• Familia ya Kiongozi wa upinzani wa Uganda Bobi Wine yafunguka kukimbia Nchi kufuatia matukio ya siasa na usalama.

    Katika taarifa iliyotolewa, Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Robert Kyagulanyi Ssentamu, maarufu kama Bobi Wine, amethibitisha mbele ya Wakaguzi wa haki za binadamu Mjini Geneva kwamba Mke wake, Barbie Itungo Kyagulanyi, na Watoto wao wametoka Uganda kwa sababu za hofu ya maisha yao kufuatia hali tete inayojitokeza nchini mwao baada ya uchaguzi wa Rais.

    Katika hotuba yake kupitia video mbele ya Geneva Summit for Human Rights and Democracy, Bobi Wine alisema wazi: “Mke wangu na Watoto walilazimika kukimbia nchi kwa hofu ya maisha yao.” - Bobi Wine.

    Alifafanua kuwa usalama wa familia yake uliathirika sana kutokana na operesheni za vikosi vya usalama zilizoendelea mara tu baada ya uchaguzi wa 15 Januari 2026, ambapo serikali ilitangaza ushindi wa Rais Yoweri Museveni ambayo Bobi Wine ameipinga kwa madai ya udanganyifu wa kura na ukandamizaji wa upinzani.

    Bobi Wine pia alidai kwamba vikosi vya usalama: “Vilivamia nyumba yangu, vikamtesa Mke wangu, kumfanya asiwe na chaguo ila kuondoka na Watoto wakiwa nje ya nchi.” amesema

    Habari kwamba familia yake imeondoka Uganda na si tu kutoroka nyumba yao ya Magere imetolewa mara tu baada ya miezi ya mvutano mkali, ikiwa ni pamoja na madai ya mashambulizi, ulinzi mkali wa nyumba yao na vitisho vilivyowekwa na baadhi ya Afisa wa usalama.

    Katika maneno yake Mjini Geneva, Bobi Wine pia alijumuisha ombi kwa Jumuiya ya kimataifa kuhusu hatua za kulinda haki za binadamu na kuzuia ukandamizaji wa upinzani nchini Uganda.

    Taarifa hii inakuja katika wakati ambapo Uganda iko chini ya uangalizi wa kimataifa kufuatia ripoti za ghasia, mashambulizi dhidi ya wapinzani wa kisiasa, na madai ya upendeleo wa vyombo vya usalama kuelekea chama tawala.

    Kwa sasa, bado haijafahamika kwa umma ni nchi gani hasa Barbie Itungo Kyagulanyi na Watoto hao wamekwenda, ila uamuzi wao wa kukimbia unachukuliwa kama hatua ya kulinda usalama wa familia katika mzozo wa kisiasa unaoendelea nchini Uganda.

    Toa maoni yako
    #Habari
    Familia ya Kiongozi wa upinzani wa Uganda Bobi Wine yafunguka kukimbia Nchi kufuatia matukio ya siasa na usalama. Katika taarifa iliyotolewa, Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Robert Kyagulanyi Ssentamu, maarufu kama Bobi Wine, amethibitisha mbele ya Wakaguzi wa haki za binadamu Mjini Geneva kwamba Mke wake, Barbie Itungo Kyagulanyi, na Watoto wao wametoka Uganda kwa sababu za hofu ya maisha yao kufuatia hali tete inayojitokeza nchini mwao baada ya uchaguzi wa Rais. Katika hotuba yake kupitia video mbele ya Geneva Summit for Human Rights and Democracy, Bobi Wine alisema wazi: “Mke wangu na Watoto walilazimika kukimbia nchi kwa hofu ya maisha yao.” - Bobi Wine. Alifafanua kuwa usalama wa familia yake uliathirika sana kutokana na operesheni za vikosi vya usalama zilizoendelea mara tu baada ya uchaguzi wa 15 Januari 2026, ambapo serikali ilitangaza ushindi wa Rais Yoweri Museveni ambayo Bobi Wine ameipinga kwa madai ya udanganyifu wa kura na ukandamizaji wa upinzani. Bobi Wine pia alidai kwamba vikosi vya usalama: “Vilivamia nyumba yangu, vikamtesa Mke wangu, kumfanya asiwe na chaguo ila kuondoka na Watoto wakiwa nje ya nchi.” amesema Habari kwamba familia yake imeondoka Uganda na si tu kutoroka nyumba yao ya Magere imetolewa mara tu baada ya miezi ya mvutano mkali, ikiwa ni pamoja na madai ya mashambulizi, ulinzi mkali wa nyumba yao na vitisho vilivyowekwa na baadhi ya Afisa wa usalama. Katika maneno yake Mjini Geneva, Bobi Wine pia alijumuisha ombi kwa Jumuiya ya kimataifa kuhusu hatua za kulinda haki za binadamu na kuzuia ukandamizaji wa upinzani nchini Uganda. Taarifa hii inakuja katika wakati ambapo Uganda iko chini ya uangalizi wa kimataifa kufuatia ripoti za ghasia, mashambulizi dhidi ya wapinzani wa kisiasa, na madai ya upendeleo wa vyombo vya usalama kuelekea chama tawala. Kwa sasa, bado haijafahamika kwa umma ni nchi gani hasa Barbie Itungo Kyagulanyi na Watoto hao wamekwenda, ila uamuzi wao wa kukimbia unachukuliwa kama hatua ya kulinda usalama wa familia katika mzozo wa kisiasa unaoendelea nchini Uganda. Toa maoni yako #Habari
    0 Comentários 0 Compartilhamentos 391 Visualizações
  • Umoja wa Ulaya wafadhili euro milioni 81 kwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

    Umoja wa Ulaya (EU) umethibitisha kutoa ufadhili wa Euro milioni 81 kwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (RDC), kwa ajili ya kusaidia mpango wa msaada wa kibinadamu katika maeneo ya mashariki ambako mizozo inazidi kuathiri Wananchi.

    Akizungumza kuhusu hatua hii, Msemaji wa Umoja wa Ulaya amesema, “Hii ni hatua yetu ya dhati ya kuhakikisha kwamba jamii zilizo hatarini zinapata msaada wa dharura na huduma za msingi zinazohitajika, hususan kwa wakimbizi na watu waliokumbwa na mizozo.”

    Aidha, Umoja wa Ulaya umesisitiza umuhimu wa kushirikiana na mamlaka za RDC pamoja na mashirika ya misaada ya kibinadamu ili kuhakikisha fedha hizi zinatumika kwa ufanisi na kufikia jamii zinazohitaji zaidi.

    Msemaji huyo aliongeza, “Tutaendelea kushirikiana na washirika wetu wa ndani na kimataifa kuhakikisha kwamba msaada unawafikia walengwa haraka na kwa uwazi, ili kupunguza madhara yanayosababishwa na mapigano yanayoendelea mashariki mwa nchi.”

    Hii ni sehemu ya jitihada kubwa za kimataifa zinazolenga kupunguza mateso ya kibinadamu na kuboresha hali ya maisha kwa familia zinazokabiliwa na mizozo, haswa katika kanda zenye migogoro ya muda mrefu.

    Toa maoni yako
    #Habari
    Umoja wa Ulaya wafadhili euro milioni 81 kwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo. Umoja wa Ulaya (EU) umethibitisha kutoa ufadhili wa Euro milioni 81 kwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (RDC), kwa ajili ya kusaidia mpango wa msaada wa kibinadamu katika maeneo ya mashariki ambako mizozo inazidi kuathiri Wananchi. Akizungumza kuhusu hatua hii, Msemaji wa Umoja wa Ulaya amesema, “Hii ni hatua yetu ya dhati ya kuhakikisha kwamba jamii zilizo hatarini zinapata msaada wa dharura na huduma za msingi zinazohitajika, hususan kwa wakimbizi na watu waliokumbwa na mizozo.” Aidha, Umoja wa Ulaya umesisitiza umuhimu wa kushirikiana na mamlaka za RDC pamoja na mashirika ya misaada ya kibinadamu ili kuhakikisha fedha hizi zinatumika kwa ufanisi na kufikia jamii zinazohitaji zaidi. Msemaji huyo aliongeza, “Tutaendelea kushirikiana na washirika wetu wa ndani na kimataifa kuhakikisha kwamba msaada unawafikia walengwa haraka na kwa uwazi, ili kupunguza madhara yanayosababishwa na mapigano yanayoendelea mashariki mwa nchi.” Hii ni sehemu ya jitihada kubwa za kimataifa zinazolenga kupunguza mateso ya kibinadamu na kuboresha hali ya maisha kwa familia zinazokabiliwa na mizozo, haswa katika kanda zenye migogoro ya muda mrefu. Toa maoni yako #Habari
    0 Comentários 0 Compartilhamentos 251 Visualizações
  • Msanii wa Afrobeats Simi aibua mjadala mzito kuhusu adhabu kwa Wabakaji wa Watoto.

    Msanii wa muziki wa Afrobeats, Simisola Kosoko maarufu kama Simi, amezua mjadala mkubwa katika vyombo vya habari na mitandao ya kijamii baada ya kutoa wito wa kuchukuliwa hatua kali dhidi ya Wanaume wanaobaka Watoto na Wasichana.

    Kwa mujibu wa taarifa zilizoripotiwa na vyombo mbalimbali vya habari nchini Nigeria, nchi hiyo kwa sasa inapitia kipindi kigumu kutokana na ongezeko la matukio ya ukatili wa kijinsia. Visa vya ubakaji dhidi ya Wanawake na Watoto vimeripotiwa katika maeneo tofauti ndani ya wiki za hivi karibuni, jambo lililoibua hasira na maumivu miongoni mwa Wananchi.

