• Rais wa Nchi Burkina Faso , Kapteni IbrahimTraoré (37) amekataa ongezeko lolote kwenye mshahara wake anaoupata kama kapteni, akisisitiza kuwa anajitolea kwa ajili ya Wananchi wa Nchi hiyo.

    Rais huyo kijana zaidi Duniani, ambaye alichukua madaraka kupitia mapinduzi ya kijeshi, alitangaza kuwa makadirio ya utajiri wake wote ni Shilingi milioni 340 za Kitanzania na ataendelea kupokea mshahara wake uleule wa kawaida kama kapteni wa Jeshi.

    Uamuzi huo wa kukataa ongezeko la mshahara ni tofauti kubwa na hatua za baadhi ya watangulizi wake, ambapo anaonyesha taswira ya Uongozi mpya kabisa katika Nchi ya Burkina Faso.

    Rais wa Nchi Burkina Faso 🇧🇫, Kapteni IbrahimTraoré (37) amekataa ongezeko lolote kwenye mshahara wake anaoupata kama kapteni, akisisitiza kuwa anajitolea kwa ajili ya Wananchi wa Nchi hiyo. Rais huyo kijana zaidi Duniani, ambaye alichukua madaraka kupitia mapinduzi ya kijeshi, alitangaza kuwa makadirio ya utajiri wake wote ni Shilingi milioni 340 za Kitanzania na ataendelea kupokea mshahara wake uleule wa kawaida kama kapteni wa Jeshi. Uamuzi huo wa kukataa ongezeko la mshahara ni tofauti kubwa na hatua za baadhi ya watangulizi wake, ambapo anaonyesha taswira ya Uongozi mpya kabisa katika Nchi ya Burkina Faso.
    0 Comments ·0 Shares ·16 Views
  • "Pengine ulitegemea baada ya kutumikia kifungo cha 'kikatili’ dhidi yangu na kilichojaa Uonevu usiomithilika,labda tukikutana ntaleta nongwa ya Kizaramo? Hapana laa hasha!! Sipo hivyo na nilishasamehe.

    Ila haiondoi ukweli pamoja na ‘ cheko hili tukikutana’ inabidi akubali kuwajibika yeye na wenzie.
    Tutacheka lakini tutaendelea kushinikiza aombe radhi na apumzike uongozi kwa sasa.

    #KariaMustGo" - Haji Manara baada ya kukutana na Rais wa Shirikisho la mpira wa miguu Nchini Tanzania (TFF).

    "Pengine ulitegemea baada ya kutumikia kifungo cha 'kikatili’ dhidi yangu na kilichojaa Uonevu usiomithilika,labda tukikutana ntaleta nongwa ya Kizaramo? Hapana laa hasha!! Sipo hivyo na nilishasamehe. Ila haiondoi ukweli pamoja na ‘ cheko hili tukikutana’ inabidi akubali kuwajibika yeye na wenzie. Tutacheka lakini tutaendelea kushinikiza aombe radhi na apumzike uongozi kwa sasa. #KariaMustGo" - Haji Manara baada ya kukutana na Rais wa Shirikisho la mpira wa miguu Nchini Tanzania (TFF).
    0 Comments ·0 Shares ·17 Views
  • Mchambuzi Farhan JR.

    Nimeona andiko la Waukae @zakazakazi kuhusu TFF kutengeneza Vijana ambalo lilipaswa kuwa jukumu la Klabu na akienda mbali kusema kwamba TFF ndio Shirikisho pekee duniani ambalo lina kituo ambacho kinazalisha na kulea vipaji vya vijana, kwanza kabla ya kupingana nae kuna kitu kwanza nataka kukiweka sawa kwenye eneo hilo.

    Duniani kote Mashirikisho kama TFF yamejikita zaidi kwenye DEVELOPMENT PROJECTS yaani Miradi ya maendeleo kisha wakaachia Mashindano kadhaa yasimamiwe na Bodi zao za Ligi kwa 90% bila kuyaingilia, TFF anachokifanya ni sahihi lakini pia sio sahihi sana kufanya yeye alipaswa kuwa na CLINICS tu ila kuna changamoto sehemu ambayo imeletwa na TFF wenyewe.

    Duniani Klabu zinaweza kuendesha miradi ya Vijana kwasababu kuna kitu kinaitwa FALSAFA ya nchi kwenye mpira, kuanzia mifumo, afya tiba, afya lishe na miundo yote ambayo portifolio hutoka Shirikisho (TFF) Klabu zinaenda kutekeleza mifumo hiyo na kuadjust baadhi ya maeneo halafu Vijana wakienda Clinics za Kitaifa wanaenda kukazia tu.

    Swali linakuja Je Waukaye @zakazakazi FALSAFA ya Tanzania kwenye mpira wa Miguu ni ipi? Iliwasilishwa lini? Anayo nani? Hilo ni Jukumu la TFF ambalo halijatekelezwa, kuna kitu kinaitwa TALENT ID FRAMEWORK ili kupata Vijana je tunayo? Ipoje, anayo nani? Inasemaje? Klabu hazina Mwongozo kutoka kwa TFF? Academy zote nchini zipite humo LAZIMA TFF wafanye wanachoweza, tupo katikati, TFF ASIMAMIE HILO KIKAMILIFU.

    TFF wasiende mbali waende tu hapo Uganda ilipo FUFA, wana Talent ID Framework ambayo Mashirikisho yoote yalipigwa huo Msasa sambamba na Kamati zao tendaji, ndio maana Uganda wapo mbali mno kwenye soka la Vijana kwenye Klabu zao na National Team, kwasababu wana ramani wanaifuata, wameintergrate mfumo wao na FIFA Talent Development Schemes (TDS) je sisi lini tutaforce Klabu zipite humo?

    TFF anajipa majukumu ambayo mengine sio ya kwake, kujadili mikataba ya kibiashara sio Jukumu lake bali Vilabu na Bodi yao, TFF anabaki kama Baba pekee, duniani kote TFF zao zina majukumu yao ukitoa michuano ya FA na Ngao basi Ligi Kuu sio mali yao, TFF ASIMAMIE HASWA JUKUMU LA MAENDELEO NI LAKE.

    Mchambuzi Farhan JR. Nimeona andiko la Waukae @zakazakazi kuhusu TFF kutengeneza Vijana ambalo lilipaswa kuwa jukumu la Klabu na akienda mbali kusema kwamba TFF ndio Shirikisho pekee duniani ambalo lina kituo ambacho kinazalisha na kulea vipaji vya vijana, kwanza kabla ya kupingana nae kuna kitu kwanza nataka kukiweka sawa kwenye eneo hilo. Duniani kote Mashirikisho kama TFF yamejikita zaidi kwenye DEVELOPMENT PROJECTS yaani Miradi ya maendeleo kisha wakaachia Mashindano kadhaa yasimamiwe na Bodi zao za Ligi kwa 90% bila kuyaingilia, TFF anachokifanya ni sahihi lakini pia sio sahihi sana kufanya yeye alipaswa kuwa na CLINICS tu ila kuna changamoto sehemu ambayo imeletwa na TFF wenyewe. Duniani Klabu zinaweza kuendesha miradi ya Vijana kwasababu kuna kitu kinaitwa FALSAFA ya nchi kwenye mpira, kuanzia mifumo, afya tiba, afya lishe na miundo yote ambayo portifolio hutoka Shirikisho (TFF) Klabu zinaenda kutekeleza mifumo hiyo na kuadjust baadhi ya maeneo halafu Vijana wakienda Clinics za Kitaifa wanaenda kukazia tu. Swali linakuja Je Waukaye @zakazakazi FALSAFA ya Tanzania kwenye mpira wa Miguu ni ipi? Iliwasilishwa lini? Anayo nani? Hilo ni Jukumu la TFF ambalo halijatekelezwa, kuna kitu kinaitwa TALENT ID FRAMEWORK ili kupata Vijana je tunayo? Ipoje, anayo nani? Inasemaje? Klabu hazina Mwongozo kutoka kwa TFF? Academy zote nchini zipite humo LAZIMA TFF wafanye wanachoweza, tupo katikati, TFF ASIMAMIE HILO KIKAMILIFU. TFF wasiende mbali waende tu hapo Uganda ilipo FUFA, wana Talent ID Framework ambayo Mashirikisho yoote yalipigwa huo Msasa sambamba na Kamati zao tendaji, ndio maana Uganda wapo mbali mno kwenye soka la Vijana kwenye Klabu zao na National Team, kwasababu wana ramani wanaifuata, wameintergrate mfumo wao na FIFA Talent Development Schemes (TDS) je sisi lini tutaforce Klabu zipite humo? TFF anajipa majukumu ambayo mengine sio ya kwake, kujadili mikataba ya kibiashara sio Jukumu lake bali Vilabu na Bodi yao, TFF anabaki kama Baba pekee, duniani kote TFF zao zina majukumu yao ukitoa michuano ya FA na Ngao basi Ligi Kuu sio mali yao, TFF ASIMAMIE HASWA JUKUMU LA MAENDELEO NI LAKE.
    0 Comments ·0 Shares ·21 Views
  • Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo wa Tanzania , Profesa Palamagamba Kabudi anatarajiwa kukutana na Viongozi wa klabu za Simba SC na Yanga SC kuzungumzia sakata la uamuzi wa klabu ya Simba SC kugomea mechi ya watani wa jadi iliyokuwa ifanyike Machi 8, 2025 kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam.

