• Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo , Félix Tshisekedi, amemshutumu kwa mara nyingine tena Mtangulizi wake Joseph Kabila kuwa anaunga mkono Kundi la Waasi la M23. Mnamo Agosti 2024, Tshisekedi alidai kuwa Kabila alikuwa nyuma ya kuunganishwa kwa muungano wa Wakuu wa kisiasa wa (AFC) unaoongozwa na Corneille Nangaa na Wapiganaji wa kundi la M23.

    Katika mahojiano, Tshisekedi alisema sababu iliyofanya Kabila kutoshiriki uchaguzi wa Desemba 2024 ni kwa sababu alikuwa na shughuli nyingi na AFC.

    “Tusimzungumzie Joseph Kabila. Amekataa kabisa kugombea uchaguzi na anajipanga kupambana na serikali kwa sababu yeye ni AFC.” - alisema Tshisekedi

    Rais huyo ameyasema hayo tena katika Baraza la Usalama la Kimataifa Mjini Munich Nchini Ujerumani Februari 14, 2025, ya kwamba Kabila alienda uhamishoni kwa sababu anafadhili Waasi wa (AFC) ikiwemo Kundi la Waasi la M23.

    Hata hivyo, Chama cha Joseph Kabila cha (PPRD) kimekanusha vikali matamshi ya Rais Félix Tshisekedi kwa kusema kuwa Kiongozi wao hausiki na Kundi hilo la Waasi.

    Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo 馃嚚馃嚛, Félix Tshisekedi, amemshutumu kwa mara nyingine tena Mtangulizi wake Joseph Kabila kuwa anaunga mkono Kundi la Waasi la M23. Mnamo Agosti 2024, Tshisekedi alidai kuwa Kabila alikuwa nyuma ya kuunganishwa kwa muungano wa Wakuu wa kisiasa wa (AFC) unaoongozwa na Corneille Nangaa na Wapiganaji wa kundi la M23. Katika mahojiano, Tshisekedi alisema sababu iliyofanya Kabila kutoshiriki uchaguzi wa Desemba 2024 ni kwa sababu alikuwa na shughuli nyingi na AFC. “Tusimzungumzie Joseph Kabila. Amekataa kabisa kugombea uchaguzi na anajipanga kupambana na serikali kwa sababu yeye ni AFC.” - alisema Tshisekedi Rais huyo ameyasema hayo tena katika Baraza la Usalama la Kimataifa Mjini Munich Nchini Ujerumani 馃嚛馃嚜 Februari 14, 2025, ya kwamba Kabila alienda uhamishoni kwa sababu anafadhili Waasi wa (AFC) ikiwemo Kundi la Waasi la M23. Hata hivyo, Chama cha Joseph Kabila cha (PPRD) kimekanusha vikali matamshi ya Rais Félix Tshisekedi kwa kusema kuwa Kiongozi wao hausiki na Kundi hilo la Waasi.
    Like
    1
    0 Comments 0 Shares 145 Views
  • Kundi la Waasi wa M23 wameingia Mjini Bukavu Mkoani Sud-Kivu ambao ni Mji wa pili (2) kwa ukubwa mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo wakati huo huo Rais wa Nchi Tshisekedi yupo zake Jijini Munich Nchini Ujerumani kwenye kikao cha usalama.

    Kundi la Waasi wa M23 wameingia Mjini Bukavu Mkoani Sud-Kivu ambao ni Mji wa pili (2) kwa ukubwa mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo 馃嚚馃嚛 wakati huo huo Rais wa Nchi Tshisekedi yupo zake Jijini Munich Nchini Ujerumani 馃嚛馃嚜 kwenye kikao cha usalama.
    Like
    Love
    2
    1 Comments 0 Shares 94 Views
  • Aliacha historria (John Jones) ni onyo kali kwa wale wanaopenda mapango.

    Kamwe usipite kwenye sehemu nyembamba sana bila uhakika wa kutoka.

    Hakikisha unakuwa na vifaa vya kutosha vya usalama.

    Usijaribu kupita kwenye njia usizozifahamu vizuri.

    Na zaidi ya yote, uhai ni wa thamani kuliko ujasiri.

    Nutty Putty Cave inabaki kuwa kaburi lililofungwa, na watu wengi wakiogopa hata kufikiria juu yake.
    Aliacha historria (John Jones) ni onyo kali kwa wale wanaopenda mapango. Kamwe usipite kwenye sehemu nyembamba sana bila uhakika wa kutoka. Hakikisha unakuwa na vifaa vya kutosha vya usalama. Usijaribu kupita kwenye njia usizozifahamu vizuri. Na zaidi ya yote, uhai ni wa thamani kuliko ujasiri. Nutty Putty Cave inabaki kuwa kaburi lililofungwa, na watu wengi wakiogopa hata kufikiria juu yake.
    Like
    1
    0 Comments 0 Shares 124 Views
  • Rais wa Urusi , Vladimir Putin amewaalika Rais China , Xi Jinping na Rais wa Marekani , Donald Trump kuhudhuria sherehe maarufu za Ushindi wa Urusi katika vita kuu ya pili ya Dunia (Russia’s Victory Parade) zitakazofanyika tarehe 9 Mwezi May Jijini Moscow Nchini Urusi. Mwaliko huu unatokana na ombi la Rais Donald Trump la tarehe 11 Feb 2025 alipoomba kuzuru Moscow kwa lengo la kumaliza mgogoro wa Ukraine, Kikao kilichotokana na ombi hili kilifanywa kwa njia ya simu ambapo pamoja na mambo mengine, Trump alimhakikishia Putin kwamba Marekani itaacha ufadhili wa kijeshi kwa Ukraine na pia Ukraine itaachia sehemu ya ardhi yake iliyotwaliwa kama dhamana ya usalama wake dhidi ya Moscow.

    Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Washington katika taarifa yake ilikazia na kusisitiza kile alichokizungumza Trump na Moscow na kwamba Marekani inakusudia kumaliza tofauti zao kidunia. Utawala wa Trump umekuwa na juhudi kubwa kumaliza mizozo mikubwa duniani ambayo Ikulu hiyo ilikuwa ikifadhili na kuanzisha uchokozi kwa muda mrefu, Ukiachiliambali mgogoro wa Ukraine, pia Washington inashughulika kumaliza mgogoro wa Mashariki ya Kati huko Gaza ambapo mamia ya watu wameuawa kwa ufadhili wa Marekani hiyohiyo.

