• Rais wa Marekani , Donald Trump ametoa siri kuwa Ofisi yake imepokea barua kutoka kwa Rais wa Ukraine , Volodymyr Zelensky, ikisema yuko tayari kwa mazungumzo na Russia na kusaini makubaliano ya madini adimu.

    “Ukraine iko tayari kukaa kwenye meza ya mazungumzo haraka iwezekanavyo ili kuleta amani ya kudumu. Hakuna anayetaka amani zaidi ya Waukraine,” Trump amesema katika hotuba yake bungeni usiku wa kuamkia leo huku akinukuu barua hiyo.

    “Mimi na timu yangu tuko tayari kufanya kazi chini ya uongozi thabiti wa Rais Trump ili kupata amani ya kudumu’,” Trump alinukuu maneno ya Zelenskyy.

    “Si hilo lingekuwa jambo zuri?” aliuliza. “Ni wakati wa kukomesha huu upuuzi. Ni wakati wa kusitisha mauaji. Ni wakati wa kumaliza vita hivi visivyo na maana. Ukitaka kumaliza vita, lazima uzungumze na pande zote mbili,” amesema Trump.

    Kauli hiyo ya Trump imekuja siku chache baada ya mvutano mkali kati yake na Zelenskyy katika Ofisi ya Oval iliyoko Ikulu ya White House, hali iliyosababisha Marekani kusitisha msaada muhimu wa kijeshi kwa Ukraine.

    Rais wa Marekani 🇺🇸, Donald Trump ametoa siri kuwa Ofisi yake imepokea barua kutoka kwa Rais wa Ukraine 🇺🇦, Volodymyr Zelensky, ikisema yuko tayari kwa mazungumzo na Russia 🇷🇺 na kusaini makubaliano ya madini adimu. “Ukraine iko tayari kukaa kwenye meza ya mazungumzo haraka iwezekanavyo ili kuleta amani ya kudumu. Hakuna anayetaka amani zaidi ya Waukraine,” Trump amesema katika hotuba yake bungeni usiku wa kuamkia leo huku akinukuu barua hiyo. “Mimi na timu yangu tuko tayari kufanya kazi chini ya uongozi thabiti wa Rais Trump ili kupata amani ya kudumu’,” Trump alinukuu maneno ya Zelenskyy. “Si hilo lingekuwa jambo zuri?” aliuliza. “Ni wakati wa kukomesha huu upuuzi. Ni wakati wa kusitisha mauaji. Ni wakati wa kumaliza vita hivi visivyo na maana. Ukitaka kumaliza vita, lazima uzungumze na pande zote mbili,” amesema Trump. Kauli hiyo ya Trump imekuja siku chache baada ya mvutano mkali kati yake na Zelenskyy katika Ofisi ya Oval iliyoko Ikulu ya White House, hali iliyosababisha Marekani kusitisha msaada muhimu wa kijeshi kwa Ukraine.
    Like
    1
    · 0 Comments ·0 Shares ·239 Views
  • Ijumaa, tarehe 28 Februari, haikuwa siku rahisi kwa Rais wa Ukraine, Volodymyr Zelensky, alipofanya ziara katika Ikulu ya White House, Marekani. Kabla hata ya mzozo wa maneno kati yake na mwenyeji wake, Rais Donald Trump, pamoja na Makamu wa Rais JD Vance, tayari kulikuwa na ishara za mivutano.

    Trump alimkaribisha Zelensky mlangoni na kusema kwa utani: “Leo amevalia kweli kweli,” kauli ambayo iliwafanya baadhi ya waandishi wa habari kuiona kama kejeli badala ya pongezi. Wakati huo, Zelensky alikuwa amevalia fulana nyeusi ya mikono mirefu, vazi ambalo amekuwa akilivaa mara kwa mara tangu Ukraine ivamiwe na Urusi mwaka 2022.

    Baadaye, Trump alipompokea Waziri Mkuu wa Uingereza, Keir Starmer, alionekana kutazama mavazi yake kwa makini kutoka juu hadi chini, kisha kunong’ona maneno yanayoweza kutafsiriwa kama pongezi kwa suti rasmi aliyovaa Starmer.

    Mjadala kuhusu mavazi ya Zelensky ulizidi kupamba moto wakati wa mkutano wa waandishi wa habari. Brian Glenn, mwandishi kutoka Real America’s Voice—chombo cha habari kinachopendelea mrengo wa kulia—alimtupia swali la moja kwa moja:

    “Kwa nini hauvai suti? Upo katika ofisi ya juu kabisa katika nchi hii, na umegoma kuvaa suti – je, unamiliki hata suti?”

    Kwa utulivu, Zelensky alijibu kwa mshangao mdogo:

    “Nitavaa suti vita hivi vitakapomalizika. Labda suti kama yako, labda bora zaidi, au pengine ya bei nafuu kuliko yako,” alisema kwa utani huku akionyesha msimamo wake wa kuendelea kuvaa mavazi ya kijeshi.

    Swali hilo la Glenn liliibua mjadala mkali mitandaoni. Wengine walimuunga mkono, wakisema kwamba kiongozi wa taifa anapaswa kuvaa mavazi rasmi anapokutana na viongozi wengine, ilhali wengine waliona swali hilo kuwa la dhihaka na lisilo na umuhimu.

    Miongoni mwa waliomkosoa Glenn ni mwandishi maarufu wa Uingereza, Piers Morgan, ambaye pia ni rafiki wa karibu wa Trump. Morgan aliandika kwenye mtandao wa X (zamani Twitter):

    “Swali la kipuuzi. Elon Musk havai suti anapoingia Ikulu.”

    Historia pia inaonyesha kuwa si Zelensky pekee aliyeingia Ikulu ya Marekani bila suti. Waziri Mkuu wa zamani wa Uingereza, Winston Churchill, alifanya hivyo katika moja ya ziara zake rasmi.
    Ijumaa, tarehe 28 Februari, haikuwa siku rahisi kwa Rais wa Ukraine, Volodymyr Zelensky, alipofanya ziara katika Ikulu ya White House, Marekani. Kabla hata ya mzozo wa maneno kati yake na mwenyeji wake, Rais Donald Trump, pamoja na Makamu wa Rais JD Vance, tayari kulikuwa na ishara za mivutano. Trump alimkaribisha Zelensky mlangoni na kusema kwa utani: “Leo amevalia kweli kweli,” kauli ambayo iliwafanya baadhi ya waandishi wa habari kuiona kama kejeli badala ya pongezi. Wakati huo, Zelensky alikuwa amevalia fulana nyeusi ya mikono mirefu, vazi ambalo amekuwa akilivaa mara kwa mara tangu Ukraine ivamiwe na Urusi mwaka 2022. Baadaye, Trump alipompokea Waziri Mkuu wa Uingereza, Keir Starmer, alionekana kutazama mavazi yake kwa makini kutoka juu hadi chini, kisha kunong’ona maneno yanayoweza kutafsiriwa kama pongezi kwa suti rasmi aliyovaa Starmer. Mjadala kuhusu mavazi ya Zelensky ulizidi kupamba moto wakati wa mkutano wa waandishi wa habari. Brian Glenn, mwandishi kutoka Real America’s Voice—chombo cha habari kinachopendelea mrengo wa kulia—alimtupia swali la moja kwa moja: “Kwa nini hauvai suti? Upo katika ofisi ya juu kabisa katika nchi hii, na umegoma kuvaa suti – je, unamiliki hata suti?” Kwa utulivu, Zelensky alijibu kwa mshangao mdogo: “Nitavaa suti vita hivi vitakapomalizika. Labda suti kama yako, labda bora zaidi, au pengine ya bei nafuu kuliko yako,” alisema kwa utani huku akionyesha msimamo wake wa kuendelea kuvaa mavazi ya kijeshi. Swali hilo la Glenn liliibua mjadala mkali mitandaoni. Wengine walimuunga mkono, wakisema kwamba kiongozi wa taifa anapaswa kuvaa mavazi rasmi anapokutana na viongozi wengine, ilhali wengine waliona swali hilo kuwa la dhihaka na lisilo na umuhimu. Miongoni mwa waliomkosoa Glenn ni mwandishi maarufu wa Uingereza, Piers Morgan, ambaye pia ni rafiki wa karibu wa Trump. Morgan aliandika kwenye mtandao wa X (zamani Twitter): “Swali la kipuuzi. Elon Musk havai suti anapoingia Ikulu.” Historia pia inaonyesha kuwa si Zelensky pekee aliyeingia Ikulu ya Marekani bila suti. Waziri Mkuu wa zamani wa Uingereza, Winston Churchill, alifanya hivyo katika moja ya ziara zake rasmi.
    Like
    Love
    2
    · 0 Comments ·0 Shares ·410 Views
  • Nikueleze kwa kifupi sana kiini cha mgogoro. Kabla ya mwaka 1991 Ukraine ilikua sehemu ya Urusi kupitia muungano wa kisovieti wa USSR. Baada ya USSR kufa ndipo taifa la Ukraine likazaliwa pamoja na mataifa mengine 14 yaliyokua majimbo ya Urusi.

    Lakini usisahau mwaka 1949 umoja wa kujihami wa nchi za magharibi (NATO) ulianzishwa dhidi ya Urusi (USSR). Makubaliano yao ni kwamba ikiwa Urusi itamgusa mmoja wao basi wote watamvamia. Marekani akiwa kinara.

    Kuanguka kwa USSR kukafanya mataifa 15 mapya kuzaliwa. Baadhi ya Mataifa hayo yakawa na hofu kuwa Urusi inaweza kurudi kuyakalia kimabavu. Kwahiyo yakaomba kujiunga NATO kwa usalama wao. Estonia, Latvia na Lithuania zikapata uanachana wa NATO chap kwa haraka. Ukraine ilipoomba uanachama Urusi ikakataa, kwa sababu ya strategic position ya Ukraine ambayo inaiweka Urusi hatarini.

