• (E)
    Kwa miaka mingi, Shipman aliendelea na mauaji yake bila kugundulika.

    Lakini mnamo 1998, alifanya kosa moja kubwa—alijaribu kughushi wosia wa mgonjwa wake mmoja, Kathleen Grundy.

    Kathleen alikuwa mama mwenye afya njema mwenye umri wa miaka 81. Alipoaga dunia ghafla, binti yake, Angela Woodruff, alishangazwa na jinsi kifo hicho kilivyotokea bila onyo.

    Lakini mshangao mkubwa zaidi ulikuja alipogundua kuwa mama yake alikuwa ameandika wosia mpya, ukisema kuwa mali yake yote iende kwa daktari wake—Harold Shipman!

    Huo ulikuwa ushahidi wa kwanza wa kweli kwamba huyu hakuwa daktari wa kawaida—alikuwa muuaji.
    (E) Kwa miaka mingi, Shipman aliendelea na mauaji yake bila kugundulika. Lakini mnamo 1998, alifanya kosa moja kubwa—alijaribu kughushi wosia wa mgonjwa wake mmoja, Kathleen Grundy. Kathleen alikuwa mama mwenye afya njema mwenye umri wa miaka 81. Alipoaga dunia ghafla, binti yake, Angela Woodruff, alishangazwa na jinsi kifo hicho kilivyotokea bila onyo. Lakini mshangao mkubwa zaidi ulikuja alipogundua kuwa mama yake alikuwa ameandika wosia mpya, ukisema kuwa mali yake yote iende kwa daktari wake—Harold Shipman! Huo ulikuwa ushahidi wa kwanza wa kweli kwamba huyu hakuwa daktari wa kawaida—alikuwa muuaji.
    Like
    1
    · 0 Comments ·0 Shares ·77 Views
  • Ndani ya masaa machache, zaidi ya waokoaji 100 walikusanyika nje ya pango kujaribu kumuokoa John.

    Walileta vifaa maalum, kamba, na vifaa vya kuchimba.

    Walijaribu kumnyoosha polepole, lakini mwili wake ulikuwa umejibana vibaya kupita kiasi.

    Kila walivyojaribu kumvuta, John alilia kwa maumivu makali.

    Baada ya masaa 19, walifanikiwa kumvuta kidogo, lakini ghafla, kamba ilikatika, na aliteleza tena chini zaidi ya alivyokuwa awali.

    Sasa alikuwa amekwama vibaya zaidi, na matumaini ya kumuokoa yalizidi kupungua.
    Ndani ya masaa machache, zaidi ya waokoaji 100 walikusanyika nje ya pango kujaribu kumuokoa John. Walileta vifaa maalum, kamba, na vifaa vya kuchimba. Walijaribu kumnyoosha polepole, lakini mwili wake ulikuwa umejibana vibaya kupita kiasi. Kila walivyojaribu kumvuta, John alilia kwa maumivu makali. Baada ya masaa 19, walifanikiwa kumvuta kidogo, lakini ghafla, kamba ilikatika, na aliteleza tena chini zaidi ya alivyokuwa awali. Sasa alikuwa amekwama vibaya zaidi, na matumaini ya kumuokoa yalizidi kupungua.
    Sad
    1
    · 0 Comments ·0 Shares ·94 Views
  • John Jones aliamua kujaribu njia ndogo iliyoitwa "Birth Canal", sehemu ya pango iliyojaa mashimo madogo na njia nyembamba sana.

    Alijaribu kupita kwenye sehemu nyembamba, akiamini anaweza kujibana kupitia.

    Ghafla, miguu yake iliteleza, na aliteleza chini kichwa kwanza.

    Aliingia katika shimo dogo lenye upana wa cm 25 tu na urefu wa cm 45.

    Alikwama vibaya, bila nafasi ya kujigeuza.

    John alipata hofu kubwa. Alijaribu kusukuma mwili wake nyuma, lakini hakuweza—shimo lilikuwa dogo sana!

    Baada ya dakika chache za kupambana, alitambua kuwa amekwama kabisa, na pango limeziba mwili wake kwa pande zote.
    John Jones aliamua kujaribu njia ndogo iliyoitwa "Birth Canal", sehemu ya pango iliyojaa mashimo madogo na njia nyembamba sana. Alijaribu kupita kwenye sehemu nyembamba, akiamini anaweza kujibana kupitia. Ghafla, miguu yake iliteleza, na aliteleza chini kichwa kwanza. Aliingia katika shimo dogo lenye upana wa cm 25 tu na urefu wa cm 45. Alikwama vibaya, bila nafasi ya kujigeuza. John alipata hofu kubwa. Alijaribu kusukuma mwili wake nyuma, lakini hakuweza—shimo lilikuwa dogo sana! Baada ya dakika chache za kupambana, alitambua kuwa amekwama kabisa, na pango limeziba mwili wake kwa pande zote.
    Love
    1
    · 0 Comments ·0 Shares ·51 Views
  • #PART5

    Baada ya M23 kukamata Goma walidai hawana mpango wa kuchukua miji mingine. Jeshi la Congo (FARDC) likarelax. Kumbe ilikua mbinu ya kivita. Ghafla M23 wakavamia na kuuteka mji wa Rutshuru wenye utajiri wa dhahabu, tin na Tungsten na mji wa Masisi wenye utajiri mkubwa wa dhahabu na cassiterite.

    Mpango wa M23 ni kufika Kinshasa na kuuangusha utawala wa Rais Felix Tshisekedi. Madai ya M23 ni yaleyale ya siku zote, ambayo ni kulinda maslahi ya Watutsi waishio mashariki mwa nchi hiyo, kupambana na wanamgambo wa Kihutu wa FDLR (Interahamwe), na kutaka Banyamulenge watambuliwe kama raia halali wa Congo.

    Mzozo wa mashariki mwa Congo umegharimu maisha ya mamilioni ya watu toka ulipoanza. Umoja wa Mataifa (UN) na Umoja wa Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) umepeleka askari wa kulinda amani. Ikumbukwe askari hao hawapigani upande wa serikali wala wa waasi. Kuna watu wanadhani askari wetu wa JWTZ walioko Congo wanapigana upande wa jeshi la serikali (FARDC). Hapana. Hawapigani upande wowote. Wanalinda amani. Lakini ikitokea kuna upande unahatarisha amani utapewa haki yake ya kikatiba.

    Kwa mfano, mwaka 2012 Umoja wa mataifa uliunda jeshi la kulinda amani Congo (MONUSCO). Ndani yake kulikua na brigedi maalumu ya kunyang'anya silaha makundi ya wapiganaji - Force Intervention Bregade (FIB). Brigedi hiyo iliundwa na askari kutoka Tanzania, Malawi, Afrika Kusini na Uruguay.

    April 2012, M23 wakashambulia kambi ya FIB iliyokua mji wa Rutshuru na kuua askari watatu. Baada ya shambulio hilo, aliyekua Mkuu FIB, Jenerali James Mwakibolwa alipanga vikosi vyake kujibu mapigo. M23 walichakazwa vibaya ambapo zaidi ya askari 600 wa M23 waliuawa na wengi kujeruhiwa. Walipigwa bila huruma na kuachia miji yote waliyokua wameishikilia ikiwemo Rubaya, Kitchanga na Rutshuru. Askari 16 wa FIB nao walipoteza maisha.

    March 2013, M23 walisalimu amri na Kiongozi wao Bosco Ntaganda akakimbilia Rwanda kujisalimisha kwenye ubalozi wa Marekani. Alipelekwa ICC akahukumiwa miaka 30 na sasa anatumikia adhabu yake gereza la Leuze-en-Hainaut lililopo Ubelgiji. Moja ya makosa ambayo Ntaganda anayajutia hadi leo ni kuingia kwenye 18 za FIB iliyokua inaongozwa na Jenerali James Aloizi Mwakibolwa.

    Kumekua na jitihada mbalimbali za kumaliza mgogoro wa DRC kwa njia za kidiplomasia ikiwemo mkutano wa viongozi wakuu wa SADC na EAC uliofanyika leo jijini Dar.

    #MyaTake:
    1. Congo imeponzwa na ukarimu wake. Wakati wa vita vya Rwanda, Congo ilipokea Watutsi wengi na kuwapa hifadhi, akiwemo Kagame. Baada ya utawala wa Habyarimana kuangushwa Wahutu nao wakakimbilia Congo na kupewa hifadhi. Sasa hicho kimekua kigezo cha Rwanda kuingiza majeshi Congo kila mara kwa madai ya kuwatafuta Wahutu wa FDLR. Kwa lugha rahisi vita ya ndugu wawili (Wahutu na Watutsi) iliyopaswa kupiganwa Rwanda sasa inapiganwa Congo.

    2. Congo inateswa na mipaka ya kikoloni. Laiti wakati wa kuchora mipaka jamii yote ya Watutsi ingewekwa Rwanda, leo kusingekuwa na Banyamulenge Congo, kwahiyo Watutsi wasingepata sababu ya kuishi Congo na kujifanya raia. Ni sawa na kukuta Wamasai 1,000 pale Longido, halafu uambiwe kati yao wapo wa Kenya. Utawajuaje? Utawatofautishaje?

    3. Congo inateswa na rasilimali zake. Kama eneo la Kivu lisingekuwa na utajiri, mgogoro usingekuwa mkubwa kama ulivyo. Rejea #Part1 kujua utajiri uliopo Kivu. Kumbuka bila Kivu dunia haina laptop wala smartphones kwa sababu 80% ya coltan yote duniani inatoka Kivu.

    4. Rwanda na Uganda ni Keyplayers kwenye mgogoro wa Congo. Kwa miaka mingi majeshi yao yameigeuza Congo shamba la bibi. Waondoe majeshi yao Congo.

    5. Viongozi wengi wa M23 ni Wanyarwanda. Huu ni udhibitisho kuwa Rwanda ni kinara kwenye mgogoro huu.

    6. Congo ni kubwa sana na hivyo inakosa jeshi imara la kutosha kulinda mipaka yake yote. Congo ni kubwa mara 90 ya Rwanda. Wapo wanaoshauri igawanywe kama njia ya kutatua mgogoro. Kama ambavyo Yugoslavia iligawanywa na kumaliza vita vya wenyewe kwa wenyewe.

    7. Kiongozi wa sasa wa M23 Corneille Nangaa alikua Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi 2019 na ndiye aliyemtangaza Tshisekedi kuwa Rais kwa ushindi wa 38%. Lakini alilaumiwa kupunguza kura za Martin Fayulu aliyepata 34%. Huenda kuna ahadi alipewa haikutimizwa ndio maana akaungana na Waasi.

    Sababu hizo hapo juu zikifanyiwa kazi, mgogoro wa Congo unaweza kupungua kwa kiasi kikubwa. Mnaopenda kujifunza zaidi, naandika Kitabu. Get ready to have your copy. MWISHO.!

    (Malisa GJ )

    #PART5 Baada ya M23 kukamata Goma walidai hawana mpango wa kuchukua miji mingine. Jeshi la Congo (FARDC) likarelax. Kumbe ilikua mbinu ya kivita. Ghafla M23 wakavamia na kuuteka mji wa Rutshuru wenye utajiri wa dhahabu, tin na Tungsten na mji wa Masisi wenye utajiri mkubwa wa dhahabu na cassiterite. Mpango wa M23 ni kufika Kinshasa na kuuangusha utawala wa Rais Felix Tshisekedi. Madai ya M23 ni yaleyale ya siku zote, ambayo ni kulinda maslahi ya Watutsi waishio mashariki mwa nchi hiyo, kupambana na wanamgambo wa Kihutu wa FDLR (Interahamwe), na kutaka Banyamulenge watambuliwe kama raia halali wa Congo. Mzozo wa mashariki mwa Congo umegharimu maisha ya mamilioni ya watu toka ulipoanza. Umoja wa Mataifa (UN) na Umoja wa Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) umepeleka askari wa kulinda amani. Ikumbukwe askari hao hawapigani upande wa serikali wala wa waasi. Kuna watu wanadhani askari wetu wa JWTZ walioko Congo wanapigana upande wa jeshi la serikali (FARDC). Hapana. Hawapigani upande wowote. Wanalinda amani. Lakini ikitokea kuna upande unahatarisha amani utapewa haki yake ya kikatiba. Kwa mfano, mwaka 2012 Umoja wa mataifa uliunda jeshi la kulinda amani Congo (MONUSCO). Ndani yake kulikua na brigedi maalumu ya kunyang'anya silaha makundi ya wapiganaji - Force Intervention Bregade (FIB). Brigedi hiyo iliundwa na askari kutoka Tanzania, Malawi, Afrika Kusini na Uruguay. April 2012, M23 wakashambulia kambi ya FIB iliyokua mji wa Rutshuru na kuua askari watatu. Baada ya shambulio hilo, aliyekua Mkuu FIB, Jenerali James Mwakibolwa alipanga vikosi vyake kujibu mapigo. M23 walichakazwa vibaya ambapo zaidi ya askari 600 wa M23 waliuawa na wengi kujeruhiwa. Walipigwa bila huruma na kuachia miji yote waliyokua wameishikilia ikiwemo Rubaya, Kitchanga na Rutshuru. Askari 16 wa FIB nao walipoteza maisha. March 2013, M23 walisalimu amri na Kiongozi wao Bosco Ntaganda akakimbilia Rwanda kujisalimisha kwenye ubalozi wa Marekani. Alipelekwa ICC akahukumiwa miaka 30 na sasa anatumikia adhabu yake gereza la Leuze-en-Hainaut lililopo Ubelgiji. Moja ya makosa ambayo Ntaganda anayajutia hadi leo ni kuingia kwenye 18 za FIB iliyokua inaongozwa na Jenerali James Aloizi Mwakibolwa. Kumekua na jitihada mbalimbali za kumaliza mgogoro wa DRC kwa njia za kidiplomasia ikiwemo mkutano wa viongozi wakuu wa SADC na EAC uliofanyika leo jijini Dar. #MyaTake: 1. Congo imeponzwa na ukarimu wake. Wakati wa vita vya Rwanda, Congo ilipokea Watutsi wengi na kuwapa hifadhi, akiwemo Kagame. Baada ya utawala wa Habyarimana kuangushwa Wahutu nao wakakimbilia Congo na kupewa hifadhi. Sasa hicho kimekua kigezo cha Rwanda kuingiza majeshi Congo kila mara kwa madai ya kuwatafuta Wahutu wa FDLR. Kwa lugha rahisi vita ya ndugu wawili (Wahutu na Watutsi) iliyopaswa kupiganwa Rwanda sasa inapiganwa Congo. 2. Congo inateswa na mipaka ya kikoloni. Laiti wakati wa kuchora mipaka jamii yote ya Watutsi ingewekwa Rwanda, leo kusingekuwa na Banyamulenge Congo, kwahiyo Watutsi wasingepata sababu ya kuishi Congo na kujifanya raia. Ni sawa na kukuta Wamasai 1,000 pale Longido, halafu uambiwe kati yao wapo wa Kenya. Utawajuaje? Utawatofautishaje? 3. Congo inateswa na rasilimali zake. Kama eneo la Kivu lisingekuwa na utajiri, mgogoro usingekuwa mkubwa kama ulivyo. Rejea #Part1 kujua utajiri uliopo Kivu. Kumbuka bila Kivu dunia haina laptop wala smartphones kwa sababu 80% ya coltan yote duniani inatoka Kivu. 4. Rwanda na Uganda ni Keyplayers kwenye mgogoro wa Congo. Kwa miaka mingi majeshi yao yameigeuza Congo shamba la bibi. Waondoe majeshi yao Congo. 5. Viongozi wengi wa M23 ni Wanyarwanda. Huu ni udhibitisho kuwa Rwanda ni kinara kwenye mgogoro huu. 6. Congo ni kubwa sana na hivyo inakosa jeshi imara la kutosha kulinda mipaka yake yote. Congo ni kubwa mara 90 ya Rwanda. Wapo wanaoshauri igawanywe kama njia ya kutatua mgogoro. Kama ambavyo Yugoslavia iligawanywa na kumaliza vita vya wenyewe kwa wenyewe. 7. Kiongozi wa sasa wa M23 Corneille Nangaa alikua Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi 2019 na ndiye aliyemtangaza Tshisekedi kuwa Rais kwa ushindi wa 38%. Lakini alilaumiwa kupunguza kura za Martin Fayulu aliyepata 34%. Huenda kuna ahadi alipewa haikutimizwa ndio maana akaungana na Waasi. Sababu hizo hapo juu zikifanyiwa kazi, mgogoro wa Congo unaweza kupungua kwa kiasi kikubwa. Mnaopenda kujifunza zaidi, naandika Kitabu. Get ready to have your copy. MWISHO.! (Malisa GJ ✍️)
    Like
    1
    · 0 Comments ·0 Shares ·707 Views
  • #PART12

    Baada ya M23 kukamata Goma walidai hawana mpango wa kuchukua miji mingine. Jeshi la Congo (FARDC) likarelax. Kumbe ilikua mbinu ya kivita. Ghafla M23 wakavamia na kuuteka mji wa Rutshuru wenye utajiri wa dhahabu, tin na Tungsten na mji wa Masisi wenye utajiri mkubwa wa dhahabu na cassiterite.

    Mpango wa M23 ni kufika Kinshasa na kuuangusha utawala wa Rais Felix Tshisekedi. Madai ya M23 ni yaleyale ya siku zote, ambayo ni kulinda maslahi ya Watutsi waishio mashariki mwa nchi hiyo, kupambana na wanamgambo wa Kihutu wa FDLR (Interahamwe), na kutaka Banyamulenge watambuliwe kama raia halali wa Congo.

    Mzozo wa mashariki mwa Congo umegharimu maisha ya mamilioni ya watu toka ulipoanza. Umoja wa Mataifa (UN) na Umoja wa Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) umepeleka askari wa kulinda amani. Ikumbukwe askari hao hawapigani upande wa serikali wala wa waasi. Kuna watu wanadhani askari wetu wa JWTZ walioko Congo wanapigana upande wa jeshi la serikali (FARDC). Hapana. Hawapigani upande wowote. Wanalinda amani. Lakini ikitokea kuna upande unahatarisha amani utapewa haki yake ya kikatiba.

    Kwa mfano, mwaka 2012 Umoja wa mataifa uliunda jeshi la kulinda amani Congo (MONUSCO). Ndani yake kulikua na brigedi maalumu ya kunyang'anya silaha makundi ya wapiganaji - Force Intervention Bregade (FIB). Brigedi hiyo iliundwa na askari kutoka Tanzania, Malawi, Afrika Kusini na Uruguay.

    April 2012, M23 wakashambulia kambi ya FIB iliyokua mji wa Rutshuru na kuua askari watatu. Baada ya shambulio hilo, aliyekua Mkuu FIB, Jenerali James Mwakibolwa alipanga vikosi vyake kujibu mapigo. M23 walichakazwa vibaya ambapo zaidi ya askari 600 wa M23 waliuawa na wengi kujeruhiwa. Walipigwa bila huruma na kuachia miji yote waliyokua wameishikilia ikiwemo Rubaya, Kitchanga na Rutshuru. Askari 16 wa FIB nao walipoteza maisha.

