• Mwigizaji wa Nollywood Maurice Sam, mtandaoni yachafukwa baada ya shambulio la risasi.

    Mwigizaji wa filamu za Nollywood, Nigeria, Maurice Sam, amesambaa kwenye vichwa vya habari mtandaoni baada ya taarifa zinazodai kuwa alishambuliwa kwa risasi jana Februari 13, 2026 akiwa kwenye seti ya filamu yake mpya. Tukio hili lilianza kuchipuka mtandaoni baada ya Mwanaharakati maarufu wa mitandao, Very Dark Man, kuposti picha na madai ya kwamba Mwigizaji huyo alikuwa amejeruhiwa vibaya na alikuwa akifikiria kuondoka Nigeria ili kulinda usalama wake.

    Ripoti kutoka tovuti ya Latest Nigerian News inaeleza kuwa baadhi ya picha zilizosambazwa mtandaoni zinaonyesha Gari lililoharibiwa na alama za risasi, jambo lililoashiria hatari kubwa aliyokabiliana nayo Mwigizaji huyo. Mada hii iliibua mjadala mkali miongoni mwa mashabiki, wadau wa filamu, na Watumiaji wa mitandao ya kijamii, huku wengi wakihoji ni nini hasa kilichosababisha tukio hili na kuzingatia juhudi za Maurice Sam kujijenga kibiashara na kupata nafasi kubwa ndani ya tasnia ya Nollywood.

    Mchambuzi mmoja wa tasnia ya filamu alisema: “Ni jambo linalotia wasiwasi kuona msanii chipukizi akikabiliwa na tukio la aina hii. Inaleta mjadala juu ya usalama wa wasanii na hali ya kazi kwenye tasnia ya filamu nchini Nigeria.”

    Hata hivyo, ripoti hizo pia zinaonyesha wazi kuwa hakuna uthibitisho rasmi kutoka kwa Mwigizaji, Polisi, au vyombo vya habari vikuu. Taarifa hizi zinazozagaa zinatokana zaidi na mitandao ya kijamii, na bado hazina uthibitisho wa moja kwa moja wa jeraha lolote lililopatikana.

    Kwa sasa, Maurice Sam yupo salama, ingawa duru zinaeleza kuwa tukio hili limemuathiri kisaikolojia kiasi cha kuanza kufikiria kuachana na uigizaji na kuwekeza katika shughuli nyingine za kibiashara. Tukio hili limeibua mjadala wa kimataifa kuhusu hatari zinazoweza kutokea kwa Wasanii chipukizi, huku wadau wa tasnia wakihimiza tahadhari na uangalizi zaidi kwenye seti za filamu.

    Toa maoni yako
    #Filamu
    #Habari
    Mwigizaji wa Nollywood Maurice Sam, mtandaoni yachafukwa baada ya shambulio la risasi. Mwigizaji wa filamu za Nollywood, Nigeria, Maurice Sam, amesambaa kwenye vichwa vya habari mtandaoni baada ya taarifa zinazodai kuwa alishambuliwa kwa risasi jana Februari 13, 2026 akiwa kwenye seti ya filamu yake mpya. Tukio hili lilianza kuchipuka mtandaoni baada ya Mwanaharakati maarufu wa mitandao, Very Dark Man, kuposti picha na madai ya kwamba Mwigizaji huyo alikuwa amejeruhiwa vibaya na alikuwa akifikiria kuondoka Nigeria ili kulinda usalama wake. Ripoti kutoka tovuti ya Latest Nigerian News inaeleza kuwa baadhi ya picha zilizosambazwa mtandaoni zinaonyesha Gari lililoharibiwa na alama za risasi, jambo lililoashiria hatari kubwa aliyokabiliana nayo Mwigizaji huyo. Mada hii iliibua mjadala mkali miongoni mwa mashabiki, wadau wa filamu, na Watumiaji wa mitandao ya kijamii, huku wengi wakihoji ni nini hasa kilichosababisha tukio hili na kuzingatia juhudi za Maurice Sam kujijenga kibiashara na kupata nafasi kubwa ndani ya tasnia ya Nollywood. Mchambuzi mmoja wa tasnia ya filamu alisema: “Ni jambo linalotia wasiwasi kuona msanii chipukizi akikabiliwa na tukio la aina hii. Inaleta mjadala juu ya usalama wa wasanii na hali ya kazi kwenye tasnia ya filamu nchini Nigeria.” Hata hivyo, ripoti hizo pia zinaonyesha wazi kuwa hakuna uthibitisho rasmi kutoka kwa Mwigizaji, Polisi, au vyombo vya habari vikuu. Taarifa hizi zinazozagaa zinatokana zaidi na mitandao ya kijamii, na bado hazina uthibitisho wa moja kwa moja wa jeraha lolote lililopatikana. Kwa sasa, Maurice Sam yupo salama, ingawa duru zinaeleza kuwa tukio hili limemuathiri kisaikolojia kiasi cha kuanza kufikiria kuachana na uigizaji na kuwekeza katika shughuli nyingine za kibiashara. Tukio hili limeibua mjadala wa kimataifa kuhusu hatari zinazoweza kutokea kwa Wasanii chipukizi, huku wadau wa tasnia wakihimiza tahadhari na uangalizi zaidi kwenye seti za filamu. Toa maoni yako #Filamu #Habari
    0 Commenti 0 condivisioni 12 Views
  • Rushaynah afunguka: Bado anamtamani Khalid Aucho.

    Mwigizaji wa filamu na Mwanamitandao maarufu Tanzania, Rushaynah, ambaye ni Mke wa zamani wa Diwani wa Kariakoo, Haji Manara, amefunguka kuhusu hisia zake za mapenzi na Mchezaji wa Singida Big Star, Khalid Aucho.

    Katika mahojiano ya hivi karibuni, Rushaynah ameeleza wazi kuwa bado anamtamani Aucho, huku akibainisha mvuto wake kwa Mchezaji huyo: "Aucho ni Mwanaume mwenye mvuto sana ananivutia sana nahitaji Mwanaume kama yeye, Hata kama ana Mwanamke lakini kwangu bado ana-nafasi."

    Kwa maneno haya, Rushaynah anaonyesha wazi kuwa ingawa Aucho ana uhusiano mwingine, kwake bado bado kuna nafasi ya hisia. Hii imemfanya Mwigizaji huyo kushiriki hadhira yake, hisia za ndani, jambo ambalo limevutia mashabiki wengi mitandaoni.

    Toa maoni yako
    Rushaynah afunguka: Bado anamtamani Khalid Aucho. Mwigizaji wa filamu na Mwanamitandao maarufu Tanzania, Rushaynah, ambaye ni Mke wa zamani wa Diwani wa Kariakoo, Haji Manara, amefunguka kuhusu hisia zake za mapenzi na Mchezaji wa Singida Big Star, Khalid Aucho. Katika mahojiano ya hivi karibuni, Rushaynah ameeleza wazi kuwa bado anamtamani Aucho, huku akibainisha mvuto wake kwa Mchezaji huyo: "Aucho ni Mwanaume mwenye mvuto sana ananivutia sana nahitaji Mwanaume kama yeye, Hata kama ana Mwanamke lakini kwangu bado ana-nafasi." Kwa maneno haya, Rushaynah anaonyesha wazi kuwa ingawa Aucho ana uhusiano mwingine, kwake bado bado kuna nafasi ya hisia. Hii imemfanya Mwigizaji huyo kushiriki hadhira yake, hisia za ndani, jambo ambalo limevutia mashabiki wengi mitandaoni. Toa maoni yako
    0 Commenti 0 condivisioni 71 Views
  • Grace Vevo afichua gharama zake za wiki: “Natumiwa zaidi ya milioni moja na nusu kwa matumizi madogo madogo”.

    Staa wa filamu anayefanya vizuri kwenye tamthilia maarufu ya Big Boss 2, Grace Vevo, amefunguka na kuweka wazi kiwango cha gharama anachotumia katika maisha yake ya kila siku, hali iliyozua gumzo miongoni mwa mashabiki na wadau wa burudani.

    Akizungumza hivi karibuni, Grace Vevo amesema kuwa kwa muda wa wiki moja tu, matumizi yake madogo madogo huzidi Shilingi milioni moja na nusu (Tsh. 1,500,000). Kauli hiyo imeonyesha wazi mtindo wake wa maisha pamoja na gharama zinazokuja sambamba na umaarufu alionao katika tasnia ya filamu na tamthilia.

    “Mimi ni mwanamke wa gharama sana, kwa wiki moja natumia zaidi ya Milioni Moja na nusu kwa vitu vidogo vidogo,” amesema Grace Vevo.

    Kauli hiyo imewafanya wengi kujadili kwa mapana suala la gharama za maisha kwa wasanii wakubwa, huku wengine wakimpongeza kwa kuwa mkweli kuhusu maisha yake halisi, na wengine wakiona ni ishara ya changamoto za kudumisha hadhi na muonekano katika tasnia ya burudani.

    Grace Vevo anaendelea kuwa miongoni mwa Waigizaji wanaofuatiliwa kwa karibu, si tu kwa kipaji chake katika Big Boss 2, bali pia kwa maisha yake binafsi yanayoendelea kuwavutia mashabiki wengi.
    Grace Vevo afichua gharama zake za wiki: “Natumiwa zaidi ya milioni moja na nusu kwa matumizi madogo madogo”. Staa wa filamu anayefanya vizuri kwenye tamthilia maarufu ya Big Boss 2, Grace Vevo, amefunguka na kuweka wazi kiwango cha gharama anachotumia katika maisha yake ya kila siku, hali iliyozua gumzo miongoni mwa mashabiki na wadau wa burudani. Akizungumza hivi karibuni, Grace Vevo amesema kuwa kwa muda wa wiki moja tu, matumizi yake madogo madogo huzidi Shilingi milioni moja na nusu (Tsh. 1,500,000). Kauli hiyo imeonyesha wazi mtindo wake wa maisha pamoja na gharama zinazokuja sambamba na umaarufu alionao katika tasnia ya filamu na tamthilia. “Mimi ni mwanamke wa gharama sana, kwa wiki moja natumia zaidi ya Milioni Moja na nusu kwa vitu vidogo vidogo,” amesema Grace Vevo. Kauli hiyo imewafanya wengi kujadili kwa mapana suala la gharama za maisha kwa wasanii wakubwa, huku wengine wakimpongeza kwa kuwa mkweli kuhusu maisha yake halisi, na wengine wakiona ni ishara ya changamoto za kudumisha hadhi na muonekano katika tasnia ya burudani. Grace Vevo anaendelea kuwa miongoni mwa Waigizaji wanaofuatiliwa kwa karibu, si tu kwa kipaji chake katika Big Boss 2, bali pia kwa maisha yake binafsi yanayoendelea kuwavutia mashabiki wengi.
    0 Commenti 0 condivisioni 86 Views
  • Vurugu mitandaoni! Ned Nwoko amvaa Regina Daniels, asema "ameharibu familia yetu".

    Mitandao ya kijamii imewaka moto kufuatia tuhuma nzito zilizotolewa na Bilionea na mwanasiasa mashuhuri kutoka Nigeria, Prince Ned Nwoko, dhidi ya Mke wake, Mwigizaji maarufu wa filamu za Nigeria (Nollywood) Regina Daniels. Kupitia chapisho la video kwenye ukurasa wake wa Instagram, Nwoko amemshutumu Regina kwa kile alichokiita "vurugu za kupindukia" pamoja na matumizi mabaya ya dawa za kulevya na pombe.

    Katika maneno yake, Ned aliandika: “Hakuwa hivi mwanzo… kile kinachotokea sasa kimeharibu kabisa utulivu wa familia yetu.”

    Nwoko alieleza kuwa ndani ya saa 48, Regina alifanya fujo kubwa nyumbani kwao akiwapiga Wafanyakazi watatu wa ndani, kuharibu mali, na kusababisha uharibifu mkubwa bila sababu ya msingi.

    Kwa mujibu wa chapisho hilo la Instagram: “Nimetoa masharti ya wazi kwake. Lazima akubali kwenda kwenye tiba ya kuacha dawa, iwe ndani au nje ya Nchi. Vinginevyo, naogopa kwa usalama wake.” - Prince Ned Nwoko.

    Katika tuhuma hizo, Ned alimtaja mtu aitwaye Sammy kama Muuzaji mkuu wa dawa kwa Regina, huku pia akilitaja jina la Ann, akisema anahusika katika kile alichokiita “mzunguko wa maovu.”

    Tukio hili limetikisa jamii ya mtandaoni, huku baadhi ya mashabiki wakionesha mshangao, wengine wakimtetea Regina, na wengi wakitaka ukweli wa kina juu ya maisha ya kifahari ya wawili hao.

    Je, hii ni drama ya ndoa ya Mastaa au kuna jambo kubwa zaidi nyuma ya pazia?
    Vurugu mitandaoni! Ned Nwoko amvaa Regina Daniels, asema "ameharibu familia yetu". Mitandao ya kijamii imewaka moto kufuatia tuhuma nzito zilizotolewa na Bilionea na mwanasiasa mashuhuri kutoka Nigeria, Prince Ned Nwoko, dhidi ya Mke wake, Mwigizaji maarufu wa filamu za Nigeria (Nollywood) Regina Daniels. Kupitia chapisho la video kwenye ukurasa wake wa Instagram, Nwoko amemshutumu Regina kwa kile alichokiita "vurugu za kupindukia" pamoja na matumizi mabaya ya dawa za kulevya na pombe. Katika maneno yake, Ned aliandika: “Hakuwa hivi mwanzo… kile kinachotokea sasa kimeharibu kabisa utulivu wa familia yetu.” Nwoko alieleza kuwa ndani ya saa 48, Regina alifanya fujo kubwa nyumbani kwao akiwapiga Wafanyakazi watatu wa ndani, kuharibu mali, na kusababisha uharibifu mkubwa bila sababu ya msingi. Kwa mujibu wa chapisho hilo la Instagram: “Nimetoa masharti ya wazi kwake. Lazima akubali kwenda kwenye tiba ya kuacha dawa, iwe ndani au nje ya Nchi. Vinginevyo, naogopa kwa usalama wake.” - Prince Ned Nwoko. Katika tuhuma hizo, Ned alimtaja mtu aitwaye Sammy kama Muuzaji mkuu wa dawa kwa Regina, huku pia akilitaja jina la Ann, akisema anahusika katika kile alichokiita “mzunguko wa maovu.” Tukio hili limetikisa jamii ya mtandaoni, huku baadhi ya mashabiki wakionesha mshangao, wengine wakimtetea Regina, na wengi wakitaka ukweli wa kina juu ya maisha ya kifahari ya wawili hao. Je, hii ni drama ya ndoa ya Mastaa au kuna jambo kubwa zaidi nyuma ya pazia?
    0 Commenti 0 condivisioni 2K Views
  • Muigizaji wa filamu kutoka Nchini Korea Kusini , O Yeong Su, ambaye alitamba kwenye Tamthilia ya "Spuid Game" katika uigizaji wake kama "Player namba 001", amehukumiwa kifungo cha mwaka mmoja Jela kwa kosa la unyanyasaji wa kingono katika tukio analilolifanya mwaka 2017.

    Muigizaji huyo mwenye umri wa miaka 80 kwa sasa, alipatikana na hatia ya kumnyanyasa kingono Mwanamke mdogo wa kikundi chake cha maigizo kwa kumlazimisha kwa nguvu kufanya nae mapenzi huku akimbusu bila ridhaa yake karibu na Nyumba yake.

    Hata hivyo, O Yeong Su amekanusha mashtaka hayo na kusema kuwa hana hatia. Amehukumiwa kifungo cha mwaka mmoja jela baada ya waendesha mashtaka Tawi la Seongnam la Mahakama ya Wilaya ya Suwon kudai kwamba alitumia vibaya mamlaka yake kama Mwigizaji Mkuu anayeheshimika dhidi ya Mwenzake.

    Mwigizaji huyo bado ameendelea kukanusha mashtaka hayo na amekata rufaa tena huku rufani yake ikitarajiwa kusikilizwa kwa mara ya mwisho Juni 3, 2025.

