• Best UPSC History Optional Coaching in Delhi

    L2A’s UPSC History Optional coaching in Delhi, under the expert guidance of Vijay Sir, offers aspirants a strategic edge in mastering History for the Civil Services Examination. With a focus on conceptual clarity, chronological understanding, and analytical answer writing, this program is tailored to meet the demands of both Paper I and Paper II.

    Students benefit from structured lectures, curated study material, regular tests, and daily answer writing practice. Vijay Sir's deep expertise, UPSC-oriented approach, and personalized mentorship make L2A the preferred choice for serious aspirants.

    If you're looking for the best UPSC History Optional coaching in Delhi, L2A provides a results-driven, mentorship-based learning environment that has helped many achieve success.

    Visit: https://l2a.in/upsc-history-optional

    #UPSC #UPSC2025 #UPSCPreparation #UPSCOptional #HistoryOptional #UPSCHistoryOptional #HistoryOptionalCoaching #HistoryOptionalStrategy #UPSCOptionalSubject #L2A #IASPreparation #HistoryByVijaySir
    Best UPSC History Optional Coaching in Delhi L2A’s UPSC History Optional coaching in Delhi, under the expert guidance of Vijay Sir, offers aspirants a strategic edge in mastering History for the Civil Services Examination. With a focus on conceptual clarity, chronological understanding, and analytical answer writing, this program is tailored to meet the demands of both Paper I and Paper II. Students benefit from structured lectures, curated study material, regular tests, and daily answer writing practice. Vijay Sir's deep expertise, UPSC-oriented approach, and personalized mentorship make L2A the preferred choice for serious aspirants. If you're looking for the best UPSC History Optional coaching in Delhi, L2A provides a results-driven, mentorship-based learning environment that has helped many achieve success. Visit: https://l2a.in/upsc-history-optional #UPSC #UPSC2025 #UPSCPreparation #UPSCOptional #HistoryOptional #UPSCHistoryOptional #HistoryOptionalCoaching #HistoryOptionalStrategy #UPSCOptionalSubject #L2A #IASPreparation #HistoryByVijaySir
    0 Commentarii ·0 Distribuiri ·117 Views
  • MindzQ Education SAT Tutoring – Proven Strategies. Real Results.

    MindzQ Education is your trusted destination for SAT Tutoring, offering personalized and results-driven instruction right here in Fair Lawn, NJ. Our expert tutors provide tailored support to help students master the SAT’s Math and Evidence-Based Reading & Writing sections. With flexible in-person and online options, MindzQ makes SAT prep convenient, effective, and accessible—ensuring every student reaches their full potential.

    Visit: https://mindzq.com/sat-test-prep-ap-exams

    #satscore #satprep #satprepfairlawn #satclassesnj #satprepclassesnj #MindzQEducation #Sattutoring
    MindzQ Education SAT Tutoring – Proven Strategies. Real Results. MindzQ Education is your trusted destination for SAT Tutoring, offering personalized and results-driven instruction right here in Fair Lawn, NJ. Our expert tutors provide tailored support to help students master the SAT’s Math and Evidence-Based Reading & Writing sections. With flexible in-person and online options, MindzQ makes SAT prep convenient, effective, and accessible—ensuring every student reaches their full potential. Visit: https://mindzq.com/sat-test-prep-ap-exams #satscore #satprep #satprepfairlawn #satclassesnj #satprepclassesnj #MindzQEducation #Sattutoring
    0 Commentarii ·0 Distribuiri ·347 Views
  • Searching for SAT Tutoring Near Me in Fair Lawn, NJ?

    MindzQ Education is your trusted destination for SAT Tutoring Near Me, offering personalized and results-driven instruction right here in Fair Lawn, NJ. Our expert tutors provide tailored support to help students master the SAT’s Math and Evidence-Based Reading & Writing sections. With flexible in-person and online options, MindzQ makes SAT prep convenient, effective, and accessible—ensuring every student reaches their full potential.

    Visit: https://mindzq.com/sat-test-prep-ap-exams
    #satscore #satprep #satprepfairlawn #satclassesnj #satprepclassesnj #MindzQEducation #Sattutoringnearme
    Searching for SAT Tutoring Near Me in Fair Lawn, NJ? MindzQ Education is your trusted destination for SAT Tutoring Near Me, offering personalized and results-driven instruction right here in Fair Lawn, NJ. Our expert tutors provide tailored support to help students master the SAT’s Math and Evidence-Based Reading & Writing sections. With flexible in-person and online options, MindzQ makes SAT prep convenient, effective, and accessible—ensuring every student reaches their full potential. Visit: https://mindzq.com/sat-test-prep-ap-exams #satscore #satprep #satprepfairlawn #satclassesnj #satprepclassesnj #MindzQEducation #Sattutoringnearme
    0 Commentarii ·0 Distribuiri ·357 Views
  • Crack the GRE with Confidence: Your Ultimate Guide to GRE Prep Success

    Planning to pursue your Master’s degree abroad? A high GRE Prep is your ticket to top universities. But cracking the GRE takes more than just knowledge—it requires a focused, smart, and strategic GRE prep approach that enhances accuracy and speed.

    With the right tools, a smart plan, and consistent practice, you can hit your target score and secure admission to your dream university. Start your GRE prep today and take charge of your future.

    Visit Now - https://www.jamboreeindia.com/gre-prep
    Crack the GRE with Confidence: Your Ultimate Guide to GRE Prep Success Planning to pursue your Master’s degree abroad? A high GRE Prep is your ticket to top universities. But cracking the GRE takes more than just knowledge—it requires a focused, smart, and strategic GRE prep approach that enhances accuracy and speed. With the right tools, a smart plan, and consistent practice, you can hit your target score and secure admission to your dream university. Start your GRE prep today and take charge of your future. Visit Now - https://www.jamboreeindia.com/gre-prep
    Gre Prep, Coaching Centres, Prep Books And Classes| Jamboree
    www.jamboreeindia.com
    Prepare for GRE with Jamboree's best GRE coaching, study material and books. Join our GRE course, classes, or coaching centers for top GRE test prep.
    0 Commentarii ·0 Distribuiri ·499 Views
  • Mixng and master are easy and simple with us.
    Mixng and master are easy and simple with us.
    0 Commentarii ·0 Distribuiri ·158 Views
  • Mzazi mwenzie na Master Jay
    Mzazi mwenzie na Master Jay 🤔
    Like
    1
    · 0 Commentarii ·0 Distribuiri ·175 Views
  • Orodha ya Watayarishaji bora kwenye historia ya muziki wa Tanzania.

    1. P Funk
    2. Master Jay
    3. Miika Mwamba
    4. Bonny Love
    5. Prof Ludigo

    6. Bizzman
    7. Enrico
    8. Marco Chali
    9. Hermy B
    10. Lamar

    11. Man Walter
    12. Alain Mapigo
    13. Said Comorean
    14. Ambrose Dunga
    15. Pancho Latino

    16. J Ryder
    17. T Touch
    18. Kameta
    19. Mona Gangster
    20. Shaddy Clever

    21. Complex
    22. Manecky
    23. Abbah
    24. KGT
    25. Bob Junior

    26. Mensen Selekta
    27. Duke
    28. S2Kezzy
    29. Laizer
    30. Abby Daddy

    31. Bonga
    32. Emma The Boy
    33. Nahreel
    34. Mangustino
    35. Kidbway

    36. Shirko
    37. Fundi Samuel
    38. Ali Baucha.

    Panga orodha yako Watayarishaji wa tano bora wa muda wote.
    Orodha ya Watayarishaji bora kwenye historia ya muziki wa Tanzania. 1. P Funk 2. Master Jay 3. Miika Mwamba 4. Bonny Love 5. Prof Ludigo 6. Bizzman 7. Enrico 8. Marco Chali 9. Hermy B 10. Lamar 11. Man Walter 12. Alain Mapigo 13. Said Comorean 14. Ambrose Dunga 15. Pancho Latino 16. J Ryder 17. T Touch 18. Kameta 19. Mona Gangster 20. Shaddy Clever 21. Complex 22. Manecky 23. Abbah 24. KGT 25. Bob Junior 26. Mensen Selekta 27. Duke 28. S2Kezzy 29. Laizer 30. Abby Daddy 31. Bonga 32. Emma The Boy 33. Nahreel 34. Mangustino 35. Kidbway 36. Shirko 37. Fundi Samuel 38. Ali Baucha. Panga orodha yako Watayarishaji wa tano bora wa muda wote.
    Like
    1
    · 0 Commentarii ·0 Distribuiri ·779 Views
  • #Repost @georgejob_gj
    MASTER KI NI MVP TUSISAHAU.

    Tusisahau kua huyu Aziz Ki ndiye MVP wa ligi yetu Tanzania Bara msimu wa 2023/2024 haya anayo yafanya sio kwa Bahati Mbaya au kwa sababu Pamba ni wabovu Master Ki is a versatile player

    Goli la pili alilo piga ukiangalia mentality yake ilivyo change kwa haraka kutoka kutaka kutoa pasi na kufanya maamuzi ya kupiga shuti la kucave golini utagundua Azizi Ki ni mchezaji Mwenye akili kubwa sana ya Mpira.

    Pamba walizidiwa kimbinu kwenye kila sehemu Substitution walizo fanya ya Nakibinge na Habib Kyombo wallijaribu kutaka kubadilisha mchezo lakini mbinu ya Yanga bado iliendelea kutawala mchezo.

    Yona Amos moja ya Makipa Bora sana nchini bahati mbaya leo kakutana na Yanga iliyo Bora sana kimbinu karibu magoli yote aliyofungwa ni magoli ambayo sio ya kumlaumu ni magoii ya kiufundi.

    NB: Ikangalombo apewe muda au Mali ipo?
    (George Job, Mchambuzi)

    #Repost @georgejob_gj MASTER KI NI MVP TUSISAHAU. Tusisahau kua huyu Aziz Ki ndiye MVP wa ligi yetu Tanzania Bara msimu wa 2023/2024 haya anayo yafanya sio kwa Bahati Mbaya au kwa sababu Pamba ni wabovu Master Ki is a versatile player 🙌 Goli la pili alilo piga ukiangalia mentality yake ilivyo change kwa haraka kutoka kutaka kutoa pasi na kufanya maamuzi ya kupiga shuti la kucave golini utagundua Azizi Ki ni mchezaji Mwenye akili kubwa sana ya Mpira. Pamba walizidiwa kimbinu kwenye kila sehemu Substitution walizo fanya ya Nakibinge na Habib Kyombo wallijaribu kutaka kubadilisha mchezo lakini mbinu ya Yanga bado iliendelea kutawala mchezo. Yona Amos moja ya Makipa Bora sana nchini bahati mbaya leo kakutana na Yanga iliyo Bora sana kimbinu karibu magoli yote aliyofungwa ni magoli ambayo sio ya kumlaumu ni magoii ya kiufundi. NB: Ikangalombo apewe muda au Mali ipo? (George Job, Mchambuzi)
    0 Commentarii ·0 Distribuiri ·801 Views
  • DUNIA NA MAAJABU YAKE
    (Muundo wa Dunia na Maajabu Yaliyomo)

    1. UMRI WA DUNIA

    HII Dunia yetu ina historia ndefu mno tangu ilipojiunda angani, miaka takribani bilioni 4.5 iliyopita.

