• Stress-Free Airport Travel for Seniors

    Make every journey comfortable with our Senior Citizen Travel Support.
    We provide wheelchair assistance, meet & assist service, baggage help, and priority airport support for a smooth travel experience.

    Book Senior Travel Assistance Today!
    www.jodogoairportassist.com
    +1(325) 225 5550

    #SeniorTravelSupport #AirportAssist #WheelchairAssistance #SeniorFriendlyTravel
    #AirportAssistance #LHR #DXB #AUH #LAX #ICN #DFW #ORD #DEL #MIA #Jeddah #RUH #EWR #JFK #MobilitySupport #TravelWithCare #HassleFreeTravel #AirportSupport #JodogoAirportAssist
    ✈️ Stress-Free Airport Travel for Seniors Make every journey comfortable with our Senior Citizen Travel Support. We provide wheelchair assistance, meet & assist service, baggage help, and priority airport support for a smooth travel experience. Book Senior Travel Assistance Today! 🌐 www.jodogoairportassist.com 📞 +1(325) 225 5550 #SeniorTravelSupport #AirportAssist #WheelchairAssistance #SeniorFriendlyTravel #AirportAssistance #LHR #DXB #AUH #LAX #ICN #DFW #ORD #DEL #MIA #Jeddah #RUH #EWR #JFK #MobilitySupport #TravelWithCare #HassleFreeTravel #AirportSupport #JodogoAirportAssist ✈️
    0 Commenti 0 condivisioni 27 Views
  • Ramadhani na Kwaresma: Msimu wa tafakari kwa Waumini Duniani.

    Kwa sasa, Waumini wa dini mbili kubwa duniani wanaishi katika kipindi muhimu cha kiroho, Waislamu wako ndani ya mfungo wa Ramadhani huku Wakristo wakitekeleza Kwaresma. Hiki ni kipindi ambacho kinahusisha kujinyima, kutafakari na kujisafisha kiroho.

    Kwaresma ni nini?

    Kwaresma ni kipindi cha siku 40 kwa Wakristo, kinachoanza rasmi Jumatano ya Majivu na kumalizika Jumapili ya Pasaka. Hata hivyo, Wakristo hawafungi siku za Jumapili katika kipindi hiki.

    Katika kipindi hiki, Waumini wanahimizwa kufanya toba, kujitathmini na kujizuia na matendo mabaya. Kufunga ni wajibu kwa baadhi ya siku maalum pekee.

    “Kufunga ni lazima tu kwa waumini siku ya Jumatano ya Majivu na Ijumaa Kuu.”

    Wanaofunga katika siku hizo huruhusiwa kula mlo mmoja kwa siku.

    Ramadhani ni nini?

    Kwa upande wa Uislamu, Ramadhani ni mwezi mtakatifu wa kufunga ambao hudumu kwa siku 29 au 30 kulingana na mwandamo wa mwezi katika kalenda ya Kiislamu.

    Kufunga katika Ramadhani ni nguzo ya nne kati ya nguzo tano za Uislamu.

    “Nguzo nyingine ni kukiri Mungu ni mmoja, kusali mara tano kwa siku, kutoa zaka kwa mwenye uwezo na kuhiji katika Mji mtakatifu wa Makka angalau mara moja katika maisha.”

    Katika mwezi huu, Waislamu huanza siku yao kwa kula kabla ya alfajiri, mlo unaojulikana kama daku.

    “Waislamu hula chakula cha mwisho kabla jua kuchomoza, kinachoitwa daku.”

    Kuanzia alfajiri hadi machweo: “Wakati wa mchana, hawatakiwi kula au kunywa chochote au kuvuta sigara au tumbaku pamoja na kuzuiwa kunywa maji au kufanya ngono.”

    Saumu hufunguliwa jioni kwa mlo uitwao futari.

    Msamaha wa Kufunga

    Sio kila Muislamu analazimika kufunga. Wapo waliosamehewa kwa sababu za kiafya au hali maalum za maisha.

    “Baadhi ya Waislamu wamesamehewa kufunga, mfano Wanawake wajawazito au wanaonyonyesha na Wanawake walio katika hedhi.”

    “Wengine ni Wagonjwa au ambao afya zao zinaweza kuathiriwa na kufunga na watu wanaosafiri.”

    Katika hali hizi: “Watatakiwa kulipa funga zao au kulisha masikini.”

    Tofauti kuu lakini lengo lilelile

    Ingawa Ramadhani na Kwaresma zinatofautiana katika utekelezaji, zote zina msingi mmoja kujinyima, toba, na kujenga ukaribu na Mungu.

    Ni kipindi kinachowakumbusha Waumini umuhimu wa nidhamu ya kiroho, huruma kwa wahitaji, na maisha yenye maadili.

    Toa maoni yako
    #Habari
    Ramadhani na Kwaresma: Msimu wa tafakari kwa Waumini Duniani. Kwa sasa, Waumini wa dini mbili kubwa duniani wanaishi katika kipindi muhimu cha kiroho, Waislamu wako ndani ya mfungo wa Ramadhani huku Wakristo wakitekeleza Kwaresma. Hiki ni kipindi ambacho kinahusisha kujinyima, kutafakari na kujisafisha kiroho. Kwaresma ni nini? Kwaresma ni kipindi cha siku 40 kwa Wakristo, kinachoanza rasmi Jumatano ya Majivu na kumalizika Jumapili ya Pasaka. Hata hivyo, Wakristo hawafungi siku za Jumapili katika kipindi hiki. Katika kipindi hiki, Waumini wanahimizwa kufanya toba, kujitathmini na kujizuia na matendo mabaya. Kufunga ni wajibu kwa baadhi ya siku maalum pekee. “Kufunga ni lazima tu kwa waumini siku ya Jumatano ya Majivu na Ijumaa Kuu.” Wanaofunga katika siku hizo huruhusiwa kula mlo mmoja kwa siku. Ramadhani ni nini? Kwa upande wa Uislamu, Ramadhani ni mwezi mtakatifu wa kufunga ambao hudumu kwa siku 29 au 30 kulingana na mwandamo wa mwezi katika kalenda ya Kiislamu. Kufunga katika Ramadhani ni nguzo ya nne kati ya nguzo tano za Uislamu. “Nguzo nyingine ni kukiri Mungu ni mmoja, kusali mara tano kwa siku, kutoa zaka kwa mwenye uwezo na kuhiji katika Mji mtakatifu wa Makka angalau mara moja katika maisha.” Katika mwezi huu, Waislamu huanza siku yao kwa kula kabla ya alfajiri, mlo unaojulikana kama daku. “Waislamu hula chakula cha mwisho kabla jua kuchomoza, kinachoitwa daku.” Kuanzia alfajiri hadi machweo: “Wakati wa mchana, hawatakiwi kula au kunywa chochote au kuvuta sigara au tumbaku pamoja na kuzuiwa kunywa maji au kufanya ngono.” Saumu hufunguliwa jioni kwa mlo uitwao futari. Msamaha wa Kufunga Sio kila Muislamu analazimika kufunga. Wapo waliosamehewa kwa sababu za kiafya au hali maalum za maisha. “Baadhi ya Waislamu wamesamehewa kufunga, mfano Wanawake wajawazito au wanaonyonyesha na Wanawake walio katika hedhi.” “Wengine ni Wagonjwa au ambao afya zao zinaweza kuathiriwa na kufunga na watu wanaosafiri.” Katika hali hizi: “Watatakiwa kulipa funga zao au kulisha masikini.” Tofauti kuu lakini lengo lilelile Ingawa Ramadhani na Kwaresma zinatofautiana katika utekelezaji, zote zina msingi mmoja kujinyima, toba, na kujenga ukaribu na Mungu. Ni kipindi kinachowakumbusha Waumini umuhimu wa nidhamu ya kiroho, huruma kwa wahitaji, na maisha yenye maadili. Toa maoni yako #Habari
    0 Commenti 0 condivisioni 205 Views
  • DRC na Burundi zafungua rasmi mpaka wa Kavimvira–Gatumba.

    Leo hii Februari 23, 2026, Mpaka wa Kavimvira–Gatumba unaounganisha Nchi za Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na Burundi umefunguliwa rasmi kuanzia asubuhi hii, katika hatua inayotajwa kuwa muhimu kwa uhusiano wa kikanda na ushirikiano wa kiuchumi kati ya mataifa hayo mawili.

    Ufunguzi huo unafuatia kipindi cha kusubiri kilichosababisha kusimama kwa sehemu ya shughuli za usafirishaji na biashara mpakani. Mamlaka za pande zote mbili zimesema hatua hiyo inalenga kurejesha hali ya kawaida katika mzunguko wa watu na bidhaa.

    Kwa mujibu wa taarifa za awali, kufunguliwa kwa mpaka huo kutaruhusu:

    - Kurejea kwa shughuli za kawaida za kibiashara

    - Kuimarika kwa usafiri wa wananchi wanaovuka mpaka

    - Kuongezeka kwa ubadilishanaji wa bidhaa na huduma

    - Kuimarisha uhusiano wa kijamii na kiuchumi kati ya jamii za mpakani

    Mashuhuda katika eneo la mpakani wameripoti kuongezeka kwa idadi ya Wasafiri na Wafanyabiashara tangu saa za mapema asubuhi, huku malori ya mizigo na mabasi yakianza kuvuka kwa utaratibu wa kawaida.