    Rais wa Urusi 馃嚪馃嚭, Vladimir Putin amewaalika Rais China 馃嚚馃嚦, Xi Jinping na Rais wa Marekani 馃嚭馃嚫, Donald Trump kuhudhuria sherehe maarufu za Ushindi wa Urusi katika vita kuu ya pili ya Dunia (Russia’s Victory Parade) zitakazofanyika tarehe 9 Mwezi May Jijini Moscow Nchini Urusi. Mwaliko huu unatokana na ombi la Rais Donald Trump la tarehe 11 Feb 2025 alipoomba kuzuru Moscow kwa lengo la kumaliza mgogoro wa Ukraine, Kikao kilichotokana na ombi hili kilifanywa kwa njia ya simu ambapo pamoja na mambo mengine, Trump alimhakikishia Putin kwamba Marekani itaacha ufadhili wa kijeshi kwa Ukraine na pia Ukraine itaachia sehemu ya ardhi yake iliyotwaliwa kama dhamana ya usalama wake dhidi ya Moscow. Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Washington katika taarifa yake ilikazia na kusisitiza kile alichokizungumza Trump na Moscow na kwamba Marekani inakusudia kumaliza tofauti zao kidunia. Utawala wa Trump umekuwa na juhudi kubwa kumaliza mizozo mikubwa duniani ambayo Ikulu hiyo ilikuwa ikifadhili na kuanzisha uchokozi kwa muda mrefu, Ukiachiliambali mgogoro wa Ukraine, pia Washington inashughulika kumaliza mgogoro wa Mashariki ya Kati huko Gaza ambapo mamia ya watu wameuawa kwa ufadhili wa Marekani hiyohiyo.
    Like
    1
    0 Comments 0 Shares 140 Views
  • Rais wa Rwanda , Paul Kagame ameweka wazi kuwa hana hofu na vitisho vya vikwazo vinavyotolewa na Mataifa ya Magharibi dhidi ya Nchi yake akisisitiza kuwa Rwanda itachukua hatua zozote zinazohitajika kulinda maslahi yake, akizungumza na Gazeti la Jeune Afrique, Kagame amezungumzia kwa kina mzozo kati ya Rwanda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo pamoja na shinikizo kutoka Ulaya na Marekani .

    Kagame amesisitiza kuwa hatakubali mashinikizo yanayoelekezwa kwa Rwanda kwa lengo la kuidhoofisha akisema Nchi yake inayo haki ya kujilinda dhidi ya vitisho vyovyote vya nje ambapo Mataifa ya Magharibi yanaishutumu Rwanda kwa kuwaunga mkono kundi la Waasi wa M23 wanaopigana mashariki mwa DR Congo jambo ambalo Rwanda imekanusha mara kadhaa.

    Kauli Kagame inakuja wakati mvutano kati ya Rwanda na DR Congo ukiendelea huku mataifa ya Magharibi yakitoa wito wa mazungumzo ya amani lakini licha ya hivyo Rwanda imeendelea kusisitiza kuwa haitakubali kushinikizwa kwa njia yoyote ikibainisha kuwa hatua zake zitalenga kulinda usalama wa Taifa lake kwa gharama yoyote.
    (DW Swahili)

    Rais wa Rwanda 馃嚪馃嚰, Paul Kagame ameweka wazi kuwa hana hofu na vitisho vya vikwazo vinavyotolewa na Mataifa ya Magharibi dhidi ya Nchi yake akisisitiza kuwa Rwanda itachukua hatua zozote zinazohitajika kulinda maslahi yake, akizungumza na Gazeti la Jeune Afrique, Kagame amezungumzia kwa kina mzozo kati ya Rwanda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo 馃嚚馃嚛 pamoja na shinikizo kutoka Ulaya na Marekani 馃嚭馃嚫. Kagame amesisitiza kuwa hatakubali mashinikizo yanayoelekezwa kwa Rwanda kwa lengo la kuidhoofisha akisema Nchi yake inayo haki ya kujilinda dhidi ya vitisho vyovyote vya nje ambapo Mataifa ya Magharibi yanaishutumu Rwanda kwa kuwaunga mkono kundi la Waasi wa M23 wanaopigana mashariki mwa DR Congo jambo ambalo Rwanda imekanusha mara kadhaa. Kauli Kagame inakuja wakati mvutano kati ya Rwanda na DR Congo ukiendelea huku mataifa ya Magharibi yakitoa wito wa mazungumzo ya amani lakini licha ya hivyo Rwanda imeendelea kusisitiza kuwa haitakubali kushinikizwa kwa njia yoyote ikibainisha kuwa hatua zake zitalenga kulinda usalama wa Taifa lake kwa gharama yoyote. (DW Swahili)
    Love
    1
    0 Comments 0 Shares 87 Views
  • Rais wa Nchi ya Rwanda , Paul Kagame ameendelea kukanusha madai kuwa wao kuwa ndiyo chanzo cha mgogoro wa Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kwa kusema kuwa huo ni mgogoro wa ndani ya DR Congo na hautoki nje ya Congo na suluhu lazima itoke kwa Serikali ya Nchi hiyo.

    Ikumbukwe kwamba Rais Paul Kagame alihudhuria mkutano wa Marais wa Afrika Mashariki na Kusini mwa Afrika Febuari 8,2025 uliojadili namna gani ya kurudisha usalama Nchini DR Congo ambapo Waasi wa kundi la M23 wameiteka Mkoa wa Kivu Kaskazini.

    Rais wa Nchi ya Rwanda 馃嚪馃嚰, Paul Kagame ameendelea kukanusha madai kuwa wao kuwa ndiyo chanzo cha mgogoro wa Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo 馃嚚馃嚛 kwa kusema kuwa huo ni mgogoro wa ndani ya DR Congo na hautoki nje ya Congo na suluhu lazima itoke kwa Serikali ya Nchi hiyo. Ikumbukwe kwamba Rais Paul Kagame alihudhuria mkutano wa Marais wa Afrika Mashariki na Kusini mwa Afrika Febuari 8,2025 uliojadili namna gani ya kurudisha usalama Nchini DR Congo ambapo Waasi wa kundi la M23 wameiteka Mkoa wa Kivu Kaskazini.
    0 Comments 0 Shares 141 Views
  • Hii joint meeting imehudhuriwa na viongozi karibu wote wa SADC na EAC kwa kutambua umuhimu wake kwa usalama eneo la maziwa makuu.

    Viongozi hawa wanajua kuwa usalama wa eneo hili ni muhimu kwa ustawi wa kanda nzima, hasa ikizingatiwa mizozo ya muda mrefu kama ile ya Mashariki mwa DRC.

    Lakini pia hata viongozi ambao nchi zao zimekuwa kwenye msuguano kwenye mgogoro wa Congo wamehushuria. Paul Kagame wa Rwanda na Cyril Ramaphosa wa Afrika Kusini wamehudhuria pia.

    Wote tunakumbuka kwamba hivi karibuni Kagame na Ramaphosa walikuwa kwenye uhasama hawa kwa sababu ya tuhuma zinazoelekewa kwa Rwanda kwamba wanawaunda mkono M23, kundi la waasi linalohusishwa na kuvuruga amani Mashariki mwa DRC.

    Hata hivyo, Tshisekedi ameshindwa kuona umuhimu wa mkutano huu mpaka kumtuma mwakilishi badala yake?

    Hii inaashiria kutokuwa na ushirikiano wa kutosha au kutokubaliana na juhudi za kutatua mgogoro huu kwa njia ya kidiplomasia.

