• "Nafahamu wote kwa pamoja tuna hamu ya kupata matokeo katika mechi hii lakini matokeo haya kuyapata kwa kushinda na kufuzu. Sisi tumeweka mazingira mazuri ambayo yataiwezesha timu yetu kufuzu.”

    “Nipo hapa kuwataka Watanzania kujitokeza kwa wingi Uwanja wa Mkapa alkini ningependa kutoa taarifa muhimu kwamba tunaendelea kushirikiana na serikali kuimarisha usalama wa siku hiyo. Tunawataka wapenzi wetu kuhakikisha kwamba wanazingatia mazingatio yote ambayo yatawekwa ya usalama. Hatutaruhusu mtu yeyote ambaye sio Mwanasimba kutuharibia shughuli yetu.”

    “Katika mchezo uliopita walisema maneno mengi kwamba kuna wazee wafupi, mbuzi lakini tuwatumie ujumbe kwamba kama mechi aikuhusu wabaki nyumbani na sisi tumejiandaa kuthibiti hilo kama klabu.”- Zubeda Sakuru, CEO wa klabu ya Simba SC.

    "Nafahamu wote kwa pamoja tuna hamu ya kupata matokeo katika mechi hii lakini matokeo haya kuyapata kwa kushinda na kufuzu. Sisi tumeweka mazingira mazuri ambayo yataiwezesha timu yetu kufuzu.” “Nipo hapa kuwataka Watanzania kujitokeza kwa wingi Uwanja wa Mkapa alkini ningependa kutoa taarifa muhimu kwamba tunaendelea kushirikiana na serikali kuimarisha usalama wa siku hiyo. Tunawataka wapenzi wetu kuhakikisha kwamba wanazingatia mazingatio yote ambayo yatawekwa ya usalama. Hatutaruhusu mtu yeyote ambaye sio Mwanasimba kutuharibia shughuli yetu.” “Katika mchezo uliopita walisema maneno mengi kwamba kuna wazee wafupi, mbuzi lakini tuwatumie ujumbe kwamba kama mechi aikuhusu wabaki nyumbani na sisi tumejiandaa kuthibiti hilo kama klabu.”- Zubeda Sakuru, CEO wa klabu ya Simba SC.
    Like
    1
    · 0 Comments ·0 Shares ·970 Views
  • Meneja wa Uwanja wa Benjamin Mkapa amekubali kujiweka pembeni kwenye kusimamia Uwanja baada ya ombi la Wazee wa klabu ya Simba SC kumtaka kufanya hivyo mpaka mwisho wa mchezo wa mkondo wa pili wa robo fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika (CAF Confederation Cup) Kati ya Simba SC dhidi ya All Masry ya Misri utakaochezwa keshokutwa April 9, 2025

    Wazee wa klabu ya Simba SC walienda kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa asubuhi wakimtaka Meneja wa Uwanja huo kuondoka mara moja kwa sababu hawana imani naye wakihofia kuwa anaweza kuwahujumu kwenye mchezo wao dhidi ya klabu ya Al Masry. Wazee hao wanadai kuwa hata mchezo wao dhidi ya klabu ya Yanga SC ulioahirishwa chanzo ilikuwa yeye Meneja

    Meneja wa Uwanja wa Benjamin Mkapa amekubali kujiweka pembeni kwenye kusimamia Uwanja baada ya ombi la Wazee wa klabu ya Simba SC kumtaka kufanya hivyo mpaka mwisho wa mchezo wa mkondo wa pili wa robo fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika (CAF Confederation Cup) Kati ya Simba SC dhidi ya All Masry ya Misri 🇪🇬 utakaochezwa keshokutwa April 9, 2025 Wazee wa klabu ya Simba SC walienda kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa asubuhi wakimtaka Meneja wa Uwanja huo kuondoka mara moja kwa sababu hawana imani naye wakihofia kuwa anaweza kuwahujumu kwenye mchezo wao dhidi ya klabu ya Al Masry. Wazee hao wanadai kuwa hata mchezo wao dhidi ya klabu ya Yanga SC ulioahirishwa chanzo ilikuwa yeye Meneja
    Like
    1
    · 0 Comments ·0 Shares ·691 Views
  • Wazee walioshauri timu isiingie Uwanjani
    Wazee walioshauri timu isiingie Uwanjani
    Like
    Love
    2
    · 0 Comments ·0 Shares ·231 Views
  • Huyu ndio fundi nguo wa kwanza Afrika Mashariki mwaka 1890, baada ya kushindwa kulitaja vizuri jina lake wazee wakamwita Cherehani.
    Anaitwa: Charan Singh.

    JE ulikua unajua hili .
    Huyu ndio fundi nguo wa kwanza Afrika Mashariki mwaka 1890, baada ya kushindwa kulitaja vizuri jina lake wazee wakamwita Cherehani. Anaitwa: Charan Singh. JE ulikua unajua hili 😂😂😂.
    Like
    2
    · 0 Comments ·0 Shares ·332 Views
  • (D)
    Shipman alikuwa daktari wa kuaminika. Wagonjwa wake walimpenda kwa sababu alikuwa mwenye huruma, na alikuwa akiwatembelea hata majumbani kwao.

    Lakini ilianza kuonekana kuwa wagonjwa wake walikuwa wakifa kwa wingi kuliko kawaida.

    Walikuwa wakifa kwa "mashambulizi ya moyo" au "udhaifu wa uzee." Hakukuwa na ishara ya mateso—ilikuwa ni kama waliaga dunia kwa utulivu.

    Mara nyingi, alikuwa daktari pekee aliyekuwepo wakati wa vifo hivyo.

    Hakuna aliyeshuku lolote, hasa kwa sababu wengi wa waliokufa walikuwa wazee.

    Lakini jambo la ajabu ni kwamba, tofauti na madaktari wengine ambao hujaribu kuwaokoa wagonjwa wao hadi dakika ya mwisho, Shipman hakuwahi kujaribu kuwapigania—hakuwahi kupiga simu kwa ambulansi.

    Alikuwa akiwapatia sindano ya morphine katika dozi kubwa—sawa na aliyowahi kuona ikitumiwa kwa mama yake alipokuwa kijana. Na ndani ya dakika chache, walikuwa wakiondoka duniani kimyakimya
    (D) Shipman alikuwa daktari wa kuaminika. Wagonjwa wake walimpenda kwa sababu alikuwa mwenye huruma, na alikuwa akiwatembelea hata majumbani kwao. Lakini ilianza kuonekana kuwa wagonjwa wake walikuwa wakifa kwa wingi kuliko kawaida. Walikuwa wakifa kwa "mashambulizi ya moyo" au "udhaifu wa uzee." Hakukuwa na ishara ya mateso—ilikuwa ni kama waliaga dunia kwa utulivu. Mara nyingi, alikuwa daktari pekee aliyekuwepo wakati wa vifo hivyo. Hakuna aliyeshuku lolote, hasa kwa sababu wengi wa waliokufa walikuwa wazee. Lakini jambo la ajabu ni kwamba, tofauti na madaktari wengine ambao hujaribu kuwaokoa wagonjwa wao hadi dakika ya mwisho, Shipman hakuwahi kujaribu kuwapigania—hakuwahi kupiga simu kwa ambulansi. Alikuwa akiwapatia sindano ya morphine katika dozi kubwa—sawa na aliyowahi kuona ikitumiwa kwa mama yake alipokuwa kijana. Na ndani ya dakika chache, walikuwa wakiondoka duniani kimyakimya
    Like
    1
    · 0 Comments ·0 Shares ·660 Views
  • WIKI YA WAZEE WENYE FURAHA.

    PUNGUZA:
    Chumvi.
    Sukari.
    Unga uliokobolewa.
    Bidhaa za maziwa.
    Bidhaa zilizochakatwa.

    VYAKULA VINAVYOHITAJIKA:
    Mboga za majani;
    Mbegu za mikunde;
    Maharage;
    Karanga;
    Mayai;
    Mafuta yaliyosindikwa baridi (Mizeituni, Nazi, …);
    Matunda.

    MAMBO MATATU UNAYOPASWA KUJARIBU KUSAHAU:
    Umri wako.
    Mambo ya zamani.
    Malalamiko yako.

    MAMBO MUHIMU UNAYOPASWA KUTHAMINI:
    Familia yako;
    Marafiki zako;
    Mawazo yako chanya;
    Nyumba safi na ya kukaribisha.

    MAMBO MATATU YA MSINGI UNAYOPASWA KUJIFUNZA:
    Daima tabasamu / cheka.
    Fanya mazoezi ya mwili mara kwa mara kwa kasi yako mwenyewe.
    Angalia na kudhibiti uzito wako.

    MTINDO WA MAISHA MUHIMU SITA UNAYOPASWA KUFANYA:
    Usisubiri hadi uwe na kiu kunywa maji.
    Usisubiri hadi uchoke kupumzika.
    Usisubiri hadi uwe mgonjwa kufanya uchunguzi wa matibabu.
    Usisubiri miujiza kumwamini Mungu.
    Usipoteze kamwe kujiamini.
    Kaa chanya na daima tumaini kesho bora.

