• Kim Jong Un ampandisha Binti yake Kim Ju Ae kuwa Mrithi wa uongozi wa Korea Kaskazini.

    Kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jong Un, anatarajiwa kumtangaza rasmi Binti yake, Kim Ju Ae, kuwa Mrithi wake wa uongozi wa taifa hilo lenye utawala wa kifamilia unaodumu kwa miongo kadhaa.

    Hatua hiyo, iwapo itathibitishwa rasmi, itaashiria mabadiliko makubwa katika siasa za Pyongyang, ambako uongozi umekuwa ukirithishwa ndani ya familia ya Kim tangu kuanzishwa kwa taifa hilo mwaka 1948.

    Kwa mujibu wa taarifa zinazoibuka kutoka duru za kisiasa na Wachambuzi wa masuala ya Korea Kaskazini, Kim Jong Un anaelekea kumpa Binti yake nafasi ya juu katika mfumo wa uongozi wa Chama cha Wafanyakazi wa Korea, hatua itakayomuweka wazi kama Mrithi halali wa madaraka.

    Chanzo kimoja cha kisiasa kimenukuliwa kikisema: "Maandalizi ya kumtambulisha Kim Ju Ae kama Mrithi yamekuwa yakifanyika kimyakimya kwa muda sasa."

    Katika miezi ya hivi karibuni, Kim Ju Ae ameonekana mara kadhaa katika hafla za kijeshi na kitaifa akiwa sambamba na Baba yake, jambo lililotafsiriwa na Wachambuzi kama ishara ya maandalizi ya kisiasa.

    Mchambuzi mmoja wa siasa za Asia Mashariki amesema: "Kuonekana kwake hadharani katika matukio ya kijeshi ni ujumbe wa wazi kwa ndani na nje ya nchi kwamba anajengwa kama kiongozi ajaye."

    Iwapo Kim Ju Ae atatangazwa rasmi kuwa Mrithi, atakuwa Mwanamke wa kwanza katika historia ya Korea Kaskazini kurithi uongozi wa taifa hilo linaloongozwa kwa mfumo wa kifalme wa kisiasa.

    Hata hivyo, serikali ya Korea Kaskazini bado haijatoa tamko rasmi kuthibitisha hatua hiyo.

    Wachambuzi wanaamini kuwa tangazo rasmi linaweza kuwa na athari kubwa kwa siasa za ndani ya nchi pamoja na uhusiano wa kimataifa, hasa kwa mataifa yenye mvutano wa muda mrefu na Pyongyang.

    Kwa sasa, dunia inasubiri kuona ikiwa hatua hiyo itathibitishwa rasmi na mamlaka za Korea Kaskazini.

    Toa maoni yako
    #Habari
    Kim Jong Un ampandisha Binti yake Kim Ju Ae kuwa Mrithi wa uongozi wa Korea Kaskazini. Kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jong Un, anatarajiwa kumtangaza rasmi Binti yake, Kim Ju Ae, kuwa Mrithi wake wa uongozi wa taifa hilo lenye utawala wa kifamilia unaodumu kwa miongo kadhaa. Hatua hiyo, iwapo itathibitishwa rasmi, itaashiria mabadiliko makubwa katika siasa za Pyongyang, ambako uongozi umekuwa ukirithishwa ndani ya familia ya Kim tangu kuanzishwa kwa taifa hilo mwaka 1948. Kwa mujibu wa taarifa zinazoibuka kutoka duru za kisiasa na Wachambuzi wa masuala ya Korea Kaskazini, Kim Jong Un anaelekea kumpa Binti yake nafasi ya juu katika mfumo wa uongozi wa Chama cha Wafanyakazi wa Korea, hatua itakayomuweka wazi kama Mrithi halali wa madaraka. Chanzo kimoja cha kisiasa kimenukuliwa kikisema: "Maandalizi ya kumtambulisha Kim Ju Ae kama Mrithi yamekuwa yakifanyika kimyakimya kwa muda sasa." Katika miezi ya hivi karibuni, Kim Ju Ae ameonekana mara kadhaa katika hafla za kijeshi na kitaifa akiwa sambamba na Baba yake, jambo lililotafsiriwa na Wachambuzi kama ishara ya maandalizi ya kisiasa. Mchambuzi mmoja wa siasa za Asia Mashariki amesema: "Kuonekana kwake hadharani katika matukio ya kijeshi ni ujumbe wa wazi kwa ndani na nje ya nchi kwamba anajengwa kama kiongozi ajaye." Iwapo Kim Ju Ae atatangazwa rasmi kuwa Mrithi, atakuwa Mwanamke wa kwanza katika historia ya Korea Kaskazini kurithi uongozi wa taifa hilo linaloongozwa kwa mfumo wa kifalme wa kisiasa. Hata hivyo, serikali ya Korea Kaskazini bado haijatoa tamko rasmi kuthibitisha hatua hiyo. Wachambuzi wanaamini kuwa tangazo rasmi linaweza kuwa na athari kubwa kwa siasa za ndani ya nchi pamoja na uhusiano wa kimataifa, hasa kwa mataifa yenye mvutano wa muda mrefu na Pyongyang. Kwa sasa, dunia inasubiri kuona ikiwa hatua hiyo itathibitishwa rasmi na mamlaka za Korea Kaskazini. Toa maoni yako #Habari
    0 Comments 0 Shares 2 Views
  • Nchi ya Kenya yakemea vitendo vya kuwapeleka Vijana wake kwenye vita Nchini Ukraine.

    Serikali ya Kenya imekemea vikali vitendo vya baadhi ya Mawakala wanaodanganya Vijana kwa ahadi za ajira, kisha kuwapeleka moja kwa moja kwenye vita vinavyoendelea nchini Ukraine.

    Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya, Musalia Mudavadi, amesema: “Tunatarajia kufanya ziara rasmi mjini Moscow kwa mazungumzo na Serikali ya Urusi, lengo likiwa kusitisha kabisa matumizi ya raia wa Kenya katika mapambano haya.”

    Mudavadi alibainisha kuwa tayari Wakenya kadhaa wamefariki dunia, huku wengine wakijeruhiwa vibaya baada ya kudanganywa kuingia mikataba ya kijeshi. Amesema: “Hatukubali upotevu wa maisha ya raia wetu. Hatua za kudumu lazima zichukuliwe.”

    Serikali ya Kenya imelaumu Mawakala wa ajira wanaoshawishi vijana kwa ahadi za mishahara mikubwa, kisha kuwapeleka mstari wa mbele vitani. Ripoti ya hivi karibuni ya shirika la habari la Ufaransa, Agence France-Presse, imethibitisha kuwepo kwa mtandao wa udanganyifu unaowaingiza vijana wasiokuwa na historia ya kijeshi kusaini mikataba na Jeshi la Urusi, kisha kupelekwa haraka kwenye Uwanja wa mapambano.

    Mudavadi amesisitiza kuwa Kenya itafuatilia pia suala la kuachiliwa kwa Wakenya waliokamatwa kama wafungwa wa kivita nchini Ukraine. Amesema hatua hizi ni muhimu ili kulinda maisha ya Raia wake.

