• 21/21.*NGUVU YA KUCHAGUA*

    Maisha ni kuchagua.
    Kila matokeo au jambo linalo onekana katika miasha limejengwa na msingi wa kuchagua.

    Ukikosea kuchagua ,umekosea kuishi . Watu wengi sana wanazani maisha ni bahati na hivyo uishia kuona kuwa wao hawana bahati kumbe bahati njema ni matokeo ya chaguo jema na bahati mbaya ni matokeo ya chaguo baya.

    Kumbukumbu la Torati 11:26
    [26]Angalieni, nawawekea mbele yenu hivi leo baraka na laana;

    Ndicho Mungu alicho kifanya katika maisha ameweka mbele yetu baraka na laana , kustawi au kutokustawi kutaamuliwa na nguvu ya chaguo .

    Kumbe nguvu ya kuchagua ndiyo itakayo kuamulia kiwango cha baraka zako au laana yako.

    Hii ni moja ya kanuni ya kuzitaka baraka baada ya kuchagua kutenda haya.

    Kumbukumbu la Torati 11:27
    [27]baraka ni hapo mtakapoyasikiza maagizo ya BWANA, Mungu wenu, niwaagizayo leo;


    Ukichagua kutii maagizo, kuwa na bidii ya bwana ndipo utakuwa umechagua baraka.

    Kumbukumbu la Torati 28:1-2
    [1]Itakuwa utakaposikia sauti ya BWANA, Mungu wako, kwa bidii, kutunza kuyafanya maagizo yake yote nikuagizayo leo, ndipo BWANA, Mungu wako, atakapokutukuza juu ya mataifa yote ya duniani;

    [2]na baraka hizi zote zitakujilia na kukupata usikiapo sauti ya BWANA, Mungu wako.

    3.lazima uchague kumjua sana Mungu.

    Ayubu 22:21
    [21]Mjue sana Mungu, ili uwe na amani;
    Ndivyo mema yatakavyokujia.

    Chagua kumjua Mungu ili mema yakufuate lakini pia usipo chagua hivyo pia lazima utapata matokeo.

    Kumbukumbu la Torati 11:28
    [28]na laana ni hapo msiposikiza maagizo ya BWANA, Mungu wenu, mkikengeuka katika njia niwaagizayo leo, kwa kuandama miungu mingine msiyoijua.

    Laaana ni matokeo ya kujiongoza vibaya na ndipo matokeo lazima uyapate tu .

    Kumbukumbu la Torati 28:15-17
    [15]Lakini itakuwa usipotaka kuisikiza sauti ya BWANA, Mungu wako, usiyaangalie kufanya maagizo yake yote na amri zake, nikuagizazo hivi leo, ndipo zitakapokujia laana hizi zote na kukupata.

    [16]Utalaaniwa mjini, utalaaniwa na mashambani.
    .
    [17]Litalaaniwa kapu lako na chombo chako cha kukandia.

    Utakuja kuona kuna watu tunaishi copy za maisha yetu sababu tu ya kutokuchagua vyema au kuichagua dunia..

    Yoshua alitangaza nguvu ya kuchagua lakini yeye alishachagua kuwa yeye na nyumba yake watamtumikia Mungu.

    Namaliza kwa kusema hakuna baraka zinazo weza kukujia ikiwa wewe uko nje ya agano la Mungu ambalo ni WOKOVU.

    Naitwa sylvester mwakabende kutoka (build new eden)
    #build new eden
    #restore men position
    21/21.*NGUVU YA KUCHAGUA* Maisha ni kuchagua. Kila matokeo au jambo linalo onekana katika miasha limejengwa na msingi wa kuchagua. Ukikosea kuchagua ,umekosea kuishi . Watu wengi sana wanazani maisha ni bahati na hivyo uishia kuona kuwa wao hawana bahati kumbe bahati njema ni matokeo ya chaguo jema na bahati mbaya ni matokeo ya chaguo baya. Kumbukumbu la Torati 11:26 [26]Angalieni, nawawekea mbele yenu hivi leo baraka na laana; Ndicho Mungu alicho kifanya katika maisha ameweka mbele yetu baraka na laana , kustawi au kutokustawi kutaamuliwa na nguvu ya chaguo . Kumbe nguvu ya kuchagua ndiyo itakayo kuamulia kiwango cha baraka zako au laana yako. Hii ni moja ya kanuni ya kuzitaka baraka baada ya kuchagua kutenda haya. Kumbukumbu la Torati 11:27 [27]baraka ni hapo mtakapoyasikiza maagizo ya BWANA, Mungu wenu, niwaagizayo leo; Ukichagua kutii maagizo, kuwa na bidii ya bwana ndipo utakuwa umechagua baraka. Kumbukumbu la Torati 28:1-2 [1]Itakuwa utakaposikia sauti ya BWANA, Mungu wako, kwa bidii, kutunza kuyafanya maagizo yake yote nikuagizayo leo, ndipo BWANA, Mungu wako, atakapokutukuza juu ya mataifa yote ya duniani; [2]na baraka hizi zote zitakujilia na kukupata usikiapo sauti ya BWANA, Mungu wako. 3.lazima uchague kumjua sana Mungu. Ayubu 22:21 [21]Mjue sana Mungu, ili uwe na amani; Ndivyo mema yatakavyokujia. Chagua kumjua Mungu ili mema yakufuate lakini pia usipo chagua hivyo pia lazima utapata matokeo. Kumbukumbu la Torati 11:28 [28]na laana ni hapo msiposikiza maagizo ya BWANA, Mungu wenu, mkikengeuka katika njia niwaagizayo leo, kwa kuandama miungu mingine msiyoijua. Laaana ni matokeo ya kujiongoza vibaya na ndipo matokeo lazima uyapate tu . Kumbukumbu la Torati 28:15-17 [15]Lakini itakuwa usipotaka kuisikiza sauti ya BWANA, Mungu wako, usiyaangalie kufanya maagizo yake yote na amri zake, nikuagizazo hivi leo, ndipo zitakapokujia laana hizi zote na kukupata. [16]Utalaaniwa mjini, utalaaniwa na mashambani. . [17]Litalaaniwa kapu lako na chombo chako cha kukandia. Utakuja kuona kuna watu tunaishi copy za maisha yetu sababu tu ya kutokuchagua vyema au kuichagua dunia.. Yoshua alitangaza nguvu ya kuchagua lakini yeye alishachagua kuwa yeye na nyumba yake watamtumikia Mungu. Namaliza kwa kusema hakuna baraka zinazo weza kukujia ikiwa wewe uko nje ya agano la Mungu ambalo ni WOKOVU. Naitwa sylvester mwakabende kutoka (build new eden) #build new eden #restore men position
    Angry
    1
    · 0 Kommentare ·0 Anteile ·405 Ansichten
  • Nguvu ya damu ya Yesu.

    Damu ni ndiyo msingi wa agano .Ili agano litimie lazima limaliswe ba damu ambayo inene kama shahidi wa agano.

    Damu ndiyo inamamlaka ya kumsafisha mtu uovu wake wa kwanza au dhambi zake.

    Na hili halikuwnza kwa mwanadamu bali alilifanya mara ya kwanza Mungu mwenyewe pale bustanini eden kwa kuchinjz ili awavike adamu na mkewe baada ya kutoka nje ya maagizo yake au agano lake.
    Mwanzo 3:21. *Mwenyezi-Mungu akawatengenezea Adamu na mkewe mavazi ya ngozi, akawavika.*

    Damu ilitumika kama ondeleo la dhambi ndiyo maana mwanadamu alipo kuwa akikosa basi alienda kwa kuhani na kupeleka sadaka yakuteketezwa na sadaka ya ondeleo ambayo ni Azazeli iliyo kuwa mbuzi anaye beba uovu na kisha kuachwa jangwani.

    Ebrania 9:21
    "Katika torati karibi vitu vyote husafishwa kwa damu na pasipo kumwaga damu hakuna ondoleo"

    Kama pasipo damu kulikuwa hakuna ondoleo basi hiyo ndilo kusudi la Yesu kuja duniani kufanyika mwili ili aweze kutupa ondoleo la dhambi.

    Ndiyo maana ukisoma ujumbe wake wa kwanza kabisa kunena alinena maneno ya nabii isaya "Roho wa Bwana yu juu yangu, Kwa maana amenitia mafuta kuwahubiri maskini habari njema. Amenituma kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao, Na vipofu kupata kuona tena, Kuwaacha huru waliosetwa.Luka 4:19

    Kwa maana alianza kusema hivyo akiainisha kusudi lake ilimlazimu yeye ndo awe mwanakondoo wa kuchinjwa ili ukombozi upatikane .

    Ili. atupe ondoleo ili mlazimu awe ndugu yetu ili kwanza ndiyo sababu akabeba mwili ili aonekane mwenzetu.

    Kupitia damu yake ndiyo tunapata ondoleo na ushindi dhidi ya dhambi .

    Nao wakamshinda kwa damu ya Mwana-Kondoo, na kwa neno la ushuhuda wao; ambao hawakupenda
    maisha yao hata kufa.(Ufunuo12:11)

    kama damu ya Abili ilinena ingali kuwa zmekufa vipi kuhusu damu ya Yesu mwenyewe ambaye ndiye kuhani mkuu kwetu na anzye tupa msamaha.

    Ukombozi wa maisha na baraka ni muhimu sana ukijua nguvu ya damu ya nwanakondoo ambaye ndiye yesu kristo

    Ebrania 10:16-19
    16 Hili ni agano nitakaloagana nao baada ya siku zile, anena Bwana,
    Nitatia sheria zangu mioyoni mwao,
    Na katika nia zao nitaziandika;
    ndipo anenapo,
    17 Dhambi zao na uasi wao sitaukumbuka tena kabisa.
    18Basi, ondoleo la hayo likiwapo, hapana toleo tena kwa ajili ya dhambi.
    Wito wa kuwa Wavumilivu
    19 Basi, ndugu, kwa kuwa tuna ujasiri wa kupaingia patakatifu kwa damu ya Yesu,

    Ukijua nguvu ya damu ya Yesu lazma utakuwa na ujasiri katka imani kwani damu yake inanguvu sawa na jina lake ni wewe tu ndo utaki kutumia damu yake kama ukombozi wako.

    Ukombozi ni jambo jema lakini lazima tujue kuwa pasipo Kristo hakuna kukombolewa ,mpe leo maisha akomboe maisha yako.

