• Familia ya Kiongozi wa upinzani wa Uganda Bobi Wine yafunguka kukimbia Nchi kufuatia matukio ya siasa na usalama.

    Katika taarifa iliyotolewa, Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Robert Kyagulanyi Ssentamu, maarufu kama Bobi Wine, amethibitisha mbele ya Wakaguzi wa haki za binadamu Mjini Geneva kwamba Mke wake, Barbie Itungo Kyagulanyi, na Watoto wao wametoka Uganda kwa sababu za hofu ya maisha yao kufuatia hali tete inayojitokeza nchini mwao baada ya uchaguzi wa Rais.

    Katika hotuba yake kupitia video mbele ya Geneva Summit for Human Rights and Democracy, Bobi Wine alisema wazi: “Mke wangu na Watoto walilazimika kukimbia nchi kwa hofu ya maisha yao.” - Bobi Wine.

    Alifafanua kuwa usalama wa familia yake uliathirika sana kutokana na operesheni za vikosi vya usalama zilizoendelea mara tu baada ya uchaguzi wa 15 Januari 2026, ambapo serikali ilitangaza ushindi wa Rais Yoweri Museveni ambayo Bobi Wine ameipinga kwa madai ya udanganyifu wa kura na ukandamizaji wa upinzani.

    Bobi Wine pia alidai kwamba vikosi vya usalama: “Vilivamia nyumba yangu, vikamtesa Mke wangu, kumfanya asiwe na chaguo ila kuondoka na Watoto wakiwa nje ya nchi.” amesema

    Habari kwamba familia yake imeondoka Uganda na si tu kutoroka nyumba yao ya Magere imetolewa mara tu baada ya miezi ya mvutano mkali, ikiwa ni pamoja na madai ya mashambulizi, ulinzi mkali wa nyumba yao na vitisho vilivyowekwa na baadhi ya Afisa wa usalama.

    Katika maneno yake Mjini Geneva, Bobi Wine pia alijumuisha ombi kwa Jumuiya ya kimataifa kuhusu hatua za kulinda haki za binadamu na kuzuia ukandamizaji wa upinzani nchini Uganda.

    Taarifa hii inakuja katika wakati ambapo Uganda iko chini ya uangalizi wa kimataifa kufuatia ripoti za ghasia, mashambulizi dhidi ya wapinzani wa kisiasa, na madai ya upendeleo wa vyombo vya usalama kuelekea chama tawala.

    Kwa sasa, bado haijafahamika kwa umma ni nchi gani hasa Barbie Itungo Kyagulanyi na Watoto hao wamekwenda, ila uamuzi wao wa kukimbia unachukuliwa kama hatua ya kulinda usalama wa familia katika mzozo wa kisiasa unaoendelea nchini Uganda.

    Toa maoni yako
    #Habari
    Familia ya Kiongozi wa upinzani wa Uganda Bobi Wine yafunguka kukimbia Nchi kufuatia matukio ya siasa na usalama. Katika taarifa iliyotolewa, Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Robert Kyagulanyi Ssentamu, maarufu kama Bobi Wine, amethibitisha mbele ya Wakaguzi wa haki za binadamu Mjini Geneva kwamba Mke wake, Barbie Itungo Kyagulanyi, na Watoto wao wametoka Uganda kwa sababu za hofu ya maisha yao kufuatia hali tete inayojitokeza nchini mwao baada ya uchaguzi wa Rais. Katika hotuba yake kupitia video mbele ya Geneva Summit for Human Rights and Democracy, Bobi Wine alisema wazi: “Mke wangu na Watoto walilazimika kukimbia nchi kwa hofu ya maisha yao.” - Bobi Wine. Alifafanua kuwa usalama wa familia yake uliathirika sana kutokana na operesheni za vikosi vya usalama zilizoendelea mara tu baada ya uchaguzi wa 15 Januari 2026, ambapo serikali ilitangaza ushindi wa Rais Yoweri Museveni ambayo Bobi Wine ameipinga kwa madai ya udanganyifu wa kura na ukandamizaji wa upinzani. Bobi Wine pia alidai kwamba vikosi vya usalama: “Vilivamia nyumba yangu, vikamtesa Mke wangu, kumfanya asiwe na chaguo ila kuondoka na Watoto wakiwa nje ya nchi.” amesema Habari kwamba familia yake imeondoka Uganda na si tu kutoroka nyumba yao ya Magere imetolewa mara tu baada ya miezi ya mvutano mkali, ikiwa ni pamoja na madai ya mashambulizi, ulinzi mkali wa nyumba yao na vitisho vilivyowekwa na baadhi ya Afisa wa usalama. Katika maneno yake Mjini Geneva, Bobi Wine pia alijumuisha ombi kwa Jumuiya ya kimataifa kuhusu hatua za kulinda haki za binadamu na kuzuia ukandamizaji wa upinzani nchini Uganda. Taarifa hii inakuja katika wakati ambapo Uganda iko chini ya uangalizi wa kimataifa kufuatia ripoti za ghasia, mashambulizi dhidi ya wapinzani wa kisiasa, na madai ya upendeleo wa vyombo vya usalama kuelekea chama tawala. Kwa sasa, bado haijafahamika kwa umma ni nchi gani hasa Barbie Itungo Kyagulanyi na Watoto hao wamekwenda, ila uamuzi wao wa kukimbia unachukuliwa kama hatua ya kulinda usalama wa familia katika mzozo wa kisiasa unaoendelea nchini Uganda. Toa maoni yako #Habari
    0 Kommentare 0 Anteile 234 Ansichten
  • Mbunge wa Congo aibua taharuki baada ya kudaiwa kuchaguliwa pia Uganda.

    Kashfa ya kisiasa imeibuka na kuzua mjadala mzito katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) baada ya taarifa kudai kuwa Mbunge wa kitaifa aliyechaguliwa mwaka 2023 nchini humo, amechaguliwa tena kuwa Mbunge wa kitaifa nchini Uganda mwaka 2026.

    Robert Agenonga, ambaye alichaguliwa mwaka 2023 katika jimbo la Mahagi, Mkoani Ituri, kwa takribani kura 20,000, sasa anatajwa kuwa katikati ya mzozo mkubwa wa kisiasa.

    Agenonga aliingia Bungeni kupitia Muungano wa kisiasa wa 4AC, unaohusishwa kwa karibu na aliyekuwa Naibu Waziri Mkuu wa zamani, Peter Kazadi, pamoja na Waziri Msaidizi wa sasa wa Ulinzi, Eliezer Ntambwe.

    Kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali vinavyoelezwa kuwa vinafanana katika taarifa zao, Mbunge huyo wa Congo alichaguliwa kuwa Mbunge wa kitaifa nchini Uganda mwaka 2026. Ikiwa madai hayo yatathibitishwa rasmi, hali hiyo inaweza kuibua maswali mazito ya kisheria na kisiasa.

    Wachambuzi wa masuala ya utawala wanaeleza kuwa tukio hilo linaweza kugusa moja kwa moja hoja ya uraia wa nchi mbili, uaminifu wa kikatiba kwa taasisi za taifa, pamoja na uhalali wa mchakato wa uchaguzi katika nchi zote mbili. Sheria za uchaguzi na katiba za mataifa hayo zina masharti yanayohusu utiifu wa Viongozi kwa dola moja, jambo linaloweza kuathiri hadhi ya uwakilishi wake.

    Hadi kufikia sasa, hakuna tamko rasmi lililotolewa na Robert Agenonga mwenyewe wala mamlaka za Congo kuhusiana na taarifa hizo. Hata hivyo, sakata hili linaelezwa kuwa linaweza kuchukua sura ya kitaifa na hata kuathiri uhusiano wa kidiplomasia kati ya Kinshasa na Kampala iwapo litathibitishwa.

    Maendeleo zaidi yanatarajiwa huku umma ukisubiri kauli ya Wahusika na taasisi husika kuhusu uhalali wa madai hayo.

    Toa maoni yako
    #Habari
    Mbunge wa Congo aibua taharuki baada ya kudaiwa kuchaguliwa pia Uganda. Kashfa ya kisiasa imeibuka na kuzua mjadala mzito katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) baada ya taarifa kudai kuwa Mbunge wa kitaifa aliyechaguliwa mwaka 2023 nchini humo, amechaguliwa tena kuwa Mbunge wa kitaifa nchini Uganda mwaka 2026. Robert Agenonga, ambaye alichaguliwa mwaka 2023 katika jimbo la Mahagi, Mkoani Ituri, kwa takribani kura 20,000, sasa anatajwa kuwa katikati ya mzozo mkubwa wa kisiasa. Agenonga aliingia Bungeni kupitia Muungano wa kisiasa wa 4AC, unaohusishwa kwa karibu na aliyekuwa Naibu Waziri Mkuu wa zamani, Peter Kazadi, pamoja na Waziri Msaidizi wa sasa wa Ulinzi, Eliezer Ntambwe. Kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali vinavyoelezwa kuwa vinafanana katika taarifa zao, Mbunge huyo wa Congo alichaguliwa kuwa Mbunge wa kitaifa nchini Uganda mwaka 2026. Ikiwa madai hayo yatathibitishwa rasmi, hali hiyo inaweza kuibua maswali mazito ya kisheria na kisiasa. Wachambuzi wa masuala ya utawala wanaeleza kuwa tukio hilo linaweza kugusa moja kwa moja hoja ya uraia wa nchi mbili, uaminifu wa kikatiba kwa taasisi za taifa, pamoja na uhalali wa mchakato wa uchaguzi katika nchi zote mbili. Sheria za uchaguzi na katiba za mataifa hayo zina masharti yanayohusu utiifu wa Viongozi kwa dola moja, jambo linaloweza kuathiri hadhi ya uwakilishi wake. Hadi kufikia sasa, hakuna tamko rasmi lililotolewa na Robert Agenonga mwenyewe wala mamlaka za Congo kuhusiana na taarifa hizo. Hata hivyo, sakata hili linaelezwa kuwa linaweza kuchukua sura ya kitaifa na hata kuathiri uhusiano wa kidiplomasia kati ya Kinshasa na Kampala iwapo litathibitishwa. Maendeleo zaidi yanatarajiwa huku umma ukisubiri kauli ya Wahusika na taasisi husika kuhusu uhalali wa madai hayo. Toa maoni yako #Habari
    0 Kommentare 0 Anteile 142 Ansichten
  • RDC: Majeshi ya Congo na Uganda yatathmini operesheni SHUJAA Beni.

    Luteni Jenerali Ychalingonza Nduru Jacques ameongoza kikao cha tathmini ya operesheni za pamoja za kijeshi kati ya Jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (FARDC) na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Uganda (UPDF) katika Mji wa Beni, Mkoa wa Nord-Kivu.

