• MACHACHE KUHUSU MFALME MKWASI ZAIDI DUNIANI

    KUNA HISTORIA ambazo ukitaka kuandika unaweza kuchukua siku mbili za kutafakari uanze wapi na au uishie wapi.....Mfalme Sulemani ni mmoja wapo.............

    Mama wa Sulemani (BATH-SHEBA) alikuwa tayari ni mke wa mtu (URIA MHITI) huyu URIA alikuwa askari wa mfalme DAUDI. so mfalme DAUDI aliponogewa na penzi la BATH SHEBA akafanya mbinu za kifo cha URIA vitani.

    ......umewahi kuwaza kwamba unahangaika na familia moja tu dhidi ya mtu anayetajwa kuwa na wenza 700 na masuria 300...hujahesabu watoto, wajakazi, shangazi, mjomba, wajukuu, nk wanaovinjari kila siku katika hemaya zake........tunaambiwa kwamba chakula kilicholiwa kwa siku moja kilikuwa magunia 240 ya unga, magunia 480 ya chakula, ng'ombe kumi kwa nyama choma, ng'ombe ishirini wa mchuzi, kondoo mia moja, ndege na wanyama wengine wa aina mbalimbali ..........

    unahangaika kutafuta mufu wa dhahabu ilihali mwenzako anapokea tani 30 za dhahabu kila mwaka .........Kwa mwaka mmoja pekee alikuwa anapokea tani si chini ya 30 ya vipande bora vya dhahabu ukiachilia mbali Vito na Madini mengine....kila nakshi na chombo ndani ya nyumba ya Sulemani ilikua ni DHAHABU tupu maana nyakati hizo madini ya fedha yalithaminishwa kwa kiwango cha vumbi dhidi ya dhahabu.... Jumba la Hukumu la Sulemani lilikuwa kubwa na lilijengwa na mwerezi na kuzungushwa na pembe zilizofunikwa na dhahabu na kusimamiwa na simba ........... Katika ukuta kulikuwa kumewekwa ngao 500 za dhahabu .................hata vyombo vya kunywea na sahani zilizokuwa kwenye nyumba hii kuu zilikuwa za “dhahabu”. Shaba “ haikuwa kitu cha kuhesabiwa katika siku za Sulemani”.................Pia alianzisha shamba la kifalme na mbuga yenye maziwa bandia, shamba la maua na matunda

    Wana-ikiolojia wamepata ushahidi dhabiti wa majengo ya Sulemani kote nchini hasa Hazori, Megido na Gezeri, mabaki ambayo yanatoa ushahidi wa ukweli wa 1 Wafalme 9:15. Megido ni muhimu kwa vibanda vyake vya magari ya farasi 450. Jeshi kubwa la Sulemani lilihitaji jengo lenye vibanda 4,000 vya farasi na vilijengwa karibu na mipaka ya Israeli na kulindwa na waendeshaji magari ya farasi..

    Sulemani alipata faida kwani Israeli ilikuwa sehemu nzuri katikati mwa bara la Asia na Afrika. Alitawala njia za kaskazini na kusini na kwa usaidizi wa Wafoeniki, alijenga meli nyingi pale Esion-geberi ili zitumike kubeba shaba iliosafishwa na bidhaa zingine. Meli hizi zilifanya safari ya kusini hadi Ethiopia, Yemen na India Arabian mara moja kila miaka mitatu, na kuleta dhahabu, fedha, na pembe, nyani na tausi

    Sulemani pia aliendeleza viwanda vya kusafisha chuma, pamoja na kuchimba madini katika Araba, kusini mwa Bahari ya Chumvi, na kiwanda kikubwa cha kuyeyusha vyuma cha Esion-geberi, mahali ambapo palikuwa bandari karibu na Bahari ya Shamu.

    Kwa Mujibu wa wanahistoria.. Mansa Musa mfalme wa Mali empire... Ndio Binadamu alie wahi kuwa tajir Dunia nzima mpaka leo hamna mtu alie wahi fikia Utajir wake.. (wakati anaenda hiji macca alipitia misri .. Na kusabisha uchumi wao kuyumba kutokana na dhahabu alizo tumia Pale misri)... UKWELI NI KWAMBA MANSA MUSA aliyetawala kati ya mwaka 1312-1337 na utajiri wake ulikadiriwa kufikia USD billion 400 ILIHALI Mfalme Sulemani alikuwa na utajiri unaokadiriwa kufikia dollar za kimarekani trillion 2.1.......Mansa Kankan Mussa ni tajiri wa kwanza katika kipindi cha baada ya Yesu. Wenyewe wanaita Anno Domino (AD)

    Hata Nathaniel Rothchild Family ( zikiwepo rockerfeller, morgan na du pont family yaani FAMILI NZIMA) Utajiri wao haufikii hata theluthi ya Mfalme Sulemani (dola bilioni 600 tu)

    Wingi wa wake za Sulemani unahalasiha kutapanyika kwa kiazazi chake karibu kote duniani, yasemekana hata hawa wahabeshi wa Somalia, Watusi wa Rwanda na wa Iraq wa Tanzania ni mbegu yake huyo jamaa baada ya kumgaragaza malkia wa Ethiopia ( QUEEN OF SHEBA) alivyompelekea kiasi kikubwa cha dhahabu kutoka Afrika kwa ajili ya kupamba hekalu alilokamilisha.

    Usiulizd iwapo alikua anatozwa kodi kwani yeye ndie alikuwa mtawala wa himaya yake kwahiyo asingeweza kutozwa kodi...na utawala wake ulidumu kwa miaka 40

    Uchaguzi wa Busara wa Sulemani kwa kumwomba Bwana “Moyo adili wa kuwahukumu watu wako” ulisababisha idhini ya Bwana na utoaji wa "moyo wa hekima na ufahamu" na kuongezewa "utajiri na heshima "

    Mhhhhhh...............yumkini kama nilivyosema si rahisi sana kumsimulia Sulemani na kuna vyanzo vingi ambavyo kila mtu anaweza kuibuka na chake walau nimeokoteza kwa vyanzo vya uhakika na kwa kuwa ni simulizi tutaendelea kuimani tu maana HATUKUWEPO................

    Mada hii itaendelea kuboreshwa kwa kadri ya vyanzo vingine....
    ..
    MACHACHE KUHUSU MFALME MKWASI ZAIDI DUNIANI KUNA HISTORIA ambazo ukitaka kuandika unaweza kuchukua siku mbili za kutafakari uanze wapi na au uishie wapi.....Mfalme Sulemani ni mmoja wapo............. Mama wa Sulemani (BATH-SHEBA) alikuwa tayari ni mke wa mtu (URIA MHITI) huyu URIA alikuwa askari wa mfalme DAUDI. so mfalme DAUDI aliponogewa na penzi la BATH SHEBA akafanya mbinu za kifo cha URIA vitani. ......umewahi kuwaza kwamba unahangaika na familia moja tu dhidi ya mtu anayetajwa kuwa na wenza 700 na masuria 300...hujahesabu watoto, wajakazi, shangazi, mjomba, wajukuu, nk wanaovinjari kila siku katika hemaya zake........tunaambiwa kwamba chakula kilicholiwa kwa siku moja kilikuwa magunia 240 ya unga, magunia 480 ya chakula, ng'ombe kumi kwa nyama choma, ng'ombe ishirini wa mchuzi, kondoo mia moja, ndege na wanyama wengine wa aina mbalimbali .......... unahangaika kutafuta mufu wa dhahabu ilihali mwenzako anapokea tani 30 za dhahabu kila mwaka .........Kwa mwaka mmoja pekee alikuwa anapokea tani si chini ya 30 ya vipande bora vya dhahabu ukiachilia mbali Vito na Madini mengine....kila nakshi na chombo ndani ya nyumba ya Sulemani ilikua ni DHAHABU tupu maana nyakati hizo madini ya fedha yalithaminishwa kwa kiwango cha vumbi dhidi ya dhahabu.... Jumba la Hukumu la Sulemani lilikuwa kubwa na lilijengwa na mwerezi na kuzungushwa na pembe zilizofunikwa na dhahabu na kusimamiwa na simba ........... Katika ukuta kulikuwa kumewekwa ngao 500 za dhahabu .................hata vyombo vya kunywea na sahani zilizokuwa kwenye nyumba hii kuu zilikuwa za “dhahabu”. Shaba “ haikuwa kitu cha kuhesabiwa katika siku za Sulemani”.................Pia alianzisha shamba la kifalme na mbuga yenye maziwa bandia, shamba la maua na matunda Wana-ikiolojia wamepata ushahidi dhabiti wa majengo ya Sulemani kote nchini hasa Hazori, Megido na Gezeri, mabaki ambayo yanatoa ushahidi wa ukweli wa 1 Wafalme 9:15. Megido ni muhimu kwa vibanda vyake vya magari ya farasi 450. Jeshi kubwa la Sulemani lilihitaji jengo lenye vibanda 4,000 vya farasi na vilijengwa karibu na mipaka ya Israeli na kulindwa na waendeshaji magari ya farasi.. Sulemani alipata faida kwani Israeli ilikuwa sehemu nzuri katikati mwa bara la Asia na Afrika. Alitawala njia za kaskazini na kusini na kwa usaidizi wa Wafoeniki, alijenga meli nyingi pale Esion-geberi ili zitumike kubeba shaba iliosafishwa na bidhaa zingine. Meli hizi zilifanya safari ya kusini hadi Ethiopia, Yemen na India Arabian mara moja kila miaka mitatu, na kuleta dhahabu, fedha, na pembe, nyani na tausi Sulemani pia aliendeleza viwanda vya kusafisha chuma, pamoja na kuchimba madini katika Araba, kusini mwa Bahari ya Chumvi, na kiwanda kikubwa cha kuyeyusha vyuma cha Esion-geberi, mahali ambapo palikuwa bandari karibu na Bahari ya Shamu. Kwa Mujibu wa wanahistoria.. Mansa Musa mfalme wa Mali empire... Ndio Binadamu alie wahi kuwa tajir Dunia nzima mpaka leo hamna mtu alie wahi fikia Utajir wake.. (wakati anaenda hiji macca alipitia misri .. Na kusabisha uchumi wao kuyumba kutokana na dhahabu alizo tumia Pale misri)... UKWELI NI KWAMBA MANSA MUSA aliyetawala kati ya mwaka 1312-1337 na utajiri wake ulikadiriwa kufikia USD billion 400 ILIHALI Mfalme Sulemani alikuwa na utajiri unaokadiriwa kufikia dollar za kimarekani trillion 2.1.......Mansa Kankan Mussa ni tajiri wa kwanza katika kipindi cha baada ya Yesu. Wenyewe wanaita Anno Domino (AD) Hata Nathaniel Rothchild Family ( zikiwepo rockerfeller, morgan na du pont family yaani FAMILI NZIMA) Utajiri wao haufikii hata theluthi ya Mfalme Sulemani (dola bilioni 600 tu) Wingi wa wake za Sulemani unahalasiha kutapanyika kwa kiazazi chake karibu kote duniani, yasemekana hata hawa wahabeshi wa Somalia, Watusi wa Rwanda na wa Iraq wa Tanzania ni mbegu yake huyo jamaa baada ya kumgaragaza malkia wa Ethiopia ( QUEEN OF SHEBA) alivyompelekea kiasi kikubwa cha dhahabu kutoka Afrika kwa ajili ya kupamba hekalu alilokamilisha. Usiulizd iwapo alikua anatozwa kodi kwani yeye ndie alikuwa mtawala wa himaya yake kwahiyo asingeweza kutozwa kodi...na utawala wake ulidumu kwa miaka 40 Uchaguzi wa Busara wa Sulemani kwa kumwomba Bwana “Moyo adili wa kuwahukumu watu wako” ulisababisha idhini ya Bwana na utoaji wa "moyo wa hekima na ufahamu" na kuongezewa "utajiri na heshima " Mhhhhhh...............yumkini kama nilivyosema si rahisi sana kumsimulia Sulemani na kuna vyanzo vingi ambavyo kila mtu anaweza kuibuka na chake walau nimeokoteza kwa vyanzo vya uhakika na kwa kuwa ni simulizi tutaendelea kuimani tu maana HATUKUWEPO................ Mada hii itaendelea kuboreshwa kwa kadri ya vyanzo vingine.... ..
    Love
    Like
    3
    · 0 Σχόλια ·0 Μοιράστηκε ·459 Views
  • #HABARI Moto wa Los Angeles Kabla ya Kutokea

    Siku tatu kabla ya moto mkubwa kutokea Los Angeles, waandaaji wa tuzo maarufu za Global Leaders Awards walikuwa wakijitayarisha kwa hafla yao ya kila mwaka. Tuzo hizi zina lengo la kutambua na kusherehekea mchango wa watu mashuhuri katika nyanja mbalimbali, ikiwemo utunzi na uandaaji wa filamu bora.

    Kwa mara ya kwanza katika historia ya tuzo hizo, waandaaji walimuweka Mungu kama mmoja wa washindani katika kipengele cha "Mchango wa kipekee wa Maisha katika Sanaa". Hili lilizua mjadala mkubwa na hisia tofauti miongoni mwa waliohudhuria hafla hiyo.

    MC wa usiku huo alipochukua kipaza sauti, alitoa kauli iliyozua mjadala:
    "Ni jambo la kushangaza kwamba tumemuweka Mungu katika orodha ya washindani kwa tuzo hii, lakini amekosa kura kabisa. Inaonekana hata Mungu anahitaji kujipanga zaidi kwa ajili ya hafla zijazo."

    Kauli hiyo ilisababisha kicheko kutoka kwa baadhi ya wageni waalikwa, huku wengine wakiwa hawakufurahishwa na utani huo.

    Katika kipengele hicho, wagombea walikuwa:

    1. Cast and Crow - waliopata kura 11

    2. Moms - waliopata kura 3

    3. Mungu - aliyepata kura 0

    Hafla hiyo ya usiku ilimalizika kwa hali ya mchanganyiko wa furaha na maoni ya kukosoa, huku watu wakitafakari zaidi nafasi ya maadili na heshima katika sanaa na burudani.
    N.B, MUNGU HADHIHAKIWI

    #neliudcosiah
    #HABARI Moto wa Los Angeles Kabla ya Kutokea Siku tatu kabla ya moto mkubwa kutokea Los Angeles, waandaaji wa tuzo maarufu za Global Leaders Awards walikuwa wakijitayarisha kwa hafla yao ya kila mwaka. Tuzo hizi zina lengo la kutambua na kusherehekea mchango wa watu mashuhuri katika nyanja mbalimbali, ikiwemo utunzi na uandaaji wa filamu bora. Kwa mara ya kwanza katika historia ya tuzo hizo, waandaaji walimuweka Mungu kama mmoja wa washindani katika kipengele cha "Mchango wa kipekee wa Maisha katika Sanaa". Hili lilizua mjadala mkubwa na hisia tofauti miongoni mwa waliohudhuria hafla hiyo. MC wa usiku huo alipochukua kipaza sauti, alitoa kauli iliyozua mjadala: "Ni jambo la kushangaza kwamba tumemuweka Mungu katika orodha ya washindani kwa tuzo hii, lakini amekosa kura kabisa. Inaonekana hata Mungu anahitaji kujipanga zaidi kwa ajili ya hafla zijazo." Kauli hiyo ilisababisha kicheko kutoka kwa baadhi ya wageni waalikwa, huku wengine wakiwa hawakufurahishwa na utani huo. Katika kipengele hicho, wagombea walikuwa: 1. Cast and Crow - waliopata kura 11 2. Moms - waliopata kura 3 3. Mungu - aliyepata kura 0 Hafla hiyo ya usiku ilimalizika kwa hali ya mchanganyiko wa furaha na maoni ya kukosoa, huku watu wakitafakari zaidi nafasi ya maadili na heshima katika sanaa na burudani. N.B, MUNGU HADHIHAKIWI ✍️ #neliudcosiah
    Like
    Love
    3
    · 1 Σχόλια ·1 Μοιράστηκε ·372 Views
  • DUNIA NA MAAJABU YAKE
    (Muundo wa Dunia na Maajabu Yaliyomo)

    1. UMRI WA DUNIA

    HII Dunia yetu ina historia ndefu mno tangu ilipojiunda angani, miaka takribani bilioni 4.5 iliyopita.