    KAMA UNA MARAFIKI KATIKA UMRI HUU (47-90 MIAKA), TAFADHALI WATUMIE HII.
    WIKI YA WAZEE WENYE FURAHA.
    WIKI YA WAZEE WENYE FURAHA. PUNGUZA: Chumvi. Sukari. Unga uliokobolewa. Bidhaa za maziwa. Bidhaa zilizochakatwa. VYAKULA VINAVYOHITAJIKA: Mboga za majani; Mbegu za mikunde; Maharage; Karanga; Mayai; Mafuta yaliyosindikwa baridi (Mizeituni, Nazi, …); Matunda. MAMBO MATATU UNAYOPASWA KUJARIBU KUSAHAU: Umri wako. Mambo ya zamani. Malalamiko yako. MAMBO MUHIMU UNAYOPASWA KUTHAMINI: Familia yako; Marafiki zako; Mawazo yako chanya; Nyumba safi na ya kukaribisha. MAMBO MATATU YA MSINGI UNAYOPASWA KUJIFUNZA: Daima tabasamu / cheka. Fanya mazoezi ya mwili mara kwa mara kwa kasi yako mwenyewe. Angalia na kudhibiti uzito wako. MTINDO WA MAISHA MUHIMU SITA UNAYOPASWA KUFANYA: Usisubiri hadi uwe na kiu kunywa maji. Usisubiri hadi uchoke kupumzika. Usisubiri hadi uwe mgonjwa kufanya uchunguzi wa matibabu. Usisubiri miujiza kumwamini Mungu. Usipoteze kamwe kujiamini. Kaa chanya na daima tumaini kesho bora. KAMA UNA MARAFIKI KATIKA UMRI HUU (47-90 MIAKA), TAFADHALI WATUMIE HII. WIKI YA WAZEE WENYE FURAHA.
    0 Comments ·0 Shares ·1K Views
  • Wazee wa mipango katika Moja na mbili
    Wazee wa mipango katika Moja na mbili👐
    Love
    1
    · 1 Comments ·0 Shares ·201 Views
  • Wazee wa mitumba
    Wazee wa mitumba 😂
    Like
    2
    · 1 Comments ·0 Shares ·213 Views
  • OPERATION ENTEBBE -2

    Tayari zilikuwa zimepita siku tatu tangu ndege ya Air France Flight 139 kuondoka Tel Aviv na hatimaye kutekwa baada ya kuruka jijini Athens iliposimama kuchukua abiria. Lakini pia zilikuwa zimepita siku mbili tangu ndege hii kutua katika uwanja wa ndege wa Entebbe nchini Uganda. Katika siku zote mbili hizi tangu ndege hii itue uwanjani hapa, rais wa Uganda Idd Amin Nduli Dadaa alikuwa anafika uwanjani hapo kila siku “kuwajulia hali” mateka hao.
    Kwa muda wa siku hizi zote mbili tangu ndege itue uwanjani hapo, magaidi hawa walioiteka ndege kwa kushirikiana na jeshi la Uganda kuchunguza majina ya kila abiria kama ambavyo yalikuwa yameandikwa kwenye pasport. Lengo lao la kufanya hivi ilikuwa ni kujaribu kufahamu uraia wa kila mateka waliye naye. Baada ya kufanya uchambuzi huu wa passport zote, hatimaye siku hii ya tatu, yaani tarehe 29 June 1976 kiongozi wa magaidi hawa Wilfred Bose akiwa na karatasi mkononi aliingi ndani ya terminal ambayo walikuwa wanaitumia kuwahifadhi mateka na kisha akaanza kusoma majina ya kila abiria. Alichokuwa anakifanya ni kusoma majina ya mateka ambao passport zao zilionyesha walikuwa ni raia wa Israel. Lakini pia alisoma majina ya mateka wengine ambao licha ya passport zao kuonyesha kuwa hawakuwa raia wa Israel lakini walikuwa na majina ya kiyahudi. Pamoja na hao pia mateka wote ambao walikuwa na uraia pacha na uraia huo mmojawapo ukiwa ni Israel basi nao waliunganishwa kwenye list hii.
    Baada ya kuwatenganisha raia wote wa Israel na kuwaweka kwenye chumba kingine peke yao hapo hapo kwenye terminal, kuna mwanadada raia wa Ufaransa aliyeitwa Jocelyne Monier yeye jina lake halikuitwa kwenye ile list ya wanaotakiwa kutengwa kwenye chumba kingine (Waisrael na Wayahudi). Lakini ‘boyfriend’ wake alikuwa ni Muisrael na aliitwa jina na kutengwa na wengine katika kile chumba kingine. Mwanadada huyu ili kuonyesha kumtia moyo mpenzi wake na kupinga huu ubaguzi uliokuwa unafanywa na hawa magaidi, kwa hiari yake alijipeleka kwenye chumba cha mateka wa Kiisrael. Si mwanadada huyu pekee ambaye alifanya kitendo hiki cha ushujaa, lakini pia kulikuwa na mwanamama mwingine aliitwa Janet Almog (rai wa Marekani) na mateka mwingine aliyeitwa Jean-Jacques Mimouni (raia wa Ufaransa) nao kwenye kuonyesha hali ya kuwaunga mkono wenzao waliotengwa kwenye chumba kingine na kupinga ubaguzi uliokuwa unafanywa na maharamia hawa, nao walijipeleka kwa hiari yao kwenye chumba ambacho mateka hao walikibatiza jina “Chumba cha Waisrael”, ambacho mateka wote walijua fika kwamba kuna jambo baya maharamia hao walikuwa wamepanga kulifanya.

    Licha ya maharamia kwa kushirikiana na jeshi la Uganda kufanya uchambuzi huu wa kina kuhusu uraia wa kila mateka waliye naye, lakini walifanya kosa kubwa sana ambalo lilkuja kuwagharimu sana hapo baadae. Kwenye uchambuzi wao wote huu walioufanya walishindwa kumng’amua mateka mmoja mwanajeshi wa Israel ambaye alikuwa ana uraia pacha na siku hiyo alikuwa anatumia passport ambayo sio ya Israel. Mateka huyu alikuja kuwa muhimu sana huko mbeleni kuwapatia Mossad Intelijensia mujarabu kabisa kuhusu watekaji, jengo wanaloshikilia mateka, na namana wanavyoshirikiana na jeshi la Uganda.
    Siku iliyofuata yaani June 30, maharamia haya wakawaachia mkupuo wa kwanza wa mateka wasio raia wa Israel au wayahudi. Katika mkupuo huu wa kwanza waliachia mateka 48 ambao walikuwa ni wazee, watoto na akina mama wenye watoto wadogo.
    Baada ya mkupuo huu wa kwanza wa kuwaachia mateka hawa wachache, maharamia wakaweka wazi matakwa yao ili waweze kuachia mateka wengine. Kwanza kabisa walitaka walipwe fedha kiasi cha dola za Kimarekani milioni 5. Na pili walitakakuachiwa kwa wafungwa 53 wenye asili ya kipalestina wanaotuhumiwa kwa ugaidi, ambao kati yao 40 walikuwa kwenye jela za Israel na 13 katika nchi nyingine za Ulaya. Watekaji hawa wakatoa ‘ultimutum’ kwamba kama matakwa yao hayatatekelezwa ndani ya masaa ishirini na nne yajayo (mpaka tarehe 1 July saa 8 mchana) basi wataanza kuua raia wa Israel mmoja baada ya mwingine.
    Dunia nzima ni kama ilisimama kwa masaa kadhaa kutokana na sintofahamu iliyogubika kila mahali. Sintofahamu hii ililetwa na ukweli kwamba, ilikuwa inajulikana wazi kwa miaka yote kwamba Israel wana sera ya kutofanya mazungumzo au makubaliano na Magaidi. Kwahiyo kila mtu alikuwa nafahamu kuwa kuna uwezekano mkubwa ndani ya masaa 24 yajayo ulimwengu ukashuhidia watu zaidi ya 200 wakichinjwa kama kuku.

    NCHINI ISRAEL: KIKAO CHA BARAZA LA MAWAZIRI
    Nchini Israel kikao cha dharura cha baraza la mawaziri kilikuwa kimeitishwa na waziri Mkuu Yitzhak Rabin kujadili kuhusu hatua za kuchukua kuokoa raia wake ambao wameshikiliwa mateka huko uwanja wa ndege wa Entebbe, Uganda.
    Hali ya kikao ilikuwa tete sana kutokana na kila dakika waliyokuwa wanaitumia kujadili ndivyo ambavyo walikuwa wanaikaribia saa 8 mchana ya tarehe 1 July. Walipowasilana na Ujerumani na Ufaransa ambao nao walikuwa na baadhi ya wafungwa wa Kipalestina ambao watekaji walitaka waachiwe… walipowaomba ushirikiano wao kuhusu kukabali kuachia hao wafungwa, Ujerumani na Ufaransa walikataa katakata kuachia hata mfungwa mmoja wa Kipalestina ambaye alikuwa kwenye magereza zao.
    Sintofahamu ilizidi kuongezeka. Masaa yalizidi kuyoyoma. Saa 8 mchana ya tarehe 1 July ilizidi kukaribia. Harufu ya damu ilikuwa inabisha hodi mlangoni kwao. Licha ya weledi wao wote walionao lakini mbele yao waliona giza.
    Inapaswa kukumbukwa kwamba Idd Amin aliwahi kupatiwa mafunzo ya weledi wa kijeshi nchini Isarel (Special Force Training). Kwa hiyo baraza la mawaziri likamuagiza Baruch Bar-Lev, kamanda mstaafu wa IDF ambaye alihusika kumpatia mafunzo ya kijeshi Amin kipindi yuko Israel na kufanikiwa kujenga naye ukaribu. Baraza la Mawaziri likamuagiza Baruck (marafiki zake humuita “Burka”) kufanya mawasiliano na Rais huyo wa Uganda ili kujaribu kumuomba awashawishi magaidi wanaoshikilia mateka kwenye uwanja wake wa ndege wa Entebbe wawaachie mateka hao bila masharti magumu.
    Kupitia kwa Burka, Israel ilifikia mpaka hatua ya kumuahidi Idd Amin kuwa kama atafanikisha kuachiwa kwa mateka hao basi watatumia ushawishi walionao kuhakikisha kuwa Amin anatunukiwa tuzo ya amani ya Nobel.
    Lakini Amin hakulegeza msimamo, akaendelea kuwasisitiza kuwa hakuna namna nyingine yeyote ambayo mateka hao wataachiwa bila masharti yaliyotolewa na watekaji kutimizwa.
    Baada ya juhudi hii ya kumuhonga ‘tuzo’ kugonga mwamba, Waziri Mkuu wa Israel akawasiliana na serikali ya Marekani na kuwaomba wamshawishi Rais wa Misri Anwar Sadat ambaye alikuwa anaheshimiana sana na Amin ili amshawishi kuwaamuru magaidi yaliyoko uwanjani kwake Entebbe waachiemateka bila masharti magumu.
    Amin bado akashikilia msimamo kwamba hakuna mateka atakayeachiwa pasipo masharti yaliyotolewa kutimizwa.
    Juhudi hizi za kumshawishi Amin zilikula muda mwingi sana na hatimaye wakajikuta tayari kulikuwa kumekucha asubuhi. Mbele yao kulikuwa kumebakia masaa chini ya manane kabla ya damu ya zaidi ya watu 200 kumwagika.
    Baraza la mawaziri la Israel likamuomba Amin aongee na watekaji wakubali kusogeza siku mbele ili kuipa serikali ya Israel muda wakutosha kushughulikia lojistiki na kushawishi Ujerumani na Ufaransa ili waweze kutimiza sharti la kuachiwa kwa wafungwa wa kipalestina 53 wanaotuhumiwa kwa ugaidi.
    Rais Idd Amin baada ya kushawishiwa sana akakubali ombi hili na akaieleza serikali ya Israel kwamba ni siku tatu tu pekee zinaongezwa, yaani ikimaanisha kwamba siku zitaongezwa mpaka tarehe 4 July, saa 8 mchana. Serikali ya Israel ikakubliana na hili.
    Mchana wa siku hiyo, serikali ilitoa taarifa rasmi kwa vyombo vya habari wakilaani vitendo vya kigaidi na hususani matukio ya utekeji wa raia wasio na hatia, na pia ikaendelea kusisitiza kuhusu sera yake ya kutojadili na magaidi. Lakini taarifa hii ikamalizia kwa kueleza kuwa kwa kujali zaidi uhai wa zaidi ya raia 200 ambao bado wanashikiliwa na magaidi hayo, na kujali maumivu ambayo familia zao na taifa zima linapitia, wamekubali kutimiza sharti la magaidi hao la kuwalipa fedha za kimarekani dola milioni tano pamoja na kuachiwa kwa wafungwa wa kipalestina 53 wenye tuhuma za ugaidi.
    Ilikuwa ni moja ya matukio machache ambayo yaliishangaza dunia kwa Israel kukubali kushindwa hadharani. Kwa upande wa maadui wa Israel hii ilikuwa ni sherehe kubwa kwao. Na kwa upande wa Isarel na maswahiba zake hii iikuwa ni maombolezo makubwa.
    Amin na wenzake kule Uganda walikuwa wanasherehekea baada ya taarifa hii kutolewa kwa vyombo vya habari. Walihsi kabisa harufu ya ushindi inanukia kwenye pua zao.
    Kitu ambacho walikuwa hawafahamu ilikuwa ni kwamba, Israel walikuwa wanawafanyia ‘mchezo’ wa kisaikolojia ili Amin, jeshi lake na watekaji wajiamini kwa kuona kuwa ushindi umeegemea upande wao na hatimaye wajisahau kutokana na kujiamini huku.