    Ukraine ilipokosa uanachama NATO ikamua kujilinda kwa kusuka mpango wa nyuklia. Marekani na Urusi zikashtuka. Kwa kutambua hatari ya nyuklia zikamsihi sana Ukraine aachane na mpango huo. Mwaka 1994 ukaandaliwa mkataba uitwao Budapest memorundum, huko Hungary. Mkataba huo ulihusisha nchi 4. Urusi na Ukraine zilisaini kwamba hakuna atakayemvamia mwenzake. Marekani na Uingereza zikasaini kwamba atakayemvamia mwenzake watampiga bila huruma. Pia Marekani na Uingereza zitagharamia fedha na vifaa vyote vya vita. Mkataba ukasainiwa na Ukraine ikasitisha mpango wake wa nyuklia.

    Lakini Mwaka 2014 Urusi ikaivamia Ukraine na kuchukua jimbo lake la Crimea kimabavu. Marekani na Uingereza hazikuipiga Urusi kama mkataba wa Budapest unavyosema. Ukraine akalalamika lakini akapuuzwa. Kwenye vita inayoendelea sasa, Urusi ameshajitwalia majimbo manne Donetsk, Luhansk, Zaporizhzhia na Kherson lakini Marekani na Uingereza ziko kimya.

    Ukraine inaona imesalitiwa. Mkataba wa Budapest ulikua kiini macho. Laiti Ukraine ingekataa kusaini na kuendelea na mpango wake wa nyuklia, leo Urusi isingethubutu kuigusa. Lakini Waliomdanganya sasa wamemgeuka na wanamfokea. Ukraine ingeyajua maneno ya Mzee Jomo Kenyatta "Learn to fight your own battle" isingeachana na mpango wake wa nyuklia mwaka 1994. Wangejifunza kupigana vita yao wenyewe bila kutegemea mtu.!
    (Malisa GJ)

    Nikueleze kwa kifupi sana kiini cha mgogoro. Kabla ya mwaka 1991 Ukraine ilikua sehemu ya Urusi kupitia muungano wa kisovieti wa USSR. Baada ya USSR kufa ndipo taifa la Ukraine likazaliwa pamoja na mataifa mengine 14 yaliyokua majimbo ya Urusi. Lakini usisahau mwaka 1949 umoja wa kujihami wa nchi za magharibi (NATO) ulianzishwa dhidi ya Urusi (USSR). Makubaliano yao ni kwamba ikiwa Urusi itamgusa mmoja wao basi wote watamvamia. Marekani akiwa kinara. Kuanguka kwa USSR kukafanya mataifa 15 mapya kuzaliwa. Baadhi ya Mataifa hayo yakawa na hofu kuwa Urusi inaweza kurudi kuyakalia kimabavu. Kwahiyo yakaomba kujiunga NATO kwa usalama wao. Estonia, Latvia na Lithuania zikapata uanachana wa NATO chap kwa haraka. Ukraine ilipoomba uanachama Urusi ikakataa, kwa sababu ya strategic position ya Ukraine ambayo inaiweka Urusi hatarini. Ukraine ilipokosa uanachama NATO ikamua kujilinda kwa kusuka mpango wa nyuklia. Marekani na Urusi zikashtuka. Kwa kutambua hatari ya nyuklia zikamsihi sana Ukraine aachane na mpango huo. Mwaka 1994 ukaandaliwa mkataba uitwao Budapest memorundum, huko Hungary. Mkataba huo ulihusisha nchi 4. Urusi na Ukraine zilisaini kwamba hakuna atakayemvamia mwenzake. Marekani na Uingereza zikasaini kwamba atakayemvamia mwenzake watampiga bila huruma. Pia Marekani na Uingereza zitagharamia fedha na vifaa vyote vya vita. Mkataba ukasainiwa na Ukraine ikasitisha mpango wake wa nyuklia. Lakini Mwaka 2014 Urusi ikaivamia Ukraine na kuchukua jimbo lake la Crimea kimabavu. Marekani na Uingereza hazikuipiga Urusi kama mkataba wa Budapest unavyosema. Ukraine akalalamika lakini akapuuzwa. Kwenye vita inayoendelea sasa, Urusi ameshajitwalia majimbo manne Donetsk, Luhansk, Zaporizhzhia na Kherson lakini Marekani na Uingereza ziko kimya. Ukraine inaona imesalitiwa. Mkataba wa Budapest ulikua kiini macho. Laiti Ukraine ingekataa kusaini na kuendelea na mpango wake wa nyuklia, leo Urusi isingethubutu kuigusa. Lakini Waliomdanganya sasa wamemgeuka na wanamfokea. Ukraine ingeyajua maneno ya Mzee Jomo Kenyatta "Learn to fight your own battle" isingeachana na mpango wake wa nyuklia mwaka 1994. Wangejifunza kupigana vita yao wenyewe bila kutegemea mtu.! (Malisa GJ)
    Like
    1
    · 0 Comments ·0 Shares ·450 Views
  • "Nimetazama Interview ya Rais wa Marekani na Rais wa Ukraine pale Oval Office ndani ya Ikulu ya Marekani, nimekuja kugundua Rais wa Ukraine anahisi anajadiliana na Mwanasiasa mwenzake ila anachosahau Trump ni Mfanyabiashara na hawezi kufanya kitu cha bure ambacho Taifa lake Marekani halinufaiki na chochote, ndio maan anamsukumia sana kuwa amalizane na Urusi wasaini mkataba wa amani.

    Pale Ukraine kuna madini adimu sana duniani, Mrusi hapigani Kichwa kichwa ndio maana maeneo ya Donbass na Zaporizhia yanabaki kuwa maeneo ya Kimkakati sana kwa Mrusi, hata Marekani hawapo kichwa kichwa maana Secretary Rubio wa Marekani alimwambia Rais wa Ukraine akubali kusaini mkataba wa madini ili wao waendelee kumlinda, Mrusi na Mmarekani wapo rada sana eneo lile na kila mmoja yupo Kitalaam.

    Kwa akili ya kawaida Marekani hataki kuendelea kugharamikia vita hivyo bila faida.

    Juzi kuna website nilisoma ya taarifa za Kiuchunguzi ni kuwa Marekani, China na Urusi kwasasa wapo meza moja na wazo lao kubwa wamekubaliana juu ya MULTIPOLAR WORLD ORDER ambapo Mataifa zaidi ya mawili yanakuwa na nguvu sawa ama yanakaribiana, kwa ufupi sana mataifa haya matatu yanataka kuitawala dunia bila kugusana.

    Ndio maana Trump alivyoingia madarakani akapush agenda chap ya BRICS kuachana na wazo lao la kuibadili dola ya Marekani kuwa sio sarafu rasmi kwenye umoja wao, ndio maana alipoingia wamerudi mezani kwa mengi ikiwemo Trump na Putin wote kukiri kuwa watashirikiana na Trump atasafiri kuelekea Urusi kwenye sherehe za Mei 9, ambapo watakutana Marais wote watatu yani Putin, Xi Jinping na Trump.

    Kifupi sana Marekani ya Donald Trump ina Approach tofauti sana, ndio maana hata Waziri Mkuu wa Uingereza Keir Stearmer alipofika White House kukutana na Trump kwenye mazungumzo yao akalisifia sana Jeshi la Uingereza ila kuna sehemu akampiga kwa kumwambia huwezi kuichukua Urusi peke yako, hata leo amesisitiza Ukraine wakubali amani nje na hapo bila msaada wake hawamuwezi Mrusi, huyo ndio Donald Trump" - Farhan JR, Mchambuzi.

    "Nimetazama Interview ya Rais wa Marekani na Rais wa Ukraine pale Oval Office ndani ya Ikulu ya Marekani, nimekuja kugundua Rais wa Ukraine anahisi anajadiliana na Mwanasiasa mwenzake ila anachosahau Trump ni Mfanyabiashara na hawezi kufanya kitu cha bure ambacho Taifa lake Marekani halinufaiki na chochote, ndio maan anamsukumia sana kuwa amalizane na Urusi wasaini mkataba wa amani. Pale Ukraine kuna madini adimu sana duniani, Mrusi hapigani Kichwa kichwa ndio maana maeneo ya Donbass na Zaporizhia yanabaki kuwa maeneo ya Kimkakati sana kwa Mrusi, hata Marekani hawapo kichwa kichwa maana Secretary Rubio wa Marekani alimwambia Rais wa Ukraine akubali kusaini mkataba wa madini ili wao waendelee kumlinda, Mrusi na Mmarekani wapo rada sana eneo lile na kila mmoja yupo Kitalaam. Kwa akili ya kawaida Marekani hataki kuendelea kugharamikia vita hivyo bila faida. Juzi kuna website nilisoma ya taarifa za Kiuchunguzi ni kuwa Marekani, China na Urusi kwasasa wapo meza moja na wazo lao kubwa wamekubaliana juu ya MULTIPOLAR WORLD ORDER ambapo Mataifa zaidi ya mawili yanakuwa na nguvu sawa ama yanakaribiana, kwa ufupi sana mataifa haya matatu yanataka kuitawala dunia bila kugusana. Ndio maana Trump alivyoingia madarakani akapush agenda chap ya BRICS kuachana na wazo lao la kuibadili dola ya Marekani kuwa sio sarafu rasmi kwenye umoja wao, ndio maana alipoingia wamerudi mezani kwa mengi ikiwemo Trump na Putin wote kukiri kuwa watashirikiana na Trump atasafiri kuelekea Urusi kwenye sherehe za Mei 9, ambapo watakutana Marais wote watatu yani Putin, Xi Jinping na Trump. Kifupi sana Marekani ya Donald Trump ina Approach tofauti sana, ndio maana hata Waziri Mkuu wa Uingereza Keir Stearmer alipofika White House kukutana na Trump kwenye mazungumzo yao akalisifia sana Jeshi la Uingereza ila kuna sehemu akampiga kwa kumwambia huwezi kuichukua Urusi peke yako, hata leo amesisitiza Ukraine wakubali amani nje na hapo bila msaada wake hawamuwezi Mrusi, huyo ndio Donald Trump" - Farhan JR, Mchambuzi.
    0 Comments ·0 Shares ·405 Views
  • Mazungunzo kati ya Rais wa Marekani , Donald Trump na Rais wa Ukraine , Volorymyr Zelensky yameishia njiani baada ya kushindwa kuelewana kuhusu hatima ya vita ya Russia dhidi ya Ukraine. Ilianza kama utani wakati wa kikao hicho ambacho kimehudhuriwa na Makamu wa Rais wa Marekani JD Vance na Waandishi wa Habari.

