• PSG ilitoa Ofa ya €250 milioni kwa Lamine Yamal, Barcelona wakataa - Laporta afunguka.

    Rais wa klabu ya FC Barcelona, Joan Laporta, ameweka wazi kuwa klabu ya Paris Saint-Germain (PSG) iliwahi kuwasilisha ofa nono ya euro milioni 250 kwa ajili ya kinda nyota Lamine Yamal lakini Barca waliikataa bila kusita.

    Akizungumza kuhusu tukio hilo, Laporta amesema ofa hiyo iliwasilishwa takribani miaka miwili iliyopita wakati Yamal akiwa na umri wa miaka 17 pekee.

    “Lamine alikuwa na miaka 17, miaka miwili iliyopita… PSG walituma pendekezo la euro milioni 250 na tulisema hapana. Nakumbuka baadhi ya watu walifikiri tulikuwa tumepoteza akili,” ameeleza Laporta.

    Kwa mujibu wa Kiongozi huyo wa Barcelona, uamuzi wa kuikataa ofa hiyo haukuwa wa kifedha bali wa kimkakati na kihistoria. Klabu hiyo inaamini Yamal ni sehemu ya mradi wa muda mrefu wa kurejesha enzi za mafanikio Camp Nou.

    “Kwa sisi, amekuwa asiyeuzwa. Hagusiki,” alisisitiza Laporta.

    Kwa kuzingatia ukubwa wa ofa hiyo, wengi walihoji kama Barcelona walipaswa kukubali kiasi hicho kikubwa cha fedha, hasa katika kipindi ambacho klabu hiyo ilikuwa inapitia changamoto za kifedha. Hata hivyo, maendeleo ya haraka ya Yamal ndani ya kikosi cha kwanza na mchango wake katika mafanikio ya timu yameanza kuhalalisha msimamo wa uongozi.

    Yamal ameonekana kuwa moja ya vipaji adimu vilivyotoka "Akademi" ya La Masia, akionesha utulivu, ubunifu na ujasiri mkubwa licha ya umri wake mdogo.

    Kauli ya Laporta inaashiria wazi kwamba Barcelona haioni thamani ya Yamal kwa mizani ya fedha pekee. Kwao, ni Mrithi wa kizazi kipya cha Nyota wa klabu hiyo, Mchezaji wa kujengwa kuzunguka mradi wa baadaye.

    Katika soko la sasa la uhamisho, euro milioni 250 ni kiwango kinachoweza kubadilisha historia ya klabu yoyote. Lakini kwa Barcelona, Lamine Yamal si bidhaa ya kuuzwa ni alama ya mustakabali wao.

    Toa maoni yako
    #Sports
    PSG ilitoa Ofa ya €250 milioni kwa Lamine Yamal, Barcelona wakataa - Laporta afunguka. Rais wa klabu ya FC Barcelona, Joan Laporta, ameweka wazi kuwa klabu ya Paris Saint-Germain (PSG) iliwahi kuwasilisha ofa nono ya euro milioni 250 kwa ajili ya kinda nyota Lamine Yamal lakini Barca waliikataa bila kusita. Akizungumza kuhusu tukio hilo, Laporta amesema ofa hiyo iliwasilishwa takribani miaka miwili iliyopita wakati Yamal akiwa na umri wa miaka 17 pekee. “Lamine alikuwa na miaka 17, miaka miwili iliyopita… PSG walituma pendekezo la euro milioni 250 na tulisema hapana. Nakumbuka baadhi ya watu walifikiri tulikuwa tumepoteza akili,” ameeleza Laporta. Kwa mujibu wa Kiongozi huyo wa Barcelona, uamuzi wa kuikataa ofa hiyo haukuwa wa kifedha bali wa kimkakati na kihistoria. Klabu hiyo inaamini Yamal ni sehemu ya mradi wa muda mrefu wa kurejesha enzi za mafanikio Camp Nou. “Kwa sisi, amekuwa asiyeuzwa. Hagusiki,” alisisitiza Laporta. Kwa kuzingatia ukubwa wa ofa hiyo, wengi walihoji kama Barcelona walipaswa kukubali kiasi hicho kikubwa cha fedha, hasa katika kipindi ambacho klabu hiyo ilikuwa inapitia changamoto za kifedha. Hata hivyo, maendeleo ya haraka ya Yamal ndani ya kikosi cha kwanza na mchango wake katika mafanikio ya timu yameanza kuhalalisha msimamo wa uongozi. Yamal ameonekana kuwa moja ya vipaji adimu vilivyotoka "Akademi" ya La Masia, akionesha utulivu, ubunifu na ujasiri mkubwa licha ya umri wake mdogo. Kauli ya Laporta inaashiria wazi kwamba Barcelona haioni thamani ya Yamal kwa mizani ya fedha pekee. Kwao, ni Mrithi wa kizazi kipya cha Nyota wa klabu hiyo, Mchezaji wa kujengwa kuzunguka mradi wa baadaye. Katika soko la sasa la uhamisho, euro milioni 250 ni kiwango kinachoweza kubadilisha historia ya klabu yoyote. Lakini kwa Barcelona, Lamine Yamal si bidhaa ya kuuzwa ni alama ya mustakabali wao. Toa maoni yako #Sports
    0 Commentarii 0 Distribuiri 114 Views
  • Liverpool wamepanga kuwatajirisha PSG..

