• Read more
    KUWA MAKINI UNAYEMSHIRIKISHA SIRI ZAKO... Nenda kwenye mitandao ya kijamii uone jinsi wanaume waliokomaa wenye ndevu na wanawake wakubwa wenye mawigi ya bei wanavyojidhalilisha. Unapoona jinsi watu wanavyoshiriki mambo ya faragha kwenye maeneo ya umma, utaelewa kwa nini mambo fulani yanakusudiwa kuwa siri. Kutoka kona moja hadi nyingine, kwa nia ya kumrudia aliyewaudhi, watu wanashuka sana, na hawajali jinsi chochote watakachofichua kitawaathiri katika siku zijazo, wanachojali ni kumpiga yule wanayehisi kukanyagwa kwenye vidole vyao. Kuanzia mazungumzo yaliyovuja, video kuvuja, hadi mazungumzo ya faragha, nilichojifunza ni kwamba sio kila mtu anayetabasamu na wewe ana uwezo wa kutunza siri zako. Mitandao ya kijamii imetufundisha somo hili kwa njia ya kikatili zaidi. Tumeona marafiki waliopendana mara moja, mahusiano ya mara moja-tamu, ushirikiano wa mara moja-imara ukiporomoka katika ushindani mkali, na siri zilizomwagika kama maji machafu mitaani. Tumeona maungamo ya kibinafsi yakigeuzwa kuwa fedheha hadharani, na uaminifu mkubwa ukivunjwa na chapisho moja, maoni moja, kufichuliwa mara moja. Watu wengine wana kuhara kwa mdomo. Hawajui jinsi ya kushikilia kile walichoambiwa kwa ujasiri. Hawaoni siri kuwa takatifu; wanaziona kama silaha, kimya kwa sasa, lakini tayari kuachiliwa wakati mawimbi yanabadilika. Na mawimbi hubadilika kila wakati. Hakuna kitu kibaya kwa kuwaamini watu, lakini kuna kitu hatari kwa kuamini kwa urahisi sana. Maisha yametufundisha kuwa sio kila anayekusikiliza anakusikiliza kwa mapenzi, wengine wanakusanya data. Wengine wanangojea, kwa subira, kwa wakati sahihi wa kutumia maneno yako dhidi yako. Rafiki leo anaweza kuwa mgeni kesho. Mpenzi leo anaweza kuwa adui wiki ijayo. Huyo mwenzako, huyo jamaa, huyo mtu unayemtajia wakati wote ni mtamu, wanaweza kuficha siri yako wakati mambo yanaharibika? Wengi hawawezi. Wengi hawataweza. Kwa hivyo, weka siri zako, siri. Ikiwa huwezi kuiweka mwenyewe, kwa nini unapaswa kutarajia mtu mwingine? Ikiwa kina kina sana kwako kubeba peke yako, kuwa mwangalifu unaiweka mikononi mwa nani. Baadhi ya watu ni wadogo. Hawaachi tu na kuondoka; lazima wachafue weupe wako kabla hawajaondoka. Ni lazima wakuvute kwenye matope, lazima wafichue kile kilichokusudiwa kuwa kitakatifu, lazima watumie wanachokijua kukuletea aibu. Na ndio maana lazima uwe na hekima. Zingatia kile unachoshiriki wakati jua linawaka katika urafiki wako. Kuwa mwangalifu kile unachosema wakati kila kitu ni cha kimapenzi na cha kupendeza. Kwa sababu upendo ni mtamu, lakini watu wengine wanapoanguka kutoka kwa upendo, hugeuka kuwa mbwa mwitu. Wapende watu, lakini usiwe mjinga. Sio kila anayekusikia atakulinda. Na misimu inapobadilika, uhusiano unapovunjika, urafiki unapoisha, utatamani ungejiwekea mambo fulani. Uwe mwenye busara. Uwe na hekima. Zuia nyeupe yako isichafuke.
    Love
    1
    · 0 Reacties ·0 aandelen ·259 Views
  • Read more
    #PART3 Dogo alianza kupiga picha na maadui wa baba yake. Unajua maana yake? Kijana wako, damu yako mwenyewe, anashirikiana na watu waliotaka kukuangusha. Hii haikuwa tu ishu ya "Hana time na baba yake," hii ilikuwa ni chuki ya makusudi. Na chuki hiyo haikutoka kwa mtoto mwenyewe, bali ilitengenezwa na mama yake. Mama ambaye baada ya kuachwa alitaka pesa nyingi kutoka kwa 50 Cent lakini ikashindikana. Mama ambaye hakuwa na njia ya kumkomoa baba, akaamua kutumia mtoto kama silaha. Na mtoto, bila kujua anatumika kama chess piece, akaingia kwenye mchezo wa mama. Huu ni ukweli mchungu. Katika ndoa au mahusiano yanayovunjika, asilimia kubwa ya wanawake hutumia watoto kama njia ya kulipiza kisasi. Ni wachache sana watakaoruhusu baba wa mtoto wao aendelee kuwa na uhusiano mzuri na mwanawe baada ya kutengana.
    0 Reacties ·0 aandelen ·333 Views
  • Read more
    Usichanganye hivi vitu viwili, ni tofauti sana. Mapenzi na upendo, hivi ni vitu tofauti. Mapenzi Yana utumwa lakini upendo una uhuru, mapenzi yana visasi lakini upendo una msamaha, mapenzi yanamiliki lakini upendo una utu, mapenzi yana mwisho lakini upendo ni wa milele. Mahusiano ya mwanaume na mwanamke ni mapenzi siyo upendo. Huu ni muungano wa kimaslahi, utake usitake ni maslahi. Kila upande una maslahi yake na siyo upendo. Angalia wanavyohesabiana waliyofanyiana aidha mema au mabaya siku wanapoachana. Upendo huwa hauhesabu na hauna kumbukumbu kabisa. Mtu akikuambia nilikupenda sana, wala usijione na hatia, huyo muongo mkubwa. Neno analotakiwa kusema ni "nilikuwa na hisia kali za mapenzi kwako". Huwezi kumpiga mtu unayempenda, wala huwezi kutamani apatwe na mabaya sababu amekuacha. Mtu unayempenda utamtakia mema hata kama kukuacha kwake kulikuumiza. Siku zote utamuunga mkono kwa lolote linalompa furaha na amani hata kama ni kukuacha. Usichanganye upendo na mapenzi ni vitu tofauti. Upendo ni nishati ya asili inayoishi ndani ya mtu lakini mapenzi ni hisia inayotokana na mvuto wa kimahaba.