    Toa maoni yako
    #Habari
    #Russia #Ukraine #MusaliaMudavadi #Moscow #BreakingNews #WorldNews #VitaUkraine #KenyaAbroad #HumanRights #AfricaNews
    Nchi ya Kenya yakemea vitendo vya kuwapeleka Vijana wake kwenye vita Nchini Ukraine. Serikali ya Kenya imekemea vikali vitendo vya baadhi ya Mawakala wanaodanganya Vijana kwa ahadi za ajira, kisha kuwapeleka moja kwa moja kwenye vita vinavyoendelea nchini Ukraine. Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya, Musalia Mudavadi, amesema: “Tunatarajia kufanya ziara rasmi mjini Moscow kwa mazungumzo na Serikali ya Urusi, lengo likiwa kusitisha kabisa matumizi ya raia wa Kenya katika mapambano haya.” Mudavadi alibainisha kuwa tayari Wakenya kadhaa wamefariki dunia, huku wengine wakijeruhiwa vibaya baada ya kudanganywa kuingia mikataba ya kijeshi. Amesema: “Hatukubali upotevu wa maisha ya raia wetu. Hatua za kudumu lazima zichukuliwe.” Serikali ya Kenya imelaumu Mawakala wa ajira wanaoshawishi vijana kwa ahadi za mishahara mikubwa, kisha kuwapeleka mstari wa mbele vitani. Ripoti ya hivi karibuni ya shirika la habari la Ufaransa, Agence France-Presse, imethibitisha kuwepo kwa mtandao wa udanganyifu unaowaingiza vijana wasiokuwa na historia ya kijeshi kusaini mikataba na Jeshi la Urusi, kisha kupelekwa haraka kwenye Uwanja wa mapambano. Mudavadi amesisitiza kuwa Kenya itafuatilia pia suala la kuachiliwa kwa Wakenya waliokamatwa kama wafungwa wa kivita nchini Ukraine. Amesema hatua hizi ni muhimu ili kulinda maisha ya Raia wake. Toa maoni yako #Habari #Russia #Ukraine #MusaliaMudavadi #Moscow #BreakingNews #WorldNews #VitaUkraine #KenyaAbroad #HumanRights #AfricaNews
    0 Comments 2 Shares 67 Views
  • Hii hapa orodha ya Wachezaji 20 Wakongwe zaidi kuwahi kushinda Kombe la Dunia la FIFA, kulingana na takwimu za FIFA:

    1. Dino Zoff – Miaka 40 na siku 133

    2. Nilton Santos – Miaka 37 na siku 32

    3. Angelo Peruzzi – Miaka 36 na siku 143

    4. Franco Armani – Miaka 36 na siku 63

    5. Miroslav Klose – Miaka 36 na siku 34

    6. Gilmar Rinaldi – Miaka 35 na siku 185

    7. Lionel Messi – Miaka 35 na siku 177

    8. Toni Turek – Miaka 35 na siku 167

    9. Bernard Lama – Miaka 35 na siku 96

    10. Nicolás Otamendi – Miaka 34 na siku 309

    11. Ángel Di María – Miaka 34 na siku 307

    12. Alejandro Gómez – Miaka 34 na siku 306

    13. Castilho – Miaka 34 na siku 202

    14. Paul Mebus – Miaka 34 na siku 25

    15. Roman Weidenfeller – Miaka 33 na siku 341

    16. Didi – Miaka 33 na siku 252

    17. Fritz Walter – Miaka 33 na siku 246

    18. Paul Steiner – Miaka 33 na siku 166

    19. Franco Causio – Miaka 33 na siku 160

    20. Djalma Santos – Miaka 33 na siku 110

    #Sports
    Hii hapa orodha ya Wachezaji 20 Wakongwe zaidi kuwahi kushinda Kombe la Dunia la FIFA, kulingana na takwimu za FIFA: 1. Dino Zoff – Miaka 40 na siku 133 2. Nilton Santos – Miaka 37 na siku 32 3. Angelo Peruzzi – Miaka 36 na siku 143 4. Franco Armani – Miaka 36 na siku 63 5. Miroslav Klose – Miaka 36 na siku 34 6. Gilmar Rinaldi – Miaka 35 na siku 185 7. Lionel Messi – Miaka 35 na siku 177 8. Toni Turek – Miaka 35 na siku 167 9. Bernard Lama – Miaka 35 na siku 96 10. Nicolás Otamendi – Miaka 34 na siku 309 11. Ángel Di María – Miaka 34 na siku 307 12. Alejandro Gómez – Miaka 34 na siku 306 13. Castilho – Miaka 34 na siku 202 14. Paul Mebus – Miaka 34 na siku 25 15. Roman Weidenfeller – Miaka 33 na siku 341 16. Didi – Miaka 33 na siku 252 17. Fritz Walter – Miaka 33 na siku 246 18. Paul Steiner – Miaka 33 na siku 166 19. Franco Causio – Miaka 33 na siku 160 20. Djalma Santos – Miaka 33 na siku 110 #Sports
    0 Comments 2 Shares 59 Views
  • Trump aonya kuhusu makubaliano ya biashara kati ya China na Canada.

    Rais wa Marekani, Donald Trump, ametoa kauli kali akizungumzia uwezekano wa makubaliano ya kibiashara kati ya China na Canada, akionya kuwa hatua hiyo inaweza kuiweka Canada katika hatari kubwa ya kiuchumi.

    Akizungumza katika muktadha wa mijadala ya biashara za kimataifa, Trump alidai kuwa China ina uwezo mkubwa wa kiuchumi na kimkakati ambao unaweza kuathiri vibaya mataifa yanayoingia nayo mikataba bila tahadhari ya kutosha. Kwa mujibu wa Trump, Canada inaweza kujikuta ikidhoofishwa endapo itafanya makubaliano ya karibu na taifa hilo la Asia.

    “Ninasema wazi kabisa, China itaimeza Canada ikiwa watafanya makubaliano kati yao,” alisema Trump.

    Kauli hiyo imeibua mjadala mpana kuhusu uhusiano wa kibiashara kati ya mataifa makubwa na yale ya kati, hasa ikizingatiwa nafasi ya China kama moja ya nguvu kubwa za uchumi duniani. Wachambuzi wa siasa na uchumi wanasema matamshi ya Trump yanaakisi msimamo wake wa muda mrefu wa tahadhari na hata upinzani dhidi ya ushawishi wa China katika biashara za kimataifa.

    Hadi sasa, serikali ya Canada haijatoa tamko rasmi kujibu kauli hiyo, huku China pia ikikaa kimya kuhusu madai hayo. Hata hivyo, mjadala unaendelea kuonyesha jinsi masuala ya biashara na diplomasia yanavyoendelea kuwa nyeti katika uhusiano wa kimataifa, hasa yanapohusisha mataifa yenye maslahi makubwa ya kiuchumi.

    Toa maoni yako
    #Habari
    #Trump #China #Canada #Biashara #UhusianoYaKimataifa
    Trump aonya kuhusu makubaliano ya biashara kati ya China na Canada. Rais wa Marekani, Donald Trump, ametoa kauli kali akizungumzia uwezekano wa makubaliano ya kibiashara kati ya China na Canada, akionya kuwa hatua hiyo inaweza kuiweka Canada katika hatari kubwa ya kiuchumi. Akizungumza katika muktadha wa mijadala ya biashara za kimataifa, Trump alidai kuwa China ina uwezo mkubwa wa kiuchumi na kimkakati ambao unaweza kuathiri vibaya mataifa yanayoingia nayo mikataba bila tahadhari ya kutosha. Kwa mujibu wa Trump, Canada inaweza kujikuta ikidhoofishwa endapo itafanya makubaliano ya karibu na taifa hilo la Asia. “Ninasema wazi kabisa, China itaimeza Canada ikiwa watafanya makubaliano kati yao,” alisema Trump. Kauli hiyo imeibua mjadala mpana kuhusu uhusiano wa kibiashara kati ya mataifa makubwa na yale ya kati, hasa ikizingatiwa nafasi ya China kama moja ya nguvu kubwa za uchumi duniani. Wachambuzi wa siasa na uchumi wanasema matamshi ya Trump yanaakisi msimamo wake wa muda mrefu wa tahadhari na hata upinzani dhidi ya ushawishi wa China katika biashara za kimataifa. Hadi sasa, serikali ya Canada haijatoa tamko rasmi kujibu kauli hiyo, huku China pia ikikaa kimya kuhusu madai hayo. Hata hivyo, mjadala unaendelea kuonyesha jinsi masuala ya biashara na diplomasia yanavyoendelea kuwa nyeti katika uhusiano wa kimataifa, hasa yanapohusisha mataifa yenye maslahi makubwa ya kiuchumi. Toa maoni yako #Habari #Trump #China #Canada #Biashara #UhusianoYaKimataifa
    0 Comments 1 Shares 73 Views
  • Cristiano Ronaldo arejea Uwanjani baada ya mvutano Al Nassr na Saudi PIF.

    Ripoti zinazonukuliwa kutoka vyanzo mbalimbali nchini Saudi Arabia zinaeleza kuwa Staa wa soka duniani, Cristiano Ronaldo, amesitisha rasmi mgomo wake na yuko tayari kurejea Uwanjani kuitumikia klabu ya Al Nassr. Hatua hiyo inakuja baada ya Wafanyakazi wote wa klabu hiyo kulipwa mishahara yao pamoja na posho walizokuwa wakidai kwa muda.

