• "Msimu uliyopita Zamalek aligomea mechi dhidi ya Al Ahly, Mamlaka za soka nchini Misri zikampa ushindi Al Ahly wa mabao mawili na alama zake tatu kisha wakailima Zamalek alama tatu na timu ikashuka mpaka nafasi ya 12 kama sikosei, Bodi na Chama wala hakikuwaza mara mbili, ni kesi kubwa sana kwenye dunia ya soka kukacha mechi.

    Jana, Al Ahly nae kaleta mbwembwe zile zile za masuala ya Kanuni akagomea mchezo, akasahau kanuni ya kutokea Uwanjani na kucheza mechi ndio kanuni yenye maana zaidi kwenye soka, amejikuta anapoteza alama tatu na mabao matatu kwa Zamalek, Kanuni hii inaweza kusema hivi ila Kanuni nyingine ikawa na maelezo mengine.

    Nikukumbushe tu Al Ahly aliyeadhibiwa ndio Klabu Tajiri zaidi Afrika, Klabu yenye Mashabiki na Wanachama wengi zaidi Afrika, ndio Klabu ya pili kwa Mataji mengi duniani baada ya Real Madrid, ila huko Misri watu hawatazami makunyanzi, ukileta maksudi, Bodi na Chama cha soka zinakufanyia bahati mbaya, Ahly inatajwa pia ina nguvu kubwa sana CAF, sio ya kufikirika ama nadharia ndio uhalisia ila wamepita nayo mapema tu.

    Nawakumbusha tena Watu wangu HAKI huenda na WAJIBU, mfano Tanzania kwa mujibu wa Katiba kuandamana ni haki yako ila unapaswa kutoa taarifa kwa Polisi masaa 72 kabla, umeelewa hapo? Ni haki yako ila huja na Wajibu, Kanuni ili ikulinde hakikisha umetekeleza Wajibu, biashara za Mamlaka za soka duniani ni mpira, kutocheza mpira ni kuzitusi, hazikuachi salama.

    Ni haki yako kuja kufanya mazoezi uwanja wa mechi siku moja kabla ila ni Wajibu wako kunijulisha kuwa nakuja, ili nikuandalie mazingira, huenda narekebisha mfumo wa Umeme? Huenda hali ya usalama sio shwari, huenda nimepulizia dawa za dudu zinaweka kukuathiri, yaani ni HAKI yako ila una WAJIBU wako huu ni mfano tu.

    Mnasemaje Watu wangu wa nchini Yemen haya hayawahusu sana, huko kwenu Kivyenu vyenu Wayemen" - Farhan JR, Mchambuzi.

    "Msimu uliyopita Zamalek aligomea mechi dhidi ya Al Ahly, Mamlaka za soka nchini Misri zikampa ushindi Al Ahly wa mabao mawili na alama zake tatu kisha wakailima Zamalek alama tatu na timu ikashuka mpaka nafasi ya 12 kama sikosei, Bodi na Chama wala hakikuwaza mara mbili, ni kesi kubwa sana kwenye dunia ya soka kukacha mechi. Jana, Al Ahly nae kaleta mbwembwe zile zile za masuala ya Kanuni akagomea mchezo, akasahau kanuni ya kutokea Uwanjani na kucheza mechi ndio kanuni yenye maana zaidi kwenye soka, amejikuta anapoteza alama tatu na mabao matatu kwa Zamalek, Kanuni hii inaweza kusema hivi ila Kanuni nyingine ikawa na maelezo mengine. Nikukumbushe tu Al Ahly aliyeadhibiwa ndio Klabu Tajiri zaidi Afrika, Klabu yenye Mashabiki na Wanachama wengi zaidi Afrika, ndio Klabu ya pili kwa Mataji mengi duniani baada ya Real Madrid, ila huko Misri watu hawatazami makunyanzi, ukileta maksudi, Bodi na Chama cha soka zinakufanyia bahati mbaya, Ahly inatajwa pia ina nguvu kubwa sana CAF, sio ya kufikirika ama nadharia ndio uhalisia ila wamepita nayo mapema tu. Nawakumbusha tena Watu wangu HAKI huenda na WAJIBU, mfano Tanzania kwa mujibu wa Katiba kuandamana ni haki yako ila unapaswa kutoa taarifa kwa Polisi masaa 72 kabla, umeelewa hapo? Ni haki yako ila huja na Wajibu, Kanuni ili ikulinde hakikisha umetekeleza Wajibu, biashara za Mamlaka za soka duniani ni mpira, kutocheza mpira ni kuzitusi, hazikuachi salama. Ni haki yako kuja kufanya mazoezi uwanja wa mechi siku moja kabla ila ni Wajibu wako kunijulisha kuwa nakuja, ili nikuandalie mazingira, huenda narekebisha mfumo wa Umeme? Huenda hali ya usalama sio shwari, huenda nimepulizia dawa za dudu zinaweka kukuathiri, yaani ni HAKI yako ila una WAJIBU wako huu ni mfano tu. Mnasemaje Watu wangu wa nchini Yemen haya hayawahusu sana, huko kwenu Kivyenu vyenu Wayemen😀" - Farhan JR, Mchambuzi.
    Like
    1
    · 0 Commentarii ·0 Distribuiri ·60 Views
  • Sahivi movie zimeoga
    Ni za kutosha
    Niwewe tu na bundle lako
    Nyimgine hii
    Sahivi movie zimeoga Ni za kutosha Niwewe tu na bundle lako Nyimgine hii
    0 Commentarii ·0 Distribuiri ·56 Views
  • Rais wa Marekani , Donald Trump ametoa siri kuwa Ofisi yake imepokea barua kutoka kwa Rais wa Ukraine , Volodymyr Zelensky, ikisema yuko tayari kwa mazungumzo na Russia na kusaini makubaliano ya madini adimu.

    “Ukraine iko tayari kukaa kwenye meza ya mazungumzo haraka iwezekanavyo ili kuleta amani ya kudumu. Hakuna anayetaka amani zaidi ya Waukraine,” Trump amesema katika hotuba yake bungeni usiku wa kuamkia leo huku akinukuu barua hiyo.

    “Mimi na timu yangu tuko tayari kufanya kazi chini ya uongozi thabiti wa Rais Trump ili kupata amani ya kudumu’,” Trump alinukuu maneno ya Zelenskyy.

    “Si hilo lingekuwa jambo zuri?” aliuliza. “Ni wakati wa kukomesha huu upuuzi. Ni wakati wa kusitisha mauaji. Ni wakati wa kumaliza vita hivi visivyo na maana. Ukitaka kumaliza vita, lazima uzungumze na pande zote mbili,” amesema Trump.

    Kauli hiyo ya Trump imekuja siku chache baada ya mvutano mkali kati yake na Zelenskyy katika Ofisi ya Oval iliyoko Ikulu ya White House, hali iliyosababisha Marekani kusitisha msaada muhimu wa kijeshi kwa Ukraine.