    Kila upande ulianza kuelezea kile ambacho wamejadiliana kuhusiana na makubaliano yaliyokuwa yanatarajiwa kutiwa saini. Awali Trump alieleza kuwa makubaliano hayo ni pamoja na kusaini mkataba unaoiruhusu Marekani kuchimba madini adimu (rare minerals) katika ardhi ya Ukraine.

    Wakati mrejesho wa hatua iliyofikiwa kuhusu makubaliano hayo ya mkataba wa madini mambo yalikuwa sawa ila yakaanza kwenda mrama pale Trump alipohamisha mada na kuingia suala la kupata mwafaka wa mzozo kati ya Ukraine na Russia ya Vladimir Putin.

    Trump kwenye suala hilo alienda moja kwa moja na kumtaka Rais Zelensky, kuingia makubaliano na Russia ya kumaliza vita hivyo, la sivyo Marekani itajindoa katika mazungumzo hayo na haitoendelea kuifadhili tena wala kuipatia misaada Ukraine. Wawili hao walikatizana mara kwa mara wakati wa majibizano yao kwa namna isiyo ya kawaida ndani ya Marekani (White House).

    Mazungunzo kati ya Rais wa Marekani 🇺🇸, Donald Trump na Rais wa Ukraine 🇺🇦, Volorymyr Zelensky yameishia njiani baada ya kushindwa kuelewana kuhusu hatima ya vita ya Russia 🇷🇺 dhidi ya Ukraine. Ilianza kama utani wakati wa kikao hicho ambacho kimehudhuriwa na Makamu wa Rais wa Marekani JD Vance na Waandishi wa Habari. Kila upande ulianza kuelezea kile ambacho wamejadiliana kuhusiana na makubaliano yaliyokuwa yanatarajiwa kutiwa saini. Awali Trump alieleza kuwa makubaliano hayo ni pamoja na kusaini mkataba unaoiruhusu Marekani kuchimba madini adimu (rare minerals) katika ardhi ya Ukraine. Wakati mrejesho wa hatua iliyofikiwa kuhusu makubaliano hayo ya mkataba wa madini mambo yalikuwa sawa ila yakaanza kwenda mrama pale Trump alipohamisha mada na kuingia suala la kupata mwafaka wa mzozo kati ya Ukraine na Russia ya Vladimir Putin. Trump kwenye suala hilo alienda moja kwa moja na kumtaka Rais Zelensky, kuingia makubaliano na Russia ya kumaliza vita hivyo, la sivyo Marekani itajindoa katika mazungumzo hayo na haitoendelea kuifadhili tena wala kuipatia misaada Ukraine. Wawili hao walikatizana mara kwa mara wakati wa majibizano yao kwa namna isiyo ya kawaida ndani ya Marekani (White House).
    Like
    1
    · 0 Comments ·0 Shares ·303 Views
  • Kikao cha mazungumzo ya kumaliza mzozo wa Nchi ya Ukraine na Nchi ya Urusi kinaendelea Nchini Saudi Arabia 🇸 ambapo Mawaziri wa Mashauri ya Kigeni wa Urusi chini ya Sergie Lavrov na Marekani chini ya Marco Rubio. Hata hivyo, Ukraine na Umoja wa Ulaya (EU) hawajashirikishwa huku Ukraine upande wake inapinga kikao hicho kuwa makubaliano yoyote haitayatambua.

    Katika kusisitiza hilo Ukraine imeendelea kusisitiza kwamba itaendelea kupigana vita kwa kutegemea Ulaya sio Marekani kama mwanzo huku Rais wa Nchi hiyo Volodmiry Zelensky akisema Ukraine ni Taifa huru, hivyo haliwezi kuamuliwa mambo yake na Marekani, itautetea uhuru wake hadi tone la mwisho. Marekani imejibu kwa kusema inaitaka Ukraine irejeshe haraka deni lote la usaidizi wa vita lililotolewa na Marekani tangu Februari 2022 Oparesheni ya Urusi ilipoanza.

    Kikao hiki kinachoendelea ni hatua muhimu kuelekea mkutano wa Rais Putin na Rais Trump uliopangwa mwezi Mei katika sherehe za Mashujaa wa Urusi utakaofanyika Jijini Moscow, Urusi ambapo pia mkutano huo utamwalika Rais wa China Xi Ping kama Mgeni mwalikwa muhimu.

    Kikao cha mazungumzo ya kumaliza mzozo wa Nchi ya Ukraine 🇺🇦 na Nchi ya Urusi 🇷🇺 kinaendelea Nchini Saudi Arabia 🇸 ambapo Mawaziri wa Mashauri ya Kigeni wa Urusi chini ya Sergie Lavrov na Marekani 🇺🇸 chini ya Marco Rubio. Hata hivyo, Ukraine na Umoja wa Ulaya (EU) hawajashirikishwa huku Ukraine upande wake inapinga kikao hicho kuwa makubaliano yoyote haitayatambua. Katika kusisitiza hilo Ukraine imeendelea kusisitiza kwamba itaendelea kupigana vita kwa kutegemea Ulaya sio Marekani kama mwanzo huku Rais wa Nchi hiyo Volodmiry Zelensky akisema Ukraine ni Taifa huru, hivyo haliwezi kuamuliwa mambo yake na Marekani, itautetea uhuru wake hadi tone la mwisho. Marekani imejibu kwa kusema inaitaka Ukraine irejeshe haraka deni lote la usaidizi wa vita lililotolewa na Marekani tangu Februari 2022 Oparesheni ya Urusi ilipoanza. Kikao hiki kinachoendelea ni hatua muhimu kuelekea mkutano wa Rais Putin na Rais Trump uliopangwa mwezi Mei katika sherehe za Mashujaa wa Urusi utakaofanyika Jijini Moscow, Urusi ambapo pia mkutano huo utamwalika Rais wa China 🇨🇳 Xi Ping kama Mgeni mwalikwa muhimu.
    0 Comments ·0 Shares ·404 Views
  • Rais wa Urusi , Vladimir Putin amewaalika Rais China , Xi Jinping na Rais wa Marekani , Donald Trump kuhudhuria sherehe maarufu za Ushindi wa Urusi katika vita kuu ya pili ya Dunia (Russia’s Victory Parade) zitakazofanyika tarehe 9 Mwezi May Jijini Moscow Nchini Urusi. Mwaliko huu unatokana na ombi la Rais Donald Trump la tarehe 11 Feb 2025 alipoomba kuzuru Moscow kwa lengo la kumaliza mgogoro wa Ukraine, Kikao kilichotokana na ombi hili kilifanywa kwa njia ya simu ambapo pamoja na mambo mengine, Trump alimhakikishia Putin kwamba Marekani itaacha ufadhili wa kijeshi kwa Ukraine na pia Ukraine itaachia sehemu ya ardhi yake iliyotwaliwa kama dhamana ya usalama wake dhidi ya Moscow.

    Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Washington katika taarifa yake ilikazia na kusisitiza kile alichokizungumza Trump na Moscow na kwamba Marekani inakusudia kumaliza tofauti zao kidunia. Utawala wa Trump umekuwa na juhudi kubwa kumaliza mizozo mikubwa duniani ambayo Ikulu hiyo ilikuwa ikifadhili na kuanzisha uchokozi kwa muda mrefu, Ukiachiliambali mgogoro wa Ukraine, pia Washington inashughulika kumaliza mgogoro wa Mashariki ya Kati huko Gaza ambapo mamia ya watu wameuawa kwa ufadhili wa Marekani hiyohiyo.

    Rais wa Urusi 🇷🇺, Vladimir Putin amewaalika Rais China 🇨🇳, Xi Jinping na Rais wa Marekani 🇺🇸, Donald Trump kuhudhuria sherehe maarufu za Ushindi wa Urusi katika vita kuu ya pili ya Dunia (Russia’s Victory Parade) zitakazofanyika tarehe 9 Mwezi May Jijini Moscow Nchini Urusi. Mwaliko huu unatokana na ombi la Rais Donald Trump la tarehe 11 Feb 2025 alipoomba kuzuru Moscow kwa lengo la kumaliza mgogoro wa Ukraine, Kikao kilichotokana na ombi hili kilifanywa kwa njia ya simu ambapo pamoja na mambo mengine, Trump alimhakikishia Putin kwamba Marekani itaacha ufadhili wa kijeshi kwa Ukraine na pia Ukraine itaachia sehemu ya ardhi yake iliyotwaliwa kama dhamana ya usalama wake dhidi ya Moscow. Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Washington katika taarifa yake ilikazia na kusisitiza kile alichokizungumza Trump na Moscow na kwamba Marekani inakusudia kumaliza tofauti zao kidunia. Utawala wa Trump umekuwa na juhudi kubwa kumaliza mizozo mikubwa duniani ambayo Ikulu hiyo ilikuwa ikifadhili na kuanzisha uchokozi kwa muda mrefu, Ukiachiliambali mgogoro wa Ukraine, pia Washington inashughulika kumaliza mgogoro wa Mashariki ya Kati huko Gaza ambapo mamia ya watu wameuawa kwa ufadhili wa Marekani hiyohiyo.
    Like
    1
    · 0 Comments ·0 Shares ·415 Views
  • Marais wa Urusi , V. Putin na yule wa Marekani , D.Trump walizungumza leo hii kwa muda saa moja na nusu kuhusu kumaliza vita Nchini Ukraine , kuboresha uhusiano kati ya Marekani na Urusi, na uwezekano wa kubadilishana Wafungwa.

