• Ushirikiano wa RDC – Monaco unakabiliwa na changamoto?

    Ushirikiano kati ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na klabu ya AS Monaco unaweza kuwa kwenye hatari, ikizingatiwa taarifa zilizotolewa na Gazeti la L’Équipe la Nchini Ufaransa.

    Taarifa hizo zinaonyesha kwamba malalamiko ya "kuficha fedha", "kufurushwa fedha za umma" (Wizi) na "ufisadi" yamewasilishwa katika Tume ya Ufilisi wa Kifedha ya Taifa (PNF) mnamo Septemba 2025.

    Malalamiko haya yanahusu mkataba uliosainiwa kati ya Wizara ya Michezo ya RDC na AS Monaco mwezi Juni mwaka jana.

    Baada ya miezi kadhaa ya uchambuzi, PNF imetuma ripoti rasmi kwa mamlaka za Monaco. Hivyo, sasa kesi hiyo ipo mikononi mwa Mahakama ya Dola la Nchi ya Monaco.

    Hali hii inachukua sura mpya katika uhusiano wa michezo na uwekezaji kati ya RDC na Monaco, huku mashabiki na wanasiasa wakilenga kuona matokeo ya kesi hii.

    Toa maoni yako
    #Habari
    Ushirikiano wa RDC – Monaco unakabiliwa na changamoto? Ushirikiano kati ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na klabu ya AS Monaco unaweza kuwa kwenye hatari, ikizingatiwa taarifa zilizotolewa na Gazeti la L’Équipe la Nchini Ufaransa. Taarifa hizo zinaonyesha kwamba malalamiko ya "kuficha fedha", "kufurushwa fedha za umma" (Wizi) na "ufisadi" yamewasilishwa katika Tume ya Ufilisi wa Kifedha ya Taifa (PNF) mnamo Septemba 2025. Malalamiko haya yanahusu mkataba uliosainiwa kati ya Wizara ya Michezo ya RDC na AS Monaco mwezi Juni mwaka jana. Baada ya miezi kadhaa ya uchambuzi, PNF imetuma ripoti rasmi kwa mamlaka za Monaco. Hivyo, sasa kesi hiyo ipo mikononi mwa Mahakama ya Dola la Nchi ya Monaco. Hali hii inachukua sura mpya katika uhusiano wa michezo na uwekezaji kati ya RDC na Monaco, huku mashabiki na wanasiasa wakilenga kuona matokeo ya kesi hii. Toa maoni yako #Habari
    0 Kommentare 0 Anteile 95 Ansichten
  • Koffi Olomide atangaza tamasha kubwa Ubelgiji baada ya kufutwa matamasha yake Ufaransa.

    Mwanamuziki Nguli wa rumba ya Congo, Koffi Olomide, ametangaza rasmi kufanya tamasha kubwa katika Ubelgiji, baada ya kukumbana na changamoto ya kufutwa kwa matamasha kadhaa nchini Ufaransa.

    Tamasha hilo limepangwa kufanyika tarehe 11 Julai 2026 katika Uwanja maarufu wa Stade Roi Baudouin uliopo Jijini Brussels. Tangazo hili limeibua msisimko mkubwa miongoni mwa mashabiki wa muziki wa Congo na rumba kwa ujumla barani Ulaya na Afrika.

    Kupitia matangazo yake ya moja kwa moja kwenye TikTok, Msanii huyo alieleza dhamira yake ya kuifanya siku hiyo kuwa ya kipekee katika maisha yake ya muziki.

    Amesema kuwa anataka tarehe hiyo iwe tukio la kihistoria, akisherehekea miaka yake 70 ya kuzaliwa akiwa pamoja na mashabiki wake.

    Tamasha hilo linatajwa kuwa uzalishaji mkubwa (grande production) unaotarajiwa kuvuta maelfu ya watu katika Uwanja huo wenye historia ya kuandaa matukio makubwa ya kimataifa ya michezo na burudani.

    Hatua hii inakuja baada ya kufutwa kwa matamasha kadhaa ya Msanii huyo nchini Ufaransa, jambo lililozua mjadala mpana katika tasnia ya muziki. Hata hivyo, tangazo la Brussels linaonekana kama kurejea kwa nguvu kwa Gwiji huyo wa rumba, akionyesha kuwa bado ana ushawishi mkubwa na soko imara barani Ulaya.

    Kwa wapenzi wa rumba na muziki wa Congo, tukio hili tayari linaonekana kuwa miongoni mwa matamasha makubwa zaidi ya mwaka 2026. Kwa historia ndefu ya Koffi Olomide katika muziki, tamasha hili linatarajiwa kuwa zaidi ya burudani bali ni sherehe ya urithi, mafanikio na mchango wake katika kukuza rumba ya Kongo kimataifa.

    Mashabiki sasa wanasubiri kwa hamu maandalizi rasmi, mauzo ya tiketi na orodha ya Wasanii watakaoshiriki katika usiku huo unaotarajiwa kuwa wa kipekee.