    Toa maoni yako
    Muigizaji wa filamu kutoka Nchini Korea Kusini 🇰🇷, O Yeong Su, ambaye alitamba kwenye Tamthilia ya "Spuid Game" katika uigizaji wake kama "Player namba 001", amehukumiwa kifungo cha mwaka mmoja Jela kwa kosa la unyanyasaji wa kingono katika tukio analilolifanya mwaka 2017. Muigizaji huyo mwenye umri wa miaka 80 kwa sasa, alipatikana na hatia ya kumnyanyasa kingono Mwanamke mdogo wa kikundi chake cha maigizo kwa kumlazimisha kwa nguvu kufanya nae mapenzi huku akimbusu bila ridhaa yake karibu na Nyumba yake. Hata hivyo, O Yeong Su amekanusha mashtaka hayo na kusema kuwa hana hatia. Amehukumiwa kifungo cha mwaka mmoja jela baada ya waendesha mashtaka Tawi la Seongnam la Mahakama ya Wilaya ya Suwon kudai kwamba alitumia vibaya mamlaka yake kama Mwigizaji Mkuu anayeheshimika dhidi ya Mwenzake. Mwigizaji huyo bado ameendelea kukanusha mashtaka hayo na amekata rufaa tena huku rufani yake ikitarajiwa kusikilizwa kwa mara ya mwisho Juni 3, 2025. Toa maoni yako
    Like
    1
    0 Commenti 0 condivisioni 1K Views
  • kwa mujibu wa Jarida la Forbes, hii hapa orodha ya Jamii ya Watu Weusi wenye utajiri mkubwa Duniani kwa Mwaka 2025 ambapo wanakadariwa kumiliki utajiri wa dola bilioni 96.2. Wengi wao utajiri wao unatokana sekta za teknolojia, fedha, nishati na burudani, huku Mfanyabiashara Aliko Dangote wa Nigeria akiongoza kwa kuwa na utajiri wa dola bilioni 23.9.

    1. Aliko Dangote (Nigeria) : $23.9B (Saruji, sukari)
    2. David Steward (Marekani) : $11.4B (Teknolojia)
    3. Robert F. Smith (Marekani) : $10.8B (Uwekezaji binafsi)

    4. Alexander Karp (Marekani) : $8.4B (Programu za uchambuzi wa data)
    5. Mike Adenuga (Nigeria) : $6.8B (Mawasiliano, mafuta)
    6. Abdulsamad Rabiu (Nigeria) : $5.1B (Saruji, sukari)

    7. Michael Jordan (Marekani) : $3.5B (Michezo, matangazo)
    8. Patrice Motsepe (Afrika Kusini) : $3B (Madini)
    9. Oprah Winfrey (Marekani) : $3B (Runinga)

    10. Jay-Z (Marekani) : $2.5B (Muziki, biashara)
    11. Adebayo Ogunlesi (Marekani) :$2.2B (Uwekezaji binafsi)
    12. Magic Johnson (Marekani) : $1.5B (Michezo, uwekezaji)

    13. Femi Otedola (Nigeria) : $1.5B (Nishati)
    14. Tope Awotona (Marekani) : $1.4B (Programu "Calendly")
    15. Tyler Perry (Marekani) : $1.4B (Filamu, Runinga)

    16. Tiger Woods (Marekani) : $1.4B (Gofu)
    17. Rihanna (Barbados) : $1.4B (Muziki, urembo)
    18. Mo Ibrahim (Uingereza) : $1.3B (Mawasiliano)

    19. LeBron James (Marekani) : $1.3B (Kikapu)
    20. Strive Masiyiwa (Zimbabwe) : $1.2B (Mawasiliano)
    21. Michael Lee-Chin (Canada) : $1.1B (Uwekezaji wa fedha)

    22. Herriot Tabuteau (Marekani) : $1.1B (Afya)
    23. Sheila Johnson (Marekani) : $1B (Runinga, hoteli)

    kwa mujibu wa Jarida la Forbes, hii hapa orodha ya Jamii ya Watu Weusi wenye utajiri mkubwa Duniani kwa Mwaka 2025 ambapo wanakadariwa kumiliki utajiri wa dola bilioni 96.2. Wengi wao utajiri wao unatokana sekta za teknolojia, fedha, nishati na burudani, huku Mfanyabiashara Aliko Dangote wa Nigeria 🇳🇬 akiongoza kwa kuwa na utajiri wa dola bilioni 23.9. 1. Aliko Dangote (Nigeria) : $23.9B (Saruji, sukari) 2. David Steward (Marekani) : $11.4B (Teknolojia) 3. Robert F. Smith (Marekani) : $10.8B (Uwekezaji binafsi) 4. Alexander Karp (Marekani) : $8.4B (Programu za uchambuzi wa data) 5. Mike Adenuga (Nigeria) : $6.8B (Mawasiliano, mafuta) 6. Abdulsamad Rabiu (Nigeria) : $5.1B (Saruji, sukari) 7. Michael Jordan (Marekani) : $3.5B (Michezo, matangazo) 8. Patrice Motsepe (Afrika Kusini) : $3B (Madini) 9. Oprah Winfrey (Marekani) : $3B (Runinga) 10. Jay-Z (Marekani) : $2.5B (Muziki, biashara) 11. Adebayo Ogunlesi (Marekani) :$2.2B (Uwekezaji binafsi) 12. Magic Johnson (Marekani) : $1.5B (Michezo, uwekezaji) 13. Femi Otedola (Nigeria) : $1.5B (Nishati) 14. Tope Awotona (Marekani) : $1.4B (Programu "Calendly") 15. Tyler Perry (Marekani) : $1.4B (Filamu, Runinga) 16. Tiger Woods (Marekani) : $1.4B (Gofu) 17. Rihanna (Barbados) : $1.4B (Muziki, urembo) 18. Mo Ibrahim (Uingereza) : $1.3B (Mawasiliano) 19. LeBron James (Marekani) : $1.3B (Kikapu) 20. Strive Masiyiwa (Zimbabwe) : $1.2B (Mawasiliano) 21. Michael Lee-Chin (Canada) : $1.1B (Uwekezaji wa fedha) 22. Herriot Tabuteau (Marekani) : $1.1B (Afya) 23. Sheila Johnson (Marekani) : $1B (Runinga, hoteli)
    0 Commenti 0 condivisioni 2K Views
  • Amesema Steve Nyerere.

    "Mstafuuu ,,, Ivi Mama Akipenda kwenda kuangalia Dabi,....Pale uwanja wa Taifa pamoja na Watanzania na mashabiki wa Simba na Yanga Si Itapendeza sana,......Naimani Timu zote zitafurahia kuazimisha Miaka 4 Ya Rais wetu Mpendwa kwa Kucheza Dabi,...Maana ndani ya Miaka 4 Ya Mh @samia_suluhu_hassan Soka Limekuwa kivutio kikubwa sana Na Muanko wa Soka umekuwa mkubwa Baada ya Mh Rais kuhakikisha sekta hii Inapiga hatua,......

    Kuazimisha Miaka 4 Ya kipenzi cha Watanzania Dr Samia Suluhu Hassan Dabi halafu mgeni Rasmi Mama Itapendeza Tutajaaaa balaaa,...Apo vipi.,.," - Steve Nyerere, Mwigizaji wa filamu Tanzania.

    Amesema Steve Nyerere. "Mstafuuu ,,, Ivi Mama Akipenda kwenda kuangalia Dabi,....Pale uwanja wa Taifa pamoja na Watanzania na mashabiki wa Simba na Yanga Si Itapendeza sana,......Naimani Timu zote zitafurahia kuazimisha Miaka 4 Ya Rais wetu Mpendwa kwa Kucheza Dabi,...Maana ndani ya Miaka 4 Ya Mh @samia_suluhu_hassan Soka Limekuwa kivutio kikubwa sana Na Muanko wa Soka umekuwa mkubwa Baada ya Mh Rais kuhakikisha sekta hii Inapiga hatua,...... Kuazimisha Miaka 4 Ya kipenzi cha Watanzania Dr Samia Suluhu Hassan Dabi halafu mgeni Rasmi Mama Itapendeza Tutajaaaa balaaa,...Apo vipi.,.," - Steve Nyerere, Mwigizaji wa filamu Tanzania.
    0 Commenti 0 condivisioni 1K Views
  • "Najisikia vibaya namna watu wanavyoniona na kuanza kuniita Yesu, wanafikia hata kutundika picha zangu katika nyumba zao, mimi ni mwigizaji tu, mimi ni mtu" - Jonathan Roumie(50), mwigizaji wa Marekani

    Aidha, Jonathan Roumie katika mahojiano amesema maisha yake binafsi alikuwa na hali mbaya kiuchumi hakuwa na uhakika siku inayofuata atakula nini, alikuwa mwigizaji ila kiuchumi alikuwa bado hajafanikiwa. Baada ya mambo kuzidi kuwa magumu siku moja ni kama alikuwa anamuomba Mungu kuhusu hali anayopitia ili mambo yake yakae sawa

    Baada ya miezi kama mitatu ndio akapata nafasi ya kuigiza kama Yesu katika series ya "The Chosen" iliyoanza kuoneshwa 2017 ambayo imejipatia umaarufu mkubwa sana hadi sasa imetazamwa na watu zaidi ya milioni 250 na misimu mipya inafuata huku ikipongezwa kwa kinachoonekana kuigizwa

    Umaarufu wa uhusika wake kama Yesu umempa umaarufu mkubwa na fursa nyingi ikiwemo katika mikutano na makongamano makubwa ya kidini na app za dini ya kikiristo

    Jonathan ambaye ni mkatoliki, alipoulizwa na New York Times, je ni tukio gani gumu analokumbuka ambalo alishakutana nalo baada ya kuigiza kama Yesu, amejibu kwa kusema kuna kipindi alikuwa katika mkutano kwenye uwanja wenye watu takribani 40,000 baadaye alishuka stejini akaenda kwenye chumba fulani uwanjani hapo, mmoja wa walinzi alikuja akamwambia nje kuna mwanamke ana mtoto kwenye kiti cha magurudumu anaomba kusalimiana na wewe

    Jonathan alitoka akaonana na mwanamke husika na mwanae ambaye kwa ufupi alieleza jinsi Yesu alivyoponya mtu katika hiyo series ya "The Chosen" na kusema angependa mwanae pia apone yaani akimtaka Jonathan amponye mtoto wake. Ilibidi Jonathan amueleze ukweli kwamba yeye sio mponyaji wala mhubiri bali ni mwigizaji tu.

    Jonathan akamueleza wafanye maombi wote ilichukua kama dakika moja, walipomaliza maombi wakafurahi na kushukuru kisha Jonathan akarudi alipokuwa huku akitokwa na machozi akihisi amewaangusha matarajio waliyokuwa nayo kwake ila amesema ni bora waujue ukweli kuwa yeye sio Yesu wala mponyaji bali ni mwigizaji tu

    Ukiacha hayo ya uhusika wake wa Yesu na dini, Jonathan Roumie amegusia pia kwamba alishafika Tanzania na Rwanda sababu kuna watoto kadhaa wanaoishi katika mazingira magumu huwa anawasaidia na familia zao

    Jonathan Roumie pia ameweka wazi kwamba anatamani watu pia wawe wanamuona katika nyuma ya pazia(behind the scene) anayopitia katika kujiandaa na uigizaji wake kama Yesu ili watu wengine waelewe wajue kumtofautisha katika maisha halisi na kisanaa

    KUMBUKA, zipo filamu nyingine miaka ya nyuma kuhusu Yesu zilizohusisha waigizaji wengine kabla ya sasa Jonathan Roumie kupata umaarufu na uhusika wa Yesu katika series maarufu ya "The Chosen"
    (Swahili Word)

    "Najisikia vibaya namna watu wanavyoniona na kuanza kuniita Yesu, wanafikia hata kutundika picha zangu katika nyumba zao, mimi ni mwigizaji tu, mimi ni mtu" - Jonathan Roumie(50), mwigizaji wa Marekani Aidha, Jonathan Roumie katika mahojiano amesema maisha yake binafsi alikuwa na hali mbaya kiuchumi hakuwa na uhakika siku inayofuata atakula nini, alikuwa mwigizaji ila kiuchumi alikuwa bado hajafanikiwa. Baada ya mambo kuzidi kuwa magumu siku moja ni kama alikuwa anamuomba Mungu kuhusu hali anayopitia ili mambo yake yakae sawa Baada ya miezi kama mitatu ndio akapata nafasi ya kuigiza kama Yesu katika series ya "The Chosen" iliyoanza kuoneshwa 2017 ambayo imejipatia umaarufu mkubwa sana hadi sasa imetazamwa na watu zaidi ya milioni 250 na misimu mipya inafuata huku ikipongezwa kwa kinachoonekana kuigizwa Umaarufu wa uhusika wake kama Yesu umempa umaarufu mkubwa na fursa nyingi ikiwemo katika mikutano na makongamano makubwa ya kidini na app za dini ya kikiristo Jonathan ambaye ni mkatoliki, alipoulizwa na New York Times, je ni tukio gani gumu analokumbuka ambalo alishakutana nalo baada ya kuigiza kama Yesu, amejibu kwa kusema kuna kipindi alikuwa katika mkutano kwenye uwanja wenye watu takribani 40,000 baadaye alishuka stejini akaenda kwenye chumba fulani uwanjani hapo, mmoja wa walinzi alikuja akamwambia nje kuna mwanamke ana mtoto kwenye kiti cha magurudumu anaomba kusalimiana na wewe Jonathan alitoka akaonana na mwanamke husika na mwanae ambaye kwa ufupi alieleza jinsi Yesu alivyoponya mtu katika hiyo series ya "The Chosen" na kusema angependa mwanae pia apone yaani akimtaka Jonathan amponye mtoto wake. Ilibidi Jonathan amueleze ukweli kwamba yeye sio mponyaji wala mhubiri bali ni mwigizaji tu. Jonathan akamueleza wafanye maombi wote ilichukua kama dakika moja, walipomaliza maombi wakafurahi na kushukuru kisha Jonathan akarudi alipokuwa huku akitokwa na machozi akihisi amewaangusha matarajio waliyokuwa nayo kwake ila amesema ni bora waujue ukweli kuwa yeye sio Yesu wala mponyaji bali ni mwigizaji tu Ukiacha hayo ya uhusika wake wa Yesu na dini, Jonathan Roumie amegusia pia kwamba alishafika Tanzania na Rwanda sababu kuna watoto kadhaa wanaoishi katika mazingira magumu huwa anawasaidia na familia zao Jonathan Roumie pia ameweka wazi kwamba anatamani watu pia wawe wanamuona katika nyuma ya pazia(behind the scene) anayopitia katika kujiandaa na uigizaji wake kama Yesu ili watu wengine waelewe wajue kumtofautisha katika maisha halisi na kisanaa KUMBUKA, zipo filamu nyingine miaka ya nyuma kuhusu Yesu zilizohusisha waigizaji wengine kabla ya sasa Jonathan Roumie kupata umaarufu na uhusika wa Yesu katika series maarufu ya "The Chosen" (Swahili Word)
    Love
    1
    0 Commenti 0 condivisioni 2K Views
  • Steve Nyerere agusia sakata la Nicole

    "Mstafuuu,.....Nani mkamilifu katika hii Ardhi Ya Mwenyezi Mungu,..

    Napokea sms Simu swala la Nicole Toka juzi kulia na kushoto lakini nikasema Mungu nitangulie nami nione Mwanga kwenye hili,....Ni Ukweli Usio pingika dada kapuyanga Sana Tena sana Ana Makosa Na Ana Kosa la kujibu, lakini nani mkamilifu,....

    Nicole Ana makosa na kibaya zaidi ni kwenda kuchangisha Watu wenye kujipambania kuitafuta kesho yao, Na kibaya zaidi walikuamini kutokana na bland yake wakiamini kuna matokeo sahihi kupitia Nicole,....

    Nicole ni mtu mzima na mwenye akili timamu Alikuwa Anafanya kitu anacho kijua na kujua matokeo na mwisho wa Matokeo lakini tukienda mbali zaidi limesha tokea naye ni Binadamu,..Sipo hapa kumtetea Mwalifu lakini naandika hapa kujaribu kuona haki ya walio fanyiwa ujinga huu wanaipataje,...Je Nicole kukaaa ndani haki ya wadai Itapatikana Maana siku ya Mwisho Nicole Anatakiwa kuwarudishia FEDHA zao wote walio guswa na yeye Anarudishaje Atajua yeye lakini Akiwa nje kwa dhamana na masharti yenye tija basi Anaweza kumaliza jambo hili.,.

