Papillon Tz
Actualizaciones Recientes
  • Nchi ya Kenya yakemea vitendo vya kuwapeleka Vijana wake kwenye vita Nchini Ukraine.

    Serikali ya Kenya imekemea vikali vitendo vya baadhi ya Mawakala wanaodanganya Vijana kwa ahadi za ajira, kisha kuwapeleka moja kwa moja kwenye vita vinavyoendelea nchini Ukraine.

    Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya, Musalia Mudavadi, amesema: “Tunatarajia kufanya ziara rasmi mjini Moscow kwa mazungumzo na Serikali ya Urusi, lengo likiwa kusitisha kabisa matumizi ya raia wa Kenya katika mapambano haya.”

    Mudavadi alibainisha kuwa tayari Wakenya kadhaa wamefariki dunia, huku wengine wakijeruhiwa vibaya baada ya kudanganywa kuingia mikataba ya kijeshi. Amesema: “Hatukubali upotevu wa maisha ya raia wetu. Hatua za kudumu lazima zichukuliwe.”

    Serikali ya Kenya imelaumu Mawakala wa ajira wanaoshawishi vijana kwa ahadi za mishahara mikubwa, kisha kuwapeleka mstari wa mbele vitani. Ripoti ya hivi karibuni ya shirika la habari la Ufaransa, Agence France-Presse, imethibitisha kuwepo kwa mtandao wa udanganyifu unaowaingiza vijana wasiokuwa na historia ya kijeshi kusaini mikataba na Jeshi la Urusi, kisha kupelekwa haraka kwenye Uwanja wa mapambano.

    Mudavadi amesisitiza kuwa Kenya itafuatilia pia suala la kuachiliwa kwa Wakenya waliokamatwa kama wafungwa wa kivita nchini Ukraine. Amesema hatua hizi ni muhimu ili kulinda maisha ya Raia wake.

    Toa maoni yako
    #Habari
    #Russia #Ukraine #MusaliaMudavadi #Moscow #BreakingNews #WorldNews #VitaUkraine #KenyaAbroad #HumanRights #AfricaNews
    0 Commentarios 0 Acciones 8 Views
  • Hii hapa orodha ya Wachezaji 20 Wakongwe zaidi kuwahi kushinda Kombe la Dunia la FIFA, kulingana na takwimu za FIFA:

    1. Dino Zoff – Miaka 40 na siku 133

    2. Nilton Santos – Miaka 37 na siku 32

    3. Angelo Peruzzi – Miaka 36 na siku 143

    4. Franco Armani – Miaka 36 na siku 63

    5. Miroslav Klose – Miaka 36 na siku 34

    6. Gilmar Rinaldi – Miaka 35 na siku 185

    7. Lionel Messi – Miaka 35 na siku 177

    8. Toni Turek – Miaka 35 na siku 167

    9. Bernard Lama – Miaka 35 na siku 96

    10. Nicolás Otamendi – Miaka 34 na siku 309

    11. Ángel Di María – Miaka 34 na siku 307

    12. Alejandro Gómez – Miaka 34 na siku 306

    13. Castilho – Miaka 34 na siku 202

    14. Paul Mebus – Miaka 34 na siku 25

    15. Roman Weidenfeller – Miaka 33 na siku 341

    16. Didi – Miaka 33 na siku 252

    17. Fritz Walter – Miaka 33 na siku 246

    18. Paul Steiner – Miaka 33 na siku 166

    19. Franco Causio – Miaka 33 na siku 160

    20. Djalma Santos – Miaka 33 na siku 110

    #Sports
    0 Commentarios 0 Acciones 10 Views
  • Trump aonya kuhusu makubaliano ya biashara kati ya China na Canada.

    Rais wa Marekani, Donald Trump, ametoa kauli kali akizungumzia uwezekano wa makubaliano ya kibiashara kati ya China na Canada, akionya kuwa hatua hiyo inaweza kuiweka Canada katika hatari kubwa ya kiuchumi.

    Akizungumza katika muktadha wa mijadala ya biashara za kimataifa, Trump alidai kuwa China ina uwezo mkubwa wa kiuchumi na kimkakati ambao unaweza kuathiri vibaya mataifa yanayoingia nayo mikataba bila tahadhari ya kutosha. Kwa mujibu wa Trump, Canada inaweza kujikuta ikidhoofishwa endapo itafanya makubaliano ya karibu na taifa hilo la Asia.