    Kupitia Fichajes imeripotiwa kuwa klabu ya Liverpool ipo tayari kutoa dau kubwa la hadi €159M ili kumpata kiungo wa Paris Saint Germain, Joao Neves.

    Liverpool wapo tayari kutajirisha vilabu vya ulaya .

    Liverpool wamepanga kuwatajirisha PSG.. Kupitia Fichajes imeripotiwa kuwa klabu ya Liverpool ipo tayari kutoa dau kubwa la hadi €159M ili kumpata kiungo wa Paris Saint Germain, Joao Neves. Liverpool wapo tayari kutajirisha vilabu vya ulaya 😐.
    0 Commentarii 0 Distribuiri 443 Views
  • Bournemouth imekataa ofa ya £50M kutoka kwa Tottenham Hotspur pamoja na Manchester United juu ya huduma ya Antoine Semenyo dirisha dogo.

    Tayari Bournemouth imeshapata kitita cha pesa £200M kutokana na mauzo ya vipaji vyao.

    Milos Kerkez - aliuzwa kwenda Liverpool ada £40M.
    Dean Huijsen -aliuzwa kwenda Real Madrid ada £50M.
    Illia Zabarnyi -aliuzwa kwenda PSG ada £58M.
    Dango Ouattara aliuzwa kwenda Brentford ada £42M.

    (Source: Telegraph)
    🚨 Bournemouth imekataa ofa ya £50M kutoka kwa Tottenham Hotspur pamoja na Manchester United juu ya huduma ya Antoine Semenyo dirisha dogo. Tayari Bournemouth imeshapata kitita cha pesa £200M kutokana na mauzo ya vipaji vyao. 🇭🇺 Milos Kerkez - aliuzwa kwenda Liverpool ada £40M. 🇪🇸 Dean Huijsen -aliuzwa kwenda Real Madrid ada £50M. 🇺🇦 Illia Zabarnyi -aliuzwa kwenda PSG ada £58M. 🇧🇫 Dango Ouattara aliuzwa kwenda Brentford ada £42M. (Source: Telegraph)
    0 Commentarii 0 Distribuiri 667 Views
  • 𝐁𝐑𝐄𝐀𝐊𝐈𝐍𝐆: Willian Pacho amefikia makubaliano ya kuongeza kandarasi ya miaka 4 kusalia PSG hadi 2030.
    🚨💣 𝐁𝐑𝐄𝐀𝐊𝐈𝐍𝐆: Willian Pacho amefikia makubaliano ya kuongeza kandarasi ya miaka 4 kusalia PSG hadi 2030.
    0 Commentarii 0 Distribuiri 708 Views
  • Lamine Yamal ni mmoja wa mawinga bora kabisa wa kulia kwenye soka kwa sasa huku Nuno Mendes akiwa beki bora kabisa wa kushoto kwa sasa Duniani wakati wawili hawa wakikutana mara mbili hivi karibuni kwenye mchezo wa UEFA Nations League (Fainali, Ureno vs Uhispania) na kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya (UCL), (Barcelona vs PSG).