    Is this a sign of deeper political divisions within the DRC or a strategic move to maintain sovereignty?..
    Hii joint meeting imehudhuriwa na viongozi karibu wote wa SADC na EAC kwa kutambua umuhimu wake kwa usalama eneo la maziwa makuu. Viongozi hawa wanajua kuwa usalama wa eneo hili ni muhimu kwa ustawi wa kanda nzima, hasa ikizingatiwa mizozo ya muda mrefu kama ile ya Mashariki mwa DRC. Lakini pia hata viongozi ambao nchi zao zimekuwa kwenye msuguano kwenye mgogoro wa Congo wamehushuria. Paul Kagame wa Rwanda na Cyril Ramaphosa wa Afrika Kusini wamehudhuria pia. Wote tunakumbuka kwamba hivi karibuni Kagame na Ramaphosa walikuwa kwenye uhasama hawa kwa sababu ya tuhuma zinazoelekewa kwa Rwanda kwamba wanawaunda mkono M23, kundi la waasi linalohusishwa na kuvuruga amani Mashariki mwa DRC. Hata hivyo, Tshisekedi ameshindwa kuona umuhimu wa mkutano huu mpaka kumtuma mwakilishi badala yake? Hii inaashiria kutokuwa na ushirikiano wa kutosha au kutokubaliana na juhudi za kutatua mgogoro huu kwa njia ya kidiplomasia. Is this a sign of deeper political divisions within the DRC or a strategic move to maintain sovereignty?..
    0 Comments 0 Shares 234 Views
  • Kwa nini rais wa Congo, Félix Tshisekedi, hakudhuria huu mkutano huu muhimu wa kujadili mambo ya kiusalama ndani ya nchi yake ya Congo?

    Hakuna excuse inayoweza kuelezea dharau na kukosa heshima ambayo amezionyesha taasisi hizi mbili—EAC & SADC.

    Shuka nayo
    Kwa nini rais wa Congo, Félix Tshisekedi, hakudhuria huu mkutano huu muhimu wa kujadili mambo ya kiusalama ndani ya nchi yake ya Congo? Hakuna excuse inayoweza kuelezea dharau na kukosa heshima ambayo amezionyesha taasisi hizi mbili—EAC & SADC. Shuka nayo 猡碉笍
    0 Comments 0 Shares 120 Views
  • Kwa mujibu wa wa kiongozi mkuu wa Korea Kaskazini Kim Jong Un , migogoro inayochochewa na Marekani katika sehemu mbalimbali za dunia, "inazidi kuongeza hatari ya kuzuka kwa vita vya dunia vipya vyenye athari kubwa sio tu kwa amani na usalama wa kimataifa bali pia nyanja nyingine zote za shughuli za binadamu."

    Pia Kim alitoa maoni kwamba mwaka 2025, mzozo wa Ukraine utasalia kuwa moja ya "mhimili mkuu wa hali ya wasiwasi ya kimataifa," nyingine ikiwa hali katika Ukanda wa Gaza na Syria "ambayo imekuwa uwanja wa migogoro ya kijiografia na makabiliano ya kimataifa mwaka jana."

    Katika hatua nyingine Kim alisema Marekani na nchi za Magharibi zinaelezea mzozo wa Ukraine kwa kushindwa kuishinda Urusi kimkakati, kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un alisema, kama ilivyonukuliwa na Shirika la Habari la Korea (KCNA).

    Katika mkutano katika Wizara ya Ulinzi, kuadhimisha kumbukumbu ya miaka 77 ya Jeshi la Wananchi wa Korea, alidai kwamba Marekani imepofushwa na tamaa mbaya huku akiionyesha wasiwasi mkubwa juu ya tabia ya kutojali ya Marekani na kundi la Magharibi kwa makusudi kuendeleza vita vya muda mrefu kwa ndoto isiyoweza kutekelezwa ili kukabiliana na kurudi kwa kimkakati kwa Urusi," shirika la habari lilibainisha.

    Kim alidokeza kuwa Pyongyang imekuwa ikipinga kila mara "kitendo chochote cha kunyima haki ya kimataifa na kuvuruga amani na usalama duniani." Aliongeza kuwa nchi yake "itaunga mkono kila wakati na kuhimiza sababu ya haki ya jeshi la Urusi na watu kutetea uhuru wao, usalama na uadilifu wa eneo kwa kuzingatia ari ya mkataba juu ya ushirikiano wa kimkakati wa kina kati ya DPRK na Urusi."
    (Zungu)

    Kwa mujibu wa wa kiongozi mkuu wa Korea Kaskazini Kim Jong Un , migogoro inayochochewa na Marekani katika sehemu mbalimbali za dunia, "inazidi kuongeza hatari ya kuzuka kwa vita vya dunia vipya vyenye athari kubwa sio tu kwa amani na usalama wa kimataifa bali pia nyanja nyingine zote za shughuli za binadamu." Pia Kim alitoa maoni kwamba mwaka 2025, mzozo wa Ukraine utasalia kuwa moja ya "mhimili mkuu wa hali ya wasiwasi ya kimataifa," nyingine ikiwa hali katika Ukanda wa Gaza na Syria "ambayo imekuwa uwanja wa migogoro ya kijiografia na makabiliano ya kimataifa mwaka jana." Katika hatua nyingine Kim alisema Marekani na nchi za Magharibi zinaelezea mzozo wa Ukraine kwa kushindwa kuishinda Urusi kimkakati, kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un alisema, kama ilivyonukuliwa na Shirika la Habari la Korea (KCNA). Katika mkutano katika Wizara ya Ulinzi, kuadhimisha kumbukumbu ya miaka 77 ya Jeshi la Wananchi wa Korea, alidai kwamba Marekani imepofushwa na tamaa mbaya huku akiionyesha wasiwasi mkubwa juu ya tabia ya kutojali ya Marekani na kundi la Magharibi kwa makusudi kuendeleza vita vya muda mrefu kwa ndoto isiyoweza kutekelezwa ili kukabiliana na kurudi kwa kimkakati kwa Urusi," shirika la habari lilibainisha. Kim alidokeza kuwa Pyongyang imekuwa ikipinga kila mara "kitendo chochote cha kunyima haki ya kimataifa na kuvuruga amani na usalama duniani." Aliongeza kuwa nchi yake "itaunga mkono kila wakati na kuhimiza sababu ya haki ya jeshi la Urusi na watu kutetea uhuru wao, usalama na uadilifu wa eneo kwa kuzingatia ari ya mkataba juu ya ushirikiano wa kimkakati wa kina kati ya DPRK na Urusi." (Zungu)
    0 Comments 0 Shares 368 Views
  • Maazimio (22) ya Marais wa Nchi Wanachama wa SADC na EAC kwenye mkutano uliofanyika leo hii Jijini Dar Es Salaam, Tanzania , Azimio la (12) limewataka Wakuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama wa Nchi zote Wanachama kukutana ndani ya siku tano (5) na kutoa mwelekeo wa kitalaam kuhusu mambo yafuatayo:

    - Kusitisha mara moja mapigano huko Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia Congo .

    - Kutoa misaada ya Kibinadamu na kuwasaidia Wahanga wa vita.

    - Kutoa mpango kazi wa ulinzi ndani ya Mji wa Goma na maeneo Jirani.