    Rais wa Marekani 🇺🇸, Donald Trump ametoa siri kuwa Ofisi yake imepokea barua kutoka kwa Rais wa Ukraine 🇺🇦, Volodymyr Zelensky, ikisema yuko tayari kwa mazungumzo na Russia 🇷🇺 na kusaini makubaliano ya madini adimu. “Ukraine iko tayari kukaa kwenye meza ya mazungumzo haraka iwezekanavyo ili kuleta amani ya kudumu. Hakuna anayetaka amani zaidi ya Waukraine,” Trump amesema katika hotuba yake bungeni usiku wa kuamkia leo huku akinukuu barua hiyo. “Mimi na timu yangu tuko tayari kufanya kazi chini ya uongozi thabiti wa Rais Trump ili kupata amani ya kudumu’,” Trump alinukuu maneno ya Zelenskyy. “Si hilo lingekuwa jambo zuri?” aliuliza. “Ni wakati wa kukomesha huu upuuzi. Ni wakati wa kusitisha mauaji. Ni wakati wa kumaliza vita hivi visivyo na maana. Ukitaka kumaliza vita, lazima uzungumze na pande zote mbili,” amesema Trump. Kauli hiyo ya Trump imekuja siku chache baada ya mvutano mkali kati yake na Zelenskyy katika Ofisi ya Oval iliyoko Ikulu ya White House, hali iliyosababisha Marekani kusitisha msaada muhimu wa kijeshi kwa Ukraine.
    Like
    1
    · 0 Commentarii ·0 Distribuiri ·240 Views
  • Ijumaa, tarehe 28 Februari, haikuwa siku rahisi kwa Rais wa Ukraine, Volodymyr Zelensky, alipofanya ziara katika Ikulu ya White House, Marekani. Kabla hata ya mzozo wa maneno kati yake na mwenyeji wake, Rais Donald Trump, pamoja na Makamu wa Rais JD Vance, tayari kulikuwa na ishara za mivutano.

    Trump alimkaribisha Zelensky mlangoni na kusema kwa utani: “Leo amevalia kweli kweli,” kauli ambayo iliwafanya baadhi ya waandishi wa habari kuiona kama kejeli badala ya pongezi. Wakati huo, Zelensky alikuwa amevalia fulana nyeusi ya mikono mirefu, vazi ambalo amekuwa akilivaa mara kwa mara tangu Ukraine ivamiwe na Urusi mwaka 2022.

    Baadaye, Trump alipompokea Waziri Mkuu wa Uingereza, Keir Starmer, alionekana kutazama mavazi yake kwa makini kutoka juu hadi chini, kisha kunong’ona maneno yanayoweza kutafsiriwa kama pongezi kwa suti rasmi aliyovaa Starmer.

    Mjadala kuhusu mavazi ya Zelensky ulizidi kupamba moto wakati wa mkutano wa waandishi wa habari. Brian Glenn, mwandishi kutoka Real America’s Voice—chombo cha habari kinachopendelea mrengo wa kulia—alimtupia swali la moja kwa moja:

    “Kwa nini hauvai suti? Upo katika ofisi ya juu kabisa katika nchi hii, na umegoma kuvaa suti – je, unamiliki hata suti?”

    Kwa utulivu, Zelensky alijibu kwa mshangao mdogo:

    “Nitavaa suti vita hivi vitakapomalizika. Labda suti kama yako, labda bora zaidi, au pengine ya bei nafuu kuliko yako,” alisema kwa utani huku akionyesha msimamo wake wa kuendelea kuvaa mavazi ya kijeshi.

    Swali hilo la Glenn liliibua mjadala mkali mitandaoni. Wengine walimuunga mkono, wakisema kwamba kiongozi wa taifa anapaswa kuvaa mavazi rasmi anapokutana na viongozi wengine, ilhali wengine waliona swali hilo kuwa la dhihaka na lisilo na umuhimu.

    Miongoni mwa waliomkosoa Glenn ni mwandishi maarufu wa Uingereza, Piers Morgan, ambaye pia ni rafiki wa karibu wa Trump. Morgan aliandika kwenye mtandao wa X (zamani Twitter):

    “Swali la kipuuzi. Elon Musk havai suti anapoingia Ikulu.”

    Historia pia inaonyesha kuwa si Zelensky pekee aliyeingia Ikulu ya Marekani bila suti. Waziri Mkuu wa zamani wa Uingereza, Winston Churchill, alifanya hivyo katika moja ya ziara zake rasmi.
    Ijumaa, tarehe 28 Februari, haikuwa siku rahisi kwa Rais wa Ukraine, Volodymyr Zelensky, alipofanya ziara katika Ikulu ya White House, Marekani. Kabla hata ya mzozo wa maneno kati yake na mwenyeji wake, Rais Donald Trump, pamoja na Makamu wa Rais JD Vance, tayari kulikuwa na ishara za mivutano. Trump alimkaribisha Zelensky mlangoni na kusema kwa utani: “Leo amevalia kweli kweli,” kauli ambayo iliwafanya baadhi ya waandishi wa habari kuiona kama kejeli badala ya pongezi. Wakati huo, Zelensky alikuwa amevalia fulana nyeusi ya mikono mirefu, vazi ambalo amekuwa akilivaa mara kwa mara tangu Ukraine ivamiwe na Urusi mwaka 2022. Baadaye, Trump alipompokea Waziri Mkuu wa Uingereza, Keir Starmer, alionekana kutazama mavazi yake kwa makini kutoka juu hadi chini, kisha kunong’ona maneno yanayoweza kutafsiriwa kama pongezi kwa suti rasmi aliyovaa Starmer. Mjadala kuhusu mavazi ya Zelensky ulizidi kupamba moto wakati wa mkutano wa waandishi wa habari. Brian Glenn, mwandishi kutoka Real America’s Voice—chombo cha habari kinachopendelea mrengo wa kulia—alimtupia swali la moja kwa moja: “Kwa nini hauvai suti? Upo katika ofisi ya juu kabisa katika nchi hii, na umegoma kuvaa suti – je, unamiliki hata suti?” Kwa utulivu, Zelensky alijibu kwa mshangao mdogo: “Nitavaa suti vita hivi vitakapomalizika. Labda suti kama yako, labda bora zaidi, au pengine ya bei nafuu kuliko yako,” alisema kwa utani huku akionyesha msimamo wake wa kuendelea kuvaa mavazi ya kijeshi. Swali hilo la Glenn liliibua mjadala mkali mitandaoni. Wengine walimuunga mkono, wakisema kwamba kiongozi wa taifa anapaswa kuvaa mavazi rasmi anapokutana na viongozi wengine, ilhali wengine waliona swali hilo kuwa la dhihaka na lisilo na umuhimu. Miongoni mwa waliomkosoa Glenn ni mwandishi maarufu wa Uingereza, Piers Morgan, ambaye pia ni rafiki wa karibu wa Trump. Morgan aliandika kwenye mtandao wa X (zamani Twitter): “Swali la kipuuzi. Elon Musk havai suti anapoingia Ikulu.” Historia pia inaonyesha kuwa si Zelensky pekee aliyeingia Ikulu ya Marekani bila suti. Waziri Mkuu wa zamani wa Uingereza, Winston Churchill, alifanya hivyo katika moja ya ziara zake rasmi.
    Like
    Love
    2
    · 0 Commentarii ·0 Distribuiri ·411 Views
  • Hii kama sijaielewa hivi.
    Hii kama sijaielewa hivi.
    Like
    Love
    5
    · 1 Commentarii ·0 Distribuiri ·211 Views
  • 7. Tel Hazor
    Katika eneo la ekari 200 hivi, eneo hili lililo katika Galilaya ya Juu (sasa ni mbuga ya kitaifa) ndilo kubwa zaidi kati ya “tels” za Israeli,