    Like
    1
    · 0 Reacties ·0 aandelen ·351 Views
  • Read more
    COMPLEX NA VIVY. Walipata ajali mbaya ya gari wakitokea Morogoro kwenda Arusha kwenye sherehe ya kumbukizi ya miaka 25 ya ndoa ya wazazi wa Vivian a.k.a Vivy. Complex na Vivy walikuwa ni wapenzi waliozaliwa tarehe moja, mwezi mmoja na mwaka mmoja. Walishangaza wengi baada ya wao kufa pamoja tar 21.08.2005. Walikutanishwa na mtaalamu Ambwene Yessayah, A.Y. Complex akiwa ni producer wa studio ya Algies Records huku Vivian akiwa Ni mtangazaji wa Clouds FM. Kisa Cha kukutana nakuwa Wapenzi Kiko hivi Vivian alifahamiana na A.Y Mkoani Iringa Kipindi A.Y anasoma Ifunda na Vivian alikuwa anasoma Mkwawa. Baada ya School, AY alikuja kukutana na Vivian Arusha alipoenda kwenye show akamshawishi Vivian kwa muonekano wake awe Mtangazaji. Vivian akaelewa Mchongo akakutanishwa na Hayati Gardener G Habash pale Clouds akapewa Mchongo wa Utangazaji. Simon Sai a.K.a Complex alikuwa anafanya kazi na A.Y Kuna ngoma walishirikishana kiufupi walikuwa Maswahiba wakubwa baada ya kufahamiana. Simon Sai a.K.a Complex akamuona Vivian pale Clouds FM kupitia A.Y akatokea kumpenda Vivian 😊 Baada ya hapo kilichofuata ni kuibuka kwa Penzi Zito kati ya Complex na Vivian.. #BURUDANI #michezoonlineupdates #mahusiano Like & follow 🙏 🙏
    Like
    1
    · 0 Reacties ·0 aandelen ·853 Views
  • Read more
    Naitwa calvin nina miaka 27, namshukuru Mungu kuniweka salama hadi leo na sina changamoto yoyote ya kiafya,Siishi nyumbani nimejitegemea(geto), Shida yangu ilianza nilipopata kazi mwaka jana Nikawa bize sana kuipambania future yangu kwani umasikini nilikuwa nisha onja radha yake, Nilipokuwa bize mpenzi wangu alianza kunihisi namcheat kwani sitengi muda mwingi kwaajili yake kama zamani,,(Nikumbushe kitu Wanaume wasio na kazi wanaharibu sana mahusiano ya watu na hii kwa sababu muda wowote wakihitajika wanapatikana),,tuendelee👇👇 Baada ya muda kidogo Akaamua kuniacha kabisa sababu alitaka niwe nae muda mwingi kama ilivyokuwa kipindi sina kazi,, Tangu hapo nikawa single nikaamua kudiri na future yangu namshukuru Mungu katika hilo nimefanikiwa Asilimia fulani,,Shida yangu kubwa iliyo nileta hapa nikutafuta mchumba,, Nimekua bize sana na kazi hata ninaowapata nikidet nao,kutokana na ubize wangu wanahisi sina malengo nao kwani siwapi muda wanaotaka wao,,wanaamua kumove on,,lakini pia Kwa eneo ninaloishi Asilimia kubwa ya mabinti ninao wapata wamerekodiwa video za faragha na ma-x zao, Unaweza pata binti fresh mkadet vizuri tu shida itakuja utakapo watambulisha marafiki zako,Watakupa kila kitu kumhusu huyo binti hadi list ya wanaume aliolala nao na ukibisha wanakuonyesha video za faragha, Hii kitu imenikuta mara kibao sana na inavunja moyo kumuona unae mpenda kavuliwa nguo na mwanaume mwingne hili eneo nililopo natamani nitoke niende sehemu nyingine,Nikakae japo kwa muda kidogo labda nitabahatika kupata wa kuendana nae lakini kazi zimenibana,,nakosa huo muda Sina mtoto na wala sijawahi kuoa,Natamani nipate mwanamke ambae hana mtoto na hajawahi kuolewa,mwenye hofu ya Mungu na mwenye Akili timamu,,Umri asinizidi awe chini yangu,Asiwe mnene sana,awe msafi wa ndani na nje,asiwe na tatoo wala brich Akipatikana nikamuelewa nipo tayari kuanza nae ukurasa mpya,,Naahidi kama ataniheshimu na kunisikiliza nitampenda na kumthamini,, Naamin huenda kupitia page hii nitampata alie sahihi,,whatsp No;0748374716,,cha kwanza tuma picha isiyo na filter La mwisho kabisa mabinti mkiwa kwenye mahusiano msikubali kurekodiwa,siku mkiachana hiyo clip itatumika kama uthibitisho kama umeshaliwa,,Nakama umerekodiwa kaa ukijua mashemeji zako wamesha onyweshwa faragha yako,,,
    Like
    2
    · 0 Reacties ·0 aandelen ·640 Views
  • Read more
    "INJINI MOJA YA BOEING787 DREAMLINER INASUKUMA TANI MOJA NA ROBO YA HEWA KWA SEKUNDE IKIWA KATIKA 'FULL POWER' (Hesabu inasema, inachukua takribani miezi isiyopungua mitatu kwa binaadam wa kawaida kutumia kiwango hiki cha hewa) Leo si vibaya kama tukifahamu juu juu kuhusu aina ya injini za ndege ili kila mmoja wetu asibaki nyuma sana. Zipo ndege zenye injini 1,2,3,4,6 hadi 8 katika ndege moja. Ndege nyingi zinaendeshwa na injini za aina 2 kwa muonekano tuliozoea. (1)-Injini za Jeti (Zenye mfano wa pipa lililolazwa) (2)-Injini za Propeller (Maarufu Mapangaboi) 1> MFUMO WA INJINI ZA JETI Huu umegawanyika kutokana na 'modification' ya ufanisi na matumizi yake ambazo pia zipo katika makundi mbalimbali mfano, *Turbojet 'PureJet'(Mfumo wa ndege nyingi za awali) *Turbofan(Mfumo wa ndege nyingi za sasa) *Turboshaft(Mfumo wa baadhi ya ndege za sasa mfano Helicopter n.k *Scramjet.(Mfumo ulio katika ndege za majaribio za mwendokasi mara nyingi ufanisi wake uanzia mara tano ya kasi ya sauti 'Hypersonic') Injini za jeti zinafanya kazi kwa: 1-Kunyonya hewa mbele (suck) 2-Kukandamiza (compression) 3-Kulipua hewa iliyokandamizwa kwa kuchanganya na mafuta(Ignition) 4-Kisha inatoka/kupulizwa nyuma kwa kasi kubwa na kuisukuma ndege mbele.