• Kikao cha mazungumzo ya kumaliza mzozo wa Nchi ya Ukraine na Nchi ya Urusi kinaendelea Nchini Saudi Arabia 🇸 ambapo Mawaziri wa Mashauri ya Kigeni wa Urusi chini ya Sergie Lavrov na Marekani chini ya Marco Rubio. Hata hivyo, Ukraine na Umoja wa Ulaya (EU) hawajashirikishwa huku Ukraine upande wake inapinga kikao hicho kuwa makubaliano yoyote haitayatambua.

    Katika kusisitiza hilo Ukraine imeendelea kusisitiza kwamba itaendelea kupigana vita kwa kutegemea Ulaya sio Marekani kama mwanzo huku Rais wa Nchi hiyo Volodmiry Zelensky akisema Ukraine ni Taifa huru, hivyo haliwezi kuamuliwa mambo yake na Marekani, itautetea uhuru wake hadi tone la mwisho. Marekani imejibu kwa kusema inaitaka Ukraine irejeshe haraka deni lote la usaidizi wa vita lililotolewa na Marekani tangu Februari 2022 Oparesheni ya Urusi ilipoanza.

    Kikao hiki kinachoendelea ni hatua muhimu kuelekea mkutano wa Rais Putin na Rais Trump uliopangwa mwezi Mei katika sherehe za Mashujaa wa Urusi utakaofanyika Jijini Moscow, Urusi ambapo pia mkutano huo utamwalika Rais wa China Xi Ping kama Mgeni mwalikwa muhimu.

    Kikao cha mazungumzo ya kumaliza mzozo wa Nchi ya Ukraine 🇺🇦 na Nchi ya Urusi 🇷🇺 kinaendelea Nchini Saudi Arabia 🇸 ambapo Mawaziri wa Mashauri ya Kigeni wa Urusi chini ya Sergie Lavrov na Marekani 🇺🇸 chini ya Marco Rubio. Hata hivyo, Ukraine na Umoja wa Ulaya (EU) hawajashirikishwa huku Ukraine upande wake inapinga kikao hicho kuwa makubaliano yoyote haitayatambua. Katika kusisitiza hilo Ukraine imeendelea kusisitiza kwamba itaendelea kupigana vita kwa kutegemea Ulaya sio Marekani kama mwanzo huku Rais wa Nchi hiyo Volodmiry Zelensky akisema Ukraine ni Taifa huru, hivyo haliwezi kuamuliwa mambo yake na Marekani, itautetea uhuru wake hadi tone la mwisho. Marekani imejibu kwa kusema inaitaka Ukraine irejeshe haraka deni lote la usaidizi wa vita lililotolewa na Marekani tangu Februari 2022 Oparesheni ya Urusi ilipoanza. Kikao hiki kinachoendelea ni hatua muhimu kuelekea mkutano wa Rais Putin na Rais Trump uliopangwa mwezi Mei katika sherehe za Mashujaa wa Urusi utakaofanyika Jijini Moscow, Urusi ambapo pia mkutano huo utamwalika Rais wa China 🇨🇳 Xi Ping kama Mgeni mwalikwa muhimu.
    0 Comments ·0 Shares ·110 Views
  • Rais wa Urusi , Vladimir Putin amewaalika Rais China , Xi Jinping na Rais wa Marekani , Donald Trump kuhudhuria sherehe maarufu za Ushindi wa Urusi katika vita kuu ya pili ya Dunia (Russia’s Victory Parade) zitakazofanyika tarehe 9 Mwezi May Jijini Moscow Nchini Urusi. Mwaliko huu unatokana na ombi la Rais Donald Trump la tarehe 11 Feb 2025 alipoomba kuzuru Moscow kwa lengo la kumaliza mgogoro wa Ukraine, Kikao kilichotokana na ombi hili kilifanywa kwa njia ya simu ambapo pamoja na mambo mengine, Trump alimhakikishia Putin kwamba Marekani itaacha ufadhili wa kijeshi kwa Ukraine na pia Ukraine itaachia sehemu ya ardhi yake iliyotwaliwa kama dhamana ya usalama wake dhidi ya Moscow.

    Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Washington katika taarifa yake ilikazia na kusisitiza kile alichokizungumza Trump na Moscow na kwamba Marekani inakusudia kumaliza tofauti zao kidunia. Utawala wa Trump umekuwa na juhudi kubwa kumaliza mizozo mikubwa duniani ambayo Ikulu hiyo ilikuwa ikifadhili na kuanzisha uchokozi kwa muda mrefu, Ukiachiliambali mgogoro wa Ukraine, pia Washington inashughulika kumaliza mgogoro wa Mashariki ya Kati huko Gaza ambapo mamia ya watu wameuawa kwa ufadhili wa Marekani hiyohiyo.

    Rais wa Urusi 🇷🇺, Vladimir Putin amewaalika Rais China 🇨🇳, Xi Jinping na Rais wa Marekani 🇺🇸, Donald Trump kuhudhuria sherehe maarufu za Ushindi wa Urusi katika vita kuu ya pili ya Dunia (Russia’s Victory Parade) zitakazofanyika tarehe 9 Mwezi May Jijini Moscow Nchini Urusi. Mwaliko huu unatokana na ombi la Rais Donald Trump la tarehe 11 Feb 2025 alipoomba kuzuru Moscow kwa lengo la kumaliza mgogoro wa Ukraine, Kikao kilichotokana na ombi hili kilifanywa kwa njia ya simu ambapo pamoja na mambo mengine, Trump alimhakikishia Putin kwamba Marekani itaacha ufadhili wa kijeshi kwa Ukraine na pia Ukraine itaachia sehemu ya ardhi yake iliyotwaliwa kama dhamana ya usalama wake dhidi ya Moscow. Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Washington katika taarifa yake ilikazia na kusisitiza kile alichokizungumza Trump na Moscow na kwamba Marekani inakusudia kumaliza tofauti zao kidunia. Utawala wa Trump umekuwa na juhudi kubwa kumaliza mizozo mikubwa duniani ambayo Ikulu hiyo ilikuwa ikifadhili na kuanzisha uchokozi kwa muda mrefu, Ukiachiliambali mgogoro wa Ukraine, pia Washington inashughulika kumaliza mgogoro wa Mashariki ya Kati huko Gaza ambapo mamia ya watu wameuawa kwa ufadhili wa Marekani hiyohiyo.
    Like
    1
    · 0 Comments ·0 Shares ·147 Views
  • TBT ya Haji Manara

    "September 2007 nikiwa kijana Mdogo na nikiwa kiongozi wa Chama changu na hapo ni fresh from School kule Beijing China.
    Kipindi hicho nna madini ya hatari kuhusu taaluma ya Propaganda na Uenezi,enzi ambazo nilikuwa naweza kukuaminisha Jiwe ni Keki

    Enzi ambazo nilikuwa naweza kuwavusha hata kuku barabarani kwa maneno tu,
    Ni zile zile zama nilizowaaminisha Barcelona haichomoki kwa Mkapa, tena Barcelona kweli ya Xavi ,Iniesta na kina Messi.
    Taaluma iliyonipa ujasiri wa kusema na kuamini tutafuzu kwa AFCON ya 2019 kule Misri,wakati huo tukiwa chini kwenye msimamo wa kundi letu, na Nchi nzima ikiwa imejikatia tamaa ya kwenda Cairo.

    Bila kusahau one day kule Paris France niliposahau Passport hotelini na siku hiyo tulisimamishwa na Manjagu njiani nikiwa na wenzangu ambao walikuwa Kamil Gado,
    Nikazuga kama naitoa kwenye mfuko wa koti, Askari wakaniamini kabla ya kuwaonyesha ,wakaturuhusu kilaini kabisa,inaitwa Blue Propaganda

    Yes: Pembeni yangu katika hiyo picha ni Marehemu Captain Barongo aliyekuwa Katibu wa CCM Mkoa wa Dar es salaam,
    Na hii ilikuwa sherehe ya harusi ya DC wa Temeke hivi sasa Mh Sixtus Mapunda ambae wakati huo alikuwa Katibu wa Umoja wa Vijana ( UV CCM ) Mkoa huu.
    Hadi leo tumebaki marafiki wakubwa na hakosi mwaliko wowote kwangu

    Nb: Usicheke ukubwa wa koti,miaka ile ilikuwa ndio fashion na wenyewe tuliyaita Majumba "

    TBT ya Haji Manara "September 2007 nikiwa kijana Mdogo na nikiwa kiongozi wa Chama changu na hapo ni fresh from School kule Beijing China. Kipindi hicho nna madini ya hatari kuhusu taaluma ya Propaganda na Uenezi,enzi ambazo nilikuwa naweza kukuaminisha Jiwe ni Keki 😀😀😀 Enzi ambazo nilikuwa naweza kuwavusha hata kuku barabarani kwa maneno tu😀😀😀, Ni zile zile zama nilizowaaminisha Barcelona haichomoki kwa Mkapa, tena Barcelona kweli ya Xavi ,Iniesta na kina Messi. Taaluma iliyonipa ujasiri wa kusema na kuamini tutafuzu kwa AFCON ya 2019 kule Misri,wakati huo tukiwa chini kwenye msimamo wa kundi letu, na Nchi nzima ikiwa imejikatia tamaa ya kwenda Cairo. Bila kusahau one day kule Paris France niliposahau Passport hotelini na siku hiyo tulisimamishwa na Manjagu njiani nikiwa na wenzangu ambao walikuwa Kamil Gado, Nikazuga kama naitoa kwenye mfuko wa koti, Askari wakaniamini kabla ya kuwaonyesha ,wakaturuhusu kilaini kabisa,inaitwa Blue Propaganda 😀😀😀 Yes: Pembeni yangu katika hiyo picha ni Marehemu Captain Barongo aliyekuwa Katibu wa CCM Mkoa wa Dar es salaam, Na hii ilikuwa sherehe ya harusi ya DC wa Temeke hivi sasa Mh Sixtus Mapunda ambae wakati huo alikuwa Katibu wa Umoja wa Vijana ( UV CCM ) Mkoa huu. Hadi leo tumebaki marafiki wakubwa na hakosi mwaliko wowote kwangu 🙏🙏 Nb: Usicheke ukubwa wa koti,miaka ile ilikuwa ndio fashion na wenyewe tuliyaita Majumba 😀😀😀"
    0 Comments ·0 Shares ·222 Views
  • Mfalme wa Nchi ya Jordan , Abdullah II amekataa pendekezo la Rais wa Marekani Donald Trump la kutaka kuwahamishia Wapalestina Nchini mwake baada ya mazungumzo na Rais Donald Trump wa Marekani, ambaye alishauri Wakazi wa Gaza wapatao milioni mbili (2) kuondolewa kutoka katika eneo lililoharibiwa na vita.

    Katika mkutano na Rais Trump, Mfalme Abdullah alijitolea kuchukua hadi Watoto 2,000 kutoka Gaza, hasa wale wanaohitaji matibabu ya dharura, ikiwemo Watoto wa saratani. Kupitia mtandao wa X, Mfalme Abdullah alisema, "Msimamo wa Jordan ni msimamo wa pamoja wa mataifa ya Kiarabu."

    Sanjari na hayo, Katibu Mkuu wa Umoja wa Nchi za Kiarabu, Ahmed Aboul Gheit, alikosoa pendekezo hilo, akisema kuwa ni lisilokubalika katika ukanda huo, huku Nchi ya China ikisisitiza kuwa Gaza ni ardhi ya Wapalestina.

    Mfalme wa Nchi ya Jordan 🇯🇴, Abdullah II amekataa pendekezo la Rais wa Marekani 🇺🇸 Donald Trump la kutaka kuwahamishia Wapalestina Nchini mwake baada ya mazungumzo na Rais Donald Trump wa Marekani, ambaye alishauri Wakazi wa Gaza wapatao milioni mbili (2) kuondolewa kutoka katika eneo lililoharibiwa na vita. Katika mkutano na Rais Trump, Mfalme Abdullah alijitolea kuchukua hadi Watoto 2,000 kutoka Gaza, hasa wale wanaohitaji matibabu ya dharura, ikiwemo Watoto wa saratani. Kupitia mtandao wa X, Mfalme Abdullah alisema, "Msimamo wa Jordan ni msimamo wa pamoja wa mataifa ya Kiarabu." Sanjari na hayo, Katibu Mkuu wa Umoja wa Nchi za Kiarabu, Ahmed Aboul Gheit, alikosoa pendekezo hilo, akisema kuwa ni lisilokubalika katika ukanda huo, huku Nchi ya China 🇨🇳 ikisisitiza kuwa Gaza ni ardhi ya Wapalestina.
    Like
    1
    · 0 Comments ·0 Shares ·138 Views
  • Putin sasa anazunguka huku na kule akitafuta suluhu ya amani, lakini Ukraine naye amegoma kusalimu amri.

    Katika ramani ya dunia, mababe wawili wamebaki, Marekani na China.

    Marekani bado inatawala masoko ya dunia, ina silaha za kisasa, na inafanya kila kitu kuhakikisha inabaki juu.

    China inakuja kwa kasi, ikitumia siasa za uchumi badala ya vita. Wanajua kuwa kushinda vita vya sasa, sio kwa mabomu tu bali kwa pesa na teknolojia.

    Urusi? Imebanwa. Vita na Ukraine imeichosha. Mipango ya kupanua mipaka imekufa. Na sasa dunia inajiuliza Putin anaweza kushindwa?

    Hii dunia ina kanuni moja kubwa, Usimwamini mtu. Na hata kama ukimwamini mtu, basi huyo mtu awe wewe mwenyewe.

    Ukraine alifanya kosa ambalo sasa linamgharimu. Aliamini ahadi za mataifa makubwa bila kuhakikisha ana kinga yake mwenyewe. Akasahau kuwa siasa za dunia haziongozwi na ahadi, bali na nguvu.

    Hili liwe somo kwa kila taifa linalotegemea misaada kutoka nje. Leo wanakupenda, kesho wakishapata wanachotaka, wanakusahau.

    Na dunia ilivyo sasa, muda wowote inaweza kulipuka. Mataifa yanapimana nguvu, migogoro inaongezeka, na tunakaribia kuona enzi mpya ya vita vya madaraka kati ya Marekani na China.

    Ukraine, Anajifunza kwa uchungu kuwa historia haimsahau mjinga.
    Putin sasa anazunguka huku na kule akitafuta suluhu ya amani, lakini Ukraine naye amegoma kusalimu amri. Katika ramani ya dunia, mababe wawili wamebaki, Marekani na China. Marekani bado inatawala masoko ya dunia, ina silaha za kisasa, na inafanya kila kitu kuhakikisha inabaki juu. China inakuja kwa kasi, ikitumia siasa za uchumi badala ya vita. Wanajua kuwa kushinda vita vya sasa, sio kwa mabomu tu bali kwa pesa na teknolojia. Urusi? Imebanwa. Vita na Ukraine imeichosha. Mipango ya kupanua mipaka imekufa. Na sasa dunia inajiuliza Putin anaweza kushindwa? Hii dunia ina kanuni moja kubwa, Usimwamini mtu. Na hata kama ukimwamini mtu, basi huyo mtu awe wewe mwenyewe. Ukraine alifanya kosa ambalo sasa linamgharimu. Aliamini ahadi za mataifa makubwa bila kuhakikisha ana kinga yake mwenyewe. Akasahau kuwa siasa za dunia haziongozwi na ahadi, bali na nguvu. Hili liwe somo kwa kila taifa linalotegemea misaada kutoka nje. Leo wanakupenda, kesho wakishapata wanachotaka, wanakusahau. Na dunia ilivyo sasa, muda wowote inaweza kulipuka. Mataifa yanapimana nguvu, migogoro inaongezeka, na tunakaribia kuona enzi mpya ya vita vya madaraka kati ya Marekani na China. Ukraine, Anajifunza kwa uchungu kuwa historia haimsahau mjinga.
    Like
    1
    · 0 Comments ·0 Shares ·464 Views
  • Mshambuliaji wa kimataifa wa Nigeria, Victor Boniface, anayeichezea Bayer Leverkusen ya Ujerumani, ameachana na mpenzi wake, Rikke Hermine, raia wa Norway. Wawili hao walikuwa katika uhusiano wa kimapenzi kwa miaka minne, lakini wameamua kuvunja uhusiano wao kutokana na kugundua kuwa Victor kwenye mali zake ameandika majina ya mama yake tu.