    #build new eden
    #restore men position
    Nguvu ya damu ya Yesu. Damu ni ndiyo msingi wa agano .Ili agano litimie lazima limaliswe ba damu ambayo inene kama shahidi wa agano. Damu ndiyo inamamlaka ya kumsafisha mtu uovu wake wa kwanza au dhambi zake. Na hili halikuwnza kwa mwanadamu bali alilifanya mara ya kwanza Mungu mwenyewe pale bustanini eden kwa kuchinjz ili awavike adamu na mkewe baada ya kutoka nje ya maagizo yake au agano lake. Mwanzo 3:21. *Mwenyezi-Mungu akawatengenezea Adamu na mkewe mavazi ya ngozi, akawavika.* Damu ilitumika kama ondeleo la dhambi ndiyo maana mwanadamu alipo kuwa akikosa basi alienda kwa kuhani na kupeleka sadaka yakuteketezwa na sadaka ya ondeleo ambayo ni Azazeli iliyo kuwa mbuzi anaye beba uovu na kisha kuachwa jangwani. Ebrania 9:21 "Katika torati karibi vitu vyote husafishwa kwa damu na pasipo kumwaga damu hakuna ondoleo" Kama pasipo damu kulikuwa hakuna ondoleo basi hiyo ndilo kusudi la Yesu kuja duniani kufanyika mwili ili aweze kutupa ondoleo la dhambi. Ndiyo maana ukisoma ujumbe wake wa kwanza kabisa kunena alinena maneno ya nabii isaya "Roho wa Bwana yu juu yangu, Kwa maana amenitia mafuta kuwahubiri maskini habari njema. Amenituma kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao, Na vipofu kupata kuona tena, Kuwaacha huru waliosetwa.Luka 4:19 Kwa maana alianza kusema hivyo akiainisha kusudi lake ilimlazimu yeye ndo awe mwanakondoo wa kuchinjwa ili ukombozi upatikane . Ili. atupe ondoleo ili mlazimu awe ndugu yetu ili kwanza ndiyo sababu akabeba mwili ili aonekane mwenzetu. Kupitia damu yake ndiyo tunapata ondoleo na ushindi dhidi ya dhambi . Nao wakamshinda kwa damu ya Mwana-Kondoo, na kwa neno la ushuhuda wao; ambao hawakupenda maisha yao hata kufa.(Ufunuo12:11) kama damu ya Abili ilinena ingali kuwa zmekufa vipi kuhusu damu ya Yesu mwenyewe ambaye ndiye kuhani mkuu kwetu na anzye tupa msamaha. Ukombozi wa maisha na baraka ni muhimu sana ukijua nguvu ya damu ya nwanakondoo ambaye ndiye yesu kristo Ebrania 10:16-19 16 Hili ni agano nitakaloagana nao baada ya siku zile, anena Bwana, Nitatia sheria zangu mioyoni mwao, Na katika nia zao nitaziandika; ndipo anenapo, 17 Dhambi zao na uasi wao sitaukumbuka tena kabisa. 18Basi, ondoleo la hayo likiwapo, hapana toleo tena kwa ajili ya dhambi. Wito wa kuwa Wavumilivu 19 Basi, ndugu, kwa kuwa tuna ujasiri wa kupaingia patakatifu kwa damu ya Yesu, Ukijua nguvu ya damu ya Yesu lazma utakuwa na ujasiri katka imani kwani damu yake inanguvu sawa na jina lake ni wewe tu ndo utaki kutumia damu yake kama ukombozi wako. Ukombozi ni jambo jema lakini lazima tujue kuwa pasipo Kristo hakuna kukombolewa ,mpe leo maisha akomboe maisha yako. #build new eden #restore men position
    Wow
    1
    · 0 Kommentare ·0 Anteile ·399 Ansichten
  • WAKO WAPI WASHITAKI WAKO ?

    Yohana 8:3-11
    Mafarisayo walimpeleka mwanamke waliye mfumania kwa Yesu ili atoe hukumu .

    *Walipo mpeleka si kwa sababu ya kuwa mwanamke amekosea peke yake walitaka kumjaribu Yesu kupitia yule mwanamke .*

    Lakini wao ambacho hawakujua ni kuwa Yesu yeye ndo anaye tazama mioyo kabla hawajafika.

    *Ukisoma torati ya Musa unaweza dhani walikuwa wameenda kwa nia njema lkn kumbe lengo ni kumtega.*

    *Na kwa sababu walienda kwa mtego Yesu naye akawapa jibu la mtego vile vile kuwa yeyote asiye na dhambi na awe wa kwanza kumpiga huyu mtu.*
    Yohana 8:7
    [7]Nao walipozidi kumhoji, alijiinua, akawaambia, Yeye asiye na dhambi miongoni mwenu na awe wa kwanza wa kumtupia jiwe.

    Yes kabla ujamshitaki mwingine lazima ujiangalie vipi kuhusu wewe hawa walikuwa washitaki wazuri lakini kumbe bado na wao ni wadhinifu tu.

    *Jiulize wewe ambaye unajiona malaika vipi wewe una dhambi yeyote kweli ni kweli umevuka zinaa lakini mbona wivu na husda bado unao*

    Baada ya hapo Yesu anampa njia impasayo *wokovu Nenda zako usitende dhambi tena*

    Kumbe njia nzuri si kumuhukumu mtu kwa kumpiga mawe badala yake mpe njia ya kushinda hiyo zinaa.

    Sababu ya kusema wengine kumeharibu mwili w Kristo hasa watu wanao jifanya wana kirohost wakati ni mafarisayo.

    Ukimkuta ndugu yako anadumbukia shimoni msaidie atoke si kwenda kumtangaza na kumbe huyo mtu kaokoka wiki moja mfuate mtie moyo na mpe njia uliyo tumia kushinda dhambi nayeye ajifunze na hapo ndipo tutita Upendo wa kristo.

    *Siyo unapeleka kwa mchungaji arafu nyuma ya pazia unamtega mchungaji akiamua kumfukuza upate la kumsema akimuonya upate la kumsema.*

    *Dada angu usikubali maneno ya watu na mashitaka ya watu yakukosanishe Mungu ni ukianguka mrudie Bwana ambaye atasimama na wewe na kukusamehe na kukupa onyo ,*

    Walokole wengi tumepoteza radha ya wokovu kwa majungu na kujihesabia sana haki kumbe ni sadukayo na farisayo.

    Kukulia machinjioni haimaanishi lazima ujue kuchinjz nyama kumbe hata wewe dada wengine unawaona wamesimama leo ni
    kwasababu waliamua kujifunza nq si kutumia uzoefu..

    Naweza kwambia kuwa Yesu anakuja ni muhimu kutengeneza.

    Ahsante.naitwa Sylvester Mwakabende wa BUILD NEW EDEN

    #RESTORE MEN POSITION
    WAKO WAPI WASHITAKI WAKO ? Yohana 8:3-11 Mafarisayo walimpeleka mwanamke waliye mfumania kwa Yesu ili atoe hukumu . *Walipo mpeleka si kwa sababu ya kuwa mwanamke amekosea peke yake walitaka kumjaribu Yesu kupitia yule mwanamke .* Lakini wao ambacho hawakujua ni kuwa Yesu yeye ndo anaye tazama mioyo kabla hawajafika. *Ukisoma torati ya Musa unaweza dhani walikuwa wameenda kwa nia njema lkn kumbe lengo ni kumtega.* *Na kwa sababu walienda kwa mtego Yesu naye akawapa jibu la mtego vile vile kuwa yeyote asiye na dhambi na awe wa kwanza kumpiga huyu mtu.* Yohana 8:7 [7]Nao walipozidi kumhoji, alijiinua, akawaambia, Yeye asiye na dhambi miongoni mwenu na awe wa kwanza wa kumtupia jiwe. Yes kabla ujamshitaki mwingine lazima ujiangalie vipi kuhusu wewe hawa walikuwa washitaki wazuri lakini kumbe bado na wao ni wadhinifu tu. *Jiulize wewe ambaye unajiona malaika vipi wewe una dhambi yeyote kweli ni kweli umevuka zinaa lakini mbona wivu na husda bado unao* Baada ya hapo Yesu anampa njia impasayo *wokovu Nenda zako usitende dhambi tena* Kumbe njia nzuri si kumuhukumu mtu kwa kumpiga mawe badala yake mpe njia ya kushinda hiyo zinaa. Sababu ya kusema wengine kumeharibu mwili w Kristo hasa watu wanao jifanya wana kirohost wakati ni mafarisayo. Ukimkuta ndugu yako anadumbukia shimoni msaidie atoke si kwenda kumtangaza na kumbe huyo mtu kaokoka wiki moja mfuate mtie moyo na mpe njia uliyo tumia kushinda dhambi nayeye ajifunze na hapo ndipo tutita Upendo wa kristo. *Siyo unapeleka kwa mchungaji arafu nyuma ya pazia unamtega mchungaji akiamua kumfukuza upate la kumsema akimuonya upate la kumsema.* *Dada angu usikubali maneno ya watu na mashitaka ya watu yakukosanishe Mungu ni ukianguka mrudie Bwana ambaye atasimama na wewe na kukusamehe na kukupa onyo ,* Walokole wengi tumepoteza radha ya wokovu kwa majungu na kujihesabia sana haki kumbe ni sadukayo na farisayo. Kukulia machinjioni haimaanishi lazima ujue kuchinjz nyama kumbe hata wewe dada wengine unawaona wamesimama leo ni kwasababu waliamua kujifunza nq si kutumia uzoefu.. Naweza kwambia kuwa Yesu anakuja ni muhimu kutengeneza. Ahsante.naitwa Sylvester Mwakabende wa BUILD NEW EDEN #RESTORE MEN POSITION
    0 Kommentare ·0 Anteile ·819 Ansichten
  • Rais wa zamani wa Marekani , Barack Obama katika mahojiano na chuo cha Hamilton College Nchini humo aliongea kuhusu hali ya Nchi chini ya muhula wa pili wa Rais wa sasa Donald Trump na alikosoa vikali hatua za hivi karibuni za utawala huo.

    Rais huyo Mstaafu ambaye alitangulia muhula wa kwanza wa Trump, alimkosoa vikali Trump kwa juhudi zake za kubadilisha mfumo wa Serikali ya Shirikisho, kukandamiza uhamiaji na upinzani, pamoja na kuwatisha Wanahabari na Taasisi ya sheria.

    “Hivyo basi, hii ndio mara yangu ya kwanza kuzungumza hadharani kwa muda sasa,” Obama alisema wakati wa mahojiano jukwaani katika Chuo cha Hamilton. “Nimekuwa nikitazama kwa muda.”

    "Hebu fikiria kama ningekuwa nimefanya chochote kati ya haya,”

    “Ni jambo lisilowezekana kufikirika kwamba vyama vilevile vinavyonyamaza sasa vingevumilia tabia kama hiyo kutoka kwangu, au hata kutoka kwa baadhi ya walionitangulia.” alisema Obama

    Obama aliendelea kusema kuwa haamini tangazo jipya la ushuru lililotolewa na Trump “litakuwa zuri kwa Marekani.” Hata hivyo, alieleza kuwa anahofia zaidi kile alichokiita kama uvunjaji wa haki unaofanywa na Ikulu.