    March 2013, M23 walisalimu amri na Kiongozi wao Bosco Ntaganda akakimbilia Rwanda kujisalimisha kwenye ubalozi wa Marekani. Alipelekwa ICC akahukumiwa miaka 30 na sasa anatumikia adhabu yake gereza la Leuze-en-Hainaut lililopo Ubelgiji. Moja ya makosa ambayo Ntaganda anayajutia hadi leo ni kuingia kwenye 18 za FIB iliyokua inaongozwa na Jenerali James Aloizi Mwakibolwa.!
    (Malisa GJ)

    #PART12 Baada ya M23 kukamata Goma walidai hawana mpango wa kuchukua miji mingine. Jeshi la Congo (FARDC) likarelax. Kumbe ilikua mbinu ya kivita. Ghafla M23 wakavamia na kuuteka mji wa Rutshuru wenye utajiri wa dhahabu, tin na Tungsten na mji wa Masisi wenye utajiri mkubwa wa dhahabu na cassiterite. Mpango wa M23 ni kufika Kinshasa na kuuangusha utawala wa Rais Felix Tshisekedi. Madai ya M23 ni yaleyale ya siku zote, ambayo ni kulinda maslahi ya Watutsi waishio mashariki mwa nchi hiyo, kupambana na wanamgambo wa Kihutu wa FDLR (Interahamwe), na kutaka Banyamulenge watambuliwe kama raia halali wa Congo. Mzozo wa mashariki mwa Congo umegharimu maisha ya mamilioni ya watu toka ulipoanza. Umoja wa Mataifa (UN) na Umoja wa Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) umepeleka askari wa kulinda amani. Ikumbukwe askari hao hawapigani upande wa serikali wala wa waasi. Kuna watu wanadhani askari wetu wa JWTZ walioko Congo wanapigana upande wa jeshi la serikali (FARDC). Hapana. Hawapigani upande wowote. Wanalinda amani. Lakini ikitokea kuna upande unahatarisha amani utapewa haki yake ya kikatiba. Kwa mfano, mwaka 2012 Umoja wa mataifa uliunda jeshi la kulinda amani Congo (MONUSCO). Ndani yake kulikua na brigedi maalumu ya kunyang'anya silaha makundi ya wapiganaji - Force Intervention Bregade (FIB). Brigedi hiyo iliundwa na askari kutoka Tanzania, Malawi, Afrika Kusini na Uruguay. April 2012, M23 wakashambulia kambi ya FIB iliyokua mji wa Rutshuru na kuua askari watatu. Baada ya shambulio hilo, aliyekua Mkuu FIB, Jenerali James Mwakibolwa alipanga vikosi vyake kujibu mapigo. M23 walichakazwa vibaya ambapo zaidi ya askari 600 wa M23 waliuawa na wengi kujeruhiwa. Walipigwa bila huruma na kuachia miji yote waliyokua wameishikilia ikiwemo Rubaya, Kitchanga na Rutshuru. Askari 16 wa FIB nao walipoteza maisha. March 2013, M23 walisalimu amri na Kiongozi wao Bosco Ntaganda akakimbilia Rwanda kujisalimisha kwenye ubalozi wa Marekani. Alipelekwa ICC akahukumiwa miaka 30 na sasa anatumikia adhabu yake gereza la Leuze-en-Hainaut lililopo Ubelgiji. Moja ya makosa ambayo Ntaganda anayajutia hadi leo ni kuingia kwenye 18 za FIB iliyokua inaongozwa na Jenerali James Aloizi Mwakibolwa.! (Malisa GJ)
    0 Comments ·0 Shares ·598 Views
  • Muda ukasonga. Dunia ikabadilika. Mataifa yakaanza kuweka mbele maslahi yao, na Ukraine akajikuta akilia peke yake kwenye uwanja wa vita.

    Aliyeahidi kumlinda Urusi ndiye huyo anayemshambulia kwa mabomu, vifaru na ndege za kivita.

    Kwa miaka mingi, Vladimir Putin alikuwa anaangalia ramani ya dunia akijiuliza, "Mbona Crimea na Donbas zipo nje ya milki yangu?"

    Halafu, ghafla mwaka 2014, Urusi ikaamua kumng'ata Ukraine kwa mara ya kwanza.

    Crimea ikachukuliwa, na dunia ikakaa kimya. Hakukuwa na hatua kubwa zilizochukuliwa na Marekani wala Uingereza. Ukraine akaanza kuona dalili za usaliti.

    Mwaka 2022, Urusi ikarudi tena, safari hii kwa nguvu kubwa zaidi.
    Tishio la silaha za nyuklia lililomfanya Ukraine kuwa mbabe, halikuwepo tena. Hakuwa na kinga tena, alikuwa mtu mwepesi wa kushambuliwa.

    Na hapa ndipo Ukraine alipogundua kosa lake kubwa aliamini makaratasi kuliko mabavu.
    Muda ukasonga. Dunia ikabadilika. Mataifa yakaanza kuweka mbele maslahi yao, na Ukraine akajikuta akilia peke yake kwenye uwanja wa vita. Aliyeahidi kumlinda Urusi ndiye huyo anayemshambulia kwa mabomu, vifaru na ndege za kivita. Kwa miaka mingi, Vladimir Putin alikuwa anaangalia ramani ya dunia akijiuliza, "Mbona Crimea na Donbas zipo nje ya milki yangu?" Halafu, ghafla mwaka 2014, Urusi ikaamua kumng'ata Ukraine kwa mara ya kwanza. Crimea ikachukuliwa, na dunia ikakaa kimya. Hakukuwa na hatua kubwa zilizochukuliwa na Marekani wala Uingereza. Ukraine akaanza kuona dalili za usaliti. Mwaka 2022, Urusi ikarudi tena, safari hii kwa nguvu kubwa zaidi. Tishio la silaha za nyuklia lililomfanya Ukraine kuwa mbabe, halikuwepo tena. Hakuwa na kinga tena, alikuwa mtu mwepesi wa kushambuliwa. Na hapa ndipo Ukraine alipogundua kosa lake kubwa aliamini makaratasi kuliko mabavu.
    Like
    1
    · 0 Comments ·0 Shares ·382 Views
  • Uamuzi huo ulizua sintofahamu kubwa, kwani upinzani ulidai kuwa matokeo hayo yalikuwa na mizengwe.

    Wapo waliodai kuwa Nangaa alihusika moja kwa moja kuhakikisha Tshisekedi anashinda ili kumaliza utawala wa muda mrefu wa Joseph Kabila.

    Lakini wakati watu walidhani kuwa jukumu lake katika siasa za Congo limeishia hapo, mambo yalibadilika ghafla.

    Badala ya kustaafu kwenye siasa, Corneille Nangaa aliibuka na Action for Change (AFC), chama kipya cha kisiasa ambacho kilionekana kuja na ajenda tofauti.

    Alianza kujenga ushawishi mkubwa ndani na nje ya Congo, huku akijitokeza kama mpinzani wa utawala wa Tshisekedi aliyechangia kumuweka madarakani.

    Lakini hatua iliyotikisa Congo ni pale ilipogundulika kuwa Nangaa sasa alikuwa na uhusiano wa karibu na kundi la waasi la M23, ambalo linajulikana kwa mapigano yake dhidi ya serikali ya Congo.

    Kwa muda mrefu, kundi la M23 limekuwa likipambana na serikali, likidai haki kwa jamii ya Watutsi wa Congo.

    Lakini sasa, kulikuwa na mabadiliko makubwa M23, haikuwa tu kundi la waasi, bali lilionekana kama jeshi binafsi la Corneille Nangaa.

    Uamuzi huo ulizua sintofahamu kubwa, kwani upinzani ulidai kuwa matokeo hayo yalikuwa na mizengwe. Wapo waliodai kuwa Nangaa alihusika moja kwa moja kuhakikisha Tshisekedi anashinda ili kumaliza utawala wa muda mrefu wa Joseph Kabila. Lakini wakati watu walidhani kuwa jukumu lake katika siasa za Congo limeishia hapo, mambo yalibadilika ghafla. Badala ya kustaafu kwenye siasa, Corneille Nangaa aliibuka na Action for Change (AFC), chama kipya cha kisiasa ambacho kilionekana kuja na ajenda tofauti. Alianza kujenga ushawishi mkubwa ndani na nje ya Congo, huku akijitokeza kama mpinzani wa utawala wa Tshisekedi aliyechangia kumuweka madarakani. Lakini hatua iliyotikisa Congo ni pale ilipogundulika kuwa Nangaa sasa alikuwa na uhusiano wa karibu na kundi la waasi la M23, ambalo linajulikana kwa mapigano yake dhidi ya serikali ya Congo. Kwa muda mrefu, kundi la M23 limekuwa likipambana na serikali, likidai haki kwa jamii ya Watutsi wa Congo. Lakini sasa, kulikuwa na mabadiliko makubwa M23, haikuwa tu kundi la waasi, bali lilionekana kama jeshi binafsi la Corneille Nangaa.
    Like
    1
    · 0 Comments ·0 Shares ·273 Views
  • #PART11

    Baada ya Ntaganda kupelekwa The Heague, M23 iliongozwa na Sultan Makenga, Mtutsi wa Rutshuru huko Kivu Kaskazini. Mwaka 1990 Makenga akiwa na miaka 17 tu alienda Rwanda kujiunga na kikundi cha waasi RPF kilichokuwa kinaongozwa na Jenerali Fredy Rwigyema. Sultan Makenga akiwa askari wa RPF alipigana msituni dhidi ya serikali ya kihutu ya Juvenile Habyarimana.

    Baada RPF ilishika dola, Askari wote wa RPF waliingizwa katika jeshi la Rwanda akiwemo Sultan Makenga. Alihudumu katika jeshi hilo kwa muda mrefu hadi kufikia cheo cha Kanali kabla ya kurudi "nyumbani" Congo, kujiunga na kikundi cha waasi cha CNDP. Baada ya mkataba wa amani wa March 23, 2009 Sultan Makenga alikuwa miongoni mwa askari 600 wa CNDP waliokataa kujiunga na jeshi la Congo (FARDC).

    Mwaka 2012 Bosco Ntaganda alipojitoa kwenye jeshi la Congo na kuunga kikundi cha waasi cha M23, Sultan Makenga alikua wa kwanza kujiunga. Baada ya Ntaganda kujisalimisha, Makenga akapewa uongozi wa M23. Akaongoza kuanzia 2013 hadi 2016 alipotoweka ghafla. Haijulikani alipo, japo inasemekana alienda Rwanda na hakurudi tena.

    Baada ya Makenga kutoweka katika mazingira ya "kutatanisha" M23 ikawa na viongozi ambao hawakuwa mashuhuri sana hadi 2022 ilipompata Corneille Nangaa. Huyu alikua Mwenyekiti wa Tume ya uchaguzi nchini Congo (CENI) na ndiye aliyemtangaza Tshikeshedi kuwa mshindi wa kiti cha Urais wa Congo kwenye uchaguzi wa December 30 mwaka 2018.

    Katika mambo yanayoshangaza na kufanya vita ya Congo kuonekana ngumu, ni jinsi Nangaa alivyotoka kuwa Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi, hadi kuanzisha coalition ya vikundi vya waasi, Congo River Alliance (CRA) kikiwemo M23. Jenerali Nangaa ndiye aliyeongoza M23 kuutwaa mji wa Goma January 2025, na kuyafurusha majeshi ya serikali. Nangaa ametangaza nia ya kumuondoa madarakani Rais Tshisekedi, ambaye mwaka 2018 ni Nangaa huyohuyo aliyemtangaza Tshikeshedi kuwa Rais.

    August 2024 Mahakama ya kijeshi mjini Kinshasa ilimhukumu Nangaa adhabu ya kunyongwa hadi kufa kwa kosa la uhaini. Hukumu hiyo ilitolewa bila yeye kuwepo mahakamani (death sentence in absentia). Nangaa amesema ikiwa M23 itashika dola, wale waliomhukumu ndio watanyongwa kwa niaba yake.!
    (Malisa GJ)

    #PART11 Baada ya Ntaganda kupelekwa The Heague, M23 iliongozwa na Sultan Makenga, Mtutsi wa Rutshuru huko Kivu Kaskazini. Mwaka 1990 Makenga akiwa na miaka 17 tu alienda Rwanda kujiunga na kikundi cha waasi RPF kilichokuwa kinaongozwa na Jenerali Fredy Rwigyema. Sultan Makenga akiwa askari wa RPF alipigana msituni dhidi ya serikali ya kihutu ya Juvenile Habyarimana. Baada RPF ilishika dola, Askari wote wa RPF waliingizwa katika jeshi la Rwanda akiwemo Sultan Makenga. Alihudumu katika jeshi hilo kwa muda mrefu hadi kufikia cheo cha Kanali kabla ya kurudi "nyumbani" Congo, kujiunga na kikundi cha waasi cha CNDP. Baada ya mkataba wa amani wa March 23, 2009 Sultan Makenga alikuwa miongoni mwa askari 600 wa CNDP waliokataa kujiunga na jeshi la Congo (FARDC). Mwaka 2012 Bosco Ntaganda alipojitoa kwenye jeshi la Congo na kuunga kikundi cha waasi cha M23, Sultan Makenga alikua wa kwanza kujiunga. Baada ya Ntaganda kujisalimisha, Makenga akapewa uongozi wa M23. Akaongoza kuanzia 2013 hadi 2016 alipotoweka ghafla. Haijulikani alipo, japo inasemekana alienda Rwanda na hakurudi tena. Baada ya Makenga kutoweka katika mazingira ya "kutatanisha" M23 ikawa na viongozi ambao hawakuwa mashuhuri sana hadi 2022 ilipompata Corneille Nangaa. Huyu alikua Mwenyekiti wa Tume ya uchaguzi nchini Congo (CENI) na ndiye aliyemtangaza Tshikeshedi kuwa mshindi wa kiti cha Urais wa Congo kwenye uchaguzi wa December 30 mwaka 2018. Katika mambo yanayoshangaza na kufanya vita ya Congo kuonekana ngumu, ni jinsi Nangaa alivyotoka kuwa Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi, hadi kuanzisha coalition ya vikundi vya waasi, Congo River Alliance (CRA) kikiwemo M23. Jenerali Nangaa ndiye aliyeongoza M23 kuutwaa mji wa Goma January 2025, na kuyafurusha majeshi ya serikali. Nangaa ametangaza nia ya kumuondoa madarakani Rais Tshisekedi, ambaye mwaka 2018 ni Nangaa huyohuyo aliyemtangaza Tshikeshedi kuwa Rais. August 2024 Mahakama ya kijeshi mjini Kinshasa ilimhukumu Nangaa adhabu ya kunyongwa hadi kufa kwa kosa la uhaini. Hukumu hiyo ilitolewa bila yeye kuwepo mahakamani (death sentence in absentia). Nangaa amesema ikiwa M23 itashika dola, wale waliomhukumu ndio watanyongwa kwa niaba yake.! (Malisa GJ)
    Like
    1
    · 0 Comments ·0 Shares ·536 Views
  • #PART10

    March 23, 2009 Mkataba wa amani uitwao "March 23 Agreement" ukasainiwa huko Goma, kati ya serikali ya Congo na Waasi wa CNDP, wasuluhishi wakiwa mzee Mkapa na mzee Obasanjo. Mapigano yakasitishwa

    Ntaganda na askari wa CNDP wakaingizwa kwenye jeshi la Congo (FARDC). Kukawepo na miaka mitatu ya amani, vita ikakoma kabisa. Lakini ghafla, April 04, mwaka 2012 Bosco Ntaganda alitangaza kujitoa kwenye jeshi la Congo (FARDC) pamoja na baadhi ya askari waliokuwa wanamgambo wa CNDP. Ntaganda alidai Serikali ya Congo imeshindwa kutekeleza mkataba wa amani wa Machi 23, 2009.

    Alisema Makataba huo uliweka masharti ya kutowabughudhi askari 600 wa CNDP waliokataa kujiunga na jeshi la Congo. Lakini serikali ya Congo iliwashughulikia. Baadhi walikamatwa na wengine kuuawa. Pia alidai serikali ya Congo imeshindwa kuwalinda Watutsi (Banyamulenge) waishio mashariki mwa nchi hiyo.

    Ntaganda akatangaza kuanzisha kikundi kipya cha waasi kiitwacho M23. Alidai kutumia jina hilo ili kuikumbusha serikali ya Congo kuheshimu mkataba wa amani wa Machi 23, 2009. Kundi la M23 likapata wafuasi wengi hasa askari wa zamani wa CNDP na Banyamulenge wa Kivu. Mapigano yakaanza upya.

    Rwanda na Uganda zikashutumiwa kuunga mkono waasi hao, lakini zikakataa. Hata hivyo Rwanda ililaumiwa kwa kuruhusu M23 kuwa na kambi za kijeshi katika miji ya Gisenyi na Rusizi. Pia Rwanda ilihusishwa na mgogoro huo kwa sababu Ntaganda hakuwa Mkongomani, bali Mnyarwanda aliyezaliwa na kukulia Rwanda. Ametumikia jeshi la Rwanda kwa miaka mingi, kabla ya kuhamia Congo kupigania haki za Banyamulenge.

    Baada ya mwaka mmoja wa mapigano makali, vikosi vya M23 vikazidiwa nguvu na jeshi la serikali. Machi 18, 2013, Bosco Ntaganda akakimbilia Rwanda na akaenda mwenyewe kujisalimisha kwenye ubalozi wa Marekani mjini Kigali. Akasafirishwa kwenda The Heague kwenye mahakama ya kimataifa ya makosa ya jinai (ICC).

    Mwaka 2015 kesi yake ikaanza kusikilizwa, na mwaka 2019 akapatikana na hatia katika makosa 18, yakiwemo ubakaji, mauaji ya raia wasio na hatia, na kutumikisha watoto jeshini. Akahukumiwa kifungo cha miaka 30 jela, adhabu ambayo anaitumikia hadi sasa.
    (Malisa GJ)

    #PART10 March 23, 2009 Mkataba wa amani uitwao "March 23 Agreement" ukasainiwa huko Goma, kati ya serikali ya Congo na Waasi wa CNDP, wasuluhishi wakiwa mzee Mkapa na mzee Obasanjo. Mapigano yakasitishwa Ntaganda na askari wa CNDP wakaingizwa kwenye jeshi la Congo (FARDC). Kukawepo na miaka mitatu ya amani, vita ikakoma kabisa. Lakini ghafla, April 04, mwaka 2012 Bosco Ntaganda alitangaza kujitoa kwenye jeshi la Congo (FARDC) pamoja na baadhi ya askari waliokuwa wanamgambo wa CNDP. Ntaganda alidai Serikali ya Congo imeshindwa kutekeleza mkataba wa amani wa Machi 23, 2009. Alisema Makataba huo uliweka masharti ya kutowabughudhi askari 600 wa CNDP waliokataa kujiunga na jeshi la Congo. Lakini serikali ya Congo iliwashughulikia. Baadhi walikamatwa na wengine kuuawa. Pia alidai serikali ya Congo imeshindwa kuwalinda Watutsi (Banyamulenge) waishio mashariki mwa nchi hiyo. Ntaganda akatangaza kuanzisha kikundi kipya cha waasi kiitwacho M23. Alidai kutumia jina hilo ili kuikumbusha serikali ya Congo kuheshimu mkataba wa amani wa Machi 23, 2009. Kundi la M23 likapata wafuasi wengi hasa askari wa zamani wa CNDP na Banyamulenge wa Kivu. Mapigano yakaanza upya. Rwanda na Uganda zikashutumiwa kuunga mkono waasi hao, lakini zikakataa. Hata hivyo Rwanda ililaumiwa kwa kuruhusu M23 kuwa na kambi za kijeshi katika miji ya Gisenyi na Rusizi. Pia Rwanda ilihusishwa na mgogoro huo kwa sababu Ntaganda hakuwa Mkongomani, bali Mnyarwanda aliyezaliwa na kukulia Rwanda. Ametumikia jeshi la Rwanda kwa miaka mingi, kabla ya kuhamia Congo kupigania haki za Banyamulenge. Baada ya mwaka mmoja wa mapigano makali, vikosi vya M23 vikazidiwa nguvu na jeshi la serikali. Machi 18, 2013, Bosco Ntaganda akakimbilia Rwanda na akaenda mwenyewe kujisalimisha kwenye ubalozi wa Marekani mjini Kigali. Akasafirishwa kwenda The Heague kwenye mahakama ya kimataifa ya makosa ya jinai (ICC). Mwaka 2015 kesi yake ikaanza kusikilizwa, na mwaka 2019 akapatikana na hatia katika makosa 18, yakiwemo ubakaji, mauaji ya raia wasio na hatia, na kutumikisha watoto jeshini. Akahukumiwa kifungo cha miaka 30 jela, adhabu ambayo anaitumikia hadi sasa. (Malisa GJ)
    Like
    1
    · 0 Comments ·0 Shares ·556 Views
  • #PART9

    Baada ya miaka mitatu ya utulivu, ghafla 2006 Jenerali Laurent Nkunda, aliasi jeshi kwa madai serikali imeshindwa kutekeleza Mkataba wa Amani wa SunCity. Ikumbukwe kabla ya kujiunga na Jeshi, alikua mpiganaji wa RCD - Goma, kundi lililoungwa mkono na Rwanda. Baada ya mkataba wa Suncity waasi wote waliingizwa jeshini akiwemo Nkunda.