(Thrust) Mfano mzuri kazi ya injini hizi ni kama Puto lililopulizwa na kuachiwa hewani pasipo kuzibwa mdomo wake.(Action and reaction) Ndege nyingi za kisasa zinatumia injini aina ya 'Turbofan' (Gas driven) katika kundi la jeti ambazo zinasemakana kuwa na nguvu kubwa na ulaji mdogo wa mafuta. (Unaweza kutambua injini hizi kwa haraka kwa kuona feni kubwa lililo mbele ya injini kwa ndani kidogo..usifananishe na mapangaboi) Injini za 'Turbojet/Purejet' ambazo moja kwa moja zinanyonya hewa mbele zinakandamiza,kulipua na kuitoa hewa moja ya moto kwa kasi nyuma ambayo ndiyo nguvu pekee inayosukuma ndege kwenda mbele, hutumia mafuta mengi kuliko Injini ya 'Turbofan' ambayo ni tofauti kidogo kwani feni lake linavuta na kusukuma hewa mbili nyuma huku hewa ya kwanza ikiwa ile inayoingia kwenye mfumo wa ndani ya injini ambayo unyonywa,kukandamizwa na kulipuliwa na hewa ya pili ni pale hewa ya kwanza iliyolipuliwa kabla ya kufika nje inazungusha visahani maalum 'turbine' zilizoungwa na 'shaft' kwenda kwenye feni lake mbele ambapo huzunguka pamoja na feni na kufanya livute na kusukuma nyuma hewa ya pili yenye nguvu zaidi inayopita nje ya mfumo wa injini(Bypass air) hivyo kuleta nguvu zaidi kwa kutumia mafuta kidogo. 2-MFUMO WA INJINI ZA MAPANGABOI Mapangaboi au 'Propeller'nazo zinafanya kazi kwa kutumia mapanga yake kuchota hewa mbele na kuisukuma nyuma kwa kasi na kuifanya ndege kwenda mbele. *Pangaboi linaweza kuwa linazungushwa na 'propeller' iliyoungwa na piston za injini, *Au kwa mapangaboi yenye injini ya 'turbo' (turbopropeller)yanazungushwa na hewa iliyolipuliwa (hii aina ya jeti engine yenye mapangaboi)kupitia visahani 'turbine' vilivyo ungwa na propela ya mapangaboi kupitia mfumo wa gear(Geared turboprop)au yanayozunguka kupitia mkandamizo 'pressure' ya hewa iliyolipuliwa pasipo kuungana na chochote (free turbine). *Pia 'turboshaft' Mapangaboi yanayozungushwa na hewa iliyolipuliwa kupitia visahani 'turbine' vilivyoungana na propela ya mapangaboi moja kwa moja,pia yaweza kuwa 'Geared' au ila si 'free turbine' Mifumo ya injini za kisasa ya mapangaboi inafanya kazi sawa na jeti (Ukiacha za piston)katika mfumo wa ufuaji wa nishati na kuzitofautisha tu katika muonekano wa nje wa injini. Injini zenye mfumo ya jeti ni fanisi zaidi kwa ndege zinazopaa anga za juu ambapo hewa ni hafifu,masafa marefu na mwendokasi hasa unaozidi spidi ya sauti 'supersonic' Wakati, Injini za mfumo wa Mapangaboi ni fanisi zaidi katika mwendo ulio chini ya spidi ya sauti 'subsonic',anga za chini na kati na masafa mafupi kwenda ya kati. Tukumbuke pia injini za ndege hazina mahusiano wala kiunganishi chochote na tairi za ndege. Tairi za ndege ni 'freewheel' na zimeunganishwa na mfumo wa 'brake' na kona tu. Hakuna kinachozungusha tairi kutoka kwenye injini bali zinafuata uelekeo wa kule ndege inaposukumwa. Crdts: Online,Aero book,wikimedia.
    0 Reacties ·0 aandelen ·653 Views
  • Read more
    CHAGUA KINACHO FAIDA, SI KILE KINACHOSISIMUA... Maisha ni safari iliyojaa chaguzi, njia panda, na maamuzi ambayo yanaunda hatima yetu. Hata hivyo, katikati ya haya yote, moja ya majaribu makubwa tunayokabiliana nayo ni chambo cha kile kinachoonekana "kuvutia." Lakini wacha nikukumbushe kwamba sio kila kitu kinachovutia ambacho kinafaa kufuata, na sio kila kitu kitamu kinaongoza kwenye uzima. Tunaishi katika ulimwengu unaotukuza kufuatia raha, mvuto wa burudani, na msisimuko wa muda mfupi tu. Lakini kumbuka hili: "Labda ni ya kuvutia, lakini inaua." Sio nyakati za msisimko za muda mfupi ambazo hufafanua ubora wa maisha yako; ni maamuzi ya muda mrefu unayofanya ambayo ni muhimu sana. Kuna meza ambapo raha hutolewa kwenye sahani za fedha, meza ambapo anasa hupongezwa, na mipaka imefichwa. Jedwali hizi zinaweza kuonekana kuwa za kuvutia, lakini mara nyingi huficha vikombe vyenye sumu. Maisha mengi yameharibiwa na ladha tamu ya anasa. Kinywaji hicho cha ziada, tabia hiyo ya kutojali, tukio hilo lisilo na madhara, yote ya kuvutia kwa sasa, lakini wengi wamelipa kwa afya zao, amani yao, na hata maisha yao. Je! ni watu wangapi wamelala kwenye vitanda vya hospitali leo kwa sababu walifuata kile "kinachovutia"? Ni ndoto ngapi zimekatishwa kwa sababu mtu alifuata kile "kinachosisimua" bila kuzingatia matokeo? Kama vile mithali ya kale inavyosema, “Iko njia ionekanayo kuwa sawa machoni pa mtu, lakini mwisho wake ni njia za mauti” (Mithali 14:12). Jedwali lingine la kuepukwa ni meza ya uvumi. Lo, ni jambo la kupendeza kama nini kuketi na kusikiliza mtu akipasuliwa, jina lake likikokotwa kwenye tope! Lakini wacha nikuambie kitu: porojo hazina marafiki wa kudumu. Vinywa vile vile vinavyowachana wengine mbele yako ndivyo vitakugeukia wewe usipokuwepo. Usidanganywe na maoni ya uwongo ya urafiki ambayo porojo hutoa. Uvumi ni kama vampire, unalisha damu ya mahusiano, uaminifu, na sifa. Inavutia, lakini inaua. Inaua urafiki, familia, na jamii. Kama msemo unavyosema, "Mtu anayeondoa kaa linalowaka kutoka kwa paa la jirani yake atalipata peke yake." Unaposhiriki katika uvumi, unafungua mlango wa uharibifu kuingia