    Rais wa zamani wa Marekani 🇺🇸, Barack Obama katika mahojiano na chuo cha Hamilton College Nchini humo aliongea kuhusu hali ya Nchi chini ya muhula wa pili wa Rais wa sasa Donald Trump na alikosoa vikali hatua za hivi karibuni za utawala huo. Rais huyo Mstaafu ambaye alitangulia muhula wa kwanza wa Trump, alimkosoa vikali Trump kwa juhudi zake za kubadilisha mfumo wa Serikali ya Shirikisho, kukandamiza uhamiaji na upinzani, pamoja na kuwatisha Wanahabari na Taasisi ya sheria. “Hivyo basi, hii ndio mara yangu ya kwanza kuzungumza hadharani kwa muda sasa,” Obama alisema wakati wa mahojiano jukwaani katika Chuo cha Hamilton. “Nimekuwa nikitazama kwa muda.” "Hebu fikiria kama ningekuwa nimefanya chochote kati ya haya,” “Ni jambo lisilowezekana kufikirika kwamba vyama vilevile vinavyonyamaza sasa vingevumilia tabia kama hiyo kutoka kwangu, au hata kutoka kwa baadhi ya walionitangulia.” alisema Obama Obama aliendelea kusema kuwa haamini tangazo jipya la ushuru lililotolewa na Trump “litakuwa zuri kwa Marekani.” Hata hivyo, alieleza kuwa anahofia zaidi kile alichokiita kama uvunjaji wa haki unaofanywa na Ikulu.
    Love
    Like
    3
    · 0 Kommentare ·0 Anteile ·787 Ansichten
  • Meneja wa Uwanja wa Benjamin Mkapa amekubali kujiweka pembeni kwenye kusimamia Uwanja baada ya ombi la Wazee wa klabu ya Simba SC kumtaka kufanya hivyo mpaka mwisho wa mchezo wa mkondo wa pili wa robo fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika (CAF Confederation Cup) Kati ya Simba SC dhidi ya All Masry ya Misri utakaochezwa keshokutwa April 9, 2025

    Wazee wa klabu ya Simba SC walienda kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa asubuhi wakimtaka Meneja wa Uwanja huo kuondoka mara moja kwa sababu hawana imani naye wakihofia kuwa anaweza kuwahujumu kwenye mchezo wao dhidi ya klabu ya Al Masry. Wazee hao wanadai kuwa hata mchezo wao dhidi ya klabu ya Yanga SC ulioahirishwa chanzo ilikuwa yeye Meneja

    Meneja wa Uwanja wa Benjamin Mkapa amekubali kujiweka pembeni kwenye kusimamia Uwanja baada ya ombi la Wazee wa klabu ya Simba SC kumtaka kufanya hivyo mpaka mwisho wa mchezo wa mkondo wa pili wa robo fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika (CAF Confederation Cup) Kati ya Simba SC dhidi ya All Masry ya Misri 🇪🇬 utakaochezwa keshokutwa April 9, 2025 Wazee wa klabu ya Simba SC walienda kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa asubuhi wakimtaka Meneja wa Uwanja huo kuondoka mara moja kwa sababu hawana imani naye wakihofia kuwa anaweza kuwahujumu kwenye mchezo wao dhidi ya klabu ya Al Masry. Wazee hao wanadai kuwa hata mchezo wao dhidi ya klabu ya Yanga SC ulioahirishwa chanzo ilikuwa yeye Meneja
    Like
    1
    · 0 Kommentare ·0 Anteile ·630 Ansichten
  • Najua umesalitiwa na wale uliowaamini, umeachwa ulipohitaji kupendwa, na umedhihakiwa wakati ulichotaka ni kuungwa mkono. Najua umechoka. Najua umepigana vita hakuna mtu aliyeona, kulia kimya, na kuvumilia maumivu ambayo maneno hayawezi kuelezea.

    Maisha hayajakuwa sawa kwako. Milango imegongwa usoni mwako. Umewatazama wengine wakiinuka huku wewe ukiwa umekwama katika sehemu moja. Umeomba, kutumaini, na kungoja, lakini hakuna kinachoonekana kubadilika. Inaumiza. Ni chungu. Inachosha.

    Lakini nisikilizeni, na nisikilize kwa makini: USIKATE TAMAA.

    Kila mtu mkubwa unayekuvutia leo alikuwa hapo ulipo sasa. Walihisi kile unachohisi. Walihangaika, walilia, na walitilia shaka wenyewe. Lakini hawakuacha. Hawakuruhusu maumivu yao yawafafanue. Waliendelea kusonga mbele, hata pale nguvu zao zilipopungua. Na ndio maana leo, ulimwengu unawaadhimisha.

    Lazima uelewe ukweli huu: Kadiri hatima yako inavyokuwa kubwa, ndivyo vita yako inavyokuwa kubwa. KILA KIWANGO KIPYA UNACHOFIKIA, KUNA SHETANI MPYA ANAKUSUBIRI. Ulipokuwa maskini, hakuna aliyekuonea wivu. Lakini unapoanza kufanya maendeleo, ghafla, watu wanaanza kukuchukia. Ulipokuwa huna kazi, hakuna aliyezungumza juu yako. Lakini mara tu unapopata kazi nzuri, wanaanza kueneza uvumi. Ulipokuwa ukihangaika, hakuna aliyejali. Lakini wakati unapoanza kufanikiwa, maadui huonekana kutoka popote.

    Ibilisi hapigani na watu ambao hawaendi popote. Sababu ya wewe kukabiliwa na vita vingi ni kwa sababu hatima yako ni kubwa; sababu ya maisha kukujaribu sana ni kwa sababu kesho yako ni kubwa. Huna mateso kwa sababu wewe ni dhaifu. Unateseka kwa sababu wewe ni IMARA, na maisha yanajua kwamba mara tu unapopitia, hautazuilika.

    Kwa hivyo, usikatishwe tamaa na vita unavyokabili sasa. Wao ni ishara kwamba unasonga mbele. Usiruhusu maumivu yakufanye uchungu. Usiruhusu tamaa kuua ndoto zako. Endelea kupigana. Endelea kusukuma. Endelea kuamini. Wakati wako utafika.

    Kuna toleo lako katika siku zijazo ambalo lina nguvu zaidi, busara, na mafanikio zaidi kuliko wewe sasa. Toleo hilo lako linasubiri. Lakini ili kuwa mtu huyo, lazima upitie moto huu. Sio rahisi, lakini nakuahidi, itafaa.

    Lia ikiwa ni lazima, lakini baada ya kulia, futa machozi yako na uendelee kusonga. Lalamika ikibidi, lakini baada ya kulalamika, simama na upigane tena. Jisikie dhaifu ikiwa ni lazima, lakini usiache kujaribu.

    Wakati wako unakuja. Ufanisi wako umekaribia. Maumivu hayatadumu milele. Siku moja, utaangalia nyuma na kugundua kuwa kila kitu ulichopitia kilikufanya kuwa mtu mwenye nguvu, aliyefanikiwa ambaye unakusudiwa kuwa.

    Kwa hivyo, endelea kusonga mbele. Ushindi wako uko njiani.

    Quadic Bangura
    Najua umesalitiwa na wale uliowaamini, umeachwa ulipohitaji kupendwa, na umedhihakiwa wakati ulichotaka ni kuungwa mkono. Najua umechoka. Najua umepigana vita hakuna mtu aliyeona, kulia kimya, na kuvumilia maumivu ambayo maneno hayawezi kuelezea. Maisha hayajakuwa sawa kwako. Milango imegongwa usoni mwako. Umewatazama wengine wakiinuka huku wewe ukiwa umekwama katika sehemu moja. Umeomba, kutumaini, na kungoja, lakini hakuna kinachoonekana kubadilika. Inaumiza. Ni chungu. Inachosha. Lakini nisikilizeni, na nisikilize kwa makini: USIKATE TAMAA. Kila mtu mkubwa unayekuvutia leo alikuwa hapo ulipo sasa. Walihisi kile unachohisi. Walihangaika, walilia, na walitilia shaka wenyewe. Lakini hawakuacha. Hawakuruhusu maumivu yao yawafafanue. Waliendelea kusonga mbele, hata pale nguvu zao zilipopungua. Na ndio maana leo, ulimwengu unawaadhimisha. Lazima uelewe ukweli huu: Kadiri hatima yako inavyokuwa kubwa, ndivyo vita yako inavyokuwa kubwa. KILA KIWANGO KIPYA UNACHOFIKIA, KUNA SHETANI MPYA ANAKUSUBIRI. Ulipokuwa maskini, hakuna aliyekuonea wivu. Lakini unapoanza kufanya maendeleo, ghafla, watu wanaanza kukuchukia. Ulipokuwa huna kazi, hakuna aliyezungumza juu yako. Lakini mara tu unapopata kazi nzuri, wanaanza kueneza uvumi. Ulipokuwa ukihangaika, hakuna aliyejali. Lakini wakati unapoanza kufanikiwa, maadui huonekana kutoka popote. Ibilisi hapigani na watu ambao hawaendi popote. Sababu ya wewe kukabiliwa na vita vingi ni kwa sababu hatima yako ni kubwa; sababu ya maisha kukujaribu sana ni kwa sababu kesho yako ni kubwa. Huna mateso kwa sababu wewe ni dhaifu. Unateseka kwa sababu wewe ni IMARA, na maisha yanajua kwamba mara tu unapopitia, hautazuilika. Kwa hivyo, usikatishwe tamaa na vita unavyokabili sasa. Wao ni ishara kwamba unasonga mbele. Usiruhusu maumivu yakufanye uchungu. Usiruhusu tamaa kuua ndoto zako. Endelea kupigana. Endelea kusukuma. Endelea kuamini. Wakati wako utafika. Kuna toleo lako katika siku zijazo ambalo lina nguvu zaidi, busara, na mafanikio zaidi kuliko wewe sasa. Toleo hilo lako linasubiri. Lakini ili kuwa mtu huyo, lazima upitie moto huu. Sio rahisi, lakini nakuahidi, itafaa. Lia ikiwa ni lazima, lakini baada ya kulia, futa machozi yako na uendelee kusonga. Lalamika ikibidi, lakini baada ya kulalamika, simama na upigane tena. Jisikie dhaifu ikiwa ni lazima, lakini usiache kujaribu. Wakati wako unakuja. Ufanisi wako umekaribia. Maumivu hayatadumu milele. Siku moja, utaangalia nyuma na kugundua kuwa kila kitu ulichopitia kilikufanya kuwa mtu mwenye nguvu, aliyefanikiwa ambaye unakusudiwa kuwa. Kwa hivyo, endelea kusonga mbele. Ushindi wako uko njiani. Quadic Bangura
    Love
    1
    · 0 Kommentare ·0 Anteile ·1KB Ansichten
  • BODI YA LIGI SIO CHOMBO HURU KWA MUJIBU WA RAIS WA TFF WALLECE KARIA.