    Tarakimu za umri huo wa miaka bilioni 4.5 ni 4,500,000,000, yaani miaka milioni elfu nne na mia tano iliyopita.

    Dunia ambayo kwa lugha ya Kiingereza inafahamika vyema kwa jina la 'Earth', pia hujulikana kama 'the World', ikimaanishwa ulimwengu.

    Aidha, Dunia ni sayari pekee kwenye himaya ya sayari zilizopo chini ya jua ambayo jina lake halitokani na majina ya "Miungu wa Dola" ya Kigiriki au ya Kirumi.

    Asili ya jina la 'earth' ni 'erde' lenye asili ya nchini Ujerumani, na maana yake ni udongo au ardhi.

    Mpaka kuweza kupata umri huo wa dunia wanasayansi walifanya kazi ya kutafiti na kisha kuwasilisha matokeo yao kwenye makongamano ya kisayansi duniani, ambapo matokeo hayo yalijadiliwa kwa kina na hatimaye kukubalika kama hivi.

    Kumbuka katika majadiliano hayo huwepo mivutano mikali miongoni mwa wanasayansi waalikwa, ambapo pia jopo la wanasayansi wanaowasilisha utafiti husika hujikuta wakitakiwa kujibu hoja mbalimbali za wanasayansi wenzao.

    Kuna wakati baadhi ya matokeo ya tafiti kadhaa hukataliwa, huku watafiti husika wakitakiwa kurejea upya tafiti zao.

    Wanasayansi hupata umri wa sayari kwa kupima umri wa miamba ya sayari husika, ambapo mwamba wenye umri mkubwa zaidi kuliko miamba yote ndiyo huchukuliwa kuwa umri wa sayari husika.

    Itakumbukwa kuwa Msahafu wa Biblia (Sura ya Mwanzo 1) husimulia jinsi Mwenyezi Mungu alivyoumba "mbingu na nchi na vyote vilivyomo kwa siku 6," lakini pia Msahafu huohuo kwenye aya zingine hueleza kuwa miaka elfu moja ya duniani yaweza kuwa sawa na siku moja kwenye ya Makazi ya Mwenyezi Mungu.

    Ni dhahiri kuwa binadamu tukiwa hatuna hoja sahihi kwa maelezo ya aina hiyo, ndipo tunaona ni vyema mambo ya Mwenyezi Mungu kumwachia Yeye Mwenyewe Mwenyezi Mungu.

    2. KUUMBIKA DUNIA, SAYARI, JUA, NYOTA

    Kimsingi, Dunia kama zilivyo sayari zingine zote ilijiunda kutokana na mabaki ya vitu vilivyotumika kuunda Jua.

    Jua ambalo ni nyota kama zilivyo nyota zote angani, lilijiunda lenyewe kwenye eneo la anga lijulikanalo kama 'Pillars of Creation' (nguzo za uumbaji) katika ukanda wa anga wenye upana ambao huonekana kutokuwa na mwisho.

    Ukanda huo ujulikanao kama 'Solar Nebula,' umegubikwa na mawingu ya vumbi la huko angani pamoja na aina mbalimbali za gesi na hewa, ikiwemo haidrojeni na heliumu.

    'Solar' ni jina la nishati itokanayo na joto la jua, na 'Nebula' kwa lugha ya Kilatini ni "wingu" au vumbi la gesi asilia mithili ya ukungu.

    Hivyo, 'Solar Nebula' ni ukanda katika anga ya mbali wenye mawingu yaliyosheheni nishati yenye joto, sawa na nishati ya joto la jua.

    Sasa basi, tunafahamu vyema kuwa jua hutoa mionzi hatari yenye joto kali mithili ya moto mkali, na ambayo ikiboreshwa kisayansi pia huweza kutoa nishati ya umeme.

    Hivyo, kwa muktadha huo, hebu ngoja sasa tuleta pamoja hewa za gesi, zikiwemo haidrojeni na heliumu, mawingu yenye nishati ya umeme wa jua, vumbi la angani na tufani itokanayo na mchafuko mbaya wa hali ya hewa huko anga za mbali.

    Na ili kuweza kupata matokeo yanayotakiwa, hebu pia tutambue uwepo wa nguvu kubwa ya asili katika kiwango kijulikanacho kwa jina la "Supernatural Power", ambayo ndiyo huwa kisababishi cha mambo yote.

    Kisayansi, "Supernatural Power" ni nguvu kubwa ya asili ambayo huendesha mifumo mbalimbali ya asili, ambapo duniani nguvu hiyo hujulikana kama Nguvu ya Mungu.

    Nguvu asili hiyo, yaani Supernatural Power, husababisha tufani ambayo huvurumisha kwa pamoja vitu vyote hivyo, (gesi, hewa, mawingu yenye nishati ya joto na vumbi la angani) ili kuunda tufani yenye umbo la duara.

    Duara hiyo ni kama ile itokanayo na kimbunga kikali duniani, na ambacho sasa tutaona kikifungamanisha pamoja vitu vyote hivyo katika mchafuko mkubwa wa hali mbaya ya hewa.

    Natumia maneno ya msisitizo kuelezea "ukubwa" wa mchafuko huo wa hali ya hewa katika eneo hilo la anga, kwani katika kuunda sayari au nyota nguvuasili kubwa hutumika.

    Aidha, tufani hiyo ya duara itakayoanza kidogo kidogo kama kimbunga kikali, itazidi kukua hadi kuwa na kipenyo cha takribani kilomita 10 hadi 200 au zaidi na kwendelea.

    Tufani hiyo ndiyo itavurumisha kwa pamoja gesi na hewa za naitrojeni na heliumu, mawingu ya nishati ya joto na vumbi la angani (kama kifanyavyo kimbunga kikali katika eneo tambarare la duniani).

    Pia, wakati mchafuko huo wa hali mbaya ya hewa ukiendelea, hebu ngoja sisi watazamaji tujibanze mahali fulani kwa mbali kushuhudia duara hiyo ya tufani ikijizungusha yenyewe bila kukoma kwa kipindi cha miaka mingi.

    Kitakachofuata ni kuanza kuona kiini cha moto kikianza kujiunda katikati ya duara hiyo ya tufani kali, huku pia nje ya duara hiyo vitu kibao vikivutwa kujiunga na mzunguko wa hiyo tufani ya duara.

    Vitu hivyo ni pamoja na vumbi zaidi la angani, na gesi zaidi zenye joto kali.

    Wakati huohuo kipenyo na mzingo wa duara hiyo vitazidi kuongezeka upana na ukubwa, mfano wa duara yenye umbo sawa na la mpira mkubwa wa miguu.

    Hivyo, baada ya miaka takribani milioni moja tutashangaa kuona lile vumbi likigeuka taratibu kuwa miamba ya moto ndani ya kiini cha tufani hiyo ya duara.

    Miamba hiyo ni kutokana na lile vumbi la angani ambalo hatimaye limeshikamana pamoja mithili ya zege, na hatimaye kuwa miamba ndani ya tufani ya duara.

    Sanjari na kuundika huko ndani ya kitovu cha hiyo tufani ya duara, pia kwelekea nje ya duara hiyo utaundika udongo ambao ardhi, mchanga na mawe.

    Kimsingi, vitu hivyo pia ni matokeo ya lile vumbi la angani ambalo lilikusanywa pamoja na kuvutwa na kasi ya mzunguko wa tufani.

    Hatua hiyo mpya inatokana na kuwepo mshikamano na mgandamizo wa zile chembechembe za lile vumbivumbi ndani ya tufani.

    Vurumai hiyo ya mzunguko wa hiyo tufani ya duara yenye vumbi, itazidi kukua hadi kuunda sumaku ya asili ndani ya kile kitovu cha duara ya tufani.

    Kutokana na duara hiyo ya tufani kuongezeka ukubwa, hatimaye sumaku iliyopo kwenye kitovu cha duara hiyo itaishiwa nguvu ya kwendelea kunasa vumbi zaidi kuja kwenye mzingo wa hiyo duara ya tufani.

    Kumbuka kuwa wakati huo hiyo duara pia itaunda kimo kutoka kwenye usawa wa ardhi yake kwenda ndani kwenye kitovu chake, na hivyo kuwa duara ya mviringo kama umbo mfano wa mpira mchezo wa miguu.

    Baada ya kupita maelfu ya miaka mingi, duara hiyo ambayo hapo awali ilianza kama umbo la tufani na kuzidi kukua huko angani, sasa itakuwa na joto kali kupita kiasi na kuanza kung'aa kama jua.

    Jua hilo, ndiyo nyota mojawapo ya zile ambazo huonekana usiku ziking'aa angani.

    Lakini pia wakati wa kujiunda nyota hiyo, kama tulivyoona hapo awali, baadhi ya mabaki yake yaliyokuwa yakitawanyika angani wakati ile tufani ya duara ikijizungusha, huweza kujikusanya pamoja na kuunda sayari ambazo huzunguka baadhi ya hizo nyota.

    Hivyo ndivyo zilivyojiunda sayari zote ambazo huelea kwa kulizunguka jua letu.

    Mathalani, sayari zote ambazo hulizunguka jua, ikiwemo dunia zilijiunda kutokana na mabaki ya vitu kama gesi, michanga na mawe ambavyo vilitawanyika angani wakati jua likijiunda (kama ambavyo imeelezwa hapo awali).

    3. KIINI CHA DUNIA

    Dunia yetu ambayo wastani wa nusu kipenyo cha umbo lake la duara ni kilomita 6,371, mzingo wake ni kilomita takribani 40,041.

    Kama zilivyo sayari zote katika himaya ya jua, dunia nayo ilijiunda wakati jua likijiunda lenyewe.

    Yaani kwamba sayari ni mabaki ya vitu vilivyotumika kuliunda jua.

    Kadhalika kama zilivyo sayari zingine zote, dunia nayo ina kiini chake ambacho kipo katikati ya ardhi yake.

    Kiini hicho kina nguvu kubwa ya sumaku ambayo, pamoja na mambo mengineyo, 'huvuta' umbo hilo la duara kutoka juu ya ardhi kwenda katikati ya kiini hicho.

    Muundo huo ndio hulifungamanisha pamoja umbo la duara la dunia, na hivyo kuzuia umbo hilo lisifumke kutoka ardhini na kusambaratika.

    Hiyo ni sawa na mpira wa miguu unavyoweza kupasuka na kusambaratika, kama utajazwa upepo kupita kiasi chake.

    Kiini hicho ambacho kipo katikati kabisa ya dunia, kinajulikanacho kwa jina la kisayansi la 'Inner Core.'

    Kiini hicho kina joto kali la sentigredi 6,230 ambacho ndio kiasi cha joto la jua.