    Lakini Juni 29, 2006, Nkunda akaasi jeshi na kuunda kundi la Congrès National pour la Défense du Peuple (CNDP). Madai yake:
    - Askari wa vikundi vya waasi walioingizwa jeshini hawakupewa vyeo.
    - Serikali ya Congo kushindwa kuwatanbua Watutsi (Banyamulenge) waishio mashariki mwa nchi hiyo kama raia wa Congo.
    - Serikali ya Congo kushindwa kuwakamata wanamgambo wa kihutu wa FDLR (Intarahanwe) waliojificha Congo baada ya kufanya mauaji ya kimbari Rwanda 1994.

    Nkunda akasema lengo la kuanzisha kundi la waasi la CNDP ni kupigania haki za Watutsi waishio mashariki mwa Congo (Banyamulenge) na kukabiliana na wanamgambo wa Kihutu wa FDLR. Nkunda akaungwa mkono na Rwanda na Uganda, akapewa silaha, vita ikaanza upyaaaaa (tamka kwa sauti ya mbunge Bwege).

    CNDP ikaua raia wengi wenye asili ya Kihutu ikiwatumu kuwa wafuasi wa FDLR. Serikali ya Burundi ikiongozwa na Piere Nkurunzinza (Mhutu) ikaingiza jeshi Congo kupambana na CNDP ili kulinda raia wake waliokua Congo. Kwa miaka mitatu kukawa na mapigano makali sana mashariki mwa Congo.

    January 2009 Waasi wa CNDP wakazidiwa. Laurent Nkunda akakimbilia Rwanda. Alipofika akakamatwa na kuwekwa kizuizini. Mpaka leo, bado anashikiliwa bila kufikishwa mahakamani. Jenerali Bosco Ntaganda, Mtutsi (Banyamulenge) wa Kivu akateuliwa kuongoza CNDP. Akafanya vitendo vingi vya kikatili kwa raia kuliko mtangulizi wake, kama ubakaji, mauaji ya halaiki, na kutumikisha watoto jeshini.

    Machi 23, 2009 serikali ya Congo na CNDP wakasaini Mkataba wa Amani, ulioitwa "March 23 Agreement" wenye masharti yafuatayo:
    - Kusitisha mapigano kwa pande zote.
    - Kuingiza askari wa CNDP kwenye jeshi la Congo.
    - Kutowashtaki askari wa CNDP kwa makosa waliyofanya wakati wa vita.
    - Wananchi wa Kivu wanufaike na rasilimali zao
    - Kulinda haki za binadamu Kivu
    (Malisa GJ)

    #PART9 Baada ya miaka mitatu ya utulivu, ghafla 2006 Jenerali Laurent Nkunda, aliasi jeshi kwa madai serikali imeshindwa kutekeleza Mkataba wa Amani wa SunCity. Ikumbukwe kabla ya kujiunga na Jeshi, alikua mpiganaji wa RCD - Goma, kundi lililoungwa mkono na Rwanda. Baada ya mkataba wa Suncity waasi wote waliingizwa jeshini akiwemo Nkunda. Lakini Juni 29, 2006, Nkunda akaasi jeshi na kuunda kundi la Congrès National pour la Défense du Peuple (CNDP). Madai yake: - Askari wa vikundi vya waasi walioingizwa jeshini hawakupewa vyeo. - Serikali ya Congo kushindwa kuwatanbua Watutsi (Banyamulenge) waishio mashariki mwa nchi hiyo kama raia wa Congo. - Serikali ya Congo kushindwa kuwakamata wanamgambo wa kihutu wa FDLR (Intarahanwe) waliojificha Congo baada ya kufanya mauaji ya kimbari Rwanda 1994. Nkunda akasema lengo la kuanzisha kundi la waasi la CNDP ni kupigania haki za Watutsi waishio mashariki mwa Congo (Banyamulenge) na kukabiliana na wanamgambo wa Kihutu wa FDLR. Nkunda akaungwa mkono na Rwanda na Uganda, akapewa silaha, vita ikaanza upyaaaaa (tamka kwa sauti ya mbunge Bwege). CNDP ikaua raia wengi wenye asili ya Kihutu ikiwatumu kuwa wafuasi wa FDLR. Serikali ya Burundi ikiongozwa na Piere Nkurunzinza (Mhutu) ikaingiza jeshi Congo kupambana na CNDP ili kulinda raia wake waliokua Congo. Kwa miaka mitatu kukawa na mapigano makali sana mashariki mwa Congo. January 2009 Waasi wa CNDP wakazidiwa. Laurent Nkunda akakimbilia Rwanda. Alipofika akakamatwa na kuwekwa kizuizini. Mpaka leo, bado anashikiliwa bila kufikishwa mahakamani. Jenerali Bosco Ntaganda, Mtutsi (Banyamulenge) wa Kivu akateuliwa kuongoza CNDP. Akafanya vitendo vingi vya kikatili kwa raia kuliko mtangulizi wake, kama ubakaji, mauaji ya halaiki, na kutumikisha watoto jeshini. Machi 23, 2009 serikali ya Congo na CNDP wakasaini Mkataba wa Amani, ulioitwa "March 23 Agreement" wenye masharti yafuatayo: - Kusitisha mapigano kwa pande zote. - Kuingiza askari wa CNDP kwenye jeshi la Congo. - Kutowashtaki askari wa CNDP kwa makosa waliyofanya wakati wa vita. - Wananchi wa Kivu wanufaike na rasilimali zao - Kulinda haki za binadamu Kivu (Malisa GJ)
    0 Comments ·0 Shares ·466 Views
  • #PART6

    Alipoingia Ikulu Kabila alifuta jina Zaire na kurudisha Congo (Jamhuri ya kidemokrasia). Baadae alifikiria kuiachia Kivu, eneo lenye utajiri mkubwa wa madini adimu duniani. Akasema "to hell with Lemera Agreement" akautupilia mbali mkataba wa Lemera. Akasema Kivu itabaki Congo na madini ya Kivu yatajenga Congo. Full stop. Ashakuwa Rais utamfanya nini?

    Kagame hakuamini macho yake. Alishawaza jinsi ambavyo Rwanda ingekuwa Dubai ya Afrika kwa rasilimali za Congo. Lakini ghafla aligeukwa na mshirika wake Laurent Désiré Kabila. Akamfuata "Godfather" wake mzee Museveni. Mzee akasema kama katugeuka tumpige. Wakatafuta kikundi cha Waasi wakiunge mkono. Wakapata Rassemblement Congolais pour la Démocratie (RCD), kilichoongozwa na Jenerali Ernest Wamba dia Wamba. Kikundi kikapewa silaha na fedha kikaanza kumshughulikia Kabila.

    RCD ikaanza kuchapana na jeshi la Congo (FARDC) ikiwa na backup ya Rwanda na Uganda. Vita vikapamba moto. Rwanda na Uganda nao wakaingiza majeshi Congo kusaidia waasi wa RCD. Kabila akaona anazidiwa, akaomba msaada Angola na Chad. Nchi hizo zikaleta vikosi vyake Congo. Mapigano yakawa makali sana. Eneo la mashariki mwa Congo likageuka machinjioni. Watu walikufa kwa wingi, mpaka maiti zikatapakaa barabarani bila kuzikwa, zikawa zinadonolewa na ndege.

    Hii iliitwa Vita ya Pili ya Congo (1998–2002), iliyokua mbaya zaidi katika historia ya vita zote Afrika. Imebatizwa jina "Vita Kuu ya Afrika". Inakadiriwa watu laki tano walipoteza maisha huku mamilioni wakikimbia nchi. Mapigano yaliendelea, huku vikosi vya Rwanda na Uganda vikichota madini. Katikati ya mapigano mgongano wa kimaslahi ukajitokeza.

    Jasin Stearns, katika kitabu chake Dancing in the Glory of Monsters, anasema Kagame alishindwa kuelewana na "godfather" wake Museveni juu ya mgawanyo wa mali. Hali hiyo ilifanya kikundi cha RCD kipasuke na kuzaliwa vikundi viwili. Cha kwanza kikajiita RCD-Goma kikiongozwa na Kanali Emile Ilunga (hiki kilisaidiwa na Rwanda) na cha pili kikajiita RCD-Kisangani, kikiongozwa na Jenerali Mbusa Nyamwisi (kikisaidiwa na Uganda).
    (Malisa GJ)

    #PART6 Alipoingia Ikulu Kabila alifuta jina Zaire na kurudisha Congo (Jamhuri ya kidemokrasia). Baadae alifikiria kuiachia Kivu, eneo lenye utajiri mkubwa wa madini adimu duniani. Akasema "to hell with Lemera Agreement" akautupilia mbali mkataba wa Lemera. Akasema Kivu itabaki Congo na madini ya Kivu yatajenga Congo. Full stop. Ashakuwa Rais utamfanya nini? Kagame hakuamini macho yake. Alishawaza jinsi ambavyo Rwanda ingekuwa Dubai ya Afrika kwa rasilimali za Congo. Lakini ghafla aligeukwa na mshirika wake Laurent Désiré Kabila. Akamfuata "Godfather" wake mzee Museveni. Mzee akasema kama katugeuka tumpige. Wakatafuta kikundi cha Waasi wakiunge mkono. Wakapata Rassemblement Congolais pour la Démocratie (RCD), kilichoongozwa na Jenerali Ernest Wamba dia Wamba. Kikundi kikapewa silaha na fedha kikaanza kumshughulikia Kabila. RCD ikaanza kuchapana na jeshi la Congo (FARDC) ikiwa na backup ya Rwanda na Uganda. Vita vikapamba moto. Rwanda na Uganda nao wakaingiza majeshi Congo kusaidia waasi wa RCD. Kabila akaona anazidiwa, akaomba msaada Angola na Chad. Nchi hizo zikaleta vikosi vyake Congo. Mapigano yakawa makali sana. Eneo la mashariki mwa Congo likageuka machinjioni. Watu walikufa kwa wingi, mpaka maiti zikatapakaa barabarani bila kuzikwa, zikawa zinadonolewa na ndege. Hii iliitwa Vita ya Pili ya Congo (1998–2002), iliyokua mbaya zaidi katika historia ya vita zote Afrika. Imebatizwa jina "Vita Kuu ya Afrika". Inakadiriwa watu laki tano walipoteza maisha huku mamilioni wakikimbia nchi. Mapigano yaliendelea, huku vikosi vya Rwanda na Uganda vikichota madini. Katikati ya mapigano mgongano wa kimaslahi ukajitokeza. Jasin Stearns, katika kitabu chake Dancing in the Glory of Monsters, anasema Kagame alishindwa kuelewana na "godfather" wake Museveni juu ya mgawanyo wa mali. Hali hiyo ilifanya kikundi cha RCD kipasuke na kuzaliwa vikundi viwili. Cha kwanza kikajiita RCD-Goma kikiongozwa na Kanali Emile Ilunga (hiki kilisaidiwa na Rwanda) na cha pili kikajiita RCD-Kisangani, kikiongozwa na Jenerali Mbusa Nyamwisi (kikisaidiwa na Uganda). (Malisa GJ)
    Like
    2
    · 0 Comments ·0 Shares ·549 Views
  • OPERATION ENTEBBE -1

    Jina mbadala: Operation Thunderstorm/Operation Yonatan

    Watekelezaji: -MOSSAD
    - IDF (ISRAEL DEFENCE FORCE)
    Kitengo cha Weledi: Sayeret Matkal
    Mwaka wa utekelezaji: July, 1976
    Nchi: Israel/Uganda

    Silaha za kukumbukwa: Lockheed C-130 Hurcules
    Wahusika wa kukumbukwa: - Yonatan Netanyahu (kaka wa Waziri Mkuu wa zamani Benjamin Netanyahu)
    -Ehud Barak (alikuja kuwa Waziri Mkuu miaka ya karibuni)

    MOSAD & IDF: OPERATION ENTEBBE

    Siku ya tarehe 27 June mwaka 1976 ilianza kama siku nyingine yioyote ndani ya uwanja wa ndege wa kimataifa katika mji mkuu wa nchi ya Israel Tel Aviv, uwanja ujulikanao kama Ben Gurion International Airport. Moja kati ya ndege ambayo ilikuwa inafanya safari yake katika siku ya elo ilikuwa ni ndege ya kampuni ya Air Frace ambao walikuwa na ndege yao ya Air France Flight 139 ambayo ni ndege aina ya Airbus A300B4-203 yenye namba ya usajili mkiani F-BVGG (c/n 019).
    Ndege hii ilikuwa inafanya safari yake katika siku ya leo kutoka Tel Aviv na ilikuwa inatarajiwa kutua katika uwanja wa ndege wa Charles DE Gaulle International Airport jijini Paris, Ufaransa. Baada ya taratibu na protokali zote za uwanja wa ndege kukamilika na abiria wote kukwea kwenye ndege, ndege iliruka kutoka kiwanjani ikiwa na abiria 190 ndani yake pamoja na ‘crew’ ya watu 12 (Marubani na wahudumu) ambamo asilimia kubwa ya abiria walikuwa ni raia wa Israel pamoja na watu wenye asili ya kiyahudi. Ndege iliruka kutoka Tel Aviv mpaka jijini Anthens, Ugiriki ambapo ilichukua abiria wengine wapatao 58. Baada ya hapo ndege iliruka pasipo kujua kwamba kati aya abiria hao 58 waliowachukua Ugiriki ndani yao kulikuwa na abiria wanne ambao walikuwa ni wanachama wawili wa kikundi cha Popular Front For The Liberation of Palestine – External Operations (PFLP-EO) kutoka Plaestina na wanachama wawili wa kikundi cha Revolutionary Cells kutoka nchini Ujerumani.

    Baada ya abiria wote kukamilisha utaratibu na kupanda ndani ya ndege, ndege iliondoka uwanjani Athens mnamo amjira ya saa 6 na dakika 30 mchana kuelekea Paris, Ufaransa.
    Dakika chache baada ya ndege kuruka rubani mkuu wa ndege ambaye ndiye alikuwa ameshikili ‘usukani’ Bw. Michel Bacos akasikia kelele nyuma ya ndege wanakokaa abiria (cabin). Ili kujiridhisha kwamba kila kitu kiko sawa, rubani Michel Bacos akamuagiza msaidizi wake mmoja wapo ambaye ndiye alikuwa injinia wa ndege aende kuangalia nini kilikuwa kinaendelea.
    Mara tu baada ya msaidizi huyo kufungua mlango wa mbele wa chumba cha marubani, alikutana uso kwa uso na bastola usoni mwake iliyoshikiliwa na mtu ambaye mkononi alikuwa amebeba bomu la kurusha kwa mkono. Huku msaidizi huyo akiwa bado ameshikwa na bumbuwazi, mtu huyu mwenye bomu mkononi na bastola (jina lake anaitwa Wilfred Bose raia wa Ujerumani) alimsukuma yule injinia nakumrudisha tena ndani ya chumba cha marubani na kisha yeye mwenyewe pia kuingia.
    Mara tu baada ya kufika ndani ya chumba cha marubani, akawaweka chini ya ulinzi marubani ambao bado walikuwa kwenye mshituko wa mshangao na kisha kumnyanyua rubani msaidizi kutoka kwenye siti yake na kukaa yeye. Baada ya kukaa kwenye siti ya rubani msaidizi kitu cha kwanza alichokifanya haramia huyu Wilfre Bose ni kuchukua microphone ambayo marubani huwa wanatumia kutoa matangazo kwa abria, na baada ya kuiweka microphone akatoa tangazo lake la kwanza, kwa sauti ya utulivu iliyojaa lafudhi nzito ya kijerumani, akawasema; *“..kuanzia sasa ndege hii inaitwa HAIFA 1, badala ya Flight 139..”*
    Haifa ni eneo (mji) maarufu ulipo kaskazini mwa nchi ambayo abiria wengi waliopanda kwenye ndege hiyo walitambua kama Israel lakini watekaji hawa na watu wengine duniani wakitambua kama Palestina.
    Mara tu baada ya tangazo hili kusikika kwenye vipaza sauti vya ndege, abiria wote licha ya kuwa kwenye mshituko mkubwa wa ghafla lakini moja kwa moja waling’amua ni nini kilikuwa kinaendelea. Flight 139 au Haifa 1 kama alivyoibatiza aliyetoa tangazo, ilikuwa imetekwa na maharamia.
    Baada ya Tangazo hili, haramaia Wilfred Bose akamuamuru rubani Michel Bacos kuendesha ndege kuelekea mji wa Bengazhi, nchini Libya.
    Baada ya kuwasili uwanja wa ndege wa Bengazhi nchini Libya, ndege ilitumia karbia masaa saba uwanjani hapo kwa ajili ya kujaza ndege mafuta. Katika masaa hayo saba kuna mwanamama Patricia Martel mwenye asili ya Uingereza lakini akiwa ameolewa nchin Israel miaka michache iliyopita alifanya ‘kituko’ ambacho kilikuja kuwa na manufaa sana baadae. Wakati ambao ndege inaendelea kujaza mafuta kwa masaa yote hayo, huyu mama ambaye ni nesi kwa taaluma, alianza kulalamika juu ya maumivu ya tumbo yaliyopitiliza. Aliwaeleza watekaji kwamba ana ujauzito. Maharamia haya yakaruhusu wahudumu wa ndege wamuhudumie mwananmke mwenzao kwa vile ambavyo wataweza kwa kuzingatia kwamba ana mimba. Baada ya kuhudumiwa kwa karibia saa nzima, Patricia akatumua ujuzi wake wa unesi akafanya alicho kifanya na ghafla akaanza kutoka damu kiduchu sehemu za siri. Baada ya damu hizi kidogo kuanza kumtoka na kulalamika kuwa maumivu yamemzidia ndipo hapa ambapo wahudumu wa ndege wakaripoti kwa maharamia kuwa mimba ilikuwa imetoka.

    Kwa huruma na ili kuepusha taharuki ndani ya ndege maharamia hawa wakamuachia huru mwanamama Patricia Martel hapo uwanja wa ndege mjini Bengazhi ili aweze kupata uangalizi mzuri zaidi wa kidaktari.
    Lakini ukweli ni kwamba Patricia hakuwa na mimba wala hakuwa na maumivu yoyote tumboni, alichokifanya ilikuwa ni uigizaji pamoja na kuchanganya utaalamu wake wa fani ya unesi na kuweza kuwahadaa maharamia hao.
    Baada ya kuachiwa Patricia alikuwa ni mtu wa kwanza muhimu kutumiwa na Mossad kujua taarifa sahihi zaidi kuhusu nini hasa kilikuwa kinaendelea ndani ya ndege, kulikuwa na watekaji wangapi, jinsia zao, silaha zao na vingine vyote ambavyo alifanikiwa kuviona.
    Baada ya hapa Bose akamuamuru tena rubani Michel Bacos kurusha tena ndege angani pasipo kumueleza kuwa wanaeelekea wapi.
    Wakiwa angani ndipo alianza kumpa maagizo wapi hasa anataka waelekee. Upande wa abiria kwenye cabin ambao nao walikuwa wamewekwa chini ya ulinzi na maharamia wengine waliosalia, wao hawaku wanafahamu hata ni wapi walikuwa wanaeleke. Ndege ilikuwa inaruka angani kwa karibia masaa 24. Abiria wengi walianza kuhisi labda ndege ilikuwa inaruka kuelekea China au labda Siberia, na vichwani mwao walikuwa wanajiuliza kwa nini walikuwa wanapelekwa huko.
    Lakini laiti kama wangelijua mahali ambako walikuwa wanapelekwa basi wangetamani ndege hiyo ielekee kweli china.
    Baada ya ya takribani masaa 24 ndege kuwa angani tangu iruke kutoka Bengazhi nchini Libya, hatimaye abiria walisikia ndege ikitua na kugusa Runway ya kiwanja cha ndege mahali fulani dunia walipowasili lakini wakiwa hawafahamu ni mwapi hasa walikuwa.
    Baada ya matairi ya ndege tu kukanyaga lami za runaway na abiria kufungua ‘pazia’ (shutters) kwenye vioo vilivyopo pemnbeni mwa siti zao na kuangalia nje, mara moja wakaelewa wako wapi. Nje uwanjani kwenye lami, kulikuwa kumesimama lijitu la miraba minne lenye ngozi nyeusi tiiii likiwa na walinzi wa kijeshi na wengine waliovalia nguo za kiraia likiwa limezungukwa pande zote na walinzi hao. Mtu huyu mwenye umbo la kutisha kwa kipindi hiki alikuwa anajulikana ulimwenguni kote kutokana na matendo yake na ukatili wake. Kwa kutupa jicho mara moja tu haukuweza kukosea kujua kuwa pale kwenye lami uwanjani, alikuwa amesimama Generali Nduli Idd Amin Dadaa, ‘Field Marshal’. Swali lilokuwepo vichwani mwao lilikuwa limejibiwa tayari, wamepelekwa kwenye ardhi ya moja ya watawala ‘watemi’ na katili kuwahi kutokea juu ya uso wa dunia. Walikuwa nchini Uganda.
    Baada ya ndege kusimama abria wote 248 ambao wengi wao walikuwa ni raia wa Israel na wayahudi, walishushwa kutoka kwenye ndege na moja kwa moja kupelekwa ‘terminal’ ambayo kwa wakati huo ilikuwa haitumiki. Mpaka muda huu wakang’amua kwamba hawakuwa ‘abiria’ tena kama ambavyo waliondoka Tel Aviv, bali sasa walikuwa ni mateka wa maharamia haya ya kijerumani, palestina na jeshi la Uganda.

