• FARDC yaishutumu AFC/M23 kwa wizi wa lami ya ujenzi wa barabara ya Mudaka.

    Mvutano mpya umezuka katika eneo la Sud-Kivu, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, baada ya Jeshi la Serikali, Forces Armées de la République Démocratique du Congo (FARDC), kuishutumu kundi la Waasi la Alliance Fleuve Congo/M23 kwa kuiba lami iliyokuwa imekusudiwa kwa ajili ya kazi za ujenzi wa barabara katika eneo la Mudaka.

    Kwa mujibu wa taarifa ya Jeshi hilo, tukio hilo limetokea wakati mamlaka za serikali zikiendelea na maandalizi ya kuboresha miundombinu ya barabara katika eneo hilo, lengo likiwa ni kurahisisha usafiri na shughuli za kiuchumi kwa wakazi wa Mudaka na maeneo jirani.

    Katika taarifa yake, FARDC imesema, “Kundi la AFC/M23 limehusika katika wizi wa lami iliyokuwa imeandaliwa kwa ajili ya ujenzi wa barabara Mudaka, hatua inayolenga kuhujumu juhudi za serikali za kuboresha miundombinu.”

    Jeshi hilo limeongeza kuwa kitendo hicho ni sehemu ya mikakati ya makundi yenye silaha kuvuruga utulivu na maendeleo katika Mkoa wa Sud-Kivu.

    Kwa upande wake, hadi sasa AFC/M23 haijatoa tamko rasmi kujibu tuhuma hizo. Hata hivyo, kundi hilo limekuwa likitajwa mara kwa mara katika matukio ya mapigano na mivutano ya kiusalama katika maeneo mbalimbali ya mashariki mwa DRC.

    Wachambuzi wa masuala ya usalama wanaeleza kuwa miundombinu kama barabara imekuwa ikilengwa mara kwa mara katika maeneo yenye migogoro, kwani hudhoofisha uwezo wa serikali kufikisha huduma na kuimarisha ushawishi wake kwa wananchi.

    Hali ya usalama katika Mkoa wa Sud-Kivu inaendelea kuwa tete, huku jamii ya kimataifa ikiendelea kutoa wito wa mazungumzo na suluhisho la kudumu la kisiasa ili kumaliza mzozo wa muda mrefu katika eneo hilo.

    Kwa sasa, mamlaka za kijeshi zimesema zinaendelea kufuatilia tukio hilo na kuchukua hatua stahiki dhidi ya wahusika.

    Toa maoni yako
    #Habari
    FARDC yaishutumu AFC/M23 kwa wizi wa lami ya ujenzi wa barabara ya Mudaka. Mvutano mpya umezuka katika eneo la Sud-Kivu, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, baada ya Jeshi la Serikali, Forces Armées de la République Démocratique du Congo (FARDC), kuishutumu kundi la Waasi la Alliance Fleuve Congo/M23 kwa kuiba lami iliyokuwa imekusudiwa kwa ajili ya kazi za ujenzi wa barabara katika eneo la Mudaka. Kwa mujibu wa taarifa ya Jeshi hilo, tukio hilo limetokea wakati mamlaka za serikali zikiendelea na maandalizi ya kuboresha miundombinu ya barabara katika eneo hilo, lengo likiwa ni kurahisisha usafiri na shughuli za kiuchumi kwa wakazi wa Mudaka na maeneo jirani. Katika taarifa yake, FARDC imesema, “Kundi la AFC/M23 limehusika katika wizi wa lami iliyokuwa imeandaliwa kwa ajili ya ujenzi wa barabara Mudaka, hatua inayolenga kuhujumu juhudi za serikali za kuboresha miundombinu.” Jeshi hilo limeongeza kuwa kitendo hicho ni sehemu ya mikakati ya makundi yenye silaha kuvuruga utulivu na maendeleo katika Mkoa wa Sud-Kivu. Kwa upande wake, hadi sasa AFC/M23 haijatoa tamko rasmi kujibu tuhuma hizo. Hata hivyo, kundi hilo limekuwa likitajwa mara kwa mara katika matukio ya mapigano na mivutano ya kiusalama katika maeneo mbalimbali ya mashariki mwa DRC. Wachambuzi wa masuala ya usalama wanaeleza kuwa miundombinu kama barabara imekuwa ikilengwa mara kwa mara katika maeneo yenye migogoro, kwani hudhoofisha uwezo wa serikali kufikisha huduma na kuimarisha ushawishi wake kwa wananchi. Hali ya usalama katika Mkoa wa Sud-Kivu inaendelea kuwa tete, huku jamii ya kimataifa ikiendelea kutoa wito wa mazungumzo na suluhisho la kudumu la kisiasa ili kumaliza mzozo wa muda mrefu katika eneo hilo. Kwa sasa, mamlaka za kijeshi zimesema zinaendelea kufuatilia tukio hilo na kuchukua hatua stahiki dhidi ya wahusika. Toa maoni yako #Habari
    0 Comentários 0 Compartilhamentos 108 Visualizações
  • AFC/M23 yasisitiza utekelezaji wa makubaliano ya Doha, yaituhumu Kinshasa kwa “Mbinu za mawasiliano”.

    Muungano wa Waasi wa AFC/M23 nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) umetangaza upya msimamo wake kuhusu wito wa kusitisha mapigano, ukisema uko tayari kutekeleza makubaliano yaliyofikiwa kupitia mchakato wa Doha, huku ukitupia lawama Serikali ya Kinshasa kwa kile ilichokiita “mbinu za mawasiliano” zenye lengo la kupotosha (kutangaza uongo) umma.

    Kupitia taarifa iliyotolewa na Kiongozi wa AFC/M23, Corneille Naanga, Muungano huo ulieleza kuwa uko tayari kuchukua hatua mara moja katika kutekeleza utaratibu wa usitishaji mapigano uliokubaliwa.

    Naanga alisema: "Kufuatia wito unaoendelea wa kusitisha mapigano, AFC/M23 inathibitisha tena dhamira yake ya kutekeleza, bila kuchelewa na kwa nia njema, utaratibu uliokubaliwa katika mfumo wa mchakato wa Doha. Hatua hii inaendana na mantiki ya uwajibikaji wa kisiasa na nia ya dhati ya kufikia suluhu ya mazungumzo, ya kudumu na shirikishi ya mzozo huu.”

    Kauli hiyo inaashiria msimamo wa AFC/M23 wa kuonyesha utayari wa kushiriki katika juhudi za kidiplomasia zinazolenga kumaliza mzozo wa muda mrefu mashariki mwa DRC.

    Hata hivyo, Muungano huo uliikosoa vikali Serikali ya DRC yenye makao yake Kinshasa, ukidai kuwa tangazo la kukubali kusitisha mapigano si la dhati.