    Kupitia ujumbe aliouchapisha katika mtandao wa X usiku wa Jumanne, tarehe 17 Februari 2026, Simi alionyesha wazi ghadhabu yake dhidi ya vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia, hasa vinavyowalenga Watoto wa kike. Msanii huyo aliitaka serikali pamoja na jamii kwa ujumla kuchukua hatua madhubuti kukomesha uhalifu huo.

    Katika ujumbe wake, aliandika: "Nimechoka na nimekasirika sana. Acheni kubaka Wanawake na Watoto. Wanaume wanaobaka Watoto na Wasichana wanapaswa kuhasiwa na kuchomwa moto wakiwa hai.”

    Kauli hiyo imeibua mjadala mpana mtandaoni, huku baadhi ya watu wakimuunga mkono kwa kuonesha uchungu na hasira juu ya matukio ya ubakaji, na wengine wakipinga aina ya adhabu aliyoipendekeza wakisisitiza umuhimu wa kufuata misingi ya sheria na haki za binadamu.

    Wachambuzi wa masuala ya kijamii wanasema kauli ya Simi inaakisi hisia kali za Wananchi wengi wanaohisi mfumo wa haki jinai haujachukua hatua za kutosha kukabiliana na ongezeko la uhalifu wa kijinsia. Hata hivyo, wanasisitiza kuwa mapambano dhidi ya ubakaji yanahitaji mchanganyiko wa hatua za kisheria, elimu ya jamii, pamoja na ulinzi madhubuti kwa waathirika.

    Mjadala unaoendelea unaweka shinikizo kwa mamlaka husika kuimarisha sheria, kuharakisha mashauri ya kesi za ubakaji, na kuhakikisha Wahusika wanawajibishwa kwa mujibu wa sheria za nchi.

    Toa maoni yako
    #Music
    #Habari
    Msanii wa Afrobeats Simi aibua mjadala mzito kuhusu adhabu kwa Wabakaji wa Watoto. Msanii wa muziki wa Afrobeats, Simisola Kosoko maarufu kama Simi, amezua mjadala mkubwa katika vyombo vya habari na mitandao ya kijamii baada ya kutoa wito wa kuchukuliwa hatua kali dhidi ya Wanaume wanaobaka Watoto na Wasichana. Kwa mujibu wa taarifa zilizoripotiwa na vyombo mbalimbali vya habari nchini Nigeria, nchi hiyo kwa sasa inapitia kipindi kigumu kutokana na ongezeko la matukio ya ukatili wa kijinsia. Visa vya ubakaji dhidi ya Wanawake na Watoto vimeripotiwa katika maeneo tofauti ndani ya wiki za hivi karibuni, jambo lililoibua hasira na maumivu miongoni mwa Wananchi. Kupitia ujumbe aliouchapisha katika mtandao wa X usiku wa Jumanne, tarehe 17 Februari 2026, Simi alionyesha wazi ghadhabu yake dhidi ya vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia, hasa vinavyowalenga Watoto wa kike. Msanii huyo aliitaka serikali pamoja na jamii kwa ujumla kuchukua hatua madhubuti kukomesha uhalifu huo. Katika ujumbe wake, aliandika: "Nimechoka na nimekasirika sana. Acheni kubaka Wanawake na Watoto. Wanaume wanaobaka Watoto na Wasichana wanapaswa kuhasiwa na kuchomwa moto wakiwa hai.” Kauli hiyo imeibua mjadala mpana mtandaoni, huku baadhi ya watu wakimuunga mkono kwa kuonesha uchungu na hasira juu ya matukio ya ubakaji, na wengine wakipinga aina ya adhabu aliyoipendekeza wakisisitiza umuhimu wa kufuata misingi ya sheria na haki za binadamu. Wachambuzi wa masuala ya kijamii wanasema kauli ya Simi inaakisi hisia kali za Wananchi wengi wanaohisi mfumo wa haki jinai haujachukua hatua za kutosha kukabiliana na ongezeko la uhalifu wa kijinsia. Hata hivyo, wanasisitiza kuwa mapambano dhidi ya ubakaji yanahitaji mchanganyiko wa hatua za kisheria, elimu ya jamii, pamoja na ulinzi madhubuti kwa waathirika. Mjadala unaoendelea unaweka shinikizo kwa mamlaka husika kuimarisha sheria, kuharakisha mashauri ya kesi za ubakaji, na kuhakikisha Wahusika wanawajibishwa kwa mujibu wa sheria za nchi. Toa maoni yako #Music #Habari
    0 Comentários 0 Compartilhamentos 315 Visualizações
  • Serikali ya Kenya yachukua hatua kali dhidi ya tuhuma za Raia wa Urusi kusambaza video za faragha.

    Serikali ya Kenya imeibuka hadharani na kulaani vikali tuhuma zinazomhusu raia mmoja wa Urusi anayeshukiwa kurekodi na kusambaza video zenye maudhui ya faragha zikihusisha Wanawake wa Kenya bila ridhaa yao.

    Kupitia taarifa rasmi iliyotolewa Jijini Nairobi, mamlaka za Kenya zimeeleza kuwa tukio hilo ni la kusikitisha na haliwezi kuvumiliwa katika jamii inayoheshimu utu na haki za binadamu.

    Katika tamko hilo, serikali imeeleza kuwa tukio hilo ni “kubwa na lisilokubalika”, ikisisitiza kuwa hatua zote muhimu zitachukuliwa ili ukweli ujulikane na haki itendeke. Aidha, imewahakikishia waathirika wanaodaiwa kuwa watapatiwa msaada stahiki wa kisheria na kisaikolojia.

    Vilevile, mamlaka hizo zimeweka bayana kuwa Wahusika wote watakaobainika kuhusika na kitendo hicho watawajibishwa kwa mujibu wa sheria. Serikali imeongeza kuwa haitasita kuchukua hatua kali dhidi ya yeyote anayekiuka faragha na heshima ya wananchi.

    Kashfa hiyo imezua hasira kubwa katika mitandao ya kijamii na miongoni mwa Wananchi, huku wengi wakitaka sheria kali zaidi zichukuliwe dhidi ya wanaosambaza maudhui ya faragha bila idhini. Tukio hili limeibua tena mjadala mpana kuhusu ulinzi wa maisha binafsi na mapambano dhidi ya usambazaji wa maudhui ya faragha bila ridhaa nchini Kenya.

    Mamlaka husika zimebainisha kuwa uchunguzi rasmi unaendelea, na matokeo yake yatatangazwa pindi yatakapokamilika.

    Toa maoni yako
    #Habari
    Serikali ya Kenya yachukua hatua kali dhidi ya tuhuma za Raia wa Urusi kusambaza video za faragha. Serikali ya Kenya imeibuka hadharani na kulaani vikali tuhuma zinazomhusu raia mmoja wa Urusi anayeshukiwa kurekodi na kusambaza video zenye maudhui ya faragha zikihusisha Wanawake wa Kenya bila ridhaa yao. Kupitia taarifa rasmi iliyotolewa Jijini Nairobi, mamlaka za Kenya zimeeleza kuwa tukio hilo ni la kusikitisha na haliwezi kuvumiliwa katika jamii inayoheshimu utu na haki za binadamu. Katika tamko hilo, serikali imeeleza kuwa tukio hilo ni “kubwa na lisilokubalika”, ikisisitiza kuwa hatua zote muhimu zitachukuliwa ili ukweli ujulikane na haki itendeke. Aidha, imewahakikishia waathirika wanaodaiwa kuwa watapatiwa msaada stahiki wa kisheria na kisaikolojia. Vilevile, mamlaka hizo zimeweka bayana kuwa Wahusika wote watakaobainika kuhusika na kitendo hicho watawajibishwa kwa mujibu wa sheria. Serikali imeongeza kuwa haitasita kuchukua hatua kali dhidi ya yeyote anayekiuka faragha na heshima ya wananchi. Kashfa hiyo imezua hasira kubwa katika mitandao ya kijamii na miongoni mwa Wananchi, huku wengi wakitaka sheria kali zaidi zichukuliwe dhidi ya wanaosambaza maudhui ya faragha bila idhini. Tukio hili limeibua tena mjadala mpana kuhusu ulinzi wa maisha binafsi na mapambano dhidi ya usambazaji wa maudhui ya faragha bila ridhaa nchini Kenya. Mamlaka husika zimebainisha kuwa uchunguzi rasmi unaendelea, na matokeo yake yatatangazwa pindi yatakapokamilika. Toa maoni yako #Habari
    0 Comentários 0 Compartilhamentos 264 Visualizações
  • AFC/M23 yasisitiza utekelezaji wa makubaliano ya Doha, yaituhumu Kinshasa kwa “Mbinu za mawasiliano”.

    Muungano wa Waasi wa AFC/M23 nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) umetangaza upya msimamo wake kuhusu wito wa kusitisha mapigano, ukisema uko tayari kutekeleza makubaliano yaliyofikiwa kupitia mchakato wa Doha, huku ukitupia lawama Serikali ya Kinshasa kwa kile ilichokiita “mbinu za mawasiliano” zenye lengo la kupotosha (kutangaza uongo) umma.

    Kupitia taarifa iliyotolewa na Kiongozi wa AFC/M23, Corneille Naanga, Muungano huo ulieleza kuwa uko tayari kuchukua hatua mara moja katika kutekeleza utaratibu wa usitishaji mapigano uliokubaliwa.