    Wakati huo huo…
    Nchini Israel katika jamii ya masuala ya usalama walikuwa wako kwenye bumbuwazi kuu, matukio ya dizaini hii huwa ni ya kushtukiza na yanatokea kipindi ambacho ‘haujajiandaa’. Pia kwa kipindi hiki bado Idara ya Ujasusi ya Mossad hawakuwa na Intelejensia ya kutosha za nchi nyingi za kiafrika, akili yao na nguvu yao yote ilikuwa kwenyekudhibiti juhudi za nchi za kiarabu kufuta Israel kutoka kwenye eneo hilo walilopo. Kwa hiyo kitendo cha raia wao wengi kiasi hiki kutekwa na kupelekwa Africa kilikuwa si tu na changamoto ya namana gani wanawaokoa bali pia kulikuwa na changamoto ya uwepo wa Intelijensia ya kutosha kuhusu eneo la Entebbe, Uganda kuweza kufanya oparesheni yoyote ya kijeshi.
    Ndipo hapa ambapo waziri mkuu wa kipindi hicho wa Israel Yitzhak Rabin akaitisha kikao cha maafisa wa ngazi za juu wa jeshi na Mossad na kuwauliza swali moja tu, *“…tunafanyeje?”*

    Itaendelea…
    #TheBold_Jf
    OPERATION ENTEBBE -1 Jina mbadala: Operation Thunderstorm/Operation Yonatan Watekelezaji: -MOSSAD - IDF (ISRAEL DEFENCE FORCE) Kitengo cha Weledi: Sayeret Matkal Mwaka wa utekelezaji: July, 1976 Nchi: Israel/Uganda Silaha za kukumbukwa: Lockheed C-130 Hurcules Wahusika wa kukumbukwa: - Yonatan Netanyahu (kaka wa Waziri Mkuu wa zamani Benjamin Netanyahu) -Ehud Barak (alikuja kuwa Waziri Mkuu miaka ya karibuni) MOSAD & IDF: OPERATION ENTEBBE Siku ya tarehe 27 June mwaka 1976 ilianza kama siku nyingine yioyote ndani ya uwanja wa ndege wa kimataifa katika mji mkuu wa nchi ya Israel Tel Aviv, uwanja ujulikanao kama Ben Gurion International Airport. Moja kati ya ndege ambayo ilikuwa inafanya safari yake katika siku ya elo ilikuwa ni ndege ya kampuni ya Air Frace ambao walikuwa na ndege yao ya Air France Flight 139 ambayo ni ndege aina ya Airbus A300B4-203 yenye namba ya usajili mkiani F-BVGG (c/n 019). Ndege hii ilikuwa inafanya safari yake katika siku ya leo kutoka Tel Aviv na ilikuwa inatarajiwa kutua katika uwanja wa ndege wa Charles DE Gaulle International Airport jijini Paris, Ufaransa. Baada ya taratibu na protokali zote za uwanja wa ndege kukamilika na abiria wote kukwea kwenye ndege, ndege iliruka kutoka kiwanjani ikiwa na abiria 190 ndani yake pamoja na ‘crew’ ya watu 12 (Marubani na wahudumu) ambamo asilimia kubwa ya abiria walikuwa ni raia wa Israel pamoja na watu wenye asili ya kiyahudi. Ndege iliruka kutoka Tel Aviv mpaka jijini Anthens, Ugiriki ambapo ilichukua abiria wengine wapatao 58. Baada ya hapo ndege iliruka pasipo kujua kwamba kati aya abiria hao 58 waliowachukua Ugiriki ndani yao kulikuwa na abiria wanne ambao walikuwa ni wanachama wawili wa kikundi cha Popular Front For The Liberation of Palestine – External Operations (PFLP-EO) kutoka Plaestina na wanachama wawili wa kikundi cha Revolutionary Cells kutoka nchini Ujerumani. Baada ya abiria wote kukamilisha utaratibu na kupanda ndani ya ndege, ndege iliondoka uwanjani Athens mnamo amjira ya saa 6 na dakika 30 mchana kuelekea Paris, Ufaransa. Dakika chache baada ya ndege kuruka rubani mkuu wa ndege ambaye ndiye alikuwa ameshikili ‘usukani’ Bw. Michel Bacos akasikia kelele nyuma ya ndege wanakokaa abiria (cabin). Ili kujiridhisha kwamba kila kitu kiko sawa, rubani Michel Bacos akamuagiza msaidizi wake mmoja wapo ambaye ndiye alikuwa injinia wa ndege aende kuangalia nini kilikuwa kinaendelea. Mara tu baada ya msaidizi huyo kufungua mlango wa mbele wa chumba cha marubani, alikutana uso kwa uso na bastola usoni mwake iliyoshikiliwa na mtu ambaye mkononi alikuwa amebeba bomu la kurusha kwa mkono. Huku msaidizi huyo akiwa bado ameshikwa na bumbuwazi, mtu huyu mwenye bomu mkononi na bastola (jina lake anaitwa Wilfred Bose raia wa Ujerumani) alimsukuma yule injinia nakumrudisha tena ndani ya chumba cha marubani na kisha yeye mwenyewe pia kuingia. Mara tu baada ya kufika ndani ya chumba cha marubani, akawaweka chini ya ulinzi marubani ambao bado walikuwa kwenye mshituko wa mshangao na kisha kumnyanyua rubani msaidizi kutoka kwenye siti yake na kukaa yeye. Baada ya kukaa kwenye siti ya rubani msaidizi kitu cha kwanza alichokifanya haramia huyu Wilfre Bose ni kuchukua microphone ambayo marubani huwa wanatumia kutoa matangazo kwa abria, na baada ya kuiweka microphone akatoa tangazo lake la kwanza, kwa sauti ya utulivu iliyojaa lafudhi nzito ya kijerumani, akawasema; *“..kuanzia sasa ndege hii inaitwa HAIFA 1, badala ya Flight 139..”* Haifa ni eneo (mji) maarufu ulipo kaskazini mwa nchi ambayo abiria wengi waliopanda kwenye ndege hiyo walitambua kama Israel lakini watekaji hawa na watu wengine duniani wakitambua kama Palestina. Mara tu baada ya tangazo hili kusikika kwenye vipaza sauti vya ndege, abiria wote licha ya kuwa kwenye mshituko mkubwa wa ghafla lakini moja kwa moja waling’amua ni nini kilikuwa kinaendelea. Flight 139 au Haifa 1 kama alivyoibatiza aliyetoa tangazo, ilikuwa imetekwa na maharamia. Baada ya Tangazo hili, haramaia Wilfred Bose akamuamuru rubani Michel Bacos kuendesha ndege kuelekea mji wa Bengazhi, nchini Libya. Baada ya kuwasili uwanja wa ndege wa Bengazhi nchini Libya, ndege ilitumia karbia masaa saba uwanjani hapo kwa ajili ya kujaza ndege mafuta. Katika masaa hayo saba kuna mwanamama Patricia Martel mwenye asili ya Uingereza lakini akiwa ameolewa nchin Israel miaka michache iliyopita alifanya ‘kituko’ ambacho kilikuja kuwa na manufaa sana baadae. Wakati ambao ndege inaendelea kujaza mafuta kwa masaa yote hayo, huyu mama ambaye ni nesi kwa taaluma, alianza kulalamika juu ya maumivu ya tumbo yaliyopitiliza. Aliwaeleza watekaji kwamba ana ujauzito. Maharamia haya yakaruhusu wahudumu wa ndege wamuhudumie mwananmke mwenzao kwa vile ambavyo wataweza kwa kuzingatia kwamba ana mimba. Baada ya kuhudumiwa kwa karibia saa nzima, Patricia akatumua ujuzi wake wa unesi akafanya alicho kifanya na ghafla akaanza kutoka damu kiduchu sehemu za siri. Baada ya damu hizi kidogo kuanza kumtoka na kulalamika kuwa maumivu yamemzidia ndipo hapa ambapo wahudumu wa ndege wakaripoti kwa maharamia kuwa mimba ilikuwa imetoka. Kwa huruma na ili kuepusha taharuki ndani ya ndege maharamia hawa wakamuachia huru mwanamama Patricia Martel hapo uwanja wa ndege mjini Bengazhi ili aweze kupata uangalizi mzuri zaidi wa kidaktari. Lakini ukweli ni kwamba Patricia hakuwa na mimba wala hakuwa na maumivu yoyote tumboni, alichokifanya ilikuwa ni uigizaji pamoja na kuchanganya utaalamu wake wa fani ya unesi na kuweza kuwahadaa maharamia hao. Baada ya kuachiwa Patricia alikuwa ni mtu wa kwanza muhimu kutumiwa na Mossad kujua taarifa sahihi zaidi kuhusu nini hasa kilikuwa kinaendelea ndani ya ndege, kulikuwa na watekaji wangapi, jinsia zao, silaha zao na vingine vyote ambavyo alifanikiwa kuviona. Baada ya hapa Bose akamuamuru tena rubani Michel Bacos kurusha tena ndege angani pasipo kumueleza kuwa wanaeelekea wapi. Wakiwa angani ndipo alianza kumpa maagizo wapi hasa anataka waelekee. Upande wa abiria kwenye cabin ambao nao walikuwa wamewekwa chini ya ulinzi na maharamia wengine waliosalia, wao hawaku wanafahamu hata ni wapi walikuwa wanaeleke. Ndege ilikuwa inaruka angani kwa karibia masaa 24. Abiria wengi walianza kuhisi labda ndege ilikuwa inaruka kuelekea China au labda Siberia, na vichwani mwao walikuwa wanajiuliza kwa nini walikuwa wanapelekwa huko. Lakini laiti kama wangelijua mahali ambako walikuwa wanapelekwa basi wangetamani ndege hiyo ielekee kweli china. Baada ya ya takribani masaa 24 ndege kuwa angani tangu iruke kutoka Bengazhi nchini Libya, hatimaye abiria walisikia ndege ikitua na kugusa Runway ya kiwanja cha ndege mahali fulani dunia walipowasili lakini wakiwa hawafahamu ni mwapi hasa walikuwa. Baada ya matairi ya ndege tu kukanyaga lami za runaway na abiria kufungua ‘pazia’ (shutters) kwenye vioo vilivyopo pemnbeni mwa siti zao na kuangalia nje, mara moja wakaelewa wako wapi. Nje uwanjani kwenye lami, kulikuwa kumesimama lijitu la miraba minne lenye ngozi nyeusi tiiii likiwa na walinzi wa kijeshi na wengine waliovalia nguo za kiraia likiwa limezungukwa pande zote na walinzi hao. Mtu huyu mwenye umbo la kutisha kwa kipindi hiki alikuwa anajulikana ulimwenguni kote kutokana na matendo yake na ukatili wake. Kwa kutupa jicho mara moja tu haukuweza kukosea kujua kuwa pale kwenye lami uwanjani, alikuwa amesimama Generali Nduli Idd Amin Dadaa, ‘Field Marshal’. Swali lilokuwepo vichwani mwao lilikuwa limejibiwa tayari, wamepelekwa kwenye ardhi ya moja ya watawala ‘watemi’ na katili kuwahi kutokea juu ya uso wa dunia. Walikuwa nchini Uganda. Baada ya ndege kusimama abria wote 248 ambao wengi wao walikuwa ni raia wa Israel na wayahudi, walishushwa kutoka kwenye ndege na moja kwa moja kupelekwa ‘terminal’ ambayo kwa wakati huo ilikuwa haitumiki. Mpaka muda huu wakang’amua kwamba hawakuwa ‘abiria’ tena kama ambavyo waliondoka Tel Aviv, bali sasa walikuwa ni mateka wa maharamia haya ya kijerumani, palestina na jeshi la Uganda. Wakati huo huo… Nchini Israel katika jamii ya masuala ya usalama walikuwa wako kwenye bumbuwazi kuu, matukio ya dizaini hii huwa ni ya kushtukiza na yanatokea kipindi ambacho ‘haujajiandaa’. Pia kwa kipindi hiki bado Idara ya Ujasusi ya Mossad hawakuwa na Intelejensia ya kutosha za nchi nyingi za kiafrika, akili yao na nguvu yao yote ilikuwa kwenyekudhibiti juhudi za nchi za kiarabu kufuta Israel kutoka kwenye eneo hilo walilopo. Kwa hiyo kitendo cha raia wao wengi kiasi hiki kutekwa na kupelekwa Africa kilikuwa si tu na changamoto ya namana gani wanawaokoa bali pia kulikuwa na changamoto ya uwepo wa Intelijensia ya kutosha kuhusu eneo la Entebbe, Uganda kuweza kufanya oparesheni yoyote ya kijeshi. Ndipo hapa ambapo waziri mkuu wa kipindi hicho wa Israel Yitzhak Rabin akaitisha kikao cha maafisa wa ngazi za juu wa jeshi na Mossad na kuwauliza swali moja tu, *“…tunafanyeje?”* Itaendelea… #TheBold_Jf
    Like
    1
    · 0 Comments ·0 Shares ·1K Views
  • OPERATION ENTEBBE -4