    Toa maoni yako
    #Habari
    Koffi Olomide atangaza tamasha kubwa Ubelgiji baada ya kufutwa matamasha yake Ufaransa. Mwanamuziki Nguli wa rumba ya Congo, Koffi Olomide, ametangaza rasmi kufanya tamasha kubwa katika Ubelgiji, baada ya kukumbana na changamoto ya kufutwa kwa matamasha kadhaa nchini Ufaransa. Tamasha hilo limepangwa kufanyika tarehe 11 Julai 2026 katika Uwanja maarufu wa Stade Roi Baudouin uliopo Jijini Brussels. Tangazo hili limeibua msisimko mkubwa miongoni mwa mashabiki wa muziki wa Congo na rumba kwa ujumla barani Ulaya na Afrika. Kupitia matangazo yake ya moja kwa moja kwenye TikTok, Msanii huyo alieleza dhamira yake ya kuifanya siku hiyo kuwa ya kipekee katika maisha yake ya muziki. Amesema kuwa anataka tarehe hiyo iwe tukio la kihistoria, akisherehekea miaka yake 70 ya kuzaliwa akiwa pamoja na mashabiki wake. Tamasha hilo linatajwa kuwa uzalishaji mkubwa (grande production) unaotarajiwa kuvuta maelfu ya watu katika Uwanja huo wenye historia ya kuandaa matukio makubwa ya kimataifa ya michezo na burudani. Hatua hii inakuja baada ya kufutwa kwa matamasha kadhaa ya Msanii huyo nchini Ufaransa, jambo lililozua mjadala mpana katika tasnia ya muziki. Hata hivyo, tangazo la Brussels linaonekana kama kurejea kwa nguvu kwa Gwiji huyo wa rumba, akionyesha kuwa bado ana ushawishi mkubwa na soko imara barani Ulaya. Kwa wapenzi wa rumba na muziki wa Congo, tukio hili tayari linaonekana kuwa miongoni mwa matamasha makubwa zaidi ya mwaka 2026. Kwa historia ndefu ya Koffi Olomide katika muziki, tamasha hili linatarajiwa kuwa zaidi ya burudani bali ni sherehe ya urithi, mafanikio na mchango wake katika kukuza rumba ya Kongo kimataifa. Mashabiki sasa wanasubiri kwa hamu maandalizi rasmi, mauzo ya tiketi na orodha ya Wasanii watakaoshiriki katika usiku huo unaotarajiwa kuwa wa kipekee. Toa maoni yako #Habari
    0 Kommentare 0 Anteile 53 Ansichten
  • Macron: “Ufaransa bila Wayahudi ni kama mti usio na shina”.

    Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron amesema kuwa Ufaransa haiwezi kujitambulisha kikamilifu bila uwepo wa Wayahudi, akisisitiza mchango wao wa kihistoria, kiutamaduni na kijamii katika taifa hilo la Ulaya.

    Akizungumza katika hafla maalum ya kumbukumbu na mshikamano wa kijamii, Macron alitoa kauli iliyogusa hisia za wengi akisema: “Ufaransa bila Wayahudi ni kama mti usio na shina.”

    Kauli hiyo imefasiriwa kama ujumbe wa wazi wa kupinga chuki dhidi ya Wayahudi (antisemitism) na kuimarisha misingi ya umoja wa kitaifa katika jamii yenye tamaduni na dini tofauti.

    Kwa miaka ya hivi karibuni, Ufaransa imekumbwa na matukio kadhaa ya chuki dhidi ya Wayahudi, hali ambayo imezua wasiwasi mkubwa ndani na nje ya nchi. Serikali ya Macron imekuwa ikisisitiza mara kwa mara umuhimu wa kulinda uhuru wa kuabudu, usawa na heshima kwa makundi yote ya kidini.

    Kwa kutumia taswira ya “mti na shina,” Rais huyo alilenga kuonyesha kuwa Wayahudi ni sehemu ya mizizi ya historia ya Ufaransa, si kundi la pembeni bali ni sehemu ya msingi wa taifa hilo.

    Ufaransa ina moja ya jamii kubwa zaidi za Wayahudi barani Ulaya. Kwa karne nyingi, Wayahudi wamechangia katika sekta mbalimbali zikiwemo elimu, biashara, sayansi, sanaa na siasa. Hata hivyo, historia hiyo pia imegubikwa na vipindi vya mateso, hususan wakati wa Vita Kuu ya Pili ya Dunia.

    Kauli ya Macron inaonekana kuendeleza msimamo wa viongozi waliotangulia katika kulinda kumbukumbu za kihistoria na kuhakikisha kuwa matukio ya ubaguzi hayajirudii.

    Kwa ujumla, kauli hiyo imechukuliwa kama wito wa kuimarisha mshikamano wa kitaifa na kulinda misingi ya kidemokrasia.

    Kwa kusema kuwa “Ufaransa bila Wayahudi ni kama mti usio na shina,” Macron amesisitiza kwamba utofauti wa kidini na kitamaduni si udhaifu bali ni nguzo muhimu ya taifa la Ufaransa.

    Toa maoni yako
    #Habari
    🇫🇷 Macron: “Ufaransa bila Wayahudi ni kama mti usio na shina”. Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron amesema kuwa Ufaransa haiwezi kujitambulisha kikamilifu bila uwepo wa Wayahudi, akisisitiza mchango wao wa kihistoria, kiutamaduni na kijamii katika taifa hilo la Ulaya. Akizungumza katika hafla maalum ya kumbukumbu na mshikamano wa kijamii, Macron alitoa kauli iliyogusa hisia za wengi akisema: “Ufaransa bila Wayahudi ni kama mti usio na shina.” Kauli hiyo imefasiriwa kama ujumbe wa wazi wa kupinga chuki dhidi ya Wayahudi (antisemitism) na kuimarisha misingi ya umoja wa kitaifa katika jamii yenye tamaduni na dini tofauti. Kwa miaka ya hivi karibuni, Ufaransa imekumbwa na matukio kadhaa ya chuki dhidi ya Wayahudi, hali ambayo imezua wasiwasi mkubwa ndani na nje ya nchi. Serikali ya Macron imekuwa ikisisitiza mara kwa mara umuhimu wa kulinda uhuru wa kuabudu, usawa na heshima kwa makundi yote ya kidini. Kwa kutumia taswira ya “mti na shina,” Rais huyo alilenga kuonyesha kuwa Wayahudi ni sehemu ya mizizi ya historia ya Ufaransa, si kundi la pembeni bali ni sehemu ya msingi wa taifa hilo. Ufaransa ina moja ya jamii kubwa zaidi za Wayahudi barani Ulaya. Kwa karne nyingi, Wayahudi wamechangia katika sekta mbalimbali zikiwemo elimu, biashara, sayansi, sanaa na siasa. Hata hivyo, historia hiyo pia imegubikwa na vipindi vya mateso, hususan wakati wa Vita Kuu ya Pili ya Dunia. Kauli ya Macron inaonekana kuendeleza msimamo wa viongozi waliotangulia katika kulinda kumbukumbu za kihistoria na kuhakikisha kuwa matukio ya ubaguzi hayajirudii. Kwa ujumla, kauli hiyo imechukuliwa kama wito wa kuimarisha mshikamano wa kitaifa na kulinda misingi ya kidemokrasia. Kwa kusema kuwa “Ufaransa bila Wayahudi ni kama mti usio na shina,” Macron amesisitiza kwamba utofauti wa kidini na kitamaduni si udhaifu bali ni nguzo muhimu ya taifa la Ufaransa. Toa maoni yako #Habari
    0 Kommentare 0 Anteile 240 Ansichten
  • Nchi ya Kenya yakemea vitendo vya kuwapeleka Vijana wake kwenye vita Nchini Ukraine.