    Dhumuni la Baba wa Taifa kupigania uhuru wa Tanganyika ilikuwa kuhitaji Tanganyika kuwa huru ili iweze kujiamulia mambo yake na kujipangia kipi ifanye kwa wakati wowote.

    Uhuru ni Jambo la msingi sana kwa binadamu yoyote kwani humsaidia katika kufanya maamuzi yake binafsi.

    Kwa mujibu wa kauli za Rais wa TFF Baba Yangu Mzee Wallece Karia ni dhahiri shahiri kuwa bodi ya ligi sio chombo huru.

    Wallece Karia akiwa katika mahojiano Wasafi Fm katika kipindi cha “Jana na Leo” Alisema kuwa

    “Kuna siku tulipokea Barua kutoka CAF Wakihitaji waamuzi wetu Wawili kwenda kuchezesha michuano ya kimataifa”

    “Wakati barua ile imekuja ofisini kuhitaji wale waamuzi kulikuwa na changamoto, Kwani mojawapo ya wale waamuzi ambae ni Ahmed Arajiga alikuwa amefungiwa na kamati ya masaa 72”

    “Ilikuwa ngumu sana kwangu, maana CAF wamemtaka mwamuzi alafu huku kwetu kamati imemfungia, lakini nikafanya maamuzi”

    “Nilifanya maamuzi nikawaambia hawa waamuzi waruhusiwe waende, Walienda wote wawili lakini bahati mbaya mmoja ndio alifuzu ambae ni Ahmed Arajiga”

    “Yalikuwa maamuzi magumu ila sikuwa na namna n Ahmed Arajiga alienda kuwakilisha Tanzania vema sana, Hata mechi aliyochezesha alichezesha vizuri sana”

    Kwa maelezo ya Wallece Karia aliingilia maamuzi ya Kamati ya Masaa 72 ambayo ipo chini ya bodi ya ligi. Kumruhusu Mwamuzi aliyefungiwa katika ligi kwenda kuchezesha mechi za kimataifa.
    (khalil ufadiga)

    BODI YA LIGI SIO CHOMBO HURU KWA MUJIBU WA RAIS WA TFF WALLECE KARIA. Dhumuni la Baba wa Taifa kupigania uhuru wa Tanganyika ilikuwa kuhitaji Tanganyika kuwa huru ili iweze kujiamulia mambo yake na kujipangia kipi ifanye kwa wakati wowote. Uhuru ni Jambo la msingi sana kwa binadamu yoyote kwani humsaidia katika kufanya maamuzi yake binafsi. Kwa mujibu wa kauli za Rais wa TFF Baba Yangu Mzee Wallece Karia ni dhahiri shahiri kuwa bodi ya ligi sio chombo huru. Wallece Karia akiwa katika mahojiano Wasafi Fm katika kipindi cha “Jana na Leo” Alisema kuwa “Kuna siku tulipokea Barua kutoka CAF Wakihitaji waamuzi wetu Wawili kwenda kuchezesha michuano ya kimataifa” “Wakati barua ile imekuja ofisini kuhitaji wale waamuzi kulikuwa na changamoto, Kwani mojawapo ya wale waamuzi ambae ni Ahmed Arajiga alikuwa amefungiwa na kamati ya masaa 72” “Ilikuwa ngumu sana kwangu, maana CAF wamemtaka mwamuzi alafu huku kwetu kamati imemfungia, lakini nikafanya maamuzi” “Nilifanya maamuzi nikawaambia hawa waamuzi waruhusiwe waende, Walienda wote wawili lakini bahati mbaya mmoja ndio alifuzu ambae ni Ahmed Arajiga” “Yalikuwa maamuzi magumu ila sikuwa na namna n Ahmed Arajiga alienda kuwakilisha Tanzania vema sana, Hata mechi aliyochezesha alichezesha vizuri sana” Kwa maelezo ya Wallece Karia aliingilia maamuzi ya Kamati ya Masaa 72 ambayo ipo chini ya bodi ya ligi. Kumruhusu Mwamuzi aliyefungiwa katika ligi kwenda kuchezesha mechi za kimataifa. (khalil ufadiga)
    0 Kommentare ·0 Anteile ·893 Ansichten
  • Jeshi la Polisi katika Kaunti ya Uasin Gishu Nchini Kenya wameanzisha uchunguzi baada ya Mwanamume mmoja kuanzisha kituo kidogo cha Polisi kinyume cha sheria na bila idhini ya mamlaka Nchini humo. Ripoti zinasema kuwa Mwanaume huyo wa Kijiji cha Asis alijipa jukumu la kufungua kituo hicho na kupaka rangi rasmi za Jeshi la Polisi

    Mamlaka bado hazijabaini sababu za Mshukiwa kuanzisha kituo hicho na amekamatwa kwa uchunguzi zaidi huku Wananchi wa eneo hilo wakishindwa kubaini kuwa kituo hicho kilikuwa "feki" badala yake waliendelea kupatiwa huduma wakidhani kuwa Jeshi la Polisi limesogezea huduma hiyo karibu ili kulinda usalama wa eneo hilo.

    Jeshi la Polisi katika Kaunti ya Uasin Gishu Nchini Kenya 🇰🇪 wameanzisha uchunguzi baada ya Mwanamume mmoja kuanzisha kituo kidogo cha Polisi kinyume cha sheria na bila idhini ya mamlaka Nchini humo. Ripoti zinasema kuwa Mwanaume huyo wa Kijiji cha Asis alijipa jukumu la kufungua kituo hicho na kupaka rangi rasmi za Jeshi la Polisi Mamlaka bado hazijabaini sababu za Mshukiwa kuanzisha kituo hicho na amekamatwa kwa uchunguzi zaidi huku Wananchi wa eneo hilo wakishindwa kubaini kuwa kituo hicho kilikuwa "feki" badala yake waliendelea kupatiwa huduma wakidhani kuwa Jeshi la Polisi limesogezea huduma hiyo karibu ili kulinda usalama wa eneo hilo.
    Like
    1
    · 0 Kommentare ·0 Anteile ·885 Ansichten
  • Mazungunzo kati ya Rais wa Marekani , Donald Trump na Rais wa Ukraine , Volorymyr Zelensky yameishia njiani baada ya kushindwa kuelewana kuhusu hatima ya vita ya Russia dhidi ya Ukraine. Ilianza kama utani wakati wa kikao hicho ambacho kimehudhuriwa na Makamu wa Rais wa Marekani JD Vance na Waandishi wa Habari.

    Kila upande ulianza kuelezea kile ambacho wamejadiliana kuhusiana na makubaliano yaliyokuwa yanatarajiwa kutiwa saini. Awali Trump alieleza kuwa makubaliano hayo ni pamoja na kusaini mkataba unaoiruhusu Marekani kuchimba madini adimu (rare minerals) katika ardhi ya Ukraine.

    Wakati mrejesho wa hatua iliyofikiwa kuhusu makubaliano hayo ya mkataba wa madini mambo yalikuwa sawa ila yakaanza kwenda mrama pale Trump alipohamisha mada na kuingia suala la kupata mwafaka wa mzozo kati ya Ukraine na Russia ya Vladimir Putin.

    Trump kwenye suala hilo alienda moja kwa moja na kumtaka Rais Zelensky, kuingia makubaliano na Russia ya kumaliza vita hivyo, la sivyo Marekani itajindoa katika mazungumzo hayo na haitoendelea kuifadhili tena wala kuipatia misaada Ukraine. Wawili hao walikatizana mara kwa mara wakati wa majibizano yao kwa namna isiyo ya kawaida ndani ya Marekani (White House).

    Mazungunzo kati ya Rais wa Marekani 🇺🇸, Donald Trump na Rais wa Ukraine 🇺🇦, Volorymyr Zelensky yameishia njiani baada ya kushindwa kuelewana kuhusu hatima ya vita ya Russia 🇷🇺 dhidi ya Ukraine. Ilianza kama utani wakati wa kikao hicho ambacho kimehudhuriwa na Makamu wa Rais wa Marekani JD Vance na Waandishi wa Habari. Kila upande ulianza kuelezea kile ambacho wamejadiliana kuhusiana na makubaliano yaliyokuwa yanatarajiwa kutiwa saini. Awali Trump alieleza kuwa makubaliano hayo ni pamoja na kusaini mkataba unaoiruhusu Marekani kuchimba madini adimu (rare minerals) katika ardhi ya Ukraine. Wakati mrejesho wa hatua iliyofikiwa kuhusu makubaliano hayo ya mkataba wa madini mambo yalikuwa sawa ila yakaanza kwenda mrama pale Trump alipohamisha mada na kuingia suala la kupata mwafaka wa mzozo kati ya Ukraine na Russia ya Vladimir Putin. Trump kwenye suala hilo alienda moja kwa moja na kumtaka Rais Zelensky, kuingia makubaliano na Russia ya kumaliza vita hivyo, la sivyo Marekani itajindoa katika mazungumzo hayo na haitoendelea kuifadhili tena wala kuipatia misaada Ukraine. Wawili hao walikatizana mara kwa mara wakati wa majibizano yao kwa namna isiyo ya kawaida ndani ya Marekani (White House).
    Like
    1
    · 0 Kommentare ·0 Anteile ·709 Ansichten
  • (E)
    Kwa miaka mingi, Shipman aliendelea na mauaji yake bila kugundulika.

    Lakini mnamo 1998, alifanya kosa moja kubwa—alijaribu kughushi wosia wa mgonjwa wake mmoja, Kathleen Grundy.

    Kathleen alikuwa mama mwenye afya njema mwenye umri wa miaka 81. Alipoaga dunia ghafla, binti yake, Angela Woodruff, alishangazwa na jinsi kifo hicho kilivyotokea bila onyo.

    Lakini mshangao mkubwa zaidi ulikuja alipogundua kuwa mama yake alikuwa ameandika wosia mpya, ukisema kuwa mali yake yote iende kwa daktari wake—Harold Shipman!

    Huo ulikuwa ushahidi wa kwanza wa kweli kwamba huyu hakuwa daktari wa kawaida—alikuwa muuaji.
    (E) Kwa miaka mingi, Shipman aliendelea na mauaji yake bila kugundulika. Lakini mnamo 1998, alifanya kosa moja kubwa—alijaribu kughushi wosia wa mgonjwa wake mmoja, Kathleen Grundy. Kathleen alikuwa mama mwenye afya njema mwenye umri wa miaka 81. Alipoaga dunia ghafla, binti yake, Angela Woodruff, alishangazwa na jinsi kifo hicho kilivyotokea bila onyo. Lakini mshangao mkubwa zaidi ulikuja alipogundua kuwa mama yake alikuwa ameandika wosia mpya, ukisema kuwa mali yake yote iende kwa daktari wake—Harold Shipman! Huo ulikuwa ushahidi wa kwanza wa kweli kwamba huyu hakuwa daktari wa kawaida—alikuwa muuaji.
    Like
    1
    · 0 Kommentare ·0 Anteile ·884 Ansichten
  • “Ukiwa Mwandishi wa Habari una vitu viwili muhimu vya kuchunga navyo ni Ulimi wako na Mikono yako, unapaswa kufahamu unaongea nini ama unaandika kitu gani, nyuma ya mauaji ya Kimbari yalikuwa ni matamshi ya Watangazaji pia ambao walieneza chuki, kwasasa kuna kazi mbili za hatari nazo ni Ualimu na Waandishi wa Habari, hawa wanaweza kutengeneza taifa la Wajinga ama Waelevu.