    “Ninasema wazi kabisa, China itaimeza Canada ikiwa watafanya makubaliano kati yao,” alisema Trump.

    Kauli hiyo imeibua mjadala mpana kuhusu uhusiano wa kibiashara kati ya mataifa makubwa na yale ya kati, hasa ikizingatiwa nafasi ya China kama moja ya nguvu kubwa za uchumi duniani. Wachambuzi wa siasa na uchumi wanasema matamshi ya Trump yanaakisi msimamo wake wa muda mrefu wa tahadhari na hata upinzani dhidi ya ushawishi wa China katika biashara za kimataifa.

    Hadi sasa, serikali ya Canada haijatoa tamko rasmi kujibu kauli hiyo, huku China pia ikikaa kimya kuhusu madai hayo. Hata hivyo, mjadala unaendelea kuonyesha jinsi masuala ya biashara na diplomasia yanavyoendelea kuwa nyeti katika uhusiano wa kimataifa, hasa yanapohusisha mataifa yenye maslahi makubwa ya kiuchumi.

    Toa maoni yako
    #Habari
    #Trump #China #Canada #Biashara #UhusianoYaKimataifa
    0 Commentarios 0 Acciones 9 Views
  • “Haijalishi wanapiga kelele kiasi gani au wanapiga mayowe kwa nguvu gani, tunachojali ni kwamba tupo upande sahihi wa historia. Tumeitambua Palestina kama taifa huru”

    - Pedro Sánchez, Waziri Mkuu wa Hispania.

    Toa maoni yako
    #Habari
    “Haijalishi wanapiga kelele kiasi gani au wanapiga mayowe kwa nguvu gani, tunachojali ni kwamba tupo upande sahihi wa historia. Tumeitambua Palestina kama taifa huru” - Pedro Sánchez, Waziri Mkuu wa Hispania. Toa maoni yako #Habari
    0 Commentarios 0 Acciones 86 Views
  • Dr. Owuor wa Kenya azua gumzo Mitandaoni baada ya kudai kuwa na mazungumzo na Mungu kupitia WhatsApp.

    Mhubiri maarufu kutoka Nchini Kenya, Dr. David Owuor, ameibua mjadala mkubwa katika mitandao ya kijamii baada ya kudai tena kuwa ana mawasiliano ya moja kwa moja na Mungu kupitia mtandao wa WhatsApp.

    Kupitia ujumbe na vielelezo vinavyosambaa mitandaoni, Dr. Owuor ameonyesha kile anachodai kuwa ni mazungumzo yake na Mungu, jambo lililozua mshangao, maswali na mitazamo tofauti miongoni mwa waumini na Watumiaji wa mitandao ya kijamii.

    Kwa mujibu wa taarifa zinazosambaa, Mhubiri huyo amesema kuwa si mara ya kwanza kwa yeye kuwasiliana na Mungu kwa njia hiyo, akieleza kuwa sasa imekuwa ni mawasiliano ya karibu yanayotokea mara kwa mara.

    “Nimekuwa nikizungumza na Mungu kila siku kupitia WhatsApp,” imedaiwa kuwa ni kauli inayohusishwa na Mhubiri huyo, kauli ambayo imezua mjadala mpana kuhusu mipaka ya imani, teknolojia na tafsiri ya mawasiliano ya kiroho katika zama za kisasa.

    Wapo wanaomuunga mkono wakisema kuwa Mungu anaweza kutumia njia yoyote kuwasiliana na Wanadamu, huku wengine wakipinga vikali wakidai madai hayo hayana uthibitisho wa wazi na yanaweza kuwapotosha Waumini.

    Hadi sasa, Dr. Owuor hajaweka wazi kwa kina namna mawasiliano hayo yanavyofanyika wala kutoa uthibitisho rasmi unaothibitisha madai yake, lakini tukio hilo limeendelea kutawala mijadala katika majukwaa mbalimbali ya kijamii Afrika Mashariki na kwingineko.

    Tukio hili linaendelea kufuatiliwa kwa karibu huku likizua maswali mapya kuhusu nafasi ya teknolojia katika masuala ya kiimani na kiroho.