    NYUMA YA PAZIA
    Huko Tel aviv, makamanda wa IDF na maafisa wa Mossad walikuwa wamekusanyika katika conference room ya mako makuu ya wizara ya ulinzi kuweka mkakati wa oparesheni ya uokozi (rescue mission) wa mateka wanaoshikiliwa katika uwanja wa ndege wa Entebbe, Uganda.
    Kati ya watu muhimu ambao walikuwepo kwenye kikao hiki alikuwa ni Waziri Mkuu Rabin na Ehud Barak ambaye kipindi hicho alikuwa kamanda wa ngazi za juu kwenye jeshi anayeongoza kitengo cha Intelijensia ya jeshi (Military Intelligence).
    Moja kati ya vitu muhimu ambavyo viliwasaidia ilikuwa ni taarifa ya intelijensia iliyoletwa na Mossad kwamba uwanja wa ndege wa Entebbe ulijengwa na kampuni ya Kiisrael inayoitwa Solel Boneh.
    Kwahiyo muwakilishi kutoka katika kampuni hii ya ujenzi naye akaitwa kikaoni kwa ajili ya kuwasilisha michoro kuhusu jengo lote na uwanja wa ndege wa Entebbe ulivyo.
    Lakini pia wakati huo huo kulikuwa na maafisa wa Mossad ambao walikuwa ufaransa kuwahoji wale mateka ambao walikuwa wameachiwa awali. Mtu muhimu zaidi ambaye alitoa taarifa nzuri kwa Mossad alikuwa ni yule afisa wa jeshi niliyemuelezea awali kwamba alikuwa na uraia wan chi mbili (Israel na Ufaransa) na siku hii alikuwa ametumia passport ya nchi ya ufaransa hivyo watekaji walimuachia pamoja na wenzake wa kundi la kwanza lile la watu 48.
    Bwana huyu alitoa taarifa muhimu zaidi kuhusu kilichokuwa kinaendelea katika uwanja wa ndege wa Entebbe, kwa kuwa yeye tofauti na wenzake kutokana na uzoefu wake wa jeshi alikuwa aliweza kuwaeleza Mossad kuhusu ni salaha za namna gani watekaji walikuwa nazo, kulikuwa na ndege za aina gani za kijeshi pale uwanjani (Idd Amin aliamuru Air Force ya Uganda kulinda uwanja huo masaa 24), pia aliweza kuwaeleza kuhusu ‘rotation’ ya ulinzi ya jeshi la Uganda pamoja na taarifa nyingine muhimu ambazo abiria wengine wasingeweza kuzitilia maanani au kkuzieleza kwa ufasaha.
    Baada ya kupata intelijensia ya kutosha, mkakati wa awali ambao ulipendekezwa na jeshi ulikuwa ni kutumia ndege ya kijeshi na kisha kudondosha makomando kwenye ziwa Viktoria na kutoka hapo watatumia boti za mpira kuvuka mpaka nchi kavu na hatimaye kuelekea uwanja wa ndege ambao haukuwa mbali sana na ziwa Viktoria.
    Mkakati huu ulikuwa ni mzuri lakini ulihairishwa baada ya kupewa taarifa kuwa ziwa Viktoria lilikuwa na mamba wengi na ingeweza kuhatarisha uhai wa hawa makomando kabla hata ya kufika kwenye uwanja wa ndege. Kwahiyo ilikuwa dhahiri kwamba mkakati wowote ambao utawekwa ni lazima uwe wa kuvamia kutokea nchi kavu na ikiwezekana kutoka nchi jirani.
    Changamoto kubwa zaidi ilikuwa ni usafiri. Yaani kwamba oparesheni hii ilikuwa si tu kwamba makomando wanaotumwa kutekeleza wanaenda kupambana na magaidi wanne tu walioteka ndege, bali ilikuwa ni kana kwamba wanaenda kupambana na jeshi zima la Uganda. Kwa hiyo kikosi cha makomando ambacho kitatumwa kwenda huko lazima kiwe na watu wengi wa kutosha na pia lazima wachukue silaha nzito za kutosha. Ili kufaniskisha safari yenye makomando wengi hivi na vifaa vizito ilikuwa ni lazima kutumia ndege kubwa za kijeshi zenye uwezo mkubwa pia na hakukuwa na chaguo zuri zaid ya kutumia ndege za kijeshi za LOCKHEED C-130 HERCULES. Sasa changamoto ilikuwa inakuja kwamba huwezi kurusha dege kubwa kama hii kwenda na kurudi kutoka Israel mpaka Uganda bila kujaza mafuta tena japo mara moja.
    Katika kipindi hiki bado Israel walikuwa hawajawa na uwezo wa kufanya ‘Aerial Refuel’, yaani ndege kujazwa mafuta kwa kutumia ndege nyingine ikiwa angani. Lakini pia ilikuwa ni lazima madege hayo yakikaribia Uganda yaruke chini chini ili kukwepa kudunguliwa na kuikwepa rada ya kijeshi. Kwa hiyo ilikuwa ni lazima kupata nchi ndani ya afrika Mashariki ambao watakubali madege hayo ya kijeshi ya Israel kutua kwenye uwanja wake wa ndege na kujaza mafuta lakini pia kujiandaa na kuanzisha operation kutokea hapo na pia anga lao kutumika kuanzisha shambulizi la kijeshi kuelekea Uganda.
    Sasa japokuwa nchi zote za Afrika Mashariki zilikuwa hazikubaliana na kitendo cha Rais wa Uganda kushirikiana na watekaji, lakini hakukuwa na hata nchi moja ambayo ilikuwa iko tayari kuingia kwenye mzozo na Idd Amin kwa kuruhusu viwanja vya vya ndege kutumika na ndege za jeshi la Israel au wanajeshi kujiandaa kuvamia Entebbe au pia kuruhusu anga lao kutumia na jeshi la Israel.
    Ndipo hapa ambapo kwa haraka sana siku hiyo hiyo Waziri Mkuu Rabin akamtuma Ehud Barak na maafisa wachache wa Mossad kwenda Kenya kushawishi serikali ya Mzee Jomo Kenyatta iruhusu ndege za jeshi la Isarel kutumia kiwanja chao cha ndege. Ehud barak na wenzake hawakwenda tu moja kwa moja kwa Mzee Kenyatta, bali kwanza walienda kwa Waziri wa kilimo wa kipindi hicho Bw. Bruce McKenzie ambaye huyu aliwahi kuwa afisa wa Idara ya ujasusi ya Uingereza, MI6 na pia alikuwa swahiba mkubwa wa Ehud Barak.

