• Mke wa Mchezaji wa kimataifa wa Burkina Faso n'a klabu ya Yanga SC, Hamisa Mobetto (Tanzania ) ameingia kwenye orodha ya WAGS (Wives And Girlfriends of Footballers) ambao ni Wake (Wapenzi au Wachumba) wa Wachezaji wenye Wafuasi (followers) wengi zaidi kwenye mtandao wa Instagram Duniani.

    1. @georginagio (Mrs. Ronaldo) :+65.5M
    2. antonelaroccuzzo (Mrs. Messi) : +39.9M
    3. @iambeckyg (Mrs. Sebastian) : +37.2M
    4. @victoriabeckham (Mrs. Beckham) : +32.9M
    5. @perrieedwards (Mrs. Alex) :+19M

    6. @alishalehmann7 (Mrs. Douglas Luiz) : +16.6M
    7. @brunabiancardi (Mrs. Neymar Jr) : +13.6M
    8. @hamisamobetto (Mrs. Aziz Ki) : +12.1M
    9. @pilarrubio (Mrs. Sergio Ramos) : +11.1M
    10. @leighannepinnock (Mrs. Andre Gray) : +10M

    Mke wa Mchezaji wa kimataifa wa Burkina Faso 🇧🇫 n'a klabu ya Yanga SC, Hamisa Mobetto (Tanzania 🇹🇿) ameingia kwenye orodha ya WAGS (Wives And Girlfriends of Footballers) ambao ni Wake (Wapenzi au Wachumba) wa Wachezaji wenye Wafuasi (followers) wengi zaidi kwenye mtandao wa Instagram Duniani. 1. @georginagio (Mrs. Ronaldo) :+65.5M 2. antonelaroccuzzo (Mrs. Messi) : +39.9M 3. @iambeckyg (Mrs. Sebastian) : +37.2M 4. @victoriabeckham (Mrs. Beckham) : +32.9M 5. @perrieedwards (Mrs. Alex) :+19M 6. @alishalehmann7 (Mrs. Douglas Luiz) : +16.6M 7. @brunabiancardi (Mrs. Neymar Jr) : +13.6M 8. @hamisamobetto (Mrs. Aziz Ki) : +12.1M 9. @pilarrubio (Mrs. Sergio Ramos) : +11.1M 10. @leighannepinnock (Mrs. Andre Gray) : +10M
    0 Yorumlar ·0 hisse senetleri ·59 Views
  • Amesema Steve Nyerere.

    "Mstafuuu ,,, Ivi Mama Akipenda kwenda kuangalia Dabi,....Pale uwanja wa Taifa pamoja na Watanzania na mashabiki wa Simba na Yanga Si Itapendeza sana,......Naimani Timu zote zitafurahia kuazimisha Miaka 4 Ya Rais wetu Mpendwa kwa Kucheza Dabi,...Maana ndani ya Miaka 4 Ya Mh @samia_suluhu_hassan Soka Limekuwa kivutio kikubwa sana Na Muanko wa Soka umekuwa mkubwa Baada ya Mh Rais kuhakikisha sekta hii Inapiga hatua,......

    Kuazimisha Miaka 4 Ya kipenzi cha Watanzania Dr Samia Suluhu Hassan Dabi halafu mgeni Rasmi Mama Itapendeza Tutajaaaa balaaa,...Apo vipi.,.," - Steve Nyerere, Mwigizaji wa filamu Tanzania.

    Amesema Steve Nyerere. "Mstafuuu ,,, Ivi Mama Akipenda kwenda kuangalia Dabi,....Pale uwanja wa Taifa pamoja na Watanzania na mashabiki wa Simba na Yanga Si Itapendeza sana,......Naimani Timu zote zitafurahia kuazimisha Miaka 4 Ya Rais wetu Mpendwa kwa Kucheza Dabi,...Maana ndani ya Miaka 4 Ya Mh @samia_suluhu_hassan Soka Limekuwa kivutio kikubwa sana Na Muanko wa Soka umekuwa mkubwa Baada ya Mh Rais kuhakikisha sekta hii Inapiga hatua,...... Kuazimisha Miaka 4 Ya kipenzi cha Watanzania Dr Samia Suluhu Hassan Dabi halafu mgeni Rasmi Mama Itapendeza Tutajaaaa balaaa,...Apo vipi.,.," - Steve Nyerere, Mwigizaji wa filamu Tanzania.
    0 Yorumlar ·0 hisse senetleri ·46 Views
  • Mchezaji wa kimataifa wa Ufaransa , N’Golo Kanté, ameonyesha moyo wa upendo kwa jamii kwa kujenga hospitali ya kisasa yenye thamani ya dola milioni tano (5) Nchini Mali, ikiwa ni msaada kwa Watoto na familia zisizojiweza kupata huduma bora za afya.

    Kanté, ambaye alizaliwa Jijini Paris, Ufaransa, ana asili ya Mali, Wazazi wake wakiwa Wahamiaji waliotoka Nchini Mali mwaka 1980. Jina lake N’Golo linatokana na Mfalme wa zamani wa Mali aliyewahi kutawala. Katika ziara yake Mali, Kanté alitumia muda na familia yake huku akitoa heshima kwa Baba yake na Kaka yake Marehemu.

    Mchezaji wa kimataifa wa Ufaransa 🇫🇷, N’Golo Kanté, ameonyesha moyo wa upendo kwa jamii kwa kujenga hospitali ya kisasa yenye thamani ya dola milioni tano (5) Nchini Mali, ikiwa ni msaada kwa Watoto na familia zisizojiweza kupata huduma bora za afya. Kanté, ambaye alizaliwa Jijini Paris, Ufaransa, ana asili ya Mali, Wazazi wake wakiwa Wahamiaji waliotoka Nchini Mali mwaka 1980. Jina lake N’Golo linatokana na Mfalme wa zamani wa Mali aliyewahi kutawala. Katika ziara yake Mali, Kanté alitumia muda na familia yake huku akitoa heshima kwa Baba yake na Kaka yake Marehemu.
    0 Yorumlar ·0 hisse senetleri ·62 Views
  • Mchezaji wa kimataifa wa Ufaransa , N’Golo Kanté, ameonyesha moyo wa upendo kwa jamii kwa kujenga hospitali ya kisasa yenye thamani ya dola milioni tano (5) Nchini Mali, ikiwa ni msaada kwa Watoto na familia zisizojiweza kupata huduma bora za afya.

    Kanté, ambaye alizaliwa Jijini Paris, Ufaransa, ana asili ya Mali, Wazazi wake wakiwa Wahamiaji waliotoka Nchini Mali mwaka 1980. Jina lake N’Golo linatokana na Mfalme wa zamani wa Mali aliyewahi kutawala. Katika ziara yake Mali, Kanté alitumia muda na familia yake huku akitoa heshima kwa Baba yake na Kaka yake Marehemu.
    Mchezaji wa kimataifa wa Ufaransa 🇫🇷, N’Golo Kanté, ameonyesha moyo wa upendo kwa jamii kwa kujenga hospitali ya kisasa yenye thamani ya dola milioni tano (5) Nchini Mali, ikiwa ni msaada kwa Watoto na familia zisizojiweza kupata huduma bora za afya. Kanté, ambaye alizaliwa Jijini Paris, Ufaransa, ana asili ya Mali, Wazazi wake wakiwa Wahamiaji waliotoka Nchini Mali mwaka 1980. Jina lake N’Golo linatokana na Mfalme wa zamani wa Mali aliyewahi kutawala. Katika ziara yake Mali, Kanté alitumia muda na familia yake huku akitoa heshima kwa Baba yake na Kaka yake Marehemu.
    0 Yorumlar ·0 hisse senetleri ·67 Views
  • Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limekutana kujadili hali ya usalama na kibinadamu Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo huku hali ikizidi kuzorota. Mwakilishi Maalum wa Umoja huo (UN) Nchini DR Congo, Bintou Keita, amesema Waasi wa kundi la M23 wanaodaiwa kuungwa mkono na Nchi ya Rwanda sasa wanadhibiti maeneo makubwa ya Mikoa ya Kivu Kaskazini na Kivu Kusini na kutishia kupanua mashambulizi yao hadi Mkoani Tshopo na Maniema.