    Serikali ya Kenya imekemea vikali vitendo vya baadhi ya Mawakala wanaodanganya Vijana kwa ahadi za ajira, kisha kuwapeleka moja kwa moja kwenye vita vinavyoendelea nchini Ukraine.

    Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya, Musalia Mudavadi, amesema: “Tunatarajia kufanya ziara rasmi mjini Moscow kwa mazungumzo na Serikali ya Urusi, lengo likiwa kusitisha kabisa matumizi ya raia wa Kenya katika mapambano haya.”

    Mudavadi alibainisha kuwa tayari Wakenya kadhaa wamefariki dunia, huku wengine wakijeruhiwa vibaya baada ya kudanganywa kuingia mikataba ya kijeshi. Amesema: “Hatukubali upotevu wa maisha ya raia wetu. Hatua za kudumu lazima zichukuliwe.”

    Serikali ya Kenya imelaumu Mawakala wa ajira wanaoshawishi vijana kwa ahadi za mishahara mikubwa, kisha kuwapeleka mstari wa mbele vitani. Ripoti ya hivi karibuni ya shirika la habari la Ufaransa, Agence France-Presse, imethibitisha kuwepo kwa mtandao wa udanganyifu unaowaingiza vijana wasiokuwa na historia ya kijeshi kusaini mikataba na Jeshi la Urusi, kisha kupelekwa haraka kwenye Uwanja wa mapambano.

    Mudavadi amesisitiza kuwa Kenya itafuatilia pia suala la kuachiliwa kwa Wakenya waliokamatwa kama wafungwa wa kivita nchini Ukraine. Amesema hatua hizi ni muhimu ili kulinda maisha ya Raia wake.

    Toa maoni yako
    #Habari
    #Russia #Ukraine #MusaliaMudavadi #Moscow #BreakingNews #WorldNews #VitaUkraine #KenyaAbroad #HumanRights #AfricaNews
    Nchi ya Kenya yakemea vitendo vya kuwapeleka Vijana wake kwenye vita Nchini Ukraine. Serikali ya Kenya imekemea vikali vitendo vya baadhi ya Mawakala wanaodanganya Vijana kwa ahadi za ajira, kisha kuwapeleka moja kwa moja kwenye vita vinavyoendelea nchini Ukraine. Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya, Musalia Mudavadi, amesema: “Tunatarajia kufanya ziara rasmi mjini Moscow kwa mazungumzo na Serikali ya Urusi, lengo likiwa kusitisha kabisa matumizi ya raia wa Kenya katika mapambano haya.” Mudavadi alibainisha kuwa tayari Wakenya kadhaa wamefariki dunia, huku wengine wakijeruhiwa vibaya baada ya kudanganywa kuingia mikataba ya kijeshi. Amesema: “Hatukubali upotevu wa maisha ya raia wetu. Hatua za kudumu lazima zichukuliwe.” Serikali ya Kenya imelaumu Mawakala wa ajira wanaoshawishi vijana kwa ahadi za mishahara mikubwa, kisha kuwapeleka mstari wa mbele vitani. Ripoti ya hivi karibuni ya shirika la habari la Ufaransa, Agence France-Presse, imethibitisha kuwepo kwa mtandao wa udanganyifu unaowaingiza vijana wasiokuwa na historia ya kijeshi kusaini mikataba na Jeshi la Urusi, kisha kupelekwa haraka kwenye Uwanja wa mapambano. Mudavadi amesisitiza kuwa Kenya itafuatilia pia suala la kuachiliwa kwa Wakenya waliokamatwa kama wafungwa wa kivita nchini Ukraine. Amesema hatua hizi ni muhimu ili kulinda maisha ya Raia wake. Toa maoni yako #Habari #Russia #Ukraine #MusaliaMudavadi #Moscow #BreakingNews #WorldNews #VitaUkraine #KenyaAbroad #HumanRights #AfricaNews
    0 Kommentare 2 Anteile 433 Ansichten
  • Mmiliki wa Sunderland, Kyril Louis-Dreyfus ana umri wa miaka 27 tuu, na alikuwa na umri wa miaka 23 kipindi aliponunua klabu hiyo ilipokuwa League one pale England...

    Yeye ni Mswisi mwenye asili ya Ufaransa na ni mmoja wa memba wa familia ya Mfaransa Louis-Dreyfus ambao walikuwa wamiliki wa zamani wa Olympic Marseille.

    Alikuwa mwenyekiti mdogo zaidi wa klabu hiyo pindi alipokuwa majority shareholder wa Sunderland na hadi sasa wakiwa wanafanya vizuri kwenye Premier League.

