• Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limekutana kujadili hali ya usalama na kibinadamu Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo huku hali ikizidi kuzorota. Mwakilishi Maalum wa Umoja huo (UN) Nchini DR Congo, Bintou Keita, amesema Waasi wa kundi la M23 wanaodaiwa kuungwa mkono na Nchi ya Rwanda sasa wanadhibiti maeneo makubwa ya Mikoa ya Kivu Kaskazini na Kivu Kusini na kutishia kupanua mashambulizi yao hadi Mkoani Tshopo na Maniema.

    "Hivi karibuni M23 imesimika utawala wake kwa kuteua gavana, makamu gavana na meya huko Bukavu, Kivu Kusini," amesema Keita.

    Ameeleza kuwa mgogoro huo unahusiana na unyonyaji wa madini mashariki mwa DR Congo na kuzua wasiwasi wa kikanda. Pia amegusia hali mbaya ya kibinadamu, akisema kumekuwa na ongezeko la ukiukwaji wa haki za binadamu, ikiwa ni pamoja na mauaji, utekaji nyara na ajira ya kulazimishwa kwa Vijana, wakiwemo Watoto.

    Licha ya makubaliano ya hivi karibuni kati ya Marais wa Rwanda na DR Congo Nchini Qatar , amani bado haijapatikana. Keita ametoa wito wa kuteuliwa kwa mpatanishi wa Umoja wa Afrika ili kuongoza juhudi za kusitisha mapigano.

    Balozi wa DR Congo katika Baraza la Umoja wa kimataifa (UN), Zénon Mukongo Ngay, ameishutumu Rwanda kwa kutotekeleza usitishaji mapigano, huku Waziri wa mambo ya nje wa Rwanda, Olivier Nduhungirehe, akisema Nchi yake itaendelea kuchukua "hatua za ulinzi" mpaka kuwe na mfumo wa kudumu wa usalama.

    Wakati huo huo, imeripotiwa kuwa DR Congo inakabiliwa na janga kubwa zaidi la njaa kuwahi kutokea, ambapo Watu zaidi ya milioni 27.7 wanakabiliwa na uhaba wa chakula kutokana na vita na ukosefu wa utulivu mashariki mwa Nchi hiyo.

    Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limekutana kujadili hali ya usalama na kibinadamu Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo 🇨🇩 huku hali ikizidi kuzorota. Mwakilishi Maalum wa Umoja huo (UN) Nchini DR Congo, Bintou Keita, amesema Waasi wa kundi la M23 wanaodaiwa kuungwa mkono na Nchi ya Rwanda 🇷🇼 sasa wanadhibiti maeneo makubwa ya Mikoa ya Kivu Kaskazini na Kivu Kusini na kutishia kupanua mashambulizi yao hadi Mkoani Tshopo na Maniema. "Hivi karibuni M23 imesimika utawala wake kwa kuteua gavana, makamu gavana na meya huko Bukavu, Kivu Kusini," amesema Keita. Ameeleza kuwa mgogoro huo unahusiana na unyonyaji wa madini mashariki mwa DR Congo na kuzua wasiwasi wa kikanda. Pia amegusia hali mbaya ya kibinadamu, akisema kumekuwa na ongezeko la ukiukwaji wa haki za binadamu, ikiwa ni pamoja na mauaji, utekaji nyara na ajira ya kulazimishwa kwa Vijana, wakiwemo Watoto. Licha ya makubaliano ya hivi karibuni kati ya Marais wa Rwanda na DR Congo Nchini Qatar 🇶🇦, amani bado haijapatikana. Keita ametoa wito wa kuteuliwa kwa mpatanishi wa Umoja wa Afrika ili kuongoza juhudi za kusitisha mapigano. Balozi wa DR Congo katika Baraza la Umoja wa kimataifa (UN), Zénon Mukongo Ngay, ameishutumu Rwanda kwa kutotekeleza usitishaji mapigano, huku Waziri wa mambo ya nje wa Rwanda, Olivier Nduhungirehe, akisema Nchi yake itaendelea kuchukua "hatua za ulinzi" mpaka kuwe na mfumo wa kudumu wa usalama. Wakati huo huo, imeripotiwa kuwa DR Congo inakabiliwa na janga kubwa zaidi la njaa kuwahi kutokea, ambapo Watu zaidi ya milioni 27.7 wanakabiliwa na uhaba wa chakula kutokana na vita na ukosefu wa utulivu mashariki mwa Nchi hiyo.
    0 Kommentare ·0 Anteile ·76 Ansichten
  • Zungu, Mtangazaji na Mchambuzi

    CPA Amos Makala kiongozi wa juu wa CCM amesema kuwa Chadema wana mpango wa kununua virusi via Ebola na Mpox ili kuzuia uchaguzi!!

    Maswali yangu kufuatia kauli ya CPA Amos Makala

    1. Hizi taarifa Makala amezipata wapi ?

    2. Idara ya usalama wa taifa (TISS) inataarifa za mpango huu ?, kama hakuna taarifa turejee kwenye swali la kwanza! Kama kuna taarifa hadi sasa ni hatua gani zimechukuliwa?

    3. Makala anatuambia kwa lugha nyingine baadhi ya viongozi wa Chadema wana mpango wa uhaini na kuhujumu uchumi wa nchi je kwanini vyombo vipo kimya kwa watu wenye tuhuma nzito kama hizi ?

    4. Je Makala amepima madhara ya kauli aliyoitoa hadharani ambayo huenda inazua taharuki na hofu kwa wananchi wa Tanzania na kwa wageni amabao wana mpango wa kuitembelea Tanzania kwa siku za usoni ?

    5. Ni hatua gani za kujibu ambazo Chadema wamezichukua hadi sasa ?

    6. Je ni kauli ya maksudi tu ili kuhamisha upepo na mjadala wa chadema ambao utashika kasi kwenye mikutano yao ya hadhara inayoanza hivi punde, kuhusu mpango wao wa no reform no election ?

    7. Je Makala anaweza kuthibitishaje kauli yake kwa Umma ?

    8.Je Chadema watanunulia wapi hivyo virusi, na kumbe vinauzwaga, Makala anaweza kuthibitisha ?

    Zungu, Mtangazaji na Mchambuzi CPA Amos Makala kiongozi wa juu wa CCM amesema kuwa Chadema wana mpango wa kununua virusi via Ebola na Mpox ili kuzuia uchaguzi!! Maswali yangu kufuatia kauli ya CPA Amos Makala 👇👇👇👇 1. Hizi taarifa Makala amezipata wapi ? 2. Idara ya usalama wa taifa (TISS) inataarifa za mpango huu ?, kama hakuna taarifa turejee kwenye swali la kwanza! Kama kuna taarifa hadi sasa ni hatua gani zimechukuliwa? 3. Makala anatuambia kwa lugha nyingine baadhi ya viongozi wa Chadema wana mpango wa uhaini na kuhujumu uchumi wa nchi je kwanini vyombo vipo kimya kwa watu wenye tuhuma nzito kama hizi ? 4. Je Makala amepima madhara ya kauli aliyoitoa hadharani ambayo huenda inazua taharuki na hofu kwa wananchi wa Tanzania na kwa wageni amabao wana mpango wa kuitembelea Tanzania kwa siku za usoni ? 5. Ni hatua gani za kujibu ambazo Chadema wamezichukua hadi sasa ? 6. Je ni kauli ya maksudi tu ili kuhamisha upepo na mjadala wa chadema ambao utashika kasi kwenye mikutano yao ya hadhara inayoanza hivi punde, kuhusu mpango wao wa no reform no election ? 7. Je Makala anaweza kuthibitishaje kauli yake kwa Umma ? 8.Je Chadema watanunulia wapi hivyo virusi, na kumbe vinauzwaga, Makala anaweza kuthibitisha ?
    0 Kommentare ·0 Anteile ·170 Ansichten
  • Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo , Felix Tshisekedi amesema Nchi yake iko tayari kuingia mkataba wa madini na Nchi Marekani kwa mabadilishano ya kupatiwa uwezo wa kujilinda dhidi ya Makundi ya Wapiganaji mashariki mwa taifa hilo kama vile kundi la M23 na mengineyo.