    Hata hivyo, mamlaka zimehimiza wananchi kuzingatia sheria na taratibu za mipakani ili kuhakikisha usalama na uendeshaji mzuri wa shughuli zote.

    Wachambuzi wa masuala ya kikanda wanasema hatua hiyo inaweza kuchochea ukuaji wa uchumi katika ukanda wa Maziwa Makuu, hususan kwa jamii zinazotegemea biashara ya kuvuka mpaka kati ya DRC na Burundi.

    Toa maoni yako
    #Habari
    DRC na Burundi zafungua rasmi mpaka wa Kavimvira–Gatumba. Leo hii Februari 23, 2026, Mpaka wa Kavimvira–Gatumba unaounganisha Nchi za Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na Burundi umefunguliwa rasmi kuanzia asubuhi hii, katika hatua inayotajwa kuwa muhimu kwa uhusiano wa kikanda na ushirikiano wa kiuchumi kati ya mataifa hayo mawili. Ufunguzi huo unafuatia kipindi cha kusubiri kilichosababisha kusimama kwa sehemu ya shughuli za usafirishaji na biashara mpakani. Mamlaka za pande zote mbili zimesema hatua hiyo inalenga kurejesha hali ya kawaida katika mzunguko wa watu na bidhaa. Kwa mujibu wa taarifa za awali, kufunguliwa kwa mpaka huo kutaruhusu: - Kurejea kwa shughuli za kawaida za kibiashara - Kuimarika kwa usafiri wa wananchi wanaovuka mpaka - Kuongezeka kwa ubadilishanaji wa bidhaa na huduma - Kuimarisha uhusiano wa kijamii na kiuchumi kati ya jamii za mpakani Mashuhuda katika eneo la mpakani wameripoti kuongezeka kwa idadi ya Wasafiri na Wafanyabiashara tangu saa za mapema asubuhi, huku malori ya mizigo na mabasi yakianza kuvuka kwa utaratibu wa kawaida. Hata hivyo, mamlaka zimehimiza wananchi kuzingatia sheria na taratibu za mipakani ili kuhakikisha usalama na uendeshaji mzuri wa shughuli zote. Wachambuzi wa masuala ya kikanda wanasema hatua hiyo inaweza kuchochea ukuaji wa uchumi katika ukanda wa Maziwa Makuu, hususan kwa jamii zinazotegemea biashara ya kuvuka mpaka kati ya DRC na Burundi. Toa maoni yako #Habari
    0 Commenti 0 condivisioni 272 Views
  • Kesi ya uhaini dhidi ya Tundu Lissu yaahirishwa tena Mahakamani.

    Kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu, imeahirishwa hadi kesho baada ya Mahakama kushindwa kuendelea na usikilizwaji wake kufuatia mjadala mzito wa kisheria. Chanzo cha mvutano huo ni notisi iliyowasilishwa na upande wa Jamhuri ikieleza nia ya kuleta ushahidi mpya Mahakamani.

    Jamhuri: Notisi Iliwasilishwa kwa mujibu wa sheria.

    Upande wa Mashtaka umeeleza kuwa uliwasilisha notisi hiyo tarehe 20 Februari 2026 kwa mujibu wa kifungu cha 308 cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai. Wakili wa Serikali alidai kuwa notisi hiyo ina maudhui ya ushahidi unaokusudiwa kuongezwa kama nyongeza ya ushahidi uliowasilishwa awali na ACP Amini Mahamba.

    Kwa hoja ya Jamhuri:

    - Kifungu cha 308(1) kinatoa mwongozo wa kuwasilisha ushahidi wa ziada.

    - Kifungu cha 308(4) kinahusu ushahidi uliopo katika jalada la kesi.

    - ACP Mahamba alikuwa Mchunguzi wa matukio yaliyotokea wakati na baada ya uchaguzi wa Oktoba 29, 2025.

    Kwa mtazamo wa Jamhuri, ushahidi huo ni wa kuimarisha hoja zao na unafuata taratibu za kisheria.

    Lissu apinga: “Si shahidi mpya”

    Hata hivyo, Tundu Lissu alipinga vikali notisi hiyo akisema haikidhi matakwa ya kisheria.

    Kwa mujibu wa hoja yake:

    - Kifungu cha 308(1) kinahusu shahidi mpya ambaye ushahidi wake haukusomwa wakati wa hatua ya awali (committal proceedings).

    - Upande wa Jamhuri hauleti shahidi mpya, bali unataka kuongeza ushahidi wa shahidi ambaye tayari alishatoa ushahidi wake.

    - Notisi hiyo haimtaji shahidi mpya kama sheria inavyotaka.

    Lissu alisisitiza kuwa hatua hiyo ni kinyume cha utaratibu wa kisheria na inalenga kupanua wigo wa kesi nje ya hati ya mashtaka.

    Aidha, Lissu alieleza kuwa maelezo yanayohusu matukio ya uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025 hayamo kwenye hati ya mashtaka.

    Alidai kuwa:

    - Serikali inaonekana kutaka kubadilisha hati ya mashtaka bila kufuata utaratibu.

    - Wakati wa matukio hayo, yeye alikuwa mahabusu kwa miezi sita na nusu.

    - Kuruhusu notisi hiyo ni sawa na kufungua “sanduku la Pandora” kwa kuingiza masuala mapya yasiyo kwenye mashtaka ya awali.

    Kutokana na mvutano huo wa kisheria, Mahakama ililazimika kuahirisha kesi hiyo hadi kesho ili kutoa mwongozo au uamuzi kuhusu uhalali wa notisi ya Jamhuri.

    Uamuzi utakaotolewa unaweza kuwa na athari kubwa katika mwelekeo wa kesi hiyo, hasa kuhusu tafsiri na matumizi ya kifungu cha 308 katika mazingira ya ushahidi wa ziada.

    Toa maoni yako
    #Habari
    Kesi ya uhaini dhidi ya Tundu Lissu yaahirishwa tena Mahakamani. Kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu, imeahirishwa hadi kesho baada ya Mahakama kushindwa kuendelea na usikilizwaji wake kufuatia mjadala mzito wa kisheria. Chanzo cha mvutano huo ni notisi iliyowasilishwa na upande wa Jamhuri ikieleza nia ya kuleta ushahidi mpya Mahakamani. Jamhuri: Notisi Iliwasilishwa kwa mujibu wa sheria. Upande wa Mashtaka umeeleza kuwa uliwasilisha notisi hiyo tarehe 20 Februari 2026 kwa mujibu wa kifungu cha 308 cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai. Wakili wa Serikali alidai kuwa notisi hiyo ina maudhui ya ushahidi unaokusudiwa kuongezwa kama nyongeza ya ushahidi uliowasilishwa awali na ACP Amini Mahamba. Kwa hoja ya Jamhuri: - Kifungu cha 308(1) kinatoa mwongozo wa kuwasilisha ushahidi wa ziada. - Kifungu cha 308(4) kinahusu ushahidi uliopo katika jalada la kesi. - ACP Mahamba alikuwa Mchunguzi wa matukio yaliyotokea wakati na baada ya uchaguzi wa Oktoba 29, 2025. Kwa mtazamo wa Jamhuri, ushahidi huo ni wa kuimarisha hoja zao na unafuata taratibu za kisheria. Lissu apinga: “Si shahidi mpya” Hata hivyo, Tundu Lissu alipinga vikali notisi hiyo akisema haikidhi matakwa ya kisheria. Kwa mujibu wa hoja yake: - Kifungu cha 308(1) kinahusu shahidi mpya ambaye ushahidi wake haukusomwa wakati wa hatua ya awali (committal proceedings). - Upande wa Jamhuri hauleti shahidi mpya, bali unataka kuongeza ushahidi wa shahidi ambaye tayari alishatoa ushahidi wake. - Notisi hiyo haimtaji shahidi mpya kama sheria inavyotaka. Lissu alisisitiza kuwa hatua hiyo ni kinyume cha utaratibu wa kisheria na inalenga kupanua wigo wa kesi nje ya hati ya mashtaka. Aidha, Lissu alieleza kuwa maelezo yanayohusu matukio ya uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025 hayamo kwenye hati ya mashtaka. Alidai kuwa: - Serikali inaonekana kutaka kubadilisha hati ya mashtaka bila kufuata utaratibu. - Wakati wa matukio hayo, yeye alikuwa mahabusu kwa miezi sita na nusu. - Kuruhusu notisi hiyo ni sawa na kufungua “sanduku la Pandora” kwa kuingiza masuala mapya yasiyo kwenye mashtaka ya awali. Kutokana na mvutano huo wa kisheria, Mahakama ililazimika kuahirisha kesi hiyo hadi kesho ili kutoa mwongozo au uamuzi kuhusu uhalali wa notisi ya Jamhuri. Uamuzi utakaotolewa unaweza kuwa na athari kubwa katika mwelekeo wa kesi hiyo, hasa kuhusu tafsiri na matumizi ya kifungu cha 308 katika mazingira ya ushahidi wa ziada. Toa maoni yako #Habari
    0 Commenti 0 condivisioni 225 Views
  • Wakili Craig Kitambala aomba ridhaa ya Fally Ipupa kufungua kesi dhidi ya Mwanahabari Gautier Sey.