    Kwa mujibu wa taarifa hizo, mgomo wa Ronaldo ulihusishwa na mvutano uliokuwepo kati yake na Tume ya Uwekezaji ya Saudi Arabia, maarufu kama Saudi PIF. Inadaiwa kuwa Nahodha huyo wa timu ya taifa ya Ureno alikuwa akilalamikia kile kilichoelezwa kuwa ni upendeleo kwa baadhi ya klabu, hususan katika masuala ya usajili wa Wachezaji na uwekezaji mkubwa unaofanywa kwenye timu fulani.

    Zaidi ya hayo, chanzo cha mgomo huo hakikujikita tu kwenye masuala ya usajili aliyoyaona kuwa hayaridhishi, bali pia katika kuhakikisha haki za Wafanyakazi wa klabu zinalindwa. Ronaldo alisisitiza kuwa Wafanyakazi wote, hasa wale wa ngazi za chini, walipaswa kulipwa stahiki zao kwa wakati na kwa ukamilifu.

    Hatua ya kulipwa kwa Wafanyakazi wote imeonekana kufungua ukurasa mpya ndani ya Al Nassr, na kurejesha hali ya utulivu kambini. Mashabiki wengi sasa wanasubiri kwa hamu kumuona Ronaldo akirejea Uwanjani, wakitumaini kuwa tukio hilo litaleta mabadiliko chanya ndani ya klabu hiyo na kwenye ligi kwa ujumla.

    Kwa kurejea kwake, Ronaldo anaonekana si tu kama Mchezaji mkubwa Uwanjani, bali pia kama sauti ya Wafanyakazi na mdau anayeonyesha kujali masuala ya haki na usawa ndani ya soka la kulipwa.

    Toa maoni yako
    #Tarifazauwakika
    Cristiano Ronaldo arejea Uwanjani baada ya mvutano Al Nassr na Saudi PIF. Ripoti zinazonukuliwa kutoka vyanzo mbalimbali nchini Saudi Arabia zinaeleza kuwa Staa wa soka duniani, Cristiano Ronaldo, amesitisha rasmi mgomo wake na yuko tayari kurejea Uwanjani kuitumikia klabu ya Al Nassr. Hatua hiyo inakuja baada ya Wafanyakazi wote wa klabu hiyo kulipwa mishahara yao pamoja na posho walizokuwa wakidai kwa muda. Kwa mujibu wa taarifa hizo, mgomo wa Ronaldo ulihusishwa na mvutano uliokuwepo kati yake na Tume ya Uwekezaji ya Saudi Arabia, maarufu kama Saudi PIF. Inadaiwa kuwa Nahodha huyo wa timu ya taifa ya Ureno alikuwa akilalamikia kile kilichoelezwa kuwa ni upendeleo kwa baadhi ya klabu, hususan katika masuala ya usajili wa Wachezaji na uwekezaji mkubwa unaofanywa kwenye timu fulani. Zaidi ya hayo, chanzo cha mgomo huo hakikujikita tu kwenye masuala ya usajili aliyoyaona kuwa hayaridhishi, bali pia katika kuhakikisha haki za Wafanyakazi wa klabu zinalindwa. Ronaldo alisisitiza kuwa Wafanyakazi wote, hasa wale wa ngazi za chini, walipaswa kulipwa stahiki zao kwa wakati na kwa ukamilifu. Hatua ya kulipwa kwa Wafanyakazi wote imeonekana kufungua ukurasa mpya ndani ya Al Nassr, na kurejesha hali ya utulivu kambini. Mashabiki wengi sasa wanasubiri kwa hamu kumuona Ronaldo akirejea Uwanjani, wakitumaini kuwa tukio hilo litaleta mabadiliko chanya ndani ya klabu hiyo na kwenye ligi kwa ujumla. Kwa kurejea kwake, Ronaldo anaonekana si tu kama Mchezaji mkubwa Uwanjani, bali pia kama sauti ya Wafanyakazi na mdau anayeonyesha kujali masuala ya haki na usawa ndani ya soka la kulipwa. Toa maoni yako #Tarifazauwakika
    0 Comments 0 Shares 66 Views
  • Sumary ya kile tulicho jifunza .

    Somo jinsi ya kusikia sauti ya MUNGU 2026.

    Lengo la MUNGU kumuumba mwanadamu ni mwanadamu asikie fresh kutoka kwa MUNGU.

    Mwanadamu akuandaliwa ili kuteseka au kuangaika aishi vipi ila kwa makosa ya Adamu wa kwanza ndiyo mwanadamu akajitenga na wanadamu.

    Kumbe sasa sauti ya MUNGU imeandaliwa moja kwa moja kwa ajiri ya wanadamu.

    #Mithali 8:4

    Ukikosea kusikia umekosea kuamua hatma yako

    Mwanadamu aliye fanikiwa kumsikia Mungu ndo mwanadamu aliye fanikiwa katika maisha.

    Sauti ya Mungu inabeba maonyo ,maelekezo,inafundisha .

    Kila ambaye mekuwa domant kwenye maisha ni mtu ambaye bado ajamsikia Mungu

    Kila unacho kiomba kimebebwa katika sauti ya Mungu,kushindwa kumsikia Mungu maombi yanapoteza maana.

    Akuna aliye wahi msikia Mungu na akabaki kuwa wakawaida.

    Wanaofundishwa na Bwana peke yake ndio wanapiga hatua.
    #Torati 4:35-36

    Kila anaye ishi kwa mafanikio duniani ananguvu inayo msimamosha either kutoka kwa Mungu au shetani.

    https://chat.whatsapp.com/LAB9tcfvKq887DB9IDHvzf

    #2026_sisi_ndio_wale _tunapiganiwa_na_Bwana.
    Sumary ya kile tulicho jifunza . Somo jinsi ya kusikia sauti ya MUNGU 2026. ⏩Lengo la MUNGU kumuumba mwanadamu ni mwanadamu asikie fresh kutoka kwa MUNGU. ⏩Mwanadamu akuandaliwa ili kuteseka au kuangaika aishi vipi ila kwa makosa ya Adamu wa kwanza ndiyo mwanadamu akajitenga na wanadamu. ⏩Kumbe sasa sauti ya MUNGU imeandaliwa moja kwa moja kwa ajiri ya wanadamu. #Mithali 8:4 ⏩Ukikosea kusikia umekosea kuamua hatma yako ⏩Mwanadamu aliye fanikiwa kumsikia Mungu ndo mwanadamu aliye fanikiwa katika maisha. ⏩Sauti ya Mungu inabeba maonyo ,maelekezo,inafundisha . ⏩Kila ambaye mekuwa domant kwenye maisha ni mtu ambaye bado ajamsikia Mungu ⏩Kila unacho kiomba kimebebwa katika sauti ya Mungu,kushindwa kumsikia Mungu maombi yanapoteza maana. ⏩Akuna aliye wahi msikia Mungu na akabaki kuwa wakawaida. Wanaofundishwa na Bwana peke yake ndio wanapiga hatua. #Torati 4:35-36 Kila anaye ishi kwa mafanikio duniani ananguvu inayo msimamosha either kutoka kwa Mungu au shetani. https://chat.whatsapp.com/LAB9tcfvKq887DB9IDHvzf #2026_sisi_ndio_wale _tunapiganiwa_na_Bwana.
    0 Comments 0 Shares 976 Views
  • Kila mwanadamu aliye wahi kupendwa na Mungu zawadi kubwa Mungu aliyo mpa huyo mtu ni watu.
    Isaya 43:4
    [4]Kwa kuwa ulikuwa wa thamani machoni pangu, na mwenye kuheshimiwa, nami nimekupenda; kwa sababu hiyo nitatoa watu kwa ajili yako; na kabila za watu kwa ajili ya maisha yako.

    Hivi umewahi kujiuliza kuwa pamoja na ujemedari wote wa Nahamani lakini ukoma wake ulibadilishwa kutoka kwa mtu aliye mpa code ya kuwa kuna mtu wa Mungu anaitwa Elisha.