    Nataka kusema nini? Nataka kusema juu ya kelele na shutuma za Yanga na Singida bado hakuna aliyetupa picha kamili zaidi ni kuwa Mashabiki wanalalamika kwa hisia, Waandishi tunalalamika kwa hisia ila hakuna anayekuja mbele kutoa usahihi, inaitwa Proving beyond reasonable doubt! Nimeona Wadau wanasema TFF haifanyi chochote, lakini wewe umewapa tip gani? Taasisi haifanyi maamuzi kwa hisia, the corporate world works differently from streets.

    Bado kizazi chetu cha Uandishi kuna kitu kinamiss ni INVESTIGATIVE JOURNALISM, binafsi nakiri wazi TUMEFELI sana eneo hili, yaani sote tunalaumu Singida kufanya rotation tunaita kupanga matokeo, tangu lini duniani kubadili kikosi chako ni kupanga matokeo? Ikitokea Coastal kabadili kikosi, ikitokea Simba kabadili ama AZAM? Yani timu inalaumiwa kwa kutumia Wachezaji wake?

    Tunaweza kuwa na hoja ila mpaka sasa hazina mashiko zaidi tunaonekana tunalalama ila tukipelekwa Mahakamani hakuna ambaye atathibitisha chochote, kama kufungwa ni kupanga matokeo mara ya mwisho Simba kumfunga Yanga ndani ya dakika 90 ni lini? Kama kufungwa ni kupanga matokeo lini Singida kamfunga Simba? Kama kufungwa ni kupanga lini Namungo kamfunga Simba lini?

    Sisi WAANDISHI tuna homework tunapaswa kufanya, tutaharibu fikra za Watanzania! Wenzetu Ulaya walipoibua kashfa ya Casciopoli pale Italia walikuja na data, hata UEFA Heated Balls Scandal watu walikuwa na data! Yanga wakisema waende kisheria nani anaweza kuja na hoja za kueleweka? Kama hakuna taarifa sahihi, mifano hai basi tunaongelea hisia, TFF atareact endapo atajitokea Mtu akaattack matter not the subject" - Farhan JR, Mchambuzi.

    “Ukiwa Mwandishi wa Habari una vitu viwili muhimu vya kuchunga navyo ni Ulimi wako na Mikono yako, unapaswa kufahamu unaongea nini ama unaandika kitu gani, nyuma ya mauaji ya Kimbari yalikuwa ni matamshi ya Watangazaji pia ambao walieneza chuki, kwasasa kuna kazi mbili za hatari nazo ni Ualimu na Waandishi wa Habari, hawa wanaweza kutengeneza taifa la Wajinga ama Waelevu. Nataka kusema nini? Nataka kusema juu ya kelele na shutuma za Yanga na Singida bado hakuna aliyetupa picha kamili zaidi ni kuwa Mashabiki wanalalamika kwa hisia, Waandishi tunalalamika kwa hisia ila hakuna anayekuja mbele kutoa usahihi, inaitwa Proving beyond reasonable doubt! Nimeona Wadau wanasema TFF haifanyi chochote, lakini wewe umewapa tip gani? Taasisi haifanyi maamuzi kwa hisia, the corporate world works differently from streets. Bado kizazi chetu cha Uandishi kuna kitu kinamiss ni INVESTIGATIVE JOURNALISM, binafsi nakiri wazi TUMEFELI sana eneo hili, yaani sote tunalaumu Singida kufanya rotation tunaita kupanga matokeo, tangu lini duniani kubadili kikosi chako ni kupanga matokeo? Ikitokea Coastal kabadili kikosi, ikitokea Simba kabadili ama AZAM? Yani timu inalaumiwa kwa kutumia Wachezaji wake? Tunaweza kuwa na hoja ila mpaka sasa hazina mashiko zaidi tunaonekana tunalalama ila tukipelekwa Mahakamani hakuna ambaye atathibitisha chochote, kama kufungwa ni kupanga matokeo mara ya mwisho Simba kumfunga Yanga ndani ya dakika 90 ni lini? Kama kufungwa ni kupanga matokeo lini Singida kamfunga Simba? Kama kufungwa ni kupanga lini Namungo kamfunga Simba lini? Sisi WAANDISHI tuna homework tunapaswa kufanya, tutaharibu fikra za Watanzania! Wenzetu Ulaya walipoibua kashfa ya Casciopoli pale Italia walikuja na data, hata UEFA Heated Balls Scandal watu walikuwa na data! Yanga wakisema waende kisheria nani anaweza kuja na hoja za kueleweka? Kama hakuna taarifa sahihi, mifano hai basi tunaongelea hisia, TFF atareact endapo atajitokea Mtu akaattack matter not the subject" - Farhan JR, Mchambuzi.
    0 Kommentare ·0 Anteile ·1KB Ansichten
  • Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo , Félix Tshisekedi, amemshutumu kwa mara nyingine tena Mtangulizi wake Joseph Kabila kuwa anaunga mkono Kundi la Waasi la M23. Mnamo Agosti 2024, Tshisekedi alidai kuwa Kabila alikuwa nyuma ya kuunganishwa kwa muungano wa Wakuu wa kisiasa wa (AFC) unaoongozwa na Corneille Nangaa na Wapiganaji wa kundi la M23.

    Katika mahojiano, Tshisekedi alisema sababu iliyofanya Kabila kutoshiriki uchaguzi wa Desemba 2024 ni kwa sababu alikuwa na shughuli nyingi na AFC.

    “Tusimzungumzie Joseph Kabila. Amekataa kabisa kugombea uchaguzi na anajipanga kupambana na serikali kwa sababu yeye ni AFC.” - alisema Tshisekedi

    Rais huyo ameyasema hayo tena katika Baraza la Usalama la Kimataifa Mjini Munich Nchini Ujerumani Februari 14, 2025, ya kwamba Kabila alienda uhamishoni kwa sababu anafadhili Waasi wa (AFC) ikiwemo Kundi la Waasi la M23.

    Hata hivyo, Chama cha Joseph Kabila cha (PPRD) kimekanusha vikali matamshi ya Rais Félix Tshisekedi kwa kusema kuwa Kiongozi wao hausiki na Kundi hilo la Waasi.

    Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo 🇨🇩, Félix Tshisekedi, amemshutumu kwa mara nyingine tena Mtangulizi wake Joseph Kabila kuwa anaunga mkono Kundi la Waasi la M23. Mnamo Agosti 2024, Tshisekedi alidai kuwa Kabila alikuwa nyuma ya kuunganishwa kwa muungano wa Wakuu wa kisiasa wa (AFC) unaoongozwa na Corneille Nangaa na Wapiganaji wa kundi la M23. Katika mahojiano, Tshisekedi alisema sababu iliyofanya Kabila kutoshiriki uchaguzi wa Desemba 2024 ni kwa sababu alikuwa na shughuli nyingi na AFC. “Tusimzungumzie Joseph Kabila. Amekataa kabisa kugombea uchaguzi na anajipanga kupambana na serikali kwa sababu yeye ni AFC.” - alisema Tshisekedi Rais huyo ameyasema hayo tena katika Baraza la Usalama la Kimataifa Mjini Munich Nchini Ujerumani 🇩🇪 Februari 14, 2025, ya kwamba Kabila alienda uhamishoni kwa sababu anafadhili Waasi wa (AFC) ikiwemo Kundi la Waasi la M23. Hata hivyo, Chama cha Joseph Kabila cha (PPRD) kimekanusha vikali matamshi ya Rais Félix Tshisekedi kwa kusema kuwa Kiongozi wao hausiki na Kundi hilo la Waasi.
    Like
    1
    · 0 Kommentare ·0 Anteile ·703 Ansichten
  • Mapigano yamezuka tena kati ya Kundi la Waasi wa M23 na Vikosi vya Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo kusini mwa Mkoa wa Kivu, licha ya tangazo la Waasi hao la kusitisha mapigano kwa sababu za kibinadamu.

    Ripoti kutoka eneo la Nyabibwe, Kalehe, zinasema kuwa mapigano yaliendelea mapema leo baada ya kundi la Waasi hao kushambulia maeneo yanayodhibitiwa na Serikali. Ikumbukwe kwamba siku ya Jumatatu, Waasi walitangaza kusitisha mapigano na kusema kuwa hawakuwa na nia ya kuchukua maeneo yoyote baada ya kuteka Mji wa Goma.

    Hata hivyo, mamlaka ya Nchi ya DR Congo inasema shambulio hilo linakiuka makubaliano ya kusitisha mapigano yaliyotolewa na Waasi siku mbili (3) zilizopita. Baada ya kuushikilia Mji wa Goma, Waasi wa M23 walikusudia kuteka Mji wa Bukavu ambao ni Mji Mkuu wa Mkoa wa Sud-Kivu, lakini walikumbana na upinzani mkali kutoka kwa Vikosi vya Serikali ya DR Congo na Burundi , ambao walirejesha Vijiji kadhaa vilivyokuwa vimetekwa na Waasi hao.

    Serikali ya DR Congo imeanzisha juhudi za kusajili Raia kujiunga na Vikosi vya Jeshi ili kuimarisha ulinzi wa Mji wa Bukavu na maeneo mengine yaliyo hatarini katika Jimboni Kivu Kusini.

    Mapigano yamezuka tena kati ya Kundi la Waasi wa M23 na Vikosi vya Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo 🇨🇩 kusini mwa Mkoa wa Kivu, licha ya tangazo la Waasi hao la kusitisha mapigano kwa sababu za kibinadamu. Ripoti kutoka eneo la Nyabibwe, Kalehe, zinasema kuwa mapigano yaliendelea mapema leo baada ya kundi la Waasi hao kushambulia maeneo yanayodhibitiwa na Serikali. Ikumbukwe kwamba siku ya Jumatatu, Waasi walitangaza kusitisha mapigano na kusema kuwa hawakuwa na nia ya kuchukua maeneo yoyote baada ya kuteka Mji wa Goma. Hata hivyo, mamlaka ya Nchi ya DR Congo inasema shambulio hilo linakiuka makubaliano ya kusitisha mapigano yaliyotolewa na Waasi siku mbili (3) zilizopita. Baada ya kuushikilia Mji wa Goma, Waasi wa M23 walikusudia kuteka Mji wa Bukavu ambao ni Mji Mkuu wa Mkoa wa Sud-Kivu, lakini walikumbana na upinzani mkali kutoka kwa Vikosi vya Serikali ya DR Congo na Burundi 🇧🇮, ambao walirejesha Vijiji kadhaa vilivyokuwa vimetekwa na Waasi hao. Serikali ya DR Congo imeanzisha juhudi za kusajili Raia kujiunga na Vikosi vya Jeshi ili kuimarisha ulinzi wa Mji wa Bukavu na maeneo mengine yaliyo hatarini katika Jimboni Kivu Kusini.
    Like
    1
    · 0 Kommentare ·0 Anteile ·630 Ansichten
  • #PART11

    Baada ya Ntaganda kupelekwa The Heague, M23 iliongozwa na Sultan Makenga, Mtutsi wa Rutshuru huko Kivu Kaskazini. Mwaka 1990 Makenga akiwa na miaka 17 tu alienda Rwanda kujiunga na kikundi cha waasi RPF kilichokuwa kinaongozwa na Jenerali Fredy Rwigyema. Sultan Makenga akiwa askari wa RPF alipigana msituni dhidi ya serikali ya kihutu ya Juvenile Habyarimana.