    - Kuzifungua njia muhimu za mawasiliano kwenye Miji ya Goma - Kibumba- Rumangambo - Kalengera- Rutshuru na Goma - Kiwanja- Rwindi lakini pia matumizi ya Ziwa Kivu kwa ajili ya usafiri.

    - Kuufungua Uwanja wa Ndege wa Mji Goma mara moja.

    Maazimio (22) ya Marais wa Nchi Wanachama wa SADC na EAC kwenye mkutano uliofanyika leo hii Jijini Dar Es Salaam, Tanzania 馃嚬馃嚳, Azimio la (12) limewataka Wakuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama wa Nchi zote Wanachama kukutana ndani ya siku tano (5) na kutoa mwelekeo wa kitalaam kuhusu mambo yafuatayo: - Kusitisha mara moja mapigano huko Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia Congo 馃嚚馃嚛. - Kutoa misaada ya Kibinadamu na kuwasaidia Wahanga wa vita. - Kutoa mpango kazi wa ulinzi ndani ya Mji wa Goma na maeneo Jirani. - Kuzifungua njia muhimu za mawasiliano kwenye Miji ya Goma - Kibumba- Rumangambo - Kalengera- Rutshuru na Goma - Kiwanja- Rwindi lakini pia matumizi ya Ziwa Kivu kwa ajili ya usafiri. - Kuufungua Uwanja wa Ndege wa Mji Goma mara moja.
    Like
    2
    0 Comments 0 Shares 282 Views
  • Rwanda inalichukulia jeshi la Burundi kama tishio jingine la usalama katika eneo la mashariki mwa Jamhuri ya demokrasi ya Congo (DRC).

    Nchi inayopakana na Rwanda na DRC imekuwa na maelfu ya wanajeshi huko kwa miaka mingi.

    Walikwenda kuwafuatilia waasi wa Burundi lakini sasa wanasaidia jeshi la Kinshasa katika vita dhidi ya M23.

    Uhusiano kati ya Rwanda na Burundi ni mbaya.

    Nchi hizi mbili zina muundo wa kikabila unaofanana lakini kinyume na Rwanda, Hutu ndiyo wanaoshikilia madaraka nchini Burundi.

    Nchi zote mbili zimekashifiana kwa kudai kujaribu kuangusha serikali zao.

    Rais wa Burundi, Evariste Ndayishimiye, ametoa onyo kali kwenye mitandao ya kijamii.

    "Ikizidi, Rwanda itaendelea na mashambulizi," aliandika, "Najua vita vitafika Burundi… Siku moja atataka kuingia Burundi - hatutakubaliana na hilo. Vita vitapanuka."

    Tishio hili litakuwa kubwa zaidi ikiwa M23 itaendelea na mashambulizi kutoka Goma kuelekea mkoa wa Kivu kusini karibu na mpaka wa Burundi, ambapo vikosi vyake viko.

    "Kile kinachotafutwa na Burundi hapa ni kuokoa utawala wake," alisema Bw. Stearns.

    "Burundi inahofia kuwa kama vikosi vya Rwanda vitaimarisha ushawishi wao katika eneo la Kivu kusini, inaweza kuteteresha serikali ya Bujumbura. Kile kilicho hatarini hapa ni kuzima uasi huu kabla haujaingilia karibu zaidi."

    Wengine wanahofia kurudi kwa vita mbili zilizoshambulia eneo hilo mwishoni mwa miaka ya 1990, ambazo zilihusisha nchi tisa na kusababisha vifo vya mamilioni ya watu.

    Mara hii, mapigano ya moja kwa moja kati ya majeshi mawili yanaweza kupelekea mgogoro wa DRC kuvuka nje ya mipaka yake.
    (BBC Swahili)

    Rwanda inalichukulia jeshi la Burundi kama tishio jingine la usalama katika eneo la mashariki mwa Jamhuri ya demokrasi ya Congo (DRC). Nchi inayopakana na Rwanda na DRC imekuwa na maelfu ya wanajeshi huko kwa miaka mingi. Walikwenda kuwafuatilia waasi wa Burundi lakini sasa wanasaidia jeshi la Kinshasa katika vita dhidi ya M23. Uhusiano kati ya Rwanda na Burundi ni mbaya. Nchi hizi mbili zina muundo wa kikabila unaofanana lakini kinyume na Rwanda, Hutu ndiyo wanaoshikilia madaraka nchini Burundi. Nchi zote mbili zimekashifiana kwa kudai kujaribu kuangusha serikali zao. Rais wa Burundi, Evariste Ndayishimiye, ametoa onyo kali kwenye mitandao ya kijamii. "Ikizidi, Rwanda itaendelea na mashambulizi," aliandika, "Najua vita vitafika Burundi… Siku moja atataka kuingia Burundi - hatutakubaliana na hilo. Vita vitapanuka." Tishio hili litakuwa kubwa zaidi ikiwa M23 itaendelea na mashambulizi kutoka Goma kuelekea mkoa wa Kivu kusini karibu na mpaka wa Burundi, ambapo vikosi vyake viko. "Kile kinachotafutwa na Burundi hapa ni kuokoa utawala wake," alisema Bw. Stearns. "Burundi inahofia kuwa kama vikosi vya Rwanda vitaimarisha ushawishi wao katika eneo la Kivu kusini, inaweza kuteteresha serikali ya Bujumbura. Kile kilicho hatarini hapa ni kuzima uasi huu kabla haujaingilia karibu zaidi." Wengine wanahofia kurudi kwa vita mbili zilizoshambulia eneo hilo mwishoni mwa miaka ya 1990, ambazo zilihusisha nchi tisa na kusababisha vifo vya mamilioni ya watu. Mara hii, mapigano ya moja kwa moja kati ya majeshi mawili yanaweza kupelekea mgogoro wa DRC kuvuka nje ya mipaka yake. (BBC Swahili)
    Like
    1
    0 Comments 0 Shares 251 Views
  • "Congo hawawezi kutuambia tukae kimya wakati wanasababisha matatizo makubwa ya kiusalama dhidi yetu, hakuna wa kutuambia tukae kimya, tumeongea na Congo mara nyingi tumewaita tukae tuongee hawataki"

    "Mimi naomba tusiwe na vikao vingi sana kama ambavyo tayari tumeshakuwa navyo, hatuwezi kila siku kukaa kujadili matatizo maana kinachoendelea pale ni vita ya Kikabila ni suala la kutambuana, kujadiliana na kuwapa haki yao, tutumie kikao hiki kupata suluhu ya kudumu na sio matatizo yatokee Congo kisha ubaya anapewa Rwanda” - Paul Kagame, Rais wa Rwanda akiongea kwenye mkutano wa EAC na SADC.