    Kwenye mechi zote mbili Yamal ameshindwa kutamba mbele ya Mreno huyo ambaye alifunga goli na kutoa 'assist' na kuwa nyota wa mchezo huku timu yake ikishinda mara zote wakati Yamal akitoka patupu bila goli huku timu yake ikipoteza.

    Je unadhani kuna winga anaweza kummudu Nuno Mendes kwa sasa?

    FAINALI: #UEFANATIONS LEAGUE
    Ureno 2-2 Uhispania (P 5-3)
    Mendes
    Ronaldo

    Zubimendi
    Oyarzabal

    #UCL
    Barcelona 1-2 PSG
    19' Torres
    38' Mayulu( Mendes)
    90' Ramos ( Hakimi)


    #SportsElite
    Lamine Yamal ni mmoja wa mawinga bora kabisa wa kulia kwenye soka kwa sasa huku Nuno Mendes akiwa beki bora kabisa wa kushoto kwa sasa Duniani wakati wawili hawa wakikutana mara mbili hivi karibuni kwenye mchezo wa UEFA Nations League (Fainali, Ureno vs Uhispania) na kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya (UCL), (Barcelona vs PSG). Kwenye mechi zote mbili Yamal ameshindwa kutamba mbele ya Mreno huyo ambaye alifunga goli na kutoa 'assist' na kuwa nyota wa mchezo huku timu yake ikishinda mara zote wakati Yamal akitoka patupu bila goli huku timu yake ikipoteza. ✍️ Je unadhani kuna winga anaweza kummudu Nuno Mendes kwa sasa? FAINALI: #UEFANATIONS LEAGUE Ureno 🇵🇹 2-2 🇪🇸 Uhispania (P 5-3) ⚽ Mendes ⚽ Ronaldo ⚽ Zubimendi ⚽ Oyarzabal #UCL Barcelona 🇪🇸 1-2 🇫🇷 PSG ⚽ 19' Torres ⚽ 38' Mayulu(🅰️ Mendes) ⚽ 90' Ramos (🅰️ Hakimi) #SportsElite
    0 Commentarii 0 Distribuiri 2K Views
  • Paris Saint-Germain pamoja na Aston Villa FC zipo mbioni kufikia makubaliano juu ya uhamisho wa Marco Asensio.

    Awali Villa ilituma ofa ya €15M lakini PSG imeomba €20M na uhamisho huo upo mbioni kukamilika.

    (Source: Tanziloic)

    #SportsElite
    🚨 Paris Saint-Germain pamoja na Aston Villa FC zipo mbioni kufikia makubaliano juu ya uhamisho wa Marco Asensio. Awali Villa ilituma ofa ya €15M lakini PSG imeomba €20M na uhamisho huo upo mbioni kukamilika. (Source: Tanziloic) #SportsElite
    0 Commentarii 0 Distribuiri 509 Views
  • Mechi za Barcelona tutakazo Anza nazo awamu ya kwanza

    Chelsea
    Paris Saint-Germain
    Eintracht Frankfurt
    Club Brugge
    Olympiacos
    Slavia Prague
    Copenhagen
    Newcastle

    Hapa PSG - Paris Saint-Germain na Chelsea Football Club ndio tishio la maisha yetu .

    #SportsElite
    🚨Mechi za Barcelona tutakazo Anza nazo awamu ya kwanza ❤️💙 🔥 ✈️ Chelsea 🏠 Paris Saint-Germain 🏠 Eintracht Frankfurt ✈️ Club Brugge 🏠 Olympiacos ✈️ Slavia Prague 🏠 Copenhagen ✈️ Newcastle Hapa PSG - Paris Saint-Germain na Chelsea Football Club ndio tishio la maisha yetu 🥶. #SportsElite
    0 Commentarii 0 Distribuiri 1K Views
  • 𝗗𝗘𝗔𝗟 𝗗𝗢𝗡𝗘: Paris FC imekamilisha usajili wa golikipa wa zamani wa PSG Trapp kutoka Eintracht Frankfurt.

