#PART4
Wakati hayo yakiendelea Congo, kule Rwanda, kikundi cha waasi cha RPF chini ya Paul Kagame kilifanikiwa kuyashinda majeshi ya serikali na kuchukua dola baada ya yale mauaji ya kimbari. Askari wa jeshi la Rwanda, ambao wengi walikuwa Wahutu (Itarahamwe), walikimbilia Congo. Walipofika kule, wakaanzisha kikundi cha waasi cha kupigana na serikali ya Rwanda kilichoitwa FDLR. Kikundi hicho kikaungwa mkono na serikali ya Mobutu. Hivyo Mobutu akawa anawapa silaha wapigane na serikali ya Kagame ili kurudisha utawala wa Wahutu madarakani.
Wakati Mobutu akisaidia waasi kuangusha serikali ya Rwanda, kulikia na vikundi vya waasi zaidi ya 40 vinapigana na jeshi lake. Moja kati ya vikundi hivyo ni Alliance of Democratic Forces for the Liberation (AFDL) kilichokuwa kinaongozwa na Mzee Laurent Kabila, ambaye ni Mluba wa Katanga, kusini mashariki mwa Congo karibu na Ziwa Tanganyika.
Baada ya miaka karibu 30 ya kupigana msituni, hatimaye nguvu zikapungua. Akawa haendi tena mstari wa mbele. Mara kwa mara alikuja kupumzika nyumbani kwake Msasani jijini DSM, akimuachia Kanali Reuben Um-Nyobe kuongoza kikosi msituni.
Mobutu alipoamua kuwasaidia askari wa FDLR (Intarahamwe) kupigana na serikali ya Rwanda, Kagame nae akaamua kumuunga mkono Laurent Kabila na kikundi chake cha AFDL ili wamng'oe Mobutu. Yaani, serikali ya Rwanda ikaunga mkono waasi wa Congo kwa sababu serikali ya Congo inaunga mkono waasi wa Rwanda. ‘Scratch my back, and I will scratch yours’.
Wakati huo, inadaiwa serikali ya Rwanda ilikuwa imepata silaha nyingi kutoka Ufaransa na UK, kwa hiyo Kagame alijipima akaona ana nguvu za kupigana na Mobutu. Wakati huo Kagame alikuwa Makamu wa Rais chini ya Pasteur Bizimungu, lakini yeye ndiye aliyeongoza kila kitu. Sababu za kumuunga mkono Kabila;
1. Ethnicity (Waluba na Watutsi wanaelewana)
2. Mobutu kuunga mkono FDLR (Intarahamwe)
3. Uwepo wa rasilimali nyingi sana eneo la Kivu, hasa madini.
(Malisa GJ)
Wakati hayo yakiendelea Congo, kule Rwanda, kikundi cha waasi cha RPF chini ya Paul Kagame kilifanikiwa kuyashinda majeshi ya serikali na kuchukua dola baada ya yale mauaji ya kimbari. Askari wa jeshi la Rwanda, ambao wengi walikuwa Wahutu (Itarahamwe), walikimbilia Congo. Walipofika kule, wakaanzisha kikundi cha waasi cha kupigana na serikali ya Rwanda kilichoitwa FDLR. Kikundi hicho kikaungwa mkono na serikali ya Mobutu. Hivyo Mobutu akawa anawapa silaha wapigane na serikali ya Kagame ili kurudisha utawala wa Wahutu madarakani.
Wakati Mobutu akisaidia waasi kuangusha serikali ya Rwanda, kulikia na vikundi vya waasi zaidi ya 40 vinapigana na jeshi lake. Moja kati ya vikundi hivyo ni Alliance of Democratic Forces for the Liberation (AFDL) kilichokuwa kinaongozwa na Mzee Laurent Kabila, ambaye ni Mluba wa Katanga, kusini mashariki mwa Congo karibu na Ziwa Tanganyika.
Baada ya miaka karibu 30 ya kupigana msituni, hatimaye nguvu zikapungua. Akawa haendi tena mstari wa mbele. Mara kwa mara alikuja kupumzika nyumbani kwake Msasani jijini DSM, akimuachia Kanali Reuben Um-Nyobe kuongoza kikosi msituni.