    "Congo hawawezi kutuambia tukae kimya wakati wanasababisha matatizo makubwa ya kiusalama dhidi yetu, hakuna wa kutuambia tukae kimya, tumeongea na Congo mara nyingi tumewaita tukae tuongee hawataki" "Mimi naomba tusiwe na vikao vingi sana kama ambavyo tayari tumeshakuwa navyo, hatuwezi kila siku kukaa kujadili matatizo maana kinachoendelea pale ni vita ya Kikabila ni suala la kutambuana, kujadiliana na kuwapa haki yao, tutumie kikao hiki kupata suluhu ya kudumu na sio matatizo yatokee Congo kisha ubaya anapewa Rwanda” - Paul Kagame, Rais wa Rwanda 馃嚪馃嚰 akiongea kwenye mkutano wa EAC na SADC.
    Haha
    1
    0 Comments 0 Shares 191 Views
  • Miaka ya 90, Ukraine alikuwa mbabe sana. Taifa hili lilikuwa lina nguvu za kijeshi ambazo ziliwafanya majirani zake kusita hata kufikiria kulivamia.

    Sababu?

    Lilikuwa na zaidi ya mabomu 1,000 ya nyuklia. Haya si mabomu ya kawaida, ni silaha za maangamizi ambazo zingeweza kuifuta dunia katika sekunde chache.

    Lakini kama ilivyo kwa kila hadithi ya usaliti, Ukraine alifanya kosa moja kubwa, aliamini watu wengine badala ya kujilinda mwenyewe.

    Marekani, Urusi na Uingereza walimfuata kwa heshima kubwa, wakampigia magoti na kumwambia.

    "Tafadhali, haribu mabomu yako. Dunia itakuwa mahali salama zaidi, na sisi tutakuwa walinzi wako. Hatutakuacha."
    Ukraine akakubali. Akayaangamiza mabomu yake yote ya nyuklia. Mikataba iliwekwa. Ahadi zikaandikwa kwa kalamu na kutiwa muhuri.

    Ukraine akaamini kabisa kuwa usalama wake hauwezi kutikiswa tena.
    Miaka ya 90, Ukraine alikuwa mbabe sana. Taifa hili lilikuwa lina nguvu za kijeshi ambazo ziliwafanya majirani zake kusita hata kufikiria kulivamia. Sababu? Lilikuwa na zaidi ya mabomu 1,000 ya nyuklia. Haya si mabomu ya kawaida, ni silaha za maangamizi ambazo zingeweza kuifuta dunia katika sekunde chache. Lakini kama ilivyo kwa kila hadithi ya usaliti, Ukraine alifanya kosa moja kubwa, aliamini watu wengine badala ya kujilinda mwenyewe. Marekani, Urusi na Uingereza walimfuata kwa heshima kubwa, wakampigia magoti na kumwambia. "Tafadhali, haribu mabomu yako. Dunia itakuwa mahali salama zaidi, na sisi tutakuwa walinzi wako. Hatutakuacha." Ukraine akakubali. Akayaangamiza mabomu yake yote ya nyuklia. Mikataba iliwekwa. Ahadi zikaandikwa kwa kalamu na kutiwa muhuri. Ukraine akaamini kabisa kuwa usalama wake hauwezi kutikiswa tena.
    Like
    1
    0 Comments 0 Shares 258 Views
  • Ripoti mbalimbali zilionesha kuwa Nangaa alikuwa akilitumia kundi hilo kama silaha yake ya kisiasa na kijeshi.

    Huku akipewa misaada ya kifedha na baadhi ya mataifa ya nje yenye maslahi katika siasa za Congo.

    Sasa Congo iko njia panda. Corneille Nangaa, ambaye miaka michache iliyopita alihusika katika kuleta utawala wa sasa, sasa anatajwa kama mmoja wa watu wanaotaka kuipindua serikali.

    Je, anataka kuwa Rais?
    Au ana ajenda nyingine ya siri?

    Wakati serikali ya Tshisekedi ikifanya kila juhudi kuhakikisha Nangaa na jeshi lake wanadhibitiwa, ukweli unabaki kuwa Congo imeingia katika mgogoro mpya

    Jeshi la M23 likiwa linazidi kuimarika, na Nangaa akiwa nyuma ya harakati hizo, taifa linakabiliwa na changamoto kubwa ya usalama na utulivu wa kisiasa.

    Ikiwa hatua hazitachukuliwa haraka, huenda Congo ikajikuta kwenye mgogoro mkubwa zaidi wa kisiasa na kijeshi na jina la Corneille Nangaa litakuwa miongoni mwa majina yatakayotajwa kwa historia ndefu katika taifa hilo.

    Ripoti mbalimbali zilionesha kuwa Nangaa alikuwa akilitumia kundi hilo kama silaha yake ya kisiasa na kijeshi. Huku akipewa misaada ya kifedha na baadhi ya mataifa ya nje yenye maslahi katika siasa za Congo. Sasa Congo iko njia panda. Corneille Nangaa, ambaye miaka michache iliyopita alihusika katika kuleta utawala wa sasa, sasa anatajwa kama mmoja wa watu wanaotaka kuipindua serikali. Je, anataka kuwa Rais? Au ana ajenda nyingine ya siri? Wakati serikali ya Tshisekedi ikifanya kila juhudi kuhakikisha Nangaa na jeshi lake wanadhibitiwa, ukweli unabaki kuwa Congo imeingia katika mgogoro mpya Jeshi la M23 likiwa linazidi kuimarika, na Nangaa akiwa nyuma ya harakati hizo, taifa linakabiliwa na changamoto kubwa ya usalama na utulivu wa kisiasa. Ikiwa hatua hazitachukuliwa haraka, huenda Congo ikajikuta kwenye mgogoro mkubwa zaidi wa kisiasa na kijeshi na jina la Corneille Nangaa litakuwa miongoni mwa majina yatakayotajwa kwa historia ndefu katika taifa hilo.
    0 Comments 0 Shares 200 Views
  • Akiwa na uelewa mkubwa wa masuala ya kifedha na uchumi wa dunia, alijiunga na Umoja wa Mataifa kupitia Shirika la Maendeleo (UNDP), ambako alifanya kazi kwa miaka kadhaa.

    Kupitia UNDP, alihusika katika miradi mbalimbali ya maendeleo ya kijamii na kiuchumi nchini Congo, jambo lililompatia uzoefu mkubwa wa utawala.

    Ndiye aliyekuwa kiungo kati ya mashirika ya kimataifa na serikali ya Congo, akisimamia miradi ya maendeleo katika nchi iliyojaa changamoto za kisiasa na kiusalama.

    Uwezo wake wa kusimamia taasisi na kuelewa siasa za ndani ulimfanya kuwa mtu mwenye ushawishi mkubwa serikalini, jambo lililomfungulia milango ya nafasi kubwa zaidi.

    Mwaka 2015, Corneille Nangaa aliteuliwa kuwa Rais wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (CENI), moja ya nafasi zenye ushawishi mkubwa nchini Congo.
    Hili lilimpa mamlaka ya kusimamia uchaguzi mkuu wa 2018, uchaguzi uliokuwa na ushindani mkubwa kati ya wapinzani wa Joseph Kabila na viongozi wa upinzani.