    "Hivi karibuni M23 imesimika utawala wake kwa kuteua gavana, makamu gavana na meya huko Bukavu, Kivu Kusini," amesema Keita.

    Ameeleza kuwa mgogoro huo unahusiana na unyonyaji wa madini mashariki mwa DR Congo na kuzua wasiwasi wa kikanda. Pia amegusia hali mbaya ya kibinadamu, akisema kumekuwa na ongezeko la ukiukwaji wa haki za binadamu, ikiwa ni pamoja na mauaji, utekaji nyara na ajira ya kulazimishwa kwa Vijana, wakiwemo Watoto.

    Licha ya makubaliano ya hivi karibuni kati ya Marais wa Rwanda na DR Congo Nchini Qatar , amani bado haijapatikana. Keita ametoa wito wa kuteuliwa kwa mpatanishi wa Umoja wa Afrika ili kuongoza juhudi za kusitisha mapigano.

    Balozi wa DR Congo katika Baraza la Umoja wa kimataifa (UN), Zénon Mukongo Ngay, ameishutumu Rwanda kwa kutotekeleza usitishaji mapigano, huku Waziri wa mambo ya nje wa Rwanda, Olivier Nduhungirehe, akisema Nchi yake itaendelea kuchukua "hatua za ulinzi" mpaka kuwe na mfumo wa kudumu wa usalama.

    Wakati huo huo, imeripotiwa kuwa DR Congo inakabiliwa na janga kubwa zaidi la njaa kuwahi kutokea, ambapo Watu zaidi ya milioni 27.7 wanakabiliwa na uhaba wa chakula kutokana na vita na ukosefu wa utulivu mashariki mwa Nchi hiyo.

    Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limekutana kujadili hali ya usalama na kibinadamu Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo 🇨🇩 huku hali ikizidi kuzorota. Mwakilishi Maalum wa Umoja huo (UN) Nchini DR Congo, Bintou Keita, amesema Waasi wa kundi la M23 wanaodaiwa kuungwa mkono na Nchi ya Rwanda 🇷🇼 sasa wanadhibiti maeneo makubwa ya Mikoa ya Kivu Kaskazini na Kivu Kusini na kutishia kupanua mashambulizi yao hadi Mkoani Tshopo na Maniema. "Hivi karibuni M23 imesimika utawala wake kwa kuteua gavana, makamu gavana na meya huko Bukavu, Kivu Kusini," amesema Keita. Ameeleza kuwa mgogoro huo unahusiana na unyonyaji wa madini mashariki mwa DR Congo na kuzua wasiwasi wa kikanda. Pia amegusia hali mbaya ya kibinadamu, akisema kumekuwa na ongezeko la ukiukwaji wa haki za binadamu, ikiwa ni pamoja na mauaji, utekaji nyara na ajira ya kulazimishwa kwa Vijana, wakiwemo Watoto. Licha ya makubaliano ya hivi karibuni kati ya Marais wa Rwanda na DR Congo Nchini Qatar 🇶🇦, amani bado haijapatikana. Keita ametoa wito wa kuteuliwa kwa mpatanishi wa Umoja wa Afrika ili kuongoza juhudi za kusitisha mapigano. Balozi wa DR Congo katika Baraza la Umoja wa kimataifa (UN), Zénon Mukongo Ngay, ameishutumu Rwanda kwa kutotekeleza usitishaji mapigano, huku Waziri wa mambo ya nje wa Rwanda, Olivier Nduhungirehe, akisema Nchi yake itaendelea kuchukua "hatua za ulinzi" mpaka kuwe na mfumo wa kudumu wa usalama. Wakati huo huo, imeripotiwa kuwa DR Congo inakabiliwa na janga kubwa zaidi la njaa kuwahi kutokea, ambapo Watu zaidi ya milioni 27.7 wanakabiliwa na uhaba wa chakula kutokana na vita na ukosefu wa utulivu mashariki mwa Nchi hiyo.
    0 Yorumlar ·0 hisse senetleri ·96 Views
  • Shirikisho la mpira wa miguu Duniani (FIFA) limetangaza zawadi zitakazotolewa kwa Washiriki wa michuano ya Kombe la Dunia la Klabu (FIFA CLUB WORLD CUP), ambapo bingwa wa michuano hiyo atapata dola milioni 125 ambazo ni zaidi ya Shilingi Bilioni 300 za kitanzania huku kukitarajiwa kutolewa jumla ya dola bilioni 1 kwa klabu 32 zitakavyoshiriki na dola milioni 250 zitatolewa kwa mashirikisho kwa ajili kukuza mpira wa miguu kwa ngazi ya klabu Duniani.

    Shirikisho hilo limepanga kutoa dola milioni 250 ili kusaidia maendeleo ya mpira wa miguu kwa kiwango cha kimataifa ambapo fedha hizi zitatumika kusaidia klabu ndogo, kuboresha miundombinu, kuwekeza katika mafunzo ya Wachezaji na Makocha pamoja na kuimarisha ushirikiano wa klabu kimataifa.

    Aidha, pango huu unalenga kuhakikisha kuwa maendeleo ya mpira wa miguu hayaishii kwa klabu kubwa pekee, bali pia yanawanufaisha hadi klabu dogo na kuinua mpira wa Duniani kote. FIFA pia imesisitiza kuwa, mapato yote ya mashindano haya yatasambazwa kwa klabu bila kugusa akiba yake, ambayo inatumiwa kwa maendeleo ya mpira wa miguu kupitia Vyama (211) Wanachama wa FIFA.

    Mfumo huu ni mkubwa zaidi katika historia ya mpira wa miguu, ukiwa na mechi saba (7) kwenye hatua ya makundi na mfumo wa mchujo.

    Shirikisho la mpira wa miguu Duniani (FIFA) limetangaza zawadi zitakazotolewa kwa Washiriki wa michuano ya Kombe la Dunia la Klabu (FIFA CLUB WORLD CUP), ambapo bingwa wa michuano hiyo atapata dola milioni 125 ambazo ni zaidi ya Shilingi Bilioni 300 za kitanzania huku kukitarajiwa kutolewa jumla ya dola bilioni 1 kwa klabu 32 zitakavyoshiriki na dola milioni 250 zitatolewa kwa mashirikisho kwa ajili kukuza mpira wa miguu kwa ngazi ya klabu Duniani. Shirikisho hilo limepanga kutoa dola milioni 250 ili kusaidia maendeleo ya mpira wa miguu kwa kiwango cha kimataifa ambapo fedha hizi zitatumika kusaidia klabu ndogo, kuboresha miundombinu, kuwekeza katika mafunzo ya Wachezaji na Makocha pamoja na kuimarisha ushirikiano wa klabu kimataifa. Aidha, pango huu unalenga kuhakikisha kuwa maendeleo ya mpira wa miguu hayaishii kwa klabu kubwa pekee, bali pia yanawanufaisha hadi klabu dogo na kuinua mpira wa Duniani kote. FIFA pia imesisitiza kuwa, mapato yote ya mashindano haya yatasambazwa kwa klabu bila kugusa akiba yake, ambayo inatumiwa kwa maendeleo ya mpira wa miguu kupitia Vyama (211) Wanachama wa FIFA. Mfumo huu ni mkubwa zaidi katika historia ya mpira wa miguu, ukiwa na mechi saba (7) kwenye hatua ya makundi na mfumo wa mchujo.
    0 Yorumlar ·0 hisse senetleri ·135 Views
  • Nchi za Niger , Burkina Faso na Mali zimetangaza rasmi kujiondoa katika Shirika la Kimataifa la Mataifa yanayozungumza Kifaransa la ‘Francophonie’ (OIF). Uamuzi huo umefanywa na Viongozi wa mataifa hayo yenye Serikali za kijeshi, Niger inaongozwa na Jenerali Abdourahamane Tchiani, Mali inaongozwa na Kanali Assimi Goïta na Burkina Faso inayoongozwa na Kapteni Ibrahim Traoré.