    Lakini Ifike mahara hii michezo ya Magroup Inayogusa FEDHA naomba sana kuwe na Utaratibu wa kumsajiri kijumbe kitambulisho chake na wanachama anao wachangisha waridhie kwa maandishi kuwa wamekubaliana kuanzisha group la kusaidia hii itasaidia sana,.lakini sio mtu anatoka tu huko anaanzisha group mara michango sio sawa.,,.

    Niombe sasa Ni wakati wa kusimama na Nicole Tusiangalie kafanya nini Tuangalie Dhamana yake na jinsi ya kumsaidia,....Haijalishi kala mzigo na nani lakini bado ni mwenzetu,....Anapitia kipindi kibaya sana Ambacho Anahitaji faraja,....

    Tusimame kumuombea Dhamana Tunajua na kutambua sheria na kuheshimu sheria kwenye Taifa letu,......

    Niombe Si muda wa kuliangalia kosa ni Muda wa kulitibu kosa Nani mkamilifu hapa Duniani,..Mimi Binafsi kama STEVEN MENGELE (NYERERE) NIPO TAYARI KUMSAIDIA NICOLE ,..KUTOKA NDANI KWA KUFATA TARATIBU ZOTE,..NA AKIPATA DHAMANA BASI ATAMBUE KULIPA KILA JASHO LA MCHANGAJI KURUDISHIWA NA MAISHA KUENDELEA,....HAKUNA MWANADAMU AMBAYE MKAMILIFU HAPA DUNIANI,...." - Steve Nyerere, Mwigizaji wa filamu Tanzania.

    Steve Nyerere agusia sakata la Nicole "Mstafuuu,.....Nani mkamilifu katika hii Ardhi Ya Mwenyezi Mungu,.. Napokea sms Simu swala la Nicole Toka juzi kulia na kushoto lakini nikasema Mungu nitangulie nami nione Mwanga kwenye hili,....Ni Ukweli Usio pingika dada kapuyanga Sana Tena sana Ana Makosa Na Ana Kosa la kujibu, lakini nani mkamilifu,.... Nicole Ana makosa na kibaya zaidi ni kwenda kuchangisha Watu wenye kujipambania kuitafuta kesho yao, Na kibaya zaidi walikuamini kutokana na bland yake wakiamini kuna matokeo sahihi kupitia Nicole,.... Nicole ni mtu mzima na mwenye akili timamu Alikuwa Anafanya kitu anacho kijua na kujua matokeo na mwisho wa Matokeo lakini tukienda mbali zaidi limesha tokea naye ni Binadamu,..Sipo hapa kumtetea Mwalifu lakini naandika hapa kujaribu kuona haki ya walio fanyiwa ujinga huu wanaipataje,...Je Nicole kukaaa ndani haki ya wadai Itapatikana Maana siku ya Mwisho Nicole Anatakiwa kuwarudishia FEDHA zao wote walio guswa na yeye Anarudishaje Atajua yeye lakini Akiwa nje kwa dhamana na masharti yenye tija basi Anaweza kumaliza jambo hili.,. Lakini Ifike mahara hii michezo ya Magroup Inayogusa FEDHA naomba sana kuwe na Utaratibu wa kumsajiri kijumbe kitambulisho chake na wanachama anao wachangisha waridhie kwa maandishi kuwa wamekubaliana kuanzisha group la kusaidia hii itasaidia sana,.lakini sio mtu anatoka tu huko anaanzisha group mara michango sio sawa.,,. Niombe sasa Ni wakati wa kusimama na Nicole Tusiangalie kafanya nini Tuangalie Dhamana yake na jinsi ya kumsaidia,....Haijalishi kala mzigo na nani lakini bado ni mwenzetu,....Anapitia kipindi kibaya sana Ambacho Anahitaji faraja,.... Tusimame kumuombea Dhamana Tunajua na kutambua sheria na kuheshimu sheria kwenye Taifa letu,...... Niombe Si muda wa kuliangalia kosa ni Muda wa kulitibu kosa Nani mkamilifu hapa Duniani,..Mimi Binafsi kama STEVEN MENGELE (NYERERE) NIPO TAYARI KUMSAIDIA NICOLE ,..KUTOKA NDANI KWA KUFATA TARATIBU ZOTE,..NA AKIPATA DHAMANA BASI ATAMBUE KULIPA KILA JASHO LA MCHANGAJI KURUDISHIWA NA MAISHA KUENDELEA,....HAKUNA MWANADAMU AMBAYE MKAMILIFU HAPA DUNIANI,...." - Steve Nyerere, Mwigizaji wa filamu Tanzania.
    0 Commenti 0 condivisioni 1K Views
  • "Kwa kipindi cha hivi karibuni kwenye maisha yangu nimekuwa nikipokea maswali mengi kutoka kwa jamii na kwenu nyinyi waandishi wa habari kwamba ni nini siri ya mafanikio yangu, nini chanzo cha pesa zangu. Leo naomba nizungumze ukweli kwamba mnamo mwaka 2018 nilifanya tafiti kutaka kujua ni kitu gani ama ni biashara gani nitakayoifanya ambayo itakuwa kama biashara yangu ya pili ya kuniingizia pesa"

    "Nilifanya utafiti kwenye biashara nyingi na hatimae mawazo yangu yalisimama kwenye kilimo, nilikuja kugundua kilimo ndicho kitakachonitoa, nikawekeza nguvu na mtaji wangu huko hatimae nikaanza kupata matunda ambayo pesa zake ndio hizi mnazoona nakula bata kila uchao, ndio maana nimekuja na kampeni yangu ya kuwasaidia wanawake kujikwamua kupitia kilimo kwasababu nimeona huko kuna pesa nyingi"- Irene Uwoya, Mwigizaji wa filamu Tanzania na Mchungaji.

    "Kwa kipindi cha hivi karibuni kwenye maisha yangu nimekuwa nikipokea maswali mengi kutoka kwa jamii na kwenu nyinyi waandishi wa habari kwamba ni nini siri ya mafanikio yangu, nini chanzo cha pesa zangu. Leo naomba nizungumze ukweli kwamba mnamo mwaka 2018 nilifanya tafiti kutaka kujua ni kitu gani ama ni biashara gani nitakayoifanya ambayo itakuwa kama biashara yangu ya pili ya kuniingizia pesa" "Nilifanya utafiti kwenye biashara nyingi na hatimae mawazo yangu yalisimama kwenye kilimo, nilikuja kugundua kilimo ndicho kitakachonitoa, nikawekeza nguvu na mtaji wangu huko hatimae nikaanza kupata matunda ambayo pesa zake ndio hizi mnazoona nakula bata kila uchao, ndio maana nimekuja na kampeni yangu ya kuwasaidia wanawake kujikwamua kupitia kilimo kwasababu nimeona huko kuna pesa nyingi"- Irene Uwoya, Mwigizaji wa filamu Tanzania na Mchungaji.
    Like
    2
    0 Commenti 0 condivisioni 511 Views
  • "Mimi sasa hivi nimetimiza miaka 35, suala la kupata mtoto nimelikatia tamaa kwasababu nimesubiri mtoto kwa hamu nikiwa binti nimekosa sasa itakuwa vipi kwenye umri huu wa kuelekea uzeeni? Nimejikatia tamaa hata Mungu akinipa mtoto sasa hivi nitampokea lakini aaah!! sasa nitamlea vipi mtoto nitakayempata katika umri huu jamani"

    "Mungu tu alinipangia niishi hivi na silaumu kwasababu huenda ningepata mtoto ningepata shida ndio maana kaamua kuniacha hivihivi. Na huyo mtoto ningempata angependwa mpaka achanganyikiwe, lakini Alhamdulillah nashukuru kwa yote nalea watoto wa dada zangu ba ndugu zangu wengine maana hao ni wangu pia"- Wema Sepetu, Mwigizaji wa filamu Tanzania.

    "Mimi sasa hivi nimetimiza miaka 35, suala la kupata mtoto nimelikatia tamaa kwasababu nimesubiri mtoto kwa hamu nikiwa binti nimekosa sasa itakuwa vipi kwenye umri huu wa kuelekea uzeeni? Nimejikatia tamaa hata Mungu akinipa mtoto sasa hivi nitampokea lakini aaah!! sasa nitamlea vipi mtoto nitakayempata katika umri huu jamani" "Mungu tu alinipangia niishi hivi na silaumu kwasababu huenda ningepata mtoto ningepata shida ndio maana kaamua kuniacha hivihivi. Na huyo mtoto ningempata angependwa mpaka achanganyikiwe, lakini Alhamdulillah nashukuru kwa yote nalea watoto wa dada zangu ba ndugu zangu wengine maana hao ni wangu pia"- Wema Sepetu, Mwigizaji wa filamu Tanzania.
    0 Commenti 0 condivisioni 562 Views
  • #HABARI Moto wa Los Angeles Kabla ya Kutokea

    Siku tatu kabla ya moto mkubwa kutokea Los Angeles, waandaaji wa tuzo maarufu za Global Leaders Awards walikuwa wakijitayarisha kwa hafla yao ya kila mwaka. Tuzo hizi zina lengo la kutambua na kusherehekea mchango wa watu mashuhuri katika nyanja mbalimbali, ikiwemo utunzi na uandaaji wa filamu bora.

    Kwa mara ya kwanza katika historia ya tuzo hizo, waandaaji walimuweka Mungu kama mmoja wa washindani katika kipengele cha "Mchango wa kipekee wa Maisha katika Sanaa". Hili lilizua mjadala mkubwa na hisia tofauti miongoni mwa waliohudhuria hafla hiyo.

    MC wa usiku huo alipochukua kipaza sauti, alitoa kauli iliyozua mjadala:
    "Ni jambo la kushangaza kwamba tumemuweka Mungu katika orodha ya washindani kwa tuzo hii, lakini amekosa kura kabisa. Inaonekana hata Mungu anahitaji kujipanga zaidi kwa ajili ya hafla zijazo."

    Kauli hiyo ilisababisha kicheko kutoka kwa baadhi ya wageni waalikwa, huku wengine wakiwa hawakufurahishwa na utani huo.

    Katika kipengele hicho, wagombea walikuwa:

    1. Cast and Crow - waliopata kura 11

    2. Moms - waliopata kura 3

    3. Mungu - aliyepata kura 0

    Hafla hiyo ya usiku ilimalizika kwa hali ya mchanganyiko wa furaha na maoni ya kukosoa, huku watu wakitafakari zaidi nafasi ya maadili na heshima katika sanaa na burudani.
    N.B, MUNGU HADHIHAKIWI

    #neliudcosiah
    #HABARI Moto wa Los Angeles Kabla ya Kutokea Siku tatu kabla ya moto mkubwa kutokea Los Angeles, waandaaji wa tuzo maarufu za Global Leaders Awards walikuwa wakijitayarisha kwa hafla yao ya kila mwaka. Tuzo hizi zina lengo la kutambua na kusherehekea mchango wa watu mashuhuri katika nyanja mbalimbali, ikiwemo utunzi na uandaaji wa filamu bora. Kwa mara ya kwanza katika historia ya tuzo hizo, waandaaji walimuweka Mungu kama mmoja wa washindani katika kipengele cha "Mchango wa kipekee wa Maisha katika Sanaa". Hili lilizua mjadala mkubwa na hisia tofauti miongoni mwa waliohudhuria hafla hiyo. MC wa usiku huo alipochukua kipaza sauti, alitoa kauli iliyozua mjadala: "Ni jambo la kushangaza kwamba tumemuweka Mungu katika orodha ya washindani kwa tuzo hii, lakini amekosa kura kabisa. Inaonekana hata Mungu anahitaji kujipanga zaidi kwa ajili ya hafla zijazo." Kauli hiyo ilisababisha kicheko kutoka kwa baadhi ya wageni waalikwa, huku wengine wakiwa hawakufurahishwa na utani huo. Katika kipengele hicho, wagombea walikuwa: 1. Cast and Crow - waliopata kura 11 2. Moms - waliopata kura 3 3. Mungu - aliyepata kura 0 Hafla hiyo ya usiku ilimalizika kwa hali ya mchanganyiko wa furaha na maoni ya kukosoa, huku watu wakitafakari zaidi nafasi ya maadili na heshima katika sanaa na burudani. N.B, MUNGU HADHIHAKIWI ✍️ #neliudcosiah
    Like
    Love
    3
    1 Commenti 1 condivisioni 1K Views
  • YAJUE MAENEO AMBAYO HURUHUSIWI KUFIKA KAMWE.

    Katika ulimwengu wa leo tunaoishi tunaweza kufanya vitu vingi vinavyotufurahisha ikiwemo kusafiri kwenda maeneo mbalimbali ulimwenguni kwa malengo mbalimbali mfano kibiashara,kiutalii na hata kwa lengo la kuburudika tu.lakini hayo yote yanaweza kufanyika isipokuwa kwa baadhi ya maeneo,yafuatayo ni maeneo manne (4) ambayo huruhusiwi kufika.

    #01.NORTH SENTINEL ISLAND (KISIWA CHA SENTINEL YA KASKAZINI)
    Kisiwa cha NORTH SENTINEL ni sehemu ya visiwa vya ANDAMAN na NICOBAR vilivyopo kwenye bay ya BENGAL kwenye bahari ya hindi kati ya MYANMAR na INDONESIA.Eneo hili ndipo mahali ambapo wakazi wake hawaruhusu mawasiliano kabisa na ulimwengu ulioendelea/mataifa mengine.
    Kuna visa kadhaa vya kuthibitisha 'marufuku' ya kuingia kisiwani huko kutoka kwa wakazi wake.
    -Mwezi DISEMBA mwaka 2004 tsunami ilipopiga kwenye bahari ya hindi waokoaji walihitaji kusaidia wahanga wa kisiwa hiko lakini haikuwa rahisi kutokana na upinzani waliokutana nao kutoka kwa wakazi wa kisiwa hicho,walijaribu kushusha vyakula wakiwa kwenye helikopta ya jeshi la maji la INDIA kilichotokea ni kwamba moja ya helikopta hizo ilishambuliwa na 'shujaa' mmoja wa kisiwa hiko aliepiga mkuki kwenye helikopta kuonesha kuwa watu hao hawakuhitaji msaada wala mawasiliano na mataifa jirani.
    Kimsingi INDIA ndio inayomiliki kisiwa hicho.
    -Kisa kingine ni cha mwaka 1896 cha mfungwa mmoja alietoroka kutoka kwenye gereza lililopo katika kisiwa cha ANDAMAN ambae alikimbilia kwenye kisiwa hiki,siku chache baadae mwili wake ulikutwa pembezoni mwa bahari ukiwa na alama za kupigwa na mishale na huku koo lake likiwa limekatwa.
    Sijui kama wakazi wa kisiwa hiki wanajua kama kuna nchi inaitwa TANZANIA,shughuli wanazofanya kuendesha maisha yao ni uwindaji,uvuvi pia wanakula matunda na asali.
    Huwezi kuamini kuwa maeneo haya hakuna SIMU wala INTANETI.