    Katika uchaguzi huo, Corneille Nangaa alisimamia na hatimaye kutangaza ushindi wa Félix Tshisekedi kuwa Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
    Akiwa na uelewa mkubwa wa masuala ya kifedha na uchumi wa dunia, alijiunga na Umoja wa Mataifa kupitia Shirika la Maendeleo (UNDP), ambako alifanya kazi kwa miaka kadhaa. Kupitia UNDP, alihusika katika miradi mbalimbali ya maendeleo ya kijamii na kiuchumi nchini Congo, jambo lililompatia uzoefu mkubwa wa utawala. Ndiye aliyekuwa kiungo kati ya mashirika ya kimataifa na serikali ya Congo, akisimamia miradi ya maendeleo katika nchi iliyojaa changamoto za kisiasa na kiusalama. Uwezo wake wa kusimamia taasisi na kuelewa siasa za ndani ulimfanya kuwa mtu mwenye ushawishi mkubwa serikalini, jambo lililomfungulia milango ya nafasi kubwa zaidi. Mwaka 2015, Corneille Nangaa aliteuliwa kuwa Rais wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (CENI), moja ya nafasi zenye ushawishi mkubwa nchini Congo. Hili lilimpa mamlaka ya kusimamia uchaguzi mkuu wa 2018, uchaguzi uliokuwa na ushindani mkubwa kati ya wapinzani wa Joseph Kabila na viongozi wa upinzani. Katika uchaguzi huo, Corneille Nangaa alisimamia na hatimaye kutangaza ushindi wa Félix Tshisekedi kuwa Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
    0 Comments 0 Shares 222 Views
  • Kutangazwa kwa serikali hii mpya kumepokelewa kwa tahadhari kubwa.

    Jumuiya za kimataifa zina wasiwasi kuhusu usalama wa raia na mali zao, huku zikiendelea kutoa mwito wa utulivu na mazungumzo ya amani.

    Mgogoro huu umeibua hofu ya kuzuka kwa janga kubwa la kibinadamu, linaloweza kusababisha vifo vingi na kuwalazimu maelfu ya watu kuyahama makazi yao.

    Serikali ya DRC imekosoa hatua hii, ikisisitiza kuwa itaendelea kupambana na waasi ili kurejesha mamlaka yake katika maeneo yote ya Kivu Kaskazini.

    Hali ya usalama katika Goma na maeneo jirani inazidi kuzorota, huku shughuli za kiuchumi zikidorora kwa kasi.

    Maelfu ya raia wameyakimbia makazi yao kutokana na mapigano yanayoendelea. Mashirika ya misaada yanafanya juhudi kusaidia waathirika wa mgogoro huu..

    Kutangazwa kwa serikali hii mpya kumepokelewa kwa tahadhari kubwa. Jumuiya za kimataifa zina wasiwasi kuhusu usalama wa raia na mali zao, huku zikiendelea kutoa mwito wa utulivu na mazungumzo ya amani. Mgogoro huu umeibua hofu ya kuzuka kwa janga kubwa la kibinadamu, linaloweza kusababisha vifo vingi na kuwalazimu maelfu ya watu kuyahama makazi yao. Serikali ya DRC imekosoa hatua hii, ikisisitiza kuwa itaendelea kupambana na waasi ili kurejesha mamlaka yake katika maeneo yote ya Kivu Kaskazini. Hali ya usalama katika Goma na maeneo jirani inazidi kuzorota, huku shughuli za kiuchumi zikidorora kwa kasi. Maelfu ya raia wameyakimbia makazi yao kutokana na mapigano yanayoendelea. Mashirika ya misaada yanafanya juhudi kusaidia waathirika wa mgogoro huu..
    Like
    1
    0 Comments 0 Shares 180 Views
  • Rais Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo , Felix Tshisekedi na Paul Kagame wa Rwanda, wanatarajia kukutana Jijini Dar es Salaam, Tanzania, Februari 8, 2025 kujadili mustakabali wa hali ya usalama inayoendelea eneo la Mashariki mwa DR Congo.

    Taarifa iliyotolewa na Rais wa Kenya, William Ruto, wawili hao watakutana katika mkutano wa pamoja wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), baada ya Rais Samia Suluhu Hassan wa Tanzania kuridhia Nchi yake ya Tanzania kuwa mwenyeji wa mkutano huo.

    Rais Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo 馃嚚馃嚛, Felix Tshisekedi na Paul Kagame wa Rwanda, wanatarajia kukutana Jijini Dar es Salaam, Tanzania, Februari 8, 2025 kujadili mustakabali wa hali ya usalama inayoendelea eneo la Mashariki mwa DR Congo. Taarifa iliyotolewa na Rais wa Kenya, William Ruto, wawili hao watakutana katika mkutano wa pamoja wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), baada ya Rais Samia Suluhu Hassan wa Tanzania kuridhia Nchi yake ya Tanzania kuwa mwenyeji wa mkutano huo.
    Like
    2
    0 Comments 0 Shares 354 Views
  • Ukisikia madai ya Rwanda kuvuruga amani ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ukarudi kuangalia ramani na takwimu za mataifa hayo hakika utaamini ukubwa wa pua sio wingi wa kamasi. Kitakwimu Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imeizidi Rwanda kila kitu ikiwemo ukubwa wa eneo, rasilimali, madini pamoja na idadi ya Watu.

    Eneo la Congo ni karibu mara mia (100) ya eneo la Rwanda. Idadi ya Watu wa Kongo ni takribani mara 10 Watu wa Rwanda. Pamoja na hayo yote Congo wanalalamika kwamba Rwanda ndio inayounga mkono makundi ya waasi mashariki mwa nchi hiyo ambayo yamelemea majeshi ya serikali na kusonga mbele kiasi cha kutwaa miji mikubwa ya kimkakati yenye utajiri mkubwa wa madini.

    Rwanda pamoja na kuzidiwa takwimu hizo ila mipango thabiti na uwekezaji wa kimkakati katika masuala ya kijeshi, ulinzi na usalama katika eneo hilo ndio umeifanya ionekane kama ndio taifa kubwa. Yaani kiufupi ukiwa hujui ramani na takwimu unaweza kudhani Rwanda ndio taifa kubwa ndio maana inalalamikiwa kuionea Kongo. Kiufupi Rwanda inanufaika mno na mipango thabiti ya kiuongozi, wakati Kongo ikiwa na uongozi usio na mipango thabiti ya kikanda na kimkakati kulinda mipaka yake na majimbo ya Mashariki yenye utajiri mkubwa wa madini

    Rwanda ina idadi kubwa ya Watutsi ambao pia wanapatikana Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na wachache Burundi na Uganda. Historia ya watutsi inasemekana walitokea Ethiopia kuja maziwa makuu na sifa yao kuu wanapenda uongozi (kwa mnaowajua mtakua mashahidi). Jamii ya watutsi ni watu ambao huwa hawapendi unyonge wala kuonewa, ni wepesi kujitetea na huwa wanaumoja sana.

    Baada ya Wakoloni kugawa mipaka ndio walisababisha watutsi kujikuta ndani ya nchi nyingi tofauti ila ni wazawa wa maeneo hayo na historia yao katika nchi hizo ni toka zama za kale hivyo ni ngumu kuwaita Wahamiaji. Watutsi ndio waliomsaidia Hayati Laurent Kabila kumpindua Mobutu Seseseko na inasemekana Mama mzazi wa Joseph Kabila alikua Mtutsi pia. Kimsingi Kongo haikupaswa kuilalamikia Rwanda, bali Rwanda ndio ingepaswa kuilalamikia Kongo.