    Kulingana na Agano la Kale, Hazori ilikuwa mahali pa ushindi muhimu wa Yoshua katika ushindi wake wa Kanaani baada ya kifo cha Musa; eti aliteketeza jiji hilo kabisa, akisafisha njia kwa ajili ya makazi ya Waisraeli.
    7. Tel Hazor Katika eneo la ekari 200 hivi, eneo hili lililo katika Galilaya ya Juu (sasa ni mbuga ya kitaifa) ndilo kubwa zaidi kati ya “tels” za Israeli, Kulingana na Agano la Kale, Hazori ilikuwa mahali pa ushindi muhimu wa Yoshua katika ushindi wake wa Kanaani baada ya kifo cha Musa; eti aliteketeza jiji hilo kabisa, akisafisha njia kwa ajili ya makazi ya Waisraeli.
    0 Commentarii ·0 Distribuiri ·315 Views
  • Katika hatua mpya ya mzozo unaoendelea Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo , kundi la Waasi wa M23 likishirikiana na Muungano wa Mto Congo (AFC) limetangaza kuwa Wanajeshi wa zamani wa Jeshi la DR Congo (FARDC) waliokamatwa au kujisalimisha wamehitimu mafunzo ya kiitikadi na mbinu za kijeshi.

    Katika taarifa ya Kundi la M23 kwenye mtandao wao wa X leo Februari 18, picha zilionyesha Wanajeshi hao wakiwa na sare na silaha rasmi za wanamgambo hao. Ujumbe uliambatana na chapisho hilo ulieleza:

    "Wanajeshi wa zamani wa FARDC, waliokamatwa au kujisalimisha, wamemaliza mafunzo ya kiitikadi na mbinu huko Rumangabo Mjini Goma chini ya AFC/M23. Sasa wakiwa na vifaa kamili na wanaolipwa, wametumwa Lubero, ambako wanashiriki kikamilifu muungano wa serikali."

    Wakati huo huo, Uganda imetangaza kuwa vikosi vyake vya kijeshi vimeanza kuelekea Bunia, DRC, ikiwa ni siku chache baada ya Jeshi la Uganda kutoa muda wa saa 24 kwa Askari waliopo eneo hilo kujisalimisha.

    Taarifa nyingine kuwa, hapo jana Kundi la Waasi hao wa M23 wamefanikiwa kuteka eneo la Kamanyola na sasa hivi wanajipanga kuelekea Uvira, Fizi kisha Mkoa wa Tanganyika (Kalemie) kabla ya kwenda Mjini Lubumbashi. Kwa mujibu wa Wananchi wa Kamanyala wanasema kuwa Kundi la Wapiganaji wa Wazalendo ambao wanapigana kwa upande wa Serikali waliibwa Silaha zao kisha wakakimbia na kuwaachia M23 kuichukua Kamanyola.

    Katika hatua mpya ya mzozo unaoendelea Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo 🇨🇩, kundi la Waasi wa M23 likishirikiana na Muungano wa Mto Congo (AFC) limetangaza kuwa Wanajeshi wa zamani wa Jeshi la DR Congo (FARDC) waliokamatwa au kujisalimisha wamehitimu mafunzo ya kiitikadi na mbinu za kijeshi. Katika taarifa ya Kundi la M23 kwenye mtandao wao wa X leo Februari 18, picha zilionyesha Wanajeshi hao wakiwa na sare na silaha rasmi za wanamgambo hao. Ujumbe uliambatana na chapisho hilo ulieleza: "Wanajeshi wa zamani wa FARDC, waliokamatwa au kujisalimisha, wamemaliza mafunzo ya kiitikadi na mbinu huko Rumangabo Mjini Goma chini ya AFC/M23. Sasa wakiwa na vifaa kamili na wanaolipwa, wametumwa Lubero, ambako wanashiriki kikamilifu muungano wa serikali." Wakati huo huo, Uganda imetangaza kuwa vikosi vyake vya kijeshi vimeanza kuelekea Bunia, DRC, ikiwa ni siku chache baada ya Jeshi la Uganda kutoa muda wa saa 24 kwa Askari waliopo eneo hilo kujisalimisha. Taarifa nyingine kuwa, hapo jana Kundi la Waasi hao wa M23 wamefanikiwa kuteka eneo la Kamanyola na sasa hivi wanajipanga kuelekea Uvira, Fizi kisha Mkoa wa Tanganyika (Kalemie) kabla ya kwenda Mjini Lubumbashi. Kwa mujibu wa Wananchi wa Kamanyala wanasema kuwa Kundi la Wapiganaji wa Wazalendo ambao wanapigana kwa upande wa Serikali waliibwa Silaha zao kisha wakakimbia na kuwaachia M23 kuichukua Kamanyola.
    0 Commentarii ·0 Distribuiri ·473 Views
  • "Wakati tunazilaumu Simba Sports na Azam Football Club Kuukosa Ubingwa,tukumbuke pia Mazingira Yao Magumu ya Kushindana

    Parameters za Simba Sports na Azam Fc Kuchukua Ubingwa zimebadilika Kabisa na ni tofauti Washindani wenzao Kwenye Ligi

    Kuna hoja Lazy sana eti Mbona Simba Sports alicheza na Tabora United Dhaifu?

    Kwenye Mechi zote 2 Tabora wana uwezo wa Ku justifie Kwanini walichezesha Vikosi vile na ukawaelewa vizuri tu.

    Mechi ya Kwanza n issue ya Vibali,na mechi ya Pili Heritier Makambo alikuwa na Kadi 3 za njano. Yacouba Sogne alikuwa ni Majeruhi..

    Kuna hoja Lazy nyingine Kwamba mbona Kikosi bora cha Singida Black Stars Kilifungwa 2-0 na KMC ambayo ilifungwa 6-1 na Yanga?

    Kwanza Kwenye hiyo hoja hapo wote tumekubaliana Kwamba Singida Black Stars wamepanga Kikosi Dhaifu

    Pili, Sisi hatusemi Singida Black Stars angepanga Kikosi bora lazima angeshinda dhidi ya Yanga au asingepoteza mechi

    Mbona ile Mechi ya Kwanza Kule Amani Complex Zanzibar Singida Black Stars waliweka Full Mkoko na bado Yanga alishinda 1-0 bao la Paccome ?

    Swali ni Sababu ipi ya Singida Black Stars Kubadilisha wachezaji 6 Kutoka Kwenye Kikosi Kilichomfunga Jkt Tanzania 1-0?

    Mbaya zaidi Kuna wachezaji walichezeshwa Kabisa nje ya Maeneo ya ya asili na wachezaji wenye nafasi zao wakiwa bench

    Singida black stars Dhaifu ilipigwa 2-0 Kipindi Cha Kwanza na Stars bora ilishinda 1-0 Kipindi cha Pili.