    Baada RPF ilishika dola, Askari wote wa RPF waliingizwa katika jeshi la Rwanda akiwemo Sultan Makenga. Alihudumu katika jeshi hilo kwa muda mrefu hadi kufikia cheo cha Kanali kabla ya kurudi "nyumbani" Congo, kujiunga na kikundi cha waasi cha CNDP. Baada ya mkataba wa amani wa March 23, 2009 Sultan Makenga alikuwa miongoni mwa askari 600 wa CNDP waliokataa kujiunga na jeshi la Congo (FARDC).

    Mwaka 2012 Bosco Ntaganda alipojitoa kwenye jeshi la Congo na kuunga kikundi cha waasi cha M23, Sultan Makenga alikua wa kwanza kujiunga. Baada ya Ntaganda kujisalimisha, Makenga akapewa uongozi wa M23. Akaongoza kuanzia 2013 hadi 2016 alipotoweka ghafla. Haijulikani alipo, japo inasemekana alienda Rwanda na hakurudi tena.

    Baada ya Makenga kutoweka katika mazingira ya "kutatanisha" M23 ikawa na viongozi ambao hawakuwa mashuhuri sana hadi 2022 ilipompata Corneille Nangaa. Huyu alikua Mwenyekiti wa Tume ya uchaguzi nchini Congo (CENI) na ndiye aliyemtangaza Tshikeshedi kuwa mshindi wa kiti cha Urais wa Congo kwenye uchaguzi wa December 30 mwaka 2018.

    Katika mambo yanayoshangaza na kufanya vita ya Congo kuonekana ngumu, ni jinsi Nangaa alivyotoka kuwa Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi, hadi kuanzisha coalition ya vikundi vya waasi, Congo River Alliance (CRA) kikiwemo M23. Jenerali Nangaa ndiye aliyeongoza M23 kuutwaa mji wa Goma January 2025, na kuyafurusha majeshi ya serikali. Nangaa ametangaza nia ya kumuondoa madarakani Rais Tshisekedi, ambaye mwaka 2018 ni Nangaa huyohuyo aliyemtangaza Tshikeshedi kuwa Rais.

    August 2024 Mahakama ya kijeshi mjini Kinshasa ilimhukumu Nangaa adhabu ya kunyongwa hadi kufa kwa kosa la uhaini. Hukumu hiyo ilitolewa bila yeye kuwepo mahakamani (death sentence in absentia). Nangaa amesema ikiwa M23 itashika dola, wale waliomhukumu ndio watanyongwa kwa niaba yake.!
    (Malisa GJ)

    #PART11 Baada ya Ntaganda kupelekwa The Heague, M23 iliongozwa na Sultan Makenga, Mtutsi wa Rutshuru huko Kivu Kaskazini. Mwaka 1990 Makenga akiwa na miaka 17 tu alienda Rwanda kujiunga na kikundi cha waasi RPF kilichokuwa kinaongozwa na Jenerali Fredy Rwigyema. Sultan Makenga akiwa askari wa RPF alipigana msituni dhidi ya serikali ya kihutu ya Juvenile Habyarimana. Baada RPF ilishika dola, Askari wote wa RPF waliingizwa katika jeshi la Rwanda akiwemo Sultan Makenga. Alihudumu katika jeshi hilo kwa muda mrefu hadi kufikia cheo cha Kanali kabla ya kurudi "nyumbani" Congo, kujiunga na kikundi cha waasi cha CNDP. Baada ya mkataba wa amani wa March 23, 2009 Sultan Makenga alikuwa miongoni mwa askari 600 wa CNDP waliokataa kujiunga na jeshi la Congo (FARDC). Mwaka 2012 Bosco Ntaganda alipojitoa kwenye jeshi la Congo na kuunga kikundi cha waasi cha M23, Sultan Makenga alikua wa kwanza kujiunga. Baada ya Ntaganda kujisalimisha, Makenga akapewa uongozi wa M23. Akaongoza kuanzia 2013 hadi 2016 alipotoweka ghafla. Haijulikani alipo, japo inasemekana alienda Rwanda na hakurudi tena. Baada ya Makenga kutoweka katika mazingira ya "kutatanisha" M23 ikawa na viongozi ambao hawakuwa mashuhuri sana hadi 2022 ilipompata Corneille Nangaa. Huyu alikua Mwenyekiti wa Tume ya uchaguzi nchini Congo (CENI) na ndiye aliyemtangaza Tshikeshedi kuwa mshindi wa kiti cha Urais wa Congo kwenye uchaguzi wa December 30 mwaka 2018. Katika mambo yanayoshangaza na kufanya vita ya Congo kuonekana ngumu, ni jinsi Nangaa alivyotoka kuwa Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi, hadi kuanzisha coalition ya vikundi vya waasi, Congo River Alliance (CRA) kikiwemo M23. Jenerali Nangaa ndiye aliyeongoza M23 kuutwaa mji wa Goma January 2025, na kuyafurusha majeshi ya serikali. Nangaa ametangaza nia ya kumuondoa madarakani Rais Tshisekedi, ambaye mwaka 2018 ni Nangaa huyohuyo aliyemtangaza Tshikeshedi kuwa Rais. August 2024 Mahakama ya kijeshi mjini Kinshasa ilimhukumu Nangaa adhabu ya kunyongwa hadi kufa kwa kosa la uhaini. Hukumu hiyo ilitolewa bila yeye kuwepo mahakamani (death sentence in absentia). Nangaa amesema ikiwa M23 itashika dola, wale waliomhukumu ndio watanyongwa kwa niaba yake.! (Malisa GJ)
    Like
    1
    · 0 Kommentare ·0 Anteile ·1KB Ansichten
  • #PART6

    Alipoingia Ikulu Kabila alifuta jina Zaire na kurudisha Congo (Jamhuri ya kidemokrasia). Baadae alifikiria kuiachia Kivu, eneo lenye utajiri mkubwa wa madini adimu duniani. Akasema "to hell with Lemera Agreement" akautupilia mbali mkataba wa Lemera. Akasema Kivu itabaki Congo na madini ya Kivu yatajenga Congo. Full stop. Ashakuwa Rais utamfanya nini?

    Kagame hakuamini macho yake. Alishawaza jinsi ambavyo Rwanda ingekuwa Dubai ya Afrika kwa rasilimali za Congo. Lakini ghafla aligeukwa na mshirika wake Laurent Désiré Kabila. Akamfuata "Godfather" wake mzee Museveni. Mzee akasema kama katugeuka tumpige. Wakatafuta kikundi cha Waasi wakiunge mkono. Wakapata Rassemblement Congolais pour la Démocratie (RCD), kilichoongozwa na Jenerali Ernest Wamba dia Wamba. Kikundi kikapewa silaha na fedha kikaanza kumshughulikia Kabila.

    RCD ikaanza kuchapana na jeshi la Congo (FARDC) ikiwa na backup ya Rwanda na Uganda. Vita vikapamba moto. Rwanda na Uganda nao wakaingiza majeshi Congo kusaidia waasi wa RCD. Kabila akaona anazidiwa, akaomba msaada Angola na Chad. Nchi hizo zikaleta vikosi vyake Congo. Mapigano yakawa makali sana. Eneo la mashariki mwa Congo likageuka machinjioni. Watu walikufa kwa wingi, mpaka maiti zikatapakaa barabarani bila kuzikwa, zikawa zinadonolewa na ndege.

    Hii iliitwa Vita ya Pili ya Congo (1998–2002), iliyokua mbaya zaidi katika historia ya vita zote Afrika. Imebatizwa jina "Vita Kuu ya Afrika". Inakadiriwa watu laki tano walipoteza maisha huku mamilioni wakikimbia nchi. Mapigano yaliendelea, huku vikosi vya Rwanda na Uganda vikichota madini. Katikati ya mapigano mgongano wa kimaslahi ukajitokeza.

    Jasin Stearns, katika kitabu chake Dancing in the Glory of Monsters, anasema Kagame alishindwa kuelewana na "godfather" wake Museveni juu ya mgawanyo wa mali. Hali hiyo ilifanya kikundi cha RCD kipasuke na kuzaliwa vikundi viwili. Cha kwanza kikajiita RCD-Goma kikiongozwa na Kanali Emile Ilunga (hiki kilisaidiwa na Rwanda) na cha pili kikajiita RCD-Kisangani, kikiongozwa na Jenerali Mbusa Nyamwisi (kikisaidiwa na Uganda).
    (Malisa GJ)

