• Trump aonya kuhusu makubaliano ya biashara kati ya China na Canada.

    Rais wa Marekani, Donald Trump, ametoa kauli kali akizungumzia uwezekano wa makubaliano ya kibiashara kati ya China na Canada, akionya kuwa hatua hiyo inaweza kuiweka Canada katika hatari kubwa ya kiuchumi.

    Akizungumza katika muktadha wa mijadala ya biashara za kimataifa, Trump alidai kuwa China ina uwezo mkubwa wa kiuchumi na kimkakati ambao unaweza kuathiri vibaya mataifa yanayoingia nayo mikataba bila tahadhari ya kutosha. Kwa mujibu wa Trump, Canada inaweza kujikuta ikidhoofishwa endapo itafanya makubaliano ya karibu na taifa hilo la Asia.

    “Ninasema wazi kabisa, China itaimeza Canada ikiwa watafanya makubaliano kati yao,” alisema Trump.

    Kauli hiyo imeibua mjadala mpana kuhusu uhusiano wa kibiashara kati ya mataifa makubwa na yale ya kati, hasa ikizingatiwa nafasi ya China kama moja ya nguvu kubwa za uchumi duniani. Wachambuzi wa siasa na uchumi wanasema matamshi ya Trump yanaakisi msimamo wake wa muda mrefu wa tahadhari na hata upinzani dhidi ya ushawishi wa China katika biashara za kimataifa.

    Hadi sasa, serikali ya Canada haijatoa tamko rasmi kujibu kauli hiyo, huku China pia ikikaa kimya kuhusu madai hayo. Hata hivyo, mjadala unaendelea kuonyesha jinsi masuala ya biashara na diplomasia yanavyoendelea kuwa nyeti katika uhusiano wa kimataifa, hasa yanapohusisha mataifa yenye maslahi makubwa ya kiuchumi.

    Toa maoni yako
    #Habari
    #Trump #China #Canada #Biashara #UhusianoYaKimataifa
    Trump aonya kuhusu makubaliano ya biashara kati ya China na Canada. Rais wa Marekani, Donald Trump, ametoa kauli kali akizungumzia uwezekano wa makubaliano ya kibiashara kati ya China na Canada, akionya kuwa hatua hiyo inaweza kuiweka Canada katika hatari kubwa ya kiuchumi. Akizungumza katika muktadha wa mijadala ya biashara za kimataifa, Trump alidai kuwa China ina uwezo mkubwa wa kiuchumi na kimkakati ambao unaweza kuathiri vibaya mataifa yanayoingia nayo mikataba bila tahadhari ya kutosha. Kwa mujibu wa Trump, Canada inaweza kujikuta ikidhoofishwa endapo itafanya makubaliano ya karibu na taifa hilo la Asia. “Ninasema wazi kabisa, China itaimeza Canada ikiwa watafanya makubaliano kati yao,” alisema Trump. Kauli hiyo imeibua mjadala mpana kuhusu uhusiano wa kibiashara kati ya mataifa makubwa na yale ya kati, hasa ikizingatiwa nafasi ya China kama moja ya nguvu kubwa za uchumi duniani. Wachambuzi wa siasa na uchumi wanasema matamshi ya Trump yanaakisi msimamo wake wa muda mrefu wa tahadhari na hata upinzani dhidi ya ushawishi wa China katika biashara za kimataifa. Hadi sasa, serikali ya Canada haijatoa tamko rasmi kujibu kauli hiyo, huku China pia ikikaa kimya kuhusu madai hayo. Hata hivyo, mjadala unaendelea kuonyesha jinsi masuala ya biashara na diplomasia yanavyoendelea kuwa nyeti katika uhusiano wa kimataifa, hasa yanapohusisha mataifa yenye maslahi makubwa ya kiuchumi. Toa maoni yako #Habari #Trump #China #Canada #Biashara #UhusianoYaKimataifa
    0 Commentarios 1 Acciones 20 Views
  • Iran yakataa mazungumzo na Trump, yakanusha madai ya uharibifu wa nyuklia.

    Katika kile kinachoonekana kuwa kuendelea kwa mvutano wa kidiplomasia kati ya Marekani na Iran, Kiongozi Mkuu wa Iran, Ayatollah Ali Khamenei, ameibuka hadharani na kukataa pendekezo la Rais wa Marekani, Donald Trump, la kurejea kwenye meza ya mazungumzo.

    Akizungumza kupitia vyombo vya habari vya Serikali, Khamenei alisema wazi kuwa pendekezo la Trump halikuwa la kweli, bali ni jaribio la kulazimisha makubaliano kwa njia ya vitisho.

    "Trump anasema yeye ni Mtaalamu wa kufanikisha makubaliano, lakini kama makubaliano hayo yanaambatana na shinikizo na matokeo yake tayari yameamuliwa, basi hiyo siyo makubaliano bali ni kulazimisha na vitisho," - Ayatollah Ali Khamenei.

    Kauli hiyo ya Khamenei imekuja kufuatia hotuba ya Trump wiki iliyopita, ambapo aliwaambia Wabunge wa Israel kwamba Marekani ingependa kufanikisha makubaliano ya amani na Tehran, hasa baada ya kutangazwa kwa usitishaji mapigano kati ya Israel na Hamas huko Gaza. Katika hotuba hiyo, Trump pia alidai kuwa:

    "Marekani imeharibu kabisa maeneo ya nyuklia ya Iran."

    Lakini Khamenei alikanusha vikali kauli hiyo, akisema:

    "Rais wa Marekani anajivunia kusema kuwa wamebomoa na kuharibu sekta ya nyuklia ya Iran. Vizuri, endeleeni kuota!"

    Kauli hizi zinaashiria kuwa uhusiano kati ya Tehran na Washington bado uko katika hali ya sintofahamu, huku Iran ikionekana kuchukua msimamo mkali dhidi ya kile inachokiona kama mbinu za mabeberu.

    Kwa sasa, haijafahamika kama juhudi za kidiplomasia zitaendelea, hasa ikizingatiwa kuwa Iran bado inashikilia haki yake ya kuendesha mpango wake wa nyuklia kama nchi huru.

    Je, unadhani mvutano huu unaweza kuzua mgogoro mpya wa kimataifa?

    Toa maoni yako
    Iran yakataa mazungumzo na Trump, yakanusha madai ya uharibifu wa nyuklia. Katika kile kinachoonekana kuwa kuendelea kwa mvutano wa kidiplomasia kati ya Marekani na Iran, Kiongozi Mkuu wa Iran, Ayatollah Ali Khamenei, ameibuka hadharani na kukataa pendekezo la Rais wa Marekani, Donald Trump, la kurejea kwenye meza ya mazungumzo. Akizungumza kupitia vyombo vya habari vya Serikali, Khamenei alisema wazi kuwa pendekezo la Trump halikuwa la kweli, bali ni jaribio la kulazimisha makubaliano kwa njia ya vitisho. "Trump anasema yeye ni Mtaalamu wa kufanikisha makubaliano, lakini kama makubaliano hayo yanaambatana na shinikizo na matokeo yake tayari yameamuliwa, basi hiyo siyo makubaliano bali ni kulazimisha na vitisho," - Ayatollah Ali Khamenei. Kauli hiyo ya Khamenei imekuja kufuatia hotuba ya Trump wiki iliyopita, ambapo aliwaambia Wabunge wa Israel kwamba Marekani ingependa kufanikisha makubaliano ya amani na Tehran, hasa baada ya kutangazwa kwa usitishaji mapigano kati ya Israel na Hamas huko Gaza. Katika hotuba hiyo, Trump pia alidai kuwa: "Marekani imeharibu kabisa maeneo ya nyuklia ya Iran." Lakini Khamenei alikanusha vikali kauli hiyo, akisema: "Rais wa Marekani anajivunia kusema kuwa wamebomoa na kuharibu sekta ya nyuklia ya Iran. Vizuri, endeleeni kuota!" Kauli hizi zinaashiria kuwa uhusiano kati ya Tehran na Washington bado uko katika hali ya sintofahamu, huku Iran ikionekana kuchukua msimamo mkali dhidi ya kile inachokiona kama mbinu za mabeberu. Kwa sasa, haijafahamika kama juhudi za kidiplomasia zitaendelea, hasa ikizingatiwa kuwa Iran bado inashikilia haki yake ya kuendesha mpango wake wa nyuklia kama nchi huru. Je, unadhani mvutano huu unaweza kuzua mgogoro mpya wa kimataifa? Toa maoni yako
    0 Commentarios 0 Acciones 1K Views
  • Raisi wa Marekani Donald Trump atakuwepo kwenye fainali ya Club World Cup hapo Jumapili..