    Viongozi hao wamedai OIF na taasisi zingine zilizo chini ya Ufaransa ni ukoloni mamboleo. OIF ni Shirila lililoundwa kwa madhumuni ya kukuza lugha ya Kifaransa na kuimarisha ushirikiano kati ya nchi zinazozungumza Kifaransa.

    Gazeti la Le Monde la Nchini Ufaransa limeripoti kuwa taarifa ya pamoja ya Nchi hizo tatu ilisema kwamba OIF imegeuka kuwa ‘chombo cha kisiasa’ kinachoendeshwa na Ufaransa ili kuongeza unyonyaji wa rasilimali za mataifa hayo.

    Nchi za Niger 🇳🇪, Burkina Faso 🇧🇫 na Mali 🇲🇱 zimetangaza rasmi kujiondoa katika Shirika la Kimataifa la Mataifa yanayozungumza Kifaransa la ‘Francophonie’ (OIF). Uamuzi huo umefanywa na Viongozi wa mataifa hayo yenye Serikali za kijeshi, Niger inaongozwa na Jenerali Abdourahamane Tchiani, Mali inaongozwa na Kanali Assimi Goïta na Burkina Faso inayoongozwa na Kapteni Ibrahim Traoré. Viongozi hao wamedai OIF na taasisi zingine zilizo chini ya Ufaransa 🇫🇷 ni ukoloni mamboleo. OIF ni Shirila lililoundwa kwa madhumuni ya kukuza lugha ya Kifaransa na kuimarisha ushirikiano kati ya nchi zinazozungumza Kifaransa. Gazeti la Le Monde la Nchini Ufaransa limeripoti kuwa taarifa ya pamoja ya Nchi hizo tatu ilisema kwamba OIF imegeuka kuwa ‘chombo cha kisiasa’ kinachoendeshwa na Ufaransa ili kuongeza unyonyaji wa rasilimali za mataifa hayo.
    0 Yorumlar ·0 hisse senetleri ·94 Views
  • Balozi wa Afrika Kusini Nchini Marekani , Ebrahim Rasool ambaye ametimuliwa na Nchi ya Marekani kutokana na kukosoa sera za Donald Trump, amerejea Afrika Kusini kwa ufakhari mkubwa na kupokewa kwa shangwe na mamia ya Wananchi waliofurika kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Cape Town Nchini Afrika Kusini.

    Balozi huyo na mkewe, Rosieda, waliwasili jana katika Uwanda wa Ndege wa Kimataifa wa Cape Town baada ya kusafari kutoka Nchini Marekani kupitia Qatar na wamekaribishwa vyema na kwa shangwe na mamia ya Wafuasi wao. Mapema mwezi huu, Balozi Rasool alitangazwa na Serikali ya Marekani kuwa ni Mtu asiyetakiwa kuweko Nchini humo baada ya kukosoa sera za Donald Trump, hatua ambayo inaonesha wazi jinsi madai ya uhuru wa kusema yasivyothaminiwa Nchini Marekani licha ya majigambo makubwa ya Nchi Marekani ya kupigania haki za Binadamu na demokrasia.

    Akiwahutubia mamia ya Mashabiki wake kwenye Uwanja wa Ndege wa Cape Town, Balozi Rasool amesema kwamba ingawa ametakiwa kuondoka huko Marekani lakini jambo hilo limeshindwa kufikia lengo lake kwani Viongozi wa Marekani wanadhani wamemdhalilisha wakati yeye anaona fakhari kwa maneno aliyotoa na Wananchi wa Afrika Kusini nao wanajivunia msimamo huo ndio maana wamejitokea kwa mamia kumpokea kishujaa.

    "Unaporejea nyumbani na kupokewa kwa shangwe na umati kama huu wa watu, mtu unaona fakhari na unajivunia msimamo wako." alisema Rasool.

    Alipoulizwa iwapo diplomasia imeshindwa, amesema ukweli kwamba matamshi yake yamemfanya Trump na Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Marco Rubio kuwa makini na hatua ya Serikali ya Marekani ya kumtangaza kuwa ni Mtu asiyetakiwa nchini humo ni ushahidi kwamba ujumbe wake umefika ngazi za juu kabisa za serikali ya Marekani.

    Balozi wa Afrika Kusini 🇿🇦 Nchini Marekani 🇺🇸, Ebrahim Rasool ambaye ametimuliwa na Nchi ya Marekani kutokana na kukosoa sera za Donald Trump, amerejea Afrika Kusini kwa ufakhari mkubwa na kupokewa kwa shangwe na mamia ya Wananchi waliofurika kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Cape Town Nchini Afrika Kusini. Balozi huyo na mkewe, Rosieda, waliwasili jana katika Uwanda wa Ndege wa Kimataifa wa Cape Town baada ya kusafari kutoka Nchini Marekani kupitia Qatar na wamekaribishwa vyema na kwa shangwe na mamia ya Wafuasi wao. Mapema mwezi huu, Balozi Rasool alitangazwa na Serikali ya Marekani kuwa ni Mtu asiyetakiwa kuweko Nchini humo baada ya kukosoa sera za Donald Trump, hatua ambayo inaonesha wazi jinsi madai ya uhuru wa kusema yasivyothaminiwa Nchini Marekani licha ya majigambo makubwa ya Nchi Marekani ya kupigania haki za Binadamu na demokrasia. Akiwahutubia mamia ya Mashabiki wake kwenye Uwanja wa Ndege wa Cape Town, Balozi Rasool amesema kwamba ingawa ametakiwa kuondoka huko Marekani lakini jambo hilo limeshindwa kufikia lengo lake kwani Viongozi wa Marekani wanadhani wamemdhalilisha wakati yeye anaona fakhari kwa maneno aliyotoa na Wananchi wa Afrika Kusini nao wanajivunia msimamo huo ndio maana wamejitokea kwa mamia kumpokea kishujaa. "Unaporejea nyumbani na kupokewa kwa shangwe na umati kama huu wa watu, mtu unaona fakhari na unajivunia msimamo wako." alisema Rasool. Alipoulizwa iwapo diplomasia imeshindwa, amesema ukweli kwamba matamshi yake yamemfanya Trump na Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Marco Rubio kuwa makini na hatua ya Serikali ya Marekani ya kumtangaza kuwa ni Mtu asiyetakiwa nchini humo ni ushahidi kwamba ujumbe wake umefika ngazi za juu kabisa za serikali ya Marekani.
    Love
    Like
    3
    · 0 Yorumlar ·0 hisse senetleri ·161 Views
  • Mchambuzi Farhan JR.

    Nimeona andiko la Waukae @zakazakazi kuhusu TFF kutengeneza Vijana ambalo lilipaswa kuwa jukumu la Klabu na akienda mbali kusema kwamba TFF ndio Shirikisho pekee duniani ambalo lina kituo ambacho kinazalisha na kulea vipaji vya vijana, kwanza kabla ya kupingana nae kuna kitu kwanza nataka kukiweka sawa kwenye eneo hilo.

    Duniani kote Mashirikisho kama TFF yamejikita zaidi kwenye DEVELOPMENT PROJECTS yaani Miradi ya maendeleo kisha wakaachia Mashindano kadhaa yasimamiwe na Bodi zao za Ligi kwa 90% bila kuyaingilia, TFF anachokifanya ni sahihi lakini pia sio sahihi sana kufanya yeye alipaswa kuwa na CLINICS tu ila kuna changamoto sehemu ambayo imeletwa na TFF wenyewe.

    Duniani Klabu zinaweza kuendesha miradi ya Vijana kwasababu kuna kitu kinaitwa FALSAFA ya nchi kwenye mpira, kuanzia mifumo, afya tiba, afya lishe na miundo yote ambayo portifolio hutoka Shirikisho (TFF) Klabu zinaenda kutekeleza mifumo hiyo na kuadjust baadhi ya maeneo halafu Vijana wakienda Clinics za Kitaifa wanaenda kukazia tu.