    Toa maoni yako
    Dr. Owuor wa Kenya azua gumzo Mitandaoni baada ya kudai kuwa na mazungumzo na Mungu kupitia WhatsApp. Mhubiri maarufu kutoka Nchini Kenya, Dr. David Owuor, ameibua mjadala mkubwa katika mitandao ya kijamii baada ya kudai tena kuwa ana mawasiliano ya moja kwa moja na Mungu kupitia mtandao wa WhatsApp. Kupitia ujumbe na vielelezo vinavyosambaa mitandaoni, Dr. Owuor ameonyesha kile anachodai kuwa ni mazungumzo yake na Mungu, jambo lililozua mshangao, maswali na mitazamo tofauti miongoni mwa waumini na Watumiaji wa mitandao ya kijamii. Kwa mujibu wa taarifa zinazosambaa, Mhubiri huyo amesema kuwa si mara ya kwanza kwa yeye kuwasiliana na Mungu kwa njia hiyo, akieleza kuwa sasa imekuwa ni mawasiliano ya karibu yanayotokea mara kwa mara. “Nimekuwa nikizungumza na Mungu kila siku kupitia WhatsApp,” imedaiwa kuwa ni kauli inayohusishwa na Mhubiri huyo, kauli ambayo imezua mjadala mpana kuhusu mipaka ya imani, teknolojia na tafsiri ya mawasiliano ya kiroho katika zama za kisasa. Wapo wanaomuunga mkono wakisema kuwa Mungu anaweza kutumia njia yoyote kuwasiliana na Wanadamu, huku wengine wakipinga vikali wakidai madai hayo hayana uthibitisho wa wazi na yanaweza kuwapotosha Waumini. Hadi sasa, Dr. Owuor hajaweka wazi kwa kina namna mawasiliano hayo yanavyofanyika wala kutoa uthibitisho rasmi unaothibitisha madai yake, lakini tukio hilo limeendelea kutawala mijadala katika majukwaa mbalimbali ya kijamii Afrika Mashariki na kwingineko. Tukio hili linaendelea kufuatiliwa kwa karibu huku likizua maswali mapya kuhusu nafasi ya teknolojia katika masuala ya kiimani na kiroho. Toa maoni yako
    0 Commentarios 0 Acciones 93 Views
  • WATUMIAJI WA DATA WA UKWELI!

    SME BANDO YA AIRTEL imerudi kwa kishindo!

    Unatumia 5K–7K kila wiki kwa bando?
    ACHANA NAYO!

    Kwa 15,000 tu unapata:
    GB 15 za mwezi mzima
    + Dakika 500 (kama ni combo)

    Hakuna longolongo, hakuna makato.
    Data safi, muda mwingi, bei ndogo!

    Wahi kabla salio halijaisha tu sasa hivi…
    DM NIKUSAIDIE KUFUNGUA

    Piga+255786711057

    #SMEBando #DataYaUkweli #AirtelSME #BandoKali #HustleSmart
    📣 WATUMIAJI WA DATA WA UKWELI! 🚨 SME BANDO YA AIRTEL imerudi kwa kishindo! 🚨 Unatumia 5K–7K kila wiki kwa bando? 🚫 ACHANA NAYO! ✅ Kwa 15,000 tu unapata: 📶 GB 15 za mwezi mzima 📞 + Dakika 500 (kama ni combo) Hakuna longolongo, hakuna makato. 💯 Data safi, muda mwingi, bei ndogo! ⏳ Wahi kabla salio halijaisha tu sasa hivi… 📲 DM NIKUSAIDIE KUFUNGUA 💬 Piga+255786711057 #SMEBando #DataYaUkweli #AirtelSME #BandoKali #HustleSmart
    0 Commentarios 0 Acciones 1K Views
  • Elimu Nchini Japani huanza bila mitihani hadi darasa la nne, karibu na umri wa miaka 10. Katika miaka mitatu ya kwanza, mkazo ni kukuza tabia njema na ukuzaji wa Maendeleo.

    Walimu hutanguliza ujuzi wa kijamii kwa kuwafundisha kazi na ukuaji wa kibinafsi, wakiamini haya ni muhimu kabla ya kuanzisha majaribio ya kitaaluma Darasani.