    #PART6 Alipoingia Ikulu Kabila alifuta jina Zaire na kurudisha Congo (Jamhuri ya kidemokrasia). Baadae alifikiria kuiachia Kivu, eneo lenye utajiri mkubwa wa madini adimu duniani. Akasema "to hell with Lemera Agreement" akautupilia mbali mkataba wa Lemera. Akasema Kivu itabaki Congo na madini ya Kivu yatajenga Congo. Full stop. Ashakuwa Rais utamfanya nini? Kagame hakuamini macho yake. Alishawaza jinsi ambavyo Rwanda ingekuwa Dubai ya Afrika kwa rasilimali za Congo. Lakini ghafla aligeukwa na mshirika wake Laurent Désiré Kabila. Akamfuata "Godfather" wake mzee Museveni. Mzee akasema kama katugeuka tumpige. Wakatafuta kikundi cha Waasi wakiunge mkono. Wakapata Rassemblement Congolais pour la Démocratie (RCD), kilichoongozwa na Jenerali Ernest Wamba dia Wamba. Kikundi kikapewa silaha na fedha kikaanza kumshughulikia Kabila. RCD ikaanza kuchapana na jeshi la Congo (FARDC) ikiwa na backup ya Rwanda na Uganda. Vita vikapamba moto. Rwanda na Uganda nao wakaingiza majeshi Congo kusaidia waasi wa RCD. Kabila akaona anazidiwa, akaomba msaada Angola na Chad. Nchi hizo zikaleta vikosi vyake Congo. Mapigano yakawa makali sana. Eneo la mashariki mwa Congo likageuka machinjioni. Watu walikufa kwa wingi, mpaka maiti zikatapakaa barabarani bila kuzikwa, zikawa zinadonolewa na ndege. Hii iliitwa Vita ya Pili ya Congo (1998–2002), iliyokua mbaya zaidi katika historia ya vita zote Afrika. Imebatizwa jina "Vita Kuu ya Afrika". Inakadiriwa watu laki tano walipoteza maisha huku mamilioni wakikimbia nchi. Mapigano yaliendelea, huku vikosi vya Rwanda na Uganda vikichota madini. Katikati ya mapigano mgongano wa kimaslahi ukajitokeza. Jasin Stearns, katika kitabu chake Dancing in the Glory of Monsters, anasema Kagame alishindwa kuelewana na "godfather" wake Museveni juu ya mgawanyo wa mali. Hali hiyo ilifanya kikundi cha RCD kipasuke na kuzaliwa vikundi viwili. Cha kwanza kikajiita RCD-Goma kikiongozwa na Kanali Emile Ilunga (hiki kilisaidiwa na Rwanda) na cha pili kikajiita RCD-Kisangani, kikiongozwa na Jenerali Mbusa Nyamwisi (kikisaidiwa na Uganda). (Malisa GJ)
    Like
    2
    · 0 Kommentare ·0 Anteile ·1KB Ansichten
  • #PART3

    Baadhi ya wanajeshi wa Kitutsi hawakuridhika na ukandamizaji uliofanywa na Habyarimana. Wakajiorganize kupambana. Wakati huo Kagame akiwa askari wa NRA ya Uganda akimsaidia Museveni vita vya msituni. Mwaka 1983 hadi 1985 alienda kozi ya kijeshi TMA, Moduli. Alipohitimu akarudi Uganda kumsaidia Museveni vita vya msituni na hatimaye mwaka 1986 wakafanikiwa kuchukua nchi. NRA ikawa sehemu ya jeshi la Uganda kabla ya kubadilishwa muundo mwaka 1995 kuwa UPDF.

    Kagame akawa mkuu wa intelijensia ya jeshi. Baadae akaenda masomoni Marekani. Akiwa huko RPF ikaanzishwa na Jenerali Fredy Rwigyema kupambana na Serikali ya Habyarimana. Lakini Jenerali Rwigyema akauawa kwa guruneti akiwa uwanja wa vita. Kagame akalazimika kukatisha masomo na kurudi Rwanda kuongoza RPF akishirikiana na Alexis Kanyarwenge. Museveni akampa msaada wa fedha, silaha na chakula. RPF ikaweka kambi Uganda eneo la Kabale, Burundi eneo la Muyinga na Congo maeneo ya Kivu, Uvira na Goma.

    Mwaka 1994, askari wa RPF wakatungua ndege ya Rais Habyarimana ikiwa inakaribia kutua uwanja wa ndege wa Kigali ikitokea Dar es Salaam kwenye mazungumzo ya Amani alikuwa na Rais Cyprien Ntaramira wa Burundi. Wote wawili walikufa papo hapo.

    Kuuawa kwa Rais Habyarimana kuliamsha hasira za Wahutu na kusabisha mauaji ya Kimbari ambapo Watutsi na Wahutu wenye msimamo wa wastani waliuawa kikatili kwa kucharangwa mapanga. Hali hiyo ilisababisha Watutsi wengi kukimbia nchi yao. Wapo waliokimbilia Tanzania, Uganda, lakini wengi zaidi walikimbilia eneo la Kivu.

    Kwa kifupi, idadi ya Watutsi eneo la Kivu iliongezeka siku hadi siku. Watutsi walioenda Kivu wengi hawakurudi Rwanda hata baada ya vita kumalizika. Ilikuwa vigumu kutofautisha Mtutsi mwenye asili ya Congo (Banyamulenge) na Mtutsi wa Rwanda, kwa sababu wote wanaongea lugha moja, mila na desturi moja.

    Kwahiyo hisia za Wakongomani kwamba Banyamulenge ni wageni zikaanza kupata nguvu kutokana na uhamiaji mkubwa wa Watutsi maeneo ya Kivu kaskazini na kusini. Wakati huo Congo ikiitwa Zaire Rais Mobutu Sese Seko alikataa kuwatambua Banyamulenge kama raia wake, na akazuia wasipewe vitambulisho vya taifa.
    (Malisa GJ)

    #PART3 Baadhi ya wanajeshi wa Kitutsi hawakuridhika na ukandamizaji uliofanywa na Habyarimana. Wakajiorganize kupambana. Wakati huo Kagame akiwa askari wa NRA ya Uganda akimsaidia Museveni vita vya msituni. Mwaka 1983 hadi 1985 alienda kozi ya kijeshi TMA, Moduli. Alipohitimu akarudi Uganda kumsaidia Museveni vita vya msituni na hatimaye mwaka 1986 wakafanikiwa kuchukua nchi. NRA ikawa sehemu ya jeshi la Uganda kabla ya kubadilishwa muundo mwaka 1995 kuwa UPDF. Kagame akawa mkuu wa intelijensia ya jeshi. Baadae akaenda masomoni Marekani. Akiwa huko RPF ikaanzishwa na Jenerali Fredy Rwigyema kupambana na Serikali ya Habyarimana. Lakini Jenerali Rwigyema akauawa kwa guruneti akiwa uwanja wa vita. Kagame akalazimika kukatisha masomo na kurudi Rwanda kuongoza RPF akishirikiana na Alexis Kanyarwenge. Museveni akampa msaada wa fedha, silaha na chakula. RPF ikaweka kambi Uganda eneo la Kabale, Burundi eneo la Muyinga na Congo maeneo ya Kivu, Uvira na Goma. Mwaka 1994, askari wa RPF wakatungua ndege ya Rais Habyarimana ikiwa inakaribia kutua uwanja wa ndege wa Kigali ikitokea Dar es Salaam kwenye mazungumzo ya Amani alikuwa na Rais Cyprien Ntaramira wa Burundi. Wote wawili walikufa papo hapo. Kuuawa kwa Rais Habyarimana kuliamsha hasira za Wahutu na kusabisha mauaji ya Kimbari ambapo Watutsi na Wahutu wenye msimamo wa wastani waliuawa kikatili kwa kucharangwa mapanga. Hali hiyo ilisababisha Watutsi wengi kukimbia nchi yao. Wapo waliokimbilia Tanzania, Uganda, lakini wengi zaidi walikimbilia eneo la Kivu. Kwa kifupi, idadi ya Watutsi eneo la Kivu iliongezeka siku hadi siku. Watutsi walioenda Kivu wengi hawakurudi Rwanda hata baada ya vita kumalizika. Ilikuwa vigumu kutofautisha Mtutsi mwenye asili ya Congo (Banyamulenge) na Mtutsi wa Rwanda, kwa sababu wote wanaongea lugha moja, mila na desturi moja. Kwahiyo hisia za Wakongomani kwamba Banyamulenge ni wageni zikaanza kupata nguvu kutokana na uhamiaji mkubwa wa Watutsi maeneo ya Kivu kaskazini na kusini. Wakati huo Congo ikiitwa Zaire Rais Mobutu Sese Seko alikataa kuwatambua Banyamulenge kama raia wake, na akazuia wasipewe vitambulisho vya taifa. (Malisa GJ)
    Like
    1
    · 0 Kommentare ·0 Anteile ·887 Ansichten
  • #PART2

    Baada ya mipaka ya Wakoloni walioangukia Rwanda na Burundi waliendelea kujiita Watutsi, lakini walioangukia Congo hawakujiita Watutsi, kwa sababu ya kukwepa ubaguzi. Ili wasitengwe wakajitambulisha kwa eneo wanalotoka, safu za Milima ya Mulenge. Kwahiyo wakajiita Banyamulenge, yani watu kutoka Mulenge. Lakini ukweli ni Watutsi, wametengwa na wenzao kwa mipaka ya wakoloni.

    Ni sawa na wamassai wa Tanzania na wale wa Kenya. Ni jamii moja ila wametengwa na mipaka ya Wakoloni. Huku Tanzania Wamasai ni wengi kuliko Kenya, lakini serikali ya Kenya haiwezi kuwafukuza wa Kenya waje Tanzania. Itakua dhambi ya ubaguzi. Mipaka ilipowekwa waliojikuta Kenya wakawa raia wa Kenya hivyo, hali kadhalika waliojikuta Tanzania.

    Watutsi wa Congo pamoja na kujiita Banyamulenge, bado wakikumbana na ubaguzi. Hawakupata ushirikiano kutoka kwa jamii nyingine za Kivu. Kwahiyo wakajikuta wameongeza "bond" na Watutsi wa Rwanda. Kukawa na mwingiliano mkubwa kati ya Watutsi wa Rwanda na wale wa Congo (Banyamulenge).

    Mwaka 1959, mfalme wa mwisho wa Rwanda, Mutara III, aliuawa kwa sumu. Baada ya kifo chake, Rwanda iliingia katika machafuko ambapo Wahutu waliokuwa zaidi ya 80% waliwashambulia Watutsi, wakiwatuhumu kupendelewa na Wakoloni wa Kibelgiji. Maelfu ya Watutsi walikimbilia Kivu kwa ajili ya usalama wao. Walipofika huko, waliungana na wenzao (Banyamulenge), idadi ikaongezeka.

    Mwaka 1962, Rwanda ilipata uhuru, na Gregoire Kayibanda akawa Rais. Kwa mara ya kwanza, Wahutu walishika madaraka baada ya utawala wa kifalme wa Watutsi kwa miaka mingi. Kayibanda alikakandamiza Watutsi na kupendelea Wahutu wenzake. Watutsi wengi walikimbilia uhamishoni, hasa maeneo ya Kivu. Wakaenda kuungana na wenzao (Banyamulenge).