    Kwa ada €1M.

    (Source: Paris FC)

    #SportsElite
    📝 𝗗𝗘𝗔𝗟 𝗗𝗢𝗡𝗘: Paris FC imekamilisha usajili wa golikipa wa zamani wa PSG Trapp kutoka Eintracht Frankfurt. Kwa ada €1M. 🧤🇩🇪 (Source: Paris FC) #SportsElite
    0 Commentarii 0 Distribuiri 297 Views
  • 𝐁𝐑𝐄𝐀𝐊𝐈𝐍𝐆: Gianluigi Donnarumma yuko mbioni kujiunga na Manchester City akitokea PSG.

    Golikipa huyo ameonesha nia ya kutaka kujiunga na miamba ya Manchester City.

    photo credit Madridista

    #SportsElite
    🚨💣 𝐁𝐑𝐄𝐀𝐊𝐈𝐍𝐆: Gianluigi Donnarumma yuko mbioni kujiunga na Manchester City akitokea PSG. Golikipa huyo ameonesha nia ya kutaka kujiunga na miamba ya Manchester City. 📷 photo credit Madridista 🙏 #SportsElite
    0 Commentarii 0 Distribuiri 400 Views
  • Tunaendelea tulipo ishia
    PSG…

    …2-0 TOTTENHAM. ⌛️
    Tunaendelea tulipo ishia PSG… 🤩🤯 …2-0 TOTTENHAM. ⏳⌛️🏆🏆
    0 Commentarii 0 Distribuiri 308 Views
  • Real Madrid pamoja na PSG ziko kwenye mbio za kuiwania saini ya beki Ibrahima Konaté.

    Kiwango cha ada ya uhamisho inaweza kutolewa na vilabu vyote viwili..

    (Source: Diario AS)

    #SportsElite
    🚨 Real Madrid pamoja na PSG ziko kwenye mbio za kuiwania saini ya beki Ibrahima Konaté. 😳🇫🇷 Kiwango cha ada ya uhamisho inaweza kutolewa na vilabu vyote viwili.. (Source: Diario AS) #SportsElite
    0 Commentarii 0 Distribuiri 402 Views
  • Meneja wa Paris Saint Germain, Luis Enrique ameweka wazi kuwa Uongozi wa klabu hiyo unamuunga mkono kwenye uamuzi wake wa kuachana na Golikipa Gianluigi Donnarumma kutokuwa sehemu ya kikosi cha Timu hiyo hivyo ataanza kwa kuukosa mchezo wa UEFA Super Cup.

    Kipa huyo raia wa Italia aliachwa nje ya kikosi kilichosafiri hadi Udine kwa mechi ya kirafiki leo dhidi ya Tottenham, huku Magolikipa Lucas Chevalier na Renato Marin wakichaguliwa badala yake.

    Katika chapisho lake kwenye mtandao wake wa Instagram, Donnarumma alisema "amesikitishwa na kuvunjika moyo" kwa kukosekana kwake.
    Nyota huyo alikuwa mmoja wa wachezaji wa PSG walioshinda taji la Ligi ya Mabingwa msimu uliopita na uamuzi huo umekuja kwa mshtuko kutokana na hadhi yake na wasifu wake.

    Enrique alisema uamuzi wake ulikuwa na lengo la kutafuta Golikipa mwenye "wasifu tofauti" na Gigi.

    "Uongozi unaniunga mkono na tunajaribu kutafuta suluhu bora," aliongea kwenye mkutano wa wanahabari Jumanne.

    "Ni uamuzi mgumu, namkubali Donnarumma kwani ni mmoja wa makipa bora na mtu bora zaidi. Lakini tulikuwa tunatafuta wasifu tofauti, na ni vigumu sana kuchukua maamuzi ya aina hii." - alimaliza kwa kusema hivyo.