    Kwa kuangazia ujenzi wa tabia mapema, shule zinalenga kulea Watoto waliokamilika ambao wanathamini heshima na kazi ya pamoja, na kutoa msingi thabiti wa kujifunza siku zijazo.

    Elimu Nchini Japani 🇯🇵 huanza bila mitihani hadi darasa la nne, karibu na umri wa miaka 10. Katika miaka mitatu ya kwanza, mkazo ni kukuza tabia njema na ukuzaji wa Maendeleo. Walimu hutanguliza ujuzi wa kijamii kwa kuwafundisha kazi na ukuaji wa kibinafsi, wakiamini haya ni muhimu kabla ya kuanzisha majaribio ya kitaaluma Darasani. Kwa kuangazia ujenzi wa tabia mapema, shule zinalenga kulea Watoto waliokamilika ambao wanathamini heshima na kazi ya pamoja, na kutoa msingi thabiti wa kujifunza siku zijazo.
    0 Commentarios 0 Acciones 767 Views
  • Mchezaji wa kimataifa wa Ufaransa , N’Golo Kanté, ameonyesha moyo wa upendo kwa jamii kwa kujenga hospitali ya kisasa yenye thamani ya dola milioni tano (5) Nchini Mali, ikiwa ni msaada kwa Watoto na familia zisizojiweza kupata huduma bora za afya.

    Kanté, ambaye alizaliwa Jijini Paris, Ufaransa, ana asili ya Mali, Wazazi wake wakiwa Wahamiaji waliotoka Nchini Mali mwaka 1980. Jina lake N’Golo linatokana na Mfalme wa zamani wa Mali aliyewahi kutawala. Katika ziara yake Mali, Kanté alitumia muda na familia yake huku akitoa heshima kwa Baba yake na Kaka yake Marehemu.

    Mchezaji wa kimataifa wa Ufaransa 🇫🇷, N’Golo Kanté, ameonyesha moyo wa upendo kwa jamii kwa kujenga hospitali ya kisasa yenye thamani ya dola milioni tano (5) Nchini Mali, ikiwa ni msaada kwa Watoto na familia zisizojiweza kupata huduma bora za afya. Kanté, ambaye alizaliwa Jijini Paris, Ufaransa, ana asili ya Mali, Wazazi wake wakiwa Wahamiaji waliotoka Nchini Mali mwaka 1980. Jina lake N’Golo linatokana na Mfalme wa zamani wa Mali aliyewahi kutawala. Katika ziara yake Mali, Kanté alitumia muda na familia yake huku akitoa heshima kwa Baba yake na Kaka yake Marehemu.
    0 Commentarios 0 Acciones 1K Views
  • Rais Donald Trump wa Marekani amemuandikia barua ya mwaliko kwenye Ikulu ya Marekani White House Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu akimuomba aende wiki ijayo wakajadili hali ya Mashariki ya Kati na maslahi yao ya pamoja katika ukanda huo (mgogoro wa Palestina na Israel).

    Kwa mwaliko huo, Benjamin Netanyahu atakuwa kiongozi Mkuu wa kwanza wa nje kufanya ziara rasmi Marekani baada ya Trump kushinda tena Urais wa Taifa hilo. Ikumbukwe maandalizi ya mkutano wa Trump na Putin pia yanaendelea ili kumaliza vita vya Ukraine.

    Rais Donald Trump wa Marekani amemuandikia barua ya mwaliko kwenye Ikulu ya Marekani White House Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu akimuomba aende wiki ijayo wakajadili hali ya Mashariki ya Kati na maslahi yao ya pamoja katika ukanda huo (mgogoro wa Palestina na Israel). Kwa mwaliko huo, Benjamin Netanyahu atakuwa kiongozi Mkuu wa kwanza wa nje kufanya ziara rasmi Marekani baada ya Trump kushinda tena Urais wa Taifa hilo. Ikumbukwe maandalizi ya mkutano wa Trump na Putin pia yanaendelea ili kumaliza vita vya Ukraine.
    Like
    1
    0 Commentarios 0 Acciones 896 Views
  • Baada ya Rais wa Marekani , Donald Trump kusaini amri ya Marekani kujitoa Shirika la afya Duniani (WHO) sanjari na kusitisha ufadhili wa kifedha kwa Mashirika yote ya kiafya Duniani kote ikiwemo yale ya kupambana na ukimwi kwa siku 90.