    Akizungumza na kituo cha Televisheni cha Fox News leo asubuhi, Rais huyo amesema makubaliano ya aina hiyo yataiwezesha Nchi ya DR Congo kuchimba madini yake kupitia Kampuni za Marekani huku yenyewe ikinufaika kwa kuimarisha mifumo yake ya ulinzi na usalama. Nchi hiyo yenye utajiri mkubwa wa madini ikiwemo kobalti na urani imekuwa inapambana na Kundi la Waasi wa M23 linadaiwa kuungwa mkono na Nchi ya Rwanda ambalo limefanikiwa tangu mwanzoni mwa mwaka huu kuchukua udhibiti wa maeneo makubwa upande wa mashariki mwa Nchi hiyo.

    Hapo jana, kundi hilo la Waasi wa M23 limeendelea kufanya mashambulizi na kuingia Mji mdogo wenye utajiri wa madini wa Walikale licha ya mwito wa kusitishwa mapigano uliotolewa na Rais Tshisekedi na mwenzake wa Rwanda Paul Kagame walipokutana Nchini Qatar mapema wiki hii.

    Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo 🇨🇩, Felix Tshisekedi amesema Nchi yake iko tayari kuingia mkataba wa madini na Nchi Marekani 🇺🇸 kwa mabadilishano ya kupatiwa uwezo wa kujilinda dhidi ya Makundi ya Wapiganaji mashariki mwa taifa hilo kama vile kundi la M23 na mengineyo. Akizungumza na kituo cha Televisheni cha Fox News leo asubuhi, Rais huyo amesema makubaliano ya aina hiyo yataiwezesha Nchi ya DR Congo kuchimba madini yake kupitia Kampuni za Marekani huku yenyewe ikinufaika kwa kuimarisha mifumo yake ya ulinzi na usalama. Nchi hiyo yenye utajiri mkubwa wa madini ikiwemo kobalti na urani imekuwa inapambana na Kundi la Waasi wa M23 linadaiwa kuungwa mkono na Nchi ya Rwanda 🇷🇼 ambalo limefanikiwa tangu mwanzoni mwa mwaka huu kuchukua udhibiti wa maeneo makubwa upande wa mashariki mwa Nchi hiyo. Hapo jana, kundi hilo la Waasi wa M23 limeendelea kufanya mashambulizi na kuingia Mji mdogo wenye utajiri wa madini wa Walikale licha ya mwito wa kusitishwa mapigano uliotolewa na Rais Tshisekedi na mwenzake wa Rwanda Paul Kagame walipokutana Nchini Qatar 🇶🇦 mapema wiki hii.
    0 Kommentare ·0 Anteile ·134 Ansichten
  • World Happiness Report 2025 imetangaza orodha ya Nchi zenye furaha zaidi Duniani huku Nchi ya Finland ikiendelea kushika nafasi ya kwanza kwa mwaka wa nane (8) mfululizo, Tanzania imeshika nafasi ya 136 kati ya Nchi 147, ikishuka kwa nafasi tano kutoka nafasi ya 131 mwaka uliopita. Nafasi ya sasa inaiweka Nchi hiyo kuwa miongoni mwa Nchi 11 za mwisho Duniani kwa viwango vya furaha.

    Cha kushangaza ni kwamba Tanzania , licha ya kuwa na amani na utajiri mkubwa wa maliasili, imepitwa hata na mataifa yenye migogoro kama Somalia . Nchi jirani kama Kenya na Uganda , ambazo mara kwa mara hukumbwa na changamoto za kisiasa na kiusalama, zimepata nafasi za juu zaidi. Hapa chini ni orodha ya Nchi zenye furaha kwa mujibu wa World Happiness Report 2025, kuonyesha kumi bora na zilizoshika mkia. Kwa Afrika Mauritius inaongoza, wakati Lebanon , Sierra Leone na Afghanistan ni Nchi tatu za mwisho Duniani.

    1. Finland
    2. Denmark
    3. Iceland
    4. Sweden
    5. Uholanzi

    6. Costa Rica
    7. Norway
    8. Israel
    9. Luxemborg
    10.Mexico

    78. Mauritius
    79. Libya
    84. Algeria
    115. Kenya
    116. Uganda

    122. Somalia
    136. Tanzania
    145. Lebanon
    146. Sierra Leone
    147. Afghanistan

    World Happiness Report 2025 imetangaza orodha ya Nchi zenye furaha zaidi Duniani huku Nchi ya Finland 🇫🇮 ikiendelea kushika nafasi ya kwanza kwa mwaka wa nane (8) mfululizo, Tanzania imeshika nafasi ya 136 kati ya Nchi 147, ikishuka kwa nafasi tano kutoka nafasi ya 131 mwaka uliopita. Nafasi ya sasa inaiweka Nchi hiyo kuwa miongoni mwa Nchi 11 za mwisho Duniani kwa viwango vya furaha. Cha kushangaza ni kwamba Tanzania 🇹🇿, licha ya kuwa na amani na utajiri mkubwa wa maliasili, imepitwa hata na mataifa yenye migogoro kama Somalia 🇸🇴. Nchi jirani kama Kenya 🇰🇪 na Uganda 🇺🇬, ambazo mara kwa mara hukumbwa na changamoto za kisiasa na kiusalama, zimepata nafasi za juu zaidi. Hapa chini ni orodha ya Nchi zenye furaha kwa mujibu wa World Happiness Report 2025, kuonyesha kumi bora na zilizoshika mkia. Kwa Afrika Mauritius 🇲🇷 inaongoza, wakati Lebanon 🇱🇧, Sierra Leone 🇸🇱na Afghanistan 🇦🇫 ni Nchi tatu za mwisho Duniani. 1. Finland 🇫🇮 2. Denmark 🇩🇰 3. Iceland 🇮🇸 4. Sweden 🇸🇪 5. Uholanzi 🇳🇱 6. Costa Rica 🇨🇷 7. Norway 🇳🇴 8. Israel 🇮🇱 9. Luxemborg 🇱🇺 10.Mexico 🇲🇽 78. Mauritius 🇲🇷 79. Libya 🇱🇾 84. Algeria 🇩🇿 115. Kenya 🇰🇪 116. Uganda 🇺🇬 122. Somalia 🇸🇴 136. Tanzania 🇹🇿 145. Lebanon 🇱🇧 146. Sierra Leone 🇸🇱 147. Afghanistan 🇦🇫
    0 Kommentare ·0 Anteile ·184 Ansichten
  • Kwenye barua ambayo Bodi ya Ligi Kuu Tanzania Bara (TPLB) imewajibu Yanga yenye kumbukumbu namba TPLB/2024/625 ya Machi 16,2025 imewaambia Yanga hawawezi kupewa alama tatu kutokana na kuwa hakuna KANUNI ya Ligi Kuu inayoamuru jambo hilo ambapo TPLB imewapa sababu takribani 10, nitazielezea kwa uchache.

    1. Mchezo ulighairishwa na Bodi majira ya saa8 Mchana ambapo baada ya Bodi huo hapakuwa na Afisa yoyote wa mchezo zaidi ya Watu wa Usalama.

    2. Hakuna taratibu zozote za mchezo zilizofanyika uwanjani kwa mujibu wa Kanuni ya 17 ikiwemo timu kukaguliwa na ili timu ipewe alama tatu na mabao matatu ilipaswa ukaguzi kufanyika na Maafisa ww Mchezo.

    3. Bodi ilishindwa kuruhusu mchezo uchezwe sio kwasababu Simba ALIGOMEA mechi bali kupitia Kamati ya Masaa 72 ikaamuru kupitia sababu mbalimbali za Kikanuni kughairisha mchezo huo baada ya kupokea pia ripoti mbalimbali kutoka Maafisa wa mchezo huo.