    #02.ROOM 39 (CHUMBA NAMBA 39)
    Kwa majina mengine huitwa BUREAU 39 au DIVISION 39 au OFFICE 39,jengo hili lipo nchini KOREA KASKAZINI na linakaliwa na tasisi ya siri ya chama cha KOREA KASKAZINI (KOREAN WORKERS' PARTY) lengo lake ni kuchangia uongezekaji wa fedha za kigeni nchini KOREA KASKAZINI,ROOM 39 inaaminika kuendesha shughuli zote zinazohusiana na uingizwaji wa fedha za kigeni nchini humo na mjini PYONGYANG ikiwa pamoja na mahoteli yaliyopo PYONGYANG na uchimbaji wa madini ya ZINC na DHAHABU. Taasisi ya ROOM 39 inaaminika kumiliki baadhi ya makampuni mafano ZOKWANG TRADING na benki ya TAESONG BANK.
    Tasisi hii iliundwa na KIM IL-SUNG miaka ya 1970,kwa mwaka tasisi hii ya siri inasadikika inaiingizia nchi ya KOREA KASKAZINI mapato ya kati ya milioni $500 (dola za kimarekani) mpaka billioni $1 (dola za kimarekani).
    Vyanzo kadhaa vya nchi za magharibi vinaeleza kuwa taasisi hii inaingiza fedha hizo kwa kuendesha shughuli za kihalifu,mfano ripoti moja ya WASHINGTON POST ilieleza ubadhilifu uliotokea katika sekta ya BIMA duniani na kudai kuwa ulifanywa na serikali ya KOREA KASKAZINI kwa kutumia taasisi yake ya KOREA NATIONAL INSURANCE CORP (KNIC).
    Jengo hili la ROOM 39 hakika huruhusiwi kuingia ndani yake,kutokana na sababu za kiusalama hivyo hutaweza kuwemo ndani yake.

    #03.AREA 51
    Hili ni eneo linalomilkiwa na JESHI LA ANGA LA MAREKANI lipo NEVADA.
    Taarifa nyingi na za uhakika kuhusu mambo yanayofanyika katika eneo hili ni 'highly classified' ila tu kuna nadharia kadhaa zinazoeleza mambo yanayofanyika katika eneo hili baadhi ya nadharia hizo ni;
    >Inaaminika kuwa AREA 51 ni mahali wanapofanya tafiti za teknolojia za viumbe wa sayari nyingine (ALLIEN) ambapo jeshi la anga la marekani limehifadhi masalia ya ndege za viumbe hao zilizopata ajali,na pia wanatengeneza ndege kutokana na teknolojia ya ALLIENS.
    >Inaaminika wanaendesha program/mpango wa kutengeneza silaha za kujilinda za awali yaani STRATEGIC DEFENSE INITIATIVE (SDI) na program za silaha nyingine.
    >Inaaminika kuwa ndani ya eneo hilo wanatengeneza teknolojia itakayoweza ku'control' hali ya hewa.
    >Inaaminika kuwa wanafanya program ya kutengeneza teknolojia ya TIME TRAVEL (uwezo wa kumwezesha mtu kurudi wakati uliopita au kwenda wakati ujao,mfano mtu atoke hivi sasa na asafiri kwenda miaka 50 ijayo) na TELEPORTATION (yaani mtu aweze kusafiri kutoka eneo moja hadi jingine pasina usafiri wowote ule na kwa haraka.nadharia hii imeelezwa kwenye filamu/movie/series ya TOMORROW PEOPLE kama ushawahi kuiona basi hivyo ndivyo watu wanavyo teleport).
    >Inaaminika kuwa pengine wanaendesha shughuli zitakazochangia kuwepo kwa serikali moja duniani (ONE WORLD GOVERMENT)
    Moja ya mambo yanayoweza kutumika kama ushahidi juu ya nadharia inayohusisha uwepo wa viumbe kutoka sayari nyingine yaani ALLIENS ndani ya AREA 51 ni baadhi ya watu waliowahi kukiri kuwa wafanyakazi wa AREA 51
    **Mmoja wao ni bwana BOB LAZAR ambae mwaka 1989 alisema kuwa alifanya kazi ndani ya AREA 51 SECTOR FOUR (S-4) ambapo eneo hili lipo chini ya ardhi,bwana BOB LAZAR alisema kuwa alipokuwa ndani ya SECTOR FOUR alifanya kazi na ndege ya anga la juu(spacecraft) ya ALLIENS ambayo inashikiliwa na serikali ya MAREKANI ndani ya AREA 51.
    **Documentary moja iitwayo DREAMLAND iliotoka mwaka 1996 ilioongozwa na BRUCE BURGESS ilijumuisha interview aliofanya na mzee wa umri wa miaka 71 ambae ni injinia (mechanical engeneer) aliekiri kuwa alishawahi kuwa muajiriwa aliefanya kazi ndani ya AREA 51 katika miaka ya 1950,alikiri kuwa alifanya kazi kwenye kitu chenye uwezo wa kupaaa angani kilicho mfano wa sahani kiitwacho "FLYING DISK SIMULATOR" alisema kitu hicho mfano wa sahani kubwa kilitokana na ndege ya anga za juu iliopoata ajali na kilitumika kuwafundishia marubani wa jeshi la MAREKANI,pia alikiri kuwa alifanya kazi na kiumbe kutoka sayari nyingine ambae aliitwa "J-ROD".
    **Mwaka 2004 DAN BURISCH alikiri kufanya kazi ndani ya AREA 51 pamoja na ALLIEN aliefahamika kwa jina la "J-ROD"
    Kuingia katika eneo hili kumezuiwa vikali, na wanajeshi wanaolinda eneo hilo wamepewa mamlaka ya kumfyatulia risasi yeyote atakaeingia ambae hana ruhusa ya kuwepo eneo hilo,Hivyo basi katika eneo hili hautaweza kufika labda uwe mfanyikazi wa humu.
    (KWA WALE WANAOCHEZA SANA VIDEO GAMES AU WALE WALIOWAHI KUCHEZA "GTA SAN ANDREAS" WANAJUA UKIFIKA SEHEMU MOJA INAYOITWA AREA 51 UNASHAMBULIWA KULIKO KAWAIDA)

    #04.ILHA DE QUEIMEDA/SNAKE ISLAND (KISIWA NA NYOKA)
    Kisiwa cha ILHA DE QUEIMEDA kipo umbali wa maili kadhaa kutoka katika pwani ya mji wa SAO PAOLO nchini BRAZIL.
    Kisiwa hiki ni makazi ya nyoka hatari zaidi duniani tena wenye sumu ilio kali kabisa,idadi ya kukadiria ya nyoka waliopo kisiwani humo ni takriban nyoka 4000,nyoka aina ya 'lancehead vipers' wapatikanao kisiwani humo wanakua kwa wastani wa urefu wa SENTIMITA 70 (70 CM) pia wanaweza kufikia hata urefu wa SENTIMITA 118 mpaka 120,vifo vingi vinavyotokea amerika ya kusini miongoni mwao husababishwa na nyoka hawa.
    > Chakula chao cha kawaida mara nyingi ni ndege na imeripotiwa kuwa huwa wanakula mijusi na kula hata nyoka wengine.
    > Nyoka wa aina hii akimng'ata/akimgonga binadamu mara moja basi binadamu anakuwa kwenye hatari ya kufa kwa aslimia 7 (7%) yaani anakuwa na uwezekano wa kufa kwa asilimia 7.
    Moja ya kisa kilichoripitiwa kutokea kisiwani huko ni cha mvuvi mmoja aliekuwa akivua samaki na mara boti yake ikapata tatizo la injini akaamua kuweka makazi kwa muda katika kisiwa hicho pasina kujua hatari iliopo ndani yake, baada ya boti kuonekana ndipo alipopatikana akiwa amekufa huku akiwa na alama za kung'atwa na nyoka.
    Kwa miaka 15 iliopita idadi ya nyoka kisiwani humo imepungua kwa asilimia 15 (15%) kutokana na magonjwa na kupungua kwa uoto ndani ya kisiwa,lakini hii leo bado maelfu ya nyoka bado ndio makazi yao ndani ya kisiwa.Serikali ya BRAZIL imezuia utembeleaji na shughuli za kitalii ndani ya kisiwa hicho isipokuwa kwa wanasayansi na wanajeshi wa majini wa BRAZIL.
    YAJUE MAENEO AMBAYO HURUHUSIWI KUFIKA KAMWE. Katika ulimwengu wa leo tunaoishi tunaweza kufanya vitu vingi vinavyotufurahisha ikiwemo kusafiri kwenda maeneo mbalimbali ulimwenguni kwa malengo mbalimbali mfano kibiashara,kiutalii na hata kwa lengo la kuburudika tu.lakini hayo yote yanaweza kufanyika isipokuwa kwa baadhi ya maeneo,yafuatayo ni maeneo manne (4) ambayo huruhusiwi kufika. #01.NORTH SENTINEL ISLAND (KISIWA CHA SENTINEL YA KASKAZINI) Kisiwa cha NORTH SENTINEL ni sehemu ya visiwa vya ANDAMAN na NICOBAR vilivyopo kwenye bay ya BENGAL kwenye bahari ya hindi kati ya MYANMAR na INDONESIA.Eneo hili ndipo mahali ambapo wakazi wake hawaruhusu mawasiliano kabisa na ulimwengu ulioendelea/mataifa mengine. Kuna visa kadhaa vya kuthibitisha 'marufuku' ya kuingia kisiwani huko kutoka kwa wakazi wake. -Mwezi DISEMBA mwaka 2004 tsunami ilipopiga kwenye bahari ya hindi waokoaji walihitaji kusaidia wahanga wa kisiwa hiko lakini haikuwa rahisi kutokana na upinzani waliokutana nao kutoka kwa wakazi wa kisiwa hicho,walijaribu kushusha vyakula wakiwa kwenye helikopta ya jeshi la maji la INDIA kilichotokea ni kwamba moja ya helikopta hizo ilishambuliwa na 'shujaa' mmoja wa kisiwa hiko aliepiga mkuki kwenye helikopta kuonesha kuwa watu hao hawakuhitaji msaada wala mawasiliano na mataifa jirani. Kimsingi INDIA ndio inayomiliki kisiwa hicho. -Kisa kingine ni cha mwaka 1896 cha mfungwa mmoja alietoroka kutoka kwenye gereza lililopo katika kisiwa cha ANDAMAN ambae alikimbilia kwenye kisiwa hiki,siku chache baadae mwili wake ulikutwa pembezoni mwa bahari ukiwa na alama za kupigwa na mishale na huku koo lake likiwa limekatwa. Sijui kama wakazi wa kisiwa hiki wanajua kama kuna nchi inaitwa TANZANIA,shughuli wanazofanya kuendesha maisha yao ni uwindaji,uvuvi pia wanakula matunda na asali. Huwezi kuamini kuwa maeneo haya hakuna SIMU wala INTANETI. #02.ROOM 39 (CHUMBA NAMBA 39) Kwa majina mengine huitwa BUREAU 39 au DIVISION 39 au OFFICE 39,jengo hili lipo nchini KOREA KASKAZINI na linakaliwa na tasisi ya siri ya chama cha KOREA KASKAZINI (KOREAN WORKERS' PARTY) lengo lake ni kuchangia uongezekaji wa fedha za kigeni nchini KOREA KASKAZINI,ROOM 39 inaaminika kuendesha shughuli zote zinazohusiana na uingizwaji wa fedha za kigeni nchini humo na mjini PYONGYANG ikiwa pamoja na mahoteli yaliyopo PYONGYANG na uchimbaji wa madini ya ZINC na DHAHABU. Taasisi ya ROOM 39 inaaminika kumiliki baadhi ya makampuni mafano ZOKWANG TRADING na benki ya TAESONG BANK. Tasisi hii iliundwa na KIM IL-SUNG miaka ya 1970,kwa mwaka tasisi hii ya siri inasadikika inaiingizia nchi ya KOREA KASKAZINI mapato ya kati ya milioni $500 (dola za kimarekani) mpaka billioni $1 (dola za kimarekani). Vyanzo kadhaa vya nchi za magharibi vinaeleza kuwa taasisi hii inaingiza fedha hizo kwa kuendesha shughuli za kihalifu,mfano ripoti moja ya WASHINGTON POST ilieleza ubadhilifu uliotokea katika sekta ya BIMA duniani na kudai kuwa ulifanywa na serikali ya KOREA KASKAZINI kwa kutumia taasisi yake ya KOREA NATIONAL INSURANCE CORP (KNIC). Jengo hili la ROOM 39 hakika huruhusiwi kuingia ndani yake,kutokana na sababu za kiusalama hivyo hutaweza kuwemo ndani yake. #03.AREA 51 Hili ni eneo linalomilkiwa na JESHI LA ANGA LA MAREKANI lipo NEVADA. Taarifa nyingi na za uhakika kuhusu mambo yanayofanyika katika eneo hili ni 'highly classified' ila tu kuna nadharia kadhaa zinazoeleza mambo yanayofanyika katika eneo hili baadhi ya nadharia hizo ni; >Inaaminika kuwa AREA 51 ni mahali wanapofanya tafiti za teknolojia za viumbe wa sayari nyingine (ALLIEN) ambapo jeshi la anga la marekani limehifadhi masalia ya ndege za viumbe hao zilizopata ajali,na pia wanatengeneza ndege kutokana na teknolojia ya ALLIENS. >Inaaminika wanaendesha program/mpango wa kutengeneza silaha za kujilinda za awali yaani STRATEGIC DEFENSE INITIATIVE (SDI) na program za silaha nyingine. >Inaaminika kuwa ndani ya eneo hilo wanatengeneza teknolojia itakayoweza ku'control' hali ya hewa. >Inaaminika kuwa wanafanya program ya kutengeneza teknolojia ya TIME TRAVEL (uwezo wa kumwezesha mtu kurudi wakati uliopita au kwenda wakati ujao,mfano mtu atoke hivi sasa na asafiri kwenda miaka 50 ijayo) na TELEPORTATION (yaani mtu aweze kusafiri kutoka eneo moja hadi jingine pasina usafiri wowote ule na kwa haraka.nadharia hii imeelezwa kwenye filamu/movie/series ya TOMORROW PEOPLE kama ushawahi kuiona basi hivyo ndivyo watu wanavyo teleport). >Inaaminika kuwa pengine wanaendesha shughuli zitakazochangia kuwepo kwa serikali moja duniani (ONE WORLD GOVERMENT) Moja ya mambo yanayoweza kutumika kama ushahidi juu ya nadharia inayohusisha uwepo wa viumbe kutoka sayari nyingine yaani ALLIENS ndani ya AREA 51 ni baadhi ya watu waliowahi kukiri kuwa wafanyakazi wa AREA 51 **Mmoja wao ni bwana BOB LAZAR ambae mwaka 1989 alisema kuwa alifanya kazi ndani ya AREA 51 SECTOR FOUR (S-4) ambapo eneo hili lipo chini ya ardhi,bwana BOB LAZAR alisema kuwa alipokuwa ndani ya SECTOR FOUR alifanya kazi na ndege ya anga la juu(spacecraft) ya ALLIENS ambayo inashikiliwa na serikali ya MAREKANI ndani ya AREA 51. **Documentary moja iitwayo DREAMLAND iliotoka mwaka 1996 ilioongozwa na BRUCE BURGESS ilijumuisha interview aliofanya na mzee wa umri wa miaka 71 ambae ni injinia (mechanical engeneer) aliekiri kuwa alishawahi kuwa muajiriwa aliefanya kazi ndani ya AREA 51 katika miaka ya 1950,alikiri kuwa alifanya kazi kwenye kitu chenye uwezo wa kupaaa angani kilicho mfano wa sahani kiitwacho "FLYING DISK SIMULATOR" alisema kitu hicho mfano wa sahani kubwa kilitokana na ndege ya anga za juu iliopoata ajali na kilitumika kuwafundishia marubani wa jeshi la MAREKANI,pia alikiri kuwa alifanya kazi na kiumbe kutoka sayari nyingine ambae aliitwa "J-ROD". **Mwaka 2004 DAN BURISCH alikiri kufanya kazi ndani ya AREA 51 pamoja na ALLIEN aliefahamika kwa jina la "J-ROD" Kuingia katika eneo hili kumezuiwa vikali, na wanajeshi wanaolinda eneo hilo wamepewa mamlaka ya kumfyatulia risasi yeyote atakaeingia ambae hana ruhusa ya kuwepo eneo hilo,Hivyo basi katika eneo hili hautaweza kufika labda uwe mfanyikazi wa humu. (KWA WALE WANAOCHEZA SANA VIDEO GAMES AU WALE WALIOWAHI KUCHEZA "GTA SAN ANDREAS" WANAJUA UKIFIKA SEHEMU MOJA INAYOITWA AREA 51 UNASHAMBULIWA KULIKO KAWAIDA) #04.ILHA DE QUEIMEDA/SNAKE ISLAND (KISIWA NA NYOKA) Kisiwa cha ILHA DE QUEIMEDA kipo umbali wa maili kadhaa kutoka katika pwani ya mji wa SAO PAOLO nchini BRAZIL. Kisiwa hiki ni makazi ya nyoka hatari zaidi duniani tena wenye sumu ilio kali kabisa,idadi ya kukadiria ya nyoka waliopo kisiwani humo ni takriban nyoka 4000,nyoka aina ya 'lancehead vipers' wapatikanao kisiwani humo wanakua kwa wastani wa urefu wa SENTIMITA 70 (70 CM) pia wanaweza kufikia hata urefu wa SENTIMITA 118 mpaka 120,vifo vingi vinavyotokea amerika ya kusini miongoni mwao husababishwa na nyoka hawa. > Chakula chao cha kawaida mara nyingi ni ndege na imeripotiwa kuwa huwa wanakula mijusi na kula hata nyoka wengine. > Nyoka wa aina hii akimng'ata/akimgonga binadamu mara moja basi binadamu anakuwa kwenye hatari ya kufa kwa aslimia 7 (7%) yaani anakuwa na uwezekano wa kufa kwa asilimia 7. Moja ya kisa kilichoripitiwa kutokea kisiwani huko ni cha mvuvi mmoja aliekuwa akivua samaki na mara boti yake ikapata tatizo la injini akaamua kuweka makazi kwa muda katika kisiwa hicho pasina kujua hatari iliopo ndani yake, baada ya boti kuonekana ndipo alipopatikana akiwa amekufa huku akiwa na alama za kung'atwa na nyoka. Kwa miaka 15 iliopita idadi ya nyoka kisiwani humo imepungua kwa asilimia 15 (15%) kutokana na magonjwa na kupungua kwa uoto ndani ya kisiwa,lakini hii leo bado maelfu ya nyoka bado ndio makazi yao ndani ya kisiwa.Serikali ya BRAZIL imezuia utembeleaji na shughuli za kitalii ndani ya kisiwa hicho isipokuwa kwa wanasayansi na wanajeshi wa majini wa BRAZIL.
    0 Commenti 0 condivisioni 4K Views
  • Mnamo Mwaka 2006, wiki kadhaa baada ya kustaafu nafasi ya ukatibu mkuu, Kofi Annan alienda nchini Italia kwa ajili ya mapumziko.