    Kiini hicho kina umbo la duara lenye nusu kipenyo cha kilomita 1,250.

    Kama ingetokea kuchimba ardhi wima kwenda kwenye kiini hicho, mchimbaji angeanza kukutana na joto la kiini hicho kuanzia kimo cha umbali wa kilomita 5,150 kutoka usawa wa juu ya ardhi tunayotembea.

    Katika historia ya uchimbaji ardhi, kina kirefu kilichowahi kuchimbwa ardhini ni mita 12,345 (kilomita 12.345) huko Sakhalini, nchini Urusi, kwa ajili ya uvunaji wa mafuta ya petroli.

    Kiini cha dunia kinaundwa na madini mchanganyiko wa nikeli (nickle), chuma (iron) na dhahabu.

    Kwa mujibu wa utafiti, inakadiriwa kuwa kama dhahabu hiyo ingechimbwa na kuchomwa mpaka kuwa kimiminika sawa na uji na kisha kumwagwa chini, ingeweza kuifunika dunia yote kwa unene wa sentimeta 45.

    Kiini hicho muhimu kwa uhai wa sayari hii ya dunia kiligunduliwa mwaka 1936 na mtaalamu wa matetemeko ya ardhi wa nchini Denmark, mwanamama Dkt. Inge Lehmann.

    Dkt. Lehmann alihitimu shahada yake ya kwanza katika fani ya Hisabati mwaka 1910, ya Uzamili mwaka 1920 (zote kutoka Chuo Kikuu cha Copenhagen nchini mwake), na ile ya Uzamivu kutoka Chuo Kikuu cha Cambridge nchini Uingereza.

    Alifariki kwa uzee mwaka 1993 akiwa na umri wa miaka 104.

    4. MAJI DUNIANI

    Kupatikana maji kwenye dunia yetu, ni mojawapo ya miundo ambayo haipo katika sayari zingine ambazo tuna taarifa za kitafiti kuzuhusu.

    Maji ni muhimili muhimu kwa ajili ya uhai wa viumbe wote na mimea, ambavyo kwa pamoja havipo katika sayari zingine za himaya ya jua.

    Kwa mujibu wa tafiti nyingi ambazo zimefanyika kwa miongo mingi ya miaka kujaribu kubaini nini chanzo cha kuwepo maji duniani, hakuna hata utafiti mmoja ulioonesha kwa usahihi matokeo ya kuridhisha.

    Miongoni mwa tafiti hizo ni pamoja na ule wa mwaka 2005, ambapo Mkuu wa Idara ya Masomo ya Sayari na Mwezi katika Chuo Kikuu cha Arizona nchini Marekani, Profesa Michael Julian Drake, na mwenzake ambaye ni mtaalamu wa Vimondo, Dkt. Huberto Campins, wa Chuo Kikuu cha Central Florida, walitafiti nini chanzo cha kuwepo maji duniani.

    Katika mawasilisho yao kwenye kongamano la kisayansi la Chama cha Wanataaluma wa Maarifa ya Anga za Juu (IAU), watafiti hao walikanusha madai ya uwezekano wa dunia hapo kale kugongwa na kimondo kikubwa na kusababisha maji kulipuka kutoka ardhini.

    Wakiwasilisha matokeo ya utafiti wao kwenye mkutano wa kongamano hilo, magwiji hao wa masuala ya sayari walieleza kwenye waraka wao uitwao "Origin of water on the terrestial planets" (chanzo cha kuwepo maji kwenye sayari).

    Walidai kuwa maji yaliyopo duniani yaliumbika kwenye ardhi ya dunia tangu mwanzo, wakati ikijiunda angani.

    Ikumbukwe kuwa eneo la uso wa dunia likiwa ni jumla ya kilomita za mraba milioni 510, asilimia 70.8 ya eneo hilo imefunikwa na maji na asilimia 29.2 ni nchi kavu, ikiwemo milima, mabonde na ardhi tambarare.

    5. HEWA YA OKSIJENI

    Muundo mwingine muhimu katika sayari hii ya dunia ni hewa ambazo ni tawala, yaani Naitrojeni ambayo kwa usahihi imeenea kwa asilimia 78.08 ya hewa yote ya dunia, Oksijeni asilimia 20.95, 'Argon' asilimia 0.93, hewa ya Ukaa (Carbon dioxide) asilimia 0.039, na asilimia moja ni hewa mithili ya mvuke wa maji (water vapour).

    Hewa ya Oksijeni ambayo ni nguzo muhimu kwa ajili ya uhai wa viumbe wote na pia haipatikani kwenye sayari nyingine chini ya jua, inadhaniwa ilianza kupatikana duniani miaka takribani bilioni 2.5 iliyopita kufuatia "kukomaa kwa kiini cha dunia."

    Kwa mujibu wa matokeo ya tafiti mbalimbali na nadharia za kisayansi, inaoneshwa kuwa kukomaa kwa kiini hicho cha dunia hatimaye ndiko kulisababisha kuzuka duniani milipuko ya volikano ambayo pia ilisababisha kuzuka mabonde na milima.

    Inaoneshwa kuwa tayari wakati huo maji yaliishakuwepo duniani, na kuwezesha kuzuka chembechembe ndogo sana za kibakteria zijulikanazo kwa jina la kisayansi la 'cyanobacteria' au 'blue-green algae'.

    Kwa kutumia mwanga wa jua, maji na hewa ya ukaa, chembechembe hizo ziliweza kuzalisha hewa mbalimbali, ikiwemo 'Carbonhydrates' na Oksijeni.

    Kwa kuwa hizo chembechembe ndogo za kibakteria huishi baharini, ilikuwa rahisi kwa oksijeni kutokea baharini kupepea na kuenea katika anga ya dunia na kuzuiliwa hapo na nguvu asili ya uvutano ya dunia ili pia ibaki ikienea pote duniani.

    Mpaka wakati wa kuzuka duniani mimea na viumbe hai miaka takribani bilioni 3.5 iliyopita, tayari oksijeni ilikwa ni tele duniani; na hivyo kutumika kudumisha uhai wa viumbe hadi wakati huu.

    6. UKANDA WA 'OZONE'

    Muundo mwingie muhimu wa asili kwa dunia ni ukanda wa anga ujulikanao kwa jina la 'ozone' ambao umetanda kama 'mwavuli' kwenye anga ya dunia, na kuikinga isidhuriwe na mionzi hatari ya sumu kutoka kwenye Jua.

    Ukanda huo maarufu kama 'ozone layer' umetanda kuanzia usawa wa kilometa 15 kutoka ardhini kwenda juu angani mpaka ukomo wa kilomita takribani 50, ambapo huchuja asilimia kati ya 97 na 99 ya mionzi hatari kwenye miale ya joto la jua.

    Miongoni mwa matatizo yanayosababishwa na mionzi hiyo hatari kutoka kwenye jua, ni pamoja na magonjwa ya saratani ya ngozi kwa bianadamu.

    Pia juu ya ukanda wa tabaka la ozone kuna ukanda mwingine uitwao "atmosphere" ambao ni madhubuti kiasi kwamba vitu vinavyotoka anga za juu na kujaribu kuupenya ili kufika duniani, hukumbana na joto kali na kusambaratishwa kwa kuunguzwa.

    Si kwamba tabaka hilo lina joto, isipokuwa kasi ya "kuanguka" vitu hivyo kutoka juu angani kuja dunia husababisha msuguano na chembechembe za gesi katika eneo hilo na kuzalisha joto mithili ya ndimi za moto.

    Picha za video za vyombo vya 'Apollo' vikirejea duniani kutoka mwezini vikiwa na wanaanga ndani yake na kupenya tabaka hilo kwa kasi ya kilomita 39,000 kwa saa, huonekana kughubikwa na ndimi za moto wa rangi ya njano na bluu.

    Rangi hizo ni ishara ya ukali wa moto huo, lakini kutokana na waundaji wa vyombo hivyo kutumia mchanganyiko wa mabati na plastiki ngumu visivyopenywa na joto, Apollo huonekana kulichana tabaka hilo na kutokea upande wa pili ambao ni anga ya dunia.

    Hivyo basi, mfano huo mdogo unaonesha uimara wa tabaka hilo la 'ozone', ambalo kama ambavyo tumeona huchuja mionzi ya sumu kutoka kwenye mwanga wa jua ili kutolete madhara kwa viumbe duniani.

    Mwanga huo ukisafiri kutoka juani umbali wa kilomita milioni 150 kwa kasi ya kilomita 299,793, hutua duniani ndani ya dakika 8 na sekunde 19 ukiwa tayari umechujwa wakati ukipenya tabaka hilo.

    'Ozone' iligunduliwa mwaka 1913 na wanasayansi wawili wa nchini Ufaransa, Charlest Fabry na Henri Buisson, ambapo kipimo cha kasi ya mwanga kiligunduliwa na mwanasayansia wa anga za juu wa nchini Denmark, Ole Roemer, mwaka 1676.

    7. NGUVU ASILI YA UVUTANO

    Muundo mwingine wa dunia ni nguvu ya asili ya uvutano ya dunia, maarufu kama 'gravitation', ambayo huvuta vitu kuvirejesha chini duniani pale vinaporushwa kwenda juu au vile vinavyoanguka kutoka juu angani.

    Nguvu hiyo ina manufaa makubwa, kwani bila kuwepo duniani binadamu na viumbe wengine wangepeperuka kama karatasi kwenda juu wakati wakitembea juu ya ardhi ya hii.

    Kadhalika, nguvu hiyo husaidia kuvuta hewa ya oksijeni na kuiweka karibu na ardhi kwa ajili ya matumizi mbalimbali.

    Pia, nguvu hiyo husaidia kuiweka dunia, mwezi, jua na sayari zingine katika uwiano wa umbali usio na madhara kutoka kila moja.

    Nguvu hiyo ya asili ndiyo huliweka joto la jua duniani na kubaki kuwa katika kiwango kinachotakiwa, na hivyo kuwezesha viumbe kupata joto la wastani na pia katika kiwango mwanana.

    Nguvu hiyo huvuta mvua kuja duniani na kuwezesha maji ya bahari, maziwa na mito kutulia duniani.

    Mathalani, bila nguvu asili hiyo kuwepo duniani, maji 'yangemwagika' kutoka duniani kwa kutawanyika kama upepo na kupaa kwenda juu angani na kutoweka kabisa.

    Na ndio maana ukirusha maji kwenda juu, hurudi chini ardhini.

    Hebu angalia mfano huu kwamba wanaanga waliokwenda mwenzini walilazimika kuvaa mavazi yenye uzito wa kilo 80 hapa duniani, lakini mavazi hayo kule mwezini yakawa na uzito wa kilo 3.

    Mavazi hayo, yaani viatu, koti, suruali, na kofia nzito yenye miwani maalumu ya kukinga macho dhidi ya mionzi hatari ya jua, vyote kwa pamoja viliunganishwa na kuwa mfano wa sare za 'ovaroli' za mafundi wa magari.