    Chanzo cha habari kinaeleza kuwa uamuzi wa Rikke kuachana na Victor ulitokana na kugundua kuwa katika mali zote za mshambuliaji huyo, majina ya mama yake mzazi pekee ndiyo yaliyoandikwa. Hali hii ilimfanya Rikke kuhisi kuwa hakuwa na nafasi ya kutosha katika maisha ya Victor, jambo lililomfanya kuchukua hatua hiyo.

    Aidha, inadaiwa kuwa Rikke alikuwa akishinikiza kufunga ndoa baada ya kuwa wapenzi kwa muda mrefu, huku Victor akiwa tayari kufunga naye ndoa lakini kwa sharti la kusaini mkataba wa awali (prenup).

    Prenup ni Mkataba wa awali kabla ya kufunga ndoa ambao unalenga kulinda mali za pande zote mbili endapo itatokea mkaachana kila mmoja anabaki na alichokuja nacho katika ndoa na sio kugawana mali, ila bibie Rikkie amekuwa mgumu kukubali hilo hivyo kuachana

    #tanzania #kenya #daressalaam #africa #zanzibar #diamondplatnumz #arusha #mwanza #dodoma #uganda #wcb #travel #life #safari #wasafi #love #millardayoupdates #mbeya #nairobi #harmonize #rwanda #eastafrica #kilimanjaro #alikiba #gainwithmchina #serengeti #wasafitv #fashion #wasafimedia #wemasepetu
    Mshambuliaji wa kimataifa wa Nigeria, Victor Boniface, anayeichezea Bayer Leverkusen ya Ujerumani, ameachana na mpenzi wake, Rikke Hermine, raia wa Norway. Wawili hao walikuwa katika uhusiano wa kimapenzi kwa miaka minne, lakini wameamua kuvunja uhusiano wao kutokana na kugundua kuwa Victor kwenye mali zake ameandika majina ya mama yake tu. Chanzo cha habari kinaeleza kuwa uamuzi wa Rikke kuachana na Victor ulitokana na kugundua kuwa katika mali zote za mshambuliaji huyo, majina ya mama yake mzazi pekee ndiyo yaliyoandikwa. Hali hii ilimfanya Rikke kuhisi kuwa hakuwa na nafasi ya kutosha katika maisha ya Victor, jambo lililomfanya kuchukua hatua hiyo. Aidha, inadaiwa kuwa Rikke alikuwa akishinikiza kufunga ndoa baada ya kuwa wapenzi kwa muda mrefu, huku Victor akiwa tayari kufunga naye ndoa lakini kwa sharti la kusaini mkataba wa awali (prenup). Prenup ni Mkataba wa awali kabla ya kufunga ndoa ambao unalenga kulinda mali za pande zote mbili endapo itatokea mkaachana kila mmoja anabaki na alichokuja nacho katika ndoa na sio kugawana mali, ila bibie Rikkie amekuwa mgumu kukubali hilo hivyo kuachana #tanzania #kenya #daressalaam #africa #zanzibar #diamondplatnumz #arusha #mwanza #dodoma #uganda #wcb #travel #life #safari #wasafi #love #millardayoupdates #mbeya #nairobi #harmonize #rwanda #eastafrica #kilimanjaro #alikiba #gainwithmchina #serengeti #wasafitv #fashion #wasafimedia #wemasepetu
    Like
    1
    · 0 Comments ·0 Shares ·2K Views
  • #JeWajua Msako mkali wa wahamiaji uliofanyika nchini Marekani siku ya Jumapili na kusababisha kukamatwa kwa watu 956, idadi hiyo ikiwa kubwa zaidi tangu Donald Trump arejee mamlakani, kulingana na shirika la Uhamiaji na Utekelezaji wa Forodha (ICE).

    Mashirika kadhaa ya serikali yenye mamlaka mapya ya kuwaweka kizuizini wasio na vibali yalihusika katika kamata kamata hiyo kwenye miji kadhaa ikiwa ni pamoja na Chicago, Newark na Miami. Moja ya ahadi alizotoa Donald Trump wakati wa kampeni yake, ni kuwafukuza nchi Marekani wahamiaji wasio na vibali.

    Mtangulizi wake Joe Biden aliwarejesha makwao wastani wa wahamiaji 311 kila siku, kulingana na ICE, wengi wao wakiwa watu ambao walikuwa wamefanya uhalifu. Tangu aingie madarakani, Trump ametekeleza maagizo 21 kurekebisha mfumo wa uhamiaji wa Marekani.

    Huko Miami siku ya Jumapili, vyombo vya kutekeleza sheria vya serikali vilichukua "hatua kadhaa za uhamiaji," Uchunguzi wa Usalama wa jiji hilo ulisema kwenye mitandao ya kijamii.

    #tanzania #kenya #daressalaam #africa #zanzibar #diamondplatnumz #arusha #mwanza #dodoma #uganda #wcb #travel #life #safari #wasafi #love #millardayoupdates #mbeya #nairobi #harmonize #rwanda #eastafrica #kilimanjaro #alikiba #gainwithmchina #serengeti #wasafitv #fashion #wasafimedia
    #JeWajua Msako mkali wa wahamiaji uliofanyika nchini Marekani siku ya Jumapili na kusababisha kukamatwa kwa watu 956, idadi hiyo ikiwa kubwa zaidi tangu Donald Trump arejee mamlakani, kulingana na shirika la Uhamiaji na Utekelezaji wa Forodha (ICE). Mashirika kadhaa ya serikali yenye mamlaka mapya ya kuwaweka kizuizini wasio na vibali yalihusika katika kamata kamata hiyo kwenye miji kadhaa ikiwa ni pamoja na Chicago, Newark na Miami. Moja ya ahadi alizotoa Donald Trump wakati wa kampeni yake, ni kuwafukuza nchi Marekani wahamiaji wasio na vibali. Mtangulizi wake Joe Biden aliwarejesha makwao wastani wa wahamiaji 311 kila siku, kulingana na ICE, wengi wao wakiwa watu ambao walikuwa wamefanya uhalifu. Tangu aingie madarakani, Trump ametekeleza maagizo 21 kurekebisha mfumo wa uhamiaji wa Marekani. Huko Miami siku ya Jumapili, vyombo vya kutekeleza sheria vya serikali vilichukua "hatua kadhaa za uhamiaji," Uchunguzi wa Usalama wa jiji hilo ulisema kwenye mitandao ya kijamii. #tanzania #kenya #daressalaam #africa #zanzibar #diamondplatnumz #arusha #mwanza #dodoma #uganda #wcb #travel #life #safari #wasafi #love #millardayoupdates #mbeya #nairobi #harmonize #rwanda #eastafrica #kilimanjaro #alikiba #gainwithmchina #serengeti #wasafitv #fashion #wasafimedia
    Like
    1
    · 0 Comments ·0 Shares ·2K Views
  • Baada ya Rais wa Marekani , Donald Trump kusaini amri ya Marekani kujitoa Shirika la afya Duniani (WHO) sanjari na kusitisha ufadhili wa kifedha kwa Mashirika yote ya kiafya Duniani kote ikiwemo yale ya kupambana na ukimwi kwa siku 90.

    Rais huyo amesema katika kipindi hicho cha mpito serikali yake itafanya tathimini ya kuona ushiriki wake na ufadhili kama unaenda sahihi na mataifa mengine au Marekani imesusiwa mzigo mkubwa peke yake wa kuhudumia Dunia. Marekani ndio mchangiaji mkubwa zaidi kwenye Mashirika hayo ya afya ikiwemo (WHO), ambapo Marekani inachangia takribani dola bilioni moja (1) huku Nchi ya China ikichangia dola milioni (86) pekee kitu ambacho Donald Trump amesema sio sahihi.

    Tayari Mashirika yanayofadhiliwa na Marekani likiwemo la USAID yamepokea waraka wa agizo la Donald Trump na kuagizwa kuanza utekelezaji Duniani kote.

    Baada ya Rais wa Marekani 🇺🇸, Donald Trump kusaini amri ya Marekani kujitoa Shirika la afya Duniani (WHO) sanjari na kusitisha ufadhili wa kifedha kwa Mashirika yote ya kiafya Duniani kote ikiwemo yale ya kupambana na ukimwi kwa siku 90. Rais huyo amesema katika kipindi hicho cha mpito serikali yake itafanya tathimini ya kuona ushiriki wake na ufadhili kama unaenda sahihi na mataifa mengine au Marekani imesusiwa mzigo mkubwa peke yake wa kuhudumia Dunia. Marekani ndio mchangiaji mkubwa zaidi kwenye Mashirika hayo ya afya ikiwemo (WHO), ambapo Marekani inachangia takribani dola bilioni moja (1) huku Nchi ya China ikichangia dola milioni (86) pekee kitu ambacho Donald Trump amesema sio sahihi. Tayari Mashirika yanayofadhiliwa na Marekani likiwemo la USAID yamepokea waraka wa agizo la Donald Trump na kuagizwa kuanza utekelezaji Duniani kote.
    Like
    1
    · 0 Comments ·0 Shares ·305 Views
  • Baada ya Rais wa Marekani , Donald Trump kusaini amri ya Marekani kujitoa Shirika la afya Duniani (WHO) sanjari na kusitisha ufadhili wa kifedha kwa Mashirika yote ya kiafya Duniani kote ikiwemo yale ya kupambana na ukimwi kwa siku 90.

    Rais huyo amesema katika kipindi hicho cha mpito serikali yake itafanya tathimini ya kuona ushiriki wake na ufadhili kama unaenda sahihi na mataifa mengine au Marekani imesusiwa mzigo mkubwa peke yake wa kuhudumia Dunia. Marekani ndio mchangiaji mkubwa zaidi kwenye Mashirika hayo ya afya ikiwemo (WHO), ambapo Marekani inachangia takribani dola bilioni moja (1) huku Nchi ya China ikichangia dola milioni (86) pekee kitu ambacho Donald Trump amesema sio sahihi.

    Tayari Mashirika yanayofadhiliwa na Marekani likiwemo la USAID yamepokea waraka wa agizo la Donald Trump na kuagizwa kuanza utekelezaji Duniani kote.

    Baada ya Rais wa Marekani 🇺🇸, Donald Trump kusaini amri ya Marekani kujitoa Shirika la afya Duniani (WHO) sanjari na kusitisha ufadhili wa kifedha kwa Mashirika yote ya kiafya Duniani kote ikiwemo yale ya kupambana na ukimwi kwa siku 90. Rais huyo amesema katika kipindi hicho cha mpito serikali yake itafanya tathimini ya kuona ushiriki wake na ufadhili kama unaenda sahihi na mataifa mengine au Marekani imesusiwa mzigo mkubwa peke yake wa kuhudumia Dunia. Marekani ndio mchangiaji mkubwa zaidi kwenye Mashirika hayo ya afya ikiwemo (WHO), ambapo Marekani inachangia takribani dola bilioni moja (1) huku Nchi ya China ikichangia dola milioni (86) pekee kitu ambacho Donald Trump amesema sio sahihi. Tayari Mashirika yanayofadhiliwa na Marekani likiwemo la USAID yamepokea waraka wa agizo la Donald Trump na kuagizwa kuanza utekelezaji Duniani kote.
    Like
    2
    · 0 Comments ·0 Shares ·302 Views
  • Nchi ya Uchina imeweka rekodi mpya ya Dunia kwa kutangaza na kuliwasha "Jua lake Bandia" kwa zaidi ya dakika (17) lenye joto la (milioni 100°C): Hii ni rekodi mpya ya Dunia baada ya kuvunja rekodi ya awali ya sekunde (403) iliyotokea mwaka 2023.

    Ufanisi huu ulifanywa na Watafiti kutoka Taasisi ya Fizikia ya Plasmas (ASIPP) na Taasisi ya Sayansi za Fizikia kutoka Hefei iliyopo katika jimbo la Anhui Nchini China.

    "Reactor" ya EAST ni sehemu ya jitihada zinazofanywa na Wanasayansi wa Kichina kukuza nishati ya "fusion". Hatua hii inawakilisha maendeleo makubwa katika utafiti wa nishati ya "fusion" ambapo kigezo cha sekunde 1000 cha kufanya kazi kinachukuliwa kama kipimo cha uwezo wa kuitumia.

    Lengo kuu la mradi huu ni kutoa chanzo cha nishati safi kisichokuwa na kikomo na kusaidia uchunguzi wa anga za nje za mfumo wa jua.

    Nchi ya Uchina 🇨🇳 imeweka rekodi mpya ya Dunia kwa kutangaza na kuliwasha "Jua lake Bandia" kwa zaidi ya dakika (17) lenye joto la (milioni 100°C): Hii ni rekodi mpya ya Dunia baada ya kuvunja rekodi ya awali ya sekunde (403) iliyotokea mwaka 2023. Ufanisi huu ulifanywa na Watafiti kutoka Taasisi ya Fizikia ya Plasmas (ASIPP) na Taasisi ya Sayansi za Fizikia kutoka Hefei iliyopo katika jimbo la Anhui Nchini China. "Reactor" ya EAST ni sehemu ya jitihada zinazofanywa na Wanasayansi wa Kichina kukuza nishati ya "fusion". Hatua hii inawakilisha maendeleo makubwa katika utafiti wa nishati ya "fusion" ambapo kigezo cha sekunde 1000 cha kufanya kazi kinachukuliwa kama kipimo cha uwezo wa kuitumia. Lengo kuu la mradi huu ni kutoa chanzo cha nishati safi kisichokuwa na kikomo na kusaidia uchunguzi wa anga za nje za mfumo wa jua.
    Love
    1
    · 0 Comments ·0 Shares ·237 Views
  • OPERATION ENTEBBE -1

    Jina mbadala: Operation Thunderstorm/Operation Yonatan

    Watekelezaji: -MOSSAD
    - IDF (ISRAEL DEFENCE FORCE)
    Kitengo cha Weledi: Sayeret Matkal
    Mwaka wa utekelezaji: July, 1976
    Nchi: Israel/Uganda

    Silaha za kukumbukwa: Lockheed C-130 Hurcules
    Wahusika wa kukumbukwa: - Yonatan Netanyahu (kaka wa Waziri Mkuu wa zamani Benjamin Netanyahu)
    -Ehud Barak (alikuja kuwa Waziri Mkuu miaka ya karibuni)

    MOSAD & IDF: OPERATION ENTEBBE

    Siku ya tarehe 27 June mwaka 1976 ilianza kama siku nyingine yioyote ndani ya uwanja wa ndege wa kimataifa katika mji mkuu wa nchi ya Israel Tel Aviv, uwanja ujulikanao kama Ben Gurion International Airport. Moja kati ya ndege ambayo ilikuwa inafanya safari yake katika siku ya elo ilikuwa ni ndege ya kampuni ya Air Frace ambao walikuwa na ndege yao ya Air France Flight 139 ambayo ni ndege aina ya Airbus A300B4-203 yenye namba ya usajili mkiani F-BVGG (c/n 019).
    Ndege hii ilikuwa inafanya safari yake katika siku ya leo kutoka Tel Aviv na ilikuwa inatarajiwa kutua katika uwanja wa ndege wa Charles DE Gaulle International Airport jijini Paris, Ufaransa. Baada ya taratibu na protokali zote za uwanja wa ndege kukamilika na abiria wote kukwea kwenye ndege, ndege iliruka kutoka kiwanjani ikiwa na abiria 190 ndani yake pamoja na ‘crew’ ya watu 12 (Marubani na wahudumu) ambamo asilimia kubwa ya abiria walikuwa ni raia wa Israel pamoja na watu wenye asili ya kiyahudi. Ndege iliruka kutoka Tel Aviv mpaka jijini Anthens, Ugiriki ambapo ilichukua abiria wengine wapatao 58. Baada ya hapo ndege iliruka pasipo kujua kwamba kati aya abiria hao 58 waliowachukua Ugiriki ndani yao kulikuwa na abiria wanne ambao walikuwa ni wanachama wawili wa kikundi cha Popular Front For The Liberation of Palestine – External Operations (PFLP-EO) kutoka Plaestina na wanachama wawili wa kikundi cha Revolutionary Cells kutoka nchini Ujerumani.