    Pamoja na Viongozi hao wa klabu ya Simba SC na Yanga SC, Wengine ambao wanatarajiwa kushiriki kikao hicho kilichopangwa kufanyika Machi 27 mwaka huu ni Viongozi wa Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania (TFF) pamoja na Viongozi kutoka Bodi ya Ligi Kuu ya Tanzania Bara (TPBL).

    Ikumbukwe kwamba klabu ya Simba Sports SC iligomea mchezo huo kwa madai ya ukiukwaji wa Kanuni namba 17(45) ya Kanuni za Ligi Kuu Tanzania Bara kwa zuiliwa kwa Vijana (Mabausa) waliodhaniwa kuwa ni wa klabu ya Yanga SC, ambayo inaruhusu klabu ngeni kufanya mazoezi kwenye Uwanja wa mechi angalau mara moja kabla ya siku ya mechi.

    Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo wa Tanzania 🇹🇿, Profesa Palamagamba Kabudi anatarajiwa kukutana na Viongozi wa klabu za Simba SC na Yanga SC kuzungumzia sakata la uamuzi wa klabu ya Simba SC kugomea mechi ya watani wa jadi iliyokuwa ifanyike Machi 8, 2025 kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam. Pamoja na Viongozi hao wa klabu ya Simba SC na Yanga SC, Wengine ambao wanatarajiwa kushiriki kikao hicho kilichopangwa kufanyika Machi 27 mwaka huu ni Viongozi wa Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania (TFF) pamoja na Viongozi kutoka Bodi ya Ligi Kuu ya Tanzania Bara (TPBL). Ikumbukwe kwamba klabu ya Simba Sports SC iligomea mchezo huo kwa madai ya ukiukwaji wa Kanuni namba 17(45) ya Kanuni za Ligi Kuu Tanzania Bara kwa zuiliwa kwa Vijana (Mabausa) waliodhaniwa kuwa ni wa klabu ya Yanga SC, ambayo inaruhusu klabu ngeni kufanya mazoezi kwenye Uwanja wa mechi angalau mara moja kabla ya siku ya mechi.
    0 Comments ·0 Shares ·51 Views
  • "Najisikia vibaya namna watu wanavyoniona na kuanza kuniita Yesu, wanafikia hata kutundika picha zangu katika nyumba zao, mimi ni mwigizaji tu, mimi ni mtu" - Jonathan Roumie(50), mwigizaji wa Marekani

    Aidha, Jonathan Roumie katika mahojiano amesema maisha yake binafsi alikuwa na hali mbaya kiuchumi hakuwa na uhakika siku inayofuata atakula nini, alikuwa mwigizaji ila kiuchumi alikuwa bado hajafanikiwa. Baada ya mambo kuzidi kuwa magumu siku moja ni kama alikuwa anamuomba Mungu kuhusu hali anayopitia ili mambo yake yakae sawa

    Baada ya miezi kama mitatu ndio akapata nafasi ya kuigiza kama Yesu katika series ya "The Chosen" iliyoanza kuoneshwa 2017 ambayo imejipatia umaarufu mkubwa sana hadi sasa imetazamwa na watu zaidi ya milioni 250 na misimu mipya inafuata huku ikipongezwa kwa kinachoonekana kuigizwa

    Umaarufu wa uhusika wake kama Yesu umempa umaarufu mkubwa na fursa nyingi ikiwemo katika mikutano na makongamano makubwa ya kidini na app za dini ya kikiristo

    Jonathan ambaye ni mkatoliki, alipoulizwa na New York Times, je ni tukio gani gumu analokumbuka ambalo alishakutana nalo baada ya kuigiza kama Yesu, amejibu kwa kusema kuna kipindi alikuwa katika mkutano kwenye uwanja wenye watu takribani 40,000 baadaye alishuka stejini akaenda kwenye chumba fulani uwanjani hapo, mmoja wa walinzi alikuja akamwambia nje kuna mwanamke ana mtoto kwenye kiti cha magurudumu anaomba kusalimiana na wewe

    Jonathan alitoka akaonana na mwanamke husika na mwanae ambaye kwa ufupi alieleza jinsi Yesu alivyoponya mtu katika hiyo series ya "The Chosen" na kusema angependa mwanae pia apone yaani akimtaka Jonathan amponye mtoto wake. Ilibidi Jonathan amueleze ukweli kwamba yeye sio mponyaji wala mhubiri bali ni mwigizaji tu.

    Jonathan akamueleza wafanye maombi wote ilichukua kama dakika moja, walipomaliza maombi wakafurahi na kushukuru kisha Jonathan akarudi alipokuwa huku akitokwa na machozi akihisi amewaangusha matarajio waliyokuwa nayo kwake ila amesema ni bora waujue ukweli kuwa yeye sio Yesu wala mponyaji bali ni mwigizaji tu

    Ukiacha hayo ya uhusika wake wa Yesu na dini, Jonathan Roumie amegusia pia kwamba alishafika Tanzania na Rwanda sababu kuna watoto kadhaa wanaoishi katika mazingira magumu huwa anawasaidia na familia zao

    Jonathan Roumie pia ameweka wazi kwamba anatamani watu pia wawe wanamuona katika nyuma ya pazia(behind the scene) anayopitia katika kujiandaa na uigizaji wake kama Yesu ili watu wengine waelewe wajue kumtofautisha katika maisha halisi na kisanaa

    KUMBUKA, zipo filamu nyingine miaka ya nyuma kuhusu Yesu zilizohusisha waigizaji wengine kabla ya sasa Jonathan Roumie kupata umaarufu na uhusika wa Yesu katika series maarufu ya "The Chosen"
    (Swahili Word)