    Aidha, Putin alimwalika Trump kwenda Mjini Moscow Nchini Urusi na akasema yuko tayari kuwakaribisha Maafisa wa Marekani kwa mazungumzo. Hii ilikuwa simu ya kwanza ya Putin na Rais wa Marekani aliyeko madarakani tangu Februari 2022, alipoongea na Biden muda mfupi kabla ya kutuma Wanajeshi Nchini Ukraine.

    Toa maoni yako
    #MvanoHabari
    #MvanoMtangazaji
    #M33
    Marais wa Urusi 🇷🇺, V. Putin na yule wa Marekani 🇺🇸, D.Trump walizungumza leo hii kwa muda saa moja na nusu kuhusu kumaliza vita Nchini Ukraine 🇮🇱, kuboresha uhusiano kati ya Marekani na Urusi, na uwezekano wa kubadilishana Wafungwa. Aidha, Putin alimwalika Trump kwenda Mjini Moscow Nchini Urusi na akasema yuko tayari kuwakaribisha Maafisa wa Marekani kwa mazungumzo. Hii ilikuwa simu ya kwanza ya Putin na Rais wa Marekani aliyeko madarakani tangu Februari 2022, alipoongea na Biden muda mfupi kabla ya kutuma Wanajeshi Nchini Ukraine. Toa maoni yako #MvanoHabari #MvanoMtangazaji #M33
    0 Comments ·0 Shares ·503 Views
  • Kwa mujibu wa wa kiongozi mkuu wa Korea Kaskazini Kim Jong Un , migogoro inayochochewa na Marekani katika sehemu mbalimbali za dunia, "inazidi kuongeza hatari ya kuzuka kwa vita vya dunia vipya vyenye athari kubwa sio tu kwa amani na usalama wa kimataifa bali pia nyanja nyingine zote za shughuli za binadamu."

    Pia Kim alitoa maoni kwamba mwaka 2025, mzozo wa Ukraine utasalia kuwa moja ya "mhimili mkuu wa hali ya wasiwasi ya kimataifa," nyingine ikiwa hali katika Ukanda wa Gaza na Syria "ambayo imekuwa uwanja wa migogoro ya kijiografia na makabiliano ya kimataifa mwaka jana."

    Katika hatua nyingine Kim alisema Marekani na nchi za Magharibi zinaelezea mzozo wa Ukraine kwa kushindwa kuishinda Urusi kimkakati, kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un alisema, kama ilivyonukuliwa na Shirika la Habari la Korea (KCNA).

    Katika mkutano katika Wizara ya Ulinzi, kuadhimisha kumbukumbu ya miaka 77 ya Jeshi la Wananchi wa Korea, alidai kwamba Marekani imepofushwa na tamaa mbaya huku akiionyesha wasiwasi mkubwa juu ya tabia ya kutojali ya Marekani na kundi la Magharibi kwa makusudi kuendeleza vita vya muda mrefu kwa ndoto isiyoweza kutekelezwa ili kukabiliana na kurudi kwa kimkakati kwa Urusi," shirika la habari lilibainisha.

    Kim alidokeza kuwa Pyongyang imekuwa ikipinga kila mara "kitendo chochote cha kunyima haki ya kimataifa na kuvuruga amani na usalama duniani." Aliongeza kuwa nchi yake "itaunga mkono kila wakati na kuhimiza sababu ya haki ya jeshi la Urusi na watu kutetea uhuru wao, usalama na uadilifu wa eneo kwa kuzingatia ari ya mkataba juu ya ushirikiano wa kimkakati wa kina kati ya DPRK na Urusi."
    (Zungu)

    Kwa mujibu wa wa kiongozi mkuu wa Korea Kaskazini Kim Jong Un , migogoro inayochochewa na Marekani katika sehemu mbalimbali za dunia, "inazidi kuongeza hatari ya kuzuka kwa vita vya dunia vipya vyenye athari kubwa sio tu kwa amani na usalama wa kimataifa bali pia nyanja nyingine zote za shughuli za binadamu." Pia Kim alitoa maoni kwamba mwaka 2025, mzozo wa Ukraine utasalia kuwa moja ya "mhimili mkuu wa hali ya wasiwasi ya kimataifa," nyingine ikiwa hali katika Ukanda wa Gaza na Syria "ambayo imekuwa uwanja wa migogoro ya kijiografia na makabiliano ya kimataifa mwaka jana." Katika hatua nyingine Kim alisema Marekani na nchi za Magharibi zinaelezea mzozo wa Ukraine kwa kushindwa kuishinda Urusi kimkakati, kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un alisema, kama ilivyonukuliwa na Shirika la Habari la Korea (KCNA). Katika mkutano katika Wizara ya Ulinzi, kuadhimisha kumbukumbu ya miaka 77 ya Jeshi la Wananchi wa Korea, alidai kwamba Marekani imepofushwa na tamaa mbaya huku akiionyesha wasiwasi mkubwa juu ya tabia ya kutojali ya Marekani na kundi la Magharibi kwa makusudi kuendeleza vita vya muda mrefu kwa ndoto isiyoweza kutekelezwa ili kukabiliana na kurudi kwa kimkakati kwa Urusi," shirika la habari lilibainisha. Kim alidokeza kuwa Pyongyang imekuwa ikipinga kila mara "kitendo chochote cha kunyima haki ya kimataifa na kuvuruga amani na usalama duniani." Aliongeza kuwa nchi yake "itaunga mkono kila wakati na kuhimiza sababu ya haki ya jeshi la Urusi na watu kutetea uhuru wao, usalama na uadilifu wa eneo kwa kuzingatia ari ya mkataba juu ya ushirikiano wa kimkakati wa kina kati ya DPRK na Urusi." (Zungu)
    0 Comments ·0 Shares ·697 Views
  • Putin sasa anazunguka huku na kule akitafuta suluhu ya amani, lakini Ukraine naye amegoma kusalimu amri.

    Katika ramani ya dunia, mababe wawili wamebaki, Marekani na China.

    Marekani bado inatawala masoko ya dunia, ina silaha za kisasa, na inafanya kila kitu kuhakikisha inabaki juu.

    China inakuja kwa kasi, ikitumia siasa za uchumi badala ya vita. Wanajua kuwa kushinda vita vya sasa, sio kwa mabomu tu bali kwa pesa na teknolojia.

    Urusi? Imebanwa. Vita na Ukraine imeichosha. Mipango ya kupanua mipaka imekufa. Na sasa dunia inajiuliza Putin anaweza kushindwa?

    Hii dunia ina kanuni moja kubwa, Usimwamini mtu. Na hata kama ukimwamini mtu, basi huyo mtu awe wewe mwenyewe.

    Ukraine alifanya kosa ambalo sasa linamgharimu. Aliamini ahadi za mataifa makubwa bila kuhakikisha ana kinga yake mwenyewe. Akasahau kuwa siasa za dunia haziongozwi na ahadi, bali na nguvu.

    Hili liwe somo kwa kila taifa linalotegemea misaada kutoka nje. Leo wanakupenda, kesho wakishapata wanachotaka, wanakusahau.

    Na dunia ilivyo sasa, muda wowote inaweza kulipuka. Mataifa yanapimana nguvu, migogoro inaongezeka, na tunakaribia kuona enzi mpya ya vita vya madaraka kati ya Marekani na China.

    Ukraine, Anajifunza kwa uchungu kuwa historia haimsahau mjinga.
    Putin sasa anazunguka huku na kule akitafuta suluhu ya amani, lakini Ukraine naye amegoma kusalimu amri. Katika ramani ya dunia, mababe wawili wamebaki, Marekani na China. Marekani bado inatawala masoko ya dunia, ina silaha za kisasa, na inafanya kila kitu kuhakikisha inabaki juu. China inakuja kwa kasi, ikitumia siasa za uchumi badala ya vita. Wanajua kuwa kushinda vita vya sasa, sio kwa mabomu tu bali kwa pesa na teknolojia. Urusi? Imebanwa. Vita na Ukraine imeichosha. Mipango ya kupanua mipaka imekufa. Na sasa dunia inajiuliza Putin anaweza kushindwa? Hii dunia ina kanuni moja kubwa, Usimwamini mtu. Na hata kama ukimwamini mtu, basi huyo mtu awe wewe mwenyewe. Ukraine alifanya kosa ambalo sasa linamgharimu. Aliamini ahadi za mataifa makubwa bila kuhakikisha ana kinga yake mwenyewe. Akasahau kuwa siasa za dunia haziongozwi na ahadi, bali na nguvu. Hili liwe somo kwa kila taifa linalotegemea misaada kutoka nje. Leo wanakupenda, kesho wakishapata wanachotaka, wanakusahau. Na dunia ilivyo sasa, muda wowote inaweza kulipuka. Mataifa yanapimana nguvu, migogoro inaongezeka, na tunakaribia kuona enzi mpya ya vita vya madaraka kati ya Marekani na China. Ukraine, Anajifunza kwa uchungu kuwa historia haimsahau mjinga.
    Like
    1
    · 0 Comments ·0 Shares ·648 Views
  • Marekani, Alitoa msaada wa miezi mitatu tu, kisha akaanza kulegeza kamba. Kwa sasa, Marekani imechoshwa na vita vya Ukraine.