    Kikao hicho kilifanyika siku ya Jana Jumanne na kuhudhuriwa pia na Luteni Jenerali Kayanja Muhanga kutoka Uganda pamoja na Makamanda wengine waandamizi wa majeshi ya mataifa hayo mawili. Mkutano huo ni mwendelezo wa kikao kilichofanyika Mjini Kinshasa mwezi Juni 2025, kilicholenga kutathmini operesheni ya kuwasaka Wapiganaji wa kundi la ADF-MTN-ISCARP na kurekebisha mikakati ya kukabiliana na vitisho vipya vya kiusalama.

    Operesheni SHUJAA ni ushirikiano wa kijeshi kati ya Congo na Uganda unaolenga kutokomeza makundi ya Waasi na magaidi yanayohatarisha usalama mashariki mwa Congo, hususan katika maeneo ya Beni, Lubero na Ituri.

    Katika tathmini hiyo, Viongozi hao wa kijeshi wamepongeza mafanikio ya kimkakati yaliyopatikana katika operesheni hizo, wakieleza kuwa mashambulizi kadhaa ya makundi yenye silaha yamezuiwa na miundombinu yao kuvurugwa. Hata hivyo, wamebainisha kuwa bado kuna mashambulizi yanayoendelea katika baadhi ya maeneo, jambo linaloashiria umuhimu wa kuimarisha zaidi operesheni za usalama.

    Maeneo ya Lubero, Beni na Ituri yamekuwa yakikumbwa na mashambulizi ya mara kwa mara kutoka kwa makundi yenye silaha, hasa ADF, hali inayosababisha vifo vya Raia na maelfu ya wananchi kulazimika kuyahama makazi yao.

    Viongozi hao wawili wa kijeshi wameisisitiza haja ya kuongeza nguvu katika operesheni za pamoja, kuimarisha uratibu wa kijasusi na kuendelea na mikakati madhubuti ili kurejesha amani ya kudumu katika ukanda huo.

    Tathmini hiyo inatajwa kuwa hatua muhimu katika kuendeleza ushirikiano wa kijeshi kati ya nchi hizo mbili, huku ikionyesha dhamira ya pamoja ya kukabiliana na vitisho vya usalama vinavyoendelea mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

    Toa maoni yako

    #Habari
    RDC: Majeshi ya Congo na Uganda yatathmini operesheni SHUJAA Beni. Luteni Jenerali Ychalingonza Nduru Jacques ameongoza kikao cha tathmini ya operesheni za pamoja za kijeshi kati ya Jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (FARDC) na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Uganda (UPDF) katika Mji wa Beni, Mkoa wa Nord-Kivu. Kikao hicho kilifanyika siku ya Jana Jumanne na kuhudhuriwa pia na Luteni Jenerali Kayanja Muhanga kutoka Uganda pamoja na Makamanda wengine waandamizi wa majeshi ya mataifa hayo mawili. Mkutano huo ni mwendelezo wa kikao kilichofanyika Mjini Kinshasa mwezi Juni 2025, kilicholenga kutathmini operesheni ya kuwasaka Wapiganaji wa kundi la ADF-MTN-ISCARP na kurekebisha mikakati ya kukabiliana na vitisho vipya vya kiusalama. Operesheni SHUJAA ni ushirikiano wa kijeshi kati ya Congo na Uganda unaolenga kutokomeza makundi ya Waasi na magaidi yanayohatarisha usalama mashariki mwa Congo, hususan katika maeneo ya Beni, Lubero na Ituri. Katika tathmini hiyo, Viongozi hao wa kijeshi wamepongeza mafanikio ya kimkakati yaliyopatikana katika operesheni hizo, wakieleza kuwa mashambulizi kadhaa ya makundi yenye silaha yamezuiwa na miundombinu yao kuvurugwa. Hata hivyo, wamebainisha kuwa bado kuna mashambulizi yanayoendelea katika baadhi ya maeneo, jambo linaloashiria umuhimu wa kuimarisha zaidi operesheni za usalama. Maeneo ya Lubero, Beni na Ituri yamekuwa yakikumbwa na mashambulizi ya mara kwa mara kutoka kwa makundi yenye silaha, hasa ADF, hali inayosababisha vifo vya Raia na maelfu ya wananchi kulazimika kuyahama makazi yao. Viongozi hao wawili wa kijeshi wameisisitiza haja ya kuongeza nguvu katika operesheni za pamoja, kuimarisha uratibu wa kijasusi na kuendelea na mikakati madhubuti ili kurejesha amani ya kudumu katika ukanda huo. Tathmini hiyo inatajwa kuwa hatua muhimu katika kuendeleza ushirikiano wa kijeshi kati ya nchi hizo mbili, huku ikionyesha dhamira ya pamoja ya kukabiliana na vitisho vya usalama vinavyoendelea mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo. Toa maoni yako #Habari
    0 Kommentare 0 Anteile 209 Ansichten
  • Waziri wa Habari Uganda akemea shambulio la kijeshi nyumbani kwa Bobi Wine.

    Waziri wa Habari nchini Uganda, Chris Baryomunsi, amelaani vikali madai ya shambulio la kijeshi lililofanyika katika makazi ya Mwanasiasa wa upinzani Bobi Wine, akisisitiza kuwa hakuna sababu ya kisheria ya kumzuia kurejea nyumbani kwake.

    Akizungumza na shirika la habari la Reuters, Baryomunsi alisema kuwa Bobi Wine hakufanya kosa lolote na anastahili kulindwa kama raia mwingine yeyote wa Uganda. Alieleza wazi kuwa hatua zozote za vitisho au uvamizi dhidi ya makazi ya raia hazikubaliki. Alisema, “Bobi Wine hana kosa lolote alilofanya, na ana haki kamili ya kurejea nyumbani kwake bila hofu.”

    Kwa upande wake, Bobi Wine amekuwa akidai kwa muda mrefu kuwa yuko mafichoni akihofia usalama wake, baada ya kudai kuwa jeshi la Uganda lilipewa maagizo ya kumtafuta na kumkamata. Kiongozi huyo wa upinzani pia amedai kuwa baadhi ya Wanafamilia wake waliwahi kukamatwa kwa nguvu, jambo lililoongeza hofu juu ya usalama wake binafsi.

    Katika mazingira hayo ya mvutano, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Uganda, Jenerali Muhoozi Kainerugaba, amekuwa akitoa kauli kupitia mtandao wa X (Zamani Twitter), akidokeza kuwa kumkamata Bobi Wine si jambo gumu kwani wanajua alipojificha. Kauli hizo zimeibua mjadala mkubwa ndani na nje ya Uganda kuhusu heshima ya haki za binadamu na uhuru wa kisiasa.

    Tukio hili linaendelea kufuatiliwa kwa karibu na wadau wa siasa pamoja na mashirika ya haki za binadamu, huku wito ukitolewa kwa mamlaka za Uganda kuheshimu sheria, kulinda raia wao, na kuhakikisha kuwa tofauti za kisiasa hazigeuki kuwa vitisho vya usalama kwa watu binafsi.

    Toa maoni yako
    #Habari
    Waziri wa Habari Uganda akemea shambulio la kijeshi nyumbani kwa Bobi Wine. Waziri wa Habari nchini Uganda, Chris Baryomunsi, amelaani vikali madai ya shambulio la kijeshi lililofanyika katika makazi ya Mwanasiasa wa upinzani Bobi Wine, akisisitiza kuwa hakuna sababu ya kisheria ya kumzuia kurejea nyumbani kwake. Akizungumza na shirika la habari la Reuters, Baryomunsi alisema kuwa Bobi Wine hakufanya kosa lolote na anastahili kulindwa kama raia mwingine yeyote wa Uganda. Alieleza wazi kuwa hatua zozote za vitisho au uvamizi dhidi ya makazi ya raia hazikubaliki. Alisema, “Bobi Wine hana kosa lolote alilofanya, na ana haki kamili ya kurejea nyumbani kwake bila hofu.” Kwa upande wake, Bobi Wine amekuwa akidai kwa muda mrefu kuwa yuko mafichoni akihofia usalama wake, baada ya kudai kuwa jeshi la Uganda lilipewa maagizo ya kumtafuta na kumkamata. Kiongozi huyo wa upinzani pia amedai kuwa baadhi ya Wanafamilia wake waliwahi kukamatwa kwa nguvu, jambo lililoongeza hofu juu ya usalama wake binafsi. Katika mazingira hayo ya mvutano, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Uganda, Jenerali Muhoozi Kainerugaba, amekuwa akitoa kauli kupitia mtandao wa X (Zamani Twitter), akidokeza kuwa kumkamata Bobi Wine si jambo gumu kwani wanajua alipojificha. Kauli hizo zimeibua mjadala mkubwa ndani na nje ya Uganda kuhusu heshima ya haki za binadamu na uhuru wa kisiasa. Tukio hili linaendelea kufuatiliwa kwa karibu na wadau wa siasa pamoja na mashirika ya haki za binadamu, huku wito ukitolewa kwa mamlaka za Uganda kuheshimu sheria, kulinda raia wao, na kuhakikisha kuwa tofauti za kisiasa hazigeuki kuwa vitisho vya usalama kwa watu binafsi. Toa maoni yako #Habari
    0 Kommentare 0 Anteile 161 Ansichten
  • YANGA PRINCESS

    #CONFIRMED;Uongozi wa Yanga Princess upo hatua za mwisho kabisa kukumilisha usajili wa kiungo RITICIA NABBOSA raia wa Uganda.

    #Rittisia #YangaPrincess #TimuYaWanchi

    #SportsElite
    YANGA PRINCESS 🚨#CONFIRMED;Uongozi wa Yanga Princess upo hatua za mwisho kabisa kukumilisha usajili wa kiungo RITICIA NABBOSA raia wa Uganda. #Rittisia #YangaPrincess #TimuYaWanchi #SportsElite
    0 Kommentare 0 Anteile 923 Ansichten
  • Aliyetiwa hatiani kuwa Mhalifu wa kivita na Mahakama ya kimataifa ya (ICC) kwa makosa mbalimbali, Thomas Lubanga, ametangaza kuunda kundi jipya la Waasi lenye lengo la kuiangusha Serikali ya Jimbo la Ituri, lililopo Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo .

    Nchi ya DR Congo imekuwa ikikabiliwa na tishio la kiusalama katika Mikoa ya mashariki ambapo makundi ya Waasi ikiwemo Muungano wa Waasi wa AFC/M23 unaoshikilia Miji ya Goma, Bukavu, Nyabibwe na Walikale.