    Rais huyo amesema katika kipindi hicho cha mpito serikali yake itafanya tathimini ya kuona ushiriki wake na ufadhili kama unaenda sahihi na mataifa mengine au Marekani imesusiwa mzigo mkubwa peke yake wa kuhudumia Dunia. Marekani ndio mchangiaji mkubwa zaidi kwenye Mashirika hayo ya afya ikiwemo (WHO), ambapo Marekani inachangia takribani dola bilioni moja (1) huku Nchi ya China ikichangia dola milioni (86) pekee kitu ambacho Donald Trump amesema sio sahihi.

    Tayari Mashirika yanayofadhiliwa na Marekani likiwemo la USAID yamepokea waraka wa agizo la Donald Trump na kuagizwa kuanza utekelezaji Duniani kote.

    Baada ya Rais wa Marekani 🇺🇸, Donald Trump kusaini amri ya Marekani kujitoa Shirika la afya Duniani (WHO) sanjari na kusitisha ufadhili wa kifedha kwa Mashirika yote ya kiafya Duniani kote ikiwemo yale ya kupambana na ukimwi kwa siku 90. Rais huyo amesema katika kipindi hicho cha mpito serikali yake itafanya tathimini ya kuona ushiriki wake na ufadhili kama unaenda sahihi na mataifa mengine au Marekani imesusiwa mzigo mkubwa peke yake wa kuhudumia Dunia. Marekani ndio mchangiaji mkubwa zaidi kwenye Mashirika hayo ya afya ikiwemo (WHO), ambapo Marekani inachangia takribani dola bilioni moja (1) huku Nchi ya China ikichangia dola milioni (86) pekee kitu ambacho Donald Trump amesema sio sahihi. Tayari Mashirika yanayofadhiliwa na Marekani likiwemo la USAID yamepokea waraka wa agizo la Donald Trump na kuagizwa kuanza utekelezaji Duniani kote.
    Like
    1
    0 Commentarios 0 Acciones 1K Views
  • Namba kwenye mtandao wa YouTube anadai kuingiza Dola milioni moja kwa siku, baadaye Tajiri namba moja Duniani kamjibu kuwa yeye anaingiza Dola milioni moja kwa dakika moja.

    Namba kwenye mtandao wa YouTube anadai kuingiza Dola milioni moja kwa siku, baadaye Tajiri namba moja Duniani kamjibu kuwa yeye anaingiza Dola milioni moja kwa dakika moja.
    Like
    1
    0 Commentarios 0 Acciones 722 Views
  • Like
    1
    0 Commentarios 0 Acciones 577 Views
  • Mwaka 2019, Nchini Japan waliweza kupitisha utafiti kwa kuweza kuwaruhusu Wanasayansi kuweza kutengeneza (kuunda) Wanadamu. Mfumo huo ambao unakusanya viungo vya Wanyama na Binadamu ili kuweza kukuza viungo vya Binadamu ndani ya Mnyama kwa njia ya kupandikiza. Watafiti hao wakiongozwa na Mwanasayansi mmoja aitwaye Hiromitsu Nakauchi.

    Utafiti huo unaruhusisha kuingiza "seli" za Binadamu kwenye "viinitete" vya Wanyama (animal embroys) kwa Nguruwe na Panya, ili kuweza kukuza vya Binadamu. Bado kuna wasiwasi wa kimaadili unaweza kujitokeza kuhusu kuchanganya "seli" za kibinadamu na Wanyama haswa kwenye ukuaji wa ubongo.

    Sheria mpya imeruhusu utafiti huo kukuza hadi kuwa Mnyama Binadamu kamili, hivyo kuzua mijadiliano mikali kati ya Sayansi ya matibabu na uumbaji wa Mwenyezi Mungu.