    Baada ya abiria wote kukamilisha utaratibu na kupanda ndani ya ndege, ndege iliondoka uwanjani Athens mnamo amjira ya saa 6 na dakika 30 mchana kuelekea Paris, Ufaransa.
    Dakika chache baada ya ndege kuruka rubani mkuu wa ndege ambaye ndiye alikuwa ameshikili ‘usukani’ Bw. Michel Bacos akasikia kelele nyuma ya ndege wanakokaa abiria (cabin). Ili kujiridhisha kwamba kila kitu kiko sawa, rubani Michel Bacos akamuagiza msaidizi wake mmoja wapo ambaye ndiye alikuwa injinia wa ndege aende kuangalia nini kilikuwa kinaendelea.
    Mara tu baada ya msaidizi huyo kufungua mlango wa mbele wa chumba cha marubani, alikutana uso kwa uso na bastola usoni mwake iliyoshikiliwa na mtu ambaye mkononi alikuwa amebeba bomu la kurusha kwa mkono. Huku msaidizi huyo akiwa bado ameshikwa na bumbuwazi, mtu huyu mwenye bomu mkononi na bastola (jina lake anaitwa Wilfred Bose raia wa Ujerumani) alimsukuma yule injinia nakumrudisha tena ndani ya chumba cha marubani na kisha yeye mwenyewe pia kuingia.
    Mara tu baada ya kufika ndani ya chumba cha marubani, akawaweka chini ya ulinzi marubani ambao bado walikuwa kwenye mshituko wa mshangao na kisha kumnyanyua rubani msaidizi kutoka kwenye siti yake na kukaa yeye. Baada ya kukaa kwenye siti ya rubani msaidizi kitu cha kwanza alichokifanya haramia huyu Wilfre Bose ni kuchukua microphone ambayo marubani huwa wanatumia kutoa matangazo kwa abria, na baada ya kuiweka microphone akatoa tangazo lake la kwanza, kwa sauti ya utulivu iliyojaa lafudhi nzito ya kijerumani, akawasema; *“..kuanzia sasa ndege hii inaitwa HAIFA 1, badala ya Flight 139..”*
    Haifa ni eneo (mji) maarufu ulipo kaskazini mwa nchi ambayo abiria wengi waliopanda kwenye ndege hiyo walitambua kama Israel lakini watekaji hawa na watu wengine duniani wakitambua kama Palestina.
    Mara tu baada ya tangazo hili kusikika kwenye vipaza sauti vya ndege, abiria wote licha ya kuwa kwenye mshituko mkubwa wa ghafla lakini moja kwa moja waling’amua ni nini kilikuwa kinaendelea. Flight 139 au Haifa 1 kama alivyoibatiza aliyetoa tangazo, ilikuwa imetekwa na maharamia.
    Baada ya Tangazo hili, haramaia Wilfred Bose akamuamuru rubani Michel Bacos kuendesha ndege kuelekea mji wa Bengazhi, nchini Libya.
    Baada ya kuwasili uwanja wa ndege wa Bengazhi nchini Libya, ndege ilitumia karbia masaa saba uwanjani hapo kwa ajili ya kujaza ndege mafuta. Katika masaa hayo saba kuna mwanamama Patricia Martel mwenye asili ya Uingereza lakini akiwa ameolewa nchin Israel miaka michache iliyopita alifanya ‘kituko’ ambacho kilikuja kuwa na manufaa sana baadae. Wakati ambao ndege inaendelea kujaza mafuta kwa masaa yote hayo, huyu mama ambaye ni nesi kwa taaluma, alianza kulalamika juu ya maumivu ya tumbo yaliyopitiliza. Aliwaeleza watekaji kwamba ana ujauzito. Maharamia haya yakaruhusu wahudumu wa ndege wamuhudumie mwananmke mwenzao kwa vile ambavyo wataweza kwa kuzingatia kwamba ana mimba. Baada ya kuhudumiwa kwa karibia saa nzima, Patricia akatumua ujuzi wake wa unesi akafanya alicho kifanya na ghafla akaanza kutoka damu kiduchu sehemu za siri. Baada ya damu hizi kidogo kuanza kumtoka na kulalamika kuwa maumivu yamemzidia ndipo hapa ambapo wahudumu wa ndege wakaripoti kwa maharamia kuwa mimba ilikuwa imetoka.

    Kwa huruma na ili kuepusha taharuki ndani ya ndege maharamia hawa wakamuachia huru mwanamama Patricia Martel hapo uwanja wa ndege mjini Bengazhi ili aweze kupata uangalizi mzuri zaidi wa kidaktari.
    Lakini ukweli ni kwamba Patricia hakuwa na mimba wala hakuwa na maumivu yoyote tumboni, alichokifanya ilikuwa ni uigizaji pamoja na kuchanganya utaalamu wake wa fani ya unesi na kuweza kuwahadaa maharamia hao.
    Baada ya kuachiwa Patricia alikuwa ni mtu wa kwanza muhimu kutumiwa na Mossad kujua taarifa sahihi zaidi kuhusu nini hasa kilikuwa kinaendelea ndani ya ndege, kulikuwa na watekaji wangapi, jinsia zao, silaha zao na vingine vyote ambavyo alifanikiwa kuviona.
    Baada ya hapa Bose akamuamuru tena rubani Michel Bacos kurusha tena ndege angani pasipo kumueleza kuwa wanaeelekea wapi.
    Wakiwa angani ndipo alianza kumpa maagizo wapi hasa anataka waelekee. Upande wa abiria kwenye cabin ambao nao walikuwa wamewekwa chini ya ulinzi na maharamia wengine waliosalia, wao hawaku wanafahamu hata ni wapi walikuwa wanaeleke. Ndege ilikuwa inaruka angani kwa karibia masaa 24. Abiria wengi walianza kuhisi labda ndege ilikuwa inaruka kuelekea China au labda Siberia, na vichwani mwao walikuwa wanajiuliza kwa nini walikuwa wanapelekwa huko.
    Lakini laiti kama wangelijua mahali ambako walikuwa wanapelekwa basi wangetamani ndege hiyo ielekee kweli china.
    Baada ya ya takribani masaa 24 ndege kuwa angani tangu iruke kutoka Bengazhi nchini Libya, hatimaye abiria walisikia ndege ikitua na kugusa Runway ya kiwanja cha ndege mahali fulani dunia walipowasili lakini wakiwa hawafahamu ni mwapi hasa walikuwa.
    Baada ya matairi ya ndege tu kukanyaga lami za runaway na abiria kufungua ‘pazia’ (shutters) kwenye vioo vilivyopo pemnbeni mwa siti zao na kuangalia nje, mara moja wakaelewa wako wapi. Nje uwanjani kwenye lami, kulikuwa kumesimama lijitu la miraba minne lenye ngozi nyeusi tiiii likiwa na walinzi wa kijeshi na wengine waliovalia nguo za kiraia likiwa limezungukwa pande zote na walinzi hao. Mtu huyu mwenye umbo la kutisha kwa kipindi hiki alikuwa anajulikana ulimwenguni kote kutokana na matendo yake na ukatili wake. Kwa kutupa jicho mara moja tu haukuweza kukosea kujua kuwa pale kwenye lami uwanjani, alikuwa amesimama Generali Nduli Idd Amin Dadaa, ‘Field Marshal’. Swali lilokuwepo vichwani mwao lilikuwa limejibiwa tayari, wamepelekwa kwenye ardhi ya moja ya watawala ‘watemi’ na katili kuwahi kutokea juu ya uso wa dunia. Walikuwa nchini Uganda.
    Baada ya ndege kusimama abria wote 248 ambao wengi wao walikuwa ni raia wa Israel na wayahudi, walishushwa kutoka kwenye ndege na moja kwa moja kupelekwa ‘terminal’ ambayo kwa wakati huo ilikuwa haitumiki. Mpaka muda huu wakang’amua kwamba hawakuwa ‘abiria’ tena kama ambavyo waliondoka Tel Aviv, bali sasa walikuwa ni mateka wa maharamia haya ya kijerumani, palestina na jeshi la Uganda.

    Wakati huo huo…
    Nchini Israel katika jamii ya masuala ya usalama walikuwa wako kwenye bumbuwazi kuu, matukio ya dizaini hii huwa ni ya kushtukiza na yanatokea kipindi ambacho ‘haujajiandaa’. Pia kwa kipindi hiki bado Idara ya Ujasusi ya Mossad hawakuwa na Intelejensia ya kutosha za nchi nyingi za kiafrika, akili yao na nguvu yao yote ilikuwa kwenyekudhibiti juhudi za nchi za kiarabu kufuta Israel kutoka kwenye eneo hilo walilopo. Kwa hiyo kitendo cha raia wao wengi kiasi hiki kutekwa na kupelekwa Africa kilikuwa si tu na changamoto ya namana gani wanawaokoa bali pia kulikuwa na changamoto ya uwepo wa Intelijensia ya kutosha kuhusu eneo la Entebbe, Uganda kuweza kufanya oparesheni yoyote ya kijeshi.
    Ndipo hapa ambapo waziri mkuu wa kipindi hicho wa Israel Yitzhak Rabin akaitisha kikao cha maafisa wa ngazi za juu wa jeshi na Mossad na kuwauliza swali moja tu, *“…tunafanyeje?”*

    Itaendelea…
    #TheBold_Jf
    OPERATION ENTEBBE -1 Jina mbadala: Operation Thunderstorm/Operation Yonatan Watekelezaji: -MOSSAD - IDF (ISRAEL DEFENCE FORCE) Kitengo cha Weledi: Sayeret Matkal Mwaka wa utekelezaji: July, 1976 Nchi: Israel/Uganda Silaha za kukumbukwa: Lockheed C-130 Hurcules Wahusika wa kukumbukwa: - Yonatan Netanyahu (kaka wa Waziri Mkuu wa zamani Benjamin Netanyahu) -Ehud Barak (alikuja kuwa Waziri Mkuu miaka ya karibuni) MOSAD & IDF: OPERATION ENTEBBE Siku ya tarehe 27 June mwaka 1976 ilianza kama siku nyingine yioyote ndani ya uwanja wa ndege wa kimataifa katika mji mkuu wa nchi ya Israel Tel Aviv, uwanja ujulikanao kama Ben Gurion International Airport. Moja kati ya ndege ambayo ilikuwa inafanya safari yake katika siku ya elo ilikuwa ni ndege ya kampuni ya Air Frace ambao walikuwa na ndege yao ya Air France Flight 139 ambayo ni ndege aina ya Airbus A300B4-203 yenye namba ya usajili mkiani F-BVGG (c/n 019). Ndege hii ilikuwa inafanya safari yake katika siku ya leo kutoka Tel Aviv na ilikuwa inatarajiwa kutua katika uwanja wa ndege wa Charles DE Gaulle International Airport jijini Paris, Ufaransa. Baada ya taratibu na protokali zote za uwanja wa ndege kukamilika na abiria wote kukwea kwenye ndege, ndege iliruka kutoka kiwanjani ikiwa na abiria 190 ndani yake pamoja na ‘crew’ ya watu 12 (Marubani na wahudumu) ambamo asilimia kubwa ya abiria walikuwa ni raia wa Israel pamoja na watu wenye asili ya kiyahudi. Ndege iliruka kutoka Tel Aviv mpaka jijini Anthens, Ugiriki ambapo ilichukua abiria wengine wapatao 58. Baada ya hapo ndege iliruka pasipo kujua kwamba kati aya abiria hao 58 waliowachukua Ugiriki ndani yao kulikuwa na abiria wanne ambao walikuwa ni wanachama wawili wa kikundi cha Popular Front For The Liberation of Palestine – External Operations (PFLP-EO) kutoka Plaestina na wanachama wawili wa kikundi cha Revolutionary Cells kutoka nchini Ujerumani. Baada ya abiria wote kukamilisha utaratibu na kupanda ndani ya ndege, ndege iliondoka uwanjani Athens mnamo amjira ya saa 6 na dakika 30 mchana kuelekea Paris, Ufaransa. Dakika chache baada ya ndege kuruka rubani mkuu wa ndege ambaye ndiye alikuwa ameshikili ‘usukani’ Bw. Michel Bacos akasikia kelele nyuma ya ndege wanakokaa abiria (cabin). Ili kujiridhisha kwamba kila kitu kiko sawa, rubani Michel Bacos akamuagiza msaidizi wake mmoja wapo ambaye ndiye alikuwa injinia wa ndege aende kuangalia nini kilikuwa kinaendelea. Mara tu baada ya msaidizi huyo kufungua mlango wa mbele wa chumba cha marubani, alikutana uso kwa uso na bastola usoni mwake iliyoshikiliwa na mtu ambaye mkononi alikuwa amebeba bomu la kurusha kwa mkono. Huku msaidizi huyo akiwa bado ameshikwa na bumbuwazi, mtu huyu mwenye bomu mkononi na bastola (jina lake anaitwa Wilfred Bose raia wa Ujerumani) alimsukuma yule injinia nakumrudisha tena ndani ya chumba cha marubani na kisha yeye mwenyewe pia kuingia. Mara tu baada ya kufika ndani ya chumba cha marubani, akawaweka chini ya ulinzi marubani ambao bado walikuwa kwenye mshituko wa mshangao na kisha kumnyanyua rubani msaidizi kutoka kwenye siti yake na kukaa yeye. Baada ya kukaa kwenye siti ya rubani msaidizi kitu cha kwanza alichokifanya haramia huyu Wilfre Bose ni kuchukua microphone ambayo marubani huwa wanatumia kutoa matangazo kwa abria, na baada ya kuiweka microphone akatoa tangazo lake la kwanza, kwa sauti ya utulivu iliyojaa lafudhi nzito ya kijerumani, akawasema; *“..kuanzia sasa ndege hii inaitwa HAIFA 1, badala ya Flight 139..”* Haifa ni eneo (mji) maarufu ulipo kaskazini mwa nchi ambayo abiria wengi waliopanda kwenye ndege hiyo walitambua kama Israel lakini watekaji hawa na watu wengine duniani wakitambua kama Palestina. Mara tu baada ya tangazo hili kusikika kwenye vipaza sauti vya ndege, abiria wote licha ya kuwa kwenye mshituko mkubwa wa ghafla lakini moja kwa moja waling’amua ni nini kilikuwa kinaendelea. Flight 139 au Haifa 1 kama alivyoibatiza aliyetoa tangazo, ilikuwa imetekwa na maharamia. Baada ya Tangazo hili, haramaia Wilfred Bose akamuamuru rubani Michel Bacos kuendesha ndege kuelekea mji wa Bengazhi, nchini Libya. Baada ya kuwasili uwanja wa ndege wa Bengazhi nchini Libya, ndege ilitumia karbia masaa saba uwanjani hapo kwa ajili ya kujaza ndege mafuta. Katika masaa hayo saba kuna mwanamama Patricia Martel mwenye asili ya Uingereza lakini akiwa ameolewa nchin Israel miaka michache iliyopita alifanya ‘kituko’ ambacho kilikuja kuwa na manufaa sana baadae. Wakati ambao ndege inaendelea kujaza mafuta kwa masaa yote hayo, huyu mama ambaye ni nesi kwa taaluma, alianza kulalamika juu ya maumivu ya tumbo yaliyopitiliza. Aliwaeleza watekaji kwamba ana ujauzito. Maharamia haya yakaruhusu wahudumu wa ndege wamuhudumie mwananmke mwenzao kwa vile ambavyo wataweza kwa kuzingatia kwamba ana mimba. Baada ya kuhudumiwa kwa karibia saa nzima, Patricia akatumua ujuzi wake wa unesi akafanya alicho kifanya na ghafla akaanza kutoka damu kiduchu sehemu za siri. Baada ya damu hizi kidogo kuanza kumtoka na kulalamika kuwa maumivu yamemzidia ndipo hapa ambapo wahudumu wa ndege wakaripoti kwa maharamia kuwa mimba ilikuwa imetoka. Kwa huruma na ili kuepusha taharuki ndani ya ndege maharamia hawa wakamuachia huru mwanamama Patricia Martel hapo uwanja wa ndege mjini Bengazhi ili aweze kupata uangalizi mzuri zaidi wa kidaktari. Lakini ukweli ni kwamba Patricia hakuwa na mimba wala hakuwa na maumivu yoyote tumboni, alichokifanya ilikuwa ni uigizaji pamoja na kuchanganya utaalamu wake wa fani ya unesi na kuweza kuwahadaa maharamia hao. Baada ya kuachiwa Patricia alikuwa ni mtu wa kwanza muhimu kutumiwa na Mossad kujua taarifa sahihi zaidi kuhusu nini hasa kilikuwa kinaendelea ndani ya ndege, kulikuwa na watekaji wangapi, jinsia zao, silaha zao na vingine vyote ambavyo alifanikiwa kuviona. Baada ya hapa Bose akamuamuru tena rubani Michel Bacos kurusha tena ndege angani pasipo kumueleza kuwa wanaeelekea wapi. Wakiwa angani ndipo alianza kumpa maagizo wapi hasa anataka waelekee. Upande wa abiria kwenye cabin ambao nao walikuwa wamewekwa chini ya ulinzi na maharamia wengine waliosalia, wao hawaku wanafahamu hata ni wapi walikuwa wanaeleke. Ndege ilikuwa inaruka angani kwa karibia masaa 24. Abiria wengi walianza kuhisi labda ndege ilikuwa inaruka kuelekea China au labda Siberia, na vichwani mwao walikuwa wanajiuliza kwa nini walikuwa wanapelekwa huko. Lakini laiti kama wangelijua mahali ambako walikuwa wanapelekwa basi wangetamani ndege hiyo ielekee kweli china. Baada ya ya takribani masaa 24 ndege kuwa angani tangu iruke kutoka Bengazhi nchini Libya, hatimaye abiria walisikia ndege ikitua na kugusa Runway ya kiwanja cha ndege mahali fulani dunia walipowasili lakini wakiwa hawafahamu ni mwapi hasa walikuwa. Baada ya matairi ya ndege tu kukanyaga lami za runaway na abiria kufungua ‘pazia’ (shutters) kwenye vioo vilivyopo pemnbeni mwa siti zao na kuangalia nje, mara moja wakaelewa wako wapi. Nje uwanjani kwenye lami, kulikuwa kumesimama lijitu la miraba minne lenye ngozi nyeusi tiiii likiwa na walinzi wa kijeshi na wengine waliovalia nguo za kiraia likiwa limezungukwa pande zote na walinzi hao. Mtu huyu mwenye umbo la kutisha kwa kipindi hiki alikuwa anajulikana ulimwenguni kote kutokana na matendo yake na ukatili wake. Kwa kutupa jicho mara moja tu haukuweza kukosea kujua kuwa pale kwenye lami uwanjani, alikuwa amesimama Generali Nduli Idd Amin Dadaa, ‘Field Marshal’. Swali lilokuwepo vichwani mwao lilikuwa limejibiwa tayari, wamepelekwa kwenye ardhi ya moja ya watawala ‘watemi’ na katili kuwahi kutokea juu ya uso wa dunia. Walikuwa nchini Uganda. Baada ya ndege kusimama abria wote 248 ambao wengi wao walikuwa ni raia wa Israel na wayahudi, walishushwa kutoka kwenye ndege na moja kwa moja kupelekwa ‘terminal’ ambayo kwa wakati huo ilikuwa haitumiki. Mpaka muda huu wakang’amua kwamba hawakuwa ‘abiria’ tena kama ambavyo waliondoka Tel Aviv, bali sasa walikuwa ni mateka wa maharamia haya ya kijerumani, palestina na jeshi la Uganda. Wakati huo huo… Nchini Israel katika jamii ya masuala ya usalama walikuwa wako kwenye bumbuwazi kuu, matukio ya dizaini hii huwa ni ya kushtukiza na yanatokea kipindi ambacho ‘haujajiandaa’. Pia kwa kipindi hiki bado Idara ya Ujasusi ya Mossad hawakuwa na Intelejensia ya kutosha za nchi nyingi za kiafrika, akili yao na nguvu yao yote ilikuwa kwenyekudhibiti juhudi za nchi za kiarabu kufuta Israel kutoka kwenye eneo hilo walilopo. Kwa hiyo kitendo cha raia wao wengi kiasi hiki kutekwa na kupelekwa Africa kilikuwa si tu na changamoto ya namana gani wanawaokoa bali pia kulikuwa na changamoto ya uwepo wa Intelijensia ya kutosha kuhusu eneo la Entebbe, Uganda kuweza kufanya oparesheni yoyote ya kijeshi. Ndipo hapa ambapo waziri mkuu wa kipindi hicho wa Israel Yitzhak Rabin akaitisha kikao cha maafisa wa ngazi za juu wa jeshi na Mossad na kuwauliza swali moja tu, *“…tunafanyeje?”* Itaendelea… #TheBold_Jf
    Like
    1
    · 0 Comments ·0 Shares ·1K Views
  • Kadiri siku ya mwisho ya amri ya kupiga marufuku au kuuzwa kwa TikTok inavyokaribia Januari 19, 2025, Watumiaji wengi wa TikTok kutoka Marekani wamehamia kwenye Xiaohongshu, jukwaa maarufu la miandao wa kijamii la Kichina.