    "Najisikia vibaya namna watu wanavyoniona na kuanza kuniita Yesu, wanafikia hata kutundika picha zangu katika nyumba zao, mimi ni mwigizaji tu, mimi ni mtu" - Jonathan Roumie(50), mwigizaji wa Marekani Aidha, Jonathan Roumie katika mahojiano amesema maisha yake binafsi alikuwa na hali mbaya kiuchumi hakuwa na uhakika siku inayofuata atakula nini, alikuwa mwigizaji ila kiuchumi alikuwa bado hajafanikiwa. Baada ya mambo kuzidi kuwa magumu siku moja ni kama alikuwa anamuomba Mungu kuhusu hali anayopitia ili mambo yake yakae sawa Baada ya miezi kama mitatu ndio akapata nafasi ya kuigiza kama Yesu katika series ya "The Chosen" iliyoanza kuoneshwa 2017 ambayo imejipatia umaarufu mkubwa sana hadi sasa imetazamwa na watu zaidi ya milioni 250 na misimu mipya inafuata huku ikipongezwa kwa kinachoonekana kuigizwa Umaarufu wa uhusika wake kama Yesu umempa umaarufu mkubwa na fursa nyingi ikiwemo katika mikutano na makongamano makubwa ya kidini na app za dini ya kikiristo Jonathan ambaye ni mkatoliki, alipoulizwa na New York Times, je ni tukio gani gumu analokumbuka ambalo alishakutana nalo baada ya kuigiza kama Yesu, amejibu kwa kusema kuna kipindi alikuwa katika mkutano kwenye uwanja wenye watu takribani 40,000 baadaye alishuka stejini akaenda kwenye chumba fulani uwanjani hapo, mmoja wa walinzi alikuja akamwambia nje kuna mwanamke ana mtoto kwenye kiti cha magurudumu anaomba kusalimiana na wewe Jonathan alitoka akaonana na mwanamke husika na mwanae ambaye kwa ufupi alieleza jinsi Yesu alivyoponya mtu katika hiyo series ya "The Chosen" na kusema angependa mwanae pia apone yaani akimtaka Jonathan amponye mtoto wake. Ilibidi Jonathan amueleze ukweli kwamba yeye sio mponyaji wala mhubiri bali ni mwigizaji tu. Jonathan akamueleza wafanye maombi wote ilichukua kama dakika moja, walipomaliza maombi wakafurahi na kushukuru kisha Jonathan akarudi alipokuwa huku akitokwa na machozi akihisi amewaangusha matarajio waliyokuwa nayo kwake ila amesema ni bora waujue ukweli kuwa yeye sio Yesu wala mponyaji bali ni mwigizaji tu Ukiacha hayo ya uhusika wake wa Yesu na dini, Jonathan Roumie amegusia pia kwamba alishafika Tanzania na Rwanda sababu kuna watoto kadhaa wanaoishi katika mazingira magumu huwa anawasaidia na familia zao Jonathan Roumie pia ameweka wazi kwamba anatamani watu pia wawe wanamuona katika nyuma ya pazia(behind the scene) anayopitia katika kujiandaa na uigizaji wake kama Yesu ili watu wengine waelewe wajue kumtofautisha katika maisha halisi na kisanaa KUMBUKA, zipo filamu nyingine miaka ya nyuma kuhusu Yesu zilizohusisha waigizaji wengine kabla ya sasa Jonathan Roumie kupata umaarufu na uhusika wa Yesu katika series maarufu ya "The Chosen" (Swahili Word)
    0 Comments ·0 Shares ·40 Views
  • Zungu, Mtangazaji na Mchambuzi

    CPA Amos Makala kiongozi wa juu wa CCM amesema kuwa Chadema wana mpango wa kununua virusi via Ebola na Mpox ili kuzuia uchaguzi!!

    Maswali yangu kufuatia kauli ya CPA Amos Makala

    1. Hizi taarifa Makala amezipata wapi ?

    2. Idara ya usalama wa taifa (TISS) inataarifa za mpango huu ?, kama hakuna taarifa turejee kwenye swali la kwanza! Kama kuna taarifa hadi sasa ni hatua gani zimechukuliwa?

    3. Makala anatuambia kwa lugha nyingine baadhi ya viongozi wa Chadema wana mpango wa uhaini na kuhujumu uchumi wa nchi je kwanini vyombo vipo kimya kwa watu wenye tuhuma nzito kama hizi ?

    4. Je Makala amepima madhara ya kauli aliyoitoa hadharani ambayo huenda inazua taharuki na hofu kwa wananchi wa Tanzania na kwa wageni amabao wana mpango wa kuitembelea Tanzania kwa siku za usoni ?

    5. Ni hatua gani za kujibu ambazo Chadema wamezichukua hadi sasa ?

    6. Je ni kauli ya maksudi tu ili kuhamisha upepo na mjadala wa chadema ambao utashika kasi kwenye mikutano yao ya hadhara inayoanza hivi punde, kuhusu mpango wao wa no reform no election ?

    7. Je Makala anaweza kuthibitishaje kauli yake kwa Umma ?

    8.Je Chadema watanunulia wapi hivyo virusi, na kumbe vinauzwaga, Makala anaweza kuthibitisha ?

    Zungu, Mtangazaji na Mchambuzi CPA Amos Makala kiongozi wa juu wa CCM amesema kuwa Chadema wana mpango wa kununua virusi via Ebola na Mpox ili kuzuia uchaguzi!! Maswali yangu kufuatia kauli ya CPA Amos Makala 👇👇👇👇 1. Hizi taarifa Makala amezipata wapi ? 2. Idara ya usalama wa taifa (TISS) inataarifa za mpango huu ?, kama hakuna taarifa turejee kwenye swali la kwanza! Kama kuna taarifa hadi sasa ni hatua gani zimechukuliwa? 3. Makala anatuambia kwa lugha nyingine baadhi ya viongozi wa Chadema wana mpango wa uhaini na kuhujumu uchumi wa nchi je kwanini vyombo vipo kimya kwa watu wenye tuhuma nzito kama hizi ? 4. Je Makala amepima madhara ya kauli aliyoitoa hadharani ambayo huenda inazua taharuki na hofu kwa wananchi wa Tanzania na kwa wageni amabao wana mpango wa kuitembelea Tanzania kwa siku za usoni ? 5. Ni hatua gani za kujibu ambazo Chadema wamezichukua hadi sasa ? 6. Je ni kauli ya maksudi tu ili kuhamisha upepo na mjadala wa chadema ambao utashika kasi kwenye mikutano yao ya hadhara inayoanza hivi punde, kuhusu mpango wao wa no reform no election ? 7. Je Makala anaweza kuthibitishaje kauli yake kwa Umma ? 8.Je Chadema watanunulia wapi hivyo virusi, na kumbe vinauzwaga, Makala anaweza kuthibitisha ?
    0 Comments ·0 Shares ·61 Views
  • Nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imetangaza rasmi kuondoa hitaji la visa kwa Watanzania wanaoingia Nchini humo, kuanzia tarehe 20 Machi, 2025. Hatua hii ni sehemu ya utekelezaji wa uanachama wa DR Congo katika Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na jitihada za kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia na kiuchumi kati ya mataifa hayo mawili.

    Ikumbukwe kwamba Nchi ya Tanzania ilikuwa imeondoa utaratibu wa malipo ya visa kwa Raia wa DRC tangu Septemba 2, 2023, ikitarajia hatua ya kurudishiwa fadhila. Uamuzi wa sasa wa DR Congo unaimarisha mahusiano ya ujirani mwema na kufungua fursa zaidi za biashara na ushirikiano wa kikanda.

    Serikali ya Tanzania imesifu hatua hiyo, ikisisitiza kuwa inalingana na ajenda za Jumuiya ya Afrika Mashariki na Mkataba wa Eneo Huru la Biashara la Afrika (AfCFTA). Hatua hii inaashiria ushirikiano bora wa kidiplomasia na unaleta unafuu mkubwa kwa Wafanyabiashara na wasafiri wa pande zote mbili.

    Nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo 🇨🇩 imetangaza rasmi kuondoa hitaji la visa kwa Watanzania wanaoingia Nchini humo, kuanzia tarehe 20 Machi, 2025. Hatua hii ni sehemu ya utekelezaji wa uanachama wa DR Congo katika Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na jitihada za kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia na kiuchumi kati ya mataifa hayo mawili. Ikumbukwe kwamba Nchi ya Tanzania 🇹🇿 ilikuwa imeondoa utaratibu wa malipo ya visa kwa Raia wa DRC tangu Septemba 2, 2023, ikitarajia hatua ya kurudishiwa fadhila. Uamuzi wa sasa wa DR Congo unaimarisha mahusiano ya ujirani mwema na kufungua fursa zaidi za biashara na ushirikiano wa kikanda. Serikali ya Tanzania imesifu hatua hiyo, ikisisitiza kuwa inalingana na ajenda za Jumuiya ya Afrika Mashariki na Mkataba wa Eneo Huru la Biashara la Afrika (AfCFTA). Hatua hii inaashiria ushirikiano bora wa kidiplomasia na unaleta unafuu mkubwa kwa Wafanyabiashara na wasafiri wa pande zote mbili.
    0 Comments ·0 Shares ·68 Views
  • Klabu ya Kengold inayoshiriki Ligi Kuu Tanzania Bara, imeiandikia barua redio ya FURAHA FM kupitia kwa Mwanasheria wake Nicky Ngale wakidai fidia ya Shilingi Billion moja na kuombwa radhi kupitia mitandao ya Kijamii baada ya Radio hiyo kupitia mtandao wake wa Kijamii wa Instagram kuchapisha taarifa kuwa:

    “Kengold yaomba alama 15 atakazokatwa Simba na TFF, wapewe wao alama tatu”

    Kufuatia kuchapisha chapisho hilo, Mwanasheria anadai Mteja wake ameathirika kwa kiasi kikubwa huku jina lao likichafuka kwa kiasi kikubwa, nje na hapo matakwa yao yote yanapaswa kutimizwa ndani ya siku saba (7).

    Klabu ya Kengold inayoshiriki Ligi Kuu Tanzania Bara, imeiandikia barua redio ya FURAHA FM kupitia kwa Mwanasheria wake Nicky Ngale wakidai fidia ya Shilingi Billion moja na kuombwa radhi kupitia mitandao ya Kijamii baada ya Radio hiyo kupitia mtandao wake wa Kijamii wa Instagram kuchapisha taarifa kuwa: “Kengold yaomba alama 15 atakazokatwa Simba na TFF, wapewe wao alama tatu” Kufuatia kuchapisha chapisho hilo, Mwanasheria anadai Mteja wake ameathirika kwa kiasi kikubwa huku jina lao likichafuka kwa kiasi kikubwa, nje na hapo matakwa yao yote yanapaswa kutimizwa ndani ya siku saba (7).
    0 Comments ·0 Shares ·142 Views
  • World Happiness Report 2025 imetangaza orodha ya Nchi zenye furaha zaidi Duniani huku Nchi ya Finland ikiendelea kushika nafasi ya kwanza kwa mwaka wa nane (8) mfululizo, Tanzania imeshika nafasi ya 136 kati ya Nchi 147, ikishuka kwa nafasi tano kutoka nafasi ya 131 mwaka uliopita. Nafasi ya sasa inaiweka Nchi hiyo kuwa miongoni mwa Nchi 11 za mwisho Duniani kwa viwango vya furaha.

    Cha kushangaza ni kwamba Tanzania , licha ya kuwa na amani na utajiri mkubwa wa maliasili, imepitwa hata na mataifa yenye migogoro kama Somalia . Nchi jirani kama Kenya na Uganda , ambazo mara kwa mara hukumbwa na changamoto za kisiasa na kiusalama, zimepata nafasi za juu zaidi. Hapa chini ni orodha ya Nchi zenye furaha kwa mujibu wa World Happiness Report 2025, kuonyesha kumi bora na zilizoshika mkia. Kwa Afrika Mauritius inaongoza, wakati Lebanon , Sierra Leone na Afghanistan ni Nchi tatu za mwisho Duniani.

    1. Finland
    2. Denmark
    3. Iceland
    4. Sweden
    5. Uholanzi

    6. Costa Rica
    7. Norway
    8. Israel
    9. Luxemborg
    10.Mexico

    78. Mauritius
    79. Libya
    84. Algeria
    115. Kenya
    116. Uganda

    122. Somalia
    136. Tanzania
    145. Lebanon
    146. Sierra Leone
    147. Afghanistan

    World Happiness Report 2025 imetangaza orodha ya Nchi zenye furaha zaidi Duniani huku Nchi ya Finland 🇫🇮 ikiendelea kushika nafasi ya kwanza kwa mwaka wa nane (8) mfululizo, Tanzania imeshika nafasi ya 136 kati ya Nchi 147, ikishuka kwa nafasi tano kutoka nafasi ya 131 mwaka uliopita. Nafasi ya sasa inaiweka Nchi hiyo kuwa miongoni mwa Nchi 11 za mwisho Duniani kwa viwango vya furaha. Cha kushangaza ni kwamba Tanzania 🇹🇿, licha ya kuwa na amani na utajiri mkubwa wa maliasili, imepitwa hata na mataifa yenye migogoro kama Somalia 🇸🇴. Nchi jirani kama Kenya 🇰🇪 na Uganda 🇺🇬, ambazo mara kwa mara hukumbwa na changamoto za kisiasa na kiusalama, zimepata nafasi za juu zaidi. Hapa chini ni orodha ya Nchi zenye furaha kwa mujibu wa World Happiness Report 2025, kuonyesha kumi bora na zilizoshika mkia. Kwa Afrika Mauritius 🇲🇷 inaongoza, wakati Lebanon 🇱🇧, Sierra Leone 🇸🇱na Afghanistan 🇦🇫 ni Nchi tatu za mwisho Duniani. 1. Finland 🇫🇮 2. Denmark 🇩🇰 3. Iceland 🇮🇸 4. Sweden 🇸🇪 5. Uholanzi 🇳🇱 6. Costa Rica 🇨🇷 7. Norway 🇳🇴 8. Israel 🇮🇱 9. Luxemborg 🇱🇺 10.Mexico 🇲🇽 78. Mauritius 🇲🇷 79. Libya 🇱🇾 84. Algeria 🇩🇿 115. Kenya 🇰🇪 116. Uganda 🇺🇬 122. Somalia 🇸🇴 136. Tanzania 🇹🇿 145. Lebanon 🇱🇧 146. Sierra Leone 🇸🇱 147. Afghanistan 🇦🇫
    0 Comments ·0 Shares ·125 Views
  • Ahmed Ally, Msemaji wa klabu ya Simba SC

    Anatokea mwehu mmoja anamdhihaki huyu Rais au kikundi cha vijana wa hovyo wanadhihaki Mamlaka za mpira wetu, Hii Nchi uhuru umepitiliza sana

    Wallace Karia, TFF na Bodi ya Ligi Wanapaswa kuheshimiwa, kuenziwa, kutunzwa na kulindwa maana wamefanya kazi kubwa na wanaendelea kufanya kazi kubwa kwenye mpira wetu

    Yote tuliyokua tunayaota kwenye mpira sasa hivi yanatokea, yale tuliyodhani ni magumu kwa Karia yamewezekana

    Na kama haitoshi tunaiona kesho njema ya mpira wa Tanzania chini ya Karia na wenzake

    President @wallacekaria na Uongozi wako wa TFF na Bodi ya ligi msirudi nyuma na msikubali mtu akaturudisha nyuma sasa hivi tunawaza World Cup tunawaza Utawala wa AFCON na Ubingwa Afrika ngazi klabu

    KAMA HUMPENDI KARIA PENDA MAFANIKIO YAKE"

    Ahmed Ally, Msemaji wa klabu ya Simba SC ✍️ Anatokea mwehu mmoja anamdhihaki huyu Rais au kikundi cha vijana wa hovyo wanadhihaki Mamlaka za mpira wetu, Hii Nchi uhuru umepitiliza sana Wallace Karia, TFF na Bodi ya Ligi Wanapaswa kuheshimiwa, kuenziwa, kutunzwa na kulindwa maana wamefanya kazi kubwa na wanaendelea kufanya kazi kubwa kwenye mpira wetu Yote tuliyokua tunayaota kwenye mpira sasa hivi yanatokea, yale tuliyodhani ni magumu kwa Karia yamewezekana Na kama haitoshi tunaiona kesho njema ya mpira wa Tanzania chini ya Karia na wenzake President @wallacekaria na Uongozi wako wa TFF na Bodi ya ligi msirudi nyuma na msikubali mtu akaturudisha nyuma sasa hivi tunawaza World Cup tunawaza Utawala wa AFCON na Ubingwa Afrika ngazi klabu KAMA HUMPENDI KARIA PENDA MAFANIKIO YAKE"
    Like
    1
    · 0 Comments ·0 Shares ·198 Views
  • Klabu ya Yanga SC imefungua malalamiko kwenye Mahakama ya usuhishi wa michezo Duniani (CAS) baada ya kutoridhishwa na majibu ya TFF. Klabu ya Yanga haina imani na Bodi ya Ligi Kuu Tanzania Bara na wameshindwa kukubaliana kabisa na majibu ya barua iliyotoka na hivyo wameamuwa kusonga mbele (CAS) ili kudai haki yao.