    (Source: ESPN)

    #SportsElite
    🚨 Raisi wa Marekani Donald Trump atakuwepo kwenye fainali ya Club World Cup hapo Jumapili.. 🇺🇸 (Source: ESPN) #SportsElite
    0 Commentarios 0 Acciones 448 Views
  • Rais wa zamani wa Marekani , Barack Obama katika mahojiano na chuo cha Hamilton College Nchini humo aliongea kuhusu hali ya Nchi chini ya muhula wa pili wa Rais wa sasa Donald Trump na alikosoa vikali hatua za hivi karibuni za utawala huo.

    Rais huyo Mstaafu ambaye alitangulia muhula wa kwanza wa Trump, alimkosoa vikali Trump kwa juhudi zake za kubadilisha mfumo wa Serikali ya Shirikisho, kukandamiza uhamiaji na upinzani, pamoja na kuwatisha Wanahabari na Taasisi ya sheria.

    “Hivyo basi, hii ndio mara yangu ya kwanza kuzungumza hadharani kwa muda sasa,” Obama alisema wakati wa mahojiano jukwaani katika Chuo cha Hamilton. “Nimekuwa nikitazama kwa muda.”

    "Hebu fikiria kama ningekuwa nimefanya chochote kati ya haya,”

    “Ni jambo lisilowezekana kufikirika kwamba vyama vilevile vinavyonyamaza sasa vingevumilia tabia kama hiyo kutoka kwangu, au hata kutoka kwa baadhi ya walionitangulia.” alisema Obama

    Obama aliendelea kusema kuwa haamini tangazo jipya la ushuru lililotolewa na Trump “litakuwa zuri kwa Marekani.” Hata hivyo, alieleza kuwa anahofia zaidi kile alichokiita kama uvunjaji wa haki unaofanywa na Ikulu.

    Rais wa zamani wa Marekani 🇺🇸, Barack Obama katika mahojiano na chuo cha Hamilton College Nchini humo aliongea kuhusu hali ya Nchi chini ya muhula wa pili wa Rais wa sasa Donald Trump na alikosoa vikali hatua za hivi karibuni za utawala huo. Rais huyo Mstaafu ambaye alitangulia muhula wa kwanza wa Trump, alimkosoa vikali Trump kwa juhudi zake za kubadilisha mfumo wa Serikali ya Shirikisho, kukandamiza uhamiaji na upinzani, pamoja na kuwatisha Wanahabari na Taasisi ya sheria. “Hivyo basi, hii ndio mara yangu ya kwanza kuzungumza hadharani kwa muda sasa,” Obama alisema wakati wa mahojiano jukwaani katika Chuo cha Hamilton. “Nimekuwa nikitazama kwa muda.” "Hebu fikiria kama ningekuwa nimefanya chochote kati ya haya,” “Ni jambo lisilowezekana kufikirika kwamba vyama vilevile vinavyonyamaza sasa vingevumilia tabia kama hiyo kutoka kwangu, au hata kutoka kwa baadhi ya walionitangulia.” alisema Obama Obama aliendelea kusema kuwa haamini tangazo jipya la ushuru lililotolewa na Trump “litakuwa zuri kwa Marekani.” Hata hivyo, alieleza kuwa anahofia zaidi kile alichokiita kama uvunjaji wa haki unaofanywa na Ikulu.
    Love
    Like
    3
    0 Commentarios 0 Acciones 1K Views
  • Rais wa Marekani , DonaldTrump, ameibua mjadala mkali baada ya kusema kuwa kuna uwezekano wa yeye kuwania muhula wa tatu, licha ya Katiba ya Marekani kupiga marufuku jambo hilo kupitia Marekebisho ya 22. Katika mahojiano na NBCNews, Rais huyo hakutaka kufuta uwezekano wa kuwania tena Urais baada ya kumaliza mihula miwili, akidai kuwa kuna njia za kufanya hilo kutokea. Alisisitiza kuwa "hakuwa anatania," jambo ambalo limeibua hofu miongoni mwa Wachambuzi wa siasa na Wanaharakati wa demokrasia Nchini humo.

    Kwa mujibu wa Katiba ya Marekani, Rais haruhusiwi kutawala kwa zaidi ya mihula miwili ya miaka minne minne. Marekebisho ya 22 yaliwekwa ili kuzuia Mtu mmoja kuwa na mamlaka ya muda mrefu kama ilivyokuwa kwa Franklin D. Roosevelt, ambaye altawala kwa zaidi ya mihula miwili kabla ya marekebisho hayo kuidhinishwa mwaka 1951.

    Kauli ya Trump imeibua maswali kuhusu mbinu anazoweza kutumia kutafuta muhula wa tatu. Wachambuzi wa sheria wanabainisha kuwa ili hilo litokee, ama katiba ibadilishwe rasmi kwa marekebisho mapya, au ipatikane tafsiri mpya ya kisheria inayomruhusu kugombea tena. Hata hivyo, mchakato wa kubadili katiba ni mgumu na unahitaji ridhaa ya Bunge pamoja na Majimbo mengi ya Marekani.

    Baadhi ya Wafuasi wa Donald Trump wameunga mkono kauli yake, wakidai kuwa anastahili muda zaidi wa kuongoza Nchi. Hata hivyo, Wakosoaji wake wanasema kuwa hatua yoyote ya kupindua Marekebisho ya 22 inaweza kuwa tishio kwa demokrasia ya Marekani na kuweka msingi wa uongozi wa kiimla.

    Rais wa Marekani 🇺🇸, DonaldTrump, ameibua mjadala mkali baada ya kusema kuwa kuna uwezekano wa yeye kuwania muhula wa tatu, licha ya Katiba ya Marekani kupiga marufuku jambo hilo kupitia Marekebisho ya 22. Katika mahojiano na NBCNews, Rais huyo hakutaka kufuta uwezekano wa kuwania tena Urais baada ya kumaliza mihula miwili, akidai kuwa kuna njia za kufanya hilo kutokea. Alisisitiza kuwa "hakuwa anatania," jambo ambalo limeibua hofu miongoni mwa Wachambuzi wa siasa na Wanaharakati wa demokrasia Nchini humo. Kwa mujibu wa Katiba ya Marekani, Rais haruhusiwi kutawala kwa zaidi ya mihula miwili ya miaka minne minne. Marekebisho ya 22 yaliwekwa ili kuzuia Mtu mmoja kuwa na mamlaka ya muda mrefu kama ilivyokuwa kwa Franklin D. Roosevelt, ambaye altawala kwa zaidi ya mihula miwili kabla ya marekebisho hayo kuidhinishwa mwaka 1951. Kauli ya Trump imeibua maswali kuhusu mbinu anazoweza kutumia kutafuta muhula wa tatu. Wachambuzi wa sheria wanabainisha kuwa ili hilo litokee, ama katiba ibadilishwe rasmi kwa marekebisho mapya, au ipatikane tafsiri mpya ya kisheria inayomruhusu kugombea tena. Hata hivyo, mchakato wa kubadili katiba ni mgumu na unahitaji ridhaa ya Bunge pamoja na Majimbo mengi ya Marekani. Baadhi ya Wafuasi wa Donald Trump wameunga mkono kauli yake, wakidai kuwa anastahili muda zaidi wa kuongoza Nchi. Hata hivyo, Wakosoaji wake wanasema kuwa hatua yoyote ya kupindua Marekebisho ya 22 inaweza kuwa tishio kwa demokrasia ya Marekani na kuweka msingi wa uongozi wa kiimla.
    0 Commentarios 0 Acciones 2K Views
  • Balozi wa Afrika Kusini Nchini Marekani , Ebrahim Rasool ambaye ametimuliwa na Nchi ya Marekani kutokana na kukosoa sera za Donald Trump, amerejea Afrika Kusini kwa ufakhari mkubwa na kupokewa kwa shangwe na mamia ya Wananchi waliofurika kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Cape Town Nchini Afrika Kusini.

