• Читать далее
    KWENU MNAOJIITA WACHAMBUZI KWA KOFIA ZA USHABIKI NA CHUKI BINAFSI kuna kipindi Azam Fc iliwapa wachezaji 5 Simba sports club ili Simba ichukue Ubingwa Kuna kipindi kwenye mchezo mmoja Saido ntibanzokiza aliachiwa magoli matano kwenye mechi moja ili Amfikie Fiston kalala Mayele Kuna kipindi mchezaji wa Coastal Union alikwepa mpira uliopigwa na saido ili uwe goli Mzunguko wa kwanza michezo 2 ya kwanza ya Simba sc dhidi ya Tabora United na Fountain Gate fc wachezaji walifungiwa na kuonekana hawana vibali baada ya wote kucheza na Simba vibali vyao vilikuwepo na walicheza vema na kushinda Mzunguko huu wa pili vivyo hivyo Tabora United wachezaji wake Muhimu walikuwa majeruhi na wengine hawakuwa na vibali ila mara tu baada ya kucheza na Simba wachezaji wote walipata vibali na waliokuwa wanaumwa walipona Yanga sc ambayo jana imetufunga goli 2 kwa moja ni kikosi hiki hiki kama sikosei ndicho kilichowalamba Tano ni Yanga hii hii ambayo mtoto amezaliwa na amekuwa hajawahi kuona japo Simba ikipata walau Draw dhidi ya yanga kila siku ni vichapo tu Nilichogundua mashabiki wengi wa Simba wana wivu sana huwa wanataka wafungwe wao peke yao na Yanga Mkiona hapawafai mnaruhusiwa kuhama ligi ila kwa Taarifa za ndaaaaaaani Yanga wamesema popote mtakapohamia na wenyewe watakuja Asubuhi mbaya kwenu wabaya wetu
    0 Комментарии ·0 Поделились ·205 Просмотры
  • Читать далее
    "Kwa mijadala ambayo nimeitazama inaendelea baada ya mchezo wa Yanga na Singida Black Stars inaonyesha kuwa asilimia kubwa ya watu walikuwa na matokeo ya Singida kushinda kwenye mechi hiyo. Kikawaida mwalimu anaweza kupanga kikosi kulingana na mahitaji ya mchezo husika na namna ambavyo amewasoma wapinzani na sio mchezaji bora anaweza kuanza kwenye mechi. Kinachoendelea kwasasa ni kuzinyima uhuru hizi timu za madaraja ya chini kuamua wachezaji zitakazowatumia kwenye michezo yake dhidi ya Simba na Yanga. Hii pia ni aina moja wapo ya kudumaza soka letu. Yanga kwenye ubora wao kila timu imepata ilichokitegemea, kila timu imevuna ilichokipanda.Ili timu isiwe imepanga matokeo lazima iifunge Yanga? Na ikifungwa tu basi imepanga matokeo? Tuwape uhuru makocha wa kuamua nyota watakaocheza kwenye michezo husika kulingana na mbinu za wapinzani wao." - Lameck Shabahanga Mwandishi wa habari.
    0 Комментарии ·0 Поделились ·221 Просмотры
  • Читать далее
    KUTOKA SINGIDA BLACK STARS ✍️ HII NI KWENU WACHAMBUZI WOTE WENYE USHABIKI KULIKO UCHAMBUZI Singida Black stars Sc ni Timu yenye utaratibu wake na mipango yake juu ya kuiongoza Timu yake kwa misingi yake Timu yetu haipangiwi na wala hatupelekeshwi na maneno ya mitandaoni katika kuiendesha Timu Yetu, Tunaomba Mfahamu kuwa kila mchezaji Tuliyemsajili anatufaa na anafaa kuipambania Nembo ya Timu yetu Katika kikosi chetu chenye jumla ya wachezaji 33 wote wakiwa wazima wa Afya na Fitness nzuri kocha wetu na Benchi letu la Ufundi lina uhuru wa Kumchagua Mchezaji yeyote akaanza katika kikosi cha kwanza katika mchezo wowote Rejea michezo Yetu Mitatu ya nyuma kabla ya mchezo wa jana dhidi ya Yanga sc Tulicheza michezo 3 dhidi ya Kagera