    Mara ya baada ya kutuma malalamiko yao CAS, klabu ya Yanga SC itasubiri taratibu kutoka katika Mahakama hiyo kisha kesi yao kuanza kusikilizwa.

    Klabu ya Yanga SC imefungua malalamiko kwenye Mahakama ya usuhishi wa michezo Duniani (CAS) baada ya kutoridhishwa na majibu ya TFF. Klabu ya Yanga haina imani na Bodi ya Ligi Kuu Tanzania Bara na wameshindwa kukubaliana kabisa na majibu ya barua iliyotoka na hivyo wameamuwa kusonga mbele (CAS) ili kudai haki yao. Mara ya baada ya kutuma malalamiko yao CAS, klabu ya Yanga SC itasubiri taratibu kutoka katika Mahakama hiyo kisha kesi yao kuanza kusikilizwa.
    Like
    Haha
    2
    · 0 Comments ·0 Shares ·152 Views
  • Kwenye barua ambayo Bodi ya Ligi Kuu Tanzania Bara (TPLB) imewajibu Yanga yenye kumbukumbu namba TPLB/2024/625 ya Machi 16,2025 imewaambia Yanga hawawezi kupewa alama tatu kutokana na kuwa hakuna KANUNI ya Ligi Kuu inayoamuru jambo hilo ambapo TPLB imewapa sababu takribani 10, nitazielezea kwa uchache.

    1. Mchezo ulighairishwa na Bodi majira ya saa8 Mchana ambapo baada ya Bodi huo hapakuwa na Afisa yoyote wa mchezo zaidi ya Watu wa Usalama.

    2. Hakuna taratibu zozote za mchezo zilizofanyika uwanjani kwa mujibu wa Kanuni ya 17 ikiwemo timu kukaguliwa na ili timu ipewe alama tatu na mabao matatu ilipaswa ukaguzi kufanyika na Maafisa ww Mchezo.

    3. Bodi ilishindwa kuruhusu mchezo uchezwe sio kwasababu Simba ALIGOMEA mechi bali kupitia Kamati ya Masaa 72 ikaamuru kupitia sababu mbalimbali za Kikanuni kughairisha mchezo huo baada ya kupokea pia ripoti mbalimbali kutoka Maafisa wa mchezo huo.

    4. Yanga SC wameambiwa kwamba hakuna Kanuni inasema Klabu Mgeni anapaswa kuwataarifu wao kwamba wanakuja kufanya mazoezi, hivyo suala la mawasiliano ni MWONGOZO tu wa Bodi hivyo Simba haikuvunja Kanuni kutowasiliana bali ilivunja MIONGOZO.

    5. Yanga SC wamejibiwa kuwa haitowapa alama tatu kwakuwa sababu za kughairisha mchezo zilikuwa ni za kiusalama, ambapo kulikuwa na tuhuma za rushwa, vitisho na kasoro za Kiusalama hivyo ingekuwa ngumu kuruhusu mchezo uendelee ambao ungeleta kasoro, kabla, wakati na baada ya mchezo.

    6. Yanga SC wanalaumiwa na Bodi kitendo cha kupeleka timu uwanjani wakati mechi imeshaghairishwa ni kinyume na Kanuni ya 47(18) na imeonesha kupingana na Mamlaka.

    7. Kuhusu gharama za mchezo ambazo Yanga wameziingia Bodi inasema itazighulikia Kikanuni.

    8. Bodi imewatakia Yanga maandalizi mema ya mchezo ujao wa Derby ambapo watawapangia rasmi tarehe.
    Etc.

    Kwenye barua ambayo Bodi ya Ligi Kuu Tanzania Bara (TPLB) imewajibu Yanga yenye kumbukumbu namba TPLB/2024/625 ya Machi 16,2025 imewaambia Yanga hawawezi kupewa alama tatu kutokana na kuwa hakuna KANUNI ya Ligi Kuu inayoamuru jambo hilo ambapo TPLB imewapa sababu takribani 10, nitazielezea kwa uchache. 1. Mchezo ulighairishwa na Bodi majira ya saa8 Mchana ambapo baada ya Bodi huo hapakuwa na Afisa yoyote wa mchezo zaidi ya Watu wa Usalama. 2. Hakuna taratibu zozote za mchezo zilizofanyika uwanjani kwa mujibu wa Kanuni ya 17 ikiwemo timu kukaguliwa na ili timu ipewe alama tatu na mabao matatu ilipaswa ukaguzi kufanyika na Maafisa ww Mchezo. 3. Bodi ilishindwa kuruhusu mchezo uchezwe sio kwasababu Simba ALIGOMEA mechi bali kupitia Kamati ya Masaa 72 ikaamuru kupitia sababu mbalimbali za Kikanuni kughairisha mchezo huo baada ya kupokea pia ripoti mbalimbali kutoka Maafisa wa mchezo huo. 4. Yanga SC wameambiwa kwamba hakuna Kanuni inasema Klabu Mgeni anapaswa kuwataarifu wao kwamba wanakuja kufanya mazoezi, hivyo suala la mawasiliano ni MWONGOZO tu wa Bodi hivyo Simba haikuvunja Kanuni kutowasiliana bali ilivunja MIONGOZO. 5. Yanga SC wamejibiwa kuwa haitowapa alama tatu kwakuwa sababu za kughairisha mchezo zilikuwa ni za kiusalama, ambapo kulikuwa na tuhuma za rushwa, vitisho na kasoro za Kiusalama hivyo ingekuwa ngumu kuruhusu mchezo uendelee ambao ungeleta kasoro, kabla, wakati na baada ya mchezo. 6. Yanga SC wanalaumiwa na Bodi kitendo cha kupeleka timu uwanjani wakati mechi imeshaghairishwa ni kinyume na Kanuni ya 47(18) na imeonesha kupingana na Mamlaka. 7. Kuhusu gharama za mchezo ambazo Yanga wameziingia Bodi inasema itazighulikia Kikanuni. 8. Bodi imewatakia Yanga maandalizi mema ya mchezo ujao wa Derby ambapo watawapangia rasmi tarehe. Etc.
    0 Comments ·0 Shares ·170 Views
  • Mchezaji wa klabu ya Yanga SC na Askari, Ibrahim Bacca amepandishwa cheo kutoka kuwa Koplo hadi Sajenti. Mchezaji huyo amepandishwa cheo kutokana na kuonyesha kiwango bora katika klabu yake ya Yanga SC pamoja na timu ya taifa ya Tanzania (Taifa stars).

    Mchezaji wa klabu ya Yanga SC na Askari, Ibrahim Bacca amepandishwa cheo kutoka kuwa Koplo hadi Sajenti. Mchezaji huyo amepandishwa cheo kutokana na kuonyesha kiwango bora katika klabu yake ya Yanga SC pamoja na timu ya taifa ya Tanzania (Taifa stars).
    0 Comments ·0 Shares ·137 Views
  • “Taratibu zitafuatwa na tuziache zifuatwe,Lakini huwezi Kusema Bodi ya Ligi Kuu (TPLB) Ijiuzulu. Hata wanaosema Bodi ijiuzulu wawaambie na Viongozi wao wenyewe wako Sawa? Hawastahili Kujiuzulu?

    “Vitu vingine Vinafanyika vya Kitoto,Vya Kijinga sijui vinataka Kutujaribu au Kutuporomoshea mpira wetu .Kama watu wamechoka Kucheza mpira basi wakaendelee na Sinema zao” - Wallace Karia, Rais wa Shirikisho la mpira wa miguu Nchini Tanzania (TFF).