    Ukisikia madai ya Rwanda 馃嚪馃嚰 kuvuruga amani ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo 馃嚚馃嚛 ukarudi kuangalia ramani na takwimu za mataifa hayo hakika utaamini ukubwa wa pua sio wingi wa kamasi. Kitakwimu Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imeizidi Rwanda kila kitu ikiwemo ukubwa wa eneo, rasilimali, madini pamoja na idadi ya Watu. Eneo la Congo ni karibu mara mia (100) ya eneo la Rwanda. Idadi ya Watu wa Kongo ni takribani mara 10 Watu wa Rwanda. Pamoja na hayo yote Congo wanalalamika kwamba Rwanda ndio inayounga mkono makundi ya waasi mashariki mwa nchi hiyo ambayo yamelemea majeshi ya serikali na kusonga mbele kiasi cha kutwaa miji mikubwa ya kimkakati yenye utajiri mkubwa wa madini. Rwanda pamoja na kuzidiwa takwimu hizo ila mipango thabiti na uwekezaji wa kimkakati katika masuala ya kijeshi, ulinzi na usalama katika eneo hilo ndio umeifanya ionekane kama ndio taifa kubwa. Yaani kiufupi ukiwa hujui ramani na takwimu unaweza kudhani Rwanda ndio taifa kubwa ndio maana inalalamikiwa kuionea Kongo. Kiufupi Rwanda inanufaika mno na mipango thabiti ya kiuongozi, wakati Kongo ikiwa na uongozi usio na mipango thabiti ya kikanda na kimkakati kulinda mipaka yake na majimbo ya Mashariki yenye utajiri mkubwa wa madini Rwanda ina idadi kubwa ya Watutsi ambao pia wanapatikana Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na wachache Burundi na Uganda. Historia ya watutsi inasemekana walitokea Ethiopia kuja maziwa makuu na sifa yao kuu wanapenda uongozi (kwa mnaowajua mtakua mashahidi). Jamii ya watutsi ni watu ambao huwa hawapendi unyonge wala kuonewa, ni wepesi kujitetea na huwa wanaumoja sana. Baada ya Wakoloni kugawa mipaka ndio walisababisha watutsi kujikuta ndani ya nchi nyingi tofauti ila ni wazawa wa maeneo hayo na historia yao katika nchi hizo ni toka zama za kale hivyo ni ngumu kuwaita Wahamiaji. Watutsi ndio waliomsaidia Hayati Laurent Kabila kumpindua Mobutu Seseseko na inasemekana Mama mzazi wa Joseph Kabila alikua Mtutsi pia. Kimsingi Kongo haikupaswa kuilalamikia Rwanda, bali Rwanda ndio ingepaswa kuilalamikia Kongo.
    Like
    1
    0 Comments 0 Shares 357 Views
  • Jamuhuri ya Kidemokrasi ya Congo imeziandikia klabu za mpira wa miguu barani Ulaya zinazoingia mikataba ya ufadhili kutoka Serikali ya Rwanda kutopokea, "Fedha zinazotokana na umwagikaji wa damu", unaoendelea mashariki mwa DR Congo.

    Kwa mujibu Waziri wa mambo ya kigeni Nchini DR Congo, Therese Kayikwamba Wagner ameziandikia klabu za Arsenal FC ya England , Paris Sint-Germaine ya Ufaransa na FC Bayern München ya Ujerumani kusitisha ushirikiano wao wa ufadhili wa mauzo chini ya mpango wa "Visit Rwanda" wakidai kwamba idadi kubwa ya Wanajeshi wa Rwanda wanapigana na Jeshi la FARDC huko Mjini Goma wakisaidiana na kundi la Waasi la M23.

    Kwenye barua hiyo kwa klabu ya Arsenal FC, Waziri Wagner amesema kwamba, Rwanda inastahili kulaumiwa kwa hatua zake ndani ya DR Congo kwani Umoja wa mataifa umeripoti kwamba kikosi cha Wanajeshi 4,000 kutoka Rwanda kiko ndani ya DR Congo na kinashikriki kwenye vita vinavyoendelea Nchini humo.

    Sanjari na klabu hizo kusubiriwa kufanya uamuzi kuhusu ombi hilo la DR Congo na shutuma dhidi ya Rwanda, DR Congo imeendelea kuwasilisha hoja yao ya hali mbaya inayoshuhudiwa mashariki mwa nchi hiyo.

    Waziri Wagner ameiambia klabu ya Arsenal kwamba, "maelfu ya Watu wamekwama Jijini Goma, ambapo hakuna njia ya kuingiza chakula, huku huduma za kusambaza maji na umeme zikiwa zimekatizwa. Hakuna usalama, Watu wameuawa na wizi unakithiri Mjini humo. Mfadhili wenu anahusika moja kwa moja kwa mahangaiko haya ya wengi"

    Barua hiyo inaangazia mpango wa, "Visit Rwanda" unafadhiliwa moja kwa moja na uchimbaji madini haramu unaoendelea katika maeneo kadhaa yaliyokaliwa mashariki mwa DR Congo na kuvukishwa mpaka hadi Rwanda ambayo inasafirisha ughaibuni kama madini yake asilii.

    Jamuhuri ya Kidemokrasi ya Congo 馃嚚馃嚛 imeziandikia klabu za mpira wa miguu barani Ulaya zinazoingia mikataba ya ufadhili kutoka Serikali ya Rwanda 馃嚪馃嚰 kutopokea, "Fedha zinazotokana na umwagikaji wa damu", unaoendelea mashariki mwa DR Congo. Kwa mujibu Waziri wa mambo ya kigeni Nchini DR Congo, Therese Kayikwamba Wagner ameziandikia klabu za Arsenal FC ya England 馃彺鬆仹鬆仮鬆仴鬆伄鬆仹鬆伩, Paris Sint-Germaine ya Ufaransa 馃嚝馃嚪 na FC Bayern München ya Ujerumani 馃嚛馃嚜 kusitisha ushirikiano wao wa ufadhili wa mauzo chini ya mpango wa "Visit Rwanda" wakidai kwamba idadi kubwa ya Wanajeshi wa Rwanda wanapigana na Jeshi la FARDC huko Mjini Goma wakisaidiana na kundi la Waasi la M23. Kwenye barua hiyo kwa klabu ya Arsenal FC, Waziri Wagner amesema kwamba, Rwanda inastahili kulaumiwa kwa hatua zake ndani ya DR Congo kwani Umoja wa mataifa umeripoti kwamba kikosi cha Wanajeshi 4,000 kutoka Rwanda kiko ndani ya DR Congo na kinashikriki kwenye vita vinavyoendelea Nchini humo. Sanjari na klabu hizo kusubiriwa kufanya uamuzi kuhusu ombi hilo la DR Congo na shutuma dhidi ya Rwanda, DR Congo imeendelea kuwasilisha hoja yao ya hali mbaya inayoshuhudiwa mashariki mwa nchi hiyo. Waziri Wagner ameiambia klabu ya Arsenal kwamba, "maelfu ya Watu wamekwama Jijini Goma, ambapo hakuna njia ya kuingiza chakula, huku huduma za kusambaza maji na umeme zikiwa zimekatizwa. Hakuna usalama, Watu wameuawa na wizi unakithiri Mjini humo. Mfadhili wenu anahusika moja kwa moja kwa mahangaiko haya ya wengi" Barua hiyo inaangazia mpango wa, "Visit Rwanda" unafadhiliwa moja kwa moja na uchimbaji madini haramu unaoendelea katika maeneo kadhaa yaliyokaliwa mashariki mwa DR Congo na kuvukishwa mpaka hadi Rwanda ambayo inasafirisha ughaibuni kama madini yake asilii.
    Like
    1
    0 Comments 0 Shares 332 Views
  • #PART2