    Yeye ndiye sababu kuu, nahodha wa Uswisi Granit Xhaka kuamua kujiunga na Sunderland Dirisha liliopita la Usajili kutokea Bayer Leverkusen, na kuwa moja ya Usajili Bora kwenye Premier League msimu huu...
    🚨 Mmiliki wa Sunderland, Kyril Louis-Dreyfus ana umri wa miaka 27 tuu, na alikuwa na umri wa miaka 23 kipindi aliponunua klabu hiyo ilipokuwa League one pale England... Yeye ni Mswisi mwenye asili ya Ufaransa na ni mmoja wa memba wa familia ya Mfaransa Louis-Dreyfus ambao walikuwa wamiliki wa zamani wa Olympic Marseille. Alikuwa mwenyekiti mdogo zaidi wa klabu hiyo pindi alipokuwa majority shareholder wa Sunderland na hadi sasa wakiwa wanafanya vizuri kwenye Premier League. Yeye ndiye sababu kuu, nahodha wa Uswisi Granit Xhaka kuamua kujiunga na Sunderland Dirisha liliopita la Usajili kutokea Bayer Leverkusen, na kuwa moja ya Usajili Bora kwenye Premier League msimu huu...
    0 Kommentare 0 Anteile 1KB Ansichten
  • Rais wa Madagascar, Andry Rajoelina, amesema amejificha “mahali salama” baada ya jaribio la kumuua, kufuatia wiki kadhaa za maandamano yanayomtaka ajiuzulu.

    Kupitia matangazo ya moja kwa moja kwenye Facebook, Rajoelina (51) alidai kuwa kundi la wanajeshi na wanasiasa lilipanga kumuua, bila kufichua alipo. Ripoti ambazo hazijathibitishwa zinadai huenda alitoroka nchini kwa ndege ya kijeshi ya Ufaransa.

    Maandamano makubwa yanayoongozwa na vijana yamekuwa yakiendelea kote nchini, wakilalamikia hali ngumu ya kiuchumi na utawala wa kiimla. Serikali haijatoa tamko rasmi kuhusu jaribio hilo, huku hali ya taharuki ikiendelea katika mji mkuu, Antananarivo.

    Tufuatilie kupitia YouTube ya NIOKOE TV
    Rais wa Madagascar, Andry Rajoelina, amesema amejificha “mahali salama” baada ya jaribio la kumuua, kufuatia wiki kadhaa za maandamano yanayomtaka ajiuzulu. Kupitia matangazo ya moja kwa moja kwenye Facebook, Rajoelina (51) alidai kuwa kundi la wanajeshi na wanasiasa lilipanga kumuua, bila kufichua alipo. Ripoti ambazo hazijathibitishwa zinadai huenda alitoroka nchini kwa ndege ya kijeshi ya Ufaransa. Maandamano makubwa yanayoongozwa na vijana yamekuwa yakiendelea kote nchini, wakilalamikia hali ngumu ya kiuchumi na utawala wa kiimla. Serikali haijatoa tamko rasmi kuhusu jaribio hilo, huku hali ya taharuki ikiendelea katika mji mkuu, Antananarivo. 🔴 Tufuatilie kupitia YouTube ya NIOKOE TV
    0 Kommentare 0 Anteile 836 Ansichten
  • Usajili: Bakambu kuwindwa Brazil… kwenye nyayo za Bolasie

    Mshambuliaji wa kimataifa wa DR Congo, Cédric Bakambu, amewekwa kwenye rada za klabu ya Brazil Atlético-MG.

    Kwa mujibu wa taarifa za Bolavip la Brazil, Bakambu ni miongoni mwa wachezaji wanaolengwa na mabingwa hao wa soka kwa ajili ya kuimarisha kikosi chao kuelekea msimu ujao.
    Kocha mpya wa Atlético-MG, Jorge Sampaoli, raia wa Argentina, amempa Bakambu kipaumbele katika usajili. Wawili hawa wana historia ya kufanya kazi pamoja wakiwa Olympique de Marseille nchini Ufaransa na wanaheshimiana sana.

    Takwimu za Bakambu akiwa Real Betis

    Bakambu alijiunga na Real Betis mwaka 2024 akitokea Galatasaray kwa ada ya euro milioni 5.
    Amecheza jumla ya michezo 52 kwenye mashindano yote, akifunga mabao 12 na kutoa asisti 4.
    Kwa sasa ana mkataba na Real Betis hadi mwaka 2026, huku thamani yake sokoni ikikadiriwa kuwa euro milioni 1.5.
    Usajili: Bakambu kuwindwa Brazil… kwenye nyayo za Bolasie Mshambuliaji wa kimataifa wa DR Congo, Cédric Bakambu, amewekwa kwenye rada za klabu ya Brazil Atlético-MG. Kwa mujibu wa taarifa za Bolavip la Brazil, Bakambu ni miongoni mwa wachezaji wanaolengwa na mabingwa hao wa soka kwa ajili ya kuimarisha kikosi chao kuelekea msimu ujao. Kocha mpya wa Atlético-MG, Jorge Sampaoli, raia wa Argentina, amempa Bakambu kipaumbele katika usajili. Wawili hawa wana historia ya kufanya kazi pamoja wakiwa Olympique de Marseille nchini Ufaransa na wanaheshimiana sana. Takwimu za Bakambu akiwa Real Betis Bakambu alijiunga na Real Betis mwaka 2024 akitokea Galatasaray kwa ada ya euro milioni 5. Amecheza jumla ya michezo 52 kwenye mashindano yote, akifunga mabao 12 na kutoa asisti 4. Kwa sasa ana mkataba na Real Betis hadi mwaka 2026, huku thamani yake sokoni ikikadiriwa kuwa euro milioni 1.5.
    Love
    1
    0 Kommentare 0 Anteile 594 Ansichten
  • ... 𝗞𝗬𝗟𝗜𝗔𝗡 𝗠𝗕𝗔𝗣𝗣𝗘

    Kwenye mchezo dhidi ya Iceland usiku wa jana, Kylian Mbappé Lottin alifunga bao lake la 52 akiwa na Ufaransa -- na kuwa mfungaji bora wa pili wa muda wote akimpita Thierry Henry .