    Hatua mpya ya kisheria imeibuka katika tasnia ya burudani ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, baada ya Wakili Craig Kitambala kuomba ruhusa rasmi kutoka kwa Msanii maarufu Fally Ipupa ili kuanzisha mashitaka dhidi ya Mwanahabari Gautier Sey kwa tuhuma za kumchafulia jina.

    Kwa mujibu wa taarifa zilizosambaa kwenye mitandao ya kijamii, Wakili Kitambala anataka kuchukua hatua za kisheria kufuatia kauli na maudhui yaliyotolewa na Gautier Sey ambayo yanaelezwa kuwa yamelenga kumdhalilisha au kumharibia taswira Msanii huyo mbele ya umma.

    Katika maelezo yake, Wakili Kitambala ameeleza kuwa anasubiri kibali cha moja kwa moja kutoka kwa Fally Ipupa kabla ya kuwasilisha rasmi malalamiko Mahakamani.

    “Ninaomba idhini ya Fally Ipupa ili niweze kuanzisha rasmi mashitaka ya kashfa dhidi ya Mwanahabari Gautier Sey,” imeelezwa katika ujumbe unaohusishwa na Wakili huyo.

    Hatua hiyo inakuja wakati mijadala mikali ikiendelea mtandaoni kuhusu uhuru wa vyombo vya habari dhidi ya heshima na hadhi ya watu maarufu. Ikiwa kibali hicho kitatolewa, kesi hiyo inaweza kufungua mjadala mpana kuhusu mipaka ya maoni ya Wanahabari na wajibu wao katika kuripoti habari zinazowahusu watu mashuhuri.

    Kwa sasa, Fally Ipupa hajatoa tamko rasmi hadharani kuhusu iwapo atatoa ruhusa hiyo au la. Vivyo hivyo, Gautier Sey naye hajajibu moja kwa moja tuhuma zinazomkabili.

    Endapo shauri hilo litafunguliwa, linaweza kuwa miongoni mwa kesi zinazovuta hisia kubwa katika tasnia ya muziki na vyombo vya habari nchini DR Congo.

    Toa maoni yako
    #Music
    Wakili Craig Kitambala aomba ridhaa ya Fally Ipupa kufungua kesi dhidi ya Mwanahabari Gautier Sey. Hatua mpya ya kisheria imeibuka katika tasnia ya burudani ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, baada ya Wakili Craig Kitambala kuomba ruhusa rasmi kutoka kwa Msanii maarufu Fally Ipupa ili kuanzisha mashitaka dhidi ya Mwanahabari Gautier Sey kwa tuhuma za kumchafulia jina. Kwa mujibu wa taarifa zilizosambaa kwenye mitandao ya kijamii, Wakili Kitambala anataka kuchukua hatua za kisheria kufuatia kauli na maudhui yaliyotolewa na Gautier Sey ambayo yanaelezwa kuwa yamelenga kumdhalilisha au kumharibia taswira Msanii huyo mbele ya umma. Katika maelezo yake, Wakili Kitambala ameeleza kuwa anasubiri kibali cha moja kwa moja kutoka kwa Fally Ipupa kabla ya kuwasilisha rasmi malalamiko Mahakamani. “Ninaomba idhini ya Fally Ipupa ili niweze kuanzisha rasmi mashitaka ya kashfa dhidi ya Mwanahabari Gautier Sey,” imeelezwa katika ujumbe unaohusishwa na Wakili huyo. Hatua hiyo inakuja wakati mijadala mikali ikiendelea mtandaoni kuhusu uhuru wa vyombo vya habari dhidi ya heshima na hadhi ya watu maarufu. Ikiwa kibali hicho kitatolewa, kesi hiyo inaweza kufungua mjadala mpana kuhusu mipaka ya maoni ya Wanahabari na wajibu wao katika kuripoti habari zinazowahusu watu mashuhuri. Kwa sasa, Fally Ipupa hajatoa tamko rasmi hadharani kuhusu iwapo atatoa ruhusa hiyo au la. Vivyo hivyo, Gautier Sey naye hajajibu moja kwa moja tuhuma zinazomkabili. Endapo shauri hilo litafunguliwa, linaweza kuwa miongoni mwa kesi zinazovuta hisia kubwa katika tasnia ya muziki na vyombo vya habari nchini DR Congo. Toa maoni yako #Music
    0 Commenti 0 condivisioni 215 Views
  • Programu ya kijamii ya UpScrolled yaondolewa Google Play Store.

    Programu mpya ya mitandao ya kijamii iitwayo UpScrolled, iliyokuwa imezinduliwa hivi karibuni na mtaalamu wa teknolojia mwenye asili ya Palestina na Australia, Issam Hijazi, imeondolewa katika jukwaa la Google Play Store.

    Hatua hiyo imeibua mjadala mpana mtandaoni, hasa miongoni mwa watumiaji waliokuwa wameanza kuipokea kama mbadala wa baadhi ya mitandao mikubwa ya kijamii.

    Kwa mujibu wa taarifa iliyosambaa kwenye majukwaa mbalimbali ya kijamii, programu hiyo “imeondolewa kwenye Google Play Store” bila maelezo ya kina kutolewa mara moja kuhusu sababu za hatua hiyo.

    UpScrolled ilikuwa imeanza kuvutia watumiaji kwa madai ya kutoa uhuru zaidi wa maudhui na mazingira mbadala ya mijadala ya kijamii mtandaoni. Hata hivyo, kuondolewa kwake ghafla kwenye duka la programu la Google kumeacha maswali mengi kuhusu vigezo na taratibu zilizotumika kufikia uamuzi huo.

    Kwa sasa, haijawekwa wazi iwapo hatua hiyo ni ya muda au ya kudumu, wala kama kutakuwa na marekebisho yatakayoruhusu kurejeshwa kwa programu hiyo sokoni.

    Tukio hili linaongeza mjadala mpana kuhusu udhibiti wa maudhui, sera za majukwaa makubwa ya kidijitali, na changamoto wanazokumbana nazo wabunifu wa programu mpya katika soko la kimataifa la teknolojia.

    Maendeleo zaidi yanatarajiwa kadri wahusika watakavyotoa ufafanuzi rasmi kuhusu hatma ya UpScrolled.

    Toa maoni yako
    #Habari
    Programu ya kijamii ya UpScrolled yaondolewa Google Play Store. Programu mpya ya mitandao ya kijamii iitwayo UpScrolled, iliyokuwa imezinduliwa hivi karibuni na mtaalamu wa teknolojia mwenye asili ya Palestina na Australia, Issam Hijazi, imeondolewa katika jukwaa la Google Play Store. Hatua hiyo imeibua mjadala mpana mtandaoni, hasa miongoni mwa watumiaji waliokuwa wameanza kuipokea kama mbadala wa baadhi ya mitandao mikubwa ya kijamii. Kwa mujibu wa taarifa iliyosambaa kwenye majukwaa mbalimbali ya kijamii, programu hiyo “imeondolewa kwenye Google Play Store” bila maelezo ya kina kutolewa mara moja kuhusu sababu za hatua hiyo. UpScrolled ilikuwa imeanza kuvutia watumiaji kwa madai ya kutoa uhuru zaidi wa maudhui na mazingira mbadala ya mijadala ya kijamii mtandaoni. Hata hivyo, kuondolewa kwake ghafla kwenye duka la programu la Google kumeacha maswali mengi kuhusu vigezo na taratibu zilizotumika kufikia uamuzi huo. Kwa sasa, haijawekwa wazi iwapo hatua hiyo ni ya muda au ya kudumu, wala kama kutakuwa na marekebisho yatakayoruhusu kurejeshwa kwa programu hiyo sokoni. Tukio hili linaongeza mjadala mpana kuhusu udhibiti wa maudhui, sera za majukwaa makubwa ya kidijitali, na changamoto wanazokumbana nazo wabunifu wa programu mpya katika soko la kimataifa la teknolojia. Maendeleo zaidi yanatarajiwa kadri wahusika watakavyotoa ufafanuzi rasmi kuhusu hatma ya UpScrolled. Toa maoni yako #Habari
    0 Commenti 0 condivisioni 287 Views
  • Mwigizaji wa Nollywood Maurice Sam, mtandaoni yachafukwa baada ya shambulio la risasi.

    Mwigizaji wa filamu za Nollywood, Nigeria, Maurice Sam, amesambaa kwenye vichwa vya habari mtandaoni baada ya taarifa zinazodai kuwa alishambuliwa kwa risasi jana Februari 13, 2026 akiwa kwenye seti ya filamu yake mpya. Tukio hili lilianza kuchipuka mtandaoni baada ya Mwanaharakati maarufu wa mitandao, Very Dark Man, kuposti picha na madai ya kwamba Mwigizaji huyo alikuwa amejeruhiwa vibaya na alikuwa akifikiria kuondoka Nigeria ili kulinda usalama wake.