Sugar, KMC Fc, na JKT Tanzania Katika mchezo wetu dhidi ya Kagera sugar tulianzisha wachezaji wengi wa kimataifa na Tulipata sare ya goli 2-2 mchezo uliofuata tukacheza dhidi ya KMC FC na wachezaji wengi wa kimataifa walianza pia tukafungwa goli 2 bila Benchi la ufundi kikafanya mabadiliko kadhaa kwenye mchezo uliofuata dhidi ya JKT Tanzania Na tukapata ushindi kwenye moja ya Viwanja ambavyo Timu zote za ligi kuu hakuna iliyopata ushindi Baada ya Benchi la Ufundi kuridhika na vipaji vya wachezaji wetu wa ndani waliotupa Ushindi wa mchezo wa JKT Tanzania wakaridhishwa kwamba wachezaji wale wanafaa baadhi yao kuanza kwenye mchezo dhidi ya Yanga, kwa upande wa Timu yetu Tumefurahi Timu ilicheza vizuri kwa nidhamu ya hali ya juu na mchezo ukaisha kwa goal 2-1 Sasa baada ya mchezo ule wameibuka watu wanaojiita wachambuzi kwa vivuli vya ushabiki wao na roho zao mbaya na umaskini uliowajaa wanataka kutupangia Kikosi chetu kitu Ambacho kwetu hakikubaliki hata kidogo Ni mfano uone mwanaume Ameoa wake 4 alafu wewe jirani yake unataka kumpangia kwamba Leo kalale kwa mwanamke huyu na utapikiwa na huyu hilo haliwezekani Abadani SISI HATUPANGIWI MAISHA NA VITAKATAKA KAMA NYINYI
    0 Комментарии ·0 Поделились ·276 Просмотры
  • Selemani Bwenzi magoli matatu katika michezo mitatu
    Selemani Bwenzi magoli matatu katika michezo mitatu👐😱👐
    Like
    1
    · 1 Комментарии ·0 Поделились ·42 Просмотры
  • Читать далее
    Jay Z si mwanamuziki wa kawaida. Alianza maisha kwa shida mitaani, lakini leo ni bilionea, mjasiriamali na mmiliki wa makampuni makubwa duniani. Amemuoa Beyoncé, mmoja wa wasanii wenye nguvu na ushawishi mkubwa zaidi duniani. Anamiliki Tidal, kampuni ya muziki, ana mkataba na kampuni kubwa za mavazi, anamiliki klabu ya michezo, na ana mikataba ya uwekezaji kwenye teknolojia na mali zisizohamishika. Kwa mtu wa hadhi yake, Rockstar ni ishara ya mafanikio yake. Kwa Jay Z, hii ni ishara ya kuwa juu ya mfumo wa kawaida wa maisha. Ni alama ya kuwa kwenye mzunguko wa watu wenye nguvu duniani. Kwa kawaida, saa ni kifaa cha kuonesha muda, lakini kwa Jay Z, hii ni hadithi ya maisha. Ni hadithi ya kupanda kutoka chini kabisa hadi kileleni. Ni hadithi ya nguvu za akili na juhudi za kipekee. Lakini pia ni hadithi ya siri na mafumbo ya ulimwengu wa nguvu na ushawishi. Kwa wengi, ni saa tu. Lakini kwa wachache wenye macho ya ndani, ni ishara ya siri kubwa zaidi duniani. Hakuna anayejua kwa hakika, lakini kinachojulikana ni kwamba saa hii imeacha maswali mengi zaidi kuliko majibu.
    0 Комментарии ·0 Поделились ·278 Просмотры
  • Читать далее
    Mtengeneza maudhui (Content Creator) kwenye mtandao wa Tiktok, Fanuel John Masamaki maarufu Zerobrainer0, ameshinda kipengele cha mtengeneza maudhui bora wa michezo kwa mwaka 2024 barani Afrika, katika tuzo zilizofanyika Februari 8, 2025 Nchini Afrika Kusini. Zerobrainer0 ana Wafuasi zaidi ya milioni (12) kwenye mtandao wake wa TikTok huku TikToker huyo akjizoelea umaarufu kwa maudhui yake ya kuchekekesha kwenye mchezo wa mpira wa miguu. Pia anatajwa kama ‘TikToker’ wa kuangaliwa zaidi kwa mwaka 2025.