    Mwaka 2019, Nchini Japan 🇯🇵 waliweza kupitisha utafiti kwa kuweza kuwaruhusu Wanasayansi kuweza kutengeneza (kuunda) Wanadamu. Mfumo huo ambao unakusanya viungo vya Wanyama na Binadamu ili kuweza kukuza viungo vya Binadamu ndani ya Mnyama kwa njia ya kupandikiza. Watafiti hao wakiongozwa na Mwanasayansi mmoja aitwaye Hiromitsu Nakauchi. Utafiti huo unaruhusisha kuingiza "seli" za Binadamu kwenye "viinitete" vya Wanyama (animal embroys) kwa Nguruwe na Panya, ili kuweza kukuza vya Binadamu. Bado kuna wasiwasi wa kimaadili unaweza kujitokeza kuhusu kuchanganya "seli" za kibinadamu na Wanyama haswa kwenye ukuaji wa ubongo. Sheria mpya imeruhusu utafiti huo kukuza hadi kuwa Mnyama Binadamu kamili, hivyo kuzua mijadiliano mikali kati ya Sayansi ya matibabu na uumbaji wa Mwenyezi Mungu.
    Like
    1
    0 Commentarios 0 Acciones 1K Views
  • Like
    Haha
    2
    0 Commentarios 0 Acciones 548 Views
  • Udaku umetazamwa (view) na Watu zaidi laki nne (4) ila wimbo mpya Watazamaji (views) ni zaidi ya elfu (59) pekee... Yaani hawa ndio Ndugu wa Watazamaji .

    Ni umbea au udaku kwanza, mengine baadaye

    Udaku umetazamwa (view) na Watu zaidi laki nne (4) ila wimbo mpya Watazamaji (views) ni zaidi ya elfu (59) pekee... Yaani hawa ndio Ndugu wa Watazamaji 😂. Ni umbea au udaku kwanza, mengine baadaye 😂
    Like
    1
    0 Commentarios 0 Acciones 733 Views
  • Kuna baadhi ya Watu kwenye "comenti" (baadhi lakini) huwa sipendi kuwajibu kwa sababu ya elimu yao. Ukiandika vibaya (matusi, dhihaka, kejeli au kunishambulia) kwa habari yoyote ile "ninayoiposti" au kama "nime-comenti" sehemu kisha ukaja kujibu. Kwanza ninaangalia "profile" yako ili nijue wewe ni Mtu wa aina gani na nikiona upo upo tu basi sijibu. Lakini nikiona kama umejitoa ufahamu (ujuaji au kudandia gari kwa mbele) basi nakujibu.

    Nimesema hayo kwa sababu gani, kuna baadhi ya Watu hapa mitandao hawajui tena hawajui kama hawajui, wapo Watu ambao ni Wajinga (sio tusi hii, tafuta kamusi ikusaidie) na hata uwaeleweshe vipi, vichwa vyao ni maji au sifuri.

    Mama Samia alikuwa anasherekea siku yake ya mfanano wa kuzaliwa yaani Birthday kwa kiingereza, basi mimi "nili-coment" sehemu fulani "Happy birthday to They". Baada ya muda mfupi nikaona Mtu anakejeli, nikamuacha, baadaye nikaona Watu wengine wanazidi kuongezeka, nikasema "Daaah Dunia haijaelimika kwa kweli".

    Sasa ipo hivi

    Kutumia "They" kumheshimu Mtu, hasa kama unataka kuepuka kuonyesha jinsia ya Mtu au unapoheshimu mamlaka yao kama vile Rais au Mfalme, ni sahihi na inaeleweka. Katika tamaduni nyingi, matumizi ya "they" kama pronomi ya jinsia isiyojulikana au isiyobainika, ni njia ya heshima na inatumika pia kama njia ya kuonyesha heshima kwa Mtu aliye katika nafasi kubwa kama Rais au Mfalme.

    Hii ni tofauti na matumizi ya "he" au "she," ambayo yanaweza kuhusisha jinsia maalum. "They" inaweza kutumika pia kwa kumheshimu Mtu bila kujali jinsia au kama njia ya kujiepusha na maelezo ya kijinsia.

    Kuna mifano ambapo Viongozi wakubwa hutumika "they" kama njia ya kumheshimu na kuonyesha hofu au hadhi ya nafasi yao.

    Hiyo tafsiri nyepesi kabisa kutoka kwa Wajuzi wa lugha ya Kiingereza.