    Tarakimu za umri huo wa miaka bilioni 4.5 ni 4,500,000,000, yaani miaka milioni elfu nne na mia tano iliyopita.

    Dunia ambayo kwa lugha ya Kiingereza inafahamika vyema kwa jina la 'Earth', pia hujulikana kama 'the World', ikimaanishwa ulimwengu.

    Aidha, Dunia ni sayari pekee kwenye himaya ya sayari zilizopo chini ya jua ambayo jina lake halitokani na majina ya "Miungu wa Dola" ya Kigiriki au ya Kirumi.

    Asili ya jina la 'earth' ni 'erde' lenye asili ya nchini Ujerumani, na maana yake ni udongo au ardhi.

    Mpaka kuweza kupata umri huo wa dunia wanasayansi walifanya kazi ya kutafiti na kisha kuwasilisha matokeo yao kwenye makongamano ya kisayansi duniani, ambapo matokeo hayo yalijadiliwa kwa kina na hatimaye kukubalika kama hivi.

    Kumbuka katika majadiliano hayo huwepo mivutano mikali miongoni mwa wanasayansi waalikwa, ambapo pia jopo la wanasayansi wanaowasilisha utafiti husika hujikuta wakitakiwa kujibu hoja mbalimbali za wanasayansi wenzao.

    Kuna wakati baadhi ya matokeo ya tafiti kadhaa hukataliwa, huku watafiti husika wakitakiwa kurejea upya tafiti zao.

    Wanasayansi hupata umri wa sayari kwa kupima umri wa miamba ya sayari husika, ambapo mwamba wenye umri mkubwa zaidi kuliko miamba yote ndiyo huchukuliwa kuwa umri wa sayari husika.

    Itakumbukwa kuwa Msahafu wa Biblia (Sura ya Mwanzo 1) husimulia jinsi Mwenyezi Mungu alivyoumba "mbingu na nchi na vyote vilivyomo kwa siku 6," lakini pia Msahafu huohuo kwenye aya zingine hueleza kuwa miaka elfu moja ya duniani yaweza kuwa sawa na siku moja kwenye ya Makazi ya Mwenyezi Mungu.

    Ni dhahiri kuwa binadamu tukiwa hatuna hoja sahihi kwa maelezo ya aina hiyo, ndipo tunaona ni vyema mambo ya Mwenyezi Mungu kumwachia Yeye Mwenyewe Mwenyezi Mungu.

    2. KUUMBIKA DUNIA, SAYARI, JUA, NYOTA

    Kimsingi, Dunia kama zilivyo sayari zingine zote ilijiunda kutokana na mabaki ya vitu vilivyotumika kuunda Jua.

    Jua ambalo ni nyota kama zilivyo nyota zote angani, lilijiunda lenyewe kwenye eneo la anga lijulikanalo kama 'Pillars of Creation' (nguzo za uumbaji) katika ukanda wa anga wenye upana ambao huonekana kutokuwa na mwisho.

    Ukanda huo ujulikanao kama 'Solar Nebula,' umegubikwa na mawingu ya vumbi la huko angani pamoja na aina mbalimbali za gesi na hewa, ikiwemo haidrojeni na heliumu.

    'Solar' ni jina la nishati itokanayo na joto la jua, na 'Nebula' kwa lugha ya Kilatini ni "wingu" au vumbi la gesi asilia mithili ya ukungu.

    Hivyo, 'Solar Nebula' ni ukanda katika anga ya mbali wenye mawingu yaliyosheheni nishati yenye joto, sawa na nishati ya joto la jua.

    Sasa basi, tunafahamu vyema kuwa jua hutoa mionzi hatari yenye joto kali mithili ya moto mkali, na ambayo ikiboreshwa kisayansi pia huweza kutoa nishati ya umeme.

    Hivyo, kwa muktadha huo, hebu ngoja sasa tuleta pamoja hewa za gesi, zikiwemo haidrojeni na heliumu, mawingu yenye nishati ya umeme wa jua, vumbi la angani na tufani itokanayo na mchafuko mbaya wa hali ya hewa huko anga za mbali.

    Na ili kuweza kupata matokeo yanayotakiwa, hebu pia tutambue uwepo wa nguvu kubwa ya asili katika kiwango kijulikanacho kwa jina la "Supernatural Power", ambayo ndiyo huwa kisababishi cha mambo yote.

    Kisayansi, "Supernatural Power" ni nguvu kubwa ya asili ambayo huendesha mifumo mbalimbali ya asili, ambapo duniani nguvu hiyo hujulikana kama Nguvu ya Mungu.

    Nguvu asili hiyo, yaani Supernatural Power, husababisha tufani ambayo huvurumisha kwa pamoja vitu vyote hivyo, (gesi, hewa, mawingu yenye nishati ya joto na vumbi la angani) ili kuunda tufani yenye umbo la duara.

    Duara hiyo ni kama ile itokanayo na kimbunga kikali duniani, na ambacho sasa tutaona kikifungamanisha pamoja vitu vyote hivyo katika mchafuko mkubwa wa hali mbaya ya hewa.

    Natumia maneno ya msisitizo kuelezea "ukubwa" wa mchafuko huo wa hali ya hewa katika eneo hilo la anga, kwani katika kuunda sayari au nyota nguvuasili kubwa hutumika.

    Aidha, tufani hiyo ya duara itakayoanza kidogo kidogo kama kimbunga kikali, itazidi kukua hadi kuwa na kipenyo cha takribani kilomita 10 hadi 200 au zaidi na kwendelea.

    Tufani hiyo ndiyo itavurumisha kwa pamoja gesi na hewa za naitrojeni na heliumu, mawingu ya nishati ya joto na vumbi la angani (kama kifanyavyo kimbunga kikali katika eneo tambarare la duniani).

    Pia, wakati mchafuko huo wa hali mbaya ya hewa ukiendelea, hebu ngoja sisi watazamaji tujibanze mahali fulani kwa mbali kushuhudia duara hiyo ya tufani ikijizungusha yenyewe bila kukoma kwa kipindi cha miaka mingi.

    Kitakachofuata ni kuanza kuona kiini cha moto kikianza kujiunda katikati ya duara hiyo ya tufani kali, huku pia nje ya duara hiyo vitu kibao vikivutwa kujiunga na mzunguko wa hiyo tufani ya duara.

    Vitu hivyo ni pamoja na vumbi zaidi la angani, na gesi zaidi zenye joto kali.

    Wakati huohuo kipenyo na mzingo wa duara hiyo vitazidi kuongezeka upana na ukubwa, mfano wa duara yenye umbo sawa na la mpira mkubwa wa miguu.

    Hivyo, baada ya miaka takribani milioni moja tutashangaa kuona lile vumbi likigeuka taratibu kuwa miamba ya moto ndani ya kiini cha tufani hiyo ya duara.

    Miamba hiyo ni kutokana na lile vumbi la angani ambalo hatimaye limeshikamana pamoja mithili ya zege, na hatimaye kuwa miamba ndani ya tufani ya duara.

    Sanjari na kuundika huko ndani ya kitovu cha hiyo tufani ya duara, pia kwelekea nje ya duara hiyo utaundika udongo ambao ardhi, mchanga na mawe.

    Kimsingi, vitu hivyo pia ni matokeo ya lile vumbi la angani ambalo lilikusanywa pamoja na kuvutwa na kasi ya mzunguko wa tufani.

    Hatua hiyo mpya inatokana na kuwepo mshikamano na mgandamizo wa zile chembechembe za lile vumbivumbi ndani ya tufani.

    Vurumai hiyo ya mzunguko wa hiyo tufani ya duara yenye vumbi, itazidi kukua hadi kuunda sumaku ya asili ndani ya kile kitovu cha duara ya tufani.

    Kutokana na duara hiyo ya tufani kuongezeka ukubwa, hatimaye sumaku iliyopo kwenye kitovu cha duara hiyo itaishiwa nguvu ya kwendelea kunasa vumbi zaidi kuja kwenye mzingo wa hiyo duara ya tufani.

    Kumbuka kuwa wakati huo hiyo duara pia itaunda kimo kutoka kwenye usawa wa ardhi yake kwenda ndani kwenye kitovu chake, na hivyo kuwa duara ya mviringo kama umbo mfano wa mpira mchezo wa miguu.

    Baada ya kupita maelfu ya miaka mingi, duara hiyo ambayo hapo awali ilianza kama umbo la tufani na kuzidi kukua huko angani, sasa itakuwa na joto kali kupita kiasi na kuanza kung'aa kama jua.

    Jua hilo, ndiyo nyota mojawapo ya zile ambazo huonekana usiku ziking'aa angani.

    Lakini pia wakati wa kujiunda nyota hiyo, kama tulivyoona hapo awali, baadhi ya mabaki yake yaliyokuwa yakitawanyika angani wakati ile tufani ya duara ikijizungusha, huweza kujikusanya pamoja na kuunda sayari ambazo huzunguka baadhi ya hizo nyota.

    Hivyo ndivyo zilivyojiunda sayari zote ambazo huelea kwa kulizunguka jua letu.

    Mathalani, sayari zote ambazo hulizunguka jua, ikiwemo dunia zilijiunda kutokana na mabaki ya vitu kama gesi, michanga na mawe ambavyo vilitawanyika angani wakati jua likijiunda (kama ambavyo imeelezwa hapo awali).

    3. KIINI CHA DUNIA

    Dunia yetu ambayo wastani wa nusu kipenyo cha umbo lake la duara ni kilomita 6,371, mzingo wake ni kilomita takribani 40,041.

    Kama zilivyo sayari zote katika himaya ya jua, dunia nayo ilijiunda wakati jua likijiunda lenyewe.

    Yaani kwamba sayari ni mabaki ya vitu vilivyotumika kuliunda jua.

    Kadhalika kama zilivyo sayari zingine zote, dunia nayo ina kiini chake ambacho kipo katikati ya ardhi yake.

    Kiini hicho kina nguvu kubwa ya sumaku ambayo, pamoja na mambo mengineyo, 'huvuta' umbo hilo la duara kutoka juu ya ardhi kwenda katikati ya kiini hicho.

    Muundo huo ndio hulifungamanisha pamoja umbo la duara la dunia, na hivyo kuzuia umbo hilo lisifumke kutoka ardhini na kusambaratika.

    Hiyo ni sawa na mpira wa miguu unavyoweza kupasuka na kusambaratika, kama utajazwa upepo kupita kiasi chake.

    Kiini hicho ambacho kipo katikati kabisa ya dunia, kinajulikanacho kwa jina la kisayansi la 'Inner Core.'

    Kiini hicho kina joto kali la sentigredi 6,230 ambacho ndio kiasi cha joto la jua.

    Kiini hicho kina umbo la duara lenye nusu kipenyo cha kilomita 1,250.

    Kama ingetokea kuchimba ardhi wima kwenda kwenye kiini hicho, mchimbaji angeanza kukutana na joto la kiini hicho kuanzia kimo cha umbali wa kilomita 5,150 kutoka usawa wa juu ya ardhi tunayotembea.

    Katika historia ya uchimbaji ardhi, kina kirefu kilichowahi kuchimbwa ardhini ni mita 12,345 (kilomita 12.345) huko Sakhalini, nchini Urusi, kwa ajili ya uvunaji wa mafuta ya petroli.

    Kiini cha dunia kinaundwa na madini mchanganyiko wa nikeli (nickle), chuma (iron) na dhahabu.

    Kwa mujibu wa utafiti, inakadiriwa kuwa kama dhahabu hiyo ingechimbwa na kuchomwa mpaka kuwa kimiminika sawa na uji na kisha kumwagwa chini, ingeweza kuifunika dunia yote kwa unene wa sentimeta 45.

    Kiini hicho muhimu kwa uhai wa sayari hii ya dunia kiligunduliwa mwaka 1936 na mtaalamu wa matetemeko ya ardhi wa nchini Denmark, mwanamama Dkt. Inge Lehmann.

    Dkt. Lehmann alihitimu shahada yake ya kwanza katika fani ya Hisabati mwaka 1910, ya Uzamili mwaka 1920 (zote kutoka Chuo Kikuu cha Copenhagen nchini mwake), na ile ya Uzamivu kutoka Chuo Kikuu cha Cambridge nchini Uingereza.

    Alifariki kwa uzee mwaka 1993 akiwa na umri wa miaka 104.

    4. MAJI DUNIANI

    Kupatikana maji kwenye dunia yetu, ni mojawapo ya miundo ambayo haipo katika sayari zingine ambazo tuna taarifa za kitafiti kuzuhusu.

    Maji ni muhimili muhimu kwa ajili ya uhai wa viumbe wote na mimea, ambavyo kwa pamoja havipo katika sayari zingine za himaya ya jua.

    Kwa mujibu wa tafiti nyingi ambazo zimefanyika kwa miongo mingi ya miaka kujaribu kubaini nini chanzo cha kuwepo maji duniani, hakuna hata utafiti mmoja ulioonesha kwa usahihi matokeo ya kuridhisha.

    Miongoni mwa tafiti hizo ni pamoja na ule wa mwaka 2005, ambapo Mkuu wa Idara ya Masomo ya Sayari na Mwezi katika Chuo Kikuu cha Arizona nchini Marekani, Profesa Michael Julian Drake, na mwenzake ambaye ni mtaalamu wa Vimondo, Dkt. Huberto Campins, wa Chuo Kikuu cha Central Florida, walitafiti nini chanzo cha kuwepo maji duniani.

    Katika mawasilisho yao kwenye kongamano la kisayansi la Chama cha Wanataaluma wa Maarifa ya Anga za Juu (IAU), watafiti hao walikanusha madai ya uwezekano wa dunia hapo kale kugongwa na kimondo kikubwa na kusababisha maji kulipuka kutoka ardhini.

    Wakiwasilisha matokeo ya utafiti wao kwenye mkutano wa kongamano hilo, magwiji hao wa masuala ya sayari walieleza kwenye waraka wao uitwao "Origin of water on the terrestial planets" (chanzo cha kuwepo maji kwenye sayari).

    Walidai kuwa maji yaliyopo duniani yaliumbika kwenye ardhi ya dunia tangu mwanzo, wakati ikijiunda angani.

    Ikumbukwe kuwa eneo la uso wa dunia likiwa ni jumla ya kilomita za mraba milioni 510, asilimia 70.8 ya eneo hilo imefunikwa na maji na asilimia 29.2 ni nchi kavu, ikiwemo milima, mabonde na ardhi tambarare.

    5. HEWA YA OKSIJENI

    Muundo mwingine muhimu katika sayari hii ya dunia ni hewa ambazo ni tawala, yaani Naitrojeni ambayo kwa usahihi imeenea kwa asilimia 78.08 ya hewa yote ya dunia, Oksijeni asilimia 20.95, 'Argon' asilimia 0.93, hewa ya Ukaa (Carbon dioxide) asilimia 0.039, na asilimia moja ni hewa mithili ya mvuke wa maji (water vapour).

    Hewa ya Oksijeni ambayo ni nguzo muhimu kwa ajili ya uhai wa viumbe wote na pia haipatikani kwenye sayari nyingine chini ya jua, inadhaniwa ilianza kupatikana duniani miaka takribani bilioni 2.5 iliyopita kufuatia "kukomaa kwa kiini cha dunia."

    Kwa mujibu wa matokeo ya tafiti mbalimbali na nadharia za kisayansi, inaoneshwa kuwa kukomaa kwa kiini hicho cha dunia hatimaye ndiko kulisababisha kuzuka duniani milipuko ya volikano ambayo pia ilisababisha kuzuka mabonde na milima.