    Akiwa huko, Siku moja aliamua kutoka nje kidogo na kwenda kununua gazeti, lakini ghafla akashangaa Watu wengi wanamzonga. Lengo lao ni kutaka sahihi kutoka kwake. (Kama uonavyo nyota wa filamu au wachezaji mpira, wanavyochora sahihi zao kwenye mashati ya wafuasi).

    Lakini kumbe, Watu hao walimfananisha Kofi Annan na yule nyota wa filamu wa marekani bwana Morgan Freeman .

    Ila, kwa kutotaka kuwaangusha Watu hao, Kofi Annan alichora sahihi kwa kutumia jina la Freeman.

    (Angalia picha zao)

    Koffi Anan, alifaliki akiwa na umri wa miaka 80 huko nchini Switzerland.

    Alihudumu nafasi ya ukatibu mkuu kwanzia Mwaka 1997 hadi 2006, akiwa ndiye mwafrika mweusi wa kwanza kushika nafasi hiyo.

    RIP koffi Annan.
    Mnamo Mwaka 2006, wiki kadhaa baada ya kustaafu nafasi ya ukatibu mkuu, Kofi Annan alienda nchini Italia kwa ajili ya mapumziko. Akiwa huko, Siku moja aliamua kutoka nje kidogo na kwenda kununua gazeti, lakini ghafla akashangaa Watu wengi wanamzonga. Lengo lao ni kutaka sahihi kutoka kwake. (Kama uonavyo nyota wa filamu au wachezaji mpira, wanavyochora sahihi zao kwenye mashati ya wafuasi). Lakini kumbe, Watu hao walimfananisha Kofi Annan na yule nyota wa filamu wa marekani bwana Morgan Freeman . Ila, kwa kutotaka kuwaangusha Watu hao, Kofi Annan alichora sahihi kwa kutumia jina la Freeman. (Angalia picha zao) Koffi Anan, alifaliki akiwa na umri wa miaka 80 huko nchini Switzerland. Alihudumu nafasi ya ukatibu mkuu kwanzia Mwaka 1997 hadi 2006, akiwa ndiye mwafrika mweusi wa kwanza kushika nafasi hiyo. RIP koffi Annan.
    Like
    2
    0 Commenti 0 condivisioni 968 Views
  • JAMBAZI MTUKUTU.

    Nchini Tanzania, kuna manju 'Dj' fulani wa muziki anayejulikana kwa jina maarufu la 'DJ JD' au kwa kirefu *'DJ John Dilinga'.* Huyu ni moja kati ya maDj wakongwe na mahiri sana tuliobahatika kuwa nao hapa nchini Tanzania. Kwa wale wapenzi na wadau wa muziki wa 'bongofleva' hususani wa miaka ya nyumanyuma kidogo, bila shaka mtakua mnamfahamu Dj huyu.

    Kwa muda mrefu nimekuwa nikitamani kufahamu ni kwanini anaitwa John Dilinga..nikiwa nataka kujua kama hilo ni jina lake halisi au ni 'a.k.a'. Maana ni kawaida kuona watu mbalimbali hususani walio kwenye tasnia ya burudani wakitumia majina ya ziada (a.k.a) kuliko majina yao halisi.

    Kitu kilichonifanya nianze na DJ JD ni baada ya kugundua kuwa leo ni tarehe 22 Julai. Tarehe ambayo ulimwengu mzima unamtaja bwana mmoja mtukutu sana, aliyewahi kusumbua vichwa vya maofisa usalama wa nchi ya Marekani, akifahamika kama *John Dillinger.* Huyu alikuwa ni moja kati ya wahuni wakubwa nchini Marekani aliyetamba sana katika miaka ya 1930 kwa kujihusisha na matukio ya kihalifu hususani uporaji wa fedha kwenye mabenki.

    Tofauti ni kwamba John Dilinga wa Tanzania ni DJ, wakati John Dillinger wa Marekani alikuwa ni jambazi mtukutu.

    Utukutu wake ulianza angali ana umri mdogo na hata aliweza kuacha shule ili kwenda kutafuta pesa!! Alianza kama mdokozi wa vitu vidogovidogo lakini tukio lake la kwanza lilikuwa ni *kuiba gari*, kisha 'kwenda misele' kwa mpenzi wake mpya. Siku chache baadae alikuja kukamatwa na mapolisi akiwa anazurula mtaani japokuwa alifanikiwa kuchoropoka na 'kutokomea kusikojulikana'.

    Baadae alipata kazi katika jeshi la majini 'navy', akifanya katika meli ya jeshi ya 'USS Uttah'. Baada ya miezi kadhaa John Dillinger alitoroka kazini.

    April 1924 akiwa hana shughuli ya kumuingizia kipato, John Dillinger alifunga ndoa na mwanadada Beryl Hovious ambapo walienda kuishi kwenye nyumba ya baba yake ambapo John Dillinger aliahidi kwamba sasa atatulia na kuacha utukutu wote. Lakini wiki chache baada ya ndoa, Dillinger alikamatwa na hata kufikishwa mahakamani kwa kosa la wizi wa kuku, "nadhani alikuwa anatafuta mboga ya kwenda kula na mkewe".

    Lakini kwa msaada wa Baba yake, kesi ya Dillinger iliweza kufutwa. Baadae Dillinger aliamua kutoka kwenye nyumba ya baba yake na kwenda kuishi kwenye nyumba ya wazazi wa mwanamke ambapo huko alibahatika kupata kazi kwenye duka la kuuza vifaa vya ujenzi. Akiwa huko, Dillinger alikutana na rafiki yake wa muda mrefu aitwaye *Edgar Singleton,* ambapo walipanga mikakati ya kuiba pesa. Ndipo tarehe 6 septemba 1924 waliiba pesa katika moja ya Grocery japokuwa walikamatwa na kufikishwa mahakamani ambapo John Dillinger alihukumiwa kifungo cha miaka 20 katika Gereza la "Indiana State Reformatory in Pendleton".

    Alipokuwa jela, alikutana na wafungwa wengine ambao walimfundisha mbinu nyingine za uhalifu mkubwa hususani uporaji wa fedha kwenye mabenki. Alitumikia kifungo chake hadi mwaka 1933 kwa paroli. Siku chache tu baada ya kutoka jela, John Dillinger alifanya uhalifu mkubwa, safari hii akivamia benki na kuiba pesa benki ingawa alikamatwa na kuhukumiwa kifungo katika gereza la Lima.

    Siku chache baada ya Dillinger kuingia jela, wafungwa 12 ambao baadhi yao ni rafiki zake Dillinger, waliweza kutoroka katika gereza la "Indiana State Prison". Hili ni gereza alilowahi kufungwa John Dillinger baada ya kuhamishwa toka kwenye gereza lile la awali.

    Miongoni mwa hao waliotoroka, ambao baadhi yao ni marafiki wa Dillinger, walifika katika gereza alilofungwa Dillinger lengo ni kumtorosha rafiki yao. Walimuua askari mmoja na kuchukua funguo kisha kufungua mlango wa selo alilomo Dillinger kisha kutoroka naye. Baada ya kutoroka, John Dillinger na wenzake walielekea mjini Chicago ambapo waliunda genge kubwa la kihalifu *Dillinger Gang*. Genge hili lilipora pesa kwenye mabenki mbalimbali, na ili kuongeza nguvu, walivamia ghala la silaha na kuiba silaha nzitonzito walizozotumia katika shughuli zao za kihalifu.

    Wahuni hao walitokea kupata umaarufu mkubwa pale Marekani, hususani huyu Dillinger ambaye alikuwa maarufu sana mithili ya 'nyota wa hollywood' kwani kila siku jina lake lilikuwa likitajwa kwenye vyombo vya habari na kuandikwa magazetini. Sifa nyingine ya genge hili ni kwamba walikuwa watanashati mno wakipendelea kuvaa suti na kofia nyeusi.

    Januari 15 1934, Dillinger alivamia benki kuiba pesa. Katika tukio la majibizano ya risasi, Dillinger alimuua askari mmoja aliyejulikana kwa jina la William O'Malley. Yeye alipigwa risasi kadhaa japokuwa hakufa kwasababu alivaa 'bullet proof'.

    Baadae, 'Dillinger Gang' walikuja kukamatwa, ambapo Dillinger alipelekwa katika gereza la *crown point* kwa kosa la kumuua Askari. Gereza hilo lilipewa jina la 'escape proof' kwakuwa lilikuwa nj ngumu kutoroka hapo. Umaarufu wake ulipelekea wananchi kufurika mahakamani na gerezani kwa ajili ya kutaka kumuona John Dillinger.

    Tarehe 3 Machi 1934, John Dillinger alifanikiwa kutoroka tena katika gereza la *Crown point,* safari hii akitoroka kwa kutumia 'bunduki feki' aliyoichonga kwa kutumia mbao na kuipaka rangi nyeusi. Aliitumia bunduki hiyo kumtisha askari kisha akapora gari la askari na kutoroka nalo. Kitendo hiko kiliwafanya polisi waombe msaada kutoka *FBI* ambao walifanya msako kabambe wa kumkamata John Dillinger.

    Alipotoroka, alikimbilia mjini Chicago ambako huko aliunda Genge jipya safari hii akimchukua mtu hatari aliyejulikana kama 'Baby Face Nelson'. Genge hilo liliendelea kufanya matukio mengi ya uporaji wa pesa benki na hata wizi wa silaha. Katika kipindi hiki, John Dillinger alianzisha mahusiano na binti aliyeitwa 'Polly Hamilton' mhudumu wa mgahawa pale Chicago ambaye hapo kabla alikuwa akijihusisha na ukahaba. Ifahamike kuwa kipindi yupo jela, Dillinger alitalikiana na yule mkewe.

    MSAKO wa kumpata John Dillinger ulikuwa ukiendelea ambapo FBI walisambaza picha za Dillinger pamoja na kutangaza dau nono kwa yeyote atakayefanikisha upatikanaji wake. FBI walitangaza dau la dola $10,000 kwa yeyote atakayefakiwa kumkamata Dillinger na $5,000 kwa yule atakayetoa taarifa za kupatikana kwake. John Dillinger alisumbua sana vichwa vya maafisa usalama kiasi cha FBI kumtangaza kuwa *"Public Enemy Nō 1".* Ukiona hadi mtu anaitwa Public Enemy Nō 1 ujue huyo alikuwa ni 'kiboko pasua kichwa'.

    John Dillinger naye hakuwa nyuma katika kuhakikisha hakamatwi. Unajua alifanyaje??.

    Aliamua kufanya operesheni ya uso *"plastic surgery"* ili kubadilisha muonekano wa sura yake. Pia alifanya uperesheni ya kubadilisha alama za vidole yaani 'finger prints'.

    Mkuu wa FBI bwana J. Edgar Hoover alimteua bwana Samuel Cowley kuongoza misheni ya kumkamata John Dillinger. Cowley naye aliungana na Afisa *Mervin Purvis* kutoka mjini Chicago. Kwa pamoja walishirikiana na polisi kuhakikisha huyu 'Adui namba moja' anapatikana.

    Ilikuwa ni siku ya tarehe 21 Julai 1934 ambapo maafisa usalama walipokea simu kutoka kwa mwanadada mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Anna. Binti huyu alitoa taarifa za siri kwamba 'kesho jioni, yeye, John Dillinger pamoja na mpenzi wake, Polly Hamilton, wataenda kuangalia filamu kwenye moja ya majumba ya sinema, akaeleza kwamba watachagua kwenda aidha Biograph Theater au Marbo Theater. Na wakapanga kwamba atavaa vazi la rangi nyekundu ili iwe rahisi kwa maofisa hao kumtambua.

    Ilipofika kesho yake, maofisa wakampigia simu Anna Sage ili 'ku-comfirm' ni wapi wataenda kati ya Biograph au Marbo??. Lakini kwakua Anna alikuwa bado hajui ni wapi haswa wataenda, tuliona maofisa usalama wakiongozwa na Marvin Purvis wakijigawa kwenda 'kukava' sehemu zote mbili.

    Hatimaye ilipofika majira ya saa 2:30 usiku, Anna, John Dillinger pamoja na Polly Hamilton, walionekana wakiingia kwenye jumba la sinema la *Biograph Theater*. Baada ya kina Dillinger kuingia, tukaona wale maofisa wengine waliokuwepo kule 'Marbo Theater' wakiwasili haraka pale 'Biograph Theater' kwa ajili ya kuongeza nguvu.

    Saa 4:30 usiku, baada ya filamu kumalizika, alionekana John Dillinger akiwa na wale warembo wake wawili, mmoja kulia mwingine kushoto, wakiwa wanatoka nje. Wakati wanakuja usawa wa aliposimama ofisa Purvis. Purvis aliwasha sigara yake kama ishara ya wale wenzake kusogea jirani. Wakati anafanya hivyo, kumbe Dillinger alikuwa *'ameshahisi hali ya hatari',* akatoa bastola yake huku akijihami kwa kujaribu kukimbia.

    Lakini kabla hajafika mbali, risasi tatu zilifika kwenye mwili wa John Dillinger. Risasi moja ikipenya upande wa nyuma wa shingo na kutokezea kwenye sikio. Dakika chache zilizofuata, hospitali ya Alexian Brothers ilitangaza kifo cha John Dillinger. Na hiyo ndio ikawa mwisho wa mtukutu huyu ambaye alifariki tarehe kama ya leo *22 Julai 1934.* Baada ya kuenea taarifa za kifo chake watu wengi walifurika eneo la tukio angalau waweze kuuona mwili wa John Dillinger.

    ****

    Lakini nafahamu utakuwa unajiuliza yule mwanadada aliyetoa taarifa za siri za kurahisisha kukamatwa kwa John Dillinger ni nani na kwanini alifanya hivyo?!! Baadae nitaeleza kisa hiko. Lakini kwa sasa tuishie hapa.

    Ahsante.

