toa maoni yako #Habari #Iran #America #Vita #Nyuklia #SiasaZaKimataifa
    0 Σχόλια 0 Μοιράστηκε 131 Views
  • Iran na Urusi kufanya mazoezi ya pamoja ya kijeshi nje ya Bahari ya Oman.

    Iran na Urusi zinatarajiwa kuanza mazoezi ya pamoja ya kijeshi kesho Alhamisi katika maeneo ya nje ya Bahari ya Oman na kaskazini mwa Bahari ya Hindi, hatua inayotafsiriwa kama ishara ya kuimarika kwa ushirikiano wa kiusalama kati ya mataifa hayo mawili.

    Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Fars, tangazo hilo limekuja siku chache baada ya Kikosi Maalum cha Walinzi wa Mapinduzi wa Iran kufanya mazoezi ya kijeshi katika mlango wa bahari wa Hormuz, eneo nyeti linalopitisha sehemu kubwa ya usafirishaji wa mafuta duniani.

    Kamanda wa Jeshi la Wanamaji la Iran, Hassan Maghsoodloo, ameeleza madhumuni ya mazoezi hayo kwa kusema: “Lengo la mazoezi haya ni kuunda nguvu za pamoja na kuimarisha uratibu wa hatua za pamoja ili kukabiliana na vitisho vinavyoathiri usalama wa majini na usalama wa nchi zetu mbili.”

    Ameongeza kuwa: "Mazoezi haya pia yanalenga kupambana na ugaidi na kuimarisha utulivu katika eneo la kimkakati la bahari.”

    Kauli hiyo inaonesha kuwa Tehran na Moscow zinaangazia zaidi usalama wa bahari na kulinda maslahi yao ya kiuchumi na kijeshi katika njia kuu za usafirishaji wa kimataifa.

    Hatua hizi zinakuja wakati wa mvutano unaoendelea kati ya Marekani na Iran. Washington imetishia hatua za kijeshi dhidi ya Tehran, ikiishutumu kwa kile ilichodai kuwa ni ukiukwaji wa haki za Waandamanaji pamoja na kushindwa kufikia makubaliano kuhusu mpango wake wa nyuklia.

    Kwa upande wake, Iran imekuwa ikisisitiza mara kwa mara uwezekano wa kuufunga mlango wa bahari wa Hormuz wakati wa mvutano mkali na Marekani. Hata hivyo, hadi sasa, haijawahi kuchukua hatua ya kulifunga rasmi lango hilo muhimu la kimataifa.

    Mazoezi haya yanaonekana kuwa na ujumbe wa wazi wa kisiasa na kijeshi kuonesha mshikamano wa Iran na Urusi katika kukabiliana na shinikizo la Magharibi, huku yakituma ishara kwa mataifa mengine kuhusu uwezo wao wa pamoja katika kulinda maslahi ya kimkakati katika Bahari ya Hindi na Ghuba ya Oman.

    Wachambuzi wa masuala ya ulinzi wanaona kuwa ushirikiano huu unaweza kuathiri mizania ya nguvu katika eneo hilo, hasa katika kipindi ambacho diplomasia ya nyuklia bado haijafikia muafaka wa kudumu.