    57 04 132 - Olivier Giroud
    52 12 092 - Kylian Mbappé
    51 02 123 - Thierry Henry

    Anakuwa mchezaji wa pili wa Europa katika karne ya 21 kuifungia timu yake ya taifa ya wakubwa mabao 52 kabla ya kufikisha umri wa miaka 27, baada ya Romelu Lukaku akiwa na Belgium .

    Kylian Mbappé akiwa na timu ya taifa ya wakubwa ya Ufaransa .

    ◉ 92 - Games.
    ◉ 52 - Goals (second top scorer)
    ◉ 33 - Assists (best assist provider)
    ◉ 85 - Goals/assists.
    ◉ 12 - Penalty.
    ◉ 03 - Hat trick.

    Key .......
    _______________
    - Games
    - Goals
    - Penalty

    Follow us.

    #imansportnews #PlayStation #WorldCupQualifiers2026
    ... 𝗞𝗬𝗟𝗜𝗔𝗡 𝗠𝗕𝗔𝗣𝗣𝗘 🔥 Kwenye mchezo dhidi ya Iceland usiku wa jana, Kylian Mbappé Lottin alifunga bao lake la 52 akiwa na Ufaransa -- na kuwa mfungaji bora wa pili wa muda wote akimpita Thierry Henry . ⚽ 57 🥅 04 🎮 132 - Olivier Giroud ⚽ 52 🥅 12 🎮 092 - Kylian Mbappé ⚽ 51 🥅 02 🎮 123 - Thierry Henry Anakuwa mchezaji wa pili wa Europa katika karne ya 21 kuifungia timu yake ya taifa 🇨🇵 ya wakubwa mabao 52 kabla ya kufikisha umri wa miaka 27, baada ya Romelu Lukaku akiwa na Belgium 🇧🇪 . Kylian Mbappé akiwa na timu ya taifa ya wakubwa ya Ufaransa 🇨🇵 . ◉ 92 - Games. ◉ 52 - Goals (second top scorer) ◉ 33 - Assists (best assist provider) ◉ 85 - Goals/assists. ◉ 12 - Penalty. ◉ 03 - Hat trick. Key ....... 🔑 _______________ 🎮 - Games ⚽ - Goals 🥅 - Penalty Follow us. #imansportnews #PlayStation #WorldCupQualifiers2026
    0 Kommentare 0 Anteile 2KB Ansichten
  • BREAKING : FC Barcelona wamejipanga kimkakati kuhakikisha wanamsajili Beki kitasa wa Liverpool FC raia wa Ufaransa Ibrahima Konaté katika dirisha hili la usajili.

    FC Barcelona wanaamini ofa waliyoiandaa, haiwezi kataliwa na Liverpool FC

    #SportsElite
    BREAKING 🔴: FC Barcelona wamejipanga kimkakati kuhakikisha wanamsajili Beki kitasa wa Liverpool FC raia wa Ufaransa 🇨🇵 Ibrahima Konaté katika dirisha hili la usajili. FC Barcelona wanaamini ofa waliyoiandaa, haiwezi kataliwa na Liverpool FC #SportsElite
    0 Kommentare 0 Anteile 517 Ansichten
  • RASMI

    Nathan Ngoy ajiunga rasmi na LOSC Lille kutoka Standard Liège kwa dau la €4.5M.

    Beki huyo mwenye umri wa miaka 22 amesaini mkataba wa miaka minne na klabu hiyo ya Ufaransa.

    #SportsElite
    📢 RASMI✅ Nathan Ngoy ajiunga rasmi na LOSC Lille kutoka Standard Liège kwa dau la €4.5M. 🔴⚪ Beki huyo mwenye umri wa miaka 22 amesaini mkataba wa miaka minne na klabu hiyo ya Ufaransa. ✍️💪 #SportsElite
    0 Kommentare 0 Anteile 292 Ansichten
  • Barcelona kunufaika kwa €2 milioni kutokana na jeraha la Ter Stegen

    Ripoti ya habari imeeleza uwezekano wa klabu ya FC Barcelona kupokea kiasi cha €2 milioni kufuatia jeraha la mlinda mlango wao wa Kijerumani, Marc-André ter Stegen .

    Kwa mujibu wa Mundo Deportivo, Barcelona waligundua kwanza jeraha la Ter Stegen baada ya mechi za UEFA Nations League dhidi ya Ureno na Ufaransa zilizochezwa Juni 4 na 8.

    Ripoti hiyo imeongeza:

    > "Barcelona waliiarifu FIFA mapema kuhusu matatizo ya mgongo aliyopata Ter Stegen, ambayo yalitokana na mechi zake za hivi karibuni na timu ya taifa ya Ujerumani ."

    Kwa hivyo, FIFA huenda ikalazimika kulipa fidia kifedha kwa Barcelona ikiwa Ter Stegen atakuwa nje ya uwanja kwa zaidi ya siku 28 mfululizo kutokana na jeraha alilopata akiwa kwenye majukumu ya kimataifa .

    Ripoti hiyo imeeleza kuwa klabu ya Catalonia inaweza kupata zaidi ya €2 milioni kutokana na hali hiyo.

    Barcelona tayari waliwahi kunufaika na mpango wa fidia wa FIFA ujulikanao kama Club Protection Program wakati Gavi alipoumia vibaya akiwa na timu ya taifa ya Hispania mwaka 2023, na pia walipopata fidia baada ya Ronald Araújo kuumia akiwa na Uruguay wakati wa Copa América 2024.

    Kwa upande wa Ter Stegen, ikiwa atakosa mashindano kwa miezi 4, Barcelona wangeweza kupokea hadi €2.46 milioni.