    Inaoneshwa kuwa tayari wakati huo maji yaliishakuwepo duniani, na kuwezesha kuzuka chembechembe ndogo sana za kibakteria zijulikanazo kwa jina la kisayansi la 'cyanobacteria' au 'blue-green algae'.

    Kwa kutumia mwanga wa jua, maji na hewa ya ukaa, chembechembe hizo ziliweza kuzalisha hewa mbalimbali, ikiwemo 'Carbonhydrates' na Oksijeni.

    Kwa kuwa hizo chembechembe ndogo za kibakteria huishi baharini, ilikuwa rahisi kwa oksijeni kutokea baharini kupepea na kuenea katika anga ya dunia na kuzuiliwa hapo na nguvu asili ya uvutano ya dunia ili pia ibaki ikienea pote duniani.

    Mpaka wakati wa kuzuka duniani mimea na viumbe hai miaka takribani bilioni 3.5 iliyopita, tayari oksijeni ilikwa ni tele duniani; na hivyo kutumika kudumisha uhai wa viumbe hadi wakati huu.

    6. UKANDA WA 'OZONE'

    Muundo mwingie muhimu wa asili kwa dunia ni ukanda wa anga ujulikanao kwa jina la 'ozone' ambao umetanda kama 'mwavuli' kwenye anga ya dunia, na kuikinga isidhuriwe na mionzi hatari ya sumu kutoka kwenye Jua.

    Ukanda huo maarufu kama 'ozone layer' umetanda kuanzia usawa wa kilometa 15 kutoka ardhini kwenda juu angani mpaka ukomo wa kilomita takribani 50, ambapo huchuja asilimia kati ya 97 na 99 ya mionzi hatari kwenye miale ya joto la jua.

    Miongoni mwa matatizo yanayosababishwa na mionzi hiyo hatari kutoka kwenye jua, ni pamoja na magonjwa ya saratani ya ngozi kwa bianadamu.

    Pia juu ya ukanda wa tabaka la ozone kuna ukanda mwingine uitwao "atmosphere" ambao ni madhubuti kiasi kwamba vitu vinavyotoka anga za juu na kujaribu kuupenya ili kufika duniani, hukumbana na joto kali na kusambaratishwa kwa kuunguzwa.

    Si kwamba tabaka hilo lina joto, isipokuwa kasi ya "kuanguka" vitu hivyo kutoka juu angani kuja dunia husababisha msuguano na chembechembe za gesi katika eneo hilo na kuzalisha joto mithili ya ndimi za moto.

    Picha za video za vyombo vya 'Apollo' vikirejea duniani kutoka mwezini vikiwa na wanaanga ndani yake na kupenya tabaka hilo kwa kasi ya kilomita 39,000 kwa saa, huonekana kughubikwa na ndimi za moto wa rangi ya njano na bluu.

    Rangi hizo ni ishara ya ukali wa moto huo, lakini kutokana na waundaji wa vyombo hivyo kutumia mchanganyiko wa mabati na plastiki ngumu visivyopenywa na joto, Apollo huonekana kulichana tabaka hilo na kutokea upande wa pili ambao ni anga ya dunia.

    Hivyo basi, mfano huo mdogo unaonesha uimara wa tabaka hilo la 'ozone', ambalo kama ambavyo tumeona huchuja mionzi ya sumu kutoka kwenye mwanga wa jua ili kutolete madhara kwa viumbe duniani.

    Mwanga huo ukisafiri kutoka juani umbali wa kilomita milioni 150 kwa kasi ya kilomita 299,793, hutua duniani ndani ya dakika 8 na sekunde 19 ukiwa tayari umechujwa wakati ukipenya tabaka hilo.

    'Ozone' iligunduliwa mwaka 1913 na wanasayansi wawili wa nchini Ufaransa, Charlest Fabry na Henri Buisson, ambapo kipimo cha kasi ya mwanga kiligunduliwa na mwanasayansia wa anga za juu wa nchini Denmark, Ole Roemer, mwaka 1676.

    7. NGUVU ASILI YA UVUTANO

    Muundo mwingine wa dunia ni nguvu ya asili ya uvutano ya dunia, maarufu kama 'gravitation', ambayo huvuta vitu kuvirejesha chini duniani pale vinaporushwa kwenda juu au vile vinavyoanguka kutoka juu angani.

    Nguvu hiyo ina manufaa makubwa, kwani bila kuwepo duniani binadamu na viumbe wengine wangepeperuka kama karatasi kwenda juu wakati wakitembea juu ya ardhi ya hii.

    Kadhalika, nguvu hiyo husaidia kuvuta hewa ya oksijeni na kuiweka karibu na ardhi kwa ajili ya matumizi mbalimbali.

    Pia, nguvu hiyo husaidia kuiweka dunia, mwezi, jua na sayari zingine katika uwiano wa umbali usio na madhara kutoka kila moja.

    Nguvu hiyo ya asili ndiyo huliweka joto la jua duniani na kubaki kuwa katika kiwango kinachotakiwa, na hivyo kuwezesha viumbe kupata joto la wastani na pia katika kiwango mwanana.

    Nguvu hiyo huvuta mvua kuja duniani na kuwezesha maji ya bahari, maziwa na mito kutulia duniani.

    Mathalani, bila nguvu asili hiyo kuwepo duniani, maji 'yangemwagika' kutoka duniani kwa kutawanyika kama upepo na kupaa kwenda juu angani na kutoweka kabisa.

    Na ndio maana ukirusha maji kwenda juu, hurudi chini ardhini.

    Hebu angalia mfano huu kwamba wanaanga waliokwenda mwenzini walilazimika kuvaa mavazi yenye uzito wa kilo 80 hapa duniani, lakini mavazi hayo kule mwezini yakawa na uzito wa kilo 3.

    Mavazi hayo, yaani viatu, koti, suruali, na kofia nzito yenye miwani maalumu ya kukinga macho dhidi ya mionzi hatari ya jua, vyote kwa pamoja viliunganishwa na kuwa mfano wa sare za 'ovaroli' za mafundi wa magari.

    Mavazi hayo pia mgongoni yakiwa yameunganishwa kwa pamoja na mtungi wa hewa ya oksijeni kwa ajili ya kupumua, yalivaaliwa mahsusi muda mfupi baada ya chombo kutua mwezini.

    Hivyo, msomaji wangu tafakari nini kilisababisha mavazi kuwa mazito hapa duniani, lakini yawe mepesi kule mwezini?

    Jibu ni kwamba nguvu asili ya uvutano hapa duniani ni kubwa kuliko ya kule mwezini.

    Na ndipo tunaona umuhimu wa muundo huo wa nguvu asili ya uvutano, ambapo hapa duniani huvuta vitu kuja chini kwa kasi ya mita 9.81 kwa sekunde, lakini kwa kuwa nguvu ya mwezi ni hafifu, huvuta vitu kwa kasi ndogo ya mita 1.62 kwa sekunde.

    Ingawa nguvu hiyo ya asili iligunduliwa kuwepo duniani miaka mingi iliyopta, mwanafizikia bingwa wa Uingereza, Sir Isaac Newton (1642-1727), ndiye anatambulika kama mgunduzi wa hesabu hizo za nguvu asili hiyo.

    Anaeleza kuwa vitu vyote vyenye maumbo asili, ikiwemo jua, sayari, dunia, mwezi, na vimondo, kila kimoja kina nguvu hiyo katika viwango tofauti.

    Kanuni hiyo, kwa mujibu wa matokeo ya utafiti wake, hueleza kuwa nguvu hiyo ndiyo hufanya jua kuvuta sayari zake ili kulizunguka, huku pia kila sayari ikitumia nguvu 'binafsi' (na kwa uwiano maalumu) kujihami isivutwe hadi kwenda kuligonga jua au kugongana na sayari zingine au vimondo.

    Nguvuasili ya jua ni mita 274 kwa sekunde, ikiwa ni zaidi ya kiasi cha nguvuasili ya kila sayari.

    Muundo huo wa kila sayari kujihami kivyake katika mstari wa njia yake hufahamika kisayansi kama "sayari kuhami mazingira ya njia yake"; yaani kwamba 'a planet has to clear the neighbourhood around its orbit.'

    Newton akiwa amezaliwa 'mtoto-njiti' na baadaye kuibuka kuwa mwenye akili nyingi kiasi cha kukaribia kuwa sawa na mtu wa miujiza, hakuwahi kuoa kutokana na kinachoelezwa kuwa ni " kutokana na kutingwa na shughuli za kimasomo."

    Huoneshwa kuwa muda mwingi alikuwa maabara akifanya tafiti mbalimbali za kisayansi, au akiwa maktaba akijisomea, ama akiandika kitabu, au akifundisha wanafunzi wake.

    Alikuwa bingwa mwenye kipaji cha taaluma nyingi, ikiwemo Fizikia, Kemia, Hisabati, Maarifa ya Anga za Juu, Uchumi, Falsafa, na Theolojia ambayo ni taaluma ya masuala ya kiroho.

    Kwa mujibu wa historia, mwanasayansi huyo gwiji wa kuigwa alihitimu shahada zake zote mbili za sayansi, yaani 'Bachelor' na 'Masters', mwaka 1665 na 1668 katika Chuo Kikuu cha Cambridge, nchini Uingereza.

    Akiwa na umri wa miaka 84, mwanasayansi huyo anayedhaniwa na wengi kuwa bingwa wa hesabu za kisayansi kuliko wote duniani, alifariki mwaka 1727 akiwa usingizini.

    Ripoti ya uchunguzi wa mwili wake huonesha kuwa alikuwa na tatizo la figo, lakini pia alikutwa na kiasi kingi cha zebaki.

