• Fungua Stationary karibu na Chuo.

    Fungua Carwash karibu na Barbershop.

    Fungua mgahawa karibu na Soko.

    Fungua Duka la nguo karibu na stand.

    Fungua mdomo ukiwa na uhakika wa unachotaka kuongea.
    Fungua Stationary karibu na Chuo. Fungua Carwash karibu na Barbershop. Fungua mgahawa karibu na Soko. Fungua Duka la nguo karibu na stand. Fungua mdomo ukiwa na uhakika wa unachotaka kuongea.
    Like
    2
    · 0 Comments ·0 Shares ·199 Views
  • (C)
    Baada ya kifo cha mama yake, Shipman aliamua kuwa daktari. Alijiunga na Chuo Kikuu cha Leeds na baadaye akawa tabibu wa familia.

    Katika mwonekano wa nje, alikuwa mtu mwema, mtu wa familia, mwenye mke na watoto, anayependwa na wagonjwa wake. Lakini ndani yake, alikuwa akijificha kwenye kivuli cha giza na mauaji l.

    Alianza kazi yake kama daktari huko Yorkshire, na ilisemekana kuwa alikuwa mzuri sana kwa wagonjwa wake.

    Hata hivyo, mnamo 1975, alinaswa akiandika dawa za opioid (pethidine) kwa matumizi yake binafsi. Alipatikana na hatia, lakini badala ya kufungwa jela, alipigwa faini na kupoteza kazi kwa muda mfupi.

    Baadaye, alihamia mji wa Hyde na kuanza upya maisha yake kama daktari wa familia.

    Huko ndipo msururu wa vifo vya ajabu ulipoanza.
    (C) Baada ya kifo cha mama yake, Shipman aliamua kuwa daktari. Alijiunga na Chuo Kikuu cha Leeds na baadaye akawa tabibu wa familia. Katika mwonekano wa nje, alikuwa mtu mwema, mtu wa familia, mwenye mke na watoto, anayependwa na wagonjwa wake. Lakini ndani yake, alikuwa akijificha kwenye kivuli cha giza na mauaji l. Alianza kazi yake kama daktari huko Yorkshire, na ilisemekana kuwa alikuwa mzuri sana kwa wagonjwa wake. Hata hivyo, mnamo 1975, alinaswa akiandika dawa za opioid (pethidine) kwa matumizi yake binafsi. Alipatikana na hatia, lakini badala ya kufungwa jela, alipigwa faini na kupoteza kazi kwa muda mfupi. Baadaye, alihamia mji wa Hyde na kuanza upya maisha yake kama daktari wa familia. Huko ndipo msururu wa vifo vya ajabu ulipoanza.
    Like
    1
    · 0 Comments ·0 Shares ·387 Views
  • #PART 2

    Na kweli dogo akasoma kwa bidii. Ila kumbe kwa nyuma kulikuwa na mpango wa siri.

    Ilikuwa ni siku ya furaha kwa kila mzazi ambaye mtoto wake amemaliza chuo. Siku ya mahafali.

    50 Cent alikuwa na mipango mikubwa kwa kijana wake. Alikuwa tayari kumpa zawadi ya maisha, gari la kifahari ambalo lingemfungulia milango ya mafanikio zaidi.

    Lakini kilichotokea siku hiyo kilimvunja moyo.

    Hakupewa hata mwaliko wa mahafali.

    Fikiria baba ambaye amehangaika kuhakikisha mtoto wake anapata elimu bora, amemlipia kila kitu, amempa maisha ya ndoto, lakini siku kubwa kama hii hatakiwi hata kufika.

    Habari za mahafali alipewa na washikaji wa dogo. Walikuwa wanataka kumuona 50 Cent siku hiyo ili wapige naye picha.

    Lakini dogo mwenyewe? Hakumwambia chochote

    Hii haikuwa bahati mbaya, ilikuwa ni mpango wa makusudi.

    50 Cent hakuelewa nini kilichotokea, akapiga simu chuoni kuuliza.

    "Leo kuna mahafali, si ndiyo?"

    Wakamwambia ndiyo!

    Lilikuwa ni pigo lisilopimika kwa baba aliyetoa kila kitu kwa mwanawe.

    Lakini kilichomvunja moyo zaidi hakikuwa kutoalikwa tu kwenye mahafali.
    #PART 2 Na kweli dogo akasoma kwa bidii. Ila kumbe kwa nyuma kulikuwa na mpango wa siri. Ilikuwa ni siku ya furaha kwa kila mzazi ambaye mtoto wake amemaliza chuo. Siku ya mahafali. 50 Cent alikuwa na mipango mikubwa kwa kijana wake. Alikuwa tayari kumpa zawadi ya maisha, gari la kifahari ambalo lingemfungulia milango ya mafanikio zaidi. Lakini kilichotokea siku hiyo kilimvunja moyo. Hakupewa hata mwaliko wa mahafali. Fikiria baba ambaye amehangaika kuhakikisha mtoto wake anapata elimu bora, amemlipia kila kitu, amempa maisha ya ndoto, lakini siku kubwa kama hii hatakiwi hata kufika. Habari za mahafali alipewa na washikaji wa dogo. Walikuwa wanataka kumuona 50 Cent siku hiyo ili wapige naye picha. Lakini dogo mwenyewe? Hakumwambia chochote Hii haikuwa bahati mbaya, ilikuwa ni mpango wa makusudi. 50 Cent hakuelewa nini kilichotokea, akapiga simu chuoni kuuliza. "Leo kuna mahafali, si ndiyo?" Wakamwambia ndiyo! Lilikuwa ni pigo lisilopimika kwa baba aliyetoa kila kitu kwa mwanawe. Lakini kilichomvunja moyo zaidi hakikuwa kutoalikwa tu kwenye mahafali.
    0 Comments ·0 Shares ·575 Views
  • Katika siasa za Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), jina la Corneille Nangaa limepita katika nyanja tofauti.

    Kutoka kuwa msomi wa uchumi, mtumishi wa Umoja wa Mataifa (UNDP), msimamizi wa uchaguzi mkuu.

    Hadi sasa kuwa mmoja wa watu wanaoitikisa nchi hiyo kwa kiwango kikubwa.

    Mwanaume huyu ambaye aliwahi kuwa miongoni mwa watendaji wakubwa wa serikali, sasa anatajwa kuwa nyuma ya moja ya harakati hatari zaidi zinazoendelea katika ardhi ya Congo.

    Akiwa na historia ndefu ya kushika nafasi za juu serikalini, alifikia hatua ya kuanzisha chama chake cha kisiasa, Action for Change (AFC).

    Lakini hatua zake zilizoibua taharuki kubwa ni uhusiano wake wa karibu na kundi la waasi la M23, ambalo hivi sasa linatajwa kuwa jeshi lake binafsi.

    Lakini vipi msomi huyu wa uchumi alihamia kutoka kuongoza uchaguzi hadi kusimamia jeshi la waasi?

    Corneille Nangaa alianza kama msomi wa uchumi, akipata elimu yake kutoka Chuo Kikuu cha Kinshasa.
    Katika siasa za Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), jina la Corneille Nangaa limepita katika nyanja tofauti. Kutoka kuwa msomi wa uchumi, mtumishi wa Umoja wa Mataifa (UNDP), msimamizi wa uchaguzi mkuu. Hadi sasa kuwa mmoja wa watu wanaoitikisa nchi hiyo kwa kiwango kikubwa. Mwanaume huyu ambaye aliwahi kuwa miongoni mwa watendaji wakubwa wa serikali, sasa anatajwa kuwa nyuma ya moja ya harakati hatari zaidi zinazoendelea katika ardhi ya Congo. Akiwa na historia ndefu ya kushika nafasi za juu serikalini, alifikia hatua ya kuanzisha chama chake cha kisiasa, Action for Change (AFC). Lakini hatua zake zilizoibua taharuki kubwa ni uhusiano wake wa karibu na kundi la waasi la M23, ambalo hivi sasa linatajwa kuwa jeshi lake binafsi. Lakini vipi msomi huyu wa uchumi alihamia kutoka kuongoza uchaguzi hadi kusimamia jeshi la waasi? Corneille Nangaa alianza kama msomi wa uchumi, akipata elimu yake kutoka Chuo Kikuu cha Kinshasa.
    0 Comments ·0 Shares ·499 Views
  • THEIA SAYARI NDOGO ILIYOGONGANA NA DUNIANI.

    ✍🏾Mapande ya sayari inayoitwa Theia ambayo iligongana na Dunia na kusababisha kuundwa kwa Mwezi yamepatikana na Wataalmu Nchini Marekani.Kwa kufafanua zaidi ni wazi kwamba kuna siri nzito Katika Uumbaji,Kweli Mungu ni fundi waungwana,Kwanza Fahamu ya kwamba Asilimia 70% ya Historia ya uuumbaji Haijulikana kisawa Sawa maana Maisha ya Binadamu hayana Umri mrefu sanaa kuzidi Umri wa Dunia maana Umri wa Dunia ni miaka Billion 4.7 na Dunia inatadhamiwa Kuishi miaka Billion 7 Ijayo kabla Haijafa na kusambalatika kama kama Cheche za Mkaa.Theia ni jina la kigiriki lenye maana ya kwamba Mungu wa kike ambapo kulingana na simulizi na imani za wagiri ni kwamba Theia ni moja wa Mungu wa kike waliokuwa wanaishi uko Mwezini.Theia ni moja wa Watoto 7 mama wa Miungu ya uko mwezini yaani Mather of All Goddes uko mwezini hivyo ambaye alifahamika kama Selene huyo Goddess mkuu wa uko mwezini.

    ✍🏾SaSa Hapo mwanzo kulikuwa na Sayari inayofahamika kama Theia ambayo ilikuwa na ukubwa Sawa sawaa na Mars uko ambako NASA wametuma Perseverance Rovers kwenda Kuangalia kama Kulikuwa na maisha Hapo Kale yaani Miaka Billion 3 Iliyopita.Sasa Kuna nadharia kama 4 zinazoelezeaa kutokea Kwa mwezi,Kuna ambao Wanadai ya kwamba Theia ilikuwa iko nje ya Mfumo wa Jua mpaka inakuja kugongana na Dunia Hata Hivyo nadharia hii BADO haijathibika wanasayansi BADO wanafanya Tafiti Mbali Mbali kuliweka Hili sawaa.

    Hata Maji Yaliyopo hapa Duniani Hususani Maji ya kwenye Bahari yalitokea Baada ya Theia Kuparamia na Kuigonga Duniani Ndio Ikasababisha Uwepo wa Bahari kubwa ambazo tunaziona leo hii.Kuna nadharia ya kwanza ambayo Inadai ya kwamba kulikuwa na Moja ya Sayari kubwa Sana, Ambapo Sayari hiyo kulingana na Sababu ambazo hazijawekwa wazi ni kwamba Sayari hiyo kubwa ilikuja Kupasuka pasuka Kwa Kishindo na Kusababisha mgawanyiko ambapo Katika mgawanyiko huo ndio ukapelekea kuwepo Kwa Mwezi Ambapo Mwezi huo ulikuja Kunaswa na Nguvu ya mvutano wa Jua ndio ukabaki ulipo leo lakini Huwenda lisingekuwa Jua Mwezi ungekuwa Umeenda Mbali Sana kuliko ilivyo leo,Wabongo wanasema ya kwamba Mungu ni Fundi kweli (Tunakubaliana ya kwamba Sayari Zote ni Viumbe kama ilivyo Kwa viumbe wengine).

    ✍🏾 kamaa hiyo haitoshi kuna Nadharia ya pili ambayo inaelezea ya kwamba Mwezi uliundwa Wakati mmoja na Wakati Dunia () inaundwa hii Ina maana ya kwamba Dunia na Mwezi viliundwa wakati mmoja Kipindi ambacho Photo planetary Disk Accreted.Kwa kuthibitisha hilo Wakati wa Apollo Project Taasisi kubwa ya Marekani yaani NATIONAL AERONAUTICS AND SPACE ADMINISTRATION (NASA) walipata baadhi ya Ushahidi wa miamba uko mwezini walipoenda uko Mwaka 1969 mpaka mwaka 1972 walikutana na miamba yenye kufanana na ya hapa Duniani na hivyo kuja na Hoja ya kwamba Huenda Dunia na Mwezi viliundwa Wakati mmoja.Kuna baadhi ya chambuzi zinadai ya kwamba Theia ilikuwa ni Earth Trojan yaani Sayari ndogo ambayo ilikuwa ipo Katika mfumo wa kulizunguka JUA yenye Ukubwa wa Km 6,102 sawaa na Mile 3792.Na kulingana na utafiti na Ushahidi wa mwaka 2019 UNAONYESHA ya kwamba Theia ni Sayari ambayo Hakuwa Katika Mfumo wetu wa Jua ILA ni Sayari ambayo Imetoka nje ya Mfumo wa Jua (Solar system Mfumo huu ambao uliatengenezwa miaka 4.6 iliyopita).

    ✍🏾Takribani miaka bilioni 4.5 iliyopita sayari ndogo inayoitwa Theia iligongana na Dunia tukio lililosababisha sayari hiyo kupasuka na baadhi ya mapande yake kuruka kwenye Space na kuundia Mwezi na mapande mengine yalifukiwa chini Duniani ambapo katika utafiti wa hivi karibuni uliofanywa na wanasayansi kutoka chuo cha Arizona Nchini Marekani wamefanikiwa kuyapata baadhi ya mawe yaliyosalia wakati sayari hiyo ilipogongana na Dunia.ndii maana naungana na Mtaalamu wangu kutoka Marekani alimaarufu kama Bari Katika masuala ya uchambuzi ya kwamba Sayari Huwa zinajizalisha zenyewe ama kuzaliana Zenyewe maana Kwamba Sayari Moja inaweza ikasababisha KUZALIWA KWA Sayari zingine ndio maana Hata baadhi mawe makubwa yaliyoko Angani yenye ukubwa Sawa na Jimbo la Alaska ama Australia ni matokeo ama masalia ya Sayari zilizokufa ama zilizowahi kuwepo miaka Mabilioni iliyopita.

    Maana tufahamu ya kwamba Sayari Huwa zinazaliwa na pia Baada ya miaka Billion 4 mpaka 7 Sayari Huwa zinakufa ndio maana Mtaalamu Bari anazichukuliaa Sayari kama ni VIUMBE Vinavyoishi kama ilivyo Kwa viumbe viumbe Vinginevyo.hivyo Miamba iliyoko mwezini na hapa Duniani Ina Uhusiano Mkubwa na kuonyesha ya kwamba Mwezi na Dunia Zote zimeumbwa wakati Mmoja ama ni matokeo ya Sayari ndogo ya THEIA yenye kutaka kufanana na MARS Kwa ukubwa ilipogngana na Dunia na Kusababisha Kutokea Kwa Mwezi.
    THEIA SAYARI NDOGO ILIYOGONGANA NA DUNIANI. ✍🏾Mapande ya sayari inayoitwa Theia ambayo iligongana na Dunia na kusababisha kuundwa kwa Mwezi yamepatikana na Wataalmu Nchini Marekani.Kwa kufafanua zaidi ni wazi kwamba kuna siri nzito Katika Uumbaji,Kweli Mungu ni fundi waungwana,Kwanza Fahamu ya kwamba Asilimia 70% ya Historia ya uuumbaji Haijulikana kisawa Sawa maana Maisha ya Binadamu hayana Umri mrefu sanaa kuzidi Umri wa Dunia maana Umri wa Dunia ni miaka Billion 4.7 na Dunia inatadhamiwa Kuishi miaka Billion 7 Ijayo kabla Haijafa na kusambalatika kama kama Cheche za Mkaa🤓🤓.Theia ni jina la kigiriki lenye maana ya kwamba Mungu wa kike ambapo kulingana na simulizi na imani za wagiri ni kwamba Theia ni moja wa Mungu wa kike waliokuwa wanaishi uko Mwezini.Theia ni moja wa Watoto 7 mama wa Miungu ya uko mwezini yaani Mather of All Goddes uko mwezini hivyo ambaye alifahamika kama Selene huyo Goddess mkuu wa uko mwezini. ✍🏾SaSa Hapo mwanzo kulikuwa na Sayari inayofahamika kama Theia ambayo ilikuwa na ukubwa Sawa sawaa na Mars uko ambako NASA wametuma Perseverance Rovers kwenda Kuangalia kama Kulikuwa na maisha Hapo Kale yaani Miaka Billion 3 Iliyopita.Sasa Kuna nadharia kama 4 zinazoelezeaa kutokea Kwa mwezi,Kuna ambao Wanadai ya kwamba Theia ilikuwa iko nje ya Mfumo wa Jua mpaka inakuja kugongana na Dunia Hata Hivyo nadharia hii BADO haijathibika wanasayansi BADO wanafanya Tafiti Mbali Mbali kuliweka Hili sawaa. Hata Maji Yaliyopo hapa Duniani Hususani Maji ya kwenye Bahari yalitokea Baada ya Theia Kuparamia na Kuigonga Duniani Ndio Ikasababisha Uwepo wa Bahari kubwa ambazo tunaziona leo hii.Kuna nadharia ya kwanza ambayo Inadai ya kwamba kulikuwa na Moja ya Sayari kubwa Sana, Ambapo Sayari hiyo kulingana na Sababu ambazo hazijawekwa wazi ni kwamba Sayari hiyo kubwa ilikuja Kupasuka pasuka Kwa Kishindo na Kusababisha mgawanyiko ambapo Katika mgawanyiko huo ndio ukapelekea kuwepo Kwa Mwezi Ambapo Mwezi huo ulikuja Kunaswa na Nguvu ya mvutano wa Jua ndio ukabaki ulipo leo lakini Huwenda lisingekuwa Jua Mwezi ungekuwa Umeenda Mbali Sana kuliko ilivyo leo,Wabongo wanasema ya kwamba Mungu ni Fundi kweli (Tunakubaliana ya kwamba Sayari Zote ni Viumbe kama ilivyo Kwa viumbe wengine). ✍🏾 kamaa hiyo haitoshi kuna Nadharia ya pili ambayo inaelezea ya kwamba Mwezi uliundwa Wakati mmoja na Wakati Dunia (🌎) inaundwa hii Ina maana ya kwamba Dunia na Mwezi viliundwa wakati mmoja Kipindi ambacho Photo planetary Disk Accreted.Kwa kuthibitisha hilo Wakati wa Apollo Project Taasisi kubwa ya Marekani yaani NATIONAL AERONAUTICS AND SPACE 🌌 ADMINISTRATION (NASA) walipata baadhi ya Ushahidi wa miamba uko mwezini walipoenda uko Mwaka 1969 mpaka mwaka 1972 walikutana na miamba yenye kufanana na ya hapa Duniani na hivyo kuja na Hoja ya kwamba Huenda Dunia na Mwezi viliundwa Wakati mmoja.Kuna baadhi ya chambuzi zinadai ya kwamba Theia ilikuwa ni Earth Trojan yaani Sayari ndogo ambayo ilikuwa ipo Katika mfumo wa kulizunguka JUA yenye Ukubwa wa Km 6,102 sawaa na Mile 3792.Na kulingana na utafiti na Ushahidi wa mwaka 2019 UNAONYESHA ya kwamba Theia ni Sayari ambayo Hakuwa Katika Mfumo wetu wa Jua ILA ni Sayari ambayo Imetoka nje ya Mfumo wa Jua (Solar system Mfumo huu ambao uliatengenezwa miaka 4.6 iliyopita). ✍🏾Takribani miaka bilioni 4.5 iliyopita sayari ndogo inayoitwa Theia iligongana na Dunia tukio lililosababisha sayari hiyo kupasuka na baadhi ya mapande yake kuruka kwenye Space na kuundia Mwezi na mapande mengine yalifukiwa chini Duniani ambapo katika utafiti wa hivi karibuni uliofanywa na wanasayansi kutoka chuo cha Arizona Nchini Marekani wamefanikiwa kuyapata baadhi ya mawe yaliyosalia wakati sayari hiyo ilipogongana na Dunia.ndii maana naungana na Mtaalamu wangu kutoka Marekani alimaarufu kama Bari Katika masuala ya uchambuzi ya kwamba Sayari Huwa zinajizalisha zenyewe ama kuzaliana Zenyewe maana Kwamba Sayari Moja inaweza ikasababisha KUZALIWA KWA Sayari zingine ndio maana Hata baadhi mawe makubwa yaliyoko Angani yenye ukubwa Sawa na Jimbo la Alaska ama Australia ni matokeo ama masalia ya Sayari zilizokufa ama zilizowahi kuwepo miaka Mabilioni iliyopita. Maana tufahamu ya kwamba Sayari Huwa zinazaliwa na pia Baada ya miaka Billion 4 mpaka 7 Sayari Huwa zinakufa ndio maana Mtaalamu Bari anazichukuliaa Sayari kama ni VIUMBE Vinavyoishi kama ilivyo Kwa viumbe viumbe Vinginevyo.hivyo Miamba iliyoko mwezini na hapa Duniani Ina Uhusiano Mkubwa na kuonyesha ya kwamba Mwezi na Dunia Zote zimeumbwa wakati Mmoja ama ni matokeo ya Sayari ndogo ya THEIA yenye kutaka kufanana na MARS Kwa ukubwa ilipogngana na Dunia na Kusababisha Kutokea Kwa Mwezi.
    Like
    3
    · 1 Comments ·0 Shares ·944 Views
  • DUNIA NA MAAJABU YAKE
    (Muundo wa Dunia na Maajabu Yaliyomo)

    1. UMRI WA DUNIA

    HII Dunia yetu ina historia ndefu mno tangu ilipojiunda angani, miaka takribani bilioni 4.5 iliyopita.

    Tarakimu za umri huo wa miaka bilioni 4.5 ni 4,500,000,000, yaani miaka milioni elfu nne na mia tano iliyopita.

    Dunia ambayo kwa lugha ya Kiingereza inafahamika vyema kwa jina la 'Earth', pia hujulikana kama 'the World', ikimaanishwa ulimwengu.

    Aidha, Dunia ni sayari pekee kwenye himaya ya sayari zilizopo chini ya jua ambayo jina lake halitokani na majina ya "Miungu wa Dola" ya Kigiriki au ya Kirumi.

    Asili ya jina la 'earth' ni 'erde' lenye asili ya nchini Ujerumani, na maana yake ni udongo au ardhi.

    Mpaka kuweza kupata umri huo wa dunia wanasayansi walifanya kazi ya kutafiti na kisha kuwasilisha matokeo yao kwenye makongamano ya kisayansi duniani, ambapo matokeo hayo yalijadiliwa kwa kina na hatimaye kukubalika kama hivi.

    Kumbuka katika majadiliano hayo huwepo mivutano mikali miongoni mwa wanasayansi waalikwa, ambapo pia jopo la wanasayansi wanaowasilisha utafiti husika hujikuta wakitakiwa kujibu hoja mbalimbali za wanasayansi wenzao.

    Kuna wakati baadhi ya matokeo ya tafiti kadhaa hukataliwa, huku watafiti husika wakitakiwa kurejea upya tafiti zao.

    Wanasayansi hupata umri wa sayari kwa kupima umri wa miamba ya sayari husika, ambapo mwamba wenye umri mkubwa zaidi kuliko miamba yote ndiyo huchukuliwa kuwa umri wa sayari husika.

    Itakumbukwa kuwa Msahafu wa Biblia (Sura ya Mwanzo 1) husimulia jinsi Mwenyezi Mungu alivyoumba "mbingu na nchi na vyote vilivyomo kwa siku 6," lakini pia Msahafu huohuo kwenye aya zingine hueleza kuwa miaka elfu moja ya duniani yaweza kuwa sawa na siku moja kwenye ya Makazi ya Mwenyezi Mungu.

    Ni dhahiri kuwa binadamu tukiwa hatuna hoja sahihi kwa maelezo ya aina hiyo, ndipo tunaona ni vyema mambo ya Mwenyezi Mungu kumwachia Yeye Mwenyewe Mwenyezi Mungu.

    2. KUUMBIKA DUNIA, SAYARI, JUA, NYOTA

    Kimsingi, Dunia kama zilivyo sayari zingine zote ilijiunda kutokana na mabaki ya vitu vilivyotumika kuunda Jua.

    Jua ambalo ni nyota kama zilivyo nyota zote angani, lilijiunda lenyewe kwenye eneo la anga lijulikanalo kama 'Pillars of Creation' (nguzo za uumbaji) katika ukanda wa anga wenye upana ambao huonekana kutokuwa na mwisho.

    Ukanda huo ujulikanao kama 'Solar Nebula,' umegubikwa na mawingu ya vumbi la huko angani pamoja na aina mbalimbali za gesi na hewa, ikiwemo haidrojeni na heliumu.

    'Solar' ni jina la nishati itokanayo na joto la jua, na 'Nebula' kwa lugha ya Kilatini ni "wingu" au vumbi la gesi asilia mithili ya ukungu.

    Hivyo, 'Solar Nebula' ni ukanda katika anga ya mbali wenye mawingu yaliyosheheni nishati yenye joto, sawa na nishati ya joto la jua.

    Sasa basi, tunafahamu vyema kuwa jua hutoa mionzi hatari yenye joto kali mithili ya moto mkali, na ambayo ikiboreshwa kisayansi pia huweza kutoa nishati ya umeme.

    Hivyo, kwa muktadha huo, hebu ngoja sasa tuleta pamoja hewa za gesi, zikiwemo haidrojeni na heliumu, mawingu yenye nishati ya umeme wa jua, vumbi la angani na tufani itokanayo na mchafuko mbaya wa hali ya hewa huko anga za mbali.

    Na ili kuweza kupata matokeo yanayotakiwa, hebu pia tutambue uwepo wa nguvu kubwa ya asili katika kiwango kijulikanacho kwa jina la "Supernatural Power", ambayo ndiyo huwa kisababishi cha mambo yote.

    Kisayansi, "Supernatural Power" ni nguvu kubwa ya asili ambayo huendesha mifumo mbalimbali ya asili, ambapo duniani nguvu hiyo hujulikana kama Nguvu ya Mungu.

    Nguvu asili hiyo, yaani Supernatural Power, husababisha tufani ambayo huvurumisha kwa pamoja vitu vyote hivyo, (gesi, hewa, mawingu yenye nishati ya joto na vumbi la angani) ili kuunda tufani yenye umbo la duara.

    Duara hiyo ni kama ile itokanayo na kimbunga kikali duniani, na ambacho sasa tutaona kikifungamanisha pamoja vitu vyote hivyo katika mchafuko mkubwa wa hali mbaya ya hewa.

    Natumia maneno ya msisitizo kuelezea "ukubwa" wa mchafuko huo wa hali ya hewa katika eneo hilo la anga, kwani katika kuunda sayari au nyota nguvuasili kubwa hutumika.