    Swali linakuja Je Waukaye @zakazakazi FALSAFA ya Tanzania kwenye mpira wa Miguu ni ipi? Iliwasilishwa lini? Anayo nani? Hilo ni Jukumu la TFF ambalo halijatekelezwa, kuna kitu kinaitwa TALENT ID FRAMEWORK ili kupata Vijana je tunayo? Ipoje, anayo nani? Inasemaje? Klabu hazina Mwongozo kutoka kwa TFF? Academy zote nchini zipite humo LAZIMA TFF wafanye wanachoweza, tupo katikati, TFF ASIMAMIE HILO KIKAMILIFU.

    TFF wasiende mbali waende tu hapo Uganda ilipo FUFA, wana Talent ID Framework ambayo Mashirikisho yoote yalipigwa huo Msasa sambamba na Kamati zao tendaji, ndio maana Uganda wapo mbali mno kwenye soka la Vijana kwenye Klabu zao na National Team, kwasababu wana ramani wanaifuata, wameintergrate mfumo wao na FIFA Talent Development Schemes (TDS) je sisi lini tutaforce Klabu zipite humo?

    TFF anajipa majukumu ambayo mengine sio ya kwake, kujadili mikataba ya kibiashara sio Jukumu lake bali Vilabu na Bodi yao, TFF anabaki kama Baba pekee, duniani kote TFF zao zina majukumu yao ukitoa michuano ya FA na Ngao basi Ligi Kuu sio mali yao, TFF ASIMAMIE HASWA JUKUMU LA MAENDELEO NI LAKE.

    Mchambuzi Farhan JR. Nimeona andiko la Waukae @zakazakazi kuhusu TFF kutengeneza Vijana ambalo lilipaswa kuwa jukumu la Klabu na akienda mbali kusema kwamba TFF ndio Shirikisho pekee duniani ambalo lina kituo ambacho kinazalisha na kulea vipaji vya vijana, kwanza kabla ya kupingana nae kuna kitu kwanza nataka kukiweka sawa kwenye eneo hilo. Duniani kote Mashirikisho kama TFF yamejikita zaidi kwenye DEVELOPMENT PROJECTS yaani Miradi ya maendeleo kisha wakaachia Mashindano kadhaa yasimamiwe na Bodi zao za Ligi kwa 90% bila kuyaingilia, TFF anachokifanya ni sahihi lakini pia sio sahihi sana kufanya yeye alipaswa kuwa na CLINICS tu ila kuna changamoto sehemu ambayo imeletwa na TFF wenyewe. Duniani Klabu zinaweza kuendesha miradi ya Vijana kwasababu kuna kitu kinaitwa FALSAFA ya nchi kwenye mpira, kuanzia mifumo, afya tiba, afya lishe na miundo yote ambayo portifolio hutoka Shirikisho (TFF) Klabu zinaenda kutekeleza mifumo hiyo na kuadjust baadhi ya maeneo halafu Vijana wakienda Clinics za Kitaifa wanaenda kukazia tu. Swali linakuja Je Waukaye @zakazakazi FALSAFA ya Tanzania kwenye mpira wa Miguu ni ipi? Iliwasilishwa lini? Anayo nani? Hilo ni Jukumu la TFF ambalo halijatekelezwa, kuna kitu kinaitwa TALENT ID FRAMEWORK ili kupata Vijana je tunayo? Ipoje, anayo nani? Inasemaje? Klabu hazina Mwongozo kutoka kwa TFF? Academy zote nchini zipite humo LAZIMA TFF wafanye wanachoweza, tupo katikati, TFF ASIMAMIE HILO KIKAMILIFU. TFF wasiende mbali waende tu hapo Uganda ilipo FUFA, wana Talent ID Framework ambayo Mashirikisho yoote yalipigwa huo Msasa sambamba na Kamati zao tendaji, ndio maana Uganda wapo mbali mno kwenye soka la Vijana kwenye Klabu zao na National Team, kwasababu wana ramani wanaifuata, wameintergrate mfumo wao na FIFA Talent Development Schemes (TDS) je sisi lini tutaforce Klabu zipite humo? TFF anajipa majukumu ambayo mengine sio ya kwake, kujadili mikataba ya kibiashara sio Jukumu lake bali Vilabu na Bodi yao, TFF anabaki kama Baba pekee, duniani kote TFF zao zina majukumu yao ukitoa michuano ya FA na Ngao basi Ligi Kuu sio mali yao, TFF ASIMAMIE HASWA JUKUMU LA MAENDELEO NI LAKE.
    Like
    2
    · 0 Yorumlar ·0 hisse senetleri ·170 Views
  • Jeshi la Nchi ya Uganda limesema limewaua Wapiganaji 242 wa kundi la Waasi Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo linalojulikana kama CODECO baada ya kushambulia kambi ya Jeshi hilo la Uganda mpakani mashariki mwa DR Congo mapema wiki hii ambapo madai yamepingwa na Kundi hilo.

    Msemaji wa Jeshi la Uganda, Chris Magezi, amesema mamia ya Wapiganaji wa kundi la CODECO walishambulia kituo cha kijeshi cha Uganda People's Defence Forces (UPDF) katika eneo la Fataki, Mkoani Ituri, siku ya Jumatano na Alhamisi. Jeshi hilo lilijibu mashambulizi hayo mara zote mbili, likiwaangamiza Wapiganaji 31 siku ya kwanza na 211 siku ya pili, Magezi alisema katika chapisho kwenye akaunti yake ya Mtandao wa X Ijumaa usiku na kuongeza kuwa askari mmoja wa UPDF aliuawa na wengine wanne kujeruhiwa.

    Msemaji wa CODECO, Basa Zukpa Gerson, alipinga taarifa ya jeshi Jumamosi, akisema kundi hilo lilipoteza wapiganaji wawili tu na kwamba idadi ya vifo vya Wanajeshi wa UPDF ilikuwa juu zaidi. Chanzo kimoja cha Umoja wa Mataifa ambacho hakikutaka kutajwa jina kilisema Waasi 70 na Wanajeshi wa Uganda 12 waliuawa.

    Kulikuwa na mapigano zaidi kati ya pande hizo mbili asubuhi ya Jumamosi, alisema Msemaji wa CODECO na kiongozi mmoja wa jamii za kiraia wa eneo hilo. Wapiganaji wa CODECO wanasema lengo lao ni kuwalinda Wakulima wa Lendu dhidi ya Wafungaji wa Hema, ambao kihistoria wamekuwa wakigombana kuhusu ardhi.

    Kundi hilo ni moja ya makundi mengi ya Waasi yanayopigania ardhi na rasilimali za madini mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, ambapo Waasi wa M23 wameongeza mashambulizi mwaka huu na kupata mafanikio makubwa. Uganda ilituma wanajeshi DR Congo mwaka 2021 kusaidia Serikali kupambana na kundi lingine la Waasi, Allied Democratic Forces (ADF), ambalo lina uhusiano na Islamic State na linafanya mashambulizi ya kikatili kwenye baadhi ya Vijiji.