    Zebaki hiyo, yamkini, ni kutokana na kudumu mno kwenye maabara za Kemia na Fizikia, ambazo hutumia kemikali aina mbalimbali, zikiwemo hewa za gesi, katika kufanya majaribio ya kisayansi.
    DUNIA NA MAAJABU YAKE (Muundo wa Dunia na Maajabu Yaliyomo) 1. UMRI WA DUNIA HII Dunia yetu ina historia ndefu mno tangu ilipojiunda angani, miaka takribani bilioni 4.5 iliyopita. Tarakimu za umri huo wa miaka bilioni 4.5 ni 4,500,000,000, yaani miaka milioni elfu nne na mia tano iliyopita. Dunia ambayo kwa lugha ya Kiingereza inafahamika vyema kwa jina la 'Earth', pia hujulikana kama 'the World', ikimaanishwa ulimwengu. Aidha, Dunia ni sayari pekee kwenye himaya ya sayari zilizopo chini ya jua ambayo jina lake halitokani na majina ya "Miungu wa Dola" ya Kigiriki au ya Kirumi. Asili ya jina la 'earth' ni 'erde' lenye asili ya nchini Ujerumani, na maana yake ni udongo au ardhi. Mpaka kuweza kupata umri huo wa dunia wanasayansi walifanya kazi ya kutafiti na kisha kuwasilisha matokeo yao kwenye makongamano ya kisayansi duniani, ambapo matokeo hayo yalijadiliwa kwa kina na hatimaye kukubalika kama hivi. Kumbuka katika majadiliano hayo huwepo mivutano mikali miongoni mwa wanasayansi waalikwa, ambapo pia jopo la wanasayansi wanaowasilisha utafiti husika hujikuta wakitakiwa kujibu hoja mbalimbali za wanasayansi wenzao. Kuna wakati baadhi ya matokeo ya tafiti kadhaa hukataliwa, huku watafiti husika wakitakiwa kurejea upya tafiti zao. Wanasayansi hupata umri wa sayari kwa kupima umri wa miamba ya sayari husika, ambapo mwamba wenye umri mkubwa zaidi kuliko miamba yote ndiyo huchukuliwa kuwa umri wa sayari husika. Itakumbukwa kuwa Msahafu wa Biblia (Sura ya Mwanzo 1) husimulia jinsi Mwenyezi Mungu alivyoumba "mbingu na nchi na vyote vilivyomo kwa siku 6," lakini pia Msahafu huohuo kwenye aya zingine hueleza kuwa miaka elfu moja ya duniani yaweza kuwa sawa na siku moja kwenye ya Makazi ya Mwenyezi Mungu. Ni dhahiri kuwa binadamu tukiwa hatuna hoja sahihi kwa maelezo ya aina hiyo, ndipo tunaona ni vyema mambo ya Mwenyezi Mungu kumwachia Yeye Mwenyewe Mwenyezi Mungu. 2. KUUMBIKA DUNIA, SAYARI, JUA, NYOTA Kimsingi, Dunia kama zilivyo sayari zingine zote ilijiunda kutokana na mabaki ya vitu vilivyotumika kuunda Jua. Jua ambalo ni nyota kama zilivyo nyota zote angani, lilijiunda lenyewe kwenye eneo la anga lijulikanalo kama 'Pillars of Creation' (nguzo za uumbaji) katika ukanda wa anga wenye upana ambao huonekana kutokuwa na mwisho. Ukanda huo ujulikanao kama 'Solar Nebula,' umegubikwa na mawingu ya vumbi la huko angani pamoja na aina mbalimbali za gesi na hewa, ikiwemo haidrojeni na heliumu. 'Solar' ni jina la nishati itokanayo na joto la jua, na 'Nebula' kwa lugha ya Kilatini ni "wingu" au vumbi la gesi asilia mithili ya ukungu. Hivyo, 'Solar Nebula' ni ukanda katika anga ya mbali wenye mawingu yaliyosheheni nishati yenye joto, sawa na nishati ya joto la jua. Sasa basi, tunafahamu vyema kuwa jua hutoa mionzi hatari yenye joto kali mithili ya moto mkali, na ambayo ikiboreshwa kisayansi pia huweza kutoa nishati ya umeme. Hivyo, kwa muktadha huo, hebu ngoja sasa tuleta pamoja hewa za gesi, zikiwemo haidrojeni na heliumu, mawingu yenye nishati ya umeme wa jua, vumbi la angani na tufani itokanayo na mchafuko mbaya wa hali ya hewa huko anga za mbali. Na ili kuweza kupata matokeo yanayotakiwa, hebu pia tutambue uwepo wa nguvu kubwa ya asili katika kiwango kijulikanacho kwa jina la "Supernatural Power", ambayo ndiyo huwa kisababishi cha mambo yote. Kisayansi, "Supernatural Power" ni nguvu kubwa ya asili ambayo huendesha mifumo mbalimbali ya asili, ambapo duniani nguvu hiyo hujulikana kama Nguvu ya Mungu. Nguvu asili hiyo, yaani Supernatural Power, husababisha tufani ambayo huvurumisha kwa pamoja vitu vyote hivyo, (gesi, hewa, mawingu yenye nishati ya joto na vumbi la angani) ili kuunda tufani yenye umbo la duara. Duara hiyo ni kama ile itokanayo na kimbunga kikali duniani, na ambacho sasa tutaona kikifungamanisha pamoja vitu vyote hivyo katika mchafuko mkubwa wa hali mbaya ya hewa. Natumia maneno ya msisitizo kuelezea "ukubwa" wa mchafuko huo wa hali ya hewa katika eneo hilo la anga, kwani katika kuunda sayari au nyota nguvuasili kubwa hutumika. Aidha, tufani hiyo ya duara itakayoanza kidogo kidogo kama kimbunga kikali, itazidi kukua hadi kuwa na kipenyo cha takribani kilomita 10 hadi 200 au zaidi na kwendelea. Tufani hiyo ndiyo itavurumisha kwa pamoja gesi na hewa za naitrojeni na heliumu, mawingu ya nishati ya joto na vumbi la angani (kama kifanyavyo kimbunga kikali katika eneo tambarare la duniani). Pia, wakati mchafuko huo wa hali mbaya ya hewa ukiendelea, hebu ngoja sisi watazamaji tujibanze mahali fulani kwa mbali kushuhudia duara hiyo ya tufani ikijizungusha yenyewe bila kukoma kwa kipindi cha miaka mingi. Kitakachofuata ni kuanza kuona kiini cha moto kikianza kujiunda katikati ya duara hiyo ya tufani kali, huku pia nje ya duara hiyo vitu kibao vikivutwa kujiunga na mzunguko wa hiyo tufani ya duara. Vitu hivyo ni pamoja na vumbi zaidi la angani, na gesi zaidi zenye joto kali. Wakati huohuo kipenyo na mzingo wa duara hiyo vitazidi kuongezeka upana na ukubwa, mfano wa duara yenye umbo sawa na la mpira mkubwa wa miguu. Hivyo, baada ya miaka takribani milioni moja tutashangaa kuona lile vumbi likigeuka taratibu kuwa miamba ya moto ndani ya kiini cha tufani hiyo ya duara. Miamba hiyo ni kutokana na lile vumbi la angani ambalo hatimaye limeshikamana pamoja mithili ya zege, na hatimaye kuwa miamba ndani ya tufani ya duara. Sanjari na kuundika huko ndani ya kitovu cha hiyo tufani ya duara, pia kwelekea nje ya duara hiyo utaundika udongo ambao ardhi, mchanga na mawe. Kimsingi, vitu hivyo pia ni matokeo ya lile vumbi la angani ambalo lilikusanywa pamoja na kuvutwa na kasi ya mzunguko wa tufani. Hatua hiyo mpya inatokana na kuwepo mshikamano na mgandamizo wa zile chembechembe za lile vumbivumbi ndani ya tufani. Vurumai hiyo ya mzunguko wa hiyo tufani ya duara yenye vumbi, itazidi kukua hadi kuunda sumaku ya asili ndani ya kile kitovu cha duara ya tufani. Kutokana na duara hiyo ya tufani kuongezeka ukubwa, hatimaye sumaku iliyopo kwenye kitovu cha duara hiyo itaishiwa nguvu ya kwendelea kunasa vumbi zaidi kuja kwenye mzingo wa hiyo duara ya tufani. Kumbuka kuwa wakati huo hiyo duara pia itaunda kimo kutoka kwenye usawa wa ardhi yake kwenda ndani kwenye kitovu chake, na hivyo kuwa duara ya mviringo kama umbo mfano wa mpira mchezo wa miguu. Baada ya kupita maelfu ya miaka mingi, duara hiyo ambayo hapo awali ilianza kama umbo la tufani na kuzidi kukua huko angani, sasa itakuwa na joto kali kupita kiasi na kuanza kung'aa kama jua. Jua hilo, ndiyo nyota mojawapo ya zile ambazo huonekana usiku ziking'aa angani. Lakini pia wakati wa kujiunda nyota hiyo, kama tulivyoona hapo awali, baadhi ya mabaki yake yaliyokuwa yakitawanyika angani wakati ile tufani ya duara ikijizungusha, huweza kujikusanya pamoja na kuunda sayari ambazo huzunguka baadhi ya hizo nyota. Hivyo ndivyo zilivyojiunda sayari zote ambazo huelea kwa kulizunguka jua letu. Mathalani, sayari zote ambazo hulizunguka jua, ikiwemo dunia zilijiunda kutokana na mabaki ya vitu kama gesi, michanga na mawe ambavyo vilitawanyika angani wakati jua likijiunda (kama ambavyo imeelezwa hapo awali). 3. KIINI CHA DUNIA Dunia yetu ambayo wastani wa nusu kipenyo cha umbo lake la duara ni kilomita 6,371, mzingo wake ni kilomita takribani 40,041. Kama zilivyo sayari zote katika himaya ya jua, dunia nayo ilijiunda wakati jua likijiunda lenyewe. Yaani kwamba sayari ni mabaki ya vitu vilivyotumika kuliunda jua. Kadhalika kama zilivyo sayari zingine zote, dunia nayo ina kiini chake ambacho kipo katikati ya ardhi yake. Kiini hicho kina nguvu kubwa ya sumaku ambayo, pamoja na mambo mengineyo, 'huvuta' umbo hilo la duara kutoka juu ya ardhi kwenda katikati ya kiini hicho. Muundo huo ndio hulifungamanisha pamoja umbo la duara la dunia, na hivyo kuzuia umbo hilo lisifumke kutoka ardhini na kusambaratika. Hiyo ni sawa na mpira wa miguu unavyoweza kupasuka na kusambaratika, kama utajazwa upepo kupita kiasi chake. Kiini hicho ambacho kipo katikati kabisa ya dunia, kinajulikanacho kwa jina la kisayansi la 'Inner Core.' Kiini hicho kina joto kali la sentigredi 6,230 ambacho ndio kiasi cha joto la jua. Kiini hicho kina umbo la duara lenye nusu kipenyo cha kilomita 1,250. Kama ingetokea kuchimba ardhi wima kwenda kwenye kiini hicho, mchimbaji angeanza kukutana na joto la kiini hicho kuanzia kimo cha umbali wa kilomita 5,150 kutoka usawa wa juu ya ardhi tunayotembea. Katika historia ya uchimbaji ardhi, kina kirefu kilichowahi kuchimbwa ardhini ni mita 12,345 (kilomita 12.345) huko Sakhalini, nchini Urusi, kwa ajili ya uvunaji wa mafuta ya petroli. Kiini cha dunia kinaundwa na madini mchanganyiko wa nikeli (nickle), chuma (iron) na dhahabu. Kwa mujibu wa utafiti, inakadiriwa kuwa kama dhahabu hiyo ingechimbwa na kuchomwa mpaka kuwa kimiminika sawa na uji na kisha kumwagwa chini, ingeweza kuifunika dunia yote kwa unene wa sentimeta 45. Kiini hicho muhimu kwa uhai wa sayari hii ya dunia kiligunduliwa mwaka 1936 na mtaalamu wa matetemeko ya ardhi wa nchini Denmark, mwanamama Dkt. Inge Lehmann. Dkt. Lehmann alihitimu shahada yake ya kwanza katika fani ya Hisabati mwaka 1910, ya Uzamili mwaka 1920 (zote kutoka Chuo Kikuu cha Copenhagen nchini mwake), na ile ya Uzamivu kutoka Chuo Kikuu cha Cambridge nchini Uingereza. Alifariki kwa uzee mwaka 1993 akiwa na umri wa miaka 104. 4. MAJI DUNIANI Kupatikana maji kwenye dunia yetu, ni mojawapo ya miundo ambayo haipo katika sayari zingine ambazo tuna taarifa za kitafiti kuzuhusu. Maji ni muhimili muhimu kwa ajili ya uhai wa viumbe wote na mimea, ambavyo kwa pamoja havipo katika sayari zingine za himaya ya jua. Kwa mujibu wa tafiti nyingi ambazo zimefanyika kwa miongo mingi ya miaka kujaribu kubaini nini chanzo cha kuwepo maji duniani, hakuna hata utafiti mmoja ulioonesha kwa usahihi matokeo ya kuridhisha. Miongoni mwa tafiti hizo ni pamoja na ule wa mwaka 2005, ambapo Mkuu wa Idara ya Masomo ya Sayari na Mwezi katika Chuo Kikuu cha Arizona nchini Marekani, Profesa Michael Julian Drake, na mwenzake ambaye ni mtaalamu wa Vimondo, Dkt. Huberto Campins, wa Chuo Kikuu cha Central Florida, walitafiti nini chanzo cha kuwepo maji duniani. Katika mawasilisho yao kwenye kongamano la kisayansi la Chama cha Wanataaluma wa Maarifa ya Anga za Juu (IAU), watafiti hao walikanusha madai ya uwezekano wa dunia hapo kale kugongwa na kimondo kikubwa na kusababisha maji kulipuka kutoka ardhini. Wakiwasilisha matokeo ya utafiti wao kwenye mkutano wa kongamano hilo, magwiji hao wa masuala ya sayari walieleza kwenye waraka wao uitwao "Origin of water on the terrestial planets" (chanzo cha kuwepo maji kwenye sayari). Walidai kuwa maji yaliyopo duniani yaliumbika kwenye ardhi ya dunia tangu mwanzo, wakati ikijiunda angani. Ikumbukwe kuwa eneo la uso wa dunia likiwa ni jumla ya kilomita za mraba milioni 510, asilimia 70.8 ya eneo hilo imefunikwa na maji na asilimia 29.2 ni nchi kavu, ikiwemo milima, mabonde na ardhi tambarare. 5. HEWA YA OKSIJENI Muundo mwingine muhimu katika sayari hii ya dunia ni hewa ambazo ni tawala, yaani Naitrojeni ambayo kwa usahihi imeenea kwa asilimia 78.08 ya hewa yote ya dunia, Oksijeni asilimia 20.95, 'Argon' asilimia 0.93, hewa ya Ukaa (Carbon dioxide) asilimia 0.039, na asilimia moja ni hewa mithili ya mvuke wa maji (water vapour). Hewa ya Oksijeni ambayo ni nguzo muhimu kwa ajili ya uhai wa viumbe wote na pia haipatikani kwenye sayari nyingine chini ya jua, inadhaniwa ilianza kupatikana duniani miaka takribani bilioni 2.5 iliyopita kufuatia "kukomaa kwa kiini cha dunia." Kwa mujibu wa matokeo ya tafiti mbalimbali na nadharia za kisayansi, inaoneshwa kuwa kukomaa kwa kiini hicho cha dunia hatimaye ndiko kulisababisha kuzuka duniani milipuko ya volikano ambayo pia ilisababisha kuzuka mabonde na milima. Inaoneshwa kuwa tayari wakati huo maji yaliishakuwepo duniani, na kuwezesha kuzuka chembechembe ndogo sana za kibakteria zijulikanazo kwa jina la kisayansi la 'cyanobacteria' au 'blue-green algae'. Kwa kutumia mwanga wa jua, maji na hewa ya ukaa, chembechembe hizo ziliweza kuzalisha hewa mbalimbali, ikiwemo 'Carbonhydrates' na Oksijeni. Kwa kuwa hizo chembechembe ndogo za kibakteria huishi baharini, ilikuwa rahisi kwa oksijeni kutokea baharini kupepea na kuenea katika anga ya dunia na kuzuiliwa hapo na nguvu asili ya uvutano ya dunia ili pia ibaki ikienea pote duniani. Mpaka wakati wa kuzuka duniani mimea na viumbe hai miaka takribani bilioni 3.5 iliyopita, tayari oksijeni ilikwa ni tele duniani; na hivyo kutumika kudumisha uhai wa viumbe hadi wakati huu. 6. UKANDA WA 'OZONE' Muundo mwingie muhimu wa asili kwa dunia ni ukanda wa anga ujulikanao kwa jina la 'ozone' ambao umetanda kama 'mwavuli' kwenye anga ya dunia, na kuikinga isidhuriwe na mionzi hatari ya sumu kutoka kwenye Jua. Ukanda huo maarufu kama 'ozone layer' umetanda kuanzia usawa wa kilometa 15 kutoka ardhini kwenda juu angani mpaka ukomo wa kilomita takribani 50, ambapo huchuja asilimia kati ya 97 na 99 ya mionzi hatari kwenye miale ya joto la jua. Miongoni mwa matatizo yanayosababishwa na mionzi hiyo hatari kutoka kwenye jua, ni pamoja na magonjwa ya saratani ya ngozi kwa bianadamu. Pia juu ya ukanda wa tabaka la ozone kuna ukanda mwingine uitwao "atmosphere" ambao ni madhubuti kiasi kwamba vitu vinavyotoka anga za juu na kujaribu kuupenya ili kufika duniani, hukumbana na joto kali na kusambaratishwa kwa kuunguzwa. Si kwamba tabaka hilo lina joto, isipokuwa kasi ya "kuanguka" vitu hivyo kutoka juu angani kuja dunia husababisha msuguano na chembechembe za gesi katika eneo hilo na kuzalisha joto mithili ya ndimi za moto. Picha za video za vyombo vya 'Apollo' vikirejea duniani kutoka mwezini vikiwa na wanaanga ndani yake na kupenya tabaka hilo kwa kasi ya kilomita 39,000 kwa saa, huonekana kughubikwa na ndimi za moto wa rangi ya njano na bluu. Rangi hizo ni ishara ya ukali wa moto huo, lakini kutokana na waundaji wa vyombo hivyo kutumia mchanganyiko wa mabati na plastiki ngumu visivyopenywa na joto, Apollo huonekana kulichana tabaka hilo na kutokea upande wa pili ambao ni anga ya dunia. Hivyo basi, mfano huo mdogo unaonesha uimara wa tabaka hilo la 'ozone', ambalo kama ambavyo tumeona huchuja mionzi ya sumu kutoka kwenye mwanga wa jua ili kutolete madhara kwa viumbe duniani. Mwanga huo ukisafiri kutoka juani umbali wa kilomita milioni 150 kwa kasi ya kilomita 299,793, hutua duniani ndani ya dakika 8 na sekunde 19 ukiwa tayari umechujwa wakati ukipenya tabaka hilo. 'Ozone' iligunduliwa mwaka 1913 na wanasayansi wawili wa nchini Ufaransa, Charlest Fabry na Henri Buisson, ambapo kipimo cha kasi ya mwanga kiligunduliwa na mwanasayansia wa anga za juu wa nchini Denmark, Ole Roemer, mwaka 1676. 7. NGUVU ASILI YA UVUTANO Muundo mwingine wa dunia ni nguvu ya asili ya uvutano ya dunia, maarufu kama 'gravitation', ambayo huvuta vitu kuvirejesha chini duniani pale vinaporushwa kwenda juu au vile vinavyoanguka kutoka juu angani. Nguvu hiyo ina manufaa makubwa, kwani bila kuwepo duniani binadamu na viumbe wengine wangepeperuka kama karatasi kwenda juu wakati wakitembea juu ya ardhi ya hii. Kadhalika, nguvu hiyo husaidia kuvuta hewa ya oksijeni na kuiweka karibu na ardhi kwa ajili ya matumizi mbalimbali. Pia, nguvu hiyo husaidia kuiweka dunia, mwezi, jua na sayari zingine katika uwiano wa umbali usio na madhara kutoka kila moja. Nguvu hiyo ya asili ndiyo huliweka joto la jua duniani na kubaki kuwa katika kiwango kinachotakiwa, na hivyo kuwezesha viumbe kupata joto la wastani na pia katika kiwango mwanana. Nguvu hiyo huvuta mvua kuja duniani na kuwezesha maji ya bahari, maziwa na mito kutulia duniani. Mathalani, bila nguvu asili hiyo kuwepo duniani, maji 'yangemwagika' kutoka duniani kwa kutawanyika kama upepo na kupaa kwenda juu angani na kutoweka kabisa. Na ndio maana ukirusha maji kwenda juu, hurudi chini ardhini. Hebu angalia mfano huu kwamba wanaanga waliokwenda mwenzini walilazimika kuvaa mavazi yenye uzito wa kilo 80 hapa duniani, lakini mavazi hayo kule mwezini yakawa na uzito wa kilo 3. Mavazi hayo, yaani viatu, koti, suruali, na kofia nzito yenye miwani maalumu ya kukinga macho dhidi ya mionzi hatari ya jua, vyote kwa pamoja viliunganishwa na kuwa mfano wa sare za 'ovaroli' za mafundi wa magari. Mavazi hayo pia mgongoni yakiwa yameunganishwa kwa pamoja na mtungi wa hewa ya oksijeni kwa ajili ya kupumua, yalivaaliwa mahsusi muda mfupi baada ya chombo kutua mwezini. Hivyo, msomaji wangu tafakari nini kilisababisha mavazi kuwa mazito hapa duniani, lakini yawe mepesi kule mwezini? Jibu ni kwamba nguvu asili ya uvutano hapa duniani ni kubwa kuliko ya kule mwezini. Na ndipo tunaona umuhimu wa muundo huo wa nguvu asili ya uvutano, ambapo hapa duniani huvuta vitu kuja chini kwa kasi ya mita 9.81 kwa sekunde, lakini kwa kuwa nguvu ya mwezi ni hafifu, huvuta vitu kwa kasi ndogo ya mita 1.62 kwa sekunde. Ingawa nguvu hiyo ya asili iligunduliwa kuwepo duniani miaka mingi iliyopta, mwanafizikia bingwa wa Uingereza, Sir Isaac Newton (1642-1727), ndiye anatambulika kama mgunduzi wa hesabu hizo za nguvu asili hiyo. Anaeleza kuwa vitu vyote vyenye maumbo asili, ikiwemo jua, sayari, dunia, mwezi, na vimondo, kila kimoja kina nguvu hiyo katika viwango tofauti. Kanuni hiyo, kwa mujibu wa matokeo ya utafiti wake, hueleza kuwa nguvu hiyo ndiyo hufanya jua kuvuta sayari zake ili kulizunguka, huku pia kila sayari ikitumia nguvu 'binafsi' (na kwa uwiano maalumu) kujihami isivutwe hadi kwenda kuligonga jua au kugongana na sayari zingine au vimondo. Nguvuasili ya jua ni mita 274 kwa sekunde, ikiwa ni zaidi ya kiasi cha nguvuasili ya kila sayari. Muundo huo wa kila sayari kujihami kivyake katika mstari wa njia yake hufahamika kisayansi kama "sayari kuhami mazingira ya njia yake"; yaani kwamba 'a planet has to clear the neighbourhood around its orbit.' Newton akiwa amezaliwa 'mtoto-njiti' na baadaye kuibuka kuwa mwenye akili nyingi kiasi cha kukaribia kuwa sawa na mtu wa miujiza, hakuwahi kuoa kutokana na kinachoelezwa kuwa ni " kutokana na kutingwa na shughuli za kimasomo." Huoneshwa kuwa muda mwingi alikuwa maabara akifanya tafiti mbalimbali za kisayansi, au akiwa maktaba akijisomea, ama akiandika kitabu, au akifundisha wanafunzi wake. Alikuwa bingwa mwenye kipaji cha taaluma nyingi, ikiwemo Fizikia, Kemia, Hisabati, Maarifa ya Anga za Juu, Uchumi, Falsafa, na Theolojia ambayo ni taaluma ya masuala ya kiroho. Kwa mujibu wa historia, mwanasayansi huyo gwiji wa kuigwa alihitimu shahada zake zote mbili za sayansi, yaani 'Bachelor' na 'Masters', mwaka 1665 na 1668 katika Chuo Kikuu cha Cambridge, nchini Uingereza. Akiwa na umri wa miaka 84, mwanasayansi huyo anayedhaniwa na wengi kuwa bingwa wa hesabu za kisayansi kuliko wote duniani, alifariki mwaka 1727 akiwa usingizini. Ripoti ya uchunguzi wa mwili wake huonesha kuwa alikuwa na tatizo la figo, lakini pia alikutwa na kiasi kingi cha zebaki. Zebaki hiyo, yamkini, ni kutokana na kudumu mno kwenye maabara za Kemia na Fizikia, ambazo hutumia kemikali aina mbalimbali, zikiwemo hewa za gesi, katika kufanya majaribio ya kisayansi.
    0 Σχόλια ·0 Μοιράστηκε ·754 Views
  • Tunaishi chini ya jua lenye ushindani mwingi na wa kipuuzi sana kwa kizazi cha sasa.Wale tuliopaswa kurithi ama kujifunza mambo mema kutoka kwao ndo hao wengi wao wanafanya ujinga na kujificha kwenye kivuli cha unavyofikiri sivyo ilivyo.
    Binadamu siku hizi anakufanyia ubaya alaf anakujia Kwa mgongo wa utani.Na bahati mbaya dini na charity siku hizi zinatumika kama kichaka cha kuficha uovu wa watu.Binadamu amekuwa si binadamu tena. Wakati mwingine anae kuchukia na asiyekutakia mema ni ndugu wa damu kabisa,ndo dunia ilipofika.
    Tunaishi kwenye hatari tuliyoamua kuibatiza jina la salama.
    Shari tumeigeuza shwari.
    Maumivu na huzuni ya mtu ni furaha ya mwingine.Huku tukitumia hadhara kutengeneza mazingira ya kuendelea kutekeleza maovu.Kwa kivuli cha nani ameniona?au nani anajua?
    Kile kitu Dunia imeshindwa kutambua majira na nyakati yamebadilika sana.
    Zamani zile kulikuwa hakuna siri ya watu wawili ila zamani hizi hakuna siri ya mtu mmoja.Wakati twasema ni siri kuna mtu mahala fulani anaijua hiyo siri.
    Na hapo ndo tunasema mtu anapigana na kivuli chake mwenyewe Kwa kujiongopea kuwa hakuna maumivi.
    Lakini swali la kujiuliza kati ya kivuli cha mtu na mtu mwenyewe ni nani anaumia? Tutafakari
    Tunaishi chini ya jua lenye ushindani mwingi na wa kipuuzi sana kwa kizazi cha sasa.Wale tuliopaswa kurithi ama kujifunza mambo mema kutoka kwao ndo hao wengi wao wanafanya ujinga na kujificha kwenye kivuli cha unavyofikiri sivyo ilivyo. Binadamu siku hizi anakufanyia ubaya alaf anakujia Kwa mgongo wa utani.Na bahati mbaya dini na charity siku hizi zinatumika kama kichaka cha kuficha uovu wa watu.Binadamu amekuwa si binadamu tena. Wakati mwingine anae kuchukia na asiyekutakia mema ni ndugu wa damu kabisa,ndo dunia ilipofika. Tunaishi kwenye hatari tuliyoamua kuibatiza jina la salama. Shari tumeigeuza shwari. Maumivu na huzuni ya mtu ni furaha ya mwingine.Huku tukitumia hadhara kutengeneza mazingira ya kuendelea kutekeleza maovu.Kwa kivuli cha nani ameniona?au nani anajua? Kile kitu Dunia imeshindwa kutambua majira na nyakati yamebadilika sana. Zamani zile kulikuwa hakuna siri ya watu wawili ila zamani hizi hakuna siri ya mtu mmoja.Wakati twasema ni siri kuna mtu mahala fulani anaijua hiyo siri. Na hapo ndo tunasema mtu anapigana na kivuli chake mwenyewe Kwa kujiongopea kuwa hakuna maumivi. Lakini swali la kujiuliza kati ya kivuli cha mtu na mtu mwenyewe ni nani anaumia? Tutafakari
    Like
    Love
    2
    · 0 Σχόλια ·0 Μοιράστηκε ·534 Views
  • HOJA/NONDO (6) SITA ZA LISSU AKIWA LIVE CLUBHOUSE LEO USIKU