    Hata hivyo, uamuzi wa Thomas Lubanga ambaye ni Mzaliwa wa Mkoa wa Ituri Nchini DR Congo na anayeishi Nchini Uganda , kutangaza kuanzisha Kundi lake la Waasi alilolipa jina Convention for the Popular Revolution (CPR) ambalo litaongeza hofu ya machafuko Nchini humo wakati huu ambao Serikali ya Rais Felix Tshisekedi inatafuta maridhiano na M23 kwa njia ya mazungumzo.

    Shirika la Habari la Reuters, limeripoti leo Jumanne Aprili Mosi, 2025, kuwa Lubanga ambaye ni Mzaliwa wa Ituri, alihukumiwa na Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) mwaka 2012 kwa makosa ya kuwasajili Watoto kama Askari na akapewa kifungo cha miaka 14 Gerezani, baadaye aliachiliwa mwaka 2020 na Rais wa DR Congo, Felix Tshisekedi kisha akamteua kuwa sehemu ya kikosi kazi cha kuleta amani Jimboni Ituri.

    Hata hivyo, mwaka 2022 alitekwa nyara kwa miezi miwili na kundi la Waasi, tukio analodai kupangwa na Serikali ya DR Congo kwa lengo kumpoteza ila kwa sasa anaishi Nchini Uganda.

    Aliyetiwa hatiani kuwa Mhalifu wa kivita na Mahakama ya kimataifa ya (ICC) kwa makosa mbalimbali, Thomas Lubanga, ametangaza kuunda kundi jipya la Waasi lenye lengo la kuiangusha Serikali ya Jimbo la Ituri, lililopo Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo 🇨🇩. Nchi ya DR Congo imekuwa ikikabiliwa na tishio la kiusalama katika Mikoa ya mashariki ambapo makundi ya Waasi ikiwemo Muungano wa Waasi wa AFC/M23 unaoshikilia Miji ya Goma, Bukavu, Nyabibwe na Walikale. Hata hivyo, uamuzi wa Thomas Lubanga ambaye ni Mzaliwa wa Mkoa wa Ituri Nchini DR Congo na anayeishi Nchini Uganda 🇺🇬, kutangaza kuanzisha Kundi lake la Waasi alilolipa jina Convention for the Popular Revolution (CPR) ambalo litaongeza hofu ya machafuko Nchini humo wakati huu ambao Serikali ya Rais Felix Tshisekedi inatafuta maridhiano na M23 kwa njia ya mazungumzo. Shirika la Habari la Reuters, limeripoti leo Jumanne Aprili Mosi, 2025, kuwa Lubanga ambaye ni Mzaliwa wa Ituri, alihukumiwa na Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) mwaka 2012 kwa makosa ya kuwasajili Watoto kama Askari na akapewa kifungo cha miaka 14 Gerezani, baadaye aliachiliwa mwaka 2020 na Rais wa DR Congo, Felix Tshisekedi kisha akamteua kuwa sehemu ya kikosi kazi cha kuleta amani Jimboni Ituri. Hata hivyo, mwaka 2022 alitekwa nyara kwa miezi miwili na kundi la Waasi, tukio analodai kupangwa na Serikali ya DR Congo kwa lengo kumpoteza ila kwa sasa anaishi Nchini Uganda.
    0 Kommentare 0 Anteile 2KB Ansichten
  • Mchambuzi Farhan JR.

    Nimeona andiko la Waukae @zakazakazi kuhusu TFF kutengeneza Vijana ambalo lilipaswa kuwa jukumu la Klabu na akienda mbali kusema kwamba TFF ndio Shirikisho pekee duniani ambalo lina kituo ambacho kinazalisha na kulea vipaji vya vijana, kwanza kabla ya kupingana nae kuna kitu kwanza nataka kukiweka sawa kwenye eneo hilo.

    Duniani kote Mashirikisho kama TFF yamejikita zaidi kwenye DEVELOPMENT PROJECTS yaani Miradi ya maendeleo kisha wakaachia Mashindano kadhaa yasimamiwe na Bodi zao za Ligi kwa 90% bila kuyaingilia, TFF anachokifanya ni sahihi lakini pia sio sahihi sana kufanya yeye alipaswa kuwa na CLINICS tu ila kuna changamoto sehemu ambayo imeletwa na TFF wenyewe.

    Duniani Klabu zinaweza kuendesha miradi ya Vijana kwasababu kuna kitu kinaitwa FALSAFA ya nchi kwenye mpira, kuanzia mifumo, afya tiba, afya lishe na miundo yote ambayo portifolio hutoka Shirikisho (TFF) Klabu zinaenda kutekeleza mifumo hiyo na kuadjust baadhi ya maeneo halafu Vijana wakienda Clinics za Kitaifa wanaenda kukazia tu.

    Swali linakuja Je Waukaye @zakazakazi FALSAFA ya Tanzania kwenye mpira wa Miguu ni ipi? Iliwasilishwa lini? Anayo nani? Hilo ni Jukumu la TFF ambalo halijatekelezwa, kuna kitu kinaitwa TALENT ID FRAMEWORK ili kupata Vijana je tunayo? Ipoje, anayo nani? Inasemaje? Klabu hazina Mwongozo kutoka kwa TFF? Academy zote nchini zipite humo LAZIMA TFF wafanye wanachoweza, tupo katikati, TFF ASIMAMIE HILO KIKAMILIFU.

    TFF wasiende mbali waende tu hapo Uganda ilipo FUFA, wana Talent ID Framework ambayo Mashirikisho yoote yalipigwa huo Msasa sambamba na Kamati zao tendaji, ndio maana Uganda wapo mbali mno kwenye soka la Vijana kwenye Klabu zao na National Team, kwasababu wana ramani wanaifuata, wameintergrate mfumo wao na FIFA Talent Development Schemes (TDS) je sisi lini tutaforce Klabu zipite humo?

    TFF anajipa majukumu ambayo mengine sio ya kwake, kujadili mikataba ya kibiashara sio Jukumu lake bali Vilabu na Bodi yao, TFF anabaki kama Baba pekee, duniani kote TFF zao zina majukumu yao ukitoa michuano ya FA na Ngao basi Ligi Kuu sio mali yao, TFF ASIMAMIE HASWA JUKUMU LA MAENDELEO NI LAKE.

    Mchambuzi Farhan JR. Nimeona andiko la Waukae @zakazakazi kuhusu TFF kutengeneza Vijana ambalo lilipaswa kuwa jukumu la Klabu na akienda mbali kusema kwamba TFF ndio Shirikisho pekee duniani ambalo lina kituo ambacho kinazalisha na kulea vipaji vya vijana, kwanza kabla ya kupingana nae kuna kitu kwanza nataka kukiweka sawa kwenye eneo hilo. Duniani kote Mashirikisho kama TFF yamejikita zaidi kwenye DEVELOPMENT PROJECTS yaani Miradi ya maendeleo kisha wakaachia Mashindano kadhaa yasimamiwe na Bodi zao za Ligi kwa 90% bila kuyaingilia, TFF anachokifanya ni sahihi lakini pia sio sahihi sana kufanya yeye alipaswa kuwa na CLINICS tu ila kuna changamoto sehemu ambayo imeletwa na TFF wenyewe. Duniani Klabu zinaweza kuendesha miradi ya Vijana kwasababu kuna kitu kinaitwa FALSAFA ya nchi kwenye mpira, kuanzia mifumo, afya tiba, afya lishe na miundo yote ambayo portifolio hutoka Shirikisho (TFF) Klabu zinaenda kutekeleza mifumo hiyo na kuadjust baadhi ya maeneo halafu Vijana wakienda Clinics za Kitaifa wanaenda kukazia tu. Swali linakuja Je Waukaye @zakazakazi FALSAFA ya Tanzania kwenye mpira wa Miguu ni ipi? Iliwasilishwa lini? Anayo nani? Hilo ni Jukumu la TFF ambalo halijatekelezwa, kuna kitu kinaitwa TALENT ID FRAMEWORK ili kupata Vijana je tunayo? Ipoje, anayo nani? Inasemaje? Klabu hazina Mwongozo kutoka kwa TFF? Academy zote nchini zipite humo LAZIMA TFF wafanye wanachoweza, tupo katikati, TFF ASIMAMIE HILO KIKAMILIFU. TFF wasiende mbali waende tu hapo Uganda ilipo FUFA, wana Talent ID Framework ambayo Mashirikisho yoote yalipigwa huo Msasa sambamba na Kamati zao tendaji, ndio maana Uganda wapo mbali mno kwenye soka la Vijana kwenye Klabu zao na National Team, kwasababu wana ramani wanaifuata, wameintergrate mfumo wao na FIFA Talent Development Schemes (TDS) je sisi lini tutaforce Klabu zipite humo? TFF anajipa majukumu ambayo mengine sio ya kwake, kujadili mikataba ya kibiashara sio Jukumu lake bali Vilabu na Bodi yao, TFF anabaki kama Baba pekee, duniani kote TFF zao zina majukumu yao ukitoa michuano ya FA na Ngao basi Ligi Kuu sio mali yao, TFF ASIMAMIE HASWA JUKUMU LA MAENDELEO NI LAKE.
    Like
    2
    0 Kommentare 0 Anteile 1KB Ansichten
  • Jeshi la Nchi ya Uganda limesema limewaua Wapiganaji 242 wa kundi la Waasi Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo linalojulikana kama CODECO baada ya kushambulia kambi ya Jeshi hilo la Uganda mpakani mashariki mwa DR Congo mapema wiki hii ambapo madai yamepingwa na Kundi hilo.

    Msemaji wa Jeshi la Uganda, Chris Magezi, amesema mamia ya Wapiganaji wa kundi la CODECO walishambulia kituo cha kijeshi cha Uganda People's Defence Forces (UPDF) katika eneo la Fataki, Mkoani Ituri, siku ya Jumatano na Alhamisi. Jeshi hilo lilijibu mashambulizi hayo mara zote mbili, likiwaangamiza Wapiganaji 31 siku ya kwanza na 211 siku ya pili, Magezi alisema katika chapisho kwenye akaunti yake ya Mtandao wa X Ijumaa usiku na kuongeza kuwa askari mmoja wa UPDF aliuawa na wengine wanne kujeruhiwa.

    Msemaji wa CODECO, Basa Zukpa Gerson, alipinga taarifa ya jeshi Jumamosi, akisema kundi hilo lilipoteza wapiganaji wawili tu na kwamba idadi ya vifo vya Wanajeshi wa UPDF ilikuwa juu zaidi. Chanzo kimoja cha Umoja wa Mataifa ambacho hakikutaka kutajwa jina kilisema Waasi 70 na Wanajeshi wa Uganda 12 waliuawa.