    Naanga aliongeza: “Kwa AFC, kile kinachodaiwa kuwa kukubali kwa Kinshasa kanuni ya kusitisha mapigano ni mbinu tu ya mawasiliano na jaribio la upotoshaji linalolenga kudanganya maoni ya kitaifa na kimataifa, kujiepusha na wajibu wake na kuficha mwendelezo wa mkakati wa kijeshi usiobadilika.”

    Kauli hiyo inaibua mvutano mpya wa kisiasa wakati juhudi za kimataifa zikiongezeka kuhimiza pande husika kurejea katika meza ya mazungumzo kupitia mchakato wa Doha.

    Mzozo kati ya serikali ya DRC na AFC/M23 umeendelea kuathiri hali ya usalama na kibinadamu mashariki mwa nchi hiyo, huku jumuiya ya kimataifa ikiendelea kusisitiza umuhimu wa suluhu ya mazungumzo badala ya mapambano ya kijeshi.

    Toa maoni yako
    #Habari
    AFC/M23 yasisitiza utekelezaji wa makubaliano ya Doha, yaituhumu Kinshasa kwa “Mbinu za mawasiliano”. Muungano wa Waasi wa AFC/M23 nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) umetangaza upya msimamo wake kuhusu wito wa kusitisha mapigano, ukisema uko tayari kutekeleza makubaliano yaliyofikiwa kupitia mchakato wa Doha, huku ukitupia lawama Serikali ya Kinshasa kwa kile ilichokiita “mbinu za mawasiliano” zenye lengo la kupotosha (kutangaza uongo) umma. Kupitia taarifa iliyotolewa na Kiongozi wa AFC/M23, Corneille Naanga, Muungano huo ulieleza kuwa uko tayari kuchukua hatua mara moja katika kutekeleza utaratibu wa usitishaji mapigano uliokubaliwa. Naanga alisema: "Kufuatia wito unaoendelea wa kusitisha mapigano, AFC/M23 inathibitisha tena dhamira yake ya kutekeleza, bila kuchelewa na kwa nia njema, utaratibu uliokubaliwa katika mfumo wa mchakato wa Doha. Hatua hii inaendana na mantiki ya uwajibikaji wa kisiasa na nia ya dhati ya kufikia suluhu ya mazungumzo, ya kudumu na shirikishi ya mzozo huu.” Kauli hiyo inaashiria msimamo wa AFC/M23 wa kuonyesha utayari wa kushiriki katika juhudi za kidiplomasia zinazolenga kumaliza mzozo wa muda mrefu mashariki mwa DRC. Hata hivyo, Muungano huo uliikosoa vikali Serikali ya DRC yenye makao yake Kinshasa, ukidai kuwa tangazo la kukubali kusitisha mapigano si la dhati. Naanga aliongeza: “Kwa AFC, kile kinachodaiwa kuwa kukubali kwa Kinshasa kanuni ya kusitisha mapigano ni mbinu tu ya mawasiliano na jaribio la upotoshaji linalolenga kudanganya maoni ya kitaifa na kimataifa, kujiepusha na wajibu wake na kuficha mwendelezo wa mkakati wa kijeshi usiobadilika.” Kauli hiyo inaibua mvutano mpya wa kisiasa wakati juhudi za kimataifa zikiongezeka kuhimiza pande husika kurejea katika meza ya mazungumzo kupitia mchakato wa Doha. Mzozo kati ya serikali ya DRC na AFC/M23 umeendelea kuathiri hali ya usalama na kibinadamu mashariki mwa nchi hiyo, huku jumuiya ya kimataifa ikiendelea kusisitiza umuhimu wa suluhu ya mazungumzo badala ya mapambano ya kijeshi. Toa maoni yako #Habari
    0 Comentários 0 Compartilhamentos 102 Visualizações
  • GOMA: Corneille Nangaa akutana na Mkuu wa MONUSCO kujadili utekelezaji wa usitishaji mapigano.

    Katika hatua inayochukuliwa kama sehemu ya juhudi za kuimarisha hali ya usalama mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Mratibu wa harakati ya Waasi ya AFC/M23, Corneille Nangaa, amekutana Ijumaa hii na Kaimu Mkuu wa MONUSCO, Vivian van de Perre, Mjini Goma.

    Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa, mkutano huo ulijikita katika kujadili utaratibu wa uhakiki na ufuatiliaji wa utekelezaji wa makubaliano ya kusitisha mapigano katika eneo la mashariki mwa nchi hiyo.

    Mazungumzo hayo yalilenga hasa kuimarisha mfumo wa kuthibitisha iwapo pande husika zinazingatia masharti ya usitishaji mapigano, pamoja na kuweka mbinu madhubuti za kufuatilia utekelezaji wake kwa uwazi na uwajibikaji.

    Eneo la mashariki mwa DRC limekuwa likikabiliwa na changamoto za kiusalama kwa muda mrefu, huku makundi yenye silaha yakihusika katika mapigano yanayosababisha madhara kwa raia na kuyumbisha hali ya utulivu.

    Mkutano kati ya AFC/M23 na uongozi wa MONUSCO unaonekana kuwa sehemu ya juhudi za kidiplomasia za kupunguza mvutano na kuimarisha mchakato wa amani, hasa katika kipindi ambacho jumuiya ya kimataifa inaendelea kusisitiza umuhimu wa kuheshimu makubaliano ya kusitisha mapigano.

    Hatua zaidi zinatarajiwa kufuatia mazungumzo hayo, huku wadau wakisubiri kuona namna ambavyo utaratibu wa uhakiki na ufuatiliaji utakavyotekelezwa kwa vitendo katika maeneo yenye migogoro.

    Toa maoni yako #Habari
    GOMA: Corneille Nangaa akutana na Mkuu wa MONUSCO kujadili utekelezaji wa usitishaji mapigano. Katika hatua inayochukuliwa kama sehemu ya juhudi za kuimarisha hali ya usalama mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Mratibu wa harakati ya Waasi ya AFC/M23, Corneille Nangaa, amekutana Ijumaa hii na Kaimu Mkuu wa MONUSCO, Vivian van de Perre, Mjini Goma. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa, mkutano huo ulijikita katika kujadili utaratibu wa uhakiki na ufuatiliaji wa utekelezaji wa makubaliano ya kusitisha mapigano katika eneo la mashariki mwa nchi hiyo. Mazungumzo hayo yalilenga hasa kuimarisha mfumo wa kuthibitisha iwapo pande husika zinazingatia masharti ya usitishaji mapigano, pamoja na kuweka mbinu madhubuti za kufuatilia utekelezaji wake kwa uwazi na uwajibikaji. Eneo la mashariki mwa DRC limekuwa likikabiliwa na changamoto za kiusalama kwa muda mrefu, huku makundi yenye silaha yakihusika katika mapigano yanayosababisha madhara kwa raia na kuyumbisha hali ya utulivu. Mkutano kati ya AFC/M23 na uongozi wa MONUSCO unaonekana kuwa sehemu ya juhudi za kidiplomasia za kupunguza mvutano na kuimarisha mchakato wa amani, hasa katika kipindi ambacho jumuiya ya kimataifa inaendelea kusisitiza umuhimu wa kuheshimu makubaliano ya kusitisha mapigano. Hatua zaidi zinatarajiwa kufuatia mazungumzo hayo, huku wadau wakisubiri kuona namna ambavyo utaratibu wa uhakiki na ufuatiliaji utakavyotekelezwa kwa vitendo katika maeneo yenye migogoro. Toa maoni yako #Habari
    0 Comentários 0 Compartilhamentos 142 Visualizações
  • Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Goma wafunguliwa upya baada ya kufungwa kwa mwaka mzima.