    Mavazi hayo pia mgongoni yakiwa yameunganishwa kwa pamoja na mtungi wa hewa ya oksijeni kwa ajili ya kupumua, yalivaaliwa mahsusi muda mfupi baada ya chombo kutua mwezini.

    Hivyo, msomaji wangu tafakari nini kilisababisha mavazi kuwa mazito hapa duniani, lakini yawe mepesi kule mwezini?

    Jibu ni kwamba nguvu asili ya uvutano hapa duniani ni kubwa kuliko ya kule mwezini.

    Na ndipo tunaona umuhimu wa muundo huo wa nguvu asili ya uvutano, ambapo hapa duniani huvuta vitu kuja chini kwa kasi ya mita 9.81 kwa sekunde, lakini kwa kuwa nguvu ya mwezi ni hafifu, huvuta vitu kwa kasi ndogo ya mita 1.62 kwa sekunde.

    Ingawa nguvu hiyo ya asili iligunduliwa kuwepo duniani miaka mingi iliyopta, mwanafizikia bingwa wa Uingereza, Sir Isaac Newton (1642-1727), ndiye anatambulika kama mgunduzi wa hesabu hizo za nguvu asili hiyo.

    Anaeleza kuwa vitu vyote vyenye maumbo asili, ikiwemo jua, sayari, dunia, mwezi, na vimondo, kila kimoja kina nguvu hiyo katika viwango tofauti.

    Kanuni hiyo, kwa mujibu wa matokeo ya utafiti wake, hueleza kuwa nguvu hiyo ndiyo hufanya jua kuvuta sayari zake ili kulizunguka, huku pia kila sayari ikitumia nguvu 'binafsi' (na kwa uwiano maalumu) kujihami isivutwe hadi kwenda kuligonga jua au kugongana na sayari zingine au vimondo.

    Nguvuasili ya jua ni mita 274 kwa sekunde, ikiwa ni zaidi ya kiasi cha nguvuasili ya kila sayari.

    Muundo huo wa kila sayari kujihami kivyake katika mstari wa njia yake hufahamika kisayansi kama "sayari kuhami mazingira ya njia yake"; yaani kwamba 'a planet has to clear the neighbourhood around its orbit.'

    Newton akiwa amezaliwa 'mtoto-njiti' na baadaye kuibuka kuwa mwenye akili nyingi kiasi cha kukaribia kuwa sawa na mtu wa miujiza, hakuwahi kuoa kutokana na kinachoelezwa kuwa ni " kutokana na kutingwa na shughuli za kimasomo."

    Huoneshwa kuwa muda mwingi alikuwa maabara akifanya tafiti mbalimbali za kisayansi, au akiwa maktaba akijisomea, ama akiandika kitabu, au akifundisha wanafunzi wake.

    Alikuwa bingwa mwenye kipaji cha taaluma nyingi, ikiwemo Fizikia, Kemia, Hisabati, Maarifa ya Anga za Juu, Uchumi, Falsafa, na Theolojia ambayo ni taaluma ya masuala ya kiroho.

    Kwa mujibu wa historia, mwanasayansi huyo gwiji wa kuigwa alihitimu shahada zake zote mbili za sayansi, yaani 'Bachelor' na 'Masters', mwaka 1665 na 1668 katika Chuo Kikuu cha Cambridge, nchini Uingereza.

    Akiwa na umri wa miaka 84, mwanasayansi huyo anayedhaniwa na wengi kuwa bingwa wa hesabu za kisayansi kuliko wote duniani, alifariki mwaka 1727 akiwa usingizini.

    Ripoti ya uchunguzi wa mwili wake huonesha kuwa alikuwa na tatizo la figo, lakini pia alikutwa na kiasi kingi cha zebaki.