    Aidha, tufani hiyo ya duara itakayoanza kidogo kidogo kama kimbunga kikali, itazidi kukua hadi kuwa na kipenyo cha takribani kilomita 10 hadi 200 au zaidi na kwendelea.

    Tufani hiyo ndiyo itavurumisha kwa pamoja gesi na hewa za naitrojeni na heliumu, mawingu ya nishati ya joto na vumbi la angani (kama kifanyavyo kimbunga kikali katika eneo tambarare la duniani).

    Pia, wakati mchafuko huo wa hali mbaya ya hewa ukiendelea, hebu ngoja sisi watazamaji tujibanze mahali fulani kwa mbali kushuhudia duara hiyo ya tufani ikijizungusha yenyewe bila kukoma kwa kipindi cha miaka mingi.

    Kitakachofuata ni kuanza kuona kiini cha moto kikianza kujiunda katikati ya duara hiyo ya tufani kali, huku pia nje ya duara hiyo vitu kibao vikivutwa kujiunga na mzunguko wa hiyo tufani ya duara.

    Vitu hivyo ni pamoja na vumbi zaidi la angani, na gesi zaidi zenye joto kali.

    Wakati huohuo kipenyo na mzingo wa duara hiyo vitazidi kuongezeka upana na ukubwa, mfano wa duara yenye umbo sawa na la mpira mkubwa wa miguu.

    Hivyo, baada ya miaka takribani milioni moja tutashangaa kuona lile vumbi likigeuka taratibu kuwa miamba ya moto ndani ya kiini cha tufani hiyo ya duara.

    Miamba hiyo ni kutokana na lile vumbi la angani ambalo hatimaye limeshikamana pamoja mithili ya zege, na hatimaye kuwa miamba ndani ya tufani ya duara.

    Sanjari na kuundika huko ndani ya kitovu cha hiyo tufani ya duara, pia kwelekea nje ya duara hiyo utaundika udongo ambao ardhi, mchanga na mawe.

    Kimsingi, vitu hivyo pia ni matokeo ya lile vumbi la angani ambalo lilikusanywa pamoja na kuvutwa na kasi ya mzunguko wa tufani.

    Hatua hiyo mpya inatokana na kuwepo mshikamano na mgandamizo wa zile chembechembe za lile vumbivumbi ndani ya tufani.

    Vurumai hiyo ya mzunguko wa hiyo tufani ya duara yenye vumbi, itazidi kukua hadi kuunda sumaku ya asili ndani ya kile kitovu cha duara ya tufani.

    Kutokana na duara hiyo ya tufani kuongezeka ukubwa, hatimaye sumaku iliyopo kwenye kitovu cha duara hiyo itaishiwa nguvu ya kwendelea kunasa vumbi zaidi kuja kwenye mzingo wa hiyo duara ya tufani.

    Kumbuka kuwa wakati huo hiyo duara pia itaunda kimo kutoka kwenye usawa wa ardhi yake kwenda ndani kwenye kitovu chake, na hivyo kuwa duara ya mviringo kama umbo mfano wa mpira mchezo wa miguu.

    Baada ya kupita maelfu ya miaka mingi, duara hiyo ambayo hapo awali ilianza kama umbo la tufani na kuzidi kukua huko angani, sasa itakuwa na joto kali kupita kiasi na kuanza kung'aa kama jua.

    Jua hilo, ndiyo nyota mojawapo ya zile ambazo huonekana usiku ziking'aa angani.

    Lakini pia wakati wa kujiunda nyota hiyo, kama tulivyoona hapo awali, baadhi ya mabaki yake yaliyokuwa yakitawanyika angani wakati ile tufani ya duara ikijizungusha, huweza kujikusanya pamoja na kuunda sayari ambazo huzunguka baadhi ya hizo nyota.

    Hivyo ndivyo zilivyojiunda sayari zote ambazo huelea kwa kulizunguka jua letu.

    Mathalani, sayari zote ambazo hulizunguka jua, ikiwemo dunia zilijiunda kutokana na mabaki ya vitu kama gesi, michanga na mawe ambavyo vilitawanyika angani wakati jua likijiunda (kama ambavyo imeelezwa hapo awali).

    3. KIINI CHA DUNIA

    Dunia yetu ambayo wastani wa nusu kipenyo cha umbo lake la duara ni kilomita 6,371, mzingo wake ni kilomita takribani 40,041.

    Kama zilivyo sayari zote katika himaya ya jua, dunia nayo ilijiunda wakati jua likijiunda lenyewe.

    Yaani kwamba sayari ni mabaki ya vitu vilivyotumika kuliunda jua.

    Kadhalika kama zilivyo sayari zingine zote, dunia nayo ina kiini chake ambacho kipo katikati ya ardhi yake.

    Kiini hicho kina nguvu kubwa ya sumaku ambayo, pamoja na mambo mengineyo, 'huvuta' umbo hilo la duara kutoka juu ya ardhi kwenda katikati ya kiini hicho.

    Muundo huo ndio hulifungamanisha pamoja umbo la duara la dunia, na hivyo kuzuia umbo hilo lisifumke kutoka ardhini na kusambaratika.

    Hiyo ni sawa na mpira wa miguu unavyoweza kupasuka na kusambaratika, kama utajazwa upepo kupita kiasi chake.

    Kiini hicho ambacho kipo katikati kabisa ya dunia, kinajulikanacho kwa jina la kisayansi la 'Inner Core.'

    Kiini hicho kina joto kali la sentigredi 6,230 ambacho ndio kiasi cha joto la jua.

    Kiini hicho kina umbo la duara lenye nusu kipenyo cha kilomita 1,250.

    Kama ingetokea kuchimba ardhi wima kwenda kwenye kiini hicho, mchimbaji angeanza kukutana na joto la kiini hicho kuanzia kimo cha umbali wa kilomita 5,150 kutoka usawa wa juu ya ardhi tunayotembea.

    Katika historia ya uchimbaji ardhi, kina kirefu kilichowahi kuchimbwa ardhini ni mita 12,345 (kilomita 12.345) huko Sakhalini, nchini Urusi, kwa ajili ya uvunaji wa mafuta ya petroli.

    Kiini cha dunia kinaundwa na madini mchanganyiko wa nikeli (nickle), chuma (iron) na dhahabu.

    Kwa mujibu wa utafiti, inakadiriwa kuwa kama dhahabu hiyo ingechimbwa na kuchomwa mpaka kuwa kimiminika sawa na uji na kisha kumwagwa chini, ingeweza kuifunika dunia yote kwa unene wa sentimeta 45.

    Kiini hicho muhimu kwa uhai wa sayari hii ya dunia kiligunduliwa mwaka 1936 na mtaalamu wa matetemeko ya ardhi wa nchini Denmark, mwanamama Dkt. Inge Lehmann.

    Dkt. Lehmann alihitimu shahada yake ya kwanza katika fani ya Hisabati mwaka 1910, ya Uzamili mwaka 1920 (zote kutoka Chuo Kikuu cha Copenhagen nchini mwake), na ile ya Uzamivu kutoka Chuo Kikuu cha Cambridge nchini Uingereza.

    Alifariki kwa uzee mwaka 1993 akiwa na umri wa miaka 104.

    4. MAJI DUNIANI

    Kupatikana maji kwenye dunia yetu, ni mojawapo ya miundo ambayo haipo katika sayari zingine ambazo tuna taarifa za kitafiti kuzuhusu.

    Maji ni muhimili muhimu kwa ajili ya uhai wa viumbe wote na mimea, ambavyo kwa pamoja havipo katika sayari zingine za himaya ya jua.

    Kwa mujibu wa tafiti nyingi ambazo zimefanyika kwa miongo mingi ya miaka kujaribu kubaini nini chanzo cha kuwepo maji duniani, hakuna hata utafiti mmoja ulioonesha kwa usahihi matokeo ya kuridhisha.

    Miongoni mwa tafiti hizo ni pamoja na ule wa mwaka 2005, ambapo Mkuu wa Idara ya Masomo ya Sayari na Mwezi katika Chuo Kikuu cha Arizona nchini Marekani, Profesa Michael Julian Drake, na mwenzake ambaye ni mtaalamu wa Vimondo, Dkt. Huberto Campins, wa Chuo Kikuu cha Central Florida, walitafiti nini chanzo cha kuwepo maji duniani.

    Katika mawasilisho yao kwenye kongamano la kisayansi la Chama cha Wanataaluma wa Maarifa ya Anga za Juu (IAU), watafiti hao walikanusha madai ya uwezekano wa dunia hapo kale kugongwa na kimondo kikubwa na kusababisha maji kulipuka kutoka ardhini.

    Wakiwasilisha matokeo ya utafiti wao kwenye mkutano wa kongamano hilo, magwiji hao wa masuala ya sayari walieleza kwenye waraka wao uitwao "Origin of water on the terrestial planets" (chanzo cha kuwepo maji kwenye sayari).

    Walidai kuwa maji yaliyopo duniani yaliumbika kwenye ardhi ya dunia tangu mwanzo, wakati ikijiunda angani.

    Ikumbukwe kuwa eneo la uso wa dunia likiwa ni jumla ya kilomita za mraba milioni 510, asilimia 70.8 ya eneo hilo imefunikwa na maji na asilimia 29.2 ni nchi kavu, ikiwemo milima, mabonde na ardhi tambarare.

    5. HEWA YA OKSIJENI

    Muundo mwingine muhimu katika sayari hii ya dunia ni hewa ambazo ni tawala, yaani Naitrojeni ambayo kwa usahihi imeenea kwa asilimia 78.08 ya hewa yote ya dunia, Oksijeni asilimia 20.95, 'Argon' asilimia 0.93, hewa ya Ukaa (Carbon dioxide) asilimia 0.039, na asilimia moja ni hewa mithili ya mvuke wa maji (water vapour).

    Hewa ya Oksijeni ambayo ni nguzo muhimu kwa ajili ya uhai wa viumbe wote na pia haipatikani kwenye sayari nyingine chini ya jua, inadhaniwa ilianza kupatikana duniani miaka takribani bilioni 2.5 iliyopita kufuatia "kukomaa kwa kiini cha dunia."

    Kwa mujibu wa matokeo ya tafiti mbalimbali na nadharia za kisayansi, inaoneshwa kuwa kukomaa kwa kiini hicho cha dunia hatimaye ndiko kulisababisha kuzuka duniani milipuko ya volikano ambayo pia ilisababisha kuzuka mabonde na milima.

    Inaoneshwa kuwa tayari wakati huo maji yaliishakuwepo duniani, na kuwezesha kuzuka chembechembe ndogo sana za kibakteria zijulikanazo kwa jina la kisayansi la 'cyanobacteria' au 'blue-green algae'.

    Kwa kutumia mwanga wa jua, maji na hewa ya ukaa, chembechembe hizo ziliweza kuzalisha hewa mbalimbali, ikiwemo 'Carbonhydrates' na Oksijeni.

    Kwa kuwa hizo chembechembe ndogo za kibakteria huishi baharini, ilikuwa rahisi kwa oksijeni kutokea baharini kupepea na kuenea katika anga ya dunia na kuzuiliwa hapo na nguvu asili ya uvutano ya dunia ili pia ibaki ikienea pote duniani.

    Mpaka wakati wa kuzuka duniani mimea na viumbe hai miaka takribani bilioni 3.5 iliyopita, tayari oksijeni ilikwa ni tele duniani; na hivyo kutumika kudumisha uhai wa viumbe hadi wakati huu.

    6. UKANDA WA 'OZONE'

    Muundo mwingie muhimu wa asili kwa dunia ni ukanda wa anga ujulikanao kwa jina la 'ozone' ambao umetanda kama 'mwavuli' kwenye anga ya dunia, na kuikinga isidhuriwe na mionzi hatari ya sumu kutoka kwenye Jua.

    Ukanda huo maarufu kama 'ozone layer' umetanda kuanzia usawa wa kilometa 15 kutoka ardhini kwenda juu angani mpaka ukomo wa kilomita takribani 50, ambapo huchuja asilimia kati ya 97 na 99 ya mionzi hatari kwenye miale ya joto la jua.

    Miongoni mwa matatizo yanayosababishwa na mionzi hiyo hatari kutoka kwenye jua, ni pamoja na magonjwa ya saratani ya ngozi kwa bianadamu.

    Pia juu ya ukanda wa tabaka la ozone kuna ukanda mwingine uitwao "atmosphere" ambao ni madhubuti kiasi kwamba vitu vinavyotoka anga za juu na kujaribu kuupenya ili kufika duniani, hukumbana na joto kali na kusambaratishwa kwa kuunguzwa.

    Si kwamba tabaka hilo lina joto, isipokuwa kasi ya "kuanguka" vitu hivyo kutoka juu angani kuja dunia husababisha msuguano na chembechembe za gesi katika eneo hilo na kuzalisha joto mithili ya ndimi za moto.

    Picha za video za vyombo vya 'Apollo' vikirejea duniani kutoka mwezini vikiwa na wanaanga ndani yake na kupenya tabaka hilo kwa kasi ya kilomita 39,000 kwa saa, huonekana kughubikwa na ndimi za moto wa rangi ya njano na bluu.

    Rangi hizo ni ishara ya ukali wa moto huo, lakini kutokana na waundaji wa vyombo hivyo kutumia mchanganyiko wa mabati na plastiki ngumu visivyopenywa na joto, Apollo huonekana kulichana tabaka hilo na kutokea upande wa pili ambao ni anga ya dunia.

    Hivyo basi, mfano huo mdogo unaonesha uimara wa tabaka hilo la 'ozone', ambalo kama ambavyo tumeona huchuja mionzi ya sumu kutoka kwenye mwanga wa jua ili kutolete madhara kwa viumbe duniani.

    Mwanga huo ukisafiri kutoka juani umbali wa kilomita milioni 150 kwa kasi ya kilomita 299,793, hutua duniani ndani ya dakika 8 na sekunde 19 ukiwa tayari umechujwa wakati ukipenya tabaka hilo.

    'Ozone' iligunduliwa mwaka 1913 na wanasayansi wawili wa nchini Ufaransa, Charlest Fabry na Henri Buisson, ambapo kipimo cha kasi ya mwanga kiligunduliwa na mwanasayansia wa anga za juu wa nchini Denmark, Ole Roemer, mwaka 1676.

    7. NGUVU ASILI YA UVUTANO

    Muundo mwingine wa dunia ni nguvu ya asili ya uvutano ya dunia, maarufu kama 'gravitation', ambayo huvuta vitu kuvirejesha chini duniani pale vinaporushwa kwenda juu au vile vinavyoanguka kutoka juu angani.

    Nguvu hiyo ina manufaa makubwa, kwani bila kuwepo duniani binadamu na viumbe wengine wangepeperuka kama karatasi kwenda juu wakati wakitembea juu ya ardhi ya hii.

    Kadhalika, nguvu hiyo husaidia kuvuta hewa ya oksijeni na kuiweka karibu na ardhi kwa ajili ya matumizi mbalimbali.

    Pia, nguvu hiyo husaidia kuiweka dunia, mwezi, jua na sayari zingine katika uwiano wa umbali usio na madhara kutoka kila moja.

    Nguvu hiyo ya asili ndiyo huliweka joto la jua duniani na kubaki kuwa katika kiwango kinachotakiwa, na hivyo kuwezesha viumbe kupata joto la wastani na pia katika kiwango mwanana.

    Nguvu hiyo huvuta mvua kuja duniani na kuwezesha maji ya bahari, maziwa na mito kutulia duniani.

    Mathalani, bila nguvu asili hiyo kuwepo duniani, maji 'yangemwagika' kutoka duniani kwa kutawanyika kama upepo na kupaa kwenda juu angani na kutoweka kabisa.

    Na ndio maana ukirusha maji kwenda juu, hurudi chini ardhini.

    Hebu angalia mfano huu kwamba wanaanga waliokwenda mwenzini walilazimika kuvaa mavazi yenye uzito wa kilo 80 hapa duniani, lakini mavazi hayo kule mwezini yakawa na uzito wa kilo 3.

    Mavazi hayo, yaani viatu, koti, suruali, na kofia nzito yenye miwani maalumu ya kukinga macho dhidi ya mionzi hatari ya jua, vyote kwa pamoja viliunganishwa na kuwa mfano wa sare za 'ovaroli' za mafundi wa magari.

    Mavazi hayo pia mgongoni yakiwa yameunganishwa kwa pamoja na mtungi wa hewa ya oksijeni kwa ajili ya kupumua, yalivaaliwa mahsusi muda mfupi baada ya chombo kutua mwezini.

    Hivyo, msomaji wangu tafakari nini kilisababisha mavazi kuwa mazito hapa duniani, lakini yawe mepesi kule mwezini?

    Jibu ni kwamba nguvu asili ya uvutano hapa duniani ni kubwa kuliko ya kule mwezini.

    Na ndipo tunaona umuhimu wa muundo huo wa nguvu asili ya uvutano, ambapo hapa duniani huvuta vitu kuja chini kwa kasi ya mita 9.81 kwa sekunde, lakini kwa kuwa nguvu ya mwezi ni hafifu, huvuta vitu kwa kasi ndogo ya mita 1.62 kwa sekunde.

    Ingawa nguvu hiyo ya asili iligunduliwa kuwepo duniani miaka mingi iliyopta, mwanafizikia bingwa wa Uingereza, Sir Isaac Newton (1642-1727), ndiye anatambulika kama mgunduzi wa hesabu hizo za nguvu asili hiyo.

    Anaeleza kuwa vitu vyote vyenye maumbo asili, ikiwemo jua, sayari, dunia, mwezi, na vimondo, kila kimoja kina nguvu hiyo katika viwango tofauti.

    Kanuni hiyo, kwa mujibu wa matokeo ya utafiti wake, hueleza kuwa nguvu hiyo ndiyo hufanya jua kuvuta sayari zake ili kulizunguka, huku pia kila sayari ikitumia nguvu 'binafsi' (na kwa uwiano maalumu) kujihami isivutwe hadi kwenda kuligonga jua au kugongana na sayari zingine au vimondo.

    Nguvuasili ya jua ni mita 274 kwa sekunde, ikiwa ni zaidi ya kiasi cha nguvuasili ya kila sayari.

    Muundo huo wa kila sayari kujihami kivyake katika mstari wa njia yake hufahamika kisayansi kama "sayari kuhami mazingira ya njia yake"; yaani kwamba 'a planet has to clear the neighbourhood around its orbit.'

    Newton akiwa amezaliwa 'mtoto-njiti' na baadaye kuibuka kuwa mwenye akili nyingi kiasi cha kukaribia kuwa sawa na mtu wa miujiza, hakuwahi kuoa kutokana na kinachoelezwa kuwa ni " kutokana na kutingwa na shughuli za kimasomo."

    Huoneshwa kuwa muda mwingi alikuwa maabara akifanya tafiti mbalimbali za kisayansi, au akiwa maktaba akijisomea, ama akiandika kitabu, au akifundisha wanafunzi wake.

    Alikuwa bingwa mwenye kipaji cha taaluma nyingi, ikiwemo Fizikia, Kemia, Hisabati, Maarifa ya Anga za Juu, Uchumi, Falsafa, na Theolojia ambayo ni taaluma ya masuala ya kiroho.

    Kwa mujibu wa historia, mwanasayansi huyo gwiji wa kuigwa alihitimu shahada zake zote mbili za sayansi, yaani 'Bachelor' na 'Masters', mwaka 1665 na 1668 katika Chuo Kikuu cha Cambridge, nchini Uingereza.

    Akiwa na umri wa miaka 84, mwanasayansi huyo anayedhaniwa na wengi kuwa bingwa wa hesabu za kisayansi kuliko wote duniani, alifariki mwaka 1727 akiwa usingizini.

    Ripoti ya uchunguzi wa mwili wake huonesha kuwa alikuwa na tatizo la figo, lakini pia alikutwa na kiasi kingi cha zebaki.