    Baada ya mipaka ya Wakoloni walioangukia Rwanda na Burundi waliendelea kujiita Watutsi, lakini walioangukia Congo hawakujiita Watutsi, kwa sababu ya kukwepa ubaguzi. Ili wasitengwe wakajitambulisha kwa eneo wanalotoka, safu za Milima ya Mulenge. Kwahiyo wakajiita Banyamulenge, yani watu kutoka Mulenge. Lakini ukweli ni Watutsi, wametengwa na wenzao kwa mipaka ya wakoloni.

    Ni sawa na wamassai wa Tanzania na wale wa Kenya. Ni jamii moja ila wametengwa na mipaka ya Wakoloni. Huku Tanzania Wamasai ni wengi kuliko Kenya, lakini serikali ya Kenya haiwezi kuwafukuza wa Kenya waje Tanzania. Itakua dhambi ya ubaguzi. Mipaka ilipowekwa waliojikuta Kenya wakawa raia wa Kenya hivyo, hali kadhalika waliojikuta Tanzania.

    Watutsi wa Congo pamoja na kujiita Banyamulenge, bado wakikumbana na ubaguzi. Hawakupata ushirikiano kutoka kwa jamii nyingine za Kivu. Kwahiyo wakajikuta wameongeza "bond" na Watutsi wa Rwanda. Kukawa na mwingiliano mkubwa kati ya Watutsi wa Rwanda na wale wa Congo (Banyamulenge).

    Mwaka 1959, mfalme wa mwisho wa Rwanda, Mutara III, aliuawa kwa sumu. Baada ya kifo chake, Rwanda iliingia katika machafuko ambapo Wahutu waliokuwa zaidi ya 80% waliwashambulia Watutsi, wakiwatuhumu kupendelewa na Wakoloni wa Kibelgiji. Maelfu ya Watutsi walikimbilia Kivu kwa ajili ya usalama wao. Walipofika huko, waliungana na wenzao (Banyamulenge), idadi ikaongezeka.

    Mwaka 1962, Rwanda ilipata uhuru, na Gregoire Kayibanda akawa Rais. Kwa mara ya kwanza, Wahutu walishika madaraka baada ya utawala wa kifalme wa Watutsi kwa miaka mingi. Kayibanda alikakandamiza Watutsi na kupendelea Wahutu wenzake. Watutsi wengi walikimbilia uhamishoni, hasa maeneo ya Kivu. Wakaenda kuungana na wenzao (Banyamulenge).

    Mwaka 1973, Kayibanda alipinduliwa na Mkuu wa Majeshi, Jenerali Juvénal Habyarimana, ambaye alijiapiza kuwatokomeza Watutsi. Kwa miaka 21 ya utawala wake, Watutsi waliteswa vikali. Waliondolewa kwenye nafasi za kijeshi, mashirika ya umma, na siasa. Wengi walifungwa gerezani au kuuawa. Hali hii iliwafanya Watutsi wengi zaidi kukimbia Rwanda na kuelekea maeneo mbalimbali ikiwemo Kivu. Walioenda Kivu wakaenda kuongeza idadi ya Banyamulenge.!
    (Malisa GJ)

    #PART2 Baada ya mipaka ya Wakoloni walioangukia Rwanda na Burundi waliendelea kujiita Watutsi, lakini walioangukia Congo hawakujiita Watutsi, kwa sababu ya kukwepa ubaguzi. Ili wasitengwe wakajitambulisha kwa eneo wanalotoka, safu za Milima ya Mulenge. Kwahiyo wakajiita Banyamulenge, yani watu kutoka Mulenge. Lakini ukweli ni Watutsi, wametengwa na wenzao kwa mipaka ya wakoloni. Ni sawa na wamassai wa Tanzania na wale wa Kenya. Ni jamii moja ila wametengwa na mipaka ya Wakoloni. Huku Tanzania Wamasai ni wengi kuliko Kenya, lakini serikali ya Kenya haiwezi kuwafukuza wa Kenya waje Tanzania. Itakua dhambi ya ubaguzi. Mipaka ilipowekwa waliojikuta Kenya wakawa raia wa Kenya hivyo, hali kadhalika waliojikuta Tanzania. Watutsi wa Congo pamoja na kujiita Banyamulenge, bado wakikumbana na ubaguzi. Hawakupata ushirikiano kutoka kwa jamii nyingine za Kivu. Kwahiyo wakajikuta wameongeza "bond" na Watutsi wa Rwanda. Kukawa na mwingiliano mkubwa kati ya Watutsi wa Rwanda na wale wa Congo (Banyamulenge). Mwaka 1959, mfalme wa mwisho wa Rwanda, Mutara III, aliuawa kwa sumu. Baada ya kifo chake, Rwanda iliingia katika machafuko ambapo Wahutu waliokuwa zaidi ya 80% waliwashambulia Watutsi, wakiwatuhumu kupendelewa na Wakoloni wa Kibelgiji. Maelfu ya Watutsi walikimbilia Kivu kwa ajili ya usalama wao. Walipofika huko, waliungana na wenzao (Banyamulenge), idadi ikaongezeka. Mwaka 1962, Rwanda ilipata uhuru, na Gregoire Kayibanda akawa Rais. Kwa mara ya kwanza, Wahutu walishika madaraka baada ya utawala wa kifalme wa Watutsi kwa miaka mingi. Kayibanda alikakandamiza Watutsi na kupendelea Wahutu wenzake. Watutsi wengi walikimbilia uhamishoni, hasa maeneo ya Kivu. Wakaenda kuungana na wenzao (Banyamulenge). Mwaka 1973, Kayibanda alipinduliwa na Mkuu wa Majeshi, Jenerali Juvénal Habyarimana, ambaye alijiapiza kuwatokomeza Watutsi. Kwa miaka 21 ya utawala wake, Watutsi waliteswa vikali. Waliondolewa kwenye nafasi za kijeshi, mashirika ya umma, na siasa. Wengi walifungwa gerezani au kuuawa. Hali hii iliwafanya Watutsi wengi zaidi kukimbia Rwanda na kuelekea maeneo mbalimbali ikiwemo Kivu. Walioenda Kivu wakaenda kuongeza idadi ya Banyamulenge.! (Malisa GJ)
    Like
    1
    0 Comments 0 Shares 498 Views
More Results