    Balozi huyo na mkewe, Rosieda, waliwasili jana katika Uwanda wa Ndege wa Kimataifa wa Cape Town baada ya kusafari kutoka Nchini Marekani kupitia Qatar na wamekaribishwa vyema na kwa shangwe na mamia ya Wafuasi wao. Mapema mwezi huu, Balozi Rasool alitangazwa na Serikali ya Marekani kuwa ni Mtu asiyetakiwa kuweko Nchini humo baada ya kukosoa sera za Donald Trump, hatua ambayo inaonesha wazi jinsi madai ya uhuru wa kusema yasivyothaminiwa Nchini Marekani licha ya majigambo makubwa ya Nchi Marekani ya kupigania haki za Binadamu na demokrasia.

    Akiwahutubia mamia ya Mashabiki wake kwenye Uwanja wa Ndege wa Cape Town, Balozi Rasool amesema kwamba ingawa ametakiwa kuondoka huko Marekani lakini jambo hilo limeshindwa kufikia lengo lake kwani Viongozi wa Marekani wanadhani wamemdhalilisha wakati yeye anaona fakhari kwa maneno aliyotoa na Wananchi wa Afrika Kusini nao wanajivunia msimamo huo ndio maana wamejitokea kwa mamia kumpokea kishujaa.

    "Unaporejea nyumbani na kupokewa kwa shangwe na umati kama huu wa watu, mtu unaona fakhari na unajivunia msimamo wako." alisema Rasool.

    Alipoulizwa iwapo diplomasia imeshindwa, amesema ukweli kwamba matamshi yake yamemfanya Trump na Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Marco Rubio kuwa makini na hatua ya Serikali ya Marekani ya kumtangaza kuwa ni Mtu asiyetakiwa nchini humo ni ushahidi kwamba ujumbe wake umefika ngazi za juu kabisa za serikali ya Marekani.

    Balozi wa Afrika Kusini 🇿🇦 Nchini Marekani 🇺🇸, Ebrahim Rasool ambaye ametimuliwa na Nchi ya Marekani kutokana na kukosoa sera za Donald Trump, amerejea Afrika Kusini kwa ufakhari mkubwa na kupokewa kwa shangwe na mamia ya Wananchi waliofurika kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Cape Town Nchini Afrika Kusini. Balozi huyo na mkewe, Rosieda, waliwasili jana katika Uwanda wa Ndege wa Kimataifa wa Cape Town baada ya kusafari kutoka Nchini Marekani kupitia Qatar na wamekaribishwa vyema na kwa shangwe na mamia ya Wafuasi wao. Mapema mwezi huu, Balozi Rasool alitangazwa na Serikali ya Marekani kuwa ni Mtu asiyetakiwa kuweko Nchini humo baada ya kukosoa sera za Donald Trump, hatua ambayo inaonesha wazi jinsi madai ya uhuru wa kusema yasivyothaminiwa Nchini Marekani licha ya majigambo makubwa ya Nchi Marekani ya kupigania haki za Binadamu na demokrasia. Akiwahutubia mamia ya Mashabiki wake kwenye Uwanja wa Ndege wa Cape Town, Balozi Rasool amesema kwamba ingawa ametakiwa kuondoka huko Marekani lakini jambo hilo limeshindwa kufikia lengo lake kwani Viongozi wa Marekani wanadhani wamemdhalilisha wakati yeye anaona fakhari kwa maneno aliyotoa na Wananchi wa Afrika Kusini nao wanajivunia msimamo huo ndio maana wamejitokea kwa mamia kumpokea kishujaa. "Unaporejea nyumbani na kupokewa kwa shangwe na umati kama huu wa watu, mtu unaona fakhari na unajivunia msimamo wako." alisema Rasool. Alipoulizwa iwapo diplomasia imeshindwa, amesema ukweli kwamba matamshi yake yamemfanya Trump na Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Marco Rubio kuwa makini na hatua ya Serikali ya Marekani ya kumtangaza kuwa ni Mtu asiyetakiwa nchini humo ni ushahidi kwamba ujumbe wake umefika ngazi za juu kabisa za serikali ya Marekani.
    Love
    Like
    3
    0 Commentarios 0 Acciones 2K Views
  • Rais wa Nchi ya Iran , Ayatollah Ali Khamenei, amesema kuwa vitisho vya Nchi ya Marekani dhidi ya Taifa lake havisaidii lolote na havitaleta matokeo yoyote kama Rais Donald Tramp anavyofikiria. Kiongozi huyo amesema hayo baada ya Rais Trump kuonya uwezekano wa hatua za kijeshi kuchukuliwa dhidi ya Iran.

    "Wamarekani wanapaswa kuelewa kwamba vitisho havitafanikiwa wanapokabiliana na Iran. Wao (Marekani) na wengine wanapaswa kufahamu kuwa wakifanya lolote baya dhidi ya taifa la Iran, watajibiwa kwa nguvu kubwa." alisema Rais Khemenei

    Mnamo Machi 7, Rais Trump alisema kuwa alimwandikia barua Rais Khamenei, akimtaka kuanzisha mazungumzo kuhusu mpango wa nyuklia wa Iran, huku akionya kuwa kuna uwezekano wa kuchukua hatua za kijeshi iwapo Iran itakataa. Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, alisema Alhamisi wiki hii kuwa barua hiyo ilikuwa zaidi ya tishio, ingawa pia ilionesha uwezekano wa mazungumzo.

    "Tunachunguza kwa kina maudhui ya barua hiyo, na tutajibu rasmi katika siku chache zijazo” alisema Waziri huyo

    Kulingana na ripoti ya tovuti ya habari ya Marekani, Axios, ikimnukuu Afisa wa Serikali ya Trump na vyanzo vingine vikisema, barua hiyo inaweka muda wa miezi miwili wa kufikia makubaliano mapya ya nyuklia. Hata hivyo, haijabainishwa ni lini muda huo utaanza au kuisha. Kwa muda mrefu, Rais Khamenei amepuuza wito wa Rais Trump wa mazungumzo ya moja kwa moja, akisema kuwa Rais huyo wa Marekani anajaribu kudanganya ulimwengu kwa kuonesha kuwa Marekani iko tayari kwa mazungumzo huku Iran ikionekana kutotaka kushiriki.

    Ikumbukwe kwamba Trump ambaye alianza muhula wake wa pili Januari 2025, amerudisha sera yake ya shinikizo la juu dhidi ya Iran. Wakati wa kipindi chake cha kwanza, Trump aliiondoa Marekani kwenye makubaliano ya kihistoria ya nyuklia ya 2015 kati ya Iran na mataifa yenye nguvu ulimwenguni na akairejeshea Tehran vikwazo vikubwa vya kiuchumi.

    Rais wa Nchi ya Iran 🇮🇷, Ayatollah Ali Khamenei, amesema kuwa vitisho vya Nchi ya Marekani 🇺🇸 dhidi ya Taifa lake havisaidii lolote na havitaleta matokeo yoyote kama Rais Donald Tramp anavyofikiria. Kiongozi huyo amesema hayo baada ya Rais Trump kuonya uwezekano wa hatua za kijeshi kuchukuliwa dhidi ya Iran. "Wamarekani wanapaswa kuelewa kwamba vitisho havitafanikiwa wanapokabiliana na Iran. Wao (Marekani) na wengine wanapaswa kufahamu kuwa wakifanya lolote baya dhidi ya taifa la Iran, watajibiwa kwa nguvu kubwa." alisema Rais Khemenei Mnamo Machi 7, Rais Trump alisema kuwa alimwandikia barua Rais Khamenei, akimtaka kuanzisha mazungumzo kuhusu mpango wa nyuklia wa Iran, huku akionya kuwa kuna uwezekano wa kuchukua hatua za kijeshi iwapo Iran itakataa. Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, alisema Alhamisi wiki hii kuwa barua hiyo ilikuwa zaidi ya tishio, ingawa pia ilionesha uwezekano wa mazungumzo. "Tunachunguza kwa kina maudhui ya barua hiyo, na tutajibu rasmi katika siku chache zijazo” alisema Waziri huyo Kulingana na ripoti ya tovuti ya habari ya Marekani, Axios, ikimnukuu Afisa wa Serikali ya Trump na vyanzo vingine vikisema, barua hiyo inaweka muda wa miezi miwili wa kufikia makubaliano mapya ya nyuklia. Hata hivyo, haijabainishwa ni lini muda huo utaanza au kuisha. Kwa muda mrefu, Rais Khamenei amepuuza wito wa Rais Trump wa mazungumzo ya moja kwa moja, akisema kuwa Rais huyo wa Marekani anajaribu kudanganya ulimwengu kwa kuonesha kuwa Marekani iko tayari kwa mazungumzo huku Iran ikionekana kutotaka kushiriki. Ikumbukwe kwamba Trump ambaye alianza muhula wake wa pili Januari 2025, amerudisha sera yake ya shinikizo la juu dhidi ya Iran. Wakati wa kipindi chake cha kwanza, Trump aliiondoa Marekani kwenye makubaliano ya kihistoria ya nyuklia ya 2015 kati ya Iran na mataifa yenye nguvu ulimwenguni na akairejeshea Tehran vikwazo vikubwa vya kiuchumi.
    0 Commentarios 0 Acciones 1K Views
  • Rais wa Marekani , Donald Trump ametupilia mbali madai kwamba Nchi ya Urusi imekataa mapendekezo ya Nchi yake ya Marekani ya kusitisha mapigano Nchini Ukraine . Kiongozi huyo wa Marekani alionyesha kwa ufanisi kuwa ni mapema kujadili kuimarisha vikwazo vya Nchi ya Marekani dhidi ya Urusi.