    Zebaki hiyo, yamkini, ni kutokana na kudumu mno kwenye maabara za Kemia na Fizikia, ambazo hutumia kemikali aina mbalimbali, zikiwemo hewa za gesi, katika kufanya majaribio ya kisayansi.
    DUNIA NA MAAJABU YAKE (Muundo wa Dunia na Maajabu Yaliyomo) 1. UMRI WA DUNIA HII Dunia yetu ina historia ndefu mno tangu ilipojiunda angani, miaka takribani bilioni 4.5 iliyopita. Tarakimu za umri huo wa miaka bilioni 4.5 ni 4,500,000,000, yaani miaka milioni elfu nne na mia tano iliyopita. Dunia ambayo kwa lugha ya Kiingereza inafahamika vyema kwa jina la 'Earth', pia hujulikana kama 'the World', ikimaanishwa ulimwengu. Aidha, Dunia ni sayari pekee kwenye himaya ya sayari zilizopo chini ya jua ambayo jina lake halitokani na majina ya "Miungu wa Dola" ya Kigiriki au ya Kirumi. Asili ya jina la 'earth' ni 'erde' lenye asili ya nchini Ujerumani, na maana yake ni udongo au ardhi. Mpaka kuweza kupata umri huo wa dunia wanasayansi walifanya kazi ya kutafiti na kisha kuwasilisha matokeo yao kwenye makongamano ya kisayansi duniani, ambapo matokeo hayo yalijadiliwa kwa kina na hatimaye kukubalika kama hivi. Kumbuka katika majadiliano hayo huwepo mivutano mikali miongoni mwa wanasayansi waalikwa, ambapo pia jopo la wanasayansi wanaowasilisha utafiti husika hujikuta wakitakiwa kujibu hoja mbalimbali za wanasayansi wenzao. Kuna wakati baadhi ya matokeo ya tafiti kadhaa hukataliwa, huku watafiti husika wakitakiwa kurejea upya tafiti zao. Wanasayansi hupata umri wa sayari kwa kupima umri wa miamba ya sayari husika, ambapo mwamba wenye umri mkubwa zaidi kuliko miamba yote ndiyo huchukuliwa kuwa umri wa sayari husika. Itakumbukwa kuwa Msahafu wa Biblia (Sura ya Mwanzo 1) husimulia jinsi Mwenyezi Mungu alivyoumba "mbingu na nchi na vyote vilivyomo kwa siku 6," lakini pia Msahafu huohuo kwenye aya zingine hueleza kuwa miaka elfu moja ya duniani yaweza kuwa sawa na siku moja kwenye ya Makazi ya Mwenyezi Mungu. Ni dhahiri kuwa binadamu tukiwa hatuna hoja sahihi kwa maelezo ya aina hiyo, ndipo tunaona ni vyema mambo ya Mwenyezi Mungu kumwachia Yeye Mwenyewe Mwenyezi Mungu. 2. KUUMBIKA DUNIA, SAYARI, JUA, NYOTA Kimsingi, Dunia kama zilivyo sayari zingine zote ilijiunda kutokana na mabaki ya vitu vilivyotumika kuunda Jua. Jua ambalo ni nyota kama zilivyo nyota zote angani, lilijiunda lenyewe kwenye eneo la anga lijulikanalo kama 'Pillars of Creation' (nguzo za uumbaji) katika ukanda wa anga wenye upana ambao huonekana kutokuwa na mwisho. Ukanda huo ujulikanao kama 'Solar Nebula,' umegubikwa na mawingu ya vumbi la huko angani pamoja na aina mbalimbali za gesi na hewa, ikiwemo haidrojeni na heliumu. 'Solar' ni jina la nishati itokanayo na joto la jua, na 'Nebula' kwa lugha ya Kilatini ni "wingu" au vumbi la gesi asilia mithili ya ukungu. Hivyo, 'Solar Nebula' ni ukanda katika anga ya mbali wenye mawingu yaliyosheheni nishati yenye joto, sawa na nishati ya joto la jua. Sasa basi, tunafahamu vyema kuwa jua hutoa mionzi hatari yenye joto kali mithili ya moto mkali, na ambayo ikiboreshwa kisayansi pia huweza kutoa nishati ya umeme. Hivyo, kwa muktadha huo, hebu ngoja sasa tuleta pamoja hewa za gesi, zikiwemo haidrojeni na heliumu, mawingu yenye nishati ya umeme wa jua, vumbi la angani na tufani itokanayo na mchafuko mbaya wa hali ya hewa huko anga za mbali. Na ili kuweza kupata matokeo yanayotakiwa, hebu pia tutambue uwepo wa nguvu kubwa ya asili katika kiwango kijulikanacho kwa jina la "Supernatural Power", ambayo ndiyo huwa kisababishi cha mambo yote. Kisayansi, "Supernatural Power" ni nguvu kubwa ya asili ambayo huendesha mifumo mbalimbali ya asili, ambapo duniani nguvu hiyo hujulikana kama Nguvu ya Mungu. Nguvu asili hiyo, yaani Supernatural Power, husababisha tufani ambayo huvurumisha kwa pamoja vitu vyote hivyo, (gesi, hewa, mawingu yenye nishati ya joto na vumbi la angani) ili kuunda tufani yenye umbo la duara. Duara hiyo ni kama ile itokanayo na kimbunga kikali duniani, na ambacho sasa tutaona kikifungamanisha pamoja vitu vyote hivyo katika mchafuko mkubwa wa hali mbaya ya hewa. Natumia maneno ya msisitizo kuelezea "ukubwa" wa mchafuko huo wa hali ya hewa katika eneo hilo la anga, kwani katika kuunda sayari au nyota nguvuasili kubwa hutumika. Aidha, tufani hiyo ya duara itakayoanza kidogo kidogo kama kimbunga kikali, itazidi kukua hadi kuwa na kipenyo cha takribani kilomita 10 hadi 200 au zaidi na kwendelea. Tufani hiyo ndiyo itavurumisha kwa pamoja gesi na hewa za naitrojeni na heliumu, mawingu ya nishati ya joto na vumbi la angani (kama kifanyavyo kimbunga kikali katika eneo tambarare la duniani). Pia, wakati mchafuko huo wa hali mbaya ya hewa ukiendelea, hebu ngoja sisi watazamaji tujibanze mahali fulani kwa mbali kushuhudia duara hiyo ya tufani ikijizungusha yenyewe bila kukoma kwa kipindi cha miaka mingi. Kitakachofuata ni kuanza kuona kiini cha moto kikianza kujiunda katikati ya duara hiyo ya tufani kali, huku pia nje ya duara hiyo vitu kibao vikivutwa kujiunga na mzunguko wa hiyo tufani ya duara. Vitu hivyo ni pamoja na vumbi zaidi la angani, na gesi zaidi zenye joto kali. Wakati huohuo kipenyo na mzingo wa duara hiyo vitazidi kuongezeka upana na ukubwa, mfano wa duara yenye umbo sawa na la mpira mkubwa wa miguu. Hivyo, baada ya miaka takribani milioni moja tutashangaa kuona lile vumbi likigeuka taratibu kuwa miamba ya moto ndani ya kiini cha tufani hiyo ya duara. Miamba hiyo ni kutokana na lile vumbi la angani ambalo hatimaye limeshikamana pamoja mithili ya zege, na hatimaye kuwa miamba ndani ya tufani ya duara. Sanjari na kuundika huko ndani ya kitovu cha hiyo tufani ya duara, pia kwelekea nje ya duara hiyo utaundika udongo ambao ardhi, mchanga na mawe. Kimsingi, vitu hivyo pia ni matokeo ya lile vumbi la angani ambalo lilikusanywa pamoja na kuvutwa na kasi ya mzunguko wa tufani. Hatua hiyo mpya inatokana na kuwepo mshikamano na mgandamizo wa zile chembechembe za lile vumbivumbi ndani ya tufani. Vurumai hiyo ya mzunguko wa hiyo tufani ya duara yenye vumbi, itazidi kukua hadi kuunda sumaku ya asili ndani ya kile kitovu cha duara ya tufani. Kutokana na duara hiyo ya tufani kuongezeka ukubwa, hatimaye sumaku iliyopo kwenye kitovu cha duara hiyo itaishiwa nguvu ya kwendelea kunasa vumbi zaidi kuja kwenye mzingo wa hiyo duara ya tufani. Kumbuka kuwa wakati huo hiyo duara pia itaunda kimo kutoka kwenye usawa wa ardhi yake kwenda ndani kwenye kitovu chake, na hivyo kuwa duara ya mviringo kama umbo mfano wa mpira mchezo wa miguu. Baada ya kupita maelfu ya miaka mingi, duara hiyo ambayo hapo awali ilianza kama umbo la tufani na kuzidi kukua huko angani, sasa itakuwa na joto kali kupita kiasi na kuanza kung'aa kama jua. Jua hilo, ndiyo nyota mojawapo ya zile ambazo huonekana usiku ziking'aa angani. Lakini pia wakati wa kujiunda nyota hiyo, kama tulivyoona hapo awali, baadhi ya mabaki yake yaliyokuwa yakitawanyika angani wakati ile tufani ya duara ikijizungusha, huweza kujikusanya pamoja na kuunda sayari ambazo huzunguka baadhi ya hizo nyota. Hivyo ndivyo zilivyojiunda sayari zote ambazo huelea kwa kulizunguka jua letu. Mathalani, sayari zote ambazo hulizunguka jua, ikiwemo dunia zilijiunda kutokana na mabaki ya vitu kama gesi, michanga na mawe ambavyo vilitawanyika angani wakati jua likijiunda (kama ambavyo imeelezwa hapo awali). 3. KIINI CHA DUNIA Dunia yetu ambayo wastani wa nusu kipenyo cha umbo lake la duara ni kilomita 6,371, mzingo wake ni kilomita takribani 40,041. Kama zilivyo sayari zote katika himaya ya jua, dunia nayo ilijiunda wakati jua likijiunda lenyewe. Yaani kwamba sayari ni mabaki ya vitu vilivyotumika kuliunda jua. Kadhalika kama zilivyo sayari zingine zote, dunia nayo ina kiini chake ambacho kipo katikati ya ardhi yake. Kiini hicho kina nguvu kubwa ya sumaku ambayo, pamoja na mambo mengineyo, 'huvuta' umbo hilo la duara kutoka juu ya ardhi kwenda katikati ya kiini hicho. Muundo huo ndio hulifungamanisha pamoja umbo la duara la dunia, na hivyo kuzuia umbo hilo lisifumke kutoka ardhini na kusambaratika. Hiyo ni sawa na mpira wa miguu unavyoweza kupasuka na kusambaratika, kama utajazwa upepo kupita kiasi chake. Kiini hicho ambacho kipo katikati kabisa ya dunia, kinajulikanacho kwa jina la kisayansi la 'Inner Core.' Kiini hicho kina joto kali la sentigredi 6,230 ambacho ndio kiasi cha joto la jua. Kiini hicho kina umbo la duara lenye nusu kipenyo cha kilomita 1,250. Kama ingetokea kuchimba ardhi wima kwenda kwenye kiini hicho, mchimbaji angeanza kukutana na joto la kiini hicho kuanzia kimo cha umbali wa kilomita 5,150 kutoka usawa wa juu ya ardhi tunayotembea. Katika historia ya uchimbaji ardhi, kina kirefu kilichowahi kuchimbwa ardhini ni mita 12,345 (kilomita 12.345) huko Sakhalini, nchini Urusi, kwa ajili ya uvunaji wa mafuta ya petroli. Kiini cha dunia kinaundwa na madini mchanganyiko wa nikeli (nickle), chuma (iron) na dhahabu. Kwa mujibu wa utafiti, inakadiriwa kuwa kama dhahabu hiyo ingechimbwa na kuchomwa mpaka kuwa kimiminika sawa na uji na kisha kumwagwa chini, ingeweza kuifunika dunia yote kwa unene wa sentimeta 45. Kiini hicho muhimu kwa uhai wa sayari hii ya dunia kiligunduliwa mwaka 1936 na mtaalamu wa matetemeko ya ardhi wa nchini Denmark, mwanamama Dkt. Inge Lehmann. Dkt. Lehmann alihitimu shahada yake ya kwanza katika fani ya Hisabati mwaka 1910, ya Uzamili mwaka 1920 (zote kutoka Chuo Kikuu cha Copenhagen nchini mwake), na ile ya Uzamivu kutoka Chuo Kikuu cha Cambridge nchini Uingereza. Alifariki kwa uzee mwaka 1993 akiwa na umri wa miaka 104. 4. MAJI DUNIANI Kupatikana maji kwenye dunia yetu, ni mojawapo ya miundo ambayo haipo katika sayari zingine ambazo tuna taarifa za kitafiti kuzuhusu. Maji ni muhimili muhimu kwa ajili ya uhai wa viumbe wote na mimea, ambavyo kwa pamoja havipo katika sayari zingine za himaya ya jua. Kwa mujibu wa tafiti nyingi ambazo zimefanyika kwa miongo mingi ya miaka kujaribu kubaini nini chanzo cha kuwepo maji duniani, hakuna hata utafiti mmoja ulioonesha kwa usahihi matokeo ya kuridhisha. Miongoni mwa tafiti hizo ni pamoja na ule wa mwaka 2005, ambapo Mkuu wa Idara ya Masomo ya Sayari na Mwezi katika Chuo Kikuu cha Arizona nchini Marekani, Profesa Michael Julian Drake, na mwenzake ambaye ni mtaalamu wa Vimondo, Dkt. Huberto Campins, wa Chuo Kikuu cha Central Florida, walitafiti nini chanzo cha kuwepo maji duniani. Katika mawasilisho yao kwenye kongamano la kisayansi la Chama cha Wanataaluma wa Maarifa ya Anga za Juu (IAU), watafiti hao walikanusha madai ya uwezekano wa dunia hapo kale kugongwa na kimondo kikubwa na kusababisha maji kulipuka kutoka ardhini. Wakiwasilisha matokeo ya utafiti wao kwenye mkutano wa kongamano hilo, magwiji hao wa masuala ya sayari walieleza kwenye waraka wao uitwao "Origin of water on the terrestial planets" (chanzo cha kuwepo maji kwenye sayari). Walidai kuwa maji yaliyopo duniani yaliumbika kwenye ardhi ya dunia tangu mwanzo, wakati ikijiunda angani. Ikumbukwe kuwa eneo la uso wa dunia likiwa ni jumla ya kilomita za mraba milioni 510, asilimia 70.8 ya eneo hilo imefunikwa na maji na asilimia 29.2 ni nchi kavu, ikiwemo milima, mabonde na ardhi tambarare. 5. HEWA YA OKSIJENI Muundo mwingine muhimu katika sayari hii ya dunia ni hewa ambazo ni tawala, yaani Naitrojeni ambayo kwa usahihi imeenea kwa asilimia 78.08 ya hewa yote ya dunia, Oksijeni asilimia 20.95, 'Argon' asilimia 0.93, hewa ya Ukaa (Carbon dioxide) asilimia 0.039, na asilimia moja ni hewa mithili ya mvuke wa maji (water vapour). Hewa ya Oksijeni ambayo ni nguzo muhimu kwa ajili ya uhai wa viumbe wote na pia haipatikani kwenye sayari nyingine chini ya jua, inadhaniwa ilianza kupatikana duniani miaka takribani bilioni 2.5 iliyopita kufuatia "kukomaa kwa kiini cha dunia." Kwa mujibu wa matokeo ya tafiti mbalimbali na nadharia za kisayansi, inaoneshwa kuwa kukomaa kwa kiini hicho cha dunia hatimaye ndiko kulisababisha kuzuka duniani milipuko ya volikano ambayo pia ilisababisha kuzuka mabonde na milima. Inaoneshwa kuwa tayari wakati huo maji yaliishakuwepo duniani, na kuwezesha kuzuka chembechembe ndogo sana za kibakteria zijulikanazo kwa jina la kisayansi la 'cyanobacteria' au 'blue-green algae'. Kwa kutumia mwanga wa jua, maji na hewa ya ukaa, chembechembe hizo ziliweza kuzalisha hewa mbalimbali, ikiwemo 'Carbonhydrates' na Oksijeni. Kwa kuwa hizo chembechembe ndogo za kibakteria huishi baharini, ilikuwa rahisi kwa oksijeni kutokea baharini kupepea na kuenea katika anga ya dunia na kuzuiliwa hapo na nguvu asili ya uvutano ya dunia ili pia ibaki ikienea pote duniani. Mpaka wakati wa kuzuka duniani mimea na viumbe hai miaka takribani bilioni 3.5 iliyopita, tayari oksijeni ilikwa ni tele duniani; na hivyo kutumika kudumisha uhai wa viumbe hadi wakati huu. 6. UKANDA WA 'OZONE' Muundo mwingie muhimu wa asili kwa dunia ni ukanda wa anga ujulikanao kwa jina la 'ozone' ambao umetanda kama 'mwavuli' kwenye anga ya dunia, na kuikinga isidhuriwe na mionzi hatari ya sumu kutoka kwenye Jua. Ukanda huo maarufu kama 'ozone layer' umetanda kuanzia usawa wa kilometa 15 kutoka ardhini kwenda juu angani mpaka ukomo wa kilomita takribani 50, ambapo huchuja asilimia kati ya 97 na 99 ya mionzi hatari kwenye miale ya joto la jua. Miongoni mwa matatizo yanayosababishwa na mionzi hiyo hatari kutoka kwenye jua, ni pamoja na magonjwa ya saratani ya ngozi kwa bianadamu. Pia juu ya ukanda wa tabaka la ozone kuna ukanda mwingine uitwao "atmosphere" ambao ni madhubuti kiasi kwamba vitu vinavyotoka anga za juu na kujaribu kuupenya ili kufika duniani, hukumbana na joto kali na kusambaratishwa kwa kuunguzwa. Si kwamba tabaka hilo lina joto, isipokuwa kasi ya "kuanguka" vitu hivyo kutoka juu angani kuja dunia husababisha msuguano na chembechembe za gesi katika eneo hilo na kuzalisha joto mithili ya ndimi za moto. Picha za video za vyombo vya 'Apollo' vikirejea duniani kutoka mwezini vikiwa na wanaanga ndani yake na kupenya tabaka hilo kwa kasi ya kilomita 39,000 kwa saa, huonekana kughubikwa na ndimi za moto wa rangi ya njano na bluu. Rangi hizo ni ishara ya ukali wa moto huo, lakini kutokana na waundaji wa vyombo hivyo kutumia mchanganyiko wa mabati na plastiki ngumu visivyopenywa na joto, Apollo huonekana kulichana tabaka hilo na kutokea upande wa pili ambao ni anga ya dunia. Hivyo basi, mfano huo mdogo unaonesha uimara wa tabaka hilo la 'ozone', ambalo kama ambavyo tumeona huchuja mionzi ya sumu kutoka kwenye mwanga wa jua ili kutolete madhara kwa viumbe duniani. Mwanga huo ukisafiri kutoka juani umbali wa kilomita milioni 150 kwa kasi ya kilomita 299,793, hutua duniani ndani ya dakika 8 na sekunde 19 ukiwa tayari umechujwa wakati ukipenya tabaka hilo. 'Ozone' iligunduliwa mwaka 1913 na wanasayansi wawili wa nchini Ufaransa, Charlest Fabry na Henri Buisson, ambapo kipimo cha kasi ya mwanga kiligunduliwa na mwanasayansia wa anga za juu wa nchini Denmark, Ole Roemer, mwaka 1676. 7. NGUVU ASILI YA UVUTANO Muundo mwingine wa dunia ni nguvu ya asili ya uvutano ya dunia, maarufu kama 'gravitation', ambayo huvuta vitu kuvirejesha chini duniani pale vinaporushwa kwenda juu au vile vinavyoanguka kutoka juu angani. Nguvu hiyo ina manufaa makubwa, kwani bila kuwepo duniani binadamu na viumbe wengine wangepeperuka kama karatasi kwenda juu wakati wakitembea juu ya ardhi ya hii. Kadhalika, nguvu hiyo husaidia kuvuta hewa ya oksijeni na kuiweka karibu na ardhi kwa ajili ya matumizi mbalimbali. Pia, nguvu hiyo husaidia kuiweka dunia, mwezi, jua na sayari zingine katika uwiano wa umbali usio na madhara kutoka kila moja. Nguvu hiyo ya asili ndiyo huliweka joto la jua duniani na kubaki kuwa katika kiwango kinachotakiwa, na hivyo kuwezesha viumbe kupata joto la wastani na pia katika kiwango mwanana. Nguvu hiyo huvuta mvua kuja duniani na kuwezesha maji ya bahari, maziwa na mito kutulia duniani. Mathalani, bila nguvu asili hiyo kuwepo duniani, maji 'yangemwagika' kutoka duniani kwa kutawanyika kama upepo na kupaa kwenda juu angani na kutoweka kabisa. Na ndio maana ukirusha maji kwenda juu, hurudi chini ardhini. Hebu angalia mfano huu kwamba wanaanga waliokwenda mwenzini walilazimika kuvaa mavazi yenye uzito wa kilo 80 hapa duniani, lakini mavazi hayo kule mwezini yakawa na uzito wa kilo 3. Mavazi hayo, yaani viatu, koti, suruali, na kofia nzito yenye miwani maalumu ya kukinga macho dhidi ya mionzi hatari ya jua, vyote kwa pamoja viliunganishwa na kuwa mfano wa sare za 'ovaroli' za mafundi wa magari. Mavazi hayo pia mgongoni yakiwa yameunganishwa kwa pamoja na mtungi wa hewa ya oksijeni kwa ajili ya kupumua, yalivaaliwa mahsusi muda mfupi baada ya chombo kutua mwezini. Hivyo, msomaji wangu tafakari nini kilisababisha mavazi kuwa mazito hapa duniani, lakini yawe mepesi kule mwezini? Jibu ni kwamba nguvu asili ya uvutano hapa duniani ni kubwa kuliko ya kule mwezini. Na ndipo tunaona umuhimu wa muundo huo wa nguvu asili ya uvutano, ambapo hapa duniani huvuta vitu kuja chini kwa kasi ya mita 9.81 kwa sekunde, lakini kwa kuwa nguvu ya mwezi ni hafifu, huvuta vitu kwa kasi ndogo ya mita 1.62 kwa sekunde. Ingawa nguvu hiyo ya asili iligunduliwa kuwepo duniani miaka mingi iliyopta, mwanafizikia bingwa wa Uingereza, Sir Isaac Newton (1642-1727), ndiye anatambulika kama mgunduzi wa hesabu hizo za nguvu asili hiyo. Anaeleza kuwa vitu vyote vyenye maumbo asili, ikiwemo jua, sayari, dunia, mwezi, na vimondo, kila kimoja kina nguvu hiyo katika viwango tofauti. Kanuni hiyo, kwa mujibu wa matokeo ya utafiti wake, hueleza kuwa nguvu hiyo ndiyo hufanya jua kuvuta sayari zake ili kulizunguka, huku pia kila sayari ikitumia nguvu 'binafsi' (na kwa uwiano maalumu) kujihami isivutwe hadi kwenda kuligonga jua au kugongana na sayari zingine au vimondo. Nguvuasili ya jua ni mita 274 kwa sekunde, ikiwa ni zaidi ya kiasi cha nguvuasili ya kila sayari. Muundo huo wa kila sayari kujihami kivyake katika mstari wa njia yake hufahamika kisayansi kama "sayari kuhami mazingira ya njia yake"; yaani kwamba 'a planet has to clear the neighbourhood around its orbit.' Newton akiwa amezaliwa 'mtoto-njiti' na baadaye kuibuka kuwa mwenye akili nyingi kiasi cha kukaribia kuwa sawa na mtu wa miujiza, hakuwahi kuoa kutokana na kinachoelezwa kuwa ni " kutokana na kutingwa na shughuli za kimasomo." Huoneshwa kuwa muda mwingi alikuwa maabara akifanya tafiti mbalimbali za kisayansi, au akiwa maktaba akijisomea, ama akiandika kitabu, au akifundisha wanafunzi wake. Alikuwa bingwa mwenye kipaji cha taaluma nyingi, ikiwemo Fizikia, Kemia, Hisabati, Maarifa ya Anga za Juu, Uchumi, Falsafa, na Theolojia ambayo ni taaluma ya masuala ya kiroho. Kwa mujibu wa historia, mwanasayansi huyo gwiji wa kuigwa alihitimu shahada zake zote mbili za sayansi, yaani 'Bachelor' na 'Masters', mwaka 1665 na 1668 katika Chuo Kikuu cha Cambridge, nchini Uingereza. Akiwa na umri wa miaka 84, mwanasayansi huyo anayedhaniwa na wengi kuwa bingwa wa hesabu za kisayansi kuliko wote duniani, alifariki mwaka 1727 akiwa usingizini. Ripoti ya uchunguzi wa mwili wake huonesha kuwa alikuwa na tatizo la figo, lakini pia alikutwa na kiasi kingi cha zebaki. Zebaki hiyo, yamkini, ni kutokana na kudumu mno kwenye maabara za Kemia na Fizikia, ambazo hutumia kemikali aina mbalimbali, zikiwemo hewa za gesi, katika kufanya majaribio ya kisayansi.
    0 Comments ·0 Shares ·1K Views
  • SAKATA LA JASUSI SERGEI SKRIPAL NA MWANAE NI UTEKELEZAJI WA OPERATION SARLISBURY ILIYOTEKELEZWA NA RUSSIA, KIMSIMGI NI VITA KATI YA URUSI NA NATO KUJIBU MAPIGO YA UCHAGUZI WA MAREKANI MWAKA 2016.

    Na mhariri wako Comred Mbwana Allyamtu

    Sakata la jaribio la mauaji ya jasusi au mpelelezi, ndumilakuwili wa Urusi na Uingereza, Sergei Skripal na binti yake Yulia katika kitongoji cha Salisbury jijini London nchini Uingereza linachukua sura mpya kila siku.

    Wawili hao walipatikana wakiwa hawajitambui katika eneo la maduka liitwalo Maltings mwanzoni mwa Machi.

    Taarifa kutoka kwa polisi wa Uingereza ambao hushughulikia matukio ya kigaidi wanaamini kuwa jasusi huyo na mwanaye, walivuta hewa iliyokuwa na kemikali yenye sumu iitwayo novichok.

    Kemikali hii hushambulia mfumo wa mfahamu na inasemekana ilitengenezwa katika maabara moja huko Urusi na ilitumika wakati wa Vita vya Pili vya Dunia mwaka 1935 hadi 1945. Kemikali hiyo iliachwa mlangoni mwa nyumba ambayo amekuwa akiishi jasusi huyo na mwanaye katika eneo hilo la Salisbury.

    Mashirika makubwa ya habari nchini Uingereza yameipa umuhimu habari hii ambapo Machi 30, yalitangaza kuwa binti wa Skripal, Yulia hakuwa katika hali tete kiafya.

    Kufuatia tukio hilo Serikali ya Uingereza chini ya Waziri Mkuu, Theresa May iliitupia lawama Serikali ya Urusi kwa kuhusika na uovu huo na ili kuonyesha kuwa imechukia iliamua kuwafukuza wanadiplomasia wa Urusi wapatao 23.

    Urusi imekanusha kuhusika na uovu huo na ikaahidi kuwa kwa kila hukumu itakayotolewa nayo itajibu kwa ukubwa huohuo au zaidi ya hapo, na ikajibu kwa kutoa hukumu ya kisasi kwa kuwafukuza wanadiplomasia 23 wa Uingereza na kufunga kituo cha Lugha na Utamaduni cha Uingereza, British Council na imeitaka Uingereza kuwaondoa wanadiplomasia wake wengine wapatao 50 katika kipindi cha mwezi mmoja.
    Ili kuonyesha mshikamano na Uingereza nchi nyingine za Ulaya Magharibi na Australia zimewafukuza wanadiplomasia wa Urusi wanaofikia 150 huku Marekani ikiongoza kwa kufunga ubalozi mdogo wa Urusi katika Jiji la Seattle na kuwafukuza wanadiplomasia 60 kutoka nchi hiyo.

    Urusi nayo haikubaki kimya, Waziri wa Mambo ya Nje, Sergei Lavrov ametangaza kuwafukuza wanadiplomasia 60 wa Marekani na vilevile kufunga ubalozi wa Marekani katika mji wa Saint Petersburg na kuahidi kuwa kila nchi iliyohusika na kufukuza wanadiplomasia wake itaadhibiwa vilivyo.

    Kwa ujumla nchi karibu 23 na Umoja wa Kujihami wa nchi za Ulaya Magharibi (Nato) kote ulimwenguni zimeonyesha kukerwa na vitendo vya Urusi kwa kuingilia mambo ya ndani ya nchi tofautitofauti, kama vile kuvamia Ukraine na kulichukua jimbo la Krimea, kuitungua ndege ya Malaysia na kuingilia uchaguzi Mkuu wa Marekani mwaka 2016.
    Siyo mara ya kwanza nchi hizi kuingia katika mzozo wa kidiplomasia kwani mwaka 1986 Ronald Reagan aliyekuwa Rais wa Marekani, aliamuru wanadiplomasia 80 wa Shirikisho la Urusi (USSR) wafukuzwe nchini humo na mwaka 2016, Rais Barak Obama aliwatimua wanadiplomasia 35 kutoka nchi hiyo kwa tuhuma za kudukua kompyuta za chama cha Democratic kwa nia ya kumhujumu mgombea wake wa Rais, Hillary Clinton.

    Mwaka 2006 Skripal alihukumiwa kifungo cha miaka 13, nchini Urusi katika kesi ambayo iliendeshwa katika mahakama ya siri, alipewa haki ya ukimbizi na ukazi nchini Uingereza mwaka 2010 baada ya makubaliano ya kubadilishana wafungwa katika mtindo ambao ulitumika enzi za vita baridi kuhusiana na shughuli za kijasusi.

    Kulingana na nyaraka za kumbukumbu ambazo vyombo vya habari vya Uingereza vilizipata kutoka makumbusho ya taifa ya Uingereza mwaka 2015, zinaonyesha kuwa Serikali ya Urusi imekuwa ikiichunguza Uingereza muda mrefu lakini kisa kinachojulikana sana ni kile kilichopewa jina la Cambridge Four, ambapo kitengo cha ujasusi cha shirikisho la Urusi (USSR), KGB, katika miaka ya 1930 kabla ya vita vya pili vya dunia kiligundua kuwa Serikali ya Uingereza ilikuwa ikitumia Chuo Kikuu cha Cambridge kama sehemu maalumu ya kuwapata majasusi wachanga wakiwa masomoni. KGB waliwafuata wanafunzi wanne wa wakati huo ambao ni Anthony Blunt, Donald Duart Maclean, Kim Phillby na Guy Burgess.
    Wasomi hao ambao kwa bahati nzuri kwao KGB walipomaliza masomo yao waliingia kufanya kazi katika Mashirika ya Ujasusi ya Uingereza, MI5 na MI6, na wakawa ni majasusi ndumilakuwili.

    Walifanya kazi yao hadi mwaka 1964 ambapo Anthony Blunt ambaye alikuwa akifanya kazi katika Shirika la Ujasusi wa ndani, MI5, alikiri kuwa jasusi ndumilakuwili ili asishtakiwe na habari hiyo ilikuja kutolewa na aliyekuwa Waziri Mkuu wa Uingereza wakati huo, Magreth Thatcher alipokuwa akihutubia Bunge mwaka 1979. Donald Duart Maclean, Kim Phillby na Guy Burgess wao walitimkia Urusi na Serikali ya Uingereza ikawa imekubali yaiishe.

    Kwa hiyo Urusi imekuwa hailali usingizi wakati wote wa miaka ya vita baridi kati ya nchi za Ulaya Mashariki na Magharibi miaka ya 1945 hadi mwanzoni mwa miaka ya 1990, imekuwa ikiingiza wapelelezi wake maeneo mbalimbali katika nchi hizo ili kupata habari nyeti kuhusiana na masuala mbalimbali katika nyanja za uchumi, biashara hasa ya silaha na teknolojia yake na hivi karibuni kuingilia mambo ya siasa za uchaguzi huko Marekani.
    Ukiangalia kisa cha safari hii hakina tofauti sana kile alichofanyiwa Jasusi mwingine wa Urusi Novemba 2006, Alexander Litvinenko ambaye aliwekewa kemikali iitwayo Polonium 210 katika kikombe cha chai katika mgahawa mmoja jijini London.

    Litvinenko alitoroka Urusi baada ya kutofautiana na wenzake katika shirika la kijasusi la nchi hiyo FSB, ambapo aliutuhumu uongozi wa juu wa nchi hiyo kuigeuza nchi hiyo kuwa Taifa la kimafia. akiwa nchini Uingereza, alifanya kazi kama mwandishi wa habari, vitabu na mshauri wa mambo ya usalama.
    Akiwa Uingereza aliandika vitabu viwili, Blowing up Russia: Terror from within na Lubyanka Criminal Group ambapo aliituhumu idara hiyo ya kijasusi kwa vitendo vya mauaji na matumizi ya mabomu na mauaji ya mwandishi wa habari, Anna Politkovskaya kwa amri kutoka kwa Rais wa nchi hiyo, Vladimir Putin.

    Litvinenko akiwa mahututi kitandani hospitalini jijini London aliwatamkia ndugu zake kuwa alikuwa na uhakika kuwa Rais wa Urusi, Vladimir Putin ndiye aliyeamuru auawe.
    Serikali ya Uingereza ya wakati huo chini ya Waziri Mkuu, Tony Blair ilifanya upelelezi na kugundua kuwa jasusi huyo siku chache kabla ya kupata mkasa huo alikuwa ametembelewa na jasusi mwingine mstaafu wa FSB ambaye kwa sasa ni mfanyabiashara, Andrey Lugovoy.
    Serikali ya Uingereza iliitaka Urusi imsalimishe kwake ili afanyiwe mahojiano lakini Urusi ilikataa kwa maelezo kuwa Katiba ya nchi hiyo inakataza raia wake kupelekwa nchi nyingine kufanyiwa mashtaka ya jinai. Uhusiano kati ya nchi hizo mbili ulififia kwa muda.