    Naanga alisema: "Kufuatia wito unaoendelea wa kusitisha mapigano, AFC/M23 inathibitisha tena dhamira yake ya kutekeleza, bila kuchelewa na kwa nia njema, utaratibu uliokubaliwa katika mfumo wa mchakato wa Doha. Hatua hii inaendana na mantiki ya uwajibikaji wa kisiasa na nia ya dhati ya kufikia suluhu ya mazungumzo, ya kudumu na shirikishi ya mzozo huu.”

    Kauli hiyo inaashiria msimamo wa AFC/M23 wa kuonyesha utayari wa kushiriki katika juhudi za kidiplomasia zinazolenga kumaliza mzozo wa muda mrefu mashariki mwa DRC.

    Hata hivyo, Muungano huo uliikosoa vikali Serikali ya DRC yenye makao yake Kinshasa, ukidai kuwa tangazo la kukubali kusitisha mapigano si la dhati.

    Naanga aliongeza: “Kwa AFC, kile kinachodaiwa kuwa kukubali kwa Kinshasa kanuni ya kusitisha mapigano ni mbinu tu ya mawasiliano na jaribio la upotoshaji linalolenga kudanganya maoni ya kitaifa na kimataifa, kujiepusha na wajibu wake na kuficha mwendelezo wa mkakati wa kijeshi usiobadilika.”

    Kauli hiyo inaibua mvutano mpya wa kisiasa wakati juhudi za kimataifa zikiongezeka kuhimiza pande husika kurejea katika meza ya mazungumzo kupitia mchakato wa Doha.

    Mzozo kati ya serikali ya DRC na AFC/M23 umeendelea kuathiri hali ya usalama na kibinadamu mashariki mwa nchi hiyo, huku jumuiya ya kimataifa ikiendelea kusisitiza umuhimu wa suluhu ya mazungumzo badala ya mapambano ya kijeshi.

    Toa maoni yako
    #Habari
    AFC/M23 yasisitiza utekelezaji wa makubaliano ya Doha, yaituhumu Kinshasa kwa “Mbinu za mawasiliano”. Muungano wa Waasi wa AFC/M23 nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) umetangaza upya msimamo wake kuhusu wito wa kusitisha mapigano, ukisema uko tayari kutekeleza makubaliano yaliyofikiwa kupitia mchakato wa Doha, huku ukitupia lawama Serikali ya Kinshasa kwa kile ilichokiita “mbinu za mawasiliano” zenye lengo la kupotosha (kutangaza uongo) umma. Kupitia taarifa iliyotolewa na Kiongozi wa AFC/M23, Corneille Naanga, Muungano huo ulieleza kuwa uko tayari kuchukua hatua mara moja katika kutekeleza utaratibu wa usitishaji mapigano uliokubaliwa. Naanga alisema: "Kufuatia wito unaoendelea wa kusitisha mapigano, AFC/M23 inathibitisha tena dhamira yake ya kutekeleza, bila kuchelewa na kwa nia njema, utaratibu uliokubaliwa katika mfumo wa mchakato wa Doha. Hatua hii inaendana na mantiki ya uwajibikaji wa kisiasa na nia ya dhati ya kufikia suluhu ya mazungumzo, ya kudumu na shirikishi ya mzozo huu.” Kauli hiyo inaashiria msimamo wa AFC/M23 wa kuonyesha utayari wa kushiriki katika juhudi za kidiplomasia zinazolenga kumaliza mzozo wa muda mrefu mashariki mwa DRC. Hata hivyo, Muungano huo uliikosoa vikali Serikali ya DRC yenye makao yake Kinshasa, ukidai kuwa tangazo la kukubali kusitisha mapigano si la dhati. Naanga aliongeza: “Kwa AFC, kile kinachodaiwa kuwa kukubali kwa Kinshasa kanuni ya kusitisha mapigano ni mbinu tu ya mawasiliano na jaribio la upotoshaji linalolenga kudanganya maoni ya kitaifa na kimataifa, kujiepusha na wajibu wake na kuficha mwendelezo wa mkakati wa kijeshi usiobadilika.” Kauli hiyo inaibua mvutano mpya wa kisiasa wakati juhudi za kimataifa zikiongezeka kuhimiza pande husika kurejea katika meza ya mazungumzo kupitia mchakato wa Doha. Mzozo kati ya serikali ya DRC na AFC/M23 umeendelea kuathiri hali ya usalama na kibinadamu mashariki mwa nchi hiyo, huku jumuiya ya kimataifa ikiendelea kusisitiza umuhimu wa suluhu ya mazungumzo badala ya mapambano ya kijeshi. Toa maoni yako #Habari
    0 Comentários 0 Compartilhamentos 159 Visualizações
  • Waziri wa Habari Uganda akemea shambulio la kijeshi nyumbani kwa Bobi Wine.

    Waziri wa Habari nchini Uganda, Chris Baryomunsi, amelaani vikali madai ya shambulio la kijeshi lililofanyika katika makazi ya Mwanasiasa wa upinzani Bobi Wine, akisisitiza kuwa hakuna sababu ya kisheria ya kumzuia kurejea nyumbani kwake.

    Akizungumza na shirika la habari la Reuters, Baryomunsi alisema kuwa Bobi Wine hakufanya kosa lolote na anastahili kulindwa kama raia mwingine yeyote wa Uganda. Alieleza wazi kuwa hatua zozote za vitisho au uvamizi dhidi ya makazi ya raia hazikubaliki. Alisema, “Bobi Wine hana kosa lolote alilofanya, na ana haki kamili ya kurejea nyumbani kwake bila hofu.”

    Kwa upande wake, Bobi Wine amekuwa akidai kwa muda mrefu kuwa yuko mafichoni akihofia usalama wake, baada ya kudai kuwa jeshi la Uganda lilipewa maagizo ya kumtafuta na kumkamata. Kiongozi huyo wa upinzani pia amedai kuwa baadhi ya Wanafamilia wake waliwahi kukamatwa kwa nguvu, jambo lililoongeza hofu juu ya usalama wake binafsi.

    Katika mazingira hayo ya mvutano, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Uganda, Jenerali Muhoozi Kainerugaba, amekuwa akitoa kauli kupitia mtandao wa X (Zamani Twitter), akidokeza kuwa kumkamata Bobi Wine si jambo gumu kwani wanajua alipojificha. Kauli hizo zimeibua mjadala mkubwa ndani na nje ya Uganda kuhusu heshima ya haki za binadamu na uhuru wa kisiasa.

    Tukio hili linaendelea kufuatiliwa kwa karibu na wadau wa siasa pamoja na mashirika ya haki za binadamu, huku wito ukitolewa kwa mamlaka za Uganda kuheshimu sheria, kulinda raia wao, na kuhakikisha kuwa tofauti za kisiasa hazigeuki kuwa vitisho vya usalama kwa watu binafsi.

    Toa maoni yako
    #Habari
    Waziri wa Habari Uganda akemea shambulio la kijeshi nyumbani kwa Bobi Wine. Waziri wa Habari nchini Uganda, Chris Baryomunsi, amelaani vikali madai ya shambulio la kijeshi lililofanyika katika makazi ya Mwanasiasa wa upinzani Bobi Wine, akisisitiza kuwa hakuna sababu ya kisheria ya kumzuia kurejea nyumbani kwake. Akizungumza na shirika la habari la Reuters, Baryomunsi alisema kuwa Bobi Wine hakufanya kosa lolote na anastahili kulindwa kama raia mwingine yeyote wa Uganda. Alieleza wazi kuwa hatua zozote za vitisho au uvamizi dhidi ya makazi ya raia hazikubaliki. Alisema, “Bobi Wine hana kosa lolote alilofanya, na ana haki kamili ya kurejea nyumbani kwake bila hofu.” Kwa upande wake, Bobi Wine amekuwa akidai kwa muda mrefu kuwa yuko mafichoni akihofia usalama wake, baada ya kudai kuwa jeshi la Uganda lilipewa maagizo ya kumtafuta na kumkamata. Kiongozi huyo wa upinzani pia amedai kuwa baadhi ya Wanafamilia wake waliwahi kukamatwa kwa nguvu, jambo lililoongeza hofu juu ya usalama wake binafsi. Katika mazingira hayo ya mvutano, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Uganda, Jenerali Muhoozi Kainerugaba, amekuwa akitoa kauli kupitia mtandao wa X (Zamani Twitter), akidokeza kuwa kumkamata Bobi Wine si jambo gumu kwani wanajua alipojificha. Kauli hizo zimeibua mjadala mkubwa ndani na nje ya Uganda kuhusu heshima ya haki za binadamu na uhuru wa kisiasa. Tukio hili linaendelea kufuatiliwa kwa karibu na wadau wa siasa pamoja na mashirika ya haki za binadamu, huku wito ukitolewa kwa mamlaka za Uganda kuheshimu sheria, kulinda raia wao, na kuhakikisha kuwa tofauti za kisiasa hazigeuki kuwa vitisho vya usalama kwa watu binafsi. Toa maoni yako #Habari
    0 Comentários 0 Compartilhamentos 217 Visualizações
  • Ubalozi wa RDC Burundi wakanusha taarifa za orodha ya Raia kurudi kwa hiari Uvira.

    Bujumbura, Burundi, Ubalozi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (RDC) nchini Burundi umekanusha taarifa zinazosambaa mitandaoni zikidai kuwa umefungua orodha ya usajili kwa Raia wa Congo wanaotaka kurejea kwa hiari katika Mji wa Uvira, Mkoani Sud-Kivu.

    Taarifa hizo, zilizosambazwa kwa kasi kupitia mitandao ya kijamii hususan makundi ya WhatsApp, zilisababisha idadi ya Raia wa Congo kujitokeza katika majengo ya ubalozi wakiamini kuwa kuna mchakato rasmi wa kurejea unaoendelea.