    4. Yanga SC wameambiwa kwamba hakuna Kanuni inasema Klabu Mgeni anapaswa kuwataarifu wao kwamba wanakuja kufanya mazoezi, hivyo suala la mawasiliano ni MWONGOZO tu wa Bodi hivyo Simba haikuvunja Kanuni kutowasiliana bali ilivunja MIONGOZO.

    5. Yanga SC wamejibiwa kuwa haitowapa alama tatu kwakuwa sababu za kughairisha mchezo zilikuwa ni za kiusalama, ambapo kulikuwa na tuhuma za rushwa, vitisho na kasoro za Kiusalama hivyo ingekuwa ngumu kuruhusu mchezo uendelee ambao ungeleta kasoro, kabla, wakati na baada ya mchezo.

    6. Yanga SC wanalaumiwa na Bodi kitendo cha kupeleka timu uwanjani wakati mechi imeshaghairishwa ni kinyume na Kanuni ya 47(18) na imeonesha kupingana na Mamlaka.

    7. Kuhusu gharama za mchezo ambazo Yanga wameziingia Bodi inasema itazighulikia Kikanuni.

    8. Bodi imewatakia Yanga maandalizi mema ya mchezo ujao wa Derby ambapo watawapangia rasmi tarehe.
    Etc.

    Kwenye barua ambayo Bodi ya Ligi Kuu Tanzania Bara (TPLB) imewajibu Yanga yenye kumbukumbu namba TPLB/2024/625 ya Machi 16,2025 imewaambia Yanga hawawezi kupewa alama tatu kutokana na kuwa hakuna KANUNI ya Ligi Kuu inayoamuru jambo hilo ambapo TPLB imewapa sababu takribani 10, nitazielezea kwa uchache. 1. Mchezo ulighairishwa na Bodi majira ya saa8 Mchana ambapo baada ya Bodi huo hapakuwa na Afisa yoyote wa mchezo zaidi ya Watu wa Usalama. 2. Hakuna taratibu zozote za mchezo zilizofanyika uwanjani kwa mujibu wa Kanuni ya 17 ikiwemo timu kukaguliwa na ili timu ipewe alama tatu na mabao matatu ilipaswa ukaguzi kufanyika na Maafisa ww Mchezo. 3. Bodi ilishindwa kuruhusu mchezo uchezwe sio kwasababu Simba ALIGOMEA mechi bali kupitia Kamati ya Masaa 72 ikaamuru kupitia sababu mbalimbali za Kikanuni kughairisha mchezo huo baada ya kupokea pia ripoti mbalimbali kutoka Maafisa wa mchezo huo. 4. Yanga SC wameambiwa kwamba hakuna Kanuni inasema Klabu Mgeni anapaswa kuwataarifu wao kwamba wanakuja kufanya mazoezi, hivyo suala la mawasiliano ni MWONGOZO tu wa Bodi hivyo Simba haikuvunja Kanuni kutowasiliana bali ilivunja MIONGOZO. 5. Yanga SC wamejibiwa kuwa haitowapa alama tatu kwakuwa sababu za kughairisha mchezo zilikuwa ni za kiusalama, ambapo kulikuwa na tuhuma za rushwa, vitisho na kasoro za Kiusalama hivyo ingekuwa ngumu kuruhusu mchezo uendelee ambao ungeleta kasoro, kabla, wakati na baada ya mchezo. 6. Yanga SC wanalaumiwa na Bodi kitendo cha kupeleka timu uwanjani wakati mechi imeshaghairishwa ni kinyume na Kanuni ya 47(18) na imeonesha kupingana na Mamlaka. 7. Kuhusu gharama za mchezo ambazo Yanga wameziingia Bodi inasema itazighulikia Kikanuni. 8. Bodi imewatakia Yanga maandalizi mema ya mchezo ujao wa Derby ambapo watawapangia rasmi tarehe. Etc.
    0 Kommentare ·0 Anteile ·215 Ansichten
  • Kutoka kwa Mchambuzi wetu Jemedari Said.

    HAKUNA ALAMA 3 ZA MEZANI, YANGA YAAMBIWA INAWEZA KUSHUSHWA DARAJA (47:18)

    Bodi ya Ligi Kuu imeijibu klabu ya Yanga barua yake ambayo ilikuwa pamoja na mambo mengine inataka ipewe alama 3 na mabao 3 kwenye mchezo ulioahirishwa wa tarehe 8 Machi,2025. Katika barua ya tarehe 16 Machi,2025 yenye Kumb.Na TPLB/CEO/2024/625, Bodi inasema mechi ILIAHIRISHWA kwa kufuata kanuni na wala sio kwa sababu Simba SC WALIGOMEA kama ambavyo Yanga walisema.

    Katika barua hiyo ya Bodi yenye kurasa 3 na vipengele 12, Bodi imewaambia Yanga mchezo uliahirishwa rasmi saa 8 mchana baada ya hapo hakukuwa na taratibu zozote kuhusu mchezo huo ambazo ziliendelea, na kwamba maafisa wote wa mchezo ambao walikuwa wakifanya shughuli za mechi Benjamin Mkapa waliondoka isipokuwa wale wa usalama pekee.

    Hakukuwa na taratibu zozote za mchezo zilizoendelea kama zinavyoelezwa kwenye kanuni 17 ambazo zilifanywa ili kuipatia timu iliyopo kiwanjani alama 3 na mabao 3 kikanuni, ikiwemo kukagua timu hiyo, inasomeka sehemu ya barua hiyo ya majibu kwa Yanga SC.

    Klabu yako inapaswa kuelewa kwamba kanuni za ligi Kuu namba 17:45 haisemi popote kwamba klabu mgeni (visiting team) inapaswa kuwasiliana na wadau wengine ili kutimiza takwa la kikanuni la wao kwenda kufanya mazoezi kwenye uwanja utakaochezwa mechi. Imesomeka barua hii ya Bodi.

    Bodi aidha imesema waliita kikao cha dharura cha Kamati ya uendeshaji na usimamizi wa Ligi baada ya kupokea ripoti tofauti tofauti Zenue mfululizo wa matukio uliojenga msingi wa mgogoro uliotokea tarehe 7 Machi,2025 pale Benjamin Mkapa wakati Simba wakitaka kufanya mazoezi.

    Kutokana na umuhimu na unyeti wa taarifa zilizopokelewa, zingine zilitishia usalama, vitisho, tuhuma za rushwa, ambazo zinachukuliwa kwa umuhimu na upekee kwenye soka, Kamati iliona umuhimu wa kuhairisha mechi, ili kuepuka changamoto za kiusalama kabla hazijatokea, kabla au baada ya mechi, ili kujipa muda na pengine kuhusisha vyombo vya kitaifa vya uchunguzi, imesema barua hii ya Bodi kwenda Yanga.

    Kamati iliona matokeo hasi ya kuahirishwa mechi ni madogo kuliko matokeo hasi ambayo yangetokea kwa mechi hiyo kuchezwa.Aidha kwa kupeleka timu kiwanjani Yanga wamekiuka kanuni 47:18.