    Ligi yetu tukufu inachezewa na watu ambao hawana nia njema na Mpira wetu na Kama tusipotwanga sasa hivi tutakuja Kuula Mbichi" - Wilson Orumo, Mchambuzi.

    "Wakati tunazilaumu Simba Sports na Azam Football Club Kuukosa Ubingwa,tukumbuke pia Mazingira Yao Magumu ya Kushindana Parameters za Simba Sports na Azam Fc Kuchukua Ubingwa zimebadilika Kabisa na ni tofauti Washindani wenzao Kwenye Ligi Kuna hoja Lazy sana eti Mbona Simba Sports alicheza na Tabora United Dhaifu? Kwenye Mechi zote 2 Tabora wana uwezo wa Ku justifie Kwanini walichezesha Vikosi vile na ukawaelewa vizuri tu. Mechi ya Kwanza n issue ya Vibali,na mechi ya Pili Heritier Makambo alikuwa na Kadi 3 za njano. Yacouba Sogne alikuwa ni Majeruhi.. Kuna hoja Lazy nyingine Kwamba mbona Kikosi bora cha Singida Black Stars Kilifungwa 2-0 na KMC ambayo ilifungwa 6-1 na Yanga? Kwanza Kwenye hiyo hoja hapo wote tumekubaliana Kwamba Singida Black Stars wamepanga Kikosi Dhaifu Pili, Sisi hatusemi Singida Black Stars angepanga Kikosi bora lazima angeshinda dhidi ya Yanga au asingepoteza mechi Mbona ile Mechi ya Kwanza Kule Amani Complex Zanzibar Singida Black Stars waliweka Full Mkoko na bado Yanga alishinda 1-0 bao la Paccome ? Swali ni Sababu ipi ya Singida Black Stars Kubadilisha wachezaji 6 Kutoka Kwenye Kikosi Kilichomfunga Jkt Tanzania 1-0? Mbaya zaidi Kuna wachezaji walichezeshwa Kabisa nje ya Maeneo ya ya asili na wachezaji wenye nafasi zao wakiwa bench Singida black stars Dhaifu ilipigwa 2-0 Kipindi Cha Kwanza na Stars bora ilishinda 1-0 Kipindi cha Pili. Ligi yetu tukufu inachezewa na watu ambao hawana nia njema na Mpira wetu na Kama tusipotwanga sasa hivi tutakuja Kuula Mbichi" - Wilson Orumo, Mchambuzi.
    0 Commentarii ·0 Distribuiri ·556 Views
  • Mchezaji wa zamani wa mpira wa miguu kutoka Nchini Liberia , George Weah, amekana kufanya mazungumzo yoyote na Mmiliki wa mtandao wa X Elon Musk kuhusiana na kununua tuzo yake ya Ballon D’or aliyoshinda mwaka 1995 kwa thamani ya Dola bilioni moja (1).

    Mchezaji huyo amesema kuwa Musk hakuwahi kutaka kununua tuzo hiyo kutoka kwake, kama ilivyoripotiwa mitandaoni hivi karibuni. Pamoja na hayo, Weah ameongeza kuwa Tuzo hiyo haiuzwi hata Watoto wake alishawaambia kuwa Tuzo hiyo ni mali ya Afrika, hata ikitokea wakapatwa na shida, haitakiwi kuuzwa kwa sababu ndio Tuzo pekee bara la Afrika inajivunia.

    Mchezaji wa zamani wa mpira wa miguu kutoka Nchini Liberia 🇱🇷, George Weah, amekana kufanya mazungumzo yoyote na Mmiliki wa mtandao wa X Elon Musk kuhusiana na kununua tuzo yake ya Ballon D’or aliyoshinda mwaka 1995 kwa thamani ya Dola bilioni moja (1). Mchezaji huyo amesema kuwa Musk hakuwahi kutaka kununua tuzo hiyo kutoka kwake, kama ilivyoripotiwa mitandaoni hivi karibuni. Pamoja na hayo, Weah ameongeza kuwa Tuzo hiyo haiuzwi hata Watoto wake alishawaambia kuwa Tuzo hiyo ni mali ya Afrika, hata ikitokea wakapatwa na shida, haitakiwi kuuzwa kwa sababu ndio Tuzo pekee bara la Afrika inajivunia.
    Love
    1
    · 0 Commentarii ·0 Distribuiri ·272 Views
  • Kaka yake, Josh Jones, alisikia sauti za John akilia kwa uchungu.

    Alipojaribu kumvuta, aligundua kuwa amekwama vibaya sana.

    John alikuwa amepinda vibaya, kifua chake kimesukumwa dhidi ya mwamba, na hawezi kupumua vizuri.

    Kila sekunde iliyopita, damu yake ilianza kushindwa kuzunguka mwilini.

    Josh alipiga mayowe ya msaada, na hivi karibuni, vikosi vya uokoaji vilifika.

    Lakini walichokiona kilikuwa cha kutisha zaidi ya walivyodhani.
    Kaka yake, Josh Jones, alisikia sauti za John akilia kwa uchungu. Alipojaribu kumvuta, aligundua kuwa amekwama vibaya sana. John alikuwa amepinda vibaya, kifua chake kimesukumwa dhidi ya mwamba, na hawezi kupumua vizuri. Kila sekunde iliyopita, damu yake ilianza kushindwa kuzunguka mwilini. Josh alipiga mayowe ya msaada, na hivi karibuni, vikosi vya uokoaji vilifika. Lakini walichokiona kilikuwa cha kutisha zaidi ya walivyodhani.
    Love
    1
    · 0 Commentarii ·0 Distribuiri ·190 Views
  • Rais wa Senegal , Bassirou Diomaye Faye ametangaza mpango wa kubadilisha majina ya mitaa yenye majina ya enzi za ukoloni na kuyapa majina ya mashujaa wa kitaifa na matukio muhimu ya kihistoria ya Nchi ya Senegal. Mpango huo ulioanzishwa wakati wa mkutano wa hivi karibuni wa Baraza la Mawaziri ni sehemu ya juhudi za kurejesha utambulisho wa kitamaduni wa Nchi hiyo.

    Mpango huyo utahusu pia kubadilisha majina na kuandika upya historia ya Nchi ya Senegal katika kwa umma, alisema Rais huyo ambapo pia aliongeza kwa kusema “Lazima tuelimishe Vijana wetu kuhusu Watu na matukio yaliyounda na kuijenga Senegal"

    Rais wa Senegal 🇸🇳, Bassirou Diomaye Faye ametangaza mpango wa kubadilisha majina ya mitaa yenye majina ya enzi za ukoloni na kuyapa majina ya mashujaa wa kitaifa na matukio muhimu ya kihistoria ya Nchi ya Senegal. Mpango huo ulioanzishwa wakati wa mkutano wa hivi karibuni wa Baraza la Mawaziri ni sehemu ya juhudi za kurejesha utambulisho wa kitamaduni wa Nchi hiyo. Mpango huyo utahusu pia kubadilisha majina na kuandika upya historia ya Nchi ya Senegal katika kwa umma, alisema Rais huyo ambapo pia aliongeza kwa kusema “Lazima tuelimishe Vijana wetu kuhusu Watu na matukio yaliyounda na kuijenga Senegal"
    0 Commentarii ·0 Distribuiri ·390 Views
  • Wapiganaji wa kundi la Waasi wa M23 na Askari wanaodhaniwa kuwa ni Rwanda wameendelea kusonga mbele katika maeneo ya mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo . Hayo ni kwa mujibu wa vyanzo vya eneo hilo pamoja na vya mashirika ya kibinadamu. Miji iliyotekwa ni Ihusi na Kalehe, iliyoko karibu kiliomita sitini (60) kutoka Mji wa Bukavu.