    Kulikuwa na mapigano zaidi kati ya pande hizo mbili asubuhi ya Jumamosi, alisema Msemaji wa CODECO na kiongozi mmoja wa jamii za kiraia wa eneo hilo. Wapiganaji wa CODECO wanasema lengo lao ni kuwalinda Wakulima wa Lendu dhidi ya Wafungaji wa Hema, ambao kihistoria wamekuwa wakigombana kuhusu ardhi.

    Kundi hilo ni moja ya makundi mengi ya Waasi yanayopigania ardhi na rasilimali za madini mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, ambapo Waasi wa M23 wameongeza mashambulizi mwaka huu na kupata mafanikio makubwa. Uganda ilituma wanajeshi DR Congo mwaka 2021 kusaidia Serikali kupambana na kundi lingine la Waasi, Allied Democratic Forces (ADF), ambalo lina uhusiano na Islamic State na linafanya mashambulizi ya kikatili kwenye baadhi ya Vijiji.

    Jeshi la Nchi ya Uganda 🇺🇬 limesema limewaua Wapiganaji 242 wa kundi la Waasi Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo 🇨🇩 linalojulikana kama CODECO baada ya kushambulia kambi ya Jeshi hilo la Uganda mpakani mashariki mwa DR Congo mapema wiki hii ambapo madai yamepingwa na Kundi hilo. Msemaji wa Jeshi la Uganda, Chris Magezi, amesema mamia ya Wapiganaji wa kundi la CODECO walishambulia kituo cha kijeshi cha Uganda People's Defence Forces (UPDF) katika eneo la Fataki, Mkoani Ituri, siku ya Jumatano na Alhamisi. Jeshi hilo lilijibu mashambulizi hayo mara zote mbili, likiwaangamiza Wapiganaji 31 siku ya kwanza na 211 siku ya pili, Magezi alisema katika chapisho kwenye akaunti yake ya Mtandao wa X Ijumaa usiku na kuongeza kuwa askari mmoja wa UPDF aliuawa na wengine wanne kujeruhiwa. Msemaji wa CODECO, Basa Zukpa Gerson, alipinga taarifa ya jeshi Jumamosi, akisema kundi hilo lilipoteza wapiganaji wawili tu na kwamba idadi ya vifo vya Wanajeshi wa UPDF ilikuwa juu zaidi. Chanzo kimoja cha Umoja wa Mataifa ambacho hakikutaka kutajwa jina kilisema Waasi 70 na Wanajeshi wa Uganda 12 waliuawa. Kulikuwa na mapigano zaidi kati ya pande hizo mbili asubuhi ya Jumamosi, alisema Msemaji wa CODECO na kiongozi mmoja wa jamii za kiraia wa eneo hilo. Wapiganaji wa CODECO wanasema lengo lao ni kuwalinda Wakulima wa Lendu dhidi ya Wafungaji wa Hema, ambao kihistoria wamekuwa wakigombana kuhusu ardhi. Kundi hilo ni moja ya makundi mengi ya Waasi yanayopigania ardhi na rasilimali za madini mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, ambapo Waasi wa M23 wameongeza mashambulizi mwaka huu na kupata mafanikio makubwa. Uganda ilituma wanajeshi DR Congo mwaka 2021 kusaidia Serikali kupambana na kundi lingine la Waasi, Allied Democratic Forces (ADF), ambalo lina uhusiano na Islamic State na linafanya mashambulizi ya kikatili kwenye baadhi ya Vijiji.
    Like
    1
    0 Kommentare 0 Anteile 1KB Ansichten
  • “…ndani ya wiki moja, majeshi ya Uganda na wapiganaji wa M23 watakuwa Kisangani, kwa amri ya Rais Yoweri Museveni, Amiri Jeshi Mkuu wa majeshi ya Uganda (UPDF)…” - Muhoozi Kainerugaba, Mkuu wa Majeshi ya Uganda .

    “…ndani ya wiki moja, majeshi ya Uganda na wapiganaji wa M23 watakuwa Kisangani, kwa amri ya Rais Yoweri Museveni, Amiri Jeshi Mkuu wa majeshi ya Uganda (UPDF)…” - Muhoozi Kainerugaba, Mkuu wa Majeshi ya Uganda 🇺🇬.
    0 Kommentare 0 Anteile 840 Ansichten
  • World Happiness Report 2025 imetangaza orodha ya Nchi zenye furaha zaidi Duniani huku Nchi ya Finland ikiendelea kushika nafasi ya kwanza kwa mwaka wa nane (8) mfululizo, Tanzania imeshika nafasi ya 136 kati ya Nchi 147, ikishuka kwa nafasi tano kutoka nafasi ya 131 mwaka uliopita. Nafasi ya sasa inaiweka Nchi hiyo kuwa miongoni mwa Nchi 11 za mwisho Duniani kwa viwango vya furaha.

    Cha kushangaza ni kwamba Tanzania , licha ya kuwa na amani na utajiri mkubwa wa maliasili, imepitwa hata na mataifa yenye migogoro kama Somalia . Nchi jirani kama Kenya na Uganda , ambazo mara kwa mara hukumbwa na changamoto za kisiasa na kiusalama, zimepata nafasi za juu zaidi. Hapa chini ni orodha ya Nchi zenye furaha kwa mujibu wa World Happiness Report 2025, kuonyesha kumi bora na zilizoshika mkia. Kwa Afrika Mauritius inaongoza, wakati Lebanon , Sierra Leone na Afghanistan ni Nchi tatu za mwisho Duniani.

    1. Finland
    2. Denmark
    3. Iceland
    4. Sweden
    5. Uholanzi

    6. Costa Rica
    7. Norway
    8. Israel
    9. Luxemborg
    10.Mexico

    78. Mauritius
    79. Libya
    84. Algeria
    115. Kenya
    116. Uganda

    122. Somalia
    136. Tanzania
    145. Lebanon
    146. Sierra Leone
    147. Afghanistan

    World Happiness Report 2025 imetangaza orodha ya Nchi zenye furaha zaidi Duniani huku Nchi ya Finland 🇫🇮 ikiendelea kushika nafasi ya kwanza kwa mwaka wa nane (8) mfululizo, Tanzania imeshika nafasi ya 136 kati ya Nchi 147, ikishuka kwa nafasi tano kutoka nafasi ya 131 mwaka uliopita. Nafasi ya sasa inaiweka Nchi hiyo kuwa miongoni mwa Nchi 11 za mwisho Duniani kwa viwango vya furaha. Cha kushangaza ni kwamba Tanzania 🇹🇿, licha ya kuwa na amani na utajiri mkubwa wa maliasili, imepitwa hata na mataifa yenye migogoro kama Somalia 🇸🇴. Nchi jirani kama Kenya 🇰🇪 na Uganda 🇺🇬, ambazo mara kwa mara hukumbwa na changamoto za kisiasa na kiusalama, zimepata nafasi za juu zaidi. Hapa chini ni orodha ya Nchi zenye furaha kwa mujibu wa World Happiness Report 2025, kuonyesha kumi bora na zilizoshika mkia. Kwa Afrika Mauritius 🇲🇷 inaongoza, wakati Lebanon 🇱🇧, Sierra Leone 🇸🇱na Afghanistan 🇦🇫 ni Nchi tatu za mwisho Duniani. 1. Finland 🇫🇮 2. Denmark 🇩🇰 3. Iceland 🇮🇸 4. Sweden 🇸🇪 5. Uholanzi 🇳🇱 6. Costa Rica 🇨🇷 7. Norway 🇳🇴 8. Israel 🇮🇱 9. Luxemborg 🇱🇺 10.Mexico 🇲🇽 78. Mauritius 🇲🇷 79. Libya 🇱🇾 84. Algeria 🇩🇿 115. Kenya 🇰🇪 116. Uganda 🇺🇬 122. Somalia 🇸🇴 136. Tanzania 🇹🇿 145. Lebanon 🇱🇧 146. Sierra Leone 🇸🇱 147. Afghanistan 🇦🇫
    0 Kommentare 0 Anteile 2KB Ansichten
  • Zambia wana Laptop zao zinaitwa NEO, Rwanda wana MARA Phones na Satelite , Uganda wana Simu zao zinaitwa SIMI, Kenya wana Laptop zao zinaitwa TAIFA Wana Starlink pia wana Satelite yao, Tanzania tuna nini ?
    Zambia wana Laptop zao zinaitwa NEO, Rwanda wana MARA Phones na Satelite , Uganda wana Simu zao zinaitwa SIMI, Kenya wana Laptop zao zinaitwa TAIFA Wana Starlink pia wana Satelite yao, Tanzania tuna nini ?
    Like
    Wow
    2
    0 Kommentare 0 Anteile 2KB Ansichten
  • Katika hatua mpya ya mzozo unaoendelea Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo , kundi la Waasi wa M23 likishirikiana na Muungano wa Mto Congo (AFC) limetangaza kuwa Wanajeshi wa zamani wa Jeshi la DR Congo (FARDC) waliokamatwa au kujisalimisha wamehitimu mafunzo ya kiitikadi na mbinu za kijeshi.

    Katika taarifa ya Kundi la M23 kwenye mtandao wao wa X leo Februari 18, picha zilionyesha Wanajeshi hao wakiwa na sare na silaha rasmi za wanamgambo hao. Ujumbe uliambatana na chapisho hilo ulieleza:

    "Wanajeshi wa zamani wa FARDC, waliokamatwa au kujisalimisha, wamemaliza mafunzo ya kiitikadi na mbinu huko Rumangabo Mjini Goma chini ya AFC/M23. Sasa wakiwa na vifaa kamili na wanaolipwa, wametumwa Lubero, ambako wanashiriki kikamilifu muungano wa serikali."

    Wakati huo huo, Uganda imetangaza kuwa vikosi vyake vya kijeshi vimeanza kuelekea Bunia, DRC, ikiwa ni siku chache baada ya Jeshi la Uganda kutoa muda wa saa 24 kwa Askari waliopo eneo hilo kujisalimisha.

    Taarifa nyingine kuwa, hapo jana Kundi la Waasi hao wa M23 wamefanikiwa kuteka eneo la Kamanyola na sasa hivi wanajipanga kuelekea Uvira, Fizi kisha Mkoa wa Tanganyika (Kalemie) kabla ya kwenda Mjini Lubumbashi. Kwa mujibu wa Wananchi wa Kamanyala wanasema kuwa Kundi la Wapiganaji wa Wazalendo ambao wanapigana kwa upande wa Serikali waliibwa Silaha zao kisha wakakimbia na kuwaachia M23 kuichukua Kamanyola.