    Mwaka 1973, Kayibanda alipinduliwa na Mkuu wa Majeshi, Jenerali Juvénal Habyarimana, ambaye alijiapiza kuwatokomeza Watutsi. Kwa miaka 21 ya utawala wake, Watutsi waliteswa vikali. Waliondolewa kwenye nafasi za kijeshi, mashirika ya umma, na siasa. Wengi walifungwa gerezani au kuuawa. Hali hii iliwafanya Watutsi wengi zaidi kukimbia Rwanda na kuelekea maeneo mbalimbali ikiwemo Kivu. Walioenda Kivu wakaenda kuongeza idadi ya Banyamulenge.!
    (Malisa GJ)

    #PART2 Baada ya mipaka ya Wakoloni walioangukia Rwanda na Burundi waliendelea kujiita Watutsi, lakini walioangukia Congo hawakujiita Watutsi, kwa sababu ya kukwepa ubaguzi. Ili wasitengwe wakajitambulisha kwa eneo wanalotoka, safu za Milima ya Mulenge. Kwahiyo wakajiita Banyamulenge, yani watu kutoka Mulenge. Lakini ukweli ni Watutsi, wametengwa na wenzao kwa mipaka ya wakoloni. Ni sawa na wamassai wa Tanzania na wale wa Kenya. Ni jamii moja ila wametengwa na mipaka ya Wakoloni. Huku Tanzania Wamasai ni wengi kuliko Kenya, lakini serikali ya Kenya haiwezi kuwafukuza wa Kenya waje Tanzania. Itakua dhambi ya ubaguzi. Mipaka ilipowekwa waliojikuta Kenya wakawa raia wa Kenya hivyo, hali kadhalika waliojikuta Tanzania. Watutsi wa Congo pamoja na kujiita Banyamulenge, bado wakikumbana na ubaguzi. Hawakupata ushirikiano kutoka kwa jamii nyingine za Kivu. Kwahiyo wakajikuta wameongeza "bond" na Watutsi wa Rwanda. Kukawa na mwingiliano mkubwa kati ya Watutsi wa Rwanda na wale wa Congo (Banyamulenge). Mwaka 1959, mfalme wa mwisho wa Rwanda, Mutara III, aliuawa kwa sumu. Baada ya kifo chake, Rwanda iliingia katika machafuko ambapo Wahutu waliokuwa zaidi ya 80% waliwashambulia Watutsi, wakiwatuhumu kupendelewa na Wakoloni wa Kibelgiji. Maelfu ya Watutsi walikimbilia Kivu kwa ajili ya usalama wao. Walipofika huko, waliungana na wenzao (Banyamulenge), idadi ikaongezeka. Mwaka 1962, Rwanda ilipata uhuru, na Gregoire Kayibanda akawa Rais. Kwa mara ya kwanza, Wahutu walishika madaraka baada ya utawala wa kifalme wa Watutsi kwa miaka mingi. Kayibanda alikakandamiza Watutsi na kupendelea Wahutu wenzake. Watutsi wengi walikimbilia uhamishoni, hasa maeneo ya Kivu. Wakaenda kuungana na wenzao (Banyamulenge). Mwaka 1973, Kayibanda alipinduliwa na Mkuu wa Majeshi, Jenerali Juvénal Habyarimana, ambaye alijiapiza kuwatokomeza Watutsi. Kwa miaka 21 ya utawala wake, Watutsi waliteswa vikali. Waliondolewa kwenye nafasi za kijeshi, mashirika ya umma, na siasa. Wengi walifungwa gerezani au kuuawa. Hali hii iliwafanya Watutsi wengi zaidi kukimbia Rwanda na kuelekea maeneo mbalimbali ikiwemo Kivu. Walioenda Kivu wakaenda kuongeza idadi ya Banyamulenge.! (Malisa GJ)
    Like
    1
    · 0 Kommentare ·0 Anteile ·983 Ansichten

  • ndugu zangu leo naomba nitoe taalifa y ndugu yetu YUSUPH MGWAB

    HUYU BABA ANATATIZO LA FIGO!! ZOTE MBILI ZIMEFAIL

    ANAISHI KWA MSAADA WA DIALYISIS! KIUKWELI KUNA CHANGAMOTO KUBWA IMEJITOKEZA KWENYE LINE YA KUFANYIA DIALYISIS

    NJIA IMEKUFA KWA MAANA AKIINGIZA KWENYE MASHINE DAMU ZINATOKA SI KAWAIDA INAPELEKEA DAMU KUMWAGIKA NA KWA SASA PANAPASWA MRIJA UWEKWE MKONONI AU MU
    MGUUNI !!!

    TUNAHITAJI 1,800,000TZSH ( MILLION MOJA NA LAKI NANE)

    WAKATI NAANDAA NAMNA YA KUMSAIDIA JANA IJUMAA ALIENDA KUFANYA TENA DIALYSIS LAKINI ALISHINDWA KABISA ALIPATA BARIDI KALI KAMA KIFAFA NA ILIBIDI AFANYIWE DIALYSIS ALIWA KWENYA MASHINE YA OXYGEN!

    HALI HII IMEKUWA HATARI NA IMEFANYA MADAKTARI WAMUANDIKIEEE

    NAOMBA NDUGU NIWAOMBE TUMSAIDIE HUYU BABA KWANI HATOWEZA KUFANYA DIALYSIS MPAKA APATE SINDANO HIZO 5 NA IKUMBUKE FIGO ZOTE MBILI ZIMEKUFA DIALYSIS NDIO UHAI WAKE





    0745787549
    Mpesa
    JABILI ALLY ISSA

    "KUTOA NI MOYO SI UTAJURI "
    ndugu zangu leo naomba nitoe taalifa y ndugu yetu YUSUPH MGWAB HUYU BABA ANATATIZO LA FIGO!! ZOTE MBILI ZIMEFAIL ANAISHI KWA MSAADA WA DIALYISIS! KIUKWELI KUNA CHANGAMOTO KUBWA IMEJITOKEZA KWENYE LINE YA KUFANYIA DIALYISIS NJIA IMEKUFA KWA MAANA AKIINGIZA KWENYE MASHINE DAMU ZINATOKA SI KAWAIDA INAPELEKEA DAMU KUMWAGIKA NA KWA SASA PANAPASWA MRIJA UWEKWE MKONONI AU MU MGUUNI !!! TUNAHITAJI 1,800,000TZSH ( MILLION MOJA NA LAKI NANE) WAKATI NAANDAA NAMNA YA KUMSAIDIA JANA IJUMAA ALIENDA KUFANYA TENA DIALYSIS LAKINI ALISHINDWA KABISA ALIPATA BARIDI KALI KAMA KIFAFA NA ILIBIDI AFANYIWE DIALYSIS ALIWA KWENYA MASHINE YA OXYGEN! HALI HII IMEKUWA HATARI NA IMEFANYA MADAKTARI WAMUANDIKIEEE NAOMBA NDUGU NIWAOMBE TUMSAIDIE HUYU BABA 😪😪😪 KWANI HATOWEZA KUFANYA DIALYSIS MPAKA APATE SINDANO HIZO 5 NA IKUMBUKE FIGO ZOTE MBILI ZIMEKUFA DIALYSIS NDIO UHAI WAKE 😣😣😥😥😥 0745787549 Mpesa JABILI ALLY ISSA "KUTOA NI MOYO SI UTAJURI " 🙏
    Sad
    1
    · 1 Kommentare ·0 Anteile ·807 Ansichten
  • Rais wa Marekani , Donald Trump alienda kwenye Kanisa moja Anglican Nchini humo linalofahamika kama Episcopal Church, alienda kwa dhumuni la Ibada ya kushukuru ila alipofika Askofu wa Kanisa hilo Bi Marrian Edgar Budde kwenye hotuba yake akasema manano yafuatayo:

    “Rais Trump tunakuomba kwa jina la Mungu uwe na huruma kwa Watu wa Mapenzi ya Jinsia moja na Wahamiaju haramu, wanaogopa sana” akamaliza Askofu huyo.

    Rais Trump hakuridhishwa na hotuba hiyo na wakati anaondoka akasema maneno yafuatayo:

    “Haikuwa hotuba nzuri, haivutii, inachafua taswira ya Kanisa lake au ninyi Waandishi mnaona inavutia, binafsi sikuipenda, haivutii na ni kweli haivutii haina maana” - Donald Trump, Rais wa Marekani .

    Msimamo wa Trump dhidi ya Mapenzi ya Jinsia moja ni mkali saaana.

    Rais wa Marekani 🇺🇸, Donald Trump alienda kwenye Kanisa moja Anglican Nchini humo linalofahamika kama Episcopal Church, alienda kwa dhumuni la Ibada ya kushukuru ila alipofika Askofu wa Kanisa hilo Bi Marrian Edgar Budde kwenye hotuba yake akasema manano yafuatayo: “Rais Trump tunakuomba kwa jina la Mungu uwe na huruma kwa Watu wa Mapenzi ya Jinsia moja na Wahamiaju haramu, wanaogopa sana” akamaliza Askofu huyo. Rais Trump hakuridhishwa na hotuba hiyo na wakati anaondoka akasema maneno yafuatayo: “Haikuwa hotuba nzuri, haivutii, inachafua taswira ya Kanisa lake au ninyi Waandishi mnaona inavutia, binafsi sikuipenda, haivutii na ni kweli haivutii haina maana” - Donald Trump, Rais wa Marekani 🇺🇸. Msimamo wa Trump dhidi ya Mapenzi ya Jinsia moja ni mkali saaana.
    0 Kommentare ·0 Anteile ·718 Ansichten
  • Rais wa Marekani , Donald Trump alienda kwenye Kanisa moja Anglican Nchini humo linalofahamika kama Episcopal Church, alienda kwa dhumuni la Ibada ya kushukuru ila alipofika Askofu wa Kanisa hilo Bi Marrian Edgar Budde kwenye hotuba yake akasema manano yafuatayo:

    “Rais Trump tunakuomba kwa jina la Mungu uwe na huruma kwa Watu wa Mapenzi ya Jinsia moja na Wahamiaju haramu, wanaogopa sana” akamaliza Askofu huyo.

    Rais Trump hakuridhishwa na hotuba hiyo na wakati anaondoka akasema maneno yafuatayo:

    “Haikuwa hotuba nzuri, haivutii, inachafua taswira ya Kanisa lake au ninyi Waandishi mnaona inavutia, binafsi sikuipenda, haivutii na ni kweli haivutii haina maana” - Donald Trump, Rais wa Marekani .

    Msimamo wa Trump dhidi ya Mapenzi ya Jinsia moja ni mkali saaana.

    Rais wa Marekani 🇺🇸, Donald Trump alienda kwenye Kanisa moja Anglican Nchini humo linalofahamika kama Episcopal Church, alienda kwa dhumuni la Ibada ya kushukuru ila alipofika Askofu wa Kanisa hilo Bi Marrian Edgar Budde kwenye hotuba yake akasema manano yafuatayo: “Rais Trump tunakuomba kwa jina la Mungu uwe na huruma kwa Watu wa Mapenzi ya Jinsia moja na Wahamiaju haramu, wanaogopa sana” akamaliza Askofu huyo. Rais Trump hakuridhishwa na hotuba hiyo na wakati anaondoka akasema maneno yafuatayo: “Haikuwa hotuba nzuri, haivutii, inachafua taswira ya Kanisa lake au ninyi Waandishi mnaona inavutia, binafsi sikuipenda, haivutii na ni kweli haivutii haina maana” - Donald Trump, Rais wa Marekani 🇺🇸. Msimamo wa Trump dhidi ya Mapenzi ya Jinsia moja ni mkali saaana.
    Like
    1
    · 0 Kommentare ·0 Anteile ·684 Ansichten
Suchergebnis