katika maisha yako mwenyewe. Maisha si msururu wa starehe za kupita muda; ni zawadi takatifu inayokusudiwa kuishi kwa makusudi. Usiishi maisha yako kwa kuzingatia kile kinachovutia. Badala yake, iishi kulingana na kile ambacho kinafaa kwako kwa muda mrefu. Mambo yanayotutegemeza, nidhamu, kazi ngumu, uadilifu, na upendo, si mara zote "yanavutia" kwa sasa, lakini yanajenga maisha yenye thamani. Epuka meza ambapo vitu vya kupendeza tu hutolewa. Jizungushe na watu wanaokupa changamoto, wanaokuhimiza kukua, wanaokuita kwa viwango vya juu zaidi. Kama vile Mtakatifu Paulo anavyoandika, “Vitu vyote ni halali kwangu, lakini si vyote vyenye faida” (1 Wakorintho 10:23). Chagua kile ambacho ni cha manufaa, sio tu kinachosisimua. Usiruhusu harakati zako za msisimko zikupoteze maisha ambayo Mungu alikusudia kwa ajili yako. Chagua maisha, chagua kusudi, na uchague njia inayoongoza kwa furaha ya kweli na amani ya kudumu. @Fr. Albert Nwosu'
    Love
    1
    · 0 Reacties ·0 aandelen ·821 Views
  • Read more
    JAMBAZI MTUKUTU. Nchini Tanzania, kuna manju 'Dj' fulani wa muziki anayejulikana kwa jina maarufu la 'DJ JD' au kwa kirefu *'DJ John Dilinga'.* Huyu ni moja kati ya maDj wakongwe na mahiri sana tuliobahatika kuwa nao hapa nchini Tanzania. Kwa wale wapenzi na wadau wa muziki wa 'bongofleva' hususani wa miaka ya nyumanyuma kidogo, bila shaka mtakua mnamfahamu Dj huyu. Kwa muda mrefu nimekuwa nikitamani kufahamu ni kwanini anaitwa John Dilinga..nikiwa nataka kujua kama hilo ni jina lake halisi au ni 'a.k.a'. Maana ni kawaida kuona watu mbalimbali hususani walio kwenye tasnia ya burudani wakitumia majina ya ziada (a.k.a) kuliko majina yao halisi. Kitu kilichonifanya nianze na DJ JD ni baada ya kugundua kuwa leo ni tarehe 22 Julai. Tarehe ambayo ulimwengu mzima unamtaja bwana mmoja mtukutu sana, aliyewahi kusumbua vichwa vya maofisa usalama wa nchi ya Marekani, akifahamika kama *John Dillinger.* Huyu alikuwa ni moja kati ya wahuni wakubwa nchini Marekani aliyetamba sana katika miaka ya 1930 kwa kujihusisha na matukio ya kihalifu hususani uporaji wa fedha kwenye mabenki. Tofauti ni kwamba John Dilinga wa Tanzania ni DJ, wakati John Dillinger wa Marekani alikuwa ni jambazi mtukutu. Utukutu wake ulianza angali ana umri mdogo na hata aliweza kuacha shule ili kwenda kutafuta pesa!! Alianza kama mdokozi wa vitu vidogovidogo lakini tukio lake la kwanza lilikuwa ni *kuiba gari*, kisha 'kwenda misele' kwa mpenzi wake mpya. Siku chache baadae alikuja kukamatwa na mapolisi akiwa anazurula mtaani japokuwa alifanikiwa kuchoropoka na 'kutokomea kusikojulikana'. Baadae alipata kazi katika jeshi la majini 'navy', akifanya katika meli ya jeshi ya 'USS Uttah'. Baada ya miezi kadhaa John Dillinger alitoroka kazini. April 1924 akiwa hana shughuli ya kumuingizia kipato, John Dillinger alifunga ndoa na mwanadada Beryl Hovious ambapo walienda kuishi kwenye nyumba ya baba yake ambapo John Dillinger aliahidi kwamba sasa atatulia na kuacha utukutu wote. Lakini wiki chache baada ya ndoa, Dillinger alikamatwa na hata kufikishwa mahakamani kwa kosa la wizi wa kuku, "nadhani alikuwa anatafuta mboga ya kwenda kula na mkewe". Lakini kwa msaada wa Baba yake, kesi ya Dillinger iliweza kufutwa. Baadae Dillinger aliamua kutoka kwenye nyumba ya baba yake na kwenda kuishi kwenye nyumba ya wazazi wa mwanamke ambapo huko alibahatika kupata kazi kwenye duka la kuuza vifaa vya ujenzi. Akiwa huko, Dillinger alikutana na rafiki yake wa muda mrefu aitwaye *Edgar Singleton,* ambapo walipanga mikakati ya kuiba pesa. Ndipo tarehe 6 septemba 1924 waliiba pesa katika moja ya Grocery japokuwa walikamatwa na kufikishwa mahakamani ambapo John Dillinger alihukumiwa kifungo cha miaka 20 katika Gereza la "Indiana State Reformatory in Pendleton". Alipokuwa jela, alikutana na wafungwa wengine ambao walimfundisha mbinu nyingine za uhalifu mkubwa hususani uporaji wa fedha kwenye mabenki. Alitumikia kifungo chake hadi mwaka 1933 kwa paroli. Siku chache tu baada ya kutoka jela, John Dillinger alifanya uhalifu mkubwa, safari hii akivamia benki na kuiba pesa benki ingawa alikamatwa na kuhukumiwa kifungo katika gereza la Lima. Siku chache baada ya Dillinger kuingia jela, wafungwa 12 ambao baadhi yao ni rafiki zake Dillinger, waliweza kutoroka katika gereza la "Indiana State Prison". Hili ni gereza alilowahi kufungwa John Dillinger baada ya kuhamishwa toka kwenye gereza lile la awali. Miongoni mwa hao waliotoroka, ambao baadhi yao ni marafiki wa Dillinger, walifika katika gereza alilofungwa Dillinger lengo ni kumtorosha rafiki yao. Walimuua askari mmoja na kuchukua funguo kisha kufungua mlango wa selo alilomo Dillinger kisha kutoroka naye. Baada ya kutoroka, John Dillinger na wenzake walielekea mjini Chicago ambapo waliunda genge kubwa la kihalifu *Dillinger Gang*. Genge hili lilipora pesa kwenye mabenki mbalimbali, na ili kuongeza nguvu, walivamia ghala la silaha na kuiba silaha nzitonzito walizozotumia katika shughuli zao za kihalifu. Wahuni hao walitokea kupata umaarufu