    Katika taarifa, Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imeitisha mkutano wa dharura wa mataifa ya Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) na Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kutathmini hali hiyo na "kutathmini hali na matokeo ya kitendo hiki kipya cha uchokozi", ikitoa wito wa vikwazo.

    Rais wa Burundi , Evariste Ndayishimiye amesema yeyote atakayeishambulia Nchi yake naye atashambuliwa. Wakati huo huo, Viongozi wa Baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki Nchini DR Congo na ule wa Kanisa la Kristo la DR Congo umekutana na kundi la Waasi wa M23 Mjini Goma katika juhudi za hivi karibuni kabisa za kusaka amani na mazungumzo. Walikutana na kiongozi wa kisiasa wa kundi la M23 Corneille Nangaa.
    (DW Swahili)

    Wapiganaji wa kundi la Waasi wa M23 na Askari wanaodhaniwa kuwa ni Rwanda 🇷🇼 wameendelea kusonga mbele katika maeneo ya mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo 🇨🇩. Hayo ni kwa mujibu wa vyanzo vya eneo hilo pamoja na vya mashirika ya kibinadamu. Miji iliyotekwa ni Ihusi na Kalehe, iliyoko karibu kiliomita sitini (60) kutoka Mji wa Bukavu. Katika taarifa, Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imeitisha mkutano wa dharura wa mataifa ya Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) na Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kutathmini hali hiyo na "kutathmini hali na matokeo ya kitendo hiki kipya cha uchokozi", ikitoa wito wa vikwazo. Rais wa Burundi 🇧🇮, Evariste Ndayishimiye amesema yeyote atakayeishambulia Nchi yake naye atashambuliwa. Wakati huo huo, Viongozi wa Baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki Nchini DR Congo na ule wa Kanisa la Kristo la DR Congo umekutana na kundi la Waasi wa M23 Mjini Goma katika juhudi za hivi karibuni kabisa za kusaka amani na mazungumzo. Walikutana na kiongozi wa kisiasa wa kundi la M23 Corneille Nangaa. (DW Swahili)
    Love
    1
    · 0 Commentarii ·0 Distribuiri ·422 Views
  • TBT ya Haji Manara

    "September 2007 nikiwa kijana Mdogo na nikiwa kiongozi wa Chama changu na hapo ni fresh from School kule Beijing China.
    Kipindi hicho nna madini ya hatari kuhusu taaluma ya Propaganda na Uenezi,enzi ambazo nilikuwa naweza kukuaminisha Jiwe ni Keki

    Enzi ambazo nilikuwa naweza kuwavusha hata kuku barabarani kwa maneno tu,
    Ni zile zile zama nilizowaaminisha Barcelona haichomoki kwa Mkapa, tena Barcelona kweli ya Xavi ,Iniesta na kina Messi.
    Taaluma iliyonipa ujasiri wa kusema na kuamini tutafuzu kwa AFCON ya 2019 kule Misri,wakati huo tukiwa chini kwenye msimamo wa kundi letu, na Nchi nzima ikiwa imejikatia tamaa ya kwenda Cairo.

    Bila kusahau one day kule Paris France niliposahau Passport hotelini na siku hiyo tulisimamishwa na Manjagu njiani nikiwa na wenzangu ambao walikuwa Kamil Gado,
    Nikazuga kama naitoa kwenye mfuko wa koti, Askari wakaniamini kabla ya kuwaonyesha ,wakaturuhusu kilaini kabisa,inaitwa Blue Propaganda

    Yes: Pembeni yangu katika hiyo picha ni Marehemu Captain Barongo aliyekuwa Katibu wa CCM Mkoa wa Dar es salaam,
    Na hii ilikuwa sherehe ya harusi ya DC wa Temeke hivi sasa Mh Sixtus Mapunda ambae wakati huo alikuwa Katibu wa Umoja wa Vijana ( UV CCM ) Mkoa huu.
    Hadi leo tumebaki marafiki wakubwa na hakosi mwaliko wowote kwangu

    Nb: Usicheke ukubwa wa koti,miaka ile ilikuwa ndio fashion na wenyewe tuliyaita Majumba "

    TBT ya Haji Manara "September 2007 nikiwa kijana Mdogo na nikiwa kiongozi wa Chama changu na hapo ni fresh from School kule Beijing China. Kipindi hicho nna madini ya hatari kuhusu taaluma ya Propaganda na Uenezi,enzi ambazo nilikuwa naweza kukuaminisha Jiwe ni Keki 😀😀😀 Enzi ambazo nilikuwa naweza kuwavusha hata kuku barabarani kwa maneno tu😀😀😀, Ni zile zile zama nilizowaaminisha Barcelona haichomoki kwa Mkapa, tena Barcelona kweli ya Xavi ,Iniesta na kina Messi. Taaluma iliyonipa ujasiri wa kusema na kuamini tutafuzu kwa AFCON ya 2019 kule Misri,wakati huo tukiwa chini kwenye msimamo wa kundi letu, na Nchi nzima ikiwa imejikatia tamaa ya kwenda Cairo. Bila kusahau one day kule Paris France niliposahau Passport hotelini na siku hiyo tulisimamishwa na Manjagu njiani nikiwa na wenzangu ambao walikuwa Kamil Gado, Nikazuga kama naitoa kwenye mfuko wa koti, Askari wakaniamini kabla ya kuwaonyesha ,wakaturuhusu kilaini kabisa,inaitwa Blue Propaganda 😀😀😀 Yes: Pembeni yangu katika hiyo picha ni Marehemu Captain Barongo aliyekuwa Katibu wa CCM Mkoa wa Dar es salaam, Na hii ilikuwa sherehe ya harusi ya DC wa Temeke hivi sasa Mh Sixtus Mapunda ambae wakati huo alikuwa Katibu wa Umoja wa Vijana ( UV CCM ) Mkoa huu. Hadi leo tumebaki marafiki wakubwa na hakosi mwaliko wowote kwangu 🙏🙏 Nb: Usicheke ukubwa wa koti,miaka ile ilikuwa ndio fashion na wenyewe tuliyaita Majumba 😀😀😀"
    0 Commentarii ·0 Distribuiri ·575 Views
  • Habari iliyobamba kwa sasa kwenye vyombo vya habari ni ndoa ya Stephane Aziz Ki na Hamisa Mobetto, ingawa wapo waliofika mbali na kudai ni kiki tu kwa ajili ya matangazo ya bidhaa fulani na wanatumika tu.