    Wameona haina faida ya kuendelea kutoa silaha zisizoleta matokeo ya haraka.

    Uingereza, Ipo kama haipo. Iliahidi mengi, lakini imetulia kimya huku Waukraine wakiteketea kwenye moto wa kivita.

    Ulaya, Inajifanya ina wasiwasi, lakini ukweli ni kwamba kila nchi inajitazama yenyewe kwanza.

    Ukraine yuko peke yake.

    Na hapa ndipo tujiulize. Je, kweli Ukraine aliangamiza kila kitu?

    Inawezekana hana mabomu ya nyuklia tena, lakini ana akili, ana wataalamu, ana formula za kuyatengeneza.

    Na kama historia ni mwalimu, basi ni suala la muda tu kabla ya Ukraine kuamua kuchukua mkondo mpya.
    Vita vya Ukraine vimekuwa mzigo mzito kwa Urusi. Jeshi lake limepoteza askari wengi, uchumi wake umebanwa, na nguvu yake ya kijeshi imetetereka.
    Marekani, Alitoa msaada wa miezi mitatu tu, kisha akaanza kulegeza kamba. Kwa sasa, Marekani imechoshwa na vita vya Ukraine. Wameona haina faida ya kuendelea kutoa silaha zisizoleta matokeo ya haraka. Uingereza, Ipo kama haipo. Iliahidi mengi, lakini imetulia kimya huku Waukraine wakiteketea kwenye moto wa kivita. Ulaya, Inajifanya ina wasiwasi, lakini ukweli ni kwamba kila nchi inajitazama yenyewe kwanza. Ukraine yuko peke yake. Na hapa ndipo tujiulize. Je, kweli Ukraine aliangamiza kila kitu? Inawezekana hana mabomu ya nyuklia tena, lakini ana akili, ana wataalamu, ana formula za kuyatengeneza. Na kama historia ni mwalimu, basi ni suala la muda tu kabla ya Ukraine kuamua kuchukua mkondo mpya. Vita vya Ukraine vimekuwa mzigo mzito kwa Urusi. Jeshi lake limepoteza askari wengi, uchumi wake umebanwa, na nguvu yake ya kijeshi imetetereka.
    Like
    1
    · 0 Comments ·0 Shares ·529 Views
  • Muda ukasonga. Dunia ikabadilika. Mataifa yakaanza kuweka mbele maslahi yao, na Ukraine akajikuta akilia peke yake kwenye uwanja wa vita.

    Aliyeahidi kumlinda Urusi ndiye huyo anayemshambulia kwa mabomu, vifaru na ndege za kivita.

    Kwa miaka mingi, Vladimir Putin alikuwa anaangalia ramani ya dunia akijiuliza, "Mbona Crimea na Donbas zipo nje ya milki yangu?"

    Halafu, ghafla mwaka 2014, Urusi ikaamua kumng'ata Ukraine kwa mara ya kwanza.

    Crimea ikachukuliwa, na dunia ikakaa kimya. Hakukuwa na hatua kubwa zilizochukuliwa na Marekani wala Uingereza. Ukraine akaanza kuona dalili za usaliti.

    Mwaka 2022, Urusi ikarudi tena, safari hii kwa nguvu kubwa zaidi.
    Tishio la silaha za nyuklia lililomfanya Ukraine kuwa mbabe, halikuwepo tena. Hakuwa na kinga tena, alikuwa mtu mwepesi wa kushambuliwa.

    Na hapa ndipo Ukraine alipogundua kosa lake kubwa aliamini makaratasi kuliko mabavu.
    Muda ukasonga. Dunia ikabadilika. Mataifa yakaanza kuweka mbele maslahi yao, na Ukraine akajikuta akilia peke yake kwenye uwanja wa vita. Aliyeahidi kumlinda Urusi ndiye huyo anayemshambulia kwa mabomu, vifaru na ndege za kivita. Kwa miaka mingi, Vladimir Putin alikuwa anaangalia ramani ya dunia akijiuliza, "Mbona Crimea na Donbas zipo nje ya milki yangu?" Halafu, ghafla mwaka 2014, Urusi ikaamua kumng'ata Ukraine kwa mara ya kwanza. Crimea ikachukuliwa, na dunia ikakaa kimya. Hakukuwa na hatua kubwa zilizochukuliwa na Marekani wala Uingereza. Ukraine akaanza kuona dalili za usaliti. Mwaka 2022, Urusi ikarudi tena, safari hii kwa nguvu kubwa zaidi. Tishio la silaha za nyuklia lililomfanya Ukraine kuwa mbabe, halikuwepo tena. Hakuwa na kinga tena, alikuwa mtu mwepesi wa kushambuliwa. Na hapa ndipo Ukraine alipogundua kosa lake kubwa aliamini makaratasi kuliko mabavu.
    Like
    1
    · 0 Comments ·0 Shares ·593 Views
  • Miaka ya 90, Ukraine alikuwa mbabe sana. Taifa hili lilikuwa lina nguvu za kijeshi ambazo ziliwafanya majirani zake kusita hata kufikiria kulivamia.

    Sababu?

    Lilikuwa na zaidi ya mabomu 1,000 ya nyuklia. Haya si mabomu ya kawaida, ni silaha za maangamizi ambazo zingeweza kuifuta dunia katika sekunde chache.

    Lakini kama ilivyo kwa kila hadithi ya usaliti, Ukraine alifanya kosa moja kubwa, aliamini watu wengine badala ya kujilinda mwenyewe.

    Marekani, Urusi na Uingereza walimfuata kwa heshima kubwa, wakampigia magoti na kumwambia.

    "Tafadhali, haribu mabomu yako. Dunia itakuwa mahali salama zaidi, na sisi tutakuwa walinzi wako. Hatutakuacha."
    Ukraine akakubali. Akayaangamiza mabomu yake yote ya nyuklia. Mikataba iliwekwa. Ahadi zikaandikwa kwa kalamu na kutiwa muhuri.

    Ukraine akaamini kabisa kuwa usalama wake hauwezi kutikiswa tena.
    Miaka ya 90, Ukraine alikuwa mbabe sana. Taifa hili lilikuwa lina nguvu za kijeshi ambazo ziliwafanya majirani zake kusita hata kufikiria kulivamia. Sababu? Lilikuwa na zaidi ya mabomu 1,000 ya nyuklia. Haya si mabomu ya kawaida, ni silaha za maangamizi ambazo zingeweza kuifuta dunia katika sekunde chache. Lakini kama ilivyo kwa kila hadithi ya usaliti, Ukraine alifanya kosa moja kubwa, aliamini watu wengine badala ya kujilinda mwenyewe. Marekani, Urusi na Uingereza walimfuata kwa heshima kubwa, wakampigia magoti na kumwambia. "Tafadhali, haribu mabomu yako. Dunia itakuwa mahali salama zaidi, na sisi tutakuwa walinzi wako. Hatutakuacha." Ukraine akakubali. Akayaangamiza mabomu yake yote ya nyuklia. Mikataba iliwekwa. Ahadi zikaandikwa kwa kalamu na kutiwa muhuri. Ukraine akaamini kabisa kuwa usalama wake hauwezi kutikiswa tena.
    Like
    1
    · 0 Comments ·0 Shares ·398 Views
  • Rais Donald Trump wa Marekani amemuandikia barua ya mwaliko kwenye Ikulu ya Marekani White House Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu akimuomba aende wiki ijayo wakajadili hali ya Mashariki ya Kati na maslahi yao ya pamoja katika ukanda huo (mgogoro wa Palestina na Israel).

    Kwa mwaliko huo, Benjamin Netanyahu atakuwa kiongozi Mkuu wa kwanza wa nje kufanya ziara rasmi Marekani baada ya Trump kushinda tena Urais wa Taifa hilo. Ikumbukwe maandalizi ya mkutano wa Trump na Putin pia yanaendelea ili kumaliza vita vya Ukraine.

    Rais Donald Trump wa Marekani amemuandikia barua ya mwaliko kwenye Ikulu ya Marekani White House Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu akimuomba aende wiki ijayo wakajadili hali ya Mashariki ya Kati na maslahi yao ya pamoja katika ukanda huo (mgogoro wa Palestina na Israel). Kwa mwaliko huo, Benjamin Netanyahu atakuwa kiongozi Mkuu wa kwanza wa nje kufanya ziara rasmi Marekani baada ya Trump kushinda tena Urais wa Taifa hilo. Ikumbukwe maandalizi ya mkutano wa Trump na Putin pia yanaendelea ili kumaliza vita vya Ukraine.
    Like
    1
    · 0 Comments ·0 Shares ·352 Views
  • Rais Donald Trump wa Marekani amemuandikia barua ya mwaliko kwenye Ikulu ya Marekani White House Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu akimuomba aende wiki ijayo wakajadili hali ya Mashariki ya Kati na maslahi yao ya pamoja katika ukanda huo (mgogoro wa Palestina na Israel).

    Kwa mwaliko huo, Benjamin Netanyahu atakuwa kiongozi Mkuu wa kwanza wa nje kufanya ziara rasmi Marekani baada ya Trump kushinda tena Urais wa Taifa hilo. Ikumbukwe maandalizi ya mkutano wa Trump na Putin pia yanaendelea ili kumaliza vita vya Ukraine.