    Jeshi la Nchi ya Uganda 🇺🇬 limesema limewaua Wapiganaji 242 wa kundi la Waasi Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo 🇨🇩 linalojulikana kama CODECO baada ya kushambulia kambi ya Jeshi hilo la Uganda mpakani mashariki mwa DR Congo mapema wiki hii ambapo madai yamepingwa na Kundi hilo. Msemaji wa Jeshi la Uganda, Chris Magezi, amesema mamia ya Wapiganaji wa kundi la CODECO walishambulia kituo cha kijeshi cha Uganda People's Defence Forces (UPDF) katika eneo la Fataki, Mkoani Ituri, siku ya Jumatano na Alhamisi. Jeshi hilo lilijibu mashambulizi hayo mara zote mbili, likiwaangamiza Wapiganaji 31 siku ya kwanza na 211 siku ya pili, Magezi alisema katika chapisho kwenye akaunti yake ya Mtandao wa X Ijumaa usiku na kuongeza kuwa askari mmoja wa UPDF aliuawa na wengine wanne kujeruhiwa. Msemaji wa CODECO, Basa Zukpa Gerson, alipinga taarifa ya jeshi Jumamosi, akisema kundi hilo lilipoteza wapiganaji wawili tu na kwamba idadi ya vifo vya Wanajeshi wa UPDF ilikuwa juu zaidi. Chanzo kimoja cha Umoja wa Mataifa ambacho hakikutaka kutajwa jina kilisema Waasi 70 na Wanajeshi wa Uganda 12 waliuawa. Kulikuwa na mapigano zaidi kati ya pande hizo mbili asubuhi ya Jumamosi, alisema Msemaji wa CODECO na kiongozi mmoja wa jamii za kiraia wa eneo hilo. Wapiganaji wa CODECO wanasema lengo lao ni kuwalinda Wakulima wa Lendu dhidi ya Wafungaji wa Hema, ambao kihistoria wamekuwa wakigombana kuhusu ardhi. Kundi hilo ni moja ya makundi mengi ya Waasi yanayopigania ardhi na rasilimali za madini mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, ambapo Waasi wa M23 wameongeza mashambulizi mwaka huu na kupata mafanikio makubwa. Uganda ilituma wanajeshi DR Congo mwaka 2021 kusaidia Serikali kupambana na kundi lingine la Waasi, Allied Democratic Forces (ADF), ambalo lina uhusiano na Islamic State na linafanya mashambulizi ya kikatili kwenye baadhi ya Vijiji.
    Like
    1
    · 0 Yorumlar ·0 hisse senetleri ·173 Views
  • “Siku yangu ya kwanza nilipoenda kufanya majaribio nilichekwa sana, nilivalia suruali ndefu na viatu vyangu vilichanika sana, watu waliniona kama kituko, sikuonekana kama mcheza soka” - Sadio Mane, Mchezaji wa kimataifa wa Senegal na klabu ya Al Nasr ya Saudi Arabia .

    Rekodi yake.

    - Mechi : 686.
    - Mabao : 277.
    - "Assists" : 136.

    “Siku yangu ya kwanza nilipoenda kufanya majaribio nilichekwa sana, nilivalia suruali ndefu na viatu vyangu vilichanika sana, watu waliniona kama kituko, sikuonekana kama mcheza soka” - Sadio Mane, Mchezaji wa kimataifa wa Senegal 🇸🇳 na klabu ya Al Nasr ya Saudi Arabia 🇸🇦. Rekodi yake. - Mechi : 686. - Mabao : 277. - "Assists" : 136.
    Like
    1
    · 0 Yorumlar ·0 hisse senetleri ·99 Views
  • Zungu, Mtangazaji na Mchambuzi

    CPA Amos Makala kiongozi wa juu wa CCM amesema kuwa Chadema wana mpango wa kununua virusi via Ebola na Mpox ili kuzuia uchaguzi!!

    Maswali yangu kufuatia kauli ya CPA Amos Makala

    1. Hizi taarifa Makala amezipata wapi ?

    2. Idara ya usalama wa taifa (TISS) inataarifa za mpango huu ?, kama hakuna taarifa turejee kwenye swali la kwanza! Kama kuna taarifa hadi sasa ni hatua gani zimechukuliwa?

    3. Makala anatuambia kwa lugha nyingine baadhi ya viongozi wa Chadema wana mpango wa uhaini na kuhujumu uchumi wa nchi je kwanini vyombo vipo kimya kwa watu wenye tuhuma nzito kama hizi ?

    4. Je Makala amepima madhara ya kauli aliyoitoa hadharani ambayo huenda inazua taharuki na hofu kwa wananchi wa Tanzania na kwa wageni amabao wana mpango wa kuitembelea Tanzania kwa siku za usoni ?

    5. Ni hatua gani za kujibu ambazo Chadema wamezichukua hadi sasa ?

    6. Je ni kauli ya maksudi tu ili kuhamisha upepo na mjadala wa chadema ambao utashika kasi kwenye mikutano yao ya hadhara inayoanza hivi punde, kuhusu mpango wao wa no reform no election ?

    7. Je Makala anaweza kuthibitishaje kauli yake kwa Umma ?

    8.Je Chadema watanunulia wapi hivyo virusi, na kumbe vinauzwaga, Makala anaweza kuthibitisha ?

    Zungu, Mtangazaji na Mchambuzi CPA Amos Makala kiongozi wa juu wa CCM amesema kuwa Chadema wana mpango wa kununua virusi via Ebola na Mpox ili kuzuia uchaguzi!! Maswali yangu kufuatia kauli ya CPA Amos Makala 👇👇👇👇 1. Hizi taarifa Makala amezipata wapi ? 2. Idara ya usalama wa taifa (TISS) inataarifa za mpango huu ?, kama hakuna taarifa turejee kwenye swali la kwanza! Kama kuna taarifa hadi sasa ni hatua gani zimechukuliwa? 3. Makala anatuambia kwa lugha nyingine baadhi ya viongozi wa Chadema wana mpango wa uhaini na kuhujumu uchumi wa nchi je kwanini vyombo vipo kimya kwa watu wenye tuhuma nzito kama hizi ? 4. Je Makala amepima madhara ya kauli aliyoitoa hadharani ambayo huenda inazua taharuki na hofu kwa wananchi wa Tanzania na kwa wageni amabao wana mpango wa kuitembelea Tanzania kwa siku za usoni ? 5. Ni hatua gani za kujibu ambazo Chadema wamezichukua hadi sasa ? 6. Je ni kauli ya maksudi tu ili kuhamisha upepo na mjadala wa chadema ambao utashika kasi kwenye mikutano yao ya hadhara inayoanza hivi punde, kuhusu mpango wao wa no reform no election ? 7. Je Makala anaweza kuthibitishaje kauli yake kwa Umma ? 8.Je Chadema watanunulia wapi hivyo virusi, na kumbe vinauzwaga, Makala anaweza kuthibitisha ?
    0 Yorumlar ·0 hisse senetleri ·174 Views
  • Zungu

    Miaka miwili ya Rais Ibrahim Traore wa Burkina Faso: na hii ni Ripoti tangu kuchukua uongozi wa Taifa hilo la Afrika Magharibi

    1. GDP ya Burkina Faso iliongezeka kutoka karibu dola bilioni 18.8 hadi $ 22.1 bilioni.

    2. Alikataa mikopo kutoka kwa Mfuko wa Fedha wa Kimataifa (IMF) na Benki ya Dunia, akisema, "Afrika haiitaji Benki ya Dunia, IMF, Ulaya, au Amerika."

    3. Alikata mishahara ya mawaziri na wabunge kwa 30% wakati akiinua mishahara ya wafanyikazi wa umma na 50%.

    4. Alisafisha deni la ndani la Burkina Faso.

    5. Alianzisha mimea ya kwanza ya usindikaji wa nyanya.

    6. Mnamo 2023, alizindua mgodi wa dhahabu wa kisasa ili kuimarisha uwezo wa usindikaji wa ndani.

    7. Alisimamisha usafirishaji wa dhahabu isiyo wazi kutoka Burkina Faso kwenda Ulaya.

    8. Aliunda mmea wa pili wa usindikaji wa pamba wa Burkina Faso, na kuongeza kwenye ile iliyopo.

    9. Alianzisha Kituo cha Msaada wa Kitaifa cha Usindikaji wa Pamba ya Artisanal, wa kwanza wa aina yake, kusaidia wakulima wa pamba wa ndani.

    10. Alikataza matumizi ya wigs za kisheria za Uingereza na gauni katika korti za mitaa, na kuzibadilisha na mavazi ya jadi ya burkinabé.

    11. Alitanguliza kilimo kwa kusambaza matrekta zaidi ya 400, viboreshaji 239, pampu 710 za gari, na pikipiki 714 ili kuongeza uzalishaji na kusaidia jamii za vijijini.

    12. Aliwezesha ufikiaji wa mbegu zilizoboreshwa na pembejeo zingine za kilimo ili kuongeza mavuno ya kilimo.

    Uzalishaji wa nyanya ulikua kutoka tani 315,000 za tani mnamo 2022 hadi tani 360,000 za tani mnamo 2024.

    Uzalishaji wa Millet uliongezeka kutoka tani 907,000 za tani 2022 hadi tani milioni 1.1 mnamo 2024.