    Akizungumza, Balozi wa RDC nchini Burundi, Willy Mulamba Mabika, amesema ubalozi hauna mamlaka ya kuandaa au kuruhusu kurejea kwa hiari kwa Wakimbizi.

    “Ubalozi hauna haki ya kufungua mpaka wala kuruhusu kurejea kwa wakimbizi nchini mwao. Jukumu hili ni la Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (HCR), Serikali ya Burundi, na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo baada ya kufanyika tathmini ya awali ya hali ya usalama,” amenukuliwa akisema Balozi huyo.

    Kwa mujibu wa taratibu za kimataifa, kurejea kwa hiari kwa Wakimbizi huratibiwa na HCR, hufanyika kwa makubaliano kati ya nchi mwenyeji na nchi ya asili, na hutegemea tathmini ya kiusalama inayohakikisha kurejea kwa usalama, heshima na kwa hiari.

    Hakuna tamko lolote kutoka kwa HCR, Serikali ya Burundi au Serikali ya RDC linalothibitisha kuwepo kwa mpango wa sasa wa kurejesha Wakimbizi wa Congo kutoka Burundi kwenda Uvira. Wachambuzi huru wanasema kujitokeza kwa Raia wa Congo mbele ya ubalozi kunaweza kuakisi hamu ya kurejea nyumbani, inayochochewa na matarajio ya kuimarika kwa hali ya usalama na juhudi zinazoendelea za kurejesha mamlaka ya dola katika eneo la Uvira.

    Ubalozi umehimiza umma kuwa makini dhidi ya taarifa zisizothibitishwa na kuzingatia mawasiliano rasmi pekee kutoka HCR na mamlaka husika.

    “Upotoshaji wa taarifa katika mazingira nyeti ya kibinadamu na kiusalama unaweza kuwaweka watu hatarini bila sababu,” balozi ameongeza.

    Hakuna orodha rasmi iliyofunguliwa katika Ubalozi wa RDC nchini Burundi kwa ajili ya kurejea kwa hiari kwa Raia wa Congo kwenda Uvira; madai hayo hayana msingi na yamekanushwa rasmi.

    Ubalozi wa RDC Burundi wakanusha taarifa za orodha ya Raia kurudi kwa hiari Uvira. Bujumbura, Burundi, Ubalozi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (RDC) nchini Burundi umekanusha taarifa zinazosambaa mitandaoni zikidai kuwa umefungua orodha ya usajili kwa Raia wa Congo wanaotaka kurejea kwa hiari katika Mji wa Uvira, Mkoani Sud-Kivu. Taarifa hizo, zilizosambazwa kwa kasi kupitia mitandao ya kijamii hususan makundi ya WhatsApp, zilisababisha idadi ya Raia wa Congo kujitokeza katika majengo ya ubalozi wakiamini kuwa kuna mchakato rasmi wa kurejea unaoendelea. Akizungumza, Balozi wa RDC nchini Burundi, Willy Mulamba Mabika, amesema ubalozi hauna mamlaka ya kuandaa au kuruhusu kurejea kwa hiari kwa Wakimbizi. “Ubalozi hauna haki ya kufungua mpaka wala kuruhusu kurejea kwa wakimbizi nchini mwao. Jukumu hili ni la Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (HCR), Serikali ya Burundi, na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo baada ya kufanyika tathmini ya awali ya hali ya usalama,” amenukuliwa akisema Balozi huyo. Kwa mujibu wa taratibu za kimataifa, kurejea kwa hiari kwa Wakimbizi huratibiwa na HCR, hufanyika kwa makubaliano kati ya nchi mwenyeji na nchi ya asili, na hutegemea tathmini ya kiusalama inayohakikisha kurejea kwa usalama, heshima na kwa hiari. Hakuna tamko lolote kutoka kwa HCR, Serikali ya Burundi au Serikali ya RDC linalothibitisha kuwepo kwa mpango wa sasa wa kurejesha Wakimbizi wa Congo kutoka Burundi kwenda Uvira. Wachambuzi huru wanasema kujitokeza kwa Raia wa Congo mbele ya ubalozi kunaweza kuakisi hamu ya kurejea nyumbani, inayochochewa na matarajio ya kuimarika kwa hali ya usalama na juhudi zinazoendelea za kurejesha mamlaka ya dola katika eneo la Uvira. Ubalozi umehimiza umma kuwa makini dhidi ya taarifa zisizothibitishwa na kuzingatia mawasiliano rasmi pekee kutoka HCR na mamlaka husika. “Upotoshaji wa taarifa katika mazingira nyeti ya kibinadamu na kiusalama unaweza kuwaweka watu hatarini bila sababu,” balozi ameongeza. Hakuna orodha rasmi iliyofunguliwa katika Ubalozi wa RDC nchini Burundi kwa ajili ya kurejea kwa hiari kwa Raia wa Congo kwenda Uvira; madai hayo hayana msingi na yamekanushwa rasmi.
    0 Comentários 0 Compartilhamentos 185 Visualizações
  • NASA yatahadharisha: uwezekano wa Dunia kukosa oksijeni Katika miaka ijayo.

    Shirika la Kitaifa la Anga na Nafasi ya Juu la Marekani (NASA) limetoa taarifa ya kisayansi inayoashiria uwezekano wa kutoweka kwa hewa safi ya oksijeni duniani katika kipindi cha miaka mingi ijayo.

    Kwa mujibu wa NASA, jambo hili halitasababishwa na shughuli za kibinadamu kama vile uchafuzi wa mazingira pekee, bali linahusiana zaidi na mabadiliko ya kiasili ya Dunia na Jua. Katika uchambuzi wake, NASA inabainisha kuwa:

    "Katika mabilioni ya miaka iliyopita, Dunia haikuwa na oksijeni ya kutosha. Kwa hiyo, kuna uwezekano kuwa hali kama hiyo ikajirudia tena katika mamilioni ya miaka ijayo," wamesema watafiti wa NASA.

    Hali hii inaweza kuathiri sio tu maisha ya binadamu bali pia viumbe hai wote wanaotegemea oksijeni kuishi. Ingawa ni tukio linalotabiriwa kutokea baada ya mamilioni ya miaka, Wanasayansi wanasema ni muhimu kwa jamii ya kimataifa kulielewa na kuendelea na utafiti zaidi kuhusu maisha ya baadaye ya Dunia.

    Kwa sasa, hakuna sababu ya hofu ya moja kwa moja, lakini onyo hili linaongeza msisitizo juu ya umuhimu wa kulinda mazingira na kuelewa kwa kina mfumo wa ikolojia wa sayari yetu.

    Toa maoni yako
    NASA yatahadharisha: uwezekano wa Dunia kukosa oksijeni Katika miaka ijayo. Shirika la Kitaifa la Anga na Nafasi ya Juu la Marekani (NASA) limetoa taarifa ya kisayansi inayoashiria uwezekano wa kutoweka kwa hewa safi ya oksijeni duniani katika kipindi cha miaka mingi ijayo. Kwa mujibu wa NASA, jambo hili halitasababishwa na shughuli za kibinadamu kama vile uchafuzi wa mazingira pekee, bali linahusiana zaidi na mabadiliko ya kiasili ya Dunia na Jua. Katika uchambuzi wake, NASA inabainisha kuwa: "Katika mabilioni ya miaka iliyopita, Dunia haikuwa na oksijeni ya kutosha. Kwa hiyo, kuna uwezekano kuwa hali kama hiyo ikajirudia tena katika mamilioni ya miaka ijayo," wamesema watafiti wa NASA. Hali hii inaweza kuathiri sio tu maisha ya binadamu bali pia viumbe hai wote wanaotegemea oksijeni kuishi. Ingawa ni tukio linalotabiriwa kutokea baada ya mamilioni ya miaka, Wanasayansi wanasema ni muhimu kwa jamii ya kimataifa kulielewa na kuendelea na utafiti zaidi kuhusu maisha ya baadaye ya Dunia. Kwa sasa, hakuna sababu ya hofu ya moja kwa moja, lakini onyo hili linaongeza msisitizo juu ya umuhimu wa kulinda mazingira na kuelewa kwa kina mfumo wa ikolojia wa sayari yetu. Toa maoni yako
    Like
    1
    0 Comentários 0 Compartilhamentos 1K Visualizações
  • Israel yasema itaendelea kusimamia usalama Gaza, licha ya makubaliano ya usitishaji vita.

    Katika taarifa mpya iliyoibua mijadala ya kisiasa na kidiplomasia, Serikali ya Israel imesisitiza kuwa haitakubali kuachia jukumu la usalama wa Ukanda wa Gaza mikononi mwa vikosi vya kimataifa, licha ya kusaini makubaliano ya usitishaji vita yaliyosimamiwa na Marekani.

    Kupitia kikao na Baraza lake la Mawaziri, Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, alinukuliwa akisema:

    “Israel itaamua yenyewe ni lini na wapi itaendelea kuwakabili maadui zake. Hatutakubali kabisa nchi yoyote kutuamulia kuhusu usalama wetu.”

    Kauli hiyo imekuja muda mfupi baada ya makubaliano ya muda ya usitishaji mapigano kuwasilishwa, yakiruhusu kuundwa kwa kikosi cha kimataifa kitakacholinda amani na usambazaji wa misaada ya kibinadamu ndani ya Gaza.

    Kulingana na taarifa zilizotolewa, kikosi hicho kitapangwa kutoka mataifa ya Kiarabu au Kiislamu, na kazi yake kuu itakuwa kuhakikisha usalama wa Raia na kusimamia utekelezaji wa masharti ya kusitisha vita.