    "Yeye (Rais wa Urusi Vladimir Putin ) hakukataa chochote. Na wana vikwazo," - Donald Trump aliwaambia Waandishi wa habari katika Ikulu ya Marekani (White House), akijibu swali ikiwa Marekani inapaswa kuimarisha vikwazo dhidi ya Urusi kwa sababu madai ya Putin kukataa usitishaji vita Nchini Ukraine.

    "Wana takriban vikwazo zaidi kuliko mtu yeyote," aliongeza

    Putin na Trump walipiga simu mnamo Machi 18, 2025 wakijadili wazo la kusitisha mapigano kwa siku thelathini katika mzozo wa Ukraine, njia za kuzuia kuongezeka zaidi kwa mvutano na masuala kadhaa ya kimataifa, Kremlin ilisema. Kulingana na maelezo yake ya wito huo, Kiongozi huyo wa Urusi aliunga mkono mpango wa Rais wa Marekani wa kusitisha mapigano ya nishati na miundombinu Nchini Ukraine.

    Ikulu ya White House ilisema katika usomaji huo kwamba Viongozi hao wawili pia walikubaliana kuanza mazungumzo ya kiufundi "juu ya utekelezaji wa usitishaji vita wa baharini katika Bahari Nyeusi, usitishaji kamili wa mapigano na amani ya kudumu."

    Rais wa Marekani 🇺🇸, Donald Trump ametupilia mbali madai kwamba Nchi ya Urusi 🇷🇺 imekataa mapendekezo ya Nchi yake ya Marekani ya kusitisha mapigano Nchini Ukraine 🇺🇦. Kiongozi huyo wa Marekani alionyesha kwa ufanisi kuwa ni mapema kujadili kuimarisha vikwazo vya Nchi ya Marekani dhidi ya Urusi. "Yeye (Rais wa Urusi Vladimir Putin ) hakukataa chochote. Na wana vikwazo," - Donald Trump aliwaambia Waandishi wa habari katika Ikulu ya Marekani (White House), akijibu swali ikiwa Marekani inapaswa kuimarisha vikwazo dhidi ya Urusi kwa sababu madai ya Putin kukataa usitishaji vita Nchini Ukraine. "Wana takriban vikwazo zaidi kuliko mtu yeyote," aliongeza Putin na Trump walipiga simu mnamo Machi 18, 2025 wakijadili wazo la kusitisha mapigano kwa siku thelathini katika mzozo wa Ukraine, njia za kuzuia kuongezeka zaidi kwa mvutano na masuala kadhaa ya kimataifa, Kremlin ilisema. Kulingana na maelezo yake ya wito huo, Kiongozi huyo wa Urusi aliunga mkono mpango wa Rais wa Marekani wa kusitisha mapigano ya nishati na miundombinu Nchini Ukraine. Ikulu ya White House ilisema katika usomaji huo kwamba Viongozi hao wawili pia walikubaliana kuanza mazungumzo ya kiufundi "juu ya utekelezaji wa usitishaji vita wa baharini katika Bahari Nyeusi, usitishaji kamili wa mapigano na amani ya kudumu."
    Love
    1
    0 Commentarios 0 Acciones 967 Views
  • "Sijui kama mnaona jinsi Trump na Marekani yake wanavyocheza na Dunia kupitia ugomvi au migogoro ya Dunia ili kuipatia faida Marekani kwa kisingizio cha kutafuta amani huku nyuma ya pazia Marekani ikipata faida kupitia migogoro au vita.

    Tazama Makubaliano ya Madini pale Ukraine
    Ambapo Marekani watafaidika na Rasilimali za madini za Ukraine, yani ili Marekani waisadie Ukraine ni lazima Ukraine kuipatia madini yake Marekani

    Congo nayo inakaribia kusaini mkataba wa kuipatia Marekani madini ili Marekani iipatie ulinzi hapo tunazungumzia rasimali za Congo amabzo zinaenda kutumika kama faida kwa Marekani kisa tu ni ugomvi wa Afrika wenyewe kwa wenyewe na hapo hapo Trump katupiga Bao

    Huko Gaza napo mpango wa kuwahamisha wakazi wa Gaza kwa kisingizio cha kuijenga upya Gaza umeiva, Trump haijengi Gaza bure anafahamu fika kuwa chini ya ardhi ya Gaza kuna utajiri mkubwa wa maliasili ya Gesi na mafuta

    Huyo ndiye Trump mfanyabiashara kutoka White House ambaye anaenda sambamba na ule msemo unaosema "no free lunch in America" yaani hakuna chakula cha mchana cha bure Marekani, ukiona unapewa cha bure ujue badae utalipia tu!!" - Zungu, Mtangazaji na Mchambuzi wa Siasa.

    "Sijui kama mnaona jinsi Trump na Marekani yake wanavyocheza na Dunia kupitia ugomvi au migogoro ya Dunia ili kuipatia faida Marekani kwa kisingizio cha kutafuta amani huku nyuma ya pazia Marekani ikipata faida kupitia migogoro au vita. Tazama Makubaliano ya Madini pale Ukraine Ambapo Marekani watafaidika na Rasilimali za madini za Ukraine, yani ili Marekani waisadie Ukraine ni lazima Ukraine kuipatia madini yake Marekani Congo nayo inakaribia kusaini mkataba wa kuipatia Marekani madini ili Marekani iipatie ulinzi hapo tunazungumzia rasimali za Congo amabzo zinaenda kutumika kama faida kwa Marekani kisa tu ni ugomvi wa Afrika wenyewe kwa wenyewe na hapo hapo Trump katupiga Bao Huko Gaza napo mpango wa kuwahamisha wakazi wa Gaza kwa kisingizio cha kuijenga upya Gaza umeiva, Trump haijengi Gaza bure anafahamu fika kuwa chini ya ardhi ya Gaza kuna utajiri mkubwa wa maliasili ya Gesi na mafuta Huyo ndiye Trump mfanyabiashara kutoka White House ambaye anaenda sambamba na ule msemo unaosema "no free lunch in America" yaani hakuna chakula cha mchana cha bure Marekani, ukiona unapewa cha bure ujue badae utalipia tu!!" - Zungu, Mtangazaji na Mchambuzi wa Siasa.
    0 Commentarios 0 Acciones 1K Views
  • Rais wa Marekani , Donald Trump ametoa siri kuwa Ofisi yake imepokea barua kutoka kwa Rais wa Ukraine , Volodymyr Zelensky, ikisema yuko tayari kwa mazungumzo na Russia na kusaini makubaliano ya madini adimu.

    “Ukraine iko tayari kukaa kwenye meza ya mazungumzo haraka iwezekanavyo ili kuleta amani ya kudumu. Hakuna anayetaka amani zaidi ya Waukraine,” Trump amesema katika hotuba yake bungeni usiku wa kuamkia leo huku akinukuu barua hiyo.