    #SportsElite
    🚨 Barcelona kunufaika kwa €2 milioni kutokana na jeraha la Ter Stegen 💰 Ripoti ya habari imeeleza uwezekano wa klabu ya FC Barcelona kupokea kiasi cha €2 milioni kufuatia jeraha la mlinda mlango wao wa Kijerumani, Marc-André ter Stegen 🤕. Kwa mujibu wa Mundo Deportivo, Barcelona waligundua kwanza jeraha la Ter Stegen baada ya mechi za UEFA Nations League dhidi ya Ureno 🇵🇹 na Ufaransa 🇫🇷 zilizochezwa Juni 4 na 8. Ripoti hiyo imeongeza: > "Barcelona waliiarifu FIFA mapema kuhusu matatizo ya mgongo aliyopata Ter Stegen, ambayo yalitokana na mechi zake za hivi karibuni na timu ya taifa ya Ujerumani 🇩🇪." Kwa hivyo, FIFA huenda ikalazimika kulipa fidia kifedha kwa Barcelona ikiwa Ter Stegen atakuwa nje ya uwanja kwa zaidi ya siku 28 mfululizo kutokana na jeraha alilopata akiwa kwenye majukumu ya kimataifa 🏥. Ripoti hiyo imeeleza kuwa klabu ya Catalonia inaweza kupata zaidi ya €2 milioni kutokana na hali hiyo. Barcelona tayari waliwahi kunufaika na mpango wa fidia wa FIFA ujulikanao kama Club Protection Program wakati Gavi alipoumia vibaya akiwa na timu ya taifa ya Hispania 🇪🇸 mwaka 2023, na pia walipopata fidia baada ya Ronald Araújo kuumia akiwa na Uruguay 🇺🇾 wakati wa Copa América 2024. Kwa upande wa Ter Stegen, ikiwa atakosa mashindano kwa miezi 4, Barcelona wangeweza kupokea hadi €2.46 milioni. #SportsElite
    0 Kommentare 0 Anteile 1KB Ansichten
  • Klabu ya Everton imemkaribisha rasmi mshambuliaji chipukizi Thierno Barry ambaye awali alikuwa Villarreal. Barry, anayewakilisha timu ya taifa ya vijana ya Ufaransa chini ya miaka 21, sasa atakuwa sehemu ya kikosi cha Everton kwa mkataba wa miaka minne. DDiili hilo linaripotiwa harimu takribani pauni milionii 27.5.

    #SportsElite
    Klabu ya Everton imemkaribisha rasmi mshambuliaji chipukizi Thierno Barry ambaye awali alikuwa Villarreal. Barry, anayewakilisha timu ya taifa ya vijana ya Ufaransa chini ya miaka 21, sasa atakuwa sehemu ya kikosi cha Everton kwa mkataba wa miaka minne. DDiili hilo linaripotiwa harimu takribani pauni milionii 27.5. 🔵 #SportsElite
    0 Kommentare 0 Anteile 460 Ansichten
  • 𝗕𝗥𝗘𝗔𝗞𝗜𝗡𝗚: Klabu ya Olympique Lyon imeshinda rufaa yake na sasa Klabu hiyo itashiriki Ligi kuu Ufaransa msimu ujao na pia itacheza Europa League.

    Olympique Lyon ilishushwa Daraja mwezi uliopita kutokana na madeni na sasa imekubaliwa rufaa yake.

    #SportsElite
    🚨 𝗕𝗥𝗘𝗔𝗞𝗜𝗡𝗚: Klabu ya Olympique Lyon imeshinda rufaa yake na sasa Klabu hiyo itashiriki Ligi kuu Ufaransa msimu ujao na pia itacheza Europa League. Olympique Lyon ilishushwa Daraja mwezi uliopita kutokana na madeni na sasa imekubaliwa rufaa yake. #SportsElite
    0 Kommentare 0 Anteile 381 Ansichten
  • 𝐁𝐑𝐄𝐀𝐊𝐈𝐍𝐆: Isak Jansson yuko mbioni kujiunga na OGC Nice kutokeanSK Rapid kwa gharama ya €10M na nyongeza zaidi..

    Anatarajia kuwasili Ufaransa ndani ya masaa 24-48 kukamilisha uhamisho wake..

    Jansson pia alikuwa anafatiliwa na vilabu kama Celtic na timu za Italia kabla kufanya maamuzi Nice.

    #SportsElite
    🚨💣 𝐁𝐑𝐄𝐀𝐊𝐈𝐍𝐆: Isak Jansson yuko mbioni kujiunga na OGC Nice kutokeanSK Rapid kwa gharama ya €10M na nyongeza zaidi.. Anatarajia kuwasili Ufaransa ndani ya masaa 24-48 kukamilisha uhamisho wake.. Jansson pia alikuwa anafatiliwa na vilabu kama Celtic na timu za Italia kabla kufanya maamuzi Nice. #SportsElite
    0 Kommentare 0 Anteile 438 Ansichten
  • Mamia ya Raia wa Burkina Faso wanaoishi Ufaransa wameandamana nchini Ufaransa kushinikiza Rais wa mpito wa Burkina Faso, Ibrahim Traore aondoke madarakani kwani wanadai kiongozi huyo ni Dikteta.

    Baada ya sakata hili baadhi ya Watu wanadai huenda Waandamanaji hao wamepangwa na Serikali ya Ufaransa baada ya hivi karibuni Ibrahim Traore kukata urafiki na mazoea na nchi hiyo ambayo kwa muda mrefu inadaiwa ilikuwa ikiinyonya Burkina Faso hasa kwenye eneo la madini.

    Traore tangu aingie madarakani amekuwa akipingwa sana na baadhi ya mataifa yenye nguvu Duniani, na hivi sasa Marekani inamtuhumu kuwa anatumia Madini ya Burkina Faso kwa manufaa yake binafsi siyo ya Wananchi wote.
    Mamia ya Raia wa Burkina Faso wanaoishi Ufaransa wameandamana nchini Ufaransa kushinikiza Rais wa mpito wa Burkina Faso, Ibrahim Traore aondoke madarakani kwani wanadai kiongozi huyo ni Dikteta. Baada ya sakata hili baadhi ya Watu wanadai huenda Waandamanaji hao wamepangwa na Serikali ya Ufaransa baada ya hivi karibuni Ibrahim Traore kukata urafiki na mazoea na nchi hiyo ambayo kwa muda mrefu inadaiwa ilikuwa ikiinyonya Burkina Faso hasa kwenye eneo la madini. Traore tangu aingie madarakani amekuwa akipingwa sana na baadhi ya mataifa yenye nguvu Duniani, na hivi sasa Marekani inamtuhumu kuwa anatumia Madini ya Burkina Faso kwa manufaa yake binafsi siyo ya Wananchi wote.
    Like
    3
    0 Kommentare 0 Anteile 1KB Ansichten
  • Muigizaji maarufu na Mkongwe Duniani, Jean-Claude Van Damme anakabiliwa na mashtaka ya kujibu baada ya kudaiwa kufanya ngono na Wanawake waliotekwa nyara Nchini Romania .