    Serikali ya Uingereza kwa matukio yote haya imekuwa ikiituhumu serikali ya Urusi kwa kile inachoeleza kuwa kemikali hizo haziwezi kuwa mikononi mwa mtu binafsi bila kuwa na kibari cha mamlaka za juu za nchi hiyo.

    Wakati Kim Phillby alipokimbilia Urusi baada ya kushtukia kuwa wenzake walikuwa wanaelekea kumgundua kuwa ni ndumilakuwili, Ofisa mmoja wa ngazi ya juu ndani ya KGB wakati huo alimsifu kuwa alikuwa jasusi mwenye thamani kubwa wa karne iliyopita.

    Urusi imekuwa ikitoa ulinzi wa kiwango cha juu kwa majasusi ndumilakuwili ambao wamefanikiwa kuingia nchini humo baada ya mambo kwenda kombo huko kwao.

    Marekani nayo haikuwahi kupona kwa taasisi zake za kijasusi kuingiliwa na wenzao wa Urusi. Mwaka 2001 Shirika la Ujasusi wa Ndani, FBI, lilimkamata Robert Hanssen ambaye alikuwa mtumishi wake kwa kupeleka taarifa za siri za nchi hiyo kwa Urusi tangu mwaka 1979 kwa kulipwa fedha na almasi.

    Kwa sehemu kubwa shughuli za ujasusi zimekuwa zikifanywa kwa njia ya teknolojia (Artificial Intelligence) ambapo mitambo ya kompyuta na setelaiti na kamera zenye nguvu za kunasa picha hutumika na pale ambapo haiwezekani, inabidi kutumia binadamu (human intelligence) ili kupata habari ambazo ni siri na mataifa karibu yote duniani yameuweka ujasusi kama ni kosa la uhaini kwa yeyote atakayejihusisha nao.
    SAKATA LA JASUSI SERGEI SKRIPAL NA MWANAE NI UTEKELEZAJI WA OPERATION SARLISBURY ILIYOTEKELEZWA NA RUSSIA, KIMSIMGI NI VITA KATI YA URUSI NA NATO KUJIBU MAPIGO YA UCHAGUZI WA MAREKANI MWAKA 2016. Na mhariri wako Comred Mbwana Allyamtu Sakata la jaribio la mauaji ya jasusi au mpelelezi, ndumilakuwili wa Urusi na Uingereza, Sergei Skripal na binti yake Yulia katika kitongoji cha Salisbury jijini London nchini Uingereza linachukua sura mpya kila siku. Wawili hao walipatikana wakiwa hawajitambui katika eneo la maduka liitwalo Maltings mwanzoni mwa Machi. Taarifa kutoka kwa polisi wa Uingereza ambao hushughulikia matukio ya kigaidi wanaamini kuwa jasusi huyo na mwanaye, walivuta hewa iliyokuwa na kemikali yenye sumu iitwayo novichok. Kemikali hii hushambulia mfumo wa mfahamu na inasemekana ilitengenezwa katika maabara moja huko Urusi na ilitumika wakati wa Vita vya Pili vya Dunia mwaka 1935 hadi 1945. Kemikali hiyo iliachwa mlangoni mwa nyumba ambayo amekuwa akiishi jasusi huyo na mwanaye katika eneo hilo la Salisbury. Mashirika makubwa ya habari nchini Uingereza yameipa umuhimu habari hii ambapo Machi 30, yalitangaza kuwa binti wa Skripal, Yulia hakuwa katika hali tete kiafya. Kufuatia tukio hilo Serikali ya Uingereza chini ya Waziri Mkuu, Theresa May iliitupia lawama Serikali ya Urusi kwa kuhusika na uovu huo na ili kuonyesha kuwa imechukia iliamua kuwafukuza wanadiplomasia wa Urusi wapatao 23. Urusi imekanusha kuhusika na uovu huo na ikaahidi kuwa kwa kila hukumu itakayotolewa nayo itajibu kwa ukubwa huohuo au zaidi ya hapo, na ikajibu kwa kutoa hukumu ya kisasi kwa kuwafukuza wanadiplomasia 23 wa Uingereza na kufunga kituo cha Lugha na Utamaduni cha Uingereza, British Council na imeitaka Uingereza kuwaondoa wanadiplomasia wake wengine wapatao 50 katika kipindi cha mwezi mmoja. Ili kuonyesha mshikamano na Uingereza nchi nyingine za Ulaya Magharibi na Australia zimewafukuza wanadiplomasia wa Urusi wanaofikia 150 huku Marekani ikiongoza kwa kufunga ubalozi mdogo wa Urusi katika Jiji la Seattle na kuwafukuza wanadiplomasia 60 kutoka nchi hiyo. Urusi nayo haikubaki kimya, Waziri wa Mambo ya Nje, Sergei Lavrov ametangaza kuwafukuza wanadiplomasia 60 wa Marekani na vilevile kufunga ubalozi wa Marekani katika mji wa Saint Petersburg na kuahidi kuwa kila nchi iliyohusika na kufukuza wanadiplomasia wake itaadhibiwa vilivyo. Kwa ujumla nchi karibu 23 na Umoja wa Kujihami wa nchi za Ulaya Magharibi (Nato) kote ulimwenguni zimeonyesha kukerwa na vitendo vya Urusi kwa kuingilia mambo ya ndani ya nchi tofautitofauti, kama vile kuvamia Ukraine na kulichukua jimbo la Krimea, kuitungua ndege ya Malaysia na kuingilia uchaguzi Mkuu wa Marekani mwaka 2016. Siyo mara ya kwanza nchi hizi kuingia katika mzozo wa kidiplomasia kwani mwaka 1986 Ronald Reagan aliyekuwa Rais wa Marekani, aliamuru wanadiplomasia 80 wa Shirikisho la Urusi (USSR) wafukuzwe nchini humo na mwaka 2016, Rais Barak Obama aliwatimua wanadiplomasia 35 kutoka nchi hiyo kwa tuhuma za kudukua kompyuta za chama cha Democratic kwa nia ya kumhujumu mgombea wake wa Rais, Hillary Clinton. Mwaka 2006 Skripal alihukumiwa kifungo cha miaka 13, nchini Urusi katika kesi ambayo iliendeshwa katika mahakama ya siri, alipewa haki ya ukimbizi na ukazi nchini Uingereza mwaka 2010 baada ya makubaliano ya kubadilishana wafungwa katika mtindo ambao ulitumika enzi za vita baridi kuhusiana na shughuli za kijasusi. Kulingana na nyaraka za kumbukumbu ambazo vyombo vya habari vya Uingereza vilizipata kutoka makumbusho ya taifa ya Uingereza mwaka 2015, zinaonyesha kuwa Serikali ya Urusi imekuwa ikiichunguza Uingereza muda mrefu lakini kisa kinachojulikana sana ni kile kilichopewa jina la Cambridge Four, ambapo kitengo cha ujasusi cha shirikisho la Urusi (USSR), KGB, katika miaka ya 1930 kabla ya vita vya pili vya dunia kiligundua kuwa Serikali ya Uingereza ilikuwa ikitumia Chuo Kikuu cha Cambridge kama sehemu maalumu ya kuwapata majasusi wachanga wakiwa masomoni. KGB waliwafuata wanafunzi wanne wa wakati huo ambao ni Anthony Blunt, Donald Duart Maclean, Kim Phillby na Guy Burgess. Wasomi hao ambao kwa bahati nzuri kwao KGB walipomaliza masomo yao waliingia kufanya kazi katika Mashirika ya Ujasusi ya Uingereza, MI5 na MI6, na wakawa ni majasusi ndumilakuwili. Walifanya kazi yao hadi mwaka 1964 ambapo Anthony Blunt ambaye alikuwa akifanya kazi katika Shirika la Ujasusi wa ndani, MI5, alikiri kuwa jasusi ndumilakuwili ili asishtakiwe na habari hiyo ilikuja kutolewa na aliyekuwa Waziri Mkuu wa Uingereza wakati huo, Magreth Thatcher alipokuwa akihutubia Bunge mwaka 1979. Donald Duart Maclean, Kim Phillby na Guy Burgess wao walitimkia Urusi na Serikali ya Uingereza ikawa imekubali yaiishe. Kwa hiyo Urusi imekuwa hailali usingizi wakati wote wa miaka ya vita baridi kati ya nchi za Ulaya Mashariki na Magharibi miaka ya 1945 hadi mwanzoni mwa miaka ya 1990, imekuwa ikiingiza wapelelezi wake maeneo mbalimbali katika nchi hizo ili kupata habari nyeti kuhusiana na masuala mbalimbali katika nyanja za uchumi, biashara hasa ya silaha na teknolojia yake na hivi karibuni kuingilia mambo ya siasa za uchaguzi huko Marekani. Ukiangalia kisa cha safari hii hakina tofauti sana kile alichofanyiwa Jasusi mwingine wa Urusi Novemba 2006, Alexander Litvinenko ambaye aliwekewa kemikali iitwayo Polonium 210 katika kikombe cha chai katika mgahawa mmoja jijini London. Litvinenko alitoroka Urusi baada ya kutofautiana na wenzake katika shirika la kijasusi la nchi hiyo FSB, ambapo aliutuhumu uongozi wa juu wa nchi hiyo kuigeuza nchi hiyo kuwa Taifa la kimafia. akiwa nchini Uingereza, alifanya kazi kama mwandishi wa habari, vitabu na mshauri wa mambo ya usalama. Akiwa Uingereza aliandika vitabu viwili, Blowing up Russia: Terror from within na Lubyanka Criminal Group ambapo aliituhumu idara hiyo ya kijasusi kwa vitendo vya mauaji na matumizi ya mabomu na mauaji ya mwandishi wa habari, Anna Politkovskaya kwa amri kutoka kwa Rais wa nchi hiyo, Vladimir Putin. Litvinenko akiwa mahututi kitandani hospitalini jijini London aliwatamkia ndugu zake kuwa alikuwa na uhakika kuwa Rais wa Urusi, Vladimir Putin ndiye aliyeamuru auawe. Serikali ya Uingereza ya wakati huo chini ya Waziri Mkuu, Tony Blair ilifanya upelelezi na kugundua kuwa jasusi huyo siku chache kabla ya kupata mkasa huo alikuwa ametembelewa na jasusi mwingine mstaafu wa FSB ambaye kwa sasa ni mfanyabiashara, Andrey Lugovoy. Serikali ya Uingereza iliitaka Urusi imsalimishe kwake ili afanyiwe mahojiano lakini Urusi ilikataa kwa maelezo kuwa Katiba ya nchi hiyo inakataza raia wake kupelekwa nchi nyingine kufanyiwa mashtaka ya jinai. Uhusiano kati ya nchi hizo mbili ulififia kwa muda. Serikali ya Uingereza kwa matukio yote haya imekuwa ikiituhumu serikali ya Urusi kwa kile inachoeleza kuwa kemikali hizo haziwezi kuwa mikononi mwa mtu binafsi bila kuwa na kibari cha mamlaka za juu za nchi hiyo. Wakati Kim Phillby alipokimbilia Urusi baada ya kushtukia kuwa wenzake walikuwa wanaelekea kumgundua kuwa ni ndumilakuwili, Ofisa mmoja wa ngazi ya juu ndani ya KGB wakati huo alimsifu kuwa alikuwa jasusi mwenye thamani kubwa wa karne iliyopita. Urusi imekuwa ikitoa ulinzi wa kiwango cha juu kwa majasusi ndumilakuwili ambao wamefanikiwa kuingia nchini humo baada ya mambo kwenda kombo huko kwao. Marekani nayo haikuwahi kupona kwa taasisi zake za kijasusi kuingiliwa na wenzao wa Urusi. Mwaka 2001 Shirika la Ujasusi wa Ndani, FBI, lilimkamata Robert Hanssen ambaye alikuwa mtumishi wake kwa kupeleka taarifa za siri za nchi hiyo kwa Urusi tangu mwaka 1979 kwa kulipwa fedha na almasi. Kwa sehemu kubwa shughuli za ujasusi zimekuwa zikifanywa kwa njia ya teknolojia (Artificial Intelligence) ambapo mitambo ya kompyuta na setelaiti na kamera zenye nguvu za kunasa picha hutumika na pale ambapo haiwezekani, inabidi kutumia binadamu (human intelligence) ili kupata habari ambazo ni siri na mataifa karibu yote duniani yameuweka ujasusi kama ni kosa la uhaini kwa yeyote atakayejihusisha nao.
    0 Comments ·0 Shares ·2K Views
  • Wanaitwa ‘MANTIS SHRIMP’ mwenye pigo sawa na nguvu ya bunduki

    ❇Hawa ni moja kati ya viumbe hatari sana wanaopatikana baharini hasa bahari ya Hindi hapa Tanzania Kitalaam anaitwa “Stamatopoda”
    .
    ❇wana urefu wa cm 20 sawa na inchi 8 na uzitowao ni Gram 90 – 100 lakini mambo yao ni konki
    .Kwa umbo wanamagamba mazuri yenye kuvutia lakini ni moja ya viumbe hatari sana baharini
    .
    ❇wanauwezo wa kupiga sehemu na kuvunja na nguvu yake ni sawa na risasi wanauwezo wa kupasua vile vioo vya mabwawa ya kuhifadhia samaki (aquarims) kwa Single Hit)
    .
    ❇Mantis huwa hawachangani, ni wakali sana hasa kwenye mipaka yao yaani ukiingia bahati mbaya kwenye anga zao umeyatimba
    .
    ❇Huwa wanatoa sauti za chini sana ambazo huwasiliana kama ikitokea wakakutana na nadra sana kuona wanapigana
    .
    ❇Macho yao yako kwa juu kama antena na yana uwezo mkubwa wa kuona na kujua direction ya predators au prey
    .pia yana uwezo wa kwenda direction tofauti tofauti yaani moja kaskazini na moja kusini, Vile vile wanakucha ambazo hutumia kumkamata prey anapokua karibu
    .
    ❇Chakula chao kikuu ni ngadu, Samaki na baadhi ya viumbe vingine na wanakula samaki ambao huwa wakubwa kuliko hata umbo lao
    .
    ❇Huwa wanatumia mechanism tofauti sana pale wanapotaka kutafuta chakula wanauwezo wa kupiga maji yakatengeneza mawimbi makubwa tu kukelekea direction ya prey na kabla ya prey hajafanya maamuzi anapigwa round kick kali sana..
    .
    ❇Wanauwezo wa kugundua Mgonjwa wa cancer kwa macho yao na hii ni kwasabu macho yanauwezo mkubwa sana wakuona na kugundua movement nampangilio wa neurons (Hii ni kwa mujibu wa Chuo Kikuu cha Queensland)
    .
    ❇Kwa kawaida huwa na life partner yaani bebi mmoja tu kwenye maisha yao na muda wa kutaga jike na dume hulalia pamoja mayai mpaka muda wa kupata watoto
    .
    ❇Adui yao mkubwa ni binadamu maana nchi kama Japan na China huwa wanawala sana na wakati mwingine huwa wanaaminishwa na imani fulani kama moja ya viumbe vyenye kuongeza sana nguvu ya mwili kwa kuimarisha seli hai nyeupe (white blood cells).
    Wanaitwa ‘MANTIS SHRIMP’ mwenye pigo sawa na nguvu ya bunduki ❇Hawa ni moja kati ya viumbe hatari sana wanaopatikana baharini hasa bahari ya Hindi hapa Tanzania Kitalaam anaitwa “Stamatopoda” . ❇wana urefu wa cm 20 sawa na inchi 8 na uzitowao ni Gram 90 – 100 lakini mambo yao ni konki .Kwa umbo wanamagamba mazuri yenye kuvutia lakini ni moja ya viumbe hatari sana baharini . ❇wanauwezo wa kupiga sehemu na kuvunja na nguvu yake ni sawa na risasi wanauwezo wa kupasua vile vioo vya mabwawa ya kuhifadhia samaki (aquarims) kwa Single Hit) . ❇Mantis huwa hawachangani, ni wakali sana hasa kwenye mipaka yao yaani ukiingia bahati mbaya kwenye anga zao umeyatimba . ❇Huwa wanatoa sauti za chini sana ambazo huwasiliana kama ikitokea wakakutana na nadra sana kuona wanapigana . ❇Macho yao yako kwa juu kama antena na yana uwezo mkubwa wa kuona na kujua direction ya predators au prey .pia yana uwezo wa kwenda direction tofauti tofauti yaani moja kaskazini na moja kusini, Vile vile wanakucha ambazo hutumia kumkamata prey anapokua karibu . ❇Chakula chao kikuu ni ngadu, Samaki na baadhi ya viumbe vingine na wanakula samaki ambao huwa wakubwa kuliko hata umbo lao . ❇Huwa wanatumia mechanism tofauti sana pale wanapotaka kutafuta chakula wanauwezo wa kupiga maji yakatengeneza mawimbi makubwa tu kukelekea direction ya prey na kabla ya prey hajafanya maamuzi anapigwa round kick kali sana.. 😀 . ❇Wanauwezo wa kugundua Mgonjwa wa cancer kwa macho yao na hii ni kwasabu macho yanauwezo mkubwa sana wakuona na kugundua movement nampangilio wa neurons (Hii ni kwa mujibu wa Chuo Kikuu cha Queensland) . ❇Kwa kawaida huwa na life partner yaani bebi mmoja tu kwenye maisha yao na muda wa kutaga jike na dume hulalia pamoja mayai mpaka muda wa kupata watoto . ❇Adui yao mkubwa ni binadamu maana nchi kama Japan na China huwa wanawala sana na wakati mwingine huwa wanaaminishwa na imani fulani kama moja ya viumbe vyenye kuongeza sana nguvu ya mwili kwa kuimarisha seli hai nyeupe (white blood cells).
    0 Comments ·0 Shares ·583 Views
  • MUONEKANO WA NABII ISSA MIAKA HIYO ULIKUWAJE ?

    Karibu kila mtu ana dhana fulani kuhusu muonekano wa Yesu Kristo.
    Ndiye mtu aliyechorwa zaidi katika sanaa ya Magharibi. Picha zake hutambuliwa kwa urahisi, ambapo huoneshwa akiwa na nywele na ndevu, akiwa amevalia vazi lefu lenye mikono mirefu linalofanana na kanzu ( la rangi nyeupe), na pia akiwa amejifunga joho (la rangi ya samawati). Muonekano wa Yesu umefahamika sana na wengi kiasi kwamba unaweza kutambuliwa ukiwa hata kwenye mikate au biskuti.

    Picha za sasa za Yesu zinatokana na enzi ya Byzantine, himaya iliyokuwa na mji mkuu wake Constantinople. Ni picha iliyoanza kutumika karne ya nne hivi. Michoro ya Yesu ya wakati wa utawala wa Byzantine ilikuwa ya ishara, na si muonekano wake. Wasanii waliangazia zaidi maana na si kumfananisha na Yesu mwenyewe.
    Picha zao ziliongozwa na dhana ya Yesu kama mtawala, kwenye kiti cha enzi, kama anavyoonyeshwa kwenye mchoro ulio kwenye altari ya kanisa la Santa Pudenziana jijini Roma.

    Yesu anaoneshwa akiwa amevalia mgolole wa rangi ya dhahabu.
    Ndiye mtawala wa dunia yote aliyetoka mbinguni, mfanano wa picha yake ni ule wa sanamu ya Zeus wa Olympus anayeonyeshwa akiwa na nywele ndefu za ndevu kwenye kiti cha enzi. Ni sanamu iliyokuwa maarufu sana wakati huo kiasi kwamba Mfalme Augustus wa Roma alishurutisha naye atengenezewe sanamu kama hiyo, lakini yake ikiwa bila nywele ndefu na ndevu, Wasanii wa Byzantine, walitaka kumuonyesha Kristo kama mtawala kutoka mbinguni, mfalme wa aina yake, na hivyo wakachora wakimuonyesha kama Zeus, lakini akiwa mdogo kidogo wa umri.

    Kilichotokea kadiri miaka ilivyosonga ni kwamba kuonyeshwa huku kwa Kristo kama mtawala kutoka mbinguni - ambapo wakati mwingine ameonyeshwa hata akiwa kama 'hippie' au 'superstar' (kama ilivyo kwenye mchoro huu hapa chini) - ndiko kumekuwa kama kigezo chetu cha Yesu alivyokuwa. Hebu tuchanganue kutoka kichwani hadi vidole vya miguuni. Wakristo wa nyakati za kwanza wakati walipokuwa wanamwonyesha Kristo si kama mtawala kutoka mbinguni, walimuonyesha kama binadamu wa kawaida tu - akiwa hana ndevu na hana nywele ndefu.

    Lakini pengine, kama msomi wa aina yake aliyekuwa akisafiri kutoka eneo moja hadi jingine, Yesu pengine alikuwa na ndevu, kwa sababu hakuwa akienda kwa vinyozi. Kwa kawaida, kuwa mchafu kiasi na kuwa na ndevu ndefu ni sifa ambazo zilihusishwa na wanafalsafa, wasomi wa ngazi ya juu, na kuwatenganisha na watu wa kawaida.
    Mwanafalsafa maarufu wa kundi la Stoic (Wanafalsafa wa Kigiriki waliofuata mafundisho ya mwanzilishi wao Zeno wa Citium mjini Athens mapema karne ya 3 kabla ya kuzaliwa kwa Yesu) Epictetus aliamini "ilifaa hivyo kwa mujibu wa maumbile." Mambo yalibadilika katika karne ya 1 baada ya kuzaliwa kwa Yesu, wakati wa enzi za Warumi na Wagiriki, ambapo kuwa na nywele fupi na kunyoa ndefu ndiyo mambo yaliyochukuliwa kuwa yafaayo na ya kistaarabu.

    Kuwa na nywele ndefu na ndevu ni mambo ambayo yaliachiwa miungu pekee, si ya watu wa kawaida. Hata wanafalsafa enzi hizo walikuwa na nywele fupi. Ndevu pia hazikuwa sifa za kuwatambulisha Wayahudi enzi hizo. Ukweli ni kwamba moja ya changamoto ambazo waliotaka kuwatesa Wayahudi vipindi mbalimbali katika historia walihangaika sana kuwatofautisha na watu wengine. Hii ni kwa sababu wote walifanana (jambo ambalo limegusiwa katika kitabu cha Wamakabayo). Hata hivyo, picha za wanaume wa Kiyahudi zilizokuwa kwenye sarafu za Judea Capta ambazo zilitolewa na utawala wa Roma baada ya kutekwa kwa mji wa Yerusalemu mwaka 70 baada ya kuzaliwa kwa Yesu zinawaonesha wanaume wakiwa na ndevu, lakini nywele zao si ndefu.

    Kwa hivyo, Yesu, kama mwanafalsafa wa muonekano wa kawaida, kuna uwezekano alikuwa na ndevu lakini si ndefu sana, sawa na wanaume hao walioonyeshwa kwenye sarafu za Judaea Capta, lakini nywele zake basi hazikuwa ndefu sana pia.
    Kama ingetokea kwamba awe na nywele ndefu hata kidogo tu kuliko kawaida, basi angezua mtafaruku Wanaume wa Kiyahudi waliokuwa na ndevu ambazo hazikuwa zimetunzwa vyema na nywele ambazo zilikuwa ndefu kidogo kuliko kawaida walitambulika mara moja kama watu waliokuwa wamekula kiapo cha kuwa Wanazari (Nazarite).

    Hii ilikuwa na maana kwamba wangejitoa wakfu kwa Mungu kwa kipindi fulani, ambapo hawangekunywa vileo wala kuzikata nywele zao. Mwisho wa kipindi hicho, wangenyolewa nywele zao katika sherehe maalum hekaluni Jerusalem (kama inavyoelezwa katika kitabu cha Matendo ya Mitume, Sura ya 21, aya ya 24).
    Lakini Yesu hakuwa amekula kiapo cha kuwa Mnazari, kwa sababu mara nyingi tunamsikia kwenye Biblia akinywa divai - wakosoaji wake hata wakati mwingine wanamshutumu kwa kunywa divai sana, kupita kiasi (Matayo Sura ya 11, aya ya 19). Kama angekuwepo na nywele ndefu, na kuonekana kama Mnazari, tungelitarajia basi kuwepo na tamko pahala fulani kuhusu tofauti ya muonekano wake na matendo aliyokuwa akiyafanya ambayo hayakuendana na Unazari. Hali kwamba alikuwa akinywa divai yenyewe ingekuwa tatizo kubwa.

    Wakati Yesu alipoishi, matajiri walizoea kuvalia kanzu na majoyo ya vitambaa vya thamani, kuonyesha hadhi yao katika jamii. Katika moja ya mahubiri yake, Yesu anasema : "Jihadharini na walimu wa sheria (waandishi). Wao hupenda kutembea wakiwa wamevaa mavazi marefu (stolai), na kusalimiwa kwa heshima masokoni. Pia wao hupenda kukaa kwenye viti vya mbele katika masinagogi, na kupewa nafasi za heshima katika karamu." Mafundisho haya ya Yesu kwa kawaida huchukuliwa kama yenye maelezo ya kuaminika zaidi kwenye Injili, hivyo tunaweza kuwa na msingi kuamini kwamba Yesu hakuvalia mavazi kama hayo marefu. Kwa jumla, mwanamume wakati huo wa Yesu angevalia gwanda au kanzu fupi hivi, na mwanamke angevalia vazi lililomfika kwenye kifundo cha mguu.

    Kwa hivyo, katika karne ya 2 kwenye kitabu cha Matendo ya Mitume, Paul na Thecla, inapotokea kwamba Thecla ambaye ni mwanamke anavalia kanzu fupi kama mwanamume, hilo ni jambo linaloshangaza sana. Kanzu hizi kwa kawaida zingekuwa na ukanda au mstari wa rangi tofauti kutoka kwenye bega hadi kwenye pindo sehemu ya chini. Ni vazi ambalo lingeshonwa au kufumwa kama kipande kimoja cha vazi. Juu ya kanzu hiyo, ungejifunga joho au vazi jingine la nje, na tunajua kwamba Yesu alivalia vazi kama hilo kwa sababu ndilo lililoguswa na mwanamke aliyetaka kuponywa naye. (Marko 5:27): Alikuwa amesikia habari za Yesu, naye akaja kwa nyuma yake kwenye umati wa watu, akaligusa vazi lake, kwa maana alisema moyoni mwake, 'Kama nikiweza kuligusa vazi lake tu, nitaponywa.') Vazi hilo la nje lilifumwa kwa manyoya, lakini halikuwa zito sana na ndipo ili uhisi joto ingemlazimu mtu kuvalia mavazi mawili kama hayo.