    Goma, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Goma umefunguliwa rasmi leo Alhamisi, baada ya kufungwa kwa karibu mwaka mzima kufuatia kukamatwa kwa Mji na Waasi wa AFC/M23.

    Ndege ya kwanza kuwasili katika Uwanja huo ilikuwa Helikopta ya MONUSCO, iliyomleta Kiongozi wa muda wa ujumbe wa Umoja wa Mataifa, Vivian van de Perre. Ziara yake inalenga kuthibitisha msaada wa Umoja wa Mataifa katika mchakato wa amani unaoendelea kati ya serikali ya Congo na Waasi.

    Akiwa na Waandishi wa habari, van de Perre alisema: "Tumekuja hapa kuthibitisha dhamira ya MONUSCO katika kuunga mkono mchakato wa amani unaoendelea kati ya serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na kundi la AFC/M23."

    Aliongeza kuwa: "Nina mpango wa kukutana na pande zote husika ili kuendeleza mfumo wa ufuatiliaji na ukaguzi wa mapatano ya kusitisha mapigano."

    Ziara hii inatekelezwa chini ya azimio la 2808 la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, linalowekwa ili MONUSCO isaidie utekelezaji wa mapatano ya amani na kuhakikisha usalama wa Raia.

    Ufunguaji upya wa Uwanja huu ni ishara ya matumaini kwa Wakazi wa Nord-Kivu, na ni hatua muhimu katika juhudi za kimataifa za kurejesha utulivu na usalama katika eneo lililoathiriwa na mizozo ya kivita.

    Toa maoni yako
    #Habari
    Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Goma wafunguliwa upya baada ya kufungwa kwa mwaka mzima. Goma, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Goma umefunguliwa rasmi leo Alhamisi, baada ya kufungwa kwa karibu mwaka mzima kufuatia kukamatwa kwa Mji na Waasi wa AFC/M23. Ndege ya kwanza kuwasili katika Uwanja huo ilikuwa Helikopta ya MONUSCO, iliyomleta Kiongozi wa muda wa ujumbe wa Umoja wa Mataifa, Vivian van de Perre. Ziara yake inalenga kuthibitisha msaada wa Umoja wa Mataifa katika mchakato wa amani unaoendelea kati ya serikali ya Congo na Waasi. Akiwa na Waandishi wa habari, van de Perre alisema: "Tumekuja hapa kuthibitisha dhamira ya MONUSCO katika kuunga mkono mchakato wa amani unaoendelea kati ya serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na kundi la AFC/M23." Aliongeza kuwa: "Nina mpango wa kukutana na pande zote husika ili kuendeleza mfumo wa ufuatiliaji na ukaguzi wa mapatano ya kusitisha mapigano." Ziara hii inatekelezwa chini ya azimio la 2808 la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, linalowekwa ili MONUSCO isaidie utekelezaji wa mapatano ya amani na kuhakikisha usalama wa Raia. Ufunguaji upya wa Uwanja huu ni ishara ya matumaini kwa Wakazi wa Nord-Kivu, na ni hatua muhimu katika juhudi za kimataifa za kurejesha utulivu na usalama katika eneo lililoathiriwa na mizozo ya kivita. Toa maoni yako #Habari
    0 Comentários 0 Compartilhamentos 141 Visualizações
  • RASMI:
    Klabu ya Napoli imethibitisha kuwa kiungo wa Cameroon Franck Zambo Anguissa amepata jeraha kubwa la misuli.

    Kwa mujibu wa taarifa za kitabibu, Anguissa atakuwa nje kwa miezi kadhaa, hali inayoweza kumfanya aukose AFCON 2025 nchini Morocco.
    Pigo kubwa kwa Cameroon.

    Anguissa ni mhimili mkubwa wa kiungo cha Cameroon, hivyo kutokuwepo kwake kunaathiri uimara wa timu katika presha kubwa ya mechi za AFCON.

    Unadhani Cameroon wataimudu AFCON bila Anguissa?
    Je, nafasi yake inapaswa kuzibwa na nani?

    🔵 RASMI: Klabu ya Napoli imethibitisha kuwa kiungo wa Cameroon 🇨🇲 Franck Zambo Anguissa amepata jeraha kubwa la misuli. Kwa mujibu wa taarifa za kitabibu, Anguissa atakuwa nje kwa miezi kadhaa, hali inayoweza kumfanya aukose AFCON 2025 nchini Morocco. Pigo kubwa kwa Cameroon. 💔 Anguissa ni mhimili mkubwa wa kiungo cha Cameroon, hivyo kutokuwepo kwake kunaathiri uimara wa timu katika presha kubwa ya mechi za AFCON. Unadhani Cameroon wataimudu AFCON bila Anguissa? Je, nafasi yake inapaswa kuzibwa na nani?
    0 Comentários 0 Compartilhamentos 752 Visualizações
  • 𝐅𝐔𝐋𝐋 𝐓𝐈𝐌𝐄 : AFC Champions League

    AL AHLI FC 4️⃣➖️0️⃣ AL GHARAFA
    ⚽️ 32" Millot
    ⚽️ 38" Kessie
    ⚽️ 41" Kessie
    ⚽️ 76" Al Shamat
    🚩 𝐅𝐔𝐋𝐋 𝐓𝐈𝐌𝐄 : AFC Champions League AL AHLI FC 🇸🇦 4️⃣➖️0️⃣ AL GHARAFA 🇶🇦 ⚽️ 32" Millot ⚽️ 38" Kessie ⚽️ 41" Kessie ⚽️ 76" Al Shamat
    0 Comentários 0 Compartilhamentos 228 Visualizações
  • Best SSB Interview Coaching Near Me

    If you are searching for SSB interview coaching near me, you need more than just a nearby academy — you need the right guidance to succeed in the Armed Forces.

    Breakthrough Point Defence Academy, located in Delhi/NCR, is trusted by aspirants from across India for NDA, CDS, and AFCAT SSB preparation. Our 15-day, 150-hour program covers psychology tests, personal interviews, GTO tasks, group discussions, and personality development sessions.