    Rais Donald Trump wa Marekani amemuandikia barua ya mwaliko kwenye Ikulu ya Marekani White House Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu akimuomba aende wiki ijayo wakajadili hali ya Mashariki ya Kati na maslahi yao ya pamoja katika ukanda huo (mgogoro wa Palestina na Israel). Kwa mwaliko huo, Benjamin Netanyahu atakuwa kiongozi Mkuu wa kwanza wa nje kufanya ziara rasmi Marekani baada ya Trump kushinda tena Urais wa Taifa hilo. Ikumbukwe maandalizi ya mkutano wa Trump na Putin pia yanaendelea ili kumaliza vita vya Ukraine.
    Like
    3
    · 1 Comments ·0 Shares ·310 Views
  • Uingereza na Ukraine zimesaini makubaliano ya miaka 100, huku Uingereza ikiahidi kuipa mkopo kwa ajili ya ununuzi wa silaha na vifaa vya kijeshi vya dola bilioni 2.6 [trilioni 6.5] kwa ajili ya kupambana na uvamizi wa Urusi.

    Waziri Mkuu wa Uingereza, Keir Starmer amesema mkopo huo hautalipwa na Ukraine bali kutoka kwenye mali za Urusi zilizozuiliwa.
    Uingereza na Ukraine zimesaini makubaliano ya miaka 100, huku Uingereza ikiahidi kuipa mkopo kwa ajili ya ununuzi wa silaha na vifaa vya kijeshi vya dola bilioni 2.6 [trilioni 6.5] kwa ajili ya kupambana na uvamizi wa Urusi. Waziri Mkuu wa Uingereza, Keir Starmer amesema mkopo huo hautalipwa na Ukraine bali kutoka kwenye mali za Urusi zilizozuiliwa.
    Like
    1
    · 0 Comments ·0 Shares ·416 Views
  • SAKATA LA JASUSI SERGEI SKRIPAL NA MWANAE NI UTEKELEZAJI WA OPERATION SARLISBURY ILIYOTEKELEZWA NA RUSSIA, KIMSIMGI NI VITA KATI YA URUSI NA NATO KUJIBU MAPIGO YA UCHAGUZI WA MAREKANI MWAKA 2016.

    Na mhariri wako Comred Mbwana Allyamtu

    Sakata la jaribio la mauaji ya jasusi au mpelelezi, ndumilakuwili wa Urusi na Uingereza, Sergei Skripal na binti yake Yulia katika kitongoji cha Salisbury jijini London nchini Uingereza linachukua sura mpya kila siku.

    Wawili hao walipatikana wakiwa hawajitambui katika eneo la maduka liitwalo Maltings mwanzoni mwa Machi.

    Taarifa kutoka kwa polisi wa Uingereza ambao hushughulikia matukio ya kigaidi wanaamini kuwa jasusi huyo na mwanaye, walivuta hewa iliyokuwa na kemikali yenye sumu iitwayo novichok.

    Kemikali hii hushambulia mfumo wa mfahamu na inasemekana ilitengenezwa katika maabara moja huko Urusi na ilitumika wakati wa Vita vya Pili vya Dunia mwaka 1935 hadi 1945. Kemikali hiyo iliachwa mlangoni mwa nyumba ambayo amekuwa akiishi jasusi huyo na mwanaye katika eneo hilo la Salisbury.

    Mashirika makubwa ya habari nchini Uingereza yameipa umuhimu habari hii ambapo Machi 30, yalitangaza kuwa binti wa Skripal, Yulia hakuwa katika hali tete kiafya.

    Kufuatia tukio hilo Serikali ya Uingereza chini ya Waziri Mkuu, Theresa May iliitupia lawama Serikali ya Urusi kwa kuhusika na uovu huo na ili kuonyesha kuwa imechukia iliamua kuwafukuza wanadiplomasia wa Urusi wapatao 23.

    Urusi imekanusha kuhusika na uovu huo na ikaahidi kuwa kwa kila hukumu itakayotolewa nayo itajibu kwa ukubwa huohuo au zaidi ya hapo, na ikajibu kwa kutoa hukumu ya kisasi kwa kuwafukuza wanadiplomasia 23 wa Uingereza na kufunga kituo cha Lugha na Utamaduni cha Uingereza, British Council na imeitaka Uingereza kuwaondoa wanadiplomasia wake wengine wapatao 50 katika kipindi cha mwezi mmoja.
    Ili kuonyesha mshikamano na Uingereza nchi nyingine za Ulaya Magharibi na Australia zimewafukuza wanadiplomasia wa Urusi wanaofikia 150 huku Marekani ikiongoza kwa kufunga ubalozi mdogo wa Urusi katika Jiji la Seattle na kuwafukuza wanadiplomasia 60 kutoka nchi hiyo.

    Urusi nayo haikubaki kimya, Waziri wa Mambo ya Nje, Sergei Lavrov ametangaza kuwafukuza wanadiplomasia 60 wa Marekani na vilevile kufunga ubalozi wa Marekani katika mji wa Saint Petersburg na kuahidi kuwa kila nchi iliyohusika na kufukuza wanadiplomasia wake itaadhibiwa vilivyo.

    Kwa ujumla nchi karibu 23 na Umoja wa Kujihami wa nchi za Ulaya Magharibi (Nato) kote ulimwenguni zimeonyesha kukerwa na vitendo vya Urusi kwa kuingilia mambo ya ndani ya nchi tofautitofauti, kama vile kuvamia Ukraine na kulichukua jimbo la Krimea, kuitungua ndege ya Malaysia na kuingilia uchaguzi Mkuu wa Marekani mwaka 2016.
    Siyo mara ya kwanza nchi hizi kuingia katika mzozo wa kidiplomasia kwani mwaka 1986 Ronald Reagan aliyekuwa Rais wa Marekani, aliamuru wanadiplomasia 80 wa Shirikisho la Urusi (USSR) wafukuzwe nchini humo na mwaka 2016, Rais Barak Obama aliwatimua wanadiplomasia 35 kutoka nchi hiyo kwa tuhuma za kudukua kompyuta za chama cha Democratic kwa nia ya kumhujumu mgombea wake wa Rais, Hillary Clinton.

    Mwaka 2006 Skripal alihukumiwa kifungo cha miaka 13, nchini Urusi katika kesi ambayo iliendeshwa katika mahakama ya siri, alipewa haki ya ukimbizi na ukazi nchini Uingereza mwaka 2010 baada ya makubaliano ya kubadilishana wafungwa katika mtindo ambao ulitumika enzi za vita baridi kuhusiana na shughuli za kijasusi.

    Kulingana na nyaraka za kumbukumbu ambazo vyombo vya habari vya Uingereza vilizipata kutoka makumbusho ya taifa ya Uingereza mwaka 2015, zinaonyesha kuwa Serikali ya Urusi imekuwa ikiichunguza Uingereza muda mrefu lakini kisa kinachojulikana sana ni kile kilichopewa jina la Cambridge Four, ambapo kitengo cha ujasusi cha shirikisho la Urusi (USSR), KGB, katika miaka ya 1930 kabla ya vita vya pili vya dunia kiligundua kuwa Serikali ya Uingereza ilikuwa ikitumia Chuo Kikuu cha Cambridge kama sehemu maalumu ya kuwapata majasusi wachanga wakiwa masomoni. KGB waliwafuata wanafunzi wanne wa wakati huo ambao ni Anthony Blunt, Donald Duart Maclean, Kim Phillby na Guy Burgess.
    Wasomi hao ambao kwa bahati nzuri kwao KGB walipomaliza masomo yao waliingia kufanya kazi katika Mashirika ya Ujasusi ya Uingereza, MI5 na MI6, na wakawa ni majasusi ndumilakuwili.

    Walifanya kazi yao hadi mwaka 1964 ambapo Anthony Blunt ambaye alikuwa akifanya kazi katika Shirika la Ujasusi wa ndani, MI5, alikiri kuwa jasusi ndumilakuwili ili asishtakiwe na habari hiyo ilikuja kutolewa na aliyekuwa Waziri Mkuu wa Uingereza wakati huo, Magreth Thatcher alipokuwa akihutubia Bunge mwaka 1979. Donald Duart Maclean, Kim Phillby na Guy Burgess wao walitimkia Urusi na Serikali ya Uingereza ikawa imekubali yaiishe.

    Kwa hiyo Urusi imekuwa hailali usingizi wakati wote wa miaka ya vita baridi kati ya nchi za Ulaya Mashariki na Magharibi miaka ya 1945 hadi mwanzoni mwa miaka ya 1990, imekuwa ikiingiza wapelelezi wake maeneo mbalimbali katika nchi hizo ili kupata habari nyeti kuhusiana na masuala mbalimbali katika nyanja za uchumi, biashara hasa ya silaha na teknolojia yake na hivi karibuni kuingilia mambo ya siasa za uchaguzi huko Marekani.
    Ukiangalia kisa cha safari hii hakina tofauti sana kile alichofanyiwa Jasusi mwingine wa Urusi Novemba 2006, Alexander Litvinenko ambaye aliwekewa kemikali iitwayo Polonium 210 katika kikombe cha chai katika mgahawa mmoja jijini London.

    Litvinenko alitoroka Urusi baada ya kutofautiana na wenzake katika shirika la kijasusi la nchi hiyo FSB, ambapo aliutuhumu uongozi wa juu wa nchi hiyo kuigeuza nchi hiyo kuwa Taifa la kimafia. akiwa nchini Uingereza, alifanya kazi kama mwandishi wa habari, vitabu na mshauri wa mambo ya usalama.
    Akiwa Uingereza aliandika vitabu viwili, Blowing up Russia: Terror from within na Lubyanka Criminal Group ambapo aliituhumu idara hiyo ya kijasusi kwa vitendo vya mauaji na matumizi ya mabomu na mauaji ya mwandishi wa habari, Anna Politkovskaya kwa amri kutoka kwa Rais wa nchi hiyo, Vladimir Putin.