    15. Uzalishaji wa mchele uliongezeka kutoka tani 280,000 za tani 2022 hadi tani 326,000 mnamo 2024.

    16. Alipiga marufuku shughuli za kijeshi za Ufaransa huko Burkina Faso.

    17. Alikataza vyombo vya habari vya Ufaransa kufanya kazi nchini.

    18. Aliwafukuza askari wa Ufaransa kutoka Burkina Faso.

    19. Serikali yake inaunda barabara mpya, kupanua zile zilizopo, na kubadilisha barabara za changarawe kuwa nyuso za lami.

    20. Anajenga kinu kikubwa cha nyuklia kwa ajili ya umeme wa uhakika wa nchi yake ya Burkina faso

    Zungu ✍️ Miaka miwili ya Rais Ibrahim Traore wa Burkina Faso: na hii ni Ripoti tangu kuchukua uongozi wa Taifa hilo la Afrika Magharibi 1. GDP ya Burkina Faso iliongezeka kutoka karibu dola bilioni 18.8 hadi $ 22.1 bilioni. 2. Alikataa mikopo kutoka kwa Mfuko wa Fedha wa Kimataifa (IMF) na Benki ya Dunia, akisema, "Afrika haiitaji Benki ya Dunia, IMF, Ulaya, au Amerika." 3. Alikata mishahara ya mawaziri na wabunge kwa 30% wakati akiinua mishahara ya wafanyikazi wa umma na 50%. 4. Alisafisha deni la ndani la Burkina Faso. 5. Alianzisha mimea ya kwanza ya usindikaji wa nyanya. 6. Mnamo 2023, alizindua mgodi wa dhahabu wa kisasa ili kuimarisha uwezo wa usindikaji wa ndani. 7. Alisimamisha usafirishaji wa dhahabu isiyo wazi kutoka Burkina Faso kwenda Ulaya. 8. Aliunda mmea wa pili wa usindikaji wa pamba wa Burkina Faso, na kuongeza kwenye ile iliyopo. 9. Alianzisha Kituo cha Msaada wa Kitaifa cha Usindikaji wa Pamba ya Artisanal, wa kwanza wa aina yake, kusaidia wakulima wa pamba wa ndani. 10. Alikataza matumizi ya wigs za kisheria za Uingereza na gauni katika korti za mitaa, na kuzibadilisha na mavazi ya jadi ya burkinabé. 11. Alitanguliza kilimo kwa kusambaza matrekta zaidi ya 400, viboreshaji 239, pampu 710 za gari, na pikipiki 714 ili kuongeza uzalishaji na kusaidia jamii za vijijini. 12. Aliwezesha ufikiaji wa mbegu zilizoboreshwa na pembejeo zingine za kilimo ili kuongeza mavuno ya kilimo. Uzalishaji wa nyanya ulikua kutoka tani 315,000 za tani mnamo 2022 hadi tani 360,000 za tani mnamo 2024. Uzalishaji wa Millet uliongezeka kutoka tani 907,000 za tani 2022 hadi tani milioni 1.1 mnamo 2024. 15. Uzalishaji wa mchele uliongezeka kutoka tani 280,000 za tani 2022 hadi tani 326,000 mnamo 2024. 16. Alipiga marufuku shughuli za kijeshi za Ufaransa huko Burkina Faso. 17. Alikataza vyombo vya habari vya Ufaransa kufanya kazi nchini. 18. Aliwafukuza askari wa Ufaransa kutoka Burkina Faso. 19. Serikali yake inaunda barabara mpya, kupanua zile zilizopo, na kubadilisha barabara za changarawe kuwa nyuso za lami. 20. Anajenga kinu kikubwa cha nyuklia kwa ajili ya umeme wa uhakika wa nchi yake ya Burkina faso
    0 Yorumlar ·0 hisse senetleri ·169 Views
  • Rais wa Nchi ya Iran , Ayatollah Ali Khamenei, amesema kuwa vitisho vya Nchi ya Marekani dhidi ya Taifa lake havisaidii lolote na havitaleta matokeo yoyote kama Rais Donald Tramp anavyofikiria. Kiongozi huyo amesema hayo baada ya Rais Trump kuonya uwezekano wa hatua za kijeshi kuchukuliwa dhidi ya Iran.

    "Wamarekani wanapaswa kuelewa kwamba vitisho havitafanikiwa wanapokabiliana na Iran. Wao (Marekani) na wengine wanapaswa kufahamu kuwa wakifanya lolote baya dhidi ya taifa la Iran, watajibiwa kwa nguvu kubwa." alisema Rais Khemenei

    Mnamo Machi 7, Rais Trump alisema kuwa alimwandikia barua Rais Khamenei, akimtaka kuanzisha mazungumzo kuhusu mpango wa nyuklia wa Iran, huku akionya kuwa kuna uwezekano wa kuchukua hatua za kijeshi iwapo Iran itakataa. Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, alisema Alhamisi wiki hii kuwa barua hiyo ilikuwa zaidi ya tishio, ingawa pia ilionesha uwezekano wa mazungumzo.

    "Tunachunguza kwa kina maudhui ya barua hiyo, na tutajibu rasmi katika siku chache zijazo” alisema Waziri huyo

    Kulingana na ripoti ya tovuti ya habari ya Marekani, Axios, ikimnukuu Afisa wa Serikali ya Trump na vyanzo vingine vikisema, barua hiyo inaweka muda wa miezi miwili wa kufikia makubaliano mapya ya nyuklia. Hata hivyo, haijabainishwa ni lini muda huo utaanza au kuisha. Kwa muda mrefu, Rais Khamenei amepuuza wito wa Rais Trump wa mazungumzo ya moja kwa moja, akisema kuwa Rais huyo wa Marekani anajaribu kudanganya ulimwengu kwa kuonesha kuwa Marekani iko tayari kwa mazungumzo huku Iran ikionekana kutotaka kushiriki.

    Ikumbukwe kwamba Trump ambaye alianza muhula wake wa pili Januari 2025, amerudisha sera yake ya shinikizo la juu dhidi ya Iran. Wakati wa kipindi chake cha kwanza, Trump aliiondoa Marekani kwenye makubaliano ya kihistoria ya nyuklia ya 2015 kati ya Iran na mataifa yenye nguvu ulimwenguni na akairejeshea Tehran vikwazo vikubwa vya kiuchumi.

    Rais wa Nchi ya Iran 🇮🇷, Ayatollah Ali Khamenei, amesema kuwa vitisho vya Nchi ya Marekani 🇺🇸 dhidi ya Taifa lake havisaidii lolote na havitaleta matokeo yoyote kama Rais Donald Tramp anavyofikiria. Kiongozi huyo amesema hayo baada ya Rais Trump kuonya uwezekano wa hatua za kijeshi kuchukuliwa dhidi ya Iran. "Wamarekani wanapaswa kuelewa kwamba vitisho havitafanikiwa wanapokabiliana na Iran. Wao (Marekani) na wengine wanapaswa kufahamu kuwa wakifanya lolote baya dhidi ya taifa la Iran, watajibiwa kwa nguvu kubwa." alisema Rais Khemenei Mnamo Machi 7, Rais Trump alisema kuwa alimwandikia barua Rais Khamenei, akimtaka kuanzisha mazungumzo kuhusu mpango wa nyuklia wa Iran, huku akionya kuwa kuna uwezekano wa kuchukua hatua za kijeshi iwapo Iran itakataa. Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, alisema Alhamisi wiki hii kuwa barua hiyo ilikuwa zaidi ya tishio, ingawa pia ilionesha uwezekano wa mazungumzo. "Tunachunguza kwa kina maudhui ya barua hiyo, na tutajibu rasmi katika siku chache zijazo” alisema Waziri huyo Kulingana na ripoti ya tovuti ya habari ya Marekani, Axios, ikimnukuu Afisa wa Serikali ya Trump na vyanzo vingine vikisema, barua hiyo inaweka muda wa miezi miwili wa kufikia makubaliano mapya ya nyuklia. Hata hivyo, haijabainishwa ni lini muda huo utaanza au kuisha. Kwa muda mrefu, Rais Khamenei amepuuza wito wa Rais Trump wa mazungumzo ya moja kwa moja, akisema kuwa Rais huyo wa Marekani anajaribu kudanganya ulimwengu kwa kuonesha kuwa Marekani iko tayari kwa mazungumzo huku Iran ikionekana kutotaka kushiriki. Ikumbukwe kwamba Trump ambaye alianza muhula wake wa pili Januari 2025, amerudisha sera yake ya shinikizo la juu dhidi ya Iran. Wakati wa kipindi chake cha kwanza, Trump aliiondoa Marekani kwenye makubaliano ya kihistoria ya nyuklia ya 2015 kati ya Iran na mataifa yenye nguvu ulimwenguni na akairejeshea Tehran vikwazo vikubwa vya kiuchumi.
    0 Yorumlar ·0 hisse senetleri ·151 Views
  • Nchi ya Ufaransa imepinga vikali kauli ya Waziri wa Ulinzi wa Israel , Israel Katz, aliyedokeza uwezekano wa Israel kutwaa baadhi ya maeneo ya Ukanda wa Gaza iwapo Kundi la Hamas haitowaachia huru mateka waliosalia. Waziri wa Mambo ya Nje wa Ufaransa, Jean-Noel Barrot, amesema kuwa Ufaransa inapinga aina yoyote ya unyakuzi wa ardhi ya Palestina, iwe Gaza au Ukingo wa Magharibi. Kauli hiyo inakuja wakati ambapo Israel imezidisha mashambulizi yake Gaza, hali iliyosababisha maelfu ya wakazi wa maeneo ya Al-Salatin, Al-Karama, na Al-Awda kusini mwa Gaza kuamriwa kuyahama makazi yao kabla ya mashambulizi mapya.