    Kutoka kwa Mchambuzi wetu Jemedari Said. HAKUNA ALAMA 3 ZA MEZANI, YANGA YAAMBIWA INAWEZA KUSHUSHWA DARAJA (47:18) Bodi ya Ligi Kuu imeijibu klabu ya Yanga barua yake ambayo ilikuwa pamoja na mambo mengine inataka ipewe alama 3 na mabao 3 kwenye mchezo ulioahirishwa wa tarehe 8 Machi,2025. Katika barua ya tarehe 16 Machi,2025 yenye Kumb.Na TPLB/CEO/2024/625, Bodi inasema mechi ILIAHIRISHWA kwa kufuata kanuni na wala sio kwa sababu Simba SC WALIGOMEA kama ambavyo Yanga walisema. Katika barua hiyo ya Bodi yenye kurasa 3 na vipengele 12, Bodi imewaambia Yanga mchezo uliahirishwa rasmi saa 8 mchana baada ya hapo hakukuwa na taratibu zozote kuhusu mchezo huo ambazo ziliendelea, na kwamba maafisa wote wa mchezo ambao walikuwa wakifanya shughuli za mechi Benjamin Mkapa waliondoka isipokuwa wale wa usalama pekee. Hakukuwa na taratibu zozote za mchezo zilizoendelea kama zinavyoelezwa kwenye kanuni 17 ambazo zilifanywa ili kuipatia timu iliyopo kiwanjani alama 3 na mabao 3 kikanuni, ikiwemo kukagua timu hiyo, inasomeka sehemu ya barua hiyo ya majibu kwa Yanga SC. Klabu yako inapaswa kuelewa kwamba kanuni za ligi Kuu namba 17:45 haisemi popote kwamba klabu mgeni (visiting team) inapaswa kuwasiliana na wadau wengine ili kutimiza takwa la kikanuni la wao kwenda kufanya mazoezi kwenye uwanja utakaochezwa mechi. Imesomeka barua hii ya Bodi. Bodi aidha imesema waliita kikao cha dharura cha Kamati ya uendeshaji na usimamizi wa Ligi baada ya kupokea ripoti tofauti tofauti Zenue mfululizo wa matukio uliojenga msingi wa mgogoro uliotokea tarehe 7 Machi,2025 pale Benjamin Mkapa wakati Simba wakitaka kufanya mazoezi. Kutokana na umuhimu na unyeti wa taarifa zilizopokelewa, zingine zilitishia usalama, vitisho, tuhuma za rushwa, ambazo zinachukuliwa kwa umuhimu na upekee kwenye soka, Kamati iliona umuhimu wa kuhairisha mechi, ili kuepuka changamoto za kiusalama kabla hazijatokea, kabla au baada ya mechi, ili kujipa muda na pengine kuhusisha vyombo vya kitaifa vya uchunguzi, imesema barua hii ya Bodi kwenda Yanga. Kamati iliona matokeo hasi ya kuahirishwa mechi ni madogo kuliko matokeo hasi ambayo yangetokea kwa mechi hiyo kuchezwa.Aidha kwa kupeleka timu kiwanjani Yanga wamekiuka kanuni 47:18.
    Like
    1
    · 0 Kommentare ·0 Anteile ·214 Ansichten
  • "Msimu uliyopita Zamalek aligomea mechi dhidi ya Al Ahly, Mamlaka za soka nchini Misri zikampa ushindi Al Ahly wa mabao mawili na alama zake tatu kisha wakailima Zamalek alama tatu na timu ikashuka mpaka nafasi ya 12 kama sikosei, Bodi na Chama wala hakikuwaza mara mbili, ni kesi kubwa sana kwenye dunia ya soka kukacha mechi.

    Jana, Al Ahly nae kaleta mbwembwe zile zile za masuala ya Kanuni akagomea mchezo, akasahau kanuni ya kutokea Uwanjani na kucheza mechi ndio kanuni yenye maana zaidi kwenye soka, amejikuta anapoteza alama tatu na mabao matatu kwa Zamalek, Kanuni hii inaweza kusema hivi ila Kanuni nyingine ikawa na maelezo mengine.

    Nikukumbushe tu Al Ahly aliyeadhibiwa ndio Klabu Tajiri zaidi Afrika, Klabu yenye Mashabiki na Wanachama wengi zaidi Afrika, ndio Klabu ya pili kwa Mataji mengi duniani baada ya Real Madrid, ila huko Misri watu hawatazami makunyanzi, ukileta maksudi, Bodi na Chama cha soka zinakufanyia bahati mbaya, Ahly inatajwa pia ina nguvu kubwa sana CAF, sio ya kufikirika ama nadharia ndio uhalisia ila wamepita nayo mapema tu.

    Nawakumbusha tena Watu wangu HAKI huenda na WAJIBU, mfano Tanzania kwa mujibu wa Katiba kuandamana ni haki yako ila unapaswa kutoa taarifa kwa Polisi masaa 72 kabla, umeelewa hapo? Ni haki yako ila huja na Wajibu, Kanuni ili ikulinde hakikisha umetekeleza Wajibu, biashara za Mamlaka za soka duniani ni mpira, kutocheza mpira ni kuzitusi, hazikuachi salama.

    Ni haki yako kuja kufanya mazoezi uwanja wa mechi siku moja kabla ila ni Wajibu wako kunijulisha kuwa nakuja, ili nikuandalie mazingira, huenda narekebisha mfumo wa Umeme? Huenda hali ya usalama sio shwari, huenda nimepulizia dawa za dudu zinaweka kukuathiri, yaani ni HAKI yako ila una WAJIBU wako huu ni mfano tu.

    Mnasemaje Watu wangu wa nchini Yemen haya hayawahusu sana, huko kwenu Kivyenu vyenu Wayemen" - Farhan JR, Mchambuzi.

    "Msimu uliyopita Zamalek aligomea mechi dhidi ya Al Ahly, Mamlaka za soka nchini Misri zikampa ushindi Al Ahly wa mabao mawili na alama zake tatu kisha wakailima Zamalek alama tatu na timu ikashuka mpaka nafasi ya 12 kama sikosei, Bodi na Chama wala hakikuwaza mara mbili, ni kesi kubwa sana kwenye dunia ya soka kukacha mechi. Jana, Al Ahly nae kaleta mbwembwe zile zile za masuala ya Kanuni akagomea mchezo, akasahau kanuni ya kutokea Uwanjani na kucheza mechi ndio kanuni yenye maana zaidi kwenye soka, amejikuta anapoteza alama tatu na mabao matatu kwa Zamalek, Kanuni hii inaweza kusema hivi ila Kanuni nyingine ikawa na maelezo mengine. Nikukumbushe tu Al Ahly aliyeadhibiwa ndio Klabu Tajiri zaidi Afrika, Klabu yenye Mashabiki na Wanachama wengi zaidi Afrika, ndio Klabu ya pili kwa Mataji mengi duniani baada ya Real Madrid, ila huko Misri watu hawatazami makunyanzi, ukileta maksudi, Bodi na Chama cha soka zinakufanyia bahati mbaya, Ahly inatajwa pia ina nguvu kubwa sana CAF, sio ya kufikirika ama nadharia ndio uhalisia ila wamepita nayo mapema tu. Nawakumbusha tena Watu wangu HAKI huenda na WAJIBU, mfano Tanzania kwa mujibu wa Katiba kuandamana ni haki yako ila unapaswa kutoa taarifa kwa Polisi masaa 72 kabla, umeelewa hapo? Ni haki yako ila huja na Wajibu, Kanuni ili ikulinde hakikisha umetekeleza Wajibu, biashara za Mamlaka za soka duniani ni mpira, kutocheza mpira ni kuzitusi, hazikuachi salama. Ni haki yako kuja kufanya mazoezi uwanja wa mechi siku moja kabla ila ni Wajibu wako kunijulisha kuwa nakuja, ili nikuandalie mazingira, huenda narekebisha mfumo wa Umeme? Huenda hali ya usalama sio shwari, huenda nimepulizia dawa za dudu zinaweka kukuathiri, yaani ni HAKI yako ila una WAJIBU wako huu ni mfano tu. Mnasemaje Watu wangu wa nchini Yemen haya hayawahusu sana, huko kwenu Kivyenu vyenu Wayemen😀" - Farhan JR, Mchambuzi.
    Like
    1
    · 0 Kommentare ·0 Anteile ·238 Ansichten
  • Taarifa kutoka Nchini Angola zinadai kuwa Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo , Felix Tshisekedi anatarajia kukutana na Waasi cha M23, Jijini Luanda Nchini Angola. Taarifa hii kwa mujibu wa Ofisi ya Rais wa Angola.