    Kwa mujibu wa CNN, Idara ya Romania ya Uchunguzi wa Uhalifu wa kupangwa na Ugaidi (DIICOT) imewasilisha malalamiko ya jinai dhidi ya Van Damme, ikidai alifanya ngono kwa kujua na Wanawake kadhaa waliokuwa wakitumiwa katika biashara haramu ya ngono.

    Kulingana na ripoti hiyo, Mwigizaji huyo Raia wa Ubelgiji anadaiwa kukutana na Watu kadhaa ambao pia wanachunguzwa kwa uhalifu wa usafirishaji wa Binadamu, ambao walimpa fursa ya kufanya ngono na Wanamitindo watano (5) wa Kiromania kama zawadi.

    Tukio hilo linaripotiwa kutokea Cannes Nchini Ufaransa hivyo, Serikali ya hiyo inapaswa kuidhinisha mashitaka hayo ya jinai lakini haikuwekwa wazi ni lini tukio hilo lilitokea hapo Ufaransa.

    Muigizaji maarufu na Mkongwe Duniani, Jean-Claude Van Damme anakabiliwa na mashtaka ya kujibu baada ya kudaiwa kufanya ngono na Wanawake waliotekwa nyara Nchini Romania 🇷🇴. Kwa mujibu wa CNN, Idara ya Romania ya Uchunguzi wa Uhalifu wa kupangwa na Ugaidi (DIICOT) imewasilisha malalamiko ya jinai dhidi ya Van Damme, ikidai alifanya ngono kwa kujua na Wanawake kadhaa waliokuwa wakitumiwa katika biashara haramu ya ngono. Kulingana na ripoti hiyo, Mwigizaji huyo Raia wa Ubelgiji 🇧🇪 anadaiwa kukutana na Watu kadhaa ambao pia wanachunguzwa kwa uhalifu wa usafirishaji wa Binadamu, ambao walimpa fursa ya kufanya ngono na Wanamitindo watano (5) wa Kiromania kama zawadi. Tukio hilo linaripotiwa kutokea Cannes Nchini Ufaransa 🇫🇷 hivyo, Serikali ya hiyo inapaswa kuidhinisha mashitaka hayo ya jinai lakini haikuwekwa wazi ni lini tukio hilo lilitokea hapo Ufaransa.
    Like
    Love
    2
    0 Kommentare 0 Anteile 1KB Ansichten
  • Mchezaji wa kimataifa wa Ufaransa , N’Golo Kanté, ameonyesha moyo wa upendo kwa jamii kwa kujenga hospitali ya kisasa yenye thamani ya dola milioni tano (5) Nchini Mali, ikiwa ni msaada kwa Watoto na familia zisizojiweza kupata huduma bora za afya.

    Kanté, ambaye alizaliwa Jijini Paris, Ufaransa, ana asili ya Mali, Wazazi wake wakiwa Wahamiaji waliotoka Nchini Mali mwaka 1980. Jina lake N’Golo linatokana na Mfalme wa zamani wa Mali aliyewahi kutawala. Katika ziara yake Mali, Kanté alitumia muda na familia yake huku akitoa heshima kwa Baba yake na Kaka yake Marehemu.

    Mchezaji wa kimataifa wa Ufaransa 🇫🇷, N’Golo Kanté, ameonyesha moyo wa upendo kwa jamii kwa kujenga hospitali ya kisasa yenye thamani ya dola milioni tano (5) Nchini Mali, ikiwa ni msaada kwa Watoto na familia zisizojiweza kupata huduma bora za afya. Kanté, ambaye alizaliwa Jijini Paris, Ufaransa, ana asili ya Mali, Wazazi wake wakiwa Wahamiaji waliotoka Nchini Mali mwaka 1980. Jina lake N’Golo linatokana na Mfalme wa zamani wa Mali aliyewahi kutawala. Katika ziara yake Mali, Kanté alitumia muda na familia yake huku akitoa heshima kwa Baba yake na Kaka yake Marehemu.
    0 Kommentare 0 Anteile 1KB Ansichten
  • Mchezaji wa kimataifa wa Ufaransa , N’Golo Kanté, ameonyesha moyo wa upendo kwa jamii kwa kujenga hospitali ya kisasa yenye thamani ya dola milioni tano (5) Nchini Mali, ikiwa ni msaada kwa Watoto na familia zisizojiweza kupata huduma bora za afya.