    Zebaki hiyo, yamkini, ni kutokana na kudumu mno kwenye maabara za Kemia na Fizikia, ambazo hutumia kemikali aina mbalimbali, zikiwemo hewa za gesi, katika kufanya majaribio ya kisayansi.
    DUNIA NA MAAJABU YAKE (Muundo wa Dunia na Maajabu Yaliyomo) 1. UMRI WA DUNIA HII Dunia yetu ina historia ndefu mno tangu ilipojiunda angani, miaka takribani bilioni 4.5 iliyopita. Tarakimu za umri huo wa miaka bilioni 4.5 ni 4,500,000,000, yaani miaka milioni elfu nne na mia tano iliyopita. Dunia ambayo kwa lugha ya Kiingereza inafahamika vyema kwa jina la 'Earth', pia hujulikana kama 'the World', ikimaanishwa ulimwengu. Aidha, Dunia ni sayari pekee kwenye himaya ya sayari zilizopo chini ya jua ambayo jina lake halitokani na majina ya "Miungu wa Dola" ya Kigiriki au ya Kirumi. Asili ya jina la 'earth' ni 'erde' lenye asili ya nchini Ujerumani, na maana yake ni udongo au ardhi. Mpaka kuweza kupata umri huo wa dunia wanasayansi walifanya kazi ya kutafiti na kisha kuwasilisha matokeo yao kwenye makongamano ya kisayansi duniani, ambapo matokeo hayo yalijadiliwa kwa kina na hatimaye kukubalika kama hivi. Kumbuka katika majadiliano hayo huwepo mivutano mikali miongoni mwa wanasayansi waalikwa, ambapo pia jopo la wanasayansi wanaowasilisha utafiti husika hujikuta wakitakiwa kujibu hoja mbalimbali za wanasayansi wenzao. Kuna wakati baadhi ya matokeo ya tafiti kadhaa hukataliwa, huku watafiti husika wakitakiwa kurejea upya tafiti zao. Wanasayansi hupata umri wa sayari kwa kupima umri wa miamba ya sayari husika, ambapo mwamba wenye umri mkubwa zaidi kuliko miamba yote ndiyo huchukuliwa kuwa umri wa sayari husika. Itakumbukwa kuwa Msahafu wa Biblia (Sura ya Mwanzo 1) husimulia jinsi Mwenyezi Mungu alivyoumba "mbingu na nchi na vyote vilivyomo kwa siku 6," lakini pia Msahafu huohuo kwenye aya zingine hueleza kuwa miaka elfu moja ya duniani yaweza kuwa sawa na siku moja kwenye ya Makazi ya Mwenyezi Mungu. Ni dhahiri kuwa binadamu tukiwa hatuna hoja sahihi kwa maelezo ya aina hiyo, ndipo tunaona ni vyema mambo ya Mwenyezi Mungu kumwachia Yeye Mwenyewe Mwenyezi Mungu. 2. KUUMBIKA DUNIA, SAYARI, JUA, NYOTA Kimsingi, Dunia kama zilivyo sayari zingine zote ilijiunda kutokana na mabaki ya vitu vilivyotumika kuunda Jua. Jua ambalo ni nyota kama zilivyo nyota zote angani, lilijiunda lenyewe kwenye eneo la anga lijulikanalo kama 'Pillars of Creation' (nguzo za uumbaji) katika ukanda wa anga wenye upana ambao huonekana kutokuwa na mwisho. Ukanda huo ujulikanao kama 'Solar Nebula,' umegubikwa na mawingu ya vumbi la huko angani pamoja na aina mbalimbali za gesi na hewa, ikiwemo haidrojeni na heliumu. 'Solar' ni jina la nishati itokanayo na joto la jua, na 'Nebula' kwa lugha ya Kilatini ni "wingu" au vumbi la gesi asilia mithili ya ukungu. Hivyo, 'Solar Nebula' ni ukanda katika anga ya mbali wenye mawingu yaliyosheheni nishati yenye joto, sawa na nishati ya joto la jua. Sasa basi, tunafahamu vyema kuwa jua hutoa mionzi hatari yenye joto kali mithili ya moto mkali, na ambayo ikiboreshwa kisayansi pia huweza kutoa nishati ya umeme. Hivyo, kwa muktadha huo, hebu ngoja sasa tuleta pamoja hewa za gesi, zikiwemo haidrojeni na heliumu, mawingu yenye nishati ya umeme wa jua, vumbi la angani na tufani itokanayo na mchafuko mbaya wa hali ya hewa huko anga za mbali. Na ili kuweza kupata matokeo yanayotakiwa, hebu pia tutambue uwepo wa nguvu kubwa ya asili katika kiwango kijulikanacho kwa jina la "Supernatural Power", ambayo ndiyo huwa kisababishi cha mambo yote. Kisayansi, "Supernatural Power" ni nguvu kubwa ya asili ambayo huendesha mifumo mbalimbali ya asili, ambapo duniani nguvu hiyo hujulikana kama Nguvu ya Mungu. Nguvu asili hiyo, yaani Supernatural Power, husababisha tufani ambayo huvurumisha kwa pamoja vitu vyote hivyo, (gesi, hewa, mawingu yenye nishati ya joto na vumbi la angani) ili kuunda tufani yenye umbo la duara. Duara hiyo ni kama ile itokanayo na kimbunga kikali duniani, na ambacho sasa tutaona kikifungamanisha pamoja vitu vyote hivyo katika mchafuko mkubwa wa hali mbaya ya hewa. Natumia maneno ya msisitizo kuelezea "ukubwa" wa mchafuko huo wa hali ya hewa katika eneo hilo la anga, kwani katika kuunda sayari au nyota nguvuasili kubwa hutumika. Aidha, tufani hiyo ya duara itakayoanza kidogo kidogo kama kimbunga kikali, itazidi kukua hadi kuwa na kipenyo cha takribani kilomita 10 hadi 200 au zaidi na kwendelea. Tufani hiyo ndiyo itavurumisha kwa pamoja gesi na hewa za naitrojeni na heliumu, mawingu ya nishati ya joto na vumbi la angani (kama kifanyavyo kimbunga kikali katika eneo tambarare la duniani). Pia, wakati mchafuko huo wa hali mbaya ya hewa ukiendelea, hebu ngoja sisi watazamaji tujibanze mahali fulani kwa mbali kushuhudia duara hiyo ya tufani ikijizungusha yenyewe bila kukoma kwa kipindi cha miaka mingi. Kitakachofuata ni kuanza kuona kiini cha moto kikianza kujiunda katikati ya duara hiyo ya tufani kali, huku pia nje ya duara hiyo vitu kibao vikivutwa kujiunga na mzunguko wa hiyo tufani ya duara. Vitu hivyo ni pamoja na vumbi zaidi la angani, na gesi zaidi zenye joto kali. Wakati huohuo kipenyo na mzingo wa duara hiyo vitazidi kuongezeka upana na ukubwa, mfano wa duara yenye umbo sawa na la mpira mkubwa wa miguu. Hivyo, baada ya miaka takribani milioni moja tutashangaa kuona lile vumbi likigeuka taratibu kuwa miamba ya moto ndani ya kiini cha tufani hiyo ya duara. Miamba hiyo ni kutokana na lile vumbi la angani ambalo hatimaye limeshikamana pamoja mithili ya zege, na hatimaye kuwa miamba ndani ya tufani ya duara. Sanjari na kuundika huko ndani ya kitovu cha hiyo tufani ya duara, pia kwelekea nje ya duara hiyo utaundika udongo ambao ardhi, mchanga na mawe. Kimsingi, vitu hivyo pia ni matokeo ya lile vumbi la angani ambalo lilikusanywa pamoja na kuvutwa na kasi ya mzunguko wa tufani. Hatua hiyo mpya inatokana na kuwepo mshikamano na mgandamizo wa zile chembechembe za lile vumbivumbi ndani ya tufani. Vurumai hiyo ya mzunguko wa hiyo tufani ya duara yenye vumbi, itazidi kukua hadi kuunda sumaku ya asili ndani ya kile kitovu cha duara ya tufani. Kutokana na duara hiyo ya tufani kuongezeka ukubwa, hatimaye sumaku iliyopo kwenye kitovu cha duara hiyo itaishiwa nguvu ya kwendelea kunasa vumbi zaidi kuja kwenye mzingo wa hiyo duara ya tufani. Kumbuka kuwa wakati huo hiyo duara pia itaunda kimo kutoka kwenye usawa wa ardhi yake kwenda ndani kwenye kitovu chake, na hivyo kuwa duara ya mviringo kama umbo mfano wa mpira mchezo wa miguu. Baada ya kupita maelfu ya miaka mingi, duara hiyo ambayo hapo awali ilianza kama umbo la tufani na kuzidi kukua huko angani, sasa itakuwa na joto kali kupita kiasi na kuanza kung'aa kama jua. Jua hilo, ndiyo nyota mojawapo ya zile ambazo huonekana usiku ziking'aa angani. Lakini pia wakati wa kujiunda nyota hiyo, kama tulivyoona hapo awali, baadhi ya mabaki yake yaliyokuwa yakitawanyika angani wakati ile tufani ya duara ikijizungusha, huweza kujikusanya pamoja na kuunda sayari ambazo huzunguka baadhi ya hizo nyota. Hivyo ndivyo zilivyojiunda sayari zote ambazo huelea kwa kulizunguka jua letu. Mathalani, sayari zote ambazo hulizunguka jua, ikiwemo dunia zilijiunda kutokana na mabaki ya vitu kama gesi, michanga na mawe ambavyo vilitawanyika angani wakati jua likijiunda (kama ambavyo imeelezwa hapo awali). 3. KIINI CHA DUNIA Dunia yetu ambayo wastani wa nusu kipenyo cha umbo lake la duara ni kilomita 6,371, mzingo wake ni kilomita takribani 40,041. Kama zilivyo sayari zote katika himaya ya jua, dunia nayo ilijiunda wakati jua likijiunda lenyewe. Yaani kwamba sayari ni mabaki ya vitu vilivyotumika kuliunda jua. Kadhalika kama zilivyo sayari zingine zote, dunia nayo ina kiini chake ambacho kipo katikati ya ardhi yake. Kiini hicho kina nguvu kubwa ya sumaku ambayo, pamoja na mambo mengineyo, 'huvuta' umbo hilo la duara kutoka juu ya ardhi kwenda katikati ya kiini hicho. Muundo huo ndio hulifungamanisha pamoja umbo la duara la dunia, na hivyo kuzuia umbo hilo lisifumke kutoka ardhini na kusambaratika. Hiyo ni sawa na mpira wa miguu unavyoweza kupasuka na kusambaratika, kama utajazwa upepo kupita kiasi chake. Kiini hicho ambacho kipo katikati kabisa ya dunia, kinajulikanacho kwa jina la kisayansi la 'Inner Core.' Kiini hicho kina joto kali la sentigredi 6,230 ambacho ndio kiasi cha joto la jua. Kiini hicho kina umbo la duara lenye nusu kipenyo cha kilomita 1,250. Kama ingetokea kuchimba ardhi wima kwenda kwenye kiini hicho, mchimbaji angeanza kukutana na joto la kiini hicho kuanzia kimo cha umbali wa kilomita 5,150 kutoka usawa wa juu ya ardhi tunayotembea. Katika historia ya uchimbaji ardhi, kina kirefu kilichowahi kuchimbwa ardhini ni mita 12,345 (kilomita 12.345) huko Sakhalini, nchini Urusi, kwa ajili ya uvunaji wa mafuta ya petroli. Kiini cha dunia kinaundwa na madini mchanganyiko wa nikeli (nickle), chuma (iron) na dhahabu. Kwa mujibu wa utafiti, inakadiriwa kuwa kama dhahabu hiyo ingechimbwa na kuchomwa mpaka kuwa kimiminika sawa na uji na kisha kumwagwa chini, ingeweza kuifunika dunia yote kwa unene wa sentimeta 45. Kiini hicho muhimu kwa uhai wa sayari hii ya dunia kiligunduliwa mwaka 1936 na mtaalamu wa matetemeko ya ardhi wa nchini Denmark, mwanamama Dkt. Inge Lehmann. Dkt. Lehmann alihitimu shahada yake ya kwanza katika fani ya Hisabati mwaka 1910, ya Uzamili mwaka 1920 (zote kutoka Chuo Kikuu cha Copenhagen nchini mwake), na ile ya Uzamivu kutoka Chuo Kikuu cha Cambridge nchini Uingereza. Alifariki kwa uzee mwaka 1993 akiwa na umri wa miaka 104. 4. MAJI DUNIANI Kupatikana maji kwenye dunia yetu, ni mojawapo ya miundo ambayo haipo katika sayari zingine ambazo tuna taarifa za kitafiti kuzuhusu. Maji ni muhimili muhimu kwa ajili ya uhai wa viumbe wote na mimea, ambavyo kwa pamoja havipo katika sayari zingine za himaya ya jua. Kwa mujibu wa tafiti nyingi ambazo zimefanyika kwa miongo mingi ya miaka kujaribu kubaini nini chanzo cha kuwepo maji duniani, hakuna hata utafiti mmoja ulioonesha kwa usahihi matokeo ya kuridhisha. Miongoni mwa tafiti hizo ni pamoja na ule wa mwaka 2005, ambapo Mkuu wa Idara ya Masomo ya Sayari na Mwezi katika Chuo Kikuu cha Arizona nchini Marekani, Profesa Michael Julian Drake, na mwenzake ambaye ni mtaalamu wa Vimondo, Dkt. Huberto Campins, wa Chuo Kikuu cha Central Florida, walitafiti nini chanzo cha kuwepo maji duniani. Katika mawasilisho yao kwenye kongamano la kisayansi la Chama cha Wanataaluma wa Maarifa ya Anga za Juu (IAU), watafiti hao walikanusha madai ya uwezekano wa dunia hapo kale kugongwa na kimondo kikubwa na kusababisha maji kulipuka kutoka ardhini. Wakiwasilisha matokeo ya utafiti wao kwenye mkutano wa kongamano hilo, magwiji hao wa masuala ya sayari walieleza kwenye waraka wao uitwao "Origin of water on the terrestial planets" (chanzo cha kuwepo maji kwenye sayari). Walidai kuwa maji yaliyopo duniani yaliumbika kwenye ardhi ya dunia tangu mwanzo, wakati ikijiunda angani. Ikumbukwe kuwa eneo la uso wa dunia likiwa ni jumla ya kilomita za mraba milioni 510, asilimia 70.8 ya eneo hilo imefunikwa na maji na asilimia 29.2 ni nchi kavu, ikiwemo milima, mabonde na ardhi tambarare. 