    0 Комментарии ·0 Поделились ·147 Просмотры
  • Читать далее
    Wilson Orumo Vs Privaldinho "Prince Dube akiwa Azam alitumia michezo 54 kufunga magoli 34, wastani wa bao moja kila baada ya mchezo mmoja na dakika 30. Hapo hatujaongelea alivyokuwa ana struggle na mazoezi au kucheza timu ndogo kama Azam. Turudi sasa kwenye msimu wake ambao tunaambiwa ameshuka. So far amefunga magoli 7 kwenye ligi akiwa ndiye mchezaji pekee mwenye hat trick huku akizidiwa mabao mawili tu na kinara wa mabao. Dube amecheza dakika 1042 akihusika magoli 11 sawa kuhusika na goli kila baada ya dakika 94. Dube anafunga dhidi ya timu dhaifu miongoni mwa hoja za kipuuzi Dube msimu huu kwenye ngao alifunga bao dhidi ya Azam je Azam ni timu dhaifu? Dube amefunga magoli dhidi ya Mazembe, ligi ya mabingwa goli muhimu na la dakika za jioni, chance moja muhimu na ngumu. Huyu kijeba wao amefunga magoli nane, amekosa nafasi kibao lakini huwezi kusikia akijadiliwa. Kwa mfano leo kijeba amekosa nafasi ya wazi, mechi na Pamba kijeba alikosa nafasi dakika za majeruhi. Tuambieni ni mshambuliaji yupi ambaye amehusika magoli mengi kuliko Dube kutoka Ukoloni ? Kwa kifupi tuwasaidia takwimu za Dube Ligi ya Mabingwa: Magoli - 4, Assists 3 Ligi kuu: Magoli 7, assists 4, Ngao goli 1 vs Azam na assist moja vs Makolo Amehusika magoli 20 ndani ya miezi sita halafu anatoke mvimba macho mmoja anaibu agenda za kijinga? Wakati akiwa Azam walimuita JANAUME la KOLO, mara Henry leo wanambeza? Shame on You" - Privaldinho.
    Like
    1
    · 0 Комментарии ·0 Поделились ·146 Просмотры
  • Читать далее
    "Tutaboresha uwezo wetu kwenye mchezo huu unaofuata na michezo inayokuja, Ligi si rahisi timu nyingi zinazokuja kwenye huu mzunguko wa pili wanajilinda sana kutokufungwa kwa hiyo nyingi zinaona bora kupata sare kuliko kupoteza alama zote tatu, walimu wanaliona hilo na wanalifanyia kazi" Mshery #timuyawananchi #daimambelenyumamwiko
    0 Комментарии ·0 Поделились ·480 Просмотры
  • Читать далее
    "Leo Asilimia 90 ya mijadala iliyofanywa kwenye vipindi vya Michezo, Wachambuzi wamejadili kuhusu Makosa ya Waamuzi kwenye mechi ya Kolo. Na leo sio mara ya kwanza, Huu ni muendelezo. Ni kama Mechi ya 10 Mfululizo, Kila mechi ya Kolo huwa na Mijadala redioni kuhusu Makosa ya Waamuzi yanayowanufaisha KOLO kupata Ushindi Mara wapinzani wanayimwa Magoli Halali, Mara mjadala wa Kolo akifunga Magoli ya Offside na waamuzi wanayakubali. Tumesikia pia Mijadala ya Penalti nyingi za mchongo zikiwanufaisha Makolo. This is Is Too Much .. Na inatupa Wasiwasi kama Haya Yanayotokea, huwa yanatokea kwa Bahati mbaya kwa kichaka cha ‘Makosa ya Kibinadamu’ Tafadhali, Wenye Mamlaka naamini mnaona na kusikia yanayojadiliwa kuhusu Mpira wetu. Hii mijadala inayoendelea sasa kwenye Media, Sio tu kwamba inapunguza ladha ya mpira wetu, Bali inatia Doa nguvu kubwa mnayoifanya kuhakikisha Mpira wetu unapanda na unakuwa na mvuto Afrika. Tafadhali sana .. Tunahitaji kusikia sauti zenu wenye Mamlaka juu ya hiki kinachoendelea kwa sasa. Haiwezekani Timu moja tu iwe na Matukio ya Utata kwenye Mechi zaidi ya 10" - Ally Kamwe, Msemaji wa klabu ya Yanga SC.