    Katika hatua mpya ya mzozo unaoendelea Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo 🇨🇩, kundi la Waasi wa M23 likishirikiana na Muungano wa Mto Congo (AFC) limetangaza kuwa Wanajeshi wa zamani wa Jeshi la DR Congo (FARDC) waliokamatwa au kujisalimisha wamehitimu mafunzo ya kiitikadi na mbinu za kijeshi. Katika taarifa ya Kundi la M23 kwenye mtandao wao wa X leo Februari 18, picha zilionyesha Wanajeshi hao wakiwa na sare na silaha rasmi za wanamgambo hao. Ujumbe uliambatana na chapisho hilo ulieleza: "Wanajeshi wa zamani wa FARDC, waliokamatwa au kujisalimisha, wamemaliza mafunzo ya kiitikadi na mbinu huko Rumangabo Mjini Goma chini ya AFC/M23. Sasa wakiwa na vifaa kamili na wanaolipwa, wametumwa Lubero, ambako wanashiriki kikamilifu muungano wa serikali." Wakati huo huo, Uganda imetangaza kuwa vikosi vyake vya kijeshi vimeanza kuelekea Bunia, DRC, ikiwa ni siku chache baada ya Jeshi la Uganda kutoa muda wa saa 24 kwa Askari waliopo eneo hilo kujisalimisha. Taarifa nyingine kuwa, hapo jana Kundi la Waasi hao wa M23 wamefanikiwa kuteka eneo la Kamanyola na sasa hivi wanajipanga kuelekea Uvira, Fizi kisha Mkoa wa Tanganyika (Kalemie) kabla ya kwenda Mjini Lubumbashi. Kwa mujibu wa Wananchi wa Kamanyala wanasema kuwa Kundi la Wapiganaji wa Wazalendo ambao wanapigana kwa upande wa Serikali waliibwa Silaha zao kisha wakakimbia na kuwaachia M23 kuichukua Kamanyola.
    0 Kommentare 0 Anteile 1KB Ansichten
  • Mkuu wa Vikosi vya Ulinzi vya Nchi ya Uganda (UPDF), Jenerali Muhoozi Kainerugaba, amesema Uganda inatoa saa (24) vikosi vyote vilivyopo katika Mji wa Bunia Mashariki mwa Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo kuacha kuuwa Raia wa kabila la Bahima (ambalo asili yake ni kutoka Nchini Uganda) lasivyo Jeshi lake litashambulia Mji huo.

    Kainerugaba ametoa kauli hiyo Februari 15 katika mtandao wake wa X. Huku akielezwa kuwa na historia ya kuchapisha maoni ya uchochezi kuhusu sera za kigeni mara kwa mara. Alisema ana mamlaka ya Rais Yoweri Museveni, ambaye pia ni Baba yake Mzazi ambako hata hivyo, alipotafutwa Msemaji wa Jeshi la Uganda alisema hawezi kuzungumzia suala hilo.

    Hata hivyo, kabla ya kusasisha ujumbe huo kwenye mtandao wa X, Jenerali huyo alikuwa alieleza bila kutoa ushahidi, kwamba Watu kutoka kabila la Bahima walikuwa wakiuawa huko Nchini DR Congo.

    Mkuu wa Vikosi vya Ulinzi vya Nchi ya Uganda 🇺🇬 (UPDF), Jenerali Muhoozi Kainerugaba, amesema Uganda inatoa saa (24) vikosi vyote vilivyopo katika Mji wa Bunia Mashariki mwa Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo 🇨🇩 kuacha kuuwa Raia wa kabila la Bahima (ambalo asili yake ni kutoka Nchini Uganda) lasivyo Jeshi lake litashambulia Mji huo. Kainerugaba ametoa kauli hiyo Februari 15 katika mtandao wake wa X. Huku akielezwa kuwa na historia ya kuchapisha maoni ya uchochezi kuhusu sera za kigeni mara kwa mara. Alisema ana mamlaka ya Rais Yoweri Museveni, ambaye pia ni Baba yake Mzazi ambako hata hivyo, alipotafutwa Msemaji wa Jeshi la Uganda alisema hawezi kuzungumzia suala hilo. Hata hivyo, kabla ya kusasisha ujumbe huo kwenye mtandao wa X, Jenerali huyo alikuwa alieleza bila kutoa ushahidi, kwamba Watu kutoka kabila la Bahima walikuwa wakiuawa huko Nchini DR Congo.
    Like
    1
    0 Kommentare 0 Anteile 1KB Ansichten
  • #PART5

    Baada ya M23 kukamata Goma walidai hawana mpango wa kuchukua miji mingine. Jeshi la Congo (FARDC) likarelax. Kumbe ilikua mbinu ya kivita. Ghafla M23 wakavamia na kuuteka mji wa Rutshuru wenye utajiri wa dhahabu, tin na Tungsten na mji wa Masisi wenye utajiri mkubwa wa dhahabu na cassiterite.

    Mpango wa M23 ni kufika Kinshasa na kuuangusha utawala wa Rais Felix Tshisekedi. Madai ya M23 ni yaleyale ya siku zote, ambayo ni kulinda maslahi ya Watutsi waishio mashariki mwa nchi hiyo, kupambana na wanamgambo wa Kihutu wa FDLR (Interahamwe), na kutaka Banyamulenge watambuliwe kama raia halali wa Congo.

    Mzozo wa mashariki mwa Congo umegharimu maisha ya mamilioni ya watu toka ulipoanza. Umoja wa Mataifa (UN) na Umoja wa Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) umepeleka askari wa kulinda amani. Ikumbukwe askari hao hawapigani upande wa serikali wala wa waasi. Kuna watu wanadhani askari wetu wa JWTZ walioko Congo wanapigana upande wa jeshi la serikali (FARDC). Hapana. Hawapigani upande wowote. Wanalinda amani. Lakini ikitokea kuna upande unahatarisha amani utapewa haki yake ya kikatiba.

    Kwa mfano, mwaka 2012 Umoja wa mataifa uliunda jeshi la kulinda amani Congo (MONUSCO). Ndani yake kulikua na brigedi maalumu ya kunyang'anya silaha makundi ya wapiganaji - Force Intervention Bregade (FIB). Brigedi hiyo iliundwa na askari kutoka Tanzania, Malawi, Afrika Kusini na Uruguay.

    April 2012, M23 wakashambulia kambi ya FIB iliyokua mji wa Rutshuru na kuua askari watatu. Baada ya shambulio hilo, aliyekua Mkuu FIB, Jenerali James Mwakibolwa alipanga vikosi vyake kujibu mapigo. M23 walichakazwa vibaya ambapo zaidi ya askari 600 wa M23 waliuawa na wengi kujeruhiwa. Walipigwa bila huruma na kuachia miji yote waliyokua wameishikilia ikiwemo Rubaya, Kitchanga na Rutshuru. Askari 16 wa FIB nao walipoteza maisha.

    March 2013, M23 walisalimu amri na Kiongozi wao Bosco Ntaganda akakimbilia Rwanda kujisalimisha kwenye ubalozi wa Marekani. Alipelekwa ICC akahukumiwa miaka 30 na sasa anatumikia adhabu yake gereza la Leuze-en-Hainaut lililopo Ubelgiji. Moja ya makosa ambayo Ntaganda anayajutia hadi leo ni kuingia kwenye 18 za FIB iliyokua inaongozwa na Jenerali James Aloizi Mwakibolwa.

    Kumekua na jitihada mbalimbali za kumaliza mgogoro wa DRC kwa njia za kidiplomasia ikiwemo mkutano wa viongozi wakuu wa SADC na EAC uliofanyika leo jijini Dar.

    #MyaTake:
    1. Congo imeponzwa na ukarimu wake. Wakati wa vita vya Rwanda, Congo ilipokea Watutsi wengi na kuwapa hifadhi, akiwemo Kagame. Baada ya utawala wa Habyarimana kuangushwa Wahutu nao wakakimbilia Congo na kupewa hifadhi. Sasa hicho kimekua kigezo cha Rwanda kuingiza majeshi Congo kila mara kwa madai ya kuwatafuta Wahutu wa FDLR. Kwa lugha rahisi vita ya ndugu wawili (Wahutu na Watutsi) iliyopaswa kupiganwa Rwanda sasa inapiganwa Congo.

    2. Congo inateswa na mipaka ya kikoloni. Laiti wakati wa kuchora mipaka jamii yote ya Watutsi ingewekwa Rwanda, leo kusingekuwa na Banyamulenge Congo, kwahiyo Watutsi wasingepata sababu ya kuishi Congo na kujifanya raia. Ni sawa na kukuta Wamasai 1,000 pale Longido, halafu uambiwe kati yao wapo wa Kenya. Utawajuaje? Utawatofautishaje?

    3. Congo inateswa na rasilimali zake. Kama eneo la Kivu lisingekuwa na utajiri, mgogoro usingekuwa mkubwa kama ulivyo. Rejea #Part1 kujua utajiri uliopo Kivu. Kumbuka bila Kivu dunia haina laptop wala smartphones kwa sababu 80% ya coltan yote duniani inatoka Kivu.

    4. Rwanda na Uganda ni Keyplayers kwenye mgogoro wa Congo. Kwa miaka mingi majeshi yao yameigeuza Congo shamba la bibi. Waondoe majeshi yao Congo.

    5. Viongozi wengi wa M23 ni Wanyarwanda. Huu ni udhibitisho kuwa Rwanda ni kinara kwenye mgogoro huu.

    6. Congo ni kubwa sana na hivyo inakosa jeshi imara la kutosha kulinda mipaka yake yote. Congo ni kubwa mara 90 ya Rwanda. Wapo wanaoshauri igawanywe kama njia ya kutatua mgogoro. Kama ambavyo Yugoslavia iligawanywa na kumaliza vita vya wenyewe kwa wenyewe.

    7. Kiongozi wa sasa wa M23 Corneille Nangaa alikua Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi 2019 na ndiye aliyemtangaza Tshisekedi kuwa Rais kwa ushindi wa 38%. Lakini alilaumiwa kupunguza kura za Martin Fayulu aliyepata 34%. Huenda kuna ahadi alipewa haikutimizwa ndio maana akaungana na Waasi.

    Sababu hizo hapo juu zikifanyiwa kazi, mgogoro wa Congo unaweza kupungua kwa kiasi kikubwa. Mnaopenda kujifunza zaidi, naandika Kitabu. Get ready to have your copy. MWISHO.!