    Bado hakijafahamika lini na Pande hizo mbili zitatakutana Nchini humo lakini taarifa hiyo inasema kuwa siku chache zijazo Rais wa Félix Tshisekedi atakutana na Waasi hao ili kutatua tatizo la usalama mdogo Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

    Taarifa kutoka Nchini Angola 🇦🇴 zinadai kuwa Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo 🇨🇩, Felix Tshisekedi anatarajia kukutana na Waasi cha M23, Jijini Luanda Nchini Angola. Taarifa hii kwa mujibu wa Ofisi ya Rais wa Angola. Bado hakijafahamika lini na Pande hizo mbili zitatakutana Nchini humo lakini taarifa hiyo inasema kuwa siku chache zijazo Rais wa Félix Tshisekedi atakutana na Waasi hao ili kutatua tatizo la usalama mdogo Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
    Like
    1
    · 0 Kommentare ·0 Anteile ·163 Ansichten
  • Jeshi la Polisi katika Kaunti ya Uasin Gishu Nchini Kenya wameanzisha uchunguzi baada ya Mwanamume mmoja kuanzisha kituo kidogo cha Polisi kinyume cha sheria na bila idhini ya mamlaka Nchini humo. Ripoti zinasema kuwa Mwanaume huyo wa Kijiji cha Asis alijipa jukumu la kufungua kituo hicho na kupaka rangi rasmi za Jeshi la Polisi

    Mamlaka bado hazijabaini sababu za Mshukiwa kuanzisha kituo hicho na amekamatwa kwa uchunguzi zaidi huku Wananchi wa eneo hilo wakishindwa kubaini kuwa kituo hicho kilikuwa "feki" badala yake waliendelea kupatiwa huduma wakidhani kuwa Jeshi la Polisi limesogezea huduma hiyo karibu ili kulinda usalama wa eneo hilo.

    Jeshi la Polisi katika Kaunti ya Uasin Gishu Nchini Kenya 🇰🇪 wameanzisha uchunguzi baada ya Mwanamume mmoja kuanzisha kituo kidogo cha Polisi kinyume cha sheria na bila idhini ya mamlaka Nchini humo. Ripoti zinasema kuwa Mwanaume huyo wa Kijiji cha Asis alijipa jukumu la kufungua kituo hicho na kupaka rangi rasmi za Jeshi la Polisi Mamlaka bado hazijabaini sababu za Mshukiwa kuanzisha kituo hicho na amekamatwa kwa uchunguzi zaidi huku Wananchi wa eneo hilo wakishindwa kubaini kuwa kituo hicho kilikuwa "feki" badala yake waliendelea kupatiwa huduma wakidhani kuwa Jeshi la Polisi limesogezea huduma hiyo karibu ili kulinda usalama wa eneo hilo.
    Like
    1
    · 0 Kommentare ·0 Anteile ·248 Ansichten
  • Nikueleze kwa kifupi sana kiini cha mgogoro. Kabla ya mwaka 1991 Ukraine ilikua sehemu ya Urusi kupitia muungano wa kisovieti wa USSR. Baada ya USSR kufa ndipo taifa la Ukraine likazaliwa pamoja na mataifa mengine 14 yaliyokua majimbo ya Urusi.

    Lakini usisahau mwaka 1949 umoja wa kujihami wa nchi za magharibi (NATO) ulianzishwa dhidi ya Urusi (USSR). Makubaliano yao ni kwamba ikiwa Urusi itamgusa mmoja wao basi wote watamvamia. Marekani akiwa kinara.

    Kuanguka kwa USSR kukafanya mataifa 15 mapya kuzaliwa. Baadhi ya Mataifa hayo yakawa na hofu kuwa Urusi inaweza kurudi kuyakalia kimabavu. Kwahiyo yakaomba kujiunga NATO kwa usalama wao. Estonia, Latvia na Lithuania zikapata uanachana wa NATO chap kwa haraka. Ukraine ilipoomba uanachama Urusi ikakataa, kwa sababu ya strategic position ya Ukraine ambayo inaiweka Urusi hatarini.

    Ukraine ilipokosa uanachama NATO ikamua kujilinda kwa kusuka mpango wa nyuklia. Marekani na Urusi zikashtuka. Kwa kutambua hatari ya nyuklia zikamsihi sana Ukraine aachane na mpango huo. Mwaka 1994 ukaandaliwa mkataba uitwao Budapest memorundum, huko Hungary. Mkataba huo ulihusisha nchi 4. Urusi na Ukraine zilisaini kwamba hakuna atakayemvamia mwenzake. Marekani na Uingereza zikasaini kwamba atakayemvamia mwenzake watampiga bila huruma. Pia Marekani na Uingereza zitagharamia fedha na vifaa vyote vya vita. Mkataba ukasainiwa na Ukraine ikasitisha mpango wake wa nyuklia.

    Lakini Mwaka 2014 Urusi ikaivamia Ukraine na kuchukua jimbo lake la Crimea kimabavu. Marekani na Uingereza hazikuipiga Urusi kama mkataba wa Budapest unavyosema. Ukraine akalalamika lakini akapuuzwa. Kwenye vita inayoendelea sasa, Urusi ameshajitwalia majimbo manne Donetsk, Luhansk, Zaporizhzhia na Kherson lakini Marekani na Uingereza ziko kimya.

    Ukraine inaona imesalitiwa. Mkataba wa Budapest ulikua kiini macho. Laiti Ukraine ingekataa kusaini na kuendelea na mpango wake wa nyuklia, leo Urusi isingethubutu kuigusa. Lakini Waliomdanganya sasa wamemgeuka na wanamfokea. Ukraine ingeyajua maneno ya Mzee Jomo Kenyatta "Learn to fight your own battle" isingeachana na mpango wake wa nyuklia mwaka 1994. Wangejifunza kupigana vita yao wenyewe bila kutegemea mtu.!
    (Malisa GJ)

    Nikueleze kwa kifupi sana kiini cha mgogoro. Kabla ya mwaka 1991 Ukraine ilikua sehemu ya Urusi kupitia muungano wa kisovieti wa USSR. Baada ya USSR kufa ndipo taifa la Ukraine likazaliwa pamoja na mataifa mengine 14 yaliyokua majimbo ya Urusi. Lakini usisahau mwaka 1949 umoja wa kujihami wa nchi za magharibi (NATO) ulianzishwa dhidi ya Urusi (USSR). Makubaliano yao ni kwamba ikiwa Urusi itamgusa mmoja wao basi wote watamvamia. Marekani akiwa kinara. Kuanguka kwa USSR kukafanya mataifa 15 mapya kuzaliwa. Baadhi ya Mataifa hayo yakawa na hofu kuwa Urusi inaweza kurudi kuyakalia kimabavu. Kwahiyo yakaomba kujiunga NATO kwa usalama wao. Estonia, Latvia na Lithuania zikapata uanachana wa NATO chap kwa haraka. Ukraine ilipoomba uanachama Urusi ikakataa, kwa sababu ya strategic position ya Ukraine ambayo inaiweka Urusi hatarini. Ukraine ilipokosa uanachama NATO ikamua kujilinda kwa kusuka mpango wa nyuklia. Marekani na Urusi zikashtuka. Kwa kutambua hatari ya nyuklia zikamsihi sana Ukraine aachane na mpango huo. Mwaka 1994 ukaandaliwa mkataba uitwao Budapest memorundum, huko Hungary. Mkataba huo ulihusisha nchi 4. Urusi na Ukraine zilisaini kwamba hakuna atakayemvamia mwenzake. Marekani na Uingereza zikasaini kwamba atakayemvamia mwenzake watampiga bila huruma. Pia Marekani na Uingereza zitagharamia fedha na vifaa vyote vya vita. Mkataba ukasainiwa na Ukraine ikasitisha mpango wake wa nyuklia. Lakini Mwaka 2014 Urusi ikaivamia Ukraine na kuchukua jimbo lake la Crimea kimabavu. Marekani na Uingereza hazikuipiga Urusi kama mkataba wa Budapest unavyosema. Ukraine akalalamika lakini akapuuzwa. Kwenye vita inayoendelea sasa, Urusi ameshajitwalia majimbo manne Donetsk, Luhansk, Zaporizhzhia na Kherson lakini Marekani na Uingereza ziko kimya. Ukraine inaona imesalitiwa. Mkataba wa Budapest ulikua kiini macho. Laiti Ukraine ingekataa kusaini na kuendelea na mpango wake wa nyuklia, leo Urusi isingethubutu kuigusa. Lakini Waliomdanganya sasa wamemgeuka na wanamfokea. Ukraine ingeyajua maneno ya Mzee Jomo Kenyatta "Learn to fight your own battle" isingeachana na mpango wake wa nyuklia mwaka 1994. Wangejifunza kupigana vita yao wenyewe bila kutegemea mtu.! (Malisa GJ)
    Like
    1
    · 0 Kommentare ·0 Anteile ·508 Ansichten
  • Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo , Félix Tshisekedi, amemshutumu kwa mara nyingine tena Mtangulizi wake Joseph Kabila kuwa anaunga mkono Kundi la Waasi la M23. Mnamo Agosti 2024, Tshisekedi alidai kuwa Kabila alikuwa nyuma ya kuunganishwa kwa muungano wa Wakuu wa kisiasa wa (AFC) unaoongozwa na Corneille Nangaa na Wapiganaji wa kundi la M23.