    #SportsElite
    🚨🚨Meneja wa Paris Saint Germain, Luis Enrique ameweka wazi kuwa Uongozi wa klabu hiyo unamuunga mkono kwenye uamuzi wake wa kuachana na Golikipa Gianluigi Donnarumma kutokuwa sehemu ya kikosi cha Timu hiyo hivyo ataanza kwa kuukosa mchezo wa UEFA Super Cup. Kipa huyo raia wa Italia aliachwa nje ya kikosi kilichosafiri hadi Udine kwa mechi ya kirafiki leo dhidi ya Tottenham, huku Magolikipa Lucas Chevalier na Renato Marin wakichaguliwa badala yake. Katika chapisho lake kwenye mtandao wake wa Instagram, Donnarumma alisema "amesikitishwa na kuvunjika moyo" kwa kukosekana kwake. Nyota huyo alikuwa mmoja wa wachezaji wa PSG walioshinda taji la Ligi ya Mabingwa msimu uliopita na uamuzi huo umekuja kwa mshtuko kutokana na hadhi yake na wasifu wake. Enrique alisema uamuzi wake ulikuwa na lengo la kutafuta Golikipa mwenye "wasifu tofauti" na Gigi. "Uongozi unaniunga mkono na tunajaribu kutafuta suluhu bora," aliongea kwenye mkutano wa wanahabari Jumanne. "Ni uamuzi mgumu, namkubali Donnarumma kwani ni mmoja wa makipa bora na mtu bora zaidi. Lakini tulikuwa tunatafuta wasifu tofauti, na ni vigumu sana kuchukua maamuzi ya aina hii." - alimaliza kwa kusema hivyo. #SportsElite
    0 Commentarii 0 Distribuiri 1K Views
  • 𝗕𝗥𝗘𝗔𝗞𝗜𝗡𝗚: Manchester united bado wapo kwenye mazungumzo na PSG ili kumpata golikipa Gigi Donnarumma . Mchakato bado inaendelea

    (Source: x/JanAageFjortoft)

    #SportsElite
    🚨 𝗕𝗥𝗘𝗔𝗞𝗜𝗡𝗚: Manchester united bado wapo kwenye mazungumzo na PSG ili kumpata golikipa Gigi Donnarumma . Mchakato bado inaendelea ✅ (Source: x/JanAageFjortoft) #SportsElite
    0 Commentarii 0 Distribuiri 439 Views
  • Club ya Manchester city imeweka dau la €60M na offer mbali Bali kwa golikipa wa FC Porto Diogo Costa na pia Club ya PSG imehusishwa juu ya kumuhitaji golikipa huyo

    #SportsElite
    Club ya Manchester city imeweka dau la €60M na offer mbali Bali kwa golikipa wa FC Porto Diogo Costa na pia Club ya PSG imehusishwa juu ya kumuhitaji golikipa huyo #SportsElite
    0 Commentarii 0 Distribuiri 335 Views
  • :Real Madrid wanaripotiwa kupokea ofa ya zaidi ya £𝟑𝟎𝟎𝐌 kumnunua Vinicius Junior

    Ofa itavunja ada inayoshikilia rekodi ya dunia ya £198m, iliyolipwa na PSG kwa Neymar mnamo 2017

    #SportsElite
    🚨⚪:Real Madrid wanaripotiwa kupokea ofa ya zaidi ya £𝟑𝟎𝟎𝐌 kumnunua Vinicius Junior 😱💰 Ofa itavunja ada inayoshikilia rekodi ya dunia ya £198m, iliyolipwa na PSG kwa Neymar mnamo 2017 #SportsElite
    0 Commentarii 0 Distribuiri 429 Views
  • Manager wa Club ya PSG Luis Enrique amesema kuwa yuko mbioni katika sakata la kumsajiri aliyekuwa kiungo wa Real Madrid Eduardo Camavinga licha ya kuwa majeruhii hayo yamesemwa na Luis Enrique manager wa PSG
    Manager wa Club ya PSG Luis Enrique amesema kuwa yuko mbioni katika sakata la kumsajiri aliyekuwa kiungo wa Real Madrid Eduardo Camavinga licha ya kuwa majeruhii hayo yamesemwa na Luis Enrique manager wa PSG
    0 Commentarii 0 Distribuiri 418 Views
  • Tottenham inavutiwa na Illia Zabarnyi na wako tayari kuzungumza na Bournemouth na thamani yake ni €70M —
    Lakini Zabarnyi ameipa kipaumbele PSG.