    Toa maoni yako
    #Habari
    Iran na Urusi kufanya mazoezi ya pamoja ya kijeshi nje ya Bahari ya Oman. Iran na Urusi zinatarajiwa kuanza mazoezi ya pamoja ya kijeshi kesho Alhamisi katika maeneo ya nje ya Bahari ya Oman na kaskazini mwa Bahari ya Hindi, hatua inayotafsiriwa kama ishara ya kuimarika kwa ushirikiano wa kiusalama kati ya mataifa hayo mawili. Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Fars, tangazo hilo limekuja siku chache baada ya Kikosi Maalum cha Walinzi wa Mapinduzi wa Iran kufanya mazoezi ya kijeshi katika mlango wa bahari wa Hormuz, eneo nyeti linalopitisha sehemu kubwa ya usafirishaji wa mafuta duniani. Kamanda wa Jeshi la Wanamaji la Iran, Hassan Maghsoodloo, ameeleza madhumuni ya mazoezi hayo kwa kusema: “Lengo la mazoezi haya ni kuunda nguvu za pamoja na kuimarisha uratibu wa hatua za pamoja ili kukabiliana na vitisho vinavyoathiri usalama wa majini na usalama wa nchi zetu mbili.” Ameongeza kuwa: "Mazoezi haya pia yanalenga kupambana na ugaidi na kuimarisha utulivu katika eneo la kimkakati la bahari.” Kauli hiyo inaonesha kuwa Tehran na Moscow zinaangazia zaidi usalama wa bahari na kulinda maslahi yao ya kiuchumi na kijeshi katika njia kuu za usafirishaji wa kimataifa. Hatua hizi zinakuja wakati wa mvutano unaoendelea kati ya Marekani na Iran. Washington imetishia hatua za kijeshi dhidi ya Tehran, ikiishutumu kwa kile ilichodai kuwa ni ukiukwaji wa haki za Waandamanaji pamoja na kushindwa kufikia makubaliano kuhusu mpango wake wa nyuklia. Kwa upande wake, Iran imekuwa ikisisitiza mara kwa mara uwezekano wa kuufunga mlango wa bahari wa Hormuz wakati wa mvutano mkali na Marekani. Hata hivyo, hadi sasa, haijawahi kuchukua hatua ya kulifunga rasmi lango hilo muhimu la kimataifa. Mazoezi haya yanaonekana kuwa na ujumbe wa wazi wa kisiasa na kijeshi kuonesha mshikamano wa Iran na Urusi katika kukabiliana na shinikizo la Magharibi, huku yakituma ishara kwa mataifa mengine kuhusu uwezo wao wa pamoja katika kulinda maslahi ya kimkakati katika Bahari ya Hindi na Ghuba ya Oman. Wachambuzi wa masuala ya ulinzi wanaona kuwa ushirikiano huu unaweza kuathiri mizania ya nguvu katika eneo hilo, hasa katika kipindi ambacho diplomasia ya nyuklia bado haijafikia muafaka wa kudumu. Toa maoni yako #Habari
    0 Σχόλια 0 Μοιράστηκε 139 Views
  • Kylian Mbappé amshambulia Gianluca Prestianni kabla ya mechi marudiano huko Bernabéu.

    Mvutano umeibuka kabla ya pambano kubwa linalotarajiwa kupigwa katika dimba la Santiago Bernabéu Stadium, baada ya mshambuliaji wa klabu ya Real Madrid, Kylian Mbappé kutoa kauli nzito dhidi ya kijana Gianluca Prestianni kisa sakata lake na Vini.

    Katika mahojiano aliyofanya na TNT Sports Brazil, Mbappé hakusita kueleza msimamo wake kuhusu uwezekano wa Prestianni kucheza katika mechi hiyo muhimu.

    “Natumaini sitamuona Prestianni katika Uwanja wa Bernabéu wiki ijayo… kwa hakika hapaswi kucheza katika Uwanja bora zaidi duniani, hastahili kuwa sehemu ya mchezo huo.”

    Kauli hiyo imezua mjadala mpana miongoni mwa mashabiki wa soka, hasa ikizingatiwa ukubwa wa mechi hiyo inayotarajiwa kuzikutanisha klabu mbili zenye historia kubwa barani Ulaya.

    Mbappé aliendelea kusisitiza kuwa, licha ya matarajio yake ya kushuhudia mechi bora, anaamini Prestianni hapaswi kupewa nafasi ya kushiriki.

    “Nina uhakika utakuwa mchezo wa kuvutia sana, klabu mbili za kihistoria zikiwa Uwanjani, lakini kwa mtazamo wangu Prestianni anapaswa kuwa nje.”

    Kauli yake ya mwisho ndiyo imeongeza moto zaidi katika sakata hilo, akitoa maoni yanayoashiria kuwa anatamani hatua kali zichukuliwe.

    “Haya ni maoni yangu, natumaini atafungiwa.”

    Hadi sasa hakuna tamko rasmi kutoka upande wa Prestianni au klabu yake kujibu kauli hizo. Hata hivyo, presha imeongezeka kuelekea mchezo huo, huku mashabiki wakisubiri kuona kama maneno hayo yatageuka kuwa chachu ya ushindani mkali zaidi Uwanjani.