    Kwa hiyo Israel ikamtumia Bruce McKenzie kumshawishi Mzee Jomo Kenyatta kuruhusu anga la Kenya na viwanjavya ndege kutumiwa na makomando wa Israel na ndege zao.
    Ehud Barak na maafisa wa Mossad hawakuishia hapa tu, bali pia walifanya vikao vya siri na wafanyabiashara wakubwa nchini Kenya wenye asili ya Israel na wale ambao walikuwa na ‘marafiki’ wa Israel kuwaomba watumie ushawishi wao wa kisiasa na kiuchumi wasaidie kumshawishi Kenyatta kukubali ombi la seriakli ya Israael viwanja vyao kutumika na ndege za kijeshi za Israel na makondo wake.
    Baada ya mashinikizo haya kutoka kila upande, Mzee Kenyatta hakuwa na chaguo linguine zaidi ya kukubali ombi lao.
    Bwana huyu McKenzie pia alikuwa na ndege yakebinafsi, na Ehud Barak akaona fursa. Walitumia ndege hii ya kiraia kuruka mpaka Uganda mijini Entebbe na kukatiza juu ya anga la uwanja wa ndege wa Entebbe na walipokuwa wanapita juu ya anga la uwanja wa ndege, Ehud Barak akatumia fursa hii kupiga picha kila eneo la uwanja. Kwa kuwa hii ilikuwa ni ndege ya kiraia, jeshi la Uganda hawakushughulika nayo.
    Picha hizi zilizopigwa na Ehud Barak zilikuja kuwa na umuhimumkubwa katika maandalizi ya mwisho ya oparesheni ya makomando wa Isarel Kuvamia uwanja huu.
    Mpaka kufikia hapa maandalizi yote muhimu yalikuwa yamekamilika.
    WAKATI HUO HUO
    Upande wa watekaji kule Uganda walikuwa wanasubria mifwedha yao dola milioni 5 za kimarekani.
    Rais Idd Amin naye baada ya kufikia makubaliano na Israel kuwa masharti ya fedha na wafungwa wa kipalestina kuachiwa tarehe 4 July, naye ‘akarelax’ na akaona huo ndio muda wa kutekeleza majukumu Mengine akisubiria tarehe 4 July ifike.
    Katika kipindi hiki Idd amin ndiye alikuwa mwenyekiti wa Umoja wa Afrika kwa kuzingatia utaratibu wa uenyekiti kuzunguka kwa kila nchi kwa mwaka mmoja mmoja na wiki hii alikuwa anatakiwa kwenye kikao cha Umoja wa Afrika kilichokuwa kinafanyika Mauritius. Kwa hiyo Amin akafunga safari kuelekea Mauritius kwenda kukabidhi kijiti cha Uenyekiti.
    Ehud Barak aliposikia taarifa hii, kwa kutumia akili yake kubwa ya kuzaliwa aliyojaliwa na uzoefu wake wa ujasusi, aliona fursa adhimu kabisa hapa. Akawasiliana na walioko kikaoni huko Tel Aviv na kuwaeleza taarifa ambazo awali wote hawakuielewa.
    Ehud Barak: “Idd Amin akiwa ndani ya Uganda huwa anatumia Mercedes Limousine katika msafara wake”
    Waziri Mkuu Rabin: “Ok! Limefanyaje?’
    Ehud Barak: “Nataka mtafute gari kama hiyo… Mercedes Limousine”
    Waziri Mkuu Rabin: “la kazi gani?”
    Ehud Barak: “siku ambayo kikosi cha makomando wakipanda kwenye ndege kutoka huko Israel kwenda Uganda, gari hilo nataka pia lipakiwe ndani ya ndge!”
    Kwa dakika kadhaa wote ambao walikuwa wanamsikiliza pale kikaoni kupitia simu hakuna ambaye alielewa nini hasa Ehud Barak alikuwa anapendekeza.
    Yalikuwa yamebaki masaa machache tu ambapo, weledi, ushujaa na uzalendo uliotukuka ulikuwa unaedna kudhihirika.