    Begin your journey today: https://breakthroughpoint.co.in/

    #SSBInterviewCoachingNearMe #BestSSBInterviewCoaching #SSBInterviewPreparation #SSBCoachingForNDA #SSBCoachingForCDS #SSBInterviewGuidance #BreakthroughPointAcademy
    Best SSB Interview Coaching Near Me If you are searching for SSB interview coaching near me, you need more than just a nearby academy — you need the right guidance to succeed in the Armed Forces. Breakthrough Point Defence Academy, located in Delhi/NCR, is trusted by aspirants from across India for NDA, CDS, and AFCAT SSB preparation. Our 15-day, 150-hour program covers psychology tests, personal interviews, GTO tasks, group discussions, and personality development sessions. 👉 Begin your journey today: https://breakthroughpoint.co.in/ #SSBInterviewCoachingNearMe #BestSSBInterviewCoaching #SSBInterviewPreparation #SSBCoachingForNDA #SSBCoachingForCDS #SSBInterviewGuidance #BreakthroughPointAcademy
    0 Comentários 0 Compartilhamentos 2KB Visualizações
  • Eberechi Eze apewa jezi namba 10 ndani ya Arsenal

    Mashabiki wanatarajia makubwa kutoka kwake akiwa sehemu ya kikosi cha Mikel Arteta.

    Eze amesema: "Ninajua majina makubwa yaliyowahi kuivaa jezi hii kabla yangu. Nafasi hii naiona kama baraka kubwa. Kuwa hapa ni heshima, na nitatoa kila kitu nilichonacho kulipa heshima hii."

    #AFC #Eze10 #PremierLeague

    ---------follow Csmahona update

    #SportsElite
    🔴⚪✨ Eberechi Eze apewa jezi namba 10 ndani ya Arsenal Mashabiki wanatarajia makubwa kutoka kwake akiwa sehemu ya kikosi cha Mikel Arteta. 🙌🔥 🗣️ Eze amesema: "Ninajua majina makubwa yaliyowahi kuivaa jezi hii kabla yangu. Nafasi hii naiona kama baraka kubwa. Kuwa hapa ni heshima, na nitatoa kila kitu nilichonacho kulipa heshima hii." #AFC #Eze10 #PremierLeague ---------follow Csmahona update #SportsElite
    0 Comentários 0 Compartilhamentos 962 Visualizações
  • Hii ni picha inayoonyesha Son Heung-min akisherehekea katika dakika za mwanzo za pambano lao dhidi ya FC Dallas – ambapo alifunga goli lake la kwanza kwa LAFC.

    #SportsElite
    Hii ni picha inayoonyesha Son Heung-min akisherehekea katika dakika za mwanzo za pambano lao dhidi ya FC Dallas – ambapo alifunga goli lake la kwanza kwa LAFC. #SportsElite
    0 Comentários 0 Compartilhamentos 551 Visualizações
  • Kesho wanakutana wakwanza na wapili nan ataendelezea kichapo Liverpool FC vs AFC Bournemouth sisi ni people
    🚨🚨Kesho wanakutana wakwanza na wapili nan ataendelezea kichapo Liverpool FC vs AFC Bournemouth sisi ni people
    0 Comentários 0 Compartilhamentos 394 Visualizações
  • Kutoka Nchini Qatar , Pande mbali hasimu katika mzozo wa Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na waasi wa AFC/M23 wanaotuhumiwa kuungwa mkono na Nchi ya Rwanda wamekubaliana kusitisha mapigano mara moja, baada ya mazungumzo ya wiki moja yaliyoandaliwa Nchini Qatar. Makubaliano hayo, yaliyoelezwa kuwa ni hatua ya matumaini, yalitangazwa kupitia taarifa rasmi zilizotolewa na kila upande baada ya Wajumbe kurejea kutoka Qatar mapema wiki hii.

    “Pande zote zimethibitisha dhamira yao ya kusitisha uhasama, kupinga matamshi ya chuki na vitisho, na kuhimiza jamii kutekeleza ahadi hizi,” ilisomeka sehemu ya taarifa. Hata hivyo, tarehe ya duru inayofuata ya mazungumzo haikutajwa.

    Kundi la M23 ambalo limekuwa likijipatia nguvu upya tangu mwaka jana, limeshambulia na kuteka Miji kadhaa Mashariki mwa DR Congo, hali iliyosababisha vifo vya maelfu na kuwafanya mamilioni kuwa Wakimbizi. Hofu ya vita vikubwa vya kikanda imetanda, hasa kutokana na mvutano kati ya DR Congo na Nchi ya Rwanda. Rwanda imeendelea kukanusha kuhusika moja kwa moja na kundi la M23, ikisema Wanajeshi wake wapo kulinda mipaka dhidi ya mashambulizi ya Wanamgambo wa Kihutu waliokimbilia DR Congo baada ya mauaji ya kimbari ya 1994.

    Juhudi hizi za upatanishi zinafuatia mkutano wa mwezi uliopita ulioandaliwa pia na Qatar, uliowakutanisha Rais wa DR Congo, Félix Tshisekedi na Rais wa Rwanda, Paul Kagame. Wito wa pamoja wa kusitisha mapigano ulitolewa, na sasa mazungumzo kati ya Serikali ya DR Congo na Kundi la M23 yanaonekana kuanza kupewa nafasi, licha ya DR Congo kulitambua Kundi hilo kama la kigaidi hapo awali.

    Kutoka Nchini Qatar 🇶🇦, Pande mbali hasimu katika mzozo wa Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo 🇨🇩 na waasi wa AFC/M23 wanaotuhumiwa kuungwa mkono na Nchi ya Rwanda 🇷🇼 wamekubaliana kusitisha mapigano mara moja, baada ya mazungumzo ya wiki moja yaliyoandaliwa Nchini Qatar. Makubaliano hayo, yaliyoelezwa kuwa ni hatua ya matumaini, yalitangazwa kupitia taarifa rasmi zilizotolewa na kila upande baada ya Wajumbe kurejea kutoka Qatar mapema wiki hii. “Pande zote zimethibitisha dhamira yao ya kusitisha uhasama, kupinga matamshi ya chuki na vitisho, na kuhimiza jamii kutekeleza ahadi hizi,” ilisomeka sehemu ya taarifa. Hata hivyo, tarehe ya duru inayofuata ya mazungumzo haikutajwa. Kundi la M23 ambalo limekuwa likijipatia nguvu upya tangu mwaka jana, limeshambulia na kuteka Miji kadhaa Mashariki mwa DR Congo, hali iliyosababisha vifo vya maelfu na kuwafanya mamilioni kuwa Wakimbizi. Hofu ya vita vikubwa vya kikanda imetanda, hasa kutokana na mvutano kati ya DR Congo na Nchi ya Rwanda. Rwanda imeendelea kukanusha kuhusika moja kwa moja na kundi la M23, ikisema Wanajeshi wake wapo kulinda mipaka dhidi ya mashambulizi ya Wanamgambo wa Kihutu waliokimbilia DR Congo baada ya mauaji ya kimbari ya 1994. Juhudi hizi za upatanishi zinafuatia mkutano wa mwezi uliopita ulioandaliwa pia na Qatar, uliowakutanisha Rais wa DR Congo, Félix Tshisekedi na Rais wa Rwanda, Paul Kagame. Wito wa pamoja wa kusitisha mapigano ulitolewa, na sasa mazungumzo kati ya Serikali ya DR Congo na Kundi la M23 yanaonekana kuanza kupewa nafasi, licha ya DR Congo kulitambua Kundi hilo kama la kigaidi hapo awali.
    Like
    Love
    2
    0 Comentários 0 Compartilhamentos 1KB Visualizações
  • Kutoka Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo , Mke wa Rais wa zamani wa Nchi hiyo Joseph Kabila Kabange, Olive Lembe Kabila, ametangaza kwamba Wanajeshi wa DR Congo waliopelekwa kwenye Shamba la Ng'ombe la Joseph Kabila lililopo Mkoani Haut-Katanga, waliiba, kuchinja na kula Ng'ombe wao waliowakuta katika Shamba hilo.