    Musa pamoja na nguvu nyingi sana za Mungu alizo kuwa nazo bado alihitaji watu ili aweze kutimiza kusudi lake na Mungu akamchagulua Haruni ,wakina Yoshua ,Huri na wengine.

    Elia pamoja na kuwa na nguvu ya kusimamisha mvua lakini kuna muda alihitaji mtu ili apate kula chakula.

    Watu ni funguo na watu ni kufuli ukichanganya nama ya kuishi na watu umechanganya maisha.

    Kila unacho kihitaji kiko mikononi mwa wengine ni muhimu sana kumuomba Mungu akupe watu ili kupitia watu upate majibu.

    Unaomba Mungu akuoe kazi lakini uhalisia kazi unayo paswa kupewa iko mikononi mwa watu.

    Zaburi 2:8
    [8]Uniombe, nami nitakupa mataifa kuwa urithi wako,
    Na miisho ya dunia kuwa milki yako.

    Usiogope omba Mungu ni mwaminifu atakupa watu ambao ndio watabadilisha maisha yako.

    Kuna kundi la watu wanaitwa destiny helper's,divine connector na destiny shapers kila unapo omba muombe Mungu akusogezeee watu hawa maisha yako hayatabaki kama ulivyo.

    Wanaweza wasiwe matajiri ila wanajua njia za kupita ambazo ukipita utakuwa gumzo kwa dunia.

    YESU pamoja na nafasi yake ya uungu lakini pia alihitaji watu ili akamilishe kusudi lake duniani.

    Nikutakie asubui njema na siku njema

    BNE , Sylvester mwakabende
    0622625340
    #buidneweden
    #restoremenposition
    Kila mwanadamu aliye wahi kupendwa na Mungu zawadi kubwa Mungu aliyo mpa huyo mtu ni watu. Isaya 43:4 [4]Kwa kuwa ulikuwa wa thamani machoni pangu, na mwenye kuheshimiwa, nami nimekupenda; kwa sababu hiyo nitatoa watu kwa ajili yako; na kabila za watu kwa ajili ya maisha yako. Hivi umewahi kujiuliza kuwa pamoja na ujemedari wote wa Nahamani lakini ukoma wake ulibadilishwa kutoka kwa mtu aliye mpa code ya kuwa kuna mtu wa Mungu anaitwa Elisha. Musa pamoja na nguvu nyingi sana za Mungu alizo kuwa nazo bado alihitaji watu ili aweze kutimiza kusudi lake na Mungu akamchagulua Haruni ,wakina Yoshua ,Huri na wengine. Elia pamoja na kuwa na nguvu ya kusimamisha mvua lakini kuna muda alihitaji mtu ili apate kula chakula. Watu ni funguo na watu ni kufuli ukichanganya nama ya kuishi na watu umechanganya maisha. Kila unacho kihitaji kiko mikononi mwa wengine ni muhimu sana kumuomba Mungu akupe watu ili kupitia watu upate majibu. Unaomba Mungu akuoe kazi lakini uhalisia kazi unayo paswa kupewa iko mikononi mwa watu. Zaburi 2:8 [8]Uniombe, nami nitakupa mataifa kuwa urithi wako, Na miisho ya dunia kuwa milki yako. Usiogope omba Mungu ni mwaminifu atakupa watu ambao ndio watabadilisha maisha yako. Kuna kundi la watu wanaitwa destiny helper's,divine connector na destiny shapers kila unapo omba muombe Mungu akusogezeee watu hawa maisha yako hayatabaki kama ulivyo. Wanaweza wasiwe matajiri ila wanajua njia za kupita ambazo ukipita utakuwa gumzo kwa dunia. YESU pamoja na nafasi yake ya uungu lakini pia alihitaji watu ili akamilishe kusudi lake duniani. Nikutakie asubui njema na siku njema BNE , Sylvester mwakabende 0622625340 #buidneweden #restoremenposition
    0 Comments 0 Shares 2K Views
  • HAYA HAPA MATAIFA YALIYOFUZU KOMBE LA DUNIA FIFA WORLD CUP 2026

    OFFICIAL Timu Zilizofuzu kucheza Kombe La Dunia 2026

    DUA Nyingi Kwa Sasa DR Congo wametoboa na sasa wanaendelea na PlayOff kama wawakilishi wa Afrika kwenye Intercontinental PlayOff.

    Mexico
    United States
    Canada

    Japan
    Iran
    South Korea
    Australia
    Qatar
    Uzbekistan
    Saudi Arabia
    Jordan
    Morocco
    Senegal
    Egypt
    Algeria
    🇨🇮 Ivory Coast
    Tunisia
    South Africa
    Cabo Verde
    Ghana
    ARGENTINA
    Brazil
    Colombia
    Uruguay
    Ecuador
    Paraguay
    New Zealand
    England
    FRANCE
    Croatia
    Portugal
    Norway
    HAYA HAPA MATAIFA YALIYOFUZU KOMBE LA DUNIA FIFA WORLD CUP 2026 OFFICIAL Timu Zilizofuzu kucheza Kombe La Dunia 2026 DUA Nyingi Kwa Sasa DR Congo 🇨🇩 wametoboa na sasa wanaendelea na PlayOff kama wawakilishi wa Afrika kwenye Intercontinental PlayOff. 🇲🇽 Mexico 🇺🇸 United States 🇨🇦 Canada 🇯🇵 Japan 🇮🇷 Iran 🇰🇷 South Korea 🇦🇺 Australia 🇶🇦 Qatar 🇺🇿 Uzbekistan 🇸🇦 Saudi Arabia 🇯🇴 Jordan 🇲🇦 Morocco 🇸🇳 Senegal 🇪🇬 Egypt 🇩🇿 Algeria 🇨🇮 Ivory Coast 🇹🇳 Tunisia 🇿🇦 South Africa 🇨🇻 Cabo Verde 🇬🇭 Ghana 🇦🇷 ARGENTINA 🏆 🇧🇷 Brazil 🇨🇴 Colombia 🇺🇾 Uruguay 🇪🇨 Ecuador 🇵🇾 Paraguay 🇳🇿 New Zealand 🏴󠁧󠁢󠁥󠁮󠁧󠁿 England 🇫🇷 FRANCE 🥈 🇭🇷 Croatia 🇵🇹 Portugal 🇳🇴 Norway
    0 Comments 0 Shares 1K Views
  • Congo DRC wamezima ndoto za Bryan Mbuemo kukiwasha Kombe la Dunia 2026, baada ya kuwatupilia nje ya playoffs timu ya Taifa ya Cameroon kwa ushindi wa goli 1-0.

    🚨 Congo DRC 🇨🇩 wamezima ndoto za Bryan Mbuemo kukiwasha Kombe la Dunia 2026, baada ya kuwatupilia nje ya playoffs timu ya Taifa ya Cameroon kwa ushindi wa goli 1-0. 😅😅😅😅😅
    0 Comments 0 Shares 729 Views
  • JUST IN

    Kocha wa Brazil Carlo Ancelotti amekanusha kuwa alimwambia mshambuliaji wa Real Madrid mwenye umri wa miaka 19, Endrick, ambaye anakaribia kujiunga na Lyon kwa mkopo, kwamba alilazimika kuihama klabu hiyo ya Uhispania ili kupata nafasi ya kukipiga katika kikosi chake kwa ajili ya Kombe la Dunia la 2026.

    Via: AS - In Spanish
    🚨JUST IN🇧🇷 Kocha wa Brazil Carlo Ancelotti amekanusha kuwa alimwambia mshambuliaji wa Real Madrid mwenye umri wa miaka 19, Endrick, ambaye anakaribia kujiunga na Lyon kwa mkopo, kwamba alilazimika kuihama klabu hiyo ya Uhispania ili kupata nafasi ya kukipiga katika kikosi chake kwa ajili ya Kombe la Dunia la 2026. Via: AS - In Spanish
    0 Comments 0 Shares 632 Views
  • NASA yatahadharisha: uwezekano wa Dunia kukosa oksijeni Katika miaka ijayo.

    Shirika la Kitaifa la Anga na Nafasi ya Juu la Marekani (NASA) limetoa taarifa ya kisayansi inayoashiria uwezekano wa kutoweka kwa hewa safi ya oksijeni duniani katika kipindi cha miaka mingi ijayo.