    Itaendelea
    #TheBOLD_JF
    OPERATION ENTEBBE -2 Tayari zilikuwa zimepita siku tatu tangu ndege ya Air France Flight 139 kuondoka Tel Aviv na hatimaye kutekwa baada ya kuruka jijini Athens iliposimama kuchukua abiria. Lakini pia zilikuwa zimepita siku mbili tangu ndege hii kutua katika uwanja wa ndege wa Entebbe nchini Uganda. Katika siku zote mbili hizi tangu ndege hii itue uwanjani hapa, rais wa Uganda Idd Amin Nduli Dadaa alikuwa anafika uwanjani hapo kila siku “kuwajulia hali” mateka hao. Kwa muda wa siku hizi zote mbili tangu ndege itue uwanjani hapo, magaidi hawa walioiteka ndege kwa kushirikiana na jeshi la Uganda kuchunguza majina ya kila abiria kama ambavyo yalikuwa yameandikwa kwenye pasport. Lengo lao la kufanya hivi ilikuwa ni kujaribu kufahamu uraia wa kila mateka waliye naye. Baada ya kufanya uchambuzi huu wa passport zote, hatimaye siku hii ya tatu, yaani tarehe 29 June 1976 kiongozi wa magaidi hawa Wilfred Bose akiwa na karatasi mkononi aliingi ndani ya terminal ambayo walikuwa wanaitumia kuwahifadhi mateka na kisha akaanza kusoma majina ya kila abiria. Alichokuwa anakifanya ni kusoma majina ya mateka ambao passport zao zilionyesha walikuwa ni raia wa Israel. Lakini pia alisoma majina ya mateka wengine ambao licha ya passport zao kuonyesha kuwa hawakuwa raia wa Israel lakini walikuwa na majina ya kiyahudi. Pamoja na hao pia mateka wote ambao walikuwa na uraia pacha na uraia huo mmojawapo ukiwa ni Israel basi nao waliunganishwa kwenye list hii. Baada ya kuwatenganisha raia wote wa Israel na kuwaweka kwenye chumba kingine peke yao hapo hapo kwenye terminal, kuna mwanadada raia wa Ufaransa aliyeitwa Jocelyne Monier yeye jina lake halikuitwa kwenye ile list ya wanaotakiwa kutengwa kwenye chumba kingine (Waisrael na Wayahudi). Lakini ‘boyfriend’ wake alikuwa ni Muisrael na aliitwa jina na kutengwa na wengine katika kile chumba kingine. Mwanadada huyu ili kuonyesha kumtia moyo mpenzi wake na kupinga huu ubaguzi uliokuwa unafanywa na hawa magaidi, kwa hiari yake alijipeleka kwenye chumba cha mateka wa Kiisrael. Si mwanadada huyu pekee ambaye alifanya kitendo hiki cha ushujaa, lakini pia kulikuwa na mwanamama mwingine aliitwa Janet Almog (rai wa Marekani) na mateka mwingine aliyeitwa Jean-Jacques Mimouni (raia wa Ufaransa) nao kwenye kuonyesha hali ya kuwaunga mkono wenzao waliotengwa kwenye chumba kingine na kupinga ubaguzi uliokuwa unafanywa na maharamia hawa, nao walijipeleka kwa hiari yao kwenye chumba ambacho mateka hao walikibatiza jina “Chumba cha Waisrael”, ambacho mateka wote walijua fika kwamba kuna jambo baya maharamia hao walikuwa wamepanga kulifanya. Licha ya maharamia kwa kushirikiana na jeshi la Uganda kufanya uchambuzi huu wa kina kuhusu uraia wa kila mateka waliye naye, lakini walifanya kosa kubwa sana ambalo lilkuja kuwagharimu sana hapo baadae. Kwenye uchambuzi wao wote huu walioufanya walishindwa kumng’amua mateka mmoja mwanajeshi wa Israel ambaye alikuwa ana uraia pacha na siku hiyo alikuwa anatumia passport ambayo sio ya Israel. Mateka huyu alikuja kuwa muhimu sana huko mbeleni kuwapatia Mossad Intelijensia mujarabu kabisa kuhusu watekaji, jengo wanaloshikilia mateka, na namana wanavyoshirikiana na jeshi la Uganda. Siku iliyofuata yaani June 30, maharamia haya wakawaachia mkupuo wa kwanza wa mateka wasio raia wa Israel au wayahudi. Katika mkupuo huu wa kwanza waliachia mateka 48 ambao walikuwa ni wazee, watoto na akina mama wenye watoto wadogo. Baada ya mkupuo huu wa kwanza wa kuwaachia mateka hawa wachache, maharamia wakaweka wazi matakwa yao ili waweze kuachia mateka wengine. Kwanza kabisa walitaka walipwe fedha kiasi cha dola za Kimarekani milioni 5. Na pili walitakakuachiwa kwa wafungwa 53 wenye asili ya kipalestina wanaotuhumiwa kwa ugaidi, ambao kati yao 40 walikuwa kwenye jela za Israel na 13 katika nchi nyingine za Ulaya. Watekaji hawa wakatoa ‘ultimutum’ kwamba kama matakwa yao hayatatekelezwa ndani ya masaa ishirini na nne yajayo (mpaka tarehe 1 July saa 8 mchana) basi wataanza kuua raia wa Israel mmoja baada ya mwingine. Dunia nzima ni kama ilisimama kwa masaa kadhaa kutokana na sintofahamu iliyogubika kila mahali. Sintofahamu hii ililetwa na ukweli kwamba, ilikuwa inajulikana wazi kwa miaka yote kwamba Israel wana sera ya kutofanya mazungumzo au makubaliano na Magaidi. Kwahiyo kila mtu alikuwa nafahamu kuwa kuna uwezekano mkubwa ndani ya masaa 24 yajayo ulimwengu ukashuhidia watu zaidi ya 200 wakichinjwa kama kuku. NCHINI ISRAEL: KIKAO CHA BARAZA LA MAWAZIRI Nchini Israel kikao cha dharura cha baraza la mawaziri kilikuwa kimeitishwa na waziri Mkuu Yitzhak Rabin kujadili kuhusu hatua za kuchukua kuokoa raia wake ambao wameshikiliwa mateka huko uwanja wa ndege wa Entebbe, Uganda. Hali ya kikao ilikuwa tete sana kutokana na kila dakika waliyokuwa wanaitumia kujadili ndivyo ambavyo walikuwa wanaikaribia saa 8 mchana ya tarehe 1 July. Walipowasilana na Ujerumani na Ufaransa ambao nao walikuwa na baadhi ya wafungwa wa Kipalestina ambao watekaji walitaka waachiwe… walipowaomba ushirikiano wao kuhusu kukabali kuachia hao wafungwa, Ujerumani na Ufaransa walikataa katakata kuachia hata mfungwa mmoja wa Kipalestina ambaye alikuwa kwenye magereza zao. Sintofahamu ilizidi kuongezeka. Masaa yalizidi kuyoyoma. Saa 8 mchana ya tarehe 1 July ilizidi kukaribia. Harufu ya damu ilikuwa inabisha hodi mlangoni kwao. Licha ya weledi wao wote walionao lakini mbele yao waliona giza. Inapaswa kukumbukwa kwamba Idd Amin aliwahi kupatiwa mafunzo ya weledi wa kijeshi nchini Isarel (Special Force Training). Kwa hiyo baraza la mawaziri likamuagiza Baruch Bar-Lev, kamanda mstaafu wa IDF ambaye alihusika kumpatia mafunzo ya kijeshi Amin kipindi yuko Israel na kufanikiwa kujenga naye ukaribu. Baraza la Mawaziri likamuagiza Baruck (marafiki zake humuita “Burka”) kufanya mawasiliano na Rais huyo wa Uganda ili kujaribu kumuomba awashawishi magaidi wanaoshikilia mateka kwenye uwanja wake wa ndege wa Entebbe wawaachie mateka hao bila masharti magumu. Kupitia kwa Burka, Israel ilifikia mpaka hatua ya kumuahidi Idd Amin kuwa kama atafanikisha kuachiwa kwa mateka hao basi watatumia ushawishi walionao kuhakikisha kuwa Amin anatunukiwa tuzo ya amani ya Nobel. Lakini Amin hakulegeza msimamo, akaendelea kuwasisitiza kuwa hakuna namna nyingine yeyote ambayo mateka hao wataachiwa bila masharti yaliyotolewa na watekaji kutimizwa. Baada ya juhudi hii ya kumuhonga ‘tuzo’ kugonga mwamba, Waziri Mkuu wa Israel akawasiliana na serikali ya Marekani na kuwaomba wamshawishi Rais wa Misri Anwar Sadat ambaye alikuwa anaheshimiana sana na Amin ili amshawishi kuwaamuru magaidi yaliyoko uwanjani kwake Entebbe waachiemateka bila masharti magumu. Amin bado akashikilia msimamo kwamba hakuna mateka atakayeachiwa pasipo masharti yaliyotolewa kutimizwa. Juhudi hizi za kumshawishi Amin zilikula muda mwingi sana na hatimaye wakajikuta tayari kulikuwa kumekucha asubuhi. Mbele yao kulikuwa kumebakia masaa chini ya manane kabla ya damu ya zaidi ya watu 200 kumwagika. Baraza la mawaziri la Israel likamuomba Amin aongee na watekaji wakubali kusogeza siku mbele ili kuipa serikali ya Israel muda wakutosha kushughulikia lojistiki na kushawishi Ujerumani na Ufaransa ili waweze kutimiza sharti la kuachiwa kwa wafungwa wa kipalestina 53 wanaotuhumiwa kwa ugaidi. Rais Idd Amin baada ya kushawishiwa sana akakubali ombi hili na akaieleza serikali ya Israel kwamba ni siku tatu tu pekee zinaongezwa, yaani ikimaanisha kwamba siku zitaongezwa mpaka tarehe 4 July, saa 8 mchana. Serikali ya Israel ikakubliana na hili. Mchana wa siku hiyo, serikali ilitoa taarifa rasmi kwa vyombo vya habari wakilaani vitendo vya kigaidi na hususani matukio ya utekeji wa raia wasio na hatia, na pia ikaendelea kusisitiza kuhusu sera yake ya kutojadili na magaidi. Lakini taarifa hii ikamalizia kwa kueleza kuwa kwa kujali zaidi uhai wa zaidi ya raia 200 ambao bado wanashikiliwa na magaidi hayo, na kujali maumivu ambayo familia zao na taifa zima linapitia, wamekubali kutimiza sharti la magaidi hao la kuwalipa fedha za kimarekani dola milioni tano pamoja na kuachiwa kwa wafungwa wa kipalestina 53 wenye tuhuma za ugaidi. Ilikuwa ni moja ya matukio machache ambayo yaliishangaza dunia kwa Israel kukubali kushindwa hadharani. Kwa upande wa maadui wa Israel hii ilikuwa ni sherehe kubwa kwao. Na kwa upande wa Isarel na maswahiba zake hii iikuwa ni maombolezo makubwa. Amin na wenzake kule Uganda walikuwa wanasherehekea baada ya taarifa hii kutolewa kwa vyombo vya habari. Walihsi kabisa harufu ya ushindi inanukia kwenye pua zao. Kitu ambacho walikuwa hawafahamu ilikuwa ni kwamba, Israel walikuwa wanawafanyia ‘mchezo’ wa kisaikolojia ili Amin, jeshi lake na watekaji wajiamini kwa kuona kuwa ushindi umeegemea upande wao na hatimaye wajisahau kutokana na kujiamini huku. NYUMA YA PAZIA Huko Tel aviv, makamanda wa IDF na maafisa wa Mossad walikuwa wamekusanyika katika conference room ya mako makuu ya wizara ya ulinzi kuweka mkakati wa oparesheni ya uokozi (rescue mission) wa mateka wanaoshikiliwa katika uwanja wa ndege wa Entebbe, Uganda. Kati ya watu muhimu ambao walikuwepo kwenye kikao hiki alikuwa ni Waziri Mkuu Rabin na Ehud Barak ambaye kipindi hicho alikuwa kamanda wa ngazi za juu kwenye jeshi anayeongoza kitengo cha Intelijensia ya jeshi (Military Intelligence). Moja kati ya vitu muhimu ambavyo viliwasaidia ilikuwa ni taarifa ya intelijensia iliyoletwa na Mossad kwamba uwanja wa ndege wa Entebbe ulijengwa na kampuni ya Kiisrael inayoitwa Solel Boneh. Kwahiyo muwakilishi kutoka katika kampuni hii ya ujenzi naye akaitwa kikaoni kwa ajili ya kuwasilisha michoro kuhusu jengo lote na uwanja wa ndege wa Entebbe ulivyo. Lakini pia wakati huo huo kulikuwa na maafisa wa Mossad ambao walikuwa ufaransa kuwahoji wale mateka ambao walikuwa wameachiwa awali. Mtu muhimu zaidi ambaye alitoa taarifa nzuri kwa Mossad alikuwa ni yule afisa wa jeshi niliyemuelezea awali kwamba alikuwa na uraia wan chi mbili (Israel na Ufaransa) na siku hii alikuwa ametumia passport ya nchi ya ufaransa hivyo watekaji walimuachia pamoja na wenzake wa kundi la kwanza lile la watu 48. Bwana huyu alitoa taarifa muhimu zaidi kuhusu kilichokuwa kinaendelea katika uwanja wa ndege wa Entebbe, kwa kuwa yeye tofauti na wenzake kutokana na uzoefu wake wa jeshi alikuwa aliweza kuwaeleza Mossad kuhusu ni salaha za namna gani watekaji walikuwa nazo, kulikuwa na ndege za aina gani za kijeshi pale uwanjani (Idd Amin aliamuru Air Force ya Uganda kulinda uwanja huo masaa 24), pia aliweza kuwaeleza kuhusu ‘rotation’ ya ulinzi ya jeshi la Uganda pamoja na taarifa nyingine muhimu ambazo abiria wengine wasingeweza kuzitilia maanani au kkuzieleza kwa ufasaha. Baada ya kupata intelijensia ya kutosha, mkakati wa awali ambao ulipendekezwa na jeshi ulikuwa ni kutumia ndege ya kijeshi na kisha kudondosha makomando kwenye ziwa Viktoria na kutoka hapo watatumia boti za mpira kuvuka mpaka nchi kavu na hatimaye kuelekea uwanja wa ndege ambao haukuwa mbali sana na ziwa Viktoria. Mkakati huu ulikuwa ni mzuri lakini ulihairishwa baada ya kupewa taarifa kuwa ziwa Viktoria lilikuwa na mamba wengi na ingeweza kuhatarisha uhai wa hawa makomando kabla hata ya kufika kwenye uwanja wa ndege. Kwahiyo ilikuwa dhahiri kwamba mkakati wowote ambao utawekwa ni lazima uwe wa kuvamia kutokea nchi kavu na ikiwezekana kutoka nchi jirani. Changamoto kubwa zaidi ilikuwa ni usafiri. Yaani kwamba oparesheni hii ilikuwa si tu kwamba makomando wanaotumwa kutekeleza wanaenda kupambana na magaidi wanne tu walioteka ndege, bali ilikuwa ni kana kwamba wanaenda kupambana na jeshi zima la Uganda. Kwa hiyo kikosi cha makomando ambacho kitatumwa kwenda huko lazima kiwe na watu wengi wa kutosha na pia lazima wachukue silaha nzito za kutosha. Ili kufaniskisha safari yenye makomando wengi hivi na vifaa vizito ilikuwa ni lazima kutumia ndege kubwa za kijeshi zenye uwezo mkubwa pia na hakukuwa na chaguo zuri zaid ya kutumia ndege za kijeshi za LOCKHEED C-130 HERCULES. Sasa changamoto ilikuwa inakuja kwamba huwezi kurusha dege kubwa kama hii kwenda na kurudi kutoka Israel mpaka Uganda bila kujaza mafuta tena japo mara moja. Katika kipindi hiki bado Israel walikuwa hawajawa na uwezo wa kufanya ‘Aerial Refuel’, yaani ndege kujazwa mafuta kwa kutumia ndege nyingine ikiwa angani. Lakini pia ilikuwa ni lazima madege hayo yakikaribia Uganda yaruke chini chini ili kukwepa kudunguliwa na kuikwepa rada ya kijeshi. Kwa hiyo ilikuwa ni lazima kupata nchi ndani ya afrika Mashariki ambao watakubali madege hayo ya kijeshi ya Israel kutua kwenye uwanja wake wa ndege na kujaza mafuta lakini pia kujiandaa na kuanzisha operation kutokea hapo na pia anga lao kutumika kuanzisha shambulizi la kijeshi kuelekea Uganda. Sasa japokuwa nchi zote za Afrika Mashariki zilikuwa hazikubaliana na kitendo cha Rais wa Uganda kushirikiana na watekaji, lakini hakukuwa na hata nchi moja ambayo ilikuwa iko tayari kuingia kwenye mzozo na Idd Amin kwa kuruhusu viwanja vya vya ndege kutumika na ndege za jeshi la Israel au wanajeshi kujiandaa kuvamia Entebbe au pia kuruhusu anga lao kutumia na jeshi la Israel. Ndipo hapa ambapo kwa haraka sana siku hiyo hiyo Waziri Mkuu Rabin akamtuma Ehud Barak na maafisa wachache wa Mossad kwenda Kenya kushawishi serikali ya Mzee Jomo Kenyatta iruhusu ndege za jeshi la Isarel kutumia kiwanja chao cha ndege. Ehud barak na wenzake hawakwenda tu moja kwa moja kwa Mzee Kenyatta, bali kwanza walienda kwa Waziri wa kilimo wa kipindi hicho Bw. Bruce McKenzie ambaye huyu aliwahi kuwa afisa wa Idara ya ujasusi ya Uingereza, MI6 na pia alikuwa swahiba mkubwa wa Ehud Barak. Kwa hiyo Israel ikamtumia Bruce McKenzie kumshawishi Mzee Jomo Kenyatta kuruhusu anga la Kenya na viwanjavya ndege kutumiwa na makomando wa Israel na ndege zao. Ehud Barak na maafisa wa Mossad hawakuishia hapa tu, bali pia walifanya vikao vya siri na wafanyabiashara wakubwa nchini Kenya wenye asili ya Israel na wale ambao walikuwa na ‘marafiki’ wa Israel kuwaomba watumie ushawishi wao wa kisiasa na kiuchumi wasaidie kumshawishi Kenyatta kukubali ombi la seriakli ya Israael viwanja vyao kutumika na ndege za kijeshi za Israel na makondo wake. Baada ya mashinikizo haya kutoka kila upande, Mzee Kenyatta hakuwa na chaguo linguine zaidi ya kukubali ombi lao. Bwana huyu McKenzie pia alikuwa na ndege yakebinafsi, na Ehud Barak akaona fursa. Walitumia ndege hii ya kiraia kuruka mpaka Uganda mijini Entebbe na kukatiza juu ya anga la uwanja wa ndege wa Entebbe na walipokuwa wanapita juu ya anga la uwanja wa ndege, Ehud Barak akatumia fursa hii kupiga picha kila eneo la uwanja. Kwa kuwa hii ilikuwa ni ndege ya kiraia, jeshi la Uganda hawakushughulika nayo. Picha hizi zilizopigwa na Ehud Barak zilikuja kuwa na umuhimumkubwa katika maandalizi ya mwisho ya oparesheni ya makomando wa Isarel Kuvamia uwanja huu. Mpaka kufikia hapa maandalizi yote muhimu yalikuwa yamekamilika. WAKATI HUO HUO Upande wa watekaji kule Uganda walikuwa wanasubria mifwedha yao dola milioni 5 za kimarekani. Rais Idd Amin naye baada ya kufikia makubaliano na Israel kuwa masharti ya fedha na wafungwa wa kipalestina kuachiwa tarehe 4 July, naye ‘akarelax’ na akaona huo ndio muda wa kutekeleza majukumu Mengine akisubiria tarehe 4 July ifike. Katika kipindi hiki Idd amin ndiye alikuwa mwenyekiti wa Umoja wa Afrika kwa kuzingatia utaratibu wa uenyekiti kuzunguka kwa kila nchi kwa mwaka mmoja mmoja na wiki hii alikuwa anatakiwa kwenye kikao cha Umoja wa Afrika kilichokuwa kinafanyika Mauritius. Kwa hiyo Amin akafunga safari kuelekea Mauritius kwenda kukabidhi kijiti cha Uenyekiti. Ehud Barak aliposikia taarifa hii, kwa kutumia akili yake kubwa ya kuzaliwa aliyojaliwa na uzoefu wake wa ujasusi, aliona fursa adhimu kabisa hapa. Akawasiliana na walioko kikaoni huko Tel Aviv na kuwaeleza taarifa ambazo awali wote hawakuielewa. Ehud Barak: “Idd Amin akiwa ndani ya Uganda huwa anatumia Mercedes Limousine katika msafara wake” Waziri Mkuu Rabin: “Ok! Limefanyaje?’ Ehud Barak: “Nataka mtafute gari kama hiyo… Mercedes Limousine” Waziri Mkuu Rabin: “la kazi gani?” Ehud Barak: “siku ambayo kikosi cha makomando wakipanda kwenye ndege kutoka huko Israel kwenda Uganda, gari hilo nataka pia lipakiwe ndani ya ndge!” Kwa dakika kadhaa wote ambao walikuwa wanamsikiliza pale kikaoni kupitia simu hakuna ambaye alielewa nini hasa Ehud Barak alikuwa anapendekeza. Yalikuwa yamebaki masaa machache tu ambapo, weledi, ushujaa na uzalendo uliotukuka ulikuwa unaedna kudhihirika. Itaendelea #TheBOLD_JF
    0 Comments ·0 Shares ·2K Views
  • Wazee hvi kiwango cha kutoa ni sh ngap
    Wazee hvi kiwango cha kutoa ni sh ngap
    0 Comments ·0 Shares ·202 Views
  • TARABUSHI - KOFIA ZA KIHISTORIA.