    Litvinenko akiwa mahututi kitandani hospitalini jijini London aliwatamkia ndugu zake kuwa alikuwa na uhakika kuwa Rais wa Urusi, Vladimir Putin ndiye aliyeamuru auawe.
    Serikali ya Uingereza ya wakati huo chini ya Waziri Mkuu, Tony Blair ilifanya upelelezi na kugundua kuwa jasusi huyo siku chache kabla ya kupata mkasa huo alikuwa ametembelewa na jasusi mwingine mstaafu wa FSB ambaye kwa sasa ni mfanyabiashara, Andrey Lugovoy.
    Serikali ya Uingereza iliitaka Urusi imsalimishe kwake ili afanyiwe mahojiano lakini Urusi ilikataa kwa maelezo kuwa Katiba ya nchi hiyo inakataza raia wake kupelekwa nchi nyingine kufanyiwa mashtaka ya jinai. Uhusiano kati ya nchi hizo mbili ulififia kwa muda.

    Serikali ya Uingereza kwa matukio yote haya imekuwa ikiituhumu serikali ya Urusi kwa kile inachoeleza kuwa kemikali hizo haziwezi kuwa mikononi mwa mtu binafsi bila kuwa na kibari cha mamlaka za juu za nchi hiyo.

    Wakati Kim Phillby alipokimbilia Urusi baada ya kushtukia kuwa wenzake walikuwa wanaelekea kumgundua kuwa ni ndumilakuwili, Ofisa mmoja wa ngazi ya juu ndani ya KGB wakati huo alimsifu kuwa alikuwa jasusi mwenye thamani kubwa wa karne iliyopita.

    Urusi imekuwa ikitoa ulinzi wa kiwango cha juu kwa majasusi ndumilakuwili ambao wamefanikiwa kuingia nchini humo baada ya mambo kwenda kombo huko kwao.

    Marekani nayo haikuwahi kupona kwa taasisi zake za kijasusi kuingiliwa na wenzao wa Urusi. Mwaka 2001 Shirika la Ujasusi wa Ndani, FBI, lilimkamata Robert Hanssen ambaye alikuwa mtumishi wake kwa kupeleka taarifa za siri za nchi hiyo kwa Urusi tangu mwaka 1979 kwa kulipwa fedha na almasi.

    Kwa sehemu kubwa shughuli za ujasusi zimekuwa zikifanywa kwa njia ya teknolojia (Artificial Intelligence) ambapo mitambo ya kompyuta na setelaiti na kamera zenye nguvu za kunasa picha hutumika na pale ambapo haiwezekani, inabidi kutumia binadamu (human intelligence) ili kupata habari ambazo ni siri na mataifa karibu yote duniani yameuweka ujasusi kama ni kosa la uhaini kwa yeyote atakayejihusisha nao.
    SAKATA LA JASUSI SERGEI SKRIPAL NA MWANAE NI UTEKELEZAJI WA OPERATION SARLISBURY ILIYOTEKELEZWA NA RUSSIA, KIMSIMGI NI VITA KATI YA URUSI NA NATO KUJIBU MAPIGO YA UCHAGUZI WA MAREKANI MWAKA 2016. Na mhariri wako Comred Mbwana Allyamtu Sakata la jaribio la mauaji ya jasusi au mpelelezi, ndumilakuwili wa Urusi na Uingereza, Sergei Skripal na binti yake Yulia katika kitongoji cha Salisbury jijini London nchini Uingereza linachukua sura mpya kila siku. Wawili hao walipatikana wakiwa hawajitambui katika eneo la maduka liitwalo Maltings mwanzoni mwa Machi. Taarifa kutoka kwa polisi wa Uingereza ambao hushughulikia matukio ya kigaidi wanaamini kuwa jasusi huyo na mwanaye, walivuta hewa iliyokuwa na kemikali yenye sumu iitwayo novichok. Kemikali hii hushambulia mfumo wa mfahamu na inasemekana ilitengenezwa katika maabara moja huko Urusi na ilitumika wakati wa Vita vya Pili vya Dunia mwaka 1935 hadi 1945. Kemikali hiyo iliachwa mlangoni mwa nyumba ambayo amekuwa akiishi jasusi huyo na mwanaye katika eneo hilo la Salisbury. Mashirika makubwa ya habari nchini Uingereza yameipa umuhimu habari hii ambapo Machi 30, yalitangaza kuwa binti wa Skripal, Yulia hakuwa katika hali tete kiafya. Kufuatia tukio hilo Serikali ya Uingereza chini ya Waziri Mkuu, Theresa May iliitupia lawama Serikali ya Urusi kwa kuhusika na uovu huo na ili kuonyesha kuwa imechukia iliamua kuwafukuza wanadiplomasia wa Urusi wapatao 23. Urusi imekanusha kuhusika na uovu huo na ikaahidi kuwa kwa kila hukumu itakayotolewa nayo itajibu kwa ukubwa huohuo au zaidi ya hapo, na ikajibu kwa kutoa hukumu ya kisasi kwa kuwafukuza wanadiplomasia 23 wa Uingereza na kufunga kituo cha Lugha na Utamaduni cha Uingereza, British Council na imeitaka Uingereza kuwaondoa wanadiplomasia wake wengine wapatao 50 katika kipindi cha mwezi mmoja. Ili kuonyesha mshikamano na Uingereza nchi nyingine za Ulaya Magharibi na Australia zimewafukuza wanadiplomasia wa Urusi wanaofikia 150 huku Marekani ikiongoza kwa kufunga ubalozi mdogo wa Urusi katika Jiji la Seattle na kuwafukuza wanadiplomasia 60 kutoka nchi hiyo. Urusi nayo haikubaki kimya, Waziri wa Mambo ya Nje, Sergei Lavrov ametangaza kuwafukuza wanadiplomasia 60 wa Marekani na vilevile kufunga ubalozi wa Marekani katika mji wa Saint Petersburg na kuahidi kuwa kila nchi iliyohusika na kufukuza wanadiplomasia wake itaadhibiwa vilivyo. Kwa ujumla nchi karibu 23 na Umoja wa Kujihami wa nchi za Ulaya Magharibi (Nato) kote ulimwenguni zimeonyesha kukerwa na vitendo vya Urusi kwa kuingilia mambo ya ndani ya nchi tofautitofauti, kama vile kuvamia Ukraine na kulichukua jimbo la Krimea, kuitungua ndege ya Malaysia na kuingilia uchaguzi Mkuu wa Marekani mwaka 2016. Siyo mara ya kwanza nchi hizi kuingia katika mzozo wa kidiplomasia kwani mwaka 1986 Ronald Reagan aliyekuwa Rais wa Marekani, aliamuru wanadiplomasia 80 wa Shirikisho la Urusi (USSR) wafukuzwe nchini humo na mwaka 2016, Rais Barak Obama aliwatimua wanadiplomasia 35 kutoka nchi hiyo kwa tuhuma za kudukua kompyuta za chama cha Democratic kwa nia ya kumhujumu mgombea wake wa Rais, Hillary Clinton. Mwaka 2006 Skripal alihukumiwa kifungo cha miaka 13, nchini Urusi katika kesi ambayo iliendeshwa katika mahakama ya siri, alipewa haki ya ukimbizi na ukazi nchini Uingereza mwaka 2010 baada ya makubaliano ya kubadilishana wafungwa katika mtindo ambao ulitumika enzi za vita baridi kuhusiana na shughuli za kijasusi. Kulingana na nyaraka za kumbukumbu ambazo vyombo vya habari vya Uingereza vilizipata kutoka makumbusho ya taifa ya Uingereza mwaka 2015, zinaonyesha kuwa Serikali ya Urusi imekuwa ikiichunguza Uingereza muda mrefu lakini kisa kinachojulikana sana ni kile kilichopewa jina la Cambridge Four, ambapo kitengo cha ujasusi cha shirikisho la Urusi (USSR), KGB, katika miaka ya 1930 kabla ya vita vya pili vya dunia kiligundua kuwa Serikali ya Uingereza ilikuwa ikitumia Chuo Kikuu cha Cambridge kama sehemu maalumu ya kuwapata majasusi wachanga wakiwa masomoni. KGB waliwafuata wanafunzi wanne wa wakati huo ambao ni Anthony Blunt, Donald Duart Maclean, Kim Phillby na Guy Burgess. Wasomi hao ambao kwa bahati nzuri kwao KGB walipomaliza masomo yao waliingia kufanya kazi katika Mashirika ya Ujasusi ya Uingereza, MI5 na MI6, na wakawa ni majasusi ndumilakuwili. Walifanya kazi yao hadi mwaka 1964 ambapo Anthony Blunt ambaye alikuwa akifanya kazi katika Shirika la Ujasusi wa ndani, MI5, alikiri kuwa jasusi ndumilakuwili ili asishtakiwe na habari hiyo ilikuja kutolewa na aliyekuwa Waziri Mkuu wa Uingereza wakati huo, Magreth Thatcher alipokuwa akihutubia Bunge mwaka 1979. Donald Duart Maclean, Kim Phillby na Guy Burgess wao walitimkia Urusi na Serikali ya Uingereza ikawa imekubali yaiishe. Kwa hiyo Urusi imekuwa hailali usingizi wakati wote wa miaka ya vita baridi kati ya nchi za Ulaya Mashariki na Magharibi miaka ya 1945 hadi mwanzoni mwa miaka ya 1990, imekuwa ikiingiza wapelelezi wake maeneo mbalimbali katika nchi hizo ili kupata habari nyeti kuhusiana na masuala mbalimbali katika nyanja za uchumi, biashara hasa ya silaha na teknolojia yake na hivi karibuni kuingilia mambo ya siasa za uchaguzi huko Marekani. Ukiangalia kisa cha safari hii hakina tofauti sana kile alichofanyiwa Jasusi mwingine wa Urusi Novemba 2006, Alexander Litvinenko ambaye aliwekewa kemikali iitwayo Polonium 210 katika kikombe cha chai katika mgahawa mmoja jijini London. Litvinenko alitoroka Urusi baada ya kutofautiana na wenzake katika shirika la kijasusi la nchi hiyo FSB, ambapo aliutuhumu uongozi wa juu wa nchi hiyo kuigeuza nchi hiyo kuwa Taifa la kimafia. akiwa nchini Uingereza, alifanya kazi kama mwandishi wa habari, vitabu na mshauri wa mambo ya usalama. Akiwa Uingereza aliandika vitabu viwili, Blowing up Russia: Terror from within na Lubyanka Criminal Group ambapo aliituhumu idara hiyo ya kijasusi kwa vitendo vya mauaji na matumizi ya mabomu na mauaji ya mwandishi wa habari, Anna Politkovskaya kwa amri kutoka kwa Rais wa nchi hiyo, Vladimir Putin. Litvinenko akiwa mahututi kitandani hospitalini jijini London aliwatamkia ndugu zake kuwa alikuwa na uhakika kuwa Rais wa Urusi, Vladimir Putin ndiye aliyeamuru auawe. Serikali ya Uingereza ya wakati huo chini ya Waziri Mkuu, Tony Blair ilifanya upelelezi na kugundua kuwa jasusi huyo siku chache kabla ya kupata mkasa huo alikuwa ametembelewa na jasusi mwingine mstaafu wa FSB ambaye kwa sasa ni mfanyabiashara, Andrey Lugovoy. Serikali ya Uingereza iliitaka Urusi imsalimishe kwake ili afanyiwe mahojiano lakini Urusi ilikataa kwa maelezo kuwa Katiba ya nchi hiyo inakataza raia wake kupelekwa nchi nyingine kufanyiwa mashtaka ya jinai. Uhusiano kati ya nchi hizo mbili ulififia kwa muda. Serikali ya Uingereza kwa matukio yote haya imekuwa ikiituhumu serikali ya Urusi kwa kile inachoeleza kuwa kemikali hizo haziwezi kuwa mikononi mwa mtu binafsi bila kuwa na kibari cha mamlaka za juu za nchi hiyo. Wakati Kim Phillby alipokimbilia Urusi baada ya kushtukia kuwa wenzake walikuwa wanaelekea kumgundua kuwa ni ndumilakuwili, Ofisa mmoja wa ngazi ya juu ndani ya KGB wakati huo alimsifu kuwa alikuwa jasusi mwenye thamani kubwa wa karne iliyopita. Urusi imekuwa ikitoa ulinzi wa kiwango cha juu kwa majasusi ndumilakuwili ambao wamefanikiwa kuingia nchini humo baada ya mambo kwenda kombo huko kwao. Marekani nayo haikuwahi kupona kwa taasisi zake za kijasusi kuingiliwa na wenzao wa Urusi. Mwaka 2001 Shirika la Ujasusi wa Ndani, FBI, lilimkamata Robert Hanssen ambaye alikuwa mtumishi wake kwa kupeleka taarifa za siri za nchi hiyo kwa Urusi tangu mwaka 1979 kwa kulipwa fedha na almasi. Kwa sehemu kubwa shughuli za ujasusi zimekuwa zikifanywa kwa njia ya teknolojia (Artificial Intelligence) ambapo mitambo ya kompyuta na setelaiti na kamera zenye nguvu za kunasa picha hutumika na pale ambapo haiwezekani, inabidi kutumia binadamu (human intelligence) ili kupata habari ambazo ni siri na mataifa karibu yote duniani yameuweka ujasusi kama ni kosa la uhaini kwa yeyote atakayejihusisha nao.
    0 Comments ·0 Shares ·2K Views
  • Ufaransa itaipatia Ukraine msaada wa kijeshi katika wiki zijazo, ikiwa ni pamoja na makombora ya Mistral na Aster, ambayo kwa kiasi kikubwa yanafadhiliwa na mapato kutoka kwa mali iliyoganda ya Urusi, Waziri wa Ulinzi wa Ufaransa Sebastien Lecornu anasema. Ufaransa pia iko tayari kuendelea kutoa mafunzo kwa wanajeshi wa Ukraine