    Ripoti kutoka tovuti ya Latest Nigerian News inaeleza kuwa baadhi ya picha zilizosambazwa mtandaoni zinaonyesha Gari lililoharibiwa na alama za risasi, jambo lililoashiria hatari kubwa aliyokabiliana nayo Mwigizaji huyo. Mada hii iliibua mjadala mkali miongoni mwa mashabiki, wadau wa filamu, na Watumiaji wa mitandao ya kijamii, huku wengi wakihoji ni nini hasa kilichosababisha tukio hili na kuzingatia juhudi za Maurice Sam kujijenga kibiashara na kupata nafasi kubwa ndani ya tasnia ya Nollywood.

    Mchambuzi mmoja wa tasnia ya filamu alisema: “Ni jambo linalotia wasiwasi kuona msanii chipukizi akikabiliwa na tukio la aina hii. Inaleta mjadala juu ya usalama wa wasanii na hali ya kazi kwenye tasnia ya filamu nchini Nigeria.”

    Hata hivyo, ripoti hizo pia zinaonyesha wazi kuwa hakuna uthibitisho rasmi kutoka kwa Mwigizaji, Polisi, au vyombo vya habari vikuu. Taarifa hizi zinazozagaa zinatokana zaidi na mitandao ya kijamii, na bado hazina uthibitisho wa moja kwa moja wa jeraha lolote lililopatikana.

    Kwa sasa, Maurice Sam yupo salama, ingawa duru zinaeleza kuwa tukio hili limemuathiri kisaikolojia kiasi cha kuanza kufikiria kuachana na uigizaji na kuwekeza katika shughuli nyingine za kibiashara. Tukio hili limeibua mjadala wa kimataifa kuhusu hatari zinazoweza kutokea kwa Wasanii chipukizi, huku wadau wa tasnia wakihimiza tahadhari na uangalizi zaidi kwenye seti za filamu.

    Toa maoni yako
    #Filamu
    #Habari
    Mwigizaji wa Nollywood Maurice Sam, mtandaoni yachafukwa baada ya shambulio la risasi. Mwigizaji wa filamu za Nollywood, Nigeria, Maurice Sam, amesambaa kwenye vichwa vya habari mtandaoni baada ya taarifa zinazodai kuwa alishambuliwa kwa risasi jana Februari 13, 2026 akiwa kwenye seti ya filamu yake mpya. Tukio hili lilianza kuchipuka mtandaoni baada ya Mwanaharakati maarufu wa mitandao, Very Dark Man, kuposti picha na madai ya kwamba Mwigizaji huyo alikuwa amejeruhiwa vibaya na alikuwa akifikiria kuondoka Nigeria ili kulinda usalama wake. Ripoti kutoka tovuti ya Latest Nigerian News inaeleza kuwa baadhi ya picha zilizosambazwa mtandaoni zinaonyesha Gari lililoharibiwa na alama za risasi, jambo lililoashiria hatari kubwa aliyokabiliana nayo Mwigizaji huyo. Mada hii iliibua mjadala mkali miongoni mwa mashabiki, wadau wa filamu, na Watumiaji wa mitandao ya kijamii, huku wengi wakihoji ni nini hasa kilichosababisha tukio hili na kuzingatia juhudi za Maurice Sam kujijenga kibiashara na kupata nafasi kubwa ndani ya tasnia ya Nollywood. Mchambuzi mmoja wa tasnia ya filamu alisema: “Ni jambo linalotia wasiwasi kuona msanii chipukizi akikabiliwa na tukio la aina hii. Inaleta mjadala juu ya usalama wa wasanii na hali ya kazi kwenye tasnia ya filamu nchini Nigeria.” Hata hivyo, ripoti hizo pia zinaonyesha wazi kuwa hakuna uthibitisho rasmi kutoka kwa Mwigizaji, Polisi, au vyombo vya habari vikuu. Taarifa hizi zinazozagaa zinatokana zaidi na mitandao ya kijamii, na bado hazina uthibitisho wa moja kwa moja wa jeraha lolote lililopatikana. Kwa sasa, Maurice Sam yupo salama, ingawa duru zinaeleza kuwa tukio hili limemuathiri kisaikolojia kiasi cha kuanza kufikiria kuachana na uigizaji na kuwekeza katika shughuli nyingine za kibiashara. Tukio hili limeibua mjadala wa kimataifa kuhusu hatari zinazoweza kutokea kwa Wasanii chipukizi, huku wadau wa tasnia wakihimiza tahadhari na uangalizi zaidi kwenye seti za filamu. Toa maoni yako #Filamu #Habari
    0 Commenti 0 condivisioni 295 Views
  • Nchi ya Kenya yakemea vitendo vya kuwapeleka Vijana wake kwenye vita Nchini Ukraine.

    Serikali ya Kenya imekemea vikali vitendo vya baadhi ya Mawakala wanaodanganya Vijana kwa ahadi za ajira, kisha kuwapeleka moja kwa moja kwenye vita vinavyoendelea nchini Ukraine.

    Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya, Musalia Mudavadi, amesema: “Tunatarajia kufanya ziara rasmi mjini Moscow kwa mazungumzo na Serikali ya Urusi, lengo likiwa kusitisha kabisa matumizi ya raia wa Kenya katika mapambano haya.”

    Mudavadi alibainisha kuwa tayari Wakenya kadhaa wamefariki dunia, huku wengine wakijeruhiwa vibaya baada ya kudanganywa kuingia mikataba ya kijeshi. Amesema: “Hatukubali upotevu wa maisha ya raia wetu. Hatua za kudumu lazima zichukuliwe.”

    Serikali ya Kenya imelaumu Mawakala wa ajira wanaoshawishi vijana kwa ahadi za mishahara mikubwa, kisha kuwapeleka mstari wa mbele vitani. Ripoti ya hivi karibuni ya shirika la habari la Ufaransa, Agence France-Presse, imethibitisha kuwepo kwa mtandao wa udanganyifu unaowaingiza vijana wasiokuwa na historia ya kijeshi kusaini mikataba na Jeshi la Urusi, kisha kupelekwa haraka kwenye Uwanja wa mapambano.

    Mudavadi amesisitiza kuwa Kenya itafuatilia pia suala la kuachiliwa kwa Wakenya waliokamatwa kama wafungwa wa kivita nchini Ukraine. Amesema hatua hizi ni muhimu ili kulinda maisha ya Raia wake.

    Toa maoni yako
    #Habari
    #Russia #Ukraine #MusaliaMudavadi #Moscow #BreakingNews #WorldNews #VitaUkraine #KenyaAbroad #HumanRights #AfricaNews
    Nchi ya Kenya yakemea vitendo vya kuwapeleka Vijana wake kwenye vita Nchini Ukraine. Serikali ya Kenya imekemea vikali vitendo vya baadhi ya Mawakala wanaodanganya Vijana kwa ahadi za ajira, kisha kuwapeleka moja kwa moja kwenye vita vinavyoendelea nchini Ukraine. Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya, Musalia Mudavadi, amesema: “Tunatarajia kufanya ziara rasmi mjini Moscow kwa mazungumzo na Serikali ya Urusi, lengo likiwa kusitisha kabisa matumizi ya raia wa Kenya katika mapambano haya.” Mudavadi alibainisha kuwa tayari Wakenya kadhaa wamefariki dunia, huku wengine wakijeruhiwa vibaya baada ya kudanganywa kuingia mikataba ya kijeshi. Amesema: “Hatukubali upotevu wa maisha ya raia wetu. Hatua za kudumu lazima zichukuliwe.” Serikali ya Kenya imelaumu Mawakala wa ajira wanaoshawishi vijana kwa ahadi za mishahara mikubwa, kisha kuwapeleka mstari wa mbele vitani. Ripoti ya hivi karibuni ya shirika la habari la Ufaransa, Agence France-Presse, imethibitisha kuwepo kwa mtandao wa udanganyifu unaowaingiza vijana wasiokuwa na historia ya kijeshi kusaini mikataba na Jeshi la Urusi, kisha kupelekwa haraka kwenye Uwanja wa mapambano. Mudavadi amesisitiza kuwa Kenya itafuatilia pia suala la kuachiliwa kwa Wakenya waliokamatwa kama wafungwa wa kivita nchini Ukraine. Amesema hatua hizi ni muhimu ili kulinda maisha ya Raia wake. Toa maoni yako #Habari #Russia #Ukraine #MusaliaMudavadi #Moscow #BreakingNews #WorldNews #VitaUkraine #KenyaAbroad #HumanRights #AfricaNews
    0 Commenti 2 condivisioni 699 Views
  • Trump afikiria kutuma Meli ya pili ya kubeba Ndege Mashariki ya Kati wakati mazungumzo na Iran yakirejea.

    Rais wa Marekani Donald Trump amesema anafikiria kuongeza uwepo wa kijeshi wa Marekani katika eneo la Mashariki ya Kati kwa kutuma Meli ya pili ya kivita ya kubeba ndege, licha ya juhudi zinazoendelea za kidiplomasia kati ya Washington na Tehran.