    Toa maoni yako
    #Sports
    #Habari
    Kylian Mbappé amshambulia Gianluca Prestianni kabla ya mechi marudiano huko Bernabéu. Mvutano umeibuka kabla ya pambano kubwa linalotarajiwa kupigwa katika dimba la Santiago Bernabéu Stadium, baada ya mshambuliaji wa klabu ya Real Madrid, Kylian Mbappé kutoa kauli nzito dhidi ya kijana Gianluca Prestianni kisa sakata lake na Vini. Katika mahojiano aliyofanya na TNT Sports Brazil, Mbappé hakusita kueleza msimamo wake kuhusu uwezekano wa Prestianni kucheza katika mechi hiyo muhimu. “Natumaini sitamuona Prestianni katika Uwanja wa Bernabéu wiki ijayo… kwa hakika hapaswi kucheza katika Uwanja bora zaidi duniani, hastahili kuwa sehemu ya mchezo huo.” Kauli hiyo imezua mjadala mpana miongoni mwa mashabiki wa soka, hasa ikizingatiwa ukubwa wa mechi hiyo inayotarajiwa kuzikutanisha klabu mbili zenye historia kubwa barani Ulaya. Mbappé aliendelea kusisitiza kuwa, licha ya matarajio yake ya kushuhudia mechi bora, anaamini Prestianni hapaswi kupewa nafasi ya kushiriki. “Nina uhakika utakuwa mchezo wa kuvutia sana, klabu mbili za kihistoria zikiwa Uwanjani, lakini kwa mtazamo wangu Prestianni anapaswa kuwa nje.” Kauli yake ya mwisho ndiyo imeongeza moto zaidi katika sakata hilo, akitoa maoni yanayoashiria kuwa anatamani hatua kali zichukuliwe. “Haya ni maoni yangu, natumaini atafungiwa.” Hadi sasa hakuna tamko rasmi kutoka upande wa Prestianni au klabu yake kujibu kauli hizo. Hata hivyo, presha imeongezeka kuelekea mchezo huo, huku mashabiki wakisubiri kuona kama maneno hayo yatageuka kuwa chachu ya ushindani mkali zaidi Uwanjani. Toa maoni yako #Sports #Habari
    0 Σχόλια 0 Μοιράστηκε 105 Views
  • Wakili Craig Kitambala aomba ridhaa ya Fally Ipupa kufungua kesi dhidi ya Mwanahabari Gautier Sey.

    Hatua mpya ya kisheria imeibuka katika tasnia ya burudani ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, baada ya Wakili Craig Kitambala kuomba ruhusa rasmi kutoka kwa Msanii maarufu Fally Ipupa ili kuanzisha mashitaka dhidi ya Mwanahabari Gautier Sey kwa tuhuma za kumchafulia jina.

    Kwa mujibu wa taarifa zilizosambaa kwenye mitandao ya kijamii, Wakili Kitambala anataka kuchukua hatua za kisheria kufuatia kauli na maudhui yaliyotolewa na Gautier Sey ambayo yanaelezwa kuwa yamelenga kumdhalilisha au kumharibia taswira Msanii huyo mbele ya umma.

    Katika maelezo yake, Wakili Kitambala ameeleza kuwa anasubiri kibali cha moja kwa moja kutoka kwa Fally Ipupa kabla ya kuwasilisha rasmi malalamiko Mahakamani.

    “Ninaomba idhini ya Fally Ipupa ili niweze kuanzisha rasmi mashitaka ya kashfa dhidi ya Mwanahabari Gautier Sey,” imeelezwa katika ujumbe unaohusishwa na Wakili huyo.

    Hatua hiyo inakuja wakati mijadala mikali ikiendelea mtandaoni kuhusu uhuru wa vyombo vya habari dhidi ya heshima na hadhi ya watu maarufu. Ikiwa kibali hicho kitatolewa, kesi hiyo inaweza kufungua mjadala mpana kuhusu mipaka ya maoni ya Wanahabari na wajibu wao katika kuripoti habari zinazowahusu watu mashuhuri.

    Kwa sasa, Fally Ipupa hajatoa tamko rasmi hadharani kuhusu iwapo atatoa ruhusa hiyo au la. Vivyo hivyo, Gautier Sey naye hajajibu moja kwa moja tuhuma zinazomkabili.

    Endapo shauri hilo litafunguliwa, linaweza kuwa miongoni mwa kesi zinazovuta hisia kubwa katika tasnia ya muziki na vyombo vya habari nchini DR Congo.