    “Mimi na timu yangu tuko tayari kufanya kazi chini ya uongozi thabiti wa Rais Trump ili kupata amani ya kudumu’,” Trump alinukuu maneno ya Zelenskyy.

    “Si hilo lingekuwa jambo zuri?” aliuliza. “Ni wakati wa kukomesha huu upuuzi. Ni wakati wa kusitisha mauaji. Ni wakati wa kumaliza vita hivi visivyo na maana. Ukitaka kumaliza vita, lazima uzungumze na pande zote mbili,” amesema Trump.

    Kauli hiyo ya Trump imekuja siku chache baada ya mvutano mkali kati yake na Zelenskyy katika Ofisi ya Oval iliyoko Ikulu ya White House, hali iliyosababisha Marekani kusitisha msaada muhimu wa kijeshi kwa Ukraine.

    Rais wa Marekani 🇺🇸, Donald Trump ametoa siri kuwa Ofisi yake imepokea barua kutoka kwa Rais wa Ukraine 🇺🇦, Volodymyr Zelensky, ikisema yuko tayari kwa mazungumzo na Russia 🇷🇺 na kusaini makubaliano ya madini adimu. “Ukraine iko tayari kukaa kwenye meza ya mazungumzo haraka iwezekanavyo ili kuleta amani ya kudumu. Hakuna anayetaka amani zaidi ya Waukraine,” Trump amesema katika hotuba yake bungeni usiku wa kuamkia leo huku akinukuu barua hiyo. “Mimi na timu yangu tuko tayari kufanya kazi chini ya uongozi thabiti wa Rais Trump ili kupata amani ya kudumu’,” Trump alinukuu maneno ya Zelenskyy. “Si hilo lingekuwa jambo zuri?” aliuliza. “Ni wakati wa kukomesha huu upuuzi. Ni wakati wa kusitisha mauaji. Ni wakati wa kumaliza vita hivi visivyo na maana. Ukitaka kumaliza vita, lazima uzungumze na pande zote mbili,” amesema Trump. Kauli hiyo ya Trump imekuja siku chache baada ya mvutano mkali kati yake na Zelenskyy katika Ofisi ya Oval iliyoko Ikulu ya White House, hali iliyosababisha Marekani kusitisha msaada muhimu wa kijeshi kwa Ukraine.
    Like
    1
    0 Commentarios 0 Acciones 838 Views
  • Ijumaa, tarehe 28 Februari, haikuwa siku rahisi kwa Rais wa Ukraine, Volodymyr Zelensky, alipofanya ziara katika Ikulu ya White House, Marekani. Kabla hata ya mzozo wa maneno kati yake na mwenyeji wake, Rais Donald Trump, pamoja na Makamu wa Rais JD Vance, tayari kulikuwa na ishara za mivutano.

    Trump alimkaribisha Zelensky mlangoni na kusema kwa utani: “Leo amevalia kweli kweli,” kauli ambayo iliwafanya baadhi ya waandishi wa habari kuiona kama kejeli badala ya pongezi. Wakati huo, Zelensky alikuwa amevalia fulana nyeusi ya mikono mirefu, vazi ambalo amekuwa akilivaa mara kwa mara tangu Ukraine ivamiwe na Urusi mwaka 2022.

    Baadaye, Trump alipompokea Waziri Mkuu wa Uingereza, Keir Starmer, alionekana kutazama mavazi yake kwa makini kutoka juu hadi chini, kisha kunong’ona maneno yanayoweza kutafsiriwa kama pongezi kwa suti rasmi aliyovaa Starmer.

    Mjadala kuhusu mavazi ya Zelensky ulizidi kupamba moto wakati wa mkutano wa waandishi wa habari. Brian Glenn, mwandishi kutoka Real America’s Voice—chombo cha habari kinachopendelea mrengo wa kulia—alimtupia swali la moja kwa moja:

    “Kwa nini hauvai suti? Upo katika ofisi ya juu kabisa katika nchi hii, na umegoma kuvaa suti – je, unamiliki hata suti?”

    Kwa utulivu, Zelensky alijibu kwa mshangao mdogo:

    “Nitavaa suti vita hivi vitakapomalizika. Labda suti kama yako, labda bora zaidi, au pengine ya bei nafuu kuliko yako,” alisema kwa utani huku akionyesha msimamo wake wa kuendelea kuvaa mavazi ya kijeshi.

    Swali hilo la Glenn liliibua mjadala mkali mitandaoni. Wengine walimuunga mkono, wakisema kwamba kiongozi wa taifa anapaswa kuvaa mavazi rasmi anapokutana na viongozi wengine, ilhali wengine waliona swali hilo kuwa la dhihaka na lisilo na umuhimu.

    Miongoni mwa waliomkosoa Glenn ni mwandishi maarufu wa Uingereza, Piers Morgan, ambaye pia ni rafiki wa karibu wa Trump. Morgan aliandika kwenye mtandao wa X (zamani Twitter):

    “Swali la kipuuzi. Elon Musk havai suti anapoingia Ikulu.”

    Historia pia inaonyesha kuwa si Zelensky pekee aliyeingia Ikulu ya Marekani bila suti. Waziri Mkuu wa zamani wa Uingereza, Winston Churchill, alifanya hivyo katika moja ya ziara zake rasmi.
    Ijumaa, tarehe 28 Februari, haikuwa siku rahisi kwa Rais wa Ukraine, Volodymyr Zelensky, alipofanya ziara katika Ikulu ya White House, Marekani. Kabla hata ya mzozo wa maneno kati yake na mwenyeji wake, Rais Donald Trump, pamoja na Makamu wa Rais JD Vance, tayari kulikuwa na ishara za mivutano. Trump alimkaribisha Zelensky mlangoni na kusema kwa utani: “Leo amevalia kweli kweli,” kauli ambayo iliwafanya baadhi ya waandishi wa habari kuiona kama kejeli badala ya pongezi. Wakati huo, Zelensky alikuwa amevalia fulana nyeusi ya mikono mirefu, vazi ambalo amekuwa akilivaa mara kwa mara tangu Ukraine ivamiwe na Urusi mwaka 2022. Baadaye, Trump alipompokea Waziri Mkuu wa Uingereza, Keir Starmer, alionekana kutazama mavazi yake kwa makini kutoka juu hadi chini, kisha kunong’ona maneno yanayoweza kutafsiriwa kama pongezi kwa suti rasmi aliyovaa Starmer. Mjadala kuhusu mavazi ya Zelensky ulizidi kupamba moto wakati wa mkutano wa waandishi wa habari. Brian Glenn, mwandishi kutoka Real America’s Voice—chombo cha habari kinachopendelea mrengo wa kulia—alimtupia swali la moja kwa moja: “Kwa nini hauvai suti? Upo katika ofisi ya juu kabisa katika nchi hii, na umegoma kuvaa suti – je, unamiliki hata suti?” Kwa utulivu, Zelensky alijibu kwa mshangao mdogo: “Nitavaa suti vita hivi vitakapomalizika. Labda suti kama yako, labda bora zaidi, au pengine ya bei nafuu kuliko yako,” alisema kwa utani huku akionyesha msimamo wake wa kuendelea kuvaa mavazi ya kijeshi. Swali hilo la Glenn liliibua mjadala mkali mitandaoni. Wengine walimuunga mkono, wakisema kwamba kiongozi wa taifa anapaswa kuvaa mavazi rasmi anapokutana na viongozi wengine, ilhali wengine waliona swali hilo kuwa la dhihaka na lisilo na umuhimu. Miongoni mwa waliomkosoa Glenn ni mwandishi maarufu wa Uingereza, Piers Morgan, ambaye pia ni rafiki wa karibu wa Trump. Morgan aliandika kwenye mtandao wa X (zamani Twitter): “Swali la kipuuzi. Elon Musk havai suti anapoingia Ikulu.” Historia pia inaonyesha kuwa si Zelensky pekee aliyeingia Ikulu ya Marekani bila suti. Waziri Mkuu wa zamani wa Uingereza, Winston Churchill, alifanya hivyo katika moja ya ziara zake rasmi.
    Like
    Love
    2
    0 Commentarios 0 Acciones 1K Views
  • "Nimetazama Interview ya Rais wa Marekani na Rais wa Ukraine pale Oval Office ndani ya Ikulu ya Marekani, nimekuja kugundua Rais wa Ukraine anahisi anajadiliana na Mwanasiasa mwenzake ila anachosahau Trump ni Mfanyabiashara na hawezi kufanya kitu cha bure ambacho Taifa lake Marekani halinufaiki na chochote, ndio maan anamsukumia sana kuwa amalizane na Urusi wasaini mkataba wa amani.