    Katika sehemmu iliyopita nilieleza namna ambavyo baada ya madege ya kivita ya Lockheed Harcules C-130 kutua katika uwanja wa ndege wa Entebbe na moja ya ndege hizo kwenda moja kwa moja karibu na geti la Terminal huku mlango wa nyuma ukiwa wazi na kutoka gari aina na Mercides pamoja na Land Rover kufanana kabisa na msafara wa Idd Amin atembeleapo uwanja wa ndege, la kini ajabu ni kwamba walijikuta wakinyooshewa bunduki na wanajeshi waliokuwa wanalinda getini…
    Walikuwa hawana taarifa kuwa Amin alikuwa amebadili rangi ya gari yake kutoka nyeusi kwenda nyeupe kabla ya safari yake ya kwenda Mauritius kwenye kikao cha O.A.U.
    Tuendelee…
    SEHEMU TA NNE
    Wanajeshi hawa wawili wa Uganda waliokuwa getini walinyanyua bunduki zao aina ya Kalashnikov na hawakuonyesha dalili kwamba labda walikuwa wanataka kufanya ukaguzi wa kawaida tu kabla ya kuwaruhusu, walionyesha dhahiri kabisa kwamba walikuwa wanataka kufanya shambulio.
    Kabla wanajeshi hao wa Uganda kufanya lolote lile, Netanyahu na komando mwingine ambao walikuwa ndani ya gari walitumia weledi wao kufanya uamuzi makini wa haraka kwa kufyatua risasi kutoka kwenye bastola zao zenye ‘silencer’ na mara moja wale wanajeshi wawili wa Uganda walienda chini.
    Lakini moja ya wale wanajeshi wa Uganda waliodondoka chini baada ya kufyatuliwa risasi, hakufa mara moja na alikuwa anajitahidi kuinuka. Hii ilisababisha komando mwingine wa Israel kufyatua risasi lakini safari hii huyu komando wa Israel alifyatua risasi kutoka kwenye bunduki ambayo haina ‘silencer’. Hii iliwashitua wanajeshi wengine wa Uganda waliokuwa nje ya Terminal na kuanza kukimbilia walipokuwa wanasikia milio ya risasi inatokea huku wanafyatua risasi.
    Kwa maneno mengine ilikuwa kwa kiasi fulani walichokuwa wamekipanga makomando wa Israel, kufanya shambulio la kushitukiza lakini mpaka muda huu tayari ile ‘element of surprise’ ilikuwa haipo tena, jeshi la Uganda lilikuwa limeshitukia ‘mchezo’.
    Bila kuchelewa sana, makomando wote walikuwa kwenye zile gari mbili (Mercedes na Land Rover) waliruka nje ya gari na kukimbia kuelekea ndani ya terminal.
    Vichwani mwao walikuwa bado hawajaondokewa na kumbukumbu ya oparesheni kama hii iliyotokea miaka miwili iliyopita nchini Israel kwenye mji wa Ma’a lot ambapowatekaji wa KIpalestina baada ya kushituka kuwa kulikuwa na makomando wa Israel wamefika kufanya uokozi, waliwapiga risasi mateka wao 25 ambao kati yao 22 walikuwa ni watoto wadogo.
    Hivyo Netanyahu na wenzake hawakutaka kitu kama hiki kjitokeze tena… Netenyahu na makomando wenzake wa Syeret Matkal kwa ustadi wa hali ya juu walikimbia na kuingia ndani ya terminal na kuwaacha vile vikosi vingine kuwadhibiti wanajeshi wa Uganda waliopo nje ya terminal (kama nilivyoeleza juzi namna kikosi kilivyogawanywa kwenye vikundi vidogo kila kimoja kikipewa jukumu lake).
    Mateka wanaeleza kwamba baada ya mpambano ya risasi kuanza huko nje ya terminal waliwaona watekaji kadhaa wakiongozwa na yule aliyeonekana kama kiongozi wao, Wilfred Bose waliingia ndani ya terminal wakiwa wanahaha kama wamechanganyikiwa wasijue wafanye nini, ilionekana dhahiri kuwa walikuwa hawajajiandaa kwa hili shambulio la ghafla, ilionekana dhahiri kwamba katika akili yao walikuwa wanasubiria Israel kutimiza masharti yao ili waweze kuachia mateka.
    Kuna muda Wilfred Bose alionekana kunyoonya bunduki yake kwa mateka kama vile anawataka kuwamininia risasi lakini alikuwa anashindwa kufanya uamuzi huo. Bose aligeuka ghafla baada ya kusikia kishindo cha mlango wa terminal ukifunguliwa.
    Makomando wa Israel walikuwa wametumia weledi na ustadi wao wa hali ya juu kuingia ndani ya terminal kwa muda sahihi kabla ya Wilfred Bose na wenzake kufanya uamuzi wowote wa kuua mateka.
    Makomando wa Israel walipoingia tu ndani ya terminal, mmoja wao mkononi walikuwa na kipaza sauti aina ya ‘megaphone’ na alikuwa anaongeea kwa nguvu kwa lugha ya kihebrania, “Lay down, Lay down. We are Israel soldiers. Lay down. Lay down!!”.
    Mateka wote wa kiisrael hata wale waliokuwa wamekaa kitako walilala chini, hivyo ndani ya sekunde chache tu kila mtu ambaye alibakia amesimama alikuwa ni halali yao kumtandika risasi.
    Kwa bahati mbaya kulikuwa na mateka kadhaa ambao wwalikuwa hawajui kihebreania sawia na hii iliwagharimu sana. Kwa mfano kulikuwa na kijana wa mika 19 aliyeitwa Jean-Jacques Maimoni, huyu alikuwa amehamia Israel siku si nyingi sana kutokea nchini ufaransa. Lilipotolewa tangazo hilo la kila mtu kulala chini hakuelewa na alibakia akiwa amesimama na alitandikwa risasi na makomando wa Israel pamoja na wale watekaji. Kijana huyu hakuwa peke yake, lakini pia kulikuwa na mateka mwingine aliyeitwa Ida Borochovitch, ambaye alihamia Israel kutoka nchini Urusi.
    Risasi zilirindima kwa takribani dakika mbili nzima na baadae ukimya wa kama sekunde 15 ukatawala na moja wa makomando wa kiisrael akauliza kwa kiebrania, “where are the rest of them?” (“wako wapi wengine?”). Mateka wakaonyesha kidole kwenye chumba kidogo kilichopo pembeni.
    Makomando wakarusha mabomu kadhaa ya kutupa kwa mkono na kisha kuingia ndani ya chumba hicho na kuwamiminia risasi wote ambao walikuwa humo.
    Milio ya risasi ndani ya terminal hatimaye ilikuwa imekoma japo bado huko nje walisikia majibizano ya risasi. Mwanajeshi mmoja wa Israel kati ya wale waliopo ndani ya terminal, kwa sauti ya utulivu kabisa na katika lugha ya kihebrania aliwatangazia mateka, “listen guys, we’ve come to take you home!” (“sikilizeni, tumekuja kuwachukua kuwarudisha nyumbani!”).
    Baada ya hapo makomando walianza kuwatoa mateka kutoka kwenye terminal na kuwapakia kwenye ndege kwa tahadhari kubwa huku wale wenzao wengine wakiendelea kuwadhibiti wanajeshi wa Uganda waliokuwa wanarusha risasi kutoka kwenye maeneo ya kujificha ndani ya uwanja wa ndege.
    Wakiwa wanaendelea kuwapakia mateka waliowaokoa kwenye ndege, kumbe kulikuwa na mwanajeshi wa Uganda amebakia juu kwenye mnara wa uongozaji (airport control tower). Kwa mujibu wa taarifa za hivi karibunui kutoka kwa mtoto wa Idd Amin anasema kwamba mwanajeshi huyu alikuwa ni binamu wa Idd Amin. Kutokea hapo kwenye mnara alimimina risasi mfululizo kwa makomando wa Israel na moja ya risasi hizi ilimpaka Koamando Yonatan Netanyahu ambaye ndiye alikuwa kiongozi wa ‘unit’ ya Sayeret Matkal iliyopo hapoa na alipoteza uhai pale pale.
    Wanajeshi wa Isarel walijibu mapigo kwa kurusha bomu la roketi ndogo ya begani na kusambaratisha kabisa kiota cha mnara na kumuua mwanajeshi wa Uganda aliyekuwa anawashambulia.
    Baada ya hapo waliwapakia kwenye ndege mateka wote ambao waliokolewa pamoja na miili ya Waisrael ambao walifariki kwenye majibizano hayo ya risasi.
    Kisha ili kuhakikisha kuwa hakuna ndege itakayowafuatia nyuma wakiondoka au kushambuliwa, walilipua ndege zote za jeshi la Uganda ambazo zilikuwa uwanjani hapo.
    Oparesheni yote hii ilichukua takribani dakika 53 ambapo dakika 30 pekee ndio zilikuwa za mapigano na 23 zilizosalia zilikuwa za kupakia mateka walio okolewa na kuondoka.
    Mpaka kufikia mwishio mwa oparesheni, jumla ya watekaji wote 7 walikuwa wameuwawa, pia wanajeshi 45 wa jeshi la Uganda walikuwa wameuwawa pia. Lakini pia ndege za kijeshi 11 aina ya MiG-17 na Mig-21 zililipuliwa na makomando wa Isarel. Ikumbukwe kwamba ndege hizi ndizo zilikuwa ni ndege zote za kijeshi ambazo zilikuwa zinamilikiwa na jeshi la anga la Uganda. Hii inaonyesha moja kati ya mapungufu makubwa ya kiuongozi ya Amin. Hakukuwa na busara yoyote au faida yoyote ya kimkakati kuweka ndege zote za jeshi lako la anga kwenye uwanja wa ndege wa kiraia ili kulinda mateka wa tukio ambalo wengine walikuwa wanaweza kuliona kama tukio la kigaidi na kwa namna Fulani kama ugomvi ambao ulikuwa haumuhusu moja kwa moja.
    Katika mateka wote 106 waliobakia (kumbuka nilieleza kuwa kulikuwa na mikupuo miwili ya mateka wasio wa Kiisrael au asili ya Kiyahudi waliachiwa kwa kupelekwa na ndege ufaransa nchini), kwahiyo kati ya wale 106 waliobakio, mateka watatu waliuwawa muda wa mapambano (hawa ndio wale ambao walikuwa hawaelewi kihebrania kwa ufasaha na kwa hiyo hawakulalala chini kama ilivyoamrishwa na makomando wa Israel), na mateka mmoja bibi wa miaka 74 aliyeitwa Dora Bloch aliachwa akiwa Hospitali mjini Entebbe ambako alipelekwa na Amin siku kadhaa nyuma kutokana na kuhitaji uangalizi maalumu wa kidaktari.
    Kati ya Makomando wa Isarel, ni mmoja tu ndiye aliuwawa tena dakika za mwisho (Yonatan Netanyahu) japo pia kuna makomando wengine kama watano ambao walijeruhiwa. Kifo cha kiongozi wa ‘unit’ ya Sayeret Mitkal, Yonatan Netanyahu katika oparesheni hii ndio iliyofanya siku kadhaa baadae oparesheni hii pia kubatizwa jina la OPERATION YONATAN kwa heshima yake na ushujaa wake wa kutoa maisha yake ili kutetea na kuooa roho za raia alioapa kuwalinda.
    Baada ya kila kitu kuwekwa sawa na watu wote kupanda ndani ya ndege, waliruka mpaka Nairobi Kenya kwa mapumziko mafupi ili kutibia wale ambao walijeruhiwa (kama ambavyo nilieleza kuwa ile moja ya Boeing 707 iliyotengwa kama ‘hospitali’ ilibaki Nairobi).
    Baada ya matibabu hapo Nairobi, madege yote yaliruka kurudi Israel. Kwa kifupi operation hii was a big SUCCESS.!
    Japokuwa baada ya ulimwengu mzima kutangaziwa juu ya kilichotokea, juu ya ‘umafia’ uliofanywa na Israel, ulimwengu uligawanyika kila nchi ukiunga mkono upande fulani, lakini nchi nyingi ziliunga mkono Israel kwa matumizi ya jeshi katika nchi nyingine, wengi walimlaumu Amin kwa kushindwa kutumia diplomasia kumaliza mzozo huu. Ajabu ni kwamba mwezi huo wa July, Mkuu wa Majeshi wa Iran moja wa mahsimu wa siku zote wa Israel aliandika barua kwa Waziri mkuu wa Israel kumpongeza kuhusu Oparation hiyo na kumpa pole kwa kifo cha Yonatan Netanyahu akimuita Yonatan kumsifu kuwa ni ‘martyr’.
    Vyovyote vile ambavyo unaweza kuitazama oparesheni hii kwenye jicho la kisiasa ua kidiplomasia, kwamba kama ilikuwa ni sahihi au si sahihi lakini katika jicho la kijeshi na ujasusi hii ni moja ya oparesheni murua kabisa kuwahi kufanyika katika historia ya majeshi duniani. Moja ya manguli wa “ulimwengu wa giza”, Bw. Henry Kissinger aliwahi kutamka kuwa hii ilikuwa ni “an immposible mission”!
    Umaridadi wa oparesheni hii umefanya hata vitengo kadhaa vya weledi vya majeshi mbali mbali kutaka kuiga mfano wake lakini bila mafanikio yoyote. Kwa mfano Wamarekani walijaribu kuiga umaridadi wa Oparesheni hii na kufanya ya kwao iliyoitwa Oparation Eagle Claw baada ya kutokea kwa utekeaji kwenye ubalozi wa Iran lakini oparesheni hiyo ilifeli vibaya.
    Sasa hivi kama wewe ni mwanajeshi katika jeshi fulani kwenye kitengo cha weledi (special force) au labda ni jasusi maalumu, lazima katika hatua fulani ya japo hata ‘darasani’ kwenye makaratasi utafundwa kuhusu Oparetion Entebbe na namna ilivyo tekelezwa.
    Oparesheni hii ilimuacha Amin na aibu kubwa kiasi kwamba akaendelea kufanya vitu ambavyo vilidhihirisha udhaifu wake wa kiungozi. Kwa mfano, yule bibi wa miaka 74 aliyeachwa hospitali mjini Entebbe, aliamuru auwawe kinyama. Lakini pia Amin alisimami kuwawa kwa McKenzie yule waziri wa kilimo wa Kenya ambaye alimsaidia Ehud Barak kumshinikiza Mzee Jomo Kenyetta kuruhusu ndege za jeshi la Israel kutumia viwanja vya ndege vya Kenya wakati wa utekelezaji wa OParesheni hiyo na pia kumsaidi kukusanya Intelijensia kwa kutumia ndege yake binafsi.
    McKenzie aliuwawa kwa bomu lililotegwa kwenye gari yake.
    Pia Amin alisimamia ulipuaji kwa bomu moja ya hoteli kubwa Nairobi kipindi hicho ambayo ilikuwa inaitwa The Norfolk Hotel, ambayo ilimilikiwa na moja ya wayahudi mashuhuri nchini Kenya.
    [6/12, 13:48] The Bold: Licha ya ‘fujo’ zote hizi ambazo Amin alizifanya baada ya jeshi lake kudhalilika kutokana na Oeration Entebbe lakini hatupawsi kusahau kwamba chini ya miaka mitatu baadae, yaani baada ya utekelezaji wa opareshini hii, Idd Amin aliondolewa kwa aibu madarakani na majeshi ya Tanzania na kumfanya akimbie nchi yake.

    ......................MWISHO..............
    #TheBOLD_JF
    OPERATION ENTEBBE -4 Katika sehemmu iliyopita nilieleza namna ambavyo baada ya madege ya kivita ya Lockheed Harcules C-130 kutua katika uwanja wa ndege wa Entebbe na moja ya ndege hizo kwenda moja kwa moja karibu na geti la Terminal huku mlango wa nyuma ukiwa wazi na kutoka gari aina na Mercides pamoja na Land Rover kufanana kabisa na msafara wa Idd Amin atembeleapo uwanja wa ndege, la kini ajabu ni kwamba walijikuta wakinyooshewa bunduki na wanajeshi waliokuwa wanalinda getini… Walikuwa hawana taarifa kuwa Amin alikuwa amebadili rangi ya gari yake kutoka nyeusi kwenda nyeupe kabla ya safari yake ya kwenda Mauritius kwenye kikao cha O.A.U. Tuendelee… SEHEMU TA NNE Wanajeshi hawa wawili wa Uganda waliokuwa getini walinyanyua bunduki zao aina ya Kalashnikov na hawakuonyesha dalili kwamba labda walikuwa wanataka kufanya ukaguzi wa kawaida tu kabla ya kuwaruhusu, walionyesha dhahiri kabisa kwamba walikuwa wanataka kufanya shambulio. Kabla wanajeshi hao wa Uganda kufanya lolote lile, Netanyahu na komando mwingine ambao walikuwa ndani ya gari walitumia weledi wao kufanya uamuzi makini wa haraka kwa kufyatua risasi kutoka kwenye bastola zao zenye ‘silencer’ na mara moja wale wanajeshi wawili wa Uganda walienda chini. Lakini moja ya wale wanajeshi wa Uganda waliodondoka chini baada ya kufyatuliwa risasi, hakufa mara moja na alikuwa anajitahidi kuinuka. Hii ilisababisha komando mwingine wa Israel kufyatua risasi lakini safari hii huyu komando wa Israel alifyatua risasi kutoka kwenye bunduki ambayo haina ‘silencer’. Hii iliwashitua wanajeshi wengine wa Uganda waliokuwa nje ya Terminal na kuanza kukimbilia walipokuwa wanasikia milio ya risasi inatokea huku wanafyatua risasi. Kwa maneno mengine ilikuwa kwa kiasi fulani walichokuwa wamekipanga makomando wa Israel, kufanya shambulio la kushitukiza lakini mpaka muda huu tayari ile ‘element of surprise’ ilikuwa haipo tena, jeshi la Uganda lilikuwa limeshitukia ‘mchezo’. Bila kuchelewa sana, makomando wote walikuwa kwenye zile gari mbili (Mercedes na Land Rover) waliruka nje ya gari na kukimbia kuelekea ndani ya terminal. Vichwani mwao walikuwa bado hawajaondokewa na kumbukumbu ya oparesheni kama hii iliyotokea miaka miwili iliyopita nchini Israel kwenye mji wa Ma’a lot ambapowatekaji wa KIpalestina baada ya kushituka kuwa kulikuwa na makomando wa Israel wamefika kufanya uokozi, waliwapiga risasi mateka wao 25 ambao kati yao 22 walikuwa ni watoto wadogo. Hivyo Netanyahu na wenzake hawakutaka kitu kama hiki kjitokeze tena… Netenyahu na makomando wenzake wa Syeret Matkal kwa ustadi wa hali ya juu walikimbia na kuingia ndani ya terminal na kuwaacha vile vikosi vingine kuwadhibiti wanajeshi wa Uganda waliopo nje ya terminal (kama nilivyoeleza juzi namna kikosi kilivyogawanywa kwenye vikundi vidogo kila kimoja kikipewa jukumu lake). Mateka wanaeleza kwamba baada ya mpambano ya risasi kuanza huko nje ya terminal waliwaona watekaji kadhaa wakiongozwa na yule aliyeonekana kama kiongozi wao, Wilfred Bose waliingia ndani ya terminal wakiwa wanahaha kama wamechanganyikiwa wasijue wafanye nini, ilionekana dhahiri kuwa walikuwa hawajajiandaa kwa hili shambulio la ghafla, ilionekana dhahiri kwamba katika akili yao walikuwa wanasubiria Israel kutimiza masharti yao ili waweze kuachia mateka. Kuna muda Wilfred Bose alionekana kunyoonya bunduki yake kwa mateka kama vile anawataka kuwamininia risasi lakini alikuwa anashindwa kufanya uamuzi huo. Bose aligeuka ghafla baada ya kusikia kishindo cha mlango wa terminal ukifunguliwa. Makomando wa Israel walikuwa wametumia weledi na ustadi wao wa hali ya juu kuingia ndani ya terminal kwa muda sahihi kabla ya Wilfred Bose na wenzake kufanya uamuzi wowote wa kuua mateka. Makomando wa Israel walipoingia tu ndani ya terminal, mmoja wao mkononi walikuwa na kipaza sauti aina ya ‘megaphone’ na alikuwa anaongeea kwa nguvu kwa lugha ya kihebrania, “Lay down, Lay down. We are Israel soldiers. Lay down. Lay down!!”. Mateka wote wa kiisrael hata wale waliokuwa wamekaa kitako walilala chini, hivyo ndani ya sekunde chache tu kila mtu ambaye alibakia amesimama alikuwa ni halali yao kumtandika risasi. Kwa bahati mbaya kulikuwa na mateka kadhaa ambao wwalikuwa hawajui kihebreania sawia na hii iliwagharimu sana. Kwa mfano kulikuwa na kijana wa mika 19 aliyeitwa Jean-Jacques Maimoni, huyu alikuwa amehamia Israel siku si nyingi sana kutokea nchini ufaransa. Lilipotolewa tangazo hilo la kila mtu kulala chini hakuelewa na alibakia akiwa amesimama na alitandikwa risasi na makomando wa Israel pamoja na wale watekaji. Kijana huyu hakuwa peke yake, lakini pia kulikuwa na mateka mwingine aliyeitwa Ida Borochovitch, ambaye alihamia Israel kutoka nchini Urusi. Risasi zilirindima kwa takribani dakika mbili nzima na baadae ukimya wa kama sekunde 15 ukatawala na moja wa makomando wa kiisrael akauliza kwa kiebrania, “where are the rest of them?” (“wako wapi wengine?”). Mateka wakaonyesha kidole kwenye chumba kidogo kilichopo pembeni. Makomando wakarusha mabomu kadhaa ya kutupa kwa mkono na kisha kuingia ndani ya chumba hicho na kuwamiminia risasi wote ambao walikuwa humo. Milio ya risasi ndani ya terminal hatimaye ilikuwa imekoma japo bado huko nje walisikia majibizano ya risasi. Mwanajeshi mmoja wa Israel kati ya wale waliopo ndani ya terminal, kwa sauti ya utulivu kabisa na katika lugha ya kihebrania aliwatangazia mateka, “listen guys, we’ve come to take you home!” (“sikilizeni, tumekuja kuwachukua kuwarudisha nyumbani!”). Baada ya hapo makomando walianza kuwatoa mateka kutoka kwenye terminal na kuwapakia kwenye ndege kwa tahadhari kubwa huku wale wenzao wengine wakiendelea kuwadhibiti wanajeshi wa Uganda waliokuwa wanarusha risasi kutoka kwenye maeneo ya kujificha ndani ya uwanja wa ndege. Wakiwa wanaendelea kuwapakia mateka waliowaokoa kwenye ndege, kumbe kulikuwa na mwanajeshi wa Uganda amebakia juu kwenye mnara wa uongozaji (airport control tower). Kwa mujibu wa taarifa za hivi karibunui kutoka kwa mtoto wa Idd Amin anasema kwamba mwanajeshi huyu alikuwa ni binamu wa Idd Amin. Kutokea hapo kwenye mnara alimimina risasi mfululizo kwa makomando wa Israel na moja ya risasi hizi ilimpaka Koamando Yonatan Netanyahu ambaye ndiye alikuwa kiongozi wa ‘unit’ ya Sayeret Matkal iliyopo hapoa na alipoteza uhai pale pale. Wanajeshi wa Isarel walijibu mapigo kwa kurusha bomu la roketi ndogo ya begani na kusambaratisha kabisa kiota cha mnara na kumuua mwanajeshi wa Uganda aliyekuwa anawashambulia. Baada ya hapo waliwapakia kwenye ndege mateka wote ambao waliokolewa pamoja na miili ya Waisrael ambao walifariki kwenye majibizano hayo ya risasi. Kisha ili kuhakikisha kuwa hakuna ndege itakayowafuatia nyuma wakiondoka au kushambuliwa, walilipua ndege zote za jeshi la Uganda ambazo zilikuwa uwanjani hapo. Oparesheni yote hii ilichukua takribani dakika 53 ambapo dakika 30 pekee ndio zilikuwa za mapigano na 23 zilizosalia zilikuwa za kupakia mateka walio okolewa na kuondoka. Mpaka kufikia mwishio mwa oparesheni, jumla ya watekaji wote 7 walikuwa wameuwawa, pia wanajeshi 45 wa jeshi la Uganda walikuwa wameuwawa pia. Lakini pia ndege za kijeshi 11 aina ya MiG-17 na Mig-21 zililipuliwa na makomando wa Isarel. Ikumbukwe kwamba ndege hizi ndizo zilikuwa ni ndege zote za kijeshi ambazo zilikuwa zinamilikiwa na jeshi la anga la Uganda. Hii inaonyesha moja kati ya mapungufu makubwa ya kiuongozi ya Amin. Hakukuwa na busara yoyote au faida yoyote ya kimkakati kuweka ndege zote za jeshi lako la anga kwenye uwanja wa ndege wa kiraia ili kulinda mateka wa tukio ambalo wengine walikuwa wanaweza kuliona kama tukio la kigaidi na kwa namna Fulani kama ugomvi ambao ulikuwa haumuhusu moja kwa moja. Katika mateka wote 106 waliobakia (kumbuka nilieleza kuwa kulikuwa na mikupuo miwili ya mateka wasio wa Kiisrael au asili ya Kiyahudi waliachiwa kwa kupelekwa na ndege ufaransa nchini), kwahiyo kati ya wale 106 waliobakio, mateka watatu waliuwawa muda wa mapambano (hawa ndio wale ambao walikuwa hawaelewi kihebrania kwa ufasaha na kwa hiyo hawakulalala chini kama ilivyoamrishwa na makomando wa Israel), na mateka mmoja bibi wa miaka 74 aliyeitwa Dora Bloch aliachwa akiwa Hospitali mjini Entebbe ambako alipelekwa na Amin siku kadhaa nyuma kutokana na kuhitaji uangalizi maalumu wa kidaktari. Kati ya Makomando wa Isarel, ni mmoja tu ndiye aliuwawa tena dakika za mwisho (Yonatan Netanyahu) japo pia kuna makomando wengine kama watano ambao walijeruhiwa. Kifo cha kiongozi wa ‘unit’ ya Sayeret Mitkal, Yonatan Netanyahu katika oparesheni hii ndio iliyofanya siku kadhaa baadae oparesheni hii pia kubatizwa jina la OPERATION YONATAN kwa heshima yake na ushujaa wake wa kutoa maisha yake ili kutetea na kuooa roho za raia alioapa kuwalinda. Baada ya kila kitu kuwekwa sawa na watu wote kupanda ndani ya ndege, waliruka mpaka Nairobi Kenya kwa mapumziko mafupi ili kutibia wale ambao walijeruhiwa (kama ambavyo nilieleza kuwa ile moja ya Boeing 707 iliyotengwa kama ‘hospitali’ ilibaki Nairobi). Baada ya matibabu hapo Nairobi, madege yote yaliruka kurudi Israel. Kwa kifupi operation hii was a big SUCCESS.! Japokuwa baada ya ulimwengu mzima kutangaziwa juu ya kilichotokea, juu ya ‘umafia’ uliofanywa na Israel, ulimwengu uligawanyika kila nchi ukiunga mkono upande fulani, lakini nchi nyingi ziliunga mkono Israel kwa matumizi ya jeshi katika nchi nyingine, wengi walimlaumu Amin kwa kushindwa kutumia diplomasia kumaliza mzozo huu. Ajabu ni kwamba mwezi huo wa July, Mkuu wa Majeshi wa Iran moja wa mahsimu wa siku zote wa Israel aliandika barua kwa Waziri mkuu wa Israel kumpongeza kuhusu Oparation hiyo na kumpa pole kwa kifo cha Yonatan Netanyahu akimuita Yonatan kumsifu kuwa ni ‘martyr’. Vyovyote vile ambavyo unaweza kuitazama oparesheni hii kwenye jicho la kisiasa ua kidiplomasia, kwamba kama ilikuwa ni sahihi au si sahihi lakini katika jicho la kijeshi na ujasusi hii ni moja ya oparesheni murua kabisa kuwahi kufanyika katika historia ya majeshi duniani. Moja ya manguli wa “ulimwengu wa giza”, Bw. Henry Kissinger aliwahi kutamka kuwa hii ilikuwa ni “an immposible mission”! Umaridadi wa oparesheni hii umefanya hata vitengo kadhaa vya weledi vya majeshi mbali mbali kutaka kuiga mfano wake lakini bila mafanikio yoyote. Kwa mfano Wamarekani walijaribu kuiga umaridadi wa Oparesheni hii na kufanya ya kwao iliyoitwa Oparation Eagle Claw baada ya kutokea kwa utekeaji kwenye ubalozi wa Iran lakini oparesheni hiyo ilifeli vibaya. Sasa hivi kama wewe ni mwanajeshi katika jeshi fulani kwenye kitengo cha weledi (special force) au labda ni jasusi maalumu, lazima katika hatua fulani ya japo hata ‘darasani’ kwenye makaratasi utafundwa kuhusu Oparetion Entebbe na namna ilivyo tekelezwa. Oparesheni hii ilimuacha Amin na aibu kubwa kiasi kwamba akaendelea kufanya vitu ambavyo vilidhihirisha udhaifu wake wa kiungozi. Kwa mfano, yule bibi wa miaka 74 aliyeachwa hospitali mjini Entebbe, aliamuru auwawe kinyama. Lakini pia Amin alisimami kuwawa kwa McKenzie yule waziri wa kilimo wa Kenya ambaye alimsaidia Ehud Barak kumshinikiza Mzee Jomo Kenyetta kuruhusu ndege za jeshi la Israel kutumia viwanja vya ndege vya Kenya wakati wa utekelezaji wa OParesheni hiyo na pia kumsaidi kukusanya Intelijensia kwa kutumia ndege yake binafsi. McKenzie aliuwawa kwa bomu lililotegwa kwenye gari yake. Pia Amin alisimamia ulipuaji kwa bomu moja ya hoteli kubwa Nairobi kipindi hicho ambayo ilikuwa inaitwa The Norfolk Hotel, ambayo ilimilikiwa na moja ya wayahudi mashuhuri nchini Kenya. [6/12, 13:48] The Bold: Licha ya ‘fujo’ zote hizi ambazo Amin alizifanya baada ya jeshi lake kudhalilika kutokana na Oeration Entebbe lakini hatupawsi kusahau kwamba chini ya miaka mitatu baadae, yaani baada ya utekelezaji wa opareshini hii, Idd Amin aliondolewa kwa aibu madarakani na majeshi ya Tanzania na kumfanya akimbie nchi yake. ......................MWISHO.............. #TheBOLD_JF
    0 Comments ·0 Shares ·2K Views
  • Mnamo Mwaka 2006, wiki kadhaa baada ya kustaafu nafasi ya ukatibu mkuu, Kofi Annan alienda nchini Italia kwa ajili ya mapumziko.