    Kuna baadhi ya Watu kwenye "comenti" (baadhi lakini) huwa sipendi kuwajibu kwa sababu ya elimu yao. Ukiandika vibaya (matusi, dhihaka, kejeli au kunishambulia) kwa habari yoyote ile "ninayoiposti" au kama "nime-comenti" sehemu kisha ukaja kujibu. Kwanza ninaangalia "profile" yako ili nijue wewe ni Mtu wa aina gani na nikiona upo upo tu basi sijibu. Lakini nikiona kama umejitoa ufahamu (ujuaji au kudandia gari kwa mbele) basi nakujibu. Nimesema hayo kwa sababu gani, kuna baadhi ya Watu hapa mitandao hawajui tena hawajui kama hawajui, wapo Watu ambao ni Wajinga (sio tusi hii, tafuta kamusi ikusaidie) na hata uwaeleweshe vipi, vichwa vyao ni maji au sifuri. Mama Samia alikuwa anasherekea siku yake ya mfanano wa kuzaliwa yaani Birthday kwa kiingereza, basi mimi "nili-coment" sehemu fulani "Happy birthday to They". Baada ya muda mfupi nikaona Mtu anakejeli, nikamuacha, baadaye nikaona Watu wengine wanazidi kuongezeka, nikasema "Daaah Dunia haijaelimika kwa kweli". Sasa ipo hivi 👇 Kutumia "They" kumheshimu Mtu, hasa kama unataka kuepuka kuonyesha jinsia ya Mtu au unapoheshimu mamlaka yao kama vile Rais au Mfalme, ni sahihi na inaeleweka. Katika tamaduni nyingi, matumizi ya "they" kama pronomi ya jinsia isiyojulikana au isiyobainika, ni njia ya heshima na inatumika pia kama njia ya kuonyesha heshima kwa Mtu aliye katika nafasi kubwa kama Rais au Mfalme. Hii ni tofauti na matumizi ya "he" au "she," ambayo yanaweza kuhusisha jinsia maalum. "They" inaweza kutumika pia kwa kumheshimu Mtu bila kujali jinsia au kama njia ya kujiepusha na maelezo ya kijinsia. Kuna mifano ambapo Viongozi wakubwa hutumika "they" kama njia ya kumheshimu na kuonyesha hofu au hadhi ya nafasi yao. Hiyo tafsiri nyepesi kabisa kutoka kwa Wajuzi wa lugha ya Kiingereza.
    Like
    2
    0 Commentarios 0 Acciones 1K Views
  • "Faida ya kwanza ya Eng. Hersi na ACA ni kuwa sauti ya VILABU kwenye Mkutano wa Kamati Tendaji ya CAF

    Na moja ya Kilio kikubwa cha VILABU hapa Afrika ni kukosa Hela ya maandalizi kushiriki LIGI YA MABINGWA na KOMBE LA SHIRIKISHO

    Unapambana kupata nafasi kwenye Ligi, kisha upambane wapi utapata Hela ili ukashiriki HATUA 2 ZA AWALI ili baadae ukapate hela ya CAF kuanzia Hatua ya Makundi

    Timu nyingi ndogo Tanzania zilipata Tabu ya kushiriki michuano hii, Mfano wa wazi BIASHARA UNITED Kutoka Mara

    ENG Hersi amefika na kuhakikisha Timu zote za Hatua ya awali zinapata Fedha.

    Msimu huu ZAIDI YA BILIONI 13 kutoka CAF zimetoka kwa VILABU vilivyoshiriki Hatua ya awali.

    Makofi Mengi kwa Eng. Hersi Said" - Ally Kamwe, Msemaji wa klabu ya Yanga SC.