    “Taratibu zitafuatwa na tuziache zifuatwe,Lakini huwezi Kusema Bodi ya Ligi Kuu (TPLB) Ijiuzulu. Hata wanaosema Bodi ijiuzulu wawaambie na Viongozi wao wenyewe wako Sawa? Hawastahili Kujiuzulu? “Vitu vingine Vinafanyika vya Kitoto,Vya Kijinga sijui vinataka Kutujaribu au Kutuporomoshea mpira wetu .Kama watu wamechoka Kucheza mpira basi wakaendelee na Sinema zao” - Wallace Karia, Rais wa Shirikisho la mpira wa miguu Nchini Tanzania (TFF).
    0 Comments ·0 Shares ·154 Views
  • BODI YA LIGI SIO CHOMBO HURU KWA MUJIBU WA RAIS WA TFF WALLECE KARIA.

    Dhumuni la Baba wa Taifa kupigania uhuru wa Tanganyika ilikuwa kuhitaji Tanganyika kuwa huru ili iweze kujiamulia mambo yake na kujipangia kipi ifanye kwa wakati wowote.

    Uhuru ni Jambo la msingi sana kwa binadamu yoyote kwani humsaidia katika kufanya maamuzi yake binafsi.

    Kwa mujibu wa kauli za Rais wa TFF Baba Yangu Mzee Wallece Karia ni dhahiri shahiri kuwa bodi ya ligi sio chombo huru.

    Wallece Karia akiwa katika mahojiano Wasafi Fm katika kipindi cha “Jana na Leo” Alisema kuwa

    “Kuna siku tulipokea Barua kutoka CAF Wakihitaji waamuzi wetu Wawili kwenda kuchezesha michuano ya kimataifa”

    “Wakati barua ile imekuja ofisini kuhitaji wale waamuzi kulikuwa na changamoto, Kwani mojawapo ya wale waamuzi ambae ni Ahmed Arajiga alikuwa amefungiwa na kamati ya masaa 72”

    “Ilikuwa ngumu sana kwangu, maana CAF wamemtaka mwamuzi alafu huku kwetu kamati imemfungia, lakini nikafanya maamuzi”

    “Nilifanya maamuzi nikawaambia hawa waamuzi waruhusiwe waende, Walienda wote wawili lakini bahati mbaya mmoja ndio alifuzu ambae ni Ahmed Arajiga”

    “Yalikuwa maamuzi magumu ila sikuwa na namna n Ahmed Arajiga alienda kuwakilisha Tanzania vema sana, Hata mechi aliyochezesha alichezesha vizuri sana”

    Kwa maelezo ya Wallece Karia aliingilia maamuzi ya Kamati ya Masaa 72 ambayo ipo chini ya bodi ya ligi. Kumruhusu Mwamuzi aliyefungiwa katika ligi kwenda kuchezesha mechi za kimataifa.
    (khalil ufadiga)

    BODI YA LIGI SIO CHOMBO HURU KWA MUJIBU WA RAIS WA TFF WALLECE KARIA. Dhumuni la Baba wa Taifa kupigania uhuru wa Tanganyika ilikuwa kuhitaji Tanganyika kuwa huru ili iweze kujiamulia mambo yake na kujipangia kipi ifanye kwa wakati wowote. Uhuru ni Jambo la msingi sana kwa binadamu yoyote kwani humsaidia katika kufanya maamuzi yake binafsi. Kwa mujibu wa kauli za Rais wa TFF Baba Yangu Mzee Wallece Karia ni dhahiri shahiri kuwa bodi ya ligi sio chombo huru. Wallece Karia akiwa katika mahojiano Wasafi Fm katika kipindi cha “Jana na Leo” Alisema kuwa “Kuna siku tulipokea Barua kutoka CAF Wakihitaji waamuzi wetu Wawili kwenda kuchezesha michuano ya kimataifa” “Wakati barua ile imekuja ofisini kuhitaji wale waamuzi kulikuwa na changamoto, Kwani mojawapo ya wale waamuzi ambae ni Ahmed Arajiga alikuwa amefungiwa na kamati ya masaa 72” “Ilikuwa ngumu sana kwangu, maana CAF wamemtaka mwamuzi alafu huku kwetu kamati imemfungia, lakini nikafanya maamuzi” “Nilifanya maamuzi nikawaambia hawa waamuzi waruhusiwe waende, Walienda wote wawili lakini bahati mbaya mmoja ndio alifuzu ambae ni Ahmed Arajiga” “Yalikuwa maamuzi magumu ila sikuwa na namna n Ahmed Arajiga alienda kuwakilisha Tanzania vema sana, Hata mechi aliyochezesha alichezesha vizuri sana” Kwa maelezo ya Wallece Karia aliingilia maamuzi ya Kamati ya Masaa 72 ambayo ipo chini ya bodi ya ligi. Kumruhusu Mwamuzi aliyefungiwa katika ligi kwenda kuchezesha mechi za kimataifa. (khalil ufadiga)
    0 Comments ·0 Shares ·198 Views
  • Taasisi ya dini ya Kiislamu ya Al-Hikma Foundation imetangaza kuwalipia mahari vijana 200 ambao wapo tayari kuoa.

    Akizungumza katika mashindano ya 25 ya kimataifa ya uhifadhi wa Qur'an yaliyofanyika leo Jumapili, Machi 16, 2023, katika Uwanja wa Mkapa na Uhuru, jijini Dar es Salaam, Sheikh Nurdin Kishki, ambaye ni Mwenyekiti wa taasisi hiyo, amesema kuwa mwaka huu Vijana 200 watakaolipiwa mahari 100 watatoka Tanzania , na wengine 100 kutoka Nchini Burundi .

    "Kutokana na idadi ya watu wasiokuwa kwenye ndoa, mwaka huu tutaozesha vijana 200. Ndoa 100 zitafungwa Tanzania na 100 nyingine kwa ndugu zetu wa Burundi. Mahari na gharama nyingine za ndoa tutatoa sisi, Al-Hikma Foundation,"

    Pia, Sheikh Kishki ameeleza kuwa taasisi hiyo itawalipia gharama za tohara kwa watoto wa kiume 1000 Nchini Tanzania. Amesema mambo hayo yanafanyika kupitia programu maalumu iliyoanzishwa na taasisi hiyo ya kurejesha kwa jamii kupitia mashindano hayo.

    Taasisi ya dini ya Kiislamu ya Al-Hikma Foundation imetangaza kuwalipia mahari vijana 200 ambao wapo tayari kuoa. Akizungumza katika mashindano ya 25 ya kimataifa ya uhifadhi wa Qur'an yaliyofanyika leo Jumapili, Machi 16, 2023, katika Uwanja wa Mkapa na Uhuru, jijini Dar es Salaam, Sheikh Nurdin Kishki, ambaye ni Mwenyekiti wa taasisi hiyo, amesema kuwa mwaka huu Vijana 200 watakaolipiwa mahari 100 watatoka Tanzania 🇹🇿, na wengine 100 kutoka Nchini Burundi 🇧🇮. "Kutokana na idadi ya watu wasiokuwa kwenye ndoa, mwaka huu tutaozesha vijana 200. Ndoa 100 zitafungwa Tanzania na 100 nyingine kwa ndugu zetu wa Burundi. Mahari na gharama nyingine za ndoa tutatoa sisi, Al-Hikma Foundation," Pia, Sheikh Kishki ameeleza kuwa taasisi hiyo itawalipia gharama za tohara kwa watoto wa kiume 1000 Nchini Tanzania. Amesema mambo hayo yanafanyika kupitia programu maalumu iliyoanzishwa na taasisi hiyo ya kurejesha kwa jamii kupitia mashindano hayo.
    0 Comments ·0 Shares ·124 Views
  • Jumatano ya Machi 17, 2021, Nchi ya Tanzania iligubikwa na simanzi zito ya kumpoteza Rais wao aliyekuwa madarakani, Dk John Pombe Magufuli maarufu JPM. Ni kwa mara ya kwanza Taifa hili la Afrika Mashariki kushuhudia Rais aliyekuwa madarakani akifariki dunia. Kifo chake kilitangazwa na Samia Suluhu Hassan, aliyekuwa Makamu wa Rais.