    Vazi hilo lingevaliwa kwa njia nyingi, na wakati mwingine lingening'inia hadi chini ya magoti na kulifunika lile kanzu fupi la ndani. (Baadhi ya wanafalsafa walizoea kuvalia vazi hilo la nje pekee bila kuvalia ile kanzu ya ndani na kuacha sehemu ya bega au kifua ikiwa wazi). Mamlaka na hadhi ya mtu ni vitu ambavyo vilidhihirishwa kupitia ubora, ukubwa na rangi ya mavazi hayo ya nje. Rangi ya zambarau na baadhi ya aina za rangi ya buluu (samawati) ni rangi zilizoashiria utajiri, hadhi na kujionea fahari. Zilikuwa ni rangi za kifahari kwa sababu viungo vya kutengeneza rangi hizo vilikuwa adimu na ghali sana.

    Lakini rangi pia huashiria kitu kingine tofauti. Mwanahistoria Josephus, anawaeleza walokole waliofahamika kama Zealots (kundi la Wayahudi wa itikadi kali waliotaka kuwafurusha Warumi kutoka Judea) kama kundi la wahalifu wauaji waliovalia mavazi ya nje yaliyopakwa rangi kwa jina - mavazi anayoyaita chlanidia - kuashiria kwamba yalikuwa ni kama mavazi yaliyovaliwa na wanawake. Hii inaashiria kwamba wanaume kamili, kama hawakuwa na cheo cha juu zaidi katika jamii, walifaa kuvalia mavazi yasiyopakwa rangi.
    Yesu hakuvalia mavazi meupe hata hivyo. Haya yalikuwa mavazi ya kipekee na yalihitaji kupaushwa mara kwa mara (kufanywa meupe tena) au kupakwa chokaa. Judea, mavazi kama hayo meupe yalihusishwa na kundi lililofahamika kama Essenes - ambao ni watu waliofuata ufasiri mkali wa sheria za Kiyahudi. Tofauti kati ya mavazi ya Yesu na mavazi mengine ya rangi nyeupe ya kung'aa inaelezwa kwenye sura ya 9 ya Marko ambapo anaandamana na mitume watatu mlimani.

    Yesu aliwachukua "Petro, Yakobo na Yohana, akawapeleka juu ya mlima mrefu, mahali walipokuwa faraghani. Huko, Yesu akageuka sura mbele yao. Mavazi yake yakawa na weupe wa kuzima macho, meupe kuliko ambavyo mtu yeyote duniani angaliweza kuyangʼarisha. Mose na Eliya wakawatokea, wakawa wanazungumza na Yesu." Marko anaeleza kwamba mavazi ya Yesu yaligeuka rangi yakawa meupe sana, hapa anarejelea vazi la ndani na si la nje. Kabla ya kugeuka sura huku kwa Yesu, anaoneshwa na Marko kama mwanamume wa kawaida, aliyevalia mavazi ya kawaida, ambayo ni ya rangi ambayo haijapaushwa. Katika hali ambayo ndipo yang'ae na kuangaza unahitaji kumpelekea fundi.

    Tunaelezwa zaidi kuhusu mavazi ya Yesu wakati wa kusulubiwa kwake, pale wanajeshi wa Kirumi wanapoyakata mavazi yake ya nje vipande vinne (Yohana19:23: Askari walipokwisha kumsulubisha Yesu, walichukua nguo zake wakazigawa mafungu manne, kila askari fungu lake. Ila walikubaliana wasilichane lile vazi lake kwa maana lilikuwa halina mshono bali limefumwa tangu juu hadi chini.) Kuna uwezekano mavazi hayo ya nje yalikuwa mavazi mawili.

    Moja ya vazi hili huenda lilikuwa ni tallith, ambalo ni vazi la kujifunga Kiyahudi wakati wa maombi. Vazi hili lenye shada (tzitzith) limetajwa moja kwa moja na Yesu katika kitabu cha Mathayo 23:5 anapozungumza kuhusu walimu wa sheria na Mafarisayo (Wao hutenda mambo yao yote ili waonekane na watu. Hupanua vikasha vyao vyenye maandiko ya sheria na kurefusha matamvua ya mavazi yao). Lilikuwa ni vazi la nje lisilo zito, ambalo kawaida lilitengenezwa kwa kitambaa cha manyoya na lilikuwa la rangi ya malai hivi (krimu), na pengine lilikuwa na ukanda au mstari wa rangi ya nili (bluu iliyoiva).

    Miguuni, Yesu angevalia ndara (kandambili au malapa). Kila mtu wakati huo alivalia ndara. Katika mapango yaliyo jangwani karibu na Bahari ya Chumvi (Bahari Mfu) na Masada, ndara za wakati alipoishi Yesu zimegunduliwa, na tunaweza kutazama ndara ambazo huenda alivaa zilivyoonekana. Zilikuwa hazijafanyiwa kazi nyingi sana ya kiufundi. Soli (nyayo au kikanyagio) zake zilikuwa vipande vigumu vya ngozi vilivyoshonwa pamoja, na juu kulikuwa ni kanda za ngozi ambazo mbele zingeingizwa katikati ya vidole, kama malapa tu ya siku hizi.

    Yesu (Nabii Issa) Alikuwa Myahudi, na uso wake pia bila shaka ungefanana na Wayahudi wa wakati huo. Hali kwamba Yesu alikuwa Myahudi (au Mjudea) ni jambo linalorejelewa katika vitabu vingi, zikiwemo barua za Mtume Paulo. Na katika barua yake kwa Waebrania, anaandika: "Kwa maana ni dhahiri kwamba Bwana wetu alitoka katika uzao wa Yuda" (Sura ya 7:14) Kwa hivyo, Myahudi wa wakati huo, mwanamume wa miaka 30 hivi alipoanza kueneza Injili kwa mujibu wa Luka 3, pia akiwa ni mwenye ngozi nyeusi kama ilivyokuwa kwa wayahudi wengi zama zile waliokuwa wakitembeleana na ndugu zao wa Misri (Kushi) kemet.

    Mwaka 2001 mwanaantholopojia (mtaalamu wa elimu ya binadamu hasa elimu ihusuyo habari zinazohusu asili na maendeleo yake ya awali) Richard Neave alitengeneza mfano wa mwanamume wa Galilaya wa zama za Yesu ambao ulitumiwa kwa jina Son of God (Mwana wa Mungu). Alitumia fuvu lililopatikana katika eneo hilo. Hakusema kwamba huo ulikuwa muonekano wa uso wa Yesu. Mfano ulikuwa tu wa kuchochea hisia na kuwafanya watu kumfikiria Yesu kama mwanamume wa zama hizo na eneo hilo, kwa sababu hakuna mchoro wala maelezo yaliyopo ya kina kuhusu muonekano wake halisi.

    Ingawa tunaweza kupata viashiria kutoka kwa teknolojia na kutumia mifupa ya watu wa kale, kiashiria cha karibu sana kuhusu pengine Yesu alionekana vipi labda kinaweza kutokana na mchoro wa Musa kwenye ukuta wa sinagogi ya karne ya 3 ya Dura-Europos, kwani mchoro huo unaonesha jinsi Myahudi wa hekima alidhaniwa kuwa wakati wa utawala wa Wagiriki na Warumi. Musa anaoneshwa akiwa na mavazi ambayo hayajapaushwa, na moja ya vazi lake la nje ni tallith.

    Katika mchoro huo wa Dura wa Musa akitenganisha maji kwenye Bahari ya Sham ili Waisraeli wapite, unaweza kuziona shada (tzitzith) kwenye kona za vazi hilo. Kwa kiwango kikubwa, picha hiyo pengine inatoa msingi bora zaidi wa kumfikiria Yesu alivyokuwa badala ya picha za sasa zinazoongozwa na busara na mawazo ya enzi ya Byzantine - alikuwa na nywele fupi, ndevu fupi, na alikuwa amevalia kanzu fupi lenye mikono mifupi, na alikuwa na joho au vazi la nje.

    Makala hii chimbuko lake ni makala ya Kiingereza ya Joan Taylor ambaye ni profesa wa kitivo cha Asili ya Ukristo na Hekalu la Pili la Wayahudi katika Chuo Kikuu cha King's College London na ndiye mwandishi wa kitabu kwa jina The Essenes, the Scrolls and the Dead Sea.
    MUONEKANO WA NABII ISSA MIAKA HIYO ULIKUWAJE ? Karibu kila mtu ana dhana fulani kuhusu muonekano wa Yesu Kristo. Ndiye mtu aliyechorwa zaidi katika sanaa ya Magharibi. Picha zake hutambuliwa kwa urahisi, ambapo huoneshwa akiwa na nywele na ndevu, akiwa amevalia vazi lefu lenye mikono mirefu linalofanana na kanzu ( la rangi nyeupe), na pia akiwa amejifunga joho (la rangi ya samawati). Muonekano wa Yesu umefahamika sana na wengi kiasi kwamba unaweza kutambuliwa ukiwa hata kwenye mikate au biskuti. Picha za sasa za Yesu zinatokana na enzi ya Byzantine, himaya iliyokuwa na mji mkuu wake Constantinople. Ni picha iliyoanza kutumika karne ya nne hivi. Michoro ya Yesu ya wakati wa utawala wa Byzantine ilikuwa ya ishara, na si muonekano wake. Wasanii waliangazia zaidi maana na si kumfananisha na Yesu mwenyewe. Picha zao ziliongozwa na dhana ya Yesu kama mtawala, kwenye kiti cha enzi, kama anavyoonyeshwa kwenye mchoro ulio kwenye altari ya kanisa la Santa Pudenziana jijini Roma. Yesu anaoneshwa akiwa amevalia mgolole wa rangi ya dhahabu. Ndiye mtawala wa dunia yote aliyetoka mbinguni, mfanano wa picha yake ni ule wa sanamu ya Zeus wa Olympus anayeonyeshwa akiwa na nywele ndefu za ndevu kwenye kiti cha enzi. Ni sanamu iliyokuwa maarufu sana wakati huo kiasi kwamba Mfalme Augustus wa Roma alishurutisha naye atengenezewe sanamu kama hiyo, lakini yake ikiwa bila nywele ndefu na ndevu, Wasanii wa Byzantine, walitaka kumuonyesha Kristo kama mtawala kutoka mbinguni, mfalme wa aina yake, na hivyo wakachora wakimuonyesha kama Zeus, lakini akiwa mdogo kidogo wa umri. Kilichotokea kadiri miaka ilivyosonga ni kwamba kuonyeshwa huku kwa Kristo kama mtawala kutoka mbinguni - ambapo wakati mwingine ameonyeshwa hata akiwa kama 'hippie' au 'superstar' (kama ilivyo kwenye mchoro huu hapa chini) - ndiko kumekuwa kama kigezo chetu cha Yesu alivyokuwa. Hebu tuchanganue kutoka kichwani hadi vidole vya miguuni. Wakristo wa nyakati za kwanza wakati walipokuwa wanamwonyesha Kristo si kama mtawala kutoka mbinguni, walimuonyesha kama binadamu wa kawaida tu - akiwa hana ndevu na hana nywele ndefu. Lakini pengine, kama msomi wa aina yake aliyekuwa akisafiri kutoka eneo moja hadi jingine, Yesu pengine alikuwa na ndevu, kwa sababu hakuwa akienda kwa vinyozi. Kwa kawaida, kuwa mchafu kiasi na kuwa na ndevu ndefu ni sifa ambazo zilihusishwa na wanafalsafa, wasomi wa ngazi ya juu, na kuwatenganisha na watu wa kawaida. Mwanafalsafa maarufu wa kundi la Stoic (Wanafalsafa wa Kigiriki waliofuata mafundisho ya mwanzilishi wao Zeno wa Citium mjini Athens mapema karne ya 3 kabla ya kuzaliwa kwa Yesu) Epictetus aliamini "ilifaa hivyo kwa mujibu wa maumbile." Mambo yalibadilika katika karne ya 1 baada ya kuzaliwa kwa Yesu, wakati wa enzi za Warumi na Wagiriki, ambapo kuwa na nywele fupi na kunyoa ndefu ndiyo mambo yaliyochukuliwa kuwa yafaayo na ya kistaarabu. Kuwa na nywele ndefu na ndevu ni mambo ambayo yaliachiwa miungu pekee, si ya watu wa kawaida. Hata wanafalsafa enzi hizo walikuwa na nywele fupi. Ndevu pia hazikuwa sifa za kuwatambulisha Wayahudi enzi hizo. Ukweli ni kwamba moja ya changamoto ambazo waliotaka kuwatesa Wayahudi vipindi mbalimbali katika historia walihangaika sana kuwatofautisha na watu wengine. Hii ni kwa sababu wote walifanana (jambo ambalo limegusiwa katika kitabu cha Wamakabayo). Hata hivyo, picha za wanaume wa Kiyahudi zilizokuwa kwenye sarafu za Judea Capta ambazo zilitolewa na utawala wa Roma baada ya kutekwa kwa mji wa Yerusalemu mwaka 70 baada ya kuzaliwa kwa Yesu zinawaonesha wanaume wakiwa na ndevu, lakini nywele zao si ndefu. Kwa hivyo, Yesu, kama mwanafalsafa wa muonekano wa kawaida, kuna uwezekano alikuwa na ndevu lakini si ndefu sana, sawa na wanaume hao walioonyeshwa kwenye sarafu za Judaea Capta, lakini nywele zake basi hazikuwa ndefu sana pia. Kama ingetokea kwamba awe na nywele ndefu hata kidogo tu kuliko kawaida, basi angezua mtafaruku Wanaume wa Kiyahudi waliokuwa na ndevu ambazo hazikuwa zimetunzwa vyema na nywele ambazo zilikuwa ndefu kidogo kuliko kawaida walitambulika mara moja kama watu waliokuwa wamekula kiapo cha kuwa Wanazari (Nazarite). Hii ilikuwa na maana kwamba wangejitoa wakfu kwa Mungu kwa kipindi fulani, ambapo hawangekunywa vileo wala kuzikata nywele zao. Mwisho wa kipindi hicho, wangenyolewa nywele zao katika sherehe maalum hekaluni Jerusalem (kama inavyoelezwa katika kitabu cha Matendo ya Mitume, Sura ya 21, aya ya 24). Lakini Yesu hakuwa amekula kiapo cha kuwa Mnazari, kwa sababu mara nyingi tunamsikia kwenye Biblia akinywa divai - wakosoaji wake hata wakati mwingine wanamshutumu kwa kunywa divai sana, kupita kiasi (Matayo Sura ya 11, aya ya 19). Kama angekuwepo na nywele ndefu, na kuonekana kama Mnazari, tungelitarajia basi kuwepo na tamko pahala fulani kuhusu tofauti ya muonekano wake na matendo aliyokuwa akiyafanya ambayo hayakuendana na Unazari. Hali kwamba alikuwa akinywa divai yenyewe ingekuwa tatizo kubwa. Wakati Yesu alipoishi, matajiri walizoea kuvalia kanzu na majoyo ya vitambaa vya thamani, kuonyesha hadhi yao katika jamii. Katika moja ya mahubiri yake, Yesu anasema : "Jihadharini na walimu wa sheria (waandishi). Wao hupenda kutembea wakiwa wamevaa mavazi marefu (stolai), na kusalimiwa kwa heshima masokoni. Pia wao hupenda kukaa kwenye viti vya mbele katika masinagogi, na kupewa nafasi za heshima katika karamu." Mafundisho haya ya Yesu kwa kawaida huchukuliwa kama yenye maelezo ya kuaminika zaidi kwenye Injili, hivyo tunaweza kuwa na msingi kuamini kwamba Yesu hakuvalia mavazi kama hayo marefu. Kwa jumla, mwanamume wakati huo wa Yesu angevalia gwanda au kanzu fupi hivi, na mwanamke angevalia vazi lililomfika kwenye kifundo cha mguu. Kwa hivyo, katika karne ya 2 kwenye kitabu cha Matendo ya Mitume, Paul na Thecla, inapotokea kwamba Thecla ambaye ni mwanamke anavalia kanzu fupi kama mwanamume, hilo ni jambo linaloshangaza sana. Kanzu hizi kwa kawaida zingekuwa na ukanda au mstari wa rangi tofauti kutoka kwenye bega hadi kwenye pindo sehemu ya chini. Ni vazi ambalo lingeshonwa au kufumwa kama kipande kimoja cha vazi. Juu ya kanzu hiyo, ungejifunga joho au vazi jingine la nje, na tunajua kwamba Yesu alivalia vazi kama hilo kwa sababu ndilo lililoguswa na mwanamke aliyetaka kuponywa naye. (Marko 5:27): Alikuwa amesikia habari za Yesu, naye akaja kwa nyuma yake kwenye umati wa watu, akaligusa vazi lake, kwa maana alisema moyoni mwake, 'Kama nikiweza kuligusa vazi lake tu, nitaponywa.') Vazi hilo la nje lilifumwa kwa manyoya, lakini halikuwa zito sana na ndipo ili uhisi joto ingemlazimu mtu kuvalia mavazi mawili kama hayo. Vazi hilo lingevaliwa kwa njia nyingi, na wakati mwingine lingening'inia hadi chini ya magoti na kulifunika lile kanzu fupi la ndani. (Baadhi ya wanafalsafa walizoea kuvalia vazi hilo la nje pekee bila kuvalia ile kanzu ya ndani na kuacha sehemu ya bega au kifua ikiwa wazi). Mamlaka na hadhi ya mtu ni vitu ambavyo vilidhihirishwa kupitia ubora, ukubwa na rangi ya mavazi hayo ya nje. Rangi ya zambarau na baadhi ya aina za rangi ya buluu (samawati) ni rangi zilizoashiria utajiri, hadhi na kujionea fahari. Zilikuwa ni rangi za kifahari kwa sababu viungo vya kutengeneza rangi hizo vilikuwa adimu na ghali sana. Lakini rangi pia huashiria kitu kingine tofauti. Mwanahistoria Josephus, anawaeleza walokole waliofahamika kama Zealots (kundi la Wayahudi wa itikadi kali waliotaka kuwafurusha Warumi kutoka Judea) kama kundi la wahalifu wauaji waliovalia mavazi ya nje yaliyopakwa rangi kwa jina - mavazi anayoyaita chlanidia - kuashiria kwamba yalikuwa ni kama mavazi yaliyovaliwa na wanawake. Hii inaashiria kwamba wanaume kamili, kama hawakuwa na cheo cha juu zaidi katika jamii, walifaa kuvalia mavazi yasiyopakwa rangi. Yesu hakuvalia mavazi meupe hata hivyo. Haya yalikuwa mavazi ya kipekee na yalihitaji kupaushwa mara kwa mara (kufanywa meupe tena) au kupakwa chokaa. Judea, mavazi kama hayo meupe yalihusishwa na kundi lililofahamika kama Essenes - ambao ni watu waliofuata ufasiri mkali wa sheria za Kiyahudi. Tofauti kati ya mavazi ya Yesu na mavazi mengine ya rangi nyeupe ya kung'aa inaelezwa kwenye sura ya 9 ya Marko ambapo anaandamana na mitume watatu mlimani. Yesu aliwachukua "Petro, Yakobo na Yohana, akawapeleka juu ya mlima mrefu, mahali walipokuwa faraghani. Huko, Yesu akageuka sura mbele yao. Mavazi yake yakawa na weupe wa kuzima macho, meupe kuliko ambavyo mtu yeyote duniani angaliweza kuyangʼarisha. Mose na Eliya wakawatokea, wakawa wanazungumza na Yesu." Marko anaeleza kwamba mavazi ya Yesu yaligeuka rangi yakawa meupe sana, hapa anarejelea vazi la ndani na si la nje. Kabla ya kugeuka sura huku kwa Yesu, anaoneshwa na Marko kama mwanamume wa kawaida, aliyevalia mavazi ya kawaida, ambayo ni ya rangi ambayo haijapaushwa. Katika hali ambayo ndipo yang'ae na kuangaza unahitaji kumpelekea fundi. Tunaelezwa zaidi kuhusu mavazi ya Yesu wakati wa kusulubiwa kwake, pale wanajeshi wa Kirumi wanapoyakata mavazi yake ya nje vipande vinne (Yohana19:23: Askari walipokwisha kumsulubisha Yesu, walichukua nguo zake wakazigawa mafungu manne, kila askari fungu lake. Ila walikubaliana wasilichane lile vazi lake kwa maana lilikuwa halina mshono bali limefumwa tangu juu hadi chini.) Kuna uwezekano mavazi hayo ya nje yalikuwa mavazi mawili. Moja ya vazi hili huenda lilikuwa ni tallith, ambalo ni vazi la kujifunga Kiyahudi wakati wa maombi. Vazi hili lenye shada (tzitzith) limetajwa moja kwa moja na Yesu katika kitabu cha Mathayo 23:5 anapozungumza kuhusu walimu wa sheria na Mafarisayo (Wao hutenda mambo yao yote ili waonekane na watu. Hupanua vikasha vyao vyenye maandiko ya sheria na kurefusha matamvua ya mavazi yao). Lilikuwa ni vazi la nje lisilo zito, ambalo kawaida lilitengenezwa kwa kitambaa cha manyoya na lilikuwa la rangi ya malai hivi (krimu), na pengine lilikuwa na ukanda au mstari wa rangi ya nili (bluu iliyoiva). Miguuni, Yesu angevalia ndara (kandambili au malapa). Kila mtu wakati huo alivalia ndara. Katika mapango yaliyo jangwani karibu na Bahari ya Chumvi (Bahari Mfu) na Masada, ndara za wakati alipoishi Yesu zimegunduliwa, na tunaweza kutazama ndara ambazo huenda alivaa zilivyoonekana. Zilikuwa hazijafanyiwa kazi nyingi sana ya kiufundi. Soli (nyayo au kikanyagio) zake zilikuwa vipande vigumu vya ngozi vilivyoshonwa pamoja, na juu kulikuwa ni kanda za ngozi ambazo mbele zingeingizwa katikati ya vidole, kama malapa tu ya siku hizi. Yesu (Nabii Issa) Alikuwa Myahudi, na uso wake pia bila shaka ungefanana na Wayahudi wa wakati huo. Hali kwamba Yesu alikuwa Myahudi (au Mjudea) ni jambo linalorejelewa katika vitabu vingi, zikiwemo barua za Mtume Paulo. Na katika barua yake kwa Waebrania, anaandika: "Kwa maana ni dhahiri kwamba Bwana wetu alitoka katika uzao wa Yuda" (Sura ya 7:14) Kwa hivyo, Myahudi wa wakati huo, mwanamume wa miaka 30 hivi alipoanza kueneza Injili kwa mujibu wa Luka 3, pia akiwa ni mwenye ngozi nyeusi kama ilivyokuwa kwa wayahudi wengi zama zile waliokuwa wakitembeleana na ndugu zao wa Misri (Kushi) kemet. Mwaka 2001 mwanaantholopojia (mtaalamu wa elimu ya binadamu hasa elimu ihusuyo habari zinazohusu asili na maendeleo yake ya awali) Richard Neave alitengeneza mfano wa mwanamume wa Galilaya wa zama za Yesu ambao ulitumiwa kwa jina Son of God (Mwana wa Mungu). Alitumia fuvu lililopatikana katika eneo hilo. Hakusema kwamba huo ulikuwa muonekano wa uso wa Yesu. Mfano ulikuwa tu wa kuchochea hisia na kuwafanya watu kumfikiria Yesu kama mwanamume wa zama hizo na eneo hilo, kwa sababu hakuna mchoro wala maelezo yaliyopo ya kina kuhusu muonekano wake halisi. Ingawa tunaweza kupata viashiria kutoka kwa teknolojia na kutumia mifupa ya watu wa kale, kiashiria cha karibu sana kuhusu pengine Yesu alionekana vipi labda kinaweza kutokana na mchoro wa Musa kwenye ukuta wa sinagogi ya karne ya 3 ya Dura-Europos, kwani mchoro huo unaonesha jinsi Myahudi wa hekima alidhaniwa kuwa wakati wa utawala wa Wagiriki na Warumi. Musa anaoneshwa akiwa na mavazi ambayo hayajapaushwa, na moja ya vazi lake la nje ni tallith. Katika mchoro huo wa Dura wa Musa akitenganisha maji kwenye Bahari ya Sham ili Waisraeli wapite, unaweza kuziona shada (tzitzith) kwenye kona za vazi hilo. Kwa kiwango kikubwa, picha hiyo pengine inatoa msingi bora zaidi wa kumfikiria Yesu alivyokuwa badala ya picha za sasa zinazoongozwa na busara na mawazo ya enzi ya Byzantine - alikuwa na nywele fupi, ndevu fupi, na alikuwa amevalia kanzu fupi lenye mikono mifupi, na alikuwa na joho au vazi la nje. Makala hii chimbuko lake ni makala ya Kiingereza ya Joan Taylor ambaye ni profesa wa kitivo cha Asili ya Ukristo na Hekalu la Pili la Wayahudi katika Chuo Kikuu cha King's College London na ndiye mwandishi wa kitabu kwa jina The Essenes, the Scrolls and the Dead Sea.
    0 Comments ·0 Shares ·858 Views
  • DOUBLE AGENTS NGULI WANNE KUWAHI KUTOKEA KATIKA ULIMWENGU WA UJASUSI

    Mustakabali wa taifa lolote lile hutegemea pamoja na mambo mengine mifumo ya ulinzi, kwani hii ndio nguzo mhimu katika kuhakikisha ustawi wa maslahi ya taifa husika

    Ni kwa msingi huo basi mataifa yote duniani yameunda vyombo tofauti tofauti vya ulinzi mojawapo ikiwemo idara za ujajusi, mifano ipo mingi, CIA, M16, BND, MOSSAD, TISS n.k!