    Toa maoni yako
    #Music
    Wakili Craig Kitambala aomba ridhaa ya Fally Ipupa kufungua kesi dhidi ya Mwanahabari Gautier Sey. Hatua mpya ya kisheria imeibuka katika tasnia ya burudani ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, baada ya Wakili Craig Kitambala kuomba ruhusa rasmi kutoka kwa Msanii maarufu Fally Ipupa ili kuanzisha mashitaka dhidi ya Mwanahabari Gautier Sey kwa tuhuma za kumchafulia jina. Kwa mujibu wa taarifa zilizosambaa kwenye mitandao ya kijamii, Wakili Kitambala anataka kuchukua hatua za kisheria kufuatia kauli na maudhui yaliyotolewa na Gautier Sey ambayo yanaelezwa kuwa yamelenga kumdhalilisha au kumharibia taswira Msanii huyo mbele ya umma. Katika maelezo yake, Wakili Kitambala ameeleza kuwa anasubiri kibali cha moja kwa moja kutoka kwa Fally Ipupa kabla ya kuwasilisha rasmi malalamiko Mahakamani. “Ninaomba idhini ya Fally Ipupa ili niweze kuanzisha rasmi mashitaka ya kashfa dhidi ya Mwanahabari Gautier Sey,” imeelezwa katika ujumbe unaohusishwa na Wakili huyo. Hatua hiyo inakuja wakati mijadala mikali ikiendelea mtandaoni kuhusu uhuru wa vyombo vya habari dhidi ya heshima na hadhi ya watu maarufu. Ikiwa kibali hicho kitatolewa, kesi hiyo inaweza kufungua mjadala mpana kuhusu mipaka ya maoni ya Wanahabari na wajibu wao katika kuripoti habari zinazowahusu watu mashuhuri. Kwa sasa, Fally Ipupa hajatoa tamko rasmi hadharani kuhusu iwapo atatoa ruhusa hiyo au la. Vivyo hivyo, Gautier Sey naye hajajibu moja kwa moja tuhuma zinazomkabili. Endapo shauri hilo litafunguliwa, linaweza kuwa miongoni mwa kesi zinazovuta hisia kubwa katika tasnia ya muziki na vyombo vya habari nchini DR Congo. Toa maoni yako #Music
    0 Σχόλια 0 Μοιράστηκε 95 Views
  • Ushirikiano wa RDC – Monaco unakabiliwa na changamoto?

    Ushirikiano kati ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na klabu ya AS Monaco unaweza kuwa kwenye hatari, ikizingatiwa taarifa zilizotolewa na Gazeti la L’Équipe la Nchini Ufaransa.

    Taarifa hizo zinaonyesha kwamba malalamiko ya "kuficha fedha", "kufurushwa fedha za umma" (Wizi) na "ufisadi" yamewasilishwa katika Tume ya Ufilisi wa Kifedha ya Taifa (PNF) mnamo Septemba 2025.

    Malalamiko haya yanahusu mkataba uliosainiwa kati ya Wizara ya Michezo ya RDC na AS Monaco mwezi Juni mwaka jana.

    Baada ya miezi kadhaa ya uchambuzi, PNF imetuma ripoti rasmi kwa mamlaka za Monaco. Hivyo, sasa kesi hiyo ipo mikononi mwa Mahakama ya Dola la Nchi ya Monaco.

    Hali hii inachukua sura mpya katika uhusiano wa michezo na uwekezaji kati ya RDC na Monaco, huku mashabiki na wanasiasa wakilenga kuona matokeo ya kesi hii.

    Toa maoni yako
    #Habari
    Ushirikiano wa RDC – Monaco unakabiliwa na changamoto? Ushirikiano kati ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na klabu ya AS Monaco unaweza kuwa kwenye hatari, ikizingatiwa taarifa zilizotolewa na Gazeti la L’Équipe la Nchini Ufaransa. Taarifa hizo zinaonyesha kwamba malalamiko ya "kuficha fedha", "kufurushwa fedha za umma" (Wizi) na "ufisadi" yamewasilishwa katika Tume ya Ufilisi wa Kifedha ya Taifa (PNF) mnamo Septemba 2025. Malalamiko haya yanahusu mkataba uliosainiwa kati ya Wizara ya Michezo ya RDC na AS Monaco mwezi Juni mwaka jana. Baada ya miezi kadhaa ya uchambuzi, PNF imetuma ripoti rasmi kwa mamlaka za Monaco. Hivyo, sasa kesi hiyo ipo mikononi mwa Mahakama ya Dola la Nchi ya Monaco. Hali hii inachukua sura mpya katika uhusiano wa michezo na uwekezaji kati ya RDC na Monaco, huku mashabiki na wanasiasa wakilenga kuona matokeo ya kesi hii. Toa maoni yako #Habari
    0 Σχόλια 0 Μοιράστηκε 87 Views
  • Umoja wa Ulaya wafadhili euro milioni 81 kwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

    Umoja wa Ulaya (EU) umethibitisha kutoa ufadhili wa Euro milioni 81 kwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (RDC), kwa ajili ya kusaidia mpango wa msaada wa kibinadamu katika maeneo ya mashariki ambako mizozo inazidi kuathiri Wananchi.