    1. SUALA LA MGAO WA RUZUKU

    "Suala la mgao wa Ruzuku ya chama kwenda kwenye ngazi za Wilaya na Mikoa hata kama ni kidogo lilishakuwa changamoto kubwa sana ndani ya chama chetu licha ya kelele nyingi tunazopiga".

    "Tumefanya ugatuaji wa madaraka kwenda kwenye Kanda, lakini masuala yote yahusuyo fedha tumeshikilia sisi Makao Makuu. Hata Mikutano ya hadhara inaandaliwa na Sekretarieti ya Taifa badala ya kugatua madaraka kwa walio chini ili chama kifanye kazi kama team work".

    "Hili tutalifanyia Kazi kwa weledi wa hali ya juu sana; baada ya uchaguzi kama tukiaminiwa na wanachama wenzetu na wakaamua kutupa dhamana ya kuunda mfumo dhabiti wa uongozi".

    2. SUALA LA WABUNGE VITI WA MAALUM

    "Siku ile ya hotuba yangu nilisema, kama wanachama wenzetu wakituamini kuunda mfumo mpya wa uongozi ndani ya chama chetu, tutaweka ukomo wa muda wa kuutumikia ubunge wa viti maalum ili kutoa fursa kwa wamama wa BAWACHA wengi zaidi kuipata hii fursa; kwa mfano, tunaweza kuweka kwamba;

    "Ukishatumikia viti maalum kwa kipindi cha miaka (5) mitano unatafuta jimbo ukapambane kwenye ubunge wa jimbo maana baada ya hiyo miaka (5) mitano xya kuwepo bungeni unakuwa umepata kianzio cha kukuwezesha ili uwapishe na wengine wapate fursa maana wote wanakipigania chama hiki kwa gharama kubwa na mapito magumu sana".

    3. KUYUMBA KWA MISIMAMO YETU YA CHAMA

    "Itakuwa ni makosa sana kuingia kwenye uchaguzi wa mwaka 2025 kama hakuna mabadiliko ya mambo ya msingi ambayo mara zote yamekuwa vipaumbele vyetu kama chama. Tumefanya makosa huko nyuma mara nyingi sana kuigeuka kama sio kuisaliti kwa maksudi kabisa misimamo yetu ya kuibana dola ya CCM ikiwemo misimamo yetu ya kutoshiriki hizi chaguzi za ajabu; na ndio maana hawa CCM na dola yao wamepata kiburi cha kufanya yale wanayotaka na tunaufyata".

    "Kama wanachama wenzetu wakituamini, tutaonyesha njia nini kifanyike ili hawa ambao miaka yote wameshindwa kutusikia tunadai yapi, watatusikia maana hakuna namna zaidi ya kusimama kwenye misimamo yetu kama chama cha upinzani kinachotegemewa na umma kuipumzisha hii CCM"

    4. SUALA LA MPANGO WA VURUGU SIKU YA UCHAGUZI

    "Nimepewa taarifa na mtu wa heshima sana kuhusu maandalizi ya vurugu kwenye uchaguzi. Kuna watu wanaandaliwa waje waingie ukumbini kama Wanachama, kumbe wapo kwa kazi maalum ya kutorosha masanduku ya kura watakapogundua kwamba, mambo ya upande wao hayako sawa; na mhusika amenidokeza kwamba;

    "Vyovyote vile itakavyokuwa, tuhakikishe uchaguzi unafanyika wakati wa mchana na ameonya uchaguzi usifanyike usiku kwa sababu kuna possibility ya wenzetu kuzima taa zote ili kufanikisha utoroshaji wa kura ama kuingiza ndani kura feki".

    "Taarifa hizi tumezipokea; lakini Katibu Mkuu wa Chama anapaswa kutoa ufafanuzi kuhusu huu mchakato wa uchaguzi utakavyokuwa ili kuhakikisha unakuwa uchaguzi ulio huru na wa haki".

    5. SUALA LA HALI YA CHAMA HUKO TUENDAKO

    "Tazameni chama chetu kinavyozidi kupoteza ile ARI na MORALI ya umma kutuunga mkono kama chama kikuu cha upinzani. Tazameni hata ile nguvu yetu ya vijana iliyokuwa inapelekea chama chetu kiitwe chama cha vijana leo hakuna tena nguvu ya vijana ambao ndio nguvu tegemeo ya chama hasa chama kama CHADEMA kinacholenga kukiondoa chama dola madarakani".

    Leo hii vijana wanaona bora wakacheze pool table na ku-bet mitaani kuliko kukipigania chama chao. Ni kwa nini tumefika kwenye hali hii? Hili ndilo swali la msingi sana ambalo wanachama wenzetu wanaokuja kwenye mkutano mkuu wanapaswa kujiuliza na watafakari hali ya hiki chama chetu itakuwaje miaka mitano mingine ijayo kama hatutabadili mifumo ya uongozi wa chama kupitia uchaguzi huu wa januari".

    6. SUALA LA WENJE NA ABDUL KUHONGA WATU

    "Katika hili niseme wazi hapa, kama kweli nimewahi kuomba msamaha kwenye Kamati Kuu kuhusu suala hilo la Abdul kama Wenje alivyosikika akisema, niombe watoe hadharani ile video nzima iliyokuwa inarekodiwa kikaoni pasipo kuihariri jambo lolote kama watathubutu kufanya hivyo".

    "Kwa kuwa walirekodi ili itumike kama ushahidi wa kuondoa sintofahamu ya jambo hili kwa umma, mimi napendekeza iwekwe hadharani ama hata sauti yake tu ili umma usikilize halafu umma wenyewe utasema umeelewa nini kuhusu chama chao kilipofika na kinapoelekea kama ni salama ama sio salama chini ya watu wale wale".

    Tundu A. Lissu,
    Mgombea Uenyekiti CHADEMA,
    Live Clubhouse Usiku.
    23 Desemba, 2024.
    HOJA/NONDO (6) SITA ZA LISSU AKIWA LIVE CLUBHOUSE LEO USIKU 1. SUALA LA MGAO WA RUZUKU "Suala la mgao wa Ruzuku ya chama kwenda kwenye ngazi za Wilaya na Mikoa hata kama ni kidogo lilishakuwa changamoto kubwa sana ndani ya chama chetu licha ya kelele nyingi tunazopiga". "Tumefanya ugatuaji wa madaraka kwenda kwenye Kanda, lakini masuala yote yahusuyo fedha tumeshikilia sisi Makao Makuu. Hata Mikutano ya hadhara inaandaliwa na Sekretarieti ya Taifa badala ya kugatua madaraka kwa walio chini ili chama kifanye kazi kama team work". "Hili tutalifanyia Kazi kwa weledi wa hali ya juu sana; baada ya uchaguzi kama tukiaminiwa na wanachama wenzetu na wakaamua kutupa dhamana ya kuunda mfumo dhabiti wa uongozi". 2. SUALA LA WABUNGE VITI WA MAALUM "Siku ile ya hotuba yangu nilisema, kama wanachama wenzetu wakituamini kuunda mfumo mpya wa uongozi ndani ya chama chetu, tutaweka ukomo wa muda wa kuutumikia ubunge wa viti maalum ili kutoa fursa kwa wamama wa BAWACHA wengi zaidi kuipata hii fursa; kwa mfano, tunaweza kuweka kwamba; "Ukishatumikia viti maalum kwa kipindi cha miaka (5) mitano unatafuta jimbo ukapambane kwenye ubunge wa jimbo maana baada ya hiyo miaka (5) mitano xya kuwepo bungeni unakuwa umepata kianzio cha kukuwezesha ili uwapishe na wengine wapate fursa maana wote wanakipigania chama hiki kwa gharama kubwa na mapito magumu sana". 3. KUYUMBA KWA MISIMAMO YETU YA CHAMA "Itakuwa ni makosa sana kuingia kwenye uchaguzi wa mwaka 2025 kama hakuna mabadiliko ya mambo ya msingi ambayo mara zote yamekuwa vipaumbele vyetu kama chama. Tumefanya makosa huko nyuma mara nyingi sana kuigeuka kama sio kuisaliti kwa maksudi kabisa misimamo yetu ya kuibana dola ya CCM ikiwemo misimamo yetu ya kutoshiriki hizi chaguzi za ajabu; na ndio maana hawa CCM na dola yao wamepata kiburi cha kufanya yale wanayotaka na tunaufyata". "Kama wanachama wenzetu wakituamini, tutaonyesha njia nini kifanyike ili hawa ambao miaka yote wameshindwa kutusikia tunadai yapi, watatusikia maana hakuna namna zaidi ya kusimama kwenye misimamo yetu kama chama cha upinzani kinachotegemewa na umma kuipumzisha hii CCM" 4. SUALA LA MPANGO WA VURUGU SIKU YA UCHAGUZI "Nimepewa taarifa na mtu wa heshima sana kuhusu maandalizi ya vurugu kwenye uchaguzi. Kuna watu wanaandaliwa waje waingie ukumbini kama Wanachama, kumbe wapo kwa kazi maalum ya kutorosha masanduku ya kura watakapogundua kwamba, mambo ya upande wao hayako sawa; na mhusika amenidokeza kwamba; "Vyovyote vile itakavyokuwa, tuhakikishe uchaguzi unafanyika wakati wa mchana na ameonya uchaguzi usifanyike usiku kwa sababu kuna possibility ya wenzetu kuzima taa zote ili kufanikisha utoroshaji wa kura ama kuingiza ndani kura feki". "Taarifa hizi tumezipokea; lakini Katibu Mkuu wa Chama anapaswa kutoa ufafanuzi kuhusu huu mchakato wa uchaguzi utakavyokuwa ili kuhakikisha unakuwa uchaguzi ulio huru na wa haki". 5. SUALA LA HALI YA CHAMA HUKO TUENDAKO "Tazameni chama chetu kinavyozidi kupoteza ile ARI na MORALI ya umma kutuunga mkono kama chama kikuu cha upinzani. Tazameni hata ile nguvu yetu ya vijana iliyokuwa inapelekea chama chetu kiitwe chama cha vijana leo hakuna tena nguvu ya vijana ambao ndio nguvu tegemeo ya chama hasa chama kama CHADEMA kinacholenga kukiondoa chama dola madarakani". Leo hii vijana wanaona bora wakacheze pool table na ku-bet mitaani kuliko kukipigania chama chao. Ni kwa nini tumefika kwenye hali hii? Hili ndilo swali la msingi sana ambalo wanachama wenzetu wanaokuja kwenye mkutano mkuu wanapaswa kujiuliza na watafakari hali ya hiki chama chetu itakuwaje miaka mitano mingine ijayo kama hatutabadili mifumo ya uongozi wa chama kupitia uchaguzi huu wa januari". 6. SUALA LA WENJE NA ABDUL KUHONGA WATU "Katika hili niseme wazi hapa, kama kweli nimewahi kuomba msamaha kwenye Kamati Kuu kuhusu suala hilo la Abdul kama Wenje alivyosikika akisema, niombe watoe hadharani ile video nzima iliyokuwa inarekodiwa kikaoni pasipo kuihariri jambo lolote kama watathubutu kufanya hivyo". "Kwa kuwa walirekodi ili itumike kama ushahidi wa kuondoa sintofahamu ya jambo hili kwa umma, mimi napendekeza iwekwe hadharani ama hata sauti yake tu ili umma usikilize halafu umma wenyewe utasema umeelewa nini kuhusu chama chao kilipofika na kinapoelekea kama ni salama ama sio salama chini ya watu wale wale". Tundu A. Lissu, Mgombea Uenyekiti CHADEMA, Live Clubhouse Usiku. 23 Desemba, 2024.
    Love
    Like
    5
    · 1 Σχόλια ·0 Μοιράστηκε ·539 Views
  • Mkuu wa kitengo cha maudhui wa klabu ya Yanga SC, Privaldinho amjia juu Wilson Orumo.