    Kwa mujibu wa NASA, jambo hili halitasababishwa na shughuli za kibinadamu kama vile uchafuzi wa mazingira pekee, bali linahusiana zaidi na mabadiliko ya kiasili ya Dunia na Jua. Katika uchambuzi wake, NASA inabainisha kuwa:

    "Katika mabilioni ya miaka iliyopita, Dunia haikuwa na oksijeni ya kutosha. Kwa hiyo, kuna uwezekano kuwa hali kama hiyo ikajirudia tena katika mamilioni ya miaka ijayo," wamesema watafiti wa NASA.

    Hali hii inaweza kuathiri sio tu maisha ya binadamu bali pia viumbe hai wote wanaotegemea oksijeni kuishi. Ingawa ni tukio linalotabiriwa kutokea baada ya mamilioni ya miaka, Wanasayansi wanasema ni muhimu kwa jamii ya kimataifa kulielewa na kuendelea na utafiti zaidi kuhusu maisha ya baadaye ya Dunia.

    Kwa sasa, hakuna sababu ya hofu ya moja kwa moja, lakini onyo hili linaongeza msisitizo juu ya umuhimu wa kulinda mazingira na kuelewa kwa kina mfumo wa ikolojia wa sayari yetu.

    Toa maoni yako
    NASA yatahadharisha: uwezekano wa Dunia kukosa oksijeni Katika miaka ijayo. Shirika la Kitaifa la Anga na Nafasi ya Juu la Marekani (NASA) limetoa taarifa ya kisayansi inayoashiria uwezekano wa kutoweka kwa hewa safi ya oksijeni duniani katika kipindi cha miaka mingi ijayo. Kwa mujibu wa NASA, jambo hili halitasababishwa na shughuli za kibinadamu kama vile uchafuzi wa mazingira pekee, bali linahusiana zaidi na mabadiliko ya kiasili ya Dunia na Jua. Katika uchambuzi wake, NASA inabainisha kuwa: "Katika mabilioni ya miaka iliyopita, Dunia haikuwa na oksijeni ya kutosha. Kwa hiyo, kuna uwezekano kuwa hali kama hiyo ikajirudia tena katika mamilioni ya miaka ijayo," wamesema watafiti wa NASA. Hali hii inaweza kuathiri sio tu maisha ya binadamu bali pia viumbe hai wote wanaotegemea oksijeni kuishi. Ingawa ni tukio linalotabiriwa kutokea baada ya mamilioni ya miaka, Wanasayansi wanasema ni muhimu kwa jamii ya kimataifa kulielewa na kuendelea na utafiti zaidi kuhusu maisha ya baadaye ya Dunia. Kwa sasa, hakuna sababu ya hofu ya moja kwa moja, lakini onyo hili linaongeza msisitizo juu ya umuhimu wa kulinda mazingira na kuelewa kwa kina mfumo wa ikolojia wa sayari yetu. Toa maoni yako
    Like
    1
    0 Comments 0 Shares 1K Views
  • Israel yasema itaendelea kusimamia usalama Gaza, licha ya makubaliano ya usitishaji vita.

    Katika taarifa mpya iliyoibua mijadala ya kisiasa na kidiplomasia, Serikali ya Israel imesisitiza kuwa haitakubali kuachia jukumu la usalama wa Ukanda wa Gaza mikononi mwa vikosi vya kimataifa, licha ya kusaini makubaliano ya usitishaji vita yaliyosimamiwa na Marekani.

    Kupitia kikao na Baraza lake la Mawaziri, Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, alinukuliwa akisema:

    “Israel itaamua yenyewe ni lini na wapi itaendelea kuwakabili maadui zake. Hatutakubali kabisa nchi yoyote kutuamulia kuhusu usalama wetu.”

    Kauli hiyo imekuja muda mfupi baada ya makubaliano ya muda ya usitishaji mapigano kuwasilishwa, yakiruhusu kuundwa kwa kikosi cha kimataifa kitakacholinda amani na usambazaji wa misaada ya kibinadamu ndani ya Gaza.

    Kulingana na taarifa zilizotolewa, kikosi hicho kitapangwa kutoka mataifa ya Kiarabu au Kiislamu, na kazi yake kuu itakuwa kuhakikisha usalama wa Raia na kusimamia utekelezaji wa masharti ya kusitisha vita.

    Hata hivyo, Netanyahu ameeleza wasiwasi mkubwa juu ya mpango huo:

    “Tutashirikiana pale inapobidi, lakini hatutawahi kukubali Gaza kuwa chini ya mamlaka ya nje bila ridhaa ya Israel. Usalama wa Raia wetu ndio kipaumbele cha kwanza.”

    Kwa mujibu wa Afisa wa Marekani, makubaliano haya ni sehemu ya juhudi za muda mrefu kurejesha utulivu katika eneo hilo, lakini yanategemea ushirikiano wa pande zote mbili, jambo ambalo linazidi kuonekana kuwa gumu kutokana na msimamo wa Israel.

    Hii ni ishara kwamba licha ya mapendekezo ya kimataifa, Israel bado inashikilia msimamo wake wa kulinda mamlaka kamili ya usalama ndani ya Gaza, hatua inayoweza kuchelewesha utekelezaji wa makubaliano haya mapya.

    Je, Israel inaweza kusimamia amani Gaza bila msaada wa Jumuiya ya kimataifa? Au je, dunia inapaswa kuingilia kati kwa nguvu zaidi?

    Toa maoni yako
    Israel yasema itaendelea kusimamia usalama Gaza, licha ya makubaliano ya usitishaji vita. Katika taarifa mpya iliyoibua mijadala ya kisiasa na kidiplomasia, Serikali ya Israel imesisitiza kuwa haitakubali kuachia jukumu la usalama wa Ukanda wa Gaza mikononi mwa vikosi vya kimataifa, licha ya kusaini makubaliano ya usitishaji vita yaliyosimamiwa na Marekani. Kupitia kikao na Baraza lake la Mawaziri, Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, alinukuliwa akisema: “Israel itaamua yenyewe ni lini na wapi itaendelea kuwakabili maadui zake. Hatutakubali kabisa nchi yoyote kutuamulia kuhusu usalama wetu.” Kauli hiyo imekuja muda mfupi baada ya makubaliano ya muda ya usitishaji mapigano kuwasilishwa, yakiruhusu kuundwa kwa kikosi cha kimataifa kitakacholinda amani na usambazaji wa misaada ya kibinadamu ndani ya Gaza. Kulingana na taarifa zilizotolewa, kikosi hicho kitapangwa kutoka mataifa ya Kiarabu au Kiislamu, na kazi yake kuu itakuwa kuhakikisha usalama wa Raia na kusimamia utekelezaji wa masharti ya kusitisha vita. Hata hivyo, Netanyahu ameeleza wasiwasi mkubwa juu ya mpango huo: “Tutashirikiana pale inapobidi, lakini hatutawahi kukubali Gaza kuwa chini ya mamlaka ya nje bila ridhaa ya Israel. Usalama wa Raia wetu ndio kipaumbele cha kwanza.” Kwa mujibu wa Afisa wa Marekani, makubaliano haya ni sehemu ya juhudi za muda mrefu kurejesha utulivu katika eneo hilo, lakini yanategemea ushirikiano wa pande zote mbili, jambo ambalo linazidi kuonekana kuwa gumu kutokana na msimamo wa Israel. Hii ni ishara kwamba licha ya mapendekezo ya kimataifa, Israel bado inashikilia msimamo wake wa kulinda mamlaka kamili ya usalama ndani ya Gaza, hatua inayoweza kuchelewesha utekelezaji wa makubaliano haya mapya. Je, Israel inaweza kusimamia amani Gaza bila msaada wa Jumuiya ya kimataifa? Au je, dunia inapaswa kuingilia kati kwa nguvu zaidi? Toa maoni yako
    Love
    1
    0 Comments 0 Shares 2K Views
  • AYRA STARR AANDIKA HISTORIA KWENYE YOUTUBE KUPITIA WIMBO WAKE “RUSH”.