    (Malisa GJ )

    #PART5 Baada ya M23 kukamata Goma walidai hawana mpango wa kuchukua miji mingine. Jeshi la Congo (FARDC) likarelax. Kumbe ilikua mbinu ya kivita. Ghafla M23 wakavamia na kuuteka mji wa Rutshuru wenye utajiri wa dhahabu, tin na Tungsten na mji wa Masisi wenye utajiri mkubwa wa dhahabu na cassiterite. Mpango wa M23 ni kufika Kinshasa na kuuangusha utawala wa Rais Felix Tshisekedi. Madai ya M23 ni yaleyale ya siku zote, ambayo ni kulinda maslahi ya Watutsi waishio mashariki mwa nchi hiyo, kupambana na wanamgambo wa Kihutu wa FDLR (Interahamwe), na kutaka Banyamulenge watambuliwe kama raia halali wa Congo. Mzozo wa mashariki mwa Congo umegharimu maisha ya mamilioni ya watu toka ulipoanza. Umoja wa Mataifa (UN) na Umoja wa Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) umepeleka askari wa kulinda amani. Ikumbukwe askari hao hawapigani upande wa serikali wala wa waasi. Kuna watu wanadhani askari wetu wa JWTZ walioko Congo wanapigana upande wa jeshi la serikali (FARDC). Hapana. Hawapigani upande wowote. Wanalinda amani. Lakini ikitokea kuna upande unahatarisha amani utapewa haki yake ya kikatiba. Kwa mfano, mwaka 2012 Umoja wa mataifa uliunda jeshi la kulinda amani Congo (MONUSCO). Ndani yake kulikua na brigedi maalumu ya kunyang'anya silaha makundi ya wapiganaji - Force Intervention Bregade (FIB). Brigedi hiyo iliundwa na askari kutoka Tanzania, Malawi, Afrika Kusini na Uruguay. April 2012, M23 wakashambulia kambi ya FIB iliyokua mji wa Rutshuru na kuua askari watatu. Baada ya shambulio hilo, aliyekua Mkuu FIB, Jenerali James Mwakibolwa alipanga vikosi vyake kujibu mapigo. M23 walichakazwa vibaya ambapo zaidi ya askari 600 wa M23 waliuawa na wengi kujeruhiwa. Walipigwa bila huruma na kuachia miji yote waliyokua wameishikilia ikiwemo Rubaya, Kitchanga na Rutshuru. Askari 16 wa FIB nao walipoteza maisha. March 2013, M23 walisalimu amri na Kiongozi wao Bosco Ntaganda akakimbilia Rwanda kujisalimisha kwenye ubalozi wa Marekani. Alipelekwa ICC akahukumiwa miaka 30 na sasa anatumikia adhabu yake gereza la Leuze-en-Hainaut lililopo Ubelgiji. Moja ya makosa ambayo Ntaganda anayajutia hadi leo ni kuingia kwenye 18 za FIB iliyokua inaongozwa na Jenerali James Aloizi Mwakibolwa. Kumekua na jitihada mbalimbali za kumaliza mgogoro wa DRC kwa njia za kidiplomasia ikiwemo mkutano wa viongozi wakuu wa SADC na EAC uliofanyika leo jijini Dar. #MyaTake: 1. Congo imeponzwa na ukarimu wake. Wakati wa vita vya Rwanda, Congo ilipokea Watutsi wengi na kuwapa hifadhi, akiwemo Kagame. Baada ya utawala wa Habyarimana kuangushwa Wahutu nao wakakimbilia Congo na kupewa hifadhi. Sasa hicho kimekua kigezo cha Rwanda kuingiza majeshi Congo kila mara kwa madai ya kuwatafuta Wahutu wa FDLR. Kwa lugha rahisi vita ya ndugu wawili (Wahutu na Watutsi) iliyopaswa kupiganwa Rwanda sasa inapiganwa Congo. 2. Congo inateswa na mipaka ya kikoloni. Laiti wakati wa kuchora mipaka jamii yote ya Watutsi ingewekwa Rwanda, leo kusingekuwa na Banyamulenge Congo, kwahiyo Watutsi wasingepata sababu ya kuishi Congo na kujifanya raia. Ni sawa na kukuta Wamasai 1,000 pale Longido, halafu uambiwe kati yao wapo wa Kenya. Utawajuaje? Utawatofautishaje? 3. Congo inateswa na rasilimali zake. Kama eneo la Kivu lisingekuwa na utajiri, mgogoro usingekuwa mkubwa kama ulivyo. Rejea #Part1 kujua utajiri uliopo Kivu. Kumbuka bila Kivu dunia haina laptop wala smartphones kwa sababu 80% ya coltan yote duniani inatoka Kivu. 4. Rwanda na Uganda ni Keyplayers kwenye mgogoro wa Congo. Kwa miaka mingi majeshi yao yameigeuza Congo shamba la bibi. Waondoe majeshi yao Congo. 5. Viongozi wengi wa M23 ni Wanyarwanda. Huu ni udhibitisho kuwa Rwanda ni kinara kwenye mgogoro huu. 6. Congo ni kubwa sana na hivyo inakosa jeshi imara la kutosha kulinda mipaka yake yote. Congo ni kubwa mara 90 ya Rwanda. Wapo wanaoshauri igawanywe kama njia ya kutatua mgogoro. Kama ambavyo Yugoslavia iligawanywa na kumaliza vita vya wenyewe kwa wenyewe. 7. Kiongozi wa sasa wa M23 Corneille Nangaa alikua Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi 2019 na ndiye aliyemtangaza Tshisekedi kuwa Rais kwa ushindi wa 38%. Lakini alilaumiwa kupunguza kura za Martin Fayulu aliyepata 34%. Huenda kuna ahadi alipewa haikutimizwa ndio maana akaungana na Waasi. Sababu hizo hapo juu zikifanyiwa kazi, mgogoro wa Congo unaweza kupungua kwa kiasi kikubwa. Mnaopenda kujifunza zaidi, naandika Kitabu. Get ready to have your copy. MWISHO.! (Malisa GJ ✍️)
    Like
    1
    0 Kommentare 0 Anteile 3KB Ansichten
  • Jumuiya ya kimataifa inafuatilia kwa karibu hali inayoendelea katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), huku mashirika ya haki za binadamu yakilaani uhalifu wa kivita unaofanywa na pande zote dhidi ya raia.

    Ripoti za Umoja wa Mataifa zinaonyesha kuwa maelfu ya watu wamelazimika kuyakimbia makazi yao kutokana na mapigano yanayoendelea, huku ukatili dhidi ya wanawake na watoto ukiongezeka kwa kiwango cha kutisha.

    Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) imetangaza kuwa inafuatilia kwa karibu mzozo huu na imeonya kuwa yeyote anayehusika na uhalifu wa kivita, dhidi ya binadamu, au mauaji ya halaiki hatosazwa na mkono wa sheria.

    Mgogoro wa DRC ni wa muda mrefu na wenye mizizi mirefu. Tangu miaka ya 1990, taifa hili limepitia machafuko ya mara kwa mara, yakichochewa na rasilimali za madini,ukosefu wa utawala thabiti, na uhusiano tata wa kisiasa kati ya mataifa jirani, hususan Rwanda na Uganda.

    M23, kundi la waasi linalotajwa kupokea msaada kutoka nje, limeendelea kushikilia maeneo muhimu, hususan Goma, na hata kutishia kuuteka mji wa Kinshasa.

    Katika mazingira haya, kama ungekuwa Rais wa DRC, Félix Tshisekedi, ungefanya nini?

    Kwa mtazamo wangu, suluhisho pekee ni mazungumzo na diplomasia.

    Historia imeonyesha kuwa vita dhidi ya makundi ya waasi kama M23 si rahisi kushinda kwa nguvu za kijeshi pekee.

    Licha ya msaada wa kijeshi kutoka kwa MONUSCO (Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini DRC) na majeshi ya kikanda kama vile EACRF (East African Community Regional Force), kundi hili limeendelea kuwa tishio kubwa kwa utawala wa Tshisekedi.

    Ikiwa Rais Tshisekedi ataendelea kulazimisha suluhisho la kijeshi bila mpango wa mazungumzo, hatari ipo kwamba mapigano yatapanuka zaidi, na hata kutishia utulivu wa taifa kwa ujumla.

    Hatua muhimu kwa sasa ni kuitisha mazungumzo ya dhati na kutafuta njia ya kidiplomasia ya kumaliza mgogoro huu kabla hali haijazidi kuwa mbaya.
    Jumuiya ya kimataifa inafuatilia kwa karibu hali inayoendelea katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), huku mashirika ya haki za binadamu yakilaani uhalifu wa kivita unaofanywa na pande zote dhidi ya raia. Ripoti za Umoja wa Mataifa zinaonyesha kuwa maelfu ya watu wamelazimika kuyakimbia makazi yao kutokana na mapigano yanayoendelea, huku ukatili dhidi ya wanawake na watoto ukiongezeka kwa kiwango cha kutisha. Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) imetangaza kuwa inafuatilia kwa karibu mzozo huu na imeonya kuwa yeyote anayehusika na uhalifu wa kivita, dhidi ya binadamu, au mauaji ya halaiki hatosazwa na mkono wa sheria. Mgogoro wa DRC ni wa muda mrefu na wenye mizizi mirefu. Tangu miaka ya 1990, taifa hili limepitia machafuko ya mara kwa mara, yakichochewa na rasilimali za madini,ukosefu wa utawala thabiti, na uhusiano tata wa kisiasa kati ya mataifa jirani, hususan Rwanda na Uganda. M23, kundi la waasi linalotajwa kupokea msaada kutoka nje, limeendelea kushikilia maeneo muhimu, hususan Goma, na hata kutishia kuuteka mji wa Kinshasa. Katika mazingira haya, kama ungekuwa Rais wa DRC, Félix Tshisekedi, ungefanya nini? Kwa mtazamo wangu, suluhisho pekee ni mazungumzo na diplomasia. Historia imeonyesha kuwa vita dhidi ya makundi ya waasi kama M23 si rahisi kushinda kwa nguvu za kijeshi pekee. Licha ya msaada wa kijeshi kutoka kwa MONUSCO (Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini DRC) na majeshi ya kikanda kama vile EACRF (East African Community Regional Force), kundi hili limeendelea kuwa tishio kubwa kwa utawala wa Tshisekedi. Ikiwa Rais Tshisekedi ataendelea kulazimisha suluhisho la kijeshi bila mpango wa mazungumzo, hatari ipo kwamba mapigano yatapanuka zaidi, na hata kutishia utulivu wa taifa kwa ujumla. Hatua muhimu kwa sasa ni kuitisha mazungumzo ya dhati na kutafuta njia ya kidiplomasia ya kumaliza mgogoro huu kabla hali haijazidi kuwa mbaya.
    0 Kommentare 0 Anteile 2KB Ansichten
  • Bunge la Nchi ya Uganda limependekeza Wabunge Wanajeshi kuvaa mavazi rasmi ya Bunge wakiwa Bungeni, badala ya kuvaa sare zao wakati wa mijadala.