    Dk Magufuli aliyezaliwa Chato Mkoani Geita, Oktoba 29, 1959 alihitimisha utawala wake wa miaka mitano na miezi minne aliouanza Novemba 5, 2015 katika Hospitali ya Mzena, Kijitonyoma Jijini Dar es Salaam kwa maradhi ya moyo.

    Leo Jumatatu Machi 17, 2025, ndugu, jamaa na marafiki watamkumbuka kwa Ibada itakayofanyikia Chato ambayo imeandaliwa na familia yake.

    Jumatano ya Machi 17, 2021, Nchi ya Tanzania 🇹🇿 iligubikwa na simanzi zito ya kumpoteza Rais wao aliyekuwa madarakani, Dk John Pombe Magufuli maarufu JPM. Ni kwa mara ya kwanza Taifa hili la Afrika Mashariki kushuhudia Rais aliyekuwa madarakani akifariki dunia. Kifo chake kilitangazwa na Samia Suluhu Hassan, aliyekuwa Makamu wa Rais. Dk Magufuli aliyezaliwa Chato Mkoani Geita, Oktoba 29, 1959 alihitimisha utawala wake wa miaka mitano na miezi minne aliouanza Novemba 5, 2015 katika Hospitali ya Mzena, Kijitonyoma Jijini Dar es Salaam kwa maradhi ya moyo. Leo Jumatatu Machi 17, 2025, ndugu, jamaa na marafiki watamkumbuka kwa Ibada itakayofanyikia Chato ambayo imeandaliwa na familia yake.
    0 Comments ·0 Shares ·117 Views
  • KLABU YA AL AHLY YAKATWA ALAMA NA ZAMALEK YAPEWA USHINDI CAIRO DERBY

    Taarifa kutoka nchini Misri zinaripoti taarifa rasmi kutoka Shirikisho la Vilabu nchini Misri kuwa Zamalek imepewa ushindi wa mabao matatu na alama tatu baada ya Al Ahly kutotokea uwanjani kwa kutumia kifungu cha 4(17) kwenye Sheria na Kanuni za Mashindano.

    Sambamba na hilo Al Ahly, wamekatwa alama tatu (zitachukuliwa mwishoni mwa msimu) huku pia wakiagizwa kulipa gharama zote za kibiashara pamoja na gharama za Warusha matangazo sambamba na gharama nyingine za ziada kwa mujibu wa kifungu cha 8(17).

    Wakati Tanzania Mashabiki wakilalamika, wakati Tanzania Mrusha Matangazo akiingia gharama ambazo mchezo haukuoneshwa, huko Misri Al Ahly kaambiwa awalipe Wadau wote akiwemo Mrusha matangazo kwa hasara aliyomletea, hapa wanalinda maslahi ya Wadhamini.

    Licha ya hivyo Al Ahly wamepeleka malalamiko yao kwa Kamati ya Olympic nchini humo ambapo Shirikisho la soka Misri likisubiri majibu ya sakata hilo.
    (Farhan JR)

    KLABU YA AL AHLY YAKATWA ALAMA NA ZAMALEK YAPEWA USHINDI CAIRO DERBY Taarifa kutoka nchini Misri zinaripoti taarifa rasmi kutoka Shirikisho la Vilabu nchini Misri kuwa Zamalek imepewa ushindi wa mabao matatu na alama tatu baada ya Al Ahly kutotokea uwanjani kwa kutumia kifungu cha 4(17) kwenye Sheria na Kanuni za Mashindano. Sambamba na hilo Al Ahly, wamekatwa alama tatu (zitachukuliwa mwishoni mwa msimu) huku pia wakiagizwa kulipa gharama zote za kibiashara pamoja na gharama za Warusha matangazo sambamba na gharama nyingine za ziada kwa mujibu wa kifungu cha 8(17). Wakati Tanzania Mashabiki wakilalamika, wakati Tanzania Mrusha Matangazo akiingia gharama ambazo mchezo haukuoneshwa, huko Misri Al Ahly kaambiwa awalipe Wadau wote akiwemo Mrusha matangazo kwa hasara aliyomletea, hapa wanalinda maslahi ya Wadhamini. Licha ya hivyo Al Ahly wamepeleka malalamiko yao kwa Kamati ya Olympic nchini humo ambapo Shirikisho la soka Misri likisubiri majibu ya sakata hilo. (Farhan JR)
    Love
    1
    · 0 Comments ·0 Shares ·162 Views
  • Steve Nyerere agusia sakata la Nicole

    "Mstafuuu,.....Nani mkamilifu katika hii Ardhi Ya Mwenyezi Mungu,..

    Napokea sms Simu swala la Nicole Toka juzi kulia na kushoto lakini nikasema Mungu nitangulie nami nione Mwanga kwenye hili,....Ni Ukweli Usio pingika dada kapuyanga Sana Tena sana Ana Makosa Na Ana Kosa la kujibu, lakini nani mkamilifu,....

    Nicole Ana makosa na kibaya zaidi ni kwenda kuchangisha Watu wenye kujipambania kuitafuta kesho yao, Na kibaya zaidi walikuamini kutokana na bland yake wakiamini kuna matokeo sahihi kupitia Nicole,....

    Nicole ni mtu mzima na mwenye akili timamu Alikuwa Anafanya kitu anacho kijua na kujua matokeo na mwisho wa Matokeo lakini tukienda mbali zaidi limesha tokea naye ni Binadamu,..Sipo hapa kumtetea Mwalifu lakini naandika hapa kujaribu kuona haki ya walio fanyiwa ujinga huu wanaipataje,...Je Nicole kukaaa ndani haki ya wadai Itapatikana Maana siku ya Mwisho Nicole Anatakiwa kuwarudishia FEDHA zao wote walio guswa na yeye Anarudishaje Atajua yeye lakini Akiwa nje kwa dhamana na masharti yenye tija basi Anaweza kumaliza jambo hili.,.

    Lakini Ifike mahara hii michezo ya Magroup Inayogusa FEDHA naomba sana kuwe na Utaratibu wa kumsajiri kijumbe kitambulisho chake na wanachama anao wachangisha waridhie kwa maandishi kuwa wamekubaliana kuanzisha group la kusaidia hii itasaidia sana,.lakini sio mtu anatoka tu huko anaanzisha group mara michango sio sawa.,,.

    Niombe sasa Ni wakati wa kusimama na Nicole Tusiangalie kafanya nini Tuangalie Dhamana yake na jinsi ya kumsaidia,....Haijalishi kala mzigo na nani lakini bado ni mwenzetu,....Anapitia kipindi kibaya sana Ambacho Anahitaji faraja,....

    Tusimame kumuombea Dhamana Tunajua na kutambua sheria na kuheshimu sheria kwenye Taifa letu,......

    Niombe Si muda wa kuliangalia kosa ni Muda wa kulitibu kosa Nani mkamilifu hapa Duniani,..Mimi Binafsi kama STEVEN MENGELE (NYERERE) NIPO TAYARI KUMSAIDIA NICOLE ,..KUTOKA NDANI KWA KUFATA TARATIBU ZOTE,..NA AKIPATA DHAMANA BASI ATAMBUE KULIPA KILA JASHO LA MCHANGAJI KURUDISHIWA NA MAISHA KUENDELEA,....HAKUNA MWANADAMU AMBAYE MKAMILIFU HAPA DUNIANI,...." - Steve Nyerere, Mwigizaji wa filamu Tanzania.