    Hii inakuja baada ya amri inayotaka kampuni mama ya TikTok, ByteDance, kuuza biashara yake ya Marekani au kukabiliwa na kupigwa marufuku kutokana na wasiwasi wa usalama wa kitaifa.

    Watumiaji wengi wa TikTok wanapigania marufuku hiyo kwa kuhamia Xiaohongshu, na kuitwa wakimbizi wa TikTok. Hali iliyopeleka pelekea Xiaohongshu kupanda kwenye orodha ya programu zinazopakuliwa zaidi.

    Hata hivyo, baadhi ya Wanaharakati wa Kichina wanakosoa hatua hii, wakisema inapuuzia mbali mateso halisi ya Watu chini ya utawala wa China. Kwa upande mwingine, mamlaka za China zinaona hili kama fursa ya kupanua ushawishi wao duniani, na Xiaohongshu inaboresha zana za tafsiri ili kuwezesha mawasiliano na Watumiaji wa kimataifa.

    Kadiri siku ya mwisho ya amri ya kupiga marufuku au kuuzwa kwa TikTok inavyokaribia Januari 19, 2025, Watumiaji wengi wa TikTok kutoka Marekani wamehamia kwenye Xiaohongshu, jukwaa maarufu la miandao wa kijamii la Kichina. Hii inakuja baada ya amri inayotaka kampuni mama ya TikTok, ByteDance, kuuza biashara yake ya Marekani au kukabiliwa na kupigwa marufuku kutokana na wasiwasi wa usalama wa kitaifa. Watumiaji wengi wa TikTok wanapigania marufuku hiyo kwa kuhamia Xiaohongshu, na kuitwa wakimbizi wa TikTok. Hali iliyopeleka pelekea Xiaohongshu kupanda kwenye orodha ya programu zinazopakuliwa zaidi. Hata hivyo, baadhi ya Wanaharakati wa Kichina wanakosoa hatua hii, wakisema inapuuzia mbali mateso halisi ya Watu chini ya utawala wa China. Kwa upande mwingine, mamlaka za China zinaona hili kama fursa ya kupanua ushawishi wao duniani, na Xiaohongshu inaboresha zana za tafsiri ili kuwezesha mawasiliano na Watumiaji wa kimataifa.
    0 Comments ·0 Shares ·534 Views
  • Wabunge wa Marekani wamemtaka Rais wa Nchi hiyo J. Biden kutohufungia mtandao wa kijamii wa TikTok nchini humo ifikapo Jumapili na kutoa tahadhari juu ya mamillioni ya Wabunifu wa mtandao huo wanaweza kuathiriwa na kitendo hicho.

    "Tunaomba iwepo njia ya kujaribu kusuluhisha suala hili kwa busara ili TikTok isijikute katika hali ngumu" amekaririwa akisema Seneta mmoja kutoka Democratic aitwaye Ed Markey

    Hata hivyo Kiongozi wa Democratic katika Baraza la Seneti Chuck Schumer alizungumza na J. Biden na kumtaka kuongeza muda wa mwisho wa siku (90) kwa kampuni inayomiliki TikTok kutoka Nchini China ya ByteDance ili kuuza mali za TikTok kwa Mmarekani na kuzuia marufuku ya mtandao huo unaotumiwa na Wamarekani zaidi millioni (170).

    Ikumbukwe kwamba ugomvi baina ya Nchi ya Marekani na Wamiliki wa TikTok ni kuwa TikTok ilikataa kutoa nafasi kwa Nchi ya Marekani kuingilia ubinafsi (Private) wa Watumiaji wa mtandao huo ambapo Nchi ya Marekani inadai kuwa mtandao huo unatumiwa na Nchi ya China kuingilia mambo ya ndani ya Marekani .

    Ili mtandao huo wa TikTok uruhusiwe Nchini Marekani, Nchi hiyo ilitoa aina mbili za makubaliao. Mosi ni mtandao huo kukubali Nchi ya Marekani kuingia ndani ya mtandao ili ifahamu kinachoendelea au kukubali kuuza hisa (share) kwa Mmarekani.

    Wabunge wa Marekani 🇺🇸 wamemtaka Rais wa Nchi hiyo J. Biden kutohufungia mtandao wa kijamii wa TikTok nchini humo ifikapo Jumapili na kutoa tahadhari juu ya mamillioni ya Wabunifu wa mtandao huo wanaweza kuathiriwa na kitendo hicho. "Tunaomba iwepo njia ya kujaribu kusuluhisha suala hili kwa busara ili TikTok isijikute katika hali ngumu" amekaririwa akisema Seneta mmoja kutoka Democratic aitwaye Ed Markey Hata hivyo Kiongozi wa Democratic katika Baraza la Seneti Chuck Schumer alizungumza na J. Biden na kumtaka kuongeza muda wa mwisho wa siku (90) kwa kampuni inayomiliki TikTok kutoka Nchini China ya ByteDance ili kuuza mali za TikTok kwa Mmarekani na kuzuia marufuku ya mtandao huo unaotumiwa na Wamarekani zaidi millioni (170). Ikumbukwe kwamba ugomvi baina ya Nchi ya Marekani na Wamiliki wa TikTok ni kuwa TikTok ilikataa kutoa nafasi kwa Nchi ya Marekani kuingilia ubinafsi (Private) wa Watumiaji wa mtandao huo ambapo Nchi ya Marekani inadai kuwa mtandao huo unatumiwa na Nchi ya China kuingilia mambo ya ndani ya Marekani . Ili mtandao huo wa TikTok uruhusiwe Nchini Marekani, Nchi hiyo ilitoa aina mbili za makubaliao. Mosi ni mtandao huo kukubali Nchi ya Marekani kuingia ndani ya mtandao ili ifahamu kinachoendelea au kukubali kuuza hisa (share) kwa Mmarekani.
    0 Comments ·0 Shares ·589 Views
  • "Wolper aliwahi kuniomba hela ya mtaji nikachukua milioni 30 nikampa ila cha kusikitisha akaenda kula pesa hizo na bishoo mmoja mwenye sura nzuri nzuri anaitwa Rich Mitindo. Alipokuwa China nikawa naona anapiga picha nyingi nyingi na jamaa, nilipomuuliza akawa anajibu "hakuna kitu babe huyu ni mdogo wangu tu" - Harmonize, Msanii wa muziki Tanzania.

    "Wolper aliwahi kuniomba hela ya mtaji nikachukua milioni 30 nikampa ila cha kusikitisha akaenda kula pesa hizo na bishoo mmoja mwenye sura nzuri nzuri anaitwa Rich Mitindo. Alipokuwa China nikawa naona anapiga picha nyingi nyingi na jamaa, nilipomuuliza akawa anajibu "hakuna kitu babe huyu ni mdogo wangu tu" - Harmonize, Msanii wa muziki Tanzania.
    Like
    1
    · 0 Comments ·0 Shares ·466 Views
  • China na Ethiopia zaadhimisha miaka 55 ya uhusiano wa kibalozi
    China na Ethiopia zimeadhimisha miaka 55 ya uhusiano wa kibalozi Jumapili mjini Addis Ababa.
    Tukio hilo kubwa lililoandaliwa na Ubalozi wa China na Chama cha Wafanyabiashara Wachina nchini Ethiopia, likiambatana na sherehe za sikukuu ijayo ya Mwaka Mpya wa Jadi wa Kichina, lilikuwa na shughuli mbalimbali, ikiwemo mnada wa hisani, maonesho ya utamaduni wa China, vyakula vya jadi vya kichina na huduma bure za matibabu.
    Sikukuu ya Mwaka Mpya wa Jadi wa Kichina itaangukia Januari 29 mwaka huu, ikifungua Mwaka wa Nyoka, kwa mujibu wa kalenda ya kilimo ya China.
    Akiongea katika hafla hiyo iliyohudhuriwa na umati mkubwa wa Wachina na wenyeji, Balozi wa China nchini Ethiopia Bw. Chen Hai amesema, China itatumia maadhimisho ya miaka 55 ya uhusiano kama mwanzo mpya, kutelekeza matokeo ya mkutano wa kilele wa Baraza la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) uliofanyika Beijing na makubaliano yaliyofikiwa na wakuu wa nchi hizo mbili, na kufanya juhudi pamoja na marafiki wa Ethiopia kuzijenga nchi hizo mbili kuwa za kisasa.
    Akikumbusha kuwa China na Ethiopia zimeinua uhusiano wao hadi kufikia ngazi ya Uhusiano wa Wenzi wa Kimkakati wa Pande Zote tangu mwezi Oktoba mwaka jana, Waziri wa Mambo ya Nje wa Ethiopia Mesganu Arga amesisitiza urafiki mkubwa katika China na Ethiopia, na kusema uhusiano huo wa karibu ni ushahidi wa kile kinachoweza kufikiwa wakati mataifa haya mawili yanaheshimiana na kutafuta maendeleo ya pamoja.
    China na Ethiopia zaadhimisha miaka 55 ya uhusiano wa kibalozi China na Ethiopia zimeadhimisha miaka 55 ya uhusiano wa kibalozi Jumapili mjini Addis Ababa. Tukio hilo kubwa lililoandaliwa na Ubalozi wa China na Chama cha Wafanyabiashara Wachina nchini Ethiopia, likiambatana na sherehe za sikukuu ijayo ya Mwaka Mpya wa Jadi wa Kichina, lilikuwa na shughuli mbalimbali, ikiwemo mnada wa hisani, maonesho ya utamaduni wa China, vyakula vya jadi vya kichina na huduma bure za matibabu. Sikukuu ya Mwaka Mpya wa Jadi wa Kichina itaangukia Januari 29 mwaka huu, ikifungua Mwaka wa Nyoka, kwa mujibu wa kalenda ya kilimo ya China. Akiongea katika hafla hiyo iliyohudhuriwa na umati mkubwa wa Wachina na wenyeji, Balozi wa China nchini Ethiopia Bw. Chen Hai amesema, China itatumia maadhimisho ya miaka 55 ya uhusiano kama mwanzo mpya, kutelekeza matokeo ya mkutano wa kilele wa Baraza la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) uliofanyika Beijing na makubaliano yaliyofikiwa na wakuu wa nchi hizo mbili, na kufanya juhudi pamoja na marafiki wa Ethiopia kuzijenga nchi hizo mbili kuwa za kisasa. Akikumbusha kuwa China na Ethiopia zimeinua uhusiano wao hadi kufikia ngazi ya Uhusiano wa Wenzi wa Kimkakati wa Pande Zote tangu mwezi Oktoba mwaka jana, Waziri wa Mambo ya Nje wa Ethiopia Mesganu Arga amesisitiza urafiki mkubwa katika China na Ethiopia, na kusema uhusiano huo wa karibu ni ushahidi wa kile kinachoweza kufikiwa wakati mataifa haya mawili yanaheshimiana na kutafuta maendeleo ya pamoja.
    Like
    Love
    3
    · 0 Comments ·0 Shares ·456 Views
  • #Security #Intelligence, #HPV, Kwa ufupi tu ni kwamba haya magari yanatengenezwa maalumu kwa ajili ya kuzuia mawasiliano ya aina yoyote 'controlled' yanayozunguka eneo ambalo mtu anayelindwa atakuwapo.