    Leo hii ni aghalabu sana kukutana na mtu aliyevaa tarabushi kutokana na kutoweka kwa kofia hizi. Ni watu wachache sana wenye nazo, hususani wazee au wenye umri wa makamo, kwa kutaja wachache ni mbunge wa Musoma vijijini, Mh. Nimrod Mkono, na msanii wa maigizo, marehemu 'mzee small.

    Hizi ni kofia zenye rangi hasa nyekundu zikiwa na shada ya nyuzi nyeusi. Kwa kingereza zikijulikana kama 'Fez', kwa kiarabu 'Tarboosh' huku waswahili tukiita Tarabushi. Katika kuelezea historia ya Tarabushi, yanipasa kurudi miaka mia mbili iliyopita, pale ambapo Sultan Mahmud II wa dola ya Ottoman alipotangaza kofia za Fez/tarabushi kutumika kama vazi rasmi la dola hiyo. Sultani alifanya hivyo kufuatia kampeni yake ya kuboresha 'empire' ambapo alitamani watu wa Ottoman kuwa na utambulisho wao utakaowatofautisha na watu wengine.

    Kufuatia kampeni hiyo, tarabushi zilipata umaarufu mkubwa ndani na nje ya Ottoman ambapo watu wengi walianza kuvaa. Mwaka 1829, Mfalme Mahmud II alipitisha sheria kwamba tarabushi zianze kutumika katika jeshi lake, hivyo kwanzia siku hiyo tuliona wanajeshi wa Ottoman Empire wakienda kwenye uwanja wa vita wakiwa wamevaa tarabushi.

    Kabla ya wazo la kutumia Tarabushi, Sultani Mahmud II alichagua aina fulani ya kofia zenye asili ya Uingereza ambazo zina umbo la pembe tatu. Lakini watu wake wa karibu walimshauri kutotumia kofia hizo, kwasababu waliona hiyo pembe tatu humaanisha 'utatu mtakatifu' hivyo isingeleta tafsiri nzuri kwa watu wa Ottoman ambao asilimia kubwa ni waislamu. Wakristo huamini katika "utatu mtakatifu" yaani Mungu, Mwana na Roho mtakatifu.

    Wakati Sultani anaendelea kuwaza mbadala wa kofia, ikatokea siku mabaharia wa Ottoman walikuwa wanarudi kutoka Morroco. Kichwani wakiwa wamevaa kofia nyekundu zenye shada ya nyuzi nyeusi. Sultani akavutiwa na kofia hizo na hapo ndio chanzo cha kuzichagua kutumika kama utamaduni wa Ottoman Empire. Morroco ndipo zilipokuwa zinatengenezwa kwa wingi kwasababu rangi ya kutengeneza kofia hizo ilikuwa inatokana na matunda fulani ambayo yalistawi kwa wingi hapo Morroco katika mji wa Fez. Ndio maana hata jina la kofia hizo 'Fez', limetokana na mji huo ambao hadi mwaka 1912 ndio ulikuwa mji mkuu wa Morroco.

    Umaarufu wa kofia hizi uliendelea kutapakaa kote ulimwenguni, ukizingatia kwamba dola ya Ottoman ilikuwa ni dola kubwa iliyoenea sehemu nyingi. Hivyo baadhi ya nchi zikaanza kutumia kofia hizi hususani katika majeshi yao-mfano Cyprus, Ugiriki, Albania. Pia India, Misri, Ufaransa n.k.

    Kwa huku kwetu Afrika Mashariki, umaarufu wa kofia hizi ulikuja baada ya ujio wa ukoloni. Hiyo ni kutokana na ukweli kwamba katika kipindi cha Uingereza, waAfrika walijumuishwa katika jeshi la kikoloni ambalo lilikuja kuitwa 'King's African Rifles KAR' wakivaa sare za rangi ya khaki na kichwani walivaa Fez/ tarabushi. Jeshi hili lilianzishwa mwaka 1902 huko Kenya na baadae kuenea katika nchi zingine za Afrika Mashariki na hata kujumuishwa kwenye vita ya kwanza ya Dunia mwaka 1914.

    Pia katika makoloni ya Ujerumani, Tanganyika ikiwemo, kuliundwa jeshi la kikoloni 'Schutztruppe' ambapo waAfrika wengi walijumuishwa humo na kuwa Askari wa kikoloni 'Polizei-Askari', ambao sare zao zilikuwa za rangi ya khaki pamoja na kofia za tarabushi.