    Akizungumza na vyombo vya habari vya Channel 12 na Axios, Trump alithibitisha kuwa wazo hilo liko mezani, akisema kuwa “anafikiria kutuma Meli ya pili ya kubeba ndege Mashariki ya Kati.” Kauli hiyo inakuja wakati Marekani na Iran zikijiandaa kuanza tena mazungumzo yanayolenga kuepusha mzozo mpya wa kijeshi au wa kisiasa katika ukanda huo wenye mvutano wa muda mrefu.

    Kwa mujibu wa taarifa za kijeshi, Manowari za kivita zinazotajwa kuweza kupelekwa ni USS George Washington iliyoko barani Asia na USS George HW Bush iliyoko katika Pwani ya mashariki ya Marekani. Aidha, Pentagon inaweza pia kupeleka Meli ya kivita ya USS Gerald R. Ford kutoka eneo la Karibiani kwenda Mashariki ya Kati, iwapo uamuzi huo utapitishwa rasmi.

    Katika mahojiano na vyombo vya habari vya Israeli, Trump alionya kuwa hatua kali zinaweza kuchukuliwa endapo mazungumzo hayatatoa matokeo. Alisema Marekani italazimika kufanya “jambo gumu sana” ikiwa makubaliano hayatafikiwa na Iran.

    Hatua hiyo inayozingatiwa na Washington inakuja wakati Oman ikiendelea kuwa msuluhishi muhimu katika juhudi za kupunguza mvutano kati ya pande hizo mbili. Wiki iliyopita, Oman iliwezesha mazungumzo kati ya Iran na Marekani, hatua ambayo imeelezwa na Tehran kuwa ya kutia matumaini.

    Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran alisema mazungumzo hayo “yameiruhusu Tehran kupima uzito wa Washington na kuonyesha makubaliano ya kutosha kwa diplomasia kuendelea.” Kauli hiyo inaashiria kuwa licha ya maandalizi ya kijeshi, milango ya mazungumzo bado iko wazi.

    Kwa sasa, macho ya jumuiya ya kimataifa yanaelekezwa katika mwenendo wa mazungumzo hayo na maamuzi ya kijeshi yatakayochukuliwa na Marekani, hatua ambazo zinaweza kuathiri kwa kiasi kikubwa utulivu wa Mashariki ya Kati.

    Toa maoni yako
    #Habari
    Trump afikiria kutuma Meli ya pili ya kubeba Ndege Mashariki ya Kati wakati mazungumzo na Iran yakirejea. Rais wa Marekani Donald Trump amesema anafikiria kuongeza uwepo wa kijeshi wa Marekani katika eneo la Mashariki ya Kati kwa kutuma Meli ya pili ya kivita ya kubeba ndege, licha ya juhudi zinazoendelea za kidiplomasia kati ya Washington na Tehran. Akizungumza na vyombo vya habari vya Channel 12 na Axios, Trump alithibitisha kuwa wazo hilo liko mezani, akisema kuwa “anafikiria kutuma Meli ya pili ya kubeba ndege Mashariki ya Kati.” Kauli hiyo inakuja wakati Marekani na Iran zikijiandaa kuanza tena mazungumzo yanayolenga kuepusha mzozo mpya wa kijeshi au wa kisiasa katika ukanda huo wenye mvutano wa muda mrefu. Kwa mujibu wa taarifa za kijeshi, Manowari za kivita zinazotajwa kuweza kupelekwa ni USS George Washington iliyoko barani Asia na USS George HW Bush iliyoko katika Pwani ya mashariki ya Marekani. Aidha, Pentagon inaweza pia kupeleka Meli ya kivita ya USS Gerald R. Ford kutoka eneo la Karibiani kwenda Mashariki ya Kati, iwapo uamuzi huo utapitishwa rasmi. Katika mahojiano na vyombo vya habari vya Israeli, Trump alionya kuwa hatua kali zinaweza kuchukuliwa endapo mazungumzo hayatatoa matokeo. Alisema Marekani italazimika kufanya “jambo gumu sana” ikiwa makubaliano hayatafikiwa na Iran. Hatua hiyo inayozingatiwa na Washington inakuja wakati Oman ikiendelea kuwa msuluhishi muhimu katika juhudi za kupunguza mvutano kati ya pande hizo mbili. Wiki iliyopita, Oman iliwezesha mazungumzo kati ya Iran na Marekani, hatua ambayo imeelezwa na Tehran kuwa ya kutia matumaini. Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran alisema mazungumzo hayo “yameiruhusu Tehran kupima uzito wa Washington na kuonyesha makubaliano ya kutosha kwa diplomasia kuendelea.” Kauli hiyo inaashiria kuwa licha ya maandalizi ya kijeshi, milango ya mazungumzo bado iko wazi. Kwa sasa, macho ya jumuiya ya kimataifa yanaelekezwa katika mwenendo wa mazungumzo hayo na maamuzi ya kijeshi yatakayochukuliwa na Marekani, hatua ambazo zinaweza kuathiri kwa kiasi kikubwa utulivu wa Mashariki ya Kati. Toa maoni yako #Habari
    0 Commenti 0 condivisioni 266 Views
  • Ubalozi wa RDC Burundi wakanusha taarifa za orodha ya Raia kurudi kwa hiari Uvira.

    Bujumbura, Burundi, Ubalozi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (RDC) nchini Burundi umekanusha taarifa zinazosambaa mitandaoni zikidai kuwa umefungua orodha ya usajili kwa Raia wa Congo wanaotaka kurejea kwa hiari katika Mji wa Uvira, Mkoani Sud-Kivu.

    Taarifa hizo, zilizosambazwa kwa kasi kupitia mitandao ya kijamii hususan makundi ya WhatsApp, zilisababisha idadi ya Raia wa Congo kujitokeza katika majengo ya ubalozi wakiamini kuwa kuna mchakato rasmi wa kurejea unaoendelea.

    Akizungumza, Balozi wa RDC nchini Burundi, Willy Mulamba Mabika, amesema ubalozi hauna mamlaka ya kuandaa au kuruhusu kurejea kwa hiari kwa Wakimbizi.

    “Ubalozi hauna haki ya kufungua mpaka wala kuruhusu kurejea kwa wakimbizi nchini mwao. Jukumu hili ni la Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (HCR), Serikali ya Burundi, na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo baada ya kufanyika tathmini ya awali ya hali ya usalama,” amenukuliwa akisema Balozi huyo.

    Kwa mujibu wa taratibu za kimataifa, kurejea kwa hiari kwa Wakimbizi huratibiwa na HCR, hufanyika kwa makubaliano kati ya nchi mwenyeji na nchi ya asili, na hutegemea tathmini ya kiusalama inayohakikisha kurejea kwa usalama, heshima na kwa hiari.

    Hakuna tamko lolote kutoka kwa HCR, Serikali ya Burundi au Serikali ya RDC linalothibitisha kuwepo kwa mpango wa sasa wa kurejesha Wakimbizi wa Congo kutoka Burundi kwenda Uvira. Wachambuzi huru wanasema kujitokeza kwa Raia wa Congo mbele ya ubalozi kunaweza kuakisi hamu ya kurejea nyumbani, inayochochewa na matarajio ya kuimarika kwa hali ya usalama na juhudi zinazoendelea za kurejesha mamlaka ya dola katika eneo la Uvira.

    Ubalozi umehimiza umma kuwa makini dhidi ya taarifa zisizothibitishwa na kuzingatia mawasiliano rasmi pekee kutoka HCR na mamlaka husika.

    “Upotoshaji wa taarifa katika mazingira nyeti ya kibinadamu na kiusalama unaweza kuwaweka watu hatarini bila sababu,” balozi ameongeza.

    Hakuna orodha rasmi iliyofunguliwa katika Ubalozi wa RDC nchini Burundi kwa ajili ya kurejea kwa hiari kwa Raia wa Congo kwenda Uvira; madai hayo hayana msingi na yamekanushwa rasmi.