    Baada ya vuta nkuvute ya stori hii hatimaye mama yake Hamisa, Shufaa Rutanga amefunga na anathibitisha kuwepo kwa ndoa hiyo na kuhusu posa ya Aziz Ki, amesema hakuna posa yoyote iliyofika kwake kutoka kwa nyota huyo wa kimataifa wa Burkina Faso ingawa amepokea nyingi kutoka kwa wanaume tofauti wanaotaka kumuoa mwanaye.

    “Sasa ngoja nikuambie ukweli, maana nilikuwa nashindwa kutoa majibu sahihi kutokana na baadhi ya ya vitu kuhusu ndoa hii vilikuwa havijakamilika, sasa vimekamilika na ndoa ipo. Kiukweli namshukuru Mungu maombi yangu kwa mwanagu yameitika, nilikuwa kila kukicha naomba apate mtu sahihi watakayependana ili aolewe, kuwa kwenye ndoa ni heshima kubwa sana" - Mama Mobetto

    Mama Hamisa anasema hekaheka za ndoa hiyo zitaanza Jumamosi Februari 15 na ndiyo siku mahari itatolewa na sherehe itafanyika Februari 19, The Superdome, Masaki, jijini Dar es Salaam.

    “Kutoka moyoni nimewapa baraka zote mkwe wangu AziZ Ki na mwanagu Hamisa na upendo mwingi sana kwake Aziz Ki kwa kupenda watoto wa Hamisa. Hiki ndiyo sababu kuu iliyonifanya nimpende zaidi Aziz Ki, maana kwa hali ya sasa hivi upate mwanamume atakayekubali kuoa mwanamke mwenye watoto ni wachache sana ila Aziz Ki ameonyesha upendo wa dhati kwa mwanangu Hamisa, kapenda boga na maua yake.” - Mama Mobetto

    Wakati huohuo mmoja wa viongozi wa Yanga, amethibitisha ni kweli wawili hao watafunga ndoa Ijumaa na kwasasa Aziz yupo kwenye maandalizi ya Ndoa ingawa atakuwepo kwenye mchezo wa Ijumaa.
    (Mwananchi)

    Habari iliyobamba kwa sasa kwenye vyombo vya habari ni ndoa ya Stephane Aziz Ki na Hamisa Mobetto, ingawa wapo waliofika mbali na kudai ni kiki tu kwa ajili ya matangazo ya bidhaa fulani na wanatumika tu. Baada ya vuta nkuvute ya stori hii hatimaye mama yake Hamisa, Shufaa Rutanga amefunga na anathibitisha kuwepo kwa ndoa hiyo na kuhusu posa ya Aziz Ki, amesema hakuna posa yoyote iliyofika kwake kutoka kwa nyota huyo wa kimataifa wa Burkina Faso ingawa amepokea nyingi kutoka kwa wanaume tofauti wanaotaka kumuoa mwanaye. “Sasa ngoja nikuambie ukweli, maana nilikuwa nashindwa kutoa majibu sahihi kutokana na baadhi ya ya vitu kuhusu ndoa hii vilikuwa havijakamilika, sasa vimekamilika na ndoa ipo. Kiukweli namshukuru Mungu maombi yangu kwa mwanagu yameitika, nilikuwa kila kukicha naomba apate mtu sahihi watakayependana ili aolewe, kuwa kwenye ndoa ni heshima kubwa sana" - Mama Mobetto Mama Hamisa anasema hekaheka za ndoa hiyo zitaanza Jumamosi Februari 15 na ndiyo siku mahari itatolewa na sherehe itafanyika Februari 19, The Superdome, Masaki, jijini Dar es Salaam. “Kutoka moyoni nimewapa baraka zote mkwe wangu AziZ Ki na mwanagu Hamisa na upendo mwingi sana kwake Aziz Ki kwa kupenda watoto wa Hamisa. Hiki ndiyo sababu kuu iliyonifanya nimpende zaidi Aziz Ki, maana kwa hali ya sasa hivi upate mwanamume atakayekubali kuoa mwanamke mwenye watoto ni wachache sana ila Aziz Ki ameonyesha upendo wa dhati kwa mwanangu Hamisa, kapenda boga na maua yake.” - Mama Mobetto Wakati huohuo mmoja wa viongozi wa Yanga, amethibitisha ni kweli wawili hao watafunga ndoa Ijumaa na kwasasa Aziz yupo kwenye maandalizi ya Ndoa ingawa atakuwepo kwenye mchezo wa Ijumaa. (Mwananchi)
    Like
    1
    · 0 Commentarii ·0 Distribuiri ·617 Views
  • Hellow cm yangu ilizingua kidg but now am back online
    Nilitaka kuuliza
    Hivi nyie dunia mnaielewa kweli inakoelekea au wameqnza kuharibu bora wangemaliza
    Hellow cm yangu ilizingua kidg but now am back online Nilitaka kuuliza Hivi nyie dunia mnaielewa kweli inakoelekea au wameqnza kuharibu bora wangemaliza
    0 Commentarii ·0 Distribuiri ·177 Views
  • SHEREHEKEENI PAMOJA SIKU YENU

    Picha inaiieleza kwamba ni ya mwaka 1948, waasisi wa klabu ya Yanga wakiwa na wenzao wa Africa Sports ya Zanzibar.

    Picha hii inatufundisha kwamba Muungano wa Tanganyika na Zanzibar haukuwa mwaka 1964 bali zamani sana...mwaka 1964 ulikuwa mkataba tu.

    Na hata kutengana kuliletwa na wakoloni, wakaweka mipaka na kuigawana ardhi...mjerumani akachukua Bara na mwingereza akachukua Zanzibar.

    Lakini kabla ya mipaka yao, hii nchi ilikuwa moja tu, na hata mji wa Dar es Salaam ulianzishwa na Sultan Majid wa Zanzibar.

    Yaani aliamua tu kutoka sehemu moja ya nchi yake na kwenda kuanzisha mji sehemu nyingine ya nchi yake.

    Lakini hilo lengo la andiko hili...

    Lengo la kuandika hapa ni kutaka kuwakumbusha watu kwamba waliopo kwenye picha ni waasisi wa Yanga, na pia hawa ndiyo waasisi wa Simba.

    Na hii ni kwa sababu walioanzisha Simba ni wale wale walioanzisha Yanga, lakini wakajitenga na wenzao.

    Ni hivi

    Kulikuwa na timu iliyoitwa New Young, ambayo ilianzishwa mwaka 1935 na kuanza kushiriki ligi mwaka huo huo.

    Wakati huo ligi ilikuwa moja tu, ya Dar es Salaam...na Dar es Salaam yenyewe ilikuwa wilaya ya jimbo la Mashariki.

    Hakukuwa na ligi nyingine yoyote nchini, japo miaka michache baadaye wilaya zingine nazo zikaanzisha ligi...ikianza wilaya ya Iringa. Stori yake itakuja siku nyingine.

    Ligi ya Dar es Salaam ambayo ilianza 1929 ikiwa na daraja moja tu, la kwanza...ilikua na kuongeza daraja la pili kwenye miaka ya 1930.

    Kwa hiyo New Young ilipojiunga na ligi mwaka 1935, ikaanzia daraja la pili.

    Ikashinda ubingwa na kupanda daraja la kwanza, mwaka 1936. Hata hivyo ilicheza ligi kwa mtindo wa VIEW ONCE kwani ilishuka mwaka huo huo.