    Umaarufu wa kofia hizi za ulikuja kupungua mara baada kuanguka kwa dola ya Ottoman na kuzaliwa kwa nchi ya Uturuki ambapo mwaka 1925 Rais wa kwanza wa Uturuki bwana *Mustapha Kemal Artatuk,* alipiga marufuku kofia hizo. Hiyo ni katika hatua ya kuanzisha Uturuki mpya isiyo na mabaki ya kisultani. Pia huko Misri, mwaka 1956 Mara baada ya Gamer Abdel Nasser kumpindua mfalme, alipiga marufuku kofia za Tarboosh.

    Pia hata huku kwetu Afrika Mashariki, muda mfupi kidogo baada ya kupata uhuru, serikali ziliamua kubadilisha sare za majeshi yetu ambapo kofia zingine zilianza kutumika badala ya Tarabushi ambazo zilionekana ni kama za kikoloni. Na huo ndio ukawa mwanzo wa kupotea kwa kofia za Tarabushi japokuwa kuna baadhi ya watu waliendelea kubaki nazo.

    TARABUSHI - KOFIA ZA KIHISTORIA. Leo hii ni aghalabu sana kukutana na mtu aliyevaa tarabushi kutokana na kutoweka kwa kofia hizi. Ni watu wachache sana wenye nazo, hususani wazee au wenye umri wa makamo, kwa kutaja wachache ni mbunge wa Musoma vijijini, Mh. Nimrod Mkono, na msanii wa maigizo, marehemu 'mzee small. Hizi ni kofia zenye rangi hasa nyekundu zikiwa na shada ya nyuzi nyeusi. Kwa kingereza zikijulikana kama 'Fez', kwa kiarabu 'Tarboosh' huku waswahili tukiita Tarabushi. Katika kuelezea historia ya Tarabushi, yanipasa kurudi miaka mia mbili iliyopita, pale ambapo Sultan Mahmud II wa dola ya Ottoman alipotangaza kofia za Fez/tarabushi kutumika kama vazi rasmi la dola hiyo. Sultani alifanya hivyo kufuatia kampeni yake ya kuboresha 'empire' ambapo alitamani watu wa Ottoman kuwa na utambulisho wao utakaowatofautisha na watu wengine. Kufuatia kampeni hiyo, tarabushi zilipata umaarufu mkubwa ndani na nje ya Ottoman ambapo watu wengi walianza kuvaa. Mwaka 1829, Mfalme Mahmud II alipitisha sheria kwamba tarabushi zianze kutumika katika jeshi lake, hivyo kwanzia siku hiyo tuliona wanajeshi wa Ottoman Empire wakienda kwenye uwanja wa vita wakiwa wamevaa tarabushi. Kabla ya wazo la kutumia Tarabushi, Sultani Mahmud II alichagua aina fulani ya kofia zenye asili ya Uingereza ambazo zina umbo la pembe tatu. Lakini watu wake wa karibu walimshauri kutotumia kofia hizo, kwasababu waliona hiyo pembe tatu humaanisha 'utatu mtakatifu' hivyo isingeleta tafsiri nzuri kwa watu wa Ottoman ambao asilimia kubwa ni waislamu. Wakristo huamini katika "utatu mtakatifu" yaani Mungu, Mwana na Roho mtakatifu. Wakati Sultani anaendelea kuwaza mbadala wa kofia, ikatokea siku mabaharia wa Ottoman walikuwa wanarudi kutoka Morroco. Kichwani wakiwa wamevaa kofia nyekundu zenye shada ya nyuzi nyeusi. Sultani akavutiwa na kofia hizo na hapo ndio chanzo cha kuzichagua kutumika kama utamaduni wa Ottoman Empire. Morroco ndipo zilipokuwa zinatengenezwa kwa wingi kwasababu rangi ya kutengeneza kofia hizo ilikuwa inatokana na matunda fulani ambayo yalistawi kwa wingi hapo Morroco katika mji wa Fez. Ndio maana hata jina la kofia hizo 'Fez', limetokana na mji huo ambao hadi mwaka 1912 ndio ulikuwa mji mkuu wa Morroco. Umaarufu wa kofia hizi uliendelea kutapakaa kote ulimwenguni, ukizingatia kwamba dola ya Ottoman ilikuwa ni dola kubwa iliyoenea sehemu nyingi. Hivyo baadhi ya nchi zikaanza kutumia kofia hizi hususani katika majeshi yao-mfano Cyprus, Ugiriki, Albania. Pia India, Misri, Ufaransa n.k. Kwa huku kwetu Afrika Mashariki, umaarufu wa kofia hizi ulikuja baada ya ujio wa ukoloni. Hiyo ni kutokana na ukweli kwamba katika kipindi cha Uingereza, waAfrika walijumuishwa katika jeshi la kikoloni ambalo lilikuja kuitwa 'King's African Rifles KAR' wakivaa sare za rangi ya khaki na kichwani walivaa Fez/ tarabushi. Jeshi hili lilianzishwa mwaka 1902 huko Kenya na baadae kuenea katika nchi zingine za Afrika Mashariki na hata kujumuishwa kwenye vita ya kwanza ya Dunia mwaka 1914. Pia katika makoloni ya Ujerumani, Tanganyika ikiwemo, kuliundwa jeshi la kikoloni 'Schutztruppe' ambapo waAfrika wengi walijumuishwa humo na kuwa Askari wa kikoloni 'Polizei-Askari', ambao sare zao zilikuwa za rangi ya khaki pamoja na kofia za tarabushi. Umaarufu wa kofia hizi za ulikuja kupungua mara baada kuanguka kwa dola ya Ottoman na kuzaliwa kwa nchi ya Uturuki ambapo mwaka 1925 Rais wa kwanza wa Uturuki bwana *Mustapha Kemal Artatuk,* alipiga marufuku kofia hizo. Hiyo ni katika hatua ya kuanzisha Uturuki mpya isiyo na mabaki ya kisultani. Pia huko Misri, mwaka 1956 Mara baada ya Gamer Abdel Nasser kumpindua mfalme, alipiga marufuku kofia za Tarboosh. Pia hata huku kwetu Afrika Mashariki, muda mfupi kidogo baada ya kupata uhuru, serikali ziliamua kubadilisha sare za majeshi yetu ambapo kofia zingine zilianza kutumika badala ya Tarabushi ambazo zilionekana ni kama za kikoloni. Na huo ndio ukawa mwanzo wa kupotea kwa kofia za Tarabushi japokuwa kuna baadhi ya watu waliendelea kubaki nazo.
    Like
    1
    · 0 Comments ·0 Shares ·879 Views
  • Wazee wa betting maumivu ya hi kitu wanajua
    Wazee wa betting maumivu ya hi kitu wanajua😂
    Like
    1
    · 0 Comments ·0 Shares ·311 Views
  • Wazee wa kubet chuma yenu ishawekwaa Telegram kajarib bahati yako

    https://t.me/duduu_mendez_store/99

    Namna ya kufungua link za telegram
    https://whatsapp.com/channel/0029VacgCaPKmCPGmTmrnT04/152

    > 𝐃𝐔𝐃𝐔𝐔_𝐌𝐄𝐍𝐃𝐄𝐙 V4
    ▶︎ ●────────── 0:41
    Wazee wa kubet chuma yenu ishawekwaa Telegram kajarib bahati yako https://t.me/duduu_mendez_store/99 Namna ya kufungua link za telegram https://whatsapp.com/channel/0029VacgCaPKmCPGmTmrnT04/152 > 𝐃𝐔𝐃𝐔𝐔_𝐌𝐄𝐍𝐃𝐄𝐙 V4 ▶︎ ●────────── 0:41
    DUDUU_MENDEZ COMMUNITY
    t.me
    Prime Betting App premium unlocked👑 ✔️Hii ni mod ya prime Betting Tips ambayo imetolewa malipo✅ #wakamalia kazi kwenu😔 𝐃𝐔𝐃𝐔𝐔_𝐌𝐄𝐍𝐃𝐄𝐙 V4 ▶︎ ●────────── 0:41
    Like
    2
    · 0 Comments ·0 Shares ·776 Views
  • KIJANA SHUJAA NA KISIMA CHA GIZA

    Kulikuwa na kijiji kilichoitwa Mwanga, kilichozungukwa na mlima mkubwa uliotisha unaoitwa Mlima Giza. Katika mlima huo, kulikuwa na kisima cha kale kilichojulikana kama "Kisima cha Giza." Wazee wa kijiji walisema kwamba kisima hicho kilikuwa na nguvu za ajabu zinazoweza kuharibu au kuokoa kijiji. Lakini kulikuwa na onyo: yeyote aliyethubutu kuingia kisima hicho alikabiliana na majaribu ya kutisha.

    Siku moja, maafa yalifika kijijini. Ukame wa ajabu ulianza, mito ikakauka, mimea ikafa, na watu wakaanza kukata tamaa. Wazee walikusanyika na kuamua kwamba mtu mmoja shupavu alipaswa kwenda kwenye Kisima cha Giza kutafuta suluhisho. Hakuna aliyethubutu kujitolea, isipokuwa kijana mdogo mwenye moyo wa ujasiri aliyeitwa Baraka.

    Baraka, akiwa na azma ya kuokoa kijiji chake, aliandaa safari yake. Akiwa amebeba upinde wake, mshale mmoja, na mfuko wa maji, alianza kupanda Mlima Giza huku upepo mkali ukivuma. Njiani, alikutana na changamoto za kutisha—nyoka wakubwa waliotokea ghafla, na kelele za ajabu zilizokuwa zikimzomea. Lakini hakurudi nyuma.

    Baada ya muda mrefu wa kupambana, Baraka alifika kwenye Kisima cha Giza. Kilikuwa na mwanga hafifu unaotoka chini ya ardhi, na sauti ya mtoa fumbo ikazungumza kutoka gizani:
    "Kuokoa kijiji chako, lazima utoe kitu cha thamani zaidi maishani mwako. Je, uko tayari?"