    Lakini kuwa na taasisi au vyombo hivyo vinahiyaji nguvu kazi, nguvu kazi hii sharti iwe yenye weledi na uzalendo wa kutukuka, kwani kazi wanayoifanya ni kazi nyeti mno na inayozungukwa na mambo mengi sana, hivyo kuteleza kwa namna yoyote ile basi kunaacha madhara makubwa mno! Na kiukweli wapo walioteleza na kuleta madhara yasiyoelezeka, sasa Leo nimeona tuangalie kwa ufupi baadhi ya wanausalama walioteleza na kujikuta walitumia pande mbili au zaidi maarufu kwa jina la *DOUBLE AGENT*

    *Lakini kwanza kabisa double agent ni nani?*

    Tunaweza tukasema ni afisa usalama wa tasisis au serikali ambaye amepewa majukumuu ya kuichunguza taasisi au nchi nyingine lakini wakati huo huo anakuwa tena anafanya kazi hiyo hiyo kwa ajiri ya taasisi au nchi anayopaswa kuichunguza dhidi ya taasisi au nchi iliyomtuma! Wengi wanasem double agent anaweza kuwa matokeo ya tamaa ya pesa, kulazimishwa( baada ya kutishiwa kufanyiwa kitu kibaya), mapenzi tu, yaani mtu anapenda tu kuwa double agent, kupandikizwa kwa makusudi( marekani wamefaidika sana na aina hii hasa Mashariki ya kati) au inaweza kuwa ni sababu ya mitazamo…

    Hawa wafuatao ni baadhi ya double agents nguli kuwahi kutokea na balaa

    *Human Khalid Al-Balawi*

    Huyu jamaa alikuwa daktari kitaaluma na alikuwa raia wa Jordan, alikamatwa na mamlaka za Jordan kipindi akiwa mwanafunzi kwenye chuo kikuu cha Isntanbul nchini Uturuki baada ya kuonekana akiwa na muelekeo wa misimamamo mikali, inasemekana baadae CIA waliingilia na kumshawishi awe double agent kwa ahadi ya kusamehewa. Jamaa alikubali na CIA wakamuandaa kikamilifu kwa kazi hiyo ambapo baada ya kuiva wakampeleka Pakistan na Afghanistan na kumpa jukumuu la kufuatilia nyendo na shughuli za alqaida nchini humo.

    Human aliifanya kazi hiyo kwa uaminifu mkubwa mno na akafanikiwa kuwashawishi CIA ambao walionekana kumwamini 100%. Kumbe hawakujua kuwa aliqaida walikuwa tayari wamembadilisha na alikuwa akifanya nao kazi.

    Siku moja akawaeleza kuwa alikuwa na taarifa muhimu kuhusu kiongozi wa juu wa alqaida bwana Ayman- Al-Zawahili na akawapa masharti kuwa angependa taarifa hizo azifikishe kwa viongozi wakuu wa CIA katika eneo hilo, kwakuwa walikuwa wanamtafuta sana Zawahili hawakusita kumkubalia na kumuagiza afike kwenye Ofisi za CIA eneo la Khost Afghanistan, Khalid alifika kwa kuchelewa na kutokana na kimuhe muhe cha taarifa waliyokuwa wanakwenda kuipokea basi wakasahau hadi kumkagua, kumbe jamaa alikuwa amevaa mabomu, baada ya kufika ndani kwa wakubwa jamaa alijilipua na kuua maafisa kadhaa wa ngazi za juu wa CIA katika eneo hilo.

    *Arthur Owens*

    Arthur alikuwa mwingereza kutoka kisiwa cha Wales na kabla ya vita ya dunia ya pili alikuwa akifanya kazi kama mkandarasi na alikuwa akifanya serikali zote mbili, Ujerumani na England, baada ya vita kuanza aliajiriwa kama mhandisi kwenye meli vita za England akifanya kazi kama fundi betri, baadae Wajerumani walianza kumuomba awape taarifa hasa kuhusu meli vita za England na yeye bila hiana akifanya kazi hiyo, baadae alijiunga nao rasmi na akawa anafanya kazi nao huku pesa na wanawake wazuri yakiwa ndo malipo kwa kazi yake hiyo tukufu.

    Baadae alirudi England na kujipeleka moja kwa moja kwa M15 na kuwaeleza ukweli wake na wajerumani, M16 walimpokea na kumtumia ambapo aliwasaidia kufichua zaidi maofisa 120 wa kijeruman nchini England na wakamtumia kuwalisha Wajerumani hao habari za uongo na zile zisixokuwa na athari kubwa kwao.

    Mwaka 1941 Arthur na mwenzake mmoja walikamatwa na wajerumani lakini cha ajabu mwenzake alinyongwa huku yeye akiachwa hali iliyowatia wasiwasi England na alivyorudi walimkamata na kumtia kolokoloni hadi baada ya vita, baadae aliwalazimisha England wamlipe fedha kwa maadai ya kumfunga bila makosa na kama watagoma basi ataweka hadharani kila kitu, England walinywea na hadi anakufa hakuwahi kusema chochote.

    *Kim Philby*

    Kim Philby alikuwa ni afisa wa idara ya usalama ya England, yeye na wenzake wanne walitengeza a spy ring iliyopewa jina la the Combridge five, na wakifanya kazi kwa niaba ya KGB, ni kipindi ambacho wote watano walikuwa wakisoma chuoni hapo, wenzake walikuwa ni pamoja na Donald MacLean, Guy borguess na Anthony Brunt ambapo mtu wa tano kwenye kundi hilo hadi Leo hajawahi kujulikana! Kimsingi Borguess ndiye aliyemsajili Kim na wakati huyo tayari yeye alikuwa ni double agent.

    Kilichomsukuma Kim ilikuwa ni imani yake katika falsafa za kijamaa, pamoja na kuwa double agent lakini Kim anasemwa kama mtu aliyefanya kazi kwa weledi mkubwa sana na alipata kutunukiwa nishani kadhaa kwa utumishi uliotukuka kabla ya kuja kumgundua kuwa alikuwa akifanya kazi na KGB, wakati wenzake wanakamatwa yeye alikuwa ameshaacha kazi na alikuwa Lebanon na hakurudi tena England Bali aliekea Jamhuri ya Usovieti ambako alipewa kazi kwenye idara kadhaa za ulinzi, alifariki mwaka 1988 akiwa huko huko Usovieti, Kim aliandika kitabu alichokipa jina la *My secret war* akieleza namna alivyopambana na ubepari.

    *Juan Pujol Garsia*

    Garsia alikuwa mhisipania ambaye maisha yake yalionekana kutokua na muelekeo kwani kwenye umri wa miaka 32 alikuwa ameshindwa karibia kila kitu, shule, biashara na hata familia, vyote alikuwa amejaribu na vikamshinda.

    Baadae wakati wa vita kuu ya pili ya dunia aliamua kwenda kuomba kazi kwenye idara za usalama za England na Marekani lakini aligonga mwamba kwa madai mtu ambaye hakuwa na uwezo hata wa kufuga kuku angeweje kufanya kazi nyeti kama hii tena katika wakati tete. Baada ya kukataliwa akaona isiwe taabu akaenda zake kwa Wajerumani na kujifanya mmoja wa wanazi kindakindaki wa Hitler, manazi baadae walimuamini na kumpa kazi ambapo walimpangia kwenda England! Alielekea huko akipitia Porto Ureno na alianza kazi kwa kukusanya habari kwenye magazeti na redio, baadae alianza kupiga hatua kwa kusajili watu mhimu kutoka wazara ya habari na mawasiliano pamoja na masekretari kwenye wizara mbalimbali, baadae pia alifanikiwa kuingia hadi jeshini na jusajili watu huko.

    Garsia alikuja kuumbuliwa na double agent wa kijerumani ambaye aliwatonya England juu ya uwepo wake nchini humo.

    Baada ya kubumbuluka Garsia akijipeleka mwenyewe kwa M15 ambapo walikubali kuendelea kutumia mara hii wakimtumia kuwalisha habari za uongo.

    Garsia anakumbukwa sana kutokana na kazi tukufu aliyoifanya wakati majeshi ya muungano wa England, Canada, Marekani na baadhi ya wanajeshi wa Ufaransa yalipoanza oparesheni ya kukomboa maeneo yaliyokuwa yamekamatwa na Ujerumani na hasa katika uvamizi wa eneo la Normandy, baada ya wanajeshi wa muungano kuelekea katika eneo hilo wajerumani walipata intelejensia na wakawa wametuma vikosi kwenda kupambana na majeshi ya muungano huku vikosi vingine vikiwekwa tayari nchini ubelgiji, lakini Garsia kwa ujasiri wa hali ya juu akamtumia telegraphy na kumwambia hakukuwa na mashambulizi yoyote katika eneo hilo na kwamba habari alizokuwa amepewa Hitler ulikuwa ni uongo, kwakuwa Hitler alikuwa anamuamini sana basi akaiamini taarifa hii na akaviamrisha vikosi vyake vilivyokuwa njiani kurejea na vile vilivyokuwa ubelgiji kuendelea kubaki.

    Wengi wanachukulia hatua hii kama mwanzo wa majeshi ya muungano kuanza kujizatiti kwani hadi hapo Ujerumani ilikuwa tayari imekamata karibu ulaya nzima na ndio maana Garsia anachukuliwa kama double agent aliyefanya kazi ya kutukuka, lakini pia anatajwa kama double agent aliyetunukiwa tunzo nyingi mno kutoka pande zote yaani Ujerumani na England, baada ya vita Garsia alikwenda zake Amerika kusini ambapo alifungua maktaba na kumalizia maisha yake huko.

    OUR MOTTO
    ========
    KIJANA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USITUMIKE VIBAYA KUICHAFUA NCHI YAKO.
    DOUBLE AGENTS NGULI WANNE KUWAHI KUTOKEA KATIKA ULIMWENGU WA UJASUSI Mustakabali wa taifa lolote lile hutegemea pamoja na mambo mengine mifumo ya ulinzi, kwani hii ndio nguzo mhimu katika kuhakikisha ustawi wa maslahi ya taifa husika Ni kwa msingi huo basi mataifa yote duniani yameunda vyombo tofauti tofauti vya ulinzi mojawapo ikiwemo idara za ujajusi, mifano ipo mingi, CIA, M16, BND, MOSSAD, TISS n.k! Lakini kuwa na taasisi au vyombo hivyo vinahiyaji nguvu kazi, nguvu kazi hii sharti iwe yenye weledi na uzalendo wa kutukuka, kwani kazi wanayoifanya ni kazi nyeti mno na inayozungukwa na mambo mengi sana, hivyo kuteleza kwa namna yoyote ile basi kunaacha madhara makubwa mno! Na kiukweli wapo walioteleza na kuleta madhara yasiyoelezeka, sasa Leo nimeona tuangalie kwa ufupi baadhi ya wanausalama walioteleza na kujikuta walitumia pande mbili au zaidi maarufu kwa jina la *DOUBLE AGENT* *Lakini kwanza kabisa double agent ni nani?* Tunaweza tukasema ni afisa usalama wa tasisis au serikali ambaye amepewa majukumuu ya kuichunguza taasisi au nchi nyingine lakini wakati huo huo anakuwa tena anafanya kazi hiyo hiyo kwa ajiri ya taasisi au nchi anayopaswa kuichunguza dhidi ya taasisi au nchi iliyomtuma! Wengi wanasem double agent anaweza kuwa matokeo ya tamaa ya pesa, kulazimishwa( baada ya kutishiwa kufanyiwa kitu kibaya), mapenzi tu, yaani mtu anapenda tu kuwa double agent, kupandikizwa kwa makusudi( marekani wamefaidika sana na aina hii hasa Mashariki ya kati) au inaweza kuwa ni sababu ya mitazamo… Hawa wafuatao ni baadhi ya double agents nguli kuwahi kutokea na balaa *Human Khalid Al-Balawi* Huyu jamaa alikuwa daktari kitaaluma na alikuwa raia wa Jordan, alikamatwa na mamlaka za Jordan kipindi akiwa mwanafunzi kwenye chuo kikuu cha Isntanbul nchini Uturuki baada ya kuonekana akiwa na muelekeo wa misimamamo mikali, inasemekana baadae CIA waliingilia na kumshawishi awe double agent kwa ahadi ya kusamehewa. Jamaa alikubali na CIA wakamuandaa kikamilifu kwa kazi hiyo ambapo baada ya kuiva wakampeleka Pakistan na Afghanistan na kumpa jukumuu la kufuatilia nyendo na shughuli za alqaida nchini humo. Human aliifanya kazi hiyo kwa uaminifu mkubwa mno na akafanikiwa kuwashawishi CIA ambao walionekana kumwamini 100%. Kumbe hawakujua kuwa aliqaida walikuwa tayari wamembadilisha na alikuwa akifanya nao kazi. Siku moja akawaeleza kuwa alikuwa na taarifa muhimu kuhusu kiongozi wa juu wa alqaida bwana Ayman- Al-Zawahili na akawapa masharti kuwa angependa taarifa hizo azifikishe kwa viongozi wakuu wa CIA katika eneo hilo, kwakuwa walikuwa wanamtafuta sana Zawahili hawakusita kumkubalia na kumuagiza afike kwenye Ofisi za CIA eneo la Khost Afghanistan, Khalid alifika kwa kuchelewa na kutokana na kimuhe muhe cha taarifa waliyokuwa wanakwenda kuipokea basi wakasahau hadi kumkagua, kumbe jamaa alikuwa amevaa mabomu, baada ya kufika ndani kwa wakubwa jamaa alijilipua na kuua maafisa kadhaa wa ngazi za juu wa CIA katika eneo hilo. *Arthur Owens* Arthur alikuwa mwingereza kutoka kisiwa cha Wales na kabla ya vita ya dunia ya pili alikuwa akifanya kazi kama mkandarasi na alikuwa akifanya serikali zote mbili, Ujerumani na England, baada ya vita kuanza aliajiriwa kama mhandisi kwenye meli vita za England akifanya kazi kama fundi betri, baadae Wajerumani walianza kumuomba awape taarifa hasa kuhusu meli vita za England na yeye bila hiana akifanya kazi hiyo, baadae alijiunga nao rasmi na akawa anafanya kazi nao huku pesa na wanawake wazuri yakiwa ndo malipo kwa kazi yake hiyo tukufu. Baadae alirudi England na kujipeleka moja kwa moja kwa M15 na kuwaeleza ukweli wake na wajerumani, M16 walimpokea na kumtumia ambapo aliwasaidia kufichua zaidi maofisa 120 wa kijeruman nchini England na wakamtumia kuwalisha Wajerumani hao habari za uongo na zile zisixokuwa na athari kubwa kwao. Mwaka 1941 Arthur na mwenzake mmoja walikamatwa na wajerumani lakini cha ajabu mwenzake alinyongwa huku yeye akiachwa hali iliyowatia wasiwasi England na alivyorudi walimkamata na kumtia kolokoloni hadi baada ya vita, baadae aliwalazimisha England wamlipe fedha kwa maadai ya kumfunga bila makosa na kama watagoma basi ataweka hadharani kila kitu, England walinywea na hadi anakufa hakuwahi kusema chochote. *Kim Philby* Kim Philby alikuwa ni afisa wa idara ya usalama ya England, yeye na wenzake wanne walitengeza a spy ring iliyopewa jina la the Combridge five, na wakifanya kazi kwa niaba ya KGB, ni kipindi ambacho wote watano walikuwa wakisoma chuoni hapo, wenzake walikuwa ni pamoja na Donald MacLean, Guy borguess na Anthony Brunt ambapo mtu wa tano kwenye kundi hilo hadi Leo hajawahi kujulikana! Kimsingi Borguess ndiye aliyemsajili Kim na wakati huyo tayari yeye alikuwa ni double agent. Kilichomsukuma Kim ilikuwa ni imani yake katika falsafa za kijamaa, pamoja na kuwa double agent lakini Kim anasemwa kama mtu aliyefanya kazi kwa weledi mkubwa sana na alipata kutunukiwa nishani kadhaa kwa utumishi uliotukuka kabla ya kuja kumgundua kuwa alikuwa akifanya kazi na KGB, wakati wenzake wanakamatwa yeye alikuwa ameshaacha kazi na alikuwa Lebanon na hakurudi tena England Bali aliekea Jamhuri ya Usovieti ambako alipewa kazi kwenye idara kadhaa za ulinzi, alifariki mwaka 1988 akiwa huko huko Usovieti, Kim aliandika kitabu alichokipa jina la *My secret war* akieleza namna alivyopambana na ubepari. *Juan Pujol Garsia* Garsia alikuwa mhisipania ambaye maisha yake yalionekana kutokua na muelekeo kwani kwenye umri wa miaka 32 alikuwa ameshindwa karibia kila kitu, shule, biashara na hata familia, vyote alikuwa amejaribu na vikamshinda. Baadae wakati wa vita kuu ya pili ya dunia aliamua kwenda kuomba kazi kwenye idara za usalama za England na Marekani lakini aligonga mwamba kwa madai mtu ambaye hakuwa na uwezo hata wa kufuga kuku angeweje kufanya kazi nyeti kama hii tena katika wakati tete. Baada ya kukataliwa akaona isiwe taabu akaenda zake kwa Wajerumani na kujifanya mmoja wa wanazi kindakindaki wa Hitler, manazi baadae walimuamini na kumpa kazi ambapo walimpangia kwenda England! Alielekea huko akipitia Porto Ureno na alianza kazi kwa kukusanya habari kwenye magazeti na redio, baadae alianza kupiga hatua kwa kusajili watu mhimu kutoka wazara ya habari na mawasiliano pamoja na masekretari kwenye wizara mbalimbali, baadae pia alifanikiwa kuingia hadi jeshini na jusajili watu huko. Garsia alikuja kuumbuliwa na double agent wa kijerumani ambaye aliwatonya England juu ya uwepo wake nchini humo. Baada ya kubumbuluka Garsia akijipeleka mwenyewe kwa M15 ambapo walikubali kuendelea kutumia mara hii wakimtumia kuwalisha habari za uongo. Garsia anakumbukwa sana kutokana na kazi tukufu aliyoifanya wakati majeshi ya muungano wa England, Canada, Marekani na baadhi ya wanajeshi wa Ufaransa yalipoanza oparesheni ya kukomboa maeneo yaliyokuwa yamekamatwa na Ujerumani na hasa katika uvamizi wa eneo la Normandy, baada ya wanajeshi wa muungano kuelekea katika eneo hilo wajerumani walipata intelejensia na wakawa wametuma vikosi kwenda kupambana na majeshi ya muungano huku vikosi vingine vikiwekwa tayari nchini ubelgiji, lakini Garsia kwa ujasiri wa hali ya juu akamtumia telegraphy na kumwambia hakukuwa na mashambulizi yoyote katika eneo hilo na kwamba habari alizokuwa amepewa Hitler ulikuwa ni uongo, kwakuwa Hitler alikuwa anamuamini sana basi akaiamini taarifa hii na akaviamrisha vikosi vyake vilivyokuwa njiani kurejea na vile vilivyokuwa ubelgiji kuendelea kubaki. Wengi wanachukulia hatua hii kama mwanzo wa majeshi ya muungano kuanza kujizatiti kwani hadi hapo Ujerumani ilikuwa tayari imekamata karibu ulaya nzima na ndio maana Garsia anachukuliwa kama double agent aliyefanya kazi ya kutukuka, lakini pia anatajwa kama double agent aliyetunukiwa tunzo nyingi mno kutoka pande zote yaani Ujerumani na England, baada ya vita Garsia alikwenda zake Amerika kusini ambapo alifungua maktaba na kumalizia maisha yake huko. OUR MOTTO ======== KIJANA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USITUMIKE VIBAYA KUICHAFUA NCHI YAKO.
    0 Comments ·0 Shares ·818 Views
  • MBONA SIJAELEWA HAPA!

    .Me:- mambo

    Dem:- poa

    Me:- unaishi wapi?

    Dem :- hapa tu Nairobi

    Me:- uko chuo?

    Dem:- ndio

    Me :- chuo gani

    Dem :- Urumah University
    Me:- Si NAMI paci unionee uruma na unipe fursa ya life yako.

    Dem:- ohooo! I am already to deserve you

    Me:- poa nimeangalia profile picture zako nimekupenda ghafla..."

    Dem:- Ahsante, una gari aina gani?!

    Me:- Nina land cruiser "

    Dem:- wahoo! Upo sahihi kunipenda najisikia raha ku chat na wewe".

    Me:- Ila Gari sio langu nimesaidiwa na rafiki yangu".

    Dem:- Nikuambie kitu!! Mimi nina boyfriend wangu na tunapendana sana

    Me:- land cruiser hiyo nimesadiwa na rafiki yangu kwasababu Gari yangu Harrier new model ilikuwa service"

    Dem:- nakutania tu sina boyfriend, Nilikua naye zamani mwenyewe tuliachana alikua mjinga mjinga sura mbaya walikua wananicheka wenzangu siku hizi nipo Single".

    Me:- wahoo Safi my dear ila Jana bank wamenipigia simu wanakuja kukamata gari yangu nakupigwa mnada kwasababu sijamaliza Deni🥹"

    Dem:- acha ni kuambie ukweli tu, Nina mume na watoto wawili"

    Me:- poa usijali ila niliongea na boss wangu amesema watanilipia ilo Deni na pia wataniamishia China, jijini Bahijing kuna tawi la kampuni yetu, kule nitakuwa General Manager.

    Dem:- jamani my dear, Nikuambie ukweli kutoka moyoni Mume wangu na Watoto wote walifariki miaka minne iliyopita.

    Wanawake mnatupeleka wapi Jameni?!!
    MBONA SIJAELEWA HAPA! .Me🧔:- mambo😊 Dem👰:- poa🤨 Me🧔:- unaishi wapi🙄? Dem 👰:- hapa tu Nairobi 😲 Me🧔:- uko chuo😊? Dem👰:- ndio😟 Me 🧔 :- chuo gani ☺️ Dem 👰:- Urumah University 🥰 Me🧔:- Si NAMI paci unionee uruma na unipe fursa ya life yako. Dem👰:- ohooo!🙆 I am already to deserve you 😍 Me🧔:- poa nimeangalia profile picture zako nimekupenda ghafla...😘" Dem👰:- Ahsante, una gari aina gani😒?! Me🧔:- Nina land cruiser 😊" Dem👰:- wahoo! Upo sahihi kunipenda najisikia raha ku chat na wewe😁". Me🧔:- Ila Gari sio langu nimesaidiwa na rafiki yangu🙄". Dem👰:- Nikuambie kitu!! Mimi nina boyfriend wangu na tunapendana sana💕 Me🧔:- land cruiser hiyo nimesadiwa na rafiki yangu kwasababu Gari yangu Harrier new model ilikuwa service😊" Dem👰:- nakutania tu sina boyfriend, Nilikua naye zamani mwenyewe tuliachana alikua mjinga mjinga sura mbaya walikua wananicheka wenzangu siku hizi nipo Single😁😁". Me🧔:- wahoo Safi my dear ila Jana bank wamenipigia simu wanakuja kukamata gari yangu nakupigwa mnada kwasababu sijamaliza Deni🥹" Dem👰:- acha ni kuambie ukweli tu, Nina mume na watoto wawili✌️" Me🧔:- poa usijali ila niliongea na boss wangu amesema watanilipia ilo Deni na pia wataniamishia China, jijini Bahijing kuna tawi la kampuni yetu, kule nitakuwa General Manager🕴️. Dem👰:- jamani my dear, Nikuambie ukweli kutoka moyoni Mume wangu na Watoto 👪wote walifariki miaka minne iliyopita. 😂😂😂😂😂😂😂😂😂 Wanawake mnatupeleka wapi Jameni?!!
    Love
    1
    · 0 Comments ·0 Shares ·976 Views
  • "Safari ya Tumaini"

    Kulikuwa na kijana anayeitwa Brian, mwenye miaka 24, msomi wa juu wa masuala ya uhandisi wa kompyuta. Brian alikuwa amezaliwa katika kijiji kidogo cha Milimani, eneo ambalo umaskini ulikuwa sehemu ya maisha ya kila siku. Pamoja na changamoto za mazingira, Brian alisimama kwa bidii yake, akifaulu shuleni kwa juhudi zisizopimika.

    Baada ya kuhitimu kutoka chuo kikuu, Brian alipata kazi jijini Nairobi katika kampuni maarufu ya teknolojia. Lakini alihisi pengo moyoni mwake. Hakuridhika kuona kijiji chake kikizidi kuzama katika matatizo ya maji safi, umeme wa kutegemewa, na ukosefu wa ajira. Akaamua kurudi kijijini kwa lengo la kubadilisha maisha ya watu wake.

    Brian alirudi na wazo la kuunda mfumo wa nishati ya jua unaoweza kutumika kwa bei nafuu. Usiku mmoja, akiwa karakana ya baba yake ya zamani, aligundua nishati ya kuhifadhiwa kwa betri za kienyeji kupitia paneli ndogo za jua. Mradi wake ulianza kwa kusambaza taa moja kwa familia masikini. Habari za uvumbuzi wake zilisambaa, na kijiji kilianza kupata matumaini mapya.

    Siku moja, mtu asiyejulikana kutoka kampuni kubwa ya nishati alisikia habari za Brian. Wakamtembelea na kumwomba kuuza uvumbuzi wake kwa malipo makubwa. Lakini Brian alikataa. Hakuwa na nia ya kunufaika peke yake; alitaka kusaidia jamii yake.

    Kampuni hiyo haikufurahia. Walimtishia Brian na hata kujaribu kuiba mipango yake. Brian, akijua kuwa hatari ilikuwa karibu, aliamua kufundisha vijana wa kijiji mbinu alizotumia. Kwa pamoja, walilinda uvumbuzi wao na kuendeleza mradi huo.

    Miezi kadhaa baadaye, mradi wa Brian ulikuwa umewasha umeme katika vijiji saba, na vijana wengi walikuwa wameajiriwa. Hatimaye, kijiji cha Milimani kilibadilika kuwa mfano wa maendeleo vijijini.