Mobutu alipoamua kuwasaidia askari wa FDLR (Intarahamwe) kupigana na serikali ya Rwanda, Kagame nae akaamua kumuunga mkono Laurent Kabila na kikundi chake cha AFDL ili wamng'oe Mobutu. Yaani, serikali ya Rwanda ikaunga mkono waasi wa Congo kwa sababu serikali ya Congo inaunga mkono waasi wa Rwanda. ‘Scratch my back, and I will scratch yours’.
Wakati huo, inadaiwa serikali ya Rwanda ilikuwa imepata silaha nyingi kutoka Ufaransa na UK, kwa hiyo Kagame alijipima akaona ana nguvu za kupigana na Mobutu. Wakati huo Kagame alikuwa Makamu wa Rais chini ya Pasteur Bizimungu, lakini yeye ndiye aliyeongoza kila kitu. Sababu za kumuunga mkono Kabila;
1. Ethnicity (Waluba na Watutsi wanaelewana)
2. Mobutu kuunga mkono FDLR (Intarahamwe)
3. Uwepo wa rasilimali nyingi sana eneo la Kivu, hasa madini.
(Malisa GJ)
#PART4
Wakati hayo yakiendelea Congo, kule Rwanda, kikundi cha waasi cha RPF chini ya Paul Kagame kilifanikiwa kuyashinda majeshi ya serikali na kuchukua dola baada ya yale mauaji ya kimbari. Askari wa jeshi la Rwanda, ambao wengi walikuwa Wahutu (Itarahamwe), walikimbilia Congo. Walipofika kule, wakaanzisha kikundi cha waasi cha kupigana na serikali ya Rwanda kilichoitwa FDLR. Kikundi hicho kikaungwa mkono na serikali ya Mobutu. Hivyo Mobutu akawa anawapa silaha wapigane na serikali ya Kagame ili kurudisha utawala wa Wahutu madarakani.
Wakati Mobutu akisaidia waasi kuangusha serikali ya Rwanda, kulikia na vikundi vya waasi zaidi ya 40 vinapigana na jeshi lake. Moja kati ya vikundi hivyo ni Alliance of Democratic Forces for the Liberation (AFDL) kilichokuwa kinaongozwa na Mzee Laurent Kabila, ambaye ni Mluba wa Katanga, kusini mashariki mwa Congo karibu na Ziwa Tanganyika.
Baada ya miaka karibu 30 ya kupigana msituni, hatimaye nguvu zikapungua. Akawa haendi tena mstari wa mbele. Mara kwa mara alikuja kupumzika nyumbani kwake Msasani jijini DSM, akimuachia Kanali Reuben Um-Nyobe kuongoza kikosi msituni.
Mobutu alipoamua kuwasaidia askari wa FDLR (Intarahamwe) kupigana na serikali ya Rwanda, Kagame nae akaamua kumuunga mkono Laurent Kabila na kikundi chake cha AFDL ili wamng'oe Mobutu. Yaani, serikali ya Rwanda ikaunga mkono waasi wa Congo kwa sababu serikali ya Congo inaunga mkono waasi wa Rwanda. ‘Scratch my back, and I will scratch yours’.
Wakati huo, inadaiwa serikali ya Rwanda ilikuwa imepata silaha nyingi kutoka Ufaransa na UK, kwa hiyo Kagame alijipima akaona ana nguvu za kupigana na Mobutu. Wakati huo Kagame alikuwa Makamu wa Rais chini ya Pasteur Bizimungu, lakini yeye ndiye aliyeongoza kila kitu. Sababu za kumuunga mkono Kabila;
1. Ethnicity (Waluba na Watutsi wanaelewana)
2. Mobutu kuunga mkono FDLR (Intarahamwe)
3. Uwepo wa rasilimali nyingi sana eneo la Kivu, hasa madini.
(Malisa GJ)
0 Comentários
·0 Compartilhamentos
·8 Visualizações