5. HEWA YA OKSIJENI Muundo mwingine muhimu katika sayari hii ya dunia ni hewa ambazo ni tawala, yaani Naitrojeni ambayo kwa usahihi imeenea kwa asilimia 78.08 ya hewa yote ya dunia, Oksijeni asilimia 20.95, 'Argon' asilimia 0.93, hewa ya Ukaa (Carbon dioxide) asilimia 0.039, na asilimia moja ni hewa mithili ya mvuke wa maji (water vapour). Hewa ya Oksijeni ambayo ni nguzo muhimu kwa ajili ya uhai wa viumbe wote na pia haipatikani kwenye sayari nyingine chini ya jua, inadhaniwa ilianza kupatikana duniani miaka takribani bilioni 2.5 iliyopita kufuatia "kukomaa kwa kiini cha dunia." Kwa mujibu wa matokeo ya tafiti mbalimbali na nadharia za kisayansi, inaoneshwa kuwa kukomaa kwa kiini hicho cha dunia hatimaye ndiko kulisababisha kuzuka duniani milipuko ya volikano ambayo pia ilisababisha kuzuka mabonde na milima. Inaoneshwa kuwa tayari wakati huo maji yaliishakuwepo duniani, na kuwezesha kuzuka chembechembe ndogo sana za kibakteria zijulikanazo kwa jina la kisayansi la 'cyanobacteria' au 'blue-green algae'. Kwa kutumia mwanga wa jua, maji na hewa ya ukaa, chembechembe hizo ziliweza kuzalisha hewa mbalimbali, ikiwemo 'Carbonhydrates' na Oksijeni. Kwa kuwa hizo chembechembe ndogo za kibakteria huishi baharini, ilikuwa rahisi kwa oksijeni kutokea baharini kupepea na kuenea katika anga ya dunia na kuzuiliwa hapo na nguvu asili ya uvutano ya dunia ili pia ibaki ikienea pote duniani. Mpaka wakati wa kuzuka duniani mimea na viumbe hai miaka takribani bilioni 3.5 iliyopita, tayari oksijeni ilikwa ni tele duniani; na hivyo kutumika kudumisha uhai wa viumbe hadi wakati huu. 6. UKANDA WA 'OZONE' Muundo mwingie muhimu wa asili kwa dunia ni ukanda wa anga ujulikanao kwa jina la 'ozone' ambao umetanda kama 'mwavuli' kwenye anga ya dunia, na kuikinga isidhuriwe na mionzi hatari ya sumu kutoka kwenye Jua. Ukanda huo maarufu kama 'ozone layer' umetanda kuanzia usawa wa kilometa 15 kutoka ardhini kwenda juu angani mpaka ukomo wa kilomita takribani 50, ambapo huchuja asilimia kati ya 97 na 99 ya mionzi hatari kwenye miale ya joto la jua. Miongoni mwa matatizo yanayosababishwa na mionzi hiyo hatari kutoka kwenye jua, ni pamoja na magonjwa ya saratani ya ngozi kwa bianadamu. Pia juu ya ukanda wa tabaka la ozone kuna ukanda mwingine uitwao "atmosphere" ambao ni madhubuti kiasi kwamba vitu vinavyotoka anga za juu na kujaribu kuupenya ili kufika duniani, hukumbana na joto kali na kusambaratishwa kwa kuunguzwa. Si kwamba tabaka hilo lina joto, isipokuwa kasi ya "kuanguka" vitu hivyo kutoka juu angani kuja dunia husababisha msuguano na chembechembe za gesi katika eneo hilo na kuzalisha joto mithili ya ndimi za moto. Picha za video za vyombo vya 'Apollo' vikirejea duniani kutoka mwezini vikiwa na wanaanga ndani yake na kupenya tabaka hilo kwa kasi ya kilomita 39,000 kwa saa, huonekana kughubikwa na ndimi za moto wa rangi ya njano na bluu. Rangi hizo ni ishara ya ukali wa moto huo, lakini kutokana na waundaji wa vyombo hivyo kutumia mchanganyiko wa mabati na plastiki ngumu visivyopenywa na joto, Apollo huonekana kulichana tabaka hilo na kutokea upande wa pili ambao ni anga ya dunia. Hivyo basi, mfano huo mdogo unaonesha uimara wa tabaka hilo la 'ozone', ambalo kama ambavyo tumeona huchuja mionzi ya sumu kutoka kwenye mwanga wa jua ili kutolete madhara kwa viumbe duniani. Mwanga huo ukisafiri kutoka juani umbali wa kilomita milioni 150 kwa kasi ya kilomita 299,793, hutua duniani ndani ya dakika 8 na sekunde 19 ukiwa tayari umechujwa wakati ukipenya tabaka hilo. 'Ozone' iligunduliwa mwaka 1913 na wanasayansi wawili wa nchini Ufaransa, Charlest Fabry na Henri Buisson, ambapo kipimo cha kasi ya mwanga kiligunduliwa na mwanasayansia wa anga za juu wa nchini Denmark, Ole Roemer, mwaka 1676. 7. NGUVU ASILI YA UVUTANO Muundo mwingine wa dunia ni nguvu ya asili ya uvutano ya dunia, maarufu kama 'gravitation', ambayo huvuta vitu kuvirejesha chini duniani pale vinaporushwa kwenda juu au vile vinavyoanguka kutoka juu angani. Nguvu hiyo ina manufaa makubwa, kwani bila kuwepo duniani binadamu na viumbe wengine wangepeperuka kama karatasi kwenda juu wakati wakitembea juu ya ardhi ya hii. Kadhalika, nguvu hiyo husaidia kuvuta hewa ya oksijeni na kuiweka karibu na ardhi kwa ajili ya matumizi mbalimbali. Pia, nguvu hiyo husaidia kuiweka dunia, mwezi, jua na sayari zingine katika uwiano wa umbali usio na madhara kutoka kila moja. Nguvu hiyo ya asili ndiyo huliweka joto la jua duniani na kubaki kuwa katika kiwango kinachotakiwa, na hivyo kuwezesha viumbe kupata joto la wastani na pia katika kiwango mwanana. Nguvu hiyo huvuta mvua kuja duniani na kuwezesha maji ya bahari, maziwa na mito kutulia duniani. Mathalani, bila nguvu asili hiyo kuwepo duniani, maji 'yangemwagika' kutoka duniani kwa kutawanyika kama upepo na kupaa kwenda juu angani na kutoweka kabisa. Na ndio maana ukirusha maji kwenda juu, hurudi chini ardhini. Hebu angalia mfano huu kwamba wanaanga waliokwenda mwenzini walilazimika kuvaa mavazi yenye uzito wa kilo 80 hapa duniani, lakini mavazi hayo kule mwezini yakawa na uzito wa kilo 3. Mavazi hayo, yaani viatu, koti, suruali, na kofia nzito yenye miwani maalumu ya kukinga macho dhidi ya mionzi hatari ya jua, vyote kwa pamoja viliunganishwa na kuwa mfano wa sare za 'ovaroli' za mafundi wa magari. Mavazi hayo pia mgongoni yakiwa yameunganishwa kwa pamoja na mtungi wa hewa ya oksijeni kwa ajili ya kupumua, yalivaaliwa mahsusi muda mfupi baada ya chombo kutua mwezini. Hivyo, msomaji wangu tafakari nini kilisababisha mavazi kuwa mazito hapa duniani, lakini yawe mepesi kule mwezini? Jibu ni kwamba nguvu asili ya uvutano hapa duniani ni kubwa kuliko ya kule mwezini. Na ndipo tunaona umuhimu wa muundo huo wa nguvu asili ya uvutano, ambapo hapa duniani huvuta vitu kuja chini kwa kasi ya mita 9.81 kwa sekunde, lakini kwa kuwa nguvu ya mwezi ni hafifu, huvuta vitu kwa kasi ndogo ya mita 1.62 kwa sekunde. Ingawa nguvu hiyo ya asili iligunduliwa kuwepo duniani miaka mingi iliyopta, mwanafizikia bingwa wa Uingereza, Sir Isaac Newton (1642-1727), ndiye anatambulika kama mgunduzi wa hesabu hizo za nguvu asili hiyo. Anaeleza kuwa vitu vyote vyenye maumbo asili, ikiwemo jua, sayari, dunia, mwezi, na vimondo, kila kimoja kina nguvu hiyo katika viwango tofauti. Kanuni hiyo, kwa mujibu wa matokeo ya utafiti wake, hueleza kuwa nguvu hiyo ndiyo hufanya jua kuvuta sayari zake ili kulizunguka, huku pia kila sayari ikitumia nguvu 'binafsi' (na kwa uwiano maalumu) kujihami isivutwe hadi kwenda kuligonga jua au kugongana na sayari zingine au vimondo. Nguvuasili ya jua ni mita 274 kwa sekunde, ikiwa ni zaidi ya kiasi cha nguvuasili ya kila sayari. Muundo huo wa kila sayari kujihami kivyake katika mstari wa njia yake hufahamika kisayansi kama "sayari kuhami mazingira ya njia yake"; yaani kwamba 'a planet has to clear the neighbourhood around its orbit.' Newton akiwa amezaliwa 'mtoto-njiti' na baadaye kuibuka kuwa mwenye akili nyingi kiasi cha kukaribia kuwa sawa na mtu wa miujiza, hakuwahi kuoa kutokana na kinachoelezwa kuwa ni " kutokana na kutingwa na shughuli za kimasomo." Huoneshwa kuwa muda mwingi alikuwa maabara akifanya tafiti mbalimbali za kisayansi, au akiwa maktaba akijisomea, ama akiandika kitabu, au akifundisha wanafunzi wake. Alikuwa bingwa mwenye kipaji cha taaluma nyingi, ikiwemo Fizikia, Kemia, Hisabati, Maarifa ya Anga za Juu, Uchumi, Falsafa, na Theolojia ambayo ni taaluma ya masuala ya kiroho. Kwa mujibu wa historia, mwanasayansi huyo gwiji wa kuigwa alihitimu shahada zake zote mbili za sayansi, yaani 'Bachelor' na 'Masters', mwaka 1665 na 1668 katika Chuo Kikuu cha Cambridge, nchini Uingereza. Akiwa na umri wa miaka 84, mwanasayansi huyo anayedhaniwa na wengi kuwa bingwa wa hesabu za kisayansi kuliko wote duniani, alifariki mwaka 1727 akiwa usingizini. Ripoti ya uchunguzi wa mwili wake huonesha kuwa alikuwa na tatizo la figo, lakini pia alikutwa na kiasi kingi cha zebaki. Zebaki hiyo, yamkini, ni kutokana na kudumu mno kwenye maabara za Kemia na Fizikia, ambazo hutumia kemikali aina mbalimbali, zikiwemo hewa za gesi, katika kufanya majaribio ya kisayansi.
    0 Commentarii ·0 Distribuiri ·2K Views
  • KISIWA CHA PALMESTON KILICHO MWISHO WA DUNIA Kisiwa hiki ni moja ya jumuiya ya watu wanaoishi pembezoni mwa dunia.Kisiwa kidogo kilicho bahari ya pacific kinaitwa kisiwa cha palmeston.Kiko chini ya usimamizi wa nchi ya New zealand wanaletewa meli ya mahitaji yao muhimu mara mbili tu kwa mwaka umbali kilipo mkubwa mno na kukifikia ni safark ndefu sana na hatari kwa wanaopenda kukitembelea. Cha ajabu zaidi wakazi wake 62 wote ni uzao wa mtu mmoja mwingereza aliyefika hapo toka mji wa Leicester miaka 150 iliyopita Mr Willim Markmaster.Kutoka Leicester hadi alipofika mtu huyo ni umbali wa km 10,000 alikuja na captain Cook akampa kazi ya kupanda minazi akabakia hapo Safari ndefu ya kukifikia usiku na mchana kwa boti na mawimbi ya bahari ya pacific ilivyo kubwa ni mbali mno binadamu wa kawaida kuweza kufikiria ndio maana kikaitwa kiko mwisho wa dunia. Markmasters alipewa umiliki huo na malikia Victoria mwaka 1850.Umbali kutoka kisiwa hicho hadi New zealand wanaowaletea mahitaji muhimu ni km 5299 baharini.Kisiwa cha karibu ambacho kwao wanaona ni jirani ni kisiwa cha Rarotonga kiko umbali wa km 3148.Kusafiri kwa boti ni siku nne safari ya usiku na mchana.Linapofika suala la huduma kuhitaji huduma ya kutibiwa jino iko kisiwa hicho cha karibu ya km 3148.Mama mzee kuliko wote kisiwa hicho mama Aka mwenye miaka 92 alikwenda kutibiwa jino kisiwa cha karibu cha Rarotonga alipotibiwa usafiri wa kurudi kisiwani kwake ilibidi asubiri miezi sita kupata meli ya kumrudisha nyumbani. Ila wananchi wake wanaishi maisha ya raha sana kuna kanisa,shule na huduma za internet kwa ujumla ni watu wanaoishi maisha ya raha na amani sana.Kisiwani humo kuna polisi mmoja tu na inasemekana ni polisi mwenye raha asiye na kazi ngumu kuliko polisi wote duniani kwa vile uzao wao wote wana damu moja.Hakuna gari wala uwanja wa ndege wala gari ila wanaishi vizuri mno.Kutoka kisiwa hicho hadi mji wa Capetown Africa kusini ni km 11,154 baharini.Picha kushoto ni kisiwa hicho kulia ni bibi Mama Aka alipokuwa hospitali anasubiri meli ije baada ya miezi sita.
    KISIWA CHA PALMESTON KILICHO MWISHO WA DUNIA Kisiwa hiki ni moja ya jumuiya ya watu wanaoishi pembezoni mwa dunia.Kisiwa kidogo kilicho bahari ya pacific kinaitwa kisiwa cha palmeston.Kiko chini ya usimamizi wa nchi ya New zealand wanaletewa meli ya mahitaji yao muhimu mara mbili tu kwa mwaka umbali kilipo mkubwa mno na kukifikia ni safark ndefu sana na hatari kwa wanaopenda kukitembelea. Cha ajabu zaidi wakazi wake 62 wote ni uzao wa mtu mmoja mwingereza aliyefika hapo toka mji wa Leicester miaka 150 iliyopita Mr Willim Markmaster.Kutoka Leicester hadi alipofika mtu huyo ni umbali wa km 10,000 alikuja na captain Cook akampa kazi ya kupanda minazi akabakia hapo Safari ndefu ya kukifikia usiku na mchana kwa boti na mawimbi ya bahari ya pacific ilivyo kubwa ni mbali mno binadamu wa kawaida kuweza kufikiria ndio maana kikaitwa kiko mwisho wa dunia. Markmasters alipewa umiliki huo na malikia Victoria mwaka 1850.Umbali kutoka kisiwa hicho hadi New zealand wanaowaletea mahitaji muhimu ni km 5299 baharini.Kisiwa cha karibu ambacho kwao wanaona ni jirani ni kisiwa cha Rarotonga kiko umbali wa km 3148.Kusafiri kwa boti ni siku nne safari ya usiku na mchana.Linapofika suala la huduma kuhitaji huduma ya kutibiwa jino iko kisiwa hicho cha karibu ya km 3148.Mama mzee kuliko wote kisiwa hicho mama Aka mwenye miaka 92 alikwenda kutibiwa jino kisiwa cha karibu cha Rarotonga alipotibiwa usafiri wa kurudi kisiwani kwake ilibidi asubiri miezi sita kupata meli ya kumrudisha nyumbani. Ila wananchi wake wanaishi maisha ya raha sana kuna kanisa,shule na huduma za internet kwa ujumla ni watu wanaoishi maisha ya raha na amani sana.Kisiwani humo kuna polisi mmoja tu na inasemekana ni polisi mwenye raha asiye na kazi ngumu kuliko polisi wote duniani kwa vile uzao wao wote wana damu moja.Hakuna gari wala uwanja wa ndege wala gari ila wanaishi vizuri mno.Kutoka kisiwa hicho hadi mji wa Capetown Africa kusini ni km 11,154 baharini.Picha kushoto ni kisiwa hicho kulia ni bibi Mama Aka alipokuwa hospitali anasubiri meli ije baada ya miezi sita.
    0 Commentarii ·0 Distribuiri ·411 Views
  • Yafuatayo Yanapaswa Kuzingitiwa kabla Ya Kufungua Channel ya YouTube ...............