    Pale Ukraine kuna madini adimu sana duniani, Mrusi hapigani Kichwa kichwa ndio maana maeneo ya Donbass na Zaporizhia yanabaki kuwa maeneo ya Kimkakati sana kwa Mrusi, hata Marekani hawapo kichwa kichwa maana Secretary Rubio wa Marekani alimwambia Rais wa Ukraine akubali kusaini mkataba wa madini ili wao waendelee kumlinda, Mrusi na Mmarekani wapo rada sana eneo lile na kila mmoja yupo Kitalaam.

    Kwa akili ya kawaida Marekani hataki kuendelea kugharamikia vita hivyo bila faida.

    Juzi kuna website nilisoma ya taarifa za Kiuchunguzi ni kuwa Marekani, China na Urusi kwasasa wapo meza moja na wazo lao kubwa wamekubaliana juu ya MULTIPOLAR WORLD ORDER ambapo Mataifa zaidi ya mawili yanakuwa na nguvu sawa ama yanakaribiana, kwa ufupi sana mataifa haya matatu yanataka kuitawala dunia bila kugusana.

    Ndio maana Trump alivyoingia madarakani akapush agenda chap ya BRICS kuachana na wazo lao la kuibadili dola ya Marekani kuwa sio sarafu rasmi kwenye umoja wao, ndio maana alipoingia wamerudi mezani kwa mengi ikiwemo Trump na Putin wote kukiri kuwa watashirikiana na Trump atasafiri kuelekea Urusi kwenye sherehe za Mei 9, ambapo watakutana Marais wote watatu yani Putin, Xi Jinping na Trump.

    Kifupi sana Marekani ya Donald Trump ina Approach tofauti sana, ndio maana hata Waziri Mkuu wa Uingereza Keir Stearmer alipofika White House kukutana na Trump kwenye mazungumzo yao akalisifia sana Jeshi la Uingereza ila kuna sehemu akampiga kwa kumwambia huwezi kuichukua Urusi peke yako, hata leo amesisitiza Ukraine wakubali amani nje na hapo bila msaada wake hawamuwezi Mrusi, huyo ndio Donald Trump" - Farhan JR, Mchambuzi.

    "Nimetazama Interview ya Rais wa Marekani na Rais wa Ukraine pale Oval Office ndani ya Ikulu ya Marekani, nimekuja kugundua Rais wa Ukraine anahisi anajadiliana na Mwanasiasa mwenzake ila anachosahau Trump ni Mfanyabiashara na hawezi kufanya kitu cha bure ambacho Taifa lake Marekani halinufaiki na chochote, ndio maan anamsukumia sana kuwa amalizane na Urusi wasaini mkataba wa amani. Pale Ukraine kuna madini adimu sana duniani, Mrusi hapigani Kichwa kichwa ndio maana maeneo ya Donbass na Zaporizhia yanabaki kuwa maeneo ya Kimkakati sana kwa Mrusi, hata Marekani hawapo kichwa kichwa maana Secretary Rubio wa Marekani alimwambia Rais wa Ukraine akubali kusaini mkataba wa madini ili wao waendelee kumlinda, Mrusi na Mmarekani wapo rada sana eneo lile na kila mmoja yupo Kitalaam. Kwa akili ya kawaida Marekani hataki kuendelea kugharamikia vita hivyo bila faida. Juzi kuna website nilisoma ya taarifa za Kiuchunguzi ni kuwa Marekani, China na Urusi kwasasa wapo meza moja na wazo lao kubwa wamekubaliana juu ya MULTIPOLAR WORLD ORDER ambapo Mataifa zaidi ya mawili yanakuwa na nguvu sawa ama yanakaribiana, kwa ufupi sana mataifa haya matatu yanataka kuitawala dunia bila kugusana. Ndio maana Trump alivyoingia madarakani akapush agenda chap ya BRICS kuachana na wazo lao la kuibadili dola ya Marekani kuwa sio sarafu rasmi kwenye umoja wao, ndio maana alipoingia wamerudi mezani kwa mengi ikiwemo Trump na Putin wote kukiri kuwa watashirikiana na Trump atasafiri kuelekea Urusi kwenye sherehe za Mei 9, ambapo watakutana Marais wote watatu yani Putin, Xi Jinping na Trump. Kifupi sana Marekani ya Donald Trump ina Approach tofauti sana, ndio maana hata Waziri Mkuu wa Uingereza Keir Stearmer alipofika White House kukutana na Trump kwenye mazungumzo yao akalisifia sana Jeshi la Uingereza ila kuna sehemu akampiga kwa kumwambia huwezi kuichukua Urusi peke yako, hata leo amesisitiza Ukraine wakubali amani nje na hapo bila msaada wake hawamuwezi Mrusi, huyo ndio Donald Trump" - Farhan JR, Mchambuzi.
    0 Commentarios 0 Acciones 1K Views
  • Mazungunzo kati ya Rais wa Marekani , Donald Trump na Rais wa Ukraine , Volorymyr Zelensky yameishia njiani baada ya kushindwa kuelewana kuhusu hatima ya vita ya Russia dhidi ya Ukraine. Ilianza kama utani wakati wa kikao hicho ambacho kimehudhuriwa na Makamu wa Rais wa Marekani JD Vance na Waandishi wa Habari.

    Kila upande ulianza kuelezea kile ambacho wamejadiliana kuhusiana na makubaliano yaliyokuwa yanatarajiwa kutiwa saini. Awali Trump alieleza kuwa makubaliano hayo ni pamoja na kusaini mkataba unaoiruhusu Marekani kuchimba madini adimu (rare minerals) katika ardhi ya Ukraine.

    Wakati mrejesho wa hatua iliyofikiwa kuhusu makubaliano hayo ya mkataba wa madini mambo yalikuwa sawa ila yakaanza kwenda mrama pale Trump alipohamisha mada na kuingia suala la kupata mwafaka wa mzozo kati ya Ukraine na Russia ya Vladimir Putin.

    Trump kwenye suala hilo alienda moja kwa moja na kumtaka Rais Zelensky, kuingia makubaliano na Russia ya kumaliza vita hivyo, la sivyo Marekani itajindoa katika mazungumzo hayo na haitoendelea kuifadhili tena wala kuipatia misaada Ukraine. Wawili hao walikatizana mara kwa mara wakati wa majibizano yao kwa namna isiyo ya kawaida ndani ya Marekani (White House).

    Mazungunzo kati ya Rais wa Marekani 🇺🇸, Donald Trump na Rais wa Ukraine 🇺🇦, Volorymyr Zelensky yameishia njiani baada ya kushindwa kuelewana kuhusu hatima ya vita ya Russia 🇷🇺 dhidi ya Ukraine. Ilianza kama utani wakati wa kikao hicho ambacho kimehudhuriwa na Makamu wa Rais wa Marekani JD Vance na Waandishi wa Habari. Kila upande ulianza kuelezea kile ambacho wamejadiliana kuhusiana na makubaliano yaliyokuwa yanatarajiwa kutiwa saini. Awali Trump alieleza kuwa makubaliano hayo ni pamoja na kusaini mkataba unaoiruhusu Marekani kuchimba madini adimu (rare minerals) katika ardhi ya Ukraine. Wakati mrejesho wa hatua iliyofikiwa kuhusu makubaliano hayo ya mkataba wa madini mambo yalikuwa sawa ila yakaanza kwenda mrama pale Trump alipohamisha mada na kuingia suala la kupata mwafaka wa mzozo kati ya Ukraine na Russia ya Vladimir Putin. Trump kwenye suala hilo alienda moja kwa moja na kumtaka Rais Zelensky, kuingia makubaliano na Russia ya kumaliza vita hivyo, la sivyo Marekani itajindoa katika mazungumzo hayo na haitoendelea kuifadhili tena wala kuipatia misaada Ukraine. Wawili hao walikatizana mara kwa mara wakati wa majibizano yao kwa namna isiyo ya kawaida ndani ya Marekani (White House).
    Like
    1
    0 Commentarios 0 Acciones 1K Views
  • Tafsiri isiyo rasmi

    "Tulikuwa na mkutano wa maana sana leo (Jana) Ikulu (whilte house) Mengi yamefundishika ambayo yasingeweza kueleweka bila mazungumzo chini ya moto na shinikizo kama hilo. Inashangaza kinachotoka kupitia hisia, na nimeamua kuwa Rais Zelenskyy hayuko tayari kwa Amani ikiwa Amerika itahusika, kwa sababu anahisi kuhusika kwetu kunampa faida kubwa katika mazungumzo. Sitaki faida, nataka AMANI.
    Ameidharau Marekani katika Ofisi yake pendwa ya Oval. Anaweza kurudi pale atakapokuwa tayari kwa Amani.” - Donald J. Trump, Rais wa Marekani .