    JAMBAZI MTUKUTU. Nchini Tanzania, kuna manju 'Dj' fulani wa muziki anayejulikana kwa jina maarufu la 'DJ JD' au kwa kirefu *'DJ John Dilinga'.* Huyu ni moja kati ya maDj wakongwe na mahiri sana tuliobahatika kuwa nao hapa nchini Tanzania. Kwa wale wapenzi na wadau wa muziki wa 'bongofleva' hususani wa miaka ya nyumanyuma kidogo, bila shaka mtakua mnamfahamu Dj huyu. Kwa muda mrefu nimekuwa nikitamani kufahamu ni kwanini anaitwa John Dilinga..nikiwa nataka kujua kama hilo ni jina lake halisi au ni 'a.k.a'. Maana ni kawaida kuona watu mbalimbali hususani walio kwenye tasnia ya burudani wakitumia majina ya ziada (a.k.a) kuliko majina yao halisi. Kitu kilichonifanya nianze na DJ JD ni baada ya kugundua kuwa leo ni tarehe 22 Julai. Tarehe ambayo ulimwengu mzima unamtaja bwana mmoja mtukutu sana, aliyewahi kusumbua vichwa vya maofisa usalama wa nchi ya Marekani, akifahamika kama *John Dillinger.* Huyu alikuwa ni moja kati ya wahuni wakubwa nchini Marekani aliyetamba sana katika miaka ya 1930 kwa kujihusisha na matukio ya kihalifu hususani uporaji wa fedha kwenye mabenki. Tofauti ni kwamba John Dilinga wa Tanzania ni DJ, wakati John Dillinger wa Marekani alikuwa ni jambazi mtukutu. Utukutu wake ulianza angali ana umri mdogo na hata aliweza kuacha shule ili kwenda kutafuta pesa!! Alianza kama mdokozi wa vitu vidogovidogo lakini tukio lake la kwanza lilikuwa ni *kuiba gari*, kisha 'kwenda misele' kwa mpenzi wake mpya. Siku chache baadae alikuja kukamatwa na mapolisi akiwa anazurula mtaani japokuwa alifanikiwa kuchoropoka na 'kutokomea kusikojulikana'. Baadae alipata kazi katika jeshi la majini 'navy', akifanya katika meli ya jeshi ya 'USS Uttah'. Baada ya miezi kadhaa John Dillinger alitoroka kazini. April 1924 akiwa hana shughuli ya kumuingizia kipato, John Dillinger alifunga ndoa na mwanadada Beryl Hovious ambapo walienda kuishi kwenye nyumba ya baba yake ambapo John Dillinger aliahidi kwamba sasa atatulia na kuacha utukutu wote. Lakini wiki chache baada ya ndoa, Dillinger alikamatwa na hata kufikishwa mahakamani kwa kosa la wizi wa kuku, "nadhani alikuwa anatafuta mboga ya kwenda kula na mkewe". Lakini kwa msaada wa Baba yake, kesi ya Dillinger iliweza kufutwa. Baadae Dillinger aliamua kutoka kwenye nyumba ya baba yake na kwenda kuishi kwenye nyumba ya wazazi wa mwanamke ambapo huko alibahatika kupata kazi kwenye duka la kuuza vifaa vya ujenzi. Akiwa huko, Dillinger alikutana na rafiki yake wa muda mrefu aitwaye *Edgar Singleton,* ambapo walipanga mikakati ya kuiba pesa. Ndipo tarehe 6 septemba 1924 waliiba pesa katika moja ya Grocery japokuwa walikamatwa na kufikishwa mahakamani ambapo John Dillinger alihukumiwa kifungo cha miaka 20 katika Gereza la "Indiana State Reformatory in Pendleton". Alipokuwa jela, alikutana na wafungwa wengine ambao walimfundisha mbinu nyingine za uhalifu mkubwa hususani uporaji wa fedha kwenye mabenki. Alitumikia kifungo chake hadi mwaka 1933 kwa paroli. Siku chache tu baada ya kutoka jela, John Dillinger alifanya uhalifu mkubwa, safari hii akivamia benki na kuiba pesa benki ingawa alikamatwa na kuhukumiwa kifungo katika gereza la Lima. Siku chache baada ya Dillinger kuingia jela, wafungwa 12 ambao baadhi yao ni rafiki zake Dillinger, waliweza kutoroka katika gereza la "Indiana State Prison". Hili ni gereza alilowahi kufungwa John Dillinger baada ya kuhamishwa toka kwenye gereza lile la awali. Miongoni mwa hao waliotoroka, ambao baadhi yao ni marafiki wa Dillinger, walifika katika gereza alilofungwa Dillinger lengo ni kumtorosha rafiki yao. Walimuua askari mmoja na kuchukua funguo kisha kufungua mlango wa selo alilomo Dillinger kisha kutoroka naye. Baada ya kutoroka, John Dillinger na wenzake walielekea mjini Chicago ambapo waliunda genge kubwa la kihalifu *Dillinger Gang*. Genge hili lilipora pesa kwenye mabenki mbalimbali, na ili kuongeza nguvu, walivamia ghala la silaha na kuiba silaha nzitonzito walizozotumia katika shughuli zao za kihalifu. Wahuni hao walitokea kupata umaarufu mkubwa pale Marekani, hususani huyu Dillinger ambaye alikuwa maarufu sana mithili ya 'nyota wa hollywood' kwani kila siku jina lake lilikuwa likitajwa kwenye vyombo vya habari na kuandikwa magazetini. Sifa nyingine ya genge hili ni kwamba walikuwa watanashati mno wakipendelea kuvaa suti na kofia nyeusi. Januari 15 1934, Dillinger alivamia benki kuiba pesa. Katika tukio la majibizano ya risasi, Dillinger alimuua askari mmoja aliyejulikana kwa jina la William O'Malley. Yeye alipigwa risasi kadhaa japokuwa hakufa kwasababu alivaa 'bullet proof'. Baadae, 'Dillinger Gang' walikuja kukamatwa, ambapo Dillinger alipelekwa katika gereza la *crown point* kwa kosa la kumuua Askari. Gereza hilo lilipewa jina la 'escape proof' kwakuwa lilikuwa nj ngumu kutoroka hapo. Umaarufu wake ulipelekea wananchi kufurika mahakamani na gerezani kwa ajili ya kutaka kumuona John Dillinger. Tarehe 3 Machi 1934, John Dillinger alifanikiwa kutoroka tena katika gereza la *Crown point,* safari hii akitoroka kwa kutumia 'bunduki feki' aliyoichonga kwa kutumia mbao na kuipaka rangi nyeusi. Aliitumia bunduki hiyo kumtisha askari kisha akapora gari la askari na kutoroka nalo. Kitendo hiko kiliwafanya polisi waombe msaada kutoka *FBI* ambao walifanya msako kabambe wa kumkamata John Dillinger. Alipotoroka, alikimbilia mjini Chicago ambako huko aliunda Genge jipya safari hii akimchukua mtu hatari aliyejulikana kama 'Baby Face Nelson'. Genge hilo liliendelea kufanya matukio mengi ya uporaji wa pesa benki na hata wizi wa silaha. Katika kipindi hiki, John Dillinger alianzisha mahusiano na binti aliyeitwa 'Polly Hamilton' mhudumu wa mgahawa pale Chicago ambaye hapo kabla alikuwa akijihusisha na ukahaba. Ifahamike kuwa kipindi yupo jela, Dillinger alitalikiana na yule mkewe. MSAKO wa kumpata John Dillinger ulikuwa ukiendelea ambapo FBI walisambaza picha za Dillinger pamoja na kutangaza dau nono kwa yeyote atakayefanikisha upatikanaji wake. FBI walitangaza dau la dola $10,000 kwa yeyote atakayefakiwa kumkamata Dillinger na $5,000 kwa yule atakayetoa taarifa za kupatikana kwake. John Dillinger alisumbua sana vichwa vya maafisa usalama kiasi cha FBI kumtangaza kuwa *"Public Enemy Nō 1".* Ukiona hadi mtu anaitwa Public Enemy Nō 1 ujue huyo alikuwa ni 'kiboko pasua kichwa'. John Dillinger naye hakuwa nyuma katika kuhakikisha hakamatwi. Unajua alifanyaje??. Aliamua kufanya operesheni ya uso *"plastic surgery"* ili kubadilisha muonekano wa sura yake. Pia alifanya uperesheni ya kubadilisha alama za vidole yaani 'finger prints'. Mkuu wa FBI bwana J. Edgar Hoover alimteua bwana Samuel Cowley kuongoza misheni ya kumkamata John Dillinger. Cowley naye aliungana na Afisa *Mervin Purvis* kutoka mjini Chicago. Kwa pamoja walishirikiana na polisi kuhakikisha huyu 'Adui namba moja' anapatikana. Ilikuwa ni siku ya tarehe 21 Julai 1934 ambapo maafisa usalama walipokea simu kutoka kwa mwanadada mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Anna. Binti huyu alitoa taarifa za siri kwamba 'kesho jioni, yeye, John Dillinger pamoja na mpenzi wake, Polly Hamilton, wataenda kuangalia filamu kwenye moja ya majumba ya sinema, akaeleza kwamba watachagua kwenda aidha Biograph Theater au Marbo Theater. Na wakapanga kwamba atavaa vazi la rangi nyekundu ili iwe rahisi kwa maofisa hao kumtambua. Ilipofika kesho yake, maofisa wakampigia simu Anna Sage ili 'ku-comfirm' ni wapi wataenda kati ya Biograph au Marbo??. Lakini kwakua Anna alikuwa bado hajui ni wapi haswa wataenda, tuliona maofisa usalama wakiongozwa na Marvin Purvis wakijigawa kwenda 'kukava' sehemu zote mbili. Hatimaye ilipofika majira ya saa 2:30 usiku, Anna, John Dillinger pamoja na Polly Hamilton, walionekana wakiingia kwenye jumba la sinema la *Biograph Theater*. Baada ya kina Dillinger kuingia, tukaona wale maofisa wengine waliokuwepo kule 'Marbo Theater' wakiwasili haraka pale 'Biograph Theater' kwa ajili ya kuongeza nguvu. Saa 4:30 usiku, baada ya filamu kumalizika, alionekana John Dillinger akiwa na wale warembo wake wawili, mmoja kulia mwingine kushoto, wakiwa wanatoka nje. Wakati wanakuja usawa wa aliposimama ofisa Purvis. Purvis aliwasha sigara yake kama ishara ya wale wenzake kusogea jirani. Wakati anafanya hivyo, kumbe Dillinger alikuwa *'ameshahisi hali ya hatari',* akatoa bastola yake huku akijihami kwa kujaribu kukimbia. Lakini kabla hajafika mbali, risasi tatu zilifika kwenye mwili wa John Dillinger. Risasi moja ikipenya upande wa nyuma wa shingo na kutokezea kwenye sikio. Dakika chache zilizofuata, hospitali ya Alexian Brothers ilitangaza kifo cha John Dillinger. Na hiyo ndio ikawa mwisho wa mtukutu huyu ambaye alifariki tarehe kama ya leo *22 Julai 1934.* Baada ya kuenea taarifa za kifo chake watu wengi walifurika eneo la tukio angalau waweze kuuona mwili wa John Dillinger. **** Lakini nafahamu utakuwa unajiuliza yule mwanadada aliyetoa taarifa za siri za kurahisisha kukamatwa kwa John Dillinger ni nani na kwanini alifanya hivyo?!! Baadae nitaeleza kisa hiko. Lakini kwa sasa tuishie hapa. Ahsante.
    Like
    1
    0 Commenti 0 condivisioni 2K Views
  • NINI ASILI YA WAYAHUDI WA LEO NCHINI ISRAEL? ,UKWELI WA MUONEKANO WAO NA HATIMA YA UTAWALA WAO.

    TUKUMBUKE Rais wa Misri wa pili wa zamani wa Umoja wa Jamhuri ya waarabu Gamal Abdel Nasser mwaka 1952 alishawahi kusema mbele ya Televisheni kwamba, watu wa ulaya wanajidai kuwa wao ni wayahudi akasema kwamba; siwezi kuwaheshimu wayahudi nyie wayahudi hamtaweza kuishi kwa amani kwasababu mliondoka hapa mkiwa weusi mkarudi mkiwa weupe.

    Msafiri wa kiitalia Ludovico di Varthema mwaka 1470 hadi mwaka 1517 alijulikana kama mtu wa kwanza Ulaya asiye muislam kuingia Makka kuhiji, karibu kila kitu kinachomuhusu maisha yake kimeandikwa katika kitabu cha "Itinerario de Ludovicode Varthema Bolognese" kilichapishwa Roma mwaka 1510. Moja ya kurasa zake unasomeka ;"mwisho wa siku 8 tukakuta mlima unaoonekana kuwa maili 10 au 12 hivi kwa mzunguko katika mlima huo paliishi wayahudi elfu nne au tano hivi waliokuwa wanatembea bila nguo na viganja vyao vipana, wenye sauti zinazofanana na zile za kike, walikuwa weusi zaidi kuliko rangi nyingine, waliishi wakitegemea kula nyama ya kondoo ,walifanyiwa tohara na kukiri kuwa wao ni wayahudi walipoulizwa ,na iwapo walimkamata mwarabu(moor) walimchuna ngozi akiwa hai ,walikuwa maadui wakubwa na waarabu weusi, hapo chini ya mlima palikuwa na tenki la maji ,maji ambayo yalitokana na mvua, tukawanywesha ngamia wetu 16,000 kwa maji hayo, hao wayahudi wakachukia wakaanza kuuzunguka mlima wao kama mbuzi pori vichaa"

    Kipindi yesu anazaliwa alikuta Israel inatawaliwa na Waroma ambapo kama alivyotabiri baada ya Yesu kukataliwa na wayahudi na baadae kupaa kwenda mbinguni, kulitokea vita kwenye utawala wa Warumi vita hiyo ilipelekea kuharibiwa lile hekalu la Suleiman na wana wa Israel kuchukuliwa mateka utumwani na wengine kukimbilia hasa kusini mwa Israel "kush" au Afrika sababu huko hapakuwa na hiyo vita na ilikuwa rahisi wao kujificha kwa watu wa Kushi sababu walikuwa wanafanana nao ndio maana hii dhana ya hawa wayahudi wa ulaya imekuwa ni moja ya hoja kubwa sana ulimwenguni kivipi wayahudi walikimbilia Ulaya wakati vita ya Roman Empire ndio ilikuwa imetokea huko inashuka Israel ,wayahudi wengi walikimbilia Afrika sio ulaya, sio hawa wanaojiita Ashkenazi au Sephardim wala Mizrahim hawa asili yao ni uturuki, hawa ni wa-- "Khazarians" sio wayahudi wa asili, sio wayahudi waliotokea kwa Yakobo.

    Hata yesu alikuwa mwafrika ,kukua kwa vyombo vya habari pamoja na kumilikiwa na mataifa makubwa imepelekea duniani kote kuamini yesu ,malaika ,na manabii wote ni wazungu ,tukiangalia (Ufunuo 1:13--16) tunaona ,"....na katikati ya vile vinara nikaona mtu mfano wa mwanadamu amevaa vazi lililofika miguuni na kufungwa mshipi wa dhahabu matitini ,kichwa chake na nywele zake zilikuwa nyeupe kama sufu nyeupe, kama theluji na macho yake kama mwali wa moto ,na miguu yake kama shaba iliyosuguliwa sana, kama kwamba imesafishwa katika tanuru, na sauti yake kama sauti ya maji mengi " hapo Ufunuo unamuongelea Yesu( Nabii Issa)

    Tunaamini wayahudi waliopo sasa hivi sio kizazi kile cha Yakobo ,kutokana na sababu lukuki tutakazozielezea hivi punde, maandishi ya mwanzo yanaelezea wayahudi watachukuliwa utumwani na kutawanywa kila sehemu ya dunia na pia Yerusalem itatekwa na mataifa mpaka muda wa mataifa uliotimilizwa ,(Luka 21:5--24) tukiingalia tunaona hili taifa la leo la Israel lipo tofauti kabisa na hayo maandiko hapo juu ndio watu walioshikilia uchumi na utajiri mkubwa duniani ,karibia 60% ya matajiri wa dunia hii ni Waisrael, watu kama familia ya kina Rothschilds, wakati ndio watu wanaoongoza kwa kuanzisha Illuminati na Freemason na ibada nyingi sana duniani.