    "Faida ya kwanza ya Eng. Hersi na ACA ni kuwa sauti ya VILABU kwenye Mkutano wa Kamati Tendaji ya CAF Na moja ya Kilio kikubwa cha VILABU hapa Afrika ni kukosa Hela ya maandalizi kushiriki LIGI YA MABINGWA na KOMBE LA SHIRIKISHO Unapambana kupata nafasi kwenye Ligi, kisha upambane wapi utapata Hela ili ukashiriki HATUA 2 ZA AWALI ili baadae ukapate hela ya CAF kuanzia Hatua ya Makundi Timu nyingi ndogo Tanzania zilipata Tabu ya kushiriki michuano hii, Mfano wa wazi BIASHARA UNITED Kutoka Mara ENG Hersi amefika na kuhakikisha Timu zote za Hatua ya awali zinapata Fedha. Msimu huu ZAIDI YA BILIONI 13 kutoka CAF zimetoka kwa VILABU vilivyoshiriki Hatua ya awali. Makofi Mengi kwa Eng. Hersi Said👏👏" - Ally Kamwe, Msemaji wa klabu ya Yanga SC.
    Like
    Love
    2
    0 Commentarios 0 Acciones 830 Views
  • Like
    2
    0 Commentarios 0 Acciones 550 Views
  • Like
    1
    0 Commentarios 0 Acciones 544 Views
  • "Mimi CAF hawawezi kunifuata kwa sababu nina ratiba ya kuandaa timu kuelekea Robo Fainali, kwahiyo CAF wanaangalia nani hana kazi, ndiyo maana wanamualika yaani Jobless" - Ahmed Ally, Msemaji wa klabu ya Simba SC akijibu swali kuhusu kutokualikwa kwenye droo ya CAF Morocco baada ya Msemaji mwenzie wa klabu ya Yanga SC Ally Kamwe kualikwa.

    "Mimi CAF hawawezi kunifuata kwa sababu nina ratiba ya kuandaa timu kuelekea Robo Fainali, kwahiyo CAF wanaangalia nani hana kazi, ndiyo maana wanamualika yaani Jobless" - Ahmed Ally, Msemaji wa klabu ya Simba SC akijibu swali kuhusu kutokualikwa kwenye droo ya CAF Morocco baada ya Msemaji mwenzie wa klabu ya Yanga SC Ally Kamwe kualikwa.
    Like
    1
    0 Commentarios 0 Acciones 1K Views
  • Like
    1
    0 Commentarios 0 Acciones 523 Views
  • Like
    1
    0 Commentarios 0 Acciones 533 Views
  • Klabu ya Singida Black Stars imetoa Wachezaji wake (16) kwa mkopo kwenda kwenye klabu zingine kulinda vipaji vyao.

    Ni klabu tano (5) pekee ambazo hazijapata Mchezaji kutoka katika klabu ya Singida Black Stars, klabu zilizobakia zote zimewahi kupokea mchezaji wa Singida kwa mkopo ikiwemo klabu za Simba SC, Azam FC, KMC,...

    Klabu ya Singida Black Stars imetoa Wachezaji wake (16) kwa mkopo kwenda kwenye klabu zingine kulinda vipaji vyao. Ni klabu tano (5) pekee ambazo hazijapata Mchezaji kutoka katika klabu ya Singida Black Stars, klabu zilizobakia zote zimewahi kupokea mchezaji wa Singida kwa mkopo ikiwemo klabu za Simba SC, Azam FC, KMC,...
    Like
    1
    0 Commentarios 0 Acciones 805 Views
  • Like
    Haha
    2
    0 Commentarios 0 Acciones 548 Views
  • "Watoto wakike leo naongea nanyie, naomba mnisikilize kwa makini tena nisikilizeni vizuri kabisa, mueshimieni Wazazi wenu na kuwasikiliza, Mzazi akikuambia usifanye acha mara moja maana Mzazi akiondoka hakuna mwingine atakae kuelekeza, leo hii mimi nimeamua kumpa Wwanangu Wema Sepetu kanga kama zawadi ya siku ya kuzaliwa kwake, yote ni kwasababu amejisahau, nilienda kwake nikamuomba anipe kanga akanipa mtandio, hii inaonesha ni kiasi gani hajitambui, heshima ya Mwanamke ni kanga sio hayo mavazi yenu" - Mama Mzazi w Sepetu.

    "Watoto wakike leo naongea nanyie, naomba mnisikilize kwa makini tena nisikilizeni vizuri kabisa, mueshimieni Wazazi wenu na kuwasikiliza, Mzazi akikuambia usifanye acha mara moja maana Mzazi akiondoka hakuna mwingine atakae kuelekeza, leo hii mimi nimeamua kumpa Wwanangu Wema Sepetu kanga kama zawadi ya siku ya kuzaliwa kwake, yote ni kwasababu amejisahau, nilienda kwake nikamuomba anipe kanga akanipa mtandio, hii inaonesha ni kiasi gani hajitambui, heshima ya Mwanamke ni kanga sio hayo mavazi yenu" - Mama Mzazi w Sepetu.
    Like
    1
    0 Commentarios 0 Acciones 646 Views
Quizás te interese…