    Akizungumza kuhusu hatua hii, Msemaji wa Umoja wa Ulaya amesema, “Hii ni hatua yetu ya dhati ya kuhakikisha kwamba jamii zilizo hatarini zinapata msaada wa dharura na huduma za msingi zinazohitajika, hususan kwa wakimbizi na watu waliokumbwa na mizozo.”

    Aidha, Umoja wa Ulaya umesisitiza umuhimu wa kushirikiana na mamlaka za RDC pamoja na mashirika ya misaada ya kibinadamu ili kuhakikisha fedha hizi zinatumika kwa ufanisi na kufikia jamii zinazohitaji zaidi.

    Msemaji huyo aliongeza, “Tutaendelea kushirikiana na washirika wetu wa ndani na kimataifa kuhakikisha kwamba msaada unawafikia walengwa haraka na kwa uwazi, ili kupunguza madhara yanayosababishwa na mapigano yanayoendelea mashariki mwa nchi.”

    Hii ni sehemu ya jitihada kubwa za kimataifa zinazolenga kupunguza mateso ya kibinadamu na kuboresha hali ya maisha kwa familia zinazokabiliwa na mizozo, haswa katika kanda zenye migogoro ya muda mrefu.

    Toa maoni yako
    #Habari
    Umoja wa Ulaya wafadhili euro milioni 81 kwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo. Umoja wa Ulaya (EU) umethibitisha kutoa ufadhili wa Euro milioni 81 kwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (RDC), kwa ajili ya kusaidia mpango wa msaada wa kibinadamu katika maeneo ya mashariki ambako mizozo inazidi kuathiri Wananchi. Akizungumza kuhusu hatua hii, Msemaji wa Umoja wa Ulaya amesema, “Hii ni hatua yetu ya dhati ya kuhakikisha kwamba jamii zilizo hatarini zinapata msaada wa dharura na huduma za msingi zinazohitajika, hususan kwa wakimbizi na watu waliokumbwa na mizozo.” Aidha, Umoja wa Ulaya umesisitiza umuhimu wa kushirikiana na mamlaka za RDC pamoja na mashirika ya misaada ya kibinadamu ili kuhakikisha fedha hizi zinatumika kwa ufanisi na kufikia jamii zinazohitaji zaidi. Msemaji huyo aliongeza, “Tutaendelea kushirikiana na washirika wetu wa ndani na kimataifa kuhakikisha kwamba msaada unawafikia walengwa haraka na kwa uwazi, ili kupunguza madhara yanayosababishwa na mapigano yanayoendelea mashariki mwa nchi.” Hii ni sehemu ya jitihada kubwa za kimataifa zinazolenga kupunguza mateso ya kibinadamu na kuboresha hali ya maisha kwa familia zinazokabiliwa na mizozo, haswa katika kanda zenye migogoro ya muda mrefu. Toa maoni yako #Habari
    0 Σχόλια 0 Μοιράστηκε 133 Views
  • “Nimemsikia Rais wa Marekani akisema, kwa zaidi ya miaka 47, Marekani imeshindwa kuivunja Jamhuri ya Kiislamu ya Iran. Sasa namuambia kwamba: hamtokuja kufanikiwa kamwe”

    - Ayatollah Sayeed Ali Khamenei, Kiongozi Mkuu wa Iran.

    Toa maoni yako
    #Habari
    #Habari
    “Nimemsikia Rais wa Marekani akisema, kwa zaidi ya miaka 47, Marekani imeshindwa kuivunja Jamhuri ya Kiislamu ya Iran. Sasa namuambia kwamba: hamtokuja kufanikiwa kamwe” - Ayatollah Sayeed Ali Khamenei, Kiongozi Mkuu wa Iran. Toa maoni yako #Habari #Habari
    0 Σχόλια 0 Μοιράστηκε 101 Views
Αναζήτηση αποτελεσμάτων