mkubwa pale Marekani, hususani huyu Dillinger ambaye alikuwa maarufu sana mithili ya 'nyota wa hollywood' kwani kila siku jina lake lilikuwa likitajwa kwenye vyombo vya habari na kuandikwa magazetini. Sifa nyingine ya genge hili ni kwamba walikuwa watanashati mno wakipendelea kuvaa suti na kofia nyeusi. Januari 15 1934, Dillinger alivamia benki kuiba pesa. Katika tukio la majibizano ya risasi, Dillinger alimuua askari mmoja aliyejulikana kwa jina la William O'Malley. Yeye alipigwa risasi kadhaa japokuwa hakufa kwasababu alivaa 'bullet proof'. Baadae, 'Dillinger Gang' walikuja kukamatwa, ambapo Dillinger alipelekwa katika gereza la *crown point* kwa kosa la kumuua Askari. Gereza hilo lilipewa jina la 'escape proof' kwakuwa lilikuwa nj ngumu kutoroka hapo. Umaarufu wake ulipelekea wananchi kufurika mahakamani na gerezani kwa ajili ya kutaka kumuona John Dillinger. Tarehe 3 Machi 1934, John Dillinger alifanikiwa kutoroka tena katika gereza la *Crown point,* safari hii akitoroka kwa kutumia 'bunduki feki' aliyoichonga kwa kutumia mbao na kuipaka rangi nyeusi. Aliitumia bunduki hiyo kumtisha askari kisha akapora gari la askari na kutoroka nalo. Kitendo hiko kiliwafanya polisi waombe msaada kutoka *FBI* ambao walifanya msako kabambe wa kumkamata John Dillinger. Alipotoroka, alikimbilia mjini Chicago ambako huko aliunda Genge jipya safari hii akimchukua mtu hatari aliyejulikana kama 'Baby Face Nelson'. Genge hilo liliendelea kufanya matukio mengi ya uporaji wa pesa benki na hata wizi wa silaha. Katika kipindi hiki, John Dillinger alianzisha mahusiano na binti aliyeitwa 'Polly Hamilton' mhudumu wa mgahawa pale Chicago ambaye hapo kabla alikuwa akijihusisha na ukahaba. Ifahamike kuwa kipindi yupo jela, Dillinger alitalikiana na yule mkewe. MSAKO wa kumpata John Dillinger ulikuwa ukiendelea ambapo FBI walisambaza picha za Dillinger pamoja na kutangaza dau nono kwa yeyote atakayefanikisha upatikanaji wake. FBI walitangaza dau la dola $10,000 kwa yeyote atakayefakiwa kumkamata Dillinger na $5,000 kwa yule atakayetoa taarifa za kupatikana kwake. John Dillinger alisumbua sana vichwa vya maafisa usalama kiasi cha FBI kumtangaza kuwa *"Public Enemy Nō 1".* Ukiona hadi mtu anaitwa Public Enemy Nō 1 ujue huyo alikuwa ni 'kiboko pasua kichwa'. John Dillinger naye hakuwa nyuma katika kuhakikisha hakamatwi. Unajua alifanyaje??. Aliamua kufanya operesheni ya uso *"plastic surgery"* ili kubadilisha muonekano wa sura yake. Pia alifanya uperesheni ya kubadilisha alama za vidole yaani 'finger prints'. Mkuu wa FBI bwana J. Edgar Hoover alimteua bwana Samuel Cowley kuongoza misheni ya kumkamata John Dillinger. Cowley naye aliungana na Afisa *Mervin Purvis* kutoka mjini Chicago. Kwa pamoja walishirikiana na polisi kuhakikisha huyu 'Adui namba moja' anapatikana. Ilikuwa ni siku ya tarehe 21 Julai 1934 ambapo maafisa usalama walipokea simu kutoka kwa mwanadada mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Anna. Binti huyu alitoa taarifa za siri kwamba 'kesho jioni, yeye, John Dillinger pamoja na mpenzi wake, Polly Hamilton, wataenda kuangalia filamu kwenye moja ya majumba ya sinema, akaeleza kwamba watachagua kwenda aidha Biograph Theater au Marbo Theater. Na wakapanga kwamba atavaa vazi la rangi nyekundu ili iwe rahisi kwa maofisa hao kumtambua. Ilipofika kesho yake, maofisa wakampigia simu Anna Sage ili 'ku-comfirm' ni wapi wataenda kati ya Biograph au Marbo??. Lakini kwakua Anna alikuwa bado hajui ni wapi haswa wataenda, tuliona maofisa usalama wakiongozwa na Marvin Purvis wakijigawa kwenda 'kukava' sehemu zote mbili. Hatimaye ilipofika majira ya saa 2:30 usiku, Anna, John Dillinger pamoja na Polly Hamilton, walionekana wakiingia kwenye jumba la sinema la *Biograph Theater*. Baada ya kina Dillinger kuingia, tukaona wale maofisa wengine waliokuwepo kule 'Marbo Theater' wakiwasili haraka pale 'Biograph Theater' kwa ajili ya kuongeza nguvu. Saa 4:30 usiku, baada ya filamu kumalizika, alionekana John Dillinger akiwa na wale warembo wake wawili, mmoja kulia mwingine kushoto, wakiwa wanatoka nje. Wakati wanakuja usawa wa aliposimama ofisa Purvis. Purvis aliwasha sigara yake kama ishara ya wale wenzake kusogea jirani. Wakati anafanya hivyo, kumbe Dillinger alikuwa *'ameshahisi hali ya hatari',* akatoa bastola yake huku akijihami kwa kujaribu kukimbia. Lakini kabla hajafika mbali, risasi tatu zilifika kwenye mwili wa John Dillinger. Risasi moja ikipenya upande wa nyuma wa shingo na kutokezea kwenye sikio. Dakika chache zilizofuata, hospitali ya Alexian Brothers ilitangaza kifo cha John Dillinger. Na hiyo ndio ikawa mwisho wa mtukutu huyu ambaye alifariki tarehe kama ya leo *22 Julai 1934.* Baada ya kuenea taarifa za kifo chake watu wengi walifurika eneo la tukio angalau waweze kuuona mwili wa John Dillinger. **** Lakini nafahamu utakuwa unajiuliza yule mwanadada aliyetoa taarifa za siri za kurahisisha kukamatwa kwa John Dillinger ni nani na kwanini alifanya hivyo?!! Baadae nitaeleza kisa hiko. Lakini kwa sasa tuishie hapa. Ahsante.