    Nyota wa muziki kutoka Nigeria, Ayra Starr, ameweka rekodi ya kipekee na kuandika jina lake kwenye vitabu vya historia ya burudani barani Afrika. Kupitia wimbo wake maarufu Rush, Ayra Starr amekuwa Msanii wa kwanza wa kike barani Afrika kufikisha zaidi ya Watazamaji milioni 500 kwenye mtandao wa YouTube kwa wimbo mmoja wa solo.

    Kupitia ukurasa wake rasmi wa Instagram, Ayra alishiriki furaha yake kwa mafanikio hayo na kusema:

    “Sauti ya Gen-Z kutoka Afrika inasikika! Rush imefanya historia, na hii ni mwanzo tu.”

    Kwa mafanikio haya, Rush imejiunga na orodha ya video tano bora za muziki za Kiafrika zilizotazamwa zaidi kila wakati kwenye YouTube.

    - Calm Down : Rema
    - Jerusalema : Master KG ft. Nomcebo Zikode
    - Love Nwantiti : CKay
    - Magic In The Air : Magic System

    Kinachovutia zaidi ni kwamba, licha ya umaarufu wa Wasanii kama Burna Boy, Wizkid, Davido, pamoja na wakali wa kimataifa kama NBA YoungBoy, Polo G, Lil Tjay, NLE Choppa, na Lil Durk, hakuna hata mmoja wao ambaye amewahi kufikisha Watazamaji zaidi ya milioni 500 kwa wimbo mmoja wa solo kwenye jukwaa la YouTube tofauti na Ayra Starr.

    Rekodi hii inaendelea kuimarisha nafasi ya Ayra Starr kama sauti muhimu ya kizazi kipya cha muziki barani Afrika, hasa kwa kizazi cha Gen-Z, na kuonyesha ukuaji wa ushawishi wa Wanawake kwenye tasnia ya muziki wa kimataifa.

    “Rush is not just a song, it’s a movement.” - Ayra Starr

    Pongezi kwa Ayra kwa kuwakilisha Afrika kwa kishindo duniani!
    AYRA STARR AANDIKA HISTORIA KWENYE YOUTUBE KUPITIA WIMBO WAKE “RUSH”. Nyota wa muziki kutoka Nigeria, Ayra Starr, ameweka rekodi ya kipekee na kuandika jina lake kwenye vitabu vya historia ya burudani barani Afrika. Kupitia wimbo wake maarufu Rush, Ayra Starr amekuwa Msanii wa kwanza wa kike barani Afrika kufikisha zaidi ya Watazamaji milioni 500 kwenye mtandao wa YouTube kwa wimbo mmoja wa solo. Kupitia ukurasa wake rasmi wa Instagram, Ayra alishiriki furaha yake kwa mafanikio hayo na kusema: “Sauti ya Gen-Z kutoka Afrika inasikika! Rush imefanya historia, na hii ni mwanzo tu.” Kwa mafanikio haya, Rush imejiunga na orodha ya video tano bora za muziki za Kiafrika zilizotazamwa zaidi kila wakati kwenye YouTube. - Calm Down : Rema - Jerusalema : Master KG ft. Nomcebo Zikode - Love Nwantiti : CKay - Magic In The Air : Magic System Kinachovutia zaidi ni kwamba, licha ya umaarufu wa Wasanii kama Burna Boy, Wizkid, Davido, pamoja na wakali wa kimataifa kama NBA YoungBoy, Polo G, Lil Tjay, NLE Choppa, na Lil Durk, hakuna hata mmoja wao ambaye amewahi kufikisha Watazamaji zaidi ya milioni 500 kwa wimbo mmoja wa solo kwenye jukwaa la YouTube tofauti na Ayra Starr. Rekodi hii inaendelea kuimarisha nafasi ya Ayra Starr kama sauti muhimu ya kizazi kipya cha muziki barani Afrika, hasa kwa kizazi cha Gen-Z, na kuonyesha ukuaji wa ushawishi wa Wanawake kwenye tasnia ya muziki wa kimataifa. “Rush is not just a song, it’s a movement.” - Ayra Starr Pongezi kwa Ayra kwa kuwakilisha Afrika kwa kishindo duniani!
    0 Comments 0 Shares 2K Views
  • Alloyce Nyanda

    Mtani wangu @gersonmsigwa mbona umekanusha kwa herufi kubwa hivyo ku likes Picha ya Mange

    Unajua acha nikusaidie Mtani ufahamu kuwa katika Hii Dunia Serikali zote Duniani huwa zinajaribu kuhakikisha zina “control information

    Uki Control Informatio utakuwa na nguvu ya kumuita Malaika-Shetani na shetani ukamuita Malaika na dunia itatii na haitahoji.

    Wenye nguvu za utoaji wa taarifa za dunia waliwahi ku control Information na kuuambia ulimwengu kuwa Muammar al-Gaddafi ni gaidi na dunia ikatii amri

    Waliandika kwa lugha zao nasi tukatafsiri kwa lugha yetu na tukamuita mwana wa Afrika Gadafi ni Gaidi.

    “Information is power”. Sasa wewe badala ya Kupambana ku Control Information wewe unapambana Kukanusha haitakusaidia wewe wala serikali yetu.

    Na Ku control Information huwa sio kuzima Internet au kufunga Mitandao kwa sababu wanaotaka taarifa wameshajua watapataje ndio wana VPN na wapo tayari Kulipia

    nataka nikushauri Msemaji ukifanyie kazi kwa haraka badala ya kukanusha na kulalamika jenga uwezo wa kumiliki nguvu ya Taarifa iliyokaribu na umma.

    Jitaidi Pages za serikali zenye kutoa taarifa zifanye ziwe na nguvu ili ziwe karibu na jamii yake sasa haiwezekani Mange Kimambi awe na ukaribu na jamii kiasi hicho kuliko serikali yenyewe.

    Unakuta wizara ya Afya badala ya kutengeneza maudhui yenye kuisogeza jamii karibu nayo wao wanaweza hata kupost picha waziri anasalimiana na Dkt na kuigeuza kuwa jambo la maana kupeleka kwa watu .

    Sasa kwa hulka hiyo utawezaje Ku control Power ya Taarifa? ukimkuta Mange amechapa Hospital X haina Vifaa wananchi wanaona huyu ndiye anatusaidia na wewe @gersonmsigwa unabakiza kazi ya kukanusha tu wakati unayo nafasi ya kueleza situation ya Hospital hata kabla ya wengine kupost

    Lazima idara za serikali zigeuzwe kuwa na uwezo wa kufanya Visibility kubwa , unadhani wewe Msigwa utaweza peke yako? Utachekwa tu

    Utakanusha ma ngapi na utapinga Ma ngapi? maana hata leo kuonekana umelikes page umehaha mbaya why? Wewe Pambana kuifanya Jamii kuiamini serikali zaidi ili wampuuze Mange

    Unataka kweli U contol Information kwa mbinu ya Mwijaku au Mzee wangu au Mafufu? (Utaishia kuchekesha tu)