    Katika mahojiano, Tshisekedi alisema sababu iliyofanya Kabila kutoshiriki uchaguzi wa Desemba 2024 ni kwa sababu alikuwa na shughuli nyingi na AFC.

    “Tusimzungumzie Joseph Kabila. Amekataa kabisa kugombea uchaguzi na anajipanga kupambana na serikali kwa sababu yeye ni AFC.” - alisema Tshisekedi

    Rais huyo ameyasema hayo tena katika Baraza la Usalama la Kimataifa Mjini Munich Nchini Ujerumani Februari 14, 2025, ya kwamba Kabila alienda uhamishoni kwa sababu anafadhili Waasi wa (AFC) ikiwemo Kundi la Waasi la M23.

    Hata hivyo, Chama cha Joseph Kabila cha (PPRD) kimekanusha vikali matamshi ya Rais Félix Tshisekedi kwa kusema kuwa Kiongozi wao hausiki na Kundi hilo la Waasi.

    Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo 🇨🇩, Félix Tshisekedi, amemshutumu kwa mara nyingine tena Mtangulizi wake Joseph Kabila kuwa anaunga mkono Kundi la Waasi la M23. Mnamo Agosti 2024, Tshisekedi alidai kuwa Kabila alikuwa nyuma ya kuunganishwa kwa muungano wa Wakuu wa kisiasa wa (AFC) unaoongozwa na Corneille Nangaa na Wapiganaji wa kundi la M23. Katika mahojiano, Tshisekedi alisema sababu iliyofanya Kabila kutoshiriki uchaguzi wa Desemba 2024 ni kwa sababu alikuwa na shughuli nyingi na AFC. “Tusimzungumzie Joseph Kabila. Amekataa kabisa kugombea uchaguzi na anajipanga kupambana na serikali kwa sababu yeye ni AFC.” - alisema Tshisekedi Rais huyo ameyasema hayo tena katika Baraza la Usalama la Kimataifa Mjini Munich Nchini Ujerumani 🇩🇪 Februari 14, 2025, ya kwamba Kabila alienda uhamishoni kwa sababu anafadhili Waasi wa (AFC) ikiwemo Kundi la Waasi la M23. Hata hivyo, Chama cha Joseph Kabila cha (PPRD) kimekanusha vikali matamshi ya Rais Félix Tshisekedi kwa kusema kuwa Kiongozi wao hausiki na Kundi hilo la Waasi.
    Like
    1
    · 0 Kommentare ·0 Anteile ·384 Ansichten
  • Kundi la Waasi wa M23 wameingia Mjini Bukavu Mkoani Sud-Kivu ambao ni Mji wa pili (2) kwa ukubwa mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo wakati huo huo Rais wa Nchi Tshisekedi yupo zake Jijini Munich Nchini Ujerumani kwenye kikao cha usalama.

    Kundi la Waasi wa M23 wameingia Mjini Bukavu Mkoani Sud-Kivu ambao ni Mji wa pili (2) kwa ukubwa mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo 🇨🇩 wakati huo huo Rais wa Nchi Tshisekedi yupo zake Jijini Munich Nchini Ujerumani 🇩🇪 kwenye kikao cha usalama.
    Like
    Love
    2
    · 1 Kommentare ·0 Anteile ·231 Ansichten
  • Aliacha historria (John Jones) ni onyo kali kwa wale wanaopenda mapango.

    Kamwe usipite kwenye sehemu nyembamba sana bila uhakika wa kutoka.

    Hakikisha unakuwa na vifaa vya kutosha vya usalama.

    Usijaribu kupita kwenye njia usizozifahamu vizuri.

    Na zaidi ya yote, uhai ni wa thamani kuliko ujasiri.

    Nutty Putty Cave inabaki kuwa kaburi lililofungwa, na watu wengi wakiogopa hata kufikiria juu yake.
    Aliacha historria (John Jones) ni onyo kali kwa wale wanaopenda mapango. Kamwe usipite kwenye sehemu nyembamba sana bila uhakika wa kutoka. Hakikisha unakuwa na vifaa vya kutosha vya usalama. Usijaribu kupita kwenye njia usizozifahamu vizuri. Na zaidi ya yote, uhai ni wa thamani kuliko ujasiri. Nutty Putty Cave inabaki kuwa kaburi lililofungwa, na watu wengi wakiogopa hata kufikiria juu yake.
    Like
    1
    · 0 Kommentare ·0 Anteile ·294 Ansichten
  • Rais wa Urusi , Vladimir Putin amewaalika Rais China , Xi Jinping na Rais wa Marekani , Donald Trump kuhudhuria sherehe maarufu za Ushindi wa Urusi katika vita kuu ya pili ya Dunia (Russia’s Victory Parade) zitakazofanyika tarehe 9 Mwezi May Jijini Moscow Nchini Urusi. Mwaliko huu unatokana na ombi la Rais Donald Trump la tarehe 11 Feb 2025 alipoomba kuzuru Moscow kwa lengo la kumaliza mgogoro wa Ukraine, Kikao kilichotokana na ombi hili kilifanywa kwa njia ya simu ambapo pamoja na mambo mengine, Trump alimhakikishia Putin kwamba Marekani itaacha ufadhili wa kijeshi kwa Ukraine na pia Ukraine itaachia sehemu ya ardhi yake iliyotwaliwa kama dhamana ya usalama wake dhidi ya Moscow.

    Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Washington katika taarifa yake ilikazia na kusisitiza kile alichokizungumza Trump na Moscow na kwamba Marekani inakusudia kumaliza tofauti zao kidunia. Utawala wa Trump umekuwa na juhudi kubwa kumaliza mizozo mikubwa duniani ambayo Ikulu hiyo ilikuwa ikifadhili na kuanzisha uchokozi kwa muda mrefu, Ukiachiliambali mgogoro wa Ukraine, pia Washington inashughulika kumaliza mgogoro wa Mashariki ya Kati huko Gaza ambapo mamia ya watu wameuawa kwa ufadhili wa Marekani hiyohiyo.