    Hata hivyo, Netanyahu ameeleza wasiwasi mkubwa juu ya mpango huo:

    “Tutashirikiana pale inapobidi, lakini hatutawahi kukubali Gaza kuwa chini ya mamlaka ya nje bila ridhaa ya Israel. Usalama wa Raia wetu ndio kipaumbele cha kwanza.”

    Kwa mujibu wa Afisa wa Marekani, makubaliano haya ni sehemu ya juhudi za muda mrefu kurejesha utulivu katika eneo hilo, lakini yanategemea ushirikiano wa pande zote mbili, jambo ambalo linazidi kuonekana kuwa gumu kutokana na msimamo wa Israel.

    Hii ni ishara kwamba licha ya mapendekezo ya kimataifa, Israel bado inashikilia msimamo wake wa kulinda mamlaka kamili ya usalama ndani ya Gaza, hatua inayoweza kuchelewesha utekelezaji wa makubaliano haya mapya.

    Je, Israel inaweza kusimamia amani Gaza bila msaada wa Jumuiya ya kimataifa? Au je, dunia inapaswa kuingilia kati kwa nguvu zaidi?

    Toa maoni yako
    Israel yasema itaendelea kusimamia usalama Gaza, licha ya makubaliano ya usitishaji vita. Katika taarifa mpya iliyoibua mijadala ya kisiasa na kidiplomasia, Serikali ya Israel imesisitiza kuwa haitakubali kuachia jukumu la usalama wa Ukanda wa Gaza mikononi mwa vikosi vya kimataifa, licha ya kusaini makubaliano ya usitishaji vita yaliyosimamiwa na Marekani. Kupitia kikao na Baraza lake la Mawaziri, Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, alinukuliwa akisema: “Israel itaamua yenyewe ni lini na wapi itaendelea kuwakabili maadui zake. Hatutakubali kabisa nchi yoyote kutuamulia kuhusu usalama wetu.” Kauli hiyo imekuja muda mfupi baada ya makubaliano ya muda ya usitishaji mapigano kuwasilishwa, yakiruhusu kuundwa kwa kikosi cha kimataifa kitakacholinda amani na usambazaji wa misaada ya kibinadamu ndani ya Gaza. Kulingana na taarifa zilizotolewa, kikosi hicho kitapangwa kutoka mataifa ya Kiarabu au Kiislamu, na kazi yake kuu itakuwa kuhakikisha usalama wa Raia na kusimamia utekelezaji wa masharti ya kusitisha vita. Hata hivyo, Netanyahu ameeleza wasiwasi mkubwa juu ya mpango huo: “Tutashirikiana pale inapobidi, lakini hatutawahi kukubali Gaza kuwa chini ya mamlaka ya nje bila ridhaa ya Israel. Usalama wa Raia wetu ndio kipaumbele cha kwanza.” Kwa mujibu wa Afisa wa Marekani, makubaliano haya ni sehemu ya juhudi za muda mrefu kurejesha utulivu katika eneo hilo, lakini yanategemea ushirikiano wa pande zote mbili, jambo ambalo linazidi kuonekana kuwa gumu kutokana na msimamo wa Israel. Hii ni ishara kwamba licha ya mapendekezo ya kimataifa, Israel bado inashikilia msimamo wake wa kulinda mamlaka kamili ya usalama ndani ya Gaza, hatua inayoweza kuchelewesha utekelezaji wa makubaliano haya mapya. Je, Israel inaweza kusimamia amani Gaza bila msaada wa Jumuiya ya kimataifa? Au je, dunia inapaswa kuingilia kati kwa nguvu zaidi? Toa maoni yako
    Love
    1
    0 Comentários 0 Compartilhamentos 2K Visualizações
  • Polisi nchini Gambia wamewafungulia mashtaka wanawake watatu kufuatia kifo cha mtoto wa kike mwenye umri wa mwezi mmoja, aliyefanyiwa ukeketaji (FGM), tukio lililoibua hasira kitaifa licha ya marufuku iliyowekwa miaka kumi iliyopita.

    Kwa mujibu wa Polisi, mashtaka hayo yamewasilishwa chini ya Sheria ya Marekebisho ya Wanawake ya mwaka 2015, inayopiga marufuku ukeketaji. Mmoja wa wanawake hao anakabiliwa na kifungo cha maisha na amewekwa rumande, huku wengine wawili wakishtakiwa kama washirika na kupewa dhamana.

    Mwenyekiti wa Tume ya Kitaifa ya Haki za Binadamu (NHRC), Emmanuel Joof, amesema tukio hilo ni onyo kwa taifa, akisisitiza kuwa ukeketaji si utamaduni tu bali ni kosa la jinai, ukiukaji wa haki za binadamu, na katika visa vingine, husababisha vifo. NHRC inasisitiza kuwa hakuna sababu za kitamaduni au kiasili zinazoweza kuhalalisha madhara kwa watoto. Licha ya marufuku, ukeketaji bado umeenea nchini Gambia, na mwaka jana wabunge walikataa muswada wa kufuta marufuku hiyo
    Polisi nchini Gambia wamewafungulia mashtaka wanawake watatu kufuatia kifo cha mtoto wa kike mwenye umri wa mwezi mmoja, aliyefanyiwa ukeketaji (FGM), tukio lililoibua hasira kitaifa licha ya marufuku iliyowekwa miaka kumi iliyopita. Kwa mujibu wa Polisi, mashtaka hayo yamewasilishwa chini ya Sheria ya Marekebisho ya Wanawake ya mwaka 2015, inayopiga marufuku ukeketaji. Mmoja wa wanawake hao anakabiliwa na kifungo cha maisha na amewekwa rumande, huku wengine wawili wakishtakiwa kama washirika na kupewa dhamana. Mwenyekiti wa Tume ya Kitaifa ya Haki za Binadamu (NHRC), Emmanuel Joof, amesema tukio hilo ni onyo kwa taifa, akisisitiza kuwa ukeketaji si utamaduni tu bali ni kosa la jinai, ukiukaji wa haki za binadamu, na katika visa vingine, husababisha vifo. NHRC inasisitiza kuwa hakuna sababu za kitamaduni au kiasili zinazoweza kuhalalisha madhara kwa watoto. Licha ya marufuku, ukeketaji bado umeenea nchini Gambia, na mwaka jana wabunge walikataa muswada wa kufuta marufuku hiyo
    0 Comentários 0 Compartilhamentos 1K Visualizações
  • Mwanzo 49:3-4
    [3]Reubeni, u mzaliwa wangu wa kwanza,
    Nguvu zangu, na malimbuko ya uwezo wangu.
    Umewapita wengine kwa ukuu na kwa nguvu.

    [4]Umeruka mpaka kama maji, basi usiwe na ukuu,
    Kwa sababu ulikipanda kitanda cha baba yako,
    Ukakitia unajisi; alikipandia kitanda changu

    Tazama athari ya uzinzi ulivyo mpotezea baraka za ukuu na nguvu Ruben

    Kwa kawaida baraka za ufalme urithi mzaliwa wa kwanza lakini sababu ya uzinzi alinyang'anywa baraka za agano za ukuu.

    Starehehe ya sekunde chache ilisababisha Ruben awa cost (awagharimu ) kizazi chake chote kwa sababu ya tamaa ya zinaa.

    Kumbukumbu la Torati 27:20
    [20]Na alaaniwe alalaye na mke wa baba yake, kwa kuwa amefunua mavazi ya babaye. Na watu wote waseme, Amina.

    Yakobo alishindwa kumpa baraka mwanae na tuona miaka ya mbele Mungu pia anapitisha kuwa sheria pia kwamba amelaaniwa alalaye kwenye kitanda cha baba yake hapa wameenda mbali kuwa amefunua mavazi ya mama yake.

    Point yangu kubwa ni namna uzinzi unavyo weza kukubebesha laana za makusudi na laana hizo zina cost kizazi na kizazi.

    Mtu ukisha okoka unapaswakuhakikisha uasherati na uzinzi havitajwi kwako kabisa kwani vikitajwa kwako unalitukanisha jina la kristo na matokeo yake unapokea laana za makusudi .

    Unajua ukikosa hofu ya Mungu, unaweza kufanya madudu ya ajabu!!! yasiyotegemewa kufanyika kwako. Wewe mwenyewe ni shahidi tu,jiangalie pale ulipokuwa huna hofu ya Mungu, kisha angalia yale uliyokuwa ukiyafanya… Ni hatariiii.!!!

    Lakini pia,bila shaka kulikuwa na ukaribu sana kati ya Bilha Sulia na Reubeni hata wakajikuta wakiangukia zinaa. Kwa sababu Rubeni hakumbaka bali walikubaliana kwa hiyo kulikuwa na ukaribu kati yao.

    Ebu fikiria pia hili,kisha jichukue wewe mwenyewe jiweke karibu sana kimazoea na mtu fulani awe mdada au mkaka ambaye ni ndugu wa damu kabisa. Kisha mkawa mnakaa nyumba moja,kisha chukulia mmezoeana sana kiasi kwamba unamfurahia na kuzungumza naye mara kwa mara muda ambao mnabakiaga wawili tu kwenye jumba kubwa namna hiyo.

    Unafikiri mwisho wake ni nini? Bila shaka ndo unasikia binadamu siyo ndugu na unaangukia kwenye zinaa na ukifanya hivyo siyo tu kuharibu kesho yako kama wanao pia wajamjua Mungu kuvunja hiyo laana inatembea mpka kizazi chako chote.