    Like
    1
    · 0 Reacties ·0 aandelen ·951 Views
  • Read more
    MADA: SAMSONI ALIMSHINDA SAMSONI, SIO WAFILISTI; JIFUNZE KUSEMA "HAPANA." Hadithi ya Samsoni si hadithi ya usaliti tu bali ni kioo kinachoakisi mapambano ya kila mwanamume na mwanamke. Samsoni alikuwa hodari, naam. Nguvu zake zingeweza kubomoa malango na simba, lakini mwili wake haungeweza kupinga minong’ono ya matamanio yake mwenyewe. Kwangu mimi, si Delila aliyemshinda Samsoni; Samsoni alishindwa na tamaa zake. Unaona, nguvu za makuri Mahibuli Mahriza, na nguvu za kiakili kusonga mbele. Nguvu ya mikono yako ina faida gani ikiwa matamanio ya moyo wako yataachwa bila kudhibitiwa? Nguvu ya kweli sio uwezo wa wengine, lakini uwezo wa kujishinda mwenyewe. Biblia inasema katika Mithali 25:28, “Mtu asiye na kujizuia kama mji uliobomolewa na kuachwa bila kuta. Kuanguka kwa Samsoni kulianza muda mrefu kabla ya kuwasili kwa Delila. Kushindwa kwake kulipandwa katika mashamba ya anasa, kumwagilia maji kwa kukosa kujizuia, na kuvunwa na adui. Tatizo halikuwepo Delila. Tukio hilo lilikuwa ni la Delila, lakini msukumo wa Samsoni ulikuwa sababu kuu. Ni mara ngapi tunalaumu wengine kwa zamani kwetu, tukikataa kukubali kwamba vita vili ndani yetu muda mrefu kabla ya kuonekana kwa ulimwengu? Ikiwa huwezi kusema "hapana" kwako mwenyewe, utakabidhi mkasi ambao utapunguza nywele za hatima yako. Nguvu ya akili ni ujasiri wa kutembea mbali na kile kinachojisikia lakini sio sawa. Ni uwezo wa kuketi kwenye meza ya majaribu na kuacha chakula bila kuguswa. Nguvu ya akili ni nguvu ya kupinga uhusiano huo unaojua utakupoteza. Ni nidhamu ya kukwepa njia za mkato, tukijua kuwa si kila kitu kinachometa katika dhahabu. Mwaka huu, jifunze kusema hapana. Sema hapana kwa mazoea ambayo yanakuchosha roho. Sema hapana kwa urafiki ambao unapunguza mwanga wako. Sema hapana kwa mahusiano ambayo yanakuvuta mbali na Mungu. Sema hapana kwa jambo lolote linalohatarisha maisha yako ya baadaye. Ni bora kuukatisha tamaa mwili wako kuliko kukatisha tamaa hatima yako. "Hapana" ndogo leo inaweza kukuokoa kutokana na maisha ya majuto. Yusufu aliposimama mbele ya mke wa Potifa, hakukaa ili kuliaana. Alikimbia! sababu wakati mwingine jambo la nguvu unaweza kukimbia kutoka kwa kile kinachotaka kukuangamiza. Samson alibaki. Na katika kukaa, alipoteza kila kitu. Hadithi yake inatufundisha kwamba maadui hatari zaidi sio nje lakini ndani. Ikiwa huwezi kuadhibu tamaa zako, tamaa zako zitakuadibu. Ikiwa huwezi kudhibiti hamu yako, hamu yako itadhibiti. Ushindi juu ya nafsi ni mkuu kuliko ushindi juu ya maadui elfu. Tunaposonga mbele mwaka huu, acha ukweli huu urudie moyoni mwako, vita vyako vikubwa zaidi havitapigana hadharani bali katika ukimya wa nafsi yako. Mungu akutie nguvu. Na jaribu linapokuja kubisha, acha jibu lako liwe wazi, "Hapana." @Fr. Albert Nwosu' (Nwachinemere)
    Love
    1
    · 0 Reacties ·0 aandelen ·501 Views
  • Hujambo kaka...Mie jina langu Mike kutoka Nairobi Kenya natafuta mchumba kwa mahusiano ambayo yatatuelekeza kwenye ndoa.Nina umri wa miaka 30 hivi awe na umri sawa na wangu au awe mdogo kwangu.Nambari yangu ya whatsapp ni +254713168463.
    Hujambo kaka...Mie jina langu Mike kutoka Nairobi Kenya 🇰🇪 natafuta mchumba kwa mahusiano ambayo yatatuelekeza kwenye ndoa.Nina umri wa miaka 30 hivi awe na umri sawa na wangu au awe mdogo kwangu.Nambari yangu ya whatsapp ni +254713168463.
    Like
    Love
    4
    · 1 Reacties ·0 aandelen ·627 Views
  • Read more
    Mwigizaji wa mrefu Tanzania, Jacqueline Wolper ametangaza rasmi kuachana na aliyekuwa Mumewe. "Hellow Mashabiki zangu, marafiki na Watanzania wote mnao nitakia mema. Ni kwa masikitiko mengi sana mmekuwa mkinitumia message, links, na Clips mbalimbali, huku mkinishauri, kuniombea na kunitia moyo. Nimepokea msg zenu zote kwa moyo wa Shukrani sana. Na Mungu awabariki wote mnao nitakia mema, na hata wale wenye nia tofauti na njema pia mbarikiwe. Lakini naomba niwatoe wasiwasi na mashaka juu ya furaha na amani ya moyo wangu. Mimi na mzazi mwenzangu Rich (Baba P) hatupo pamoja (TUMEACHANA). Nipo kwenye process za Divorce/Talaka. Hivyo, mashauri yote na huruma juu ya mambo yanayo endelea na mzazi mwenzangu, msiyalete kwangu tena. Ni mtu ambae yupo huru kufanya chochote kinacho mpendeza. Na hii niseme tu si kwa ubaya haijalishi mtalipokeaje wengine lakini maisha halisi ya ndoa yangu nayajua mimi na mwenzangu kwahiyo tutabaki kuheshimiana kama wazazi na kulea watoto wetu lakini swala la mahusiano ya ndoa hilo halipo! Nawapenda sana nashukuru kwa msg zenu nyingi za kunitia moyo kutokana na mambo mnayoyaona huko lakini niwaambie tu mimi nipo sawa na muache kunihusisha na mambo yanayoendelea kwa mzazi mwenzangu kwasababu hayanihusu na nisingependa kuongelea hayo 🙏🏾🙏🏾" ameandika Wolper.