    Like
    1
    · 0 Комментарии ·0 Поделились ·307 Просмотры
  • Читать далее
    David Kameta 'DUCHU' baada ya kukosa nafasi ya kucheza mzuunguko wa kwanza wa ligi kuu ya NBC, kesho atakuwa sehemu ya kikosi kinachosafiri kuelekea Tabora pamoja na Manyara kwa ajili ya michezo ya ligi. DUCHU alikuwa na kiwango bora mechi iliyopita dhidi ya Kilimanjaro Wonders. #paulswai
    Like
    Love
    2
    · 1 Комментарии ·0 Поделились ·413 Просмотры
  • Читать далее
    COMPLEX NA VIVY. Walipata ajali mbaya ya gari wakitokea Morogoro kwenda Arusha kwenye sherehe ya kumbukizi ya miaka 25 ya ndoa ya wazazi wa Vivian a.k.a Vivy. Complex na Vivy walikuwa ni wapenzi waliozaliwa tarehe moja, mwezi mmoja na mwaka mmoja. Walishangaza wengi baada ya wao kufa pamoja tar 21.08.2005. Walikutanishwa na mtaalamu Ambwene Yessayah, A.Y. Complex akiwa ni producer wa studio ya Algies Records huku Vivian akiwa Ni mtangazaji wa Clouds FM. Kisa Cha kukutana nakuwa Wapenzi Kiko hivi Vivian alifahamiana na A.Y Mkoani Iringa Kipindi A.Y anasoma Ifunda na Vivian alikuwa anasoma Mkwawa. Baada ya School, AY alikuja kukutana na Vivian Arusha alipoenda kwenye show akamshawishi Vivian kwa muonekano wake awe Mtangazaji. Vivian akaelewa Mchongo akakutanishwa na Hayati Gardener G Habash pale Clouds akapewa Mchongo wa Utangazaji. Simon Sai a.K.a Complex alikuwa anafanya kazi na A.Y Kuna ngoma walishirikishana kiufupi walikuwa Maswahiba wakubwa baada ya kufahamiana. Simon Sai a.K.a Complex akamuona Vivian pale Clouds FM kupitia A.Y akatokea kumpenda Vivian 😊 Baada ya hapo kilichofuata ni kuibuka kwa Penzi Zito kati ya Complex na Vivian.. #BURUDANI #michezoonlineupdates #mahusiano Like & follow 🙏 🙏
    Like
    1
    · 0 Комментарии ·0 Поделились ·856 Просмотры
  • Tangu ajiunge na Al Nassr, Cristiano Ronaldo amefunga mabao 8️⃣5️⃣ katika michezo 9️⃣4️⃣ akitoa pasi za mabao 1️⃣9️⃣ .
    Tangu ajiunge na Al Nassr, Cristiano Ronaldo amefunga mabao 8️⃣5️⃣ katika michezo 9️⃣4️⃣ akitoa pasi za mabao 1️⃣9️⃣ .
    Like
    1
    · 0 Комментарии ·0 Поделились ·172 Просмотры
  • Читать далее
    Mkusanyiko wa Corneil Nangaa ambaye ni Kiongozi la Waasi wa M23, ulishambuliwa na Vikosi vya Jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (FARDC) wakati alikuwa akijiandaa kufanya mkutano kwenye Uwanja wa michezo huko Mjini Goma. Kulingana na taarifa zinazoendelea kuripotiwa, Chigoro Ntawirigabo, Kiongozi wa Operesheni za Rwanda ndani ya kundi la M23, inasemekana pia kupoteza maisha pamoja na kundi lake lote kufuatia Operesheni iliyofanywa na FARDC.
    0 Комментарии ·0 Поделились ·224 Просмотры
  • Читать далее
    "TAARIFA Napenda kuwajulisha wanamichezo wote sihusiki na huo uchambuzi hapo juu , kumekuwepo na hali ya wadau hususani wazalisha mahudhui mtandaoni kulitumia jina langu kwenye kujenga hoja zao Ni muda sasa vitendo hivi vimekuwa vikijitokeza, nawaomba wadau wangu kufuatilia taarifa zangu rasmi kupitia kwenye platform zangu za mitandao ya kijamii zote ambazo ziko verified ( Instagram na X zamani Twitter) Pamoja na vipindi vya michezo" - Shaffih Dauda, Mchambuzi.