    *Sina lugha nzuri ya kuioma zinaa kama kitu chema katika maisha haya tunayo ishi .usipo kubali kulinda mwili wako shetani atautumia kama sehemu ya kupitisha ajenda zake matokeo yake utaangukia zambini.*

    Yatazame matokeo yq uzinzi wrqfu tazama faida yake kisha amua kipi ulicho amua kukiishi .

    Ruben wakati Yusuph watoto zake wanaingizwa kuwa kabira kutokana na ushujaa wa baba yao yeye Rubeni kutokana na uzinzi aliwaachia sehemu ya laana zake.

    Matokeo ya uzinzi hayakuathiri wewe tu yanaathiri mpaka kizazi chako kama usipo omba.

    Natamani uombe Mungu leo akutoe kabisa katika mateso ya uzinzi na uasherati kwani hayawezi kukusaidia zaidi ya kukuangamiza.

    Nashukuru sana kwa kusoma jumbe hii na Mungu akageuza moyo wako nitafarijika sana.

    Naitwa Sylvester Mwakabende kutoka (build new eden)

    Karibu katika group letu la Whatsapp
    https://chat.whatsapp.com/IxkPEsnxi02ExNGrlmbWR4

    Simu :0622625340
    #Restore men position
    #Build new eden
    Mwanzo 49:3-4 [3]Reubeni, u mzaliwa wangu wa kwanza, Nguvu zangu, na malimbuko ya uwezo wangu. Umewapita wengine kwa ukuu na kwa nguvu. [4]Umeruka mpaka kama maji, basi usiwe na ukuu, Kwa sababu ulikipanda kitanda cha baba yako, Ukakitia unajisi; alikipandia kitanda changu Tazama athari ya uzinzi ulivyo mpotezea baraka za ukuu na nguvu Ruben Kwa kawaida baraka za ufalme urithi mzaliwa wa kwanza lakini sababu ya uzinzi alinyang'anywa baraka za agano za ukuu. Starehehe ya sekunde chache ilisababisha Ruben awa cost (awagharimu ) kizazi chake chote kwa sababu ya tamaa ya zinaa. Kumbukumbu la Torati 27:20 [20]Na alaaniwe alalaye na mke wa baba yake, kwa kuwa amefunua mavazi ya babaye. Na watu wote waseme, Amina. Yakobo alishindwa kumpa baraka mwanae na tuona miaka ya mbele Mungu pia anapitisha kuwa sheria pia kwamba amelaaniwa alalaye kwenye kitanda cha baba yake hapa wameenda mbali kuwa amefunua mavazi ya mama yake. Point yangu kubwa ni namna uzinzi unavyo weza kukubebesha laana za makusudi na laana hizo zina cost kizazi na kizazi. Mtu ukisha okoka unapaswakuhakikisha uasherati na uzinzi havitajwi kwako kabisa kwani vikitajwa kwako unalitukanisha jina la kristo na matokeo yake unapokea laana za makusudi . Unajua ukikosa hofu ya Mungu, unaweza kufanya madudu ya ajabu!!! yasiyotegemewa kufanyika kwako. Wewe mwenyewe ni shahidi tu,jiangalie pale ulipokuwa huna hofu ya Mungu, kisha angalia yale uliyokuwa ukiyafanya… Ni hatariiii.!!! Lakini pia,bila shaka kulikuwa na ukaribu sana kati ya Bilha Sulia na Reubeni hata wakajikuta wakiangukia zinaa. Kwa sababu Rubeni hakumbaka bali walikubaliana kwa hiyo kulikuwa na ukaribu kati yao. Ebu fikiria pia hili,kisha jichukue wewe mwenyewe jiweke karibu sana kimazoea na mtu fulani awe mdada au mkaka ambaye ni ndugu wa damu kabisa. Kisha mkawa mnakaa nyumba moja,kisha chukulia mmezoeana sana kiasi kwamba unamfurahia na kuzungumza naye mara kwa mara muda ambao mnabakiaga wawili tu kwenye jumba kubwa namna hiyo. Unafikiri mwisho wake ni nini? Bila shaka ndo unasikia binadamu siyo ndugu na unaangukia kwenye zinaa na ukifanya hivyo siyo tu kuharibu kesho yako kama wanao pia wajamjua Mungu kuvunja hiyo laana inatembea mpka kizazi chako chote. *Sina lugha nzuri ya kuioma zinaa kama kitu chema katika maisha haya tunayo ishi .usipo kubali kulinda mwili wako shetani atautumia kama sehemu ya kupitisha ajenda zake matokeo yake utaangukia zambini.* Yatazame matokeo yq uzinzi wrqfu tazama faida yake kisha amua kipi ulicho amua kukiishi . Ruben wakati Yusuph watoto zake wanaingizwa kuwa kabira kutokana na ushujaa wa baba yao yeye Rubeni kutokana na uzinzi aliwaachia sehemu ya laana zake. Matokeo ya uzinzi hayakuathiri wewe tu yanaathiri mpaka kizazi chako kama usipo omba. Natamani uombe Mungu leo akutoe kabisa katika mateso ya uzinzi na uasherati kwani hayawezi kukusaidia zaidi ya kukuangamiza. Nashukuru sana kwa kusoma jumbe hii na Mungu akageuza moyo wako nitafarijika sana. Naitwa Sylvester Mwakabende kutoka (build new eden) Karibu katika group letu la Whatsapp https://chat.whatsapp.com/IxkPEsnxi02ExNGrlmbWR4 Simu :0622625340 #Restore men position #Build new eden
    0 Comentários 0 Compartilhamentos 2K Visualizações
  • *Roho mtakatifu kama mlinzi wetu*

    Isaya 4:5-6
    [5]Tena juu ya makao yote ya mlima Sayuni, na juu ya makusanyiko yake, BWANA ataumba *wingu na moshi wakati wa mchana, na mwangaza wa miali ya moto wakati wa usiku;* kwa maana juu ya utukufu wote itatandazwa sitara.
    .
    [6]Kisha kutakuwa na hema kuwa uvuli wakati wa mchana kwa sababu ya hari, na kuwa mahali pa kukimbilia na kujificha wakati wa tufani na mvua.


    Wingu linalozungumzwa hapo kwenye agano la kale ni *Roho mtakatifu*

    Kumbe ukimkubali Kristo na kuuoshi wokovu roho wa Bwana anakuwa ndani yako na kazi moja wapo ya huyo *roho ni kukulinda wewe ulieamini*

    Mtu aliye mshika kristo ns kumuamini na kumpokea roho wake wakati wa mchana anafunikwa na kutulizwa na *Bwana na wakati wa usiku anamulikwa na Bwana*


    Kumbe kama roho wa Mungu anatumulika na kutukinga nini kinafanya watu wa Mungu tushindwe kuziishi ahadi ,*tumemuwekea mipaka roho mtakatifu* tukiamini *kunena kwa lugha ndo kipawa na jukumu la roho mtakatifu*

    Sasa tukitizama wakati taifa la islaeri limetoka misri lilikuwa linaongozwa na wingu la Bwana.

    Kutoka 13:21-22
    [21] *BWANA naye akawatangulia mchana ndani ya wingu mfano wa nguzo, ili awaongoze njia*; na usiku, *ndani ya moto mfano wa nguzo, ili kuwapa nuru*; wapate kusafiri mchana na usiku;*

    [22]ile nguzo ya wingu *haikuondoka mchana, wala ile nguzo ya moto haikuondoka usiku,* mbele ya hao watu.

    Hivi ndivyo roho wa Mungu anavyo paswa kukuongoza wakati wa mchana na wakati wa usiku .

    Ukiwa na roho wa Bwana na akawa rafiki yako na kiongozi wako utafanya biashara kwa kubahatisha badala yake yeye atakuongoza uza kitu chenye wateja.

    Unaweza mkaribisha jirani yako kujifunza neno na sisi kwa kujoin link hapa chini
    https://chat.whatsapp.com/IxkPEsnxi02ExNGrlmbWR4

    Walokole tunakosa jicho la kuona fursa sababu tumemuwekea mipaka roho mtakatifu na wakati mwingine anatupa wazo tunalizimisha kwa kuto kujiamini na matokeo yake tunabaki jinsi tulivyo.

    Mtu aliye okoka na *akakubali kutii ndiye anayepaswa kula mema ya nchi* lakini imekuwa tofauti na uhalisia mtu ameokoka anaoshi dhana ya kuamini kuwa atakula kwa jasho iyo ilifanya kazi kabla ya wewe kuokoka saizi wewe unakula kwa wazo la kiMungu linalo shushwa na roho mtakatifu na wewe ukichukua hatua linageuka na kuleta matokeo .

    Musa aliijua siri hii ndo mana pasipo wingu akuenda mbele au kurudi nyuma.

    Kutoka 40:37
    [37]bali kama lile wingu halikuinuliwa, wakati ule hawakusafiri hata siku ile lilipoinuliwa tena.

    Cha kujiuliza mimi na wewe ni hatua ngapi yumepiga bila kuongozwa na roho mtakatifu na tukapelekea kupoteza thamani zetu .

    Iko haja turudi kuitafuta toba kwani ni hatua tulienda mbele lakini kumbe ni shetani *alitutenda tu kwa akiri*

    Ni kweli tuliyaona matokeo lakini hayakuwa ya bwana turudi tuitafute tona kwani ya matokeo ya Bwana yanakuja.