    Kamati ya Bunge inayosimamia masuala ya utaratibu na nidhamu imesema si sahihi kwa Wabunge hao wanaowakilisha Wanajeshi kuingia na magwanda yao, kwa kuwa yanaonyesha ishara ya kuwa vitani.

    Ikumbukwe kwamba Nchi ya Uganda ndio Nchi pekee barani Afrika wenye Wabunge Wanajeshi. Wanajeshi hao huteuliwa Jeshini kisha kupigiwa kura na kupatikana Wabunge hao huku Watatu (3) kati yao lazima wawe Wanawake.

    Bunge la Nchi ya Uganda 🇺🇬 limependekeza Wabunge Wanajeshi kuvaa mavazi rasmi ya Bunge wakiwa Bungeni, badala ya kuvaa sare zao wakati wa mijadala. Kamati ya Bunge inayosimamia masuala ya utaratibu na nidhamu imesema si sahihi kwa Wabunge hao wanaowakilisha Wanajeshi kuingia na magwanda yao, kwa kuwa yanaonyesha ishara ya kuwa vitani. Ikumbukwe kwamba Nchi ya Uganda ndio Nchi pekee barani Afrika wenye Wabunge Wanajeshi. Wanajeshi hao huteuliwa Jeshini kisha kupigiwa kura na kupatikana Wabunge hao huku Watatu (3) kati yao lazima wawe Wanawake.
    Like
    1
    0 Kommentare 0 Anteile 729 Ansichten
  • RASMI : Young Africans vs Ken Gold ni Khalid Aucho na Maokoto Day....

    Mashabiki wa klab ya Young Africans wameuomba Uongozi wa klab yao Juu ya kumtaarifu kiungo wao Mkabaji Raia wa Uganda Khalid Aucho 'Doctor' kuwa ndiye watakaye mpa zawadi ya pesa 'Maokoto kwenye kibegi' siku ya Jumatano kwenye mchezo wao wa ligi kuu ya NBC dhidi ya Klab ya Ken Gold,

    Ameyasema hayo Mkuu wa kitengo cha habari Ali kamwe baada ya kupokea maombi hayo kutoka kwa mashabiki wa klab yao,

    Mashabiki wa klab ya Yanga wamekuwa na utaratibu huo na baadhi ya wachezaji ambao wamepata maokoto hayo ni:

    Bacca
    Kibwana
    Mzize
    Maxi
    Pacome

    Next game:

    🫶Young Africans vs Ken Gold
    05-02-2025
    16:00 Hrs
    Kmc Complex
    RASMI : Young Africans vs Ken Gold ni Khalid Aucho na Maokoto Day.... Mashabiki wa klab ya Young Africans wameuomba Uongozi wa klab yao Juu ya kumtaarifu kiungo wao Mkabaji Raia wa Uganda Khalid Aucho 'Doctor' kuwa ndiye watakaye mpa zawadi ya pesa 'Maokoto kwenye kibegi' siku ya Jumatano kwenye mchezo wao wa ligi kuu ya NBC dhidi ya Klab ya Ken Gold, Ameyasema hayo Mkuu wa kitengo cha habari Ali kamwe baada ya kupokea maombi hayo kutoka kwa mashabiki wa klab yao, Mashabiki wa klab ya Yanga wamekuwa na utaratibu huo na baadhi ya wachezaji ambao wamepata maokoto hayo ni: 👉Bacca 👉Kibwana 👉Mzize 👉Maxi 👉Pacome Next game: 🫶Young Africans vs Ken Gold 📌05-02-2025 🕑16:00 Hrs ⛳Kmc Complex
    Like
    2
    0 Kommentare 0 Anteile 1KB Ansichten
  • #PART10

    March 23, 2009 Mkataba wa amani uitwao "March 23 Agreement" ukasainiwa huko Goma, kati ya serikali ya Congo na Waasi wa CNDP, wasuluhishi wakiwa mzee Mkapa na mzee Obasanjo. Mapigano yakasitishwa

    Ntaganda na askari wa CNDP wakaingizwa kwenye jeshi la Congo (FARDC). Kukawepo na miaka mitatu ya amani, vita ikakoma kabisa. Lakini ghafla, April 04, mwaka 2012 Bosco Ntaganda alitangaza kujitoa kwenye jeshi la Congo (FARDC) pamoja na baadhi ya askari waliokuwa wanamgambo wa CNDP. Ntaganda alidai Serikali ya Congo imeshindwa kutekeleza mkataba wa amani wa Machi 23, 2009.

    Alisema Makataba huo uliweka masharti ya kutowabughudhi askari 600 wa CNDP waliokataa kujiunga na jeshi la Congo. Lakini serikali ya Congo iliwashughulikia. Baadhi walikamatwa na wengine kuuawa. Pia alidai serikali ya Congo imeshindwa kuwalinda Watutsi (Banyamulenge) waishio mashariki mwa nchi hiyo.

    Ntaganda akatangaza kuanzisha kikundi kipya cha waasi kiitwacho M23. Alidai kutumia jina hilo ili kuikumbusha serikali ya Congo kuheshimu mkataba wa amani wa Machi 23, 2009. Kundi la M23 likapata wafuasi wengi hasa askari wa zamani wa CNDP na Banyamulenge wa Kivu. Mapigano yakaanza upya.

    Rwanda na Uganda zikashutumiwa kuunga mkono waasi hao, lakini zikakataa. Hata hivyo Rwanda ililaumiwa kwa kuruhusu M23 kuwa na kambi za kijeshi katika miji ya Gisenyi na Rusizi. Pia Rwanda ilihusishwa na mgogoro huo kwa sababu Ntaganda hakuwa Mkongomani, bali Mnyarwanda aliyezaliwa na kukulia Rwanda. Ametumikia jeshi la Rwanda kwa miaka mingi, kabla ya kuhamia Congo kupigania haki za Banyamulenge.

    Baada ya mwaka mmoja wa mapigano makali, vikosi vya M23 vikazidiwa nguvu na jeshi la serikali. Machi 18, 2013, Bosco Ntaganda akakimbilia Rwanda na akaenda mwenyewe kujisalimisha kwenye ubalozi wa Marekani mjini Kigali. Akasafirishwa kwenda The Heague kwenye mahakama ya kimataifa ya makosa ya jinai (ICC).

    Mwaka 2015 kesi yake ikaanza kusikilizwa, na mwaka 2019 akapatikana na hatia katika makosa 18, yakiwemo ubakaji, mauaji ya raia wasio na hatia, na kutumikisha watoto jeshini. Akahukumiwa kifungo cha miaka 30 jela, adhabu ambayo anaitumikia hadi sasa.
    (Malisa GJ)

    #PART10 March 23, 2009 Mkataba wa amani uitwao "March 23 Agreement" ukasainiwa huko Goma, kati ya serikali ya Congo na Waasi wa CNDP, wasuluhishi wakiwa mzee Mkapa na mzee Obasanjo. Mapigano yakasitishwa Ntaganda na askari wa CNDP wakaingizwa kwenye jeshi la Congo (FARDC). Kukawepo na miaka mitatu ya amani, vita ikakoma kabisa. Lakini ghafla, April 04, mwaka 2012 Bosco Ntaganda alitangaza kujitoa kwenye jeshi la Congo (FARDC) pamoja na baadhi ya askari waliokuwa wanamgambo wa CNDP. Ntaganda alidai Serikali ya Congo imeshindwa kutekeleza mkataba wa amani wa Machi 23, 2009. Alisema Makataba huo uliweka masharti ya kutowabughudhi askari 600 wa CNDP waliokataa kujiunga na jeshi la Congo. Lakini serikali ya Congo iliwashughulikia. Baadhi walikamatwa na wengine kuuawa. Pia alidai serikali ya Congo imeshindwa kuwalinda Watutsi (Banyamulenge) waishio mashariki mwa nchi hiyo. Ntaganda akatangaza kuanzisha kikundi kipya cha waasi kiitwacho M23. Alidai kutumia jina hilo ili kuikumbusha serikali ya Congo kuheshimu mkataba wa amani wa Machi 23, 2009. Kundi la M23 likapata wafuasi wengi hasa askari wa zamani wa CNDP na Banyamulenge wa Kivu. Mapigano yakaanza upya. Rwanda na Uganda zikashutumiwa kuunga mkono waasi hao, lakini zikakataa. Hata hivyo Rwanda ililaumiwa kwa kuruhusu M23 kuwa na kambi za kijeshi katika miji ya Gisenyi na Rusizi. Pia Rwanda ilihusishwa na mgogoro huo kwa sababu Ntaganda hakuwa Mkongomani, bali Mnyarwanda aliyezaliwa na kukulia Rwanda. Ametumikia jeshi la Rwanda kwa miaka mingi, kabla ya kuhamia Congo kupigania haki za Banyamulenge. Baada ya mwaka mmoja wa mapigano makali, vikosi vya M23 vikazidiwa nguvu na jeshi la serikali. Machi 18, 2013, Bosco Ntaganda akakimbilia Rwanda na akaenda mwenyewe kujisalimisha kwenye ubalozi wa Marekani mjini Kigali. Akasafirishwa kwenda The Heague kwenye mahakama ya kimataifa ya makosa ya jinai (ICC). Mwaka 2015 kesi yake ikaanza kusikilizwa, na mwaka 2019 akapatikana na hatia katika makosa 18, yakiwemo ubakaji, mauaji ya raia wasio na hatia, na kutumikisha watoto jeshini. Akahukumiwa kifungo cha miaka 30 jela, adhabu ambayo anaitumikia hadi sasa. (Malisa GJ)
    Like
    1
    0 Kommentare 0 Anteile 2KB Ansichten
  • #PART9

    Baada ya miaka mitatu ya utulivu, ghafla 2006 Jenerali Laurent Nkunda, aliasi jeshi kwa madai serikali imeshindwa kutekeleza Mkataba wa Amani wa SunCity. Ikumbukwe kabla ya kujiunga na Jeshi, alikua mpiganaji wa RCD - Goma, kundi lililoungwa mkono na Rwanda. Baada ya mkataba wa Suncity waasi wote waliingizwa jeshini akiwemo Nkunda.

    Lakini Juni 29, 2006, Nkunda akaasi jeshi na kuunda kundi la Congrès National pour la Défense du Peuple (CNDP). Madai yake:
    - Askari wa vikundi vya waasi walioingizwa jeshini hawakupewa vyeo.
    - Serikali ya Congo kushindwa kuwatanbua Watutsi (Banyamulenge) waishio mashariki mwa nchi hiyo kama raia wa Congo.
    - Serikali ya Congo kushindwa kuwakamata wanamgambo wa kihutu wa FDLR (Intarahanwe) waliojificha Congo baada ya kufanya mauaji ya kimbari Rwanda 1994.