    Tafsiri isiyo rasmi "Tulikuwa na mkutano wa maana sana leo (Jana) Ikulu (whilte house) Mengi yamefundishika ambayo yasingeweza kueleweka bila mazungumzo chini ya moto na shinikizo kama hilo. Inashangaza kinachotoka kupitia hisia, na nimeamua kuwa Rais Zelenskyy hayuko tayari kwa Amani ikiwa Amerika itahusika, kwa sababu anahisi kuhusika kwetu kunampa faida kubwa katika mazungumzo. Sitaki faida, nataka AMANI. Ameidharau Marekani katika Ofisi yake pendwa ya Oval. Anaweza kurudi pale atakapokuwa tayari kwa Amani.” - Donald J. Trump, Rais wa Marekani 🇺🇸.
    0 Commentarios 0 Acciones 377 Views
  • Kikao cha mazungumzo ya kumaliza mzozo wa Nchi ya Ukraine na Nchi ya Urusi kinaendelea Nchini Saudi Arabia 🇸 ambapo Mawaziri wa Mashauri ya Kigeni wa Urusi chini ya Sergie Lavrov na Marekani chini ya Marco Rubio. Hata hivyo, Ukraine na Umoja wa Ulaya (EU) hawajashirikishwa huku Ukraine upande wake inapinga kikao hicho kuwa makubaliano yoyote haitayatambua.

    Katika kusisitiza hilo Ukraine imeendelea kusisitiza kwamba itaendelea kupigana vita kwa kutegemea Ulaya sio Marekani kama mwanzo huku Rais wa Nchi hiyo Volodmiry Zelensky akisema Ukraine ni Taifa huru, hivyo haliwezi kuamuliwa mambo yake na Marekani, itautetea uhuru wake hadi tone la mwisho. Marekani imejibu kwa kusema inaitaka Ukraine irejeshe haraka deni lote la usaidizi wa vita lililotolewa na Marekani tangu Februari 2022 Oparesheni ya Urusi ilipoanza.

    Kikao hiki kinachoendelea ni hatua muhimu kuelekea mkutano wa Rais Putin na Rais Trump uliopangwa mwezi Mei katika sherehe za Mashujaa wa Urusi utakaofanyika Jijini Moscow, Urusi ambapo pia mkutano huo utamwalika Rais wa China Xi Ping kama Mgeni mwalikwa muhimu.

    Kikao cha mazungumzo ya kumaliza mzozo wa Nchi ya Ukraine 🇺🇦 na Nchi ya Urusi 🇷🇺 kinaendelea Nchini Saudi Arabia 🇸 ambapo Mawaziri wa Mashauri ya Kigeni wa Urusi chini ya Sergie Lavrov na Marekani 🇺🇸 chini ya Marco Rubio. Hata hivyo, Ukraine na Umoja wa Ulaya (EU) hawajashirikishwa huku Ukraine upande wake inapinga kikao hicho kuwa makubaliano yoyote haitayatambua. Katika kusisitiza hilo Ukraine imeendelea kusisitiza kwamba itaendelea kupigana vita kwa kutegemea Ulaya sio Marekani kama mwanzo huku Rais wa Nchi hiyo Volodmiry Zelensky akisema Ukraine ni Taifa huru, hivyo haliwezi kuamuliwa mambo yake na Marekani, itautetea uhuru wake hadi tone la mwisho. Marekani imejibu kwa kusema inaitaka Ukraine irejeshe haraka deni lote la usaidizi wa vita lililotolewa na Marekani tangu Februari 2022 Oparesheni ya Urusi ilipoanza. Kikao hiki kinachoendelea ni hatua muhimu kuelekea mkutano wa Rais Putin na Rais Trump uliopangwa mwezi Mei katika sherehe za Mashujaa wa Urusi utakaofanyika Jijini Moscow, Urusi ambapo pia mkutano huo utamwalika Rais wa China 🇨🇳 Xi Ping kama Mgeni mwalikwa muhimu.
    0 Commentarios 0 Acciones 1K Views
  • Rais wa Urusi , Vladimir Putin amewaalika Rais China , Xi Jinping na Rais wa Marekani , Donald Trump kuhudhuria sherehe maarufu za Ushindi wa Urusi katika vita kuu ya pili ya Dunia (Russia’s Victory Parade) zitakazofanyika tarehe 9 Mwezi May Jijini Moscow Nchini Urusi. Mwaliko huu unatokana na ombi la Rais Donald Trump la tarehe 11 Feb 2025 alipoomba kuzuru Moscow kwa lengo la kumaliza mgogoro wa Ukraine, Kikao kilichotokana na ombi hili kilifanywa kwa njia ya simu ambapo pamoja na mambo mengine, Trump alimhakikishia Putin kwamba Marekani itaacha ufadhili wa kijeshi kwa Ukraine na pia Ukraine itaachia sehemu ya ardhi yake iliyotwaliwa kama dhamana ya usalama wake dhidi ya Moscow.

    Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Washington katika taarifa yake ilikazia na kusisitiza kile alichokizungumza Trump na Moscow na kwamba Marekani inakusudia kumaliza tofauti zao kidunia. Utawala wa Trump umekuwa na juhudi kubwa kumaliza mizozo mikubwa duniani ambayo Ikulu hiyo ilikuwa ikifadhili na kuanzisha uchokozi kwa muda mrefu, Ukiachiliambali mgogoro wa Ukraine, pia Washington inashughulika kumaliza mgogoro wa Mashariki ya Kati huko Gaza ambapo mamia ya watu wameuawa kwa ufadhili wa Marekani hiyohiyo.

    Rais wa Urusi 🇷🇺, Vladimir Putin amewaalika Rais China 🇨🇳, Xi Jinping na Rais wa Marekani 🇺🇸, Donald Trump kuhudhuria sherehe maarufu za Ushindi wa Urusi katika vita kuu ya pili ya Dunia (Russia’s Victory Parade) zitakazofanyika tarehe 9 Mwezi May Jijini Moscow Nchini Urusi. Mwaliko huu unatokana na ombi la Rais Donald Trump la tarehe 11 Feb 2025 alipoomba kuzuru Moscow kwa lengo la kumaliza mgogoro wa Ukraine, Kikao kilichotokana na ombi hili kilifanywa kwa njia ya simu ambapo pamoja na mambo mengine, Trump alimhakikishia Putin kwamba Marekani itaacha ufadhili wa kijeshi kwa Ukraine na pia Ukraine itaachia sehemu ya ardhi yake iliyotwaliwa kama dhamana ya usalama wake dhidi ya Moscow. Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Washington katika taarifa yake ilikazia na kusisitiza kile alichokizungumza Trump na Moscow na kwamba Marekani inakusudia kumaliza tofauti zao kidunia. Utawala wa Trump umekuwa na juhudi kubwa kumaliza mizozo mikubwa duniani ambayo Ikulu hiyo ilikuwa ikifadhili na kuanzisha uchokozi kwa muda mrefu, Ukiachiliambali mgogoro wa Ukraine, pia Washington inashughulika kumaliza mgogoro wa Mashariki ya Kati huko Gaza ambapo mamia ya watu wameuawa kwa ufadhili wa Marekani hiyohiyo.
    Like
    1
    0 Commentarios 0 Acciones 1K Views
  • Marais wa Urusi , V. Putin na yule wa Marekani , D.Trump walizungumza leo hii kwa muda saa moja na nusu kuhusu kumaliza vita Nchini Ukraine , kuboresha uhusiano kati ya Marekani na Urusi, na uwezekano wa kubadilishana Wafungwa.

