0 التعليقات
·0 المشاركات
·183 مشاهدة
-
0 التعليقات ·0 المشاركات ·288 مشاهدة
-
-
-
-
-
-
-
#PART1
Kuna gereza, na kuna Guantanamo Bay.
Hili si gereza la kawaida. Ni shimo la mateso, mahali ambapo sheria za haki za binadamu zinaonekana kama hadithi za kufikirika.
Lipo Cuba, lakini linamilikiwa na Marekani.
Wanasema gereza ni sehemu ya kutumikia adhabu, lakini Guantanamo ni sehemu ambapo unatakiwa kusahau kama ulikuwa binadamu.
Kama umewekwa hapa, ni ishara kwamba dunia imeshakusahau.
Na hata kama hauna hatia, hutaweza kuthibitisha chochote.
Marekani ni taifa la haki, Ndio! angalau kwenye makaratasi.
Lakini hata Wamarekani wenyewe walikuwa hawapendi Guantanamo.
Kila mwaka, wanaharakati wa haki za binadamu walikuwa wakiandamana, wakitaka gereza hilo lifungwe.
Ilipofika mwaka 2008, Barack Obama alipoingia kwenye kinyang'anyiro cha urais, akaahidi jambo moja kubwa.
"Nikichaguliwa kuwa Rais, gereza la Guantanamo litafungwa mara moja!"
Ilionekana kama ahadi ya kweli.
Wamarekani wakashangilia, wakaamini kwamba hatimaye heshima ya taifa lao itarudi.
#PART1 Kuna gereza, na kuna Guantanamo Bay. Hili si gereza la kawaida. Ni shimo la mateso, mahali ambapo sheria za haki za binadamu zinaonekana kama hadithi za kufikirika. Lipo Cuba, lakini linamilikiwa na Marekani. Wanasema gereza ni sehemu ya kutumikia adhabu, lakini Guantanamo ni sehemu ambapo unatakiwa kusahau kama ulikuwa binadamu. Kama umewekwa hapa, ni ishara kwamba dunia imeshakusahau. Na hata kama hauna hatia, hutaweza kuthibitisha chochote. Marekani ni taifa la haki, Ndio! angalau kwenye makaratasi. Lakini hata Wamarekani wenyewe walikuwa hawapendi Guantanamo. Kila mwaka, wanaharakati wa haki za binadamu walikuwa wakiandamana, wakitaka gereza hilo lifungwe. Ilipofika mwaka 2008, Barack Obama alipoingia kwenye kinyang'anyiro cha urais, akaahidi jambo moja kubwa. "Nikichaguliwa kuwa Rais, gereza la Guantanamo litafungwa mara moja!" Ilionekana kama ahadi ya kweli. Wamarekani wakashangilia, wakaamini kwamba hatimaye heshima ya taifa lao itarudi.0 التعليقات ·0 المشاركات ·785 مشاهدة -
#PART2
Na kweli, wakampigia kura, Obama akaingia madarakani.
Mwaka wa kwanza ukapita.
Mwaka wa pili ukapita.
Mwaka wa tatu ukapita.
Gereza bado liko palepale.
Kila alipoulizwa juu ya ahadi yake, alitoa majibu yasiyoeleweka.
Ndani ya miaka yake minane madarakani, Guantanamo Bay liliendelea kuwepo.
Ndipo Wamarekani wakagundua kitu.
Hata Rais hana nguvu juu ya gereza hili.
Wakati Trump akaingia madarakani, yeye hakutumia Guantanamo kama njia ya kuombea kura.
Hakusema atalifunga.
Hakusema atalifungua.
Lakini alipoingia, akatoa amri ya kuhamisha wafungwa zaidi ya 30,000.
Lengo lake lilikuwa moja tu.
"Tuhakikishe gereza linajaa wale ambao kweli wanastahili kuwepo humo."
#PART2 Na kweli, wakampigia kura, Obama akaingia madarakani. Mwaka wa kwanza ukapita. Mwaka wa pili ukapita. Mwaka wa tatu ukapita. Gereza bado liko palepale. Kila alipoulizwa juu ya ahadi yake, alitoa majibu yasiyoeleweka. Ndani ya miaka yake minane madarakani, Guantanamo Bay liliendelea kuwepo. Ndipo Wamarekani wakagundua kitu. Hata Rais hana nguvu juu ya gereza hili. Wakati Trump akaingia madarakani, yeye hakutumia Guantanamo kama njia ya kuombea kura. Hakusema atalifunga. Hakusema atalifungua. Lakini alipoingia, akatoa amri ya kuhamisha wafungwa zaidi ya 30,000. Lengo lake lilikuwa moja tu. "Tuhakikishe gereza linajaa wale ambao kweli wanastahili kuwepo humo."0 التعليقات ·0 المشاركات ·648 مشاهدة