    Akiwa huko, Siku moja aliamua kutoka nje kidogo na kwenda kununua gazeti, lakini ghafla akashangaa Watu wengi wanamzonga. Lengo lao ni kutaka sahihi kutoka kwake. (Kama uonavyo nyota wa filamu au wachezaji mpira, wanavyochora sahihi zao kwenye mashati ya wafuasi).

    Lakini kumbe, Watu hao walimfananisha Kofi Annan na yule nyota wa filamu wa marekani bwana Morgan Freeman .

    Ila, kwa kutotaka kuwaangusha Watu hao, Kofi Annan alichora sahihi kwa kutumia jina la Freeman.

    (Angalia picha zao)

    Koffi Anan, alifaliki akiwa na umri wa miaka 80 huko nchini Switzerland.

    Alihudumu nafasi ya ukatibu mkuu kwanzia Mwaka 1997 hadi 2006, akiwa ndiye mwafrika mweusi wa kwanza kushika nafasi hiyo.

    RIP koffi Annan.
    Mnamo Mwaka 2006, wiki kadhaa baada ya kustaafu nafasi ya ukatibu mkuu, Kofi Annan alienda nchini Italia kwa ajili ya mapumziko. Akiwa huko, Siku moja aliamua kutoka nje kidogo na kwenda kununua gazeti, lakini ghafla akashangaa Watu wengi wanamzonga. Lengo lao ni kutaka sahihi kutoka kwake. (Kama uonavyo nyota wa filamu au wachezaji mpira, wanavyochora sahihi zao kwenye mashati ya wafuasi). Lakini kumbe, Watu hao walimfananisha Kofi Annan na yule nyota wa filamu wa marekani bwana Morgan Freeman . Ila, kwa kutotaka kuwaangusha Watu hao, Kofi Annan alichora sahihi kwa kutumia jina la Freeman. (Angalia picha zao) Koffi Anan, alifaliki akiwa na umri wa miaka 80 huko nchini Switzerland. Alihudumu nafasi ya ukatibu mkuu kwanzia Mwaka 1997 hadi 2006, akiwa ndiye mwafrika mweusi wa kwanza kushika nafasi hiyo. RIP koffi Annan.
    Like
    2
    · 0 Comments ·0 Shares ·294 Views
  • VITA FUPI.

    Je unaifahamu vita fupi kuliko zote kuwahi kutokea duniani?.

    Kama hufahamu, basi leo inabidi ujue kwamba miaka 122 iliyopita, kulitokea vita iliyodumu kwa dakika 38 tu, na hivyo kuweka rekodi ya kuwa ndio vita fupi kuliko zote kuwahi kutokea duniani. Vita hiyo iliyojulikana kama 'Anglo- Zanzibar war' iliyotokea mwaka 1896 kati ya uingereza na Zanzibar, ikipiganwa katika ardhi ya Zanzibar iliyokuwa chini ya utawala wa kisultani.

    Kabla ya kuelezea vita hiyo, kwanza inabidi tufahamu jinsi historia ya Zanzibar hapo kabla ya mwaka 1698 ambapo ilikuwa chini ya utawala wa wareno waliotawala hapo kuanzia mwishoni mwa miaka 1490.

    Wareno hao waliondoka baada ya ujio wa waarabu kutoka Oman, waliokuja pwani ya Afrika Mashariki mnamo mwaka 1698. Hivyo kuanzia hapo, Zanzibar ikawa ni sehemu ya himaya ya Oman, ikiongozwa na masultani walioko mjini Muscat, Oman. Ilipofika mwaka 1804, Oman ikapata sultan mpya, aitwaye Sayyid Said ambaye aliweza kuanzisha mashamba ya mikarafuu huku akiwatumia watumwa kutoka Tanganyika wakitumika kama nguvu kazi katika mashamba hayo.

    Mwaka 1832, Sultan Sayyid Said alihamisha mji mkuu wa Omani kutoka Muskat kwenda Unguja. Hiyo ikapelekea ukuaji wa maendeleo katika mji wa Unguja kutokana na watu wengi kufurika hapo wakitoka sehemu mbalimbali ikiwemo Oman. Nchi mbalimbali zikaanza kujenga balozi zao hapo Zanzibar, mfano Marekani ilijenga balozi yake mwaka 1837, Uingereza mwaka 1841 kisha Ufaransa mwaka 1844.

    Ilipofika mwaka 1840, Sultani Sayyid said alihama kabisa mjini Muskat na kuja kuishi Zanzibar huku akiendelea kujulikana kama Sultan wa Oman na Zanzibar hadi mwaka alipofariki mwaka 1856. Baada ya kufariki Sayyid Said, waliokuwa watoto wake Majid bin Said na mwingine aliyeitwa Thuwaini bin Said, wakaanza mgogoro kuhusu nani wa kurithi kiti cha usultani wa Oman.

    Mgogoro huo ulipelekea himaya ya Oman kugawanyika katika sehemu mbili, Thuwaini bin Said alichukua Oman na hivyo kuwa Sultani wa Oman. Lakini Majid bin Said akiichukua Zanzibar na hivyo kuwa Sultani wa kwanza wa Zanzibar.

    Sultan Majid bin Said alitawala Zanzibar hadi mwaka 1870, akifuatiwa na sultan Barghash ambaye kwa kushirikiana na waingereza anakumbukwa kwa kusitisha biashara ya watumwa hapo Zanzibar mwaka 1876 japokuwa utumwa ulikuwa unaendelea.

    Mnamo mwaka 1890, kulisainiwa mkataba baina ya ujerumani na uingereza uliojulikana kama mkataba wa Heligoland uliopelekea Zanzibar kuwa chini ya uangalizi wa Uingereza huku ikiendelea kuongozwa na Sultani. Mwaka 1893 Uingereza 'ilifanya figisu' na hatimaye kumpandikiza kibaraka wao, Hamad bin Thuwaini kuwa sultani mpya wa Zanzibar, akitawala kwa miaka mitatu hadi tarehe 25 Agosti 1896 alipofariki ghafla akiwa ofisini kwake. Ingawa kuna tetesi kwamba aliyesababisha kifo chake ni binamu yake aitwaye Khalid bin Barghash ambaye inasemekana kuwa alimtilia sumu kwenye chakula.

    Tetesi hizo zilionekana ni kweli kutokana na kitendo cha Khalid bin Barghash kurithi kiti cha usultani punde tuu baada ya kifo cha nduguye akifanya hivyo bila ya kuthibitishwa na serikali ya uingereza.Maana ilikuwa ni kanuni kwamba serikali ya uingereza lazima ipitishe mchakato wa kumpata sultani.

    Kitendo cha Khalid bin Barghash kujitwalia madaraka ya kisultani, kiliwafanya waingereza kuchukia sana. Hivyo aliyekuwa balozi wa uingereza nchini Zanzibar, Basil Cave alimpa onyo kali sana sultan Khalid akitaka aachie madaraka. Waingereza walimpendelea Hamud bin Muhammed, awe sultani kwasababu waliona huyo ndiye wangeweza kufanya nae kazi vizuri kwani watamfanya kama kibaraka wao.

    Kitendo cha Khalid bin Barghash kujitwalia madaraka ya kisultani, kiliwafanya waingereza kuchukia sana. Hivyo aliyekuwa balozi wa uingereza nchini Zanzibar, Basil Cave alimpa onyo kali sana sultan Khalid akitaka aachie madaraka. Waingereza walimpendelea Hamud bin Muhammed, awe sultani kwasababu waliona huyo ndiye wangeweza kufanya nae kazi vizuri kwani watamfanya kama kibaraka wao.

    Mgogoro ulikuwa mkubwa baada ya Sultan Khalid bin Barghash kukaidi kuachia madaraka, badala yake akazidi kujiimarisha kiulinzi kwa kuongeza askari 3000 kwa ajili ya kulinda kasri yake.

    Wakati huohuo, uingereza nao walikuwa tayari wameshatega meli zao za kivita kwenye bandari huku wanajeshi wakisambazwa sehemu mbalimbali kwa ajili ya kujiandaa na lolote litakalotokea. Basil Cave aliwasiliana na makao makuu huko London akiomba aongezewe meli nyingine ya kivita. Hatimaye meli aina ya HMS Sparrow ikitia nanga katika bandari ya Zanzibar.

    Japokuwa alikuwa tayari kwa pambano, Basil Cave hakuwa na mamlaka ya kuanzisha vita pasipo kupokea amri kutoka makao makuu Uingereza. Akatuma ujumbe makao makuu akisema hivi;

    *_" Tumefanya njia zote za amani lakini zimeshindikana, sasa tunaruhusiwa kuanza mashambulizi??"*_

    Wakati anasubiria majibu kutoka makao makuu, Cave alituma tena ujumbe kwa Sultani akimtaka aachie madaraka, lakini Sultan hakujibu.

    Siku iliyofuata Cave alipokea majibu kutoka makao makuu ukisema kwamba, *" unaruhusiwa kufanya chochote unachodhani kinafaa na sisi tutakupa ushirikiano."*

    Wakati huohuo tuliona meli zingine za kivita zinaingia Zanzibar zikitokea uingereza.

    Usiku wa tarehe 26, Basil Cave akatuma Ujumbe wa mwisho kwa sultani akimtaka kuondoka ofisini kesho yake saa tatu asubuhi. Huku akiziamuru boti zote zisizo za kivita ziondolewe baharini ili kujiandaa na vita.

    Siku iliyofuata saa 2 asubuhi, Sultani Khalid akajibu, akasema hivi, *" Sina mpango wa kuachia madaraka na sitegemei kama mtaanzisha vita dhidi yetu"*

    Basil Cave naye akajibu akasema;
    "Hatuna haja ya kuanzisha vita, ila tutafanya hivyo kama ukikaidi maagizo yetu."

    Sultani hakujibu tena. Na ilipofika saa 3 kamili meli zote za kivita zilipokea amri ya kuanza kushambulia kasri ya sultani. Saa 3:02 asubuhi, majengo na silaha za Sultani zilianza kulipuliwa, huku majeshi ya sultani nayo yakijibu mashambulizi kwa kurusha makombora yao.

    Inaelezwa kwamba dakika chache tuu baada ya kuanza kwa mashambulizi, Sultan Khalid *alitoroka kupitia mlango wa nyuma* wa kasri hiyo akiwaacha wapiganaji wake wakiendelea na vita. Hadi kufikia saa 3:40, sehemu kubwa ya kasri ya sultani ilikuwa tayari imeshalipuliwa na bendera ya sultani ikashushwa.

    Na hapo ndipo ikawa mwisho wa vita hiyo fupi.

    Katika vita hiyo fupi, inaelezwa kwamba wapiganaji 500 wa sultani walifariki na kujeruhiwa huku mwanajeshi mmoja tuu wa kingereza alijeruhiwa lakini akapona baadae.

    Baada ya sultan Khalid kukimbia, ndipo Uingereza ikampitisha mtu wao *Hamud bin Muhammed,* kuwa sultani wa Zanzibar kwa miaka 6 iliyofuata.

    Inaelezwa kwamba Khalid alipotoroka kumbe alipewa hifadhi na balozi ya ujerumani hapo Zanzibar na kisha baadae akasafirishwa na meli za wajerumani kuja Tanganyika (koloni la ujerumani)

    Ilipofika mwaka 1916, wakati wa vita ya kwanza ya dunia tuliona majeshi ya Uingereza yanavamia makoloni ya ujerumani ikiwemo Tanganyika, ambapo *Khalid* alikamatwa na kupelekwa Seychelles , lakini baada ya miaka michache alirudishwa Mombasa ambapo alifariki Mwaka 1927.

    ***

    Na hiyo ndiyo vita fupi kuliko zote kuwahi kutokea Duniani.