    Olive Lembe amesema hayo kwamba Wanajeshi hao walikuwa kwenye Shamba la Kundelungu lililoko katika Mkoa wa Haut-Katanga na kwamba hawakuwa na ruhusa ya kuingia kwenye mali ya familia yao. Mbali na kuchukua kompyuta na simu za mkononi za Wafanyakazi wa shamba hilo, Mwanamama huyo alieleza pia kuwa Wanajeshi hao walikuwa wakichinja Ng'ombe wao kwa ajili ya kula kwa sababu hawakuwa na chakula walichobeba.

    "Wanajeshi hawa walikuwa wakiiba kompyuta na simu za Wafanyakazi wa shamba. Walikuja bila chakula, sasa walichinja Ng'ombe wetu ili kula." alisema Lembe.

    Ikumbukwe kwamba Serikali ya DR Congo ilitangaza kuchukua mali zote za Kabila (kustaafisha) baada ya ziara yake ya tarehe 18 Aprili katika Jiji la Goma linalodhibitiwa na Muungano wa AFC/M23. Serikali ilikuwa ilituma Wanajeshi wa upelelezi kwenye mali zake, ikiwemo Nyumba yake iliyo katika eneo la Limete Mjini Kinshasa, wakisema walikuwa wakitafuta vifaa vya kijeshi ambavyo vinaweza kuwa vimefichwa.

    Lembe anasema kuwa Serikali ya DR Congo inaendelea kufanya mateso kwa familia yao, na kudai kwamba ina mpango wa kuwaangamiza.

    Kutoka Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo 🇨🇩, Mke wa Rais wa zamani wa Nchi hiyo Joseph Kabila Kabange, Olive Lembe Kabila, ametangaza kwamba Wanajeshi wa DR Congo waliopelekwa kwenye Shamba la Ng'ombe la Joseph Kabila lililopo Mkoani Haut-Katanga, waliiba, kuchinja na kula Ng'ombe wao waliowakuta katika Shamba hilo. Olive Lembe amesema hayo kwamba Wanajeshi hao walikuwa kwenye Shamba la Kundelungu lililoko katika Mkoa wa Haut-Katanga na kwamba hawakuwa na ruhusa ya kuingia kwenye mali ya familia yao. Mbali na kuchukua kompyuta na simu za mkononi za Wafanyakazi wa shamba hilo, Mwanamama huyo alieleza pia kuwa Wanajeshi hao walikuwa wakichinja Ng'ombe wao kwa ajili ya kula kwa sababu hawakuwa na chakula walichobeba. "Wanajeshi hawa walikuwa wakiiba kompyuta na simu za Wafanyakazi wa shamba. Walikuja bila chakula, sasa walichinja Ng'ombe wetu ili kula." alisema Lembe. Ikumbukwe kwamba Serikali ya DR Congo ilitangaza kuchukua mali zote za Kabila (kustaafisha) baada ya ziara yake ya tarehe 18 Aprili katika Jiji la Goma linalodhibitiwa na Muungano wa AFC/M23. Serikali ilikuwa ilituma Wanajeshi wa upelelezi kwenye mali zake, ikiwemo Nyumba yake iliyo katika eneo la Limete Mjini Kinshasa, wakisema walikuwa wakitafuta vifaa vya kijeshi ambavyo vinaweza kuwa vimefichwa. Lembe anasema kuwa Serikali ya DR Congo inaendelea kufanya mateso kwa familia yao, na kudai kwamba ina mpango wa kuwaangamiza.
    Like
    Love
    3
    0 Comentários 0 Compartilhamentos 1KB Visualizações
  • Aliyetiwa hatiani kuwa Mhalifu wa kivita na Mahakama ya kimataifa ya (ICC) kwa makosa mbalimbali, Thomas Lubanga, ametangaza kuunda kundi jipya la Waasi lenye lengo la kuiangusha Serikali ya Jimbo la Ituri, lililopo Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo .

    Nchi ya DR Congo imekuwa ikikabiliwa na tishio la kiusalama katika Mikoa ya mashariki ambapo makundi ya Waasi ikiwemo Muungano wa Waasi wa AFC/M23 unaoshikilia Miji ya Goma, Bukavu, Nyabibwe na Walikale.

    Hata hivyo, uamuzi wa Thomas Lubanga ambaye ni Mzaliwa wa Mkoa wa Ituri Nchini DR Congo na anayeishi Nchini Uganda , kutangaza kuanzisha Kundi lake la Waasi alilolipa jina Convention for the Popular Revolution (CPR) ambalo litaongeza hofu ya machafuko Nchini humo wakati huu ambao Serikali ya Rais Felix Tshisekedi inatafuta maridhiano na M23 kwa njia ya mazungumzo.

    Shirika la Habari la Reuters, limeripoti leo Jumanne Aprili Mosi, 2025, kuwa Lubanga ambaye ni Mzaliwa wa Ituri, alihukumiwa na Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) mwaka 2012 kwa makosa ya kuwasajili Watoto kama Askari na akapewa kifungo cha miaka 14 Gerezani, baadaye aliachiliwa mwaka 2020 na Rais wa DR Congo, Felix Tshisekedi kisha akamteua kuwa sehemu ya kikosi kazi cha kuleta amani Jimboni Ituri.

    Hata hivyo, mwaka 2022 alitekwa nyara kwa miezi miwili na kundi la Waasi, tukio analodai kupangwa na Serikali ya DR Congo kwa lengo kumpoteza ila kwa sasa anaishi Nchini Uganda.