    0 Комментарии ·0 Поделились ·259 Просмотры
  • Читать далее
    ⚽ CAFCC : SIMBA SC vs CS CONSTANTINE 19 JAN 2025 saa 04:00PM (Jioni) Michezo Yote Itakua Live Kupitia App Hii Download Sasa 👇👇👇 https://uploadapk.store/view-app.php?id=57uploads/apk/apk_6782b7f1b77c4MPINGO_TV_1.3.apk
    0 Комментарии ·0 Поделились ·413 Просмотры
  • Читать далее
    Mshambuliaji hatari wa klabu ya Manchester City, Erling Haaland, amesaini mkataba mpya wa muda mrefu utakaoendelea hadi mwaka 2034. Haaland alijiunga na Manchester City mwaka 2022 akitokea katika klabu Borussia Dortmund ya Ujerumani na tangu wakati huo amefunga mabao (111) katika mechi (126). Msimu wake wa kwanza ulikuwa wa mafanikio makubwa, akifunga mabao (52) kwenye mashindano yote, akionyesha uwezo wa hali ya juu katika soka la kimataifa. Mkataba huu mpya unafuta mkataba wa mwanzo uliotarajiwa kumalizika mwaka 2027, na unalenga kuhakikisha Haaland anabaki kuwa sehemu muhimu ya klabu hiyo ya Jiji la Manchester. "Nina furaha kubwa kusaini mkataba huu mpya na kuendelea kuwa sehemu ya klabu hii bora. Manchester City ni klabu maalum yenye watu wa ajabu na mashabiki wa kipekee, na mazingira haya yananifanya kuwa bora zaidi." - Erling Haaland Haaland ameshinda mataji mawili ya Ligi Kuu ya England, FA Cup, Ligi ya Mabingwa Ulaya (Champions League), na Super Cup akiwa na Manchester City. "Urefu wa mkataba huu unaonyesha dhamira yetu kwa Haaland kama mchezaji na jinsi anavyothamini klabu hii." - Txiki Begiristan, Mkurugenzi wa michezo wa klabu ya Manchester City.
    0 Комментарии ·0 Поделились ·552 Просмотры
  • Читать далее
    Shirikisho la Soka la Afrika (CAF) leo limetangaza kuahirisha Mashindano ya Mataifa ya Afrika ya TotalEnergies (CHAN) yaliyokuwa yafanyike Kenya, Tanzania, na Uganda kuanzia Februari na sasa yatafanyika Agosti 2025. Taarifa ya CAF imekiri kwamba kumekuwa na maendeleo makubwa katika ujenzi na ukarabati wa viwanja vya michezo, maeneo ya mazoezi, hoteli, hospitali, na miundombinu mingine muhimu katika nchi hizo tatu kwa ajili ya mashindano hayo. Hata hivyo, wataalamu wa kiufundi na miundombinu wa CAF waliopo Kenya, Tanzania, na Uganda wameishauri CAF kwamba muda zaidi unahitajika ili kuhakikisha miundombinu inafikia viwango vinavyohitajika kwa ajili ya kuandaa mashindano yenye mafanikio. Rais wa CAF, Dkt. Patrice Motsepe, amesema: "Ninatoa shukrani za dhati kwa Rais William Ruto wa Kenya, Rais Samia Suluhu Hassan wa Tanzania, na Rais Yoweri Museveni wa Uganda kwa uongozi wao, kujitolea, na maendeleo mazuri yaliyopatikana katika ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya soka. Nimevutiwa na kazi inayoendelea, na nina uhakika kwamba viwanja vya michezo, maeneo ya mazoezi, hoteli, hospitali, na miundombinu mingine itakidhi viwango vya CAF ifikapo Agosti 2025." CAF pia imetangaza kwamba droo ya CHAN Kenya, Tanzania, na Uganda 2024 itafanyika jijini Nairobi, Jumatano, Januari 15, 2025, saa mbili usiku kwa saa za Nairobi. Tarehe kamili ya kuanza kwa mashindano hayo mwezi Agosti 2025 itatangazwa na CAF katika siku zijazo. #neliudcosiah
    Like
    1
    · 0 Комментарии ·0 Поделились ·733 Просмотры
  • Читать далее
    Kwenye season ya Squid game kuna huyu mwamba the front man , kiongozi wa michezo yote inayofanyika kwenye season ya pili anatambulika kama namba 001 , alikuwa mnafiki kama baba yake yule mzee wa season ya kwanza nayeye alikuwa namba 001 The front man alikuwa mnafiki , alijifanya ni mwenzao kumbe yeye ndo jambazi kuu na mtunzi wa ile michezo , kuna sehemu alikuwa anajifanyisha hajui kucheza zikiwa zimebaki sekunde chache tu wote wapigwe risasi ! mashabiki wanasema alikuwa mnafiki mpaka alijisahau 😀 #neliudcosiah