    Katika tukio jingine, Jeshi la Israel lilidungua makombora mawili yaliyofyatuliwa na Hamas kuelekea mji wa Ashkelon, ambapo Hamas ilidai kuwa shambulio hilo ni jibu kwa mashambulizi dhidi ya raia wa Gaza. Waziri wa Ulinzi wa Israel ameapa kuendeleza mashambulizi ya angani, majini, na ardhini hadi mateka wote waachiliwe na Hamas ishindwe kabisa.

    Hatua hizi za Israel zimezua ukosoaji mkubwa kimataifa. Uturuki imelaani shambulio la Israel dhidi ya hospitali iliyojengwa na nchi hiyo huko Gaza, huku Rais wa Urusi , Vladimir Putin, akielezea kusikitishwa kwake na mashambulizi hayo.

    Nchi ya Ufaransa 🇫🇷 imepinga vikali kauli ya Waziri wa Ulinzi wa Israel 🇮🇱, Israel Katz, aliyedokeza uwezekano wa Israel kutwaa baadhi ya maeneo ya Ukanda wa Gaza iwapo Kundi la Hamas haitowaachia huru mateka waliosalia. Waziri wa Mambo ya Nje wa Ufaransa, Jean-Noel Barrot, amesema kuwa Ufaransa inapinga aina yoyote ya unyakuzi wa ardhi ya Palestina, iwe Gaza au Ukingo wa Magharibi. Kauli hiyo inakuja wakati ambapo Israel imezidisha mashambulizi yake Gaza, hali iliyosababisha maelfu ya wakazi wa maeneo ya Al-Salatin, Al-Karama, na Al-Awda kusini mwa Gaza kuamriwa kuyahama makazi yao kabla ya mashambulizi mapya. Katika tukio jingine, Jeshi la Israel lilidungua makombora mawili yaliyofyatuliwa na Hamas kuelekea mji wa Ashkelon, ambapo Hamas ilidai kuwa shambulio hilo ni jibu kwa mashambulizi dhidi ya raia wa Gaza. Waziri wa Ulinzi wa Israel ameapa kuendeleza mashambulizi ya angani, majini, na ardhini hadi mateka wote waachiliwe na Hamas ishindwe kabisa. Hatua hizi za Israel zimezua ukosoaji mkubwa kimataifa. Uturuki 🇹🇷 imelaani shambulio la Israel dhidi ya hospitali iliyojengwa na nchi hiyo huko Gaza, huku Rais wa Urusi 🇷🇺, Vladimir Putin, akielezea kusikitishwa kwake na mashambulizi hayo.
    0 Yorumlar ·0 hisse senetleri ·122 Views
  • Nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imetangaza rasmi kuondoa hitaji la visa kwa Watanzania wanaoingia Nchini humo, kuanzia tarehe 20 Machi, 2025. Hatua hii ni sehemu ya utekelezaji wa uanachama wa DR Congo katika Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na jitihada za kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia na kiuchumi kati ya mataifa hayo mawili.

    Ikumbukwe kwamba Nchi ya Tanzania ilikuwa imeondoa utaratibu wa malipo ya visa kwa Raia wa DRC tangu Septemba 2, 2023, ikitarajia hatua ya kurudishiwa fadhila. Uamuzi wa sasa wa DR Congo unaimarisha mahusiano ya ujirani mwema na kufungua fursa zaidi za biashara na ushirikiano wa kikanda.

    Serikali ya Tanzania imesifu hatua hiyo, ikisisitiza kuwa inalingana na ajenda za Jumuiya ya Afrika Mashariki na Mkataba wa Eneo Huru la Biashara la Afrika (AfCFTA). Hatua hii inaashiria ushirikiano bora wa kidiplomasia na unaleta unafuu mkubwa kwa Wafanyabiashara na wasafiri wa pande zote mbili.

    Nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo 🇨🇩 imetangaza rasmi kuondoa hitaji la visa kwa Watanzania wanaoingia Nchini humo, kuanzia tarehe 20 Machi, 2025. Hatua hii ni sehemu ya utekelezaji wa uanachama wa DR Congo katika Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na jitihada za kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia na kiuchumi kati ya mataifa hayo mawili. Ikumbukwe kwamba Nchi ya Tanzania 🇹🇿 ilikuwa imeondoa utaratibu wa malipo ya visa kwa Raia wa DRC tangu Septemba 2, 2023, ikitarajia hatua ya kurudishiwa fadhila. Uamuzi wa sasa wa DR Congo unaimarisha mahusiano ya ujirani mwema na kufungua fursa zaidi za biashara na ushirikiano wa kikanda. Serikali ya Tanzania imesifu hatua hiyo, ikisisitiza kuwa inalingana na ajenda za Jumuiya ya Afrika Mashariki na Mkataba wa Eneo Huru la Biashara la Afrika (AfCFTA). Hatua hii inaashiria ushirikiano bora wa kidiplomasia na unaleta unafuu mkubwa kwa Wafanyabiashara na wasafiri wa pande zote mbili.
    0 Yorumlar ·0 hisse senetleri ·202 Views
  • Rais wa Marekani , Donald Trump ametupilia mbali madai kwamba Nchi ya Urusi imekataa mapendekezo ya Nchi yake ya Marekani ya kusitisha mapigano Nchini Ukraine . Kiongozi huyo wa Marekani alionyesha kwa ufanisi kuwa ni mapema kujadili kuimarisha vikwazo vya Nchi ya Marekani dhidi ya Urusi.

    "Yeye (Rais wa Urusi Vladimir Putin ) hakukataa chochote. Na wana vikwazo," - Donald Trump aliwaambia Waandishi wa habari katika Ikulu ya Marekani (White House), akijibu swali ikiwa Marekani inapaswa kuimarisha vikwazo dhidi ya Urusi kwa sababu madai ya Putin kukataa usitishaji vita Nchini Ukraine.

    "Wana takriban vikwazo zaidi kuliko mtu yeyote," aliongeza

    Putin na Trump walipiga simu mnamo Machi 18, 2025 wakijadili wazo la kusitisha mapigano kwa siku thelathini katika mzozo wa Ukraine, njia za kuzuia kuongezeka zaidi kwa mvutano na masuala kadhaa ya kimataifa, Kremlin ilisema. Kulingana na maelezo yake ya wito huo, Kiongozi huyo wa Urusi aliunga mkono mpango wa Rais wa Marekani wa kusitisha mapigano ya nishati na miundombinu Nchini Ukraine.