    "Ukiniuliza miongoni mwa wachambuzi wenye uelewa mzuri wa soka nisipotaja jina la @wilsonoruma_ basi ulizia natumia kinywaji gani muda pengine nimepiga vyombo.

    Namfahamu Udom. Najua uwezo wake. Sijui shida gani imempata. Anyway twende kwenye hoja yake.

    Kwamba kumkejeli Pacome hujagusa biashara ya watu? Sijaona ukiongelea hili bali umejikita kwenye ishu ya mtengeneza jezi. Kuna nyakati tuliitwa maiti? Kuna nyakati walisema jezi zetu ni mbaya mno. Je mzee wangu ulikemea? Je Yanga tulisema chochote?

    Iko hivi

    Utani wa jadi ni mbwembwe za Makolo na mabingwa wa kihistoria. Ni kama mchezo wa ngumi tu. Mbwembwembwe na kejeli zeru ndio tambo zetu. Ipo hivo miaka na miaka. Kama hutaki kutaniwa usije kwenye hizi timu mbili. Pengine kauze suti za wanasheria huko kidogo kuna maadili.

    Uvumilivu wa utani wa jadi umegusa wengi. Huyu Oruma mwenyewe amewahi kuingia kwenye utani wa jadi. Mara kadhaa ametumia maneno makali dhidi ya Yanga na Yanga haijawahi kumgusa.

    Oruma ni bingwa kuitania Yanga ametuita gongo wazi. Hakuna mtu kutoka Yanga aliyewahi kwenda mahakamani. Gongo wazi ni neno la kejeli kwa Yanga.

    Pengine basi kwa kuwa anaharibu brand ya Yanga twende mahakamani na invoice? Mtu ambaye tulitegemea awe mchambuzi na mtenda haki anaingia kwenye utani na Yanga inaona sawa tu. Lakini walipohisi ally amemlenga mtu wao wanatoka na Mapanga.

    Oruma, ni mtu mwenye akili na uelewa mkubwa wa mambo. Kwa bahati mbaya hivi karibuni amechagua njia ambayo binafsi simwelewi. Ni kama anapigana na Yanga hadharani.

    Ni rafiki yangu na mara kadhaa huwa namwambia. Uwezo wake wa kuchanganua mambo ni hazina kubwa kwa taifa letu. Lakini matumizi yake amejikita kwenye siasa za mpira ambazo mara nyingi kwangu sioni kama zina afya.

    Moja kati ya wachambuzi ambao wangeamua kujikita kwenye tactically analysis angesaidia sana TAIFA hili. Leo hii anaita Yanga Gongowazi hivi na sisi tukiamua kuitafutia jina baya EFM atakaa kimya?

    Mimi nafikiri rafiki yangu huyu afanye tafakuri ya kutosha. Kwanza afaham kuwa taifa linamhitaji zaidi kuliko vijana wanaochipukia wanavyosaka comments na likes. Atafakari vyema njia zake.

    Shalom."
    Mkuu wa kitengo cha maudhui wa klabu ya Yanga SC, Privaldinho amjia juu Wilson Orumo. "Ukiniuliza miongoni mwa wachambuzi wenye uelewa mzuri wa soka nisipotaja jina la @wilsonoruma_ basi ulizia natumia kinywaji gani muda pengine nimepiga vyombo. Namfahamu Udom. Najua uwezo wake. Sijui shida gani imempata. Anyway twende kwenye hoja yake. Kwamba kumkejeli Pacome hujagusa biashara ya watu? Sijaona ukiongelea hili bali umejikita kwenye ishu ya mtengeneza jezi. Kuna nyakati tuliitwa maiti? Kuna nyakati walisema jezi zetu ni mbaya mno. Je mzee wangu ulikemea? Je Yanga tulisema chochote? Iko hivi Utani wa jadi ni mbwembwe za Makolo na mabingwa wa kihistoria. Ni kama mchezo wa ngumi tu. Mbwembwembwe na kejeli zeru ndio tambo zetu. Ipo hivo miaka na miaka. Kama hutaki kutaniwa usije kwenye hizi timu mbili. Pengine kauze suti za wanasheria huko kidogo kuna maadili. Uvumilivu wa utani wa jadi umegusa wengi. Huyu Oruma mwenyewe amewahi kuingia kwenye utani wa jadi. Mara kadhaa ametumia maneno makali dhidi ya Yanga na Yanga haijawahi kumgusa. Oruma ni bingwa kuitania Yanga ametuita gongo wazi. Hakuna mtu kutoka Yanga aliyewahi kwenda mahakamani. Gongo wazi ni neno la kejeli kwa Yanga. Pengine basi kwa kuwa anaharibu brand ya Yanga twende mahakamani na invoice? Mtu ambaye tulitegemea awe mchambuzi na mtenda haki anaingia kwenye utani na Yanga inaona sawa tu. Lakini walipohisi ally amemlenga mtu wao wanatoka na Mapanga. Oruma, ni mtu mwenye akili na uelewa mkubwa wa mambo. Kwa bahati mbaya hivi karibuni amechagua njia ambayo binafsi simwelewi. Ni kama anapigana na Yanga hadharani. Ni rafiki yangu na mara kadhaa huwa namwambia. Uwezo wake wa kuchanganua mambo ni hazina kubwa kwa taifa letu. Lakini matumizi yake amejikita kwenye siasa za mpira ambazo mara nyingi kwangu sioni kama zina afya. Moja kati ya wachambuzi ambao wangeamua kujikita kwenye tactically analysis angesaidia sana TAIFA hili. Leo hii anaita Yanga Gongowazi hivi na sisi tukiamua kuitafutia jina baya EFM atakaa kimya? Mimi nafikiri rafiki yangu huyu afanye tafakuri ya kutosha. Kwanza afaham kuwa taifa linamhitaji zaidi kuliko vijana wanaochipukia wanavyosaka comments na likes. Atafakari vyema njia zake. Shalom."
    0 Σχόλια ·0 Μοιράστηκε ·587 Views
  • KIJANA SHUJAA NA KISIMA CHA GIZA

    Kulikuwa na kijiji kilichoitwa Mwanga, kilichozungukwa na mlima mkubwa uliotisha unaoitwa Mlima Giza. Katika mlima huo, kulikuwa na kisima cha kale kilichojulikana kama "Kisima cha Giza." Wazee wa kijiji walisema kwamba kisima hicho kilikuwa na nguvu za ajabu zinazoweza kuharibu au kuokoa kijiji. Lakini kulikuwa na onyo: yeyote aliyethubutu kuingia kisima hicho alikabiliana na majaribu ya kutisha.

    Siku moja, maafa yalifika kijijini. Ukame wa ajabu ulianza, mito ikakauka, mimea ikafa, na watu wakaanza kukata tamaa. Wazee walikusanyika na kuamua kwamba mtu mmoja shupavu alipaswa kwenda kwenye Kisima cha Giza kutafuta suluhisho. Hakuna aliyethubutu kujitolea, isipokuwa kijana mdogo mwenye moyo wa ujasiri aliyeitwa Baraka.

    Baraka, akiwa na azma ya kuokoa kijiji chake, aliandaa safari yake. Akiwa amebeba upinde wake, mshale mmoja, na mfuko wa maji, alianza kupanda Mlima Giza huku upepo mkali ukivuma. Njiani, alikutana na changamoto za kutisha—nyoka wakubwa waliotokea ghafla, na kelele za ajabu zilizokuwa zikimzomea. Lakini hakurudi nyuma.

    Baada ya muda mrefu wa kupambana, Baraka alifika kwenye Kisima cha Giza. Kilikuwa na mwanga hafifu unaotoka chini ya ardhi, na sauti ya mtoa fumbo ikazungumza kutoka gizani:
    "Kuokoa kijiji chako, lazima utoe kitu cha thamani zaidi maishani mwako. Je, uko tayari?"

    Baraka alitafakari kwa muda mfupi. Alijua maisha yake mwenyewe yalikuwa ya thamani zaidi kwake, lakini pia alihisi uzito wa dhiki ya kijiji chake. Bila kusita, alisema, "Niko tayari."

    Ghafla, mwanga mkali ulilipuka kutoka kisimani, na mafuriko ya maji safi yalitoka yakiteremka kuelekea kijijini. Mlima Giza ulianza kutikisika, lakini Baraka alishikilia imani. Wakati maji yalipokuwa yakiendelea kutiririka, sauti ile ilisema, "Ujasiri wako umeokoa kijiji chako. Furahi, kijana shujaa."

    Baraka alirejea kijijini akiwa salama, akishangiliwa na wakazi waliokuwa wakicheza kwa furaha huku wakinywa maji safi yaliyokuwa yamerejea. Kutoka siku hiyo, Baraka aliheshimiwa kama shujaa wa kijiji, na jina lake lilisimuliwa kwa vizazi kama mfano wa ujasiri na kujitolea kwa ajili ya wengine.

    Mafundisho: "Ujasiri wa kujitoa kwa ajili ya wengi una nguvu ya kubadilisha historia."
    KIJANA SHUJAA NA KISIMA CHA GIZA Kulikuwa na kijiji kilichoitwa Mwanga, kilichozungukwa na mlima mkubwa uliotisha unaoitwa Mlima Giza. Katika mlima huo, kulikuwa na kisima cha kale kilichojulikana kama "Kisima cha Giza." Wazee wa kijiji walisema kwamba kisima hicho kilikuwa na nguvu za ajabu zinazoweza kuharibu au kuokoa kijiji. Lakini kulikuwa na onyo: yeyote aliyethubutu kuingia kisima hicho alikabiliana na majaribu ya kutisha. Siku moja, maafa yalifika kijijini. Ukame wa ajabu ulianza, mito ikakauka, mimea ikafa, na watu wakaanza kukata tamaa. Wazee walikusanyika na kuamua kwamba mtu mmoja shupavu alipaswa kwenda kwenye Kisima cha Giza kutafuta suluhisho. Hakuna aliyethubutu kujitolea, isipokuwa kijana mdogo mwenye moyo wa ujasiri aliyeitwa Baraka. Baraka, akiwa na azma ya kuokoa kijiji chake, aliandaa safari yake. Akiwa amebeba upinde wake, mshale mmoja, na mfuko wa maji, alianza kupanda Mlima Giza huku upepo mkali ukivuma. Njiani, alikutana na changamoto za kutisha—nyoka wakubwa waliotokea ghafla, na kelele za ajabu zilizokuwa zikimzomea. Lakini hakurudi nyuma. Baada ya muda mrefu wa kupambana, Baraka alifika kwenye Kisima cha Giza. Kilikuwa na mwanga hafifu unaotoka chini ya ardhi, na sauti ya mtoa fumbo ikazungumza kutoka gizani: "Kuokoa kijiji chako, lazima utoe kitu cha thamani zaidi maishani mwako. Je, uko tayari?" Baraka alitafakari kwa muda mfupi. Alijua maisha yake mwenyewe yalikuwa ya thamani zaidi kwake, lakini pia alihisi uzito wa dhiki ya kijiji chake. Bila kusita, alisema, "Niko tayari." Ghafla, mwanga mkali ulilipuka kutoka kisimani, na mafuriko ya maji safi yalitoka yakiteremka kuelekea kijijini. Mlima Giza ulianza kutikisika, lakini Baraka alishikilia imani. Wakati maji yalipokuwa yakiendelea kutiririka, sauti ile ilisema, "Ujasiri wako umeokoa kijiji chako. Furahi, kijana shujaa." Baraka alirejea kijijini akiwa salama, akishangiliwa na wakazi waliokuwa wakicheza kwa furaha huku wakinywa maji safi yaliyokuwa yamerejea. Kutoka siku hiyo, Baraka aliheshimiwa kama shujaa wa kijiji, na jina lake lilisimuliwa kwa vizazi kama mfano wa ujasiri na kujitolea kwa ajili ya wengine. Mafundisho: "Ujasiri wa kujitoa kwa ajili ya wengi una nguvu ya kubadilisha historia."
    Like
    Love
    2
    · 0 Σχόλια ·0 Μοιράστηκε ·378 Views
  • "Unafanya kazi masaa 8 kuishi 4.
    Unafanya kazi kwa siku 6 ili kufurahiya 1.
    Unafanya kazi masaa 8 kula katika dakika 15.
    Unafanya kazi masaa 8 kulala 5.
    Unafanya kazi mwaka mzima ili kuchukua likizo ya wiki moja au mbili.
    Unafanya kazi maisha yako yote ili uweze kustaafu uzee.
    Na kutafakari tu mihemko yako ya mwisho.
    Hatimaye unagundua kuwa maisha si chochote ila ni mbishi wa kujizoeza usahaulifu wako.
    Tumezoea sana utumwa wa mali, kijamii hivi kwamba hatuoni tena minyororo"
    Maisha ni safari fupi, iishi!
    "Unafanya kazi masaa 8 kuishi 4. Unafanya kazi kwa siku 6 ili kufurahiya 1. Unafanya kazi masaa 8 kula katika dakika 15. Unafanya kazi masaa 8 kulala 5. Unafanya kazi mwaka mzima ili kuchukua likizo ya wiki moja au mbili. Unafanya kazi maisha yako yote ili uweze kustaafu uzee. Na kutafakari tu mihemko yako ya mwisho. Hatimaye unagundua kuwa maisha si chochote ila ni mbishi wa kujizoeza usahaulifu wako. Tumezoea sana utumwa wa mali, kijamii hivi kwamba hatuoni tena minyororo" Maisha ni safari fupi, iishi!
    Like
    Love
    2
    · 0 Σχόλια ·0 Μοιράστηκε ·191 Views
  • Mapenzi yana tabia ya kumuweka mtu njia panda, Na ilivyo kawaida ya Mapenzi unapokuwa huna mtu unakuwa salama kiafya na kiakili japo moyo unahangaika kutafuta faraja. Ukimpata mtu "MPENZI" ujue atakuja na mwingine ili kukupa changamoto.