    Rais wa Urusi 🇷🇺, Vladimir Putin amewaalika Rais China 🇨🇳, Xi Jinping na Rais wa Marekani 🇺🇸, Donald Trump kuhudhuria sherehe maarufu za Ushindi wa Urusi katika vita kuu ya pili ya Dunia (Russia’s Victory Parade) zitakazofanyika tarehe 9 Mwezi May Jijini Moscow Nchini Urusi. Mwaliko huu unatokana na ombi la Rais Donald Trump la tarehe 11 Feb 2025 alipoomba kuzuru Moscow kwa lengo la kumaliza mgogoro wa Ukraine, Kikao kilichotokana na ombi hili kilifanywa kwa njia ya simu ambapo pamoja na mambo mengine, Trump alimhakikishia Putin kwamba Marekani itaacha ufadhili wa kijeshi kwa Ukraine na pia Ukraine itaachia sehemu ya ardhi yake iliyotwaliwa kama dhamana ya usalama wake dhidi ya Moscow. Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Washington katika taarifa yake ilikazia na kusisitiza kile alichokizungumza Trump na Moscow na kwamba Marekani inakusudia kumaliza tofauti zao kidunia. Utawala wa Trump umekuwa na juhudi kubwa kumaliza mizozo mikubwa duniani ambayo Ikulu hiyo ilikuwa ikifadhili na kuanzisha uchokozi kwa muda mrefu, Ukiachiliambali mgogoro wa Ukraine, pia Washington inashughulika kumaliza mgogoro wa Mashariki ya Kati huko Gaza ambapo mamia ya watu wameuawa kwa ufadhili wa Marekani hiyohiyo.
    Like
    1
    · 0 Kommentare ·0 Anteile ·463 Ansichten
  • Rais wa Rwanda , Paul Kagame ameweka wazi kuwa hana hofu na vitisho vya vikwazo vinavyotolewa na Mataifa ya Magharibi dhidi ya Nchi yake akisisitiza kuwa Rwanda itachukua hatua zozote zinazohitajika kulinda maslahi yake, akizungumza na Gazeti la Jeune Afrique, Kagame amezungumzia kwa kina mzozo kati ya Rwanda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo pamoja na shinikizo kutoka Ulaya na Marekani .

    Kagame amesisitiza kuwa hatakubali mashinikizo yanayoelekezwa kwa Rwanda kwa lengo la kuidhoofisha akisema Nchi yake inayo haki ya kujilinda dhidi ya vitisho vyovyote vya nje ambapo Mataifa ya Magharibi yanaishutumu Rwanda kwa kuwaunga mkono kundi la Waasi wa M23 wanaopigana mashariki mwa DR Congo jambo ambalo Rwanda imekanusha mara kadhaa.

    Kauli Kagame inakuja wakati mvutano kati ya Rwanda na DR Congo ukiendelea huku mataifa ya Magharibi yakitoa wito wa mazungumzo ya amani lakini licha ya hivyo Rwanda imeendelea kusisitiza kuwa haitakubali kushinikizwa kwa njia yoyote ikibainisha kuwa hatua zake zitalenga kulinda usalama wa Taifa lake kwa gharama yoyote.
    (DW Swahili)

    Rais wa Rwanda 🇷🇼, Paul Kagame ameweka wazi kuwa hana hofu na vitisho vya vikwazo vinavyotolewa na Mataifa ya Magharibi dhidi ya Nchi yake akisisitiza kuwa Rwanda itachukua hatua zozote zinazohitajika kulinda maslahi yake, akizungumza na Gazeti la Jeune Afrique, Kagame amezungumzia kwa kina mzozo kati ya Rwanda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo 🇨🇩 pamoja na shinikizo kutoka Ulaya na Marekani 🇺🇸. Kagame amesisitiza kuwa hatakubali mashinikizo yanayoelekezwa kwa Rwanda kwa lengo la kuidhoofisha akisema Nchi yake inayo haki ya kujilinda dhidi ya vitisho vyovyote vya nje ambapo Mataifa ya Magharibi yanaishutumu Rwanda kwa kuwaunga mkono kundi la Waasi wa M23 wanaopigana mashariki mwa DR Congo jambo ambalo Rwanda imekanusha mara kadhaa. Kauli Kagame inakuja wakati mvutano kati ya Rwanda na DR Congo ukiendelea huku mataifa ya Magharibi yakitoa wito wa mazungumzo ya amani lakini licha ya hivyo Rwanda imeendelea kusisitiza kuwa haitakubali kushinikizwa kwa njia yoyote ikibainisha kuwa hatua zake zitalenga kulinda usalama wa Taifa lake kwa gharama yoyote. (DW Swahili)
    Love
    1
    · 0 Kommentare ·0 Anteile ·334 Ansichten
  • Rais wa Nchi ya Rwanda , Paul Kagame ameendelea kukanusha madai kuwa wao kuwa ndiyo chanzo cha mgogoro wa Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kwa kusema kuwa huo ni mgogoro wa ndani ya DR Congo na hautoki nje ya Congo na suluhu lazima itoke kwa Serikali ya Nchi hiyo.

    Ikumbukwe kwamba Rais Paul Kagame alihudhuria mkutano wa Marais wa Afrika Mashariki na Kusini mwa Afrika Febuari 8,2025 uliojadili namna gani ya kurudisha usalama Nchini DR Congo ambapo Waasi wa kundi la M23 wameiteka Mkoa wa Kivu Kaskazini.

    Rais wa Nchi ya Rwanda 🇷🇼, Paul Kagame ameendelea kukanusha madai kuwa wao kuwa ndiyo chanzo cha mgogoro wa Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo 🇨🇩 kwa kusema kuwa huo ni mgogoro wa ndani ya DR Congo na hautoki nje ya Congo na suluhu lazima itoke kwa Serikali ya Nchi hiyo. Ikumbukwe kwamba Rais Paul Kagame alihudhuria mkutano wa Marais wa Afrika Mashariki na Kusini mwa Afrika Febuari 8,2025 uliojadili namna gani ya kurudisha usalama Nchini DR Congo ambapo Waasi wa kundi la M23 wameiteka Mkoa wa Kivu Kaskazini.
    0 Kommentare ·0 Anteile ·246 Ansichten
  • Hii joint meeting imehudhuriwa na viongozi karibu wote wa SADC na EAC kwa kutambua umuhimu wake kwa usalama eneo la maziwa makuu.

    Viongozi hawa wanajua kuwa usalama wa eneo hili ni muhimu kwa ustawi wa kanda nzima, hasa ikizingatiwa mizozo ya muda mrefu kama ile ya Mashariki mwa DRC.

    Lakini pia hata viongozi ambao nchi zao zimekuwa kwenye msuguano kwenye mgogoro wa Congo wamehushuria. Paul Kagame wa Rwanda na Cyril Ramaphosa wa Afrika Kusini wamehudhuria pia.

    Wote tunakumbuka kwamba hivi karibuni Kagame na Ramaphosa walikuwa kwenye uhasama hawa kwa sababu ya tuhuma zinazoelekewa kwa Rwanda kwamba wanawaunda mkono M23, kundi la waasi linalohusishwa na kuvuruga amani Mashariki mwa DRC.

    Hata hivyo, Tshisekedi ameshindwa kuona umuhimu wa mkutano huu mpaka kumtuma mwakilishi badala yake?

    Hii inaashiria kutokuwa na ushirikiano wa kutosha au kutokubaliana na juhudi za kutatua mgogoro huu kwa njia ya kidiplomasia.

    Is this a sign of deeper political divisions within the DRC or a strategic move to maintain sovereignty?..
    Hii joint meeting imehudhuriwa na viongozi karibu wote wa SADC na EAC kwa kutambua umuhimu wake kwa usalama eneo la maziwa makuu. Viongozi hawa wanajua kuwa usalama wa eneo hili ni muhimu kwa ustawi wa kanda nzima, hasa ikizingatiwa mizozo ya muda mrefu kama ile ya Mashariki mwa DRC. Lakini pia hata viongozi ambao nchi zao zimekuwa kwenye msuguano kwenye mgogoro wa Congo wamehushuria. Paul Kagame wa Rwanda na Cyril Ramaphosa wa Afrika Kusini wamehudhuria pia. Wote tunakumbuka kwamba hivi karibuni Kagame na Ramaphosa walikuwa kwenye uhasama hawa kwa sababu ya tuhuma zinazoelekewa kwa Rwanda kwamba wanawaunda mkono M23, kundi la waasi linalohusishwa na kuvuruga amani Mashariki mwa DRC. Hata hivyo, Tshisekedi ameshindwa kuona umuhimu wa mkutano huu mpaka kumtuma mwakilishi badala yake? Hii inaashiria kutokuwa na ushirikiano wa kutosha au kutokubaliana na juhudi za kutatua mgogoro huu kwa njia ya kidiplomasia. Is this a sign of deeper political divisions within the DRC or a strategic move to maintain sovereignty?..
    0 Kommentare ·0 Anteile ·472 Ansichten
  • Kwa nini rais wa Congo, Félix Tshisekedi, hakudhuria huu mkutano huu muhimu wa kujadili mambo ya kiusalama ndani ya nchi yake ya Congo?