    Andiko la Torati 28:1--13 ,halipo kabisa kwa wayahudi wa sasa wa Israel ,ili mtu apate baraka za mungu anatakiwa afuate masharti ya Mungu ,hawa wamemuasi Mungu lakini ndio wanasemwa wamebarikiwa, kilichopo kwa hili taifa la Israel ni kinyume, wana wa Israel halisi bado wapo utumwani bado wanaishi maisha ya shida ,ufukara na umaskini zile laana za kumbukumbu la Torati 28 bado ziko juu yao sio hawa Walioko Israel kwa sasa wanaishi maisha ya anasa na utajiri mkubwa.

    Dhumuni la makala haya ni kuangalia muonekano wa wayahudi wa mwanzo walionekanaje, ndio hawa waliopo sasa hivi au kuna wengine? Tukiangalia historia ya biblia na Koran tunaona wayahudi walipokuwa wakiasi lazima laana ije juu yao ,ama hata kutokea kwa magonjwa kama tauni, ukoma ,nk au kupigwa vitani na taifa lao kuchukuliwa mateka na wakiwa huko wakimrudia mungu wao ,Mungu huwainulia nabii mmoja na huenda kuwarudisha kwenye nchi ya baba yao, nchi ya ahadi ,manabii kama Musa,Joshua,Samsoni,Eliya ,Elisha,nk walitumiwa na mungu kuwarudisha toka mateka au utumwani.

    Mei 14 mwaka 1948 wayahudi walirudishwa nchini mwao, haifahamiki kilitumiwa kigezo gani kutambua kuwa huyu ni myahudi na yule sio ,baada ya miaka 2000 hivi ya kupoteana , ni Mungu pekee tu anayeweza kuwatambua na ni pekee tu ndiye anayeweza kuwatambua na ni pekee atawarudisha pale sio hawa wazungu waliojirudisha wenyewe na kujitangaza wana wa Israel ,Luka 21---24 inasema Yerusalem itachukuliwa na kukaliwa na mataifa mpaka muda wa mataifa utakapotimilizwa na pia kitabu cha yeremia 23:5--6 kinasema wayahudi halisi hawatarudi katika nchi yao mpaka masihi yesu atakapokuja.

    Kitabu cha Ufunuo 2:9 kinasema"Naijua dhiki yako na umaskini wako ( Lakini u tajiri) najua na matukano ya hao wasemao ya kuwa ni wayahudi , na sio ,bali ni sinagogi la shetani " mstari huu unatuaminisha kwamba kuna wayahudi halisi na sio halisi ambao ni pandikizi la shetani ,mstari unaweka wazi, wayahudi halisi wapo kwenye dhiki, wapo kwenye umaskini ingawa ni matajiri( utajiri wa kiroho na kimwili) kwa sababu hawakulitii andiko la Torati 28.

    Hata hawa wa sasa wanaojiita Waisrael tunaona hawajawahi kupelekwa utumwani ,ni wayahudi weusi tu ndio wanajua adha ya utumwa ,ndio wao waliouzwa kwenye minada kama bidhaa, na kudhalilishwa na kuteswa na ndio watu waliotapakaa dunia nzima, wakitumika kama watumwa sehemu mbalimbali duniani, kwa sababu Luka 21:19;;24 inazungumzia wayahudi watapigwa na Wengi wataanguka kwa makali ya upanga na watachukuliwa utumwani katika mataifa yote , na Yerusalem itakaliwa na mataifa hata majira ya mataifa yatakapotimia ,mataifa hayo ndio yanayoikalia Israel sasa hivi.

    Sio kwamba watu weusi wote ni wayahudi ,au sio wayahudi ,wayahudi wana wa yakobo walikuwa weusi na kipindi kile watu weusi walikuwa wengi sana kuliko sasa hivi, baada ya ile gharika kuisha katika mstari wa 24 imeandikwa Yerusalem itakaliwa na watu wasio wayahudi mpaka muda utimie ,yaani yesu ( nabii Issa) atakaposhuka.

    Yeremia 23:5--8 Mungu atawatoa Waisrael toka pande zote duniani kuja kuishi Salama katika taifa lao na hawa wazungu wa ulaya kina Netanyau hawa sio Waisrael ndio maana kipigo chao kinaandaliwa ,ndio ile vita ya Armagedoni ya kwenye kitabu cha Ufunuo 16:13 upanga uliotajwa mule ndio maalum kwa Waisrael wa sasa hivi.

    Tunavigusa sana vitabu ili kukazia hoja na kuweka uhalisia juu ya makala haya, katika kitabu cha Ufunuo 7:17 kinaeleza watatumwa malaika wawawekee alama wale wayahudi halisi 144,000 watakaokuwepo duniani kipindi hicho ili wasipate kile kipigo kisichowahusu ,ndio maana kipigo chao kinaandaliwa miaka hii kwasababu tupo nyakati za mwisho , tuliona Urusi kapeleka majeshi Syria ,Marekani na mataifa mengine walipeleka tunaweza kudhani anayepigwa ni Syria ,kibao kitageuka na wale wanaojiita waisrael ndio watakaopata kipigo hicho.

    Tunaamini Waisrael wa sasa sio, kwa kukazia hoja kupitia Vitabu kadhaa ,katika kitabu cha mwanzo Yakobo alioa wake wawili ,Leah na Rachel ,akazaa na vijakazi wawili kwa kila wake zake ,wa Leah ,aliitwa Zilpha aliyemzaa Gadi na Asheri na wa Rachel aliitwa Bilhah aliyemzaa Dani na Naftari kipindi kile wajakazi walitoka Afrika ( kushi) kama alivyokuwa mke wa Musa ,Zupporah, Hesabu 12:1 katika kabila 12 za Israel walikuwa ni watu wa rangi mbalimbali walikuwa ni watu mchanganyiko sio wazungu ( Albinos).

    Tukimwangalia Ayubu 30:30 anaielezea rangi yake ilivyo "anasema" Ngozi yangu ni nyeusi ,nayo yanitoka ,Na mifupa yangu ineteketea kwa hari, " Hata kwenye wimbo ulio bora 1:5 mfalme Suleiman anajielezea rangi yake ilivyo anasema " Mimi ni mweusi -mweusi ,lakini ninao uzuri ,enyi binti wa Yerusalem ,mfano wa hewa za Kedari ,kama mapazia yake Suleiman " Tukumbuke mtu mweusi akipata shida ama ya hali ya hewa, au mateso ule weusi wake huongezeka maradufu na akiwa na raha weusi wake hung'aa.

    Katika wimbo ulio bora 1:6 tunasoma, " msinichunguze kwa kuwa ni mweusi ,kwa sababu jua limeniunguza. ,wana wa mama yangu walinikasirikia wameniweka niwe mlinzi wa mashamba ya mizabibu ,bali shamba langu mwenyewe sikulilinda, Hata tukiangalia kitabu cha 2 Maombolezo 4:8 "Nyuso zao ni nyeusi kwasababu ya hali ya hewa kuliko makaa ,hawajulikani katika njia kuu, ngozi yao yagandamana na mifupa yao imekauka ,imekuwa kama mti " Pia 3 maombolezo 5:10 inaelezea " Ngozi yetu ni nyeusi kama tanuru kwa sababu ya hali ya njaa ituteketezayo" Humu kwenye Vitabu vitakatifu hakuna kifungu chenye historia ya ngozi nyeupe kwasababu mtu mweusi ndiye aliyeijaza dunia.

    Wakati mzee Yakobo alipowatuma watoto wake kwenda Misri kununua mikate walipomkuta Yusufu ndugu yao, walishindwa kumtambua kwa kuwa anafanana na wamisri na wamisri walikuwa weusi sio wazungu. Walishindwa kumtambua ndugu yao. Hata Yusufu na maria waliposikia Kwamba Herode anataka kumuua mtoto yesu walikimbilia kumficha huko Misri mpaka Herode alipofariki kwasababu wayahudi walikuwa wanafananana rangi na wamisri na vibao vilivyovumbuliwa miaka ya karibu vilionyesha walikuwa watu wanaotembeleana , itakuwa kichekesho miaka hii mtanzania akimbilie China kwa nia ya kujificha wakati hafanani na wachina , ndio maana wayahudi wengi sana walikuwa wanakimbilia kusini mwa Israel ,Misri na Kush kujificha sababu walikuwa wanafanana na watu wa huko kuanzia rangi ya ngozi zao mpaka maumbo yao.

    Ukweli filamu za Nuhu, Yesu, Samsoni, Musa nk zinazoonyesha wayahudi ni wazungu ndio kitu kinachofanya wengi tumaini,tunaweza kujiuliza kama studio zote za Hollywood zlizorekodi filamu hizo kwa nini wasijipendelee muonekano na maumbile yao ?(English figure) watoto wa Abraham wasingeweza kutoa mateso kwa wapalestina wa sasa ambao kila siku watoto wao na wanawake wa kipalestina wanapoteza maisha na wengine kujeruhiwa ,utafiti wa mwaka 1980 uligundua kwamba wengi wa wayahudi waliopo Israel asili yao ni uturuki, karibu asilimia 98 ya wayahudi hao hawakuwa wayahudi halisia.

    Katika vitabu pia kwa kutaja vichache ili kupunguza urefu wa makala , kuna watu kama Henry Ford, ambaye sio myahudi Lakini alifanya utafiti kuhusu wayahudi akagundua hawa wanaojiita wayahudi sio wayahudi halisi akaandika kitabu chake cha "International Jews". Haitoshi nae John Beaty kaandika kitabu kinaitwa " The Iron Curtain over America" kuzungumzia uhalisia wa wayahudi ,Aidha naye Col. Curtis B. Dall kaandika kitabu chake ," Israel Five Trililion Dollar Secret " tukija kwa mwanazuoni mwingine ,Arthur Koestler kaandika kitabu, "Thirteen Tribes Book" huyu hapa anamaanisha wao ni kabila la 13 badala ya yale 12 ya wayahudi wa Israel, vinginevyo ni pamoja na kile cha;Freedman , na Shlomo Sands.

    Ushahidi mwingine ili kukazia hoja hii ni kwenye kitabu cha Walawi katika Agano la kale hii ni katika kuthibitisha kwamba Agano la kale wahusika walikuwa waafrika na sio filamu za Hollywood, ambapo tunaona Walawi sura ya 13, 1--10 ,Mungu anawapiga ukoma Waisrael walipoamua kumuasi, walipopigwa ukoma ngozi yao nyeusi ilibadilika kuwa nyeupe ,vinyweleo vyao vinabadilika toka weusi na kuwa vyeupe. Mtu mweupe akipata ukoma huwezi kumtambua sababu ngozi yake ya ndani na nje Zipo sawasawa, ( hakuna melanin) lakini mtu mweusi tu ana rangi tofauti ya nje na ya ndani ,ndio maana anaitwa " coloured people " yaani wengi ni watu wa rangi mbalimbali, Aidha mtu mweusi anaweza akabadili rangi yake nyeusi kuwa nyeupe hata kwa (mkorogo) lakini mweupe hawezi kujibadili rangi yake kuwa nyeusi.

    Ndio maana mweusi akiungua moto ngozi yake inakuwa nyeupe kama kapigwa ukoma ,Kwenye walawi 13:4 tunasoma " kama vinyweleo ( malaika) havigeuki rangi kutoka vyeusi kuwa nyeupe basi huo sio ukoma " hizi ni dalili mungu alikuwa anawaambia makuhani wa Israel jinsi ya kuutambua ukoma katika jamii zao, na jinsi ya kuutibu. Kwa Waisrael wa sasa hili andiko haliwahusu , Waisrael wa sasa wanavinyweleo na ngozi tofauti kabisa ndio maana wa sasa akijitokeza mtu na kuhoji au Kuchambua walipotokea wana kusema kuwa unaanza kuleta Ubaguzi.