    Ni teknolojia yenye gharama kubwa duniani na hutumiwa na Viongozi wakuu wa Serikali na wafanyabiashara wenye ukwasi mkubwa.

    Ni magari yanayotumia teknolojia ya 'HPV' na yenye vifaa maalumu kwa ajili ya kufanya kitu kinaitwa "Communication Jamming''. Yaani unaingilia mawasiliano na kuyafanya kutokweza kuwasilishwa sehemu husika kwa kutumia vifaa vyenye uwezo wa teknolojia ya JAMMING.

    Mfano ukiwa eneo hilo ambalo gari hilo lipo na ukawaza kupanga njama za shambulio kwa kutuma ujumbe wa maandishi au wa kupiga simu, hautapata mtandao na wala hutafanya mawasiliano. 'Unaweza kupiga simu zisitoke' 'jamming'

    Mawasiliano yanazuiwa kupitia Frequencies. Zinauwezo wa kugundua Frequency za Mabomu yaliyotegwa ardhini kutoka umbali usio mrefu sana na kuyazuia yasiripuke iwapo yatakuwa yametegwa katika njia ambamo msafara unapita.

    Ni magari maalumu kama yanatumiwa na kiongozi mkuu wa nchi yanakuwa na Mawasiliano ya moja kwa moja na Vyombo vingine vya Ulinzi na usalama, kama makao makuu ya Jeshi, Makao mkuu ya Idara ya Ujasusi, Kitengo Maalumu cha Ulinzi wa Rais na kitengo maalumu cha Ulinzi wa Familia yake na vifaa vingine kama helkopta za kiusalama.

    Magari 'kama' haya pia yanaonekana katika misafara ya RAISI hasa anapokuwa katika ziara za mikoani, na yametengenezwa maalumu kwa ajili ya safari za umbali mrefu.

    Musa makongoro
    Nueve, China.
    #Security #Intelligence, #HPV, Kwa ufupi tu ni kwamba haya magari yanatengenezwa maalumu kwa ajili ya kuzuia mawasiliano ya aina yoyote 'controlled' yanayozunguka eneo ambalo mtu anayelindwa atakuwapo. Ni teknolojia yenye gharama kubwa duniani na hutumiwa na Viongozi wakuu wa Serikali na wafanyabiashara wenye ukwasi mkubwa. Ni magari yanayotumia teknolojia ya 'HPV' na yenye vifaa maalumu kwa ajili ya kufanya kitu kinaitwa "Communication Jamming''. Yaani unaingilia mawasiliano na kuyafanya kutokweza kuwasilishwa sehemu husika kwa kutumia vifaa vyenye uwezo wa teknolojia ya JAMMING. Mfano ukiwa eneo hilo ambalo gari hilo lipo na ukawaza kupanga njama za shambulio kwa kutuma ujumbe wa maandishi au wa kupiga simu, hautapata mtandao na wala hutafanya mawasiliano. 'Unaweza kupiga simu zisitoke' 'jamming' Mawasiliano yanazuiwa kupitia Frequencies. Zinauwezo wa kugundua Frequency za Mabomu yaliyotegwa ardhini kutoka umbali usio mrefu sana na kuyazuia yasiripuke iwapo yatakuwa yametegwa katika njia ambamo msafara unapita. Ni magari maalumu kama yanatumiwa na kiongozi mkuu wa nchi yanakuwa na Mawasiliano ya moja kwa moja na Vyombo vingine vya Ulinzi na usalama, kama makao makuu ya Jeshi, Makao mkuu ya Idara ya Ujasusi, Kitengo Maalumu cha Ulinzi wa Rais na kitengo maalumu cha Ulinzi wa Familia yake na vifaa vingine kama helkopta za kiusalama. Magari 'kama' haya pia yanaonekana katika misafara ya RAISI hasa anapokuwa katika ziara za mikoani, na yametengenezwa maalumu kwa ajili ya safari za umbali mrefu. Musa makongoro Nueve, China.
    0 Comments ·0 Shares ·794 Views
  • "SPACE SHUTTLE AU ORBITER " CHOMBO KINACHO KWENDA MWENDO MKALI MARA TISA ZAIDI YA RISASI NA MARA ISHIRINI YA SPIDI YA SAUTI "

    > Hiki chombo kina mwendo mkali, mara 9 zaidi ya risasi au mara20 ya spidi ya sauti pindi kinapotoka hapa duniani.

    Hapa tunaongelea chombo cha anga za mbali au kile kiendacho nje ya dunia. "Space shuttle" au "Orbiter" ambayo ni aina ya ndege maalum.

    "HAPO AWALI"

    Nakumbuka baadhi yetu tulipokuwa tunaona chombo kinapita umbali wa juu huku kikiacha moshi mweupe nyuma tunasema "rocket" lakini leo tunafahamu kuwa ile ni ndege ya kawaida ya abiria na ule moshi mweupe tunao uona nyuma ni matokeo ya kukutana hewa yenye joto itokayo kenye injini na hali ya hewa ya baridi iliyopo usawa ule ambapo "condensation trail" vikikutana vinaganda na kutengeneza lile wingu moshi tulionalo nyuma.
    wanasema hata mawingu yanapatikana kwa njia inayofanana kidogo na hiyo, Kwa mujibu wa wataalam.
    (kumbuka pia hata 'rocket' ina tabia ya kuacha moshi nyuma pale inapokuwa imewashwa).

    "UZITO"

    Chombo hiki 'space shuttle' mara nyingi huwa kinabeba wataalam mbalimbali wa masuala ya anga za juu "Astronauts", vifaa mbalimbali vya ujenzi wa maabara ya nje ya dunia, spare, satelite n.k
    Pia kinabeba hewa yake yenyewe ya oxygen kwasababu ya uhai wa watu waliomo ndani kwaajili ya kuendesha injini zake kinapokuwa nje ya dunia kwasababu huko hakuna hewa."vacuum space"
    Mara nyingi kinafikia jumla ya uzito wa hadi tani 2000 au kg 2,000,000 pindi kinapoondoka hapa duniani.

    "NGUVU"

    Chombo hiki kimeundwa na injini tatu lakini kinaongezewa injini mbili za ziada "Solid Rocket Booster" 'SRB' na ndiyo jina la rocket lilipozaliwa, (picha chini inaonesha rocket booster hizo mbili nyeupe) ambazo ndani hubeba mafuta ya aina yake.

    Lakini pia inabeba tank kubwa la mafuta tumboni lenye rangi ya Orange, ambalo nalo linabeba mamilioni ya lita za mafuta ambayo yote huwa yanaisha ndani ya dakika8 tangu ikianza safari.

    Kutokana na uzito na umbali wa safari yake kwa ujumla injini hizo mbili za Solid Rocket Booster "SRB" zinazalisha nguvu kufikia horse power million44 au linganisha nguvu ya vichwa vya train 14,000.

    Rocket injini hizi na tank la mafuta zikifika umbali fulani hujiachia na kurudi duniani hasa pale yanapoisha mafuta yake na kukiacha chombo kinaendelea chenyewe na injini zake ambapo kinakuwa kimefikishwa umbali ambao hakihitaji tena nguvu kubwa.

    Umbali wa kufikia anga za huko kwenye "Space" au anga za mbali uanzia kilometa 100 kutoka hapa duniani kwenda angani wanasema wataalam wa mambo ya anga.

    "MWENDO"

    Wakati kinawashwa kuondoka kutoka katika sehemu yake "launch pad" ndani ya dakika 8 huwa kinafikia mwendo wa 25000 M/hr au 40,000 k/hr hivyo kufanya kwenda kasi mara9 zaidi ya risasi au mara10 ya kasi ya sauti.
    Mwendo wa sauti ni zaidi ya 1200 k/h.

    "GHARAMA"

    Chombo hiki huwa akiruki mara kwa mara isipokuwa kwa misheni maalum tu.
    Mara nyingi, mara moja kwa miezi miwili au zaidi ya hapo.

    NASA ambao ndiyo Mamlaka ya Usafiri wa Anga za karibu na mbali huko Marekani ndiyo wahusika wakuu kwenye kurusha chombo hiki.

    Pia alikuwa anarusha Mrusi na kuna taarifa za Mchina pia alikuwa na program ya kwenda.

    Marekani ameviita majina vyombo hivyo,
    >Enteprise-kimestaafu zamani
    >Colombia-kilipata ajali kikaua wote
    >Discovery-2011
    >Atlantis-2011
    >Endeavour- 2011 kiliziba nafasi ya challenger
    >Challenge-kilipata ajali kikaua wote

    Mrusi aliita
    >Buran-na kilienda safari moja tu.

    Gharama waliyotoa NASA mwaka 2011 kurusha chombo hiki kwa safari moja ni sawa na bei ya kununua Boeing 787 Dreamliner mbili hadi Tano inategemea na misheni husika.
    Tukumbuke pia sio kila "rocket launch" roketi inayorushwa ni lazima ihusishe chombo hiki, zipo misheni nyengine za anga za mbali ambazo zinapeleka mizigo tu kama satelite n.k pasipo kuwemo watu katika chombo na huwa kinaendeshwa kwa remote control.
    "SPACE SHUTTLE AU ORBITER " CHOMBO KINACHO KWENDA MWENDO MKALI MARA TISA ZAIDI YA RISASI NA MARA ISHIRINI YA SPIDI YA SAUTI " > Hiki chombo kina mwendo mkali, mara 9 zaidi ya risasi au mara20 ya spidi ya sauti pindi kinapotoka hapa duniani. Hapa tunaongelea chombo cha anga za mbali au kile kiendacho nje ya dunia. "Space shuttle" au "Orbiter" ambayo ni aina ya ndege maalum. "HAPO AWALI" Nakumbuka baadhi yetu tulipokuwa tunaona chombo kinapita umbali wa juu huku kikiacha moshi mweupe nyuma tunasema "rocket" lakini leo tunafahamu kuwa ile ni ndege ya kawaida ya abiria na ule moshi mweupe tunao uona nyuma ni matokeo ya kukutana hewa yenye joto itokayo kenye injini na hali ya hewa ya baridi iliyopo usawa ule ambapo "condensation trail" vikikutana vinaganda na kutengeneza lile wingu moshi tulionalo nyuma. wanasema hata mawingu yanapatikana kwa njia inayofanana kidogo na hiyo, Kwa mujibu wa wataalam. (kumbuka pia hata 'rocket' ina tabia ya kuacha moshi nyuma pale inapokuwa imewashwa). "UZITO" Chombo hiki 'space shuttle' mara nyingi huwa kinabeba wataalam mbalimbali wa masuala ya anga za juu "Astronauts", vifaa mbalimbali vya ujenzi wa maabara ya nje ya dunia, spare, satelite n.k Pia kinabeba hewa yake yenyewe ya oxygen kwasababu ya uhai wa watu waliomo ndani kwaajili ya kuendesha injini zake kinapokuwa nje ya dunia kwasababu huko hakuna hewa."vacuum space" Mara nyingi kinafikia jumla ya uzito wa hadi tani 2000 au kg 2,000,000 pindi kinapoondoka hapa duniani. "NGUVU" Chombo hiki kimeundwa na injini tatu lakini kinaongezewa injini mbili za ziada "Solid Rocket Booster" 'SRB' na ndiyo jina la rocket lilipozaliwa, (picha chini inaonesha rocket booster hizo mbili nyeupe) ambazo ndani hubeba mafuta ya aina yake. Lakini pia inabeba tank kubwa la mafuta tumboni lenye rangi ya Orange, ambalo nalo linabeba mamilioni ya lita za mafuta ambayo yote huwa yanaisha ndani ya dakika8 tangu ikianza safari. Kutokana na uzito na umbali wa safari yake kwa ujumla injini hizo mbili za Solid Rocket Booster "SRB" zinazalisha nguvu kufikia horse power million44 au linganisha nguvu ya vichwa vya train 14,000. Rocket injini hizi na tank la mafuta zikifika umbali fulani hujiachia na kurudi duniani hasa pale yanapoisha mafuta yake na kukiacha chombo kinaendelea chenyewe na injini zake ambapo kinakuwa kimefikishwa umbali ambao hakihitaji tena nguvu kubwa. Umbali wa kufikia anga za huko kwenye "Space" au anga za mbali uanzia kilometa 100 kutoka hapa duniani kwenda angani wanasema wataalam wa mambo ya anga. "MWENDO" Wakati kinawashwa kuondoka kutoka katika sehemu yake "launch pad" ndani ya dakika 8 huwa kinafikia mwendo wa 25000 M/hr au 40,000 k/hr hivyo kufanya kwenda kasi mara9 zaidi ya risasi au mara10 ya kasi ya sauti. Mwendo wa sauti ni zaidi ya 1200 k/h. "GHARAMA" Chombo hiki huwa akiruki mara kwa mara isipokuwa kwa misheni maalum tu. Mara nyingi, mara moja kwa miezi miwili au zaidi ya hapo. NASA ambao ndiyo Mamlaka ya Usafiri wa Anga za karibu na mbali huko Marekani ndiyo wahusika wakuu kwenye kurusha chombo hiki. Pia alikuwa anarusha Mrusi na kuna taarifa za Mchina pia alikuwa na program ya kwenda. Marekani ameviita majina vyombo hivyo, >Enteprise-kimestaafu zamani >Colombia-kilipata ajali kikaua wote >Discovery-2011 >Atlantis-2011 >Endeavour- 2011 kiliziba nafasi ya challenger >Challenge-kilipata ajali kikaua wote Mrusi aliita >Buran-na kilienda safari moja tu. Gharama waliyotoa NASA mwaka 2011 kurusha chombo hiki kwa safari moja ni sawa na bei ya kununua Boeing 787 Dreamliner mbili hadi Tano inategemea na misheni husika. Tukumbuke pia sio kila "rocket launch" roketi inayorushwa ni lazima ihusishe chombo hiki, zipo misheni nyengine za anga za mbali ambazo zinapeleka mizigo tu kama satelite n.k pasipo kuwemo watu katika chombo na huwa kinaendeshwa kwa remote control.
    0 Comments ·0 Shares ·682 Views
  • VIETNAM WAR VITA AMBAYO MAREKANI ILISHINDWA VIBAYA

    Vita maarufu ya Vietnam ni moja ya vita katika historia ya Marekani ambazo taifa kubwa na lenye nguvu duniani lililazimika kuondoka uwanja wa mapambano baada ya kushindwa vibaya.
    Vita hii ilipiganwa kuanzia mwaka 1955 mpaka 1975, na ilipiganwa maeneo ya Vietnam kwenyewe, Laos na Cambodia.

    Kwa juu juu ilikuwa ni vita iliyopiganwa kati ya Vietnam Kaskazini na Vietnam Kusini lakini nyuma ya pazia ilikuwa ni vita ya kijasusi kati ya wababe wa dunia wa wakati huo yaani Marekani na Urusi ya Kisovieti(proxy war), huku kila mbabe akitaka kupandikiza itikadi yake kwa upande huo, Marekani akitaka Ubepari utawale na Mrusi akitaka Ukomunisti utawale.

    Vietnam ya Kaskazini ilisapotiwa na Urusi ya wakati huo(USSR), China na nchi nyingine za Kikomunisti huku Vietnam ya Kusini ikisapotiwa na Marekani, Korea Kusini, Australia, Thailand na nchi nyingine zilizokuwa zikipinga Ukomunisti.

    Wakati vuguvugu la vita limeanza kukolea mwaka 1950 Marekani ilituma kikosi cha majasusi wake nchini Vietnam wakati huo ikiwa Koloni la Mfaransa ikijulikana kama French IndoChina kwa ajili ya mafunzo, udukuzi na kukusanya taarifa za kijasusi kabla ya kuanza mashambulizi mazito, lengo likiwa kutoa mafunzo ya kijeshi na kijasusi kwa askari wa Vietnam ya Kusini na kuviandaa vikosi vyake kwa ajili ya mapigano ya kukata na shoka.