    USIWAZE HELA KWANZA

    1: Uwe na Idea ( Topic ) ya Kitu Cha kufanya / Content Gani Unataka ufanye na Katika Hilo uwe Interested ( Uwe unakipenda unachotaka kufanya )

    Baada ya kujua Topic / Idea fanya kifuatacho

    A: Tafuta Watu wanaofanya Hiyo idea Yako kama wapo angalia video zao zipoje Katika Mitandao yote ( YouTube,,, Facebook,, Instagram na TikTok and X( Twita )

    Then Unapoangalia Video hizo hakikisha unazingatia yafuatayo

    1A: Jinsi wanavyo andaa content/ Maudhui Yao wanafanyeje mpaka zinapata watazamaji wengi

    1B: Tittle/ Vichwa vyao vya Habari vinaandikwaje angalia maneno ambayo mara nyingi wanatumia Hasa kwenye video Zenye watazamaji wengi Kuanzia 5k-100k nakuendelea Kisha Note Pembeni

    1C: Angalia namna wanavyo edit / Hariri video zao wanatumia picha / Video na wanatumia video Kwa kuzipata wapi ila muhimu Kuzingatia Haki miliki unashauriwa kutumia picha kabla hujajua video wanatoa wapi usije pewa Copyright strike au claim

    1D: Angalia Mda ambao wanaaplod video zao na urefu wa video zao upoje Ili na wewe ucheze ndani ya ule mda mpaka watazamaji wako watakapo Kupata mda sahihi ndani ya YouTube studio as day goes utaona..

    1E: Katika hayo yote angalia Mtiririko na mpangilio wa Sauti Zao upoje Kisha tengeneza Sauti Yako Wala usiwaige ila kujifunza Muhimu

    1F: Baada ya hapo jifunze kuediti video Kwa kutumia Simu au computer hili pia linategemeana na kifaa ambacho unacho kama unatumia Simu bas application za kueditia zipo nyingi

    NB: Zipo ambazo Zina logo na nyingine hazina Logo

    Mfano wa Application Ambazo zinapatikana Kwa urahisi

    1: KineMaster
    2: Inshort
    3: Yo Cut
    3: Free Mora kama sijakosea kuandika Watasahihisha

    Baada ya hayo Jifunze yafuatayo

    1: Kuandika Script/ Kuandika Nini Unataka Kuzungumza kwenye video zako hata kama unafanya Movie za kushuti lazima ziwe na Script

    2: Usitumie Background yeyote kama hujaitengeneza mwenyewe ila Ushauri Mzuri kabla ya monitization Tumia sauti Yako Tu na baada ya monitization unaweza tengeneza Music Yako ukaitumia chini ya Sauti

    3: Tumia Picha/ Video nzuri If possible unapoandaa video zako Ili kuwavutia watazamaji wako

    4: Usitumia lugha ya matusi au Lugha isiyo Rafiki Kwa watazamaji hutaonja pesa NG'O

    5: Penda kutumia Tittle ambayo inafanana au kuwiana na kile ulicho andaa ndani ya video ( uongo ni mzuri Kupata Temporary views ila Ukweli utakufanya udumu na watu wakupende zaidi)
    Uongo unaweza futiwa channel endapo wakaripoti channel Yako

    Then Fanya pia yafuatayo

    Hakikisha una email ambayo itakuruhusu Kufungu channel ,,, weka password strong fanya verification Kwa kufuata maelekezo Yao.

    Hamia kipengele Cha Kujua Channel Yako utaipa jina Gani na kwanini uipe jina Hilo? Usiweke jina gumu linaloshindwa kutafutwa na watu mfano ( Ngedere Media / Ngedere Movie/ Ngedere/ Ngedere Mitini ni Simple sana mtu kusearch channel Yako Sasa unakuta mtu

    kaandika ( Hy information today Upload ) jina refu kama njaa ya Asubuhi

    3: Tengeneza Animation intro ya sec kuanzia 5-10 Hivi itakayo kusaidia kubust masaa

    4: Tengeneza Logo Safi

    5: Bana ya YouTube nayo iwe Bomba

    6: Subscription Button yenye logo Yako nayo iwepo

    NB: Kwa MAHITAJI ya Animation intro, logo, Bana , subscription button nipo hapa gharama yake ni 15K Kwa Kila Kimoja na ofa flan ya kipekee utapata

    7: Usipende kufuta video baada ya Kuwekewa matangazo na Kuanza kulipwa futa video ambayo unahisi haiko poa before monitization la sivyo utaja Kujuta... ( USHAURI WANGU USIFUTE VIDEO HATA 1 Hivyo hakikisha unapoandaa video zako zisiwe na kiashiria Cha baadae inakuja kufutwa noooo

    8: Ukiaplod video zako YouTube usiangalie Either Kwa Simu Yako au Email Nyingine iliyopo kwenye Simu Yako ukifanya hivyo hutadumu Daima YouTube watakupa invalid click na kukufitia channel panapo bidi
    9: Zingatia Device kifaa ambacho unaweza Tumia kuhifadhi au Kufungua account Yako ya YouTube kiwe salama kisiwe na Tatizo la kufutiwa channel Kwa copyright strike 3 za nguvu Tena ikiwezekana nunua Simu mpya kama Ulivyo nayo unamashaka nayo

    10: Share video zako kwenye Mitandao ya kijamii Kwa kuwapa link kabla hujaingia Monitization then Baada ya hapo unaweza share video only sio link Tena

    11: Kila video mpya unayopakia YouTube hakikisha inaubunifu mpya tofauti na wajana

    12: Usikate Tamaa Kwa Kuanza Kupata views Wachache mwanzo labda wawili au 10 safari ya YouTube huanza chini Kisha kwenda juu japo wapo wanaoanza na views 100k then wanaishia 11 views pee day




    📌 Yafuatayo Yanapaswa Kuzingitiwa kabla Ya Kufungua Channel ya YouTube ............... USIWAZE HELA KWANZA 😁😁 1: Uwe na Idea ( Topic ) ya Kitu Cha kufanya / Content Gani Unataka ufanye na Katika Hilo uwe Interested ( Uwe unakipenda unachotaka kufanya ) Baada ya kujua Topic / Idea fanya kifuatacho A: Tafuta Watu wanaofanya Hiyo idea Yako kama wapo angalia video zao zipoje Katika Mitandao yote ( YouTube,,, Facebook,, Instagram na TikTok and X( Twita ) Then Unapoangalia Video hizo hakikisha unazingatia yafuatayo 1A: Jinsi wanavyo andaa content/ Maudhui Yao wanafanyeje mpaka zinapata watazamaji wengi 1B: Tittle/ Vichwa vyao vya Habari vinaandikwaje angalia maneno ambayo mara nyingi wanatumia Hasa kwenye video Zenye watazamaji wengi Kuanzia 5k-100k nakuendelea Kisha Note Pembeni 1C: Angalia namna wanavyo edit / Hariri video zao wanatumia picha / Video na wanatumia video Kwa kuzipata wapi ila muhimu Kuzingatia Haki miliki unashauriwa kutumia picha kabla hujajua video wanatoa wapi usije pewa Copyright strike au claim 1D: Angalia Mda ambao wanaaplod video zao na urefu wa video zao upoje Ili na wewe ucheze ndani ya ule mda mpaka watazamaji wako watakapo Kupata mda sahihi ndani ya YouTube studio as day goes utaona.. 1E: Katika hayo yote angalia Mtiririko na mpangilio wa Sauti Zao upoje Kisha tengeneza Sauti Yako Wala usiwaige ila kujifunza Muhimu 1F: Baada ya hapo jifunze kuediti video Kwa kutumia Simu au computer hili pia linategemeana na kifaa ambacho unacho kama unatumia Simu bas application za kueditia zipo nyingi NB: Zipo ambazo Zina logo na nyingine hazina Logo Mfano wa Application Ambazo zinapatikana Kwa urahisi 1: KineMaster 2: Inshort 3: Yo Cut 3: Free Mora kama sijakosea kuandika Watasahihisha 😁😁😁 Baada ya hayo Jifunze yafuatayo 1: Kuandika Script/ Kuandika Nini Unataka Kuzungumza kwenye video zako hata kama unafanya Movie za kushuti lazima ziwe na Script 2: Usitumie Background yeyote kama hujaitengeneza mwenyewe ila Ushauri Mzuri kabla ya monitization Tumia sauti Yako Tu na baada ya monitization unaweza tengeneza Music Yako ukaitumia chini ya Sauti 3: Tumia Picha/ Video nzuri If possible unapoandaa video zako Ili kuwavutia watazamaji wako 4: Usitumia lugha ya matusi au Lugha isiyo Rafiki Kwa watazamaji hutaonja pesa NG'O 😳😳 5: Penda kutumia Tittle ambayo inafanana au kuwiana na kile ulicho andaa ndani ya video ( uongo ni mzuri Kupata Temporary views ila Ukweli utakufanya udumu na watu wakupende zaidi) Uongo unaweza futiwa channel endapo wakaripoti channel Yako Then Fanya pia yafuatayo Hakikisha una email ambayo itakuruhusu Kufungu channel ,,, weka password strong fanya verification Kwa kufuata maelekezo Yao. Hamia kipengele Cha Kujua Channel Yako utaipa jina Gani na kwanini uipe jina Hilo? Usiweke jina gumu linaloshindwa kutafutwa na watu mfano ( Ngedere Media / Ngedere Movie/ Ngedere/ Ngedere Mitini ni Simple sana mtu kusearch channel Yako Sasa unakuta mtu kaandika ( Hy information today Upload ) jina refu kama njaa ya Asubuhi 3: Tengeneza Animation intro ya sec kuanzia 5-10 Hivi itakayo kusaidia kubust masaa 4: Tengeneza Logo Safi 5: Bana ya YouTube nayo iwe Bomba 6: Subscription Button yenye logo Yako nayo iwepo NB: Kwa MAHITAJI ya Animation intro, logo, Bana , subscription button nipo hapa gharama yake ni 15K Kwa Kila Kimoja na ofa flan ya kipekee utapata 7: Usipende kufuta video baada ya Kuwekewa matangazo na Kuanza kulipwa futa video ambayo unahisi haiko poa before monitization la sivyo utaja Kujuta... ( USHAURI WANGU USIFUTE VIDEO HATA 1 Hivyo hakikisha unapoandaa video zako zisiwe na kiashiria Cha baadae inakuja kufutwa noooo 8: Ukiaplod video zako YouTube usiangalie Either Kwa Simu Yako au Email Nyingine iliyopo kwenye Simu Yako ukifanya hivyo hutadumu Daima YouTube watakupa invalid click na kukufitia channel panapo bidi 9: Zingatia Device kifaa ambacho unaweza Tumia kuhifadhi au Kufungua account Yako ya YouTube kiwe salama kisiwe na Tatizo la kufutiwa channel Kwa copyright strike 3 za nguvu Tena ikiwezekana nunua Simu mpya kama Ulivyo nayo unamashaka nayo 10: Share video zako kwenye Mitandao ya kijamii Kwa kuwapa link kabla hujaingia Monitization then Baada ya hapo unaweza share video only sio link Tena 11: Kila video mpya unayopakia YouTube hakikisha inaubunifu mpya tofauti na wajana 12: Usikate Tamaa Kwa Kuanza Kupata views Wachache mwanzo labda wawili au 10 safari ya YouTube huanza chini Kisha kwenda juu japo wapo wanaoanza na views 100k then wanaishia 11 views pee day 🙏🙏🙏🙏🙏
    Like
    Love
    3
    · 0 Commentarii ·0 Distribuiri ·2K Views
  • program Bora za kuediti video kwenye simu yako ambazo zimeshalipiwa unatumia Bure tu
    1.inshot
    https://inshotpro.app/dl-mod