    Wow
    1
    · 0 Reacties ·0 aandelen ·662 Views
  • Read more
    .JEMEDARI SAID: MWENDA NI BONGE LA MCHEZAJI,YANGA WAMERAMBA DUME. . "Kumuona Israh kutoka Singida Black Stars kwenda Yanga sio kitu cha ajabu sana maana tumewaona wengi mfano Feisal kutoka Yanga kwenda Azam ni vitu vya kawaida, Yanga wamepata mchezaji mzuri sana sina shaka nae" "Nina imani kocha amehusika kwa asilimia 100% maana wapo viongozi walisemaga kuwa sio rahisi kocha kusajili mwenyewe lazima ashirikishe viongozi ila inawezekana alimuhitaji mchezaji akaonyeshwa video zake nae akaridhika naye" "Ni ushamba tu wa mashabiki kuwasema wachezaji wakitanzania, watu walitaka kuona Simba au Yanga wanasajili wachezaji kutoka nje tu...huu ni ushamba na niwapongeze Yanga kufanya usajili wa Mwenda hata Kelvin Nashon" "Yanga wamefanya kitu cha maana isipokuwa wanahitaji kuvumilia hadi watakapokuwa vizuri kwenye kikosi chao" . “ Israel Mwenda ni mchezaji mzuri. Namjua tangu 2016. Dogo ana kipaji kizuri maana amefanya vyema akiwa na timu za Simba SC, KMC hadi timu ya Taifa. Kilichomuondoa Simba SC ni nafasi ya kucheza. Nifichue siri leo, hakuwa na mahusiano mazuri na Shomary Kapombe. Hawa wote ni wanangu. Muda mwingine unaona bora uondoke tu kutafuta changamoto nyingine" . "Kutoka Singida Black Stars kwenda Yanga SC ni kitu cha kawaida kabisa. Lakini Yanga SC wamepata mchezaji mwenye uwezo, lakini arekebishwe mentality yake. Huyu ni mchezaji ambaye unaweza kumtumia katika mifumo mingi. Naamini kocha wa Yanga SC amehusika moja kwa moja na usajili huu “ . JEMEDARI SAID,Mchambuzi CROWN FM.
    Like
    Love
    5
    · 0 Reacties ·0 aandelen ·624 Views
  • MAHUSIANO MABAYA
    MAHUSIANO MABAYA
    Like
    Love
    Haha
    6
    · 0 Reacties ·0 aandelen ·314 Views
  • Read more
    .🚨TRANSFER NEWS Yanga yarudi tena DR Congo sasa ni zamu ya winga hatari JONATHAN LOMBO. Winga wa kulia wa AS Vita Jonathan Ikangalombo Kapela yupo katika hatua za mwisho za kujiunga na yanga sc kwenye dirisha dogo la usajili na tayari viongozi wa yanga sc wapo DR Congo na wanaendelea na mazungumzo ambayo yanakwenda vizuri hadi sasa. Winga huyu msumbufu na hatari mwenye umri wa miaka 22 alisajiliwa na As Vita club mwaka 2023 akitokea DC Motema Pembe na sasa akiwa chini ya Kocha wa Zaman wa Azam fc Youssouph Dabo amekuwa na kiwango kizuri huku akishinda tuzo ya mchezaji bora wa mechi mwaka huu kwenye Derby baina ya As Vita club Vs Dc Motema Pembe Yanga imeamua kurudia asili yake ya kutumia mawinga kama ilivyo kuwa tamaduni yao huku kukiwa na mahusiano mazuri na As Vita Club ambapo yanga iliwahi kuwasajili Ducapel Moloko 2021-22,Djuma shabani na winga Tuisila Kisinda msimu wa 2020-21 hivyo kwa sasa ni dhahiri shahiri Jonathan Lombo anakwenda kuwa mchezaji wa yanga huku akiwa na kasi na mnyumbulifu sana. Utambulisho wake ni suala la Muda tu dirisha dogo litakapo funguliwa mapema.
    Like
    Love
    4
    · 0 Reacties ·0 aandelen ·478 Views
  • Read more
    Yamesemwa na Shafii Dauda, Mchambuzi Klabu ya Yanga imemtaka Meneja habari na mawasiliano wa Simba SC , Ahmed Ally kutoka hadharani na Kauli ya Ahmed iliyosababisha haya 👇 “Pacome amemaliza mkataba tukiona anafaa tutahangaika nae , Pacome amemaliza mkataba ndani ya Yanga na hana mpango wa kuongeza ..mtanyoa ndevu mwaka huu hana mpango wa kuongeza amechoka kuchomwa sindano kila siku kama anazuia mimba” “Tunaangalia kiwango chake kama kitaturidhisha tutahangaika nae lakini kama ataendelea na mwenendo wake anaoendelea nao tutawaachia…kama tulivyowaachia Chama na tunataja majina Live hakuna kutumia code” Demand letter ya Yanga imeeleza kuwa kauli hiyo ni ya upotoshaji na imejaa dharau kwa klabu yao , hivyo imeharibu mahusiano yao na wadau wa kibiashara na wadhamini Yanga wanamtaka Ahmed afanye yafuatayo ndani ya siku tano (5) 1.Kuomba radhi kwa njia sawa na aliyotumia kutoa kauli yake 2.Kufidia malipo ya Tsh Bilioni 10 ( 10,000,000,000) Yanga wamemaliza kwa kusema kama hayo maagizi hayatafanyiwa kazi watafuata hatua za kisheria zaidi ✍️✍️✍️✍️ SHAFII DAUDA Kutoka chanzo cha kuaminika.