    VITA FUPI. Je unaifahamu vita fupi kuliko zote kuwahi kutokea duniani?. Kama hufahamu, basi leo inabidi ujue kwamba miaka 122 iliyopita, kulitokea vita iliyodumu kwa dakika 38 tu, na hivyo kuweka rekodi ya kuwa ndio vita fupi kuliko zote kuwahi kutokea duniani. Vita hiyo iliyojulikana kama 'Anglo- Zanzibar war' iliyotokea mwaka 1896 kati ya uingereza na Zanzibar, ikipiganwa katika ardhi ya Zanzibar iliyokuwa chini ya utawala wa kisultani. Kabla ya kuelezea vita hiyo, kwanza inabidi tufahamu jinsi historia ya Zanzibar hapo kabla ya mwaka 1698 ambapo ilikuwa chini ya utawala wa wareno waliotawala hapo kuanzia mwishoni mwa miaka 1490. Wareno hao waliondoka baada ya ujio wa waarabu kutoka Oman, waliokuja pwani ya Afrika Mashariki mnamo mwaka 1698. Hivyo kuanzia hapo, Zanzibar ikawa ni sehemu ya himaya ya Oman, ikiongozwa na masultani walioko mjini Muscat, Oman. Ilipofika mwaka 1804, Oman ikapata sultan mpya, aitwaye Sayyid Said ambaye aliweza kuanzisha mashamba ya mikarafuu huku akiwatumia watumwa kutoka Tanganyika wakitumika kama nguvu kazi katika mashamba hayo. Mwaka 1832, Sultan Sayyid Said alihamisha mji mkuu wa Omani kutoka Muskat kwenda Unguja. Hiyo ikapelekea ukuaji wa maendeleo katika mji wa Unguja kutokana na watu wengi kufurika hapo wakitoka sehemu mbalimbali ikiwemo Oman. Nchi mbalimbali zikaanza kujenga balozi zao hapo Zanzibar, mfano Marekani ilijenga balozi yake mwaka 1837, Uingereza mwaka 1841 kisha Ufaransa mwaka 1844. Ilipofika mwaka 1840, Sultani Sayyid said alihama kabisa mjini Muskat na kuja kuishi Zanzibar huku akiendelea kujulikana kama Sultan wa Oman na Zanzibar hadi mwaka alipofariki mwaka 1856. Baada ya kufariki Sayyid Said, waliokuwa watoto wake Majid bin Said na mwingine aliyeitwa Thuwaini bin Said, wakaanza mgogoro kuhusu nani wa kurithi kiti cha usultani wa Oman. Mgogoro huo ulipelekea himaya ya Oman kugawanyika katika sehemu mbili, Thuwaini bin Said alichukua Oman na hivyo kuwa Sultani wa Oman. Lakini Majid bin Said akiichukua Zanzibar na hivyo kuwa Sultani wa kwanza wa Zanzibar. Sultan Majid bin Said alitawala Zanzibar hadi mwaka 1870, akifuatiwa na sultan Barghash ambaye kwa kushirikiana na waingereza anakumbukwa kwa kusitisha biashara ya watumwa hapo Zanzibar mwaka 1876 japokuwa utumwa ulikuwa unaendelea. Mnamo mwaka 1890, kulisainiwa mkataba baina ya ujerumani na uingereza uliojulikana kama mkataba wa Heligoland uliopelekea Zanzibar kuwa chini ya uangalizi wa Uingereza huku ikiendelea kuongozwa na Sultani. Mwaka 1893 Uingereza 'ilifanya figisu' na hatimaye kumpandikiza kibaraka wao, Hamad bin Thuwaini kuwa sultani mpya wa Zanzibar, akitawala kwa miaka mitatu hadi tarehe 25 Agosti 1896 alipofariki ghafla akiwa ofisini kwake. Ingawa kuna tetesi kwamba aliyesababisha kifo chake ni binamu yake aitwaye Khalid bin Barghash ambaye inasemekana kuwa alimtilia sumu kwenye chakula. Tetesi hizo zilionekana ni kweli kutokana na kitendo cha Khalid bin Barghash kurithi kiti cha usultani punde tuu baada ya kifo cha nduguye akifanya hivyo bila ya kuthibitishwa na serikali ya uingereza.Maana ilikuwa ni kanuni kwamba serikali ya uingereza lazima ipitishe mchakato wa kumpata sultani. Kitendo cha Khalid bin Barghash kujitwalia madaraka ya kisultani, kiliwafanya waingereza kuchukia sana. Hivyo aliyekuwa balozi wa uingereza nchini Zanzibar, Basil Cave alimpa onyo kali sana sultan Khalid akitaka aachie madaraka. Waingereza walimpendelea Hamud bin Muhammed, awe sultani kwasababu waliona huyo ndiye wangeweza kufanya nae kazi vizuri kwani watamfanya kama kibaraka wao. Kitendo cha Khalid bin Barghash kujitwalia madaraka ya kisultani, kiliwafanya waingereza kuchukia sana. Hivyo aliyekuwa balozi wa uingereza nchini Zanzibar, Basil Cave alimpa onyo kali sana sultan Khalid akitaka aachie madaraka. Waingereza walimpendelea Hamud bin Muhammed, awe sultani kwasababu waliona huyo ndiye wangeweza kufanya nae kazi vizuri kwani watamfanya kama kibaraka wao. Mgogoro ulikuwa mkubwa baada ya Sultan Khalid bin Barghash kukaidi kuachia madaraka, badala yake akazidi kujiimarisha kiulinzi kwa kuongeza askari 3000 kwa ajili ya kulinda kasri yake. Wakati huohuo, uingereza nao walikuwa tayari wameshatega meli zao za kivita kwenye bandari huku wanajeshi wakisambazwa sehemu mbalimbali kwa ajili ya kujiandaa na lolote litakalotokea. Basil Cave aliwasiliana na makao makuu huko London akiomba aongezewe meli nyingine ya kivita. Hatimaye meli aina ya HMS Sparrow ikitia nanga katika bandari ya Zanzibar. Japokuwa alikuwa tayari kwa pambano, Basil Cave hakuwa na mamlaka ya kuanzisha vita pasipo kupokea amri kutoka makao makuu Uingereza. Akatuma ujumbe makao makuu akisema hivi; *_" Tumefanya njia zote za amani lakini zimeshindikana, sasa tunaruhusiwa kuanza mashambulizi??"*_ Wakati anasubiria majibu kutoka makao makuu, Cave alituma tena ujumbe kwa Sultani akimtaka aachie madaraka, lakini Sultan hakujibu. Siku iliyofuata Cave alipokea majibu kutoka makao makuu ukisema kwamba, *" unaruhusiwa kufanya chochote unachodhani kinafaa na sisi tutakupa ushirikiano."* Wakati huohuo tuliona meli zingine za kivita zinaingia Zanzibar zikitokea uingereza. Usiku wa tarehe 26, Basil Cave akatuma Ujumbe wa mwisho kwa sultani akimtaka kuondoka ofisini kesho yake saa tatu asubuhi. Huku akiziamuru boti zote zisizo za kivita ziondolewe baharini ili kujiandaa na vita. Siku iliyofuata saa 2 asubuhi, Sultani Khalid akajibu, akasema hivi, *" Sina mpango wa kuachia madaraka na sitegemei kama mtaanzisha vita dhidi yetu"* Basil Cave naye akajibu akasema; "Hatuna haja ya kuanzisha vita, ila tutafanya hivyo kama ukikaidi maagizo yetu." Sultani hakujibu tena. Na ilipofika saa 3 kamili meli zote za kivita zilipokea amri ya kuanza kushambulia kasri ya sultani. Saa 3:02 asubuhi, majengo na silaha za Sultani zilianza kulipuliwa, huku majeshi ya sultani nayo yakijibu mashambulizi kwa kurusha makombora yao. Inaelezwa kwamba dakika chache tuu baada ya kuanza kwa mashambulizi, Sultan Khalid *alitoroka kupitia mlango wa nyuma* wa kasri hiyo akiwaacha wapiganaji wake wakiendelea na vita. Hadi kufikia saa 3:40, sehemu kubwa ya kasri ya sultani ilikuwa tayari imeshalipuliwa na bendera ya sultani ikashushwa. Na hapo ndipo ikawa mwisho wa vita hiyo fupi. Katika vita hiyo fupi, inaelezwa kwamba wapiganaji 500 wa sultani walifariki na kujeruhiwa huku mwanajeshi mmoja tuu wa kingereza alijeruhiwa lakini akapona baadae. Baada ya sultan Khalid kukimbia, ndipo Uingereza ikampitisha mtu wao *Hamud bin Muhammed,* kuwa sultani wa Zanzibar kwa miaka 6 iliyofuata. Inaelezwa kwamba Khalid alipotoroka kumbe alipewa hifadhi na balozi ya ujerumani hapo Zanzibar na kisha baadae akasafirishwa na meli za wajerumani kuja Tanganyika (koloni la ujerumani) Ilipofika mwaka 1916, wakati wa vita ya kwanza ya dunia tuliona majeshi ya Uingereza yanavamia makoloni ya ujerumani ikiwemo Tanganyika, ambapo *Khalid* alikamatwa na kupelekwa Seychelles , lakini baada ya miaka michache alirudishwa Mombasa ambapo alifariki Mwaka 1927. *** Na hiyo ndiyo vita fupi kuliko zote kuwahi kutokea Duniani.
    0 Comments ·0 Shares ·662 Views
  • MAMBO 8 YA KUSHANGAZA YANAYOFANYWA NA MWILI WAKO KUKULINDA PASIPO WEWE KUJUA.

    C&P

    Mwili wa binadamu unafanya mambo mengi ya kibaiolojia ambayo mara nyingi ni vigumu kuyaelewa.

    Mwili una mifumo mbalimbali ya ulinzi ambayo inatulinda na hatari zinazoweza kutudhuru. Mifumo hiyo inatulinda masaa 24 ya siku, Siku zote 7 za wiki, katika mambo yote yanayoweza kuhatarisha maisha yetu.

    Yafuatayo ni mambo yanayofanywa na mwili ambayo ni kati ya hiyo mifumo ya ulinzi wa mwili wa binadamu.

    1. KUPIGA MIAYO (YAWNING)
    Lengo kubwa la kupiga muayo ni kuupoza ubongo baada ya joto kuzidi kwenye ubongo au baada ya ubongo kuchoka kufanya kazi.

    Vile vile kama ukiwa umechoka au una njaa husabababisha oxygen kupungua kwenye damu na kwenye mapafu, hii hupelekea tatizo la kupumua, hivyo kupiga miayo husaidia kuingiza oxygen ya ziada mwilini ili irudishe mwili katika hali yake ya kawaida.

    2. KUPIGA CHAFYA (SNEEZING)
    Mara nyingi tunapiga chafya pale pua zetu zinapokua zimejaa bakteria wa magonjwa ambao hawahitajiki mwilini, Vumbi pamoja na takataka mbali mbali zilizoingia kupitia pua.

    Hivyo kupiga chafya ni kitenda cha mwili kujisafisha kwa kuyatoa hayo matakataka nje yaliyoingia mwilini.

    3. KUJINYOOSHA (STRETCHING)
    Kuninyoosha mwili ni kitendo kisicho cha hiari ambacho lengo lake ni kuuandaa mwili kwa ajili ya kazi mbalimbali za kutumia nguvu utakazokabiliana nazo kwa siku nzima. Lakini pia kujinyoosha kunaipa misuli ya mwili mazoezi na kuiweka sawa vilevile kunarudisha mzunguko wa damu katika hali yake ya kawaida na kumtoa mtu katika uchovu.

    4. KWIKWI (HICCUPING)
    Najua umewahi kupata kwikwi, na mara nyingi mara baada ya kumaliza kula chakula. Je umeshawahi kujiuliza ile sauti ya ajabu ya kwikwi inasababishwa na nini au kwa sabababu gani watu hushikwa na kwikwi?

    Hiyo yote husababishwa na DIAPHRAGM (tamka DAYA - FRAM) kiungo kinachopatikana ndani ya mwili wa binadamu chini kabisa ya kifua baada ya mapafu(lungs). Kazi kubwa ya diaphragm ni kusaidia katika upumuaji, (inhale) na (exhale). Pale unapoingiza hewa ndani (inhale) diaphragm hushuka chini ili kusaidia kuivuta hewa ifike kwenye mapafu. Na unapotoa hewa nje (exhale) diaphragm hutulia kwa kubakia sehem yake ili kuwezesha hewa chafu kutoka nje kupitia pua na mdomo.

    Sasa basi, kuna wakati diaphragm kubugudhiwa na kuisababisha kushuka chini kwa kasi sana jambo linalosababisha wewe kuvuta hewa (inhale) kwa kasi isiyo ya kawaida kupitia koromeo la sauti, hewa ikifika kwenye box la sauti (larynx), sehem hiyo hujifunga kwa haraka sana ili kuzuia hewa isipite huko na ndipo KWIKWI hutokea.

    Mambo mengine yanayoweza kuibugudhi diaphragm na kuisababisha kufanya kazi vibaya mpaka kupelekea kwikwi ni kitendo cha kula haraka haraka au kuvimbewa.

    5. KUJIKUNJA KWA NGOZI YA VIDOLE VYA MIKONO BAADA YA KULOWA AU KUKAA MUDA MREFU KWENYE MAJI.
    Je umewahi shuhudia jinsi ngozi ya vidole vyako inavyojikunja baada ya kufua nguo muda mrefu au kushika maji muda mrefu? Unajua ni kwa sababu gani ngozi hujikunja kama ya mtu aliyezeeka angali yu kijana mara baada ya kukaa sana kwenye maji?

    Watu wengi kabla walizani kwamba kujikunja kwa ngozi hiyo hutokana na maji kuingia kwenye ngozi na hivyo ngozi hujikunja baada ya kulowa.

    Lakini wanasayansi baada ya kufanya utafiti kwa muda merefu juu ya nini hasa hupelekea ngozi kujikunja? Walisema HAPANA si kwa sababu ya ngozi kulowana. Na walikuja na majibu haya.

    Mwili unapokutana na majimaji mara moja hupeleka taarifa na kutafsiri kwamba mazingira hayo yana UTELEZI (Slippery) hivyo kutasababisha mikono kushindwa kushika (Grip) au kukamata vitu kwa urahisi kutokana na utelezi huo. Hapo mwili huchukua hatua ya haraka kuikunja ngozi ya mikono yako ili kurahisisha ushikaji wa vitu vinavyoteleza ndani ya maji pamoja na kutembea kwenye utelezi.

    6. VIPELE VIPELE VYA BARIDI KWENYE NGOZI (GOOSEBUMPS)
    Kazi kubwa ya vipele hivi ni kupunguza kiasi cha joto la mwili linalopotea kupitia matundu ya ngozi. Hivyo kwa kufanya hivi humfanya binadamu kutunza joto la mwili hata katika mazingira ambayo hali yake ya hewa si rafiki kwa mwili wa mwanadamu au ni yenye baridi sana.

    7. MACHOZI (TEARS)
    Zaidi ya kuwa majimaji (MUCOUS MEMBRANE ) yanayopatikana kwenye Macho ambayo kazi zake ni kulilinda jicho dhidi ya kitu chochote kigeni kinachoingia jichoni (mfano unapokata vitunguu au mdudu anapoingia jichoni huwa unatoa machozi mengi eeeh!! Pia dhidi ya upepo na moshi) na pia hutumika kama kilainishi cha jicho pale linapokuwa linazunguka zunguka (blink).

    Vilevile machozi yana kazi ya kupunguza HISIA ZA HUDHUNI zinazozalishwa mwilini. Wanasayansi wanaamini kuwa mtu anapokua mwenye msongo wa mawazo (stress) mwili hutengeneza kitu kipya ili kwenda kubugudhi na kuharibu maumivu yote ambayo mtu anajisikia. Hivyo machozi yanayozalishwa hapa huwa na kemikali na yanafahamika kama NATURAL PAINKILLER. Machozi haya ni tofauti na machozi ya kawaida, lengo lake hasa la kuzalishwa ni kwa ajili ya kuondoa kabisa maumivu yaliyozalishwa mwilini

    Hivyo mpaka hapa tumeona kua kuna machozi ya aina tatu ambayo ni
    i. Basal tears (vilainishi)
    ii. Reflex tears (mlinzi)
    iii. Emotion tears (mtuliza maumivu)

    8. KUSHTUKA USINGIZINI (MYOCLONIC JERKS or HYPNIC JERK).
    Je! Ushawahi kutokewa na hali hii? umelala halafu ghafla unashtuka usingizini kwa mguvu nyingi kama umepigwa na shoti ya umeme na akili inakurudi ghafla huku mapigo ya moyo yakikuenda mbio? Na hali hii ikakutokea pasipo hata kuota ndoto yoyote?

    Basi usiogope au kuwasingizia watu uchawi, hii ni hali ya sayansi ya mwili.na ni njia moja wapo katika ile mifumo ya mwili kujilinda.

    Je hutokeaje?

    Hii ni hali ya ajabu sana isiyofanywa kwa hiari ambayo huwatokea watu mara tu wamejinyoosha kitandani na kupitiwa na usingizi, mwili hutetemeshwa na kusukumwa kwa nguvu na mtu hushtuka katika hali kama vile kapigwa na shoti ya umeme. Hali hii inaweza kupelekea mtu hata kuanguka kitandani na humwamsha mara moja kutoka usingizini.

    Wanasayansi wanatuambia kua, pale tu unapopata usingizi kiwango cha upumuaji kinashuka ghafla, mapigo ya moyo nayo taratibu yanapungua, misuli inatulia kwa ku-relax, Kitu cha AJABU hapa ubongo unatafsiri hali hii kama ni DALILI ZA KIFO (brain's misinterpretation of muscle relaxation), hivyo huchukua hatua za haraka za kuushtua mwili kwa kuutetemesha au kuuskuma kwa nguvu, hali ambayo humfanya mtu kuamka kutoka usingizini kwa KURUKA kitu ambacho ni hali isiyo ya kawaida.

    Hali hii ikimtokea mtu huambatana na kuongezeka kwa mapigo ya moyo (rapid heartbeat), kuhema haraka haraka, na wakati mwingine mtu hutokwa na jasho jingi.

    Wakati mwingine mtu huamka ametoa macho na kama ukimwangalia, nae huishia hukuangalia tu huku akikosa la kukujibu endapo utamuuliza vipi kuna tatizo gani?

    MWILI WAKO NI ZAIDI YA UNAVYOUJUA. JAMBO LA MSINGI NI KUONDOA HOFU KWANI MWILI WAKO UNAJUA NINI UFANYE NA WAKATI GANI ILI KUKULINDA USIKU NA MCHANA KATIKA SIKU ZOTE ZA MAISHA YAKO.