    Samson kwenye kitabu cha Waamuzi 16:13 kinasema ,Mungu alimuibua Nabii aliyeitwa Samson baada ya kuwaweka wana wa Israel mikononi mwa wafilisti kwa miaka 40 , alimleta baada ya Waisrael kutubu dhambi zao, tukiangalia nywele za Samson zilikuwa ndefu na zenye vishungi ( Dreadlocks) kwa sasa tunaweza kumwita alikuwa ni Rastafari wa kipindi hicho, na ndio chimbuko la marastafari walianzia hapa, kwamba mtu mweusi akiacha nywele zake bila kuzikata zinatengeneza vishungi ,za mzungu haziwezi wala hazishikamani kama walivyo weusi, kuna utofauti kati ya Rastafari mweusi na yule wa kizungu katika nywele zao
    NINI ASILI YA WAYAHUDI WA LEO NCHINI ISRAEL? ,UKWELI WA MUONEKANO WAO NA HATIMA YA UTAWALA WAO. TUKUMBUKE Rais wa Misri wa pili wa zamani wa Umoja wa Jamhuri ya waarabu Gamal Abdel Nasser mwaka 1952 alishawahi kusema mbele ya Televisheni kwamba, watu wa ulaya wanajidai kuwa wao ni wayahudi akasema kwamba; siwezi kuwaheshimu wayahudi nyie wayahudi hamtaweza kuishi kwa amani kwasababu mliondoka hapa mkiwa weusi mkarudi mkiwa weupe. Msafiri wa kiitalia Ludovico di Varthema mwaka 1470 hadi mwaka 1517 alijulikana kama mtu wa kwanza Ulaya asiye muislam kuingia Makka kuhiji, karibu kila kitu kinachomuhusu maisha yake kimeandikwa katika kitabu cha "Itinerario de Ludovicode Varthema Bolognese" kilichapishwa Roma mwaka 1510. Moja ya kurasa zake unasomeka ;"mwisho wa siku 8 tukakuta mlima unaoonekana kuwa maili 10 au 12 hivi kwa mzunguko katika mlima huo paliishi wayahudi elfu nne au tano hivi waliokuwa wanatembea bila nguo na viganja vyao vipana, wenye sauti zinazofanana na zile za kike, walikuwa weusi zaidi kuliko rangi nyingine, waliishi wakitegemea kula nyama ya kondoo ,walifanyiwa tohara na kukiri kuwa wao ni wayahudi walipoulizwa ,na iwapo walimkamata mwarabu(moor) walimchuna ngozi akiwa hai ,walikuwa maadui wakubwa na waarabu weusi, hapo chini ya mlima palikuwa na tenki la maji ,maji ambayo yalitokana na mvua, tukawanywesha ngamia wetu 16,000 kwa maji hayo, hao wayahudi wakachukia wakaanza kuuzunguka mlima wao kama mbuzi pori vichaa" Kipindi yesu anazaliwa alikuta Israel inatawaliwa na Waroma ambapo kama alivyotabiri baada ya Yesu kukataliwa na wayahudi na baadae kupaa kwenda mbinguni, kulitokea vita kwenye utawala wa Warumi vita hiyo ilipelekea kuharibiwa lile hekalu la Suleiman na wana wa Israel kuchukuliwa mateka utumwani na wengine kukimbilia hasa kusini mwa Israel "kush" au Afrika sababu huko hapakuwa na hiyo vita na ilikuwa rahisi wao kujificha kwa watu wa Kushi sababu walikuwa wanafanana nao ndio maana hii dhana ya hawa wayahudi wa ulaya imekuwa ni moja ya hoja kubwa sana ulimwenguni kivipi wayahudi walikimbilia Ulaya wakati vita ya Roman Empire ndio ilikuwa imetokea huko inashuka Israel ,wayahudi wengi walikimbilia Afrika sio ulaya, sio hawa wanaojiita Ashkenazi au Sephardim wala Mizrahim hawa asili yao ni uturuki, hawa ni wa-- "Khazarians" sio wayahudi wa asili, sio wayahudi waliotokea kwa Yakobo. Hata yesu alikuwa mwafrika ,kukua kwa vyombo vya habari pamoja na kumilikiwa na mataifa makubwa imepelekea duniani kote kuamini yesu ,malaika ,na manabii wote ni wazungu ,tukiangalia (Ufunuo 1:13--16) tunaona ,"....na katikati ya vile vinara nikaona mtu mfano wa mwanadamu amevaa vazi lililofika miguuni na kufungwa mshipi wa dhahabu matitini ,kichwa chake na nywele zake zilikuwa nyeupe kama sufu nyeupe, kama theluji na macho yake kama mwali wa moto ,na miguu yake kama shaba iliyosuguliwa sana, kama kwamba imesafishwa katika tanuru, na sauti yake kama sauti ya maji mengi " hapo Ufunuo unamuongelea Yesu( Nabii Issa) Tunaamini wayahudi waliopo sasa hivi sio kizazi kile cha Yakobo ,kutokana na sababu lukuki tutakazozielezea hivi punde, maandishi ya mwanzo yanaelezea wayahudi watachukuliwa utumwani na kutawanywa kila sehemu ya dunia na pia Yerusalem itatekwa na mataifa mpaka muda wa mataifa uliotimilizwa ,(Luka 21:5--24) tukiingalia tunaona hili taifa la leo la Israel lipo tofauti kabisa na hayo maandiko hapo juu ndio watu walioshikilia uchumi na utajiri mkubwa duniani ,karibia 60% ya matajiri wa dunia hii ni Waisrael, watu kama familia ya kina Rothschilds, wakati ndio watu wanaoongoza kwa kuanzisha Illuminati na Freemason na ibada nyingi sana duniani. Andiko la Torati 28:1--13 ,halipo kabisa kwa wayahudi wa sasa wa Israel ,ili mtu apate baraka za mungu anatakiwa afuate masharti ya Mungu ,hawa wamemuasi Mungu lakini ndio wanasemwa wamebarikiwa, kilichopo kwa hili taifa la Israel ni kinyume, wana wa Israel halisi bado wapo utumwani bado wanaishi maisha ya shida ,ufukara na umaskini zile laana za kumbukumbu la Torati 28 bado ziko juu yao sio hawa Walioko Israel kwa sasa wanaishi maisha ya anasa na utajiri mkubwa. Dhumuni la makala haya ni kuangalia muonekano wa wayahudi wa mwanzo walionekanaje, ndio hawa waliopo sasa hivi au kuna wengine? Tukiangalia historia ya biblia na Koran tunaona wayahudi walipokuwa wakiasi lazima laana ije juu yao ,ama hata kutokea kwa magonjwa kama tauni, ukoma ,nk au kupigwa vitani na taifa lao kuchukuliwa mateka na wakiwa huko wakimrudia mungu wao ,Mungu huwainulia nabii mmoja na huenda kuwarudisha kwenye nchi ya baba yao, nchi ya ahadi ,manabii kama Musa,Joshua,Samsoni,Eliya ,Elisha,nk walitumiwa na mungu kuwarudisha toka mateka au utumwani. Mei 14 mwaka 1948 wayahudi walirudishwa nchini mwao, haifahamiki kilitumiwa kigezo gani kutambua kuwa huyu ni myahudi na yule sio ,baada ya miaka 2000 hivi ya kupoteana , ni Mungu pekee tu anayeweza kuwatambua na ni pekee tu ndiye anayeweza kuwatambua na ni pekee atawarudisha pale sio hawa wazungu waliojirudisha wenyewe na kujitangaza wana wa Israel ,Luka 21---24 inasema Yerusalem itachukuliwa na kukaliwa na mataifa mpaka muda wa mataifa utakapotimilizwa na pia kitabu cha yeremia 23:5--6 kinasema wayahudi halisi hawatarudi katika nchi yao mpaka masihi yesu atakapokuja. Kitabu cha Ufunuo 2:9 kinasema"Naijua dhiki yako na umaskini wako ( Lakini u tajiri) najua na matukano ya hao wasemao ya kuwa ni wayahudi , na sio ,bali ni sinagogi la shetani " mstari huu unatuaminisha kwamba kuna wayahudi halisi na sio halisi ambao ni pandikizi la shetani ,mstari unaweka wazi, wayahudi halisi wapo kwenye dhiki, wapo kwenye umaskini ingawa ni matajiri( utajiri wa kiroho na kimwili) kwa sababu hawakulitii andiko la Torati 28. Hata hawa wa sasa wanaojiita Waisrael tunaona hawajawahi kupelekwa utumwani ,ni wayahudi weusi tu ndio wanajua adha ya utumwa ,ndio wao waliouzwa kwenye minada kama bidhaa, na kudhalilishwa na kuteswa na ndio watu waliotapakaa dunia nzima, wakitumika kama watumwa sehemu mbalimbali duniani, kwa sababu Luka 21:19;;24 inazungumzia wayahudi watapigwa na Wengi wataanguka kwa makali ya upanga na watachukuliwa utumwani katika mataifa yote , na Yerusalem itakaliwa na mataifa hata majira ya mataifa yatakapotimia ,mataifa hayo ndio yanayoikalia Israel sasa hivi. Sio kwamba watu weusi wote ni wayahudi ,au sio wayahudi ,wayahudi wana wa yakobo walikuwa weusi na kipindi kile watu weusi walikuwa wengi sana kuliko sasa hivi, baada ya ile gharika kuisha katika mstari wa 24 imeandikwa Yerusalem itakaliwa na watu wasio wayahudi mpaka muda utimie ,yaani yesu ( nabii Issa) atakaposhuka. Yeremia 23:5--8 Mungu atawatoa Waisrael toka pande zote duniani kuja kuishi Salama katika taifa lao na hawa wazungu wa ulaya kina Netanyau hawa sio Waisrael ndio maana kipigo chao kinaandaliwa ,ndio ile vita ya Armagedoni ya kwenye kitabu cha Ufunuo 16:13 upanga uliotajwa mule ndio maalum kwa Waisrael wa sasa hivi. Tunavigusa sana vitabu ili kukazia hoja na kuweka uhalisia juu ya makala haya, katika kitabu cha Ufunuo 7:17 kinaeleza watatumwa malaika wawawekee alama wale wayahudi halisi 144,000 watakaokuwepo duniani kipindi hicho ili wasipate kile kipigo kisichowahusu ,ndio maana kipigo chao kinaandaliwa miaka hii kwasababu tupo nyakati za mwisho , tuliona Urusi kapeleka majeshi Syria ,Marekani na mataifa mengine walipeleka tunaweza kudhani anayepigwa ni Syria ,kibao kitageuka na wale wanaojiita waisrael ndio watakaopata kipigo hicho. Tunaamini Waisrael wa sasa sio, kwa kukazia hoja kupitia Vitabu kadhaa ,katika kitabu cha mwanzo Yakobo alioa wake wawili ,Leah na Rachel ,akazaa na vijakazi wawili kwa kila wake zake ,wa Leah ,aliitwa Zilpha aliyemzaa Gadi na Asheri na wa Rachel aliitwa Bilhah aliyemzaa Dani na Naftari kipindi kile wajakazi walitoka Afrika ( kushi) kama alivyokuwa mke wa Musa ,Zupporah, Hesabu 12:1 katika kabila 12 za Israel walikuwa ni watu wa rangi mbalimbali walikuwa ni watu mchanganyiko sio wazungu ( Albinos). Tukimwangalia Ayubu 30:30 anaielezea rangi yake ilivyo "anasema" Ngozi yangu ni nyeusi ,nayo yanitoka ,Na mifupa yangu ineteketea kwa hari, " Hata kwenye wimbo ulio bora 1:5 mfalme Suleiman anajielezea rangi yake ilivyo anasema " Mimi ni mweusi -mweusi ,lakini ninao uzuri ,enyi binti wa Yerusalem ,mfano wa hewa za Kedari ,kama mapazia yake Suleiman " Tukumbuke mtu mweusi akipata shida ama ya hali ya hewa, au mateso ule weusi wake huongezeka maradufu na akiwa na raha weusi wake hung'aa. Katika wimbo ulio bora 1:6 tunasoma, " msinichunguze kwa kuwa ni mweusi ,kwa sababu jua limeniunguza. ,wana wa mama yangu walinikasirikia wameniweka niwe mlinzi wa mashamba ya mizabibu ,bali shamba langu mwenyewe sikulilinda, Hata tukiangalia kitabu cha 2 Maombolezo 4:8 "Nyuso zao ni nyeusi kwasababu ya hali ya hewa kuliko makaa ,hawajulikani katika njia kuu, ngozi yao yagandamana na mifupa yao imekauka ,imekuwa kama mti " Pia 3 maombolezo 5:10 inaelezea " Ngozi yetu ni nyeusi kama tanuru kwa sababu ya hali ya njaa ituteketezayo" Humu kwenye Vitabu vitakatifu hakuna kifungu chenye historia ya ngozi nyeupe kwasababu mtu mweusi ndiye aliyeijaza dunia. Wakati mzee Yakobo alipowatuma watoto wake kwenda Misri kununua mikate walipomkuta Yusufu ndugu yao, walishindwa kumtambua kwa kuwa anafanana na wamisri na wamisri walikuwa weusi sio wazungu. Walishindwa kumtambua ndugu yao. Hata Yusufu na maria waliposikia Kwamba Herode anataka kumuua mtoto yesu walikimbilia kumficha huko Misri mpaka Herode alipofariki kwasababu wayahudi walikuwa wanafananana rangi na wamisri na vibao vilivyovumbuliwa miaka ya karibu vilionyesha walikuwa watu wanaotembeleana , itakuwa kichekesho miaka hii mtanzania akimbilie China kwa nia ya kujificha wakati hafanani na wachina , ndio maana wayahudi wengi sana walikuwa wanakimbilia kusini mwa Israel ,Misri na Kush kujificha sababu walikuwa wanafanana na watu wa huko kuanzia rangi ya ngozi zao mpaka maumbo yao. Ukweli filamu za Nuhu, Yesu, Samsoni, Musa nk zinazoonyesha wayahudi ni wazungu ndio kitu kinachofanya wengi tumaini,tunaweza kujiuliza kama studio zote za Hollywood zlizorekodi filamu hizo kwa nini wasijipendelee muonekano na maumbile yao ?(English figure) watoto wa Abraham wasingeweza kutoa mateso kwa wapalestina wa sasa ambao kila siku watoto wao na wanawake wa kipalestina wanapoteza maisha na wengine kujeruhiwa ,utafiti wa mwaka 1980 uligundua kwamba wengi wa wayahudi waliopo Israel asili yao ni uturuki, karibu asilimia 98 ya wayahudi hao hawakuwa wayahudi halisia. Katika vitabu pia kwa kutaja vichache ili kupunguza urefu wa makala , kuna watu kama Henry Ford, ambaye sio myahudi Lakini alifanya utafiti kuhusu wayahudi akagundua hawa wanaojiita wayahudi sio wayahudi halisi akaandika kitabu chake cha "International Jews". Haitoshi nae John Beaty kaandika kitabu kinaitwa " The Iron Curtain over America" kuzungumzia uhalisia wa wayahudi ,Aidha naye Col. Curtis B. Dall kaandika kitabu chake ," Israel Five Trililion Dollar Secret " tukija kwa mwanazuoni mwingine ,Arthur Koestler kaandika kitabu, "Thirteen Tribes Book" huyu hapa anamaanisha wao ni kabila la 13 badala ya yale 12 ya wayahudi wa Israel, vinginevyo ni pamoja na kile cha;Freedman , na Shlomo Sands. Ushahidi mwingine ili kukazia hoja hii ni kwenye kitabu cha Walawi katika Agano la kale hii ni katika kuthibitisha kwamba Agano la kale wahusika walikuwa waafrika na sio filamu za Hollywood, ambapo tunaona Walawi sura ya 13, 1--10 ,Mungu anawapiga ukoma Waisrael walipoamua kumuasi, walipopigwa ukoma ngozi yao nyeusi ilibadilika kuwa nyeupe ,vinyweleo vyao vinabadilika toka weusi na kuwa vyeupe. Mtu mweupe akipata ukoma huwezi kumtambua sababu ngozi yake ya ndani na nje Zipo sawasawa, ( hakuna melanin) lakini mtu mweusi tu ana rangi tofauti ya nje na ya ndani ,ndio maana anaitwa " coloured people " yaani wengi ni watu wa rangi mbalimbali, Aidha mtu mweusi anaweza akabadili rangi yake nyeusi kuwa nyeupe hata kwa (mkorogo) lakini mweupe hawezi kujibadili rangi yake kuwa nyeusi. Ndio maana mweusi akiungua moto ngozi yake inakuwa nyeupe kama kapigwa ukoma ,Kwenye walawi 13:4 tunasoma " kama vinyweleo ( malaika) havigeuki rangi kutoka vyeusi kuwa nyeupe basi huo sio ukoma " hizi ni dalili mungu alikuwa anawaambia makuhani wa Israel jinsi ya kuutambua ukoma katika jamii zao, na jinsi ya kuutibu. Kwa Waisrael wa sasa hili andiko haliwahusu , Waisrael wa sasa wanavinyweleo na ngozi tofauti kabisa ndio maana wa sasa akijitokeza mtu na kuhoji au Kuchambua walipotokea wana kusema kuwa unaanza kuleta Ubaguzi. Samson kwenye kitabu cha Waamuzi 16:13 kinasema ,Mungu alimuibua Nabii aliyeitwa Samson baada ya kuwaweka wana wa Israel mikononi mwa wafilisti kwa miaka 40 , alimleta baada ya Waisrael kutubu dhambi zao, tukiangalia nywele za Samson zilikuwa ndefu na zenye vishungi ( Dreadlocks) kwa sasa tunaweza kumwita alikuwa ni Rastafari wa kipindi hicho, na ndio chimbuko la marastafari walianzia hapa, kwamba mtu mweusi akiacha nywele zake bila kuzikata zinatengeneza vishungi ,za mzungu haziwezi wala hazishikamani kama walivyo weusi, kuna utofauti kati ya Rastafari mweusi na yule wa kizungu katika nywele zao
    Like
    1
    0 Commenti 0 condivisioni 3K Views
  • Kutoka kwa Rapa bora kwa sasa hivi na mwenye mvuto kwa maneno ya Juma Lokole

    "Lile cheko baada ya kujua watu wangu wa nguvu wanaenjoy ngoma kali kutoka kwa EP,Kama hujapata nafasi ya kusikiliza pata muda bonyeza Link juu ya Bio

    kwetu sigara inawashwa na Pilipili,Mama alinifunza vitu viwili kutumia Pesa kutumia akili " - Rose Ndauka, Mwigizaji wa filamu wa muda mrefu na Msanii wa muziki wa Hip-hop kwa sasa hivi.

    Kutoka kwa Rapa bora kwa sasa hivi na mwenye mvuto kwa maneno ya Juma Lokole 😂 "Lile cheko baada ya kujua watu wangu wa nguvu wanaenjoy ngoma kali kutoka kwa EP,Kama hujapata nafasi ya kusikiliza pata muda bonyeza Link juu ya Bio kwetu sigara inawashwa na Pilipili,Mama alinifunza vitu viwili kutumia Pesa kutumia akili 🔥🔥🔥🔥" - Rose Ndauka, Mwigizaji wa filamu wa muda mrefu na Msanii wa muziki wa Hip-hop kwa sasa hivi.
    Love
    1
    0 Commenti 0 condivisioni 336 Views
  • Baada ya Mwigizaji wa filamu wa muda mrefu Tanzania, Rose Ndauka kutoa EP yake mpya ya muziki wa Hip-hop, Wanzengo wamemshambulia kwenye mitandao ya jamii. Msanii huyo ameshindwa kuvumilia na kuwajibu kama inavyoonekana pichani.

    Baada ya Mwigizaji wa filamu wa muda mrefu Tanzania, Rose Ndauka kutoa EP yake mpya ya muziki wa Hip-hop, Wanzengo wamemshambulia kwenye mitandao ya jamii. Msanii huyo ameshindwa kuvumilia na kuwajibu kama inavyoonekana pichani.
    0 Commenti 0 condivisioni 177 Views
  • "Pole yenu mnaodhani mimi ni mgumba sina mtoto sina kizazi, kwa taarifa yenu ni kwamba nina Mtoto mmoja ana miaka nane (8)"- Johari, Mwigizaji wa filamu Tanzania.

    "Pole yenu mnaodhani mimi ni mgumba sina mtoto sina kizazi, kwa taarifa yenu ni kwamba nina Mtoto mmoja ana miaka nane (8)"- Johari, Mwigizaji wa filamu Tanzania.
    Like
    2
    0 Commenti 0 condivisioni 121 Views