    Power of Informations
    Alloyce Nyanda ✍️ Mtani wangu @gersonmsigwa mbona umekanusha kwa herufi kubwa hivyo ku likes Picha ya Mange Unajua acha nikusaidie Mtani ufahamu kuwa katika Hii Dunia Serikali zote Duniani huwa zinajaribu kuhakikisha zina “control information Uki Control Informatio utakuwa na nguvu ya kumuita Malaika-Shetani na shetani ukamuita Malaika na dunia itatii na haitahoji. Wenye nguvu za utoaji wa taarifa za dunia waliwahi ku control Information na kuuambia ulimwengu kuwa Muammar al-Gaddafi ni gaidi na dunia ikatii amri Waliandika kwa lugha zao nasi tukatafsiri kwa lugha yetu na tukamuita mwana wa Afrika Gadafi ni Gaidi. “Information is power”. Sasa wewe badala ya Kupambana ku Control Information wewe unapambana Kukanusha haitakusaidia wewe wala serikali yetu. Na Ku control Information huwa sio kuzima Internet au kufunga Mitandao kwa sababu wanaotaka taarifa wameshajua watapataje ndio wana VPN na wapo tayari Kulipia nataka nikushauri Msemaji ukifanyie kazi kwa haraka badala ya kukanusha na kulalamika jenga uwezo wa kumiliki nguvu ya Taarifa iliyokaribu na umma. Jitaidi Pages za serikali zenye kutoa taarifa zifanye ziwe na nguvu ili ziwe karibu na jamii yake sasa haiwezekani Mange Kimambi awe na ukaribu na jamii kiasi hicho kuliko serikali yenyewe. Unakuta wizara ya Afya badala ya kutengeneza maudhui yenye kuisogeza jamii karibu nayo wao wanaweza hata kupost picha waziri anasalimiana na Dkt na kuigeuza kuwa jambo la maana kupeleka kwa watu . Sasa kwa hulka hiyo utawezaje Ku control Power ya Taarifa? ukimkuta Mange amechapa Hospital X haina Vifaa wananchi wanaona huyu ndiye anatusaidia na wewe @gersonmsigwa unabakiza kazi ya kukanusha tu wakati unayo nafasi ya kueleza situation ya Hospital hata kabla ya wengine kupost Lazima idara za serikali zigeuzwe kuwa na uwezo wa kufanya Visibility kubwa , unadhani wewe Msigwa utaweza peke yako? Utachekwa tu Utakanusha ma ngapi na utapinga Ma ngapi? maana hata leo kuonekana umelikes page umehaha mbaya why? Wewe Pambana kuifanya Jamii kuiamini serikali zaidi ili wampuuze Mange Unataka kweli U contol Information kwa mbinu ya Mwijaku au Mzee wangu au Mafufu? (Utaishia kuchekesha tu) Power of Informations
    0 Comments 0 Shares 2K Views
  • Mlinzi wa kushoto wa Bayern Munich Alphonso Davies akielezea namna anavyojiona amepoteza uhuru wake baada ya kuwa mchezaji professional

    “Nipo mbali na familia yangu , siishi na girlfriend wangu marafiki zangu hawafiki watano yote haya yananifanya nijione nimepoteza kila kitu kwenye maisha”

    “Maisha ya kuwa mchezaji ni magumu sana ,kuna muda baada ya mazoezi unatakiwa kulala na sio kufanya chochote”

    Mpira wa miguu ni mchezo unaohitaji kujitoa sana hasa unapokuwa professional , ili kuishi mpira unavyotaka basi ni lazima uipe mgongo dunia na hiko ndicho anachopitia Davies hadi kujiona amepoteza kila kitu , imagine pesa unayo ya kutosha ila unapangiwa vitamu usile

    #SportsElite
    Mlinzi wa kushoto wa Bayern Munich Alphonso Davies akielezea namna anavyojiona amepoteza uhuru wake baada ya kuwa mchezaji professional “Nipo mbali na familia yangu , siishi na girlfriend wangu marafiki zangu hawafiki watano yote haya yananifanya nijione nimepoteza kila kitu kwenye maisha” “Maisha ya kuwa mchezaji ni magumu sana ,kuna muda baada ya mazoezi unatakiwa kulala na sio kufanya chochote” Mpira wa miguu ni mchezo unaohitaji kujitoa sana hasa unapokuwa professional , ili kuishi mpira unavyotaka basi ni lazima uipe mgongo dunia na hiko ndicho anachopitia Davies hadi kujiona amepoteza kila kitu , imagine pesa unayo ya kutosha ila unapangiwa vitamu usile #SportsElite
    0 Comments 0 Shares 1K Views
  • Lamine Yamal ni mmoja wa mawinga bora kabisa wa kulia kwenye soka kwa sasa huku Nuno Mendes akiwa beki bora kabisa wa kushoto kwa sasa Duniani wakati wawili hawa wakikutana mara mbili hivi karibuni kwenye mchezo wa UEFA Nations League (Fainali, Ureno vs Uhispania) na kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya (UCL), (Barcelona vs PSG).

    Kwenye mechi zote mbili Yamal ameshindwa kutamba mbele ya Mreno huyo ambaye alifunga goli na kutoa 'assist' na kuwa nyota wa mchezo huku timu yake ikishinda mara zote wakati Yamal akitoka patupu bila goli huku timu yake ikipoteza.

    Je unadhani kuna winga anaweza kummudu Nuno Mendes kwa sasa?

    FAINALI: #UEFANATIONS LEAGUE
    Ureno 2-2 Uhispania (P 5-3)
    Mendes
    Ronaldo

    Zubimendi
    Oyarzabal

    #UCL
    Barcelona 1-2 PSG
    19' Torres
    38' Mayulu( Mendes)
    90' Ramos ( Hakimi)


    #SportsElite
    Lamine Yamal ni mmoja wa mawinga bora kabisa wa kulia kwenye soka kwa sasa huku Nuno Mendes akiwa beki bora kabisa wa kushoto kwa sasa Duniani wakati wawili hawa wakikutana mara mbili hivi karibuni kwenye mchezo wa UEFA Nations League (Fainali, Ureno vs Uhispania) na kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya (UCL), (Barcelona vs PSG). Kwenye mechi zote mbili Yamal ameshindwa kutamba mbele ya Mreno huyo ambaye alifunga goli na kutoa 'assist' na kuwa nyota wa mchezo huku timu yake ikishinda mara zote wakati Yamal akitoka patupu bila goli huku timu yake ikipoteza. ✍️ Je unadhani kuna winga anaweza kummudu Nuno Mendes kwa sasa? FAINALI: #UEFANATIONS LEAGUE Ureno 🇵🇹 2-2 🇪🇸 Uhispania (P 5-3) ⚽ Mendes ⚽ Ronaldo ⚽ Zubimendi ⚽ Oyarzabal #UCL Barcelona 🇪🇸 1-2 🇫🇷 PSG ⚽ 19' Torres ⚽ 38' Mayulu(🅰️ Mendes) ⚽ 90' Ramos (🅰️ Hakimi) #SportsElite
    0 Comments 0 Shares 1K Views
  • Timu ya Argentina's wamezindua jezi ya ugenini itakayotumika katika kombe la dunia 2026


    #SportsElite
    🚨🚨 🇦🇷Timu ya Argentina's wamezindua jezi ya ugenini itakayotumika katika kombe la dunia 2026 #SportsElite
    0 Comments 0 Shares 808 Views
  • Leonardo Bonucci : " Nilipokabiliana na Messi kwenye Fainali ya 2022, nilimpongeza kwa kushinda Copa America na nikamwambia, "Messi, unastahili. Ulijitolea kwa ajili ya Argentina. Sasa huna chochote cha kuthibitisha kwa ulimwengu. Umeshinda kila kitu kwenye soka. Unaweza kustaafu ukiwa na amani ya akili.”

    Alitabasamu na kuniambia, "Nilifanya hivi kwa ajili ya nchi yangu, si kwa ajili yangu mwenyewe. Ni hayo tu. Sifikirii kuhusu mafanikio ya mtu binafsi zaidi ya mataji ya nchi yangu, lakini ikiwa sitashinda Kombe la Dunia, sitastaafu." [Anacheka] Kwa hivyo nikamwambia, "Umefanya kila kitu kwenye soka. Hata kama hutashinda Kombe la Dunia, wewe ni mchezaji bora zaidi katika historia."

    Lakini baada ya Messi kushinda Kombe la Dunia, niliiambia familia yangu, "Hii ni haki ya mpira wa miguu. Messi anastahili kuwa na Kombe la Dunia zaidi ya moja kwa sababu ya muujiza wa soka aliofanya na jinsi ulimwengu ulivyofurahia kile alichokifanya. Nikikutana naye tena, nitamwambia, "Sasa unaweza kustaafu na utulivu wa akili." Hata neno bora katika historia halitoshi kwa Messi."