    #everyone
    #ukraine
    #urusi
    Ufaransa itaipatia Ukraine msaada wa kijeshi katika wiki zijazo, ikiwa ni pamoja na makombora ya Mistral na Aster, ambayo kwa kiasi kikubwa yanafadhiliwa na mapato kutoka kwa mali iliyoganda ya Urusi, Waziri wa Ulinzi wa Ufaransa Sebastien Lecornu anasema. Ufaransa pia iko tayari kuendelea kutoa mafunzo kwa wanajeshi wa Ukraine #everyone #ukraine #urusi
    Love
    1
    · 0 Comments ·0 Shares ·377 Views
  • Pima .uzimwe fasta..
    .me ni mafia .usi-complain..
    Vina bado staza, kama russia.. Na ukraine..
    Unapowaza linli Utaheshimika..kwanza Anza kujieshimu..
    Af Mahala bangi inatumika.. We tumia elimu..
    kuna tofauti ndogo sana kati ya 'kujua' na kuelewa'..
    Ila kunatofauti kubwa sana kati ya 'mjuaji' na 'mwelewa..
    Sikuiz unaweza ukakaa.. Uchi..
    ukitazama kioo cha jamii unajiona umevaa..suti..
    Ufundi..unatengwa..
    Upuuzi..unapendwa..
    Unaweza ukageuza hatua na ukajikuta haurudi..unaenda..
    Naifanya kama normal..
    Naifanya kama somo..
    Ila Ukiendelea kuiwaza itaonekana. Kama onyo..
    Real Hip hop ndio ..shule ..adimu..
    Kama umeshndikana kwa mamako
    .njoo upate ..bure..hii elimu..
    Ule muda, mnajichubua et mnaonekane mna-swaga..
    Ndo muda ambao washua, tunaona kama mna-sagwa..
    Coke u'r mind.
    twende sawa, apa ni facts tu na-prove..
    Bongo bongo sioni power kwny hiyo New school..
    mkitoa ngoma zenu zinakaa kaa basi..
    In 24 hours zinapotea kama status..
    Lengo letu sio kuish milele..
    Bali nikuacha vitu ambavyo vitaish milele..
    Pima .uzimwe fasta.. .me ni mafia .usi-complain.. Vina bado staza, kama russia.. Na ukraine.. Unapowaza linli Utaheshimika..kwanza Anza kujieshimu.. Af Mahala bangi inatumika.. We tumia elimu.. kuna tofauti ndogo sana kati ya 'kujua' na kuelewa'.. Ila kunatofauti kubwa sana kati ya 'mjuaji' na 'mwelewa.. Sikuiz unaweza ukakaa.. Uchi.. ukitazama kioo cha jamii unajiona umevaa..suti.. Ufundi..unatengwa.. Upuuzi..unapendwa.. Unaweza ukageuza hatua na ukajikuta haurudi..unaenda.. Naifanya kama normal.. Naifanya kama somo.. Ila Ukiendelea kuiwaza itaonekana. Kama onyo.. Real Hip hop ndio ..shule ..adimu.. Kama umeshndikana kwa mamako .njoo upate ..bure..hii elimu.. Ule muda, mnajichubua et mnaonekane mna-swaga.. Ndo muda ambao washua, tunaona kama mna-sagwa.. Coke u'r mind. twende sawa, apa ni facts tu na-prove.. Bongo bongo sioni power kwny hiyo New school.. mkitoa ngoma zenu zinakaa kaa basi.. In 24 hours zinapotea kama status.. Lengo letu sio kuish milele.. Bali nikuacha vitu ambavyo vitaish milele..
    Like
    Love
    4
    · 1 Comments ·0 Shares ·651 Views
  • Kipindi mjuzi...nachanganya shisha-coffeine...
    Ndo kipindi mrusi...anapigana vita-ukraine...
    Kipindi kigumu...hali taight haiko fine...
    Ni chagundu...ma dealer tuna drug cocaine...
    Tunapigwa chain.. isitumike...hasara...
    nopain... iruhusiwe.. . maana Haina madhara...
    Kipindi msaka-tonge...bila kula Nalala...
    Ndo kipindi boy-konde...anakula Kajala...
    Muun natoroka pindi...la mathe...
    Ndichi tuwashe...Zigi ipakwe.. mate iwake..
    bila makeke...
    Kipindi unalia lia... et baby...usiniache...
    Ndo kipindi mchepuko dia..aje geto nimchape...
    Kipindi cha babu...Hadithi vitabu...miksa kiko pushabu...
    Kipindi cha magu..
    Kumbukumbu ghazabu leo tunaishi kwa tabu...
    Bado hatuna majibu...
    blue anaimba mapozi..
    Ndo kipindi ambacho jaydee analia machozi...
    Trend hakuna kulala...
    Ndo kipindi Zila anotoka na rakunchupa salasala...
    Kipindi mjuzi...nachanganya shisha-coffeine... Ndo kipindi mrusi...anapigana vita-ukraine... Kipindi kigumu...hali taight haiko fine... Ni chagundu...ma dealer tuna drug cocaine... Tunapigwa chain.. isitumike...hasara... nopain... iruhusiwe.. . maana Haina madhara... Kipindi msaka-tonge...bila kula Nalala... Ndo kipindi boy-konde...anakula Kajala... Muun natoroka pindi...la mathe... Ndichi tuwashe...Zigi ipakwe.. mate iwake.. bila makeke... Kipindi unalia lia... et baby...usiniache... Ndo kipindi mchepuko dia..aje geto nimchape... Kipindi cha babu...Hadithi vitabu...miksa kiko pushabu... Kipindi cha magu.. Kumbukumbu ghazabu leo tunaishi kwa tabu... Bado hatuna majibu... blue anaimba mapozi.. Ndo kipindi ambacho jaydee analia machozi... Trend hakuna kulala... Ndo kipindi Zila anotoka na rakunchupa salasala...
    Like
    Love
    2
    · 0 Comments ·0 Shares ·669 Views
More Results