    Kushuka kwao ndiko kulikoleta mpasuko na wengine kujitenga.

    Waliojitenga ndiyo hawa ambao sasa ni Simba, na waliobaki wakabadili jina kutoka New Young na kujiita Young Africans ambao ndiyo Yanga.

    Lakini hawa watu walikuwa pamoja mwaka mmoja tu uliopita...na ndiyo waliopo kwenye picha hii.

    Kwa hiyo leo inatakiwa hii sherehe iwe yao wote! Happy Birthday Yanga na Simba. Furahieni siku yenu kwa amani. Sisi tunajua nyinyi ni ndugu ila mnatuzuga tu!
    (Zakazakazi )

    SHEREHEKEENI PAMOJA SIKU YENU Picha inaiieleza kwamba ni ya mwaka 1948, waasisi wa klabu ya Yanga wakiwa na wenzao wa Africa Sports ya Zanzibar. Picha hii inatufundisha kwamba Muungano wa Tanganyika na Zanzibar haukuwa mwaka 1964 bali zamani sana...mwaka 1964 ulikuwa mkataba tu. Na hata kutengana kuliletwa na wakoloni, wakaweka mipaka na kuigawana ardhi...mjerumani akachukua Bara na mwingereza akachukua Zanzibar. Lakini kabla ya mipaka yao, hii nchi ilikuwa moja tu, na hata mji wa Dar es Salaam ulianzishwa na Sultan Majid wa Zanzibar. Yaani aliamua tu kutoka sehemu moja ya nchi yake na kwenda kuanzisha mji sehemu nyingine ya nchi yake. Lakini hilo lengo la andiko hili... Lengo la kuandika hapa ni kutaka kuwakumbusha watu kwamba waliopo kwenye picha ni waasisi wa Yanga, na pia hawa ndiyo waasisi wa Simba. Na hii ni kwa sababu walioanzisha Simba ni wale wale walioanzisha Yanga, lakini wakajitenga na wenzao. Ni hivi Kulikuwa na timu iliyoitwa New Young, ambayo ilianzishwa mwaka 1935 na kuanza kushiriki ligi mwaka huo huo. Wakati huo ligi ilikuwa moja tu, ya Dar es Salaam...na Dar es Salaam yenyewe ilikuwa wilaya ya jimbo la Mashariki. Hakukuwa na ligi nyingine yoyote nchini, japo miaka michache baadaye wilaya zingine nazo zikaanzisha ligi...ikianza wilaya ya Iringa. Stori yake itakuja siku nyingine. Ligi ya Dar es Salaam ambayo ilianza 1929 ikiwa na daraja moja tu, la kwanza...ilikua na kuongeza daraja la pili kwenye miaka ya 1930. Kwa hiyo New Young ilipojiunga na ligi mwaka 1935, ikaanzia daraja la pili. Ikashinda ubingwa na kupanda daraja la kwanza, mwaka 1936. Hata hivyo ilicheza ligi kwa mtindo wa VIEW ONCE kwani ilishuka mwaka huo huo. Kushuka kwao ndiko kulikoleta mpasuko na wengine kujitenga. Waliojitenga ndiyo hawa ambao sasa ni Simba, na waliobaki wakabadili jina kutoka New Young na kujiita Young Africans ambao ndiyo Yanga. Lakini hawa watu walikuwa pamoja mwaka mmoja tu uliopita...na ndiyo waliopo kwenye picha hii. Kwa hiyo leo inatakiwa hii sherehe iwe yao wote! Happy Birthday Yanga na Simba. Furahieni siku yenu kwa amani. Sisi tunajua nyinyi ni ndugu ila mnatuzuga tu! (Zakazakazi ✍️)
    Love
    1
    · 0 Commentarii ·0 Distribuiri ·479 Views
  • Hii joint meeting imehudhuriwa na viongozi karibu wote wa SADC na EAC kwa kutambua umuhimu wake kwa usalama eneo la maziwa makuu.

    Viongozi hawa wanajua kuwa usalama wa eneo hili ni muhimu kwa ustawi wa kanda nzima, hasa ikizingatiwa mizozo ya muda mrefu kama ile ya Mashariki mwa DRC.

    Lakini pia hata viongozi ambao nchi zao zimekuwa kwenye msuguano kwenye mgogoro wa Congo wamehushuria. Paul Kagame wa Rwanda na Cyril Ramaphosa wa Afrika Kusini wamehudhuria pia.

    Wote tunakumbuka kwamba hivi karibuni Kagame na Ramaphosa walikuwa kwenye uhasama hawa kwa sababu ya tuhuma zinazoelekewa kwa Rwanda kwamba wanawaunda mkono M23, kundi la waasi linalohusishwa na kuvuruga amani Mashariki mwa DRC.

    Hata hivyo, Tshisekedi ameshindwa kuona umuhimu wa mkutano huu mpaka kumtuma mwakilishi badala yake?

    Hii inaashiria kutokuwa na ushirikiano wa kutosha au kutokubaliana na juhudi za kutatua mgogoro huu kwa njia ya kidiplomasia.

    Is this a sign of deeper political divisions within the DRC or a strategic move to maintain sovereignty?..
    Hii joint meeting imehudhuriwa na viongozi karibu wote wa SADC na EAC kwa kutambua umuhimu wake kwa usalama eneo la maziwa makuu. Viongozi hawa wanajua kuwa usalama wa eneo hili ni muhimu kwa ustawi wa kanda nzima, hasa ikizingatiwa mizozo ya muda mrefu kama ile ya Mashariki mwa DRC. Lakini pia hata viongozi ambao nchi zao zimekuwa kwenye msuguano kwenye mgogoro wa Congo wamehushuria. Paul Kagame wa Rwanda na Cyril Ramaphosa wa Afrika Kusini wamehudhuria pia. Wote tunakumbuka kwamba hivi karibuni Kagame na Ramaphosa walikuwa kwenye uhasama hawa kwa sababu ya tuhuma zinazoelekewa kwa Rwanda kwamba wanawaunda mkono M23, kundi la waasi linalohusishwa na kuvuruga amani Mashariki mwa DRC. Hata hivyo, Tshisekedi ameshindwa kuona umuhimu wa mkutano huu mpaka kumtuma mwakilishi badala yake? Hii inaashiria kutokuwa na ushirikiano wa kutosha au kutokubaliana na juhudi za kutatua mgogoro huu kwa njia ya kidiplomasia. Is this a sign of deeper political divisions within the DRC or a strategic move to maintain sovereignty?..
    0 Commentarii ·0 Distribuiri ·429 Views
  • #PART4

    Lakini cha kushangaza, wanaume wengi hawafanyi hivi.

    Kwa nini?

    Kwa sababu mwanaume hapendi kuonekana amefeli.

    Dogo akimuuliza baba yake, "Kwanini ulimuacha mama?" baba atapata kigugumizi.

    Hakuna mwanaume anayependa aonekane alishindwa kufanya kitu sahihi.

    Ndiyo maana wanaume wengi husema mambo mazuri kuhusu mama wa mtoto wao, hata kama waliachana kwa mabaya.