    Brian hakujulikana tu kama mhandisi, bali pia kama shujaa wa kweli wa jamii yake. Aliwaonyesha watu kuwa maarifa si kwa ajili ya mafanikio ya mtu binafsi pekee, bali kwa kubadilisha maisha ya wengi. Safari yake ikawa somo la matumaini, mshikamano, na nguvu ya mabadiliko.
    "Safari ya Tumaini" Kulikuwa na kijana anayeitwa Brian, mwenye miaka 24, msomi wa juu wa masuala ya uhandisi wa kompyuta. Brian alikuwa amezaliwa katika kijiji kidogo cha Milimani, eneo ambalo umaskini ulikuwa sehemu ya maisha ya kila siku. Pamoja na changamoto za mazingira, Brian alisimama kwa bidii yake, akifaulu shuleni kwa juhudi zisizopimika. Baada ya kuhitimu kutoka chuo kikuu, Brian alipata kazi jijini Nairobi katika kampuni maarufu ya teknolojia. Lakini alihisi pengo moyoni mwake. Hakuridhika kuona kijiji chake kikizidi kuzama katika matatizo ya maji safi, umeme wa kutegemewa, na ukosefu wa ajira. Akaamua kurudi kijijini kwa lengo la kubadilisha maisha ya watu wake. Brian alirudi na wazo la kuunda mfumo wa nishati ya jua unaoweza kutumika kwa bei nafuu. Usiku mmoja, akiwa karakana ya baba yake ya zamani, aligundua nishati ya kuhifadhiwa kwa betri za kienyeji kupitia paneli ndogo za jua. Mradi wake ulianza kwa kusambaza taa moja kwa familia masikini. Habari za uvumbuzi wake zilisambaa, na kijiji kilianza kupata matumaini mapya. Siku moja, mtu asiyejulikana kutoka kampuni kubwa ya nishati alisikia habari za Brian. Wakamtembelea na kumwomba kuuza uvumbuzi wake kwa malipo makubwa. Lakini Brian alikataa. Hakuwa na nia ya kunufaika peke yake; alitaka kusaidia jamii yake. Kampuni hiyo haikufurahia. Walimtishia Brian na hata kujaribu kuiba mipango yake. Brian, akijua kuwa hatari ilikuwa karibu, aliamua kufundisha vijana wa kijiji mbinu alizotumia. Kwa pamoja, walilinda uvumbuzi wao na kuendeleza mradi huo. Miezi kadhaa baadaye, mradi wa Brian ulikuwa umewasha umeme katika vijiji saba, na vijana wengi walikuwa wameajiriwa. Hatimaye, kijiji cha Milimani kilibadilika kuwa mfano wa maendeleo vijijini. Brian hakujulikana tu kama mhandisi, bali pia kama shujaa wa kweli wa jamii yake. Aliwaonyesha watu kuwa maarifa si kwa ajili ya mafanikio ya mtu binafsi pekee, bali kwa kubadilisha maisha ya wengi. Safari yake ikawa somo la matumaini, mshikamano, na nguvu ya mabadiliko.
    0 Comments ·0 Shares ·846 Views
  • MWALIMU NA MWANAFUNZI.

    Mtoto: Mwalimu mimi nataka nisome darasa la nne kwani hili la3 halinifai.

    Mwalimu: Kwa nini unasema hivyo?

    Mtoto: Nina akili…

    Basi mwalimu akamueleza mkuu wa shule na mkuu kaitisha interview kwa dogo. Maswali ni haya….

    Mwalimu: Kwenye ndege kuna matofali 20 tukitoa moja tukalidondosha chini yatabaki mangapi?

    Dogo: Yatabaki 19.

    Mwalimu: Nipe hatua za kumuweka tembo kwenye friji.

    Dogo: Unafungua friji unamuweka tembo kisha unafunga.

    Mwalimu: Nipe hatua za kumuweka nyani kwenye friji.

    Dogo: Unafungua friji unamtoa tembo ulemuweka..unamueka nyani kisha unafunga friji.

    Mwalimu: Kuna sherehe ya siku ya kuzaliwa kwa simba, wanyama wote wameenda kasoro mmoja. Ni nani na kwa nini?

    Dogo: Ni nyani kwa sababu tumemuweka kwenye friji.

    Mwalimu: Bibi kizee amevuka mto unaokuwaga na mamba na viboko wakali, aliwezaje?

    Dogo: Aliweza kwani mamba na viboko nao walienda kwenye sherehe ya kuzaliwa kwa simba.

    Mwalimu: Ingawa bibi kizee alivuka mto, baadae alikufa. Unadhani ni kwanini alikufa?

    Dogo: Alidondokewa na lile tofali tulotoa kwenye ndege na kutupa chini.

    Mwalimu mkuu: Huyu dogo akasome chuo kikuu….


    NIMEAMUA KUONDOKA NAE ATANIFAHA SANA
    MWALIMU NA MWANAFUNZI. Mtoto: Mwalimu mimi nataka nisome darasa la nne kwani hili la3 halinifai. Mwalimu: Kwa nini unasema hivyo? Mtoto: Nina akili… Basi mwalimu akamueleza mkuu wa shule na mkuu kaitisha interview kwa dogo. Maswali ni haya…. Mwalimu: Kwenye ndege kuna matofali 20 tukitoa moja tukalidondosha chini yatabaki mangapi? Dogo: Yatabaki 19. Mwalimu: Nipe hatua za kumuweka tembo kwenye friji. Dogo: Unafungua friji unamuweka tembo kisha unafunga. Mwalimu: Nipe hatua za kumuweka nyani kwenye friji. Dogo: Unafungua friji unamtoa tembo ulemuweka..unamueka nyani kisha unafunga friji. Mwalimu: Kuna sherehe ya siku ya kuzaliwa kwa simba, wanyama wote wameenda kasoro mmoja. Ni nani na kwa nini? Dogo: Ni nyani kwa sababu tumemuweka kwenye friji. Mwalimu: Bibi kizee amevuka mto unaokuwaga na mamba na viboko wakali, aliwezaje? Dogo: Aliweza kwani mamba na viboko nao walienda kwenye sherehe ya kuzaliwa kwa simba. Mwalimu: Ingawa bibi kizee alivuka mto, baadae alikufa. Unadhani ni kwanini alikufa? Dogo: Alidondokewa na lile tofali tulotoa kwenye ndege na kutupa chini. Mwalimu mkuu: Huyu dogo akasome chuo kikuu…. 😆😆😆😆😆😆😆😆 😁😁😁😂😂😂NIMEAMUA KUONDOKA NAE ATANIFAHA SANA
    Like
    1
    · 0 Comments ·0 Shares ·367 Views
  • Uswahilini sijui usingizi unapata saa ngapi*

    Ukisema ulale sa 5 usiku.. saa 6 unaamshwa na story za sungusungu dirishani.
    Kausingizi kanakuja
    Saa nane unaamshwa na kelele za mwizi huyoo
    Saa kumi-kumi hivi alfajiri tena kausingizi kanakuja..ghafla Saa 12 unaamshwa na muuza bagia vitumbua..

    Ukasema labda saa tanotano asubuhi ujipumzishe baada ya kupata chai, ghafla muuza mboga mchicha chinese spinachi majan ya kunde huyooo!!
    Kwa hasira unaamka unasema utalala saa tisa alasiri..
    Saa 9 tena ...Utasikia machumachuma tunanunua friji mbovu compressor mbovu tunanunua
    .. Huyo kapita.
    Ile usingizi unakujakuja jitu na spika lake " tunasajili laini za chuo bure kwa alama za vidole...

    Kwa hasira unaenda zako kukaa nje upunge upepo, unashangaa madogo na jezi zao..kaka shkamoo kesho tuna mechi tunaomba mchango...
    Uswahilini sijui usingizi unapata saa ngapi🤔* Ukisema ulale sa 5 usiku.. saa 6 unaamshwa na story za sungusungu dirishani. Kausingizi kanakuja Saa nane unaamshwa na kelele za mwizi huyoo Saa kumi-kumi hivi alfajiri tena kausingizi kanakuja..ghafla Saa 12 unaamshwa na muuza bagia vitumbua..😇😇😀 Ukasema labda saa tanotano asubuhi ujipumzishe baada ya kupata chai, ghafla muuza mboga mchicha chinese spinachi majan ya kunde huyooo!!😅 Kwa hasira unaamka unasema utalala saa tisa alasiri.. Saa 9 tena ...Utasikia machumachuma tunanunua friji mbovu compressor mbovu tunanunua😆😆 .. Huyo kapita. Ile usingizi unakujakuja jitu na spika lake " tunasajili laini za chuo bure kwa alama za vidole... Kwa hasira unaenda zako kukaa nje upunge upepo, unashangaa madogo na jezi zao..kaka shkamoo kesho tuna mechi tunaomba mchango😁😁😁...
    Haha
    2
    · 0 Comments ·0 Shares ·487 Views
  • *UKIWA NA HIZI TABIA 9, JIANDAE KUFA MASKINI*......

    _"Umasikini hauji kwa bahati mbaya kama ubaguzi wa rangi au ukoloni, umaskini hutokana na matendo ya kila siku ya mwanadamu" (Nelson Mandela, R.I.P)_

    _"Kila mtu anataka kufanikiwa, lakini si kila mtu yuko tayari kushika majukumu na wajibu wa kumpeleka kwenye mafanikio"(Mwl Nyerere, R.I.P)._

    _"Kile unachokifanya muda huu ndicho kinachoashiria na kutoa picha kamili ya baadae kwako"(Mahatma Gandhi, R.I.P)_

    _"Ukizaliwa maskini sio kosa lako, ila ukifa maskini hilo ni kosa"(Bill Gate, The richest man in the world)._

    Mwalimu wangu wa chuo aliwahi kuniambia kuwa, "mstari unaomtenganisha maskini na tajiri ni mwembamba sana, kwa hiyo ni rahisi sana kuwa tajiri pia ni rahisi sana kuwa maskini". Mpaka leo sijaelewa alimaanisha nini.

    *Watu wote waliofanikiwa katika nyanja mbalimbali za maisha, kwenye uongozi, biashara, kilimo, elimu, siasa, michezo, uandishi, muziki, afya, imani, utangazaji, nk huwa hawana hizi tabia 9 nilizokuandalia leo, kwa hiyo kama una kiu ya mafanikio kwa hicho unachopambania, achana na haya mambo 9 yafuatayo;*

    *1. KUTOKUJARIBU.*
    Katika kutafuta mafanikio huwa kuna vitu viwili tu vya kuchagua. Tambua kuwa maisha ni vita. "Chagua kufa, au kupambana". "Siogopi kufa, naogopa kutokujaribu' (Jay Z). Hakuna alie zaliwa anajua, jiamini, jaribu utafanikiwa.

    *2. KUTOKUJIFUNZA.*
    Che Guava mpaka anafariki library yake ilikuwa na vitabu zaidi ya 2000, mwenzangu na Mimi sijui hata kama una Biblia au Quran ghetoni kwako. Nkwameh Nkrumah library yake ilikuwa na vitabu zaidia ya 3000, Obama anakuambia kila akiamka asbuhi lazima asome kitu kipya. "JOSEPH=Jifunze, Ona, Soma, Elimika, Pitia, Hamasika.(Prof Jay)

    *3. WOGA & WASIWASI.*
    "Tunaweza tukamsamehe mtoto anayeogopa gizani, lakini sio mtu mzima anaeogopa mchana"(Plato, R.I.P). Kitu cha kuogopa katika maisha ni woga wenyewe. Kama hujiamini hutakuja kuwa mshindi katika jambo lolote. Fanya hicho unachofikiria kukifanya kwa moyo wa dhati, kama unaamini ni cha halali na kina manufaa kwako na familia yako, na jamii nzima. Acha tabia ya kuogopa kitu ambacho hakijatokea.

    *4. KUJILINGANISHA.*
    Kuna baadhi ya watu, huwa wangetamani kuwa kama watu Fulani. Kuwa wewe pia jiamini. Usitamani kuwa Magufuli, Kassim Majaliwa au Paul Makonda. Kila mtu ni wa pekee na maalumu. Jikubali kwanza afu wengine ndo watakukubali wewe. Weka nguvu kwenye ubora wako na sio kwenye madhaifu yako. Ukijilinganisha sana utakosa furaha ya nafsi maisha yako yote.

    *5. KUWEKA VINYONGO.*

    "Kuweka chuki na konyongo moyoni ni sawa na kunywa sumu ukidhani atakufa mtu mwingine". Onesha upendo, sambaza upendo, hayo ndo mafanikio ya kweli.

    *6. UONGO*
    "Uongo utakupa ushindi wa siku moja, ukweli utaishi milele" (WEUSI), "Muongo hata akiongoea ukweli usimuamini" (FID Q). Ukiwa muongo huwezi kufanikiwa hata siku moja. "Unaweza ukawadanganya watu, lakini huwezi kuwadanganya watu wote, wakati wote" (Bob Marley). Ukweli kama jua, katika safari ya mafanikio huwezi kuvificha.

    *7. UVIVU & UZEMBE*
    "Nyumba yenye njaa ukisizi unapata zero"(Fid Q). Mafanikio huja kwa kupenda unachokifanya. Neno "kazi" katika biblia limeandikwa mara 600. Dangote analala masaa 3 tu kila siku, Mohammed Dewj anaamka saa 11 asbuhi kila siku. We kwepa majukumu tu, kesho utakula magodoro. "Uvivu unalipa muda huu, bidii & juhudi vinalipa baadae".

    *8. STAREHE & ANASA KUPINDUKIA*
    Pombe, sigara, ngono, unga, bange, shisha, cocaine, nk vitu vibaya sana. Ni ngumu sana kufikia mafanikio makubwa kama una tabia kama hizi. "Sisi ni kile tunacho kula". Mafanikio ya kwanza huanzia kwenye afya yako". Afya ni utajiri. Pia starehe hupoteza muda sana. "Mavuno ya uzee, ni swaga za ujana, kwa ukila ujana kumbuka kula kiungwana"(Nikki Mbishi,).

    *9. LAWAMA & UMBEA*
    "Watu wenye uwezo mkubwa wa kufikiria hujadili kuhusu mawazo, uwezo wa kati hujadili kuhusu matukio na wale wenye uwezo wa chini, hujadili kuhusu watu" We upo kwenye kundi gani? Bora ukawa kundi la kati kuliko hilo la chini kabisa, hilo ni la "wachawi", tupambane, tuache lawama hazisaidii chochote. Ukiweka malengo yako, vizuri na ukaacha hizo tabia hapo juu, muda si mrefu utazifikia ndoto zako.

    Share tafadhali ukipenda
    *UKIWA NA HIZI TABIA 9, JIANDAE KUFA MASKINI*......

    _"Umasikini hauji kwa bahati mbaya kama ubaguzi wa rangi au ukoloni, umaskini hutokana na matendo ya kila siku ya mwanadamu" (Nelson Mandela, R.I.P)_

    _"Kila mtu anataka kufanikiwa, lakini si kila mtu yuko tayari kushika majukumu na wajibu wa kumpeleka kwenye mafanikio"(Mwl Nyerere, R.I.P)._

    _"Kile unachokifanya muda huu ndicho kinachoashiria na kutoa picha kamili ya baadae kwako"(Mahatma Gandhi, R.I.P)_

    _"Ukizaliwa maskini sio kosa lako, ila ukifa maskini hilo ni kosa"(Bill Gate, The richest man in the world)._

    Mwalimu wangu wa chuo aliwahi kuniambia kuwa, "mstari unaomtenganisha maskini na tajiri ni mwembamba sana, kwa hiyo ni rahisi sana kuwa tajiri pia ni rahisi sana kuwa maskini". Mpaka leo sijaelewa alimaanisha nini.

    *Watu wote waliofanikiwa katika nyanja mbalimbali za maisha, kwenye uongozi, biashara, kilimo, elimu, siasa, michezo, uandishi, muziki, afya, imani, utangazaji, nk huwa hawana hizi tabia 9 nilizokuandalia leo, kwa hiyo kama una kiu ya mafanikio kwa hicho unachopambania, achana na haya mambo 9 yafuatayo;*

    *1. KUTOKUJARIBU.*
    Katika kutafuta mafanikio huwa kuna vitu viwili tu vya kuchagua. Tambua kuwa maisha ni vita. "Chagua kufa, au kupambana". "Siogopi kufa, naogopa kutokujaribu' (Jay Z). Hakuna alie zaliwa anajua, jiamini, jaribu utafanikiwa.

    *2. KUTOKUJIFUNZA.*
    Che Guava mpaka anafariki library yake ilikuwa na vitabu zaidi ya 2000, mwenzangu na Mimi sijui hata kama una Biblia au Quran ghetoni kwako. Nkwameh Nkrumah library yake ilikuwa na vitabu zaidia ya 3000, Obama anakuambia kila akiamka asbuhi lazima asome kitu kipya. "JOSEPH=Jifunze, Ona, Soma, Elimika, Pitia, Hamasika.(Prof Jay)

    *3. WOGA & WASIWASI.*
    "Tunaweza tukamsamehe mtoto anayeogopa gizani, lakini sio mtu mzima anaeogopa mchana"(Plato, R.I.P). Kitu cha kuogopa katika maisha ni woga wenyewe. Kama hujiamini hutakuja kuwa mshindi katika jambo lolote. Fanya hicho unachofikiria kukifanya kwa moyo wa dhati, kama unaamini ni cha halali na kina manufaa kwako na familia yako, na jamii nzima. Acha tabia ya kuogopa kitu ambacho hakijatokea.

    *4. KUJILINGANISHA.*
    Kuna baadhi ya watu, huwa wangetamani kuwa kama watu Fulani. Kuwa wewe pia jiamini. Usitamani kuwa Magufuli, Kassim Majaliwa au Paul Makonda. Kila mtu ni wa pekee na maalumu. Jikubali kwanza afu wengine ndo watakukubali wewe. Weka nguvu kwenye ubora wako na sio kwenye madhaifu yako. Ukijilinganisha sana utakosa furaha ya nafsi maisha yako yote.

    *5. KUWEKA VINYONGO.*

    "Kuweka chuki na konyongo moyoni ni sawa na kunywa sumu ukidhani atakufa mtu mwingine". Onesha upendo, sambaza upendo, hayo ndo mafanikio ya kweli.

    *6. UONGO*
    "Uongo utakupa ushindi wa siku moja, ukweli utaishi milele" (WEUSI), "Muongo hata akiongoea ukweli usimuamini" (FID Q). Ukiwa muongo huwezi kufanikiwa hata siku moja. "Unaweza ukawadanganya watu, lakini huwezi kuwadanganya watu wote, wakati wote" (Bob Marley). Ukweli kama jua, katika safari ya mafanikio huwezi kuvificha.

    *7. UVIVU & UZEMBE*
    "Nyumba yenye njaa ukisizi unapata zero"(Fid Q). Mafanikio huja kwa kupenda unachokifanya. Neno "kazi" katika biblia limeandikwa mara 600. Dangote analala masaa 3 tu kila siku, Mohammed Dewj anaamka saa 11 asbuhi kila siku. We kwepa majukumu tu, kesho utakula magodoro. "Uvivu unalipa muda huu, bidii & juhudi vinalipa baadae".

    *8. STAREHE & ANASA KUPINDUKIA*
    Pombe, sigara, ngono, unga, bange, shisha, cocaine, nk vitu vibaya sana. Ni ngumu sana kufikia mafanikio makubwa kama una tabia kama hizi. "Sisi ni kile tunacho kula". Mafanikio ya kwanza huanzia kwenye afya yako". Afya ni utajiri. Pia starehe hupoteza muda sana. "Mavuno ya uzee, ni swaga za ujana, kwa ukila ujana kumbuka kula kiungwana"(Nikki Mbishi,).

    *9. LAWAMA & UMBEA*
    "Watu wenye uwezo mkubwa wa kufikiria hujadili kuhusu mawazo, uwezo wa kati hujadili kuhusu matukio na wale wenye uwezo wa chini, hujadili kuhusu watu" We upo kwenye kundi gani? Bora ukawa kundi la kati kuliko hilo la chini kabisa, hilo ni la "wachawi", tupambane, tuache lawama hazisaidii chochote. Ukiweka malengo yako, vizuri na ukaacha hizo tabia hapo juu, muda si mrefu utazifikia ndoto zako.
    *UKIWA NA HIZI TABIA 9, JIANDAE KUFA MASKINI*...... _"Umasikini hauji kwa bahati mbaya kama ubaguzi wa rangi au ukoloni, umaskini hutokana na matendo ya kila siku ya mwanadamu" (Nelson Mandela, R.I.P)_ _"Kila mtu anataka kufanikiwa, lakini si kila mtu yuko tayari kushika majukumu na wajibu wa kumpeleka kwenye mafanikio"(Mwl Nyerere, R.I.P)._ _"Kile unachokifanya muda huu ndicho kinachoashiria na kutoa picha kamili ya baadae kwako"(Mahatma Gandhi, R.I.P)_ _"Ukizaliwa maskini sio kosa lako, ila ukifa maskini hilo ni kosa"(Bill Gate, The richest man in the world)._ Mwalimu wangu wa chuo aliwahi kuniambia kuwa, "mstari unaomtenganisha maskini na tajiri ni mwembamba sana, kwa hiyo ni rahisi sana kuwa tajiri pia ni rahisi sana kuwa maskini". Mpaka leo sijaelewa alimaanisha nini. *Watu wote waliofanikiwa katika nyanja mbalimbali za maisha, kwenye uongozi, biashara, kilimo, elimu, siasa, michezo, uandishi, muziki, afya, imani, utangazaji, nk huwa hawana hizi tabia 9 nilizokuandalia leo, kwa hiyo kama una kiu ya mafanikio kwa hicho unachopambania, achana na haya mambo 9 yafuatayo;* *1. KUTOKUJARIBU.* Katika kutafuta mafanikio huwa kuna vitu viwili tu vya kuchagua. Tambua kuwa maisha ni vita. "Chagua kufa, au kupambana". "Siogopi kufa, naogopa kutokujaribu' (Jay Z). Hakuna alie zaliwa anajua, jiamini, jaribu utafanikiwa. *2. KUTOKUJIFUNZA.* Che Guava mpaka anafariki library yake ilikuwa na vitabu zaidi ya 2000, mwenzangu na Mimi sijui hata kama una Biblia au Quran ghetoni kwako. Nkwameh Nkrumah library yake ilikuwa na vitabu zaidia ya 3000, Obama anakuambia kila akiamka asbuhi lazima asome kitu kipya. "JOSEPH=Jifunze, Ona, Soma, Elimika, Pitia, Hamasika.(Prof Jay) *3. WOGA & WASIWASI.* "Tunaweza tukamsamehe mtoto anayeogopa gizani, lakini sio mtu mzima anaeogopa mchana"(Plato, R.I.P). Kitu cha kuogopa katika maisha ni woga wenyewe. Kama hujiamini hutakuja kuwa mshindi katika jambo lolote. Fanya hicho unachofikiria kukifanya kwa moyo wa dhati, kama unaamini ni cha halali na kina manufaa kwako na familia yako, na jamii nzima. Acha tabia ya kuogopa kitu ambacho hakijatokea. *4. KUJILINGANISHA.* Kuna baadhi ya watu, huwa wangetamani kuwa kama watu Fulani. Kuwa wewe pia jiamini. Usitamani kuwa Magufuli, Kassim Majaliwa au Paul Makonda. Kila mtu ni wa pekee na maalumu. Jikubali kwanza afu wengine ndo watakukubali wewe. Weka nguvu kwenye ubora wako na sio kwenye madhaifu yako. Ukijilinganisha sana utakosa furaha ya nafsi maisha yako yote. *5. KUWEKA VINYONGO.* "Kuweka chuki na konyongo moyoni ni sawa na kunywa sumu ukidhani atakufa mtu mwingine". Onesha upendo, sambaza upendo, hayo ndo mafanikio ya kweli. *6. UONGO* "Uongo utakupa ushindi wa siku moja, ukweli utaishi milele" (WEUSI), "Muongo hata akiongoea ukweli usimuamini" (FID Q). Ukiwa muongo huwezi kufanikiwa hata siku moja. "Unaweza ukawadanganya watu, lakini huwezi kuwadanganya watu wote, wakati wote" (Bob Marley). Ukweli kama jua, katika safari ya mafanikio huwezi kuvificha. *7. UVIVU & UZEMBE* "Nyumba yenye njaa ukisizi unapata zero"(Fid Q). Mafanikio huja kwa kupenda unachokifanya. Neno "kazi" katika biblia limeandikwa mara 600. Dangote analala masaa 3 tu kila siku, Mohammed Dewj anaamka saa 11 asbuhi kila siku. We kwepa majukumu tu, kesho utakula magodoro. "Uvivu unalipa muda huu, bidii & juhudi vinalipa baadae". *8. STAREHE & ANASA KUPINDUKIA* Pombe, sigara, ngono, unga, bange, shisha, cocaine, nk vitu vibaya sana. Ni ngumu sana kufikia mafanikio makubwa kama una tabia kama hizi. "Sisi ni kile tunacho kula". Mafanikio ya kwanza huanzia kwenye afya yako". Afya ni utajiri. Pia starehe hupoteza muda sana. "Mavuno ya uzee, ni swaga za ujana, kwa ukila ujana kumbuka kula kiungwana"(Nikki Mbishi,). *9. LAWAMA & UMBEA* "Watu wenye uwezo mkubwa wa kufikiria hujadili kuhusu mawazo, uwezo wa kati hujadili kuhusu matukio na wale wenye uwezo wa chini, hujadili kuhusu watu" We upo kwenye kundi gani? Bora ukawa kundi la kati kuliko hilo la chini kabisa, hilo ni la "wachawi", tupambane, tuache lawama hazisaidii chochote. Ukiweka malengo yako, vizuri na ukaacha hizo tabia hapo juu, muda si mrefu utazifikia ndoto zako. Share tafadhali ukipenda *UKIWA NA HIZI TABIA 9, JIANDAE KUFA MASKINI*...... _"Umasikini hauji kwa bahati mbaya kama ubaguzi wa rangi au ukoloni, umaskini hutokana na matendo ya kila siku ya mwanadamu" (Nelson Mandela, R.I.P)_ _"Kila mtu anataka kufanikiwa, lakini si kila mtu yuko tayari kushika majukumu na wajibu wa kumpeleka kwenye mafanikio"(Mwl Nyerere, R.I.P)._ _"Kile unachokifanya muda huu ndicho kinachoashiria na kutoa picha kamili ya baadae kwako"(Mahatma Gandhi, R.I.P)_ _"Ukizaliwa maskini sio kosa lako, ila ukifa maskini hilo ni kosa"(Bill Gate, The richest man in the world)._ Mwalimu wangu wa chuo aliwahi kuniambia kuwa, "mstari unaomtenganisha maskini na tajiri ni mwembamba sana, kwa hiyo ni rahisi sana kuwa tajiri pia ni rahisi sana kuwa maskini". Mpaka leo sijaelewa alimaanisha nini. *Watu wote waliofanikiwa katika nyanja mbalimbali za maisha, kwenye uongozi, biashara, kilimo, elimu, siasa, michezo, uandishi, muziki, afya, imani, utangazaji, nk huwa hawana hizi tabia 9 nilizokuandalia leo, kwa hiyo kama una kiu ya mafanikio kwa hicho unachopambania, achana na haya mambo 9 yafuatayo;* *1. KUTOKUJARIBU.* Katika kutafuta mafanikio huwa kuna vitu viwili tu vya kuchagua. Tambua kuwa maisha ni vita. "Chagua kufa, au kupambana". "Siogopi kufa, naogopa kutokujaribu' (Jay Z). Hakuna alie zaliwa anajua, jiamini, jaribu utafanikiwa. *2. KUTOKUJIFUNZA.* Che Guava mpaka anafariki library yake ilikuwa na vitabu zaidi ya 2000, mwenzangu na Mimi sijui hata kama una Biblia au Quran ghetoni kwako. Nkwameh Nkrumah library yake ilikuwa na vitabu zaidia ya 3000, Obama anakuambia kila akiamka asbuhi lazima asome kitu kipya. "JOSEPH=Jifunze, Ona, Soma, Elimika, Pitia, Hamasika.(Prof Jay) *3. WOGA & WASIWASI.* "Tunaweza tukamsamehe mtoto anayeogopa gizani, lakini sio mtu mzima anaeogopa mchana"(Plato, R.I.P). Kitu cha kuogopa katika maisha ni woga wenyewe. Kama hujiamini hutakuja kuwa mshindi katika jambo lolote. Fanya hicho unachofikiria kukifanya kwa moyo wa dhati, kama unaamini ni cha halali na kina manufaa kwako na familia yako, na jamii nzima. Acha tabia ya kuogopa kitu ambacho hakijatokea. *4. KUJILINGANISHA.* Kuna baadhi ya watu, huwa wangetamani kuwa kama watu Fulani. Kuwa wewe pia jiamini. Usitamani kuwa Magufuli, Kassim Majaliwa au Paul Makonda. Kila mtu ni wa pekee na maalumu. Jikubali kwanza afu wengine ndo watakukubali wewe. Weka nguvu kwenye ubora wako na sio kwenye madhaifu yako. Ukijilinganisha sana utakosa furaha ya nafsi maisha yako yote. *5. KUWEKA VINYONGO.* "Kuweka chuki na konyongo moyoni ni sawa na kunywa sumu ukidhani atakufa mtu mwingine". Onesha upendo, sambaza upendo, hayo ndo mafanikio ya kweli. *6. UONGO* "Uongo utakupa ushindi wa siku moja, ukweli utaishi milele" (WEUSI), "Muongo hata akiongoea ukweli usimuamini" (FID Q). Ukiwa muongo huwezi kufanikiwa hata siku moja. "Unaweza ukawadanganya watu, lakini huwezi kuwadanganya watu wote, wakati wote" (Bob Marley). Ukweli kama jua, katika safari ya mafanikio huwezi kuvificha. *7. UVIVU & UZEMBE* "Nyumba yenye njaa ukisizi unapata zero"(Fid Q). Mafanikio huja kwa kupenda unachokifanya. Neno "kazi" katika biblia limeandikwa mara 600. Dangote analala masaa 3 tu kila siku, Mohammed Dewj anaamka saa 11 asbuhi kila siku. We kwepa majukumu tu, kesho utakula magodoro. "Uvivu unalipa muda huu, bidii & juhudi vinalipa baadae". *8. STAREHE & ANASA KUPINDUKIA* Pombe, sigara, ngono, unga, bange, shisha, cocaine, nk vitu vibaya sana. Ni ngumu sana kufikia mafanikio makubwa kama una tabia kama hizi. "Sisi ni kile tunacho kula". Mafanikio ya kwanza huanzia kwenye afya yako". Afya ni utajiri. Pia starehe hupoteza muda sana. "Mavuno ya uzee, ni swaga za ujana, kwa ukila ujana kumbuka kula kiungwana"(Nikki Mbishi,). *9. LAWAMA & UMBEA* "Watu wenye uwezo mkubwa wa kufikiria hujadili kuhusu mawazo, uwezo wa kati hujadili kuhusu matukio na wale wenye uwezo wa chini, hujadili kuhusu watu" We upo kwenye kundi gani? Bora ukawa kundi la kati kuliko hilo la chini kabisa, hilo ni la "wachawi", tupambane, tuache lawama hazisaidii chochote. Ukiweka malengo yako, vizuri na ukaacha hizo tabia hapo juu, muda si mrefu utazifikia ndoto zako.
    0 Comments ·0 Shares ·860 Views
  • HALI HALISI YA MAISHA HUKO MTAANI .