    Aliyetiwa hatiani kuwa Mhalifu wa kivita na Mahakama ya kimataifa ya (ICC) kwa makosa mbalimbali, Thomas Lubanga, ametangaza kuunda kundi jipya la Waasi lenye lengo la kuiangusha Serikali ya Jimbo la Ituri, lililopo Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo 🇨🇩. Nchi ya DR Congo imekuwa ikikabiliwa na tishio la kiusalama katika Mikoa ya mashariki ambapo makundi ya Waasi ikiwemo Muungano wa Waasi wa AFC/M23 unaoshikilia Miji ya Goma, Bukavu, Nyabibwe na Walikale. Hata hivyo, uamuzi wa Thomas Lubanga ambaye ni Mzaliwa wa Mkoa wa Ituri Nchini DR Congo na anayeishi Nchini Uganda 🇺🇬, kutangaza kuanzisha Kundi lake la Waasi alilolipa jina Convention for the Popular Revolution (CPR) ambalo litaongeza hofu ya machafuko Nchini humo wakati huu ambao Serikali ya Rais Felix Tshisekedi inatafuta maridhiano na M23 kwa njia ya mazungumzo. Shirika la Habari la Reuters, limeripoti leo Jumanne Aprili Mosi, 2025, kuwa Lubanga ambaye ni Mzaliwa wa Ituri, alihukumiwa na Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) mwaka 2012 kwa makosa ya kuwasajili Watoto kama Askari na akapewa kifungo cha miaka 14 Gerezani, baadaye aliachiliwa mwaka 2020 na Rais wa DR Congo, Felix Tshisekedi kisha akamteua kuwa sehemu ya kikosi kazi cha kuleta amani Jimboni Ituri. Hata hivyo, mwaka 2022 alitekwa nyara kwa miezi miwili na kundi la Waasi, tukio analodai kupangwa na Serikali ya DR Congo kwa lengo kumpoteza ila kwa sasa anaishi Nchini Uganda.
    0 Comentários 0 Compartilhamentos 2KB Visualizações
  • Nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imetangaza rasmi kuondoa hitaji la visa kwa Watanzania wanaoingia Nchini humo, kuanzia tarehe 20 Machi, 2025. Hatua hii ni sehemu ya utekelezaji wa uanachama wa DR Congo katika Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na jitihada za kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia na kiuchumi kati ya mataifa hayo mawili.

    Ikumbukwe kwamba Nchi ya Tanzania ilikuwa imeondoa utaratibu wa malipo ya visa kwa Raia wa DRC tangu Septemba 2, 2023, ikitarajia hatua ya kurudishiwa fadhila. Uamuzi wa sasa wa DR Congo unaimarisha mahusiano ya ujirani mwema na kufungua fursa zaidi za biashara na ushirikiano wa kikanda.

    Serikali ya Tanzania imesifu hatua hiyo, ikisisitiza kuwa inalingana na ajenda za Jumuiya ya Afrika Mashariki na Mkataba wa Eneo Huru la Biashara la Afrika (AfCFTA). Hatua hii inaashiria ushirikiano bora wa kidiplomasia na unaleta unafuu mkubwa kwa Wafanyabiashara na wasafiri wa pande zote mbili.

    Nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo 🇨🇩 imetangaza rasmi kuondoa hitaji la visa kwa Watanzania wanaoingia Nchini humo, kuanzia tarehe 20 Machi, 2025. Hatua hii ni sehemu ya utekelezaji wa uanachama wa DR Congo katika Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na jitihada za kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia na kiuchumi kati ya mataifa hayo mawili. Ikumbukwe kwamba Nchi ya Tanzania 🇹🇿 ilikuwa imeondoa utaratibu wa malipo ya visa kwa Raia wa DRC tangu Septemba 2, 2023, ikitarajia hatua ya kurudishiwa fadhila. Uamuzi wa sasa wa DR Congo unaimarisha mahusiano ya ujirani mwema na kufungua fursa zaidi za biashara na ushirikiano wa kikanda. Serikali ya Tanzania imesifu hatua hiyo, ikisisitiza kuwa inalingana na ajenda za Jumuiya ya Afrika Mashariki na Mkataba wa Eneo Huru la Biashara la Afrika (AfCFTA). Hatua hii inaashiria ushirikiano bora wa kidiplomasia na unaleta unafuu mkubwa kwa Wafanyabiashara na wasafiri wa pande zote mbili.
    0 Comentários 0 Compartilhamentos 1KB Visualizações
  • Ahmed Ally, Msemaji wa klabu ya Simba SC

    Anatokea mwehu mmoja anamdhihaki huyu Rais au kikundi cha vijana wa hovyo wanadhihaki Mamlaka za mpira wetu, Hii Nchi uhuru umepitiliza sana

    Wallace Karia, TFF na Bodi ya Ligi Wanapaswa kuheshimiwa, kuenziwa, kutunzwa na kulindwa maana wamefanya kazi kubwa na wanaendelea kufanya kazi kubwa kwenye mpira wetu

    Yote tuliyokua tunayaota kwenye mpira sasa hivi yanatokea, yale tuliyodhani ni magumu kwa Karia yamewezekana

    Na kama haitoshi tunaiona kesho njema ya mpira wa Tanzania chini ya Karia na wenzake

    President @wallacekaria na Uongozi wako wa TFF na Bodi ya ligi msirudi nyuma na msikubali mtu akaturudisha nyuma sasa hivi tunawaza World Cup tunawaza Utawala wa AFCON na Ubingwa Afrika ngazi klabu

    KAMA HUMPENDI KARIA PENDA MAFANIKIO YAKE"

    Ahmed Ally, Msemaji wa klabu ya Simba SC ✍️ Anatokea mwehu mmoja anamdhihaki huyu Rais au kikundi cha vijana wa hovyo wanadhihaki Mamlaka za mpira wetu, Hii Nchi uhuru umepitiliza sana Wallace Karia, TFF na Bodi ya Ligi Wanapaswa kuheshimiwa, kuenziwa, kutunzwa na kulindwa maana wamefanya kazi kubwa na wanaendelea kufanya kazi kubwa kwenye mpira wetu Yote tuliyokua tunayaota kwenye mpira sasa hivi yanatokea, yale tuliyodhani ni magumu kwa Karia yamewezekana Na kama haitoshi tunaiona kesho njema ya mpira wa Tanzania chini ya Karia na wenzake President @wallacekaria na Uongozi wako wa TFF na Bodi ya ligi msirudi nyuma na msikubali mtu akaturudisha nyuma sasa hivi tunawaza World Cup tunawaza Utawala wa AFCON na Ubingwa Afrika ngazi klabu KAMA HUMPENDI KARIA PENDA MAFANIKIO YAKE"
    Like
    1
    0 Comentários 0 Compartilhamentos 1KB Visualizações
  • Muungano wa Waasi wa kundi la AFC/M23 umetangaza kutoshiriki mazungumzo ya amani huku wakiituhumu Serikali ya Kinshasa kwa kuendeleza vita. Katika taarifa ya Kundi hilo iliyotolewa Februari 17, 2025, Waasi hao wa M23 wameituhumu Serikali ya Rais Félix Tshisekedi kwa kuendesha mashambulizi ya ardhini kwa kutumia Ndege za kivita wakati wanajua fike wapo kwenye hatua za mwisho kuelekea kwenye mkutano wa amani Nchini Angola .