    Ilipofika mwaka 1961 wakati vita imekolea Marekani kwa kutumia taarifa za kijasusi ilizokusanya ilipeleka kikosi maalumu cha makomando wa Jeshi la Anga maarufu kama Green Berets kwa kazi kuu ya kufanya operations za kimya kimya za anga ili kulidhoofisha jeshi la Vietnam Kaskazini.
    Kikosi hiki kiliungana baadaye na kikosi cha makomando wa anga waliojulikana kama ECO 31 na US Marines.

    Hata hivyo kutokana na udhaifu wa taarifa za kijasusi vikosi hivi havikufanikiwa sana hali iliyopelekea kuvunjwa na kuundwa kikosi maalumu kingine mwaka 1962 kilichoitwa U.S. Military Assistance Command, Vietnam (MACV) kilichokuwa chini ya Idara ya Usalama ya Marekani.

    Pamoja na uwezo mkubwa wa Marekani kimafunzo na kisilaha lakini kulikuwa na udhaifu mkubwa wa idara za kijasusi hali iliyopelekea Idara nyeti za usalama za Marekani
    ikiwemo C.I.A kushindwa kutoa makadirio hasa ya kijeshi juu ya uzito wa Vita ile.

    Kutokana na nature ya nchi za Kikomunisti kuendeshwa kwa uzalendo uliotukuka, Marekani alishindwa kukusanya taarifa za msingi za kivita kwa kutumia ujasusi wa kitaaluma, badala yake alitegemea zaidi kuwahoji askari wa adui waliokamatwa na kuteswa.

    Vietnam Kaskazini kwa kusaidiwa na Majasusi wa Russia aliweza "kuwauzia taarifa feki" majasusi wa Kimarekani, na Marekani ikaingia mkenge kwa ku-underestimate uwezo wa Vietnam Kaskazini katika ulingo wa vita, kifupi taarifa za Kijasusi zilizopelekwa Washington na washirika wake zilikuwa tofauti kabisa na kilichokuwa uwanja wa mapambano.

    Kwa mfano Majasusi wa Marekani walishindwa kujua Formation ya Vita(Battle Formation) waliyokuwa wanatumia Wavietnam.
    Wavietnam wakiwa chini ya Majasusi wao wa VCSS waliweza kuunda vikosi vinne ya kimapambano vilivyopambana kwa wakati mmoja huku makamanda na wale wapiganaji mahiri wa kikosi kimoja wakibadilishana na wa Kikosi kingine huku mapambano yakiendelea.

    Kwamba unaweza kumuona leo kamanda fulani anapigana eneo A na kikosi chake akitumia mbinu fulani za msituni, mara baada ya siku tatu unashangaa imefanyika substitution kama ya kwenye mpira kaingia kamanda mpya na mbinu mpya kwa kutumia kikosi kile kile au akaleta wapiganaji wapya kabisa, huku yule wa eneo A akipelekwa eneo B na akabadili pia mbinu za kimapambano.

    Hali hii ilidumu kwa miaka 11 mfululizo mpaka mwaka 1966 Marekani ilipostukia mchezo huu wa kubadilishana makamanda na wapiganaji waliyokuwa wakitumia wa Vietnam, na ikapelekea idara za Kijasusi za Marekani husasani C.I.A na N.A.S.A kutuma upya majasusi maalumu wa kukusanya intelijensia nyingine mpya mwaka 1967.

    Lakini pia Majasusi wa Marekani walishindwa kujua uwezo wao majasusi wa Kivietnam kujipenyeza kwenye kambi ya adui(Inflitration Capabilities) waliokuwa nao Wa Vietnam.
    Inasadikika wengi wa askari wa Kivetman ya Kusini waliokula mafunzo na mbinu za Kivita kutoka Marekani na washirika wake mwanzoni kabisa mwa vuguvugu la kivita walikuwa wa Vietnam ya Kaskazini.
    Kifupi Vikosi vya Marekani viliwapa mafunzo ya kijeshi adui zao na wakauziwa Intelijensi ya uongo.

    Kubwa kuliko Yote Marekani na washirika wake hawakujua hasa Vietnam ana askari wangapi walio mstari wa mbele kwenye mapambano na wale wa akiba, iwapo wa mstari wa mbele
    wakilemewa, hali hii ilisababishwa na ukweli kuwa Vietnam Kaskazini ilikuwa inafuata itikadi za Kikomunisti, kila mtu alikuwa askari wa kuilinda nchi yake.

    Hata kama ungefanya shambulizi ukaua askari 1000 leo, kesho watakuja wengine wapya 1000 walio na morale ya kupambana mpaka kufa kama wale wa kwanza.
    Mwanzoni hili Wamarekani hawakulijua ila kadri mapigano yalivyopamba moto, askari wengi wa Marekani na Washirika wao walianza kuogopa kwenda mstari wa mbele hasa baada ya kugundua wanapambana na askari wengi wasioisha waliokuwa tayari kufa kwa ajili ya nchi yao.

    Baada ya Ripoti ya Kikosi kipya kilichoundwa na C.I.A kuja na taarifa zao za kijasusi walizokusanya uwanja wa mapambano, mwishoni mwa mwaka 1967 walikuja kupata taarifa
    za kustua sana kuwa Vietnam nao walikuwa na Shirika lao la Kijasusi lenye nguvu kubwa na lililokuwa limebobea katika tasnia ya Ujasusi lililokuwa linapewa mafunzo ya Kijasusi toka KGB Na China, Shirika hili liliojulikana kama Viet Cong Security Service (VCSS).

    Mwanzoni taarifa za Kijasusi walizozipata Wamarekani zilikuwa feki kuwa VCSS walikuwa kikosi maalum tu cha wapambanaji walio na silaha dhaifu na si majasusi.

    VCSS walikuwa wababe wa mapigano ya msituni na guilera war huku wakiwa na maajenti wengi zaidi ya 100,000.

    Walikuwa mabingwa wa vita vya kuviziana huku askari wachache wakijificha na kufanya ambush za kijeshi dhidi ya askari wa adui zao, wakati mwingine walivaa nguo za Kiraia na kuingia mtaani na kuishi maisha ya kawaiada kabisa huku wakipanga mikakati yao ya mashambulizi ya kuvizia.

    Ilikuwa ni ngumu sana kujua yupi ni raia yupi ni askari, hali hii iliwatia hofu mno askari wa Kimarekani na washirika wao waliokuwa mstari wa mbele wa mapambano, wengi wa waliokuwa wakidhani ni raia wa kawaida walikuwa ni maajenti wa VCSS.

    Kutokana na usiri mkubwa na umakini wa hali ya juu wa VCSS ilikuwa ni ngumu kwa Marekani kupata intelijensia kutoka vyanzo vya kuaminika, taarifa nyingi zilizokusanywa zilikuwa kupitia kukamata na kutesa askari wa adui waliokamatwa uwanja wa mapambano ambao wengi walikuwa ni askari wa vyeo vya chini au raia waliojitolea kupigana waliopewa mafunzo ya muda mfupi kwa ajili ya kupambana.
    Wengi wao walikuwa na taarifa za kupikwa walizopewa makusudi kwa ajili ya kupotosha iwapo wangekamatwa.

    Moja ya mbinu iliyowashusha morale askari wa kimarekani uwanja wa vita ni hit-and-run technique waliyotumia Wavietnam, Marekani alitegemea sana jeshi la anga na vikosi maalumu kupambana huku wakiwa na silaha nzito nzito za kubeba kwa magari.
    Wavietnam walichimba mahandaki njiani kuzuia magari ya silaha na mizinga kupita msituni,
    wali-block njia za kupitishia silaha za adui kwa kuangusha miti mikubwa kabla ya kufanya ambush, walitengeneza kambi za feki za kijeshi msituni na kila mbinu ya guilera war inayofahamika katika uwanja wa mapambano kubwa ikiwa kuviziana.

    Mfano askari wa ki-Vietnam walivizia kambi ya adui na kufanya ambush ndani ya saa moja na kisha kila askari kutimuka njia yake kilomita kadhaa baada ya kufanya shambulio kabla ya kukukutana tena eneo fulani kwa ajili ya kupanga shambulio jingine, na endapo wakizidiwa katika ambush zao iliwabidi askari hao kuficha silaha kwenye mahandaki na kisha kujichanganya na raia mtaani.

    Nyingi ya kambi za kupambana za Kivietnam hazikuwa zile zilizoonekana, nyingi zilikuwa chini ya mahandaki, madege ya kimarekani yaliposhambulia kambi kwa makombora yao, nyingi ya kambi hizo zilikuwa ni feki, zilizojengwa maalumu kwa ajili ya kum-distract adui, huku silaha nzito kutoka Urusi na China zikifichwa chini ya mahandaki makubwa.

    Wamarekani na Vikosi vyao walitumia teknolojia kupambana, huku wakitumia madege ya B-52, mizinga mikubwa, helkopta, kemikali za kupukutisha majani kwenye miti maarufu kama defoliants, lakini zote hazifua dafu.

    Baada ya makamanda wa vikosi vya Marekani kuona mbinu na silaha zao hazifanikiwi wakaamua kuwahamisha raia wote ambao wengi walikuwa wakulima wadogo wadogo kutoka maeneo ambayo maajenti wa VCSS walikuwa wanayamiliki kwenda sehemu salama ambazo zilikuwa chini ya ulinzi wao, hali hii ilizaa tatizo jingine pia kwani maajenti wengi wa VCSS walijifanya raia wakajipenyeza na kuingia maeneo yaliyokuwa hayana mapigano yaliyokuwa chini ya umiliki wa Vikosi vya Wamarekani na kuanza operations upya kwenye maeneo ambayo yalikuwa
    chini ya umiliki wa adui zao.

    Hili lilipelekea mashambulizi ya kuviziana kuongezeka kwenye maeneo mbayo Wamarekani walikuwa wanayashikilia, patrol zao zilivamiwa na askari kupokonywa silaha hali iliyopelekea morale ya askari kushuka sana, ikabidi Askari wa Kimarekani waandae ndege standby kwa ajili ya kutoa msaada muda wowote patrol zao zitakapostambuliwa,
    lakini bado haikusaidia kitu kwani wengi wa askari wa patrol hawakutaka kabisa kuingia maeneo ya ndani ndani walipita njia kuu na maeneo ya wazi kuogopa mashambulizi ya kushtukiza ambayo Shirika la Kijasusi la VCSS lilikuwa limesambaza maajenti zaidi ya 100,000.

    Kutokana na ripoti za Kijasusi kuvuja nchini Marekani kuwa probability ya kuuwawa kwa askari wao walio vitani nchini Vietnam kuwa ni zaidi ya 20% na kuwa askari waliokuwa mapiganoni wengi walikuwa wanaogopa gorilla war iliyokuwa ikiendeshwa na Wavietnam, ripoti za siri za kijasusi zinasema C.I.A kwa kutumia mbinu za kijasusi waliandaa exit strategy ambayo ilikuwa ni
    kuhamasisha maandamano na propaganda ya kile kilichoitwa vuguvugu la wananchi wa Marekani kupinga nchi yao kujiingiza katika vita ya Vietnam.

    Hatimaye Marekani kwa kisingizio cha maandamano ya wananchi kupinga nchi yao kujiingiza Vietnam mwaka 1973 waliondoa vikosi vyao na kuikabidhi Vietnam Kusini jukumu la kuendelea na mapambano dhidi ya Kaskazini.

    Vietnam ya Kaskazini iliendesha mapigano kwa miaka miwili mfululizo na hatimaye mwaka 1975 ikaukamata mji mashuhuri sana wa Saigon uliokuwa unamilikiwa na Vietnam Kusini na mwaka mmoja baadaye Kusini na Kaskazini zikaungana na kutengeneza nchi moja ya Jamhuri ya watu wa Vietnam.

    Inakadiriwa kuwa vita hiyo iligharimu maisha ya WaVietnam kati ya 966,000 mpaka Milioni 3.8 Wakambodia kati ya 240,000–300,000, Walaotia kati ya 20,000–62,000 na Wamarekani zaidi ya 58,220 huku Wamarekani zaidi ya 1,626 wakipotea na hawakujulikana walipo mpaka leo