    Baada ya kumaliza shule
    Wale wote uliosoma nao wanaenda maeneo mbalimbali duniani.

    Wengine wamemaliza chuo na sasa ni Madaktari, Wahandisi, Waalimu, Wanasheria, Wahasibu nk.

    Wengine wameoa/kuolewa. Wengine wana watoto. Wengine ndo bado wanatafuta ajira. Wengine wamekufa, usisahau hilo pia. Wengine ni wagonjwa vitandani, wengine wameendelea na elimu ya juu zaidi nk. Wengine wanamiliki kampuni, wengine ni mabosi na wanamiliki hisa katika makampuni makubwa duniani.

    Ila vipi wewe UNAJISIKIAJE unapokutana na wale uliosoma nao, ambao inaonekana wamefanikiwa katika NDOTO zao, wakati wewe bado unasuasua hata hujafanya chochote na hata kimshahara ulicho nacho hakikusogezi popote isipokuwa kula na kubadili nguo pamoja na kodi ya nyumba tu?

    Ni mawazo mengi huja akilini, Je huwa unawaonea wivu? Na huo wivu wako ni wa aina gani? Je ni wa kuwachukia au ule wivu wa wewe kupambana ufikie mafanikio kama wao?
    Kwanza watu wa namna hii huwa wanafikiria Mungu hawapendi kabisa.

    Usisahau pia kuna wale waliofariki... Bado unafikiria vilevile na unawaonea wivu?

    MY TAKE

    Usiruhusu nafasi ya KUKATA TAMAA. Sisi ni tofauti na njia zetu za kufanikiwa ni tofauti.

    Wengine wanafanikiwa haraka kabla yako na wengine baada yako na wewe unakuja kufanikiwa baada yao ndivyo ilivyo katika maisha. Ila katika hali yoyote unayojikuta upo sasa, tafadhali endelea kuvunja vizuizi na songa mbele huenda njia uliyo nayo ndiyo itakayo kutoa kamwe usijaribu kuishi maisha wanayoishi wengine kumbuka maisha ni vile unavyoamua kuishi wewe na si mwingine anavoishi.

    Unapoona wengine wanafanikiwa basi jitume na wewe uweze kufanikiwa, kubwa ni kuongeza juhudi katika kazi zako.

    Rafiki yako akinunua gari leo, furahi, kumbuka wakati utakaponunua la kwako litakuwa jipya zaidi kuliko la kwake na utatamba kwa wakati huo kiasi cha wao kukuonea wivu pia.
    Hakuna washindi wa kudumu katika maisha, ila kuna washindi kwa muda.

    Maisha siyo mashindano, usishindane na yoyote, kumbuka, kuwa maisha ni kama kitabu kwamba tunasoma kitabu kimoja lakini kurasa tofauti katika muda tofauti na kila mtu anafanikiwa kwa nafasi na wakati wake, inategemea unaanda mazingira yapi ya kufanikiwa...

    Usiruhusu woga ndani yako kuuwa ndoto ndani yako, baki ukichochea matamanio yako pia jaribu kuthubutu kufanya usiwe mtu wa kuogopa hasara katika jambo la mafanikio kwani bila changamoto huwezi kutoboa.

    Ni nini unatamani Leo...!?
    Andika kwa sababu siku moja dunia itatamani kukusoma, na itakuwa ni sehemu ya historia yako ya mafanikio.

    Hakuna mahali usipoweza kufika isipokuwa juani tu, jiamini, fanyia kazi malengo yako, tambua changamoto na zisikukatize tamaa. Usiumie kwa kuona wenzako wanafanikiwa, kumbuka anga ni pana sana na kila ndege anaweza kupaa bila kumgusa mwenzake.

    Thamini kila jambo dogo ambalo linakujia katika maisha. Chini ya dunia kila kitu kinawezekana ukiamua epuka kupoteza muda mwingi kuumizwa na vitu visivyo na msingi katika maisha yako na pindi litokeapo jambo ambalo unaona litakurudisha nyuma basi weka pembeni jambo hilo kisha elekeza akili katika njia ya kutafuta mafanikio ipo siku utafanikiwa na mambo yote yataenda sawa.

    Nahitimisha kwa kusema "Katika harakati za mafanikio kuna vitu vingi sana ambavyo huwa tunatamani viende kwa pamoja lakini kwa bahati mbaya kuna vingine huangukia njiani hivyo basi vyote ambavyo vinaonekana kukukwamisha fanya kuviweka kando kwa muda kisha chukua hata moja katika vingi hivyo lipeleke hadi mwisho kisha anza kuyarudia haya mengine baada ya mafanikio.
    HALI HALISI YA MAISHA HUKO MTAANI . Baada ya kumaliza shule Wale wote uliosoma nao wanaenda maeneo mbalimbali duniani. Wengine wamemaliza chuo na sasa ni Madaktari, Wahandisi, Waalimu, Wanasheria, Wahasibu nk. Wengine wameoa/kuolewa. Wengine wana watoto. Wengine ndo bado wanatafuta ajira. Wengine wamekufa, usisahau hilo pia. Wengine ni wagonjwa vitandani, wengine wameendelea na elimu ya juu zaidi nk. Wengine wanamiliki kampuni, wengine ni mabosi na wanamiliki hisa katika makampuni makubwa duniani. Ila vipi wewe UNAJISIKIAJE unapokutana na wale uliosoma nao, ambao inaonekana wamefanikiwa katika NDOTO zao, wakati wewe bado unasuasua hata hujafanya chochote na hata kimshahara ulicho nacho hakikusogezi popote isipokuwa kula na kubadili nguo pamoja na kodi ya nyumba tu? Ni mawazo mengi huja akilini, Je huwa unawaonea wivu? Na huo wivu wako ni wa aina gani? Je ni wa kuwachukia au ule wivu wa wewe kupambana ufikie mafanikio kama wao? Kwanza watu wa namna hii huwa wanafikiria Mungu hawapendi kabisa. Usisahau pia kuna wale waliofariki... Bado unafikiria vilevile na unawaonea wivu? MY TAKE Usiruhusu nafasi ya KUKATA TAMAA. Sisi ni tofauti na njia zetu za kufanikiwa ni tofauti. Wengine wanafanikiwa haraka kabla yako na wengine baada yako na wewe unakuja kufanikiwa baada yao ndivyo ilivyo katika maisha. Ila katika hali yoyote unayojikuta upo sasa, tafadhali endelea kuvunja vizuizi na songa mbele huenda njia uliyo nayo ndiyo itakayo kutoa kamwe usijaribu kuishi maisha wanayoishi wengine kumbuka maisha ni vile unavyoamua kuishi wewe na si mwingine anavoishi. Unapoona wengine wanafanikiwa basi jitume na wewe uweze kufanikiwa, kubwa ni kuongeza juhudi katika kazi zako. Rafiki yako akinunua gari leo, furahi, kumbuka wakati utakaponunua la kwako litakuwa jipya zaidi kuliko la kwake na utatamba kwa wakati huo kiasi cha wao kukuonea wivu pia. Hakuna washindi wa kudumu katika maisha, ila kuna washindi kwa muda. Maisha siyo mashindano, usishindane na yoyote, kumbuka, kuwa maisha ni kama kitabu kwamba tunasoma kitabu kimoja lakini kurasa tofauti katika muda tofauti na kila mtu anafanikiwa kwa nafasi na wakati wake, inategemea unaanda mazingira yapi ya kufanikiwa... Usiruhusu woga ndani yako kuuwa ndoto ndani yako, baki ukichochea matamanio yako pia jaribu kuthubutu kufanya usiwe mtu wa kuogopa hasara katika jambo la mafanikio kwani bila changamoto huwezi kutoboa. Ni nini unatamani Leo...!? Andika kwa sababu siku moja dunia itatamani kukusoma, na itakuwa ni sehemu ya historia yako ya mafanikio. Hakuna mahali usipoweza kufika isipokuwa juani tu, jiamini, fanyia kazi malengo yako, tambua changamoto na zisikukatize tamaa. Usiumie kwa kuona wenzako wanafanikiwa, kumbuka anga ni pana sana na kila ndege anaweza kupaa bila kumgusa mwenzake. Thamini kila jambo dogo ambalo linakujia katika maisha. Chini ya dunia kila kitu kinawezekana ukiamua epuka kupoteza muda mwingi kuumizwa na vitu visivyo na msingi katika maisha yako na pindi litokeapo jambo ambalo unaona litakurudisha nyuma basi weka pembeni jambo hilo kisha elekeza akili katika njia ya kutafuta mafanikio ipo siku utafanikiwa na mambo yote yataenda sawa. Nahitimisha kwa kusema "Katika harakati za mafanikio kuna vitu vingi sana ambavyo huwa tunatamani viende kwa pamoja lakini kwa bahati mbaya kuna vingine huangukia njiani hivyo basi vyote ambavyo vinaonekana kukukwamisha fanya kuviweka kando kwa muda kisha chukua hata moja katika vingi hivyo lipeleke hadi mwisho kisha anza kuyarudia haya mengine baada ya mafanikio.
    0 Comments ·0 Shares ·849 Views
  • KWA WANANDOA NA WALE WANAOTARAJIA KUINGIA KATIKA NDOA.

    Mbebe mke wako pale anaposinzia akiwa sebuleni na mpeleke kulala, muda mwingine mfanye ajisikie kama mtoto mdogo.

    Ukweli ni kwamba kila mwanamke anapenda kudekezwa kama mtoto wa miaka miwili. Ndio maana muda mwingine wanawake hufanya mambo ya kitoto.

    Inawezekana ukawa na mabishano na mkeo na ukaona anafungasha mabegi yake na anataka kuondoka.

    Hiyo haimaanishi anataka kukuacha, ni utoto tu, anachotaka ni wewe umshike mkono, umvutie kwako, umtizame usoni kwake na umwambie 'Samahani kwa mabishano na kukukashifu, haitajirudia tena"

    Huyo ndiye mwanamke wako, ubavu wako, Eva wako. Kila Brother anahitaji kusoma chuo cha wanawake kabla hajaoa, soma vitabu kuhusu wao, soma vitabu vya dini vinasemaje juu ya kuishi nao na kamwe hautakuwa na tatizo la kuishi nae.

    Ingawa kunaweza kuwa na changamoto za hapa na pale, hiyo ni kwa sababu wote mmetoka katika familia tofauti, zenye malezi ya tofauti na historia tofauti.

    Hivyo basi soma vitabu kuhusu ndoa, pitia mafundisho mbalimbali ya walimu wa mahusiano kama Dr. Chris Mauki, Dr. Naahj Naahjum, Hezron, tizama mafunzo ya Dr. Myles Munroe katika Youtube, Ongeza maarifa kuhusu malezi ya watoto na umuhimu wa Ndoa na mengineyo.

    Usikimbilie tu ndoa kisa Washikaji zako wote wameshaoa au umechoka kula msosi wa hotelini, na huku kichwani bado kweupe kuhusiana na ndoa, utajiletea matatizo.

    Ni wanaume wangapi wanaeza vumilia wake zao wanaoongea sana na kushout kwa kila jambo? Kama vile ilivyo shida kwa mwenye miguu ya mzee kupanda mlima uliojaa
    mchanga, ndivyo ilivyo kwa mume mpole kuishi na mke mwenye makelele.

    Unaambiwa uwe mkimya pale mmoja wenu anapokuwa na hasira na kuongea sana, Mmoja wenu anapokuwa moto basi mwingine awe maji. Hapo mambo yataenda sawia.

    Kaka zangu, ukiwa kama mwanaume jifunze kupotezea baadhi ya vitu, sio kila jambo unakua mkali kama pilipili mpaka watoto wanaenda kujificha chini ya uvungu wa vitanda.

    Cheza michezo ya kitoto na mkeo, imba nae siku za weekend huku ukimsaidia kufua au kutengeneza bustani, kuwa serious sana kunamuogopesha mkeo na hawezi kuwa rafiki yako wa karibu.

    Msaidie kazi za nyumbani, yeye si mfanyakazi wako wa ndani bali ni msaidizi, ulikuwa bachelor na kazi zote ulifanya mwenyewe sasa amekuja mke kukusaidia na sio kubadili kuwa kazi zake, menya viazi, teka maji, Oga nae, muamshe kwa ajili ya sala, mfindishe kupika chakula ambacho hajawahi kupika.

    Mpigie simu ukiwa kazini mwambie umemkumbuka na unampenda sana. Andika neno "I Love you" na uweke chini ya mto wake au pochi yake kabla hujaenda kazin.

    Mbusu siku zote, mkumbatie, mbembeleze. Siku zote mueleze kwamba yeye ni mzuri na una bahati ya kuwa mume wake.

    Yote haya ni sehemu ya kuwa romantic, pale mke anaposema kwamba hauko romantic, anamaanisha humfanyii haya mambo, hamaanishi romance mkiwa chumbani.

    Ni vitu fulani vidogo sana na vya kipuuzi ila kwa mwanamke vina maana kubwa sana, niamini mimi.

    Tamati nawashauri kaka zangu, gawanya usiku wako katika sehemu tatu.
    Moja ni kwa ajili yako (kuwaza mipango yako ya maendeleo na kulala).
    Mbili ni kwa ajili ya mke wako (ongea nae, kama uwezekano upo make love with her) na Tatu ni kwa ajili ya Mungu wako (Mshukuru kwa kukulinda siku nzima na kukufanikishia mipango yako)

    Nakuahidi huo utakuwa usiku bora kabisa ambao hujawahi kuupata!

    Mambo mawili ya kuzingatia na mtakua mmemaliza, wanawake watiini wanaume zenu, na wanaume wapendeni wake zenu. utii ni bora kuliko sadaka!

    Busara yangu, "A happy man, marry the woman he loves, but the happiest man keep loving the woman he marry!"
    KWA WANANDOA NA WALE WANAOTARAJIA KUINGIA KATIKA NDOA. Mbebe mke wako pale anaposinzia akiwa sebuleni na mpeleke kulala, muda mwingine mfanye ajisikie kama mtoto mdogo. Ukweli ni kwamba kila mwanamke anapenda kudekezwa kama mtoto wa miaka miwili. Ndio maana muda mwingine wanawake hufanya mambo ya kitoto. Inawezekana ukawa na mabishano na mkeo na ukaona anafungasha mabegi yake na anataka kuondoka. Hiyo haimaanishi anataka kukuacha, ni utoto tu, anachotaka ni wewe umshike mkono, umvutie kwako, umtizame usoni kwake na umwambie 'Samahani kwa mabishano na kukukashifu, haitajirudia tena" Huyo ndiye mwanamke wako, ubavu wako, Eva wako. Kila Brother anahitaji kusoma chuo cha wanawake kabla hajaoa, soma vitabu kuhusu wao, soma vitabu vya dini vinasemaje juu ya kuishi nao na kamwe hautakuwa na tatizo la kuishi nae. Ingawa kunaweza kuwa na changamoto za hapa na pale, hiyo ni kwa sababu wote mmetoka katika familia tofauti, zenye malezi ya tofauti na historia tofauti. Hivyo basi soma vitabu kuhusu ndoa, pitia mafundisho mbalimbali ya walimu wa mahusiano kama Dr. Chris Mauki, Dr. Naahj Naahjum, Hezron, tizama mafunzo ya Dr. Myles Munroe katika Youtube, Ongeza maarifa kuhusu malezi ya watoto na umuhimu wa Ndoa na mengineyo. Usikimbilie tu ndoa kisa Washikaji zako wote wameshaoa au umechoka kula msosi wa hotelini, na huku kichwani bado kweupe kuhusiana na ndoa, utajiletea matatizo. Ni wanaume wangapi wanaeza vumilia wake zao wanaoongea sana na kushout kwa kila jambo? Kama vile ilivyo shida kwa mwenye miguu ya mzee kupanda mlima uliojaa mchanga, ndivyo ilivyo kwa mume mpole kuishi na mke mwenye makelele. Unaambiwa uwe mkimya pale mmoja wenu anapokuwa na hasira na kuongea sana, Mmoja wenu anapokuwa moto basi mwingine awe maji. Hapo mambo yataenda sawia. Kaka zangu, ukiwa kama mwanaume jifunze kupotezea baadhi ya vitu, sio kila jambo unakua mkali kama pilipili mpaka watoto wanaenda kujificha chini ya uvungu wa vitanda. Cheza michezo ya kitoto na mkeo, imba nae siku za weekend huku ukimsaidia kufua au kutengeneza bustani, kuwa serious sana kunamuogopesha mkeo na hawezi kuwa rafiki yako wa karibu. Msaidie kazi za nyumbani, yeye si mfanyakazi wako wa ndani bali ni msaidizi, ulikuwa bachelor na kazi zote ulifanya mwenyewe sasa amekuja mke kukusaidia na sio kubadili kuwa kazi zake, menya viazi, teka maji, Oga nae, muamshe kwa ajili ya sala, mfindishe kupika chakula ambacho hajawahi kupika. Mpigie simu ukiwa kazini mwambie umemkumbuka na unampenda sana. Andika neno "I Love you" na uweke chini ya mto wake au pochi yake kabla hujaenda kazin. Mbusu siku zote, mkumbatie, mbembeleze. Siku zote mueleze kwamba yeye ni mzuri na una bahati ya kuwa mume wake. Yote haya ni sehemu ya kuwa romantic, pale mke anaposema kwamba hauko romantic, anamaanisha humfanyii haya mambo, hamaanishi romance mkiwa chumbani. Ni vitu fulani vidogo sana na vya kipuuzi ila kwa mwanamke vina maana kubwa sana, niamini mimi. Tamati nawashauri kaka zangu, gawanya usiku wako katika sehemu tatu. Moja ni kwa ajili yako (kuwaza mipango yako ya maendeleo na kulala). Mbili ni kwa ajili ya mke wako (ongea nae, kama uwezekano upo make love with her) na Tatu ni kwa ajili ya Mungu wako (Mshukuru kwa kukulinda siku nzima na kukufanikishia mipango yako) Nakuahidi huo utakuwa usiku bora kabisa ambao hujawahi kuupata! Mambo mawili ya kuzingatia na mtakua mmemaliza, wanawake watiini wanaume zenu, na wanaume wapendeni wake zenu. utii ni bora kuliko sadaka! Busara yangu, "A happy man, marry the woman he loves, but the happiest man keep loving the woman he marry!"
    0 Comments ·0 Shares ·795 Views
  • "Rodri alitoa hotuba ya kushangaza. Alizungumza kuhusu familia, Man City na soka ya Uhispania. Nadhani soka la Uhispania katika muongo mmoja uliopita lilifanya jambo la kushangaza, na wakufunzi tofauti wa kitaifa, na wachezaji wa ajabu hapo zamani, na kushinda Kombe la Dunia, Kombe la Euro, na kamwe, kamwe hawakuweza kushinda tuzo hii.

    "Na nadhani Rodri anawakilisha vyema, bila shaka City kwa sababu tunajivunia, lakini soka la Uhispania - ushawishi wao katika soka la dunia katika miaka 10, 15 iliyopita, umekuwa muhimu sana. Sio tu kushinda mataji, jinsi wanavyocheza, vizazi vya wasimamizi, vizazi vya wachezaji na nadhani labda wakati huo nakumbuka wachezaji watatu kutoka Chuo cha Barcelona, ​​La Masia, waliteuliwa, wote watatu, kushinda Ballon d'Or, na Xavi na Iniesta hawakuweza kushinda kwa sababu. kulikuwa na monster huko.

    "Na Messi, hakuna mtu angeweza kumshinda. Cristiano tu. Cristiano alikuwa mnyama mkubwa, na baba wa mnyama huyo ni Messi. Na wote wawili wamefanya kitu cha ajabu katika miaka 15 au 20 iliyopita. Na labda katika wakati huo, Xavi na Iniesta walistahili. Ballon d'Or pia, kwa hivyo nadhani Rodri, jana, alipata kile ambacho soka la Uhispania lilistahili duniani kote." - Pep Guadiola, Kocha Mkuu wa klabu ya Manchester City akizungumza kuhusu Rodri.
    "Rodri alitoa hotuba ya kushangaza. Alizungumza kuhusu familia, Man City na soka ya Uhispania. Nadhani soka la Uhispania katika muongo mmoja uliopita lilifanya jambo la kushangaza, na wakufunzi tofauti wa kitaifa, na wachezaji wa ajabu hapo zamani, na kushinda Kombe la Dunia, Kombe la Euro, na kamwe, kamwe hawakuweza kushinda tuzo hii. "Na nadhani Rodri anawakilisha vyema, bila shaka City kwa sababu tunajivunia, lakini soka la Uhispania - ushawishi wao katika soka la dunia katika miaka 10, 15 iliyopita, umekuwa muhimu sana. Sio tu kushinda mataji, jinsi wanavyocheza, vizazi vya wasimamizi, vizazi vya wachezaji na nadhani labda wakati huo nakumbuka wachezaji watatu kutoka Chuo cha Barcelona, ​​La Masia, waliteuliwa, wote watatu, kushinda Ballon d'Or, na Xavi na Iniesta hawakuweza kushinda kwa sababu. kulikuwa na monster huko. "Na Messi, hakuna mtu angeweza kumshinda. Cristiano tu. Cristiano alikuwa mnyama mkubwa, na baba wa mnyama huyo ni Messi. Na wote wawili wamefanya kitu cha ajabu katika miaka 15 au 20 iliyopita. Na labda katika wakati huo, Xavi na Iniesta walistahili. Ballon d'Or pia, kwa hivyo nadhani Rodri, jana, alipata kile ambacho soka la Uhispania lilistahili duniani kote." - Pep Guadiola, Kocha Mkuu wa klabu ya Manchester City akizungumza kuhusu Rodri.
    Love
    1
    · 1 Comments ·0 Shares ·527 Views
  • Influencer

    Tsh50000 - Tsh50001 / Month
    Location
    All University of Tanzania
    Type
    Contract
    Status
    Open
    Wanahitajika Mwawakala wa Socialpop Vyuoni kote nchini.

    Soma Vizuri:
    Mtandao wa Socialpop Unahitaji Influencer kwa ajiri ya kuutangaza na kuwaingiza watumiaji wapya wa Vyouni kote Tanzania.

    Vigezo:
    Uwe unaujua vyema mtandao wa SocialPop.
    Uwe unasoma chuo kinachotambulika na uwe na Cheti au kitambulisho cha Chuo.
    Uwe na Uhakika wa Kupata watumiaji mpya walau 20 kwa Siku.
    Maelezo menfine wasiliana nasi kwa ajiri ya Kusaini Mkataba.
    Wanahitajika Mwawakala wa Socialpop Vyuoni kote nchini. Soma Vizuri: Mtandao wa Socialpop Unahitaji Influencer kwa ajiri ya kuutangaza na kuwaingiza watumiaji wapya wa Vyouni kote Tanzania. Vigezo: Uwe unaujua vyema mtandao wa SocialPop. Uwe unasoma chuo kinachotambulika na uwe na Cheti au kitambulisho cha Chuo. Uwe na Uhakika wa Kupata watumiaji mpya walau 20 kwa Siku. Maelezo menfine wasiliana nasi kwa ajiri ya Kusaini Mkataba.
    Like
    Love
    9
    · 3 Comments ·0 Shares ·1K Views
  • KAMA NI HIVI CHUO WATU WATAPUNGUA
    KAMA NI HIVI CHUO WATU WATAPUNGUA
    Like
    Love
    3
    · 1 Comments ·0 Shares ·289 Views
More Results