    Aidha, Putin alimwalika Trump kwenda Mjini Moscow Nchini Urusi na akasema yuko tayari kuwakaribisha Maafisa wa Marekani kwa mazungumzo. Hii ilikuwa simu ya kwanza ya Putin na Rais wa Marekani aliyeko madarakani tangu Februari 2022, alipoongea na Biden muda mfupi kabla ya kutuma Wanajeshi Nchini Ukraine.

    Toa maoni yako
    #MvanoHabari
    #MvanoMtangazaji
    #M33
    Marais wa Urusi 🇷🇺, V. Putin na yule wa Marekani 🇺🇸, D.Trump walizungumza leo hii kwa muda saa moja na nusu kuhusu kumaliza vita Nchini Ukraine 🇮🇱, kuboresha uhusiano kati ya Marekani na Urusi, na uwezekano wa kubadilishana Wafungwa. Aidha, Putin alimwalika Trump kwenda Mjini Moscow Nchini Urusi na akasema yuko tayari kuwakaribisha Maafisa wa Marekani kwa mazungumzo. Hii ilikuwa simu ya kwanza ya Putin na Rais wa Marekani aliyeko madarakani tangu Februari 2022, alipoongea na Biden muda mfupi kabla ya kutuma Wanajeshi Nchini Ukraine. Toa maoni yako #MvanoHabari #MvanoMtangazaji #M33
    0 Commentarios 0 Acciones 1K Views
  • Mfalme wa Nchi ya Jordan , Abdullah II amekataa pendekezo la Rais wa Marekani Donald Trump la kutaka kuwahamishia Wapalestina Nchini mwake baada ya mazungumzo na Rais Donald Trump wa Marekani, ambaye alishauri Wakazi wa Gaza wapatao milioni mbili (2) kuondolewa kutoka katika eneo lililoharibiwa na vita.

    Katika mkutano na Rais Trump, Mfalme Abdullah alijitolea kuchukua hadi Watoto 2,000 kutoka Gaza, hasa wale wanaohitaji matibabu ya dharura, ikiwemo Watoto wa saratani. Kupitia mtandao wa X, Mfalme Abdullah alisema, "Msimamo wa Jordan ni msimamo wa pamoja wa mataifa ya Kiarabu."

    Sanjari na hayo, Katibu Mkuu wa Umoja wa Nchi za Kiarabu, Ahmed Aboul Gheit, alikosoa pendekezo hilo, akisema kuwa ni lisilokubalika katika ukanda huo, huku Nchi ya China ikisisitiza kuwa Gaza ni ardhi ya Wapalestina.

    Mfalme wa Nchi ya Jordan 🇯🇴, Abdullah II amekataa pendekezo la Rais wa Marekani 🇺🇸 Donald Trump la kutaka kuwahamishia Wapalestina Nchini mwake baada ya mazungumzo na Rais Donald Trump wa Marekani, ambaye alishauri Wakazi wa Gaza wapatao milioni mbili (2) kuondolewa kutoka katika eneo lililoharibiwa na vita. Katika mkutano na Rais Trump, Mfalme Abdullah alijitolea kuchukua hadi Watoto 2,000 kutoka Gaza, hasa wale wanaohitaji matibabu ya dharura, ikiwemo Watoto wa saratani. Kupitia mtandao wa X, Mfalme Abdullah alisema, "Msimamo wa Jordan ni msimamo wa pamoja wa mataifa ya Kiarabu." Sanjari na hayo, Katibu Mkuu wa Umoja wa Nchi za Kiarabu, Ahmed Aboul Gheit, alikosoa pendekezo hilo, akisema kuwa ni lisilokubalika katika ukanda huo, huku Nchi ya China 🇨🇳 ikisisitiza kuwa Gaza ni ardhi ya Wapalestina.
    Like
    1
    0 Commentarios 0 Acciones 998 Views
  • Hatua ya Rais wa Marekani , Donald Trump ya kusitisha misaada yote kwenye baadhi ya Nchi za Afrika ikiwemo Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo iliyokuwa ikitolewa na Marekani imeongeza hali ya wasiwasi Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, ambako mamilioni ya Wakimbizi walikuwa wakitegemea misaada hiyo.

    Afisa kutoka Umoja wa Mataifa, Bruno Lemarquis, amenukuliwa akisema kuwa Nchi ya DR Congo ilikuwa ikipokea asilimia sabini (70) ya misaada ya kibinadamu kutoka Nchini Marekani. Uamuzi wa Trump umesababisha upungufu mkubwa wa mahitaji muhimu kwa Wakimbizi. Afisa huyo ameongeza kuwa kwa mwaka 2024 pekee, DR Congo ilipokea dola milioni 910 kutoka Nchini Marekani pamoja na misaada mingine kwa Waathirika wa mapigano kati ya Majeshi ya Serikali na Waasi Nchini humo.

    Hatua ya Rais wa Marekani 🇺🇸, Donald Trump ya kusitisha misaada yote kwenye baadhi ya Nchi za Afrika ikiwemo Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo iliyokuwa ikitolewa na Marekani imeongeza hali ya wasiwasi Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, ambako mamilioni ya Wakimbizi walikuwa wakitegemea misaada hiyo. Afisa kutoka Umoja wa Mataifa, Bruno Lemarquis, amenukuliwa akisema kuwa Nchi ya DR Congo ilikuwa ikipokea asilimia sabini (70) ya misaada ya kibinadamu kutoka Nchini Marekani. Uamuzi wa Trump umesababisha upungufu mkubwa wa mahitaji muhimu kwa Wakimbizi. Afisa huyo ameongeza kuwa kwa mwaka 2024 pekee, DR Congo ilipokea dola milioni 910 kutoka Nchini Marekani pamoja na misaada mingine kwa Waathirika wa mapigano kati ya Majeshi ya Serikali na Waasi Nchini humo.
    Like
    1
    0 Commentarios 0 Acciones 1K Views
  • Kikundi cha misaada cha Denmark kimetoa dola trilioni moja (1) kwa ajili ya kulinunua Jimbo la California Nchini Marekani siku chache baada ya Rais wa Marekani Donald Trump kusema anataka kulinunua eneo la Greenland lililoko Nchini Denmark. Raia Denmark hao ambao wameonesha kumkejeli Rais trump wamesema watasambaza keki za Denmark katika Jimbo hilo bila kikomo ikiwa wazo lao litapokelewa.

    Trump amekuwa akijadili mara kwa mara kuhusu ununuzi wa Greenland eneo lenye uhuru la Denmark akionyesha thamani yake ya kimkakati na kiuchumi kwa Marekani. Hata hivyo, Maafisa wa Denmark na Greenland wamepinga vikali wazo hilo.

    Trump amesisitiza anaweza kutumia nguvu za kijeshi na kiuchumi ili kupata eneo hilo. Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Marco Rubio, alisisitiza mwezi uliopita kwamba ununuzi wa Greenland ni lengo la kweli na "si jambo la kuchekesha."

    Kikundi cha misaada cha Denmark 🇩🇰 kimetoa dola trilioni moja (1) kwa ajili ya kulinunua Jimbo la California Nchini Marekani 🇺🇸 siku chache baada ya Rais wa Marekani Donald Trump kusema anataka kulinunua eneo la Greenland lililoko Nchini Denmark. Raia Denmark hao ambao wameonesha kumkejeli Rais trump wamesema watasambaza keki za Denmark katika Jimbo hilo bila kikomo ikiwa wazo lao litapokelewa. Trump amekuwa akijadili mara kwa mara kuhusu ununuzi wa Greenland eneo lenye uhuru la Denmark akionyesha thamani yake ya kimkakati na kiuchumi kwa Marekani. Hata hivyo, Maafisa wa Denmark na Greenland wamepinga vikali wazo hilo. Trump amesisitiza anaweza kutumia nguvu za kijeshi na kiuchumi ili kupata eneo hilo. Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Marco Rubio, alisisitiza mwezi uliopita kwamba ununuzi wa Greenland ni lengo la kweli na "si jambo la kuchekesha."
    Love
    1
    0 Commentarios 0 Acciones 354 Views
Resultados de la búsqueda