    Ubalozi wa RDC Burundi wakanusha taarifa za orodha ya Raia kurudi kwa hiari Uvira. Bujumbura, Burundi, Ubalozi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (RDC) nchini Burundi umekanusha taarifa zinazosambaa mitandaoni zikidai kuwa umefungua orodha ya usajili kwa Raia wa Congo wanaotaka kurejea kwa hiari katika Mji wa Uvira, Mkoani Sud-Kivu. Taarifa hizo, zilizosambazwa kwa kasi kupitia mitandao ya kijamii hususan makundi ya WhatsApp, zilisababisha idadi ya Raia wa Congo kujitokeza katika majengo ya ubalozi wakiamini kuwa kuna mchakato rasmi wa kurejea unaoendelea. Akizungumza, Balozi wa RDC nchini Burundi, Willy Mulamba Mabika, amesema ubalozi hauna mamlaka ya kuandaa au kuruhusu kurejea kwa hiari kwa Wakimbizi. “Ubalozi hauna haki ya kufungua mpaka wala kuruhusu kurejea kwa wakimbizi nchini mwao. Jukumu hili ni la Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (HCR), Serikali ya Burundi, na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo baada ya kufanyika tathmini ya awali ya hali ya usalama,” amenukuliwa akisema Balozi huyo. Kwa mujibu wa taratibu za kimataifa, kurejea kwa hiari kwa Wakimbizi huratibiwa na HCR, hufanyika kwa makubaliano kati ya nchi mwenyeji na nchi ya asili, na hutegemea tathmini ya kiusalama inayohakikisha kurejea kwa usalama, heshima na kwa hiari. Hakuna tamko lolote kutoka kwa HCR, Serikali ya Burundi au Serikali ya RDC linalothibitisha kuwepo kwa mpango wa sasa wa kurejesha Wakimbizi wa Congo kutoka Burundi kwenda Uvira. Wachambuzi huru wanasema kujitokeza kwa Raia wa Congo mbele ya ubalozi kunaweza kuakisi hamu ya kurejea nyumbani, inayochochewa na matarajio ya kuimarika kwa hali ya usalama na juhudi zinazoendelea za kurejesha mamlaka ya dola katika eneo la Uvira. Ubalozi umehimiza umma kuwa makini dhidi ya taarifa zisizothibitishwa na kuzingatia mawasiliano rasmi pekee kutoka HCR na mamlaka husika. “Upotoshaji wa taarifa katika mazingira nyeti ya kibinadamu na kiusalama unaweza kuwaweka watu hatarini bila sababu,” balozi ameongeza. Hakuna orodha rasmi iliyofunguliwa katika Ubalozi wa RDC nchini Burundi kwa ajili ya kurejea kwa hiari kwa Raia wa Congo kwenda Uvira; madai hayo hayana msingi na yamekanushwa rasmi.
    0 Commenti 0 condivisioni 196 Views
  • OFFICIAL Arsenal kwa sasa haina majeruhi kwenye chumba cha Wagonjwa kuelekea mchezo ujao wachezaji wote wamepona

    Kai Havertz
    Gabriel Jesus
    Gabriel Martinelli
    Viktor Gyokeres
    Noni Madueke
    Martin Ordegaard
    🚨 OFFICIAL Arsenal kwa sasa haina majeruhi kwenye chumba cha Wagonjwa kuelekea mchezo ujao wachezaji wote wamepona 🇩🇪 Kai Havertz 🇧🇷 Gabriel Jesus 🇧🇷 Gabriel Martinelli 🇸🇪 Viktor Gyokeres 🏴󠁧󠁢󠁥󠁮󠁧󠁿 Noni Madueke 🇳🇴 Martin Ordegaard
    0 Commenti 0 condivisioni 593 Views
  • Israel yasema itaendelea kusimamia usalama Gaza, licha ya makubaliano ya usitishaji vita.

    Katika taarifa mpya iliyoibua mijadala ya kisiasa na kidiplomasia, Serikali ya Israel imesisitiza kuwa haitakubali kuachia jukumu la usalama wa Ukanda wa Gaza mikononi mwa vikosi vya kimataifa, licha ya kusaini makubaliano ya usitishaji vita yaliyosimamiwa na Marekani.

    Kupitia kikao na Baraza lake la Mawaziri, Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, alinukuliwa akisema:

    “Israel itaamua yenyewe ni lini na wapi itaendelea kuwakabili maadui zake. Hatutakubali kabisa nchi yoyote kutuamulia kuhusu usalama wetu.”

    Kauli hiyo imekuja muda mfupi baada ya makubaliano ya muda ya usitishaji mapigano kuwasilishwa, yakiruhusu kuundwa kwa kikosi cha kimataifa kitakacholinda amani na usambazaji wa misaada ya kibinadamu ndani ya Gaza.

    Kulingana na taarifa zilizotolewa, kikosi hicho kitapangwa kutoka mataifa ya Kiarabu au Kiislamu, na kazi yake kuu itakuwa kuhakikisha usalama wa Raia na kusimamia utekelezaji wa masharti ya kusitisha vita.

    Hata hivyo, Netanyahu ameeleza wasiwasi mkubwa juu ya mpango huo:

    “Tutashirikiana pale inapobidi, lakini hatutawahi kukubali Gaza kuwa chini ya mamlaka ya nje bila ridhaa ya Israel. Usalama wa Raia wetu ndio kipaumbele cha kwanza.”

    Kwa mujibu wa Afisa wa Marekani, makubaliano haya ni sehemu ya juhudi za muda mrefu kurejesha utulivu katika eneo hilo, lakini yanategemea ushirikiano wa pande zote mbili, jambo ambalo linazidi kuonekana kuwa gumu kutokana na msimamo wa Israel.

    Hii ni ishara kwamba licha ya mapendekezo ya kimataifa, Israel bado inashikilia msimamo wake wa kulinda mamlaka kamili ya usalama ndani ya Gaza, hatua inayoweza kuchelewesha utekelezaji wa makubaliano haya mapya.

    Je, Israel inaweza kusimamia amani Gaza bila msaada wa Jumuiya ya kimataifa? Au je, dunia inapaswa kuingilia kati kwa nguvu zaidi?

    Toa maoni yako
    Israel yasema itaendelea kusimamia usalama Gaza, licha ya makubaliano ya usitishaji vita. Katika taarifa mpya iliyoibua mijadala ya kisiasa na kidiplomasia, Serikali ya Israel imesisitiza kuwa haitakubali kuachia jukumu la usalama wa Ukanda wa Gaza mikononi mwa vikosi vya kimataifa, licha ya kusaini makubaliano ya usitishaji vita yaliyosimamiwa na Marekani. Kupitia kikao na Baraza lake la Mawaziri, Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, alinukuliwa akisema: “Israel itaamua yenyewe ni lini na wapi itaendelea kuwakabili maadui zake. Hatutakubali kabisa nchi yoyote kutuamulia kuhusu usalama wetu.” Kauli hiyo imekuja muda mfupi baada ya makubaliano ya muda ya usitishaji mapigano kuwasilishwa, yakiruhusu kuundwa kwa kikosi cha kimataifa kitakacholinda amani na usambazaji wa misaada ya kibinadamu ndani ya Gaza. Kulingana na taarifa zilizotolewa, kikosi hicho kitapangwa kutoka mataifa ya Kiarabu au Kiislamu, na kazi yake kuu itakuwa kuhakikisha usalama wa Raia na kusimamia utekelezaji wa masharti ya kusitisha vita. Hata hivyo, Netanyahu ameeleza wasiwasi mkubwa juu ya mpango huo: “Tutashirikiana pale inapobidi, lakini hatutawahi kukubali Gaza kuwa chini ya mamlaka ya nje bila ridhaa ya Israel. Usalama wa Raia wetu ndio kipaumbele cha kwanza.” Kwa mujibu wa Afisa wa Marekani, makubaliano haya ni sehemu ya juhudi za muda mrefu kurejesha utulivu katika eneo hilo, lakini yanategemea ushirikiano wa pande zote mbili, jambo ambalo linazidi kuonekana kuwa gumu kutokana na msimamo wa Israel. Hii ni ishara kwamba licha ya mapendekezo ya kimataifa, Israel bado inashikilia msimamo wake wa kulinda mamlaka kamili ya usalama ndani ya Gaza, hatua inayoweza kuchelewesha utekelezaji wa makubaliano haya mapya. Je, Israel inaweza kusimamia amani Gaza bila msaada wa Jumuiya ya kimataifa? Au je, dunia inapaswa kuingilia kati kwa nguvu zaidi? Toa maoni yako
    Love
    1
    0 Commenti 0 condivisioni 2K Views
  • Arnold Schwarzenegger awasilisha mpango wa kuokoa demokrasia Marekani.

    Mwigizaji Nguli wa Hollywood na Gavana wa zamani wa Jimbo la California, Arnold Schwarzenegger, ameibuka na pendekezo la kina la kuimarisha demokrasia Nchini Marekani. Katika mahojiano yake kwenye kipindi maarufu cha Real Time with Bill Maher, Schwarzenegger alifichua mpango wa hatua tatu ambao anauona kama njia ya “kupatanisha pande zote mbili” yaani Republican na Democratic. Katika maelezo yake rasmi, Schwarzenegger alisema:

    “Tunapaswa kutangaza Siku ya Uchaguzi kuwa likizo ya kitaifa, kuhakikisha kuwa ramani za kisiasa zinatengenezwa na tume huru zisizoegemea upande wowote, na kuimarisha mifumo ya utambulisho wa wapiga kura.”

    Mpango huu, ambao una lengo la kuhamasisha ushiriki mpana wa Wananchi na kulinda uadilifu wa chaguzi, umeungwa mkono na hoja za kisera zinazoegemea misingi ya haki, usawa na uwazi.

    Schwarzenegger pia hakusita kuelezea wasiwasi wake kuhusu Pendekezo la 50 la California, akiliona kama:

    “Hila kubwa ambayo inaweza kurudisha ramani za uchaguzi mikononi mwa Wanasiasa badala ya Wataalamu huru.”

    Kwa mujibu wake, hatua hiyo ya kuruhusu Wanasiasa kushiriki katika uundwaji wa ramani ya majimbo inaweza kuathiri vibaya uwakilishi wa haki kwa Wananchi.