    Ikumbukwe kwamba Waasi hao wa AFC/M23 walikuwa tayari wameshawateua Wawakilishi wao na kuthibitisha kuwa watatuma Wawakilishi hao Nchini Jijini Luanda, Angola kwa ajili ya mazungumzo ya maani ambayo yamepangwa kufanyika Machi 18, 2025.

    Muungano wa Waasi wa kundi la AFC/M23 umetangaza kutoshiriki mazungumzo ya amani huku wakiituhumu Serikali ya Kinshasa kwa kuendeleza vita. Katika taarifa ya Kundi hilo iliyotolewa Februari 17, 2025, Waasi hao wa M23 wameituhumu Serikali ya Rais Félix Tshisekedi kwa kuendesha mashambulizi ya ardhini kwa kutumia Ndege za kivita wakati wanajua fike wapo kwenye hatua za mwisho kuelekea kwenye mkutano wa amani Nchini Angola 🇦🇴. Ikumbukwe kwamba Waasi hao wa AFC/M23 walikuwa tayari wameshawateua Wawakilishi wao na kuthibitisha kuwa watatuma Wawakilishi hao Nchini Jijini Luanda, Angola kwa ajili ya mazungumzo ya maani ambayo yamepangwa kufanyika Machi 18, 2025.
    Like
    1
    0 Comentários 0 Compartilhamentos 920 Visualizações
  • Katika hatua mpya ya mzozo unaoendelea Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo , kundi la Waasi wa M23 likishirikiana na Muungano wa Mto Congo (AFC) limetangaza kuwa Wanajeshi wa zamani wa Jeshi la DR Congo (FARDC) waliokamatwa au kujisalimisha wamehitimu mafunzo ya kiitikadi na mbinu za kijeshi.

    Katika taarifa ya Kundi la M23 kwenye mtandao wao wa X leo Februari 18, picha zilionyesha Wanajeshi hao wakiwa na sare na silaha rasmi za wanamgambo hao. Ujumbe uliambatana na chapisho hilo ulieleza:

    "Wanajeshi wa zamani wa FARDC, waliokamatwa au kujisalimisha, wamemaliza mafunzo ya kiitikadi na mbinu huko Rumangabo Mjini Goma chini ya AFC/M23. Sasa wakiwa na vifaa kamili na wanaolipwa, wametumwa Lubero, ambako wanashiriki kikamilifu muungano wa serikali."

    Wakati huo huo, Uganda imetangaza kuwa vikosi vyake vya kijeshi vimeanza kuelekea Bunia, DRC, ikiwa ni siku chache baada ya Jeshi la Uganda kutoa muda wa saa 24 kwa Askari waliopo eneo hilo kujisalimisha.

    Taarifa nyingine kuwa, hapo jana Kundi la Waasi hao wa M23 wamefanikiwa kuteka eneo la Kamanyola na sasa hivi wanajipanga kuelekea Uvira, Fizi kisha Mkoa wa Tanganyika (Kalemie) kabla ya kwenda Mjini Lubumbashi. Kwa mujibu wa Wananchi wa Kamanyala wanasema kuwa Kundi la Wapiganaji wa Wazalendo ambao wanapigana kwa upande wa Serikali waliibwa Silaha zao kisha wakakimbia na kuwaachia M23 kuichukua Kamanyola.

    Katika hatua mpya ya mzozo unaoendelea Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo 🇨🇩, kundi la Waasi wa M23 likishirikiana na Muungano wa Mto Congo (AFC) limetangaza kuwa Wanajeshi wa zamani wa Jeshi la DR Congo (FARDC) waliokamatwa au kujisalimisha wamehitimu mafunzo ya kiitikadi na mbinu za kijeshi. Katika taarifa ya Kundi la M23 kwenye mtandao wao wa X leo Februari 18, picha zilionyesha Wanajeshi hao wakiwa na sare na silaha rasmi za wanamgambo hao. Ujumbe uliambatana na chapisho hilo ulieleza: "Wanajeshi wa zamani wa FARDC, waliokamatwa au kujisalimisha, wamemaliza mafunzo ya kiitikadi na mbinu huko Rumangabo Mjini Goma chini ya AFC/M23. Sasa wakiwa na vifaa kamili na wanaolipwa, wametumwa Lubero, ambako wanashiriki kikamilifu muungano wa serikali." Wakati huo huo, Uganda imetangaza kuwa vikosi vyake vya kijeshi vimeanza kuelekea Bunia, DRC, ikiwa ni siku chache baada ya Jeshi la Uganda kutoa muda wa saa 24 kwa Askari waliopo eneo hilo kujisalimisha. Taarifa nyingine kuwa, hapo jana Kundi la Waasi hao wa M23 wamefanikiwa kuteka eneo la Kamanyola na sasa hivi wanajipanga kuelekea Uvira, Fizi kisha Mkoa wa Tanganyika (Kalemie) kabla ya kwenda Mjini Lubumbashi. Kwa mujibu wa Wananchi wa Kamanyala wanasema kuwa Kundi la Wapiganaji wa Wazalendo ambao wanapigana kwa upande wa Serikali waliibwa Silaha zao kisha wakakimbia na kuwaachia M23 kuichukua Kamanyola.
    0 Comentários 0 Compartilhamentos 1KB Visualizações
  • Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo , Félix Tshisekedi, amemshutumu kwa mara nyingine tena Mtangulizi wake Joseph Kabila kuwa anaunga mkono Kundi la Waasi la M23. Mnamo Agosti 2024, Tshisekedi alidai kuwa Kabila alikuwa nyuma ya kuunganishwa kwa muungano wa Wakuu wa kisiasa wa (AFC) unaoongozwa na Corneille Nangaa na Wapiganaji wa kundi la M23.

    Katika mahojiano, Tshisekedi alisema sababu iliyofanya Kabila kutoshiriki uchaguzi wa Desemba 2024 ni kwa sababu alikuwa na shughuli nyingi na AFC.

    “Tusimzungumzie Joseph Kabila. Amekataa kabisa kugombea uchaguzi na anajipanga kupambana na serikali kwa sababu yeye ni AFC.” - alisema Tshisekedi

    Rais huyo ameyasema hayo tena katika Baraza la Usalama la Kimataifa Mjini Munich Nchini Ujerumani Februari 14, 2025, ya kwamba Kabila alienda uhamishoni kwa sababu anafadhili Waasi wa (AFC) ikiwemo Kundi la Waasi la M23.

    Hata hivyo, Chama cha Joseph Kabila cha (PPRD) kimekanusha vikali matamshi ya Rais Félix Tshisekedi kwa kusema kuwa Kiongozi wao hausiki na Kundi hilo la Waasi.

    Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo 🇨🇩, Félix Tshisekedi, amemshutumu kwa mara nyingine tena Mtangulizi wake Joseph Kabila kuwa anaunga mkono Kundi la Waasi la M23. Mnamo Agosti 2024, Tshisekedi alidai kuwa Kabila alikuwa nyuma ya kuunganishwa kwa muungano wa Wakuu wa kisiasa wa (AFC) unaoongozwa na Corneille Nangaa na Wapiganaji wa kundi la M23. Katika mahojiano, Tshisekedi alisema sababu iliyofanya Kabila kutoshiriki uchaguzi wa Desemba 2024 ni kwa sababu alikuwa na shughuli nyingi na AFC. “Tusimzungumzie Joseph Kabila. Amekataa kabisa kugombea uchaguzi na anajipanga kupambana na serikali kwa sababu yeye ni AFC.” - alisema Tshisekedi Rais huyo ameyasema hayo tena katika Baraza la Usalama la Kimataifa Mjini Munich Nchini Ujerumani 🇩🇪 Februari 14, 2025, ya kwamba Kabila alienda uhamishoni kwa sababu anafadhili Waasi wa (AFC) ikiwemo Kundi la Waasi la M23. Hata hivyo, Chama cha Joseph Kabila cha (PPRD) kimekanusha vikali matamshi ya Rais Félix Tshisekedi kwa kusema kuwa Kiongozi wao hausiki na Kundi hilo la Waasi.
    Like
    1
    0 Comentários 0 Compartilhamentos 1KB Visualizações
  • TBT ya Haji Manara

    "September 2007 nikiwa kijana Mdogo na nikiwa kiongozi wa Chama changu na hapo ni fresh from School kule Beijing China.
    Kipindi hicho nna madini ya hatari kuhusu taaluma ya Propaganda na Uenezi,enzi ambazo nilikuwa naweza kukuaminisha Jiwe ni Keki

    Enzi ambazo nilikuwa naweza kuwavusha hata kuku barabarani kwa maneno tu,
    Ni zile zile zama nilizowaaminisha Barcelona haichomoki kwa Mkapa, tena Barcelona kweli ya Xavi ,Iniesta na kina Messi.
    Taaluma iliyonipa ujasiri wa kusema na kuamini tutafuzu kwa AFCON ya 2019 kule Misri,wakati huo tukiwa chini kwenye msimamo wa kundi letu, na Nchi nzima ikiwa imejikatia tamaa ya kwenda Cairo.

    Bila kusahau one day kule Paris France niliposahau Passport hotelini na siku hiyo tulisimamishwa na Manjagu njiani nikiwa na wenzangu ambao walikuwa Kamil Gado,
    Nikazuga kama naitoa kwenye mfuko wa koti, Askari wakaniamini kabla ya kuwaonyesha ,wakaturuhusu kilaini kabisa,inaitwa Blue Propaganda

    Yes: Pembeni yangu katika hiyo picha ni Marehemu Captain Barongo aliyekuwa Katibu wa CCM Mkoa wa Dar es salaam,
    Na hii ilikuwa sherehe ya harusi ya DC wa Temeke hivi sasa Mh Sixtus Mapunda ambae wakati huo alikuwa Katibu wa Umoja wa Vijana ( UV CCM ) Mkoa huu.
    Hadi leo tumebaki marafiki wakubwa na hakosi mwaliko wowote kwangu

    Nb: Usicheke ukubwa wa koti,miaka ile ilikuwa ndio fashion na wenyewe tuliyaita Majumba "

    TBT ya Haji Manara "September 2007 nikiwa kijana Mdogo na nikiwa kiongozi wa Chama changu na hapo ni fresh from School kule Beijing China. Kipindi hicho nna madini ya hatari kuhusu taaluma ya Propaganda na Uenezi,enzi ambazo nilikuwa naweza kukuaminisha Jiwe ni Keki 😀😀😀 Enzi ambazo nilikuwa naweza kuwavusha hata kuku barabarani kwa maneno tu😀😀😀, Ni zile zile zama nilizowaaminisha Barcelona haichomoki kwa Mkapa, tena Barcelona kweli ya Xavi ,Iniesta na kina Messi. Taaluma iliyonipa ujasiri wa kusema na kuamini tutafuzu kwa AFCON ya 2019 kule Misri,wakati huo tukiwa chini kwenye msimamo wa kundi letu, na Nchi nzima ikiwa imejikatia tamaa ya kwenda Cairo. Bila kusahau one day kule Paris France niliposahau Passport hotelini na siku hiyo tulisimamishwa na Manjagu njiani nikiwa na wenzangu ambao walikuwa Kamil Gado, Nikazuga kama naitoa kwenye mfuko wa koti, Askari wakaniamini kabla ya kuwaonyesha ,wakaturuhusu kilaini kabisa,inaitwa Blue Propaganda 😀😀😀 Yes: Pembeni yangu katika hiyo picha ni Marehemu Captain Barongo aliyekuwa Katibu wa CCM Mkoa wa Dar es salaam, Na hii ilikuwa sherehe ya harusi ya DC wa Temeke hivi sasa Mh Sixtus Mapunda ambae wakati huo alikuwa Katibu wa Umoja wa Vijana ( UV CCM ) Mkoa huu. Hadi leo tumebaki marafiki wakubwa na hakosi mwaliko wowote kwangu 🙏🙏 Nb: Usicheke ukubwa wa koti,miaka ile ilikuwa ndio fashion na wenyewe tuliyaita Majumba 😀😀😀"
    0 Comentários 0 Compartilhamentos 2KB Visualizações
  • Mahakama ya ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu (AfCHPR) imeanza kusikiliza shauri la Nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo dhidi ya Nchi ya Rwanda , ambalo limefunguliwa kwenye mahakama hiyo iliyoko Jijini Arusha Nchini Tanzania .

    Aidha, DR Congo ilifungua kesi dhidi ya Rwanda, Agosti 21 2023, ikiituhumu Nchi hiyo kwa ukiukwaji mkubwa wa haki za kibinadamu. Kupitia kesi namba 007/2023, DR Congo inadai kuwa Nchi ya Rwanda inahusika na mgogoro unaeondelea Mashariki mwa Nchi hiyo hasa Mkoa wa Sud-Kivu.

    Mahakama ya ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu (AfCHPR) imeanza kusikiliza shauri la Nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo 🇨🇩 dhidi ya Nchi ya Rwanda 🇷🇼, ambalo limefunguliwa kwenye mahakama hiyo iliyoko Jijini Arusha Nchini Tanzania 🇹🇿. Aidha, DR Congo ilifungua kesi dhidi ya Rwanda, Agosti 21 2023, ikiituhumu Nchi hiyo kwa ukiukwaji mkubwa wa haki za kibinadamu. Kupitia kesi namba 007/2023, DR Congo inadai kuwa Nchi ya Rwanda inahusika na mgogoro unaeondelea Mashariki mwa Nchi hiyo hasa Mkoa wa Sud-Kivu.
    Like
    1
    0 Comentários 0 Compartilhamentos 2KB Visualizações
Páginas impulsionada