    Hakuna excuse inayoweza kuelezea dharau na kukosa heshima ambayo amezionyesha taasisi hizi mbili—EAC & SADC.

    Shuka nayo
    Kwa nini rais wa Congo, Félix Tshisekedi, hakudhuria huu mkutano huu muhimu wa kujadili mambo ya kiusalama ndani ya nchi yake ya Congo? Hakuna excuse inayoweza kuelezea dharau na kukosa heshima ambayo amezionyesha taasisi hizi mbili—EAC & SADC. Shuka nayo ⤵️
    0 Kommentare ·0 Anteile ·269 Ansichten
  • Kwa mujibu wa wa kiongozi mkuu wa Korea Kaskazini Kim Jong Un , migogoro inayochochewa na Marekani katika sehemu mbalimbali za dunia, "inazidi kuongeza hatari ya kuzuka kwa vita vya dunia vipya vyenye athari kubwa sio tu kwa amani na usalama wa kimataifa bali pia nyanja nyingine zote za shughuli za binadamu."

    Pia Kim alitoa maoni kwamba mwaka 2025, mzozo wa Ukraine utasalia kuwa moja ya "mhimili mkuu wa hali ya wasiwasi ya kimataifa," nyingine ikiwa hali katika Ukanda wa Gaza na Syria "ambayo imekuwa uwanja wa migogoro ya kijiografia na makabiliano ya kimataifa mwaka jana."

    Katika hatua nyingine Kim alisema Marekani na nchi za Magharibi zinaelezea mzozo wa Ukraine kwa kushindwa kuishinda Urusi kimkakati, kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un alisema, kama ilivyonukuliwa na Shirika la Habari la Korea (KCNA).

    Katika mkutano katika Wizara ya Ulinzi, kuadhimisha kumbukumbu ya miaka 77 ya Jeshi la Wananchi wa Korea, alidai kwamba Marekani imepofushwa na tamaa mbaya huku akiionyesha wasiwasi mkubwa juu ya tabia ya kutojali ya Marekani na kundi la Magharibi kwa makusudi kuendeleza vita vya muda mrefu kwa ndoto isiyoweza kutekelezwa ili kukabiliana na kurudi kwa kimkakati kwa Urusi," shirika la habari lilibainisha.

    Kim alidokeza kuwa Pyongyang imekuwa ikipinga kila mara "kitendo chochote cha kunyima haki ya kimataifa na kuvuruga amani na usalama duniani." Aliongeza kuwa nchi yake "itaunga mkono kila wakati na kuhimiza sababu ya haki ya jeshi la Urusi na watu kutetea uhuru wao, usalama na uadilifu wa eneo kwa kuzingatia ari ya mkataba juu ya ushirikiano wa kimkakati wa kina kati ya DPRK na Urusi."
    (Zungu)

    Kwa mujibu wa wa kiongozi mkuu wa Korea Kaskazini Kim Jong Un , migogoro inayochochewa na Marekani katika sehemu mbalimbali za dunia, "inazidi kuongeza hatari ya kuzuka kwa vita vya dunia vipya vyenye athari kubwa sio tu kwa amani na usalama wa kimataifa bali pia nyanja nyingine zote za shughuli za binadamu." Pia Kim alitoa maoni kwamba mwaka 2025, mzozo wa Ukraine utasalia kuwa moja ya "mhimili mkuu wa hali ya wasiwasi ya kimataifa," nyingine ikiwa hali katika Ukanda wa Gaza na Syria "ambayo imekuwa uwanja wa migogoro ya kijiografia na makabiliano ya kimataifa mwaka jana." Katika hatua nyingine Kim alisema Marekani na nchi za Magharibi zinaelezea mzozo wa Ukraine kwa kushindwa kuishinda Urusi kimkakati, kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un alisema, kama ilivyonukuliwa na Shirika la Habari la Korea (KCNA). Katika mkutano katika Wizara ya Ulinzi, kuadhimisha kumbukumbu ya miaka 77 ya Jeshi la Wananchi wa Korea, alidai kwamba Marekani imepofushwa na tamaa mbaya huku akiionyesha wasiwasi mkubwa juu ya tabia ya kutojali ya Marekani na kundi la Magharibi kwa makusudi kuendeleza vita vya muda mrefu kwa ndoto isiyoweza kutekelezwa ili kukabiliana na kurudi kwa kimkakati kwa Urusi," shirika la habari lilibainisha. Kim alidokeza kuwa Pyongyang imekuwa ikipinga kila mara "kitendo chochote cha kunyima haki ya kimataifa na kuvuruga amani na usalama duniani." Aliongeza kuwa nchi yake "itaunga mkono kila wakati na kuhimiza sababu ya haki ya jeshi la Urusi na watu kutetea uhuru wao, usalama na uadilifu wa eneo kwa kuzingatia ari ya mkataba juu ya ushirikiano wa kimkakati wa kina kati ya DPRK na Urusi." (Zungu)
    0 Kommentare ·0 Anteile ·755 Ansichten
  • Maazimio (22) ya Marais wa Nchi Wanachama wa SADC na EAC kwenye mkutano uliofanyika leo hii Jijini Dar Es Salaam, Tanzania , Azimio la (12) limewataka Wakuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama wa Nchi zote Wanachama kukutana ndani ya siku tano (5) na kutoa mwelekeo wa kitalaam kuhusu mambo yafuatayo:

    - Kusitisha mara moja mapigano huko Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia Congo .

    - Kutoa misaada ya Kibinadamu na kuwasaidia Wahanga wa vita.

    - Kutoa mpango kazi wa ulinzi ndani ya Mji wa Goma na maeneo Jirani.

    - Kuzifungua njia muhimu za mawasiliano kwenye Miji ya Goma - Kibumba- Rumangambo - Kalengera- Rutshuru na Goma - Kiwanja- Rwindi lakini pia matumizi ya Ziwa Kivu kwa ajili ya usafiri.

    - Kuufungua Uwanja wa Ndege wa Mji Goma mara moja.

    Maazimio (22) ya Marais wa Nchi Wanachama wa SADC na EAC kwenye mkutano uliofanyika leo hii Jijini Dar Es Salaam, Tanzania 🇹🇿, Azimio la (12) limewataka Wakuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama wa Nchi zote Wanachama kukutana ndani ya siku tano (5) na kutoa mwelekeo wa kitalaam kuhusu mambo yafuatayo: - Kusitisha mara moja mapigano huko Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia Congo 🇨🇩. - Kutoa misaada ya Kibinadamu na kuwasaidia Wahanga wa vita. - Kutoa mpango kazi wa ulinzi ndani ya Mji wa Goma na maeneo Jirani. - Kuzifungua njia muhimu za mawasiliano kwenye Miji ya Goma - Kibumba- Rumangambo - Kalengera- Rutshuru na Goma - Kiwanja- Rwindi lakini pia matumizi ya Ziwa Kivu kwa ajili ya usafiri. - Kuufungua Uwanja wa Ndege wa Mji Goma mara moja.
    Like
    2
    · 0 Kommentare ·0 Anteile ·431 Ansichten
Suchergebnis