    Mpango huu wa Schwarzenegger una mvuto wa kipekee kwa kuwa unachanganya ushawishi wa jina kubwa na hoja nzito za kisera. Hata hivyo, utekelezaji wake unategemea mabadiliko ya kisheria, mjadala wa kina wa kitaifa, na maridhiano kati ya vyama viwili vikuu vya siasa.

    Kwa mujibu wa Wachambuzi wa siasa za Marekani, hoja za Schwarzenegger zinaibua maswali mapana kuhusu:

    - Usawa katika chaguzi,
    - Usalama wa mfumo wa upigaji kura,
    - Na mwelekeo wa demokrasia ya Marekani kwa vizazi vijavyo.

    Mpaka sasa, bado haijajulikana iwapo pendekezo hili litaungwa mkono na Wabunge, lakini bila shaka, Schwarzenegger amejipambanua tena, safari hii siyo kwenye sinema au siasa za majimbo tu, bali kwenye uwanja mpana wa mustakabali wa kidemokrasia wa taifa lake.
    Arnold Schwarzenegger awasilisha mpango wa kuokoa demokrasia Marekani. Mwigizaji Nguli wa Hollywood na Gavana wa zamani wa Jimbo la California, Arnold Schwarzenegger, ameibuka na pendekezo la kina la kuimarisha demokrasia Nchini Marekani. Katika mahojiano yake kwenye kipindi maarufu cha Real Time with Bill Maher, Schwarzenegger alifichua mpango wa hatua tatu ambao anauona kama njia ya “kupatanisha pande zote mbili” yaani Republican na Democratic. Katika maelezo yake rasmi, Schwarzenegger alisema: “Tunapaswa kutangaza Siku ya Uchaguzi kuwa likizo ya kitaifa, kuhakikisha kuwa ramani za kisiasa zinatengenezwa na tume huru zisizoegemea upande wowote, na kuimarisha mifumo ya utambulisho wa wapiga kura.” Mpango huu, ambao una lengo la kuhamasisha ushiriki mpana wa Wananchi na kulinda uadilifu wa chaguzi, umeungwa mkono na hoja za kisera zinazoegemea misingi ya haki, usawa na uwazi. Schwarzenegger pia hakusita kuelezea wasiwasi wake kuhusu Pendekezo la 50 la California, akiliona kama: “Hila kubwa ambayo inaweza kurudisha ramani za uchaguzi mikononi mwa Wanasiasa badala ya Wataalamu huru.” Kwa mujibu wake, hatua hiyo ya kuruhusu Wanasiasa kushiriki katika uundwaji wa ramani ya majimbo inaweza kuathiri vibaya uwakilishi wa haki kwa Wananchi. Mpango huu wa Schwarzenegger una mvuto wa kipekee kwa kuwa unachanganya ushawishi wa jina kubwa na hoja nzito za kisera. Hata hivyo, utekelezaji wake unategemea mabadiliko ya kisheria, mjadala wa kina wa kitaifa, na maridhiano kati ya vyama viwili vikuu vya siasa. Kwa mujibu wa Wachambuzi wa siasa za Marekani, hoja za Schwarzenegger zinaibua maswali mapana kuhusu: - Usawa katika chaguzi, - Usalama wa mfumo wa upigaji kura, - Na mwelekeo wa demokrasia ya Marekani kwa vizazi vijavyo. Mpaka sasa, bado haijajulikana iwapo pendekezo hili litaungwa mkono na Wabunge, lakini bila shaka, Schwarzenegger amejipambanua tena, safari hii siyo kwenye sinema au siasa za majimbo tu, bali kwenye uwanja mpana wa mustakabali wa kidemokrasia wa taifa lake.
    0 Commenti 0 condivisioni 1K Views
  • Ameandika Mtangazaji wa kabumbu Nazareth Upete

    Sikutaka kuandika update yoyote ya Fadlu kwa Jana kwa sababu Simba walikuwa na mechi ngumu, muhimu na serious zaidi ambayo isingekuwa vyema kuandika chochote chenye mapelekeo yoyote hasi kwa mtu yoyote anayehusiana na Simba SC.

    THE SAGA…!
    Tarehe 07/09 siku 3 kabla ya Simba Day kuna mtu ninayemwamini sana kutoka Morocco alinipatia taarifa ya Fadlu kuridhiana na klabu ya Raja Casablanca kwenda kuhudumu hapo…!

    Pamoja na kutoachana vyema sana na Raja akiwa Kocha msaidizi haikuwarudisha nyuma huku inaelezwa Wydad pia waliulizia upatikanaji wake lakini mkataba wa Raja ulikuwa na sababu nyingi za kuridhiwa kuliko kukataliwa.

    Tarehe 11 baada ya Simba Day, Wydad walikuwa serious kuulizia taarifa za Fadlu kwa baadhi ya watu hususani mwenendo wake kwenye maeneo yote ya msingi…! Wakataka kuingilia kati deal.

    Bado Ofa ya Raja ikasimama kiume…! Fadlu yupo tayari kuibeba Ofa ya Raja na project yao ya #BringBackCasablanca⚽️

    Wakati hali ikiwa hivyo inaelezwa mmoja wa wasaidizi wake anataka kusalia Msimbazi akiamini project yao italipa punde!

    Inaelezwa Fadlu anahisi kuna vitu havipo sawa na zigo la lawama analitupa kwa uongozi wa timu huku yeye akitafuta mlango wa kutokea!

    Kwa sasa kuna urafiki wa mashaka baina ya pande mbili na Simba wamefanya kila kitu kumbakisha ila msimamo wa Fadlu umebebwa mazima na Ofa za waManga pale Morocco

    95% mechi ya Jana ilikuwa ya mwisho kwa Fadlu kama Kocha wa Simba na sasa kilichobaki ni yeye tu awalipe Simba SC kuvunja mkataba ingali analazimisha wamruhusu aende Free!

    MTAZAMO WANGU!?
    Simba hawatakuwa na Pengo kuondoka kwa Fadlu…! Amefanya kazi nzuri ila makocha ni wengi sana barani Afrika! Kikubwa ni kutuliza Kichwa wakati wa uchaguzi wa Kocha na kuachana na % za maslahi.

    Fadlu ni Kocha mzuri ila kwa mtazamo wangu pengo linazibika…! Bahati nzuri hajacheza mechi yoyote ya Ligi…! Yoyote atakayekuja ni rahisi tu kuendeleza kitu bora kwa sababu wachezaji Quality yao sio ya kubeza!

    Salaaam!
    Ameandika Mtangazaji wa kabumbu Nazareth Upete ✍️ Sikutaka kuandika update yoyote ya Fadlu kwa Jana kwa sababu Simba walikuwa na mechi ngumu, muhimu na serious zaidi ambayo isingekuwa vyema kuandika chochote chenye mapelekeo yoyote hasi kwa mtu yoyote anayehusiana na Simba SC. THE SAGA…! Tarehe 07/09 siku 3 kabla ya Simba Day kuna mtu ninayemwamini sana kutoka Morocco alinipatia taarifa ya Fadlu kuridhiana na klabu ya Raja Casablanca kwenda kuhudumu hapo…! Pamoja na kutoachana vyema sana na Raja akiwa Kocha msaidizi haikuwarudisha nyuma huku inaelezwa Wydad pia waliulizia upatikanaji wake lakini mkataba wa Raja ulikuwa na sababu nyingi za kuridhiwa kuliko kukataliwa. Tarehe 11 baada ya Simba Day, Wydad walikuwa serious kuulizia taarifa za Fadlu kwa baadhi ya watu hususani mwenendo wake kwenye maeneo yote ya msingi…! Wakataka kuingilia kati deal. Bado Ofa ya Raja ikasimama kiume…! Fadlu yupo tayari kuibeba Ofa ya Raja na project yao ya #BringBackCasablanca⚽️ Wakati hali ikiwa hivyo inaelezwa mmoja wa wasaidizi wake anataka kusalia Msimbazi akiamini project yao italipa punde! Inaelezwa Fadlu anahisi kuna vitu havipo sawa na zigo la lawama analitupa kwa uongozi wa timu huku yeye akitafuta mlango wa kutokea! Kwa sasa kuna urafiki wa mashaka baina ya pande mbili na Simba wamefanya kila kitu kumbakisha ila msimamo wa Fadlu umebebwa mazima na Ofa za waManga pale Morocco ✍️ 95% mechi ya Jana ilikuwa ya mwisho kwa Fadlu kama Kocha wa Simba na sasa kilichobaki ni yeye tu awalipe Simba SC kuvunja mkataba ingali analazimisha wamruhusu aende Free! MTAZAMO WANGU!? Simba hawatakuwa na Pengo kuondoka kwa Fadlu…! Amefanya kazi nzuri ila makocha ni wengi sana barani Afrika! Kikubwa ni kutuliza Kichwa wakati wa uchaguzi wa Kocha na kuachana na % za maslahi. Fadlu ni Kocha mzuri ila kwa mtazamo wangu pengo linazibika…! Bahati nzuri hajacheza mechi yoyote ya Ligi…! Yoyote atakayekuja ni rahisi tu kuendeleza kitu bora kwa sababu wachezaji Quality yao sio ya kubeza! Salaaam!
    Love
    1
    0 Commenti 0 condivisioni 1K Views
  • Alexander Anord huwenda akawa nje ya uwanja zaidi ya wiki 6-8 baada ya kuwa majeruhii.