    Baraka alitafakari kwa muda mfupi. Alijua maisha yake mwenyewe yalikuwa ya thamani zaidi kwake, lakini pia alihisi uzito wa dhiki ya kijiji chake. Bila kusita, alisema, "Niko tayari."

    Ghafla, mwanga mkali ulilipuka kutoka kisimani, na mafuriko ya maji safi yalitoka yakiteremka kuelekea kijijini. Mlima Giza ulianza kutikisika, lakini Baraka alishikilia imani. Wakati maji yalipokuwa yakiendelea kutiririka, sauti ile ilisema, "Ujasiri wako umeokoa kijiji chako. Furahi, kijana shujaa."

    Baraka alirejea kijijini akiwa salama, akishangiliwa na wakazi waliokuwa wakicheza kwa furaha huku wakinywa maji safi yaliyokuwa yamerejea. Kutoka siku hiyo, Baraka aliheshimiwa kama shujaa wa kijiji, na jina lake lilisimuliwa kwa vizazi kama mfano wa ujasiri na kujitolea kwa ajili ya wengine.

    Mafundisho: "Ujasiri wa kujitoa kwa ajili ya wengi una nguvu ya kubadilisha historia."
    KIJANA SHUJAA NA KISIMA CHA GIZA Kulikuwa na kijiji kilichoitwa Mwanga, kilichozungukwa na mlima mkubwa uliotisha unaoitwa Mlima Giza. Katika mlima huo, kulikuwa na kisima cha kale kilichojulikana kama "Kisima cha Giza." Wazee wa kijiji walisema kwamba kisima hicho kilikuwa na nguvu za ajabu zinazoweza kuharibu au kuokoa kijiji. Lakini kulikuwa na onyo: yeyote aliyethubutu kuingia kisima hicho alikabiliana na majaribu ya kutisha. Siku moja, maafa yalifika kijijini. Ukame wa ajabu ulianza, mito ikakauka, mimea ikafa, na watu wakaanza kukata tamaa. Wazee walikusanyika na kuamua kwamba mtu mmoja shupavu alipaswa kwenda kwenye Kisima cha Giza kutafuta suluhisho. Hakuna aliyethubutu kujitolea, isipokuwa kijana mdogo mwenye moyo wa ujasiri aliyeitwa Baraka. Baraka, akiwa na azma ya kuokoa kijiji chake, aliandaa safari yake. Akiwa amebeba upinde wake, mshale mmoja, na mfuko wa maji, alianza kupanda Mlima Giza huku upepo mkali ukivuma. Njiani, alikutana na changamoto za kutisha—nyoka wakubwa waliotokea ghafla, na kelele za ajabu zilizokuwa zikimzomea. Lakini hakurudi nyuma. Baada ya muda mrefu wa kupambana, Baraka alifika kwenye Kisima cha Giza. Kilikuwa na mwanga hafifu unaotoka chini ya ardhi, na sauti ya mtoa fumbo ikazungumza kutoka gizani: "Kuokoa kijiji chako, lazima utoe kitu cha thamani zaidi maishani mwako. Je, uko tayari?" Baraka alitafakari kwa muda mfupi. Alijua maisha yake mwenyewe yalikuwa ya thamani zaidi kwake, lakini pia alihisi uzito wa dhiki ya kijiji chake. Bila kusita, alisema, "Niko tayari." Ghafla, mwanga mkali ulilipuka kutoka kisimani, na mafuriko ya maji safi yalitoka yakiteremka kuelekea kijijini. Mlima Giza ulianza kutikisika, lakini Baraka alishikilia imani. Wakati maji yalipokuwa yakiendelea kutiririka, sauti ile ilisema, "Ujasiri wako umeokoa kijiji chako. Furahi, kijana shujaa." Baraka alirejea kijijini akiwa salama, akishangiliwa na wakazi waliokuwa wakicheza kwa furaha huku wakinywa maji safi yaliyokuwa yamerejea. Kutoka siku hiyo, Baraka aliheshimiwa kama shujaa wa kijiji, na jina lake lilisimuliwa kwa vizazi kama mfano wa ujasiri na kujitolea kwa ajili ya wengine. Mafundisho: "Ujasiri wa kujitoa kwa ajili ya wengi una nguvu ya kubadilisha historia."
    Like
    Love
    2
    · 0 Comments ·0 Shares ·622 Views
  • .BIN KAZUMARI: VIONGOZI WA SIMBA WAJIFUNZE KWA YANGA.
    .
    "Tofauti ya Yanga SC na Simba SC inaanzia hapa, RED CARD ya Bacca jana ungesikia maneno na shutuma kibao zingeandikwa hadi mitandaoni kwamba tutafika mpaka Zenji na tutajua kilakitu, Yanga SC wamepigwa wamekubali na maisha yanaendelea, kama wana jambo linaongelewa ndani linaisha"
    .
    "Yanga SC kwa hili nawapongeza kuwnzia viongozi, wapambe (CHAWA), wanachama na mashabiki, wamechapwa wamekung’uta makalio wamesepa zao mjini kuko kimyaaa!!! Hakuna aliyeuza wala kununua, ndiyo soka.


    NB: Siku 7 za wale Wazee hazijafika bado? . Hii nchi ina shida nyingi sana.
    .
    AMEANDIKA MCHAMBUZI, JEMEDARI SAID.

    Follow #jeyytv kwa habari zote
    #michezo #jeyytvupdates
    .BIN KAZUMARI: VIONGOZI WA SIMBA WAJIFUNZE KWA YANGA. . "Tofauti ya Yanga SC na Simba SC inaanzia hapa, RED CARD ya Bacca jana ungesikia maneno na shutuma kibao zingeandikwa hadi mitandaoni kwamba tutafika mpaka Zenji na tutajua kilakitu, Yanga SC wamepigwa wamekubali na maisha yanaendelea, kama wana jambo linaongelewa ndani linaisha" . "Yanga SC kwa hili nawapongeza kuwnzia viongozi, wapambe (CHAWA), wanachama na mashabiki, wamechapwa wamekung’uta makalio wamesepa zao mjini kuko kimyaaa!!! Hakuna aliyeuza wala kununua, ndiyo soka. NB: Siku 7 za wale Wazee hazijafika bado? 😂😂😂. Hii nchi ina shida nyingi sana. . AMEANDIKA MCHAMBUZI, JEMEDARI SAID. Follow #jeyytv kwa habari zote #michezo #jeyytvupdates
    Like
    1
    · 1 Comments ·0 Shares ·855 Views
  • .Kwenye press ya Wazee waliojitambulisha kuwa ni “Wazee wa Simba” wamekuja na matakwa yafuatayo:

    1- GSM aache mara moja kudhamini klabu nane za Ligi Kuu, kwa kufanya hivyo wanaamini wanajitengenezea mazingira ya alama za bure.

    2- Wamewakataa Waamuzi watatu kwa majina Ahmed Arajiga, Herri Sasii na Ramadhan Kayoko, wamesema wanataka Marefa wa nje ya nchi sio Tanzania.

    Baadhi ya vitu wanavyodai ambavyo vinasababisha mvurugano katimu yao wametoa siku saba wawe wameviondoa.
    .Kwenye press ya Wazee waliojitambulisha kuwa ni “Wazee wa Simba” wamekuja na matakwa yafuatayo: 1- GSM aache mara moja kudhamini klabu nane za Ligi Kuu, kwa kufanya hivyo wanaamini wanajitengenezea mazingira ya alama za bure. 2- Wamewakataa Waamuzi watatu kwa majina Ahmed Arajiga, Herri Sasii na Ramadhan Kayoko, wamesema wanataka Marefa wa nje ya nchi sio Tanzania. Baadhi ya vitu wanavyodai ambavyo vinasababisha mvurugano katimu yao wametoa siku saba wawe wameviondoa.
    Like
    Love
    5
    · 36 Comments ·0 Shares ·247 Views
  • Hii Simba itakuja kuua wazee wetu
    Hii Simba itakuja kuua wazee wetu
    Like
    Love
    Haha
    Wow
    5
    · 1 Comments ·1 Shares ·309 Views ·79
  • Acheni tamaa wazee waache watoto wakike wakue kidgo
    Acheni tamaa wazee waache watoto wakike wakue kidgo
    Like
    1
    · 0 Comments ·0 Shares ·193 Views
  • Wazee wenzangu nipen support bac hata kwa like na comment tufahamiane
    Wazee wenzangu nipen support bac hata kwa like na comment tufahamiane
    Like
    2
    · 0 Comments ·0 Shares ·666 Views
  • Kuna siku nilisikia wapangaji wenzagu wananiteta kwamba ninafanya kazi gani.

    Maana nipo tu wao wanaamka asubuhi purukushani za kwenda kazini na kurudi jioni.

    Mimi niko ndani. Nikitoka naenda gym, Kariakoo one time, au sokoni.

    Assumptions zilikuwa nyingi ikiwemo kuhisiwa naiba au ***** kwasababu ninajenga six pack na kutanua kifua tu.

    Guys, sisi ni pioneers.

    Wazee hawatuelewi. Wengi wa rika letu waliokuwa serious sana shule nao hawatuelewi pia.

    Sema I have a feelings fainali uzeeni we will have the last laugh.
    #NaongeaNaWewe
    Kuna siku nilisikia wapangaji wenzagu wananiteta kwamba ninafanya kazi gani. Maana nipo tu wao wanaamka asubuhi purukushani za kwenda kazini na kurudi jioni. Mimi niko ndani. Nikitoka naenda gym, Kariakoo one time, au sokoni. Assumptions zilikuwa nyingi ikiwemo kuhisiwa naiba au shoga kwasababu ninajenga six pack na kutanua kifua tu. Guys, sisi ni pioneers. Wazee hawatuelewi. Wengi wa rika letu waliokuwa serious sana shule nao hawatuelewi pia. Sema I have a feelings fainali uzeeni we will have the last laugh. #NaongeaNaWewe
    0 Comments ·0 Shares ·1K Views
More Results