    Mwisho
    VIETNAM WAR VITA AMBAYO MAREKANI ILISHINDWA VIBAYA Vita maarufu ya Vietnam ni moja ya vita katika historia ya Marekani ambazo taifa kubwa na lenye nguvu duniani lililazimika kuondoka uwanja wa mapambano baada ya kushindwa vibaya. Vita hii ilipiganwa kuanzia mwaka 1955 mpaka 1975, na ilipiganwa maeneo ya Vietnam kwenyewe, Laos na Cambodia. Kwa juu juu ilikuwa ni vita iliyopiganwa kati ya Vietnam Kaskazini na Vietnam Kusini lakini nyuma ya pazia ilikuwa ni vita ya kijasusi kati ya wababe wa dunia wa wakati huo yaani Marekani na Urusi ya Kisovieti(proxy war), huku kila mbabe akitaka kupandikiza itikadi yake kwa upande huo, Marekani akitaka Ubepari utawale na Mrusi akitaka Ukomunisti utawale. Vietnam ya Kaskazini ilisapotiwa na Urusi ya wakati huo(USSR), China na nchi nyingine za Kikomunisti huku Vietnam ya Kusini ikisapotiwa na Marekani, Korea Kusini, Australia, Thailand na nchi nyingine zilizokuwa zikipinga Ukomunisti. Wakati vuguvugu la vita limeanza kukolea mwaka 1950 Marekani ilituma kikosi cha majasusi wake nchini Vietnam wakati huo ikiwa Koloni la Mfaransa ikijulikana kama French IndoChina kwa ajili ya mafunzo, udukuzi na kukusanya taarifa za kijasusi kabla ya kuanza mashambulizi mazito, lengo likiwa kutoa mafunzo ya kijeshi na kijasusi kwa askari wa Vietnam ya Kusini na kuviandaa vikosi vyake kwa ajili ya mapigano ya kukata na shoka. Ilipofika mwaka 1961 wakati vita imekolea Marekani kwa kutumia taarifa za kijasusi ilizokusanya ilipeleka kikosi maalumu cha makomando wa Jeshi la Anga maarufu kama Green Berets kwa kazi kuu ya kufanya operations za kimya kimya za anga ili kulidhoofisha jeshi la Vietnam Kaskazini. Kikosi hiki kiliungana baadaye na kikosi cha makomando wa anga waliojulikana kama ECO 31 na US Marines. Hata hivyo kutokana na udhaifu wa taarifa za kijasusi vikosi hivi havikufanikiwa sana hali iliyopelekea kuvunjwa na kuundwa kikosi maalumu kingine mwaka 1962 kilichoitwa U.S. Military Assistance Command, Vietnam (MACV) kilichokuwa chini ya Idara ya Usalama ya Marekani. Pamoja na uwezo mkubwa wa Marekani kimafunzo na kisilaha lakini kulikuwa na udhaifu mkubwa wa idara za kijasusi hali iliyopelekea Idara nyeti za usalama za Marekani ikiwemo C.I.A kushindwa kutoa makadirio hasa ya kijeshi juu ya uzito wa Vita ile. Kutokana na nature ya nchi za Kikomunisti kuendeshwa kwa uzalendo uliotukuka, Marekani alishindwa kukusanya taarifa za msingi za kivita kwa kutumia ujasusi wa kitaaluma, badala yake alitegemea zaidi kuwahoji askari wa adui waliokamatwa na kuteswa. Vietnam Kaskazini kwa kusaidiwa na Majasusi wa Russia aliweza "kuwauzia taarifa feki" majasusi wa Kimarekani, na Marekani ikaingia mkenge kwa ku-underestimate uwezo wa Vietnam Kaskazini katika ulingo wa vita, kifupi taarifa za Kijasusi zilizopelekwa Washington na washirika wake zilikuwa tofauti kabisa na kilichokuwa uwanja wa mapambano. Kwa mfano Majasusi wa Marekani walishindwa kujua Formation ya Vita(Battle Formation) waliyokuwa wanatumia Wavietnam. Wavietnam wakiwa chini ya Majasusi wao wa VCSS waliweza kuunda vikosi vinne ya kimapambano vilivyopambana kwa wakati mmoja huku makamanda na wale wapiganaji mahiri wa kikosi kimoja wakibadilishana na wa Kikosi kingine huku mapambano yakiendelea. Kwamba unaweza kumuona leo kamanda fulani anapigana eneo A na kikosi chake akitumia mbinu fulani za msituni, mara baada ya siku tatu unashangaa imefanyika substitution kama ya kwenye mpira kaingia kamanda mpya na mbinu mpya kwa kutumia kikosi kile kile au akaleta wapiganaji wapya kabisa, huku yule wa eneo A akipelekwa eneo B na akabadili pia mbinu za kimapambano. Hali hii ilidumu kwa miaka 11 mfululizo mpaka mwaka 1966 Marekani ilipostukia mchezo huu wa kubadilishana makamanda na wapiganaji waliyokuwa wakitumia wa Vietnam, na ikapelekea idara za Kijasusi za Marekani husasani C.I.A na N.A.S.A kutuma upya majasusi maalumu wa kukusanya intelijensia nyingine mpya mwaka 1967. Lakini pia Majasusi wa Marekani walishindwa kujua uwezo wao majasusi wa Kivietnam kujipenyeza kwenye kambi ya adui(Inflitration Capabilities) waliokuwa nao Wa Vietnam. Inasadikika wengi wa askari wa Kivetman ya Kusini waliokula mafunzo na mbinu za Kivita kutoka Marekani na washirika wake mwanzoni kabisa mwa vuguvugu la kivita walikuwa wa Vietnam ya Kaskazini. Kifupi Vikosi vya Marekani viliwapa mafunzo ya kijeshi adui zao na wakauziwa Intelijensi ya uongo. Kubwa kuliko Yote Marekani na washirika wake hawakujua hasa Vietnam ana askari wangapi walio mstari wa mbele kwenye mapambano na wale wa akiba, iwapo wa mstari wa mbele wakilemewa, hali hii ilisababishwa na ukweli kuwa Vietnam Kaskazini ilikuwa inafuata itikadi za Kikomunisti, kila mtu alikuwa askari wa kuilinda nchi yake. Hata kama ungefanya shambulizi ukaua askari 1000 leo, kesho watakuja wengine wapya 1000 walio na morale ya kupambana mpaka kufa kama wale wa kwanza. Mwanzoni hili Wamarekani hawakulijua ila kadri mapigano yalivyopamba moto, askari wengi wa Marekani na Washirika wao walianza kuogopa kwenda mstari wa mbele hasa baada ya kugundua wanapambana na askari wengi wasioisha waliokuwa tayari kufa kwa ajili ya nchi yao. Baada ya Ripoti ya Kikosi kipya kilichoundwa na C.I.A kuja na taarifa zao za kijasusi walizokusanya uwanja wa mapambano, mwishoni mwa mwaka 1967 walikuja kupata taarifa za kustua sana kuwa Vietnam nao walikuwa na Shirika lao la Kijasusi lenye nguvu kubwa na lililokuwa limebobea katika tasnia ya Ujasusi lililokuwa linapewa mafunzo ya Kijasusi toka KGB Na China, Shirika hili liliojulikana kama Viet Cong Security Service (VCSS). Mwanzoni taarifa za Kijasusi walizozipata Wamarekani zilikuwa feki kuwa VCSS walikuwa kikosi maalum tu cha wapambanaji walio na silaha dhaifu na si majasusi. VCSS walikuwa wababe wa mapigano ya msituni na guilera war huku wakiwa na maajenti wengi zaidi ya 100,000. Walikuwa mabingwa wa vita vya kuviziana huku askari wachache wakijificha na kufanya ambush za kijeshi dhidi ya askari wa adui zao, wakati mwingine walivaa nguo za Kiraia na kuingia mtaani na kuishi maisha ya kawaiada kabisa huku wakipanga mikakati yao ya mashambulizi ya kuvizia. Ilikuwa ni ngumu sana kujua yupi ni raia yupi ni askari, hali hii iliwatia hofu mno askari wa Kimarekani na washirika wao waliokuwa mstari wa mbele wa mapambano, wengi wa waliokuwa wakidhani ni raia wa kawaida walikuwa ni maajenti wa VCSS. Kutokana na usiri mkubwa na umakini wa hali ya juu wa VCSS ilikuwa ni ngumu kwa Marekani kupata intelijensia kutoka vyanzo vya kuaminika, taarifa nyingi zilizokusanywa zilikuwa kupitia kukamata na kutesa askari wa adui waliokamatwa uwanja wa mapambano ambao wengi walikuwa ni askari wa vyeo vya chini au raia waliojitolea kupigana waliopewa mafunzo ya muda mfupi kwa ajili ya kupambana. Wengi wao walikuwa na taarifa za kupikwa walizopewa makusudi kwa ajili ya kupotosha iwapo wangekamatwa. Moja ya mbinu iliyowashusha morale askari wa kimarekani uwanja wa vita ni hit-and-run technique waliyotumia Wavietnam, Marekani alitegemea sana jeshi la anga na vikosi maalumu kupambana huku wakiwa na silaha nzito nzito za kubeba kwa magari. Wavietnam walichimba mahandaki njiani kuzuia magari ya silaha na mizinga kupita msituni, wali-block njia za kupitishia silaha za adui kwa kuangusha miti mikubwa kabla ya kufanya ambush, walitengeneza kambi za feki za kijeshi msituni na kila mbinu ya guilera war inayofahamika katika uwanja wa mapambano kubwa ikiwa kuviziana. Mfano askari wa ki-Vietnam walivizia kambi ya adui na kufanya ambush ndani ya saa moja na kisha kila askari kutimuka njia yake kilomita kadhaa baada ya kufanya shambulio kabla ya kukukutana tena eneo fulani kwa ajili ya kupanga shambulio jingine, na endapo wakizidiwa katika ambush zao iliwabidi askari hao kuficha silaha kwenye mahandaki na kisha kujichanganya na raia mtaani. Nyingi ya kambi za kupambana za Kivietnam hazikuwa zile zilizoonekana, nyingi zilikuwa chini ya mahandaki, madege ya kimarekani yaliposhambulia kambi kwa makombora yao, nyingi ya kambi hizo zilikuwa ni feki, zilizojengwa maalumu kwa ajili ya kum-distract adui, huku silaha nzito kutoka Urusi na China zikifichwa chini ya mahandaki makubwa. Wamarekani na Vikosi vyao walitumia teknolojia kupambana, huku wakitumia madege ya B-52, mizinga mikubwa, helkopta, kemikali za kupukutisha majani kwenye miti maarufu kama defoliants, lakini zote hazifua dafu. Baada ya makamanda wa vikosi vya Marekani kuona mbinu na silaha zao hazifanikiwi wakaamua kuwahamisha raia wote ambao wengi walikuwa wakulima wadogo wadogo kutoka maeneo ambayo maajenti wa VCSS walikuwa wanayamiliki kwenda sehemu salama ambazo zilikuwa chini ya ulinzi wao, hali hii ilizaa tatizo jingine pia kwani maajenti wengi wa VCSS walijifanya raia wakajipenyeza na kuingia maeneo yaliyokuwa hayana mapigano yaliyokuwa chini ya umiliki wa Vikosi vya Wamarekani na kuanza operations upya kwenye maeneo ambayo yalikuwa chini ya umiliki wa adui zao. Hili lilipelekea mashambulizi ya kuviziana kuongezeka kwenye maeneo mbayo Wamarekani walikuwa wanayashikilia, patrol zao zilivamiwa na askari kupokonywa silaha hali iliyopelekea morale ya askari kushuka sana, ikabidi Askari wa Kimarekani waandae ndege standby kwa ajili ya kutoa msaada muda wowote patrol zao zitakapostambuliwa, lakini bado haikusaidia kitu kwani wengi wa askari wa patrol hawakutaka kabisa kuingia maeneo ya ndani ndani walipita njia kuu na maeneo ya wazi kuogopa mashambulizi ya kushtukiza ambayo Shirika la Kijasusi la VCSS lilikuwa limesambaza maajenti zaidi ya 100,000. Kutokana na ripoti za Kijasusi kuvuja nchini Marekani kuwa probability ya kuuwawa kwa askari wao walio vitani nchini Vietnam kuwa ni zaidi ya 20% na kuwa askari waliokuwa mapiganoni wengi walikuwa wanaogopa gorilla war iliyokuwa ikiendeshwa na Wavietnam, ripoti za siri za kijasusi zinasema C.I.A kwa kutumia mbinu za kijasusi waliandaa exit strategy ambayo ilikuwa ni kuhamasisha maandamano na propaganda ya kile kilichoitwa vuguvugu la wananchi wa Marekani kupinga nchi yao kujiingiza katika vita ya Vietnam. Hatimaye Marekani kwa kisingizio cha maandamano ya wananchi kupinga nchi yao kujiingiza Vietnam mwaka 1973 waliondoa vikosi vyao na kuikabidhi Vietnam Kusini jukumu la kuendelea na mapambano dhidi ya Kaskazini. Vietnam ya Kaskazini iliendesha mapigano kwa miaka miwili mfululizo na hatimaye mwaka 1975 ikaukamata mji mashuhuri sana wa Saigon uliokuwa unamilikiwa na Vietnam Kusini na mwaka mmoja baadaye Kusini na Kaskazini zikaungana na kutengeneza nchi moja ya Jamhuri ya watu wa Vietnam. Inakadiriwa kuwa vita hiyo iligharimu maisha ya WaVietnam kati ya 966,000 mpaka Milioni 3.8 Wakambodia kati ya 240,000–300,000, Walaotia kati ya 20,000–62,000 na Wamarekani zaidi ya 58,220 huku Wamarekani zaidi ya 1,626 wakipotea na hawakujulikana walipo mpaka leo Mwisho
    0 Comments ·0 Shares ·1K Views
  • WATU 10 AMBAO WALIPOTEA NA HAWAJAWI ONEKANA
    #1
    Kupotea kwa mwanasiasa Ben Saanane takribani miaka miwili iliyopita pamoja na kupotea kwa mwanahabari Azory Agwanda mwaka mmoja uliopita,kuliwashtua Watanzania walio wengi na kuibua minong'ono juu ya mahali walipo watu hao. Mpaka leo hatujui walipo Ben Saanane pamoja na Azory Agwanda. Miaka ya nyuma, aliwahi kupotea mwanasiasa mahiri wa miaka hiyo hapa nchini Abdallah Kassim Hanga, ambaye mpaka leo hajulikani alipelekwa wapi licha ya kuwa mpaka kupotea kwake alikuwa kwenye mikono ya dola. Hayo ni machache.

    Leo tujionee watu maarufu ambao walipotea, hawajulikani walipo na hawakuwahi kuonekana tena hapa Duniani. Baadhi yao ni viongozi, wahalifu na watu wa kawaida tu.

    10.Jim Sullivan

    Huyu alikuwa ni mwanamuziki wa kimarekani. Mwaka 1969 alitoa albamu iliyoitwa U.F.O. Ndani ya albamu hiyo kulikuwa na vibao vyenye utata wa majina, kama vile Aliens, I"never die na vinginevyo vingi. Alitoweka mwaka 1975 na mpaka leo hajulikani ni wapi alipo.

    9.Bison Dele

    Alikuwa ni mchezaji wa mpira wakikapu katika ligi ya NBA na alichezea vilabu kadhaa vikiwemo Detroit Pistons, Chicago bulls nk. Alitoweka mwaka 2002 wakati akiwa na mchumba wake kwenye boti yao huko Tahiti katika bahari ya Pacific. Vyanzo mbalimbali vinadai kuwa Bison Dele alikuwa na kaka yake siku ya safari katika boti, pia aligombana na kaka yake hivyo walipigana wakiwa katika boti na kupelekea kuuliwa na bastola yeye pamoja na mchumba wake. Boti yao ilikuja kupatikana ikiwa haina mtu yoyote ndani yake.

    8.Frank Morris

    Huyu alikuwa ni mfungwa aliyekuwa anatumikia kifungo cha miaka 10 katika gereza la Alcatraz huko nchini Marekani. Alipelekwa katika gereza Alcatraz baada ya kutoroka gereza la Louisiana. Hivyo baada ya kukamatwa alipelekwa kwenye gereza lenye ulinzi mkali na lililopo kisiwani Alcatraz, gereza hilo limezungukwa ma maji yenye kina kirefu na eneo lenye samaki wengi aina ya papa.

    Mwanaume huyu na mapacha wawili walifanikiwa kutoroka mwaka 1962 na mpaka leo hajulikani alipo licha ya msako mkali wa FBI. Kuna wanaoamini huenda Frank aliuwawa na papa ndani ya bahari lakini hakuna aliyethibitisha. Mpaka leo jalada la kesi yake bado lipo wazi.

    7. Mapacha John and Clarence Anglin

    Hawa ni mapacha ambao kwa pamoja waliungana na Jambazi Frank Morris kutoroka katika jela yenye ulinzi mkali na iliyozungukwa na maji ya Alcatraz. Walitoroka mwaka 1962 na mpaka leo hawajwahi kuonekana tena. Inasemekana baada ya kutoroka walikimbilia nchini Brazil ambapo wamekuwa wakiishi na kwasiliana na familia zao kwa siri lakini hakuna aliyewahi kuthibitisha madai hayo. Sasa ni zaidi ya miaka 56 toka watoroke jela hawajawahi kuonekana tena na jalada lao lipo wazi bado halijafungwa.

    6.Oscar Zeta Acosta

    Alikuwa ni mwanasiasa, mwanafasihi na mwanasheria nguli kutoka nchini Marekani ambapo alikuwa ni mkosoaji mkubwa sana wa biashara ya madawa ya kulevya. Alipotea mwaka 1974 alipokuwa anaelekea Mexico. Inaaminika Acosta aliuwawa na wafanya biashara wa madawa ya kulevya na kuna wanaoamini Acosta aliuwawa kwasababu za kisiasa lakini mpaka leo hakuwahi kupatikana tena.

    5.Amelia Earhart

    Alikuwa ni rubani mahiri wa ndege huko Marekani. Pia alikuwa ni mwalimu, mwanamitindo na Mhariri wa majarida mbalimbali. Alikuwa mwanamke wa kwanza kurusha ndege peke yake na kuzunguka bahari ya Pacific.

    Alitoweka na ndege yake mwaka 1937 akiwa angani na mpaka leo hajulikani alipo. Japo kuna wanaoamini kuwa alipewa kazi ya ujasusi na utawala wa Rais wa kipindi hiko Marekani ndugu Franklin D. Roosevelt ya kwenda kuichunguza Japan. Pia wapo wanaoamini kuwa aliamua kujibadilisha kimwili na jina na kuishi maisha yake nje ya awali. Mpaka leo hajawahi kupatikana tena.

    4.Camilo Cienfuegos

    Ni mwanamapinduzi wa Cuba aliyeshiriki kikamilifu Mapinduzi ya Nchi hiyo akiwa sambamba na akina Fidel castro, Che Guevara na wengineo. Ndege aliyopanda akitokea Camaguey alikotoka kumkamata mwanamapinduzi mwenzake aliyeasi Huber Matos, ilipotea angani na haijaonekana tena mpaka leo hii. Wengi wanadai Camilo alifanyiwa faulo na wenzake hasa Fidel Castro ili kuizima nyota yake iliyokuwa inang'aa kwa kasi.

    3.Jimmy Hoffa

    Alikuwa ni kiongozi wa chama cha wafanyakazi nchini Marekani. Pia alikuwa anajihusisha na makundi ya kihalifu. Anajulikana kama kiongozi mtata, mpendwa rushwa na mwizi ambapo kuna wakati alihukumiwa kifungo cha miaka 13 jela kwa kosa la utakatishaji pesa. Aliachiwa kwa msamaha wa Rais wa kipindi hiko wa Marekani Richard Nixon.

    Mchana wa july 30 mwaka 1975 katika parking ya Mgahawa wa Red Fox, Jimmy hoffa alitoweka na hakuonekana tena mpaka leo. Haijulikani ni akina nani haswa walihusika katika kumteka, kuna wanaosema Serikali, kuna wanaosema Mafia. Licha ya msako mkali wa FBI kiongozi huyo hakuwahi kupatikana tena.