    #SportsElite
    🚨Alexander Anord huwenda akawa nje ya uwanja zaidi ya wiki 6-8 baada ya kuwa majeruhii. #SportsElite
    0 Commenti 0 condivisioni 769 Views
  • Wokovu ni matokeo ya kinywa yaani kwa kinywa ndiyo mtu hupata wokovu.

    Wokovu huo unaongozwa na imani ,kumbuka mtu anaruhusiwa kukiri kile tu anacho kiamini.

    #warumi 10:8-10.

    Kumbe pamoja na wokovu kuwa wa thamani lakini ili uingie kwa mtu kwa njia ya imani na ukiri.

    Kumbe hata kama ungeamini lakini ujakili bado unakuwa uko katika njia panda.

    Kinywa ndicho kinacho kupa mamlaka ya kumshinda shetani na kukupa ujasiri wa kushinda .

    # 2 Corinth 4:4

    Kumbe kama moyo wako ujaamini injiri huwezi kupokea kwa ukubwa unao takiwa.

    Lazima uiamini injiri au neno la Mungu ligeuke kuwa maisha na ndipo utakuwa na ujasiri wa kukiri vyema na kuushinda ulimi wako kujinenea vibay.

    #mathayo 28:18

    Yesu ndiye mamlaka na alisema tumfuate na ukimfuata yeye lazima unakiwa na mamlaka.

    Nikutakie jion njema
    Kama unapenda kujifunza tuma neno add kwa namba 0622625340.

    Naitwa sylvester Mwakabende kutoka (build new eden ministry)

    #restore men position
    #build new eden
    Wokovu ni matokeo ya kinywa yaani kwa kinywa ndiyo mtu hupata wokovu. Wokovu huo unaongozwa na imani ,kumbuka mtu anaruhusiwa kukiri kile tu anacho kiamini. #warumi 10:8-10. Kumbe pamoja na wokovu kuwa wa thamani lakini ili uingie kwa mtu kwa njia ya imani na ukiri. Kumbe hata kama ungeamini lakini ujakili bado unakuwa uko katika njia panda. Kinywa ndicho kinacho kupa mamlaka ya kumshinda shetani na kukupa ujasiri wa kushinda . # 2 Corinth 4:4 Kumbe kama moyo wako ujaamini injiri huwezi kupokea kwa ukubwa unao takiwa. Lazima uiamini injiri au neno la Mungu ligeuke kuwa maisha na ndipo utakuwa na ujasiri wa kukiri vyema na kuushinda ulimi wako kujinenea vibay. #mathayo 28:18 Yesu ndiye mamlaka na alisema tumfuate na ukimfuata yeye lazima unakiwa na mamlaka. Nikutakie jion njema Kama unapenda kujifunza tuma neno add kwa namba 0622625340. Naitwa sylvester Mwakabende kutoka (build new eden ministry) #restore men position #build new eden
    0 Commenti 0 condivisioni 2K Views
  • Ofa ya klabu ya £25m ya Real Betis ilikubaliwa na Man United Kuhusu kumsajili Antony na tayari Man United ilimpa ruhusa Antony kusafiri kuelekea Spain

    Lakini saa chache baadae Real Betis imebadilishaa msimamo wake na kujiondoa kwenye mazungumzo wakidai kuwa mshahara wa Antony ni mkubwa hivyo hawataweza vinginevyo Man United wapungize Bei ya Antony au Antony apunguze Mshahara wake. .

    Source Ben Jacobs

    #SportsElite
    🚨 Ofa ya klabu ya £25m ya Real Betis ilikubaliwa na Man United Kuhusu kumsajili Antony na tayari Man United ilimpa ruhusa Antony kusafiri kuelekea Spain Lakini saa chache baadae Real Betis imebadilishaa msimamo wake na kujiondoa kwenye mazungumzo wakidai kuwa mshahara wa Antony ni mkubwa hivyo hawataweza vinginevyo Man United wapungize Bei ya Antony au Antony apunguze Mshahara wake. 🥴🇧🇷. Source Ben Jacobs #SportsElite
    0 Commenti 0 condivisioni 847 Views
  • #BREAKING

    Klabu imelazimika kuweka rehani vitu vyao vya thamani vyenye thamani ya £7m Ili waweza kufanikisha Mchakato wa kuwasajili wachezaji wao wapya waliosajiliwa katika dirisha hili la usajili.

    Mpaka kufikia Sasa hakuna mchezaji yoyote mpya wa FC Barcelona ambae ataruhusiwa kucheza mashindano yoyote msimu ujao, kwasababu jina lake halitambuliki na Laliga.

    Wachezaji ambao Laliga haiwatambui mpaka Sasa ni:

    - Marcus Rashford
    - Joan García
    - Roony Bardghi
    - Gerard Martín
    - Wojciech Szczęsny.

    Wachezaji wote hawa hawatoshiriki Mchezo wowote wakiwa na FC Barcelona mpaka klabu hiyo ikamilishe taratibu zote za kuwasajili kwenye mifumo ya Laliga,na Laliga wanahitaji Sheria zifuatwe tu,hawahitaji mazungumzo Wala busara.

    Source: [ The AthleticFC ]

    #SportsElite
    #BREAKING 🔴 Klabu imelazimika kuweka rehani vitu vyao vya thamani vyenye thamani ya £7m Ili waweza kufanikisha Mchakato wa kuwasajili wachezaji wao wapya waliosajiliwa katika dirisha hili la usajili. Mpaka kufikia Sasa hakuna mchezaji yoyote mpya wa FC Barcelona ambae ataruhusiwa kucheza mashindano yoyote msimu ujao, kwasababu jina lake halitambuliki na Laliga. Wachezaji ambao Laliga haiwatambui mpaka Sasa ni: - Marcus Rashford - Joan García - Roony Bardghi - Gerard Martín - Wojciech Szczęsny. Wachezaji wote hawa hawatoshiriki Mchezo wowote wakiwa na FC Barcelona mpaka klabu hiyo ikamilishe taratibu zote za kuwasajili kwenye mifumo ya Laliga,na Laliga wanahitaji Sheria zifuatwe tu,hawahitaji mazungumzo Wala busara. Source: [ The AthleticFC ] #SportsElite
    0 Commenti 0 condivisioni 904 Views
  • Hizi ndizo sheria mpya za Ligi Kuu Uingereza(EPL);

    Waamuzi sasa wanaweza kueleza maamuzi yao ya VAR kupitia mfumo wa sauti wa uwanjani.

    Ni nahodha pekee anayeruhusiwa kumkaribia mwamuzi wakati wa kujadili uamuzi.

    Mchezaji akipiga penalti mara mbili mfululizo(double-kick), penalti hiyo itarudiwa.

    Kipa haruhusiwi kushikilia mpira kwa zaidi ya sekunde nane; akifanya hivyo, kona itapewa kwa timu pinzani.

    Kocha anaruhusiwa kuzungumza na wachezaji wakati wa mapumziko ikiwa timu yake inaongoza.

    Kamera zinaruhusiwa kuingia katika chumba cha kubadilishia nguo (dressing room).

    Mchezaji aliyetolewa uwanjani anaweza kuhojiwa wakati mechi bado inaendelea.

    #SportsElite
    👨‍⚖️🏴󠁧󠁢󠁥󠁮󠁧󠁿Hizi ndizo sheria mpya za Ligi Kuu Uingereza(EPL); ✅Waamuzi sasa wanaweza kueleza maamuzi yao ya VAR kupitia mfumo wa sauti wa uwanjani. ✅Ni nahodha pekee anayeruhusiwa kumkaribia mwamuzi wakati wa kujadili uamuzi. ✅Mchezaji akipiga penalti mara mbili mfululizo(double-kick), penalti hiyo itarudiwa. ✅Kipa haruhusiwi kushikilia mpira kwa zaidi ya sekunde nane; akifanya hivyo, kona itapewa kwa timu pinzani. ✅Kocha anaruhusiwa kuzungumza na wachezaji wakati wa mapumziko ikiwa timu yake inaongoza. ✅Kamera zinaruhusiwa kuingia katika chumba cha kubadilishia nguo (dressing room). ✅Mchezaji aliyetolewa uwanjani anaweza kuhojiwa wakati mechi bado inaendelea. #SportsElite
    0 Commenti 0 condivisioni 463 Views
  • Manager wa Club ya PSG Luis Enrique amesema kuwa yuko mbioni katika sakata la kumsajiri aliyekuwa kiungo wa Real Madrid Eduardo Camavinga licha ya kuwa majeruhii hayo yamesemwa na Luis Enrique manager wa PSG
    Manager wa Club ya PSG Luis Enrique amesema kuwa yuko mbioni katika sakata la kumsajiri aliyekuwa kiungo wa Real Madrid Eduardo Camavinga licha ya kuwa majeruhii hayo yamesemwa na Luis Enrique manager wa PSG
    0 Commenti 0 condivisioni 433 Views
Pagine in Evidenza