    Unasema na sema nini muulize samweli alipo enda nyumbani kwa mzee Yese aliletewa watu 6 ambao ni expert na ni mashujaa kwa kuwaona na yey mwenyewe akazani kuwa yupo mmoja wapo lakini msikie bwana alivyo mwambia

    1 Samweli 16:7
    [7]Lakini BWANA akamwambia Samweli, Usimtazame uso wake, wala urefu wa kimo chake; kwa maana mimi nimemkataa. BWANA haangalii kama binadamu aangaliavyo; maana wanadamu huitazama sura ya nje, bali BWANA huutazama moyo.

    Samweli aljvyo mtazama Abnadabu aliona sifa zote za kuwa mfalme lakini roho akuona kama samweli alivyo kuwa anaona.

    Kumbe hata sisi hatupaswi kuingia kazini ,au kwenye biashara hata kwenye kilimo sababu tu watu wamesema kilimo cha matikiti kinatoa tunapaswa kutazama *Bwana anasema nini*

    Yakobo alimtazama bwana na bwana akamwambia nenda nami nitakuwa pamoja nawe na kukurejesha tena .

    Ok ahsante sana tusiache kuomba toba ungana nami toba hii

    *BWANA YESU TUNAKUJA MBELE ZAKO KUNA HATUA NILISOGEA BILA WEWE ROHO NAOMBA TOBA NISAMEHE YESU NA TANGU LEO NAOMBA ROHO WAKO MTAKATIFU ATEMBEE NA MIMI KAMA MUSA NA WANAISLAERI WALIVYO TEMBEA NA WINGU LAKO WAKATI WA MCHANA UNIPE KIVULI NA WAKATI WA USIKU UNIPE MWANGA SAWA SAWA NA KWENYE MAISHA YANGU* .AMEN

    Ahsante sana naitwa sylvester Mwakabende kutoka (build new eden ministry)

    Unaweza mkaribisha jirani yako kujifunza neno na sisi kwa kujoin link hapa chini
    https://chat.whatsapp.com/IxkPEsnxi02ExNGrlmbWR4

    #Restoremenposition
    #build new eden
    #youth reformation and revival
    *Roho mtakatifu kama mlinzi wetu* Isaya 4:5-6 [5]Tena juu ya makao yote ya mlima Sayuni, na juu ya makusanyiko yake, BWANA ataumba *wingu na moshi wakati wa mchana, na mwangaza wa miali ya moto wakati wa usiku;* kwa maana juu ya utukufu wote itatandazwa sitara. . [6]Kisha kutakuwa na hema kuwa uvuli wakati wa mchana kwa sababu ya hari, na kuwa mahali pa kukimbilia na kujificha wakati wa tufani na mvua. Wingu linalozungumzwa hapo kwenye agano la kale ni *Roho mtakatifu* Kumbe ukimkubali Kristo na kuuoshi wokovu roho wa Bwana anakuwa ndani yako na kazi moja wapo ya huyo *roho ni kukulinda wewe ulieamini* Mtu aliye mshika kristo ns kumuamini na kumpokea roho wake wakati wa mchana anafunikwa na kutulizwa na *Bwana na wakati wa usiku anamulikwa na Bwana* Kumbe kama roho wa Mungu anatumulika na kutukinga nini kinafanya watu wa Mungu tushindwe kuziishi ahadi ,*tumemuwekea mipaka roho mtakatifu* tukiamini *kunena kwa lugha ndo kipawa na jukumu la roho mtakatifu* Sasa tukitizama wakati taifa la islaeri limetoka misri lilikuwa linaongozwa na wingu la Bwana. Kutoka 13:21-22 [21] *BWANA naye akawatangulia mchana ndani ya wingu mfano wa nguzo, ili awaongoze njia*; na usiku, *ndani ya moto mfano wa nguzo, ili kuwapa nuru*; wapate kusafiri mchana na usiku;* [22]ile nguzo ya wingu *haikuondoka mchana, wala ile nguzo ya moto haikuondoka usiku,* mbele ya hao watu. Hivi ndivyo roho wa Mungu anavyo paswa kukuongoza wakati wa mchana na wakati wa usiku . Ukiwa na roho wa Bwana na akawa rafiki yako na kiongozi wako utafanya biashara kwa kubahatisha badala yake yeye atakuongoza uza kitu chenye wateja. Unaweza mkaribisha jirani yako kujifunza neno na sisi kwa kujoin link hapa chini https://chat.whatsapp.com/IxkPEsnxi02ExNGrlmbWR4 Walokole tunakosa jicho la kuona fursa sababu tumemuwekea mipaka roho mtakatifu na wakati mwingine anatupa wazo tunalizimisha kwa kuto kujiamini na matokeo yake tunabaki jinsi tulivyo. Mtu aliye okoka na *akakubali kutii ndiye anayepaswa kula mema ya nchi* lakini imekuwa tofauti na uhalisia mtu ameokoka anaoshi dhana ya kuamini kuwa atakula kwa jasho iyo ilifanya kazi kabla ya wewe kuokoka saizi wewe unakula kwa wazo la kiMungu linalo shushwa na roho mtakatifu na wewe ukichukua hatua linageuka na kuleta matokeo . Musa aliijua siri hii ndo mana pasipo wingu akuenda mbele au kurudi nyuma. Kutoka 40:37 [37]bali kama lile wingu halikuinuliwa, wakati ule hawakusafiri hata siku ile lilipoinuliwa tena. Cha kujiuliza mimi na wewe ni hatua ngapi yumepiga bila kuongozwa na roho mtakatifu na tukapelekea kupoteza thamani zetu . Iko haja turudi kuitafuta toba kwani ni hatua tulienda mbele lakini kumbe ni shetani *alitutenda tu kwa akiri* Ni kweli tuliyaona matokeo lakini hayakuwa ya bwana turudi tuitafute tona kwani ya matokeo ya Bwana yanakuja. Unasema na sema nini muulize samweli alipo enda nyumbani kwa mzee Yese aliletewa watu 6 ambao ni expert na ni mashujaa kwa kuwaona na yey mwenyewe akazani kuwa yupo mmoja wapo lakini msikie bwana alivyo mwambia 1 Samweli 16:7 [7]Lakini BWANA akamwambia Samweli, Usimtazame uso wake, wala urefu wa kimo chake; kwa maana mimi nimemkataa. BWANA haangalii kama binadamu aangaliavyo; maana wanadamu huitazama sura ya nje, bali BWANA huutazama moyo. Samweli aljvyo mtazama Abnadabu aliona sifa zote za kuwa mfalme lakini roho akuona kama samweli alivyo kuwa anaona. Kumbe hata sisi hatupaswi kuingia kazini ,au kwenye biashara hata kwenye kilimo sababu tu watu wamesema kilimo cha matikiti kinatoa tunapaswa kutazama *Bwana anasema nini* Yakobo alimtazama bwana na bwana akamwambia nenda nami nitakuwa pamoja nawe na kukurejesha tena . Ok ahsante sana tusiache kuomba toba ungana nami toba hii *BWANA YESU TUNAKUJA MBELE ZAKO KUNA HATUA NILISOGEA BILA WEWE ROHO NAOMBA TOBA NISAMEHE YESU NA TANGU LEO NAOMBA ROHO WAKO MTAKATIFU ATEMBEE NA MIMI KAMA MUSA NA WANAISLAERI WALIVYO TEMBEA NA WINGU LAKO WAKATI WA MCHANA UNIPE KIVULI NA WAKATI WA USIKU UNIPE MWANGA SAWA SAWA NA KWENYE MAISHA YANGU* .AMEN Ahsante sana naitwa sylvester Mwakabende kutoka (build new eden ministry) Unaweza mkaribisha jirani yako kujifunza neno na sisi kwa kujoin link hapa chini https://chat.whatsapp.com/IxkPEsnxi02ExNGrlmbWR4 #Restoremenposition #build new eden #youth reformation and revival
    0 Comentários 0 Compartilhamentos 2K Visualizações
  • Muigizaji maarufu na Mkongwe Duniani, Jean-Claude Van Damme anakabiliwa na mashtaka ya kujibu baada ya kudaiwa kufanya ngono na Wanawake waliotekwa nyara Nchini Romania .

    Kwa mujibu wa CNN, Idara ya Romania ya Uchunguzi wa Uhalifu wa kupangwa na Ugaidi (DIICOT) imewasilisha malalamiko ya jinai dhidi ya Van Damme, ikidai alifanya ngono kwa kujua na Wanawake kadhaa waliokuwa wakitumiwa katika biashara haramu ya ngono.

    Kulingana na ripoti hiyo, Mwigizaji huyo Raia wa Ubelgiji anadaiwa kukutana na Watu kadhaa ambao pia wanachunguzwa kwa uhalifu wa usafirishaji wa Binadamu, ambao walimpa fursa ya kufanya ngono na Wanamitindo watano (5) wa Kiromania kama zawadi.

    Tukio hilo linaripotiwa kutokea Cannes Nchini Ufaransa hivyo, Serikali ya hiyo inapaswa kuidhinisha mashitaka hayo ya jinai lakini haikuwekwa wazi ni lini tukio hilo lilitokea hapo Ufaransa.