    Sasa basi utakuta Mmoja atakuwa na MVUTO lakini hana wazo la kuishi nawe, Mwingine hana MVUTO lakini anayo haja ya kuishi nawe kama MUME/MKE..!

    Hapo ndipo palipomshinda Binadam hata akajikuta anakuwa njia panda,

    *UFANYE NINI KUKABILIANA NA HILI?*

    Kwanza kabisa lazima ujue kuwa Mapenzi ni HISIA... Ni jambo la kwanza kwa Mtu yeyote, Sikiliza hisia zako kabla ya kuingia kwenye mahusiano, Uangalie MOYO wako kama una furaha na nani Kati ya hao wanaosema I LOVE YOU...

    Jiweke mahala kuyaishi maisha ya AMANI kuliko chochote, Amani inatokana na utulivu wa moyo, Asiye na MVUTO kama una hisia nae pambana kumpa mvuto wako mwenyewe, Kama ni mwenye MVUTO basi itetee nafsi yako, Maana kwenye MAPENZI hakuna linaloshindikana ikiwa penzi litaongozwa na UKARIBU, MAELEWANO, UPOLE NA UVUMILIVU...!

    Hata chizi Ukiwa nae Karibu na mkaelewana sana, hawezi kukudhuru kwa asilimia kubwa... Wengi husimama njia panda na kushindwa kuamua vyema mwisho wao huwa mbaya, ni bora sana kujitafakari kabla ya kuamua ili kujiweka sehemu salama.

    Mapenzi yanayodumu ni yenye HISIA maana moyo huongea kwa mazuri tu, Ole wako UOE/UOLEWE na mtu asiye na hisia nawe then aje kumpata wa hisia zake Mweeee UTAJUTA MBONA... Hakunaga kusikilizwa wala kupewa nafasi ya kujieleza, Uwe na cheti cha NDOA ama mna MTOTO/WATOTO hayo hayatakuwa na nafasi tena maana mwenzio atakuwa anautetea moyo wake tu.

    Chagua zaidi kuwa na MTU MWENYE HISIA NAWE ili ufurahie Mapenzi, Vinginevyo UTAISHI KWA TAABU SANA JUU YA MAPENZI HAYA YA KARNE YA KIZAZI cha KIDUKU, VISHETI, SERIES NA UONGO MKUBWA....
    Mapenzi yana tabia ya kumuweka mtu njia panda, Na ilivyo kawaida ya Mapenzi unapokuwa huna mtu unakuwa salama kiafya na kiakili japo moyo unahangaika kutafuta faraja. Ukimpata mtu "MPENZI" ujue atakuja na mwingine ili kukupa changamoto. Sasa basi utakuta Mmoja atakuwa na MVUTO lakini hana wazo la kuishi nawe, Mwingine hana MVUTO lakini anayo haja ya kuishi nawe kama MUME/MKE..! Hapo ndipo palipomshinda Binadam hata akajikuta anakuwa njia panda, *UFANYE NINI KUKABILIANA NA HILI?* Kwanza kabisa lazima ujue kuwa Mapenzi ni HISIA... Ni jambo la kwanza kwa Mtu yeyote, Sikiliza hisia zako kabla ya kuingia kwenye mahusiano, Uangalie MOYO wako kama una furaha na nani Kati ya hao wanaosema I LOVE YOU... Jiweke mahala kuyaishi maisha ya AMANI kuliko chochote, Amani inatokana na utulivu wa moyo, Asiye na MVUTO kama una hisia nae pambana kumpa mvuto wako mwenyewe, Kama ni mwenye MVUTO basi itetee nafsi yako, Maana kwenye MAPENZI hakuna linaloshindikana ikiwa penzi litaongozwa na UKARIBU, MAELEWANO, UPOLE NA UVUMILIVU...! Hata chizi Ukiwa nae Karibu na mkaelewana sana, hawezi kukudhuru kwa asilimia kubwa... Wengi husimama njia panda na kushindwa kuamua vyema mwisho wao huwa mbaya, ni bora sana kujitafakari kabla ya kuamua ili kujiweka sehemu salama. Mapenzi yanayodumu ni yenye HISIA maana moyo huongea kwa mazuri tu, Ole wako UOE/UOLEWE na mtu asiye na hisia nawe then aje kumpata wa hisia zake Mweeee UTAJUTA MBONA... Hakunaga kusikilizwa wala kupewa nafasi ya kujieleza, Uwe na cheti cha NDOA ama mna MTOTO/WATOTO hayo hayatakuwa na nafasi tena maana mwenzio atakuwa anautetea moyo wake tu. Chagua zaidi kuwa na MTU MWENYE HISIA NAWE ili ufurahie Mapenzi, Vinginevyo UTAISHI KWA TAABU SANA JUU YA MAPENZI HAYA YA KARNE YA KIZAZI cha KIDUKU, VISHETI, SERIES NA UONGO MKUBWA....
    0 Σχόλια ·0 Μοιράστηκε ·587 Views
  • Kuna hali ngumu sana unaipitia leo, maumivu ni makali na maswali ni mengi sana unajiuliza. Dalili zote zinaonyesha umefika mwisho na kila unakogeuka haupati msaada.

    Ulipofika ni kama unajiambia “sina thamani tena, sitaweza kuinuka tena na hakuna faida ya kuishi tena”. Ukitafakari hakuna ubishi kuwa sio rahisi kuinuka tena. Unajiambia “kama ni kulia basi nimelia hadi machozi yameisha, kama kuomba nimeshaomba sana, kama ni kufanya bidii nimejaribu kila mbinu ila sijaona matokeo”.

    Sasa naomba nikukumbushe yafuatayo:

    1)Usijaribu kufikiri kuwa MUNGU amekuacha na hakujali tena: Bado anakuwazia mema. Ingawa wewe unayo njia nzuri, kumbuka yeye anaona zaidi yako na anajua zaidi yako-Badala ya kulaumu, endelea kumuamini.

    2)Na hili nalo utashinda. Kumbuka lile gumu ambalo ulipitia huko nyuma na uliona kama hautavuka lakini ulivuka-NA HILI NALO UTASHINDA na itabakia historia.

    3)Usijifungie peke yako, usijitenge peke yako. Kuna mawazo yanakuambia kila mtu hayuko tayari kukusaidia, hilo sio kweli na usiliamini. Mungu bado anao watu wanaokuthamini, wanaokupenda, wanaokuwazia mema na wako tayari kukusaidia. Hata kama wengi wameonekana hawako tayari kukusaidia BADO wapo ambao WANAKUTHAMINI na WATASIMAMA na wewe. Toka ndani na kutana na watu, kuna mtu amendaliwa ili ukutane naye lazima utoke.

    Nasubiria siku ambayo utaibuka mshindi na utakuwa umelivuka hili kwa ushindi.

    NA HILI NALO LITAPITA.
    Kuna hali ngumu sana unaipitia leo, maumivu ni makali na maswali ni mengi sana unajiuliza. Dalili zote zinaonyesha umefika mwisho na kila unakogeuka haupati msaada. Ulipofika ni kama unajiambia “sina thamani tena, sitaweza kuinuka tena na hakuna faida ya kuishi tena”. Ukitafakari hakuna ubishi kuwa sio rahisi kuinuka tena. Unajiambia “kama ni kulia basi nimelia hadi machozi yameisha, kama kuomba nimeshaomba sana, kama ni kufanya bidii nimejaribu kila mbinu ila sijaona matokeo”. Sasa naomba nikukumbushe yafuatayo: 1)Usijaribu kufikiri kuwa MUNGU amekuacha na hakujali tena: Bado anakuwazia mema. Ingawa wewe unayo njia nzuri, kumbuka yeye anaona zaidi yako na anajua zaidi yako-Badala ya kulaumu, endelea kumuamini. 2)Na hili nalo utashinda. Kumbuka lile gumu ambalo ulipitia huko nyuma na uliona kama hautavuka lakini ulivuka-NA HILI NALO UTASHINDA na itabakia historia. 3)Usijifungie peke yako, usijitenge peke yako. Kuna mawazo yanakuambia kila mtu hayuko tayari kukusaidia, hilo sio kweli na usiliamini. Mungu bado anao watu wanaokuthamini, wanaokupenda, wanaokuwazia mema na wako tayari kukusaidia. Hata kama wengi wameonekana hawako tayari kukusaidia BADO wapo ambao WANAKUTHAMINI na WATASIMAMA na wewe. Toka ndani na kutana na watu, kuna mtu amendaliwa ili ukutane naye lazima utoke. Nasubiria siku ambayo utaibuka mshindi na utakuwa umelivuka hili kwa ushindi. NA HILI NALO LITAPITA.
    Like
    1
    · 0 Σχόλια ·0 Μοιράστηκε ·380 Views
  • Ndege Aliye mtini Ni ngumu Kumshusha Chini akiwa ameshiba.
    Tafakari
    Ndege Aliye mtini Ni ngumu Kumshusha Chini akiwa ameshiba. Tafakari
    Like
    2
    · 0 Σχόλια ·0 Μοιράστηκε ·310 Views
  • Mtu akikuomba ushauri, tafakari kwanza kabla ya kumshauri.
    Mtu akikuomba ushauri, tafakari kwanza kabla ya kumshauri.
    Like
    2
    · 2 Σχόλια ·0 Μοιράστηκε ·190 Views
  • *TABIA 12 ZITAKAZOKUFANYA UWE MWENYE FURAHA MAISHANI*

    *1. SAMEHE*
    Samehee hata wasiostahili kusamehewa.
    Usikubali kuwa na kinyongo au ugomvi na mtu yeyeto.
    Jifunze kupotezea.
    Usimjibu kila mtu kila kitu.
    Hata ukimya ni majibu.

    *2. JIAMINI*

    Hakuna lisilowezekana chini ya jua. Anza sasa.
    Wenye imani wana amani kila wakati.
    Wenye imani wanakuwa na uhakika wa kile wanachokitarajia.

    *3. JIFUNZE*

    Mungu hakumuumba mtu kuweza kila kitu wakati wowote.

    *4. JIPENDE*

    Umeumbwa kwa sura na mfano wa Mungu. Usijidharau wala kujishusha kiwango. Jitamkia mambo mazuri kila wakati.

    *5. TABASAMU*

    Furaha ni tiba ya moyo
    Jifunze kuhesabu baraka ambazo Mungu amekupatia itakisaidia kutabasamu kila wakati.

    *6. USIHUKUMU*

    Hakuna mwaminifu chini ya jua. Kila mmoja anakosea hata wewe huwa unakosea na kuwakosea wengine.

    *7. JIHESHIMU*

    Mfumo wa maisha yako ndio utakuwa msaada kwa wengine. Wewe ndiye utakayewafanya wengine kukutafasiri.

    *8. PANGA MALENGO*

    Malengo ni taa, dira, ramani,kesho, mwelekeo, matumaini. Usiishi pasipo kujua kesho yako au pasipo kujua unapoelekea.

    *9. FANYA IBADA*

    Mahusiano yako pamoja na Mungu ndio chanzo cha kubarikiwa kwako.

    *10. KULA VIZURI*

    Mwili wako ni hekalu la Roho Mtakatifu kuwa makini sana kwenye ulaji wako. Usile chochote unachotaka Bali kula chochote kinachohitajika mwilini mwako.

    *11. KUWA MKARIMU*

    Hukuja duniani na kitu Bali vyote ulivyonavyo chanzo chake ni Mungu. Lakini pia vyote utaviacha duniani siku yako ya kufa itakapofika. Ukarimu ni akiba ya baadae kwa ajili yako na kizazi chako.

    *12. KUWA NA SHUKRANI*

    Ukitambua na kutafakari ulipotolewa na huyu Mungu hakika hautashindwa kusema asante kwake.
    Mshukuru Mungu kwa kila jambo hata kama mengine yanaenda vibaya endelea kumwambia Mungu asante.

    *MAISHA NI WATU*
    *TABIA 12 ZITAKAZOKUFANYA UWE MWENYE FURAHA MAISHANI* *1. SAMEHE* Samehee hata wasiostahili kusamehewa. Usikubali kuwa na kinyongo au ugomvi na mtu yeyeto. Jifunze kupotezea. Usimjibu kila mtu kila kitu. Hata ukimya ni majibu. *2. JIAMINI* Hakuna lisilowezekana chini ya jua. Anza sasa. Wenye imani wana amani kila wakati. Wenye imani wanakuwa na uhakika wa kile wanachokitarajia. *3. JIFUNZE* Mungu hakumuumba mtu kuweza kila kitu wakati wowote. *4. JIPENDE* Umeumbwa kwa sura na mfano wa Mungu. Usijidharau wala kujishusha kiwango. Jitamkia mambo mazuri kila wakati. *5. TABASAMU* Furaha ni tiba ya moyo Jifunze kuhesabu baraka ambazo Mungu amekupatia itakisaidia kutabasamu kila wakati. *6. USIHUKUMU* Hakuna mwaminifu chini ya jua. Kila mmoja anakosea hata wewe huwa unakosea na kuwakosea wengine. *7. JIHESHIMU* Mfumo wa maisha yako ndio utakuwa msaada kwa wengine. Wewe ndiye utakayewafanya wengine kukutafasiri. *8. PANGA MALENGO* Malengo ni taa, dira, ramani,kesho, mwelekeo, matumaini. Usiishi pasipo kujua kesho yako au pasipo kujua unapoelekea. *9. FANYA IBADA* Mahusiano yako pamoja na Mungu ndio chanzo cha kubarikiwa kwako. *10. KULA VIZURI* Mwili wako ni hekalu la Roho Mtakatifu kuwa makini sana kwenye ulaji wako. Usile chochote unachotaka Bali kula chochote kinachohitajika mwilini mwako. *11. KUWA MKARIMU* Hukuja duniani na kitu Bali vyote ulivyonavyo chanzo chake ni Mungu. Lakini pia vyote utaviacha duniani siku yako ya kufa itakapofika. Ukarimu ni akiba ya baadae kwa ajili yako na kizazi chako. *12. KUWA NA SHUKRANI* Ukitambua na kutafakari ulipotolewa na huyu Mungu hakika hautashindwa kusema asante kwake. Mshukuru Mungu kwa kila jambo hata kama mengine yanaenda vibaya endelea kumwambia Mungu asante. *MAISHA NI WATU*
    Like
    Love
    2
    · 0 Σχόλια ·0 Μοιράστηκε ·473 Views
  • Usivutiwe na muonekano wake wa nje,maana hujui ndani yake Kuna nini

    Usivutiwe na upole wake maana hujui nafsi yake inawaza nini


    Usidanganyike na ucheshi wake hujui moyo wake una mshauri nini

    Usivutiwe na utajiri alionao maana hujui amepitia mangapi Katika maisha yake

    Yule usiye mtegemea na kumdhania Katika maisha yako, ndiye anaweza kuwa msaada wakati wa shida yako

    Yule umuonaye hana u muhimu Katika maisha yako na asiyefaa kusimama mbele ya macho yako, ipo siku ndiye atakaye kuwa malaika wako wa nuru siku yakikukuta

    Usidhani wewe ni bora kuliko wengine,jifunze kuheshimu wengine maana hujui ni nani atakaye kufadhili siku yakikufika

    Fikiria kabla ya kutenda kisha tafakari kabla ya kuamua kitu chochote, maana hatima yako haipo mikononi mwako
    *#Jose Bambo #*




    Usivutiwe na muonekano wake wa nje,maana hujui ndani yake Kuna nini Usivutiwe na upole wake maana hujui nafsi yake inawaza nini Usidanganyike na ucheshi wake hujui moyo wake una mshauri nini Usivutiwe na utajiri alionao maana hujui amepitia mangapi Katika maisha yake Yule usiye mtegemea na kumdhania Katika maisha yako, ndiye anaweza kuwa msaada wakati wa shida yako Yule umuonaye hana u muhimu Katika maisha yako na asiyefaa kusimama mbele ya macho yako, ipo siku ndiye atakaye kuwa malaika wako wa nuru siku yakikukuta Usidhani wewe ni bora kuliko wengine,jifunze kuheshimu wengine maana hujui ni nani atakaye kufadhili siku yakikufika Fikiria kabla ya kutenda kisha tafakari kabla ya kuamua kitu chochote, maana hatima yako haipo mikononi mwako *#Jose Bambo #*
    Like
    1
    · 1 Σχόλια ·0 Μοιράστηκε ·357 Views
  • TAFAKARI :

    Kulikuwa na Mwalimu mmoja aliyezoea kumchapa viboko mwanafunzi mmoja mchelewaji shuleni, Mwanafunzi huyo alikuwa ni mtoto wa kimasikini pia mpole sana na mwenye huruma na alikuwa akiishi eneo lenye umbali kiasi mpaka kufika shuleni, kwa hivyo Mwanafunzi yule takriban miaka 3 alikuwa akichelewa kipindi cha kwanza kila siku. Kwa hiyo siku ambazo Mwalimu huyo alikuwa na kipindi cha kwanza darasani kwao Mwanafunzi huyo alikuwa anachapwa kwanza kabla ya kuingia darasani. Hali hii iliendelea kwa muda mrefu, jambo la kushangaza wiki moja ilipita bila yule mwanafunzi kuonekana kabisa shuleni!