    Kanté, ambaye alizaliwa Jijini Paris, Ufaransa, ana asili ya Mali, Wazazi wake wakiwa Wahamiaji waliotoka Nchini Mali mwaka 1980. Jina lake N’Golo linatokana na Mfalme wa zamani wa Mali aliyewahi kutawala. Katika ziara yake Mali, Kanté alitumia muda na familia yake huku akitoa heshima kwa Baba yake na Kaka yake Marehemu.
    Mchezaji wa kimataifa wa Ufaransa 🇫🇷, N’Golo Kanté, ameonyesha moyo wa upendo kwa jamii kwa kujenga hospitali ya kisasa yenye thamani ya dola milioni tano (5) Nchini Mali, ikiwa ni msaada kwa Watoto na familia zisizojiweza kupata huduma bora za afya. Kanté, ambaye alizaliwa Jijini Paris, Ufaransa, ana asili ya Mali, Wazazi wake wakiwa Wahamiaji waliotoka Nchini Mali mwaka 1980. Jina lake N’Golo linatokana na Mfalme wa zamani wa Mali aliyewahi kutawala. Katika ziara yake Mali, Kanté alitumia muda na familia yake huku akitoa heshima kwa Baba yake na Kaka yake Marehemu.
    0 Kommentare 0 Anteile 1KB Ansichten
  • Rais wa Nchi ya Ukraine , Volodymyr Zelensky, ametabiri kuea Rais wa Urusi , Vladimir Putin, "atakufa hivi karibuni" huku kukiwa na tetesi kuwa afya ya Kiongozi huyo wa Urusi inazorota. Zelensky alitoa kauli hiyo katika mahojiano na Waandishi wa habari Jijini Paris, Ufaransa baada ya kukutana na Rais wa Ufaransa, Emmanuel Macron na kusema kuwa "Putin atakufa hivi karibuni, na hilo ni jambo la uhakika."

    Picha za Putin zilizochunguzwa kwa muda zimezua uvumi kuhusu hali yake ya afya, hasa baada ya kuonekana na macho mekundu na alama ya ajabu kwenye mkono wake. Aidha, picha zingine zimeonyesha kovu shingoni mwake, likizua dhana kuwa huenda alipitia upasuaji wa saratani ya tezi dume.

    Ripoti za awali zilidai kuwa Putin alikuwa akifuatana mara kwa mara na Daktari bingwa wa saratani, huku uvujaji wa taarifa za kijasusi za Marekani ukionyesha kuwa alikuwa akipokea tiba ya saratani. Sanjari na hayo, amekuwa akionekana akiwa na miguu isiyo imara, akishika meza kwa nguvu, au akitikisa mguu wake mara kwa mara, hali inayoongeza mashaka kuhusu afya yake.

    Rais wa Nchi ya Ukraine 🇺🇦, Volodymyr Zelensky, ametabiri kuea Rais wa Urusi 🇷🇺, Vladimir Putin, "atakufa hivi karibuni" huku kukiwa na tetesi kuwa afya ya Kiongozi huyo wa Urusi inazorota. Zelensky alitoa kauli hiyo katika mahojiano na Waandishi wa habari Jijini Paris, Ufaransa 🇫🇷 baada ya kukutana na Rais wa Ufaransa, Emmanuel Macron na kusema kuwa "Putin atakufa hivi karibuni, na hilo ni jambo la uhakika." Picha za Putin zilizochunguzwa kwa muda zimezua uvumi kuhusu hali yake ya afya, hasa baada ya kuonekana na macho mekundu na alama ya ajabu kwenye mkono wake. Aidha, picha zingine zimeonyesha kovu shingoni mwake, likizua dhana kuwa huenda alipitia upasuaji wa saratani ya tezi dume. Ripoti za awali zilidai kuwa Putin alikuwa akifuatana mara kwa mara na Daktari bingwa wa saratani, huku uvujaji wa taarifa za kijasusi za Marekani 🇺🇸 ukionyesha kuwa alikuwa akipokea tiba ya saratani. Sanjari na hayo, amekuwa akionekana akiwa na miguu isiyo imara, akishika meza kwa nguvu, au akitikisa mguu wake mara kwa mara, hali inayoongeza mashaka kuhusu afya yake.
    0 Kommentare 0 Anteile 2KB Ansichten
  • Nchi za Niger , Burkina Faso na Mali zimetangaza rasmi kujiondoa katika Shirika la Kimataifa la Mataifa yanayozungumza Kifaransa la ‘Francophonie’ (OIF). Uamuzi huo umefanywa na Viongozi wa mataifa hayo yenye Serikali za kijeshi, Niger inaongozwa na Jenerali Abdourahamane Tchiani, Mali inaongozwa na Kanali Assimi Goïta na Burkina Faso inayoongozwa na Kapteni Ibrahim Traoré.

    Viongozi hao wamedai OIF na taasisi zingine zilizo chini ya Ufaransa ni ukoloni mamboleo. OIF ni Shirila lililoundwa kwa madhumuni ya kukuza lugha ya Kifaransa na kuimarisha ushirikiano kati ya nchi zinazozungumza Kifaransa.

    Gazeti la Le Monde la Nchini Ufaransa limeripoti kuwa taarifa ya pamoja ya Nchi hizo tatu ilisema kwamba OIF imegeuka kuwa ‘chombo cha kisiasa’ kinachoendeshwa na Ufaransa ili kuongeza unyonyaji wa rasilimali za mataifa hayo.

    Nchi za Niger 🇳🇪, Burkina Faso 🇧🇫 na Mali 🇲🇱 zimetangaza rasmi kujiondoa katika Shirika la Kimataifa la Mataifa yanayozungumza Kifaransa la ‘Francophonie’ (OIF). Uamuzi huo umefanywa na Viongozi wa mataifa hayo yenye Serikali za kijeshi, Niger inaongozwa na Jenerali Abdourahamane Tchiani, Mali inaongozwa na Kanali Assimi Goïta na Burkina Faso inayoongozwa na Kapteni Ibrahim Traoré. Viongozi hao wamedai OIF na taasisi zingine zilizo chini ya Ufaransa 🇫🇷 ni ukoloni mamboleo. OIF ni Shirila lililoundwa kwa madhumuni ya kukuza lugha ya Kifaransa na kuimarisha ushirikiano kati ya nchi zinazozungumza Kifaransa. Gazeti la Le Monde la Nchini Ufaransa limeripoti kuwa taarifa ya pamoja ya Nchi hizo tatu ilisema kwamba OIF imegeuka kuwa ‘chombo cha kisiasa’ kinachoendeshwa na Ufaransa ili kuongeza unyonyaji wa rasilimali za mataifa hayo.
    Love
    1
    0 Kommentare 0 Anteile 1KB Ansichten
Suchergebnis