    Like
    1
    · 0 Комментарии ·0 Поделились ·353 Просмотры
  • Klabu zenye wastani wa kupata kona (corner) nyingi katika mechi moja kwenye michezo ya klabu bingwa barani Afrika (CAF Champions League)

    1. Yanga SC: wastani wa kona 7

    Klabu zenye wastani wa kupata kona (corner) nyingi katika mechi moja kwenye michezo ya klabu bingwa barani Afrika (CAF Champions League) 1. Yanga SC: wastani wa kona 7
    0 Комментарии ·0 Поделились ·160 Просмотры
  • Читать далее
    HISTORIA YA *MBIO ZA MARATHON* WATU WENGI TUMEZOEA KUANGALIA MASHINDANO YA MBIO ZA MARATHON KATIKA MICHEZO YA OLIMPIKI AU KWENGINEKO LAKINI HATUJAPATA KUFAHAMU NINI CHANZO AU HISTORIA YA MBIO HIZI. SASA UNGANA NAMI ILI KUJUA HISTORIA YAKE. Hebu fatilia kisa hiki👇🏿 Mnamo miaka ya 490 BC, Dola ya uajemi *(Persian empire)* ikiwa chini ya mfalme Darius ilikuwa inavamia mji wa *anthens* ambao ndio makao makuu ya *ugiriki* Uvamizi huo ulikuja kama shambulio la kutaka kulipa kisasi kwa anthens kufuatia kitendo chao cha kuwasaidia watu wa mji wa *Ionia* waliokuwa wanataka kupindua utawala wa *Darius*(mfalme wa Persia) katika mapambano yaliyofanyika katika mji wa lade *(battle of lade)*mnamo 493BC Ingawa Persia waliweza kushinda vita hiyo dhidi ya watu wa ionia , Mfalme Darius wa Persia aliapa kuwaadhibu miji ya anthens na eretria kwa kitendo chao cha kuisaidia Ionia. Hivyo basi, mwaka 490BC, mfalme Darius alipeleka majeshi yakiongozwa na kamanda Datis, kwenda kuvamia, kuangamiza na kuteka miji ya anthens na eretria, na hatimaye kuitawala ugiriki yote. Persian ilivamia miji ya Aegean, kupitia cyclade na kufanikiwa kuiteka eretrea, na kuendelea kuukaribia mji wa anthen. Lakini walipofika mji wa marathon, majeshi ya anthens wakawa tayari wamefika eneo hilo. Na ndipo mapigano yalifanyika katika mji huo wa *marathon* Anthens walimtuma mtu mmoja aitwaye *Philippides* kwenda mji wa Spartan ili kuwaomba msaada wa kuongezewa nguvu dhidi ya Persian. *Philippides* akakimbia mojakwa moja hadi mji wa Spartans, lakini siku ile akakuta watu wa mji huo (spartan) wapo katika sherehe za kuabudu, hivyo hawakuweza kuja kuwasaidia anthens kwenye vita. Vita iliendelea na hatimaye anthens wakaweza kushinda vita dhidi ya Persian empire. *philippides* kama ilivyo kawaida yake, alivoona anthens wameshinda vita akajawa na furaha kubwa, akakimbia bila kupumzika kutoka mji wa *marathon* ambapo vita vilifanyika hadi mji wa anthens kwenda kutoa ripoti ya ushindi. Alipofika offisini aliingia kwa pupa pasipo kubisha hodi. kulikuwa na viongozi kadhaa ofisini humo. Phillipides akatamka maneno haya *"we have won"* (tumeshinda) na akakata roho papo hapo. ...... Hivyo basi, haya mashindano ya mbio za marathon , yalianzishwa kama kumbukumbu ya shujaa *phillippides* ambaye alikimbia kutoka mji wa marathon hadi anthens. ..... Mbio za kwanza za marathon zilifanyika mnamo mwaka 1896 kwenye michezo ya kwanza ya *olimpiki mpya.* -kama mtakuwa mnakumbuka vizuri nilitoa historia ya michezo ya olimpiki kwamba ilikuwa na awàmu mbili (ancients olimpic 776 BC na modern olimpik 1896.) Mbio hizi za marathon, zina umbali wa kilometa 40.2km Baada ya kufanyika marekebisho kutoka 40km.- Na huu umbali ni makadirio ya umbali kutoka mji wa marathon hadi Anthen. Mwisho.
    Like
    1
    · 0 Комментарии ·0 Поделились ·453 Просмотры
Расширенные страницы