    Like
    1
    · 0 Reacties ·0 aandelen ·263 Views
  • Read more
    Klabu ya Yanga imemtaka Meneja habari na mawasiliano wa Simba SC , Ahmed Ally kutoka hadharani na kuomba radhi kwa matanshi wanayodai yameichafua klabu yao (Yanga) mbali na hili wanadai fidia ya Tsh Bilioni 10 Kauli ya Ahmed iliyosababisha haya 👇 “Pacome amemaliza mkataba tukiona anafaa tutahangaika nae , Pacome amemaliza mkataba ndani ya Yanga na hana mpango wa kuongeza ..mtanyoa ndevu mwaka huu hana mpango wa kuongeza amechoka kuchomwa sindano kila siku kama anazuia mimba” “Tunaangalia kiwango chake kama kitaturidhisha tutahangaika nae lakini kama ataendelea na mwenendo wake anaoendelea nao tutawaachia…kama tulivyowaachia Chama na tunataja majina Live hakuna kutumia code” Demand letter ya Yanga imeeleza kuwa kauli hiyo ni ya upotoshaji na imejaa dharau kwa klabu yao , hivyo imeharibu mahusiano yao na wadau wa kibiashara na wadhamini Yanga wanamtaka Ahmed afanye yafuatayo ndani ya siku tano (5) 1.Kuomba radhi kwa njia sawa na aliyotumia kutoa kauli yake 2.Kufidia malipo ya Tsh Bilioni 10 ( 10,000,000,000) Yanga wamemaliza kwa kusema kama hayo maagizo hayatafanyiwa kazi watafuata hatua za kisheria zaidi
    Like
    Love
    5
    · 0 Reacties ·0 aandelen ·357 Views
  • Read more
    Chakula kizuri na salama ni kile ulichokipika mwenyewe Umekiangaikia Kwa muda fulani Hadi kufika mezani kukifurahia. Chakula Cha kuandaliwa kinaweza kisikizi vigezo. kinaweza kuwa kizuri lakini kisitoshe. Kinaweza kitoshe lakini kisiwe kizuri. Ndivyo yalivyo maisha. Maisha mazuri na yenye amani ni yale uliyoyasotea mwenyewe.unajua panda shuka zote hadi kufika ulipo. kIla ukijitazama utajiongeza uzidi kuwa bora. Hali kadhalika mahusiano.Ukikubali kutengeneza yale unayoyapenda itapata kile unachokipenda.
    Like
    Love
    2
    · 0 Reacties ·0 aandelen ·260 Views
  • Read more
    Siyo kila tatizo unalokutana nalo barabarani pindi uendeshapo gari litahitaji ukamate brake... Mengine yanahitaji ukanyage mafuta ili gari ipite kikwazo hiko... Hivyo basi hata kwenye ndoa na mahusiano siyo kila tatizo ukimbilie kwa wazazi au ulireact.. Kuna matatizo mengine unatakiwa uwe muelewa na uyachukulie kama yalivyo ili yapite salama.. Mengine yanahiyaji kujibebisha zaidi ili uilinde furaha yako isipotee...
    Like
    1
    · 0 Reacties ·0 aandelen ·396 Views
  • Mwanamke hutegemea MOYO kuanzisha mahusiano kichwa wanasukia nywele, ila Mwanaume hutumia KICHWA (BRAIN) kuanzisha mahusiano, sasa iko hivi, shida huja pale ambapo hata huoo MOYO wenyewe unaweza penda hata ujinga wakati mwingine.
    Mwanamke hutegemea MOYO kuanzisha mahusiano kichwa wanasukia nywele, ila Mwanaume hutumia KICHWA (BRAIN) kuanzisha mahusiano, sasa iko hivi, shida huja pale ambapo hata huoo MOYO wenyewe unaweza penda hata ujinga wakati mwingine.
    0 Reacties ·0 aandelen ·288 Views
  • Read more
    My Sister! Are you Under a Spell?. Naona wadada wengi ambao hawajaolewa, wazuri na wengine wakiwa na careers zao nzuri tu wapo kwenye mahusiano ya hovyo kupata kutokea. Sijajua ni kwanini lakini nashangaa bado waking'ang'ania hali hiyo. Mwanaume anakupiga, lakini bado upo, anakusaliti mbele ya macho yako lakini bado umeng'ang'ana tu...anakuumiza hisia zako, anakuongelea vibaya, haku-support, hajawahi kukununulia hata nguo ya ndani na hakuheshimu lakini bado upo tu. Sehemu pekee anayokupeleka ni kitandani au Bar, hamjawahi kutembea pamoja maeneo ya wazi, sehemu mnayoonekana pamoja ni kwenye giza giza lakini bado unaona sawa tu. Anakwambia anaweka mahusiano yenu private, lakini wewe bado unajionyesha kwake na unamuacha ana-enjoy sehemu zako za siri za mwili wako mzuri. Nafikiri unahitaji semina binafsi...watu pekee wanaokufahamu kwa upande wake ni marafiki na binamu zake basi, mwanaume anaekutambulisha kwa marafiki tu sio wa kumuamini moja kwa moja..yeye hajali ni kwa kiasi gani hao watu wanamfahamu kwa kuwa obvious watamfichia siri yake tu. Umefungwa na nini..? Nani amekuroga...? Ngoja nikwambie kitu kuhusiana na sisi wanaume. Hatuna tofauti sana na yule mwajiriwa wa kawaida...mwajiriwa wa kawaida yuko radhi afanye chochote kile ilimradi mwisho wa mwezi alipwe mshahara..sawa na sisi: hufanya lolote lile ilimradi tupate sex. Ndio, hata kuwadanganyeni kuwa tutawaoa, hata kuonekana kwa wazazi wenu as long as you guarantee us a sex...sasa imagine unaolewa na mwanaume wa hivyo, unafikiri atakua mume bora? Unafikiri atakupa furaha? Au unafikiri atabadilika? Hilo sahau..unaloliona ndilo utakalolipata. My sister, unatakiwa ujue thamani yako. Hata siku moja usijaribu kujishushia heshima na thamani yako ili tu umkamate mwanaume. Mwanaume ambae hawezi kukuheshimu na kuku-treat vizuri hakustahili hata kidogo. Ni bora uwe single, ukijigeuza huku na huku kitandani pekeyako kuhangaika na network ya Tigo kuliko kugeuzwa geuzwa kitandani na mwanaume ambae hastahili kupewa hiyo asali. Kamwe usiuze utu wako kwa minajili kwamba na wewe ujiite "am in a relationship"... hapana dada yangu hayo sio mahusiano, hizo ni personal benefits na tena anafaidi kweli, maana kila anapokuhitaji anakupata na unampa tu, anakuchafua na baada ya hapo maumivu tu kwa upande wako ukitarajia atabadilika na kuja kukuoa. My sister, hold yourself in so high esteem kiasi ya kwamba hata ukipita katikati ya kundi la wanaume, hakuna hata mmoja atainua kidole chake na kusema kwamba "nimeshakula ile mambo". Jiheshimu na heshimu hisia na mwili wako, hilo tunda anastahili mume wako tu, litunze ili usije ukampa likiwa limeliwa vya kutosha na limechacha...It's starts with you, if you don't know your value, you will be as common as a coin... Know your value and never be demeaned by anyone. Najua wanaume hawataipenda hii, ila muda mwingine lazima tuwaelimishe hawa dada zetu, ndio walezi wa kizazi kijacho. #KnowYourValueAndAct #MarriageUnderGodFoundation #MarriageIsBeautifu
    0 Reacties ·0 aandelen ·1K Views
Zoekresultaten