    (Source: @DiMarzio)

    #SportsElite
    🚨 Tottenham inavutiwa na Illia Zabarnyi na wako tayari kuzungumza na Bournemouth na thamani yake ni €70M — Lakini Zabarnyi ameipa kipaumbele PSG. 💰🤯 (Source: @DiMarzio) #SportsElite
    0 Commentarii 0 Distribuiri 379 Views
  • 𝗥𝗔𝗦𝗠𝗜

    Paris Saint-Germain (PSG) wamemsajili kipa wa Kiitaliano Renato Marin kutoka AS Roma kwa uhamisho huru.

    Renato Marin amesaini mkataba wa miaka 5 utakaomuweka klabuni hadi mwaka 2030. ✍🏻

    #SportsElite
    𝗥𝗔𝗦𝗠𝗜 ✅ Paris Saint-Germain (PSG) wamemsajili kipa wa Kiitaliano Renato Marin kutoka AS Roma kwa uhamisho huru.🔵🔴🇮🇹 Renato Marin amesaini mkataba wa miaka 5 utakaomuweka klabuni hadi mwaka 2030. ✍🏻📝🆓 #SportsElite
    0 Commentarii 0 Distribuiri 427 Views
  • Klabu ya Chelsea itapata heshima ya kuvaa nembo ya Fifa Club World Cup kwa muda wa miaka minne kwenye jezi zao na hii imekuja baada ya Michuano hiyo kuanza kufanyika kila baada ya miaka minne baada ya mabadiliko yaliyofanyika ikiwa ni pamoja na kuongeza idadi ya timu shiriki.

    Pia Chelsea wamepewa heshima hiyo baada ya kutwaa ubingwa wa kombe la dunia kwa ngazi ya klabu kwa kuwachapa Psg mabao 3-0 usiku wa kuamkia leo katika uwanja wa Metlife Nchini Marekani.

    #SportsElite
    🚨Klabu ya Chelsea itapata heshima ya kuvaa nembo ya Fifa Club World Cup kwa muda wa miaka minne kwenye jezi zao na hii imekuja baada ya Michuano hiyo kuanza kufanyika kila baada ya miaka minne baada ya mabadiliko yaliyofanyika ikiwa ni pamoja na kuongeza idadi ya timu shiriki. Pia Chelsea wamepewa heshima hiyo baada ya kutwaa ubingwa wa kombe la dunia kwa ngazi ya klabu kwa kuwachapa Psg mabao 3-0 usiku wa kuamkia leo katika uwanja wa Metlife Nchini Marekani. #SportsElite
    0 Commentarii 0 Distribuiri 978 Views
  • Baada ya kurejea timu yake ya zamani Rosario de Central, Angel de Maria leo ataanza kwenye mchezo wake wa kwanza dhidi ya Godoy Cruz mchezo wa ligi kuu nchini Argentina.

    Rosario de Central ndio timu iliyomtoa Di maria kabla ya kutimkia vilabu vya ulaya kama vile Benfica, Real Madrid, Manchester united pamoja na PSG.

    #SportsElite
    Baada ya kurejea timu yake ya zamani Rosario de Central, Angel de Maria leo ataanza kwenye mchezo wake wa kwanza dhidi ya Godoy Cruz mchezo wa ligi kuu nchini Argentina. Rosario de Central ndio timu iliyomtoa Di maria kabla ya kutimkia vilabu vya ulaya kama vile Benfica, Real Madrid, Manchester united pamoja na PSG. #SportsElite
    Love
    1
    0 Commentarii 0 Distribuiri 669 Views
Sponsorizeaza Paginile