    Steve Nyerere agusia sakata la Nicole "Mstafuuu,.....Nani mkamilifu katika hii Ardhi Ya Mwenyezi Mungu,.. Napokea sms Simu swala la Nicole Toka juzi kulia na kushoto lakini nikasema Mungu nitangulie nami nione Mwanga kwenye hili,....Ni Ukweli Usio pingika dada kapuyanga Sana Tena sana Ana Makosa Na Ana Kosa la kujibu, lakini nani mkamilifu,.... Nicole Ana makosa na kibaya zaidi ni kwenda kuchangisha Watu wenye kujipambania kuitafuta kesho yao, Na kibaya zaidi walikuamini kutokana na bland yake wakiamini kuna matokeo sahihi kupitia Nicole,.... Nicole ni mtu mzima na mwenye akili timamu Alikuwa Anafanya kitu anacho kijua na kujua matokeo na mwisho wa Matokeo lakini tukienda mbali zaidi limesha tokea naye ni Binadamu,..Sipo hapa kumtetea Mwalifu lakini naandika hapa kujaribu kuona haki ya walio fanyiwa ujinga huu wanaipataje,...Je Nicole kukaaa ndani haki ya wadai Itapatikana Maana siku ya Mwisho Nicole Anatakiwa kuwarudishia FEDHA zao wote walio guswa na yeye Anarudishaje Atajua yeye lakini Akiwa nje kwa dhamana na masharti yenye tija basi Anaweza kumaliza jambo hili.,. Lakini Ifike mahara hii michezo ya Magroup Inayogusa FEDHA naomba sana kuwe na Utaratibu wa kumsajiri kijumbe kitambulisho chake na wanachama anao wachangisha waridhie kwa maandishi kuwa wamekubaliana kuanzisha group la kusaidia hii itasaidia sana,.lakini sio mtu anatoka tu huko anaanzisha group mara michango sio sawa.,,. Niombe sasa Ni wakati wa kusimama na Nicole Tusiangalie kafanya nini Tuangalie Dhamana yake na jinsi ya kumsaidia,....Haijalishi kala mzigo na nani lakini bado ni mwenzetu,....Anapitia kipindi kibaya sana Ambacho Anahitaji faraja,.... Tusimame kumuombea Dhamana Tunajua na kutambua sheria na kuheshimu sheria kwenye Taifa letu,...... Niombe Si muda wa kuliangalia kosa ni Muda wa kulitibu kosa Nani mkamilifu hapa Duniani,..Mimi Binafsi kama STEVEN MENGELE (NYERERE) NIPO TAYARI KUMSAIDIA NICOLE ,..KUTOKA NDANI KWA KUFATA TARATIBU ZOTE,..NA AKIPATA DHAMANA BASI ATAMBUE KULIPA KILA JASHO LA MCHANGAJI KURUDISHIWA NA MAISHA KUENDELEA,....HAKUNA MWANADAMU AMBAYE MKAMILIFU HAPA DUNIANI,...." - Steve Nyerere, Mwigizaji wa filamu Tanzania.
    0 Comments ·0 Shares ·173 Views
  • "Msimu uliyopita Zamalek aligomea mechi dhidi ya Al Ahly, Mamlaka za soka nchini Misri zikampa ushindi Al Ahly wa mabao mawili na alama zake tatu kisha wakailima Zamalek alama tatu na timu ikashuka mpaka nafasi ya 12 kama sikosei, Bodi na Chama wala hakikuwaza mara mbili, ni kesi kubwa sana kwenye dunia ya soka kukacha mechi.

    Jana, Al Ahly nae kaleta mbwembwe zile zile za masuala ya Kanuni akagomea mchezo, akasahau kanuni ya kutokea Uwanjani na kucheza mechi ndio kanuni yenye maana zaidi kwenye soka, amejikuta anapoteza alama tatu na mabao matatu kwa Zamalek, Kanuni hii inaweza kusema hivi ila Kanuni nyingine ikawa na maelezo mengine.

    Nikukumbushe tu Al Ahly aliyeadhibiwa ndio Klabu Tajiri zaidi Afrika, Klabu yenye Mashabiki na Wanachama wengi zaidi Afrika, ndio Klabu ya pili kwa Mataji mengi duniani baada ya Real Madrid, ila huko Misri watu hawatazami makunyanzi, ukileta maksudi, Bodi na Chama cha soka zinakufanyia bahati mbaya, Ahly inatajwa pia ina nguvu kubwa sana CAF, sio ya kufikirika ama nadharia ndio uhalisia ila wamepita nayo mapema tu.

    Nawakumbusha tena Watu wangu HAKI huenda na WAJIBU, mfano Tanzania kwa mujibu wa Katiba kuandamana ni haki yako ila unapaswa kutoa taarifa kwa Polisi masaa 72 kabla, umeelewa hapo? Ni haki yako ila huja na Wajibu, Kanuni ili ikulinde hakikisha umetekeleza Wajibu, biashara za Mamlaka za soka duniani ni mpira, kutocheza mpira ni kuzitusi, hazikuachi salama.

    Ni haki yako kuja kufanya mazoezi uwanja wa mechi siku moja kabla ila ni Wajibu wako kunijulisha kuwa nakuja, ili nikuandalie mazingira, huenda narekebisha mfumo wa Umeme? Huenda hali ya usalama sio shwari, huenda nimepulizia dawa za dudu zinaweka kukuathiri, yaani ni HAKI yako ila una WAJIBU wako huu ni mfano tu.

    Mnasemaje Watu wangu wa nchini Yemen haya hayawahusu sana, huko kwenu Kivyenu vyenu Wayemen" - Farhan JR, Mchambuzi.

    "Msimu uliyopita Zamalek aligomea mechi dhidi ya Al Ahly, Mamlaka za soka nchini Misri zikampa ushindi Al Ahly wa mabao mawili na alama zake tatu kisha wakailima Zamalek alama tatu na timu ikashuka mpaka nafasi ya 12 kama sikosei, Bodi na Chama wala hakikuwaza mara mbili, ni kesi kubwa sana kwenye dunia ya soka kukacha mechi. Jana, Al Ahly nae kaleta mbwembwe zile zile za masuala ya Kanuni akagomea mchezo, akasahau kanuni ya kutokea Uwanjani na kucheza mechi ndio kanuni yenye maana zaidi kwenye soka, amejikuta anapoteza alama tatu na mabao matatu kwa Zamalek, Kanuni hii inaweza kusema hivi ila Kanuni nyingine ikawa na maelezo mengine. Nikukumbushe tu Al Ahly aliyeadhibiwa ndio Klabu Tajiri zaidi Afrika, Klabu yenye Mashabiki na Wanachama wengi zaidi Afrika, ndio Klabu ya pili kwa Mataji mengi duniani baada ya Real Madrid, ila huko Misri watu hawatazami makunyanzi, ukileta maksudi, Bodi na Chama cha soka zinakufanyia bahati mbaya, Ahly inatajwa pia ina nguvu kubwa sana CAF, sio ya kufikirika ama nadharia ndio uhalisia ila wamepita nayo mapema tu. Nawakumbusha tena Watu wangu HAKI huenda na WAJIBU, mfano Tanzania kwa mujibu wa Katiba kuandamana ni haki yako ila unapaswa kutoa taarifa kwa Polisi masaa 72 kabla, umeelewa hapo? Ni haki yako ila huja na Wajibu, Kanuni ili ikulinde hakikisha umetekeleza Wajibu, biashara za Mamlaka za soka duniani ni mpira, kutocheza mpira ni kuzitusi, hazikuachi salama. Ni haki yako kuja kufanya mazoezi uwanja wa mechi siku moja kabla ila ni Wajibu wako kunijulisha kuwa nakuja, ili nikuandalie mazingira, huenda narekebisha mfumo wa Umeme? Huenda hali ya usalama sio shwari, huenda nimepulizia dawa za dudu zinaweka kukuathiri, yaani ni HAKI yako ila una WAJIBU wako huu ni mfano tu. Mnasemaje Watu wangu wa nchini Yemen haya hayawahusu sana, huko kwenu Kivyenu vyenu Wayemen😀" - Farhan JR, Mchambuzi.
    Like
    1
    · 0 Comments ·0 Shares ·227 Views
More Results