    #SportsElite
    🎙️Leonardo Bonucci🇮🇹 : " Nilipokabiliana na Messi kwenye Fainali ya 2022, nilimpongeza kwa kushinda Copa America na nikamwambia, "Messi, unastahili. Ulijitolea kwa ajili ya Argentina. Sasa huna chochote cha kuthibitisha kwa ulimwengu. Umeshinda kila kitu kwenye soka. Unaweza kustaafu ukiwa na amani ya akili.” Alitabasamu na kuniambia, "Nilifanya hivi kwa ajili ya nchi yangu, si kwa ajili yangu mwenyewe. Ni hayo tu. Sifikirii kuhusu mafanikio ya mtu binafsi zaidi ya mataji ya nchi yangu, lakini ikiwa sitashinda Kombe la Dunia, sitastaafu." [Anacheka] Kwa hivyo nikamwambia, "Umefanya kila kitu kwenye soka. Hata kama hutashinda Kombe la Dunia, wewe ni mchezaji bora zaidi katika historia." Lakini baada ya Messi kushinda Kombe la Dunia, niliiambia familia yangu, "Hii ni haki ya mpira wa miguu. Messi anastahili kuwa na Kombe la Dunia zaidi ya moja kwa sababu ya muujiza wa soka aliofanya na jinsi ulimwengu ulivyofurahia kile alichokifanya. Nikikutana naye tena, nitamwambia, "Sasa unaweza kustaafu na utulivu wa akili." Hata neno bora katika historia halitoshi kwa Messi." #SportsElite
    0 Comments 0 Shares 2K Views
  • 5.WATU WANAO WEZA KUKUTAMBULISHA.

    Zawadi kubwa mtu anayo pewa na Mungu ni watu .

    Ukipata watu wanao weza kukutambulisha au kutambulisha maono yako basi jua umepiga hatua.

    Kila aliye fanikiwa anao watu walimshikaga mkono na kuntambulisha kwebye jamii na jamii ikaanza kumuamini kama inavyo muamini aliye kutambulisha.

    Daudi pamoja na kupakwa mafuta lakini bado ili ufalme ukamilike alijitaji mtu anaye weza kutambulisha .

    1 Samweli 16:17-18
    [17]Basi Sauli akawaambia, Vema, nitafutieni mtu aliye stadi wa kupiga kinubi, mkaniletee.

    [18]Ndipo akajibu mmoja wa watumishi wake akasema, Tazama, nimemwona mwana mmoja wa Yese, Mbethlehemi, aliye stadi wa kupiga kinubi, tena ni mtu shujaa, hodari wa vita, anenaye kwa busara, mtu mzuri, ambaye BWANA yu pamoja naye.

    Ile Daudi kupakwa mafuta peke yake haikumfanya awe mfalme ni mpaka alipo patikana mtu anayeweza kuntambulisha na huyu akikutambulisha vyema umeiteka dunia.

    Mfano mwingine Yusuph aliota ndoto akiwa mdogo kuwa ndugu zake na baba yake wote wanamtumikia .

    Lakini ili itimie ndoto ile ilihitaji mtu anaye weza mtambulisha

    Mwanzo 41:9-14
    [9]Basi mkuu wa wanyweshaji akamwambia Farao akisema, Nayakumbuka makosa yangu leo.

    [10]Farao aliwakasirikia watumwa wake, akanitia nifungwe nyumbani mwa mkuu wa askari, mimi na mkuu wa waokaji.

    [11]Tukaota ndoto usiku mmoja, mimi na yeye; kila mtu kwa tafsiri ya ndoto yake tukaota.
    .
    [12]Na huko pamoja nasi palikuwa na kijana; Mwebrania, mtumishi wa mkuu wa askari, tukamhadithia, naye akatufasiria ndoto zetu; akamfasiria kila mtu kama ilivyokuwa ndoto yake.
    .
    [13]Ikawa, kama vile alivyotufasiria ndivyo ilivyotokea; mimi nalirudishwa katika kazi yangu, na yeye alitundikwa.
    .
    [14]Ndipo Farao akapeleka watu, akamwita Yusufu, wakamleta upesi kutoka gerezani. Akanyoa, akabadili nguo zake, na kuingia kwa Farao.

    Kukamilika kwa ndoto alizo ota akiwa mdogo Yusuph ni mpaka alipo patikana mtu anayeweza kuntambulisha tu.

    Jifunze kuwa na prayer point ya kumuomba Mungu akupe mtu anaye weza kukutambulisha na watu wakamkubali hakika

    Changamoto kubwa ya vijana wengi leo hawako tayari kuwa heshimu watu hivyo wanakosa watu wanao weza kuwapa mkono wa shirika na kuwatambulisha.

    Nikwambie ukweli akuna chochote duniani kinakuwa bila watu kukupa mkono wa shirika na kukutambulisha.

    Niwatakie asubui njema na siku njema. Usisahau kutufollow sikiliza mwanangu

    Sylvester Mwakabende
    Build new eden
    0622625340
    5.WATU WANAO WEZA KUKUTAMBULISHA. Zawadi kubwa mtu anayo pewa na Mungu ni watu . Ukipata watu wanao weza kukutambulisha au kutambulisha maono yako basi jua umepiga hatua. Kila aliye fanikiwa anao watu walimshikaga mkono na kuntambulisha kwebye jamii na jamii ikaanza kumuamini kama inavyo muamini aliye kutambulisha. Daudi pamoja na kupakwa mafuta lakini bado ili ufalme ukamilike alijitaji mtu anaye weza kutambulisha . 1 Samweli 16:17-18 [17]Basi Sauli akawaambia, Vema, nitafutieni mtu aliye stadi wa kupiga kinubi, mkaniletee. [18]Ndipo akajibu mmoja wa watumishi wake akasema, Tazama, nimemwona mwana mmoja wa Yese, Mbethlehemi, aliye stadi wa kupiga kinubi, tena ni mtu shujaa, hodari wa vita, anenaye kwa busara, mtu mzuri, ambaye BWANA yu pamoja naye. Ile Daudi kupakwa mafuta peke yake haikumfanya awe mfalme ni mpaka alipo patikana mtu anayeweza kuntambulisha na huyu akikutambulisha vyema umeiteka dunia. Mfano mwingine Yusuph aliota ndoto akiwa mdogo kuwa ndugu zake na baba yake wote wanamtumikia . Lakini ili itimie ndoto ile ilihitaji mtu anaye weza mtambulisha Mwanzo 41:9-14 [9]Basi mkuu wa wanyweshaji akamwambia Farao akisema, Nayakumbuka makosa yangu leo. [10]Farao aliwakasirikia watumwa wake, akanitia nifungwe nyumbani mwa mkuu wa askari, mimi na mkuu wa waokaji. [11]Tukaota ndoto usiku mmoja, mimi na yeye; kila mtu kwa tafsiri ya ndoto yake tukaota. . [12]Na huko pamoja nasi palikuwa na kijana; Mwebrania, mtumishi wa mkuu wa askari, tukamhadithia, naye akatufasiria ndoto zetu; akamfasiria kila mtu kama ilivyokuwa ndoto yake. . [13]Ikawa, kama vile alivyotufasiria ndivyo ilivyotokea; mimi nalirudishwa katika kazi yangu, na yeye alitundikwa. . [14]Ndipo Farao akapeleka watu, akamwita Yusufu, wakamleta upesi kutoka gerezani. Akanyoa, akabadili nguo zake, na kuingia kwa Farao. Kukamilika kwa ndoto alizo ota akiwa mdogo Yusuph ni mpaka alipo patikana mtu anayeweza kuntambulisha tu. Jifunze kuwa na prayer point ya kumuomba Mungu akupe mtu anaye weza kukutambulisha na watu wakamkubali hakika Changamoto kubwa ya vijana wengi leo hawako tayari kuwa heshimu watu hivyo wanakosa watu wanao weza kuwapa mkono wa shirika na kuwatambulisha. Nikwambie ukweli akuna chochote duniani kinakuwa bila watu kukupa mkono wa shirika na kukutambulisha. Niwatakie asubui njema na siku njema. Usisahau kutufollow sikiliza mwanangu Sylvester Mwakabende Build new eden 0622625340
    0 Comments 0 Shares 2K Views
  • Kuna jamaa alisema... kama hapa duniani unatafuta hela kwa lengo la kula, kunywa, na kulala, basi huna utofauti sana na chura au kunguru

    Ouch! Unfiltered, brutal, reality.
    Kuna jamaa alisema... kama hapa duniani unatafuta hela kwa lengo la kula, kunywa, na kulala, basi huna utofauti sana na chura au kunguru Ouch! Unfiltered, brutal, reality.
    Like
    1
    0 Comments 0 Shares 630 Views
More Results