    Lakini wanawake wengi hawawezi kufanya hivyo. Wengi hujaza chuki kwa mtoto. Wanaangalia maisha yao kwa sasa, wanasahau mtoto atakua na atagundua ukweli wenyewe.

    50 Cent ni role model wa wanaume wengi kwa sababu moja kubwa, anajua dunia ilivyo.

    Ndiyo maana hata Chris Brown, kabla ya kuingia kwenye ndoa, alikwenda kwa 50 Cent kumuuliza ushauri.

    50 Cent alimwambia USITHUBUTU!
    #PART4 Lakini cha kushangaza, wanaume wengi hawafanyi hivi. Kwa nini? Kwa sababu mwanaume hapendi kuonekana amefeli. Dogo akimuuliza baba yake, "Kwanini ulimuacha mama?" baba atapata kigugumizi. Hakuna mwanaume anayependa aonekane alishindwa kufanya kitu sahihi. Ndiyo maana wanaume wengi husema mambo mazuri kuhusu mama wa mtoto wao, hata kama waliachana kwa mabaya. Lakini wanawake wengi hawawezi kufanya hivyo. Wengi hujaza chuki kwa mtoto. Wanaangalia maisha yao kwa sasa, wanasahau mtoto atakua na atagundua ukweli wenyewe. 50 Cent ni role model wa wanaume wengi kwa sababu moja kubwa, anajua dunia ilivyo. Ndiyo maana hata Chris Brown, kabla ya kuingia kwenye ndoa, alikwenda kwa 50 Cent kumuuliza ushauri. 50 Cent alimwambia USITHUBUTU!
    0 Commentarii ·0 Distribuiri ·530 Views
  • Katika siasa za Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), jina la Corneille Nangaa limepita katika nyanja tofauti.

    Kutoka kuwa msomi wa uchumi, mtumishi wa Umoja wa Mataifa (UNDP), msimamizi wa uchaguzi mkuu.

    Hadi sasa kuwa mmoja wa watu wanaoitikisa nchi hiyo kwa kiwango kikubwa.

    Mwanaume huyu ambaye aliwahi kuwa miongoni mwa watendaji wakubwa wa serikali, sasa anatajwa kuwa nyuma ya moja ya harakati hatari zaidi zinazoendelea katika ardhi ya Congo.

    Akiwa na historia ndefu ya kushika nafasi za juu serikalini, alifikia hatua ya kuanzisha chama chake cha kisiasa, Action for Change (AFC).

    Lakini hatua zake zilizoibua taharuki kubwa ni uhusiano wake wa karibu na kundi la waasi la M23, ambalo hivi sasa linatajwa kuwa jeshi lake binafsi.

    Lakini vipi msomi huyu wa uchumi alihamia kutoka kuongoza uchaguzi hadi kusimamia jeshi la waasi?

    Corneille Nangaa alianza kama msomi wa uchumi, akipata elimu yake kutoka Chuo Kikuu cha Kinshasa.
    Katika siasa za Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), jina la Corneille Nangaa limepita katika nyanja tofauti. Kutoka kuwa msomi wa uchumi, mtumishi wa Umoja wa Mataifa (UNDP), msimamizi wa uchaguzi mkuu. Hadi sasa kuwa mmoja wa watu wanaoitikisa nchi hiyo kwa kiwango kikubwa. Mwanaume huyu ambaye aliwahi kuwa miongoni mwa watendaji wakubwa wa serikali, sasa anatajwa kuwa nyuma ya moja ya harakati hatari zaidi zinazoendelea katika ardhi ya Congo. Akiwa na historia ndefu ya kushika nafasi za juu serikalini, alifikia hatua ya kuanzisha chama chake cha kisiasa, Action for Change (AFC). Lakini hatua zake zilizoibua taharuki kubwa ni uhusiano wake wa karibu na kundi la waasi la M23, ambalo hivi sasa linatajwa kuwa jeshi lake binafsi. Lakini vipi msomi huyu wa uchumi alihamia kutoka kuongoza uchaguzi hadi kusimamia jeshi la waasi? Corneille Nangaa alianza kama msomi wa uchumi, akipata elimu yake kutoka Chuo Kikuu cha Kinshasa.
    0 Commentarii ·0 Distribuiri ·503 Views
  • Usichanganye hivi vitu viwili, ni tofauti sana. Mapenzi na upendo, hivi ni vitu tofauti. Mapenzi Yana utumwa lakini upendo una uhuru, mapenzi yana visasi lakini upendo una msamaha, mapenzi yanamiliki lakini upendo una utu, mapenzi yana mwisho lakini upendo ni wa milele.

    Mahusiano ya mwanaume na mwanamke ni mapenzi siyo upendo. Huu ni muungano wa kimaslahi, utake usitake ni maslahi. Kila upande una maslahi yake na siyo upendo. Angalia wanavyohesabiana waliyofanyiana aidha mema au mabaya siku wanapoachana. Upendo huwa hauhesabu na hauna kumbukumbu kabisa.

    Mtu akikuambia nilikupenda sana, wala usijione na hatia, huyo muongo mkubwa. Neno analotakiwa kusema ni "nilikuwa na hisia kali za mapenzi kwako". Huwezi kumpiga mtu unayempenda, wala huwezi kutamani apatwe na mabaya sababu amekuacha. Mtu unayempenda utamtakia mema hata kama kukuacha kwake kulikuumiza. Siku zote utamuunga mkono kwa lolote linalompa furaha na amani hata kama ni kukuacha.

    Usichanganye upendo na mapenzi ni vitu tofauti. Upendo ni nishati ya asili inayoishi ndani ya mtu lakini mapenzi ni hisia inayotokana na mvuto wa kimahaba.
    Usichanganye hivi vitu viwili, ni tofauti sana. Mapenzi na upendo, hivi ni vitu tofauti. Mapenzi Yana utumwa lakini upendo una uhuru, mapenzi yana visasi lakini upendo una msamaha, mapenzi yanamiliki lakini upendo una utu, mapenzi yana mwisho lakini upendo ni wa milele. Mahusiano ya mwanaume na mwanamke ni mapenzi siyo upendo. Huu ni muungano wa kimaslahi, utake usitake ni maslahi. Kila upande una maslahi yake na siyo upendo. Angalia wanavyohesabiana waliyofanyiana aidha mema au mabaya siku wanapoachana. Upendo huwa hauhesabu na hauna kumbukumbu kabisa. Mtu akikuambia nilikupenda sana, wala usijione na hatia, huyo muongo mkubwa. Neno analotakiwa kusema ni "nilikuwa na hisia kali za mapenzi kwako". Huwezi kumpiga mtu unayempenda, wala huwezi kutamani apatwe na mabaya sababu amekuacha. Mtu unayempenda utamtakia mema hata kama kukuacha kwake kulikuumiza. Siku zote utamuunga mkono kwa lolote linalompa furaha na amani hata kama ni kukuacha. Usichanganye upendo na mapenzi ni vitu tofauti. Upendo ni nishati ya asili inayoishi ndani ya mtu lakini mapenzi ni hisia inayotokana na mvuto wa kimahaba.
    Like
    1
    · 0 Commentarii ·0 Distribuiri ·457 Views
Sponsorizeaza Paginile