    Muigizaji maarufu na Mkongwe Duniani, Jean-Claude Van Damme anakabiliwa na mashtaka ya kujibu baada ya kudaiwa kufanya ngono na Wanawake waliotekwa nyara Nchini Romania 🇷🇴. Kwa mujibu wa CNN, Idara ya Romania ya Uchunguzi wa Uhalifu wa kupangwa na Ugaidi (DIICOT) imewasilisha malalamiko ya jinai dhidi ya Van Damme, ikidai alifanya ngono kwa kujua na Wanawake kadhaa waliokuwa wakitumiwa katika biashara haramu ya ngono. Kulingana na ripoti hiyo, Mwigizaji huyo Raia wa Ubelgiji 🇧🇪 anadaiwa kukutana na Watu kadhaa ambao pia wanachunguzwa kwa uhalifu wa usafirishaji wa Binadamu, ambao walimpa fursa ya kufanya ngono na Wanamitindo watano (5) wa Kiromania kama zawadi. Tukio hilo linaripotiwa kutokea Cannes Nchini Ufaransa 🇫🇷 hivyo, Serikali ya hiyo inapaswa kuidhinisha mashitaka hayo ya jinai lakini haikuwekwa wazi ni lini tukio hilo lilitokea hapo Ufaransa.
    Like
    Love
    2
    0 Comentários 0 Compartilhamentos 1K Visualizações
  • Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limekutana kujadili hali ya usalama na kibinadamu Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo huku hali ikizidi kuzorota. Mwakilishi Maalum wa Umoja huo (UN) Nchini DR Congo, Bintou Keita, amesema Waasi wa kundi la M23 wanaodaiwa kuungwa mkono na Nchi ya Rwanda sasa wanadhibiti maeneo makubwa ya Mikoa ya Kivu Kaskazini na Kivu Kusini na kutishia kupanua mashambulizi yao hadi Mkoani Tshopo na Maniema.

    "Hivi karibuni M23 imesimika utawala wake kwa kuteua gavana, makamu gavana na meya huko Bukavu, Kivu Kusini," amesema Keita.

    Ameeleza kuwa mgogoro huo unahusiana na unyonyaji wa madini mashariki mwa DR Congo na kuzua wasiwasi wa kikanda. Pia amegusia hali mbaya ya kibinadamu, akisema kumekuwa na ongezeko la ukiukwaji wa haki za binadamu, ikiwa ni pamoja na mauaji, utekaji nyara na ajira ya kulazimishwa kwa Vijana, wakiwemo Watoto.

    Licha ya makubaliano ya hivi karibuni kati ya Marais wa Rwanda na DR Congo Nchini Qatar , amani bado haijapatikana. Keita ametoa wito wa kuteuliwa kwa mpatanishi wa Umoja wa Afrika ili kuongoza juhudi za kusitisha mapigano.

    Balozi wa DR Congo katika Baraza la Umoja wa kimataifa (UN), Zénon Mukongo Ngay, ameishutumu Rwanda kwa kutotekeleza usitishaji mapigano, huku Waziri wa mambo ya nje wa Rwanda, Olivier Nduhungirehe, akisema Nchi yake itaendelea kuchukua "hatua za ulinzi" mpaka kuwe na mfumo wa kudumu wa usalama.

    Wakati huo huo, imeripotiwa kuwa DR Congo inakabiliwa na janga kubwa zaidi la njaa kuwahi kutokea, ambapo Watu zaidi ya milioni 27.7 wanakabiliwa na uhaba wa chakula kutokana na vita na ukosefu wa utulivu mashariki mwa Nchi hiyo.

    Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limekutana kujadili hali ya usalama na kibinadamu Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo 🇨🇩 huku hali ikizidi kuzorota. Mwakilishi Maalum wa Umoja huo (UN) Nchini DR Congo, Bintou Keita, amesema Waasi wa kundi la M23 wanaodaiwa kuungwa mkono na Nchi ya Rwanda 🇷🇼 sasa wanadhibiti maeneo makubwa ya Mikoa ya Kivu Kaskazini na Kivu Kusini na kutishia kupanua mashambulizi yao hadi Mkoani Tshopo na Maniema. "Hivi karibuni M23 imesimika utawala wake kwa kuteua gavana, makamu gavana na meya huko Bukavu, Kivu Kusini," amesema Keita. Ameeleza kuwa mgogoro huo unahusiana na unyonyaji wa madini mashariki mwa DR Congo na kuzua wasiwasi wa kikanda. Pia amegusia hali mbaya ya kibinadamu, akisema kumekuwa na ongezeko la ukiukwaji wa haki za binadamu, ikiwa ni pamoja na mauaji, utekaji nyara na ajira ya kulazimishwa kwa Vijana, wakiwemo Watoto. Licha ya makubaliano ya hivi karibuni kati ya Marais wa Rwanda na DR Congo Nchini Qatar 🇶🇦, amani bado haijapatikana. Keita ametoa wito wa kuteuliwa kwa mpatanishi wa Umoja wa Afrika ili kuongoza juhudi za kusitisha mapigano. Balozi wa DR Congo katika Baraza la Umoja wa kimataifa (UN), Zénon Mukongo Ngay, ameishutumu Rwanda kwa kutotekeleza usitishaji mapigano, huku Waziri wa mambo ya nje wa Rwanda, Olivier Nduhungirehe, akisema Nchi yake itaendelea kuchukua "hatua za ulinzi" mpaka kuwe na mfumo wa kudumu wa usalama. Wakati huo huo, imeripotiwa kuwa DR Congo inakabiliwa na janga kubwa zaidi la njaa kuwahi kutokea, ambapo Watu zaidi ya milioni 27.7 wanakabiliwa na uhaba wa chakula kutokana na vita na ukosefu wa utulivu mashariki mwa Nchi hiyo.
    0 Comentários 0 Compartilhamentos 2K Visualizações
  • Balozi wa Afrika Kusini Nchini Marekani , Ebrahim Rasool ambaye ametimuliwa na Nchi ya Marekani kutokana na kukosoa sera za Donald Trump, amerejea Afrika Kusini kwa ufakhari mkubwa na kupokewa kwa shangwe na mamia ya Wananchi waliofurika kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Cape Town Nchini Afrika Kusini.

    Balozi huyo na mkewe, Rosieda, waliwasili jana katika Uwanda wa Ndege wa Kimataifa wa Cape Town baada ya kusafari kutoka Nchini Marekani kupitia Qatar na wamekaribishwa vyema na kwa shangwe na mamia ya Wafuasi wao. Mapema mwezi huu, Balozi Rasool alitangazwa na Serikali ya Marekani kuwa ni Mtu asiyetakiwa kuweko Nchini humo baada ya kukosoa sera za Donald Trump, hatua ambayo inaonesha wazi jinsi madai ya uhuru wa kusema yasivyothaminiwa Nchini Marekani licha ya majigambo makubwa ya Nchi Marekani ya kupigania haki za Binadamu na demokrasia.

    Akiwahutubia mamia ya Mashabiki wake kwenye Uwanja wa Ndege wa Cape Town, Balozi Rasool amesema kwamba ingawa ametakiwa kuondoka huko Marekani lakini jambo hilo limeshindwa kufikia lengo lake kwani Viongozi wa Marekani wanadhani wamemdhalilisha wakati yeye anaona fakhari kwa maneno aliyotoa na Wananchi wa Afrika Kusini nao wanajivunia msimamo huo ndio maana wamejitokea kwa mamia kumpokea kishujaa.

    "Unaporejea nyumbani na kupokewa kwa shangwe na umati kama huu wa watu, mtu unaona fakhari na unajivunia msimamo wako." alisema Rasool.

    Alipoulizwa iwapo diplomasia imeshindwa, amesema ukweli kwamba matamshi yake yamemfanya Trump na Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Marco Rubio kuwa makini na hatua ya Serikali ya Marekani ya kumtangaza kuwa ni Mtu asiyetakiwa nchini humo ni ushahidi kwamba ujumbe wake umefika ngazi za juu kabisa za serikali ya Marekani.

    Balozi wa Afrika Kusini 🇿🇦 Nchini Marekani 🇺🇸, Ebrahim Rasool ambaye ametimuliwa na Nchi ya Marekani kutokana na kukosoa sera za Donald Trump, amerejea Afrika Kusini kwa ufakhari mkubwa na kupokewa kwa shangwe na mamia ya Wananchi waliofurika kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Cape Town Nchini Afrika Kusini. Balozi huyo na mkewe, Rosieda, waliwasili jana katika Uwanda wa Ndege wa Kimataifa wa Cape Town baada ya kusafari kutoka Nchini Marekani kupitia Qatar na wamekaribishwa vyema na kwa shangwe na mamia ya Wafuasi wao. Mapema mwezi huu, Balozi Rasool alitangazwa na Serikali ya Marekani kuwa ni Mtu asiyetakiwa kuweko Nchini humo baada ya kukosoa sera za Donald Trump, hatua ambayo inaonesha wazi jinsi madai ya uhuru wa kusema yasivyothaminiwa Nchini Marekani licha ya majigambo makubwa ya Nchi Marekani ya kupigania haki za Binadamu na demokrasia. Akiwahutubia mamia ya Mashabiki wake kwenye Uwanja wa Ndege wa Cape Town, Balozi Rasool amesema kwamba ingawa ametakiwa kuondoka huko Marekani lakini jambo hilo limeshindwa kufikia lengo lake kwani Viongozi wa Marekani wanadhani wamemdhalilisha wakati yeye anaona fakhari kwa maneno aliyotoa na Wananchi wa Afrika Kusini nao wanajivunia msimamo huo ndio maana wamejitokea kwa mamia kumpokea kishujaa. "Unaporejea nyumbani na kupokewa kwa shangwe na umati kama huu wa watu, mtu unaona fakhari na unajivunia msimamo wako." alisema Rasool. Alipoulizwa iwapo diplomasia imeshindwa, amesema ukweli kwamba matamshi yake yamemfanya Trump na Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Marco Rubio kuwa makini na hatua ya Serikali ya Marekani ya kumtangaza kuwa ni Mtu asiyetakiwa nchini humo ni ushahidi kwamba ujumbe wake umefika ngazi za juu kabisa za serikali ya Marekani.
    Love
    Like
    3
    0 Comentários 0 Compartilhamentos 2K Visualizações