    Nkunda akasema lengo la kuanzisha kundi la waasi la CNDP ni kupigania haki za Watutsi waishio mashariki mwa Congo (Banyamulenge) na kukabiliana na wanamgambo wa Kihutu wa FDLR. Nkunda akaungwa mkono na Rwanda na Uganda, akapewa silaha, vita ikaanza upyaaaaa (tamka kwa sauti ya mbunge Bwege).

    CNDP ikaua raia wengi wenye asili ya Kihutu ikiwatumu kuwa wafuasi wa FDLR. Serikali ya Burundi ikiongozwa na Piere Nkurunzinza (Mhutu) ikaingiza jeshi Congo kupambana na CNDP ili kulinda raia wake waliokua Congo. Kwa miaka mitatu kukawa na mapigano makali sana mashariki mwa Congo.

    January 2009 Waasi wa CNDP wakazidiwa. Laurent Nkunda akakimbilia Rwanda. Alipofika akakamatwa na kuwekwa kizuizini. Mpaka leo, bado anashikiliwa bila kufikishwa mahakamani. Jenerali Bosco Ntaganda, Mtutsi (Banyamulenge) wa Kivu akateuliwa kuongoza CNDP. Akafanya vitendo vingi vya kikatili kwa raia kuliko mtangulizi wake, kama ubakaji, mauaji ya halaiki, na kutumikisha watoto jeshini.

    Machi 23, 2009 serikali ya Congo na CNDP wakasaini Mkataba wa Amani, ulioitwa "March 23 Agreement" wenye masharti yafuatayo:
    - Kusitisha mapigano kwa pande zote.
    - Kuingiza askari wa CNDP kwenye jeshi la Congo.
    - Kutowashtaki askari wa CNDP kwa makosa waliyofanya wakati wa vita.
    - Wananchi wa Kivu wanufaike na rasilimali zao
    - Kulinda haki za binadamu Kivu
    (Malisa GJ)

    #PART9 Baada ya miaka mitatu ya utulivu, ghafla 2006 Jenerali Laurent Nkunda, aliasi jeshi kwa madai serikali imeshindwa kutekeleza Mkataba wa Amani wa SunCity. Ikumbukwe kabla ya kujiunga na Jeshi, alikua mpiganaji wa RCD - Goma, kundi lililoungwa mkono na Rwanda. Baada ya mkataba wa Suncity waasi wote waliingizwa jeshini akiwemo Nkunda. Lakini Juni 29, 2006, Nkunda akaasi jeshi na kuunda kundi la Congrès National pour la Défense du Peuple (CNDP). Madai yake: - Askari wa vikundi vya waasi walioingizwa jeshini hawakupewa vyeo. - Serikali ya Congo kushindwa kuwatanbua Watutsi (Banyamulenge) waishio mashariki mwa nchi hiyo kama raia wa Congo. - Serikali ya Congo kushindwa kuwakamata wanamgambo wa kihutu wa FDLR (Intarahanwe) waliojificha Congo baada ya kufanya mauaji ya kimbari Rwanda 1994. Nkunda akasema lengo la kuanzisha kundi la waasi la CNDP ni kupigania haki za Watutsi waishio mashariki mwa Congo (Banyamulenge) na kukabiliana na wanamgambo wa Kihutu wa FDLR. Nkunda akaungwa mkono na Rwanda na Uganda, akapewa silaha, vita ikaanza upyaaaaa (tamka kwa sauti ya mbunge Bwege). CNDP ikaua raia wengi wenye asili ya Kihutu ikiwatumu kuwa wafuasi wa FDLR. Serikali ya Burundi ikiongozwa na Piere Nkurunzinza (Mhutu) ikaingiza jeshi Congo kupambana na CNDP ili kulinda raia wake waliokua Congo. Kwa miaka mitatu kukawa na mapigano makali sana mashariki mwa Congo. January 2009 Waasi wa CNDP wakazidiwa. Laurent Nkunda akakimbilia Rwanda. Alipofika akakamatwa na kuwekwa kizuizini. Mpaka leo, bado anashikiliwa bila kufikishwa mahakamani. Jenerali Bosco Ntaganda, Mtutsi (Banyamulenge) wa Kivu akateuliwa kuongoza CNDP. Akafanya vitendo vingi vya kikatili kwa raia kuliko mtangulizi wake, kama ubakaji, mauaji ya halaiki, na kutumikisha watoto jeshini. Machi 23, 2009 serikali ya Congo na CNDP wakasaini Mkataba wa Amani, ulioitwa "March 23 Agreement" wenye masharti yafuatayo: - Kusitisha mapigano kwa pande zote. - Kuingiza askari wa CNDP kwenye jeshi la Congo. - Kutowashtaki askari wa CNDP kwa makosa waliyofanya wakati wa vita. - Wananchi wa Kivu wanufaike na rasilimali zao - Kulinda haki za binadamu Kivu (Malisa GJ)
    0 Kommentare 0 Anteile 1KB Ansichten
  • #PART7

    Baada ya kundi la RCD kuvunjika, yalizaliwa makundi mawili ambayo ni RCD Goma (liliungwa mkono na Rwanda) na RCD Kisangani (likiungwa mkono na Uganda). Aliyekua Kiongozi wa RCD Ernest Wamba Dia Wamba akaamua kukaa pembeni baada ya kugundua wanatumika kupigana kwa maslahi ya watu wengine.

    Kwahiyo makundi haya yakapata viongozi wapya. RCD-Goma ikaongozwa na Kanali Emile Ilunga na RCD-Kisangani, ikaongozwa na Jenerali Mbusa Nyamwisi. Ikumbukwe kabla kundi la RCD halijavunjika, lilikuwa limeshikilia maeneo mengi ya migodi huko Goma, Bukavu, na Katanga. Sasa baada ya kuvunjika, ukatokea mgogoro wa kugawana maeneo. Mgodi upi uende RCD Goma na upi uende RCD Kisangani.

    Kwa hiyo wakaanza kupigana tena wao kwa wao. Ikapigwa vita moja kali sana pale Kisangani, ikabatizwa jina la ‘Six Day War’ maana ilipiganwa kwa siku sita. RCD-Goma, ikawatandika vibaya sana RCD-Kisangani. Tar.10 June 2000 RCD Kisangani ikaachia migodi yote na kukimbia. RCD-Goma wakataka RCD-Kisangani wabadili jina lao maana mji wa Kisangani haukuwa chini yao tena. Hatimaye, RCD-Kisangani wakabadili na kujiita RCD-ML, yaani Rally for Congolese Democracy - Liberation Movement.

    RCD - ML walikimbilia kwenye milima Mikeno karibu na hifadhi ya Virunga kujipanga upya. RCD-Goma wakaendeleza mapigano kuelekea Kinshasa. Lakini kufika Bukavu wakakumbana na upinzani kutoka wanamgambo wa Maï-Maï waliokua wamepewa silaha na serikali za majimbo kupigana na askari yoyote mgeni kwenye ardhi yao.

    Maï-Maï waliongozwa na Kanali Musa Sindi upande wa Kivu Kusini na Sheikh Ntabo Ntaberi kwa Kivu Kaskazini. Kwa hiyo safari ya RCD Goma kwenda Kinshasa kumng’oa Laurent Kabila ikakutana na kizuizi cha Maï-Maï. Wakachapana sana. Watu zaidi ya 1,000 wakapoteza maisha.

    Kwahiyo vita ya kumng'oa Laurent Kabila ikawa ngumu maana vikundi vingi vya waasi vilianza kupigana vyenyewe kwa vyenyewe. Hali hiyo ilifanya vita kuwa ngumu zaidi, maana watu walipigana bila mpangilio. Risasi zikafyatuliwa hovyo hovyo na wananchi wengi wakapoteza maisha.
    (Malisa GJ)

    #PART7 Baada ya kundi la RCD kuvunjika, yalizaliwa makundi mawili ambayo ni RCD Goma (liliungwa mkono na Rwanda) na RCD Kisangani (likiungwa mkono na Uganda). Aliyekua Kiongozi wa RCD Ernest Wamba Dia Wamba akaamua kukaa pembeni baada ya kugundua wanatumika kupigana kwa maslahi ya watu wengine. Kwahiyo makundi haya yakapata viongozi wapya. RCD-Goma ikaongozwa na Kanali Emile Ilunga na RCD-Kisangani, ikaongozwa na Jenerali Mbusa Nyamwisi. Ikumbukwe kabla kundi la RCD halijavunjika, lilikuwa limeshikilia maeneo mengi ya migodi huko Goma, Bukavu, na Katanga. Sasa baada ya kuvunjika, ukatokea mgogoro wa kugawana maeneo. Mgodi upi uende RCD Goma na upi uende RCD Kisangani. Kwa hiyo wakaanza kupigana tena wao kwa wao. Ikapigwa vita moja kali sana pale Kisangani, ikabatizwa jina la ‘Six Day War’ maana ilipiganwa kwa siku sita. RCD-Goma, ikawatandika vibaya sana RCD-Kisangani. Tar.10 June 2000 RCD Kisangani ikaachia migodi yote na kukimbia. RCD-Goma wakataka RCD-Kisangani wabadili jina lao maana mji wa Kisangani haukuwa chini yao tena. Hatimaye, RCD-Kisangani wakabadili na kujiita RCD-ML, yaani Rally for Congolese Democracy - Liberation Movement. RCD - ML walikimbilia kwenye milima Mikeno karibu na hifadhi ya Virunga kujipanga upya. RCD-Goma wakaendeleza mapigano kuelekea Kinshasa. Lakini kufika Bukavu wakakumbana na upinzani kutoka wanamgambo wa Maï-Maï waliokua wamepewa silaha na serikali za majimbo kupigana na askari yoyote mgeni kwenye ardhi yao. Maï-Maï waliongozwa na Kanali Musa Sindi upande wa Kivu Kusini na Sheikh Ntabo Ntaberi kwa Kivu Kaskazini. Kwa hiyo safari ya RCD Goma kwenda Kinshasa kumng’oa Laurent Kabila ikakutana na kizuizi cha Maï-Maï. Wakachapana sana. Watu zaidi ya 1,000 wakapoteza maisha. Kwahiyo vita ya kumng'oa Laurent Kabila ikawa ngumu maana vikundi vingi vya waasi vilianza kupigana vyenyewe kwa vyenyewe. Hali hiyo ilifanya vita kuwa ngumu zaidi, maana watu walipigana bila mpangilio. Risasi zikafyatuliwa hovyo hovyo na wananchi wengi wakapoteza maisha. (Malisa GJ)
    Like
    1
    0 Kommentare 0 Anteile 2KB Ansichten
Suchergebnis