    2. Harlod Holt

    Alikuwa ni Waziri Mkuu wa 17 wa Australia mpaka kupotea kwake. Jioni ya 17 december mwaka 1967 wananchi wa Australia hawatoisahau katika kumbukumbu zao baada ya kupotea kwa Waziri Mkuu wao.

    Waziri Mkuu Holt alipotea alipokuwa anaogelea baharini huko Portsea, Victoria nchini Australia alipokuwa katika likizo ya mwisho wa mwaka.Licha ya msako mkali wa kwenye maji, mwili wa Waziri Mkuu Holt hakuwahi kuoekana tena. Minong'ono ilizuka kuwa Waziri mkuu huyo alitekwa na Submarine (nyambizi) ya China kwakuwa alikuwa ni jasusi wao lakini hakuna aliyethibitisha. Kuna wanaosema Harold Holt alifeki kifo chake ili aishi kwa uhuru mara baada ya kuchoshwa na maisha ya siasa ikiwa ni miaka miwili tu toka achaguliwe kuwa Waziri Mkuu. Mpaka leo mwili wake haukuwahi kupatikana tena.

    1.D.B Cooper

    D.B.Cooper ni jina linalotumika kumrejelea mwanaume mmoja wa makamo ambaye jioni ya November 24, mwaka 1971 alichukua kiasi cha Dola za Kimarekani 200,000 kama malipo mara baada ya kuiteka ndege huko portland nchini Marekani.

    Licha ya msako mkali wa zaidi ya miaka 45 uliofanywa na FBI kwa kushirikiana na idara nyingine za kiusalama nchini Marekani, bado D.B Cooper hafahamiki ni wapi alipo wala pesa alizopewa hazikuwahi kuingia kwenye mzunguko wala kupatikana. kuna wanaoamini kuwa D.B Cooper alitengenezwa na kusaidiwa na FBI wenyewe ili wajipatie pesa. Kuna wanaoamini Cooper alifariki mara baada ya kuruka toka kwenye ndege angani lakini mbona pesa hazijapatikana? D.B Cooper ameacha maswali mengi kuliko majibu na mpaka leo hajawahi kuonekana tena baada ya jioni ile ya mwaka 1971.

    MWISHO
    WATU 10 AMBAO WALIPOTEA NA HAWAJAWI ONEKANA #1 Kupotea kwa mwanasiasa Ben Saanane takribani miaka miwili iliyopita pamoja na kupotea kwa mwanahabari Azory Agwanda mwaka mmoja uliopita,kuliwashtua Watanzania walio wengi na kuibua minong'ono juu ya mahali walipo watu hao. Mpaka leo hatujui walipo Ben Saanane pamoja na Azory Agwanda. Miaka ya nyuma, aliwahi kupotea mwanasiasa mahiri wa miaka hiyo hapa nchini Abdallah Kassim Hanga, ambaye mpaka leo hajulikani alipelekwa wapi licha ya kuwa mpaka kupotea kwake alikuwa kwenye mikono ya dola. Hayo ni machache. Leo tujionee watu maarufu ambao walipotea, hawajulikani walipo na hawakuwahi kuonekana tena hapa Duniani. Baadhi yao ni viongozi, wahalifu na watu wa kawaida tu. 10.Jim Sullivan Huyu alikuwa ni mwanamuziki wa kimarekani. Mwaka 1969 alitoa albamu iliyoitwa U.F.O. Ndani ya albamu hiyo kulikuwa na vibao vyenye utata wa majina, kama vile Aliens, I"never die na vinginevyo vingi. Alitoweka mwaka 1975 na mpaka leo hajulikani ni wapi alipo. 9.Bison Dele Alikuwa ni mchezaji wa mpira wakikapu katika ligi ya NBA na alichezea vilabu kadhaa vikiwemo Detroit Pistons, Chicago bulls nk. Alitoweka mwaka 2002 wakati akiwa na mchumba wake kwenye boti yao huko Tahiti katika bahari ya Pacific. Vyanzo mbalimbali vinadai kuwa Bison Dele alikuwa na kaka yake siku ya safari katika boti, pia aligombana na kaka yake hivyo walipigana wakiwa katika boti na kupelekea kuuliwa na bastola yeye pamoja na mchumba wake. Boti yao ilikuja kupatikana ikiwa haina mtu yoyote ndani yake. 8.Frank Morris Huyu alikuwa ni mfungwa aliyekuwa anatumikia kifungo cha miaka 10 katika gereza la Alcatraz huko nchini Marekani. Alipelekwa katika gereza Alcatraz baada ya kutoroka gereza la Louisiana. Hivyo baada ya kukamatwa alipelekwa kwenye gereza lenye ulinzi mkali na lililopo kisiwani Alcatraz, gereza hilo limezungukwa ma maji yenye kina kirefu na eneo lenye samaki wengi aina ya papa. Mwanaume huyu na mapacha wawili walifanikiwa kutoroka mwaka 1962 na mpaka leo hajulikani alipo licha ya msako mkali wa FBI. Kuna wanaoamini huenda Frank aliuwawa na papa ndani ya bahari lakini hakuna aliyethibitisha. Mpaka leo jalada la kesi yake bado lipo wazi. 7. Mapacha John and Clarence Anglin Hawa ni mapacha ambao kwa pamoja waliungana na Jambazi Frank Morris kutoroka katika jela yenye ulinzi mkali na iliyozungukwa na maji ya Alcatraz. Walitoroka mwaka 1962 na mpaka leo hawajwahi kuonekana tena. Inasemekana baada ya kutoroka walikimbilia nchini Brazil ambapo wamekuwa wakiishi na kwasiliana na familia zao kwa siri lakini hakuna aliyewahi kuthibitisha madai hayo. Sasa ni zaidi ya miaka 56 toka watoroke jela hawajawahi kuonekana tena na jalada lao lipo wazi bado halijafungwa. 6.Oscar Zeta Acosta Alikuwa ni mwanasiasa, mwanafasihi na mwanasheria nguli kutoka nchini Marekani ambapo alikuwa ni mkosoaji mkubwa sana wa biashara ya madawa ya kulevya. Alipotea mwaka 1974 alipokuwa anaelekea Mexico. Inaaminika Acosta aliuwawa na wafanya biashara wa madawa ya kulevya na kuna wanaoamini Acosta aliuwawa kwasababu za kisiasa lakini mpaka leo hakuwahi kupatikana tena. 5.Amelia Earhart Alikuwa ni rubani mahiri wa ndege huko Marekani. Pia alikuwa ni mwalimu, mwanamitindo na Mhariri wa majarida mbalimbali. Alikuwa mwanamke wa kwanza kurusha ndege peke yake na kuzunguka bahari ya Pacific. Alitoweka na ndege yake mwaka 1937 akiwa angani na mpaka leo hajulikani alipo. Japo kuna wanaoamini kuwa alipewa kazi ya ujasusi na utawala wa Rais wa kipindi hiko Marekani ndugu Franklin D. Roosevelt ya kwenda kuichunguza Japan. Pia wapo wanaoamini kuwa aliamua kujibadilisha kimwili na jina na kuishi maisha yake nje ya awali. Mpaka leo hajawahi kupatikana tena. 4.Camilo Cienfuegos Ni mwanamapinduzi wa Cuba aliyeshiriki kikamilifu Mapinduzi ya Nchi hiyo akiwa sambamba na akina Fidel castro, Che Guevara na wengineo. Ndege aliyopanda akitokea Camaguey alikotoka kumkamata mwanamapinduzi mwenzake aliyeasi Huber Matos, ilipotea angani na haijaonekana tena mpaka leo hii. Wengi wanadai Camilo alifanyiwa faulo na wenzake hasa Fidel Castro ili kuizima nyota yake iliyokuwa inang'aa kwa kasi. 3.Jimmy Hoffa Alikuwa ni kiongozi wa chama cha wafanyakazi nchini Marekani. Pia alikuwa anajihusisha na makundi ya kihalifu. Anajulikana kama kiongozi mtata, mpendwa rushwa na mwizi ambapo kuna wakati alihukumiwa kifungo cha miaka 13 jela kwa kosa la utakatishaji pesa. Aliachiwa kwa msamaha wa Rais wa kipindi hiko wa Marekani Richard Nixon. Mchana wa july 30 mwaka 1975 katika parking ya Mgahawa wa Red Fox, Jimmy hoffa alitoweka na hakuonekana tena mpaka leo. Haijulikani ni akina nani haswa walihusika katika kumteka, kuna wanaosema Serikali, kuna wanaosema Mafia. Licha ya msako mkali wa FBI kiongozi huyo hakuwahi kupatikana tena. 2. Harlod Holt Alikuwa ni Waziri Mkuu wa 17 wa Australia mpaka kupotea kwake. Jioni ya 17 december mwaka 1967 wananchi wa Australia hawatoisahau katika kumbukumbu zao baada ya kupotea kwa Waziri Mkuu wao. Waziri Mkuu Holt alipotea alipokuwa anaogelea baharini huko Portsea, Victoria nchini Australia alipokuwa katika likizo ya mwisho wa mwaka.Licha ya msako mkali wa kwenye maji, mwili wa Waziri Mkuu Holt hakuwahi kuoekana tena. Minong'ono ilizuka kuwa Waziri mkuu huyo alitekwa na Submarine (nyambizi) ya China kwakuwa alikuwa ni jasusi wao lakini hakuna aliyethibitisha. Kuna wanaosema Harold Holt alifeki kifo chake ili aishi kwa uhuru mara baada ya kuchoshwa na maisha ya siasa ikiwa ni miaka miwili tu toka achaguliwe kuwa Waziri Mkuu. Mpaka leo mwili wake haukuwahi kupatikana tena. 1.D.B Cooper D.B.Cooper ni jina linalotumika kumrejelea mwanaume mmoja wa makamo ambaye jioni ya November 24, mwaka 1971 alichukua kiasi cha Dola za Kimarekani 200,000 kama malipo mara baada ya kuiteka ndege huko portland nchini Marekani. Licha ya msako mkali wa zaidi ya miaka 45 uliofanywa na FBI kwa kushirikiana na idara nyingine za kiusalama nchini Marekani, bado D.B Cooper hafahamiki ni wapi alipo wala pesa alizopewa hazikuwahi kuingia kwenye mzunguko wala kupatikana. kuna wanaoamini kuwa D.B Cooper alitengenezwa na kusaidiwa na FBI wenyewe ili wajipatie pesa. Kuna wanaoamini Cooper alifariki mara baada ya kuruka toka kwenye ndege angani lakini mbona pesa hazijapatikana? D.B Cooper ameacha maswali mengi kuliko majibu na mpaka leo hajawahi kuonekana tena baada ya jioni ile ya mwaka 1971. MWISHO
    Like
    2
    · 0 Comments ·0 Shares ·1K Views
  • Wanaitwa ‘MANTIS SHRIMP’ mwenye pigo sawa na nguvu ya bunduki

    ❇Hawa ni moja kati ya viumbe hatari sana wanaopatikana baharini hasa bahari ya Hindi hapa Tanzania Kitalaam anaitwa “Stamatopoda”
    .
    ❇wana urefu wa cm 20 sawa na inchi 8 na uzitowao ni Gram 90 – 100 lakini mambo yao ni konki
    .Kwa umbo wanamagamba mazuri yenye kuvutia lakini ni moja ya viumbe hatari sana baharini
    .
    ❇wanauwezo wa kupiga sehemu na kuvunja na nguvu yake ni sawa na risasi wanauwezo wa kupasua vile vioo vya mabwawa ya kuhifadhia samaki (aquarims) kwa Single Hit)
    .
    ❇Mantis huwa hawachangani, ni wakali sana hasa kwenye mipaka yao yaani ukiingia bahati mbaya kwenye anga zao umeyatimba
    .
    ❇Huwa wanatoa sauti za chini sana ambazo huwasiliana kama ikitokea wakakutana na nadra sana kuona wanapigana
    .
    ❇Macho yao yako kwa juu kama antena na yana uwezo mkubwa wa kuona na kujua direction ya predators au prey
    .pia yana uwezo wa kwenda direction tofauti tofauti yaani moja kaskazini na moja kusini, Vile vile wanakucha ambazo hutumia kumkamata prey anapokua karibu
    .
    ❇Chakula chao kikuu ni ngadu, Samaki na baadhi ya viumbe vingine na wanakula samaki ambao huwa wakubwa kuliko hata umbo lao
    .
    ❇Huwa wanatumia mechanism tofauti sana pale wanapotaka kutafuta chakula wanauwezo wa kupiga maji yakatengeneza mawimbi makubwa tu kukelekea direction ya prey na kabla ya prey hajafanya maamuzi anapigwa round kick kali sana..
    .
    ❇Wanauwezo wa kugundua Mgonjwa wa cancer kwa macho yao na hii ni kwasabu macho yanauwezo mkubwa sana wakuona na kugundua movement nampangilio wa neurons (Hii ni kwa mujibu wa Chuo Kikuu cha Queensland)
    .
    ❇Kwa kawaida huwa na life partner yaani bebi mmoja tu kwenye maisha yao na muda wa kutaga jike na dume hulalia pamoja mayai mpaka muda wa kupata watoto
    .
    ❇Adui yao mkubwa ni binadamu maana nchi kama Japan na China huwa wanawala sana na wakati mwingine huwa wanaaminishwa na imani fulani kama moja ya viumbe vyenye kuongeza sana nguvu ya mwili kwa kuimarisha seli hai nyeupe (white blood cells).
    Wanaitwa ‘MANTIS SHRIMP’ mwenye pigo sawa na nguvu ya bunduki ❇Hawa ni moja kati ya viumbe hatari sana wanaopatikana baharini hasa bahari ya Hindi hapa Tanzania Kitalaam anaitwa “Stamatopoda” . ❇wana urefu wa cm 20 sawa na inchi 8 na uzitowao ni Gram 90 – 100 lakini mambo yao ni konki .Kwa umbo wanamagamba mazuri yenye kuvutia lakini ni moja ya viumbe hatari sana baharini . ❇wanauwezo wa kupiga sehemu na kuvunja na nguvu yake ni sawa na risasi wanauwezo wa kupasua vile vioo vya mabwawa ya kuhifadhia samaki (aquarims) kwa Single Hit) . ❇Mantis huwa hawachangani, ni wakali sana hasa kwenye mipaka yao yaani ukiingia bahati mbaya kwenye anga zao umeyatimba . ❇Huwa wanatoa sauti za chini sana ambazo huwasiliana kama ikitokea wakakutana na nadra sana kuona wanapigana . ❇Macho yao yako kwa juu kama antena na yana uwezo mkubwa wa kuona na kujua direction ya predators au prey .pia yana uwezo wa kwenda direction tofauti tofauti yaani moja kaskazini na moja kusini, Vile vile wanakucha ambazo hutumia kumkamata prey anapokua karibu . ❇Chakula chao kikuu ni ngadu, Samaki na baadhi ya viumbe vingine na wanakula samaki ambao huwa wakubwa kuliko hata umbo lao . ❇Huwa wanatumia mechanism tofauti sana pale wanapotaka kutafuta chakula wanauwezo wa kupiga maji yakatengeneza mawimbi makubwa tu kukelekea direction ya prey na kabla ya prey hajafanya maamuzi anapigwa round kick kali sana.. 😀 . ❇Wanauwezo wa kugundua Mgonjwa wa cancer kwa macho yao na hii ni kwasabu macho yanauwezo mkubwa sana wakuona na kugundua movement nampangilio wa neurons (Hii ni kwa mujibu wa Chuo Kikuu cha Queensland) . ❇Kwa kawaida huwa na life partner yaani bebi mmoja tu kwenye maisha yao na muda wa kutaga jike na dume hulalia pamoja mayai mpaka muda wa kupata watoto . ❇Adui yao mkubwa ni binadamu maana nchi kama Japan na China huwa wanawala sana na wakati mwingine huwa wanaaminishwa na imani fulani kama moja ya viumbe vyenye kuongeza sana nguvu ya mwili kwa kuimarisha seli hai nyeupe (white blood cells).
    0 Comments ·0 Shares ·489 Views
More Results