    Ikulu ya White House ilisema katika usomaji huo kwamba Viongozi hao wawili pia walikubaliana kuanza mazungumzo ya kiufundi "juu ya utekelezaji wa usitishaji vita wa baharini katika Bahari Nyeusi, usitishaji kamili wa mapigano na amani ya kudumu."

    Rais wa Marekani 🇺🇸, Donald Trump ametupilia mbali madai kwamba Nchi ya Urusi 🇷🇺 imekataa mapendekezo ya Nchi yake ya Marekani ya kusitisha mapigano Nchini Ukraine 🇺🇦. Kiongozi huyo wa Marekani alionyesha kwa ufanisi kuwa ni mapema kujadili kuimarisha vikwazo vya Nchi ya Marekani dhidi ya Urusi. "Yeye (Rais wa Urusi Vladimir Putin ) hakukataa chochote. Na wana vikwazo," - Donald Trump aliwaambia Waandishi wa habari katika Ikulu ya Marekani (White House), akijibu swali ikiwa Marekani inapaswa kuimarisha vikwazo dhidi ya Urusi kwa sababu madai ya Putin kukataa usitishaji vita Nchini Ukraine. "Wana takriban vikwazo zaidi kuliko mtu yeyote," aliongeza Putin na Trump walipiga simu mnamo Machi 18, 2025 wakijadili wazo la kusitisha mapigano kwa siku thelathini katika mzozo wa Ukraine, njia za kuzuia kuongezeka zaidi kwa mvutano na masuala kadhaa ya kimataifa, Kremlin ilisema. Kulingana na maelezo yake ya wito huo, Kiongozi huyo wa Urusi aliunga mkono mpango wa Rais wa Marekani wa kusitisha mapigano ya nishati na miundombinu Nchini Ukraine. Ikulu ya White House ilisema katika usomaji huo kwamba Viongozi hao wawili pia walikubaliana kuanza mazungumzo ya kiufundi "juu ya utekelezaji wa usitishaji vita wa baharini katika Bahari Nyeusi, usitishaji kamili wa mapigano na amani ya kudumu."
    0 Yorumlar ·0 hisse senetleri ·146 Views
  • “Wazazi wangu waliniita N’golo kwa sababu ni jina la mfalme wa zamani huko Mali. Mfalme ambaye alianza kutoka chini kushinda ufalme. Nilikuwa nakusanya taka. Leo nacheza mpira na wananitazama kwenye TV. Hadithi yangu pia ni nzuri, nilianzia chini.” - N'golo Kante, Mchezaji wa kimataifa wa Ufaransa mwenye asili ya Mali.

    “Wazazi wangu waliniita N’golo kwa sababu ni jina la mfalme wa zamani huko Mali. Mfalme ambaye alianza kutoka chini kushinda ufalme. Nilikuwa nakusanya taka. Leo nacheza mpira na wananitazama kwenye TV. Hadithi yangu pia ni nzuri, nilianzia chini.” - N'golo Kante, Mchezaji wa kimataifa wa Ufaransa mwenye asili ya Mali.
    0 Yorumlar ·0 hisse senetleri ·147 Views
  • Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo , Felix Tshisekedi amesema Nchi yake iko tayari kuingia mkataba wa madini na Nchi Marekani kwa mabadilishano ya kupatiwa uwezo wa kujilinda dhidi ya Makundi ya Wapiganaji mashariki mwa taifa hilo kama vile kundi la M23 na mengineyo.

    Akizungumza na kituo cha Televisheni cha Fox News leo asubuhi, Rais huyo amesema makubaliano ya aina hiyo yataiwezesha Nchi ya DR Congo kuchimba madini yake kupitia Kampuni za Marekani huku yenyewe ikinufaika kwa kuimarisha mifumo yake ya ulinzi na usalama. Nchi hiyo yenye utajiri mkubwa wa madini ikiwemo kobalti na urani imekuwa inapambana na Kundi la Waasi wa M23 linadaiwa kuungwa mkono na Nchi ya Rwanda ambalo limefanikiwa tangu mwanzoni mwa mwaka huu kuchukua udhibiti wa maeneo makubwa upande wa mashariki mwa Nchi hiyo.

    Hapo jana, kundi hilo la Waasi wa M23 limeendelea kufanya mashambulizi na kuingia Mji mdogo wenye utajiri wa madini wa Walikale licha ya mwito wa kusitishwa mapigano uliotolewa na Rais Tshisekedi na mwenzake wa Rwanda Paul Kagame walipokutana Nchini Qatar mapema wiki hii.

    Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo 🇨🇩, Felix Tshisekedi amesema Nchi yake iko tayari kuingia mkataba wa madini na Nchi Marekani 🇺🇸 kwa mabadilishano ya kupatiwa uwezo wa kujilinda dhidi ya Makundi ya Wapiganaji mashariki mwa taifa hilo kama vile kundi la M23 na mengineyo. Akizungumza na kituo cha Televisheni cha Fox News leo asubuhi, Rais huyo amesema makubaliano ya aina hiyo yataiwezesha Nchi ya DR Congo kuchimba madini yake kupitia Kampuni za Marekani huku yenyewe ikinufaika kwa kuimarisha mifumo yake ya ulinzi na usalama. Nchi hiyo yenye utajiri mkubwa wa madini ikiwemo kobalti na urani imekuwa inapambana na Kundi la Waasi wa M23 linadaiwa kuungwa mkono na Nchi ya Rwanda 🇷🇼 ambalo limefanikiwa tangu mwanzoni mwa mwaka huu kuchukua udhibiti wa maeneo makubwa upande wa mashariki mwa Nchi hiyo. Hapo jana, kundi hilo la Waasi wa M23 limeendelea kufanya mashambulizi na kuingia Mji mdogo wenye utajiri wa madini wa Walikale licha ya mwito wa kusitishwa mapigano uliotolewa na Rais Tshisekedi na mwenzake wa Rwanda Paul Kagame walipokutana Nchini Qatar 🇶🇦 mapema wiki hii.
    0 Yorumlar ·0 hisse senetleri ·140 Views
  • Kwa mujibu wa Magazeti Nchini Burkina Faso , Aziz K alitoa sharti la kusafiri na Mke wake Hamisa Mobeto kwenda kuitumikia Timu ya Taifa (Les Étalons) na alipiwe gharama zote za safari hadi Nchini Burkina Faso. Lakini Jambo ambalo lilikaliwa na Kocha Mkuu wa Timu ya Taifa ya Burkina Faso, Brama Traoré.

    Ikumbukwe kwamba Kocha Traoré alitangaza kikosi chake kwa mechi za kufuzu Kombe la Dunia 2026 huku Aziz K hajaitwa. Timu ya Taifa ya Burkina Faso inajiandaa na mchezo dhidi ya Timu ya Taifa ya Djibouti Machi 21, na baadae itacheza dhidi ya Timu ya Taifa ya Guinea-Bissau Machi 24, 2025

    Burkina Faso wapo nafasi ya 3 wakiwa na alama tano 5, katika kundi A linaloongozwa na Misri wenye alama 10.

    Kwa mujibu wa Magazeti Nchini Burkina Faso 🇧🇫, Aziz K alitoa sharti la kusafiri na Mke wake Hamisa Mobeto kwenda kuitumikia Timu ya Taifa (Les Étalons) na alipiwe gharama zote za safari hadi Nchini Burkina Faso. Lakini Jambo ambalo lilikaliwa na Kocha Mkuu wa Timu ya Taifa ya Burkina Faso, Brama Traoré. Ikumbukwe kwamba Kocha Traoré alitangaza kikosi chake kwa mechi za kufuzu Kombe la Dunia 2026 huku Aziz K hajaitwa. Timu ya Taifa ya Burkina Faso inajiandaa na mchezo dhidi ya Timu ya Taifa ya Djibouti 🇩🇯 Machi 21, na baadae itacheza dhidi ya Timu ya Taifa ya Guinea-Bissau 🇬🇼 Machi 24, 2025 Burkina Faso 🇧🇫 wapo nafasi ya 3 wakiwa na alama tano 5, katika kundi A linaloongozwa na Misri 🇪🇬 wenye alama 10.
    0 Yorumlar ·0 hisse senetleri ·148 Views
Arama Sonuçları