    2. KineMaster
    https://kinemastermodapk.org/files3/download/file-4/

    3. Youcut
    https://download-new.apkmody.fun/apps/youcut/download/mod

    4. Capcut
    https://hole.apkdone.download/s/qHNEgLzEYHYS9jG/download

    5. Filmora
    https://www.filmora.cc/get/download/file-1/

    6. Powerdirector
    https://powerdirector.pro/download/download/file-1/

    program Bora za kuediti video kwenye simu yako ambazo zimeshalipiwa unatumia Bure tu 👇 1.inshot https://inshotpro.app/dl-mod 2. KineMaster https://kinemastermodapk.org/files3/download/file-4/ 3. Youcut https://download-new.apkmody.fun/apps/youcut/download/mod 4. Capcut https://hole.apkdone.download/s/qHNEgLzEYHYS9jG/download 5. Filmora https://www.filmora.cc/get/download/file-1/ 6. Powerdirector https://powerdirector.pro/download/download/file-1/
    Like
    Love
    2
    · 0 Commentarii ·0 Distribuiri ·586 Views
  • HOW TO DEPLOY WHATSAPP BOT

    > Prepared by *DUDUU_MENDEZ* with credit from *GIFTED-MD*


    https://youtu.be/1ODAvpW9D98?si=-PQvLFpHyo6CLyXP


    Many sincere thanks to my following teachers and masters

    > SUHAIL XMD
    > GIFTED-MD
    > BMX
    > BLACK PANTHER
    > PRABHAT
    > ETHIX MD
    > SPIDER
    > FLASH MD
    > VENOCYBER

    For more coins join
    https://whatsapp.com/channel/0029VacgCaPKmCPGmTmrnT04

    > 𝐃𝐔𝐃𝐔𝐔_𝐌𝐄𝐍𝐃𝐄𝐙 V4
    ▶︎ ●────────── 0:41
    HOW TO DEPLOY WHATSAPP BOT > Prepared by *DUDUU_MENDEZ* with credit from *GIFTED-MD* https://youtu.be/1ODAvpW9D98?si=-PQvLFpHyo6CLyXP Many sincere thanks to my following teachers and masters > SUHAIL XMD🇵🇰 > GIFTED-MD🇰🇪 > BMX🇰🇪 > BLACK PANTHER🇰🇪 > PRABHAT 🇵🇰 > ETHIX MD 🇵🇰 > SPIDER 🇰🇪 > FLASH MD 🇰🇪 > VENOCYBER 🇹🇿 For more coins join https://whatsapp.com/channel/0029VacgCaPKmCPGmTmrnT04 > 𝐃𝐔𝐃𝐔𝐔_𝐌𝐄𝐍𝐃𝐄𝐙 V4 ▶︎ ●────────── 0:41
    Like
    Angry
    2
    · 1 Commentarii ·0 Distribuiri ·517 Views
  • Sex Master ila huyu jamaa balaa Wanawake wote hao duh!!!
    Sex Master 😂😂 ila huyu jamaa balaa Wanawake wote hao duh!!!
    0 Commentarii ·0 Distribuiri ·63 Views
  • Zungu

    "Mbali na matokeo inaelezwa kuwa Master Gamondi alipoteza mvuto kwenye dressing room

    Maelewano hafifu na viongozi wenzake, kingine kukubali Yanga kutokukaa kambini yani wachezaji kutokea makwao lilikuwa kosa kubwa ,Wenyeji wa mikocheni Masaki na Mbezi beach si ajabu kwao kukutana na wachezaji wa Yanga mtaani siku chache hata kabla ya mechi

    Kwa mfano mechi kati ya Yanga na Tabora wachezaji wa Yanga waliingia kambini masaa 24 kabla ya mechi husika yani waliingia kambini saa 12 jioni ya tarehe 6 jumatano na mechi ni alhamisi ya tarehe 7 !!!

    Kingine ni baadhi ya wachezaji muhimu vwa Yanga wanaoongoza kutoka na wadada wa mjini kuna kiungo wao mmoja mkabaji anatoka hapo nchi jirani kafa kaoza kwa dada yetu mmoja white, achilia mbali wale viungo wawili wa Ivor coast, na hivi hawana kambi ni mwendo wa kujiachia tu ,

    Hakuna shaka Yanga wanaenda kuvunja utaratibu wa kutokuwa na kambi, kambi ni muhimu Sana kwa mazingira ya wachezaji wa Tanzania , ukiwaachia uhuru umeumia

    Haya Matejoo tunalala sasa!!"
    Zungu ✍️ "Mbali na matokeo inaelezwa kuwa Master Gamondi alipoteza mvuto kwenye dressing room Maelewano hafifu na viongozi wenzake, kingine kukubali Yanga kutokukaa kambini yani wachezaji kutokea makwao lilikuwa kosa kubwa ,Wenyeji wa mikocheni Masaki na Mbezi beach si ajabu kwao kukutana na wachezaji wa Yanga mtaani siku chache hata kabla ya mechi Kwa mfano mechi kati ya Yanga na Tabora wachezaji wa Yanga waliingia kambini masaa 24 kabla ya mechi husika yani waliingia kambini saa 12 jioni ya tarehe 6 jumatano na mechi ni alhamisi ya tarehe 7 !!! Kingine ni baadhi ya wachezaji muhimu vwa Yanga wanaoongoza kutoka na wadada wa mjini 🤣 kuna kiungo wao mmoja mkabaji anatoka hapo nchi jirani kafa kaoza kwa dada yetu mmoja white, achilia mbali wale viungo wawili wa Ivor coast, na hivi hawana kambi ni mwendo wa kujiachia tu , Hakuna shaka Yanga wanaenda kuvunja utaratibu wa kutokuwa na kambi, kambi ni muhimu Sana kwa mazingira ya wachezaji wa Tanzania , ukiwaachia uhuru umeumia 🧐 Haya Matejoo tunalala sasa!!"
    Haha
    1
    · 1 Commentarii ·0 Distribuiri ·223 Views
  • Boyka master
    Boyka master
    Like
    Love
    4
    · 0 Commentarii ·0 Distribuiri ·164 Views
  • Master macapture
    Master macapture 💥💯
    Like
    1
    · 0 Commentarii ·0 Distribuiri ·214 Views
  • Master macapture
    Master macapture💥💯💯💥😛🧐
    0 Commentarii ·1 Distribuiri ·560 Views
  • Master mwenyewe akiwa kwe mipanga ya kunoa kikosi
    Master mwenyewe akiwa kwe mipanga ya kunoa kikosi
    Like
    1
    · 0 Commentarii ·0 Distribuiri ·123 Views
  • 🖥 Computer Kama Bunduki

    Mwanafunzi mwenye kipaji kutoka Thailand ametengeneza casing ya kipekee kwa ajili ya kompyuta yake ya michezo, inayofanana na bunduki ya kisasa ya mtafuta shabaha. Alikusanya mashine hii kwa ajili ya shindano la Cooler Master, ambapo washiriki wanashindania taji la casing ya kipekee zaidi.

    Ingawa sifa kamili za kompyuta hiyo hazijafichuliwa, inajulikana kuwa zina ubora wa juu kabisa. Mtengenezaji huyu ametumia $2700 (sawa na takriban TZS 6,345,000) kwa ajili ya kuunda Computer hii. Ikiwa atashinda shindano hilo, atapata zawadi ya $5000 (takriban TZS 11,750,000).

    #Hora_Tech
    #Computer #Thailand #mwanafunzi
    🖥 Computer Kama Bunduki 😱 Mwanafunzi mwenye kipaji kutoka Thailand ametengeneza casing ya kipekee kwa ajili ya kompyuta yake ya michezo, inayofanana na bunduki ya kisasa ya mtafuta shabaha. Alikusanya mashine hii kwa ajili ya shindano la Cooler Master, ambapo washiriki wanashindania taji la casing ya kipekee zaidi. 💾 Ingawa sifa kamili za kompyuta hiyo hazijafichuliwa, inajulikana kuwa zina ubora wa juu kabisa. Mtengenezaji huyu ametumia $2700 (sawa na takriban TZS 6,345,000) kwa ajili ya kuunda Computer hii. Ikiwa atashinda shindano hilo, atapata zawadi ya $5000 (takriban TZS 11,750,000). ➤ #Hora_Tech #Computer #Thailand #mwanafunzi
    Like
    Love
    2
    · 0 Commentarii ·0 Distribuiri ·1K Views
Sponsorizeaza Paginile