    Share pia wengine wajue sio kila kitu ni uchawi
    MAMBO 8 YA KUSHANGAZA YANAYOFANYWA NA MWILI WAKO KUKULINDA PASIPO WEWE KUJUA. C&P Mwili wa binadamu unafanya mambo mengi ya kibaiolojia ambayo mara nyingi ni vigumu kuyaelewa. Mwili una mifumo mbalimbali ya ulinzi ambayo inatulinda na hatari zinazoweza kutudhuru. Mifumo hiyo inatulinda masaa 24 ya siku, Siku zote 7 za wiki, katika mambo yote yanayoweza kuhatarisha maisha yetu. Yafuatayo ni mambo yanayofanywa na mwili ambayo ni kati ya hiyo mifumo ya ulinzi wa mwili wa binadamu. 1. KUPIGA MIAYO (YAWNING) Lengo kubwa la kupiga muayo ni kuupoza ubongo baada ya joto kuzidi kwenye ubongo au baada ya ubongo kuchoka kufanya kazi. Vile vile kama ukiwa umechoka au una njaa husabababisha oxygen kupungua kwenye damu na kwenye mapafu, hii hupelekea tatizo la kupumua, hivyo kupiga miayo husaidia kuingiza oxygen ya ziada mwilini ili irudishe mwili katika hali yake ya kawaida. 2. KUPIGA CHAFYA (SNEEZING) Mara nyingi tunapiga chafya pale pua zetu zinapokua zimejaa bakteria wa magonjwa ambao hawahitajiki mwilini, Vumbi pamoja na takataka mbali mbali zilizoingia kupitia pua. Hivyo kupiga chafya ni kitenda cha mwili kujisafisha kwa kuyatoa hayo matakataka nje yaliyoingia mwilini. 3. KUJINYOOSHA (STRETCHING) Kuninyoosha mwili ni kitendo kisicho cha hiari ambacho lengo lake ni kuuandaa mwili kwa ajili ya kazi mbalimbali za kutumia nguvu utakazokabiliana nazo kwa siku nzima. Lakini pia kujinyoosha kunaipa misuli ya mwili mazoezi na kuiweka sawa vilevile kunarudisha mzunguko wa damu katika hali yake ya kawaida na kumtoa mtu katika uchovu. 4. KWIKWI (HICCUPING) Najua umewahi kupata kwikwi, na mara nyingi mara baada ya kumaliza kula chakula. Je umeshawahi kujiuliza ile sauti ya ajabu ya kwikwi inasababishwa na nini au kwa sabababu gani watu hushikwa na kwikwi? Hiyo yote husababishwa na DIAPHRAGM (tamka DAYA - FRAM) kiungo kinachopatikana ndani ya mwili wa binadamu chini kabisa ya kifua baada ya mapafu(lungs). Kazi kubwa ya diaphragm ni kusaidia katika upumuaji, (inhale) na (exhale). Pale unapoingiza hewa ndani (inhale) diaphragm hushuka chini ili kusaidia kuivuta hewa ifike kwenye mapafu. Na unapotoa hewa nje (exhale) diaphragm hutulia kwa kubakia sehem yake ili kuwezesha hewa chafu kutoka nje kupitia pua na mdomo. Sasa basi, kuna wakati diaphragm kubugudhiwa na kuisababisha kushuka chini kwa kasi sana jambo linalosababisha wewe kuvuta hewa (inhale) kwa kasi isiyo ya kawaida kupitia koromeo la sauti, hewa ikifika kwenye box la sauti (larynx), sehem hiyo hujifunga kwa haraka sana ili kuzuia hewa isipite huko na ndipo KWIKWI hutokea. Mambo mengine yanayoweza kuibugudhi diaphragm na kuisababisha kufanya kazi vibaya mpaka kupelekea kwikwi ni kitendo cha kula haraka haraka au kuvimbewa. 5. KUJIKUNJA KWA NGOZI YA VIDOLE VYA MIKONO BAADA YA KULOWA AU KUKAA MUDA MREFU KWENYE MAJI. Je umewahi shuhudia jinsi ngozi ya vidole vyako inavyojikunja baada ya kufua nguo muda mrefu au kushika maji muda mrefu? Unajua ni kwa sababu gani ngozi hujikunja kama ya mtu aliyezeeka angali yu kijana mara baada ya kukaa sana kwenye maji? Watu wengi kabla walizani kwamba kujikunja kwa ngozi hiyo hutokana na maji kuingia kwenye ngozi na hivyo ngozi hujikunja baada ya kulowa. Lakini wanasayansi baada ya kufanya utafiti kwa muda merefu juu ya nini hasa hupelekea ngozi kujikunja? Walisema HAPANA si kwa sababu ya ngozi kulowana. Na walikuja na majibu haya. Mwili unapokutana na majimaji mara moja hupeleka taarifa na kutafsiri kwamba mazingira hayo yana UTELEZI (Slippery) hivyo kutasababisha mikono kushindwa kushika (Grip) au kukamata vitu kwa urahisi kutokana na utelezi huo. Hapo mwili huchukua hatua ya haraka kuikunja ngozi ya mikono yako ili kurahisisha ushikaji wa vitu vinavyoteleza ndani ya maji pamoja na kutembea kwenye utelezi. 6. VIPELE VIPELE VYA BARIDI KWENYE NGOZI (GOOSEBUMPS) Kazi kubwa ya vipele hivi ni kupunguza kiasi cha joto la mwili linalopotea kupitia matundu ya ngozi. Hivyo kwa kufanya hivi humfanya binadamu kutunza joto la mwili hata katika mazingira ambayo hali yake ya hewa si rafiki kwa mwili wa mwanadamu au ni yenye baridi sana. 7. MACHOZI (TEARS) Zaidi ya kuwa majimaji (MUCOUS MEMBRANE ) yanayopatikana kwenye Macho ambayo kazi zake ni kulilinda jicho dhidi ya kitu chochote kigeni kinachoingia jichoni (mfano unapokata vitunguu au mdudu anapoingia jichoni huwa unatoa machozi mengi eeeh!! Pia dhidi ya upepo na moshi) na pia hutumika kama kilainishi cha jicho pale linapokuwa linazunguka zunguka (blink). Vilevile machozi yana kazi ya kupunguza HISIA ZA HUDHUNI zinazozalishwa mwilini. Wanasayansi wanaamini kuwa mtu anapokua mwenye msongo wa mawazo (stress) mwili hutengeneza kitu kipya ili kwenda kubugudhi na kuharibu maumivu yote ambayo mtu anajisikia. Hivyo machozi yanayozalishwa hapa huwa na kemikali na yanafahamika kama NATURAL PAINKILLER. Machozi haya ni tofauti na machozi ya kawaida, lengo lake hasa la kuzalishwa ni kwa ajili ya kuondoa kabisa maumivu yaliyozalishwa mwilini Hivyo mpaka hapa tumeona kua kuna machozi ya aina tatu ambayo ni i. Basal tears (vilainishi) ii. Reflex tears (mlinzi) iii. Emotion tears (mtuliza maumivu) 8. KUSHTUKA USINGIZINI (MYOCLONIC JERKS or HYPNIC JERK). Je! Ushawahi kutokewa na hali hii? umelala halafu ghafla unashtuka usingizini kwa mguvu nyingi kama umepigwa na shoti ya umeme na akili inakurudi ghafla huku mapigo ya moyo yakikuenda mbio? Na hali hii ikakutokea pasipo hata kuota ndoto yoyote? Basi usiogope au kuwasingizia watu uchawi, hii ni hali ya sayansi ya mwili.na ni njia moja wapo katika ile mifumo ya mwili kujilinda. Je hutokeaje? Hii ni hali ya ajabu sana isiyofanywa kwa hiari ambayo huwatokea watu mara tu wamejinyoosha kitandani na kupitiwa na usingizi, mwili hutetemeshwa na kusukumwa kwa nguvu na mtu hushtuka katika hali kama vile kapigwa na shoti ya umeme. Hali hii inaweza kupelekea mtu hata kuanguka kitandani na humwamsha mara moja kutoka usingizini. Wanasayansi wanatuambia kua, pale tu unapopata usingizi kiwango cha upumuaji kinashuka ghafla, mapigo ya moyo nayo taratibu yanapungua, misuli inatulia kwa ku-relax, Kitu cha AJABU hapa ubongo unatafsiri hali hii kama ni DALILI ZA KIFO (brain's misinterpretation of muscle relaxation), hivyo huchukua hatua za haraka za kuushtua mwili kwa kuutetemesha au kuuskuma kwa nguvu, hali ambayo humfanya mtu kuamka kutoka usingizini kwa KURUKA kitu ambacho ni hali isiyo ya kawaida. Hali hii ikimtokea mtu huambatana na kuongezeka kwa mapigo ya moyo (rapid heartbeat), kuhema haraka haraka, na wakati mwingine mtu hutokwa na jasho jingi. Wakati mwingine mtu huamka ametoa macho na kama ukimwangalia, nae huishia hukuangalia tu huku akikosa la kukujibu endapo utamuuliza vipi kuna tatizo gani? MWILI WAKO NI ZAIDI YA UNAVYOUJUA. JAMBO LA MSINGI NI KUONDOA HOFU KWANI MWILI WAKO UNAJUA NINI UFANYE NA WAKATI GANI ILI KUKULINDA USIKU NA MCHANA KATIKA SIKU ZOTE ZA MAISHA YAKO. Share pia wengine wajue sio kila kitu ni uchawi
    0 Comments ·0 Shares ·749 Views
  • JINSI SHIRIKA LA KIJASUSI LA URUSI FSB {KGB} LILIVYO HATARI....

    Kama waswahili wasemavyo maisha ni safari ndefu na kifo ni Siri, pengine hili ni kweli kutokana na sintofahamu iliyochukua uhai wa Alexander Litvinenko, jasusi wa zamañi wa KGB na baadae FSB ya Urusi ya sasa.

    Tutarudi Sasa tuendelee mwishoni mwa wiki za mwezi wa kumi mwaka 2006 Alexander Litvinenko alipokuwa jijini London alipotorokea baada ya rabsha dhidi ya serikali mjini Moscow, siku hiyo Litvinenko alikuwa ametembelewa na marafiki zake wawili walikuwa wanausalama ndani ya FSB na iliyokuwa KGB Dmitri Kovtun na Andrei Lugovoi, asichokijua ni kwamba wale wawili walikuwa moja ya watu hatari na pia kama wasafirishaji mahiri wa msafiri kama Litvinenko kuliendelea kaburi

    Waliikutana hotelini jijini London wakinywa na kufurahi, siku hiyo Lugovoi na Kovtun wao waliagiza bia wakanywa wakifurahi, unajua nini Litvinenko ye aliagizwa chai ya rangi akanywa huku akiwachekea wasafirishaji wa ule msemo wa kiswahili " maisha ni safari"

    Maskinii Litvinenko alipojichanganya tu Lugovoi na Kovtun wakifanya kazi yao moja waliotumwa na FSB, kumnyamazisha " traitor of the mother Russia"

    Unajua walifanya Nini? Walichukua kemikali hatari sana duniani inayoua taratibu sana jina lake Polonium 210 wakatia katika chai ya Litvinenko. Inavyosemekana alivyorudi walimchekea na kufurahi zaidi kuona Litvinenko alikuwa amesahau mbinu muhimu kabisa ya wanaintelijensia kote duniani ! Kutomwamini mtu hata mama na baba yako.
    Litvinenko alikunywa chai ile

    **********
    Lugovoi na Kovtun walichukua ndege siku tatu baadae haoo Moscow, huko walifanyiwa sherehe ya uhakika wa kazi iliyofanyika isiyo na shaka, Kovtun aliamua kuwa mfanyabiashara mkubwa wakati Lugovoi alipandishwa cheo siku chache baadae.
    ******
    Maskini Litvinenko aliagana na wanyama wale wa kwenye barafu Kama wajiitavyo wao " "bear " lakini akiwapachika majina mazuri yaani marafiki, ndugu, wapenzi kutoka home Russia. Pia aliwauliza vipi watarudi lini kumuona, kimoyomoyo Kovtun na Lugovoi walikua wakicheka na kusikitika kiunafiki,wakijua huyu mtu hana mwezi duniani. Wiki tatu nyingi! atakufa kifo Cha mateso akiwa kitandani amelala.

    ***
    November 1 mwaka 2006 Litvinenko aliugua homa ya ghafla mwili ukiungua kwa namna ya kutisha sana, alipelekwa hospitali mjini London akaishi kwa wiki 3 akiwa hoi kitandani! Wakati akifa akitoa laana kwa Putin akamshutumu amemuua.

    Huo ukawa mwisho wa Litvinenko mtu aliyekuwa ameaminiwa kutunza siri za Russia yeye alizitoa hadharani kwa m16 . Pengine ni chafu sana zenye damu lakini bila shaka kulikuwa pigo kwa vitu hivyo kuwa hadharani. Putin alivuliwa nguo hata asiijifunike.

    Tuzungimzapo Leo ni miaka karibu 12 toka mnyama huyu atutoke.

    Mwaka fulani Putin aliulizwa na mwanahabari mmoja ni kitu gani asichoweza kuvumilia na kusamehe alisema hivi.. Ye ni ngumu sana kuwasamehe wasaliti wa mother Russia.

    Ohh ndo hivyo Litvinenko hakupata bahati ya kusamehewa na Putin hivyo alikwenda.

    Chanzo: na Google
    JINSI SHIRIKA LA KIJASUSI LA URUSI FSB {KGB} LILIVYO HATARI.... Kama waswahili wasemavyo maisha ni safari ndefu na kifo ni Siri, pengine hili ni kweli kutokana na sintofahamu iliyochukua uhai wa Alexander Litvinenko, jasusi wa zamañi wa KGB na baadae FSB ya Urusi ya sasa. Tutarudi Sasa tuendelee mwishoni mwa wiki za mwezi wa kumi mwaka 2006 Alexander Litvinenko alipokuwa jijini London alipotorokea baada ya rabsha dhidi ya serikali mjini Moscow, siku hiyo Litvinenko alikuwa ametembelewa na marafiki zake wawili walikuwa wanausalama ndani ya FSB na iliyokuwa KGB Dmitri Kovtun na Andrei Lugovoi, asichokijua ni kwamba wale wawili walikuwa moja ya watu hatari na pia kama wasafirishaji mahiri wa msafiri kama Litvinenko kuliendelea kaburi Waliikutana hotelini jijini London wakinywa na kufurahi, siku hiyo Lugovoi na Kovtun wao waliagiza bia wakanywa wakifurahi, unajua nini Litvinenko ye aliagizwa chai ya rangi akanywa huku akiwachekea wasafirishaji wa ule msemo wa kiswahili " maisha ni safari" Maskinii Litvinenko alipojichanganya tu Lugovoi na Kovtun wakifanya kazi yao moja waliotumwa na FSB, kumnyamazisha " traitor of the mother Russia" Unajua walifanya Nini? Walichukua kemikali hatari sana duniani inayoua taratibu sana jina lake Polonium 210 wakatia katika chai ya Litvinenko. Inavyosemekana alivyorudi walimchekea na kufurahi zaidi kuona Litvinenko alikuwa amesahau mbinu muhimu kabisa ya wanaintelijensia kote duniani ! Kutomwamini mtu hata mama na baba yako. Litvinenko alikunywa chai ile ********** Lugovoi na Kovtun walichukua ndege siku tatu baadae haoo Moscow, huko walifanyiwa sherehe ya uhakika wa kazi iliyofanyika isiyo na shaka, Kovtun aliamua kuwa mfanyabiashara mkubwa wakati Lugovoi alipandishwa cheo siku chache baadae. ****** Maskini Litvinenko aliagana na wanyama wale wa kwenye barafu Kama wajiitavyo wao " "bear " lakini akiwapachika majina mazuri yaani marafiki, ndugu, wapenzi kutoka home Russia. Pia aliwauliza vipi watarudi lini kumuona, kimoyomoyo Kovtun na Lugovoi walikua wakicheka na kusikitika kiunafiki,wakijua huyu mtu hana mwezi duniani. Wiki tatu nyingi! atakufa kifo Cha mateso akiwa kitandani amelala. *** November 1 mwaka 2006 Litvinenko aliugua homa ya ghafla mwili ukiungua kwa namna ya kutisha sana, alipelekwa hospitali mjini London akaishi kwa wiki 3 akiwa hoi kitandani! Wakati akifa akitoa laana kwa Putin akamshutumu amemuua. Huo ukawa mwisho wa Litvinenko mtu aliyekuwa ameaminiwa kutunza siri za Russia yeye alizitoa hadharani kwa m16 . Pengine ni chafu sana zenye damu lakini bila shaka kulikuwa pigo kwa vitu hivyo kuwa hadharani. Putin alivuliwa nguo hata asiijifunike. Tuzungimzapo Leo ni miaka karibu 12 toka mnyama huyu atutoke. Mwaka fulani Putin aliulizwa na mwanahabari mmoja ni kitu gani asichoweza kuvumilia na kusamehe alisema hivi.. Ye ni ngumu sana kuwasamehe wasaliti wa mother Russia. Ohh ndo hivyo Litvinenko hakupata bahati ya kusamehewa na Putin hivyo alikwenda. Chanzo: na Google
    0 Comments ·0 Shares ·756 Views
  • Mwamuzi maarufu wa Italia Colina alipoulizwa kuhusu wakati mkubwa wa kazi yake:

    "Ilikuwa dakika mbili za mwisho, niliona wachezaji wa Bayern wakiwa kwenye benchi wakijiandaa kusherehekea ubingwa, mashabiki walifurahi uwanjani huku timu yao ikitawazwa taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya.

    Ghafla, Manchester ilifunga mabao mawili katika dakika mbili na kubadilisha matokeo. Sitasahau jinsi timu ya Uingereza ilivyokuwa ikipasuka kwa kelele kubwa kana kwamba walikuwa simba wakinguruma, wakati kulikuwa na ukimya wa mazishi katika uwanja wa Bayern,

    Wachezaji wa Man United walikuwa wakisherehekea bao lao la pili kwa hysterically wakati niliona mchezaji wa Bayern akianguka chini bila matumaini na alikuwa anajisikia kukata tamaa sana. Nilimkaribia na sikupata chochote cha kumwambia isipokuwa, "Amka na upigane bado una sekunde ishirini!.

    Wakati huo, niliona sura ya kweli ya mpira wa miguu, kifo na maisha katika uwanja mmoja, watu wakisherehekea wazimu na watu wanaotamani kifo !! ”
    Mwamuzi maarufu wa Italia Colina alipoulizwa kuhusu wakati mkubwa wa kazi yake: "Ilikuwa dakika mbili za mwisho, niliona wachezaji wa Bayern wakiwa kwenye benchi wakijiandaa kusherehekea ubingwa, mashabiki walifurahi uwanjani huku timu yao ikitawazwa taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya. Ghafla, Manchester ilifunga mabao mawili katika dakika mbili na kubadilisha matokeo. Sitasahau jinsi timu ya Uingereza ilivyokuwa ikipasuka kwa kelele kubwa kana kwamba walikuwa simba wakinguruma, wakati kulikuwa na ukimya wa mazishi katika uwanja wa Bayern, Wachezaji wa Man United walikuwa wakisherehekea bao lao la pili kwa hysterically wakati niliona mchezaji wa Bayern akianguka chini bila matumaini na alikuwa anajisikia kukata tamaa sana. Nilimkaribia na sikupata chochote cha kumwambia isipokuwa, "Amka na upigane bado una sekunde ishirini!. Wakati huo, niliona sura ya kweli ya mpira wa miguu, kifo na maisha katika uwanja mmoja, watu wakisherehekea wazimu na watu wanaotamani kifo !! ”
    Like
    1
    · 0 Comments ·0 Shares ·307 Views
  • JE UNAFAHAMU: Wachezaji wanakumbana na mambo mengi sana uwanjani hivyo ukiona ghafla kiwango kinashuka usimtukane muombee.

    Iko hivi kuna siku Real Madrid walikuwa wanaenda kukutana na Atletico Madrid, kumbuka ni dabi hii hivyo lazima mtifuano uwe mkubwa.

    Wachezaji huwa wanapeana mbinu mbalimbali ili kushinda sasa beki Filipe Luis aliamua kutafuta udhaifu wa Di Maria ili aweze kumtawala, akapewa mbinu Sergio Aguero ambaye alikuwa anacheza Taifa Moja na Di Maria ambayo hadi leo anajutia.

    Filipe Luis anasema: "Majuto yangu makubwa katika kazi yangu? Ilikuwa na Di Maria.

    "Ikiwa kuna kitu najuta kukifanya, labda ndicho kitu pekee ninachojutia, ilikuwa dhidi ya Di Maria na ningependa kurejesha nyuma ili nisurudie...

    "Tulikuwa tunaenda kucheza dhidi ya Real Madrid na Agüero aliniambia: 'Filipe, zungumza naye kuhusu mke wake (vitu vibaya), atapoteza, ataacha mchezo.

    “Wakati wa mchezo, NILIMTUKANA, nilizungumza kuhusu MKE wake, Alinitazama, alikuwa AMEPOTEA, nilishinda mchezo mzima dhidi yake.

    “Nilirudi nyumbani na KUJUTA sana. Samahani kwa kufanya hivyo na Maria. Di Maria, samahani, samahani nilifanya hivyo, samahani."
    JE UNAFAHAMU: Wachezaji wanakumbana na mambo mengi sana uwanjani hivyo ukiona ghafla kiwango kinashuka usimtukane muombee. Iko hivi kuna siku Real Madrid walikuwa wanaenda kukutana na Atletico Madrid, kumbuka ni dabi hii hivyo lazima mtifuano uwe mkubwa. Wachezaji huwa wanapeana mbinu mbalimbali ili kushinda sasa beki Filipe Luis aliamua kutafuta udhaifu wa Di Maria ili aweze kumtawala, akapewa mbinu Sergio Aguero ambaye alikuwa anacheza Taifa Moja na Di Maria ambayo hadi leo anajutia. Filipe Luis anasema: "Majuto yangu makubwa katika kazi yangu? Ilikuwa na Di Maria. "Ikiwa kuna kitu najuta kukifanya, labda ndicho kitu pekee ninachojutia, ilikuwa dhidi ya Di Maria na ningependa kurejesha nyuma ili nisurudie... "Tulikuwa tunaenda kucheza dhidi ya Real Madrid na Agüero aliniambia: 'Filipe, zungumza naye kuhusu mke wake (vitu vibaya), atapoteza, ataacha mchezo. “Wakati wa mchezo, NILIMTUKANA, nilizungumza kuhusu MKE wake, Alinitazama, alikuwa AMEPOTEA, nilishinda mchezo mzima dhidi yake. “Nilirudi nyumbani na KUJUTA sana. Samahani kwa kufanya hivyo na Maria. Di Maria, samahani, samahani nilifanya hivyo, samahani."
    0 Comments ·0 Shares ·284 Views
  • #FAHAMU Miongoni mwa viumbe hatari zaidi vinavyopatikana kwenye maji ni aina ya samaki anayefahamika kwa jina la (Eel), uhatari mkubwa wa samaki huyu ni kwamba mwili wake una uwezo wa kuzalisha umeme wa mpaka kufikia volti 650.

    Samaki huyu anauwezo wa kuyapa maji shoti ya volti zaidi ya 600 ili tu kufanikiwa kumdhuru kiumbe yeyote ndani ya maji. Kiumbo anaweza kukua kwa urefu mpaka futi 8 au mita 2.5 na awapo kwenye maji hufanana na nyoka.

    Zipo baadhi ya video zinazoonyesha baadhi ya watu tofauti tofauti ulimwenguni wakionekana kupoteza maisha ghafla kwa mtetemesho wawapo ndani ya maji na wengi wao wamethibitishwa kufariki kutokana na shoti ya samaki huyo.
    #FAHAMU Miongoni mwa viumbe hatari zaidi vinavyopatikana kwenye maji ni aina ya samaki anayefahamika kwa jina la (Eel), uhatari mkubwa wa samaki huyu ni kwamba mwili wake una uwezo wa kuzalisha umeme wa mpaka kufikia volti 650. Samaki huyu anauwezo wa kuyapa maji shoti ya volti zaidi ya 600 ili tu kufanikiwa kumdhuru kiumbe yeyote ndani ya maji. Kiumbo anaweza kukua kwa urefu mpaka futi 8 au mita 2.5 na awapo kwenye maji hufanana na nyoka. Zipo baadhi ya video zinazoonyesha baadhi ya watu tofauti tofauti ulimwenguni wakionekana kupoteza maisha ghafla kwa mtetemesho wawapo ndani ya maji na wengi wao wamethibitishwa kufariki kutokana na shoti ya samaki huyo.
    Like
    Love
    2
    · 1 Comments ·0 Shares ·352 Views
More Results