    Wiki ililoyofuata yule Mwanafunzi alifika shuleni mapema kabla ya Mwanafunzi mwingine yeyote. Mwalimu yule alishangaa sana alipomwona alifurahi sana alipoingia Darasani alimwita na kumsifia sana mbele ya Darasa kabla ya kumuuliza jambo lo lote.

    "Mwalimu akamwambia yule Mwanafunzi hebu simama akatii amri ya Mwalimu wake akasimama, Mwalimu akawaambia wanafunzi wenzake wampigie makofi kwa sababu leo kawa wa kwanza kufika shuleni. Mwalim akasema kumbe zile fimbo ninazomchapa zimesaidia sana eeeeenh?"

    Wanafunzi walipiga makofi huku wengine wakimcheka na kumdhihaki. Baada ya dakika kadhaa yule Mwanafunzi akamwomba Mwalimu ampe nafasi aseme jambo kidogo ili wapate kujua ni nini anataka kuwaelezea, Mwalimu akamruhusu huku akiwa amemkodolea macho haya tuambie.

    "Kwanza akawaomba radhi kwa kusema Mwalimu pamoja na wanafunzi wenzangu nyote kwa jumla, nakuombeni unisamehe iwapo nilikuwa nikiwaudhi kwa sababu siku zote nilizokuwa nikichelewa kufika shuleni nilikuwa namuuguza Mama yangu mzazi. Baba yangu alifariki kabla sijazaliwa, kwa hivyo sikujaaliwa kumuona nililelewa na Mama yangu tu naye alitengwa na ndugu kutokana na ufukara kwa hakika unyonge ni kitu kibaya sana simjui ndugu ye yote, Mama yangu alipopatwa na Maradhi tulimpeleka hospitalini Mimi ni jirani zetu lakini maradhi yake hayakuonekana. Akaruhusiwa kurudi nyumbani akiwa na Dawa za kutuliza maumivu tu." Kwa sababu hatukuwa na pesa sikuweza kumpeleka popote kwa vipimo zaidi."

    Mara akafuta machozi yaliyoanza kumtiririka kwa wingi mashavuni, na akasema kwa unyonge ewe Mwalimu wangu pamoja na wanafunzi wenzangu.

    "Kwa hivyo kila siku nilitakiwa kufanya usafi wa nyumba kuchota maji, kumsafisha Mama yangu pamoja na kumstiri, kumwandalia chakula chake kabla ya kuondoka kuja hapa shuleni na kazi zingine zote." Akanyamaza kidogo kwa uchungu."

    "Na sikitika kusema leo hii nimewahi kuja Shuleni kwa sababu Mama yangu alifariki wiki moja iliyopita ambayo sikuonekana shuleni nilikuwa nikimalizia msiba wa Mama yangu. Yote ndio mipango yake Mwenyezi Mungu kwa hiyo kilichokuwa kinanichelewesha kimeondoka ndio maana leo nimewahi kufika mapema shuleni."

    Hakuweza kuongea tena kutokana na uchungu, akakaa taratibu kitini huku akilia kwa kwikwi

    Hatimae Darasa zima nalo liligeuka mahala pa msiba kila mmoja akilia pamoja na Mwalimu wao, huku wakimpa pole na kumuomba msamaha kwa jinsi walivyokuwa wakimdhihaki. Naye akawaambia nimekusameheni kwa moyo safi kabisa.

    WITO:

    Msiharakishe kuadhibu wenzenu bila kuwapa nafasi ya kujieleza, sababu huwezi kujua jambo gani linalowasibu bila kuwapa fursa ya kujielezea au kukwambia ili upatikane ufumbuzi wa tatizo.

    Unapo muona mwenzako hayupo sawa kifikra, kiafya, au jambo lo lote muulize kwanza kabla ya kuanza kumshutumu.

    Tunamuomba Mwenyezi Mungu atujalie tuwe ni wenye kupendana, kuuliza na kusaidiana kwa kila jambo.
    TAFAKARI : Kulikuwa na Mwalimu mmoja aliyezoea kumchapa viboko mwanafunzi mmoja mchelewaji shuleni, Mwanafunzi huyo alikuwa ni mtoto wa kimasikini pia mpole sana na mwenye huruma na alikuwa akiishi eneo lenye umbali kiasi mpaka kufika shuleni, kwa hivyo Mwanafunzi yule takriban miaka 3 alikuwa akichelewa kipindi cha kwanza kila siku. Kwa hiyo siku ambazo Mwalimu huyo alikuwa na kipindi cha kwanza darasani kwao Mwanafunzi huyo alikuwa anachapwa kwanza kabla ya kuingia darasani. Hali hii iliendelea kwa muda mrefu, jambo la kushangaza wiki moja ilipita bila yule mwanafunzi kuonekana kabisa shuleni! Wiki ililoyofuata yule Mwanafunzi alifika shuleni mapema kabla ya Mwanafunzi mwingine yeyote. Mwalimu yule alishangaa sana alipomwona alifurahi sana alipoingia Darasani alimwita na kumsifia sana mbele ya Darasa kabla ya kumuuliza jambo lo lote. "Mwalimu akamwambia yule Mwanafunzi hebu simama akatii amri ya Mwalimu wake akasimama, Mwalimu akawaambia wanafunzi wenzake wampigie makofi kwa sababu leo kawa wa kwanza kufika shuleni. Mwalim akasema kumbe zile fimbo ninazomchapa zimesaidia sana eeeeenh?" Wanafunzi walipiga makofi huku wengine wakimcheka na kumdhihaki. Baada ya dakika kadhaa yule Mwanafunzi akamwomba Mwalimu ampe nafasi aseme jambo kidogo ili wapate kujua ni nini anataka kuwaelezea, Mwalimu akamruhusu huku akiwa amemkodolea macho haya tuambie. "Kwanza akawaomba radhi kwa kusema Mwalimu pamoja na wanafunzi wenzangu nyote kwa jumla, nakuombeni unisamehe iwapo nilikuwa nikiwaudhi kwa sababu siku zote nilizokuwa nikichelewa kufika shuleni nilikuwa namuuguza Mama yangu mzazi. Baba yangu alifariki kabla sijazaliwa, kwa hivyo sikujaaliwa kumuona nililelewa na Mama yangu tu naye alitengwa na ndugu kutokana na ufukara kwa hakika unyonge ni kitu kibaya sana simjui ndugu ye yote, Mama yangu alipopatwa na Maradhi tulimpeleka hospitalini Mimi ni jirani zetu lakini maradhi yake hayakuonekana. Akaruhusiwa kurudi nyumbani akiwa na Dawa za kutuliza maumivu tu." Kwa sababu hatukuwa na pesa sikuweza kumpeleka popote kwa vipimo zaidi." Mara akafuta machozi yaliyoanza kumtiririka kwa wingi mashavuni, na akasema kwa unyonge ewe Mwalimu wangu pamoja na wanafunzi wenzangu. "Kwa hivyo kila siku nilitakiwa kufanya usafi wa nyumba kuchota maji, kumsafisha Mama yangu pamoja na kumstiri, kumwandalia chakula chake kabla ya kuondoka kuja hapa shuleni na kazi zingine zote." Akanyamaza kidogo kwa uchungu." "Na sikitika kusema leo hii nimewahi kuja Shuleni kwa sababu Mama yangu alifariki wiki moja iliyopita ambayo sikuonekana shuleni nilikuwa nikimalizia msiba wa Mama yangu. Yote ndio mipango yake Mwenyezi Mungu kwa hiyo kilichokuwa kinanichelewesha kimeondoka ndio maana leo nimewahi kufika mapema shuleni." Hakuweza kuongea tena kutokana na uchungu, akakaa taratibu kitini huku akilia kwa kwikwi Hatimae Darasa zima nalo liligeuka mahala pa msiba kila mmoja akilia pamoja na Mwalimu wao, huku wakimpa pole na kumuomba msamaha kwa jinsi walivyokuwa wakimdhihaki. Naye akawaambia nimekusameheni kwa moyo safi kabisa. WITO: Msiharakishe kuadhibu wenzenu bila kuwapa nafasi ya kujieleza, sababu huwezi kujua jambo gani linalowasibu bila kuwapa fursa ya kujielezea au kukwambia ili upatikane ufumbuzi wa tatizo. Unapo muona mwenzako hayupo sawa kifikra, kiafya, au jambo lo lote muulize kwanza kabla ya kuanza kumshutumu. Tunamuomba Mwenyezi Mungu atujalie tuwe ni wenye kupendana, kuuliza na kusaidiana kwa kila jambo.
    Like
    3
    · 0 Σχόλια ·0 Μοιράστηκε ·859 Views
  • #Bad_Boy

    Saa zimepita, maisha yanaendelea, lakini kumbukumbu za "Mapito" bado ziko hai. Wimbo huu wa Kiswahili wenye mvuto unatupeleka kwenye safari ya kutafakari binafsi, ukichunguza changamoto na furaha za kuishi.

    Mapito
    https://youtu.be/V6ufZ6OeTsM?si=nIgp68yGKumUseZS

    Usiache ku support kwa ku subscribe , Like ,comment . Utatisha kama @Bad_Boy Uki Share na marafiki
    #Bad_Boy Saa zimepita, maisha yanaendelea, lakini kumbukumbu za "Mapito" bado ziko hai. Wimbo huu wa Kiswahili wenye mvuto unatupeleka kwenye safari ya kutafakari binafsi, ukichunguza changamoto na furaha za kuishi. 👇 Mapito 👇 https://youtu.be/V6ufZ6OeTsM?si=nIgp68yGKumUseZS Usiache ku support kwa ku subscribe , Like ,comment . Utatisha kama @Bad_Boy Uki Share na marafiki
    Like
    Love
    6
    · 1 Σχόλια ·0 Μοιράστηκε ·822 Views
  • #Bad_Boy

    Saa zimepita, maisha yanaendelea, lakini kumbukumbu za "Mapito" bado ziko hai. Wimbo huu wa Kiswahili wenye mvuto unatupeleka kwenye safari ya kutafakari binafsi, ukichunguza changamoto na furaha za kuishi.

    Mapito
    https://youtu.be/V6ufZ6OeTsM?si=nIgp68yGKumUseZS

    Usiache ku support kwa ku subscribe , Like ,comment . Utatisha kama @Bad_Boy Uki Share na marafiki
    #Bad_Boy Saa zimepita, maisha yanaendelea, lakini kumbukumbu za "Mapito" bado ziko hai. Wimbo huu wa Kiswahili wenye mvuto unatupeleka kwenye safari ya kutafakari binafsi, ukichunguza changamoto na furaha za kuishi. 👇 Mapito 👇 https://youtu.be/V6ufZ6OeTsM?si=nIgp68yGKumUseZS Usiache ku support kwa ku subscribe , Like ,comment . Utatisha kama @Bad_Boy Uki Share na marafiki
    Like
    Love
    5
    · 1 Σχόλια ·0 Μοιράστηκε ·819 Views
  • #Bad_Boy

    Saa zimepita, maisha yanaendelea, lakini kumbukumbu za "Mapito" bado ziko hai. Wimbo huu wa Kiswahili wenye mvuto unatupeleka kwenye safari ya kutafakari binafsi, ukichunguza changamoto na furaha za kuishi.

    Mapito
    https://youtu.be/V6ufZ6OeTsM?si=nIgp68yGKumUseZS

    Usiache ku support kwa ku subscribe , Like ,comment . Utatisha kama @Bad_Boy Uki Share na marafiki
    #Bad_Boy Saa zimepita, maisha yanaendelea, lakini kumbukumbu za "Mapito" bado ziko hai. Wimbo huu wa Kiswahili wenye mvuto unatupeleka kwenye safari ya kutafakari binafsi, ukichunguza changamoto na furaha za kuishi. 👇 Mapito 👇 https://youtu.be/V6ufZ6OeTsM?si=nIgp68yGKumUseZS Usiache ku support kwa ku subscribe , Like ,comment . Utatisha kama @Bad_Boy Uki Share na marafiki
    Like
    Love
    5
    · 1 Σχόλια ·0 Μοιράστηκε ·789 Views
  • #Bad_Boy

    Saa zimepita, maisha yanaendelea, lakini kumbukumbu za "Mapito" bado ziko hai. Wimbo huu wa Kiswahili wenye mvuto unatupeleka kwenye safari ya kutafakari binafsi, ukichunguza changamoto na furaha za kuishi.

    Mapito
    https://youtu.be/V6ufZ6OeTsM?si=nIgp68yGKumUseZS

    Usiache ku support kwa ku subscribe , Like ,comment . Utatisha kama @Bad_Boy Uki Share na marafiki
    #Bad_Boy Saa zimepita, maisha yanaendelea, lakini kumbukumbu za "Mapito" bado ziko hai. Wimbo huu wa Kiswahili wenye mvuto unatupeleka kwenye safari ya kutafakari binafsi, ukichunguza changamoto na furaha za kuishi. 👇 Mapito 👇 https://youtu.be/V6ufZ6OeTsM?si=nIgp68yGKumUseZS Usiache ku support kwa ku subscribe , Like ,comment . Utatisha kama @Bad_Boy Uki Share na marafiki
    Like
    Love
    5
    · 1 Σχόλια ·0 Μοιράστηκε ·793 Views
  • #Bad_Boy

    Saa zimepita, maisha yanaendelea, lakini kumbukumbu za "Mapito" bado ziko hai. Wimbo huu wa Kiswahili wenye mvuto unatupeleka kwenye safari ya kutafakari binafsi, ukichunguza changamoto na furaha za kuishi.

    Mapito
    https://youtu.be/V6ufZ6OeTsM?si=nIgp68yGKumUseZS

    Usiache ku support kwa ku subscribe , Like ,comment . Utatisha kama @Bad_Boy Uki Share na marafiki
    #Bad_Boy Saa zimepita, maisha yanaendelea, lakini kumbukumbu za "Mapito" bado ziko hai. Wimbo huu wa Kiswahili wenye mvuto unatupeleka kwenye safari ya kutafakari binafsi, ukichunguza changamoto na furaha za kuishi. 👇 Mapito 👇 https://youtu.be/V6ufZ6OeTsM?si=nIgp68yGKumUseZS Usiache ku support kwa ku subscribe , Like ,comment . Utatisha kama @Bad_Boy Uki Share na marafiki
    Like
    Love
    5
    · 1 Σχόλια ·0 Μοιράστηκε ·744 Views
Αναζήτηση αποτελεσμάτων